Msongo wa mawazo ni nini? Ni shinikizo au mfadhaiko wa kiakili, unaomkumba mwanadamu, pale anapokutana na matatizo, au taabu, au dhiki au shida Fulani. Hivyo inapotokea mtu huyu anashindwa kuzitatua changamoto hizo, ndipo msongo huo huja.
Kwamfano labda mtu amegundulika, ana ugonjwa usiotibika, na kaambiwa na daktari hawezi kupona, mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa na msongo wa mawazo,
Au labda mwingine hana kazi na akiangalia familia inamtegemea, na bado hajafikia malengo yake kulinganisha na umri alionao, moja kwa moja mtu kama huyu ni rahisi kukumbwa pia na msongo wa mawazo. N.k.
Na kama tiba isipopatikana matokeo yake yanaweza kuwa mtu huyo, kupata matatizo ya kiafya, wengine kuchanganyikiwa, wengine kujitenga na watu, wengine kujifungia ndani kulia tu usiku kucha, wengine kutenda vitendo viovu, hata kujiua.
Je! Mkristo anaweza kuwa na msongo wa kimawazo? Jibu ni ndio anaweza kuwa nao. Lakini tiba imeshatolewa. Tutaona katika somo hili kwa namna gani, kwasababu yawezekana wewe ni mmoja wapo ambaye unakutana na hali hii na hujui cha kufanya.
Embu tuone kwanza baadhi ya watu katika maandiko ambao walipitia misongo ya mawazo
Eliya wakati amemaliza kuwaua manabii wa Baali, akatazama huku na huku na kujiona kama ni yeye peke yake ndiye nabii wa Mungu aliyebaki, hivyo ikampelekea ajitenge, na kukimbilia jangwani, akae huko mpaka afe. Lakini Mungu alikuja kumtokea baada ya siku 40, akampa majibu ya faraja, kwamba asidhani yupo peke yake kuna wengine 7,000 amejisazia, rudi Israeli, kanitumikie. (1Wafalme 18-19)
Alikumbwa mara nyingi na msongo wa mawazo katika maficho yake alipokuwa anawindwa na mfalme Sauli. Mara nyingi alifikia hatua ya kukata tamaa ya maisha. Embu tafakari haya maneno aliyoyasema Daudi.
Zaburi 69:1 Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. 2 Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha. 3 Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu. 4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua. 5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu
Baada ya kupotelewa na mali zake, na watoto wake, hadi mwili wake kubaki mifupa tu. Mkandamizo ulimjia. Ayubu anasema;
Ayubu6:2 Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja! 3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka
Mpaka akanza kusema maneno magumu, ya kulaani siku aliyozaliwa. Mtu kama huyu alikuwa katika hali mbaya sana kifikra na kiakili.
Petro na Yuda walipitia jambo moja, kukana na kusaliti, ni dhambi pacha. Isipokuwa Yuda alikwenda kujinyonga kwasababu msongo wa mawazo ulimshinda, lakini Petro hakujinyonga. Yeye alikwenda kujificha na kulia sana kwa “majonzi”. Tengeneza picha ni wewe unamkana Mungu wako, tena kwa maneno ya dhihaka mbele za watu. Hali hiyo unadhani itakufanya ujionaje kama sio mateso ya kiakili baada ya hapo?. Wengine wanapitia hali kama hizi, wanapojiona wamemtenda Mungu dhambi kubwa sana, isiyosameheka, wakidhani kuwa Mungu hawajali tena, hawathamini.(Mathayo 26:75)
Baada ya Bwana Yesu kufa, hofu ya wayahudi ikawavaa mitume, wakiona kuwa wao ndio wanaofuata kuuliwa baada ya kiongozi wao kufa.. Hivyo hiyo ikawapelekea kujifungia ndani, wasitoke. Msongo mkubwa sana wa mawazo uliwavaa, kutoka kwa wayahudi.(Yohana 20:19-29)
Itoshe tu kutumia mifano hiyo michache, kwani wapo wengine wengi sana katika biblia waliopitia hali kama hizi, mfano ni Musa, Yusufu, Yeremia, Nebukadreza, Hana (mamaye Samweli), Danieli, Mtume Paulo wote hawa ukisoma habari zao katika biblia utayathibitisha hayo.
Utagundua, walipopitia taabu zao, walilikumbuka TUMANI la Mungu. Ndilo lililowapa nguvu ya kuweza kuvuka nyakati hizo mbaya walizozipitia. Waliyazingatia haya maneno;
1Petro 5:6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; 7 HUKU MKIMTWIKA YEYE FADHAA ZENU ZOTE, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
Na lile alolisema Yesu..
Mathayo 11:28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha
Pale akili zilipogoma, fikra kuzima, moyo kuwa baridi, walijifunza kumtwika Mungu, huzuni zao, mateso yao, shida zao. Hata pale ambapo hazikutatulika kwa wakati walioutarajia, lakini waliendelea na mwisho wa siku Bwana alikuja kuyaweka yote sawa. Kwasababu yeye mwenyewe alisema.
Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi TUMAINI siku zenu za mwisho
Hivyo ndugu, ikiwa na wewe upo katika hali hii ya msongo wa kimawazo, katika eneo lolote lile, iwe la kiroho, kihuduma, kifamilia, kikazi, kiafya, kimaendeleo. Umeshindwa kuendelea mbele, Usiogope. Kwa Mungu lipo TUMAINI, zaidi ya Matumaini yote ya kibinadamu.
Haijalishi msongo huo, umekupata kutokana na dhambi zako, au kutokana na hali zilizo nje ya uwezo wako. Usiogope. Mponyaji, mfajiri, mtatuaji wa matatizo yupo. Huyu si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwokozi.
