Shetani huwa ana kauli zake, za uongo ambazo hupenda kuwaaminisha watu, kuwa kuna mambo mwanadamu hawezi kuyafanya akiwa hapa duniani hata iweje.
Tukisoma habari ya Ayubu wakati ule shetani alipokwenda kumshitaka kwa Mungu.
Mungu alipomuuliza kuhusu mwenendo wake, majibu ya shetani yalikuwa ni kwamba Mungu amemzungushia wigo, kutunza alivyonavyo, Na kama atapotezewa alivyonavyo, basi atamkufuru Mungu waziwazi. Hivyo Mungu akaruhusu shetani amjaribu Ayubu, amchukulie alivyo navyo vyote, lakini uongo wa kwanza, ukashindwa, alipoona Ayubu anamtukuza Bwana katika misiba yake. Hiyo ni kuonyesha kuwa mwanadamu yoyote anaweza kuishi bila msukumo wa mali,wala mtu wala kitu chochote katika hii dunia.
Lakini baadaye tena, akaendelea mbele kuzungumza uongo mwingine, alipoona Ayubu bado yupo na Mungu, akamwambia Mungu, yote yanawezekana kwa mwanadamu kuvumilia, lakini hili la kuugusa mfupa wake,kumtesa, kamwe hawezi kuvumilia atakukufuru tu. Mimi ninawajua wanadamu uwezo huo hawana, nilishawafundisha pia huko duniani.
Ayubu 2:4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. 5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako. 6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake. 7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa. 8 Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni. 9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. 10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Ayubu 2:4 Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
5 Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako.
6 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake. 7 Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.
8 Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni. 9 Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.
10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.
Hilo nalo likashindikana. Kumbe mtu, hata kuupoteza uhai wake kwa ajili ya Kristo, linawezekana.
Ni nini Bwana anatufundisha kwa mawazo ya adui kwetu sisi ?
Leo hii ni rahisi sana kusikia, kauli kama, hakuna mtakatifu duniani! Ni rahisi kuona mtu anaanguka ovyo katika dhambi, na kutumia kisingizio kuwa yeye sio malaika. Utasikia kauli kama haiwezekani mtu kuacha vyote alivyonacho kwa ajili ya Kristo. Ndugu tambua kuwa hizo ni kauli za ibilisi ndani ya moyo wako. Adui anapenda kumshusha thamani mtu, kumweka kama kiumbe ambaye hawezi kujisimamia, hafundishiki, haaminiki.
Ni kweli mwanadamu kuwa na ukamilifu wa Mungu haiwezekani (Ndio sababu Yesu akaja kutukomboa), lakini kuna viwango Fulani Mungu anajua tunaweza kuvifikia, akalithibitisha hilo kwa Ayubu. Kama Ayubu ameweza kwanini wewe ushindwe, usijishushe thamani.
Neema haijaja kutuambia kuwa sisi hatuwezi, bali imekuja kutuwezesha zaidi kuwa wakamilifu mbele za Mungu, yaani pale Ayubu aliposhindwa sisi tunasaidiwa kwa hiyo, na kutufanya tupokelewe kikamilifu mbele za Mungu, hiyo ndio kazi ya Neema (Soma Tito 2:11-12).
Kamwe usiruhusu hayo maneno ya kushushwa thamani na ibilisi, kwamba wewe huwezi mpendeza Mungu, huwezi kuacha vyote kwa ajili yake. Yesu alisema tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu alivyomkamilifu. Tunachopaswa kufanya ni kuamini kuwa hilo linawezekana na kuonyesha bidii katika hilo kumpendeza yeye. Na neema ya Mungu itatusaidia kufikia kilele Hicho cha juu kabisa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).
ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.
Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)
Rudi Nyumbani
Print this post
Warumi 7:18 “Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa KUTAKA NATAKA, bali KUTENDA LILILO JEMA SIPATI. 19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo”.
Warumi 7:18 “Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa KUTAKA NATAKA, bali KUTENDA LILILO JEMA SIPATI.
19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo”.
Je na wewe ni miongoni mwa watu wanaosumbuliwa na utumwa wa namna hiyo?.. UNATAKA na kutamani lakini unajikuta HUPATI au HUWEZI au HUFANYI au HUPOKEI?.
> Unataka kumtumikia Mungu lakini unajikuta huwezi..
> Unataka kuwa msomaji wa Neno lakini unajikuta hufanikiwi.
> Unataka na kutamani kufanya mema na mazuri kwaajili ya Mungu wako lakini hufanikiwi n.k
Kama UMETAKA mambo mengi na huoni uelekeo wa kulipata, basi huwenda NJIA unayoitumia kutaka na kutafuta hayo mambo ina kasoro..
