Ikiwa wewe ni mwanandoa, ni busara kuwa na maombi yako maalumu kwa ajili ya ndoa yako.
Waweza kutenga siku kadhaa katika wiki, au mara mbili katika wiki, kuwa na maombi maaalimu marefu kwa ajili ya ndoa yako.
Maombi ni nyenzo muhimu katika kuendesha na kufanikisha sehemu zote zamaisha yetu, huduma inahitaji maombi, kanisa linahitaji maombi, taifa linahitaji maombi, wewe unahitaji maombi, vivyo hivyo na ndoa yako pia inahitaji maombi ili iwe na ustawi Bora katika nyanja zote..hata kama huoni tatizo lolote ndani ya ndoa ..bado unahitaji maombi sana.
Kwanini maombi? Ni kwasababu njia pekee ambayo Mungu huweza kuyaingilia maisha yetu ili ayatengeneze vema basi ni kwa njia ya maombi.
Ndoa inaweza ikadumu lakini isiwe na amani, ndoa inaweza ikawa na amani lakini isiwe na mafanikio, ndoa inaweza ikawa na mafanikio lakini imekosa Mungu, vilevile inaweza ikawa na umoja lakini imejaa wivu, inaweza ikawa haina shida lakini watoto wanaokuja wakawa na matatizo, inaweza pia ikawa sawa leo, lakini kesho shetani akaishambulia….Hivyo suala la kuombea ndoa ni jambo la muhimu sana.
Huu ni mwongozo wa maeneo muhimu ya kuombea kila uingiapo katika maombi ya namna hii. (Kila kipengele tumia dakika 30)
Mungu alipomuumba mwanaume na mwanamke na kuwaleta katika ndoa aliwafanya mwili mmoja tena..Maana yake aliweka Muunganiko usiowezekana kibinadamu Wa umoja..
Mathayo 19:5
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
Hivyo hakikisha unaombea ndoa yako Bwana adumishe umoja wenu, uwe umoja kwelikweli, na kamwe pasiwepo matengano. Maana huo ndio mwanzo wa ndoa thabiti
Omba kwa nguvu, huku ukivunja roho za matengano, ukiangalia zaidi maeneo ambayo unaona kabisa yanahatarisha umoja wenu, yenye dalili ya kutaka kuwaachanisha hayo ndio uyaombee zaidi, ikiwa ni kazi, au watu, au magonjwa, mwambie Bwana apatengeneze hapo..tumia si Chini ya dk. 30 kuombea eneo hilo moja tu.
Hivi viwili navyo ni nyenzo kubwa sana katika ndoa thabiti. Bwana aliagiza mwanamume ampende mke wake kama mtu apendavyo mwili wake mwenyewe.. vivyo hivyo aliagiza mke amtii mumewe Kama mtumwa kwa Bwana wake.
Waefeso 5:22-25
[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. [23]Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. [24]Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. [25]Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
[22]Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.
[23]Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
[24]Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
[25]Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
Hivyo ikiwa wewe ni mke, mwombee sana mumeo Bwana alidumishe pendo lake kwako, lakini pia ikiwa wewe ni mume mwombee mkeo Bwana amjengee utii kwako.
Lakini pia jiombee wewe sawasawa na jinsia yako Bwana akuzidishie upendo na utii..kwasababu vyote hivi ni nyenzo kwa wote, vizidi bila kupungua nguvu kwa jinsi siku zinavyokwenda.
Ndoa ikikosa maelewano hupoteza dira yake.
i) Omba Mungu ajenge usemi mmoja yaani lugha ya maelewano kwanza katika eneo lenu la kiroho.. Maana yake wote msisimame katika Bwana (muokoke), ikiwa mmojawapo hajaokoka mwombee neema Ya wokovu, injili imchome abadilike na kumpokea Kristo, na huku ukimhubiria pia.
ii) Omba pia Mungu awape Maelewano Katika majukumu yenu ya kiroho(utumishi). Mfano ratiba za ibadaza nyumbani, maombi, mikesha, mifungo, ushuhudiaji, na utoajik.
Ikitokea mmoja wenu haafiki majukumu hayo, si rahisi mwingine kutekeleza na matokeo yake inakuwa ni kushindwa kutimiza lengo kuu la kindoa. Kumbuka mmewekwa katika ndoa ili mumtumikie Mungu pamoja..hivyo jambo hilo ni lazima Lipewe nafasi ya kwanza na kubwa katika ndoa.
iii) Lakini pia omba maelewano katika mambo Yote ya kimaisha.
Mfano mikakati ya kimaendeleo, matumizi ya kifedha, n.k. huku ukigusia Maeneo yako yote ambayo unaona mikwaruzano inatokea, Au dalili hizo kutokea..ukiharibu hivyo vyanzo kwa maombi yako.
iv) Lakini pia Bwana awajengee mioyo ya kusamehe na kuachilia.
Ndoa nyingi zimeingia dosari, kupoa hata kufikia hatua ya kuvunjika kabisa kutokana na kuwa zimepoteza mioyo wa kusamehe na kuachilia Kwasababu ya majeraha au makosa yaliyofanyika nyuma..
Wakolosai 3:13
[13]mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
Mwambie Bwana sikuzote, wote mpewe mioyo ya kusamehe na kuachilia.
Hapa pia ni mahali pa kupaombea sana.. Wengi wanadhani wanaweza linda ndoa zao kwa kuweka sheria kali, kwa kufuatilia nyendo zao, kwa kuwavisha mavazi ya kuficha mpaka nyuso, Lakini uhalisia ni kwamba ikiwa mtu amekosa uaminifu, huyo kamwe halindiki, atakuzunguka tu, Hivyo omba kwa Bwana juu ya mwenzi wako, na kwako pia Bwana awaumbie moyo wa uaminifu. Hilo linatosha kuwa ulinzi mkubwa kwa ndoa yako.
Nyuma ya mafanikio ya kitu chochote chema, ni lazima utaona uvumilivu ulipewa nafasi, hata huduma ya kufanikiwa hutegemea uvumilivu. Ndoa haimaanishi kila siku itakuwa ni furaha tu, zipo nyakati za kupishana kibinadamu, za kusemwa vibaya, za kuudhiwa zipo nyakati za kupungukiwa, yapo madhaifu pia.. Hivyo omba moyo wa uvumilivu thabiti uwe juu ya kila mwanandoa.. kuanzia wewe mwenyewe.Ili nyakati ngumu zitakapopita pasiwe na wepesi wa kuiacha ndoa au kuchukua Hatua za madhara.
Ndoa ikikosa mwelekeo wa ki-Mungu huishia pagumu. Omba Mungu awape dira sahihi isiyo na majuto katika mikakati yenu yote ya kimaisha.
