Category Archive Home

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Shalom, Karibu tujifunze Biblia,

Huu ni mwendelezo wa uchambuzi wa vitabu vya Biblia leo tutasogea mbele kitabu kimoja kinachofuata cha Ezra.Katika vitabu vilivyotangulia vya Wafalme na Mambo ya Nyakati, tuliona ni kwa jinsi gani, Mungu alishughulika na Taifa la Israeli kupitia Wafalme wake, na Tumeona ni jinsi gani wafalme hao ambao walitaka wawatawale jinsi walivyokuwa mwiba kwao, mpaka kuwasababishia waingie katika matatizo mazito..

Tunamwona kwamfano Mfalme Sulemani japokuwa alikuwa ni mpakwa Mafuta wa Bwana lakini aliwatumikisha Israeli vikali sana, (1 Wafalme 12:4 ) jambo ambalo halikuwa mpango wa Mungu tangu mwanzo, tunalisoma hilo katika 1Samweli 8:11-18 na Pia ndiye aliyesababisha Taifa la Israeli kugawanyika sehemu mbili (Upande wa kaskazini na upande wa kusini), jambo ambalo pia halikuwa mpango kamili wa Mungu watu wake wagawanyike.


Na wafalme wengine wote waliofuata wa Israeli na Yuda kama Mfalme Yeroboamu, Mfalme Ahabu na Mfalme Manase waliwakosesha waisraeli sana, na kuwafanya watu waabudu sanamu na miungu migeni…Kwamfano Mfalme Manase hakuishia tu kuabudu sanamu bali pia aliitengeneza madhabahu ya mungu mgeni ndani ya lile Hekalu la Sulemani na kuiabudu huko,(2 Wafalme 21) na pia alimtoa sadaka ya kuteketezwa mwanawe, na alikuwa anafanya uchawi na uganga pamoja na kutazama bao na kujihusisha na wachawi na wapunga pepo. Huyo ni Mfalme anafanya mambo hayo yote, akafanya dhambi kuliko hata mataifa wasio mjua Mungu wa kweli.

Kwasababu hiyo basi Mungu akaghadhibika sana kuahidi kuwa watakwenda utumwani. Na wakati ulipofika walichukuliwa utumwani, ambapo mataifa 10 yalichukuliwa utumwani Ashuru na Yuda wakachukuliwa Babeli, na huko wakakaa miaka 70 sawasawa na unabii Mungu aliompa Nabii Yeremia. Na baada ya miaka hiyo sabini kuisha Mungu alitabiri kuwa watatoka. Sasa kama hujapitia uchambuzi wa vitabu hivi kwa ufupi ni vyema ukapitia ili tuende pamoja.

Sasa Ni mambo gani yalikuwa yanaendelea walipokuwa huko Babeli?..Tutakuja kuona tutakapofika katika kitabu cha Danieli na Ezekieli…Lakini kitabu hichi cha EZRA kinaruka mpaka wakati wana wa Israeli wanatoka Babeli…Kwa mpangilio mzuri kingepaswa kianze kwanza kitabu cha Danieli ndipo kifuate cha Ezra lakini biblia haijaviweka vitabu katika mfululizo huo.Kitabu cha Ezra kimeandikwa na Ezra mwenyewe.

EZRA NI NANI?

Biblia inasema Ezra alikuwa ni mwandishi mwepesi katika sheria ya Musa.

Ezra 7: 6 “.. huyo Ezra akakwea kutoka Babeli; naye alikuwa MWANDISHI MWEPESI KATIKA SHERIA YA MUSA, aliyokuwa ameitoa Bwana, Mungu wa Israeli; naye mfalme akamjalia matakwa yake yote, kama mkono wa Bwana, Mungu wake, ulivyokuwa pamoja naye”

Maana ya mwandishi mwepesi ni mtu ambaye YUPO TAYARI kufanya jambo, yaani mwepesi katika kufanya jambo fulani, sio mzito..Ndio maana hapo biblia imemtaja Ezra kama Mwandishi mwepesi.

Kadhalika Mwandishi katika desturi za wayahudi alikuwa ni mtu anayefanya kazi kama za sasahivi za uwakili, alikuwa ni mtu anayeijua sheria ya Musa vizuri na hivyo ni rahisi kufahamu kipengele fulani cha sheria kinasema hivi au vile…Katika Agano jipya utaona Bwana Yesu amewataja waandishi sehemu kadha wa kadha..soma (Mathayo 17:10, Mathayo 20:18, Mathayo 21:15, Mathayo 23:2 n.k).

Pamoja na kwamba walikuwa na kazi ya kuhukumu kwa kupitia vipande vya sheria na kufundisha watu, lakini pia walikuwa na kazi nyingine wanayoifanya ya kunakili torati…Kumbuka zamani hizo hakukuwa na mashine za photocopy kama tulizonazo leo…Hivyo Nakala zote zilikuwa zinatengenezwa kwa kunakiliwa tena mahali pengine…

Kwahiyo kazi ilikuwepo kubwa ya kutengeneza nakala nyingi kila siku, waandishi hawa walikuwa wanaandika usiku na mchana, Katika kunakili walikuwa na vigezo vyao vya kufuata, kwanza mwandishi lazima ayatamke maneno Dhahiri ndipo ayaandike, na pia wakati wa kuandika anapokutana na jina la Mungu takatifu YEHOVA alikuwa anasimama kwanza ananawa mwili wote na kuisafisha kalamu yake ndipo aliandike. Na nakala ikishakamilika, itahakikiwa kwa siku 30 kabla ya kuruhusiwa itumike, na endapo zitaonekana kurasa mbili au tatu zitahitaji marekebisho basi nakala nzima inaachwa, kazi inaanza upya. Na kila aya na kila Neno lilikuwa linahesabiwa kuhakikisha na kitabu halisi. Kulikuwa na sheria nyingine nyingi tu katika uandishi…

Hivyo kazi ya uandishi ilikuwa inaheshimiwa sana katika Israeli, na huyu Ezra alikuwa mmoja wao wa hao waandishi, lakini biblia inamtaja alikuwa ni mwandishi mwepesi, yaani alikuwa anaifanya kazi yake kwa kupenda pasipo kusukumwa, na katika ufasaha, tofauti na wengine, Ndiye aliyekiandika kitabu cha Mambo ya nyakati tulichotangulia kukipitia…
Na katika kitabu hichi Roho ya Bwana ilimjia na kuanza kuandika hatua kwa hatua jinsi wana wa Israeli walivyotoka Babeli na kurudi Israeli, kuanzia Kundi la kwanza lililotoka Babeli na kurudi Nchi ya Ahadi mara baada tu ya Mfalme Koreshi kutoa amri ya uhuru wao. Na Kundi hilo ndio tunalolisoma katika Ezra Mlango wa 2.