Hebu jaribu njia hii, ya kutaka mambo halafu uone kama hutapata uyatakayo,
Na njia hii si nyingine Zaidi ya ile aliyoitumia Danieli.
Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ILI KUTAKA kwa MAOMBI, NA DUA, PAMOJA NA KUFUNGA, NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU. 4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ILI KUTAKA kwa MAOMBI, NA DUA, PAMOJA NA KUFUNGA, NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU.
4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Umeona kanuni Danieli aliyoitumia??… HAKUTAKA mambo kwa kupiga ramli, au kwenda kwa waganga wa kienyeji, wala kwa kwenda Kuwadhulumu watu au kukorofishana na watu au kula rushwa, au kujipendekeza kwa watu bali KWA MAOMBI, NA DUA NA KUFUNGA NA KUVAA NGUO ZA MAGUNIA NA MAJIVU, na matokeo yake alipata alichokuwa anakitafuta..
Na sisi tunajifunza mambo hayo hayo…
> Tukitaka Amani nyumbani.. kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Amani katika ndoa.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Amani kazini.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Akili darasani.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Ulinzi na afya.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
> Tukitaka Ujazo wa Roho Mtakatifu.. Kanuni ni hiyo > Kufunga na Kuomba.
Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
Kama Bwana YESU alivyosema kuwa “kuna mambo hayawezekaniki, isipokuwa kwa kufunga na kuomba”
Wafilipi 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, KUTAKA KWENU na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema. 14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano”
Wafilipi 2:13 “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, KUTAKA KWENU na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano”
Bwana atusaidie.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
KANUNI JUU YA KANUNI.
NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.
Yafuatayo ni mambo saba (7) ya kuzingatia wakati wa Mfungo.
1.MAOMBI
Mfungo wowote ili uwe ni mfungo ni lazima uambatane na Maombi.. Mfungo usiokuwa na maombi ni sawasawa na bunduki isiyo na risasi.
Marko 9:28 “Hata alipoingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kwa faragha, Mbona sisi hatukuweza kumtoa? 29 Akawaambia, Namna hii haiwezi kutoka kwa neno lo lote, isipokuwa kwa kuomba”.
Marko 9:28 “Hata alipoingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kwa faragha, Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
29 Akawaambia, Namna hii haiwezi kutoka kwa neno lo lote, isipokuwa kwa kuomba”.
Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Kila siku utakayofunga hakikisha unaomba, (tena maombi ya masafa marefu, tofauti na siku nyingine).
2. KUWA MTULIVU.
Unapofunga usiwe mtu wa kuhangaika na kuzurura huku na kule, bali kuwa mtu wa faragha muda mwingi, wakati wa mfungo si wakati wa kuzurura kwenye makao ya watu, au vijiwe..kuwa mtulivu, tafuta maeno tulivu na omba.
3. ZUIA KINYWA.
Mfungo sio tu kujizuia kula na kunywa, bali pia kujizuia kuzungumza kupita kiasi…. Unapofunga si wakati wa kusema na kila mtu, si wakati wa kujiachia (hususani kwa watu wasio wa kiroho) bali ni wakati wa faragha wewe na Mungu wako (kwa kutafuta sauti ya Mungu kupitia maneno yake)
4. EPUKA MATENDO YA MWILI.
Kama ni mwanandoa jizuie kwa kiwango kikubwa au chote kukutana kimwili na mwenzi wako..Vile vile Kama unafanya shughuli fulani inayohusisha mwili wako, ipunguze kwa kiwango kikubwa..
5. PUNGUZA KIWANGO CHA KULA.
Mfungo sio kuhamisha mlo wa asubuhi na mchana na kuupeleka jioni..La! bali ni kuunyima mwili ili roho yako ije juu (inufaike).. Maana yake wakati wa kufungua (kufuturu) usile kiwango kikubwa cha chakula, kwa kufidia mlo wa asubuhi na mchana.. Ukifanya hivyo utakuwa hutendi dhambi, lakini mfungo wako unaweza usiwe na matokeo makubwa kama wa yule ajizuiaye kweli kweli.
6.USILE VYAKULA VITAMU-TAMU.
Wakati wa kufungua epuka kula vyakula vitamu tamu, hususani vile unavyovipenda sana, ambavyo vinakuburudisha sana.. “Kumbuka tena mfungo ni kuunyima mwili na si kuupendeza mwili”… Sasa unapoupa vile vitu ambavyo unavipenda sana, hapo bado kuna kaukasoro katika mfungo wako..
Danieli alikuwa ni mtu aliyejinyima vitu vitamu wakati wa mfungo… na hatimaye mfungo wake ukawa na matokeo makubwa.
Danieli 10:2 “Katika siku zile mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili. 3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.