Omba Bwana ayanyoshe mapito yenu, awafanikishe, awaepushe na njia ya majuto na upotevu wa yule mwovu.. kwasababu maandiko yanatuonyesha ndoa ya kwanza ilivamiwa na uharibifu kwasababu ya udanganyifu wa ibilisi, kwa kitendo cha Hawa kusikiliza na kuifuata njia nyingine ambayo hakuagizwa na Mungu, na matokeo yake alipokula tu lile tunda ikasababisha matatizo makubwa ambayo mpaka sasa tunayaona ..
Mafanikio Ya ndoa hutegemea pia mahusiano mema kwa ndugu na wakwe..Musa alifanikiwa kuiongoza huduma vizuri kwasababu alikuwa na mahusiano mazuri na mkwe wake Yethro. Ruthu alifanikiwa kuolewa na Boazi mtu mkuu na mwenye uwezo kwasababu alikuwa na ukaribu na mama mkwe wake Naomi hata baada ya kufiwa na mumewe.
Vivyo hivyo na wewe pia uhusiano wako ukiwa mzuri na watu wa upande wa mwenzi wako unaharakisha baraka na neema nyingi za Mungu.
Lakini pia ikiwa mahusiano ni mabovu, basi ndio utumie fursa hii kuombea utapatanisho haraka, sana. Eneo hili ni muhimu sana kuliombea, ijapokuwa wengi hulipuuzia.
Ikiwa ni ndoa ambayo tayari inayo watoto ni muhimu kuwaombea watoto wako daima, wasiwe chanzo cha nyinyi kufarakana, lakini kuwa mwiba na uchungu kwenye ndoa yenu.
Lakini ikiwa bado hamjawa na watoto, ombea uzao wako ujao ukawe faraja na neema kwenu. Watoto wakiwa wabovu wanaweza kuihatarisha ndoa yako, au kuifanya isiwe na amani. Hivyo waombee sana wokovu, ulinzi, afya, adabu.
Shalom.
Ukizingatia kuviombea vipengele hivyo, kila kipengele si chini ya nusu saa. (dakika 30), utaona neema kubwa sana ya Mungu ikifanya kazi katika maisha yako.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
NDOA NA TALAKA:
Print this post
Katika agano la lake, iliruhusiwa Kufanya hivyo, ikiwa mtu amefiwa na ndugu yake na hana mtoto, aliruhusiwa kwenda kumwoa mke wa ndugu yake ili amwinulie uzao, lakini halikuwa kwa lengo la kimahisiano ya kindoa kana kwamba ni wapenzi. Bali kwa kusudi tu la kumwinulia uzao.
Kumbukumbu la Torati 25:5-10
[5]Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe. [6]Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli. [7]Na yule mtu kwamba hapendi kumtwaa mke wa nduguye, aende huyo mke wa nduguye langoni kwa wazee, akawaambie, Nduguye mume wangu yuakataa kumsimamishia nduguye jina katika Israeli, hataki kunitimizia yampasayo nduguye mume wangu. [8]Ndipo wamwite wazee wa mji wake waseme naye; naye akisimama na kusema, Sitaki mimi kumtwaa mwanamke huyu, [9]ndipo mke wa nduguye amkaribie mbele ya hao wazee, amvue kiatu chake mguuni mwake, na kumtemea mate ya uso; kisha atajibu yule mwanamke, aseme, Mume akataaye kumjengea nduguye nyumba yake na afanywe hivi. [10]Na jina lake katika Israeli liitwe, Nyumba ya mvuliwa kiatu.
[5]Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe.
[6]Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli.
[7]Na yule mtu kwamba hapendi kumtwaa mke wa nduguye, aende huyo mke wa nduguye langoni kwa wazee, akawaambie, Nduguye mume wangu yuakataa kumsimamishia nduguye jina katika Israeli, hataki kunitimizia yampasayo nduguye mume wangu.
[8]Ndipo wamwite wazee wa mji wake waseme naye; naye akisimama na kusema, Sitaki mimi kumtwaa mwanamke huyu,
[9]ndipo mke wa nduguye amkaribie mbele ya hao wazee, amvue kiatu chake mguuni mwake, na kumtemea mate ya uso; kisha atajibu yule mwanamke, aseme, Mume akataaye kumjengea nduguye nyumba yake na afanywe hivi.
[10]Na jina lake katika Israeli liitwe, Nyumba ya mvuliwa kiatu.
Halikadhalika tunapokuja kwenye agano jipya hatuoni pia agizo lolote la moja kwa moja linalokatazama ndugu kuoa mke wa ndugu yake aliyekufa…
Zaidi inasema mwanamke Yeyote anapokuwa mjane yupo huru kuolewa na ‘Yeyote’ amtakaye katika Bwana..
1 Wakorintho 7:39
[39]Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.
Warumi 7:3
[3]Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.
Hiyo ikimaanisha kuwa anaweza akawa huru kuolewa hata na ndugu wa kaka yake (aliyefariki)…
Lakini lazima tufahamu kuwa si kila jambo linalohalalishwa kibiblia linaweza likafaa katika mazingira yote au majira yote, yapo mambo mengine ya kuzingatia, mfano utamaduni wa mahali fulani..
Kwasababu Biblia bado inatuambia…
1 Wakorintho 10:23
[23]Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.
Kwa mfano kwa wayahudi ilikuwa ni tamaduni Watu kusalimiana kwa ‘busu’ la upendo. Lakini katika mazingira ya jamii zetu jambo kama hilo huleta ukakasi, au kutoa tafsiri nyingine hata kama nia sio mbaya..ndio maana tunaishia kipeana mikono, na ikizidi sana kukumbatiana kwa jinsia tu zinazofanana.
Vivyo hivyo katika jambo hili, kuoa mke wa ndugu yako aliyefariki, kijamii halina munyu ndani yake.
Hivyo twaweza sema kijamii halikubaliki, lakini kibiblia halijakatazwa..ukiniomba mimi ushauri nitakuambia usifanye hivyo..kaoe pengine..lakini ukimwoa mke wa ndugu yako aliyekufa pia hujafanya dhambi ikiwa tu, pana makubaliano kamili katika pande zote mbili, lakini pia wewe mwenye uwe haupo katika ndoa.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.
https://wingulamashahidi.org/2019/08/31/bwana-yesu-alikuwa-anamaanisha-nini-kusema-marko-219%e2%80%b3walioalikwa-harusini-wawezaje-kufunga-maada
SWALI: Je! tunalisoma wapi kwenye maandiko panasema ndoa inapaswa ifungwe kanisani. Utaratibu huo upoje?
JIBU: Ili kujibu swali hili tuanzie mbali kidogo.
kufahamu ndoa ni nini? aina za ndoa, kisha mahali sahihi pa kufungia ndoa ni wapi?.
Ndoa ni muunganiko kati ya watu wawili(mwanaume na mwanamke ) unaotambulika na kuheshika kijamii, au kisheria.
Pale mwanaume anapomwona mwanamke na kupatana naye waishi pamoja kama mume na mke, kwa kufuata taratibu husika za kijamii, labda kukutanishwa kwanza wazazi, au walezi, wazee wa ukoo, kupokea mahari, kisha kuidhinisha jambo hilo, au serikali kuidhinisha, hiyo tayari inaitwa ndoa.
Aina mbili za ndoa.
Ndoa za wapagani. Hizi ni ndoa lakini hazijadhibitiwa na kanuni timilifu za Mungu. Mfano wa hizi, ndio hizo kama za kijamii, na kiserikali, au za dini nyingine zote mfano wa ki-hindu, kiislamu, ki-budha n.k. zote hizi ni ndoa za wapagani.
Zingatia: (Hapa hatumaanishi zile za mashetani, kama za jinsia moja, au za wanadamu na wanyama hapana kwasababu hizo sio ndoa, bali tunazungumzia hizi za kawaida kabisa za asili).
Kiuhalisia mtu anaweza akawa katika mojawapo ya ndoa hizi, na asihesabike kuwa ni mkosaji kwasababu ndoa hasa ni jambo la kiutamaduni, ambalo huusisha wanadamu wote, bila kuchagua dini, rangi, au kabila.
Hivyo si sawa kudhani kuwa kwasababu watu fulani hawajafungishwa ndoa kikristo(kanisani) basi, zote hizo sio ndoa kwamba ni sawa tu hata kwenda kuoa tena hapo, au kuivuruga, wasiishi pamoja. Ukifanya hivyo Mungu atakuwajibisha kwa kuzivuruga ndoa za watu wengine.
Aina ya pili ya ndoa ni ndoa ya kikristo.
Hii ni ndoa inayofungwa katika kanuni timilifu za Mungu alizozikusudia tangu mwanzo.
Kanuni zenyewe ni hizi
i) Wote wawe waamini.
(1Wakorintho 7:39, 1Wakorintho 9:5, 2Wakorintho 6:14 – 16)
Kuamini si lazima muwe katika viwango sawa kiroho, lakini wote muwe upande mmoja wa Kristo, (Kwasababu hayo mengine yanaweza rekebika). Lakini mmoja ni mganga wa kienyeji, mwingine mkristo,.au mmoja ni muislamu mwingine mkristo. Hilo si sawa ni sharti wote wawe wakristo. Kwasababu hakuna ushirika wowote kati ya nuru na giza.
Kwasababu Ndoa ya kikristo ni lazima iwe katika jina la Bwana, vinginevyo, itaangukia katika lile kundi lingine.
ii) Mume mmoja, mke mmoja.
Tofauti na ndoa za wapagani. Ambazo kwao unaweza kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini mtu anayetaka ndoa yake itimilike mbele za Kristo, basi mume/mke atambue kuwa hana ruhusa ya kuongoza mwenza mwingine.
Mathayo 19:4-5
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, [5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? a
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? a
iii) Malazi yawe safi:
Waebrania 13:4
[4]Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
Malazi kuwa safi maana yake ni nidhamu ya kiasi, katika kukutana kimwili. Mkristo hapaswi kuwa mtu wa hulka ambaye wakati wote anawaza zinaa, mpaka anakosa muda wa kujishughulisha na mambo ya rohoni.
1 Wakorintho 7:5
[5]Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Vilevile viitendo kama kuingiliana kinyume na maumbile haviruhusiwi ndani ya ndoa (1Wakorintho 6:9).
iv) Hakuna talaka.
Tofauti na ndoa za wapagani, mtu anaweza kuacha/kuachwa kwa sababu yoyote, labda mfano wamechokana, au wameudhiana, lakini katika ukristo hilo jambo halipo mtaendelea kuishi pamoja mpaka kifo kitakapowatenganisha.
Bwana alitoa ruhusa hiyo katika eneo la uasherati tu lakini ukumbuke, alisema pia ‘samehe mara saba sabini’. Hivyo kwa kauli hiyo hakuna popote tunaona wigo wa wanandoa kuachana kwa sababu yoyote ile.(1Wakorintho 7:39-40)
V) Mume ni sharti ampende mkewe.
Mume kumpenda mkewe ni amri ya kindoa, anawajibu wa kumtunza na kumuhudumia na kujitoa kwa ajili yake, kama Kristo alivyolipenda kanisa.(Waefeso 5:25-31)
Vi) Mke ni sharti amtii mumewe.
Ni amri mke amtii mumewe kwa agizo atakaloambiwa/ elekezwa. Tofauti na ndoa za wapagani ambazo hili linaweza lisiwe la muhimu. Kwenye ukristo, ni lazima utii wa mwanamke uonekane kwa mumewe.
Waefeso 5:22
Sasa vigezo hivi wakivikidhi hawa wakristo ambao wameokoka na wanatarajia kuishi kama mke na mume. Basi hiyo huitwa ndoa ya Kikristo iliyokidhi vigezo vitimilifu vya Mungu,.haijalishi imefungwa kanisani au kwenye familia, .
Swali ni je? kwanini watu wafungie kanisani? Na Je ni takwa?
Mkristo ambaye anathamini ukamilifu wote wa ki-Mungu, katika maeneo yake yote ya kiroho na kimwili, kufungia ndoa yake kanisani itakuwa ndio chaguo lake bora. Kwanini iwe hivyo?
Hizi ndio faida za ndoa kufungiwa kanisani
Biblia inatueleza mashtaka yetu, hayapaswi kutatuliwa na watu wa ulimwengu, bali ndani ya kanisa. Kwasababu kanisa ni zaidi ya mahakama yoyote, ambayo Mungu ameiheshimu mpaka akaamua malaika zake wahukumiwe katika hiyo.
Hivyo endapo kuna migogoro, au kutoelewana, au kupatiwa misaada, au mashauri, au maonyo, au maongozi, basi kanisa, limewekwa na Mungu kwa ajili yako kukusaidia katika hayo yote.
Lakini ikiwa hukuifungia ndoa yako kanisani. Fahamu kuna mambo kama hayo yatakupita, au yatakuwa magumu kwetu kutatulika.
1 Wakorintho 6:1-3
[1]Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? [2]Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? [3]Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
[1]Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?
[2]Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?
[3]Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?
2) Ushuhuda mwema.
Mungu anapenda mambo mema atufanyiayo tumtukuze mbele ya kusanyiko la watakatifu. Tunajua Ndoa ni kitu chema, hivyo tunapoweka wazi mbele za Bwana, na mbele ya kanisa lake, yeye hutukuzwa lakini pia tunapokea baraka za kanisa, Ikiwa tunapoumwa na kuponywa hatuoni sawa kukaa na shuhuda zetu ndani, tunakwenda kushuhudia mbele ya kanisa, si zaidi ndoa zetu?, ni ushuhuda mkubwa, ambao utawafariji wengine, lakini pia utaihubiri injili ya Kristo.
Zaburi 35:18
[18]Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; Nitakusifu kati ya watu wengi.
[18]Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa;
Nitakusifu kati ya watu wengi.
Hivyo, kwa maelezo hayo tunaweza kusema hakuna sababu ya Mkristo yoyote kuifungia ndoa yake, mbali na kanisa.
Lakini hiyo haimaanishi kuwa usipofungia kanisani, ndoa yake haitambuliwi na Mungu. Maadamu umekidhi vigezo “mama”, tulivyoviorodhesha juu. Hiyo ni ndoa.
Bwana akubariki
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
MAFUNDISHO YA NDOA.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?
Rudi Nyumbani
WhatsApp
Mafundisho maalumu kwa wanandoa – Wanawake.
Ikiwa utapenda kupata mafundisho mengine ya namna hii, basi fungua link hii uweze kuyasoma. >>.
https://wingulamashahidi.org/category/mafundisho-ya-wanandoa/
Habari ya Samsoni na Delila inafundisho kubwa nyuma yake kwa wanandoa. Wengi wanafikiri Delila alikuwa mwanamke kahaba ambaye Samsoni alimuokota tu na kukutana naye. Lakini uhalisia ni kwamba Delila alikuwa ni mke wa Samsoni.
Lakini mwanamke huyu, aliweza kubadilishwa akili kwa tamaa tu ya fedha. Ni mwanamke ambaye alipendwa sana na Samsoni, chochote ambacho angetaka kwa Samsoni angepatiwa. Lakini Wafilisti walipoona mwenendo wa Samsoni jinsi alivyompenda sana mwanamke huyu. Wakatumia fursa ile, kumshawishi Delila, kwa kumuahidia donge kubwa la fedha. Ili tu atoe siri ya asili ya nguvu zake.
Delila, akakubali, akaanza kumshawishi Samsoni, kwa kipindi kirefu, na hatimaye akafunuliwa siri ya nguvu zake. Akaenda akaziuza kwa wafilisti, kwa vipande vya fedha.
Waamuzi 16:4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila. 5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja. 6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.
Waamuzi 16:4 Ikawa baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la Soreki, jina lake akiitwa Delila.
5 Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.
6 Delila akamwambia Samsoni, Tafadhali uniambie asili ya nguvu zako nyingi, na jinsi uwezavyo kufungwa, ili uteswe.
Kama mke, upendo wako unapohamia kwenye fedha, ni dalili madhubuti kuwa unaua nguvu ya ndoa yako (ambayo ipo kwa mume). Usitangulize mali mbele ya ndoa yako, wala usishawishiwe na fedha kwa chochote ukadharau thamani ya mumeo. Samsoni hakuwa mfanya biashara au mwajiriwa wa kampuni Fulani, hakuwa hata na akaunti benki. Lakini alikuwa mwamuzi wa Taifa teule la Mungu. Mtetezi wa wanyonge, na mkombozi wa walioonewa, hakujitajirisha yeye, alilitajirisha taifa,. Jambo ambalo Delila hakulithamini. Akawa tayari kuoelewa na fedha(wafilisti) na sio nguvu zake(Samsoni).
Leo wapo wamama, ambao wanachotafuta kwa waume zao ni fedha tu,fedha tu, fedha tu.. wakikosa hiyo wapo tayari kufanya chochote. Wengine hata kuanzisha mahusiano na watu wengine wenye uwezo wa juu, hawajua kuwa mwanaume anaweza asiwe tajiri kifedha, lakini ana nguvu za kuiendesha na kuilinda familia yako, jamii yako, ndugu zako, kipawa alichonacho kikaweza kukufanya wewe ukae vizuri au kuistaajabisha jamii au taifa, Lakini endapo tu utakiona hicho na kukithamini ndani yake.
Hivyo, kama mwanamke, toa moyo wako hapo kabisa.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?
KITENDAWILI CHA SAMSONI
Je! mtu anapofunga kwa muda wa SAA 24,anapaswa kunywa maji au kitu chochote?
Ndoa za wake wengi ni za ibilisi!..ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!… ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!!. Hali kadhalika ndoa za waume wengi ni za ibilisi, kama tu zilivyo za jinsi moja (zote ni zao la ibilisi).
Zipo hoja kuwa kwasababu Daudi, Sulemani na manabii wengine wakale walioa wake wengi, basi hata leo ni halali kuoa wake wengi.. tena zipo hoja zifananishazo wanyama wa porini na wa kufungwa na uhalali wa kuoa wake wengi.
Hoja zote hizi ni za ibilisi… Ndugu, usiongeze wake, wala wala usiongezee waume.
Bwana YESU alipokutana na yule mwanamke Msamaria kisimani hakumwambia akawalete WAUME ZAKE!.. Ingawa alikuwa ana wanaume wengi (na Bwana alilijua hilo), lakini alimwambia nenda “kamlete mumeo”… ikimaanisha kuwa ndoa halali na takatifu ni ya mume mmoja na mke mmoja.
Sasa Kristo alikuwa anamjua Sulemani, na Daudi..
Yohana 4:15 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka. 16 Yesu akamwambia, NENDA KAMWITE MUMEO, uje naye hapa. 17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli”.
Yohana 4:15 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
16 Yesu akamwambia, NENDA KAMWITE MUMEO, uje naye hapa.
17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;
18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli”.
Bwana YESU kabla ya kukutana na huyu mama, alikuwa anamjua Daudi pamoja na Sulemani na idadi ya wake wake waliooa!.. Lakini tunaona hakumwambia huyu mwanamke Msamaria, kwamba akawalete waume zake!!.. Bali alimwambia kamlete mumeo! (maana yake mmoja tu).. bado huoni tu, kuwa ndoa za mitara ni batili na za ibilisi!.
Na tena biblia inasema hapo Mwanzo Mungu alimwumba mwanaume na mwanamke, na si mwanaume na wanawake, au mwanamke na wanaume (soma Mwanzo 1:27 na Mathayo 19:4).
Huoni kuwa ndoa hizo za wake wengi zitakukosesha maji ya uzima!.. Na pia fahamu kuwa ndoa za wake wengi sio zile tu zinazohusisha mtu kuwa na wake wengi katika boma moja kwa wakati mmoja…la! Hata zile za kuacha na kuoa mwingine ilihali yule wa kwanza bado yupo hai.. hiyo ni mitara! Ndicho kilichokuwa kwa huyu mwanamke Msamaria.
