Category Archive maswali na majibu

Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Swali: Je mtu aliyeishi miaka mingi kwenye biblia alikuwa nani?..na Mtu aliyeishi miaka mingi duniani ni nani?.


Jibu: Katika biblia mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote, ni METHUSELA, mwana wa Henoko aliyetwaliwa na Mungu..Biblia inasema huyu Methusela aliishi miaka 969, na hakuna mwingine aliyerekodiwa kuishi miaka mingi kuliko yeye.

Mwanzo 5:25 “Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.

26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.

27 Siku zote za Methusela ni miaka MIA KENDA NA SITINI NA KENDA, AKAFA”.

Wengine walioishi miaka mingi katika biblia ni pamoja na;

  1. Yaredi, aliishi miaka 962, (Soma Mwanzo 5:20).
  2. Nuhu, Miaka 950 (Soma Mwanzo 9:29)
  3. Adamu, Miaka 930 (Soma Mwanzo 5:5)
  4. Sethi, Miaka 912 (Soma Mwanzo 5:8)
  5. Kenani, Miaka 910 (Soma Mwanzo 5:14)
  6. Enoshi, Miaka 905 (Soma Mwanzo 5:11)
  7. Mahalaleli, Miaka 895 (Soma Mwanzo 5:17)
  8. Lameki, Miaka 777 (Soma Mwanzo 5:31)
  9. Henoko, Miaka 365 (Soma Mwanzo 5:18-24)

Baada ya “Gharika ya Nuhu” miaka ya wanadamu ilishushwa mpaka kufikia miaka 120.. Ambapo ni wachache sana walivuka miaka hiyo, wengi waliishi chini ya hiyo..

Mwanzo 6:3 “Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini”.

Lakini kwajinsi siku zinavyozidi kwenda Miaka ya mwanadamu kuishi duniani ilizidi kushuka.. kutoka 120 mpaka 80

Zaburi 90:9 “Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10 Siku za miaka yetu ni MIAKA SABINI, NA IKIWA TUNA NGUVU MIAKA THEMANINI; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara”.

Lakini swali kuu ni hili; kwanini miaka ya wanadamu inazidi kupungua siku baada ya siku? Je ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa au mabadiliko ya vyakula?

Jibu rahisi ni kwasababu ya “kuongezeka kwa Maasi”. Wala si mabadiliko ya hali ya hewa! Bali ni DHAMBI!.. Kitu cha kwanza kilichopunguza miaka ya Adamu na Hawa kutoka kuishi MILELE mpaka kufikia kuishi miaka 930 si kingine Zaidi ya DHAMBI!.. wala si kwasababu walikuwa hawazingatii mazoezi au milo kamili!..La!! bali ni dhambi!..

Na kanuni hiyo hiyo ndiyo inayopunguza maisha ya mwanadamu inaendelea mpaka sasa… Na wakati huo huo upande wa pili shetani anajaribu kuwaaminisha watu kuwa ni “Milo wanayokula ndiyo inayopunguza miaka” kwamba wapunguze ulaji wa nyama, na mafuta, na wazingatie mazoezi wataishi miaka mingi.

Mambo hayo ni mazuri, na yanafaa..lakini hayafai katika kuongeza UREFU WA MAISHA YA MTU, Kwani kuna wengi ambao wamezingatia hayo yote lakini wamewahi kuondoka duniani!.. na kuna ambao hawajazingatia hayo yote lakini wanayo miaka mingi duniani.

Kanuni ya kuishi miaka mingi na ya heri NI KUMCHA MUNGU NA KUEPUKANA NA UOVU, hiyo tu… Zishike Amri, fanya mapenzi ya Mungu, maisha yako yatakuwa marefu, hapa na katika ulimwengu ujao.

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

Maandiko hayaelezi moja kwa moja kifo cha Farao. Lakini baadhi ya hivi vifungu vinatuonyesha Farao alizama na jeshi lake katika bahari ya shamu.

Zaburi 136:15

[15]Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;  Kwa maana fadhili zake ni za milele. 

Kuonyesha kwamba sio tu jeshi lake, lakini pia pamoja na yeye..walizamishwa baharini.