Danieli 10:2 “Katika siku zile mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.
3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.
7. USIWE MTU WA KUJITANGAZA.
Mathayo 6:16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. 17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso; 18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Mathayo 6:16 “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.
17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;
18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.
Mfungo unapaswa uwe siri hususani kwa watu walio wa nje (yaani wasiohusiana na wewe).. Kwa ndugu yako wa karibu sana, au mke au mume au watoto, mfungo wako ni ngumu kuwa siri kwao, kwasababu unaishi nao katika maisha ya kila siku (hata usipowaambia watafahamu tu)..Hivyo unaweza kuwashirikisha ikiwa lengo lako si upokee utukufu kutoka kwao.
Vile vile kiongozi wako wa kiroho, au mpendwa mwenzako (wa Imani moja na wewe) unaweza kumshirikisha mfungo wako (ikiwa lengo lako si kupata utukufu kutoka kwake) bali kupokea hamasa au kumhamasisha (Hilo ni jambo jema).
Lakini kama lengo lako ni wewe uonekane kwao ili utukuzwe, basi mfungo huo unaweza usizae matunda yale mtu anayoyategemea..
Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?
Kwanini tunafunga na kuomba?
KWARESMA IPO KIMAANDIKO?
JUMATANO YA MAJIVU NI TENDO LA KIMAANDIKO?
REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.
SWALI: Neno ‘huisingizia sheria na kuihukumu sheria’ maana yake nini? (Yokobo 4:11)
Yakobo 4:11 Ndugu, msisingiziane; amsingiziaye ndugu yake, au kumhukumu ndugu yake, huisingizia sheria na kuihukumu sheria. Lakini ukiihukumu sheria, huwi mtenda sheria, bali umekuwa hakimu.
JIBU: Ili kuelewa vifungu hivyo Mtume Yakobo kwa uongozo wa Roho alikuwa na maana gani aliposema Mtu amsingiziaye ndugu yake au amuhukumuye ndugu yake huisingizia sheria na kuihukumu sheria, Tafakari mfano huu.
Raisi ya nchi amendea mahali Fulani kwa ajili ya shughuli zake za kimaendeleo, lakini katika kupita pita kwake akaona familia moja iliyo fukara sana, na alipotathimini tatizo nini akaona walikuwa wote ni walemavu hawawezi kufanya kazi kabisa, hivyo kwa huruma zake akaagiza wajengewe nyumba, wapewe na msaada wa chakula kutoka serikali kila mwezi, walipiwe na pia bili za maji na chakula kwa kipindi chote wawapo hai.
Lakini Yule raisi alipoondoka, mkuu wa mkoa wa eneo lile, akaenda kuitazama ile familia ikoje, badala ya kutekeleza agizo la mkuu wake, akaanza kuwashitaki na kusema hawa hawana ulemavu wa kuwafanya wasifanye kazi, wanajifanya tu wadhaifu, ni wavivu, wanaweza kuendesha maisha yao, hakuna haja ya kuwapa chochote, hivyo akaanza kuwaonea na kuwashutumu, na kuwanyima mahitaji yao kwa wakati, na kuwashurutisha wajitume.
Sasa Kimsingi mtu kama huyu, ni rahisi kudhani, anawaudhi na kuwashutumu tu wale maskini, Lakini kiuhalisia anamudhi na kumshitaki raisi aliyetoa amri ile kwamba walishwe. Kwa tabia hiyo ni kwamba anamshtaki raisi hafikirii vizuri, anatumia fedha za uma vibaya, anatafuta sifa kwa watu, ana maamuzi yasiyokuwa na maana, hata kama huyo mkuu wa mkoa hawazi hivyo, anampenda raisi wake, na anathamini mali zake, lakini kitendo tu cha kuwashutumu wale, ni sawa na anamshutumu aliyewafadhili.
Ndivyo ilivyo na katika kifungu hicho, Wewe kama mwamini, unapomsingizia ndugu yako, Maana yake unakwenda kinyume na sheria ya Kristo tuliyopewa ya kupendana, unapomhukumu ndugu yako unakwenda kinyume na sheria ya Kristo inayosema Usikuhukumu (Mathayo 7:1).
Hivyo unaihukumu hiyo sheria kwamba ina makosa, wakati Bwana aliiona ni bora, lakini wewe unakwenda kinyume na hiyo.
Hivyo sisi kama wana wa Mungu hatujaitwa tuwashutumu watu, tutafute kasoro ndani ya ndugu zetu, kana kwamba sisi, hatuna maboriti kwenye macho yetu, ila tumeitwa tuitende sheria, na kuonyana, na kuelekezana, na kujengana, katika upendo, lakini sio kutoa hukumu kwa wengine, kana kwamba sisi ni mahakimu.