Huyu mwanamke msamaria alikuwa na wanaume watano kulingana na darubini ya kimbingu! Ingawa haishi nao, lakini alikuwa nao watano, na anayeishi naye ni wa 6, vile vile kuna watu leo hii wamecha wake zao na kuoa wengine, na kuacha tena na kuoa wengine, (hawa hawana tofauti na wale waliooa wake wawili na kuishi nao wote kwa pamoja).
Na madhara ya ndoa za mitara ni “KUKOSA MAJI YA UZIMA”..
Yapo maji ya Uzima tuyanywayo hapa Duniani, na yapo yale tutakayoyanywa katika mbingu mpya na nchi mpya.
Maji ya Uzima duniani ni YESU KRISTO, tumpatapo yeye tunapata uzima wa milele (Yohana 4:14), lakini ukijiunganisha na hizi ndoa za mitara hawezi kuingia ndani yako!.. vile vile maji ya uzima baada ya maisha haya tutayanywa kutoka katika ule mto wa maji ya Uzima katika mbingu mpya na nchi mpya.
Ufunuo 22:1 “Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, 2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa. 3 Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia; 4 nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao. 5 Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele”.
Ufunuo 22:1 “Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.
3 Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;
4 nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.
5 Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele”.
Neema ya Bwana YESU itufunike.
VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.
NDOA NI NINI?
KUWA NA MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.
Kwanza ni vema kufahamu uzazi wa mpango ni nini na kama ni dhambi au la!.
Uzazi wa mpango ni kuzaa kwa mpangilio ulioutaka wewe, kwamfano ukijiwekea malengo ya kuzaa watoto 30, huo ni uzazi wa mpango maadamu yalikuwa ni malengo yako, au ukijiwekea malengo ya kuzaa mmoja maisha yako yote huo pia ni uzazi wa mpango. Kinyume chake uzao usio wa mpango, ni ule wa kutojali idadi ya watoto utakaouzaa, wala kutojali muda wa uzaaji wako.
Ukweli ni kwamba uzazi wa mpango si dhambi. Kwasababu gani?
Licha ya kwamba Mungu ameweka maagizo yake kupitia biblia takatifu, lakini pia, ameweka hekima yake kupitia mambo ya asili (1Wakorintho 11:14, Warumi 1:20), Hivyo mambo ya asili yanatufundisha pia agizo la Mungu .
Si kila wakati mama atashika ujauzito, bali upo wakati wa hatari na wakati usio wa hatari. Sasa kwa hekima huo tayari ni utaratibu Mungu kamwekea mtu, atambue majira yake, achukue tahadhari. Umeona? Kwa namna nyingine Mungu anasema, kuna majira utapata mtoto, na kuna majira hutapata mtoto. Hivyo uamuzi ni wako, ukitaka kuzingatia mazunguko huo, ni wewe, usipojali pia ni wewe.
Sasa mtu ambaye anayechagua kuzingatia mzunguko huo wa asili wa Mungu, huyo tayari yupo katika uzazi wa mpango. Na pia ni agizo la Mungu tuwe na uwezo wa kuwatunza wale wa nyumbani kwetu (1Timotheo 5:8)
Lakini je! Vipi ambao wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango je na wao wapo sawa?
Tukisema njia za kisasa, ni kama zile za kutumia vidonge, kutumia sindano, kutumia vizuizi kama mipira (kwa wanaume na wanawake), kuweka kitanzi, na kuweka vipandiki/vijiti. Zote hizi ni njia za kisasa.
Hapa ni lazima tufahamu pia lengo ni nini?. Bila shaka lengo ni lile lile moja la uzazi wa mpango kwa wanandoa, na si vinginevyo. Lakini mwanadamu ameamua kutumia njia zake za kisasa, ili kufanikisha hilo?
Je! Ni kosa?
Ili kujibu swali hilo, tufikirie pia mambo mengine ya kisasa, leo hii tuna vitu vingi vya kisasa vimebuniwa na wanadamu, kwamfano kuna kuku wa kienyeji lakini pia wapo wa kisasa, kuna mchicha wa kienyeji lakini pia ipo ya kisasa, kuna matunda ya kienyeji lakini pia yapo ya kisasa. Je! Ni dhambi kutumia vitu hivyo, kwasababu vimebuniwa na mwanadamu?
Jibu ni hapana.
Lakini vinaweza kuwa na madhara yake, kwasababu mwanadamu hawezi kuumba kitu kiukamilifu. Ndio maana asilimia kubwa ya vitu hivi vya kisasa, huwa si vizuri kiafya. Vivyo hivyo katika matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Yaweza isiwe dhambi kwako kutumia. Lakini madhara ya kiafya, pia waweza kukumbana nayo. Wengine hupata shida ya vizazi, wengine ugumba kabisa kulingana na njia iliyotumika, lakini wengine hawapatwi na madhara. Hivyo amani ya Kristo iamue ndani yako.
Lakini ile y asili ni bora zaidi. Ukitumia njia ya kalenda, ni salama lakini pia Mungu ametubunia hiyo, ukijizoesha kuifuatilia utaweza tu kupangilia uzazi wako.
Lakini fahamu pia uzazi wa mpango, maadamu amani ya Kristo imeamua moyoni mwako, si dhambi mbele za Mungu.
Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?
JE! KUBET NI DHAMBI?
Je Kutoa Mimba ni dhambi?
SWALI: Nini maana ya Kumbukumbu 25:11
Kumbukumbu 25:11 “Washindanapo waume wao kwa wao, akakaribia mke wa mmojawapo, ili kumwokoa mumewe katika mkono wa ampigaye, yule mke akatoa mkono wake, na kumkamata tupu yake; 12 umkate ule mkono wake, lisiwe na huruma jicho lako”
JIBU: Bwana asifiwe, Haya ni mafundisho maalumu wayahusuyo wana-ndoa. Lakini pia kanisa la Kristo.
Kama ukiutafakari mstari huu, utaona picha ya mwanamke mwenye huruma, ambaye, ameona mume wake, anapigana na adui yake, na pengine alikuwa anakaribia kushindwa. Hivyo kwasababu ya upendo wake kwa mumewe, akaamua kwenda kumwokoa. Lakini tunaona njia aliyoitumia badala imletee alilolitarajia, ikamletea matatizo yeye mwenyewe.
Kwasababu gani? Kwasababu alikwenda kugusa sehemu zake za siri, Na hiyo ikawa kosa kwake, lililostahili adhabu ya kukatwa mkono. Laiti kama angemkamata mahali pengine labda tuseme mguuni, au penginepo, ni wazi kuwa kusingekuwa na adhabu yoyote au adhabu iliyo kali namna ile.
