Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu wetu lililo Mwanga wa Njia zetu, na Taa iongozayo miguu yetu (Zaburi 119:105).
Neno hili lililo Taa linasema..
Yuda 1:5 “Tena napenda kuwakumbusha, ijapokuwa mmekwisha kujua haya yote, ya kwamba Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, ALIWAANGAMIZA BAADAYE WALE WASIOAMINI”
Maandiko hayo yanatufundisha kuwa KUOKOLEWA sio Mwisho wa safari. Kwani ni kweli wana wa Israeli waliokolewa kutoka Misri jeshi lote.. lakini si wote walioingia nchi ya Ahadi, bali watu wawili tu ambao ni Yoshua na Kalebu, na watoto wao ambao walizaliwa jangwani, lakini wengine wote MUNGU aliwaangamiza jangwani ijapokuwa aliwatoa Misri.
Leo wanaookolewa ni WENGI, wanaomkiri YESU ni wengi!, lakini pia ni wengi wanaoangamizwa na Bwana, kwasababu ya kutotembea na Mungu katika wokovu wao.
Wengi wa wana wa Israeli walijaa viburi (Mfano wa Dathani na Kora, soma Hesabu 16:1-50) na wengine walijaa mioyoni mwao manung’uniko na ibada za sanamu, na wengine walikuwa ni watu wa kumjaribu Mungu kila wakati..ingawa wote walikuwa wameokoka na utumwa wa Farao, lakini kwa bahati mbaya hawakuiona ile nchi ya Ahadi.
WALIOKOLEWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA!…. WALIFUNGULIWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA…. WALIPONYWA lakini baadaye WALIANGAMIZWA… Na jambo linalohuzinisha Zaidi ni kwamba waliangamizwa jangwani wakiwa bado wanakula Mana (Baraka za mbinguni), Vile vile waliangamizwa wakiwa chini ya WINGU NA NGUZO YA MOTO (Upako na Utumishi) na Zaidi ya yote walikuwa wameshabatizwa katika roho katika bahari ya Shamu.
Mambo haya yanabaki kuwa funzo na onyo kwetu ili tusifanya makosa kama hayo, kama maandiko yasemavyo..
1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; 2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; 3 wote wakala chakula kile kile cha roho; 4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. 5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. 6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. 7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. 8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. 9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. 10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu. 11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. 12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;
2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;
3 wote wakala chakula kile kile cha roho;
4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.
5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.
6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.
7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.
8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.
10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.
11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
Je unajivunia ubatizo?… Unajivunia dhehebu?…unajivunia Karama uliyo nayo?… unajivunia upako?.. Vyote hivyo wana wa Israeli walikuwa navyo, lakini wengi wao waliangamizwa.
Utakase ukristo wako, kaa mbali na dhambi!, usimjaribu Mungu, usiabudu sanamu baada ya kuokoka, jitenge na mambo ya ulimwengu, tembea na Mungu kama Yoshua na Kalebu, na Bwana atusaidie sote katika hayo.
Amen.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.
Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)
MNGOJEE BWANA
ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.
NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.
Rudi Nyumbani
Print this post
Swali: Neno “Kututa” lina maana gani kama tusomavyo katika Mhubiri 2:26?
Jibu: Turejee..
Mhubiri 2:26 “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KUTUTA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
“Kututa” maana yake ni “KULIMBIKIZA”..
Kwahiyo maneno hayo tunaweza kuyaweka katika Kiswahili hiki.. “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KULIMBIKIZA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
Andiko hili linatufundisha hatari ya kukusanya mali na kulimbikiza, ikiwa tupo nje ya KRISTO. Kwa maana hapo maandiko yanasema, mali za mtu huyo (mkosaji), alizojikusanyia na kujilimbikizia, atanyang’anywa na kupewa yule Mungu aliyemridhia.
Lakini pia mstari huo unatuonyesha thawabu kuu ambazo Mungu humpa yule aliyemridhia. Na hizo si nyingine Zaidi ya HEKIMA, MAARIFA na FURAHA.
