Category Archive maswali na majibu

Je Malaika wana maamuzi binafsi?

Swali: Je Malaika wa mbinguni wana maamuzi binafsi kama tuliyonayo sisi wanadamu, mfano wakiamua kufanya jambo fulani wanafanya pasipo kuongozwa wala kuamuliwa?


Jibu: Maandiko yanatuonyesha kuwa viumbe pekee walioumbwa na Mwenyezi MUNGU walio na utashi ni Wanadamu pamoja na Malaika.

Na kama vile wanadamu tulivyo na utashi pamoja na maamuzi binafsi, (kwamba kuna mambo tunaweza kuamua wenyewe na mengine kuamuliwa) vile vile na malaika nao waliumbwa kwa mfumo huo huo,  wanayo maamuzi yao binafsi, na mengine kuamuliwa na MUNGU…

Na tena maamuzi mengine ya Malaika ni magumu kuliko hata yetu wanadamu..

Kwamfano tukirejea kabla ya Uasi wa shetani kule juu mbinguni, wakati ambao alikuwa ni malaika mkuu (Kerubi), biblia inatuambia kuwa ilifika wakati moyo wake ulinyanyuka na kuanza uasi, wa kutaka kuwa kama MUNGU, (yaani kuabudiwa).. sasa kitendo cha kuchukua hatua ya kutaka kuabudiwa hayo sio maamuzi madogo, na wala si hisia za kawaida… Kwahiyo malaika wa mbinguni na wale walioasi (yaani mapepo) wanayo maamuzi na hisia..

Sasa na malaika wengine wote wa mbinguni ni hivyo hivyo, wanayo maamuzi na hisia, na wana akili timamu…Ndio maana Bwana katika kutufundisha kuomba alisema tuombea “mapenzi ya yake yafanyike duniani kama kule juu mbinguni (Mathayo 6:10)”.

Ikiwa na maana kuwa mbinguni kuna shughuli zinaendelea, na malaika waliosalia mbinguni wanayafanya mapenzi ya MUNGU kila siku, na si kwamba wapo tu wamekaa wakisubiri amri Fulani!.. La wanaendelea na shughuli zao ambazo nyingi ya hizo sisi wanadamu hatuzijui, (lakini zote zipo ndani ya mapenzi ya MUNGU).

Zaidi tunaweza kusoma maandiko machache yanayozidi kutuonyesha kuwa Malaika wanayo maamuzi binafsi na ya kipekee..

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea. 

21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake”.

Hapo anasema “huyo malaika” hatawasamehe, kuonyesha kuwa yeye si robot.. bali anatafakari na kapewa mamlaka na Mungu juu ya watu hao..soma tena Waamuzi 2:2-3.

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi; 

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?

3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

 4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia”.

Tusome tena habari za Balaamu na Punda…

Hesabu 22:31 “Ndipo Bwana akafunua macho ya Balaamu akamwona malaika wa Bwana amesimama njiani, ana upanga mkononi mwake, umekwisha kufutwa naye akainama kichwa, akaanguka kifudifudi. 

32 Malaika wa Bwana akamwambia, Mbona umempiga punda wako mara tatu hizi? Tazama mimi nimekuja ili kukupinga, KWA SABABU NJIA YAKO IMEPOTOKA MBELE ZANGU,

 33 punda akaniona, akageuka upande mbele zangu mara tatu hizi; kama asingejiepusha nami, bila shaka ningalikuua wewe, nikamwacha yeye hai”.

Hapo Malaika anamwambia Balaamu kuwa njia za Balaamu zimepotoka mbele zake (huyo Malaika)

Lakini pamoja na na kwamba Malaika waliopo mbinguni wanayo maamuzi, lakini bado maamuzi yao hayavuki Neno la MUNGU,.. kwahiyo hawawezi kufanya lolote lililo kinyume na Neno la MUNGU, na wanafanya kazi pamoja na watu wa Mungu katika kuwahudumia (Soma Waebrania 1:14), na wanafurahi wanadamu wanapookoka.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”.