Pia vifungu hivi…

Kutoka 14:28

[28]Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja. 

Maandiko hayo, hapo mwishoni yanasema hakusalia hata “mtu mmoja”. Ikiwa na maana hata Farao mwenyewe alikwenda na maji.

Lakini pia andiko linaendelea kusema zaidi…

Kutoka 15:19

[19]Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari. 

Maana yake ikiwa kama magari yake mwenyewe yalizama baharini, ni uthibitisho kuwa hata na yeye mwenyewe alikuwa juu ya gari lake. Haiwezekani yeye kama mfalme aruhusu gari lake liende halafu abakie kwa miguu.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Farao alikufa katika bahari ile, pamoja na jeshi lake. Na Mungu ilimpasa awahakikishie wokovu kamili watu wake. Kwa kumwangamiza aliye kichwa cha adui zao. Kwasababu tangu mwanzo, masumbufu yote yalishinikizwa na Farao, hivyo alikuwa hana budi kuondolewa na yeye. Ili Israeli waufurahie wokovu mkuu wa Mungu.

Bwana akubariki.

Kutufundisha nini?

Mungu huwa anawahakikishia wokovu kamili watu wake, hata sasa tunao ukombozi mkamilifu ndani ya Yesu Kristo kwa kumwimini yeye, adui yetu shetani na mapepo yake yanafukuzwa,mbali na sisi. Lakini yatupasa tusiwe watu wa kutokuamini kama wana wa Israeli jangwani kwa kuishi kama wapagani, kwasababu ijapokuwa Mungu aliwaahidia nchi nzuri iliyobubujika maziwa na asali, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kuiingia isipokuwa wawili. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kuishindania Imani yetu. Ili tusionekane tumekosa kuingia kwenye ufalme wa Mungu wetu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

YONA: Mlango 1

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

USIMWABUDU SHETANI!

Rudi nyumbani

Print this post

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Swali: Je zamani marubani wanaoendesha ndege walikuwepo kama tunavyosoma katika Ezekieli 27:8?


Jibu: Turejee mstari huo..

Ezekieli 27:8 “Wakaao Sidoni na Arvadi ndio waliovuta makasia yako; wana wako wenye akili, Ee Tiro, walikuwa ndani yako, ndio WALIOKUWA RUBANI ZAKE”.

“Marubani” wanaozungumziwa hapo si Marubani wanaorusha ndege kwamaana kipindi hicho ndege zilikuwa hazijavumbuliwa…bali marubani wanaozungumziwa hapo ni wana-maji (manahodha)..Kwasababu asili ya neno hilo rubani si mwana-anga, bali ni mwana-maji.

Isipokuwa kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda na kumavumbuzi mengi kuibuka, basi maneno mengi yanakuwa yanapata maana Zaidi ya moja.

Kwamfano katika biblia yametajwa magari (Mwanzo 45:21)..sasa magari ya zamani si sawa na haya sasahivi, ingawa yote ni magari… vile vile katika biblia kuna mahali pametajwa “Risasi” (Kutoka 15:10) lakini Risasi hiyo si sawa na hii inayojulikana sasa.. Vile vile pametajwa neno “Ufisadi“ (2Petro 2:7).. Lakini ufisadi huo wa biblia ni tofauti kabisa na huu unaofahamika sasa. N.k

Kwahiyo tukirudi katika Rubani, anayetajwa hapo katika Ezekieli 27:8, ni rubani mwana-maji, na si mwana-anga. Ndio maana ukiendelea mbele Zaidi katika mstari wa 29 utaona biblia imeweka sawa…

Ezekieli 27:29 “Na wote wavutao kasia, wana-maji, na RUBANI ZOTE WA BAHARINI, watashuka katika merikebu zao, na kusimama katika nchi kavu”.

Hapo anasema “Rubani zote za baharini” ikiashiria kuwa ni wana-maji na si wana-anga.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.

Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

Rudi nyumbani

Print this post

Ubani ni nini?.. Na je wakristo tunaruhusiwa kuchoma ubani?

Swali: Je kuna ubani katika biblia?.. Na kazi ya Ubani ni nini?