Mungu akikupa tumaini, ujue ni lazima litokee, lakini mwanadamu akikupa tumaini, ni kusudi tu kukufariji, lakini tatizo linaweza kubaki palepale. Yesu hayupo hivyo. Mtazame tu yeye. Wakati wa shida, ndio wakati wa kukimbilia chini ya mbawa zake, sio kuwakimbilia wanadamu.
JE! UFANYEJE?
Na hakika, katika muda fulani, utaona Mungu anakuvusha, anakuponya, anakufariji, anakuondolea huo mzigo. Huo ni uhakika sio makisio. Usiache tu kuendelea na Bwana..
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Mafundisho Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
TUMAINI NI NINI?
UKIOKOKA,HIZI FIKRA ZIKIJA NDANI YAKO, ZIKATAE.
VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI
TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.
Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?
Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?
Rudi nyumbani
Print this post
Huu ni mwendelezo wa Mafundisho maalumu yawahusuyo wanawake.
Mwanamke aliyepoteza shilingi moja.
Luka 15:8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? 9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.
Bwana Yesu alipenda kutumia mifano halisi ya kimaisha kutufundisha habari za rohoni. Kwamfano katika habari hiyo tunafahamu mfano huo ulikuwa analenga mambo ya ufalme wa mbinguni, jinsi Mungu anavyomthamini mtu wake mmoja aliyepotea katika dhambi, pindi atubupo na kurejea. Kwamba tendo hilo linamfanya yeye pamoja na malaika zake mbinguni kufurahi sana.
Lakini leo nataka tujifunze kuhusu mfano huo katika uhalisia wake wa kimaisha kama ulivyoandikwa. Kuna maswali lazima ujiulize kwanini amtaje mwanamke na sio mwanaume. Kisha aipoteze shilingi yake pale NYUMBANI kwake, na sio sehemu nyingine, labda barabarani au sokoni? Tofauti na mfano uliotangulia ambao unamzungumzia Yule mtu aliyepotelewa na kondoo mmoja akawaacha wale 99 akaenda kumtafuta Yule mmoja huko maporini.
Na hatua ambazo alitumia kuitafuta shilingi ile hadi kuipata, kuna funzo gani pia?.
Kumbuka kimaandiko aliyekabidhiwa nyumba aisimamie ni mwanamke, ndio maana biblia inasema,
Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Na hazina yake inapatikana humo, lakini pia ikipotea, basi hupotelea humo humo.
Tukisema nyumba hatumaanishi, gorofa, na sebule na jiko. Hapana, bali tunamaanisha wale waliomo mule. Hao ndio hazina yake hasaa.
Sasa katika mfano huo mwanamke huyu alikuwa na shilingi 10, labda tuseme hao ni watoto 10, au ndugu 10, lakini mmoja akapotea, huwenda akawa mtundu, au mwizi, au kibaka, au shoga, au jambazi n.k. Lakini Mwanamke huyu hakukata tamaa na kukaa chini na kusema, Ahh! Ninao hawa 9, wenye kujitambua na wenye nidhani. Embu ngoja niachane na Yule pasua kichwa mtukutu, mwenye kiburi, asinipe presha, nifarijiwe na hawa wanangu 9 wazuri. Hapana, bali alilazimika kufanya jambo ili kuhakikisha amempata na Yule.
Hivyo kama tunavyosoma, hakukaa tu hivi hivi, na kuzungumza. Bali alichukua hatua fulani, na hatua zenyewe ndio hizi tatu.
Hii ikiwa na maana gani? mpaka anafikia hatua ya kuwasha tamaa, maana yake ni kuwa chumba hicho kilikuwa na giza, hivyo asingeweza kuipata shilingi yake katika mazingira yale. Tafsiri yake ni nini? Alimkaribisha Kristo. Ambaye ndio Nuru ya ulimwengu katika nyumba yake.
Hivyo hatua ya kwanza katika kutatua tatizo lake, alimtambua Kristo kwenye nyumba yake. Na sasa Nuru ilipomulika ndipo akatambua kuwa nyumba ilikuwa chafu. Kama asingewasha taa, kamwe asingeweza kugundua kuwa Vitu havipo katika mpangalio wake. Hivyo ikampasa aanze kwanza kuifagia nyumba ile, aipangilie vizuri. Makombo yaliyodondoka sakafuni ayafagie, vikombe na vijiko vilivyokaa hoe hae, aviweke mahali pake, nguo ambazo hazijakunjwa aziweke kabatini, uwazi uwepo. Hakukimbilia kuitafuta shilingi yake katika hatua hiyo. alijua hawezi kuipata katika mazingira yale, machafu, imejificha sana.
Hivyo ikamchukua muda Fulani mrefu kuisafisha nyumba yake, mpaka hatimaye, pengine baada ya saa 6, ikawa safi. Kila kitu kikawa katika mpangilio wake.
Ndipo sasa akaenda katika hatua ya mwisho ya “kuitafuta kwa bidii ile shilingi”. Akaanza kupita eneo moja baada ya lingine, hakutoka nje ya nyumba kwenda kuitafuta barabarani, hapana bali pale pale ndani kwasababu alijua fedha zake hazijawahi kutoka nje ya nyumba.
Na hatimaye akaipata. Na mwisho wa siku akawaalika na marafiki zake, wakafurahi pamoja. Kwasababu ilimgharimu kuipata tena.
Hii ni kufunua nini?
Wanawake wengi wanapoona aidha ndugu zao nyumbani, au watoto wao, au ndoa zao zimeharibika,. Wengine wanakimbilia kwa waganga ili wasaidike, hapo umepotea, wengine wanakimbilia kwa washauri wa kijamii, bado hujapata suluhisho. Suluhisho pekee ni Nuru ya ulimwengu. Yesu Kristo, aimulikie kwanza nyumba yako.
Na Yesu anachokifanya ni kukuonyesha madhaifu uliyokuwa nayo, uchafu uliomo nyumbani mwako, ili urekebishe (ndio ufagie). Sasa wengine wanapofikia hatua hii, wanapoona wanahubiriwa waishi maisha ya utakatifu, wawe watu wa ibada majumbani mwao, wawe waombaji, wafungaji, wafukuze tabia zisiojenga majumbani mwao, waweke mipaka Fulani kwenye familia zao. Wanaona kama wanatwikwa mzigo juu ya mzigo. Wanamkimbia Kristo, wanabakia kulia tu, na kuhuzunika..
Wanachofikiria tu, ni utatuzi wa tatizo, mume aache pombe (aokoke), watoto wawe wasikivu, nyuma iwe na amani, n.k. lakini hawataki wao wenyewe kurekebisha baadhi ya mambo makwao. Hapo ndugu ukikwepa hatua hii, sahau kukipata unachokitafuta. Hata upewe bahari nzima ya mafuta ya upako, na pipa la chumvi. Unapoteza muda, hutatui jambo lolote.
Kristo anataka usafi kwanza, ndipo akupe jicho la kuiona shilingi yako iliyopotea. Sasa ikiwa utatimiza mambo hayo mawili yaani KRISTO ndani yako, na usafi wako. Kinachofuata ni kutafuta ulichokipoteza.
Hii ndio hatua sasa ya kumuhubiria, kumshauri, kumwonya, kumvuta kwa Bwana. Sasa ukiendelea hivyo hivyo, muda si mwingi utampata kiwepesi sana haijalishi alikuwa amepotea kiasi gani, au alikuwa sugu namna gani. Hakuna linaloweza kujificha mbele ya Nuru. Tatizo lolote sugu unalolijua wewe la kifamilia, kwa kufuata kanuni hizo litatatulika tu.
Hivyo wewe kama mwanamke, itambue huduma hii iliyopewa na Bwana, laiti kama wanawake wote, wangekuwa ni wa kujiwajibisha kwa namna hii, jamii zetu na familia zetu zisingekuwa na migogoro mingi,wala injili isingekuwa ngumu sana kuihubiri kwasababu tayari walishatangulia walioweka misingi bora nyuma. Hii ni huduma kubwa sana kwa mwanamke na Bwana anaithamini sana.
Simama katika nafasi yako wewe kama mama, wewe kama Dada, nyumba au familia itasimama, endapo wewe utasimama.
Bwana akubariki
Shalom.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
MAFUNDISHO KWA WANAWAKE
MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?
Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?
BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.
Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
Ikiwa wewe una kazi ya kusimama madhabahuni/Mimbarani mara kwa mara kuwahudumia watu wa Mungu, basi ujue umewekwa mahali pa heshima sana, lakini pia pa kuwa makini sana. Kwa namna gani? Mahali pa heshima kwasababu ndio sehemu Mungu hushukia kuwahudumia watu wake, Hivyo wewe unakuwa kama lango la kwanza la Mungu, kusema au kutenda kazi kwa watu wake. Lakini pia usipopatumia ipasavyo una hatari kubwa sana ya kuuharibu utukufu wa Mungu. Na matokeo yake ni kuliathiri kundi zima kabisa, au ibada yote kutokuwa na maana.
Mara nyingine ibada kutofikia kilele cha Roho Mtakatifu, sio wale watu wasikiao kutokuwa makini, hapana ni kutokana na wahudumu kutokuwa na maandalizi ya kutosha ya kiroho na ki-mwili pindi haudumupo. Kwa mfano ikiwa wewe ni mhubiri/Mchungaji, na unajua unaingia katika semina, au jumapili utahudumu, halafu inafika asubuhi ya jumapili ndio uwaza ni nini cha kwenda kufundisha. Unaanda somo dakika 15tu, kisha unakwenda kusimama kuwahudumia watu wa Mungu, ambao wanatazamia walishwe Neno litakalowageuza maisha yao. Hapo ndugu usijidanganye, kuhudumu kwa namna hiyo sio kama Bwana anavyotaka.
Kumbuka kuwa machachari madhabahuni, kuwa na sauti kubwa, kuwa na uwezo wa kutoa vionjo mbalimbali, na watu kushangilia na kuruka-ruka, wakasema AMEEEN! Kubwa, ukadhani hiyo ndio ibada iliyowabariki watu. Hapo umejidanganya. Ibada isiyo na maandalizi haijalishi, imewarukisha watu kiasi gani. Hakuna uvuvio wa Roho!.
Ibada inaweza isiwe na makelele yoyote, mhubiri akawa ni mwenye kigugumizi, lakini ikiwa imeandaliwa vema kiroho. Maneno machache yanaweza yakawa na maana zaidi ya maneno elfu, na ya milio ya vinanda na gitaa. Watu wakajengwa, wakaguswa, wakafarijiwa, roho zao kwa namna ambayo wewe mhubiri unaweza ukadhani hujafanya jambo lolote. Isipokuwa wao wenyewe ndio wanaelewa mioyoni mwao.
Hivyo epuka njia za kisiasa na za kijamii, katika habari za kiroho. Mungu anataka amwachie Roho wake Mtakatifu kushughulika na hali za mioyo ya watu. Hivyo ni lazima ujue namna ya kumwandalia mazingira hayo Roho wake, ili afanye kazi kama apendavyo.
Kama wewe ni mhudumu yoyote, aidha mhubiri/ mwana-kwaya. Jifunze kuwa na maandalizi marefu. Andaa somo lako, ukianza siku kadhaa kabla, au kama umetingwa sana, siku moja kabla, ukitenga saa za kutosha za kukaa uweponi kwenye utulivu walau SAA 4-5, tena ikizidi hapo inakuwa ni vizuri zaidi. Katika hizo, Tumia saa 2 na nusu Kuombea Somo na ibada, tena Tumia Saa 2 na nusu kuandaa somo lako. Ikiwa mchana kuna usumbufu, Muda wa usiku ni mzuri zaidi.
Sasa katika maombi yako omba Roho Mtakatifu akufanyie mambo yafuatayo;
Wakati mwingine unaweza ukawa na somo lako kichwani, hiyo ni vema. Lakini liondoe hilo kwanza, msihi Roho Mtakatifu akufunulie alilolikusudia kuwafikia watu wake siku hiyo. Na kwa kufanya hivyo aidha atakupa jipya kabisa pale utakapokuwa unatafakari, au ataliboresha hilo ulilokuwa umeliwaza, au siku ile ile atayazungumza maneno mapya kwa kinywa chako. Hivyo usikimbilie moja kwa moja kuhitimisha na kile ulichokipanga kukisema. (Yohana 16:13)
Ni rahisi kama mwanadamu, kuhubiri mawazo yako, au injili nusu-nusu, aidha kwa kuwaogopa watu, au kuwapendeza watu, au kuwahurumia watu. Hivyo omba Bwana akusaidie hapo. Ili usilighoshi Neno lake na mawazo au hisia zako. Bwana Yesu alisimamia kweli katika mafundisho yake yote.
Yohana 8:40 Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo.
Yohana 7:7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu
Wakati mwingine lazima tuombe kuhubiri kama Bwana alivyohubiri. Yeye alitumia mifano mingi katika kuwasilisha Neno la Mungu. Na sisi pia hatuna budi kumwomba Roho Mtakatifu atujalie hekima hiyo. Husaidia sana watu kulielewa Neno kiurahisi na kulifurahia. Ukiomba Roho Mtakatifu anaweza kukufunulia wakati unaandaa somo, au wakati ule ule utakaokuwa unafundisha.
Marko 4:33 “Kwa mifano mingi ya namna hii alikuwa akisema nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulisikia; 34 wala pasipo mfano hakusema nao;..”
Maneno yenye uweza, ni maneno yenye mamlaka. Bwana akitujalia karama hii ambayo ilikuwa ndani ya Yesu, tutaweza kuitiisha madhabahu, na watu kulisikiliza Neno la Mungu kwa hofu ya Mungu, na kwa nidhamu, na kwa bubujiko, mpaka watu Kuokoka na kuacha maovu.
Luka 4:32 “wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo”.
Katika kuhubiri kwako ni muhimu sana, kuomba jina la Yesu litukuzwe. Wahubiri wengi wasimamapo hujijengea mazingira yao ili watukuzwe. Ili waonekane wanaupako, wanashuhuda n.k.. Lakini sio Kristo ainuliwe. Msihi Mungu akupe unyenyekevu madhahabuni pake, Ibada isiyo mtukuza Kristo, haijalishi itakuwa na uzuri kiasi gani, ni bure. Watu watoke wamemwona Kristo na sio mtu au vitu (Wakolosai 3:17).
Tuhudumupo hatuna budi kumwomba Mungu daima atupe upambanuzi, ni maombi ya daima, inaweza isiwe katika ibada zote, lakini pale ambapo anataka kufanya jambo basi atupe kuona rohoni. Ili tuweza kutembea katika wazo lake. Kwamfano labda mtu anatatizo Fulani, na Bwana anataka afunguliwe kwa wakati huo. Hivyo ni vema tumwombe Mungu karama hii. (Yohana 16:30)
7) Bwana akujalie usiathiriwe na mazingira:(Dk 15)
Mazingira huwaarithi wahudumu, kwamfano pale unapoona watu hawazingatii unachowafundisha, wengine wamelala, au mazingira ya sauti za mbali, au watu wanaozungumza, janga Fulani n.k.. Huweza kukutoa katika umakini wa Roho Mtakatifu. Hivyo Bwana akufanye kipofu katika eneo hilo ili usiuzimishe mtiririko bora wa Roho Mtakatifu. Adui hupenda kutumia mbinu hii, kukuvuruga. (Matendo 20:7-12)
Omba Kwa kupitia mahubiri au mafundisho watu wafunguliwe, waponywe, wabarikiwe, wafarijiwe, ishara. Ibada isiwe baridi, au ya maneno matupu tu. Shuhuda zitokee, ili watu wamtukuze Mungu.
Luka 5:17 Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya
Adui huwawinda sana wahudumu, na wahubiri na hivyo mishale mingi huwa inatumwa rohoni kukuvuruga, aidha kihisia, au kiafya, au kiakili. Omba Bwana akuzungushie wigo wake. Uchawi wowote, au roho zozote nyemelezi zisipate nafasi ya kupakaribia pale ulipo, au kuvuruga unachokifundisha. (Zaburi 127:1)
Kumbuka maombi haya sio kwa wahubiri tu, bali pia kwa wengine wote wahudumuo, kama vile Wana-kwaya, waalimu wa watoto, vijana, wakina-mama, wainjilisti, wamishionari.n.k. maadamu unahudumu hakikisha unakuwa na maandalizi, ili huduma yako isiwe bure. Zingatia sana maandalizi ya muda mrefu. Ukimaliza walau Dakika hizo zote 135 kwenye maombi. Sawa na SAA MBILI NA NUSU. Ukatumia tena muda kama huo kuandaa chakula chako cha kiroho. Utajiweka vizuri sana Roho Mtakatifu kufanya kazi vema kupitia wewe.
Bwana akubariki. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Pia tazama >>> JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI
Bwana
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?
Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha
NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?
Nini maana ya kuabudu?
EPUKA KUCHELEWA IBADA.
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Ikiwa wewe umeokoka, na una kiu kweli ya kumkaribia Mungu wako katika viwango vya juu. Basi fahamu huna budi ujikuze kiroho. Na ukuaji huo hutegemea mambo mawili makuu “Neno pamoja na maombi”. Katika tovuti hii yapo mafundisho mbalimbali yatakayokusaidia kupiga hatua hizo.
Makala hii imeegemea zaidi katika Maombi. Hivyo huu ni mwongozo wa Wiki kwa Wiki, mfululizo wa vipengele muhimu vya kuombea. Uwapo nyumbani, uwapo kanisani. Jiwekee ratiba Kisha kuwa mwombaji. Na hakika baada ya wakati fulani utaona matokeo makubwa sana ndani yako.
Mwendelezo utakuja…
MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.
MAFUNDISHO MAALUMU KWA WAONGOFU WAPYA.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Orodha ya mafundisho yote.
KUONGOZWA SALA YA TOBA
Makwazo ni mambo yanayozuia mwendelezo wa jambo Fulani lililokuwa limekwisha anza, au linalotaka kuanza. Kwamfano ulikuwa unasafiri lakini ghafla kwenye safari yako unakutana na mto mpana, unaokufanya ushindwe kuvuka, hicho kinaitwa kikwazo. Au ulikuwa unapika chakula chako, halafu ghafla gesi ikaishia katikati na chakula bado hakijaiva, hicho kinatiwa kikwazo.
Na rohoni pia vivyo hivyo yapo makwazo ambayo yanamzuia mtu asimalize mwendo wake wa imani, au asiendelee mbele tena katika kumtafuta Mungu. Na muhimu sana kuyajua na kujiepusha nayo.
Kibiblia makwazo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu.
Tukianzana na hilo kundi la kwanza, wapendwa tunaowazungumzia hapa ni wale ambao hawajasimama vema katika kweli. Ndio hawa ambayo Bwana Yesu anawazungumzia katika vifungu hivi;
Luka 17:1 Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake! 2 Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa. 3 Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. 4 Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Kwa namna gani hawa wanaweza kumkosesha ndugu. Kwamfano ni pale, Mpendwa mwezako anaposikia umemsengenya, Sasa Kama ni mdhaifu kiimani Hili linaweza kuwa ni kwazo kubwa sana kwake ambalo likamfanya hata nguvu yake ya kuendelea kudumu katika kusanyiko ikapoa. Zipo shuhuda nyingi sana za wapendwa ambao wamerudi nyuma kiwokovu kwasababu ya maisha haya. Hivyo kama mwanaminio hakikisha, kinywa chako, unakichunga. Jifunze kuwa na kiasi na uvumilivu. Jifunze kujiepusha na mambo mabaya Kwa wapendwa wenzio.
Kwazo hili linaweza pia kuwa katika ufahamu wa kiroho .
Utakumbuka Ayubu, alipopitia majaribu yake mazito, hakuna mahali popote alinena maneno yasiyo faa, lakini wale marafiki zake watatu, yaani Sofari, Elifazi na Bildadi, (ambao wanawawakilisha watumishi wa Mungu), walipofika, walitumia ujuzi wao wa kibinadamu kumuhukumu Ayubu, kwamba ni kwasababu alitenda dhambi, hiyo ikampelekea Ayubu kunena hata maneno yasiyofaa.
Kama mtumishi wa Mungu, epuka hukumu ya macho,ukiletewa tatizo la mtu/ watu, usiangalie kwa jicho la nje, mwingine ni Mungu mwenyewe anampitisha katika madarasa yake, ukajikuta badala ya kutatua tatizo ndio unaongeza tatizo juu yake. Usianze kuhukumu matukio, bali kuwa katika Roho, tegemea zaidi uongozo wa Roho Mtakatifu. Hekima itakusaidia.
Pia lipo katika ujuzi.
Ukisoma Warumi 14, maandiko yanaeleza kwa upana jinsi ujuzi wetu unaweza kuwa kwazo kwa wengine wadhaifu was imani, kwamfano wewe ukipewa chakula ambacho umesikia kimepitishwa kwenye matambiko, ukashukuru, ukakila, ukijua kabisa chakula hakiwezi kukuondoa kwenye mpango wa Mungu. Lakini kwa ujuzi huo mwingine mwenye imani haba akakuona, na yeye akaanza kula vyakula vya kimatambiko na mila, akajikuta anashirikiana na uganga na mizimu, utakuwa umemsababishia kwazo kubwa kwa Mungu.
Lolote tunalolifanya, lazima tuangalie wengine wanaiga nini kwetu sisi wenye ujuzi. Uvaaji wako, wewe kama mkristo, unaweza ukajiona hauna shida kwako, lakini wengine wakaona ni sawa, hata kuvaa mavazi hayo ambayo hayana utukufu mbele za Mungu, utakuwa umefanyika kwazo kwao
Wapagani wanaweza kuzuia injili, isihubiriwe mahali, wakawapiga au wakawafunga watu wa Mungu n.k. Utaona Herode alimpinga Yohana akamweka gerezani hakuweza tena kuhubiri injili, wapagani waliwapinga watakatifu wengi. Hata mitume katika ziara zao walikutana na vikwazo vingi kutoka kwa watu wa mataifa, mahali pengine hawakuweza kuhubiri kwa utulivu (1Wakorintho 15:32, 1Wathesalonike 2:2).
Watu ambao hawajakamilika katika imani. Kwamfano ni mpendwa lakini mzinzi, sasa wale watu wa nje, ambao walikuwa wanakaribia kuvutwa katika imani, wanapoona matendo ya watu kama hawa, wanasema kama ukristo wenyewe ndio huu ni heri niendelee kuwa mpagani. Hayo ni makwazo. Au unakuta mwingine ni tapeli, mwingine ni mtukanaji, mambo kama haya hufanyika kwazo kubwa sana kwa wapagani kuihubiri injili.
2Wakorintho 6:3 Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe; 4 bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;
Hitimisho:
Hivyo wewe kama ni mkristo jitahidi sana kuyaepuka makwazo kwa waaminio wenzako au kwa wapagani. Lakini pia kama ulikwazwa na ndugu yako, basi, suluhisho sio kuvunjika moyo au kuuacha wokovu, bali ni kunyanyuka tena na kuendelea mbele. Biblia inasema;
Mithali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Amka tena, mtumikie Bwana, kwasababu alishatujuza tangu mwanzo kwamba hayana budi kuja, hivyo hilo liwe ni jambo la kawaida kwako, jitie nguvu uendelee mbele.
Mpagani ni nani?
USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.
Kutoka 21:10 ina maana gani?
Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).
MIMI SIOMBI KWAMBA UWATOE KATIKA ULIMWENGU.
HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.
KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.
Neno hilo utalisoma katika andiko hili;
Yohana 19:13 Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha
Maana ya Gabatha ni “eneo lililoinuka”. Ni sehemu iliyojengwa mbele ya jumba la kifalme la Pilato ambapo hukumu zake alizitolea hapo. Kama biblia inavyosema paliitwa sakafu ya mawe. Maana yake palikuwa ni eneo la sakafu iliyojengwa kwa mawe. (Tazama picha juu).
Hapo ndipo hukumu ya Bwana wetu Yesu Kristo ilipotolewa ya yeye kusulibiwa.
Lakini jambo ambalo unapaswa utafakari kuhusiana na tukio hilo, ni kuwa Mungu, ambaye ndiye muhukumu wa wanadamu wote, anasimama mbele ya kiti cha hukumu cha wanadamu kuhukumiwa. Mungu kukubali kuhukumiwa Ni ishara ya unyenyekevu usiokuwa wa kawaida. Na hapo tunathibitisha kuwa hukumu za wanadamu hazitendi haki. Lakini utafika wakati na yeye mhukumu mkuu ataketi katika kiti chake cha enzi kuwahukumu wanadamu wote. Ambapo kwa haki kila mtu atalipwa sawasawa na matendo yake.
Jiulize wakati huo utakuwa upande upi?. Kwake hakuna upendeleo wa kibinadamu kama alivyofanya Pilato kwa wayahudi, kwake hakuna rushwa, kwake hakuna siri, yote yatamulikwa na kuwekwa wazi, na kama jina lako halipo katika kitabu cha uzima, utatupwa katika lile ziwa la moto, ambapo utateketea huko usiku na mchana.
Ufunuo 20:11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Je! Umejiandaaje kukutana na mhukumu wa haki? Kumbuka huwezi kuokoka, ikiwa bado upo nje ya Kristo Yesu. Unachopaswa kufanya ni kutubu leo, ili upate ondoleo la dhambi zako. Ndipo kuanzia huo wakati na kuendelea uwe na amani na Mungu wako,. Hakuna ukombozi kwa yoyote Yule zaidi ya Yesu Kristo.Huwezi kuokoka kwa nguvu zako mwenyewe. Yesu alikufa tayari kwa dhambi zako, ili aziondoe, akuhesabie sio mkosaji.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Bwana maisha yako ayaokoe na kuyaongoza, Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)
Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?
Chetezo ni nini katika biblia? (Walawi 10:1)
“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?
Kila mwanadamu, kuna aina Fulani ya mizigo anayo. Mizigo tunayoizungumzia hapa sio mizigo ile ya dhambi n.k. Hapana, bali ile ya kimajukumu. Kama vile utafutaji wa rizki, kodi, ada, elimu, ujenzi n.k. Hii ni mizigo ambayo inatufanya tusiwe katika hali Fulani ya utulivu.
Wakati mwingine haiepukiki, ni lazima tukumbane nayo. Lakini kosa linafanyika ni pale tunapotaka kuibeba mizigo hiyo yote ndani ya siku moja. Au tuyatatue matatizo yote kwa kipindi kifupi.
Ukiwa mtu wa namna hiyo hata ukiwa tajiri wa namna gani, Bado utaona maisha ni magumu, tena yenye shida na taabu isiyokuwa ya kawaida, na wengine wanaishia hadi kujinyonga kwa namna hii. Kwasababu gani? Kwasababu Mungu hajatuumbia tuibebe mizigo kwa namna hiyo? Leo tutaona ni kwa namna gani tunaweza kuibeba mizigo yote.
Kwamfano unapofikiria, changamoto za chakula cha mwaka mzima uzimalize leo, hivyo unafikiria ni wapi utapata pesa ya kununua mapipa 5 ya mahindi, wakati huo huo unafikiria ada za watoto za miaka 5 mbele itakuwaje, hivyo unahangaika uzipate nazo leo, tena wakati huo huo unafikiria uende katika mafunzo ya kujiongezea aina 7 za elimu, ambazo ungepaswa uzisomee kwa miaka 10, unataka uzimalize ndani ya miezi 3. Tena uanze kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanja vya watoto wako watano, ambapo ndio kwanza wananyonya, na wengine wapo tumboni.
Yaani kwa ufupi ufanye mambo yote chap-chap ndani ya kipindi hiki hiki kifupi. Ukweli ni kwamba kamwe hutakuwa na raha katika maisha yako. Utaona maisha ni mazito sana, hayabebeki, hata kama utakuwa unapata vingi kiasi gani. Kumbuka, Kusema hivi haimaanishi tusifikirie kuwekeza, hapana, lakini fikiria hivyo tayari kipo mkononi, lakini kama hakipo, usijijengee akili hiyo.
Hivyo Mungu ametusaidia kwa kutupa njia ya kuibeba mizigo hiyo yote. Nayo si nyingine zaidi ya ile ya “kuimega siku kwa siku”.
Luka 11:3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.
Bwana ameivunja vunja mizigo yetu katika siku. Ametaka kukupa rizki ya siku, kesho usiwe na presha nayo sana, Bwana ataifungulia milango yake, amekupa ada ya muhula mmoja, shukuru, ile ya muhula wa pili ikifika atakupa, usiwe na wasiwasi wa ada ya miaka 3 mbele, utapata ugonjwa wa moyo. Acha hata kufikiria kodi ya miaka 2 mbele, ikiwa umejaliwa ya mwezi mmoja, shukuru. Hujui mwaka ujao utahama hapo, au Bwana atakufungulia milango ya Baraka zaidi ukanunua pako.
Jukumu lolote ulilonalo, embu livunje vunje kwenye vipindi vifupi, Kwasababu hujaumbiwa uibebe mizigo yote kwa wakati mmoja. Ukiitabikia sana “kesho yako” leo, ujue unajijengea mazingira ya stress.
Ni kwa faida yako mwenyewe., Lakini ukiwa mtu wa kushughulika na siku yako utashangaa tu mbeleni umeweza litatua hilo tatizo kubwa kirahisi, kwa njia mbalimbali Mungu atakazokufungulia, kwasababu ni hekima ya Mungu imetumika hapo si ya mwanadamu.
Mathayo 6:31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
Fahamu Namna ya Kuomba.
Kupiga ramli ni nini katika biblia?
Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)
Mungu mara nyingi huwa anatumia lugha ya picha au maumbo, ili kutupa sisi uelewa mzuri kuhusiana na mambo ya rohoni. Kama tunavyojua inapotokea mtawala, labda raisi amekualika uketi pamoja naye meza moja ule chakula, ni wazi kuwa kwa tendo hilo litakuwa limekupandisha hadhi sana.
Sasa zamani, za wafalme ilikuwa mtu aliyepewa heshima kubwa aliwekewa kiti chake kidogo pembeni mwa mfalme upande wake wa kuume. Na hiyo ilikuwa inamaana kubwa zaidi ya heshima peke yake, bali pia ilimaanisha kupewa mamlaka.
Hivyo katika biblia unapokutana na “mkono wa kuume” Mungu ametumia picha hiyo kumaanisha aidha mambo haya makuu matatu;
1. HESHIMA.
Maandiko kutuambia Kristo, ameketi mkono wa kuume wa Mungu, ni kutuonyesha, hadhi na ukuu alionao sasa. Mbinguni wapo malaika wengi wenye nguvu, wapo wenye uhai wanne, wapo maserafi na mamilioni ya malaika, lakini hakuna hata mmoja alipewa hadhi ya kuwa karibu/sawa na Mungu zaidi ya Kristo, Bwana wetu.
Waebrania 1:13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Kwahiyo, aliyepokea heshima, ya juu zaidi ya viumbe vyote ni Kristo Yesu Bwana wetu. Na ndio maana tunamwabudu na kumtukuza. Na heshima zote na shukrani zinamwelekea yeye tu peke yake. Ndiye Mfalme wa Wafalme, na Bwana wa Mabwana. Hafananishwi na mwanadamu yoyote duniani, au malaika yoyote mbinguni.
2. MAMLAKA.
Lakini pia mkono wa kuume sio tu heshima bali pia huwakilisha mamlaka, Kuketi kwake kule, ni kuonyesha mamlaka ya kumiliki na kutenda jambo lolote na kutiisha vitu vyote chini yake anayo.
Waefeso 1:20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote
> Vilevile anayo mamlaka ya kutuombea na kutuondolea dhambi, kama kuhani mkuu,
Warumi 8:34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
>Mamlaka ya kutumwagia vipawa vya rohoni na nguvu ya kushuhudia habari njema.
Matendo 2:33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia,
Luka 16:19 Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. 20 Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo
3. ULINZI.
Uwapo karibu na mfalme, maana yake upo salama, chini ya mfumo wa ulinzi wake. Hivyo Mungu kumweka Kristo kuumeni mwake ni kutuonyesha sisi,ufalme wa Kristo hauhasiki. Na wanaompinga kazi yao ni bure. Na Mungu atawaweka maadui zake chini ya miguu yake.
Zaburi 110:1 Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.
Lakini jambo ambalo watu wengi hawajua ni kwamba Bwana anataka na sisi tumweke yeye mkono wetu wa kuume, maana yake tumpe heshima yake, katika mambo yetu, na yeye, atatuheshimisha, atatuinua, na atatulinda.
Matendo 2:25 Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.
Usiweke Mali kuumeni kwako, usiweke elimu, au mwanadamu kuumeni kwako. Bali Kristo tu peke yake.
Unaweza pia kupitia vifungu hivi Kwa maarifa zaidi; Mathayo 22:44 , Matendo 7:55, Wakolosai 3:1, Waebrania 1:3,13, 10:12, 1Petro 3:22.
Je! Kristo yupo kuumeni kwako? Fahamu tu ili Kristo awe pembeni yako, na wewe pembeni yake wakati wote, ni sharti uwe umeokoka. Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu (, yaani kukubali kuacha njia mbaya), na hapo hapo unaupokea msamaha wa dhambi, kisha Kristo anaingia moyoni mwako. Na baada ya hapo unaitimiza haki yote kwa kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu, na Roho atakuwa tayari ameshakuja ndani yako kuanzia huo wakati na kuendelea. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo akusamehe dhambi zako, basi fungua hapa kwa mwongozo mfupi wa sala ya toba>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ubarikiwe.
Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?
Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?
Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?
NI KWASABABU YA YESU KRISTO.