Malaika walioasi, yaani shetani na mapepo yake hao wanafanya maamuzi yao, yaliyo kinyume na mapenzi ya MUNGU na ndio chanzo cha matatizo yote ya wanadamu leo.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Swali: Tunasoma unabii wa Bwana YESU kuwa atakula siagi na maziwa, je ni kwa namna gani hilo lilitimia?


Jibu: Turejee..

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli. 

15 Siagi na ASALI ATAKULA, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema”. 

Siagi inayozungumziwa hapo ni ile inayotokana na maziwa..

Mithali 30:33 “Kwa maana kupiga maziwa HULETA SIAGI….”.

Kwahiyo kusema “Siagi na Asali” ni sawa kabisa na kusema “Maziwa na Asali”.. Hivyo unabii unaonyesha kuwa Mtoto YESU atakula Maziwa na Asali sawasawa ahadi Bwana aliowapa wana wa Israeli kipindi anawapandisha kutoka Misri..

Hesabu 14:8 “Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali”.

Lakini kabla ya kuangalia kwa undani ni kwa namna gani Bwana alikula Maziwa/siagi na Asali, tujifunze kwanza hatua wana wa Israeli walizopitia mpaka kuingia nchi imiminikayo maziwa na asali.

   1.KUITWA KUTOKA MISRI.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Kutoka 3:17 “Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.”

Na tukirudi kwa upande wa mtoto YESU naye pia aliitwa kutoka Misri, na kupandishwa mpaka nchi ya Israeli wakati akiwa mchanga..

Mathayo 2:14  “Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15  akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, KUTOKA MISRI NALIMWITA MWANANGU.”

    2. KUFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Ili ahadi ya kufaidi maziwa na asali katika nchi ya ahadi ni lazima wawe wanamcha MUNGU na kumpendeza, kwa kufanya mema, lakini kama watafanya mabaya basi hiyo nchi itawatapika..

Kumbukumbu 6:18 “Nawe fanya yaliyo sawa, na mema, machoni pa Bwana; ili mpate kufanikiwa, nawe upate kuingia na kuimiliki nchi nzuri Bwana aliyowaapia baba zako”

Kwa upande wa wana wa Israeli wapo waliofanya mema wakafanikiwa, na wako waliofanya mabaya na wakaikosa ahadi hiyo ya maziwa na asali, Lakini kwa upande wa Bwana YESU baada ya kupanda kutoka Misri maandiko yanasema alichagua MEMA, na kuyakataa MABAYA hivyo basi akashiriki ahadi ya kula Siagi na Maziwa sawasawa na ahadi ya Bwana..

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli. 

15 SIAGI na ASALI ATAKULA, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema”. 

Umeona?.. kumbe Kristo alijifunza kuyakaa mabaya tangu utoto wake na kuchagua mema?..na hiyo ikawa sababu ya kubarikiwa sana katika nchi ile aliyokuwepo, Kristo hakuishi maisha ya tabu, wala hakuwa na haja na kitu, vyote alipewa na Baba na alishabarikiwa tangu utoto, hakutawaliwa na magonjwa ya Misri, wala shida za kiMisri.

Sasa swali lingine ni hili, ni kwanini hatumsomi Bwana akiwa na mali nyingi?.. sababu kuu ni kwamba hakuwa anajilimbukizia, vyote alivyobarikiwa alivitoa kwa watu, na vingine hakutaka kuchukua, lakini haimaanishi kwamba alikosa, laiti angefungua mlango wa kupokea  vyote vya mwilini alivyopewa na Baba na kujilimbikizia, huenda ndani ya siku moja angekuwa mtu tajiri Zaidi ya mtu yeyote aliyewahi kutokea.

Lakini alijiweka katika hali hiyo kwasababu alijua upo utajiri mkuu Zaidi ya huu wa duniani, ambao ataupokea hapo baadaye,  

Kwahiyo Siagi na Asali inawakilisha Baraka zote za rohoni na mwilini katika nchi mtu aliyepo, ijapokuwa alijiweka katika hali ya umasikini lakini alikuwa ni tajiri sana, na rohoni alibarikiwa sana kwa Roho Mtakatifu zaidi ya mtu mwingine yoyote, miujiza aliyoifanya ni ya kupita kawaida na neema aliyoibeba ni kubwa sana kiasi cha kumtoa mwanadamu katika hukumu ya milele na kumwingiza katika uzima wa milele.