Jibu: Ubani ni moja ya viungo vilivyotumika zamani kutengenezea manukato matakatifu yaliyoitwa “Uvumba”..

Viungo hivi (ubani) vinatokana na utomvu unaozalishwa na mmea ujulikanao kama “Boswelia” (Tazama picha juu). Mti wa Boswelia unaanza kutoa utomvu kati ya miaka 8 mpaka 10 baada ya kupandwa kwake, miti hii pia inastawi Zaidi sehemu zenye ukame.

Katika biblia “ubani” ulichanganywa pamoja na viungo vingine vitatu (3) ambavyo ni NATAFI, SHEKELETHI na KELBENA, kutengeneza Manukato matakatifu yaliyoitwa Uvumba ambapo Kuhani mkuu aliyachoma pamoja na kisha kuvukiza moshi ndani ya ile Hema kabla ya kufanya shughuli za upatanisho.

ubani katika biblia

Na uvumba wa aina hiyo, haukuruhusiwa kutengenezwa mfano wa huo kwa matumizi yoyote yale tofauti na hayo ya nyumba ya Mungu.. (maana yake haikuruhusiwa mtu kutengeneza kwa fomula hiyo na kufanya kama marashi nyumbani kwake, au ibada nyumbani kwake, ilikuwa ni kosa).

Kutoka 30:34 “Bwana akamwambia Musa, Jitwalie manukato mazuri, yaani, natafi, na shekelethi, na kelbena; viungo vya manukato vizuri pamoja na ubani safi; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;

35 nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu;

36 nawe baadhi yake utayaponda sana, na kuyaweka mbele ya ushuhuda ndani ya hema ya kukutania, hapo nitakapokutana nawe; nayo yatakuwa kwenu matakatifu sana.

37 Na uvumba utakaofanya, hamtajifanyia uvumba wenye viungo sawasawa na uvumba huo; utakuwa kwenu mtakatifu kwa ajili ya Bwana.

38 Mtu ye yote atakayefanya mfano wa huo, ili kuunusa, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake”

Sasa kuelewa kwa upana Zaidi kuhusu “Uvumba” na maana yake kiroho basi fungua hapa >>KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Lakini swali ni je! Sisi wakristo tunaruhusiwa kuchoma Ubani katika ibada au manyumbani mwetu?

Jibu ni La!.. Wakristo hatujapewa maagizo yoyote ya kuchoma ubani wala kujishughulisha nao. Manukato ya Ubani yalitumika katika agano la kale katika hema ya kukutania, na baada ya agano jipya kuanza, mambo hayo yakawa ni ya KIROHO na si ya kimwili tena, hivyo hakuna Uvumba, wala ubani wala hivyo viungo vingine unaopaswa kuhusishwa na ibada yoyote katika agano hili jipya.

Kwanini Ibada hizo za Kuvukiza uvumba na ubani hazipo tena sasa?

Ni kwasababu ile ile za kuondoka ibada za kafara za wanyama.. Hatuwezi sasa kutumia Ng’ombe au kondoo kwaajili ya utakaso wa dhambi zetu, na wakati kuna damu ya YESU, ambayo inatusafisha sasa katika ulimwengu wa roho.

Vile vile hatuwezi kuchoma ubani, na kuvukiza uvumba kama njia ya kuvuta uwepo wa Mungu na wakati tunaweza kufanya hivyo kwa njia ya sala na maombi.

Zaburi 141:2 “Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni”

Sasa Kafara za wanyama (Ng’ombe, mbuzi, kondoo na njiwa) na kuchoma ubani zimebaki kuwa ibada za miungu!… Wote wanaofanya hizo, wanavuta uwepo wa mapepo na si wa Mungu! Hivyo ni muhimu kuwa makini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MADHABAHU NI NINI?

Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)

NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

Dhamiri ni nini kibiblia?

Dhamiri au Dhamira ni nini kibiblia?


“Dhamiri” au kwa lugha nyingine “Dhamira” ni hisia ya ndani ya mtu (ya asili) inayompa kupambanua lililo jema na lililo baya, lililo zuri na lisilo zuri, linalofaa na lisilofaa. Hisia hii kila mtu anayo na haitokani na mafundisho au maelekezo, bali mtu anakuwa anazaliwa nayo.

Dhamiri ni kama mtu mwingine wa pili, aliyeko ndani yako ambaye anasahihisha hisia zako au maamuzi yako, kabla hujayafanya au baada ya kuyafanya. Kama jambo halipo sawa basi dhamiri inakushuhudia aidha kwa kukosa Amani au raha au ujasiri..

Vile vile kama jambo lipo sawa basi dhamiri yako ya ndani inakushuhudia kwamba kile ufanyacho ni chema, aidha kwa kupata furaha Fulani au Amani au ujasiri.

Kwamfano mtu anapofikiri “kuua/ kumwaga damu” au “kuiba”.. kabla ya kufanya kile kitu “dhamiri” ya ndani itamshuhudia kuwa kile kitu si sawa! Pasipo hata kuambiwa na mtu au kuhubiriwa, kuna kitu tu ndani yake kinamwambia hicho si sawa!.. Na kama ni mtu wa kujali basi haraka sana atahairisha maamuzi yake hayo.

Katika biblia neno Dhamiri limeonekana mara kadhaa.

Sehemu ya kwanza maarufu ni ule wakati ambao baadhi ya Waandishi na Mafarisayo walimletea Bwana YESU mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, kwa lengo la kutaka kumwua lakini pia kumjaribu Bwana. Lakini maandiko yanasema walipopewa ruhusa ya kumtupia mawe, wote walichomwa dhamiri zao na hakuna aliyemhukumu.

Yohana 8:3  “Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.

4  Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.

5  Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?

6  Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

7  Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

8  Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

9  Nao waliposikia, WAKASHITAKIWA NA DHAMIRI ZAO, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

10  Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?

11  Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]”

Vile vile biblia inatabiri kuwa katika siku za mwisho, watatokea watu ambao watasema uongo ijapokuwa dhamiri zao zinawashuhudia, lakini hawatazisikiliza, na watu hawa watawafundisha watu mafundisho ya mashetani.

1Timotheo 4:1  “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2  kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3  wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli”

Mistari mingine ihusuyo dhamiri ni pamoja na Matendo 23:1, Warumi 2:15, Warumi 9:1, Warumi 13:5, na 1Timotheo 1:9.

Ikiwa ndani yako unahisi “Dhamiri yako imekufa” au “imepungua nguvu”… maana yake husikii chochote kikikuzuia au kukuhukumu unapofanya jambo lisilo sawa, basi fahamu kuwa adui kaharibu utu wako wa ndani, na hivyo unamhitaji Bwana YESU akuhuishe utu wako wa ndani kwa damu yake.

Unapompokea BWANA YESU, na kubatizwa na kujazwa na Roho wake mtakatifu, ule utu wako wa ndani uliokufa au uliofifia yeye (Bwana YESU) anauhuisha upya…na hivyo Dhamiri yako inafufuka na inakuwa safi. Hivyo fanya maamuzi leo ya kumsogelea yeye karibu na imarisha mahusiano yako naye.

Waebrania 9:14  “basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

Rudi nyumbani

Print this post

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

Kwa tafsiri za kiulimwengu, ulimwengu wa roho Ni ulimwengu usioonekana kwa macho ambao unasadikika viumbe kama malaika, mapepo, au roho za wafu huishi na kutenda kazi. Na kwamba vyenyewe ndio vinavyoyaathiri maisha ya ulimwengu huu unaoonekana.

Na kwamba ili mtu aweze kutembea vizuri hapa duniani hana budi kufahamu au kuwasiliana navyo, ili viwape taarifa, au kushindana navyo pale vinapokinzana nao, kwa kuzingatia misingi Fulani maalumu ya kiroho. Na wengine wanaamini kuwa ni mahali ambapo pana mifumo kama hii ya kidunia, mfano  majumba, magari, falme na mamlaka, isipokuwa tu hapaonekani kwa macho n.k. ipo mitazamo mingi.

Lakini kibiblia Mungu anataka tufahamu kwa picha ipi juu ya huu ulimwengu wa Roho?

Awali ya yote biblia inatuambia ulimwengu wa roho upo. Na hauonekani kwa macho.

Waebrania 11:3  Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

Umeona, kumbe vitu vyote tunavyoviona kwa macho vilitokea mahali ambapo hapaonekani. Na huko si pengine zaidi ya rohoni.

Lakini jinsi unavyotazamwa kiulimwengu ni tofauti na jinsi Mungu anavyotaka sisi tuutazame.

Mungu anataka tutambue kuwa ulimwengu wa Roho, ni mahali ambapo sisi tunakutana na yeye kuwasiliana, pia kumwabudu, na kumiliki, na kutawala, na kubarikiwa, kuumba, kujenga, kufunga na kufungua, na kupokea mahitaji yetu yote kutoka kwake. Kwasababu yeye ni Roho,  zaidi ya kufikiri ni mahali ambapo tunakwenda kupambana na wachawi na mapepo au kuona vibwengo na mizimu.

Alisema..

Yohana 4:23  Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Hivyo, pale tu mtu anapoonyesha Nia ya kutaka kumjua Mungu (asiyeonekana), muumba wa mbingu na nchi. Tayari hapo anaanza hatua ya kuingia katika ulimwengu wa roho ambao Mungu aliuumba kwa ajili yake, na si kitu kingine.

Ndipo hapo sasa anapofahamu kuwa anauhitaji wokovu ili aweze kumkaribia Mungu.  Anaanza kumwamini Yesu, anapokea msamaha wa dhambi, kisha Roho Mtakatifu, na baada ya hapo anaishi kwa kulifuata Neno la Mungu aliloliamini. Sasa huyu mtu ambaye Ameokoka, anaitwa mtu wa rohoni, lakini Yule ambaye anaishi katika Neno la Mungu kwa kulitii, huyu sasa ndiye anayetembea rohoni.

Hivyo haijalishi kama alishawahi kuona malaika, au pepo, au kusikia sauti, au kuona maono. Maadamu analiamini Neno la Mungu, na nguvu zake, na kuliishi. Huyo yupo katika ulimwengu wa Roho tena katika viwango vya juu sana. Kwasababu maandiko yanasema kwa kupitia hilo (NENO), vitu vyote viliumbwa.

Kuishi katika Neno ndio kuishi rohoni. Maana yake ni kuwa  unaishi kwenye ulimwengu wa Neno.

Sasa utauliza, na haya mashetani sehemu yao ni ipi katika ulimwengu wa roho?

Haya nayo yanaingia rohoni, kwa lengo moja tu kuwapinga wale watu ambao wanatembea katika ulimwengu wa roho (yaani ulimwengu wa Neno). Hivyo yanajiundia mikakati, falme, ngome, na milki, ili tu yakuangushe wewe, uache kumwamini Mungu na Neno lake, na mpango wake wa wokovu kupitia Yesu Kristo. Uendelee kuwa mtu wa mwilini.

Ndio hapo sasa Bwana anatutahadharisha kuwa yatupasa tuwapo rohoni tusiwe hivi hivi tu. Bali tuhakikishe kweli silaha zote tumezivaa, kwasababu, mashetani haya pamoja na wajumbe wake wapo kwa lengo la kutuondoa kwenye Neno la Mungu.

Waefeso 6:10  Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

11  Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.

13  Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa unapookoka, wewe tayari ni mtu wa rohoni. Ni mlango wa wewe kuonana na Mungu. Umeshaingia ulimwengu wa roho. Hivyo ili uweze kuona matunda yote ya Mungu, ni sharti uliishi kwa kuliamini Neno lake na ahadi zake, maisha yako yote yawe hivyo. Uwe mtu wa Neno. Lakini mtazamo wa kwamba siku unaona maono na malaika, au kusikia sauti ya Mungu kwenye masikio yako, au wachawi na mapepo ndio mara ya kwanza umeingia rohoni,. Si kweli. Bali Uanzapo kuliamini na kulitendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Hivyo ni vifungu baadhi ambavyo utakutana na hilo neno, kwenye maandiko, vitakavyokusaidia kuelewa vema.

