Title June 2024

Wagerasi ni nchi gani? (Luka 8:26-39)

Wagerasi ni watu waliokuwa wanaishi katika mji ulioitwa Gerasi ambao ulikuwa kusini mashariki mwa bahari ya Galilaya. (Tazama kwenye picha)

Ulikuwa ni moja ya miji ya Nchi ya Dekapoli. Nchi ya watu wa mataifa.

ndio kule ambako Yesu alivuka na kukatana na wale watu waliokuwa vichaa wakali, akawafungua.

Marko 5:1-3

[1]Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 

[2]Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 

[3]makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 

Urefu wa habari hii fungua hapa >>ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Mathayo 8:28-34, na Luka 8:26-39.

Ni nini ambacho Bwana anataka tujifunze kwa hawa wagerasi? 

Ni watu ambao walithamini, hazina zao, mali zao, utajiri wao, zaidi ya kufunguliwa kwao, ndio maana mara tu walipoona nguruwe wao wamekufa wote, jambo hilo liliwafanya wawe na hofu, na hiyo ikawapelekea kumsihi Yesu aondoke katika nchi yao, asije akaleta hasara zaidi.

hawakuona wokovu ule mkuu uliowafikia, waliona hasara waliyopata. Hiyo ni mbaya sana,  kwa urefu ya jambo hilo pitia hili somo.

Kamwe usiwe mgerasi.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine: 

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Rudi Nyumbani

Print this post

Apitaye cheo ni mtu wa namna gani?

Jibu: Turejee..

2Yohana 1:9 “KILA APITAYE CHEO, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia”.

“Cheo” ni neno lenye maana ya “Kipimo”..

> Kwamfano Mtu mwenye kipimo kikubwa cha heshima katika kazi/shughuli fulani maana yake huyo mtu ana cheo kikubwa  katika kazi hiyo…

> Au mtu mwenye kipimo kikubwa che heshima kuliko wenzake katika Serikali/mamlaka, maana yake mtu huyo ana cheo kikubwa..

Marko 6:21 “Hata ilipotokea siku ya kufaa, na Herode, sikukuu ya kuzaliwa kwake, alipowafanyia karamu wakubwa wake, na majemadari, na watu wenye cheo wa Galilaya”

> Vile vile mtu mwenye kipimo kikubwa cha umri, ni sawa na kusema ana cheo kikubwa cha umri..

Mwanzo 43:33 “Wakaketi mbele yake, mzaliwa wa kwanza kwa cheo cha kuzaliwa kwake, na mdogo kwa udogo wake; watu hao wakastaajabu wao kwa wao”.

Sasa tukirudi kwenye swali, mtu apitaye cheo ni mtu wa namna gani?

Mtu “apitaye cheo” kulingana na andiko hilo, ni mtu avukaye kipimo au mipaka ya Mafundisho ya KRISTO.

Maana yake kama neno la Mungu linasema “Usiibe”  au “Usizini” yeye atatafuta namna ya kuhalalisha wizi au uzinzi au ushoga kwa namna yoyote ile (ambapo hapo kwanza tayari alikuwa amekwisha kuamini kuwa wizi na uzinzi ni dhambi) lakini sasa anataka kuhalalisha zinaa au wizi anaoufanya au anaoutamani.

Mtu wa namna hiyo ni mtu aliyevuka cheo cha mafundisho ya Kristo, (maana yake alikuwa katika mafundisho sahihi lakini sasa amevuka mipaka)..na mtu wa hivyo biblia inasema hana Mungu ndani yake.

Hivyo hatuna budi daima kudumu na kusimama katika Neno la Mungu.. Kwasababu biblia inasema limehakikiwa na halina kasoro, na hivyo hatuhitaji sisi kulirekebisha..

Mithali 30:5 “Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.

6 Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo”.

Tukivuka kipimo (cheo) kwasababu aidha ya kiburi au tamaa ya kuhalalisha mambo mabaya na tukalipindisha Neno la lake (mafundisho yake), basi tutaangukia katika hukumu ile iliyotajwa katika Ufunuo 22:18…

Ufunuo 22:18 “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki”.

Bwana atusaidie tufikie cheo na si tuvuke cheo. (Waefeso 4:13).

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIKWEPE CHUO CHA UTAKATIFU.

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Fahamu Namna ya Kuomba.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

Rudi Nyumbani

Print this post

JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.

2Timotheo 4:21  “Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia”

Mtume Paulo ni mtu aliyetambua kuwa kustawi kwa huduma yake kunategemea sana sapoti ya watendazi wenzake wengine wenye ni moja na yeye. Hivyo tunasoma wakati akiwa Rumi kama mfungwa, alimwandikia waraka mwanawe Timotheo, aiharakishe huduma yake, ili amfuate kule Rumi wasaidiane katika huduma kabla ya wakati wa bariki kuanza.

“Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi”.

Paulo alijua mazingira yanaweza kukawiisha kusudi la Mungu. Hivyo alitambua kuwa mtu akiongeza jitihada anaweza kukamilisha mambo yake mapema kabla mazingira Fulani hayajamuathiri kutenda kusudi lingine la Mungu.

Kwa ukanda waliokuwa, ilikuwa ni ngumu sana, meli kusafiri nyakati za baridi kwasababu ya barafu baharini, hivyo safari zote za majini zilisitishwa kwa miezi kadhaa mpaka baridi itakapoisha ndipo safari zianze tena, Paulo aliliona hilo akatambua ni jambo la asili haliwezi kuepukika kwa kufunga na kuomba, isipokuwa kwa kupangilia tu ratiba vizuri.

Hii ni kutufundisha sisi, tufahamu kuwa mazingira Fulani, au nyakati Fulani zisizo rafiki sana huwa zinapita, au zitakuja mbele yetu ambazo zinaweza zikawa ni kikwazo cha utumishi kwa sehemu Fulani.

Kwamfano wakati wa baridi kwako, unaweza kuwa ni wakati wa ndoa. Kama wewe ni kijana hujaoa/ hujaolewa, unanafasi sasa ya kumtumikia Mungu kwa uhuru wote. Titahidi sana kufanya hivyo sasa, kwasababu nafasi hiyo inaweza ikapungua kwa sehemu uingiapo katika majukumu ya kindoa. Usipojitahidi sasa kujiwekea msingi mzuri kwa Mungu wako, utataabika sana kuujenga huo uwapo kwenye ndoa.

Wakati wa baridi unaweza ukawa ni kipindi cha kazini au masomoni. Ikiwa bado hujapata kazi, au upo likizo kazini au shuleni, embu tumia vema wakati wako, kuongeza kitu kikubwa katika ufalme wa Mungu, kwasababu shughuli zitakapokulemea, kuujenga tena huo msingi itakuwia ngumu sana, na kama ikiwezekana yaweza kukuchukua wakati mrefu. Uwapo ‘free’ usilale, bali tumia sasa kuongeza mikesha, maombi ya masafa marefu, kusoma biblia yote.

Wakati wa baridi waweza kuwa uzee. Kwa jinsi umri unavyokwenda ndivyo uwezo wa mwili wako unavyopungua, Hivyo utengenezapo mambo yako mapema na Bwana, basi wakati huo ukikukuta hautakuathiri sana, kwasababu tayari yale ya msingi uliyopaswa uyafanye umeshayafanya mapema, uzeeni ni kumalizia tu.

Zipo nyakati nyingi za baridi. Chunguza tu maisha yako ujue wakati wako wa baridi unafika lini na ni upi, kisha jitahidi sana, kuwekeza kwa Mungu sasa, kimaombi, kiusomaji Neno, na kiuinjilisti.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.(Opens in a new browser tab)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

(Opens in a new browser tab)Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Rudi Nyumbani

Print this post

SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.

Ufunuo 3:11 “Naja upesi. SHIKA SANA ULICHO NACHO, asije mtu akaitwaa taji yako”.

Hapo anasema “..Asije mtu.” na si “..Asije shetani”. Maana yake anayeitwaa taji ya mtu ni MTU, kwasababu shetani yeye taji lako au langu halimsaidii kitu, kwasababu haendi kulivaa.. lakini mwingine akilichukua litaenda kumfaa anakokwenda!.

Labda tuzidi kuliweka hili vizuri..

Aliyelichukua Taji la “Yuda Iskariote” ni mtu aliyeitwa “Mathiya”… baada ya Yuda kushindwa kushikilia alichopewa…

Matendo 1:24  “Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25  ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

26  Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja”.

Vile vile aliyeichukua Taji ya “ESAU” ni ndugu yake “YAKOBO”…Baada ya kuidharau ile haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa tamaa ya chakula kimoja tu.

Waebrania 12:16 “Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja.

17  Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi”

Umeona unapoacha kuthamini kile ulichopewa, basi mwingine atakichukua,..unapoacha kuthamini nafasi yako mwingine ataichukua.. Unapoacha kuthamini huduma yako uliyopewa na Mungu, mwingine ataichukua na utapoteza thawabu zako.