Tumeagizwa tunapomwona ndugu yetu ameghafilika tumrejeshe kwa upendo, sio kwa mashutumu, hiyo ndio sheria ya Kristo.
Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
2 Mchukuliane mizigo na KUITIMIZA HIVYO SHERIA YA KRISTO. 3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
Je Yesu ni Mungu au Nabii?
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
JE! UMEYABATILISHA MAMBO YA KITOTO?
Jibu: Turejee..
Wakolosai 4:6 “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea MUNYU, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.
“Munyu” ni kiswahili kingine cha “chumvi”. Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia..
Hivyo hapo maandiko hayo yanaweza kusomeka hivi…
“Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea CHUMVI, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.
Sasa swali; Maneno yaliyokolea Munyu/chumvi ndio maneno gani?.
Kabla ya kuyaangalia haya maneno hebu tujifunze matumizi ya chumvi.
Mbali na kwamba chumvi ni kiungo cha kuongeza ladha ya chakula, lakini pia ilitumika kwaajili ya kuhifadhia vitu ili visiharibike.
Enzi za zamani hakukuwa na friji kama tulizo nazo sasa, hivyo kitu pekee kilichotumika kuhifadhia chakula ambacho hakijapikwa ilikuwa ni chumvi?.
Kwahiyo chakula kilichotiwa chumvi kilidumu muda mrefu, na kitu kingine chochote..
Soma zaidi kuhusu Agano la chumvi hapa》》Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Sasa tukirudi katika “maneno” ni hivyo hivyo… “maneno yaliyokolea chumvi/munyu” mbali na kwamba ni maneno yaliyokolea ladha za kiroho..Lakini pia ni “maneno yenye kidumu muda mrefu”…yasiyopita!
Ni maneno yenye kidumu si mengine zaidi ya yale yenye kutangaza habari za uzima wa milele.
Ni maneno yenye kutangaza tumaini lililopo ndani ya YESU..maneno yenye kumpa mtu hamasa ya kumtumikia Mungu ili awe na nafasi katika ule mji mtakatifu..
Ni maneno yote yaliyonenwa na YESU mwenyewe…
Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.
Lakini maneno yasiyo na munyu ni yale yote yenye kunia na kutukuza mambo ya duniani ambayo yapo leo na kesho hayapo..
Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; 14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.
Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;
14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.
Bwana atusaidie maneno yetu yakolee munyu daima.
IMANI YENYE MATENDO
Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?
HAMJAFAHAMU BADO?
JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.
Ipo hali ambayo tunapaswa tukutwe nayo wakati wa kuja kwake Bwana YESU…na endapo akitukuta tupo nje na hiyo hali basi hatutaenda naye, badala yake tutabaki na kukumbana na hukumu ya MUNGU.
Sasa “hali” hiyo ni ipi?..
Hebu tusome maandiko yafuatayo.
1 Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, WAKATI WA KUJA KWAKE BWANA WETU YESU KRISTO”.
Kumbe Bwana YESU atarudi tena!!!!….. na wakati atakaporudi anatazamia tuwe tumetakasika katika maeneo hayo matatu 1) NAFSI 2) ROHO na 3)MWILI.
Vinginevyo mambo hayo matatu yasipokuwa masafi wakati wa kuja kwake Bwana YESU basi kuna hatari kubwa sana.
1.NAFSI.
Ndani ya nafsi kuna maamuzi, hisia na mawazo.. Hivi vinapaswa viwe visafi daima.
Na vinakuwaje visafi?… Kwa kumpokea YESU, kusoma Neno na kuomba.
Usipokuwa mwombaji nafsi yako haiwezi kuwa safi utakuwa mtu wa hasira tu, mtu wa uchungu tu..usipokuwa msomaji wa Neno la Mungu kamwe nafsi yako haiwezi kustahimili majaribu na pia utakuwa mtu usiye na mwongozo n.k.
2.ROHO.
Ndani ya roho ya mtu kuna uzima, na ndio chumba pekee cha ibada ambacho kinaongozwa na Imani.
Roho ya mtu isipokuwa safi, mtu huyo hawezi kwenda na Bwana siku ya unyakuo…na hata maisha yake ya duniani hawezi kumwona Mungu.
3. MWILI.
Mwili ni vazi la roho ya mtu, na ndilo limejumuisha viungo vyote vya ndani na nje.
Na mwili unapaswa uwe safi (usafi wa kimatendo)..Mwili mchafu kibiblia sio ule wenye jasho au vumbi…mwili mchafu ni ule unaofanya uasherati na zinaa, ni ule unaojichua, ni ule unaotembezwa uchi barabarani, ni ule unaoshika fedha za wizi na utapeli.