Na tunapomwamini na sisi tunaingia katika mkondo huo wa Baraka zake, kwanza tutapata uzima wa milele na pili tutapata baraka za mwilini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 30:33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi

Print this post

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

Jibu: Biblia haijata umri wa Mariamu kipindi ametembelewa na Malaika Gabrieli na kupewa taarifa za kubeba ujauzito wa Bwana YESU kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

Na si miaka yake tu ambayo haijatajwa bali hata kabila lake Mariamu, wala ukoo wake….Na kwanini biblia haijarekodi mambo hayo yamhusuyo Mariamu?….Jibu: Ni kwasababu si wa muhimu sana sisi kuujua…

Tunachojua ni kuwa Mariamu alikuwa ameshafikia umri wa kutosha wa kujitambua ndio maana tayari alikuwa ametolewa posa.. Hivyo alikuwa na umri wa kutosha na alikuwa mnyenyekevu na aliyemcha MUNGU.

Umri wa Mariamu, au familia aliyotokea au kabila alilotokea havikuwa vya umuhimu sana sisi kuvijua, kwasababu Mariamu alikuwa ni mwanamke tu kama wanawake wengine, alipata tu neema ya kumzaa Bwana YESU lakini hakuwa na utofauti na wanawake wengine waliomcha MUNGU.

Kwahiyo kilichokuwa cha muhimu sana sisi kujua ni kwamba “bikira atachukua mimba”…sawasawa na unabii wa Isaya.

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli”.

Na hapo hasemi… “ bikira atachukua mimba akiwa na miaka 20 au 25 au 30”.. La! haisemi hivyo.. ikimaanisha kuwa lililo la msingi kwetu kulifahamu ni hilo la bikira kuchukua mimba basi, hayo mengine hayana umuhimu hivyo yanabaki kuwa ya Mungu na ya wale waliokuwepo wakati Mariamu anachukua ujauzito..

Kumbukumbu 29:29 “Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii”.

Wapo wanaomwona Mariamu kama mwanamke aliye tofauti na wanawake wengine wote, kwamba anaweza kusimama katika nafasi ya kutuombea au hata kutubariki, na hivyo anapaswa apewe heshima ya kipekee, na hata inaaminika pia kwa baadhi ya watu kuwa alipaa, jambo ambalo pia ni uongo.

Dhana ya kuwaamini manabii na watu waliopokea neema kwenye biblia kuwa ni watu wakuu sana wa kusimama katika nafasi ya kuombwa au kutukuzwa ilianza tangu zamani kabla hata ya ujio wa Bwana YESU.

Wapo waliokuwa wanamwabudu Henoko aliyetwaliwa, wapo waliokuwa wanamwabudu Musa, wengine Eliya wengine Daudi, na sasa wapo wanaomwabudu Mariamu n.k, lakini hawa wote biblia inasema ni watu kama sisi tu..

Yakobo 5:17 “Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita”.

Sasa kama Eliya aliyepaa mbinguni biblia inasema alikuwa ni mtu kama sisi vipi hao wengine ambao walikufa??…

Ambaye hakuwa mtu wa kawaida ni Bwana YESU tu na huyo ndiye maandiko yanasema anastahili kuabudiwa kwa kuwa alimwaga damu yake kwaajili yetu..

Ufunuo wa Yohana 5:8 “Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”.

Je umempokea Bwana YESU…Umebatizwa katika ubatizo sahihi?.

Kama bado basi fanya uamuzi leo, kwasababu hizi ni siku za mwisho na YESU yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

Print this post

Nini Maana ya kauli “atakatiliwa mbali na watu wake”. (Walawi 7:27)

SWALI: Kwanini sehemu kadha wa kadha wana wa Israeli walipoonekana wanakwenda kinyume na Torati hutumia kauli ya 

“atakatiliwa mbali na watu wake”. Nini maana ya hii kauli?