> Umepewa huduma ya Uinjilisti, usiipuuzie na kuifanya kilegevu.. Bwana anaweza kuiondoa kwako na kumpa mwingine atakayeifanya vizuri na kwa ushujaa.

> Umepewa huduma ya maombezi, fanya hayo kwa bidii, usipuuze kwani Bwana anaweza kuiondoa kwako na kumpa mwingine ikiwa utaipuuza.. na thawabu yako (Taji yako) utakuwa umeipoteza.

> Umepewa huduma ya kukirimu (kwamba kupitia ulivyopewa unahudumia watumishi na kazi ya Mungu) basi usidharau neema hiyo kwasababu Bwana anaweza kuiondoa kwako na kumpa mwingine na hivyo Taji yako ikaondoka, fanya uliyojaliwa na BWANA kwa bidii sana..(Na huduma nyingine zote ni hivyo hivyo).

SHIKA SANA ULICHO NACHO!!.. SHIKA SANA ULICHO NACHO!!!… SHIKA SANA ULICHO NACHO!! Kwasababu kina thamani kubwa!.. Hakikisha unakizalia matunda.

Na majira haya, shoka lipo kwenye mashina ya miti kukata kila tawi lisilozaa,

Luka 3:9 “Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.

Bwana atusaidie tusikatwe. Lakini Neno ni moja tu kwetu. TUSHIKE SANA TULIYO NAYO!!!

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Je vazi alilovikwa Bwana Yesu lilikuwa la Zambarau au Jekundu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nyapara/ wanyapara ni watu gani? (Kutoka 5:14)

Jibu: Turejee..

Kutoka 5:14 “Na WANYAPARA wa wana wa Israeli, ambao wasimamizi wa Farao wamewaweka juu yao, wakapigwa, wakiambiwa, Kwa nini hamkutimiza kazi yenu jana na leo; kwa kufanya matofali kama hapo kwanza?

15 Basi WANYAPARA wa wana wa Israeli wakaenda, wakamlilia Farao, wakisema, Mbona umetutendea hivi, sisi watumwa wako?

16 Watumwa wako hawapewi majani, nao wanatuambia, Fanyeni matofali; na tazama, watumwa wako wapigwa; lakini kosa hilo ni la watu wako mwenyewe”.

“Wanyapara” ni wasimamizi wa wafungwa au watumwa.

Katika magereza, wale wafungwa wanaoteuliwa kuwa kama viongozi wa wafungwa wenzao ndio wanaoitwa “wanyapara”. Hivyo yule askari ambaye ni mkuu wa gereza anapotoa agizo basi yule Nyapara ndiye anayelichukua na kuliwasilisha kwa wafungwa wenzake na yeye mwenyewe anakuwa ni msimamizi juu yao, ingawa naye pia ni mfungwa.

Sasa kipindi wana wa Israeli wapo Misri utumwani, wale wasimamizi wa Farao (Maaskari) waliwachagua baadhi ya wafungwa na kuwafanya wanyapara kwa wafungwa wenzao.

Na Wasimamizi hao walipotoa amri ya kazi Fulani, basi waliwaangalia hao wanyapara na hao wanyapara ndio waliowaongoza watumwa wenzao, na ikitokea watumwa (wana wa Israeli) wamekaidi au wanafanya kazi kwa ulegevu basi wanaoathirika wa kwanza ni wanyapara wao, kwani wale wasimamizi wa Farao walikuwa wanashughulika kwanza na hao wanyapara kabla ya watumwa wenyewe.

Kutoka 5:14 “Na wanyapara wa wana wa Israeli, ambao wasimamizi wa Farao wamewaweka juu yao, wakapigwa, wakiambiwa, Kwa nini hamkutimiza kazi yenu jana na leo; kwa kufanya matofali kama hapo kwanza?”

Shetani naye anao wanyapara wake aliowaweka juu ya wote wanaotumikishwa na dhambi!.. kwasababu biblia inasema atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi, na kama ni mtumwa basi ni lazima atakuwa na nyapara wake.

Kama unaishi katika uzinzi na uasherati, yule unayeishi naye kama mume/mke ni nyapara wa ibilisi kwako, ndio maana dhambi inakutesa na huyo naye anakutesa, kwasababu wote mpo katika dhambi na ni hivyo hivyo katika dhambi nyingine zote…ni lazima shetani akupe nyapara juu yako.