Naye pia Ezra alikuwa ni miongoni mwa waliotoka Babeli na kurudi nchi ya Ahadi lakini yeye alikuwa katika lile kundi la pili ambalo tunalisoma katika mlango wa 7. Wakati Ezra anarudi kulikuwa tayari kuna lile kundi la kwanza lililotangulia miaka kadhaa nyuma, hivyo kuna mambo ambayo walikuwa wameyasahau yahusuyo sheria za Mungu, na kadhalika hata nyumba ya Mungu ambayo walikuwa wanaijenga upya ilisimama… hivyo Ezra alikusudia moyoni mwake atakaporudi awafundishe na kuwakumbusha wana wa Israeli sheria zote za Mungu wa Israeli na nini torati ya Musa inasema, na Bwana alimsaidia kupata kibali mbele ya Mfalme wa Uajemi, na kusapitiwa kwa kila kitu alichokihitaji ili tu akawafundishe sheria za Mungu.

Ezra 7: 6 “huyo Ezra akakwea kutoka Babeli; naye alikuwa mwandishi mwepesi katika sheria ya Musa, aliyokuwa ameitoa Bwana, Mungu wa Israeli; naye mfalme akamjalia matakwa yake yote, kama mkono wa Bwana, Mungu wake, ulivyokuwa pamoja naye.

7 Nao wakakwea baadhi ya wana wa Israeli, na wa makuhani, na wa Walawi, na waimbaji, na mabawabu, na Wanethini, ili kwenda Yerusalemu, katika mwaka wa saba wa mfalme Artashasta.

8 Naye Ezra akafika Yerusalemu mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa huyo mfalme.

9 Maana alianza kukwea kutoka Babeli siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akafika Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kama mkono mwema wa Mungu wake ulivyokuwa pamoja naye.

10 Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake kuitafuta sheria ya Bwana, na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli”.

Utaona mbeleni baada ya Ezra kuingia nchi ya Ahadi, alikuta kasoro nyingi watu tayari walikuwa wameshaanza kufanya machukizo ya kuoa wanawake wageni, kama alivyofanya Sulemani jambo lililosababisha Israeli kugawanyika, na Ezra kama Mwandishi aliijua vizuri Torati hivyo akawaonya na kuwasaidia Wana wa Israeli na kuwarejesha tena kwa Mungu wao.

Na kwa ushujaa wote huo Mungu alimuheshimu, hakuwa Nabii, hakuwa anaona maono, hakuwa mtu mkubwa sana, lakini kwa Moyo wake wa kuwasaidia ndugu zake na kuwarejesha kwenye Torati Mungu alimheshimu, mpaka leo hii tunazisoma habari zake. Hiyo yote ni kwasababu alikuwa msaada kwa wengine kama jina lake lilivyo EZRA Maana yake MSAADA. Hivyo ni vizuri ukakipita kitabu hichi mwenyewe utapata vitu vingi vipya usivyokuwa unavijua hapo kwanza.

Bwana akubariki. Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA ELOHIMU?

MATOWASHI NI WAKINA NANI?

KITABU CHA UZIMA.

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

MIHURI SABA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

Shalom, mtu wa Mungu karibu tujifunze maneno ya Mungu, ambayo ndio kweli pekee inayoweza kumfungua mtu moja kwa moja bila kubakisha chembe zozote za vifungo nyuma..

Leo kwa neema za Bwana tutamtazama mtu anayeitwa Nehemia, Jina lake limekuwa kubwa kutokana na kuwa tunakiona kitabu chake kikiwa miongoni mwa vitabu vitakatifu (BIBLIA), Lakini Nehemia kama tunavyomsoma hakuwa mtu wa maana sana tukizungumza kwa ngazi za kibiblia, hakuwa nabii, wala hakuzaliwa katika familia za kikuhani, Nehemia alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme, mhudumu aliyekuwa anayepanga vinywaji mezani pa mfalme.

Lakini leo hii tunaisoma bidii yake, na sio tu kuisoma bali pia tunaiona sehemu ya kazi yake kwa macho yetu, Ukienda pale Yerusalemu utakutana na watu wengi ikiwemo wayahudi na watu wa mataifa mbalimbali wakisimama mbele ya kipande cha ukuta, na kuomba dua zao mbele za Mungu usiku na mchana..Sasa ukuta ule ulijengwa na Nehemia miaka karibia 2500 iliyopita, na mpaka sasa upo.

Nehemia hakuwa mtu wa kuona maono, lakini ni mtu aliyejitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu zaidi hata ya manabii na watu wengine..Wakati mwingine aliifanya kazi ya Mungu akidhani kama Mungu vile hayupo karibu naye mpaka akawa anafikia hatua ya kusema Unikumbuke Ee Mungu wangu kwa mema yote niliyowafanyia watu hawa (Nehemia 5:19, 13:14, 13:22)..
Leo hii sisi ndio tunaojua ni jinsi gani Mungu amemkumbuka..Kumbukumbu lake linasomwa vizazi baada ya vizazi,

Hivyo hatutaenda sana kwa undani kuutazama ujenzi aliofanya lakini tutajifunza kitu kimoja kwake ambacho kitatufaa sisi hata katika mambo yetu ya kawaida tunayoyapitia kila siku..Ukisoma pale utaona mwanzoni kabisa Nehemia alipokuwa anafanya kazi yake ya kuhudumu mezani pa mfalme, baadhi ya ndugu zake walimletea taarifa kuwa Yerusalemu umebomolewa, na kuta zake zimetoketezwa na moto, hivyo hilo lilimuhuzunisha sana na kumfanya alie na kuomboleza kwa muda mrefu, mbele za Mungu na kufunga..


