NENO LA FARAJA KWA WAFIWA.

NENO LA FARAJA KWA WAFIWA.

Maandiko ya faraja kwa wafiwa/ Neno la kufariji wafiwa (waliopatwa na msiba).


Ikiwa Mtu kafariki katika Kristo, basi lipo tumaini la kumwona tena..lakini kwa namna moja au nyingine, wafiwa watakuwa katika huzuni kwasababu hawatamwona tena kwa kitambo…hivyo yafuatayo ni maneno machache yanayoweza kuwafaa waliofiwa.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”

Yoshua 1:9 “Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako”.

Yakobo 1:2  “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3  mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”

Yohana 16:22  “Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye”.

Mathayo 5:4  “Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika”

Zaburi 34:18 “Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa”.

Zaburi 116:15 “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake”

Zaburi 73:26 “Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”

Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu”

Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Mistari ya biblia kuhusu maombi.

Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

MAOMBI YA YABESI.

JE! MUNGU NI NANI?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments