Hebu jaribu kufikiria, leo vita vitokee, mabomu yakapigwa huku na kule, barabara zikaharibika, miundo mbinu ya maji na umeme ikaharibika…unadhani na wewe mtu wa Mungu utaacha kuathirika kwa namna moja au nyingine?..utaathirika tu!
Kwasababu na wewe unahitaji barabara kwenda kazini kwako au kwenda kuhubiri, unahitaji umeme kuendesha biashara yako kama unayo, unahitaji maji kwa ajili ya kuishi, n.k sasa hivyo vyote vimeharibika unadhani na wewe utaacha kupata shida hata kama unamtumainia Mungu?..Ni kweli Bwana anaweza akakuhifadhi wewe kupona lakini kwa shida sana! Katika wengi watakaokufa kwa matatizo hayo unaweza usiwe mmoja wao kwasababu unamcha Mungu, lakini utakuwa katika dhiki nyingi…Nuhu alisalimika kwenye gharika lakini maisha ndani ya gharika hayakuwa ya raha kabisa..kukaa miezi mitano kwenye boti, ndani giza, hakuna kutembe tembea..wewe ni kitandani, kwenye kiti na kusikia sauti za wanyama tu, na watu wale wale uliowazoea! Yalikuwa ni maisha ya shida ingawa kasalimika.