Ukichunguza pale utagundua Nehemia alikuwa katika hali ya uzuni na maombolezo kwa muda wa miezi minne, akimwomba Mungu ampe kibali kutoka kwa mfalme kwenda kuikarabati nyumba ya Mungu iliyokuwa Yerusalemu na mji, lakini cha ajabu ambacho ninataka ukione hapa, ni kuwa wakati wote huo Nehemia akiwa katika maombolezo, mfalme hakugundua kitu chochote kinachoendelea ndani ya Nehemia..Mpaka wakati ambapo Nehemia ameacha sasa kuhuzunika, anacheka, anamuhudumia mfalme, ndipo mfalme akaona kitu cha tofauti katika uso wa Nehemia..

Nehemia 2:1 “Ikawa katika mwezi wa Nisani, mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta, na divai imewekwa mbele yake, nikaishika ile divai, nikampa mfalme. NAMI MPAKA SASA SIKUWA NA HUZUNI MBELE YA MFALME WAKATI WO WOTE.

2 Basi mfalme akaniambia, Mbona umesikitika uso wako, nawe huna ugonjwa? Nini hii, isipokuwa ni huzuni ya moyo? Ndipo nikaogopa sana.

3 Nikamwambia mfalme, Mfalme na aishi milele; kwani uso wangu usiwe na huzuni, iwapo mji, ulio mahali pa makaburi ya baba zangu, unakaa ukiwa, na malango yake yameteketezwa kwa moto?

4 Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka kuniomba? Basi nikamwomba Mungu wa mbinguni.

5 Nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na ikiwa mimi, mtumishi wako, nimepata kibali machoni pako, tafadhali unipeleke mpaka Yuda, niuendee mji wa makaburi ya baba zangu, nipate kuujenga.”

Unaona? Ukiangalia utaona kile kitendo cha yeye kutokuonyesha dalili yoyote ya nje kuwa yupo katika maombolezo halafu mtu anamwambia yupo katika maombolezo ndicho kilichomwogopesha Nehemia, pengine alijiuliza kwanini wakati wote wa nyuma nikiwa katika huzuni inayoonekana mfalme hakugundua chochote iweje iwe leo?.Mungu tangu zamani huwa hategemei hisia za mtu kumsaidia kuleta majibu ya maombi yake..

Mungu hataki wakati mmoja tumlilie yeye, na wakati huo huo tumlilie mwanadamu, au wakati mmoja tumwonyeshe yeye hisia Fulani na wakati huo huo tumwonyeshe mwanadamu hisia hizo hizo, kwamfano unaweza ukawa unapitia shida Fulani, au unataka upandishe ngazi fulani kazini, au unamdai mtu na unafahamu kabisa mtu Fulani anaweza kukusaidia, na wewe ukafanya uamuzi wa busara kwenda kumwomba Mungu kwa kufunga, sasa ukianza kujionyesha tena kwa Yule mtu unashida Fulani, kwa vitendo Fulani Fulani ili akuone, nataka nikuambie Mungu atasubiri kwanza uache vitimbwi hivyo ndipo akusaidie,..Lakini ukitulia na kuishi kwa njia ya kuonyesha kama haupitii shida yoyote au huna haja ya chochote lakini ndani unapitia,..bali huku nyuma ni Mungu tu ndio unayemlilia kila siku, nataka nikuambie utauvuta muujiza wako haraka kuliko unavyodhani.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema,

Mathayo 6.16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.

17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Unaona? Mungu hapendi mambo yetu ya siri mtu mwingine ayajue, Embu jaribu kufikiria kama Nehemia angeonwa na mfalme wakati wa kuonesha huzuni zake mbele ya watu, ni wazi kuwa angedhani ni kwasababu ya kulia kwake ndio maana kaonewa huruma na mfalme, lakini siku alipobadilisha uso wake, ndipo alipomshangaa Mungu.
Na sisi tutumie kanuni hii ya Mungu ili tufanikiwe..Bwana akubariki sana.
Ikiwa bado maisha yako bado yapo mbali na wokovu, mlango wa neema bado upo wazi kwa ajili yako, nakushauri uingie sasa nawe uanze kuufurahia uzuri wa Mungu..Wewe mwenyewe unaona dunia inavyochosha, hakuna haya ya kueleza ulitazamia ingekupa amani moyoni mwako, lakini hiyo amani mpaka sasa huioni, Nataka nikuambie ni mmoja tu ndiye aliyeahidi kutoa AMANI ya kweli ambayo ulimwengu hautoi naye ni Yesu mwenyewe huipati kwa mwingine yeyote..

Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.”

Maran atha!


Mada zinazoendana:

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

NGUVU YA UPOTEVU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KISASI NI JUU YA BWANA.

Moja ya dhambi kuu inayopeleka wengi kuzimu ni kutokusamehe…Bwana alisema, msipowasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni naye hatawasamehe ninyi makosa yenu (Mathayo 6:15). Ikiwa na maana kuwa, unaweza ukaomba toba kuanzia asubuhi mpaka jioni, lakini ikawa ni bure mbele za Mungu endapo ukiwa ndani ya moyo wako hujamsamehe mtu Fulani aliyekukosea.

Maadamu tupo hapa duniani, hatutaachwa kukosewa, kila siku tutaudhiwa, tutakasirishwa, tutaumizwa n.k lakini hatuna budi kusamehe kutoka moyoni, huo ndio mtihani wetu.Kama hujamsamehe mtu aliyekutukana kipindi Fulani nyuma, fahamu kuwa Bwana hajakusamehe tusi ulilomtukana mtu Fulani huko nyuma, aidha kwa mdogo au kwa moyo. Kama hujamsamehe mtu aliyekuudhi huko nyuma fahamu kuwa Mungu hajakusamehe maudhi yako uliyomwudhi mtu mwingine huko nyuma…

Kama hujamsamehe mtu aliyekusengenya fahamu kuwa na wewe hujasamehewa dhambi uliyowahi kumsengenya mtu mwingine, na makosa mengine yote, kama hujamsamehe aliyekutendea tambua na ya kwako pia hayajasamehewa, hali kadhalika kama ulimsamehe mtu na baadaye ukarudia tena kuukumbuka uovu wake na kumwekea kinyongo, Mungu naye ataukumbuka uovu wako uliowahi kumfanyia mtu Fulani huko nyuma, na hivyo toba zako zote ulizowahi kuzifanya zikawa ni bure.…Maandiko yanasema hivyo (Mathayo 18:23-35).

Kadhalika biblia imetuonya juu ya kisasi. Kisasi ni kitendo cha kumrudishia uovu mtu aliye kutendea uovu. Mafundisho yoyote yanayohusiana na kumlipizia mtu kisasi ni mafundisho ya uongo, yanayopalilia roho ya kutokusamehe, na yanalenga kuwapeleka watu jehanamu. Hubiri lolote linalokufanya utoke na hasira dhidi ya adui yako, limetengenezwa na roho ya Adui, Hubiri lolote linalokuachia hamu kubwa ya mtu Fulani anayekuchukia, au aliyekuudhi, kufa, au kuteseka, au kupigwa ni hubiri la shetani…Hubiri lolote linalokuacha katika hali ya kumpania mtu Fulani aliyekudharau ni fundisho lililotengenezwa na yule adui shetani..Biblia inasema…


Mithali 20:22 “Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa”.


Waebrania 10:30 “Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake. 31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”


Warumi 12:19 “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana. 20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake. 21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema”

Roho wa Kristo anatupigania kwa namna isiyoweza kuonekana kwa macho, ukiona kuna mtu anakuchukia jua ni sehemu ndogo sana ya roho ya shetani inayojidhihirisha juu yako…, laiti ungefunuliwa macho katika ulimwengu wa roho uone ni maroho gani yanakuwinda usiku na mchana, na jinsi gani Mungu amekuepusha nayo, usingeona kama ndugu yako kukuchukia au kukusengenye ni Adui…Laiti ungeona ni kwa jinsi gani hata usiku wa leo ulikuwa umepaniwa maangamizi, na Mungu kaepusha huo mpango wa mapepo..usingeona mtu aliyekutukana kama ni Adui.

Hivyo leo hii kama ulikuwa una mpango wa kumlipizia mtu Fulani mabaya, uzike huo mpango leo na utaona Mungu atakavyokupa mema, utapata amani ambayo hujawahi kuipata na utaona mzigo Fulani mzito umeondoka ndani yako, huo mzigo utakaoona umeondoka ndio mzigo wa dhambi zako na wewe Mungu kaziondoa, tenga muda kumbuka ni wangapi hujawasamehe kwa moyo, ukishawapata tamka kuanzia leo umewasamehe, utaona kuna mzigo Fulani umeutua ndani ya moyo wako, hiyo hali ni konesha kuwa na wewe Kristo katua mzigo wako chini.
Bwana atusaidie katika jambo hili, tuweze kuishi Maisha ya msamaha na ya kujiepusha na visasi.

Bwana akubariki.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

Katika Marko 2:2-12, Kwanini Bwana Yesu alichukua hatua ya KUSAMEHE dhambi kwanza kabla ya kumponya yule kiwete?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

Swali ambalo ni wajibu wetu sote kulijua ni juu ya Roho saba za Mungu, kwamba zenyewe ni nini na zinatendaje kazi. Na pia ni muhimu kufahamu juu ya makanisa saba

JIBU: Tukisoma mandiko yanatuambia kuwa Mungu ni mmoja, agano la kale linatuthibitishia hilo, (Kumb 6:4), vile vile agano jipya linatuthibitishia hilo, tukisoma katika (Marko 12:29) pale Bwana Yesu alipofuatwa na Yule mwandishi na kuulizwa ni amri ipi iliyo ya kwanza alijibu..


“….Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; 30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.”

Hivyo maagano yote mawili yanathibitisha kuwa Mungu ni mmoja, lakini sasa kwanini tunamwona YESU kama Mungu, kwanini tunamwona Roho kama Mungu, tena tukiendelea kusoma tunaziona kuna Roho nyingine saba za Mungu, swali ni je! hawa wote wametokea wapi, ikiwa Mungu ni mmoja?.Hili ni moja ya swali lililoleta migawanyiko mikubwa sana sio tu katika ukristo, bali hata kwa wale wasioamini limewafanya wazidi kwenda mbali zaidi kwa kushindwa kuelewa utendaji kazi wa Mungu.

Tukiweza kujua kuwa kitu kinachoitwa Dhambi na kutengwa mbali na uso wa Mungu ndicho chanzo kilichopelekea tumwone Mungu katika taswira nyingi tofauti tofauti, tukilifahamu hilo basi hatutashindwa kumwelewa Mungu katika nafasi yake ya Uungu.. Na ameamua kufanya hivyo makusudi kwa lengo la kuturejesha sisi asingefanya hivyo leo hii tungekuwa makapi sisi. Laiti kama tusingeanguka katika dhambi, tungemwona Mungu na kuzungmza na Mungu kama yeye tu tusingejua kitu kingine cha ziada kumuhusu yeye, tabia zake zilivyo.

Kwamfano kulikuwa hakuna sababu ya Mungu kuutafuta mwili na kuiweka Roho yake mwenyewe ndani yake aje asulubiwe ili atupatanishe sisi na yeye kama tusingepotea katika dhambi, vile vile kulikuwa hakuna haja ya Roho Mtakatifu kuwa msaidizi wetu kama tungekuwa tunazungumza na Mungu uso kwa uso kama ilivyokuwa pale Edeni Adamu alipokuwa anazungumza na Mungu..

