Title 2024

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

Karama tisa (9) za Roho mtakatifu tunazisoma katika kitabu cha 1Wakorintho 12.

Tusome,

1Wakorintho 12:4  “Basi pana tofauti za KARAMA; bali Roho ni yeye yule.

5  Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.

6  Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

7  Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.

8  Maana mtu mmoja kwa Roho apewa NENO LA HEKIMA; na mwingine NENO LA MAARIFA, apendavyo Roho yeye yule;

9  mwingine IMANI katika Roho yeye yule; na mwingine KARAMA ZA KUPONYA katika Roho yule mmoja;

10  na mwingine MATENDO YA MIUJIZA; na mwingine UNABII; na mwingine KUPAMBANUA ROHO; mwingine AINA ZA LUGHA; na mwingine TAFSIRI ZA LUGHA;

11  lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye”.

Tuangalie utendaji kazi wa moja baada ya nyingine.

      1. NENO LA HEKIMA.

Hii ni karama ya upambanuzi wa jambo lililo gumu kutatulika.. Kwamfano kunaweza kutokea jambo katika kanisa ambalo ni gumu sana kutatulika au kufahamika, (fumbo kubwa)..sasa mtu mwenye karama hii ya Neno la Hekima anaweza kulijua jambo hilo na kulitatua, au kutoa mapendekezo ya kulitatua kwa njia ya mafundisho au matendo..

Mfano wa mtu aliyekuwa na karama hii ni Sulemani..

Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa, basi ndoa nyingi zitasimama, na wizi na mambo ya kando kando hayataweza kupata nafasi kwasababu yatawekwa wazi.

     2. NENO LA MAARIFA.

Hii ni karama ya MAARIFA kama jina lake lilivyo.. Mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo mkubwa wa kujua mambo mengi..ya kidunia na kibiblia.. (Maarifa aliyonayo kuhusu biblia yanamtofautisha na mtu mwingine).. Vile vile maarifa anayokuwa nayo juu ya mambo mengine ya ulimwengu yanamtofuatisha na mkristo mwingine.

Watu wenye karama hii wakiwemo ndano ya kanisa, mafundisho ya manabii wa uongo ni ngumu kupata nafasi, (kwasababu manabii wa uongo wanawadanganya watu wasio na maarifa ya kutosha) sasa wakiwepo watu wenye karama hii ya maarifa, basi wanaweza kulifundisha kundi au kulielekeza mambo mengi kiusahihi kabisa.

Lakini wakikosekana ndio linatimia lile Neno “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa (Hosea 4:6)”

     3. IMANI

Hii ni karama ya kutenda matendo ya Imani.. Watu wenye karama hii katika kanisa ni wale wenye kutenda au kuhamasisha watu katika kanisa kufanya matendo ya Imani. Na maisha yao yote yakijaa matendo ya Imani.

Huwa hawaogopi magonjwa, changamoto, wala dhoruba yoyote.. Kukitokea hofu wamesimama imara!, kanisa likiishiwa nguvu, watu wenye hii karama wanalitia nguvu na kulihamasisha..

Watu kama hawa wakiwepo katika kanisa basi kanisa hilo haliwezi kupungua nguvu ya kuendelea mbele, wala watu wake hawawezi kukata tamaa daima.

     4. KARAMA ZA KUPONYA.

Zinaitwa “Karama za kuponya” na si “Karama ya kuponya”… Maana yake ni Karama hii inafanya kazi ya kuponya vitu vingi, ikiwemo magonjwa, maisha, roho, nafsi na vitu vingine vilivyoharibika.

Mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo wa kumwombea mtu na akapona kirahisi, au kumfundisha mtu na akapokea uponyaji kirahisi.. Vile vile ana uwezo wa kumwekea mtu mikono akapokea uponyaji kirahisi ikiwa ana ugonjwa au maisha yake yameharibika.

Vile vile anaweza kumfundisha mtu na mtu yule akaponyeka roho yake na majeraha ya adui.