Kabla ya kumpa mtu Mali humpa Hekima, Maarifa na Furaha na hivi vitatu ndivyo vitu vya kuvitafuta kwa MUNGU kabla ya kuomba vitu vingine kama Mali. Kama Sulemani aliomba Hekima kwanza na Mungu akampa Hekima na Mali ikawa ni nyongeza.
Hali kadhalika na sisi hatuna budi kutafuta hekima, Maarifa, Ufahamu na Furaha kwa bidii kwani tukiyapata hayo basi hayo mengine tutazidishiwa, na hata tusipoyapokea, bado hekima na maarifa vitabaki kuwa utajiri mkuu.
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. 14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi. 15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye. 16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto. 17 Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani. 18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.
16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.
17 Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”
Tafuta Hekima, tafuta Maarifa, tafuta Ufahamu, Busara na Furaha..
Bwana atusaidie.
Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?
NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?.
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.
Swali: Katika Kutoka 3:2 tunasoma kuwa Mungu alisema na Nabii Musa kupitia kile kijiti ambacho kilikuwa kinawaka moto lakini hakikuteketea, je kulikuwa kuna sababu gani au ufunuo gani katika ishara ile?
Jibu: Tuanze kusoma mstari ule wa kwanza mpaka ule wa tatu, ili tupate kuielewa vizuri habari..
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. 2 Malaika wa Bwana akamtokea, KATIKA MWALI WA MOTO ULIOTOKA KATIKATI YA KIJITI; AKATAZAMA, NA KUMBE! KILE KIJITI KILIWAKA MOTO, NACHO KIJITI HAKIKUTEKETEA. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei”
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
2 Malaika wa Bwana akamtokea, KATIKA MWALI WA MOTO ULIOTOKA KATIKATI YA KIJITI; AKATAZAMA, NA KUMBE! KILE KIJITI KILIWAKA MOTO, NACHO KIJITI HAKIKUTEKETEA.
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei”
Lengo la Mungu kumwonyesha Musa Ono hilo kubwa, halikuwa kumburudisha au kumsisimua, bali ulikuwa ni ujumbe wa MUNGU kwa Musa na kwa Israeli wote ambao watasumiliwa baadae.
Na ujumbe huo si mwingine Zaidi ya ule tuusomao katika Isaya 43:1-4..
Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. 2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA. 3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. 4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”
Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA.
3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako.
4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”
Hapo katika mstari wa Pili (2) anasema… “UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA”.
Na hiyo ndio sababu ya Mungu kumwonesha Musa ono lile, kwamba watakapopita (wana wa Israeli) katika Moto (yaani majaribu mbalimbali) hawataungua..mfano wa kile kijiti kilichowaka moto lakini hakikuteketea.
Hivyo kwa ufunuo huo Israeli walielewa kuwa Mungu anasema nao, kwamba atakuwa pamoja nao katika mapito yote, hivyo wasiogope majaribu wala moto watakaokutana nao, kwani hautawateketeza, kinyume chake utawateketeza maadui zao…mfano wa akina Shadraka, Meshaki na Abednego, ambao walitupwa katika tanuru la moto, na badala ya moto ule kuwala wao, uligeuka na kuwala maadui zao wale walioshika na kuwatupa motoni.
Danieli 3:20 “Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto. 21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto. 22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego. 23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. 24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme. 25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu”
Danieli 3:20 “Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego.
23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu”
Ni hivyo hivyo hata sasa, Mungu anawalinda wale wote wamwaminio na kumtumainia yeye, wanakuwa kama kijiti kilichopo motoni lakini hakiteketei.. Wengine wakipitia majaribu wanapotea kabisa, lakini watu wa Mungu wanapita katikati ya moto na wanatoka salama.
Je umempokea Bwana YESU?. Je yeye ni tumaini lako na ngao yako?..Kama upo nje ya Kristo fahamu kuwa Moto utakuunguza, na ibilisi atakumaliza. Lakini ukiwa ndani ya YESU utakuwa salama.
Mpokee YESU kama bado hujampokea, hizi ni siku za mwisho naye amekaribia kurudi sana.
Waebrani 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. 38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”.
Waebrani 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
DUNIANI MNAYO DHIKI.