Ni sawa tu ni kifaa kinachoitwa simu, kama sio suala la umbali kati ya mtu mmoja na mwingine, simu isingehitajika katika jamii, kusingekuwa na haja ya wewe kuisikia sauti yangu kwenye kifaa kinachoitwa simu..Lakini je! Fikiria pia siku ile uliposikia mimi ninazungumza ndani ya kifaa kile, je ulisema nimegawanyika?, na kuwa wawili, kwamba mimi unayeniona tukizungumza uso kwa uso ni tofauti na Yule unayenisikia kwenye kifaa-simu? Ukweli ni kuwa utasema ni kifaa tu lakini mimi ni Yule Yule..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu kuja kwake duniani, ..yule ni Mungu yule yule kauvaa mwili lakini sio MUNGU wa pili katika UUNGU, kama wengi wanavyodhani…YESU na Mungu BABA, sio Mtu na Mtu mwenzake, Ni Mungu yule Yule mmoja isipokuwa amekuja kwetu katika vazi lingine.
Kwa maelezo marefu ya kufahamu kwanini Yesu alikuja duniani, tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Vivyo hivyo na Roho wake Mtakatifu, Yule sio Nafsi ya Tatu katika uungu bali ni ofisi ya tatu ya Mungu Yule Yule mmoja katika hatua zake za kuturejesha sisi katika mstari wake wa ukamilifu..Kama tusingekuwa katika hali ya dhambi na kumsahau Mungu, basi hakukuwa na haja ya sisi kupewa msaidizi, lakini Mungu aliona ajitoe sehemu ya nafsi yake iliyo moja aje kwetu kama Roho Mtakatifu ili atukumbushe yale yote Bwana Yesu aliyotuagiza.(Yohana 14:26).

Vile vile Roho Mtakatifu alipoachiwa pale Pentekoste, hakuachiwa kwa mtu mmoja mmoja tu peke yake kama wengi wanavyodhani, bali aliachiwa pia na kwa kanisa kwa ujumla..Hivyo kulikuwa na makanisa tofauti tofauti kulingana na wakati na majira..Sasa Roho huyu huyu aliyetenda pia kazi tofauti tofauti kulingana na kanisa husika..Ndio yale makanisa saba tunayoyasoma katika kitabu cha ufunuo sura ya 2&3, ..


Ufunuo 1:4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;

makanisa saba

Sasa biblia inaposema Roho saba za Mungu nadhani utakuwa umeelewa kuwa hakuna tena Roho nyingine 7 zilizo mbele za Mungu, bali ni Roho Yule Yule mmoja akitenda kazi katika yale makanisa saba, Biblia inasema pia ndio macho 7 ya Mungu (Ufunuo 5:6), Na Taa 7 za moto (Ufunuo 4:5).
Kwa maelezo marefu juu ya nyakati saba za Kanisa,pia tutumie ujumbe inbox tukutumie somo lake..

Hivyo hizo zote ni hatua za Mungu za utendaji kazi lakini ni yeye Yule Yule, Mungu mmoja, hajagawanyika..


Lakini Swali lingine mtu anaweza kuuliza je! Tunafanya makosa kumwabudu YESU au Roho Mtakatifu? Jibu ni hapana, unapomwabudu Bwana YESU umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, Unapomwabudu Roho Umemwabudu Mungu Yule Yule mmoja, ni ofisi tu imebadilika, lakini Mungu ni Yule Yule umwabuduye..

Hivyo YESU ni Mungu mwenyewe katika mwili (1Timotheo 3:16), Roho Mtakatifu ni Mungu mwenyewe katika roho, vile vile zile Roho 7 za Mungu ndio Yule Yule Roho mmoja na ndio Mungu mwenyewe YEHOVA muumba wa mbingu na nchi, Hana mwanzo wala hana mwisho, ALFA NA OMEGA. Haleluya!

Je unampenda kwa moyo wako wote? Jibu unalo.


Ubarikiwe.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Washirikishe na wengine habari hizi

 


Mada zinazoendana:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MJUE SANA YESU KRISTO.

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Huyu Azazeli ni nani tunayemsoma katika(Walawi 16:8)

SWALI: Huyu AZAZELI ni nani? Kwa sababu ukisoma maandiko naye aikuwa anapewa kafara? (Walawi 16:8).



JIBU: Neno Azazeli linaonekana likitajwa mara moja tu katika kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 16, Azazeli sio mtu au kuhani bali ni mbuzi aliyetengwa kwa ajili ya upatanisho wa dhambi za Wana wa Israeli ndiye aliyejulikana kwa jina hilo, ambaye yeye hakuwa anachinjwa kwa ajili ya dhambi kama mbuzi wengine hapana bali yeye alikuwa anachukuliwa akiwa hai mpaka jangwani na kutelekezwa huko.


Maagizo hayo Mungu aliwapa wana wa Israeli, wayafanye katika siku ile kuu ya Upatanisho ambayo ilikuwa inafanyika mara moja tu kwa mwaka, tarehe 10 mwezi wa 7 wa kalenda ya Kiyahudi, wakati huo ndio ule Kuhani Mkuu anakwenda kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za wayahudi wote siku hiyo kila mtu alipaswa asifanye kazi yoyote, bali unatulia nyumbani kwake ukiitesa nafsi yake kwa dhambi zake.


Sasa katika siku hii Kuhani Mkuu kwanza anawajibika kufanya upatanisho kwanza kwa ajili ya nafsi yake yeye mwenyewe na ya watu wake (wa nyumbani kwake), kisha ndio aende kufanya upatanisho wa dhambi za watu wengine, vinginevyo atakufa. Sasa katika kufanya upatanisho wa wana wa Israeli aliagizwa atwae mbuzi wawili kutoka katika mkusanyiko wa Wayahudi kwa sadaka ya dhambi na kondoo mmoja mume kwa sadaka ya kuteketezwa (Walawi 16:5), baada ya hapo kuhani mkuu anasimama mbele ya hema na kupiga kura kati ya wale mbuzi wawili.

Walawi 16:7 “Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweka mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania.

8 Na Haruni atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya Bwana; na kura ya pili kwa ajili ya Azazeli.”

Akishamaliza mmoja anachukuliwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa dhambi za watu wote,
kisha damu yake inachukuliwa na kwenda kunyunyizwa katika hema ya kukutania na madhabahu, na yule wa pili hauliwi bali kuhani mkuu anamchukua na kuweka mikono yake yote miwili juu ya pembe za Yule mbuzi ambaye ndio anaitwa Azazeli kisha kuhani anaungama makosa yote na dhambi zote za wana wa Waisraeli walizozifanya juu ya mbuzi Yule,..baada ya hapo mbuzi huyo anakabidhiwa kwa mtu mmojawapo kisha anapelekwa jangwani mbali kabisa na makazi ya watu na kutelekezwa huko. Ndipo ouvu wa Israeli unafunikwa.


Walawi 16:21 “Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.

22 Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani.”


