Category Archive Mafundisho

Thenashara ni nini? (Marko3:16)

Thenashara ni neno la kiebrania linalomaanisha namba “kumi na mbili” (12). Kwahiyo badala ya kusema watu 12, ni sahihi kabisa kusema “watu Thenashara”, au badala ya kusema “miezi 12” ni sahihi kusema “miezi Thenashara”…badala ya kusema makabila 12 ni sawa na kusema “Makabila thenashara” n.k

Biblia imelitumia Neno hilo Thenashara kuwakilisha wale Wanafunzi 12 wa Bwana Yesu, ambao baadaye waliitwa Mitume.

Marko 3:16  “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17  na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;

18  na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,

19  na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani”

Na ni kwanini wanafunzi hawa 12, watenganishwe kwa kuitwa hivyo Thenashara?.. Ni kwasababu Bwana Yesu alikuwa anao wanafunzi wengine wengi zaidi ya 70,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.”

 hivyo ili kuwatofautisha hawa wanafunzi 70 na wale 12 aliowateua kwanza kndio likatumika hilo neno “Thenashara”

Unaweza kulisoma neno hilo pia katika Mathayo 26:14-16, Marko 4:10, Marko 9:35, na Yohana 20:24

Je umefanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu? kwa kutubu dhambi zako zote, na kumaanisha kuziacha na vile vile kuchukua msalaba wako na kumfuata yeye?

Luka 14:27  “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Wahuni ni watu gani katika biblia?

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Jibu: Kutoka 40:20 “Akautwaa ule ushuhuda, akautia ndani ya sanduku, akaiweka miti ya kuchukulia juu ya sanduku, akakiweka kiti cha rehema juu ya sanduku”.

Kiti cha Rehema kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano hakikuwa “kiti” kama viti hivi tuvijuavyo, vyenye miguu minne, na vyenye nafasi ya Mtu kuketi.. Bali neno “kiti” kama lilivyotumika hapo limemaanisha “Nafasi ya wazi”.

Kwahiyo juu ya sanduku la Agano hakukuwa na Kitu Fulani mfano wa “Stuli” juu yake, hapana! bali palikuwa na nafasi wazi ambayo ndiyo iliyoitwa “kiti cha rehema”. Nafasi hiyo ilikuwa ipo katikati ya wale Makerubi wawili wa dhahabu ambao walikuwa wanatazamana, na mbawa zao kukutana kwa juu na kuifunika hiyo sehemu ya wazi (yaani kiti cha rehema).

Nafasi hiyo haikuwa kubwa sana, na pia ilikuwa ni sehemu ya mfuniko wa Sanduku zima (maana yake wale Makerubi wawili pamoja na kile kiti cha rehema vilikuwa vimeungana, na kwa pamoja kufanya mfuniko wa sanduku), na ndani ya sanduku kulikuwa na Mana, zile Mbao za mawe zenye amri kumi pamoja na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka. (Tazama picha juu).

Hivyo ulipofika muda wa Upatanisho, Kuhani Mkuu aliingia na damu Ng’ombe na kwenda kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema mara saba, na damu hiyo inakuwa ni upatanisho kwa wana wa Israeli, dhidi ya dhambi zao.

Walawi 16: 14 “Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na kuinyunyiza kwa kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba”.

Katika Agano la kale, Israeli walikitazama hicho kiti cha Rehema kama kitovu chao cha kwenda kupata msamaha, kupitia kuhani mkuu wao aliyeteuliwa kwa wakati huo.

Lakini kiti hicho cha rehema kilikuwa na mapungufu yake, kwasababu watu hawakuwa wanapata msamaha wa dhambi, bali dhambi zao zilikuwa zinafunikwa tu!, na kulikuwa na kumbukumbu la dhambi kila mwaka….kwamaana damu za Ng’ombe na Kondoo haziwezi kuondoa dhambi za mtu, vile vile Makuhani wa kibinadamu ambao nao pia wamejaa kasoro hawawezi kuwapatanisha wanadamu na Mungu, kwasababu wao pia ni wakosaji!.. Na pia kiti cha rehema ambacho kipo duniani, kilichotengenezwa na mikono ya wanadamu hakiwezi kufanya utakaso mkamilifu wa dhambi, kwasababu na chenyewe kimetengenezwa na mikono ya watu wenye dhambi..

Hivyo ni lazima kiihitajike kiti kingine cha Rehema kilicho kikamilifu ambacho hakijatengenezwa na mikono ya wanadamu, na vile vile ni lazima ipatikane damu kamilifu ya Mwanadamu asiye na kasoro, na hali kadhalika ni lazima apatikane kuhani Mkuu ambaye hana dhambi..Ndipo UTAKASO na UPATANISHO WA MWANADAMU UWE KAMILI.