Mambo ya Walawi 7:27

[27]Mtu ye yote alaye damu, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.


JIBU: Ni kauli ya ujumla inayomaanisha huyo mtu atatengwa na kusanyiko la Israeli. Kutengwa huko kunaweza kuwa Kwa namna mbalimbali kutegemeana na aina ya kosa.

Hizi ndio aina kuu tatu za kukatiliwa mbali

 

1) Kifo.

Kifo kilihusika katika baadhi ya hukumu, ambazo Nyingine ni Mungu mwenyewe aliyezitekeleza (Walawi 20:3-6). Na nyingine Wanadamu. Kwamfano mtu yeyote aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa Mawe Mpaka kufa. 

Vivyo hivyo katika kuihalifu sabato, adhabu ilikuwa ni hiyo soma;

Kutoka 31:14

[14]Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. 

 

2) Kutengwa na jamii ya watu.

Hii nayo ilikuwa ni aina nyingine ya kukatiliwa mbali, ambapo ulifutwa katika hesabu ya waisraeli, inayokufanya kupoteza haki ya kushiriki Ibada yoyote katika makusanyiko, au vipaumbele.

Hesabu 19:20

[20]Lakini mtu atakayekuwa najisi, naye hataki kujitakasa, mtu huyo atakatiliwa mbali katika mkutano, kwa sababu amepatia unajisi mahali patakatifu pa BWANA; hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake; yeye yu najisi. 

 

3) Kupoteza baraka za maagano

Maana yake ni kuwa hauwi mshirika tena wa baraka za maagano ya Mungu, kama vile ulinzi na ahadi.

Mwanzo 17:14

[14]Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu. 

 Hata leo, katika agano jipya mambo mambo tunaweza kufanya yakatusababishia kukatiliwa mbali na rehema za Mungu. 

Na adhabu hizo zinaweza kutekelezwa na wanadamu(watakatifu), na nyingine Mungu mwenyewe.

Kwamfano Biblia inatoa ruhusu kanisa kumtenga mtu ambaye anazoelea dhambi, (1Wakorintho 5:1-5)

Mungu mwenyewe anaweza kutekeleza hukumu hiyo, kwamfano tunaweza kuona kwa Anania na Safira, ambao walitumia njia ya hila katika mapatano ya Roho.(Matendo 5:1-11). Lakini pia kwa mtu ambaye anakusudia kuurudia ulimwengu baada ya kuipokea neema, hukumu kama hii huweza kumkuta. (Waebrania 10:26-27)

Kwahiyo jambo hili halikuwa tu kwa wana wa Israeli, lakini lipo hata sasa rohoni. Tusiwe watu wa kuzoelea dhambi tukidhani kuwa wakati wote Mungu ataturehemu. Usidanganyike ukishakatiliwa mbali si rahisi tena kumgeukia Mungu wako.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Print this post

Swali: Je Kula nyama mbichi ni dhambi?.

Swali: Je kula nyama mbichi ni dhambi kibiblia?…Maana zamani tulikuwa tunakula maini mabichi na utumbo mbichi ule wa taulo.


Jibu: Hakuna maelezo ya moja kwa moja katika biblia yanayoonyesha kuwa kula nyama mbichi ni dhambi,

Lakini vipo vielelezo vichache katika maandiko vinavyoonyesha kuwa si vizuri/si sahihi kula nyama mbichi.

Wakati wana wa Israeli wanatolewa Misri, ule usiku Bwana MUNGU aliwaambia waile pasaka, ambapo waliagizwa wamtwae mwanakondoo na kumooka motoni, wamle pamoja na mboga chungu lakini wasimle mbichi.

Kutoka 12:8 “Watakula nyama yake usiku ule ule, imeokwa motoni, pamoja na mkate usiotiwa chachu; tena pamoja na mboga zenye uchungu.

9 MSIILE MBICHI, wala ya kutokoswa majini, bali imeokwa motoni; kichwa chake pamoja na miguu yake, na nyama zake za ndani”.