UJIO WA BWANA YESU.
Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani?
Kitabu cha Waebrania ni moja ya nyaraka ambazo waandishi wake hawajajitambulisha aidha ndani au mwanzoni au mwishoni mwa nyaraka hizo. Lakini kwa kutathimini baadhi ya nukuu za mwandishi, huwenda alikuwa ni mtume Paulo aliyeuandika. Kufuata na kumtaja Timotheo kwenye waraka huo, na tunajua Timotheo alikuwa chini ya utume wa Paulo, kwani ndiye aliyeongozana naye na kumtaja sana katika nyaraka zake nyingi.
Waebrania 13:23 Jueni ya kuwa ndugu yetu Timotheo amekwisha kufunguliwa; ambaye, akija upesi, nitaonana nanyi pamoja naye.
Na pia jinsi mwandishi alivyomalizia waraka wake, kwa kusema “neema na iwe nanyi nyote”. Ni salamu inafanana na nyaraka zote za mtume Paulo, kila alipomaliza alihitimisha na baraka hizo.
Japo wengine wanasema namna ya uandishi haifanani na mtume Paulo, yawezekana alikuwa ni Apolo, au Barnaba, au sila au mtu mwingine tofauti na Paulo.
Lakini kwa vyovyote vile kumtambua mwandishi, si lengo la uandishi, lengo ni kufahamu kilichoandikwa ndani humo.
Kwa ufupi, kama kitabu hichi kinavyoanza kujitambulisha, kinasema
WARAKA KWA WAEBRANIA.
Maana yake ni kitabu kilichoelekezwa kwa wayahudi-wakristo waliokuwa katika kanisa wakati ule. Ndio maana kwa jinsi ulivyoandikwa waraka huu, mwandishi anazungumza na mtu ambaye mwenye uelewa wa dini ya kiyahudi na taratibu zake za kiibada.
Dhumuni kuu ni kueleza UKUU WA YESU JUU YA WATU WOTE, NA MAMBO YOTE YA AGANO LA KALE.
Kwamfano anaeleza Yesu alikuwa mkuu juu ya;
Waebrania 1:1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu
Waebrania 1:13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Waebrania 10:11 Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi. 12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu; 13 tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
Waebrania 10:11 Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.
12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;
13 tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
Hivyo kitabu hichi kinamfafanua Kristo kwa undani, jinsi alivyo na ukuu zaidi ya mambo yote ya agano la kale. Na kwamba watu wote tangu Adamu mpaka Ibrahimu wasingeweza kukamilishwa bila Kristo. Waliishi wa ahadi hiyo ya kuja mkombozi, wakiingojea kwa shauku na hamu (Waebrania 11).
Lakini pia kitabu hichi kinatoa angalizo kwa wayahudi wasirudi nyuma kwasababu ya dhiki na mateso yanayowapata kwa ajili ya imani ya Yesu Kristo. (Waebrania 12:1-13, 10:26-31), Bali wamtazame Kristo kama kielelezo chao, jinsi alivyostahimili mashutumu makuu namna ile. Hii ni kutuhamasisha na sisi kuwa tunapopitia dhiki leo basi nasi tumtazame Kristo aliyestahili, mapingamizi yale, wala hakuutupa ujasiri wake.
Waebrania 12:1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, 2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
Waebrania 12:1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.
Ielewe kwa kina Waebrania 13:5 maana yake.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2
Je ni Mungu au Malaika?
WhatsApp
Mafundisho maalumu kwa wanandoa – Wanawake.
Ikiwa utapenda kupata mafundisho mengine ya namna hii, basi fungua link hii uweze kuyasoma. >>.
https://wingulamashahidi.org/category/mafundisho-ya-wanandoa/
Habari ya Samsoni na Delila inafundisho kubwa nyuma yake kwa wanandoa. Wengi wanafikiri Delila alikuwa mwanamke kahaba ambaye Samsoni alimuokota tu na kukutana naye. Lakini uhalisia ni kwamba Delila alikuwa ni mke wa Samsoni.