Waefeso 1:3  Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ULIMWENGU WA ROHO, ndani yake Kristo;

Waefeso 1:17  “Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye;18  macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; 19  na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; 20  aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ULIMWENGU WA ROHO”

Soma pia Waefeso 2:6,  3:10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

CHAKULA CHA ROHONI.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

SWALI: Je! ni sahihi kwa mkristo kufanya biashara za kifedha mitandaoni kama vile Forex, na crypto-currency mfano wa bitcons?


JIBU: Ni vema kufahamu biashara za kifedha mitandaoni kama forex ni nini?

Ni biashara ya ubadilishaji wa fedha za kigeni katika soko la dunia. Yaani ununuaji na uuzaji wa fedha za kigeni, sawa tu ile tuliyowahi kuisikia, ijulikanayo kama Bureau de change, ambayo watu wanakwenda kununua/kuuza pesa za kigeni, isipokuwa hii hufanyika mitandaoni, tofauti na bureau ambayo hufanyika kwa makarati ndani ya ofisi Fulani maalumu. Biashara hii ya forex na nyinginezo Mara nyingi hufanywa na taasisi kubwa za kifedha kama mabenki na makampuni, lakini pia hata watu binafsi.

Ni biashara ya bahati nasibu, inayofanana na michezo ya kubahatisha kitabia.. Lakini ni tofauti kabisa kimaudhui.

Biashara  hii ni ya uwekezaji, ambayo imehalalishwa ki-ulimwengu, japokuwa hatusemi kuwa kila biashara iliyohalalishwa na taifa kuwa ni halali kwa mkristo kufanya, hapana mfano zipo pombe zimehalalishwa kitaifa lakini kwa mkristo sio sawa kufanya biashara kama hizo.

Lakini, biashara hii, haihusishi katika kumdhulumu mtu, au kumlaghai mtu kiakili, apoteze kitu Fulani ili wewe ujilimbikizie fedha zake ambazo hazina mzungumko wowote wa kimaendeleo. Mfano wa hizo ni kama vile “Betting na kamari”. Kwa mkristo kushiriki katika biashara hizo za betting na kamari sio sawa. Kwa urefu wa somo lake pitia link hii >>>JE! KUBET NI DHAMBI?

Lakini Forex na nyinginezo zijulikanazo kama biashara za uwekezaji, zinahitajika sana, kwasababu kama zikikosekana, basi mzunguko wa fedha za kigeni, ungekuwa mgumu sana, na hivyo kupunguza kasi ya ukuaji uchumi, katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia.

Hivyo tukirudi kwa mkristo, je kufanya biashara hii ni dhambi?

Kimsingi ikiwa anafanya kwa lengo la uwekezaji wake, huku akijua pia ni kwa faida ya uchumi, na hamdhulumu au kumlaghai mtu. Hafanyi kosa. Lakini akiwa na fikra za kikamari, kama vile afanyavyo kwenye betting, Kwake itakuwa ni kosa, kwasababu dhamiri yake inamshuhudia, ameigeuza kama kamari moyoni mwake.

Ndio hapo hili andiko linakuja.

Warumi 14:22  Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

23  Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. NA KILA TENDO LISILOTOKA KATIKA IMANI NI DHAMBI.

Maana yake ni kuwa ukiwa na mashaka moyoni mwako kuifanya kazi hii, basi ni heri usifanye kabisa, kwasababu mashaka yoyote ni dhambi. Lakini kimsingi biashara hii sio kosa kwa mkristo, ambaye ana maarifa/elimu ya kutosha juu ya biashara za kifedha katika ulimwengu wa sasa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

Toba ni nini?

Swali: Toba maana yake nini?.. na je ina umuhimu gani kwetu?


Jibu: Neno “Toba” liinatokana na neno “kutubu”. Mtu anayetubu maana yake kafanya “TOBA”. Na kutubu maana yake ni “kugeuka, kutoka katika njia uliyokuwa unaiendea”.. Maana yake kama mtu ameshawishika kugeuka kutoka katika njia au mwenendo aliyokuwa anauendea kwa njia ya majuto na maombi ya kuomba msamaha kama njia hiyo ilikuwa ni kwanzo kwa mwingine, mtu huyo anakuwa ametubu, au amefanya TOBA.