Kwa asili Ulaji wa nyama mbichi ni hatari kwa afya ya mwili, kwani nyama mbichi ina minyoo na wadudu wengi wasiionekana kwa macho ambao ni hatari kwa afya na tumepewa maagizo ya kuitunza hii miili..lakini nyama iliyopikwa inakuwa salama kwani inaea vimelea hivyo…

Na pia ulaji wa nyama mbichi unaweza kuashiria uwepo wa roho nyingine ndani ya mtu, na mara nyingi roho ya ukatili inawaingia watu walao nyama mbichi (kwani wanyama ndio walao nyama mbichi).

Na pia ulaji wa nyama mbichi unahusiana na imani za kishirikina na imani nyingine potofu…

Hivyo si vyema kula nyama mbichi kama wanyama.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Madongoa ni nini? (Ayubu 7:5)

Swali: Madongoa kama inavyosomeka katika Ayubu 7:5, ni kitu gani, na ina ujumbe gani kiroho?.


Jibu: Turejee..

Ayubu 7:5 “Mwili wangu unavikwa mabuu na MADONGOA YA UDONGO; Ngozi yangu hufumba, kisha ikatumbuka tena”.

Madongoa ni udongo ulioshikamana pamoja, sawasawa na Ayubu 38:38..

Ayubu 38:38 “Wakati mavumbi yagandamanapo, Na madongoa kushikamana pamoja?”

Kikawaida ardhi yenye Madongoa haifai kwa kilimo, bali mpaka madongoa hayo yatakapovunjwa na kulainishwa, ndipo mbegu ziweze kupandwa…

Isaya 29:23 “Tegeni masikio, sikieni sauti yangu, sikilizeni mkasikie neno langu.

24 Je! Mwenye kulima alima daima, ili apande? Afunua daima MADONGOA YA NCHI YAKE, na kuyavunja?

25 Akiisha kuulainisha uso wa nchi yake, je! Hamwagi huko na huko kunde, na kutupa-tupa jira, na kuitia ngano safu safu, na shayiri mahali pake palipochaguliwa, na kusemethi karibu na mipaka yake?

26 Kwa maana Mungu wake anamwagiza vizuri na kumfundisha”.

Neno hili pia tunaweza kulisoma katika kile kitabu cha Hosea 10:11..

Ni ni nini tunachoweza kujifunza??

Kama vile ardhi yenye madongo ilivyokuwa ngumu kwa kilimo, hali kadhalika mioyo yetu inafananishwa na shamba sawasawa na ule mfano wa Mpanzi (Mathayo 13:18-23), na kama mioyo yetu ni migumu kwa namna hiyo basi ni ngumu pia kumzalia MUNGU matunda.

Mfano wa moyo wenye madongoa ni ule ulio mgumu kusikia Neno, mtu mwenye moyo wa kupuuzia, na kutokujali pale asikiapo Neno la MUNGU, mtu wa namna hii anahitaji sana kusaidiwa.

Je ni wewe mtu huyo?. Kama ndio basi mkimbilie YESU leo kwa kumaanisha kabisa naye ataufanya maoyo wako kuwa mlaini, na utayaona matunda ya BWANA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tufanyaje ili tuonekane tunampenda Mungu?

KWANINI MIMI?

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi, maana yake nini? (Zab.18:26)

Swali: Je Mungu ni mkaidi kulingana na Zaburi 18:26, au kwanini Mungu aseme maneno hayo?


Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 24, ili tupate maana kamili..

Zaburi  18:24 “Mradi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

25 Kwa mtu mwenye fadhili UTAKUWA MWENYE FADHILI; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

26 KWAKE AJITAKASAYE UTAJIONYESHA KUWA MTAKATIFU; Na KWA MPOTOVU UTAJIONYESHA KUWA MKAIDI”

Hapo anasema kwa mtu mwenye fadhili Bwana atajionyesha mwenye fadhili kwake, na kwa ajitakasaye Bwana atajionyesha ni mtakatifu kwake, vile vile na kwa mpotovu atajionyesha mkaidi.

Sasa kwa maneno hayo haimaanishi kuwa Bwana ni MKAIDI..La! yeye ni mwema siku zote na hawezi kufananishwa na sisi wanadamu…Lakini sasa swali ni kwanini aseme hivyo?

Ili tuelewe vizuri tafakari mfano huu; Unaye mtoto halafu ukaanza kuona anaonyesha tabia za kukosa nidhamu, na anafanya mabaya mengi, na ulipomwonya haonyeki, kisha ukaamua kumwambia kuwa endapo akiendelea kuwa na tabia hiyo, utakuwa mbaya kwake!..na akibadilika kuwa mzuri basi utakuwa mzuri kwake…

Je kwa kauli hiyo utakuwa umemaanisha kuwa wewe ni ni MTU MBAYA na MWOVU?.. bila shaka hutakuwa umemaanisha hivyo, bali utakuwa umemaanisha kuwa endapo akiendelea kufanya mabaya, basi utambadilikia na kumwadhibu, jambo ambalo ni baya machoni pa huyo mtoto, na ndicho Bwana Mungu alichomaanisha hapo kuwa kwa “mtu mpotovu atajionyesha kuwa Mkaidi”… Na si kwamba MUNGU ni Mkaidi.

Kwamba kwa mtu anayefanya mabaya Bwana na maovu na hakubali kuonyeka basi atapata mabaya kutoka kwa Mungu, kwani BWANA atamwadhibu,…Na adhabu za Bwana ni za lengo la kuonya, na kumfanya mtu aache njia mbaya, na si za kumpoteza mtu.

Waebrania 12:10 “Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.

12 Kwa hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza,

13 mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe.

14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

Na kinyume chake ni kweli, kwa mtu ajitakasaye, yeye Bwana atajionyesha mtakatifu kwake, Maana yake ataona mema mengi kutoka kwa Bwana..

Hivyo hiyo ni tahadhari kwetu na pia ni faraja kwetu, kwamba tukae katika usafi na utakatifu, ili tuuone wema wa Mungu, na tusikae katika upotovu, tusije tukauona ukaidi wa MUNGU, kwani Bwana atajionyesha kwa kila mtu sawasawasa na matendo yake.

Zaburi  18:24 “Mradi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

25 Kwa mtu mwenye fadhili UTAKUWA MWENYE FADHILI; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

26 KWAKE AJITAKASAYE UTAJIONYESHA KUWA MTAKATIFU; Na KWA MPOTOVU UTAJIONYESHA KUWA MKAIDI”

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

TAA YA MWILI NI JICHO

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa pili (2Wakorintho)

Rudi Nyumbani

Print this post

Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?

SWALI: Konstantino mkuu ni nani, na je umuhimu wake katika ukristo ni upi?


JIBU: Konstantino mkuu ni Mmoja wa wafalme waliotawala chini ya dola ya Rumi, Kuanzia mwaka wa 306BK mpaka 337BK.

Dola hii ya Rumi ndiyo dola iliyokuwa na nguvu sana, zaidi ya zote zilizowahi kutokea katika historia, ilifanikiwa kutawala kikamilifu katika nyanja karibia zote, za kijeshi, kisiasi hadi kiuchumi, na ndio ngome iliyodumu kwa muda mrefu kuliko zote.

Itakumbukwa kuwa hata wakati Kristo anakuja duniani, dola hii ndio ilikuwa inatawala ulimwenguni kote na Kaisari ndiye aliyekuwa mfalme. Israeli wakati huo halikuwa taifa huru kama tunavyoliona sasa, bali ilikuwa koloni la Rumi, na watalawa na maliwali wake wote akiwemo, Pilato na Herode walikuwa ni Warumi.

Utawala huu ndio uliomsulubisha Kristo kwa shinikizo la wayahudi. Lakini tunaona katika historia, injili ilipoanza kuhubiriwa na jamii kubwa ya watu kugeuzwa kuwa wakristo duniani kote, Utawala huu ulianza kulitesa kanisa, na hata baadhi ya wafalme wao waovu waliotokea walitunga sheria kwamba ikionekana mtu yeyote anajiita mkristo, basi adhabu yake ilikuwa ni kifungo kama sio kifo.