Ni mipaka ya mwanamke awapo ndani ya ndoa yake. Fikiria hata kwa adui ya mume wake huyu mwanamke, hukupaswa kuvuka mipaka ya kindoa, si zaidi kama angefanya hivyo kwa rafiki wa karibu wa mume wake ndio ingekuwa kosa kubwa kabisaa?. Leo hii kumekuwa na migogoro mingi ndani ya ndoa, na ukitazama utagundua tabia ya wanawake kutojiwekea mipaka yao, wakutanapo na wanaume wengine wa nje.
Kwamfano mwanamke yupo kazini. Halafu Boss wake/ mfanyakazi mwenzake anazungumza mazungumzo ya mizaha, ya kizinzi, utaona na yeye analiridhia hilo, au kulifurahia au anaona ni kawaida tu. Anashindwa kujiwekea mipaka, Anaipoteza nidhamu yake, anaruhusu mazoea yaliyopitiliza ambayo hayampasi mtu kama yeye kuwa nayo. Sasa hiyo ni hatari kubwa.
Wewe kama mwanamke unapaswa ujiwekee mipaka ya hali ya juu. Ukiona migororo inaendelea baina ya wanaume, jiwekee mipaka ya kitabia na kimwenendo. Uwe salama, ili mkono wako usifike kusikostahili. Uvaaji wako, usemi wako, uwe kama mtu aliye kwenye “KIFUNGO” cha ndoa. Watu wakuheshimu, wenye mizaha wakuonapo wakae kimya. Usiruhusu kabisa mazungumzo yako na mtu mwingine yafike kwenye maeneo ya sirini, iwe kwenye simu, ofisini, njiani, shuleni, mtaani, nyumbani, au popote pale. Weka MLANGO mkubwa wenye makomeo ya chuma . Mazungumzo hayo yawe na mume wako tu, na sio mwingine yoyote.
Halikadhalika inatupa na picha ya rohoni pia. Sisi kama kanisa ni lazima tufahamu kuwa wote ni “WAKE” wa Bwana wetu Yesu Kristo. Na hivyo anataka tuwe na tahadhari tuendapo kumuhubiri yeye kwa watu wa nje, tujichunge tusijaribiwe wenyewe, kwa vitendo vyao. Kwasababu itatugharimu kinyume chake.
Tukutanapo na wazinzi kuwahubiria, tusivutwe kwenye uzinzi wako, tukutanapo wa watukanaji, tusirudishe matusi, tukutanapo na wenye fedha, tusigeuzwe injili yetu. Bali tubaki kwenye mipaka yetu ile ile.
Wagalatia 6:1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”
Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?
Rudi nyumbani
(Masomo maalumu kwa wanandoa).
Je unamjua Klopa au Kleopa kwenye biblia?.. na tena unamjua Mke wake?
Tuanze kwa mke wa Klopa, kabla hatujaenda kwa Klopa mwenyewe…
Jibu: Tusome,
Yohana 19:25 “Na penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, MARIAMU WA KLOPA, na Mariamu Magdalene”.
Mariamu wa Klopa alikuwa ni mke wa mtu aliyeitwa Klopa. Na kwanini aliitwa vile kwa sifa ya jina la Mume wake?.. ni kwasababu ya mwenendo wa mume wake. Laiti kama mume wake angekuwa na sifa mbaya, basi biblia isingemtaja huyu Mariamu kwa sifa ya jina la mumewe, lakini mpaka imemtaja mumewe ni kuonyesha kuwa alikuwa na kitu cha kipekee.
Sasa huyu Klopa/Kleopa ni nani?
Huyu Klopa au Kleopa ndio yule aliyetokewa na Bwana Yesu akiwa na mwenzake walipokuwa wanaelekea kijiji kimoja kilichoitwa Emau, baada ya Kristo kufufuka,.. wakiwa katika mazungumzo yao, maandiko yanasema Yesu mwenyewe aliungana nao pasipo wao kumtambua, na baadaye walifumbuliwa macho na kumtambua na kutoweka.
Tusome,
Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. 14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. 15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. 16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue. 17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao. 18 AKAJIBU MMOJA WAO, JINA LAKE KLEOPA, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? 19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; 20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. 21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo; 22 tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, 23 wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. 24 Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona…” Umeona? Kumbe Kleopa alikuwa ni miongoni mwa wafuasi wa Bwana Yesu, lakini cha kipekee ni kwamba na mke wake pia alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana na ndiye aliyekuwa pale msalabani pamoja na Mariamu Magdalena na Mariamu mamaye Yesu. Kwa kifupi walikuwa ni watu waliompenda sana Bwana Yesu, ni watu waliokuwa wanafuatilia sana habari za Bwana Yesu, wakati mke wa Kleopa akiwa kule kaburini pamoja na akina Mariamu Magdalena, Bwana aliwatokea wao wa kwanza, kabla hata ya akina Petro, na Yohana, na Andrea na mitume wengine wote. Na kabla Bwana hajawatokea mitume wake (akina Petro na wengineo), aliwatokea Kleopa na mwenzake ( hawa wawili ndio wanaume wa kwanza kumwona Bwana aliyefufuka). Akina Petro baada ya kupewa taarifa walienda kaburini lakini hawakumwona, lakini akina Kleopa hawakufika kaburini lakini walimwona wa kwanza, tena Zaidi sana walikuwa wanaondoka Yerusalemu lakini Bwana aliwafuata huko na kuwatokea wao kwanza, na tena Bwana ndiye aliyekula nao wa kwanza, na zaidi sana aliwatumia hao kwenda kuwashuhudia mitume 12 kuwa Bwana kafufuka kweli kweli, na walipokwenda Yerusalemu kuwashuhudia ndipo Kristo alipojidhihirisha kwa mitume wake. Luka 24:31 “Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao. 32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko? 33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao, 34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni. 35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate. 36 Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu. 37 Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho. 38 Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? 39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”. Ni nini tunajifunza kwa Kleopa na Mkewe?
Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.
14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.
15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.
16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue.
17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.
18 AKAJIBU MMOJA WAO, JINA LAKE KLEOPA, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?
19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;
20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.
21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;
22 tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema,
23 wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai.
24 Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona…”
Umeona? Kumbe Kleopa alikuwa ni miongoni mwa wafuasi wa Bwana Yesu, lakini cha kipekee ni kwamba na mke wake pia alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana na ndiye aliyekuwa pale msalabani pamoja na Mariamu Magdalena na Mariamu mamaye Yesu.