Huo ndio mwili mchafu, ambao kama hautatakaswa wakati wa kuja kwake Bwana utampoteza mtu huyo.
Na mtu hautakasi mwili wake kwa kuoga na maji moto, au kwa kumeza vidonge vya matibabu au mitishamba…bali kwa kuacha matendo yote ya mwili yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-20.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Kwa hitimisho ni kwamba kila mtu lazima ajitakase na kuhifadhi utakaso wake ambao ndio tiketi ya kumwona Bwana siku atakaporudi.
Je umempokea Bwana YESU?…Kama bado unasubiri nini??… Na kama tayari umeshampokea je! umetakaswa nafso yako, roho yako na mwili wako?..
Kwa mwongozo wa maombi ya kujijenga kiroho juu ya mambo hayo matatu (nafsi, mwili na roho) basi wasiliana nasi inbox.
Maran atha!.
MCHE MWORORO.
KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.
Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?
(Masomo ya kanuni za kuomba).
Mathayo 9:38 “Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.
Maombi ni jambo kuu na la msingi sana.
Hapa biblia inasema TUOMBE (Bwana apeleke watenda kazi).
Kumbe Maombi ya kuomba uamsho wa watenda kazi ni muhumu!. Kwasababu hiyo basi ni lazima tujiwekee utaratibu wa mara kwa mara kuomba Bwana aongezee watenda kazi.
Na yafuatayo ni baadhi ya maeneno yanayohitaji watenda kazi zaidi.
1.KANISANI.
Hii ni sehemu ya kwanza inayohitaji watenda kazi. Waalimu wa madarasa ya jumapili wanahitajika zaidi ndani ya kanisa, halikadhalika waalimu wa watoto, pia watendakazi katika kuongoza sifa na maombi na wengine wengi.
Hivyo ni muhimu kutenga muda wa kutosha kumwomba BWANA anyanyue watenda kazi yeye anajua yupi anatafaa mahali fulani sisi kazi yetu ni kuzidi kumsihi Bwana awanyanyue wengi.
2. MASHULENI.
Shule kuanzia zile za awali (chekechea) mpaka zile za juu (vyuoni) panahitajika sana watenda kazi, watakaofanya kazi ya mavuno..
Hivyo ni muhimu watu wa Mungu kuomba ili Bwana anyanyue jeshi la watenda kazi (wahubiri) kwenye mashule.
Kwani mbali na mambo mazuri yanayopatikana mashuleni lakini.huko huko pia ndio kitovu cha watoto kujifunza tabia chafu na kupokea maroho ya mapepo.
Na wakati mwingine ni ngumu mtu wa nje kuwafikia na kuwahubiria, hivyo mimi na wewe tukisimama kumwomba Bwana anyanyue watenda kazi katikati yao, basi Bwana atatusikia na kunyanyua vijana miongoni mwao huko huko waliko ambao watawatengeneza wenzao au atawanyanyulia walimu miongoni mwa walimu wanaowafundisha na watawafundisha na kuwakuza kiroho.
3. MAHOSPITALINI.
Hii ni sehemu ya tatu inayohitaji watenda kazi. Vituo vingi vya afya vinategemea kupokea watumishi kutoka nje kwaajili ya maombi kwa wagonjwa…
Wakati mwingine jambo hili linakuwa ni gumu sana, kutokana ni vizuizi vya kiserikali na uchache wa watenda kazi…na hivyo wagonjwa wengi wanakufa katika dhambi na wengine kuonewa vikali na ibilisi na mapepo yake yachocheayo magonjwa.
Lakini tukisimama kuomba kwamba Bwana anyanyue watenda kazi basi, Bwana atasikia kwasababu ndiye aloyetuambia tuombe.
Na matokeo ya kuomba ni madaktari wengi kuokoka na manesi na wahudumu wa vituo hivyo vya afya na hivyo wagonjwa wengi wataombewa na kufunguliwa na kumpokea BWANA YESU, pasipo kusubiri watumishi kutoka nje.
4. SERIKALINI.
Hii ni sehemu ya nne inayohitaji watenda kazi wengi…kwani huko serikalini ikiwemo katika mabunge, wizara na mahakama, adui anadhulumu wengi na kuwapoteza wengi, na hiyo ni kutokana na upungufu wa watenda kazi.
Lakini tukisimama kuomba, Bwana YESU atasikia na kunyanyua watenda kazi ndani ya serikali..Watanyanyuka watu mfano wa akina Danieli na Yusufu ambao watahubiri na kufundisha na kukemea kazi za ibilisi katika mahakama, bunge na katika asasi zote za serikali.