Na kiti hicho cha Rehema kipo Mbinguni sasa, na kuhani Mkuu mkamilifu tayari tumepewa, ambaye si mwingine zaidi ya YESU, na damu kamilifu isiyo na kasoro imeshamwagwa kwaajili yetu, na damu hiyo si NYINGINE ZAIDI YA DAMU YA YESU. Hivyo Msamaha mkamilifu unapatikana sasa, na upatanisho mkamilifu unapatikana sasa kupitia Damu ya YESU, kwa kila aaminiye.

Waebrania 9:11  “Lakini Kristo akiisha kuja, ALIYE KUHANI MKUU wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa HEMA ILIYO KUBWA NA KAMILIFU ZAIDI, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu

12  wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali KWA DAMU YAKE MWENYEWE aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele”.

Je umemwamini Yesu na kuoshwa dhambi zako? Na kupata ukombozi mkamilifu?. Kama Bado unasubiri nini? Kiti cha Rehema kipo wazi sasa, lakini hakitakuwa hivyo siku zote, siku si nyingi baada ya unyakuo kupita mlango wa Neema utafungwa.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.

BABA UWASAMEHE

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Ukuta uliopakwa chokaa (Matendo23:3)?

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa kwanza..

Matendo 23:1 “Paulo akawakazia macho watu; wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.

2 Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.

3 Ndipo Paulo akamwambia, Mungu atakupiga wewe, UKUTA ULIOPAKWA CHOKAA. Wewe umeketi kunihukumu sawasawa na sheria, nawe unaamuru nipigwe kinyume cha sheria?”

Makaburi ya zamani sio kama ya zama hizi.. Haya ya wakati yanachimbwa kuelekea chini, na mtu anawekwa kwenye jeneza na kisha kufukiwa chini, lakini makaburi ya zamani hayakuwa hivyo.. Bali yalikuwa katika mfumo wa pango, ambayo linafunguliwa na watu wanawekwa ndani ya hayo mapango, na kisha kwa nje yanarembwa kwa kupakwa chokaa au rangi nyingine ya kuvutia.

Sasa Bwana Yesu alitumia mfano wa makaburi hayo yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje yanaonekana ni mazuri na kuvutia kana kwamba kuna kitu cha thamani ndani, kumbe ndani yake ni mifupa tu imejaa. Alitumia mfano huo kuwalinganisha na watu ambao kwa mwonekano wa nje wanaonekana wanafaa, wanaonekana na wacha Mungu, wanaonekana ni Watumishi wazuri, wanaonekana ni waimbaji wazuri, ni wakristo wa zuri, kumbe ndani yao ni MIFUPA TU!.. Ni wanafiki.. Bwana alisema Ole wa hao!!.

Mathayo 23;27 ‘Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na MAKABURI YALIYOPAKWA CHOKAA, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa MIFUPA YA WAFU, na uchafu wote.

28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani MMEJAA UNAFIKI NA MAASI’.

Hizo ndizo tabia walizokuwa nazo makuhani na mafarisayo wa wakati huo, walikuwa wamejaa unafiki ndani yao, na wana maasi mengi ingawa kwa nje wanasifiwa na watu wote!!.

Na katika siku hizi zetu tunazoishi, mambo haya haya yanajirudia katikati ya watu wa Mungu.. tunaonekana kwa nje ni wakristo wazuri, ni wahubiri wazuri, ni waimbaji wazuri…lakini ndani tuna unafiki uliopitiliza.. Ndani tumejaa viburi, uongo, kutokusamehe, vinyongo, visasi na kila aina ya uchafu!

Bwana Yesu atusaidie tusiwe kuta zilizopakwa chokaa, bali tuwe wakamilifu nje na ndani..

1Wathesalonike 5:22 “jitengeni na ubaya wa kila namna.

23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAKABURI YAKAFUNUKA; IKAINUKA MIILI MINGI YA WATAKATIFU WALIOLALA;

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

TIMAZI NI NINI

Na ulimi laini huvunja mfupa (Mithali 25:15)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Wakati ni “kipindi cha Muda” kwa kusudi Fulani, Kwamfano ukipanga kesho saa 7 mchana uende sokoni kununua bidhaa.. sasa huo muda wa “Saa 7 mchana” ndio unaoitwa “wakati wa kwenda kununua bidhaa”

Lakini “Majira” ni kipindi cha Muda ambacho ni cha “Msimu” Kwamfano Msimu wa mvua za masika hayo ni “majira ya masika”..msimu wa matunda ya maembe “hayo ni majira ya maembe”.. Msimu wa baridi, unaitwa “Majira ya baridi”.. Msimu wa joto huo unaitwa “majira ya joto”.

Mwanzo 8:22 “Muda nchi idumupo, MAJIRA YA KUPANDA, na mavuno, wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma”

Sulemani alizidi kuliweka hili vizuri kitabu cha Mhubiri..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna MAJIRA YAKE, Na WAKATI kwa kila kusudi chini ya mbingu. 