Lakini mwanamke huyu, aliweza kubadilishwa akili kwa tamaa tu ya fedha. Ni mwanamke ambaye alipendwa sana na Samsoni, chochote ambacho angetaka kwa Samsoni angepatiwa. Lakini Wafilisti walipoona mwenendo wa Samsoni jinsi alivyompenda sana mwanamke huyu. Wakatumia fursa ile, kumshawishi Delila, kwa kumuahidia donge kubwa la fedha. Ili tu atoe siri ya asili ya nguvu zake.
Delila, akakubali, akaanza kumshawishi Samsoni, kwa kipindi kirefu, na hatimaye akafunuliwa siri ya nguvu zake. Akaenda akaziuza kwa wafilisti, kwa vipande vya fedha.
Waamuzi 16:4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila. 5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja. 6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.
Waamuzi 16:4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila.
5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.
6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.
Kama mke, upendo wako unapohamia kwenye fedha, ni dalili madhubuti kuwa unaua nguvu ya ndoa yako (ambayo ipo kwa mume). Usitangulize mali mbele ya ndoa yako, wala usishawishiwe na fedha kwa chochote ukadharau thamani ya mumeo. Samsoni hakuwa mfanya biashara au mwajiriwa wa kampuni Fulani, hakuwa hata na akaunti benki. Lakini alikuwa mwamuzi wa Taifa teule la Mungu. Mtetezi wa wanyonge, na mkombozi wa walioonewa, hakujitajirisha yeye, alilitajirisha taifa,. Jambo ambalo Delila hakulithamini. Akawa tayari kuoelewa na fedha(wafilisti) na sio nguvu zake(Samsoni).
Leo wapo wamama, ambao wanachotafuta kwa waume zao ni fedha tu,fedha tu, fedha tu.. wakikosa hiyo wapo tayari kufanya chochote. Wengine hata kuanzisha mahusiano na watu wengine wenye uwezo wa juu, hawajua kuwa mwanaume anaweza asiwe tajiri kifedha, lakini ana nguvu za kuiendesha na kuilinda familia yako, jamii yako, ndugu zako, kipawa alichonacho kikaweza kukufanya wewe ukae vizuri au kuistaajabisha jamii au taifa, Lakini endapo tu utakiona hicho na kukithamini ndani yake.
Hivyo, kama mwanamke, toa moyo wako hapo kabisa.
Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?
KITENDAWILI CHA SAMSONI
Je! mtu anapofunga kwa muda wa SAA 24,anapaswa kunywa maji au kitu chochote?
1 Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi”.
Sasa kuvaa mavazi si vibaya, hata hivyo tunapaswa tuvae mavazi, (hilo ni agizo la Bwana tangia Edeni, Bwana Mungu alipowafanyia mavazi ya ngozi wazazi wetu wa kwanza).
Lakini hapo katika 1Petro 3:3 hasemi “kuvaa mavazi”..bali na anasema “kuvalia mavazi”.
Kuna tofauti ya “kuvaa” na “kuvalia”.
Kuvalia maana yake “hayo mavazi yamelengwa kwa kusudi maalumu la kutazamwa na watu”
Kwamfano makahaba (wanawavalia mavazi ya kikahaba wateja wao ili miili yao iuzike vizuri). vile vile wahuni wanawavalia mavazi wahuni wenzao ili watazamwe na wao.
Kijana wa kiume anayevaa suruali ya kubana huyo hajavaa mavazi bali “amevalia mavazi”…. amewavalia mavazi aina fulani ya watu (wahuni wa kike), ili wamtazamapo wamtamani.
Dada anayevaa suruali ya aina yoyote ile, anakuwa hajavaa mavazi bali kavalia mavazi (kamvalia mtu),
Na lengo lake si lingine zaidi ya kutaka kutamaniwa, na Neno la Mungu linasema “yeyote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake”
Kwahiyo mwanamke anayetazamwa na kutamaniwa kwa uvaaji wake, naye pia kazini na yule aliyemtamani (hiyo ni kulingana na Neno la Mungu).
Kama unavyokuwa makini na kile kinachoingia ndani yako (yaani chakula)...vile vile ongeza umakini kwa kila unachojivika nje.