Leo hii mkatae shetani na manyapara wake,..mkubali Bwana YESU upate uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA

USIMWABUDU SHETANI!

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

Rudi Nyumbani

Print this post

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

SWALI: Nini maana ya hivi vifungu?

Zekaria 13:7-9

[7]Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.

[8]Hata itakuwa, ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, asema BWANA; lakini fungu la tatu litabaki humo.

[9]Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.


JIBU: Unabii huu ulimtabiri Yesu, wakati wa kukamatwa kwake na wayahudi ili auawe, ukisoma Mathayo 26:31 utaona Bwana alinukuu yeye mwenyewe maneno hayo kwa kusema..

“Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Na kweli tunaona baada ya Yesu kukamatwa mwanafunzi wake wote wakamkimbia.

Kama mstari wa nane unavyosema mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, lakini fungu la tatu litabaki humo.

Ni kuonyesha kwa lugha ya mifano kuwa ni idadi ndogo tu ya wanafunzi ambao hawakumuacha kabisa kabisa, mfano wa “theluthi moja”, lakini theluthi mbili zote zilirejea nyuma moja kwa moja. Na ndio maana utaona siku ile ya pentekoste ni watu 120 tu waliokuwepo pale kuingojea ahadi ya roho. Lakini yale maelfu ya makutano yaliyokuwa yakimfuata yalitawanyika.

Lakini katika mstari wa 9, anasema;

“Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.”

na hao ndio waliopitishwa katika moto, wakabatizwa na Roho, wakawa vyombo vikamilifu vimfaavyo Mungu kwa kazi ya uvuvi.

Lakini adui hakujua ulikuwa ni mpango wa Mungu iwe vile kwamba mchungaji afe, ili wokovu mkuu zaidi ya ule wa kwanza uje kwa kupitia kifo chake.Angelijua hilo hata asingedhubutu kumgusa.

Ndio hapo shetani hakuamini alipoona wale wachache waliojazwa Roho, wakivuta maelfu kwa mamilioni ya watu  kwa kipindi kifupi mpaka dunia nzima ikawa imepinduliwa. Shetani hakujua misheni ya mchungaji ilikuwa ni kuingia ndani ya kondoo, sio kuwachunga tena kwa nje, kama hapo mwanzo.

Je nini tunajifunza?

Je! Wewe ni kundi lipi? Lile la tatu, au yale mawili ya kwanza. Ambayo yanapoona mtikisiko kidogo tu wa kimaisha hurudi nyuma, yanapoona kuyumba kidogo tu kwa kanisa hutoroka, yanapoona kutetereka kidogo kwa kiongozi wao yanarudi Misri? Kumbuka ni kusudi la Kristo wote tupitishwe katika moto, ili tuimarishwe tufae kwa ajili ya kazi njema ya utumishi wake.

Aliwapitisha wana wa Israeli jangwani, ili kuwaimarisha kabla ya kwenda kuwaangusha maadui zao kule Kaanani. Aliwapitishwa mitume wako, kwanini na wewe usipitishwe?

Vivyo hivyo ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, ambaye utapenda Bwana akutumie, basi liweke kichwani kwamba kuna mahali fulani utapitishwa ili kuimarishwa, huo ndio ubatizo wa Moto ulio wa Roho Mtakatifu. Wakati huo usimwache Bwana, kuwa fungu la tatu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI KRISTO AFE?

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

(Opens in a new browser tab)MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.(Opens in a new browser tab)

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)

Swali: Agano la chumvi kama tunavyolisoma katika 2Nyakati 13:5 ni agano la namna gani?


Jibu: Turejee..

2Nyakati 13:5 “Je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa AGANO LA CHUMVI”

Neno hili “Agano la Chumvi” limeonekana mara tatu (3) katika biblia.. sehemu ya kwanza ni hii tunayoisoma ya 2Nyakati 13:5, na nyingine ni katika Hesabu 18:19, pamoja na Walawi 2:13.

Sasa swali nini maana ya Agano la Chumvi?

Nyakati za zamani na hata sasa katika baadhi ya maeneo na baadhi ya jamii, mbali na matumizi ya chumvi katika kuongeza ladha ya chakula, lakini pia chumvi ilitumika na inatumika kama kiungo cha kuhifadhia chakula ili kiweze kudumu kwa muda mrefu bila kuharibika.

Zamani hakukuwa na friji kama zilizopo leo, hivyo kitu pekee kilichokuwa kinatumika kuhifadhia vyakula ambavyo bado havijapikwa (kibichi/kikavu) kilikuwa ni CHUMVI.