2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;

3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; 

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”

Unaweza kusoma zaidi juu ya Majira na Nyakati katika Mwanzo 7:21, Zaburi 1:3, Walawi 15:25,  na Ayubu 39:1.

Lakini pia yapo majira na nyakati katika makusudi ya Mungu. Na kusudi kuu ambalo ni muhimu kulijua majira yake ya kurudi kwa BWANA YESU MARA YA PILI!.. Hatuwezi kujua “Wakati” lakini “majira” ya kurudi kwake, tunaweza kuyajua… Ni kama vile hatuwezi kujua siku au wakati mvua itanyesha, lakini tunajua msimu, kuwa tukishaufikia huo msimu basi tunajua  siku yoyote mvua itaanza kunyesha.

Vile vile Bwana Yesu hakutoa wakati wa kurudi kwake, lakini alitoa “MAJIRA” Kwamba tuyafikiapo hayo majira basi tutajua kuwa WAKATI wowote atatokea mawinguni.

Marko 13:32 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.

33  Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui WAKATI ule utakapokuwapo”

Sasa Majira ya kurudi kwake ni yapi, ambayo tukiyatazama tutajua kuwa yupo mlangoni?.

Si mengine zaidi ya yale tunayoyasoma katika Mathayo 24, Luka 21 na Marko 13... kwamba kutatokea “Tauni” mahali na mahali, kutasikika tetesi za vita mahali na mahali, kutatokea na magonjwa mfano wa Tauni mahali na mahali, vile vile kutatokea na manabii wengi wa uongo ambao watawadanganya wengi na upendo wa wengi utapoa na maasi yataongezeka.

Hivyo tukishaona hizo dalili basi tunajua kuwa tayari tumeingia katika MAJIRA YA KURUDI KWAKE…na kwamba wakati wowote atatokea mawinguni, na hivyo tunapaswa tuchukue tahadhari… Na majira yenyewe ndio haya tuliyopo mimi na wewe..

Ndugu yangu Yesu anarudi wakati wowote!!, na yeye mwenyewe alituonya tuwe macho!, tukeshe katika roho kila siku, ili siku ile isije ikatujia ghafla..

Lakini tukifumba macho yetu na kukataa kuyatazama haya majira na kuchukua tahadhari.. basi tutaangukia katika like kundi la wanafiki Bwana Yesu alilolitaja katika Luka 12:54-56 na siku ile itatujia ghafla na hatutapona.

Luka 12:54  “Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55  Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56  Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, BASI, KUWA HAMJUI KUTAMBUA MAJIRA HAYA?”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

KUOTA UNAENDESHA GARI.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Rudi nyumbani

Print this post

Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?

Swali: Hawa wadudu, tunaowasoma katika Yoeli 2:25  (Nzige,Parare, madumadu na tunutu) ni wadudu gani na wanabeba ujumbe gani kiroho?

Tusome,

Yoeli 2:25 “Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na NZIGE, NA PARARE, NA MADUMADU, NA TUNUTU, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu”.

Hizi ni jamii za wadudu waharibifu wanaokula mazao hususani ya nafaka!.(Tazama picha juu)

1. NZIGE.

Hii ni jamii ya Panzi, ambayo ndio jamii kubwa kimaumbile kuliko jamii zote za panzi, Nzige wanasifa ya kutembea kimakundi na wanahama kutoka ukanda mmoja kwenda mwingine, na wanapotua mahali wanaharibu mazao ndani ya muda mfupi sana. Sifa ya nzige ni kwamba hawana kiongozi kama walivyo wadudu wengine kama Nyuki au Mchwa. (Soma Mithali 30:27).

Mfano wa hao Nzige ni wale Wamisri walioletewa na Mungu, ambapo walitua na kula kila mmea uliopo juu ya uso wa nchi yote ya Misri kasome (Kutoka 10:12-15), Na pia jamii ya mfano wa Nzige ni wale waliotua katika sehemu ya ukanda wa Afrika mashariki, wajulikanao kama Nzige wa Jangwani.

Lakini Nzige wanatabia ya kula Matawi ya Nafaka na kubakisha mapengo mapengo na kisha kuondoka.

2. PARARE.

Parare ni jamii nyingine ya Panzi, ambayo yenyewe inakula sehemu zile Nzige (walizobakisha/walizosaza). Parare kimaumbile ni wadogo kuliko Nzige, na kimwonekano wanayo miiba katika Miguu.. Parare si waharibifu kama Nzige, ingawa kwa nafaka ambazo tayari zimeshaharibika basi wenyewe wanaongezea uharibifu kwa kula vile vilivyosalia.

3. MADUMADU.

Madumadu ni jamii ya Panzi wadogo, wale (wanaokaa katika Nyasi)..Hii ndio jamii ya panzi wadogo kuliko wote, na sifa yao kubwa ni kula sehemu za majani zilizo ndogo sana, ambazo Nzige wala Parare hawawezi kula.