Usiwe mwepesi wa kwenda na kila fasheni inayoingia…kiasi kwamba kila mtindo unaoingia unaupokea, ni lazima uchague kama unavyochagua chakula.
Ni lazima uwe na uchaguzi unaokufaa kama vile ulivyo na uchaguzi wa baadhi ya vyakula vikufaavyo.
Jiulize je hilo vazi la mgongo wazi kama umevaa au umevalia,?…
Hilo vazi linaloonyesha kitovu na mapaja je umevaa au umevalia?
Hiyo kaptura kijana uliyoivaa na kutembea nayo barabarani umevaa kwa lengo gani?..je unamvalia nani?
Jisitiri, na pia jiheshimu.
SWALI: Huyu “Yeye ashindaye” anayezungumziwa katika kila mwisho wa jumbe za makanisa saba. Ni mtu mmoja maalumu au wengi?
JIBU: Tunasoma Bwana Yesu alipotoa agizo au onyo kwa yale kanisa saba mwishoni alimalizia na kutoa thawabu. Lakini thawabu hiyo aliielekeza kwa yule ashindaye tu.
Kwa mfano ukisoma juu ya lile kanisa la Thiathira alisema..
Ufunuo wa Yohana 2:26
[26]Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
Sasa swali huulizwa je? kuna mtu mmoja maalumu ambaye anaonekana atashinda? na kupokea tuzo hiyo ya kuwa na mamlaka juu ya mataifa au ni mjumuiko wa watu.
Ni raisi kudhani tuzo hiyo imeelekezwa kwa mtu fulani mmoja lakini ukweli ni kwamba inamuhusu kila mtu…ni sawa na mwalimu awaambie wanafunzi wake atakayefaulu mtihani wangu..nitamlipia ada ya muhula mmoja.
Sasa yeye kutumia lugha ya umoja “atakaye” na sio “watakao”…hamaanishi kuwa amemlenga mtu fulani mmoja.
maana yake ni kuwa yeyote yule atakayefaulu, basi atalipiwa ada, iwe ni mmoja, au wawili au wote. watalipiwa. Kwasababu wamefaulu. Kigezo ni kufaulu sio atakayefaulu kuliko wote.
Vivyo hivyo na Bwana alichokimaanisha hapo kwenye hayo makanisa saba. Lengo lake ni wote washinde lakini inaonekana ni kama si wote watakaoshinda…bali wale watakaoshinda watazipokea hizo thawabu.
Hivyo ni kujitahidi…kwasababu kuna uwezekano wa wengi kukosa thawabu hizo.
Mtume Paulo alitumia mfano wa wachezaji ambao hushiriki katika mchezo, kwamba wachezao ni wengi lakini apokeaye tuzo ni mmoja..(1Wakor 9:24)
Lakini hakumaanishi kwetu sisi atakuwa mmoja, ni mfano tu alitumia kueleza uhalisia kwamba kuna kunga’ng’ana ,sio jambo rahisi rahisi…fahamu kuwa sisi wakristo hatuna mashindano ya ukubwa na nafasi mbinguni…tunashindana ili tuyatende yale tuliyoagizwa na Bwana kikamilifu na sio kuzidiana…
Ndio maana mahali pengine akasema watatoka wengi, kutoka mashariki, na magharibi kuja kuketi na Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote, (Luka 13:28-29) Umeona kumbe wazee wetu hao, ni kama vile wamewekwa sehemu moja na wengine watakuja kuungana nao. Na wote watakua kitu kimoja na wao, lakini pia angalizo ni kwamba watakaofikia hapo si wengi sana.
Mathayo 8:11
[11]Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
Kwahiyo ni kujitahidi hapo tusikose..Kwa kumaanisha kweli kweli kujitwika misalaba yetu na kumfuata Yesu. Na kujitenga na dhambi, na hakika thawabu hizo tutazifikia wote.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)
Lipo jiwe Yakobo aliloliweka chini ya kichwa chake kabla ya kulala na baada ya kuamka alilisimamisha likanyanyuka.
Jiwe hili lilibeba ufunuo wa YESU KRISTO, ambao napenda tuutazame leo.