Kwahiyo Chumvi, tunaweza kusema inalo AGANO BORA la kuhifadhi kitu kwa muda mrefu pasipo kuharibika kuliko kitu kingine chochote (Ni kiungo cha uhakika kinachodumisha kitu kwa muda mrefu).

Ndio maana utaona sadaka zote katika agano la kale, ziwe za Unga, au za wanyama ziliwekwa chumvi, kuwakilisha uthabiti wa agano la Mungu.

Walawi 2:13 “Tena, kila toleo la sadaka yako ya unga UTALITIA CHUMVI; wala usiiache sadaka yako ya unga kupungukiwa na chumvi ya agano la Mungu wako; utatoa chumvi pamoja na matoleo yako yote”.

Ezekieli 43:22 “Na siku ya pili utamtoa beberu mkamilifu awe sadaka ya dhambi; nao wataisafisha madhabahu, kama walivyoisafisha kwa ng’ombe huyo.

23 Utakapokwisha kuitakasa, utatoa ng’ombe mume mchanga mkamilifu, na kondoo mume wa kundini mkamilifu.

24 Nawe utawaleta karibu mbele za Bwana, na MAKUHANI WATAMWAGA CHUMVI JUU YAO, nao watawatoa wawe sadaka za kuteketezwa kwa Bwana”.

Hivyo kitu kilichotiwa Chumvi maana yake kinadumu muda mrefu, na kilichodumu muda mrefu maana yake kimetiwa chumvi nyingi… ndio maana upo usemi unaowatambulisha wakongwe kama “WATU WALIOKULA CHUMVI NYINGI”.. Na usemi huu pia upo katika biblia, kuwakilisha kuwa Wakongwe ni watu wenye chumvi mwilini.

Ezra 4:11 “Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta;watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.

12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.

13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.

14 Na sisi, KWA KUWA TUNAKULA CHUMVI YA NYUMBA YA MFALME, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme”.

Hivyo tukirudi katika mstari huo wa 2Nyakati 13:5 unaosema “Je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa AGANO LA CHUMVI”..

Maana yake ni kwamba Agano Mungu aliloingia na Daudi la kumpatia Ufalme, basi ni Agano thabiti lenye kudumu muda mrefu (milele) lisilo haribika kama tu vile chumvi itiwavyo katika vyakula na kukidumisha chakula hicho.

Na sisi tunapomwamini Bwana YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, basi TUNATIWA CHUMVI katika roho (ambayo inatufanya tudumu milele katika ahadi za Mungu, na kuwa na uzima wa milele).

Na tunatiwaje Chumvi ili tuweze kupata uzima wa milele?

JIBU, “TUNATIWA CHUMVI KWA MOTO”.

Marko 9:49 “Kwa sababu kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”.

Moto unaozungumziwa hapo ni moto wa Roho Mtakatifu (soma Mathayo 3:11 na Matendo 2:3) ambao ukishuka ndani ya mtu unachoma kila kitu cha kidunia, na kusafisha kama vile chuma kisafishwavyo katika moto, (moto huo unamtenga mtu na vile vitu vilivyoshikamana na maisha yake) Ambapo wakati mwingine unaweza kuleta maumivu, kwasababu unaondoa vile viungo vyote vinavyomkosesha mtu.

Ambapo baada ya hapo mtu anakuwa mpya kabisa (kiumbe kipya) na anakuwa ana uzima wa milele ndani yake, kwasababu katika chumvi.. Hilo ndilo Agano la Chumvi kwetu.

Je umetiwa Chumvi?..Kama utamkubali Bwana YESU siku ya leo, basi utatiwa chumvi na Roho Mtakatifu, na utakuwa chumvi ya dunia (Mathayo 5:13) na utakuwa na uhakika wa maisha ya Milele. Hivyo mkaribishe leo maishani mwako kama bado hujafanya hivyo.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ninyi ni chumvi ya dunia; Andiko hilo lina maana gani?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto;

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

Siri za Mungu ni zipi? (1Wakorintho 4:1)

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! kufanya mazoezi kwa mkristo ni dhambi?

Swali: Je mkristo aliyeokoka kw enda “Gym” /kunyanyua vyuma na kufanya mazoezi mengine ya viungo ni dhambi?.


Jibu: Kufanya mazoezi kwa asili si dhambi, kwasababu hata kutembea kutoka nyumbani kwenda kanisani kumwabudu Mungu au kwenda kazini tayari hayo ni mazoezi hata kama hujarasimisha. Bwana hajatuumba kutulia sehemu moja kama vile “MTI”, bali kujongea.