4. TUNUTU.

Tunutu ni vimelea vidogo kabisa vya wadudu, ambavyo vipo kama minyoo. Wadudu wengi warukao kabla ya kufikia hatua ya kukomaa huwa wanapitia hii hatua, ambapo wanakuwa kama viminyoo vidogo ambayo huwa vinakula mabua au sehemu ya majani ambayo Nzige, Parare, au Madumadu hawawezi kula. (Tazama picha chini)

Sasa tukirudi katika hiyo Yoeli 2 kwanini Bwana awataje wadudu hao?

Ili tuelewe vizuri hebu tusome tena kuanzia mstari wa 1.

Yoeli 1:1 “Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.

 2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? 

3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.

 4 YALIYOSAZWA NA TUNUTU YAMELIWA NA NZIGE; NA YALIYOSAZWA NA NZIGE YAMELIWA NA PARARE; NA YALIYOSAZWA NA PARARE YAMELIWA NA MADUMADU

5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu”

Umeona hapo?.. Bwana anamwonesha Yoeli hali ya kimwili ya wana wa Israeli jinsi alivyowapiga kwa Hawa wadudu Nzige, Parare, Madumadu, na Tunutu kutokana na Makosa yao. (Ambapo janga hili lilitokea dhahiri kabisa katika Israeli kwa miaka kadhaa, wakaishiwa chakula mpaka sadaka za unga zikakoma kutolewa katika nyumba ya Mungu kutokana na upungufu wa chakula).

Sasa wadudu hawakuishia kuwa wa kimwili tu, bali waliendelea kuwa hadi wa kiroho.. Maana yake ni kwamba Bwana kawaletea Nzige katika roho, Parare katika roho, Madumadu katika roho, na Tunutu katika roho, na kuyaharibu maisha yao. Na hiyo ikasababisha maisha yao kupukutika hata vile vichache walivyobakiwa navyo pia vikapukutika kama vile madumadu wanavyokula hata vile vidogo kabisa visivyoonekana.

Maana yake ni kwamba Mungu aliyaharibu maisha yao hata hawakubakiwa na kitu.. aliwaletea mikosi, na maafa na hasara, na wakaishiwa kabisa..kwasababu walimwacha!.

Hiyo ikifunua kuwa Na sisi tukimwacha Mungu, basi atalituma jeshi hili kuyaharibu maisha yetu, Utajikuta unafanya kazi kweli unapata pesa nyingi au faida nyingi, lakini itakapoishia hutajua, utajikuta tu hujasalia na chochote, utajikuta mara hili limezuka mara lile.. Ukiona hali kama hiyo basi jua kuwa ni Mungu kalituma jeshi hilo la Nzige, parare, madumadu na tunutu katika roho kula kila kitu ulicho nacho, na hata kukufanya usibakiwe na chochote.

Hagai 1:5 “Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.

 6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.

 7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu”.

Hivyo kama hujaokoka!..Fahamu kuwa maisha yako ya kimwili na kiroho kila siku yatazidi kuharibika, lakini kama leo hii ukiamua kumgeukia Mwokozi Yesu, kwa kutubu na kumaanisha kugeuka na kuacha dhambi kwa matendo, basi Bwana Yesu mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu na zaidi ya yote, atairejesha ile miaka yote ambayo imeliwa na Parare na Nzige, na Madumadu sawasawa na Neno lake katika Yoeli 2:25

Yoeli 2:22 “Msiogope, enyi wanyama wa kondeni; maana malisho ya jangwani yanatoa miche, na huo mti unazaa matunda yake, mtini na mzabibu inatoa nguvu zake.

 23 Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza. 

24 Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta.

25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na NZIGE, NA PARARE, NA MADUMADU, NA TUNUTU, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.

 26 Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

Bwana Yesu atukuzwe daima. Karibu tena tuyasogelee maneno matukufu ya Mungu wetu Yehova; 

Maandiko yanasema hivi; 

Waefeso 2:1-2

[1]Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

[2]ambazo mliziendea zamani KWA KUIFUATA KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

Kumbe hii dunia ina “kawaida yake”..yaani kwa ufupi ina desturi yake ambayo imeshajizoesha tangu enzi na enzi, tangu Adamu alipoasi hata sasa, kuendana nayo.

Kwamfano leo ukienda nchi nyingi za magharibi au Asia kama vile Japan na Nepal, utakuta wanaume na wanawake sehemu za umma wanashea vyoo . Tofauti na huku kwetu, jambo hilo halikubaliwi kabisa na ni ajabu sana ukikutwa mtu unatumia choo cha jinsia tofauti.

Hivyo huku kwetu ni jambo lisilo na heshima lakini kwao ni “la kawaida”..ndio desturi yao.

Mataifa mengine kama Jamaika kuvuta bangi, ni haki kisheria lakini kwetu sisi, ni kosa..kwao ni “kawaida” kwetu sisi ni kosa la jinai..