Kipindi Yakobo anamkimbia Esau ndugu yake, alifika mahali fulani ambapo ni pa kawaida, lakini baadaye pakawa si pa kawaida.
Kabla ya kulala, alitwaa jiwe na kuliweka chini ya kichwa chake kama mto, huenda aliliona tu ni kama jiwe la kawaida lakini baada ya kuamka aligundua limebeba ufunuo mkubwa.
Mwanzo 28:10 “Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani. 11 Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale. 12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake. 13 Na tazama, BWANA amesimama juu yake, akasema, Mimi ni BWANA, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako…………… 16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli BWANA yupo mahali hapa, wala mimi sikujua. 17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. 18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. 19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu. 20 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi”.
Mwanzo 28:10 “Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.
11 Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.
12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.
13 Na tazama, BWANA amesimama juu yake, akasema, Mimi ni BWANA, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako……………
16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli BWANA yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.
17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.
18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.
19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
20 Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi”.
Unaona?..baada ya Yakobo kuamka usingizini aliona jiwe lile halipaswi tena kuwa kama Mto wa kulalia bali nguzo inayosimama.
Je na wewe jiwe hii umelisimamisha au unaendelea kulilalia tu.
Na Jiwe hilo si mwingine zaidi ya Bwana YESU.
1 Petro 2:4 “Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima”.
Jiwe hilo lililofungua ufahamu wa Yakobo na akamwona Mungu na Malaika wake usiku ule na hilo akalifanya kuwa NGUZO.
Akalifanya kuwa Nguzo ya nadhiri zake, akalifanya kuwa nguzo za hekalu la Mungu.
Je na wewe jiwe hili (YESU) umelisimamisha katika maisha yako au umelilaza?.
Kama jiwe hili limelala chini yako basi matokeo yake kwa nje ni tufani na maangamizi ya ibilisi, lisimamishe kuanzia leo.
Mitume wa Bwana YESU walijua umuhimu wa kulisimamisha Jiwe Bwana YESU katika ile tufani ilipotokea baharini..
Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo. 35 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye. 37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji. 38 Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia? 39 Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu”
Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
35 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.
37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
38 Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?
39 Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu”
Ukiwa Yesu uliye naye ni yule wa kidini tu, yule wa kurithi kwa wazazi….basi fahamu kuwa ni Jiwe lililolala chini yako.
Ukiwa ukristo wako ni ule wa mazoea tu, usio na hofu na Mungu, basi jua kuwa unalo jiwe lililo lala.
Ikiwa ukristo wako ni ule wa ndoto na maono tu, na hutaki kujifunza Neno la Mungu basi fahamu ya kuwa jiwe lako limelala.
Yakobo baada ya kuona maono yale hakuendelea kulifanya lile jiwe kuwa Mto badala yake alilisimamisha mbele yake, lakini utaona wakristo wa leo baada ya kuona maono mawili matatu ya kiMungu, basi hata Neno la Mungu halisomwi tena, wanabaki tu kuendelea kuishi kwa ndoto na maono, jambo ambalo ni hatari sana.
Lisimamishe jiwe, lisimamishe jiwe.
Zipo aina tatu za Utakatifu, na leo tutaangalia moja baada ya nyingine, na tutajua ni upi unaotufaa sisi.
Aina hizi za utakatifu ni kama ifuatavyo.
1.UTAKATIFU WA MWILINI
2. UTAKATIFU WA ROHONI
3. UTAKATIFU WA MWILINI NA ROHONI.
1.UTAKATIFU WA MWILINI.
Ni ile hali ya kuuweka mwili katika viwango vya kumpendeza MUNGU, ikiwemo kuvaa vizuri kiasi kwamba mtu akikutazama basi anaona ushuhuda wa Kristo katika uvaaji wako na mwonekano wako.
Vile vile utakatifu wa mwilini unahusisha, kujilinda na matendo yote ya mwili yanayotajwa katika Wagalatia 5:19-20…ikiwemo uasherati, ulevi, kujichua, kujichubua na mengineyo.
Mtu anaweza kuwa na utakatifu huu wa mwilini na ule wa rohoni akaukosa. Anaweza kuwa na mwonekano mzuri sana wenye ushuhuda lakini akaukosa ule wa rohoni.