Ni picha kamili tunayoiona katika agano jipya, Kristo akiwa kama Azazeli wetu alichukua dhambi zetu na mashutumu yetu yote, akasulibiwa nje ya mji, alihesabiwa kuwa si Kitu kwa ajili yetu.. Na kwa kupitia yeye dhambi zetu zinaondolewa moja kwa moja, tofauti na mbuzi Yule ambaye ikifika mwakani anapaswa atolewe mwingine…Ni raha kiasi gani ukikombolewa na Kristo,.Ukisamehewa dhambi zako, umesamehewa milele. Haleluya.


Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

NAOMBA KUJUA WATAKAOENDA MBINGUNI JE! NI WENGI AU WACHACHE?

UNYAKUO.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

JIBU: Ndoto ni mfululizo wa picha na mawazo na hisia zinazokuja wakati mtu amelala, Na hizo zinakuja pasipo hiyari ya mtu, kwamba mtu hapangi au haamui ni nini cha kuota! zinakuwa zinajitengeneza zenyewe tu!..Na ndoto zinaweza kuathiriwa na shughuli zetu tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au yaliyokuwa yanatuzunguka kipindi kifupi nyuma (Mhubiri 5:3, Isaya 29:8),

Na kuna ndoto zinatokana na shetani na nyingine zinazotokana na Mungu (Mwanzo 28:12, 37:5-10).


Na Maono hayana tofauti sana na ndoto, Maono ni mawazo ya picha na hisia yanayokuja wakati mtu akiwa hajalala…Na haya vile vile hayaji kama atakavyo mtu, wala mtu haamui ni aina gani ya maono ayaone wala huwezi kuyavuta kama mtu anavyovuta usingizi…. anajikuta tu ghafla anaona kitu ambacho sio cha kawaida au cha kawaida, au unakuta anaona tukio Fulani kama vile anaota, na anaporudi anajikuta alikuwa hajalala, pengine alikuwa anatembea au amesimama au alikuwa anaongea na mtu na analikumbuka lile tukio aliloliona kwenye hilo ono.

Na maono yapo yanayotokana na shughuli nyingi, hususani watu ambao wana msongo mkubwa wa mawazo na walioathirika na matumizi ya madawa makali, kadhalika yapo yanayoletwa na shetani haya yanawatokea wengi ambao ni wachawi au wenye roho za mapepo..na yapo yanayoletwa na Mungu.

Tofauti na inavyoaminiwa na wengi kuwa ni lazima kila mtu aliyezaliwa mara ya pili aone maono ya kiMungu, ukweli ni kwamba sio lazima kila mtu aone maono, mtu anaweza akazaliwa mara ya pili na hadi anakufa akawa hajawahi kuona ono hata moja na akaenda mbinguni..Kwasababu suala la kuona maono au kutabiri hivyo ni vipawa vya Roho Mtakatifu, na anapanga nani ampe na nani asimpe, ambaye hajapewa basi atakuwa amepewa kipawa kingine cha kipekee tofauti na hicho, na aliyepewa atakuwa amenyimwa vipawa vingine vya Roho. Haiwezekani watu wote wafanane au wawe na karama zinazofanana na haiwezekani mtu mmoja akawa na karama zote yeye peke yake (1 Wakorintho 12:29-31).


Jambo la muhimu ni kuzaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya,(Wagalatia 6:15) na kuishi kulingana na Neno, kuona maono au kutabiri au kufundisha hivyo sio vipimo vya utakatifu au tiketi za kwenda mbinguni (Mathayo 7:22).


Bwana akubariki.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618

 
 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mana zinazoendana:

NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA.

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

NI TAMAA IPI HIYO HAWA ALIAMBIWA ITAKUWA KWA MUMEWE?

JE! ASKARI MAGEREZA AKIAMURIWA KUMNYONGA MTU ANATENDA DHAMBI?

 


Rudi Nyumbani:

Print this post

Tunaposema tuishi kwa Neno, Inamaanisha tuishi maisha ya namna gani?


JIBU: Kuishi kwa Neno ni sawa mtu aseme ishi Kwa sheria au katiba ya nchi.Sasa unaishije kwa sheria ya nchi?, kwanza ni lazima uzijue sheria zenyewe kisha uziishi bila kuzivunja kwa namna yeyote ile, sheria ya nchi inasema usiibe mali ya mwingine, usiue, usile rushwa, usifanye biashara isiyo halali n.k unapozitii hapo ni sawa na kusema unaishi kwa sheria za nchi.

Na maana ya pili ya kuishi kwa sheria za nchi ni kuitumia sheria hiyo hiyo kupata haki yako..Kwamfano mtu haruhusiwi kukutesa, kwasababu sheria inakataza hilo, hivyo unatumia sheria kumshitaki au kumwonya, mtu anayetaka kukudhulu haki yako, kukudhalilisha, kukutapeli, au kukuua, au kukuibia unatumia sheria hiyo hiyo kujilinda…Kwasababu usipoijua haki yako utaonewa.
Na kwenye Neno la Mungu ni hivyo hivyo, unaishi kwanza kwa kulitii Neno la Mungu, Neno linaposema usizini, unapaswa usizini, linaposema mwanamke avae mavazi ya kujisitiri unapaswa ujisitiri, usiabudu sanamu, mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, nguvu zako zote na akili zako zote na jirani yako kama nafsi yako..Yote hayo unapaswa uyatii bila shuruti, Na hapo utakuwa umeishi kwa Neno. Hiyo ni namna ya kwanza.


Namna ya pili pia unalitumia Neno hilo hilo kujilinda dhidi ya yule mwovu, na kudai haki yako… mwovu akija na kusema utakufa wewe unasema Neno linasema sitakufa bali nitaishi (Zaburi 118:17), akija tena na kusema hutapona wewe unasema Neno linasema “kwa kupigwa kwake sisi tumepona (Isaya 53:5)”, unapopita katika bonde la mauti na misukosuko na dhoruba unasema Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu n.k. hivyo tu!..Kwa kufanya hivyo utaishi na wala hakutakuwa na jambo lolote litakalokushinda hapa duniani.
Hiyo ndio maana ya kuishi kwa Neno.


Ubarikiwe!