Mfano wa watawala hawa alikuwa Nero, trajan, na Domitian, Na hiyo ilipelekea jamii kubwa sana ya wakristo kuuawa kikatili, wengine kuchomwa moto, wengine kusulubiwa, wengine kuwekwa katika viwanja vya mauaji na kuachiwa wanyama wakali wawaue, idadi ya mamilioni ya wakristo walipoteza maisha kwa njia hii. Historia hiyo utaipata vema katika kitabu maarufu kijulikanacho kama (Foxes book of martyrs). Kumbuka utawala uliohusika ulikuwa ni huu wa Rumi, chini ya watawala wao mbalimbali.

Hivyo kwa wakati wote huo ukristo ulionekana kama imani ya vikundi fulani vya wavuruga amani..

Wakati huo Rumi lilikuwa ni taifa la kipagani likiongozwa kisiasa, chini ya dini zao za miungu mingi.

Lakini alipokuja kutokea huyu mtawala mpya aliyeitwa Kostantino baada ya watawala 59 kupita nyuma yake,

Kwa mujibu wa ushuhuda wake anasema wakati anakwenda kupigana vita mojawapo kuu iliyomkabili, katika maono aliona..msalaba angani, akaambiwa kwa ishara hii utashinda. Hivyo Konstantino akaichukua nembo ya ukristo na kuipachika katika ngao za jeshi lake, na hivyo akashinda vita ile iliyokuwa inamkabili, ushindi huo ulimuimarishia sana ufalme wake.

Huo ndio ukawa mwanzo wake wa kuwa mkristo. Aliendelea kuupa sana kipaumbele ukristo, Kuanzia huo wakati ndio ukawa mwisho wa mauaji ya watakatifu. Na mwanzo wa dini ya Kikatoliki.

Lakini historia inaonyesha Konstantini hakuwa ameupokea ukristo katika ukamilifu wote, kama madhehebu baadhi yanavyoamini. Bali ukristo wake ulikuwa na msukumo wa kisiasi pia nyuma yake, ambao ulilenga kuwaunganisha wakristo na warumi wakipagani, kwasababu hakuacha pia kuabudu miungu yake ya kirumi. Ndio maana ibada gheni za miungu zilichanganywa na imani ya mitume, kwa kuzaliwa kanisa katoliki na kulipelekea kanisa kuingia katika kipindi kirefu sana cha ukimya kijulikanacho kama kipindi cha giza.

Pamoja na hayo ni kweli alifanikiwa kukomesha mateso kwa wakristo, na kuuthaminisha ukristo, na wakati mwingine kuruhusu mabaraza ya Wakristo, kuthibitisha vipengele kadha wa kadha vya imani, vilivyoleta msaada mwingi.

Lakini pia hakuuingiza Ukristo Katika misingi yake yote, ndio maana kanisa liliongia katika kipindi cha giza.

Je! ni nini tunajifunza kwa Mtawala huyu?

Hata hivyo kwa sehemu yake alisimama kuanzisha Imani ijapokuwa hakufanya katika utimilifu wote. Ilikuwa ni wajibu wa mabaraza Na wazee na watakatifu, Kuyatengeneza yaliyosalia, lakini hawakupiga hatua yoyote zaidi ya pale kwa miaka mingi.

Lakini ashukuriwe Mungu wakati wa matengenezo ulipofika (Karne ya 15)..Bwana aliwanyanyua watu wake mbalimbal8 mfano wa Martin Luther, Zwingli, Calvin na wengineo kulitengeneza upya kanisa kutoka katika misingi mibovu Mpaka wakati wa Pentekoste, ambapo kanuni zote za Kibiblia zilirejeshwa. Na mpaka sasa Kanisa linazidi kupanda katika utumilifu wake wote.