SWALI: Siku ya kwanza Mungu aliumba Nuru, Je ilitokea wapi wakati Tunafahamu jua ambalo ndio lenye kutoa Nuru liliumbwa siku ya Nne?(Mwanzo 1:14-19)
Mwanzo 1:3-5
[3]Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. [4]Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. [5]Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
JIBU: Mungu si kama sisi wanadamu ambao tukitaka kuunda jambo ni lazima tuwe na chanzo Fulani husika. Kwamfano hatuwezi kumleta mtu duniani Kwa kumchukua mwanamke na kumfungia ndani tu peke yake bila mwanaume tukitarajia baadaye ajifungue .
Lakini Mungu ni tofauti anaweza kumpa uzao pasipo kumkutanisha na mwanaume. Tunaona alifanya Kwa Mariamu. Lakini ameamua kuunda njia rasmi ya sisi kuzaliana, ambayo ndio hiyo ya watu wawili kukutana.
Vivyo hivyo na pale mwanzo Mungu kutanguliza Nuru, SI jambo la kushangaza kwake. Yeye ni mweza wa yote, Dunia hii ingeweza kumulika sikuzote Daima pasipo kutegemea jua Wala mwezi Wala nyote.
Lakini aliamua aviundie na chanzo chake, Kwa lengo la kutenganisha majira.
Lakini pia ni vema tukapata ufunuo, wa tukio lile, Nuru Ile ilimwakilisha nani. SI mwingine zaidi ya Yesu. Kumbuka Yesu katika agano la kale alijifunua katika maumbo. Lakini katika agano jipya waziwazi. Hivyo ilihitaji Nuru iwepo ili shughuli zote za uumbaji ziendelee.
Yohana 1:1-5
[1]Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.[2]Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. [3]Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. [4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
Je! Kristo Ameangaza ndani Yako? Tambua kuwa pasipo Kristo hakuna maisha, hakuna uhai, Tubu Leo mgeukie Kristo Akusamehe dhambi zako.Ili uumbwe upya na Mungu. Hivyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa fungua hapa Kwa mwongozo wa Sala ya Toba>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Nini maana ya huu mstari Ayubu 23:10 ‘Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu’?
Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?
JE UMEKUFA PAMOJA NA NANI?
JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?
Je ni sawa kuomba novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia?
Kwanini Mungu anasema tusiwe na ‘tabia’ ya kupenda fedha? Tuwe radhi na vitu tulivyo navyo?. Ujasiri gani unaotaka kutuaminisha kwa kauli hiyo katika zama hizi ambazo tunajua bila fedha huwezi kutatua changamoto nyingi za kimaisha?
Waebrania 13:5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. 6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
JIBU: Ametuagiza hivyo kwasababu ya hakikisho alilotuahidia katika kauli yake aliyosema “sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”. Ukiitafakari kauli hiyo haimaanishi kuwa hatutakaa kamwe kupitia vipindi vya kupungukiwa, hapana, lakini anasema sitakupungukia ‘kabisa’, yaani ikafikia hatua ya kukosa kabisa hitaji Fulani, mpaka kufa na kuwa omba-omba barabarani, hapo hatutapafikia.
Daudi anasema..
Zaburi 37:25 Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa Wala mzao wake akiomba chakula
Umeona ameahidi kuwa nasi nyakati zote,
Ni kweli upo wakati ambapo ukiitazama baadaye yako au kesho yako unaona giza, lakini bado Bwana anasema usiwe na hofu, kwasababu hiyo kesho yenyewe itajisumbukia, yeye mwenyewe atatengeneza njia ya namna ya kukusaidia katika siku hiyo uliyopo.
Lakini ubaya ni pale ambapo tutataka Mungu atupe sawasawa na wingi tunaoutarajia. Kibiblia hilo sio hakikisho la Bwana, anaweza kukupa cha wakati huo tu, au akakupa zaidi ya hivyo ulivyomwomba. Ni jinsi yeye apendavyo, na anafanya hivyo kwa sababu zake mwenyewe ambazo ni njema kwako, lakini mwisho wa siku yote yatakuwa sawa tu, usiwe na hofu.
Pia ni vema kufahamu kuwa kauli hiyo haitufanyi sisi kuwa wavivu tusubirie tu kitu kutoka kwake. Hapana, anataka tujishughulishe katika sehemu mbili.
Sehemu ya kwanza ni kuutafuta ufalme wake, na haki yake.
Mathayo 6:33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Yaani uwe katika utumishi wa Bwana, unamtafuta na unaifanya kazi yake, kama vile mwajiriwa, alivyo katika utumishi wake. Ukifanya hivyo kwa uaminifu Bwana hawezi kukupungukia kabisa atakupa tu rizki yako, kwa njia zake mwenyewe.
Na sehemu ya pili ni aidha tuwe katika kufanya kazi za mikono. Tunapojishughulisha, na kitu Fulani cha kutupatia kipato, Bwana atatusaidia huko huko, tutajazwa mema yake.
Na kwasababu Bwana hataki mioyo yetu izame kule moja kwa moja, anataka tupate na nafasi ya kumfanyia ibada, na ndio maana ameahidi hatatuacha kabisa, Hivyo usione shida kufunga biashara yako, na kwenda kwenye maombi muda wa maombi ufikapo, jumapili kuahirisha kazi zako zote na kwenda nyumbani kwa Bwana, ondoa hofu kuwa utapoteza wateja. Kumbuka tu ile kauli ya sitakuacha kabisa, wala kukupungukia kabisa.
Hata kama utapoteza hiyo, Bwana atakufungulia rehema zake na kukupatia iliyo bora zaidi ya ile.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa wewe kama mwana wa Mungu, hupaswi kuweka moyo wako kwenye mali au fedha, yaani kufikiria kwamba bila kuwekeza sana maisha yako huko utapata shida mbeleni. Hapana, bali upatapo kingi au kidogo, basi ridhika maadamu Kristo yupo ndani yako, ameahidi kukusaidia nyakati zote.
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.
JUA HALITAKUPIGA MCHANA, WALA MWEZI WAKATI WA USIKU.