Na kujongea kuna faida katika mwili endapo kukiambatana na “Kuyafanya mapenzi ya Mungu”. Maana yake ni hii, kama utakuwa upo sawa na MUNGU aliyekuumba kimahusiano, basi mazoezi utakayoyafanya yatakuwa na faida katika mwili wako.

Lakini kama Mahusiano yako na Mungu ni hafifu au hayapo kabisa, basi  hata mazoezi utakayofanya hatayakuletea matokeo yoyote katika mwili wako.

Lakini suala la Msingi, ni je.. Aina gani ya Mazoezi Mkristo anayopaswa kuyafanya?? Hili ndilo SWALI LA MSINGI.

Mazoezi Mkristo anayopaswa kuyafanya ni yale yasiyo na NIA YA KIDUNIA, wala YASIYOJIFUNGAMANISHA NA MIFUMO YA KIDUNIA. Tuangalie moja baada ya nyingine.

   1. MAZOEZI YENYE NIA YA KIDUNIA NI YAPI?

Mfano wa mazoezi yaliyobeba Nia ya kidua ni yale yote yanayochochea tamaa za kimwili..mfano wa hayo ni yale ya kunyanyua vyuma ili kutanua misuli kwa lengo la kutazamwa na watu, au kuvutia jinsia nyingine…mazoezi ya namna hii ni haramu kwa mkristo.

Lakini kama mkristo atafanya mazoezi ya kutanua misuli aidha kwasababu kazi yake ya mikono aifanyayo itahitaji ukakamavu, hiyo sio kosa.

Mfano mwingine wa mazoezi haramu ni yale ya kupunguza mwili kwa lengo la kutumia mwili huo kama kivutio cha matangazo ya urembo au mitindo.(Maarufu kama Umiss, au Umodel), mazoezi ya namna hii mkristo hapaswi kufanya..

Lakini kama lengo lake si hilo, bali anafanya tu mazoezi ya kupunguza mwili kwa lengo la  kujiongeza wepesi katika viungo vyake afanyapo kazi au aendeleapo na majukumu yake ya kila hapo afanyi kosa.

    2. MAZOEZI YALIYOJIFUNGAMANISHA NA MIFUMO YA KIDUNIA.

Mazoezi yaliyojifungamanisha na mifumo ya kidunia ni yale yote yaliyobeba tamaduni za kidunia kuendesha/kuongoza  mazoezi hayo…(Mazoezi ya dizaini hii haijalishi yana NIA nzuri, lakini maadamu tu tayari yamejifungamanisha na mifumo ya kidunia, basi yanakuwa Najisi kwa mkristo).

Mfano wa mazoezi haya ni yale ambayo Mtu atakimbia barabarani huku kavaa nguo ya kubana au nguo ya ndani tu peke yake!!…kwasababu tu ndio mfumo wa ukimbiaji ulioidhinishwa au ulio katika wakati. Mkristo kwa vyovyote vile hapaswi kufanya mazoezi kwa mtindo huo… haijalishi nia yake ni kupunguza mwili ili awe mwepesi katika kazi au kuongeza ili imsaidia katika kazi zake.

Maana yake kama wewe ni mkristo na unataka kufanya mazoezi ya kukimbia ili kupunguza mwili, na kujifanya mwepesi, vaa nguo zako za kujisitiri, (Uwe mwanamke au mwanaume) na fanya mazoezi yako kwa staha.. na tena si sehemu za kujionyesha onyesha..

Mfano mwingine wa mazoezi yaliyochanganyikana na udunia ni yale yanayofanyika katika majumba maalumu almaarufu kama “Gym”. Majumba ya Gym hayana tofauti na DISKO, kwani kama vile disko kulivyo na kule kumo vivyo hivyo, Disko utakuta watu wamevaa nusu uchi, na GYM ni hivyo hivyo.

Disko utakuta watu (wakike na wakiume) wanaserebuka na midundo ya miziki, na Gym ni hivyo hivyo, utakuta wamepanga mistari na wanafanya mazoezi huku wanaongozwa na ile midundo wakiwa nusu uchi, na hata wakati mwingine kupapasana kana kwamba wanaelekezana au kusaidiana kanuni za mazoezi n.k

Sasa mazoezi kama hayo, Mkristo hapaswi kushiriki wala kufanya kwasababu yamejifungamanisha na mifumo ya kidunia. (1Yohana 2:15)

Kama mkristo ni lazima kuenenda tofuati na dunia siku zote. Kwasababu mambo yanayofanyika duniani karibu yote maudhui yake ni ya kishetani.