Vile vile kama kazi ya mtu au maisha yake yameharibika mtu mwenye karama hii anaweza kumjenga upya kwa kumfundisha au kumwombea na mtu yule akaponyeka kabisa kabisa dhidi ya mapigo yote ya yule adui.

Watu kama wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa, basi kanisa hilo litakuwa na watu wanaosimama kila siku na hakuna atakayekuwa anaanguka.

     5. MATENDO YA MIUJIZA.

Hii ni karama ya Ishara ndani ya kanisa. Watu wenye karama hii ni wale ambao maisha yao yamejaa miujiza na ishara.. Wakiwemo ndani ya kanisa basi ni lazima kuna miujiza itaonekana ambayo itawashangaza wengi na kuwafanya waaamini mahali pale kuna Mungu.

Kuna watu wakiingia mahali au wakienda mahali lazima kuna tukio la ajabu litatokea pasipo hata kupanga au kusema (ni ishara ambazo zinafuatana nao).

Kunatokea ajali ghafla anatoka mzima bila dhara lolote.. hajala wiki 2 lakini bado anaonekana ana nguvu zile zile.. Anafika mahali kivuli chake kinaponya watu.. anaimba tu au anaongea!, watu wanajazwa Roho Mtakatifu n.k

Watu wa namna hii kwa ufupi, wanakuwa wanafanya vitu vya ajabu, na kuwa na matukio mengi ya kushangaza shangaza na wengi wenye karama hii wanakuwa na vipindi vya kukutana/kutokewa na malaika. Yote ni kwa lengo la kuthibitisha uwepo wa Mungu katika kanisa.

     6. UNABII

Hii ni karama inayohusika na kutabiri mambo yajayo au yanayoendelea sasa, au kuelezea yaliyopita.

Watu wenye karama hii wanakuwa na uwezo wa kuona mambo yajayo ya Mtu, Watu, kanisa au Taifa. Na nabii zao zinaegemea biblia. Na Mungu anawafunulia kwa njia aidha ya Ndoto, Neno au Maono.

Pia wana uwezo wa kumfundisha na kumwombea mtu au kumshauri kuhusiana na kile walichooneshwa! (kilichopita, kinachooendelea au kijacho).

Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa basi kanisa litasimama na kuendelea.

    7. KUPAMBANUA ROHO.

Hii ni karama ya kupambanua au kuzijaribu roho. Mtu mwenye karama hii anakuwa mwepesi wa kuzitambua roho (kama ni roho wa Mungu au roho nyingine).

Kama kuna roho ya uchawi inaingia basi anakuwa na uwezo wa kupambanua, kama ni roho ya uzinzi, wizi, uadui, fitina, n.k anakuwa na uwezo wa kuiona kabla ya wengine na hivyo kutoa mashauri au kuomba iondoke.

Vile vile mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo wa kujua utendaji kazi wa Roho Mtakatifu, ni rahisi kujua karama za watu katika migawanyo yake..(kwamba huyu ana karama hii na yule ile).. Na pia anakuwa na uwezo mkubwa wa kufundisha juu ya karama za roho.

Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa.. ni ngumu sana kanisa hilo kushambuliwa na roho nyingine..

     8. AINA ZA LUGHA.

Hii ni karama ya ishara ndani ya kanisa, ambayo madhumuni yake ni kama yale ya karama ya MIUJIZA.

Mtu mwenye karama ya lugha, anakuwa na uwezo wa kuzungumza lugha nyingi kimiujiza, (lugha za rohoni na za mwilini).. Lugha za rohoni ambazo (maarufu kama kunena kwa lugha).. mtu anakuwa na uwezo wa kuzinena na wakati mwingine kutoa tafsiri zake.

Lakini Zaidi sana anakuwa na uwezo wa kunena lugha nyingine za jamii nyingine.. Pindi anapojaa Roho Mtakatifu anajikuta anauwezo wa kunena lugha ya taifa lingine au kabila lingine ambalo sio lake, tena anazungumza vizuri sana.

Na watu wa wanapoona huyu mtu hajasoma kabisa lakini anaongea kiingereza kizuri namna hiyo, basi wanamshangaa Mungu na kumtukuza na kumwamini, na baadaye yule mtu akimaliza kunena basi anarudi katika hali yake ya kawaida ya kuongea lugha yake ya asili.