5. MITAANI.
Hili ni eneo la tano linalohitaji watenda kazi wengi…Kwani katika mitaa ndiko watu wanakofanyia kazi, wanakokusanyika katika vigenge vya mizaha, au wanakofanyia mabaya.
Hivyo kunahitajika injili sana, ili watu waokolewe… na wakati mwingine inakuwa ni ngumu kufika kila mtaa kuhibiri, au watumishi wa Mungu kuzunguka kila mahali kuhubiri na kuombea watu.
Lakini kama tukisimama kumwomba BWANA anyanyue watenda huko basi kazi (katikati ya hao hao wahuni, au hao hao wanaofanya kazi haramu, au wanaoketi katika vijiwe vya mizaha) basi kazi ya injil itakuwa nyepesi sana na yenye matunda mengi.
Tutashangaa kuona wale waliokuwa walevi namba moja ndio wahubiri namba moja, wale waliokuwa makahaba namba moja ndio wainjilisti namba moja n.k
6. MITANDAONI
Hii ni sehemu ya sita na muhimu sana inayohitaji watenda kazi.
Kwani katika mitandao ndiko watu wanakojifunzia mambo yote maovu, ndani ya mitandao watu wanajifunza mauaji, kiburi, uasherati, uchawi, utapeli, wizi na mambo yote mabaya ambayo biblia inayataja kama malango ya kuzimu.
Na wanaotumia mitandao hiyo kuhubiri habari njema ni wachache ukikinganisha na wale wanaoitumia kusambaza maovu.
Lakini tukisimama na kumwomba Bwana awageuze watu na kuwafanya watenda kazi shambani mwake, tutaona mageuzi makubwa.
Kwani wale waliokuwa wanahamasisha wizi, uasherati, utapeli na uhuni ndio watakaokuwa vipaumbele kuitumia mitandao hiyo hiyo kumhubiri YESU na kusaidia wengi,..
Wale waliokuwa watangazaji watageuzwa na kutangaza habari njema, wale waliokuwa waigizaji wa tamthilia za mapenzi ya kishetani sasa wanatengeneza mafundisha ya kuwajenga watu kiroho n.k
Lakini ikiwa tutaomba kwa bidii sana.
Hayo ni meneo sita yanayohitaji watenda kazi, yapo na maeneo mengine mengi lakini haya sita ndio yenye vipaumbele zaidi.
Hivyo kama mtu uliyeokoka usiishie tu kuombea familia yako, au kazi zako au ndugu zako au kanisa lako..
Piga hatua zaidi kuombea ongezeko la watenda kazi katika shamba la Mungu, kwani maombi hayo ni ya muhimu na yenye thawabu nyingi.
Maran atha.
MAVUNO NI MENGI
MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
Fahamu Namna ya Kuomba.
VIACHENI VYOTE VIKUE HATA WAKATI WA MAVUNO.
Je ni malaika wawili au mmoja
Swali: Katika Luka 24:4-6, biblia inasema ni malaika wawili..lakini tukirudi katika Marko 16:5-6 tunasoma ni malaika mmoja. Je biblia inajichanganya, au mwandishi yupi yupo sahihi?.
Marko 16:5 “Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu”.
Ni kweli hapa biblia inasema ni malaika mmoja, tena ni kijana.
Lakini hebu twende kwenye Luka, tuanzie ule mstari wa 4 hadi wa 6.
Luka 24:4“Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta; 5 nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? 6 Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya”
Luka 24:4“Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta;
5 nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?
6 Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya”
Je ni kwamba biblia inajichanganya? Au kuna mwandishi ambaye hayupo sahihi?.
Jibu ni la! Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya kabisa isipokuwa tafakari zetu ndio zinajichanganya.
Sasa katika maandiko hayo hakuna mwandishi aliyekosea wala anayempiga mwenzake.
Waandishi wote wapo sahihi na malaika waliowatokea ni wanawake wale walikuwa ni wawili na si mmoja.
Isipokuwa malaika aliyesema na wanawake wale ni mmoja kati ya wale wawili na ndiye huyo aliyetajwa na Marko.
Tunajuaje kuwa ni malaika mmoja ndiye aliyekuwa anazungumza na mwingine amenyamaza?.
Tunafahamu kupitia mwandishi wa kitabu cha Luka ule mstari wa 5 unaosema…. “nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, HAO WALIWAAMBIA, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?….
Hapo anasema “Hao waliwaambia”…sasa kwa kauli hiyo isingewezekana wote waseme kwa pamoja maneno hayo kama maroboti…Ni wazi kuwa ni malaika mmoja ndiye aliyetoa hiyo kauli na hivyo ikawa ni sawa wote wamesema.
Na huyo mmoja aliyetoa hiyo kauli ndiye anayetajwa na Marko…lakini Luka anataja uwepo wa wote wawili.