Sasa utakatifu wa rohoni ni upi?.
2. UTAKATIFU WA ROHONI.
Utakatifu wa rohoni ni ule unaohusisha, matendo yote ya rohoni yanayompendeza MUNGU.
Ikiwemo kuomba, kutoa sadaka (Mathayo 6:4), kumwabudu Mungu katika roho, kujifunza na kutafakari Neno la Mungu, vile vile upendo, uvumilivu, utu wema, kiasi.
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Mtu akiwa na matunda hayo basi kibiblia ni mtakatifu rohoni.
Sasa ni rahisi sana mtu kuwa mtakatifu mwilini na asiwe mtakatifu rohoni, lakini ni jambo la Nadra sana kukuta mtu mtakatifu rohoni na mwilini akawa si mtakatifu.
Watu wengi wenye utakatifu rohoni halafu nje mwonekano wao hauna ushuhuda, wengi wao ni watu wanaovaa viatu vinavyowabana, huwa wanajua kabisa kuwa mionekano yao haina ushuhuda kwasababu ya Roho Mtakatifu aliye ndani yao, isipokuwa kuna mazingira yanayowafanya wabaki katika hiyo hali.
Na mazingira hayo yamegawanyika katika sehemu mbili.
Sehemu ya kwanza: Viongozi wao wa kiroho wanawachanganya.
Wengi wanaotamani kubadili mionekano yao ya nje, wanapowatazama viongozi wao wa kiroho kuwa ndio watu wanaoongoza katika kuvaa ovyo, wanachanganyikiwa na kubaki kufikiri kwamba wao wana makosa na viongozi wao wapo sawa, hivyo wanabaki katika hali ya ubumbuazi wa kiroho, wanashindwa kujua nini cha kufanya na wanaishia kupokea yale viongozi wao wanayoyasema na kuyatenda.
Dada/kaka kama upo katika hili kundi, basi sikia sauti ya Roho Mtakatifu leo. KAMILISHA UTAKATIFU WAKO WA MWILINI, ni kweli matendo yako ya rohoni ni mema na mazuri, sasa umebakisha hilo moja tu la Rohoni, ondoa hayo mapambo ya kidunia mwilini mwako, ondoa hizo hereni, ondoa hiyo mikufu, ondoa hizo bangili, ondoa hizo rangi usoni, ondoa huo mtindo wa nywele na uvaaji usio na ushuhuda, na utapanda viwango vingine vya kiroho.
Usichanganywe na miujiza inayofanywa na viongozi wako wa kiroho, hata kama ndiye aliyekuleta kwa Kristo, basi asikuogopeshe na kukufunga usilifuate Neno la Mungu.
Hata kama ana hubiri vizuri, usiogope, hata kama aliwahi kukuombea ukapona, bado uasiogope..Neno la MUNGU ni nyundo na upanga ukatao kuwili, na Bwana alisema wengi watakuja siku ile na kusema walitoa pepo na kufanya miujiza kwa jina lake lakini atawafukuza.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”
Sehemu ya pili: Wazazi na Ndugu.
Wazazi na ndugu ni sehemu kubwa na kuuzia utakatifu wa mwilini kwa mtu, kwani wengi wanapoona na kusikia ushauri wa ndugu, bali ule ushauri unaweza kuwa mzito sana zaidi hata ya mtu mwingine yeyote.
Utakatifu wa mwilini na rohoni ni ile hali ambapo mtu anakuwa na ushuhuda wa ndani roho yake na nje ya mwili wake. Na huu ndio utakatifu Mungu anaouhitaji kwetu.
1 Wakorintho 7:34 “….. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho….”
Utakatifu wa mwilini na rohoni ndio msingi wa sisi kumwona Mungu sawasawa na ile Waebrania 12:14.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.
Timiza utakatifu wako Mteule wa MUNGU..
2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”
VIWANGO VYA UTAKATIFU.
Katika kuwa watakatifu wa mwilini na rohoni ni lazima viwango vyetu viwe juu zaidi ya watu wasio wa Kristo.