Watu wenye karama hii wakiwepo ndani ya kanisa..basi hofu ya Mungu inaongezeka na kuthibitisha kuwa Mungu yupo katikati ya kanisa lake.

     9. TAFSIRI ZA LUGHA.

Hii ni karama ya 9 na ya mwisho iliyotajwa katika orodha hii..  Karama hii inahusiana pakubwa sana na ile ya “Aina za lugha”.. Kwani mwenye karama ya Aina za lugha, mara nyingine atamwitaji huyu mwenye Tafsiri za lugha ili aweze kutafsiri kinachozungumzwa.. ili kanisa lisiingie katika machafuko. (Soma 1Wakorintho 14:27).

Hizi ndizo karama 9 maarufu katika biblia. Zipo karama nyingine kama za kukirimu, au Uimbaji hizo zinaangukia katika kundi la huduma ya UINJILISTI, Mtu anayeimba anafanya uinjilisti, hivyo ni mwinjilisti!.

Na mtu anaweza kuwa na karama Zaidi ya moja, (Maana yake mtu anaweza kuwa na karama ya Imani na pia ya kinabii au ya Aina za Lugha, na Tafsiri za lugha hapo hapo) ingawa jambo hilo linakuwa ni nadra sana!…. Lakini Roho Mtakatifu ndiye anayemgawia mtu na si mtu anajipachikia!.

Na kumbuka!. Karama za Roho Mtakatifu ni kwa lengo la kufaidiana na si kuonyeshana au biashara.. Karama nyingi shetani kaziua kwa njia hiyo (anawapachikia watu kiburi, au kupenda sifa na utukufu na fedha).. mwisho wa siku kile kipawa kinazima!.

Ili kufufua karama iliyozima, njia ni kujishusha, kuwa mnyenyekevu, vile vile uwe na nia ya Kristo ya kulijenga kanisa, na pia ukubali na uheshimu kujengwa na karama nyingine, lakini ukijiona wewe ni wewe huhitaji wengine, fahamu kuwa hata cha kwako hakitaweza kufanya kazi.

Kanisa la siku za mwisho, tuna tatizo kubwa sana wa kuruhusu utendaji kazi wa Roho Mtakatifu kupitia karama zilizowekwa ndani yetu.. Na tatizo kubwa lipo kwa “viongozi” na “wasio viongozi (washirika)”.

Viongozi wengi hawaruhusu vipawa hivi vitende kazi aidha kutokana na wivu, au kutokuwa na maarifa ya kutosha kuhusiana na vipawa hivyo…

Lakini pia na watu wengine ndani ya kanisa (washirika) wanaoujenga mwili wa Kristo. Wanapokataa kujishughulisha vya kutosha na mwili wa Kristo, basi vile vipawa vilivyopo ndani yao vinazima, na hivyo kanisa linabaki na karama moja au mbili zinazofanya kazi.

Fahamu kuwa unapoenda kanisani, unacho kitu cha kiroho kwaajili ya ule mwili.. Ni wajibu wako kupambana mpaka kitokee, na kionekanane na kifanye kazi…usinyooshee tu kidole, wala usilaumu tu, na wakati huo wewe mwenyewe karama imekufa ndani yako (hujijui wewe ni nani/wala nafasi yako ni ipi), kanisani unaenda tu kama mtu anayeangalia Tv asiyehusika na mambo yanayoendelea kule (Hiyo haifai kabisa kwa mkristo aliyeokoka).

Ukiambiwa uombe huombi!! Karama yako itatendaje kazi ndani yako??,..ukiambiwa ufunge hufungi!! kuhudhuria tu kwenye ibada ni lazima ukumbushwe kumbushwe!..na bado unalaumu kanisani hakuna karama?..hiyo karama ipo kwa nani kama si ndani yako, na wewe umeiua kwa ukaidi wako???

Katika nyumba ya Mungu kila mtu lazima awe kiungo, ndipo udhihirisho mkamilifu wa Roho utaonekana.