Ili tuelewe vizuri tutafakari mfano huu… wanahabari wawili wanaripoti hotuba ya Raisi na wa kwanza akasema hivi…. “Raisi wa nchi ya Tanzania amezuia matumizi ya vifungashio vya plastiki”…
Na mwandishi mwingine wa nje aripoti hivi..”Watanzania wazuia matumizi ya vifungashio vya plastiki”.
Je waandishi hawa watakuwa waongo?…au je kuna mmoja atakuwa anampinga mwenzake?..
Jibu ni la! Wote watakuwa sahihi kwani kauli na Raisi ni kauli ya watazania wote…atakalosema Raisi ni sawa na watanzania wote wamesema.
Sawa sawa kabisa na hiyo mwandishi wa Luka…alitaja kauli ya ujumla ya malaika wote wawili na Marko akataja ya mmoja tu (yule aliyetoa kauli).
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?.
Kama bado unasubiri nini?..ule mwisho umekaribia sana na Bwana YESU amekaribia kurudi sana.
Ikiwa utahitaji msaada wa kumpokea Bwana YESU basi waweza wasiliana nasi na tutakuongoza sala ya kumkiri Bwana YESU baada ya wewe kumwamini.
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO
Forodhani ni mahali gani?
Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?
DANIELI: Mlango wa 11
SWALI: Naomba kufahamu maana ya unabii unaozungumzia taifa la Tiro (Isaya 23). Kwamba litafanya ukahaba na falme zote ulimwenguni kisha utajiri wake utakuwa wakfu kwa Bwana. Tafsiri yake ni nini?
Isaya 23:17-18 inasema..
[17]Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, BWANA ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia. 18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
[17]Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, BWANA ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia.
18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
JIBU: Ukianza kusoma toka mstari wa kwanza wa hiyo sura ya ishirini na tatu (23), utaona Mungu anazungumzia adhabu, aliyoitoa kwa hilo taifa la Tiro lililokuwa na utajiri na mali nyingi kutokana na biashara zake lilizofanya na dunia nzima. Hata kuyakosesha na mataifa mengine, kwa bidhaa zake. Na jambo hilo Mungu akalihesabu kama ni ukahaba, hivyo akalipiga na kuliangusha kabisa likawa si kitu tena kwa muda wa miaka sabini(70).
Ni mfano tu, mataifa yanayokosesha ulimwengu sasa, kwa kuuza bidhaa ambazo ni machukizo kwa Mungu, utakuta taifa linazalisha nguo za mitindo ya nusu uchi, na kuyauzia mataifa mengine, au linatengeneza sinema zenye maudhui za kizinzi na kuyasambazia mataifa mengine yaliyokuwa na maadili.. Huo ndio mfano wa ukahaba ambao taifa la Tiro lilikuwa linafanya.
Isaya 23:15
[15]Basi, itakuwa katika siku ile, Tiro utasahauliwa miaka sabini, kadiri ya siku za mfalme mmoja; hata mwisho wa miaka sabini, Tiro utakuwa kama vile ulivyo wimbo wa kahaba.
Lakini baadaye Mungu alilirudia tena, na kuruhusu lifanikiwe, kama pale mwanzo. Likajikusanyia tena utajiri mwingi sana kwa biashara zake.. Lakini Kwasababu halikutubu, kitabia Mungu akalipiga kwa namna nyingine kwa kuzuia utajiri wao wasiule au kwa lugha nyingine hazina zao zisitunzwe kwa maendeleo yao, Bali Bwana atazizuia zije kutumika kwa kazi yake yeye mwenyewe na watu wake.
Na unabii huo ulikuja kutimia..
ndio maana ya huo mstari wa 18, unaosema..
[18]Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa BWANA, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za BWANA, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
Hii ni kufunua nini?
Kufanikiwa kwake mwovu, kunatimiza makusudi mawili la kwanza ni aidha kwenda kujiangamiza mwenyewe (Mithali 1:32, Zab 92:7), au kumkusanyia mtu mwingine mwenye haki.
biblia inasema..
Mithali 28:8
[8]Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Watu wengi wanaofanikiwa isivyo halali,mara nyingi mali zao, hula wengine..Ndicho alichokifanya Mungu kwa taifa la Tiro.
Ni kutufundisha pia fedha na dhahabu ni mali ya Bwana. Yeye ana uwezo wa kuzuia na kuachilia, anauwezo wa kuwapa watu wake hazina za gizani ambazo hawajazisumbukia, kwa ajili ya kazi yake.