Vivyo hivyo na hii dunia ina kawaida yake ambayo inakinzana na kanuni za ufalme wa mbinguni, Na sisi kama wakristo hatupaswi kuiiga, hata kidogo…japokuwa tutaonekana ni watu wa ajabu sana, kama mtume Petro alivyosema katika;

1 Petro 4:3-5

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

[4]MAMBO AMBAYO WAO HUONA KUWA NI AJABU YA NINYI KUTOKWENDA MBIO PAMOJA NAO katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.

[5]Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

Mwanamke mmoja alinifuata na kuniambia mwanaume kama huna mojawapo ya starehe hizi yaani; 1) Ushabiki wa mpira, 2) wanawake,  3) pombe.. Wewe sio mwanaume kamili, una mapungufu. Nikasema ni kweli kwasababu kawaida ya ulimwengu huu, inalazimisha watu wawe na tabia hizo.

Binti unaambiwa usipokuwa na boyfriend, usipotumia kidogo mkorogo, usipovaa visuruali na visketi vifupi vifupi utaitwa mama/mbibi.. Wala usishangae kwasababu kawaida ya ulimwengu huu ni lazima utaonekana hivyo.

Lakini sisi kama wapitaji, makao yetu yaliyo mbinguni wala sio hapa duniani, hatuna ruhusu ya kuifuata, haijalishi itaonekana ni njema mbele ya dunia nzima..Sisi tunaifuata ‘kawaida ya mbinguni’..ambayo inatufundisha kuishi maisha ya utakatifu na usafi, kama Mungu mwenyewe na malaika zake walivyo watakatifu.

Hatuna desturi ya kuzini kabla ya ndoa, hatuna desturi ya kutembea na vimini, na mavazi ya utupu barabarani, hatuna ruhusa ya kuzifurahia anasa za ulimwengu huu, miziki, disco, kamari, pombe.

Warumi 12:2

[2]WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Hivyo ndugu uliyeokoka, kamwe usitake kumpendeza mtu, ukafaraka na Mungu. Mambo mengi ya ulimwengu huu yamefaraka na Mungu..Huo ndio ukweli, Ukiupenda ulimwengu ukasema unampenda na Mungu pia hapo unajidanganya.

1 Yohana 2:15-17

[15]Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

[16]Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

[17]Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Chagua leo ni kawaida ipi, unasimama nayo..Je! ile ya mbinguni au ya duniani hii. Kamwe usijaribu kuwa hapo katikati, yaani vuguvugu..una hatari kubwa sana ya kutapikwa..kumchanganya Mungu na udunia, ni hatari kubwa sana.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

HAMA KUTOKA GIZANI

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

Rudi nyumbani

Print this post

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

1Timotheo 5:22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi”.

Hapa tunaona mtume Paulo, anampa Timotheo maagizo ya namna ya kuwa kiongozi bora (Askofu bora) wa makanisa la Mungu. Utaona anampa maagizo ya utaratibu wa kuwaandika wajane, kwamba ahakikishe wanaoandikwa ni wale walio wajane kweli kweli. (soma 1Timotheo 5:9-16).

Pia utaona anampa vigezo vya uongozi kwa viongozi wapya wa makanisa mapya, kwamba wanapaswa wawe wameshuhudiwa kuwa na sifa njema…ndipo awawekee Mikono!, lakini asiwe mwepesi wa kuwawekea mikono kwa haraka.

Na pia viongozi wa makanisa (yaani wachungaji, maaskofu na wote wanaosimama kama viongozi wa kanisa) basi wanapaswa wapewe heshima maradufu, maana yake Wakumbukwe katika riziki na mahitaji yao mara dufu zaidi ya wengine, kwasababu wanakesha kwaajili ya roho za watu, kuwaombea na kuwachunga na kufundisha.

1Timotheo 5:17  “Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

18  Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng’ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake”

Na zaidi sana asikubali Mashitaka ya Wazee kwa haraka, (Juu ya wachungaji, au mashemasi)..isipokuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.. kwamaana ibilisi anapenda kuwatumia watu kuzusha jambo Fulani la uongo juu ya kiongozi wa kanisa, lengo lake likiwa ni kuliharibu kundi hilo..

Kwahiyo hapa Mtume kwa uongozo wa Roho anamwonya Timotheo asiwe mwepesi kusikiliza au kuamini maneno yazungumzwayo au mashitaka yaletwayo dhidi ya viongozi wa makanisa.. Bali alichunguze jambo kwa makini mpaka atakapopata uthibitisho kamilifu kwa vinywa vya mashahidi wengi.

Lakini la mwisho kabisa Paulo anamwambia Timotheo kuwa ASIZISHIRIKI DHAMBI ZA WENGINE!.

1Timotheo 5:22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, WALA USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE. UJILINDE NAFSI YAKO UWE SAFI”.

SASA NINI MAANA YA KUZISHIRIKI DHAMBI ZA WENGINE?