Bwana akubariki na atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?

Rudi nyumbani

Print this post

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Mstari huu unaeleza uhalisia wa mambo kwa ujumla wake katika maisha ya wanadamu hapa duniani.

Tunafahamu kwamba maskini wengi hutumia maombi kupata kitu, huwa wanyenyekevu pale wanapotaka kupewa kitu, kwasababu hawana. 

Lakini matajiri hawawezi kujishusha (japo si wote) kauli zao huwa ni za lazima na zenye amri. Kwani mali zake humpa kiburi. Hivyo waombe ya nini?

Sasa biblia haitufundishi tuwe matajiri ili tuwe wakali (wenye sauti) hapana, bali inatutahadharisha matokeo ya mafanikio yoyote. Jinsi yanavyoweza kumpotezea mtu unyenyekevu wake.

Bwana akunyanyuapo, ndio uwe wakati wako wa kujishusha. Kwasababu mali, fedha, mafanikio visipowekewa mipaka yake vinaweza kuyaharibu maisha ya mwaminio kwa sehemu kubwa. (1Timotheo 16:10)

Lakini pia katika eneo la kiroho. Kuna maneno haya Bwana Yesu aliyasema.

Mathayo 5:3

[3]Heri walio maskini wa roho;  Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 

Ikiwa na maana watu walio maskini rohoni, ni wale wanaojiona kila siku wana haja na Mungu, bado hawajafika. Na hivyo humlilia Mungu sikuzote kwa unyenyekevu ili Bwana ayaongoze maisha yao.

Lakini wale wanaojiona wamefika wanajua kila kitu hawawezi kufanya hivyo. Ndio wale mafarisayo enzi za Bwana Yesu ambao hata kuomba kwao kulikuwa ni kwa majivuno (Luka 18:9-14). Hawawezi kujishusha, maneno yao ni ya ukali, wala hawaoni shida kumwita hata  Bwana wao Beelzebuli.

Hata kama tutakuwa tumepiga hatua kubwa kiasi gani rohoni, Bwana hataki tujidhani kuwa sisi tumefika, sisi ni matajiri, bali tumtegemee yeye sikuzote haijalishi wewe ni mtumishi mkubwa au uliyeokoka leo. 

Unyenyekevu kwa Bwana unapaswa uwe ni uleule. Usiende mbele za Mungu kama mtumishi wa Mungu, nenda kama mtoto wa Mungu mfano tu wa yule ambaye kaokoka leo. Jinyenyekeze kama vile ndio umeokoka leo. Kwasababu kumjua Bwana itatuchukua milele.

Lakini tukijiona ni matajiri tutaishia katika anguko hili alilolisema katika..

Ufunuo 3:17-19

[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 

[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 

[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 

Hivyo katika utajri wowote (wa kiroho /kimwili). Bwana atupe unyenyekevu kama wa maskini. Ndio kiini cha mstari huo.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 25:13

Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;  Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao. 


JIBU: Kwa wanaoishi maeneo ambayo kuna misimu ya theluji, wanafahamu kuwa vipindi hivyo vya baridi vinapofika, huwa kunakuwa na upepo-baridi unaovuma.

Sasa kwa mujibu wa vifungu hivyo, anasema, Kama upepo huo ukivuma kipindi cha mavuno, ambacho kimsingi ni wakati wa kiangazi,na sio baridi, kingekuwa ni shangwe kubwa sana kwa wavunaji.

Kwa namna gani?

Kazi ya uvunaji inafanyika wakati wa jua kali, kwasababu mazao pia wakati huo yanakuwa yamekauka. Lakini pia mfano jua lile likapoozwa na upepo wa baridi, huuburudisha sana moyo wa mvunaji.

Vivyo hivyo anafananisha na wajumbe waaminifu wanaotumwa kupeleka habari fulani anasema; 

“Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao”. 

Mjumbe wa kwanza mwaminifu aliyetumwa ni Bwana wetu Yesu Kristo. Alimburudisha Baba moyo wake, kwasababu yote, na kusudi alilopewa kulifanya la kutukomboa sisi alilitimiza lote.