Lakini jambo la mwisho la kuzingatia ni kwamba, hata kama umeokoka usitie kipaumbele sana kufikiri kutengeneza mwili, lakini ni heri kufikiri kutafuta afya ya rohoni, kwani ukiipata hiyo hata hiyo ya mwilini itajiweka tu katika uwiano..

1Timotheo 4:8 “Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?

USIWE ADUI WA BWANA

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).

Jibu: Turejee..

Zaburi 69:8 “Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu”.

Msikwao ni Kiswahili cha “Mgeni aliyetoka nchi nyingine”… Mtu aliyetoka Taifa lingine na kuingia katika Taifa lisilo lake ndio anayeitwa “Msikwao”.

Hivyo katika hilo andiko, aliposema nimekuwa Msikwao kwa wana wa mama yangu, maana yake amekuwa kama mgeni asiye wa nchi ile mbele ya ndugu zake (wana wa mamaye).

Maneno hayo Daudi aliyaandika kumhusu yeye, lakini pia yalikuwa ni unabii wa maisha ya Bwana YESU KRISTO. Ukisoma Zaburi nyingi za Daudi zilikuwa ni unabii wa maisha ya BWANA YESU, Kwa mfano Zaburi ya 22 ule mstari wa kwanza unasema…

Zaburi 22:1 “Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu?”

Maneno hayo utayaona Bwana YESU anayataja alipokuwa pale msalabani (soma Mathayo 27:46).

Vile vile unabii wa Yuda kumsaliti Bwana YESU, umeandikwa katika Zaburi 41:9..

Zaburi 41:9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake.”

Na Bwana YESU anakuja kunukuu maneno hayo katika Yohana 13:18…

Yohana 13:18 “Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake”

Sasa tukirejea katika Zaburi hiyo ya 69, ilikuwa inaelezea maisha ya BWANA YESU KRISTO, kwamba kuna wakati ataonekana mbele ya ndugu zake kama mtu aliyetoka nchi ya mbali, maana yake hata ndugu zake watamkataa.. (na ndugu zake wa kwanza ni Taifa la Israeli, na wa pili ni ndugu zake wa damu).

Utauliza ni wakati gani ndugu zake walimwona kama mtu wa ajabu asiye wa kwao (msikwao)?..

Marko 3:21 “Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili”.

Soma pia Yohana 7:5.

Hivyo Zaburi hiyo ya 69 ni unabii wa maisha ya Bwana YESU asilimia zote… Na tunazidi kulithibitisha hilo katika mstari unaofuata wa 9, ambao tunaona baadaye Bwana YESU anakuja kuurejea..

Zaburi 69:8 “Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.

9 MAANA WIVU WA NYUMBA YAKO UMENILA, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata”.

Utaona hapo aliposema “Wivu wa nyumba yako umenila”.. panakuja kujifunua katika Yohana 2:16-17.

Yohana 2:1 “Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.

17  Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, WIVU WA NYUMBA YAKO UTANILA.”

Ni nini tunajifunza?..

Kikubwa tunachojifunza ni UNABII uliopo katika kitabu cha Zaburi, kwamba kumbe sehemu kubwa ya kitabu hiko ni unabii wa maisha ya BWANA YESU, ili kutumiza yale maneno yake aliyoyasema katika Luka 24:44. 

Luka 24:44  “Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii NA ZABURI”.

Hivyo tukisoma kitabu hiko kwa uongozo wa ROHO MTAKATIFU, Tutaona mambo mengi sana yamhusuyo YESU.

Lakini pia mambo mengi yaliyoandikwa katika kitabu hiko yanatuhusu pia sisi, kwani Kristo akiwa ndani yetu nasi tunafanana na yeye, na hivyo sehemu ya maandiko hayo pia yanatimia juu ya maisha yetu..

Maana yake ni kwamba kama KRISTO alionekana Msikwao mbele ya ndugu zake kwasababu anafanya mapenzi ya Baba wa mbinguni, hali kadhalika na sisi tutakutana na vipindi kama hivyo tukiwa katika kuyafanya mapenzi ya Mungu, hivyo endapo yakitokea hayo hatuna budi kusimama na kujitia moyo, kwasababu tayari yalishatabiriwa.

Yohana 16:32 “Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.