Kwanza ni muhimu kufahamu hao “wengine” wanaotajwa hapo ni akina nani?.. Wengine wanaotajwa hapo sio watu wa mataifa (yaani ambao hawajaokoka), la! Bali wengine wanaotajwa hapo ni “watu walio ndani ya Kanisa”. Watenda dhambi hawapo tu Bar!, au kwenye madanguro..bali wapo wengi pia kanisani.

Sasa Mtu wa kanisani anapofanya dhambi na wewe ukaiona na kuifanya kama hiyo hiyo? Maana yake na “wewe umeishiriki ile dhambi”, Kwamfano unapomwona mtu kaingia kanisani kavaa Nusu tupu, au kavaa nguzo zinazobana au zisizo na maadili, na wewe ukaona na ukamwiga, siku inayofuata na wewe ukavaa kama yeye..basi hapo kibiblia umeshiriki dhambi za huyo mwingine, hata kama kanisa zima linafanya mambo yasiyofaa sisi tunapaswa kushiriki dhambi zao, Kwasababu kuna madhara makubwa sana ya kushiriki dhambi za wengine.

Vile vile inawezekana wewe ni Mwimbaji ndani ya kanisa, lakini kuna waimbaji wenzako matendo yao ni ya giza, maandiko yanatuonya tusishiriki dhambi zao, maana yake tusiwe kama wao..

Vile vile wewe kama ni kiongozi (Mchungaji, askofu, shemasi)..halafu ukamwona kiongozi mwingine anafanya mambo yaliyo kinyume na maandiko, aidha ni mla rushwa, au ni mwizi, au mzinzi, au mlevi na anafanya mambo mengine mabaya na wewe ukaiga ule ubaya au ukaufumbia macho..kibiblia umeshiriki dhambi zake huyo kiongozi.

Na hapa Mtume Paulo anamwonya Timotheo kuwa ajihadhari asije akashiriki dhambi za wengine, ajilinde nafsi yake awe safi.

SASA MADHARA YA KUSHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE NI NINI?

Unaposhiriki dhambi za mwingine, maana yake MAPIGO nayo mnashiriki sawasawa, na LAANA pia mtashiriki sawasawa, maana yake kama Mungu amemkusudia kumwangamiza kabisa mtu huyo kutokana na tabia yake ya wizi anaoufanya kila siku ndani ya Nyumba ya Mungu, na wewe ukamwiga kwakufanya mara moja moja tu.. basi mtashiriki kiwango cha adhabu sawa.. Wewe unayeiba mara moja moja na Yule anayeiba kila siku wote kiwango chenu cha adhabu kitafanana, kwahiyo utajikuta wewe unayefanya kidogo mnapata adhabu sawa na Yule anayefanya sana.

Ndio maana Paulo anamwonya Timotheo asizishiriki dhambi za wengine, bali ajilinde nafsi yake awe safi.. Na sisi hatuna budi kuzilinda nafsi zetu ziwe safi.. Na tujiepushe na dhambi za wengine.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).

Rudi nyumbani

Print this post

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Je Sipora, mke wa Musa alikuwa Mkushi mwenye ngozi nyeusi?, Kulingana na  Hesabu 12:1? Na ni kwanini Miriamu na Haruni wamkasirikie Musa kwa kumwoa mwanamke Mkushi?, na kama alikuwa Mkushi mbona maandiko sehemu nyingine yanasema Yethro baba yake Sipora alikuwa ni Mmidiani na sio Mkushi?.. Au je! Musa alikuwa na mke mwingine tofauti na Sipora?

Jibu: Hapana! Maandiko hayaonyeshi kuwa Musa alioa mwanamke mwingine zaidi ya Sipora.

Sasa ili tujue kama Sipora alikuwa Mkushi au hebu kwanza tusome mistari ifuatayo..

Hesabu 12:1 “Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.

 2 Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao. 

3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”

Sasa Kushi lilikuwa ni Taifa gani?

Kushi ni taifa lijulikanalo kama Ethiopia kwasasa, Taifa hili lipo kaskazini mwa nchi ya Kenya, na kusini-mashariki mwa nchi ya Sudani. Wenyeji wa Taifa la Kushi(Ethiopia) ni watu wenye ngozi nyeusi tangu zamani za biblia na hata sasa. Tunalithibitisha hilo katika Yeremia 13:23.

Yeremia 13:23 “Je! Mkushi aweza kuibadili ngozi yake, au chui madoa-doa yake? Kama aweza, ndipo na ninyi mwaweza kutenda mema, ninyi mliozoea kutenda mabaya”

Umeona?.. hapo inamtaja Mkushi pamoja na ngozi yake, kwamba haiwezi kubadilika.. Kwahiyo mpaka hapo tumeshajua ngozi ya Sipora ilikuwaje?.. kwamba ilikuwa ni ngozi ya Kikushi.