Vivyo hivyo na sisi, tumewekwa kuwa wajumbe wa Bwana, wa kuenenda  kuihubiri injili ya Kristo kwa kila kiumbe, ulimwenguni kote. Yatupasa tuwe waaminifu, mfano wa Bwana na mitume wake, ili moyo wa Kristo wetu ufurahi.

Na thawabu ya kuuburudisha moyo wa Bwana ni sisi kupewa mamlaka kubwa kule ng’ambo tufikapo, kwa mfano ambao Bwana Yesu aliutoa katika vifungu hivi;

Luka 19:12-26

[12]Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi. 

[13]Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja. 

[14]Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale. 

[15]Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake. 

[16]Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

[17]Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. 

[18]Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida. 

[19]Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

[20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 

[21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 

[22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 

[23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 

[24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 

[25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 

[26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho. 

Je na sisi tunaweza kuwa mbele za Bwana Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; ?

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Je! Umeokoka?

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

SWALI: Je! ni sahihi kwa mkristo kufanya biashara za kifedha mitandaoni kama vile Forex, na crypto-currency mfano wa bitcons?


JIBU: Ni vema kufahamu biashara za kifedha mitandaoni kama forex ni nini?

Ni biashara ya ubadilishaji wa fedha za kigeni katika soko la dunia. Yaani ununuaji na uuzaji wa fedha za kigeni, sawa tu ile tuliyowahi kuisikia, ijulikanayo kama Bureau de change, ambayo watu wanakwenda kununua/kuuza pesa za kigeni, isipokuwa hii hufanyika mitandaoni, tofauti na bureau ambayo hufanyika kwa makarati ndani ya ofisi Fulani maalumu. Biashara hii ya forex na nyinginezo Mara nyingi hufanywa na taasisi kubwa za kifedha kama mabenki na makampuni, lakini pia hata watu binafsi.

Ni biashara ya bahati nasibu, inayofanana na michezo ya kubahatisha kitabia.. Lakini ni tofauti kabisa kimaudhui.

Biashara  hii ni ya uwekezaji, ambayo imehalalishwa ki-ulimwengu, japokuwa hatusemi kuwa kila biashara iliyohalalishwa na taifa kuwa ni halali kwa mkristo kufanya, hapana mfano zipo pombe zimehalalishwa kitaifa lakini kwa mkristo sio sawa kufanya biashara kama hizo.

Lakini, biashara hii, haihusishi katika kumdhulumu mtu, au kumlaghai mtu kiakili, apoteze kitu Fulani ili wewe ujilimbikizie fedha zake ambazo hazina mzungumko wowote wa kimaendeleo. Mfano wa hizo ni kama vile “Betting na kamari”. Kwa mkristo kushiriki katika biashara hizo za betting na kamari sio sawa. Kwa urefu wa somo lake pitia link hii >>>JE! KUBET NI DHAMBI?

Lakini Forex na nyinginezo zijulikanazo kama biashara za uwekezaji, zinahitajika sana, kwasababu kama zikikosekana, basi mzunguko wa fedha za kigeni, ungekuwa mgumu sana, na hivyo kupunguza kasi ya ukuaji uchumi, katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia.

Hivyo tukirudi kwa mkristo, je kufanya biashara hii ni dhambi?

Kimsingi ikiwa anafanya kwa lengo la uwekezaji wake, huku akijua pia ni kwa faida ya uchumi, na hamdhulumu au kumlaghai mtu. Hafanyi kosa. Lakini akiwa na fikra za kikamari, kama vile afanyavyo kwenye betting, Kwake itakuwa ni kosa, kwasababu dhamiri yake inamshuhudia, ameigeuza kama kamari moyoni mwake.

Ndio hapo hili andiko linakuja.

Warumi 14:22  Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23  Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. NA KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI.

Maana yake ni kuwa ukiwa na mashaka moyoni mwako kuifanya kazi hii, basi ni heri usifanye kabisa, kwasababu mashaka yoyote ni dhambi. Lakini kimsingi biashara hii sio kosa kwa mkristo, ambaye ana maarifa/elimu ya kutosha juu ya biashara za kifedha katika ulimwengu wa sasa.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

Neno kupomoka linamaana gani kwenye biblia?(Hesabu 16:22)

Hesabu 16:20 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,  21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja.  22 Nao WAKAPOMOKA kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?

Soma pia

Yoshua 5:13 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? 

14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshua AKAPOMOKA kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake?

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi baadhi; Hesabu  16:4, 16:45,

Ni Kiswahili cha zamani cha Neno kuporomoka.  Yaani kuanguka chini, kwamfano maji yanayoelekea chini kwa wingi tunasema maporomoko ya maji, au udongo unaoanguka kutoka milimani kwa wingi tunasema maporomoko ya udongo.

Hivyo, katika vifungu anaposema Musa na Haruni wakapomoka kifudifudi, anamaanisha wakaanguka chini kifudi fudi mbele za Mungu kumlilia Bwana rehema.

Je! Na sisi tuombapo rehema au  tumtakapo Bwana kwa jambo Fulani muhimu ni lazima tupomoke chini ili tusikiwe ?

Jibu lake ni kwamba sio takwa kufanya hivyo. Kwasababu Mungu anaangalia moyo, kupomoka kwetu kunapaswa kuwe moyoni. Lakini pia si vibaya kuomba kwa namna hiyo, na ni vema, kwasababu pia ni ishara moja wapo ya unyenyekevu wa moyo. Ni sawa tu na tunapopiga magoti, au kunyosha mikono juu wakati wa kumwomba Mungu, kama ishara ya unyenyekevu mbele zake.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni kwanini tunambariki Mungu? Je! Mungu huwa anabarikiwa?

LAANA YA YERIKO.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Kuwatema farasi, maana yake ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

UJAZO WA BIBLIA KATIKA MGAWANYO WAKE.

> Kuna vitabu vingapi katika Agano Jipya na Agano la Kale?,

> Kuna sura/milango mingapi katika kila mgawanyo?

> Na watu gani waliotajwa sana katika biblia zaidi ya wengine wote?

KUJUA HAYO YOTE, TAZAMA MAJEDWALI YAFUATAYO 

(Slide kushoto kusoma zaidi taarifa katika jedwali).

N/AMGAWANYOIDADI YA VITABUIDADI YA SURA (MILANGO)IDADI YA MISTARI
1.AGANO LA KALE3926023,145
2.AGANO JIPYA279297,957
JUMLA661,18931,102

JINANAFASI (KATIKA BIBLIA)IDADI ALIZOTAJWA (Mara ngapi)NAFASI
YOABUJemedari wa Mfalme Daudi12916
ISAKAMwana wa Ibrahimu12915
SAMWELINabii (Mwana wa Elkana)14214
YEREMIANabii (Mwana wa Hilkia)14513
PETROMtume (Mwana wa Yona)19312
YOSHUAJemedari wa Israeli21911
PAULOMtume (Mwenyeji wa Tarso)22810
YUSUFUMwana wa Yakobo2469
SULEMANIMfalme (Mwana wa Daudi)2728
ABRAHAMUBaba wa Imani2947
HARUNIKuhani Mkuu3426
SAULIMfalme (Mwana wa Kishi)3625
YAKOBOIsraeli (Mwana wa Isaka)3634
MUSANabii (Mwana wa Amramu)8033
DAUDIMfalme (Mwana wa Yese)9712
YESU KRISTOMFALME wa Wafalme, Bwana wa mabwana, Mwana wa Mungu, Mwokozi, Simba wa kabila Yuda, Mesia, Mwokozi na Mchungaji Mkuu.1,2811

Kwanini YESU KRISTO ndiye anayeonekana kutajwa sana katika Biblia??.. Ni kwasababu yeye ndiye kitovu cha UZIMA, na Biblia yote inamhusu yeye, na kutuelekeza kwake.