Kibiblia mtu aliyegeuka na kuiacha njia ya dhambi aliyokuwa anaiende na kuomba msamaha kwa Mungu wake aliyemkosea, basi mtu huyo anakuwa amefanya TOBA, na ndio hatua ya kwanza kabisa ya Mtu kumsogelea MUNGU, hakuna njia nyingine tofauti na hiyo!.

Injili ya Yohana Mbatizaji na ya BWANA YESU (Mjumbe wa Agano jipya) ilianza na Toba.

Yohana 3:1  “Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,

TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, TUBUNI; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Maana yake watu waageuke na kuacha maisha ya kuabudu sanamu, waache maisha ya mauaji, waache maisha ya uzinzi na uasherati, waache maisha ya ulevi na utukanaji n.k.. kwasababu Ufalme wa mbinguni hautawapokea watu wa namna hiyo.

Lakini pia si kutubu tu, bali ni pamoja na “KUZAA MATUNDA YAPATANAYO NA HIYO TOBA”.. Maana yake baada ya kugeuka na kuacha dhambi, basi mwongofu huyo anapaswa ajifunze kuishi maisha yanayoendana na toba yake hiyo, maana yake asirudie tena machafu ya nyuma yatawale maisha yake.

Luka 3:8 “Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto”.

Je na wewe umetubia dhambi zako na kumkaribisha YESU maishani mwako? Kama bado basi fungua hapa ufuatilize sala hii ya TOBA na KRISTO YESU ataingia maishani mwako kwa Imani >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

Rudi nyumbani

Print this post

Je watu waliookoka wanaruhusiwa kukopa?

Swali: Je wakristo tunaruhusiwa kukopa benki au kutoka kwa watu?..kama ni ndio, kwanini maandiko yaseme mtakopesha wala hamtakopa? (Kumbukumbu 15:6).


Jibu: Turejee..

Kumbukumbu 15:6 “Kwani Bwana, Mungu wako, atakubarikia, kama alivyokuahidi; nawe utakopesha mataifa mengi, lakini hutakopa; tena utayatawala mataifa mengi, usitawaliwe na wao”

Kuna kukupa kwa aina mbili; 1) KWA AJILI YA KUTATUA TATIZO/JANGA…. 2) KWAAJILI YA KUJITANUA.

    1. KUKOPA KWAJILI YA KUTATUA MATATIZO.

Kukopa kwa namna hii ni ile hali ambayo, mtu anapatwa na baa Fulani au janga, hivyo ili kujikimu au kujikidhi anakwenda kutafuta msaada kwa njia ya kukopa!.. Sasa kukopa kwa namna hii ndiko kunakozungumziwa hapo katika Kumbukumbu 15:6 (kwamba tutakopesha wala hatutakopa).

Na kwanini tutakuwa watu wa namna hiyo (ya kutokukopa)?.. ni kwasababu Mungu ni msaada wetu ambaye hataruhusu tupate matatizo hayo pasipo kuwa na sababu yoyote. Hivyo tutabaki katika usalama wake ambao utatuhifadhi dhidi ya madhara yote ya yule adui.

Hivyo kama mkristo ukiona unapitia vipindi vya mfululizo vya kukopa ili kukidhi mahitaji yako ikiwemo chakula, basi jaribu kulitazama jambo hilo kiroho Zaidi, na Bwana atakusaidia kukutoa hapo!.

       2. KUKOPA KWAAJILI YA KUJITANUA.

Hii ni aina ya pili ya UKOPAJI, ambayo biblia haijaikataza!.. Inapotokea huna janga lolote, huna baa lolote, na unaishi vizuri kwa katika neema ya Mungu, kiasi kwamba ukipatacho kinakidhi hali ya kutokuwa na haja ya kukopa!.. Lakini ukapenda kujitanua Zaidi ya hapo kifedha au kibiashara au kimiradi kama mtu wa Mungu, na ukaamua kwenda kukopa ili kuongeza labda ule mtaji ulio nao ili kutanua kazi au biashara..