Sasa swali ni je! Kama alikuwa ni Mkushi, kwanini biblia iseme baba yake alikuwa ni Mmidiani, Taifa la mbali kabisa, lililopo Mashariki ya kati, tena lenye watu wenye ngozi ijulikanayo kama nyeupe?.. na zaidi sana hata Sipora mwenyewe Musa alimpatia akiwa huko huko Midiani na sio Kushi?.

Jibu ni kwamba Yethro, baba yake Sipora, alikuwa ni Mmidiani kwa kuzaliwa, lakini kwaasili hakuwa mmidiani bali alikuwa ni Mkushi.

Ni sawa na Mzungu,au Mchina, au Mhindi aliyezaliwa katika Taifa la Tanzania, akakulia Tanzania, akaishi na watanzania, akasoma shule za kitanzania, na  hata lugha ya Kiswahili ya kitanzania akawa anaiongea.. kwa utambulisho wake ataitwa mtanzania, na atapata haki zote za kiraia…lakini  kwa asili sio Mtanzania bali ni Mzungu, au Mchina au Mhindi.

Ndivyo alivyokuwa Yethro, baba yake Sipora, alikuwa ni Mkushi kwaasili lakini Mmidiani kiuraia..(au kwa lugha rahisi, ni kwamba alikuwa ni Mkushi ambaye hakuzaliwa Kushi bali Midiani).

Ni sawa na Musa kipindi anakutana na hao mabinti wa Yethro, walikwenda kumtaja mbele ya baba yao kama Mmisri, lakini kiuhalisia Musa hakuwa Mmisri, bali mwebrania… Hivyo walimwita Mmisri kwasababu huenda aliwaambia katokea Misri.. Jambo ambalo ni kweli, Musa alikuwa ni Mmisri, kwa kuzaliwa, na kiuraia lakini hakuwa mwenye asili ya waMisri.

Kutoka 2:15 “Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani; akaketi karibu na kisima.

 16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao. 

17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao.

 18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?

 19 Wakasema, MMISRI MMOJA ALITUOKOA KATIKA MIKONO YA WACHUNGAJI, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi. 

20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula.

 21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora.

 22 Huyo akamzalia mwana, akamwita jina lake Gershomu, maana alisema, Nimekuwa mgeni katika nchi ya ugeni”

Swali lingine; Ni kwanini Miriamu na Haruni,  wakamkasirikie Musa kwasababu ya Mwanamke, Mkushi aliyemwoa?.. Je ni kwasababu alikuwa mweusi? Na ngozi nyeusi imelaaniwa?.

Jibu ni La!.. Hawakumkasirikia Musa kwasababu ya Rangi ya mke wake!..kwamba alikuwa mweusi na wao hawaipendi ngozi nyeusi,… la! Hiyo haikuwa sababu….

Sababu iliyowafanya wakasirike, ni kwasababu Yule alikuwa ni mwanamke wa kimataifa…

Maana yake ni kwamba hata kama asingekuwa Mkushi, lakini ni Mmisri, bado wangemkasirikia… vivyo hivyo hata kama angekuwa ni mzungu Yule mwenye uso mweupe kuliko wote, bado Miriamu na Haruni wangenung’unika.. kwasababu wayahudi na mataifa hawachangamani(kuoana).. Na mataifa walikuwa ni watu wote, nje na Taifa la Israeli.

Sasa swali la mwisho.. Kwanini Musa amwoe mwanamke wa kimataifa, na ilihali anajua kabisa haitakiwi kuwa hivyo?

Musa alimpata Sipora kabla ya sheria. Na ilipokuja sheria kuwa si ruhusa wao kuoa wanawake wa kimataifa, tayari Musa alikuwa na Sipora, hivyo asingeweza kumwacha!!!… na kipindi Mungu anatoa hiyo sheria ya kutooa wanawake wa kimataifa, ndio hicho hicho kipindi ambacho Musa na Haruni walinyanyuka kumlaumu. Kabla ya hapo utaona hawakuongea chochote.

Ni nini tunajifunza hapo?

Kwanza tunajifunza kuwa biblia haijichanganyi ni fahamu zetu ndizo zinazojichanganya.. Pili tunajifunza kuwa si sawa kumwacha mke wako baada ya wewe kuokoka, hata kama huyo mwanamke ni mpagani kiasi gani, wala si sawa kumwacha mume wako baada ya wewe kuokoka hata kama huyo mwanaume ni mpagani kiasi gani.. Ndicho biblia inachotufunza pia katika…

1Wakorintho 7:12  “Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13  Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14  Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu”

Lakini hiyo pia haitupi ruhusa kuoa wanawake wa kipagani, ikiwa tumeshaokoka tayari na tunataka kuoa, vile vile haitoi ruhusa kuolewa na mwanaume wa kipagani kama bado hujaolewa na unataka kuoelewa..