Mada Nyinginezo:

BIBLIA INASEMA USIONGEZE WALA USIPUNGUZE NENO LA MUNGU, HUKO KUONGEZA NA KUPUNGUZA KUKOJE?

AYUBU ALIJARIBIWA KWA MUDA GANI?

WAPUNGA PEPO WANAOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NI WATU WA NAMNA GANI?

NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

NYOTA YA ASUBUHI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

JIBU: Vita vipo vya aina mbili, 1) Vita vya kuishindania Imani …na 2) Vita vya kuishindania Injili,

 Vita vya kuishindania Imani Tunasoma katika

Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.

4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.” 

Na hii ndio vita dhidi ya mafundisho potofu ambayo ambayo yanapindua imani zetu na dhidi ya dhambi ambayo inatenda kazi katika viungo vyetu …Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”.

Waebrania 12:4 “Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;”… 

Na kila mtu aliyezaliwa mara ya pili anapambana kwenye hii vita. 2. Aina ya pili ya Vita ni vita vya kuipigania injili, na hivi ndivyo Mtume Paulo alivyokuwa anavizungumziwa hapo katika hiyo 2 Timeotheo 4:7 , si vita vya kimwili bali ni vita katika safari yake ya kuhubiri injili, akipambana na majaribu na nguvu zote za yule mwovu katika kuwaleta watu kwa Kristo,

….. 2 Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo”; 

Kazi ya kuhubiri Injili, siku zote shetani haifurahii hata kidogo, atanyanyua vikwazo vingi, na kuleta majaribu mengi..hivyo kusababisha vita vikali vya mapambano visivyoisha, ndio maana utaona Mtume Paulo alipitia kufungwa magerezani, kuchapwa bakora, kupigwa mawe kusalitiwa na kukumbwa na kila hatari katika safari yake ya kuhubiri injili.…

2 Wakorintho 11:3 “……. mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.

24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.

25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”. 

Kwahiyo hapo aliposema amevipiga vita vizuri anamaanisha, “kuwa Ameishindania injili ipasavyo” hakuacha kuishindania kwasababu ya mateso amevumilia na kuvuta wengi kwa Kristo, na ndio maana juu kidogo mstari wa 5 utaona anamwambia Timotheo naye ashindanie Injili vivyo hivyo. Na kila mtu ambaye atakwenda kuhubiri Injili ni lazima akutane na hivyo vita na lazima apambane, na kushinda na kuhakikisha kwa gharama yoyote, anakwenda kuzivua roho za watu..Bwana Yesu alisema

 Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”. 

2) Nitailindaje imani maana mimi nahitaji kulindwa na Mungu.

Ni vipi mkristo wa leo atailea na kuilinda imani?Utailinda Imani, kwa kuishika Imani…Na unaishika Imani kwa kukaa na kudumu katika Neno la Mungu..kila siku ukihakiki ni lipi limpendezalo Bwana,(Waefeso 5:10) na kujiepusha na Ulimwengu…Na jukumu la kuilinda Imani ni la mwanadamu si la Mungu, sisi ndio tunajukumu la kushika kile tulichonacho asije mtu akaitwa taji yetu Biblia inasema hivyo…

soma Ufunuo 3:11 na 1 Wakorintho 10:12. 3).je! kunao Mwendo wa kuumaliza, ni upi? Maandishi haya yamekua maarufu sana kwa mazishi, nisaidie tafadhali.Mwendo unaozungumziwa hapo, ni mwendo wa riadha, Safari yetu ya kwenda mbinguni inafananishwa na mashindano ya kukimbia mbio ndefu…tunapompa Kristo Maisha yetu ndio tunaanza mbio, na tunapoondoka duniani ndio tunakuwa tumeumaliza mwendo, kwahiyo hapo Mtume Paulo aliposema Mwendo ameumaliza, alikuwa yupo karibu sana na wakati wa kufariki kwake, Roho Mtakatifu alimshuhudia kuwa muda wake wa kuishi uliobakia sio mwingi…

Ukisoma juu kidogo mstari wa 6, utaona jambo hilo. Na maandishi haya yamekuwa yakiandikwa kwenye makaburi ya wapendwa wetu kuwafariji wafiwa, lakini kimsingi kama Maisha ya aliyekufa hayakuwa ya kikristo, wala hakupigana vita vyoyote vya kuitetea injili wala kushindana na dhambi, basi maneno hayo ni hewa tu! Hayana msaada wowote kwa aliyekufa. 

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

LULU YA THAMANI.

BEI YA UFALME WA MBINGUNI:

BARUA INAYOSOMWA

KISASI NI JUU YA BWANA.

BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini kabila la Dani na Efraimu hayaonekani yakiorodheshwa miongoni mwa yale makabila 12 ya Israeli katika Ufunuo 7?

SWALI: Yakobo aliyeitwa ISRAELI:Alikuwa na wana 12 (Benyamini,Yusufu,Yuda,Lawi,Asheri,Isakari,Gadi,DANI,Zabuloni,Naftali,Reubeni,&Simeoni) Ambao kabila za Taifa la Israeli ziliitwa kwa majina ya hao wana 12 wa Israeli. Wana wawili wa Yusufu, Benyamini na Manase nao pia wanatajwa kuwa miongoni mwa makabila ya ISRAEL..Hivyo wana wa watoto wakiume wa Yakobo (WALIOFICHWA KUTAJWA KAMA KABILA ZA ISRAEL.Mfano wa Manase & Efraimu) nao pia wakitajwa kama kabila za Israel, hilo ni ono tosha kwamba Nchi ya ISRAELI imeundwa na zaidi ya KABILA 12 hivi? (SWALI:Bwana Mungu anapoenda kuupachika mzeituni halisi kwenye shina lake kulingana na Warumi 11} tunafunuliwa watakaopata hii neema ya mzeituni halisi kupachikwa ni KABILA12 tu za ISRAELI tunazizoma kwenye Ufunuo7:

Swali hapo ni kwanini hapo KABILA LA DANI na lile la Efraimu Yamenyimwa hiyo Neema (hayajatajwa hapo) kwenye hiyo ufunuo mlango wa 7?