Kwa kifupi walikuwa ni watu waliompenda sana Bwana Yesu, ni watu waliokuwa wanafuatilia sana habari za Bwana Yesu, wakati mke wa Kleopa akiwa kule kaburini pamoja na akina Mariamu Magdalena, Bwana aliwatokea wao wa kwanza, kabla hata ya akina Petro, na Yohana, na Andrea na mitume wengine wote. Na kabla Bwana hajawatokea mitume wake (akina Petro na wengineo), aliwatokea Kleopa na mwenzake ( hawa wawili ndio wanaume wa kwanza kumwona Bwana aliyefufuka).
Akina Petro baada ya kupewa taarifa walienda kaburini lakini hawakumwona, lakini akina Kleopa hawakufika kaburini lakini walimwona wa kwanza, tena Zaidi sana walikuwa wanaondoka Yerusalemu lakini Bwana aliwafuata huko na kuwatokea wao kwanza, na tena Bwana ndiye aliyekula nao wa kwanza, na zaidi sana aliwatumia hao kwenda kuwashuhudia mitume 12 kuwa Bwana kafufuka kweli kweli, na walipokwenda Yerusalemu kuwashuhudia ndipo Kristo alipojidhihirisha kwa mitume wake.
Luka 24:31 “Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao.
32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?
33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,
34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.
35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate. 36 Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.
37 Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho.
38 Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
Ni nini tunajifunza kwa Kleopa na Mkewe?
Kikubwa tunachoweza kujifunza kutoka kwao ni roho na moyo wa kumpenda na kumfuatilia Bwana sana, Kleopa na Mke wake walikuwa ni watu waliomsogelea sana Bwana ndio maana hata taarifa za kufufuka kwa Bwana wao ndio wa kwanza kuzipata. Wote wawili walikuwa ni watu waliompenda Bwana, hakuna hata mmoja aliyemzuia mwenzake katika kumtafuta Bwana.
Na wewe kama Baba kuwa kama Kleopa, usimzuie mke wako kumtafuta Mungu, au kuwa karibu na Mungu muda mwingi, vile vile na wewe mama, kuwa kama mke wa Kleopa, usimzuie mume wako kwenda katika kutafuta uso wa Mungu, wote mfanyeni Kristo kuwa wa Kwanza, na Kristo atawachagua nyie kumwona yeye wa kwanza kabla ya wengine.
Mtamwona Yesu katika familia yenu wa kwanza kabla ya wengine.
Mtaona wema wa Kristo kwenye ndoa yenu kabla ya wengine wote.
Nyie ndio mtakuwa wa kwanza kutoa ushuhuda wa maajabu ya Yesu kwenye maisha yenu kabla ya wengine.
Hiyo yote ni kama mtamfanya Kristo wa kwanza, na kama hamtazuiana katika kumtafuta Yesu.
Maran atha!
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
NEEMA YA MUNGU KWA MARIAMU.
Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”
MAMA, TAZAMA, MWANAO.
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?
Usiwe na Uchungu na Mke wako!.
(Masomo maalumu kwa Wanandoa)-UPANDE WA WANAUME/ MAJUKUMU YA WANAUME.
Neno la Mungu linasema..
Wakolosai 3:19 “Ninyi waume, wapendeni wake zenu MSIWE NA UCHUNGU NAO”
Hapo biblia imetoa maagizo mawili; 1)Kupenda na 2)Kutokuwa na uchungu.
1.Kupenda:
Kila mwanaume analo jukumu la kumpenda Mke wake kuanzia siku ile alipofunga naye ndoa mpaka siku ile kifo kitakapowatenganisha!. (Na hiyo ni Amri sio ombi). Tena anapaswa ampende kwa viwango vile vile vya kama Kristo alivyolipenda kanisa..
Waefeso 5:25 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake”
Kwahiyo kila Mwanaume ana wajibu wa kumpenda Mke wake siku zote za maisha yake… Ukiona upendo kwa mke wako unapungua, basi tafuta kuurejesha huo upendo kwa gharama zote!.(Jambo hilo linawezekana kabisa endapo ukimwomba Mungu, na wewe ukitia bidii katika kuurejesha upendo)
2. Kutokuwa na uchungu nao:
Amri ya pili waliyopewa wanaume juu ya wake zao, ni “KUTOKUWA NA UCHUNGU NAO” . Na mpaka biblia inasema “wanaume wasiwe na uchungu na wake zao” maana yake ni kwamba “wanawake wana mambo mengi ambayo wakati mwingine yanaleta machungu mengi”.
Kwamfano Matumizi mabaya ya Pesa… Hili ni moja ya jambo ambalo linaweza kumletea Mwanaume uchungu, hususani kama sehemu kubwa ya fedha anazitoa yeye, na pia tabia ya kuzungusha maneno ya siri ya familia kwa marafiki au kwa watu wasio na uhusiano wowote na familia, jambo hili pia linaweza kuleta uchungu kwa mwanaume. Na pia tabia ya kurudia makosa yale yale, na tabia ya kutokusikia au kukosa umakini wa baadhi ya mambo na hivyo kusababisha hasara Fulani, au kuwa wazito kufanya baadhi ya mambo, hizi zinaweza kuleta uchungu kwa mwanaume.
Lakini kwa sababu hizo au nyingine zozote, ni amri wanaume wote kutokubali uchungu ndani yao kwasababu ya kasoro hizo za wanawake.
Sasa Kwanini ipo hivyo?
Biblia imeweka wazi kuwa ni kwasababu “wanawake ni vyombo visivyo na nguvu”..
1Petr3:7 “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, KAMA CHOMBO KISICHO NA NGUVU; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe”
Kwahiyo kama mwanamke ni chombo dhaifu, ni lazima tu kitakuwa hivyo siku zote!.. hivyo ni lazima kuchukuliana nacho katika hali hiyo.. Lakini usipokichukulia kama ni vyombo dhaifu, na kukifanya kuwa ni chombo chenye nguvu, basi utakuwa ni mtu wa kuumia moyo kila wakati, na kujikuta unakuwa mtu uliyejaa uchungu na hasira na hata kufikia kuwa mtu wa ugomvi na makelele ndani ya nyumba. Jambo ambalo ni dhambi!!
Waefeso 4:31 “UCHUNGU WOTE NA GHADHABU NA HASIRA NA KELELE na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya”
Hivyo ni wajibu wa kila mwanaume aliyeoa kutokuwa na uchungu na Mke wake.
Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Neno “Uchungu wa mauti” lina maana gani kibiblia?
Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18
SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.
Shalom
Hii ni sehemu ya pili ya maswali na majibu yahusuyo ndoa.. Sehemu ya Kwanza unaweza kuisoma kupitia link hii >> MASWALI-NDOA
SWALI 01: Je Mkristo anaruhusiwa kuoa mtu wa Imani nyingine? Yaani akafunga naye ndoa tu, na kila mmoja akaendelea na imani yake.