Kama umeshaokoka, na umesimama na  unataka kuoa/kuolewa.. ni sharti uolewe au uoe mtu mwenye imani moja na wewe, Bwana mmoja, roho mmoja, na Ubatizo mmoja.  Ukienda kutafuta binti wa kidunia na kumwoa hapo utakuwa umejifunga nira na wasioamini, jinsi isivyo sawa(2Wakorintho 6:14)..na unafanya machukizo yale yale walioyafanya watu wa kipindi cha Nuhu, yaliyowasababishia kuangamizwa kwa gharika (kwani wana wa Mungu waliowaona binti za wanadamu, wakawatamani na kuwaoa).

Hizi ni siku za Mwisho, kama hujampokea Yesu, fahamu kuwa hata uwe na maarifa kiasi gani, bado utapotea tu!, hivyo wokovu ni lazima!, kama unapenda maisha.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Midiani ni nchi gani kwasasa?.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Rudi nyumbani

Print this post

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe karibu tuyatafakari maneno ya uzima.

Neno la Mungu linasema…

1Samweli 15:22 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, KUTII ni bora kuliko dhabihu, Na KUSIKIA kuliko mafuta ya beberu.

23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; KWA KUWA UMELIKATAA NENO LA BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Ni vizuri kumtolea Bwana, tena ni moja ya maagizo yake ambayo tukiyatenda kwa hiari yetu wenyewe basi tutapata thawabu nyingi. Lakini ni vizuri pia kujua jambo moja kuwa Mungu wa Mbingu na nchi si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji kitu kutoka kwetu.

 Zaidi sana vyote tunavyomtolea yeye kama sadaka, vinaenda kutumika kwaajili ya watumishi wake na huduma alizowapa.. lakini yeye mwenyewe hakuna chochote anachokipokea.  Kwasababu yeye hahitaji kupokea chochote kutoka kwetu, kwamaana vitu vyote vinatoka kwake.

Kwahiyo kama fedha zetu haziendi mbinguni aliko yeye, wala matoleo yetu mengine hayapai mbinguni kumfikia, maana yake ni kwamba lipo jambo lingine ambalo ni muhimu sana kwake kupokea kutoka kwetu, Zaidi ya sadaka na matoleo tunayomtolea. Na jambo lenyewe si lingine Zaidi ya KULITII NENO LAKE.

Bwana anataka mioyo ya kutii tunapolisikia NENO LAKE.. Hiyo ndiyo dhabihu na sadaka anayoikubali kuliko zote..

Isaya 66:1 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?

2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, ATETEMEKAYE ASIKIAPO NENO LANGU”.

Unaona?..Unaposoma kwenye biblia kuwa “waasherati na wazinzi hawataurithi ufalme wa Mbinguni (Wagalatia 5:20)”.. na ukaacha kulitii hili NENO, na kinyume chake ukaendelea na uzinzi wako, huku ukijitumainisha kwa sadaka zako nyingi unazoendelea kuzitoa.. fahamu kuwa UNAFANYA MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU!!..Kwasababu maandiko yanasema…

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA…..”.

Unaposoma kuwa Wenye dhambi sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la Moto, kwasababu wamekataa kutubu dhambi zao, na wewe unajijua kabisa bado hujatubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, bado ukawa unaendelea na kulipa zaka zako, bado ukawa unaendelea na kuchangia kazi ya Mungu..nataka nikukumbushe kuwa UNAFANYA MACHUKIZO!!.. Mungu wetu si mkusanya mapato kutoka kwetu, na wala hahitaji fedha zetu… Yeye mwenyewe(Yesu Kristo) alisema maneno yafuatayo..

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA”.

Bwana Yesu anachotaka kuona kutoka kwetu, MIOYO YA TOBA, iliyosikia Neno lake na kutetemeka na kuamua KUGEUKA!..Kumbuka kutii ni bora kuliko dhabihu. Kamwe usijitumainishe katika matoleo unayoyatoa na ukasahau kulitii NENO LA MUNGU. Bwana amelitukuza Neno lake kuliko kitu kingine chochote.

Kabla ya kufikiria kumtolea Mungu, fikiria kujitakasa kwanza, fikiria kuacha uzinzi na ukahaba kwanza, fikiria kuacha kuacha ulevi, fikiria kuacha wizi, fikiria kuacha Ugomvi na baada ya kuacha hayo yote, ndipo ufikirie kumtolea Bwana matoleo yako, lakini kamwe usitangulize dhambi zako mbele ndipo sadaka zako zifuate, kwasababu ukifanya hivyo utakuwa unajitafutia laana badala ya baraka..

Mithali 15:8 “SADAKA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Kumbukumbu 23:7 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.

18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”

Siku zote Litii Neno la Bwana, kwasababu hilo ndilo MWANGA WA NJIA YETU, YA KWENDA MBINGUNI.

Bwana akubariki,

Maran atha!!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dhabihu ni nini?

CHAMBO ILIYO BORA.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

NINI MAANA YA KUTUBU

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Rudi nyumbani

Print this post