JIBU: Shalom ndugu.. Makabila ya Israeli ni 12 tu, Efraimu na Manase, walihesabiwa tu miongoni mwa makabila 12 kwa upendeleo wa Yusufu kutoka kwa baba yake lakini makabila halisi yaani watoto wa Yakobo ni 12 tu, ambao wanatambulika kuliunda taifa la Israeli…na ndio wale ambao majina yao yanaonekana katika milango ya kuta za mji ule Yerusalemu mpya..(Ufunuo 21:12)..

Hao ni wale watoto halisi 12 wa Yakobo, kama tu vile misingi ya mji ule ilivyokuwa 12 kufunua wale mitume 12 wa Bwana… Sasa ni kwanini Efraimu na Dani, hawaonekani pale kwenye Ufunuo 7…Sasa kitu cha kutazama hapo ni kwamba kiuhalisi ni kabila moja tu halipo pale, nalo ni kabila la DANI, lakini kabila la Efraimu lipo, ndio lile kabila la Yusufu lililotajwa pale…Ikumbukwe kuwa Yusufu aligawanyika mara 2, Manase na Efraimu, Haiwezekani liwepo kabila la Yusufu halafu tena liwepo kabila la manase na Efraimu kwa mpigo, hapo basi Yusufu angepaswa awe na watoto wengine tofuati na hao wawili ili atengeneze kabila lake mwenyewe, lakini kama wale ni watoto wake, basi Kabila lake lazima ligawanyike tu,..

Hivyo unapoona Biblia inasema Kabila la manase halafu tena inasema kabila Yusufu ujue basi alimaanisha kabila la manase na kabila la Efraimu, vile vile unapoona mahali biblia inasema Kabila la Yusufu halafu tena kabila la Efraimu, basi ujue linamaanisha kabila la Manase na kabila la Efraimu…

Soma (Hesabu 1:32, 13:11)   Lakini tukirudi kwenye kabila la Dani ambalo tunaona limeondolewa, biblia haijatoa sababu ya moja kwa moja kwanini limetolewa, lakini tukirudi nyuma, tunaweza tukahisi sababu moja, kumbuka Mungu huwa hapendezwi na mambo maovu hususani uabuduji sanamu,..Na ukirudi kwenye agano la kale utaona ni kabila moja tu la Dani ndio lililokuwa ovu kiasi cha kutokumwogopa Mungu hadi kwenda kunyanyua sanamu na kuiweka katika mji wao (soma Waamuzi 18)..Hilo likawa chukizo kufikia hatua ya Mungu kuwaondoa katika neema ya wokovu aliokusudia kuuleta baadaye juu ya Israeli,..Hiyo inaweza kuwa ni sababu mojawapo zinaweza kuwepo sababu nyingine tusizozijua, pengine hadi hapo Mungu atakapotufunulia..

Lakini katika ulimwengu ujao Dani atakuwepo, Efraimu na Manase watarudi chini ya viuno vya Baba yao Yusufu na kuhesabiwa kuwa kabila moja.  

Ubarikiwe sana.


 

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 7 & 11

UFUNUO: MLANGO WA 14

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

CHAKULA CHA ROHONI.

SWALI LA KUJIULIZA!

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!


Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni laana ipi hiyo Mungu alimaanisha ataipiga dunia nayo katika Malaki 4:5-6?

SWALI: Malaki 4: 5”Angalieni,nitawatumia Eliya nabii,kabla siku ile ya BWANA,iliyo kuu na ya kuogofya haijafika.Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao,na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ILI NISIJE NIKAIPIGA DUNIA KWA ‘Laana’…Hapo anamaanisha [LAANA kwa namna gani] au LAANA Ipi?.


JIBU: Mahali popote Mungu anapozungumzia kuipiga dunia, anamaanisha kwa mapigo kama yale yaliyotokea wakati wa Nuhu, na ule wakati wa Sodoma na Gomora,..

Kumbuka wakati ule wa Nuhu, watu walikuwa sio wa kujizuia na hiyo ikasababisha watu kujisahau kupindukia na hiyo yote ni kwasababu hakukuwa na manabii wa kutosha wa kuwaonya..Vile vile hata wakati wa utawala wa Mfalme ahabu, kama Eliya asingetumwa na Mungu kuwageuza watu mioyo iwaelekee Mungu, katika kipindi kile cha kilele cha maovu Israeli ambapo ibada za sanamu na miungu ilikuwa ni jambo la kawaida vikiongozwa na Yezebeli, walikuwa wamebakiwa na muda mchache sana kabla ya kuangamizwa kwao..Lakini kwasababu Mungu alilihurumia Taifa lake teule na viapo alivyomuapia Ibrahimu, basi alikuwa akiwatumia manabii wake wengi wawe wanawaonya mara kwa mara. 

Vivyo hivyo katika agano jipya, kama Mungu asingeachia Roho wake mtakatifu, na asingepeleka watumishi wake mitume na manabii kuhubiri duniani kote kuwaonya watu wamgeukie Mungu, dunia hii isingekuwepo mpaka leo hii..Tunaona tokea kipindi cha kanisa la kwanza Mungu amekuwa akiwatuma watumishi wake kwa Roho ile ile ya Eliya kuwarejesha watu wamegukie Mungu.. 

Hadi kanisa hili la mwisho la Laodikia tulilopo sasa tunaona aliwatuma watumishi wake wengi, akiwemo William Branham kwa ujumbe wa kuwarejesha watu wamgeukie Mungu..Na hata sasa bado anaendelea kuwatuma wengine wengi kwa huduma hiyo….. ikiwa utapenda kufahamu kuwa urefu juu ya huduma ya Eliya jinsi inavyotenda kazi katika agano jipya, nitumie ujumbe inbox nikutumie somo lake kwa urefu kwasababu hapa hatuwezi kuliandika lote.. Lakini ipo siku Injili hii ya kuonywa na kukumbushwa itakoma..Wala Mungu hataipeleka Roho yake tena juu ya watumishi wake kuigeuza mioyo ya watu imwelekee Mungu..Wakati huo ukifika basi ndio KIAMA chenyewe..

Hasira ya Mungu au LAANA ya Mungu itaakwenda kuachiliwa juu ya dunia nzima.. Kama Mtume Petro alivyoandika.. 

2 Petro 3:9 “Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?”.

Bwana akubariki.

HOME

Print this post