Kukopa kwa namna hii “hakujakatazwa kwa mkristo” na wala hakumaanishi kuwa wewe ni maskini, kwasababu hata watu wengi walio matajiri sana pia wanakopa!!.. lengo lao la kukopa si kukidhi mahitaji (kwamba wana janga fulani au baa fulani, hivyo wasipopata huo mkopo wanaweza kudhurika) bali mara nyingi ni kwa lengo la kutanua biashara zao wazifanyazo au miradi yao.

Na Mkristo anapofikia mahali anahitaji kutanuka Zaidi anaweza kuchukua mkopo, na isiwe na tafsiri yoyote kwamba ni maskini au muhitaji, na kwamba pasipo huo hawezi kuishi.

Kanuni ya KUKOPA ni sawa na ile ya KUUZA tu!… Mtu anayeuza shamba kwaajili ya matatizo, ni tofauti na yule anayeuza shamba kama biashara!..kadhalika mtu anayekopa kwaajili ya kutatua matatizo/au janga Fulani ni tofauti na yule anayekopa kwaajili ya kujitanua.

Bwana atusaidie katika yote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Rehani ni nini katika biblia?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Rehani ni nini katika biblia?

Rehani ni nini kibiblia?, na je sisi wakristo tunaruhusiwa kuweka kitu rehani?


Rehani ni mali iliyowekwa kama dhamana kwa mkopo uliochukuliwa, maana yake mkopo usipolipwa basi mali ile inachukuliwa ili kufidia ule mkopo.

Katika biblia (Agano la kale), Rehani iliruhusiwa lakini kwa kuiangalia hali ya mtu. Kama mtu alikuwa ni tajiri mwenye uwezo basi alipokopa alipaswa aweke rehani mali itakayosimama badala ya ule mkopo endapo atashindwa kuulipa.

Lakini kama mtu alikuwa ni maskini sana, na hana kitu isipokuwa jiwe la kusagia tu na mavazi, basi hakupaswa kutozwa rehani katika hivyo alivyo navyo, ilikuwa ni dhambi kubwa kutwaa jiwe la kusagia la maskini au mavazi yake kama Rehani.

Kumbukumbu 28: 6 “Mtu awaye yote asitwae jiwe la kusagia, la juu wala la chini, kuwa rehani; kwani hivi ni kutwaa maisha ya mtu kuwa rehani”.

Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani;

18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”.

Kwa urefu kwanini si sawa kutwaa jiwe la kusagia la maskini kama rehani waweza kufungua hapa >>>Kwanini jiwe la kusagia Mungu alikataza lisiwekwe rehani? (Kumbukumbu 24:6).

Sasa swali je na sisi wakristo ni sahihi kuweka kitu rehani au kupokea rehani kutoka kwa mtu tuliyemkopesha?

Jibu: Rehani haijakatazwa katika biblia, kama umemkopesha mtu kitu cha thamani, na mtu huyo si ndugu yako katika Imani (yaani mpendwa mwenzako) au si ndugu yako katika mwili (yaani mwanafamilia) waweza kupokea Rehani, ili kumhamasisha kurejesha lile deni, (ikiwa lengo lako si kumkandamiza bali kumhamasisha na kama mtu huyo uwezo huo anao). 

Lakini kama ni maskini na kaja kukopa kwako, si vizuri kuchukua rehani. Waweza kumkopa bila rehani yoyote, ni itakuwa baraka kwako.

Lakini kama ni ndugu yako katika Imani na katika damu, si vyema kumtoza rehani,  wala riba, katika mazingira yoyote yale, awe tajiri au maskini,  waweza kumkopa ukitumai kuwa atakulipa tu pasipo kutaka dhamana.

Lakini pia kama wewe ni mkopaji, (maana yake unakopa kutoka kwa mtu/taasisi kwaajili ya shughuli fulani) si dhambi kusimamisha kitu kama rehani itakayosimama kwaajili ya mkopo wako (kama mtu huyo au taasisi hiyo inahitaji hayo yote).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

LIONDOE JIWE.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Rudi nyumbani

Print this post