YESU KRISTO, ndiye Njia, KWELI na UZIMA.. Mtu hawezi kumwona MUNGU nje ya YESU KRISTO (Yohana 1:18 na 14:6)

Tafadhali shea na wengine;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU

Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia

TAKWIMU ZA KIBIBLIA

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi nyumbani

Print this post

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

Ifutayo ni mistari kadhaa ya biblia ihusuyo shukrani/ kushukuru.


Zaburi 9:1 “Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote; Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu”.

Zaburi 18:49 “Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako”

2Samweli 22:50 “Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako”.

Zaburi 30:12 “Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele”

Zaburi 35:18 “Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; Nitakusifu kati ya watu wengi”

Zaburi 52: 9 “Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako”

Zaburi 118: 21 “Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu”.

Zaburi 71:22 “Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu. Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli”.

Zaburi 119: 7 “Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako”

Zaburi 106:1 “Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele”.

Zaburi 28:7 “Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru”.

2Wakorintho 2:14  “Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu”.

Ikiwa uko kwenye soko, https://www.swisswatch.is/product-category/rolex/explorer/ jukwaa letu ni chaguo lako bora! Duka kubwa zaidi la ununuzi!

Wakolosai 4:2 “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani”.

Zaburi 100:4 “Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake”

Zaburi 107:7 “Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa

8 Na wamshukuru Bwana, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu”.

1Wakorintho 15:57  “Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo”.

Zaburi 95: 2 “Tuje mbele zake kwa shukrani, Tumfanyie shangwe kwa zaburi”.

Wakolosai 3:15  “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani”.

Ufunuo 11:17 “wakisema, Tunakushukuru wewe, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa sababu umeutwaa uweza wako ulio mkuu, na kumiliki”

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

NENO LA FARAJA KWA WAFIWA.

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Rudi nyumbani

Print this post

NENO LA FARAJA KWA WAFIWA.

Maandiko ya faraja kwa wafiwa/ Neno la kufariji wafiwa (waliopatwa na msiba).


Ikiwa Mtu kafariki katika Kristo, basi lipo tumaini la kumwona tena..lakini kwa namna moja au nyingine, wafiwa watakuwa katika huzuni kwasababu hawatamwona tena kwa kitambo…hivyo yafuatayo ni maneno machache yanayoweza kuwafaa waliofiwa.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”

Yoshua 1:9 “Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako”.

Yakobo 1:2  “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3  mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”

Yohana 16:22  “Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye”.

Mathayo 5:4  “Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika”

Zaburi 34:18 “Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa”.

Zaburi 116:15 “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake”

Zaburi 73:26 “Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”

Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu”

Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”

Makala haya yanatoa usafirishaji wa bila malipo kwa bidhaa zinazostahiki, http://swisswatch.is au ununue mtandaoni na uchukue dukani leo katika Idara ya Matibabu.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Mistari ya biblia kuhusu maombi.

Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

MAOMBI YA YABESI.

JE! MUNGU NI NANI?

Rudi nyumbani

Print this post

WEKA ANWANI HII KATIKA MAHUBIRI YAKO!

(Masomo maamulu kwa watumishi wa Mungu).

Je wewe ni mtumishi wa MUNGU?..Basi fuatilia mfululizo wa masomo haya katika tovuti yetu hii (www.wingulamashahidi.org).

Kama mtumishi wa Mungu kuna  Anwani au nembo au Lebo ambayo inapaswa iambatane na kila fundisho unalolitoa kwa wahusika. Na Anwani/lebo hiyo/nembo hiyo si nyingine Zaidi ya “TOBA”. Hakikisha mahubiri yako yanalenga Toba, au kuwakumbusha watu umuhimu wa kujitakasa.

Kwanini iko hivyo?

Hebu tujifunze kwa mmoja ambaye ni mjumbe wa Agano, tena ndiye Mwalimu wetu MKUU na Mwinjilisti MKUU YESU KRISTO.

Yeye katika mahubiri yake yote alihubiri “Toba”.. Huenda unaweza kusoma mahali akiwa anafundisha na  usione likitajwa neno Toba, lakini fahamu kuwa alikuwa anahubiri Toba kila siku katika mafundisho yake yote… Kwani biblia inasema kama yote aliyoyafanya BWANA YESU kama yangeandikwa basi dunia isingetosha kwa wingi wa vitabu.