Mathayo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.
Maana yake ni kwamba kama kumcha Mungu basi ni lazima tuwazidi wa imani nyingine, kama kuvaa kwa staha ni lazima tuwazidi watu wengine wote wasio wa Imani n.k.
Bwana YESU atusaidie sana.
Danieli 2:2[2]Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.
Wasihiri ni kundi la wachawi, lililojikita kwenye mazingaumbwe. Linatumia uchawi kubadili vitu kwa hila, mbele ya macho ya watu kuwafanya waone kama ni muujiza umetendeka, na wakati mwingine kutumia njia hiyo kuleta madhara kwa watu.
kwamfano wale yane na yambre kipindi cha Musa walikuwa ni wasihiri, walijaribu kubadili fimbo kuwa nyoka, na kuleta vyura.(Kutoka 8:7)
Mfano mwingine ni yule Simoni mchawi, tunayemsoma katika;
Matendo 8:9-11
[9]Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. [10]Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu. [11]Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
[9]Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
[10]Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
[11]Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
Tofauti na waganga ambao, wenyewe wanajifanya kama matabibu, na wachawi na wale wakaldayo ambao ni wanajibu(wasoma nyota)…hawa wasihiri kazi yao hasaa ni ile ya kiini macho.
Lakini Mungu anathibitisha kwamba makundi yote haya, hakuna hata moja lenye uwezo wa kufikia hekima ya Mungu ipitayo vyote Hayana nguvu ya kupambanua mambo. au kufanya miujiza. Hakuna mganga wala wachawi, mwenye uwezo wa kufanya muujiza.
Sasa utauliza ni nini kile wanachokifanya kama sio miujiza?
Awezaye kutenda miujiza ni Mungu tu. wasihiri na waganga wanafanya kazi ya kulaghai fikra za watu kwa elimu ambayo ni ya siri (ya mashetani), ndio maana wanaofanya hizo kazi huenda kujifunza kufanya hivyo, namna ya kuchezea fikra za watu, na si kingine.
Sasa wewe kwasababu hujaijua hiyo elimu unaweza ukasema umeona muujuza kumbe ni uongo tu..wamekudanganya.
ni sawa na leo unapoona mtu akiwasiliana na mtu mwingine akiwa mbali na kuiona sura yake kwenye kioo, kama huijui elimu ya darasani, utasema ni muujiza lakini kumbe ni maarifa tu ya kibinadamu.
vivyo hivyo na hawa wachawi na wasihiri, hawana jipya kusema wanafanya muujiza fulani, ni elimu zao tu za kipepo
Hawawezi kuumba chochote. wale vyura waliofanya kutokea kipindi cha Farao, hawakuumba vyura wao wapya kimiujiza..Vinginevyo mpaka leo shetani angekuwa na uwezo wa kuumba na angeumba vyura wake wengi tu na viumbe vyake vimwabudu. Alichokifanya pale ni kuchukua vyura walioumbwa na Mungu, na kuwapumbaza watu macho, waone ni mawe yamegeuzwa vyura kumbe hakuna kitu. Ndio maana ujinga wao ulikuwa wazi baadaye…walipodhani kila eneo ni kiini macho, walipojaribu kwa chawa wakashindwa, kibao kikawageukia, wakakiri ni Mungu tu awezaye.
Kwahiyo wewe uliye na Yesu, shetani anakuona kama mungu duniani, mwenye nguvu nyingi sana, hekima mamlaka zaidi ya yeye. Wewe unaweza kutenda muujiza kabisa kwa jina la Yesu. yeye hawezi
mwamini Yesu mtegemee yeye tu, kwanini kutafuta msaada kwa vitu dhaifu, ukamtia Mungu wivu?. Kwenda kwa waganga ni kupungukiwa akili, ni kujitenga na fadhili zako, mwenyewe, ni kumdharau muumba wa mbingu na nchi, Yehova, atupaye vyote.
Okoka sasa, mpokee Yesu, upate uzima wa milele. Wachawi waliokutana na Yesu walisalimu amri na kuchoma mikoba yao. sasa wewe unaenda kufanya nini huko?
Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.