33  Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; LAKINI JIPENI MOYO; MIMI NIMEUSHINDA ULIMWENGU”.

BWANA YESU AKUBARIKI.

KUMBUKA KUSOMA NENO LA MUNGU KILA SIKU!!!!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je Adamu na Hawa waliokoka?

Biblia haielezi moja kwa moja kama waliokoka, au hawakuokoka, kwasababu Neno “Kuokoka”, tunalisoma kwenye agano jipya, likimaanisha kukombolewa kutoka katika uharibifu wa hukumu ya Mungu kwasababu ya dhambi kwa kupitia kifo cha Yesu Kristo mwokozi wetu.

Lakini tunaweza kufahamu watu wa agano la kale waliokolewa, kwa kutii kwao ile ahadi ya Mungu aliyoahidi ya kumletea mkombozi duniani baadaye, yaani Yesu Kristo. Hivyo wote waliotembea katika mpango huo wa Mungu, waliokoka. Na mpango wa Mungu wote ulimuakisi Yesu Kristo.

Kwamfano ile safina aliyoijenga Nuhu ilikuwa ni Yesu Kristo, Ule mwamba walionywea wana wa Israeli jangwani ulikuwa ni Kristo, wote waliokataa kuunywea walimkataa Kristo, (1Wakorintho 10:4), Yule nyoka wa shamba alikuwa ni Kristo waliokataa kuitazama, walimkataa Kristo(Yohana 3:14), zile mbao mbili (Amri 10), zilikuwa ni Kristo waliozikataa kuzitii, walimkataa Kristo.  Yule melkizedeki aliyemtokea Ibrahimu alikuwa ni Kristo, wale malaika wawili walioshuka sodoma kuhubiri alikuwa ni Kristo ndani yao, waliowatii walimtii Kristo. Wale wanyama waliochinjwa na damu zao kunyunyizwa katika madhabahu kwa ajili ya upatanisho wa  dhambi za watu walimfunua Kristo, wote waliotii,. Walimtii Kristo ajaye.

Hivyo kila mahali walipotembea, Kristo alijidhirisha kwao kwa lugha ya maumbo na vivuli, na mifano, na maagizo, ili wamwamini yeye. Kwahiyo wote waliomtii katika nyakati zote, waliingizwa katika jopo la watu ambao Kristo atakapofunuliwa basi wataokolewa. Ndio maana baada ya Yesu kufufuka katika wafu miili mingi ya watakatifu ikatoka makaburini, wakahamishiwa peponi, rahani mwa Yesu, kwani hapo kabla watakatifu wote waliokufa walikuwa chini makaburini.

Hivyo kwa msingi huo, tutachunguza kama Adamu na Hawa walimtii Kristo au la, baada ya anguko. Biblia inatuonyesha walipojiona wapo uchi, hawakuendelea kufurahia anguko lile, bali walijificha, kuonyesha majuto ya dhambi zao, ndipo Mungu akamchinja mnyama Yule, akawavika vazi lake. Sasa Mnyama Yule alimfunua Kristo,(Mwanzo 3:21) lakini kama wangekataa basi wasingeweza kuokoka, ndio maana Yesu alisema..pia maneno haya haya kwetu sisi wa siku za mwisho, tuvikwe vazi lake, ili aibu yetu iondoke.

Ufunuo 3:18  Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona

Halikadhali, biblia inataja uzao wa mwanamke kwamba utauponda kichwa uzao wa nyoka. Kuashiria kuwa Hawa hakuwa mwana wa Adui (Mwanzo 3:15). Bali ni zao mbili tofauti kabisa.

Lakini pia watoto wao, mpaka sethi, tunaona walifundishwa njia ya kumtolea Bwana sadaka, na sadaka zile zilikuwa ni Kristo katika maumbo. Ni wazi kuwa wasingeweza kufanya vile kama hawakupokea au kuona kwa wazazi wao.

Na sababu nyingine ya mwisho, Kristo anatajwa kama mwana wa Adamu, hata katika vizazi vile vilivyoorodheshwa anatajwa kama “wa Adamu” (Luka 3:23-38). Asingeitwa hivyo wa Adamu  kama angekuwa ni wa ibilisi,. Mungu hawezi anza na mguu usio sahihi. Atashinda mwanzo, vilevile atashinda mwisho.

Kwa hitimisho ni kwamba Adamu na Hawa hawakupotea, bali walimwamini Kristo, baada ya anguko.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?(Opens in a new browser tab)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?(Opens in a new browser tab)

Nini Maana ya Adamu?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post