Yohana 21:25 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”

Kwahiyo Mahubiri ya BWANA WETU YESU yote Yalikuwa yamejaa toba.. sasa tunazidi kulithibitishaje hilo?.. hebu tusome maandiko yafuatayo..

Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”

Nataka tuutafakari kwa undani huu mstari… anasema “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”…. Zingatia hilo neno “TOKEA WAKATI HUO….TOKEA WAKATI HUO…TOKEA WAKATI HUO”.. Maana yake “kilikuwa ni kitu endelevu”, sio kitu cha kusema mara moja na kuacha, (hiyo ndiyo ilikuwa lebo ya mafundisho yake daima).. Kila alipohubiri lazima aliwahubiria pia watu watubu.

Umeona?. Je na wewe Mchungaji, na wewe Mwalimu wa injili, na Wewe nabii, na wewe Mtume, na wewe Mwimbaji wa injili.. LEBO YA MAHUBIRI YAKO NI IPI????.

Je! injili yako unayohubiri ni ya TOBA, au ya kuwafariji watu katika dhambi zao??.. Je unazunguka huku na kule kuhubiri injili ya namna gani?..Je ni injili ya Toba au ya Mali tu!.

Luka 24:45  “Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.

46  Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47  na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.

48  Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya”

Hakuna furaha, hakuna mafanikio, hakuna Amani ikiwa mtu yupo katika maisha ya dhambi.. utamhubiria afanikiwe lakini hata akiyapata hayo mafanikio basi dhambi itamuua tu na kumkosesha raha.. Raha pekee na Amani mtu ataipata baada ya kutubu, ndivyo maandiko yasemavyo..

Matendo 3:19 “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana”

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Toba ni nini?

VYA MUNGU MPENI MUNGU.

NAYAJUA MATENDO YAKO.

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Rudi nyumbani

Print this post

Toba ni nini?

Swali: Toba maana yake nini?.. na je ina umuhimu gani kwetu?


Jibu: Neno “Toba” liinatokana na neno “kutubu”. Mtu anayetubu maana yake kafanya “TOBA”. Na kutubu maana yake ni “kugeuka, kutoka katika njia uliyokuwa unaiendea”.. Maana yake kama mtu ameshawishika kugeuka kutoka katika njia au mwenendo aliyokuwa anauendea kwa njia ya majuto na maombi ya kuomba msamaha kama njia hiyo ilikuwa ni kwanzo kwa mwingine, mtu huyo anakuwa ametubu, au amefanya TOBA.

Kibiblia mtu aliyegeuka na kuiacha njia ya dhambi aliyokuwa anaiende na kuomba msamaha kwa Mungu wake aliyemkosea, basi mtu huyo anakuwa amefanya TOBA, na ndio hatua ya kwanza kabisa ya Mtu kumsogelea MUNGU, hakuna njia nyingine tofauti na hiyo!.

Injili ya Yohana Mbatizaji na ya BWANA YESU (Mjumbe wa Agano jipya) ilianza na Toba.

Yohana 3:1  “Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,

TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Maana yake watu waageuke na kuacha maisha ya kuabudu sanamu, waache maisha ya mauaji, waache maisha ya uzinzi na uasherati, waache maisha ya ulevi na utukanaji n.k.. kwasababu Ufalme wa mbinguni hautawapokea watu wa namna hiyo.

Lakini pia si kutubu tu, bali ni pamoja na “KUZAA MATUNDA YAPATANAYO NA HIYO TOBA”.. Maana yake baada ya kugeuka na kuacha dhambi, basi mwongofu huyo anapaswa ajifunze kuishi maisha yanayoendana na toba yake hiyo, maana yake asirudie tena machafu ya nyuma yatawale maisha yake.

Luka 3:8 “Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto”.

Je na wewe umetubia dhambi zako na kumkaribisha YESU maishani mwako? Kama bado basi fungua hapa ufuatilize sala hii ya TOBA na KRISTO YESU ataingia maishani mwako kwa Imani >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi nyumbani

Print this post