Jibu: Ndoa ya kikristo ni ndio inayohusisha Imani moja, Bwana mmoja, Roho mmoja, tumaini moja, Ubatizo mmoja na Mungu mmoja..
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. 5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. 6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”
Kwahiyo kabla ya Ndoa ni lazima wawili hao wafikie kuwa na imani moja, na ubatizo mmoja na Roho Mmoja na Mungu mmoja, wasipofikia huo umoja basi hiyo sio ndoa ya kikristo.
Sasa nini cha kufanya endapo ikitokea mmoja si wa imani ya kikristo?, Jibu: Huyo ambaye tayari kashaokoka anapaswa amhubirie mwenzake habari za Wokovu kwanza, na aamini na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu (kwaufupi awe mkristo aliyesimama kweli kweli) na baada ya hapo ndipo wafunge ndoa, lakini kumbuka, si abadilike kwasababu tu anataka kuoa au kuolewa!, hapana bali anapaswa apate badiliko la kweli kiasi kwamba hata kama asipoolewa na huyo basi bado Kristo atabaki kuwa Mwokozi wake siku zote za maisha yake.
SWALI 02: Je kuna umuhimu wowote wa kupima afya kabla ya kufunga Ndoa?
Jibu: Ndio upo umuhimu wa kufanya hivyo kama kuna huo ulazima. Kuhakikisha afya zenu zipo sawa kabla ya kufanya lolote, maandiko hayajakataza kufanya hivyo. Na endapo ikitokea mmoja kakutwa na maradhi ambayo yatawafanya wawili hao wasiweze kukutana kimwili!.. Basi hapo ni uchaguzi wa Yule aliye salama, kama upendo wake ni mwingi kama ule wa Kristo, anaweza kuishi na huyo anayemchagua, lakini kamba si hawezi basi yupo huru kutafuta mwingine aliye chaguo lake hafanyi dhambi.
Lakini kama tayari wameshafunga ndoa na mmoja akapata maambukizi ya maradhi hayo basi Yule aliye salama hapaswi kumwacha huyo aliye na maradhi, wataendelea kubaki pamoja siku zote. Vile vile kama mmojawapo kapata ulemavu ambao utamfanya asiweze kabisa kukutana na mwenzake basi Yule aliye mzima pia hapaswi kumwacha mwenzake aliye na udhaifu, siku zote za maisha yake.
SWALI 03: Je wakristo wanaruhusiwa kutoa Ujauzito (Mimba)?
Jibu: Mkristo haruhusiwi kutoa ujauzito (mimba), kwasababu yoyote ile isipokuwa ya kiafya kwa maelezo ya madaktari:
Kwamfano Ikitokea mtoto kafia tumboni hapo ni lazima ile mimba changa iondolewe ili kuokoa maisha ya mama, vile vile ikitokea itilafu katika tumbo la mama, ambayo ili mama awe salama (asipoteze maisha) na kama mama huyo hana imani ya kutosha ya kuamini kuwa anaweza kuishi bila kuitoa na akawa salama, na hivyo akakubali itolewe kufuatia maelezo hayo ya daktari, mama huyo hafanyi dhambi!, kwasababu ya usalama wake mwenyewe.
Lakini sababu nyingine yoyote ya kutoa mimba tofauti na hiyo ya kiafya, ni dhambi!..Kwamfano mwanamke kapata ujauzito bahati mbaya na alikuwa hana mpango wa kuipata hiyo, hapo hapaswi kuutoa huo ujauzito, au kapata ujauzito kwa njia ya ukahaba, hapo hapaswi kuitoa hiyo mimba, atabaki nao mpaka hatua ya kujifungua.
SWALI 04: Ni nani mtu sahihi wa kumpelekea matatizo ya ndoa? Endapo kukitokea kutokuelewana?
Jibu: Endapo kukitokea kutoelewana, ni vizuri kuomba kwa Bwana suluhisho na kurejea biblia kujua ni nini biblia inasema kuhusu hali hiyo, lakini kama bado mwanandoa anahisi anahitaji msaada zaidi basi anapaswa ayafuate makundi yafuatayo.
1: MCHUNGAJI WA KWELI WA BWANA:
Si wachungaji wote ni waaminifu, lakini pia wapo walio wa kweli na waaminifu, watu hao ni kituo bora cha kupata ushauri wa kiMungu na maombezi.
2. MZAZI:
Kama unaye mzazi aliyeokoka basi hicho pia ni kituo bora sana cha kupokea mashauri bora..na yenye msingi mkubwa.
Kamwe usitafute ushauri kwa marafiki, majirani, ndugu wa mbali, au watu usiowajua kuhusiana na mambo ya kindoa.
SWALI 05: Endapo nikagundua baada ya kufunga ndoa Mwenzangu ana matatizo katika uzazi wake (hana uwezo wa kuzaa au kuzalisha)..Je naweza kwenda kupata mtoto nje na kuendelea kuwa naye?
Jibu: Kama mwanandoa mmoja anamatatizo ya uzazi yanayomfanya asiweze kuwa na mtoto, hapo mwanandoa mwingine asiyekuwa na matatizo hayo hapaswi kumwacha Yule mwenye matatizo, wala kuondoka na kwenda kupata mtoto wa kando, atabaki naye huyo huyo siku zote za maisha yake, huku wakimwomba Bwana awafungue!.
Na kama ni mapenzi ya Bwana wao kuwa na watoto, basi Bwana atawapa mtoto haijalishi ni miaka mingapi itapita (Ibrahimu na Sara walipata watoto katika uzee), na Mungu ni Yule Yule hajabadilika.
Lakini pia kama wanaona ahadi za Mungu bado zipo mbali wanaweza ku-adopt mtoto/watoto na kuwalea kama watoto wao.. Vipo vichanga vingi visivyo na wazazi, na mtu akiwalea hao mbele za Mungu ni zaidi hata ya Yule mwenye watoto 100 waliotoka katika uzazi wake.
SWALI 06: Je mkristo anaruhusiwa kupanga uzazi?
Jibu: Ndio wakristo wanaweza kupanga idadi ya watoto wanaotaka kuwa nao!. Biblia haijatoa amri ya kuzaa idadi ya watoto 10 au 50, ni kila mtu atakavyotaka yeye. Lakini imetoa tu angalizo kuwa tuwe watu wenye uwezo wa kuwatunza wakwetu (1Timotheo 5:8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.)
Kwahiyo ni lazima Mkristo awe na uwezo wa kuwatunza watoto wake, hivyo ni lazima awe na uzazi wa mpango.
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA-1
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?
Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue? Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).