Hivyo kumbuka Bwana akufanikishapo, tembea na Kristo, kinyume na hapo, mambo hayo mawili yanaweza kukukuta, aidha mafanikio hayo yazidi kukuangamiza ufe uende kuzimu, au yaliwe na watu wengine kabisa wema usiowajua na kazi yako ikawa bure.
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Masomo mengine:
Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?
Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)
Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?
(Masomo maalumu kwa wahubiri).
Kama Mhubiri basi fahamu mambo haya manne..
2 Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki”.
Nataka tuone mambo haya manne (4), ambayo Neno la Mungu linafanya, ili tusikose shabaha katika utumishi wetu.
Hapo anasema “kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa MAFUNDISHO, na KUONYA na KUONGOZA na KUADIBISHA”
Na hakusema kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa “kuchekesha na kuburudisha na kuchangamsha na kusisimua”
Hebu tuangalie jambo moja baada ya lingine ambalo Neno la Mungu linafanya.
1. KUFUNDISHA.
Hapo Neno linasema “..lafaa kwa mafundisho”.. sasa mafundisho yanayozungumziwa hapa si yale ya jeografia au sayansi bali yale ya Uzima (yampayo mtu uzima wa roho yake).
Tito 2:1 “Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima”.
Mafundisho yenye uzima ni yale yote yamtoayo mtu katika mkondo wa dhambi, kwani dhambi ndio adui wa kwanza wa mtu aletaye mauti (Warumi 6:23).
Hivyo msingi wa mafundisho ya kila mhubiri ni lazima yategemee Neno la Mungu (yaani biblia).
2. KUWAONYA WATU MAKOSA YAO.
Kuna tofauti ya kuonya na kuhukumu.
Kuhukumu ni kutoa tamko la mwisho la mwenendo wa mtu, jambo ambalo ni Mungu pekee ndiye awezaye kufanya..
Lakini “Kuonya” ni kumtahadharisha mtu kuhusiana na hatari iliyopo mbele yake kulingana na mwenendo anaoenda nao, ikiwa hatabadilika.
Kwamfano mtu anayeiba, ukimwambia aache wizi na ukamtahadharisha madhara yake kuwa yanaweza kumpelekea hata kifo (kuchomwa moto na watu)....hapo hujamhukumu bali umemwonya.
Na vivyo hivyo unapomtahadharisha mtu kuhusiana na madhara ya kuiba au dhambi/mwenendo mwingine wowote ulio mbaya kwamba ataenda kuchomwa kwenye moto wa milele kama asipobadilika hapo hujamhukumu bali umemwonya, na ndio kazi ya Neno la Mungu lenye pumzi ya uhai, ni kuwaonya watu makosa yao.
2 Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.
Na kuonya inapaswa iwe sehemu ya mahubiri kwa kila mhubiri ya kila siku..
Waebrania 3:13 “Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi”.
Wapo watu wasemao kuwa zisihubiriwe sana habari za hukumu ijayo kwani kwa kufanya hivyo ni kuhukumu na kuwatisha watu.
Ni kweli mambo yajayo yanatisha, lakini sasa yamewekwa wazi katika biblia pasipo vificho, sasa kama kwenye biblia imeyaweka wazi pasipo maficho kuna haja gani ya mhubiri kuyaficha??.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Soma tena Wagalatia 5:19-20 na 1Wakorintho 6:9 utaona mambo hayohayo.
Kwahiyo kama mhubiri Onya, karipia na kemea.
3. KUONGOZA.
Biblia inasema Neno la Mungu ni mwanga na taa ya njia yetu (Zaburi 119:105).
Kama vile taa inavyoweza kumwongoza mtu katika giza nene vivyo hivyo na Neno la Mungu.
Mtu anaposikia Neno la Mungu na kulitii basi lile Neno linakuwa ni dira ya maisha yako, na mwongozo sahihi wa namna ya kuishi.
Kwasababu ndani ya biblia kuna mwongozo sahihi wa namna ya kuishi duniani, ( kiroho na kimwili)..
Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?
Kwa kutii, akilifuata neno lako”
4. KUADIBISHA.
Kuadibisha maana yake ni kumfanyaa mtu awe na adabu.
Ili mtu awe na adabu katika mwenendo ni sharti apokee Neno la Mungu lenye uzima, na ni lazima kila mtu aliyempokea Bwana YESU awe na adabu.
Warumi 13:12 “Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru. 13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”.
Warumi 13:12 “Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”.
1 Wathesalonike 4:12 “…mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote”.
Bwana atusaidie tuyafanye hayo na zaidi ya hayo, tuwapo katika kufundisha au kuhubiri, vile vile tuadibike, na kuonyeka, na kufundishika na kuongozeka tusikiapo Neno la MUNGU.
Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)
Adabu ni nini biblia?
HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.
MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.
MAFUNDISHO YA NDOA.