Hivyo ni wajibu wetu, sote kusoma biblia na kuifahamu kwa kina kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu, lakini pia kuhubiri injili kwasababu kwa njia hiyo ndivyo tutakavyoujenga ufalme Wa Kristo Na kuufanya uenee duniani kote, kiufasaha.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Naliupata wenyeji huu kwa mali nyingi, maana yake nini (Matendo 22:28)

UKristo Ni Nini?

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

Print this post

Ile Mizeituni mwili na wale wana wawili wa mafuta vinawakilisha nini? (Zekaria 4)

Sura hii inaeleza maono aliyoonyeshwa nabii Zekaria, kuhusu ujenzi wa hekalu la pili. Anaanza kwa kuonyeshwa na malaika kinara cha taa cha dhahabu, chenye taa saba juu yake. Ambacho pia  kina mirija saba, inayotoka katika matawi ya mizeituni miwili inayohusika kuleta mafuta katika kinara hiyo.

Hivyo nabii Zekaria kuona maono hayo, alitamani kuelewa tafsiri yake ni nini. Tusome.

Zekaria 4:1 Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kama mtu aamshwavyo katika usingizi wake.

2 Akaniuliza, Unaona nini? Nikasema, Nimeona, na tazama, kinara cha taa cha dhahabu tupu, nacho kinabakuli juu yake, na taa zake saba juu yake; tena iko mirija saba ya kuleta mafuta, kwa taa zote zilizo juu yake;

3 na mizeituni miwili karibu yake, mmoja upande wa kuume walile bakuli, na mmoja upande wake wa kushoto. 4 Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee Bwana wangu, vitu hivi ni nini?

5 Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.

6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala sikwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi.

7 Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe lakuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.

8 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,

9 Mikono yake Zerubabeli imeiweka misingi ya nyumba hii, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza; nawe

utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwenu.

10 Maana ni nani aliyeidharau siku ya mambo madogo? Kwa kuwa watafurahi, nao wataiona timazi katika mkono wa Zerubabeli; naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote.

11 Ndipo nikajibu, nikamwambia, Ni nini mizeituni hii miwili iliyo upande wa kuume wa kinara cha taa kile na upande wake wa kushoto?

12 Nami nikajibu mara ya pili, nikamwuliza, Ni nini haya matawi mawili ya mizeituni, ambayo kwa njia ya ile mifereji miwili ya dhahabu hutoa mafuta yao?

13 Akanijibu, akasema, Hujui hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.

14 Ndipo akasema, Hivi ni hao wana wawili wa mafuta, wasimamao karibu na Bwana wa dunia yote.

Tafsiri yake ni kuwa matawi yale mawili walimwakilisha Yoshua kuhani mkuu, na Zerubabeli liwawi wa Yuda. Hawa ndio wana wawili wa mafuta. Yoshua alisimama katika mambo yote yahusuyo dini na ibada na Zerubabeli katika mambo yote ya  kiutawala,

Na ile mizeituni miwili iliwakilisha Neno la Mungu lililowajia wao, kuwaongoza na kuwatia nguvu.  aidha kwa njia ya Torati au kwa Manabii. Maana yake ni kuwa Yoshua kama kuhani mkuu akiongozwa na Torati na Zerubabeli kama akida akiongozwa na manabii waliopokea ujumbe kutoka kwa Mungu ili walisimamie kusudi lake. Na manabii ambao walihusika hapa kuwatia nguvu walikuwa ni Hagai na Zekaria.

Katika ono hili Mungu alikuwa anamfunulia Zerubabeli uweza wake, kwamba si yeye atendaye hiyo kazi kubwa ambayo inaonekana kibinadamu haiwezekani, kutokana na hofu ya maadui zao, kupungukiwa fedha, na lile agizo lililotolewa na mfalme kuwa mji ule usiendelezwe. Bali ni Roho wa Mungu atendaye kazi yote, kwasababu si kwa uweza wao wala kwa nguvu.

Mungu akamuhakikishia Zerubabeli kuwa mikono yake ndiyo imetia msingi, na mikono yake ndiyo itakayoimaliza nyumba ile yote. Akimwonyesha kimaono jinsi wao wanavyosimama tu kama matawi ndani ya mzeituni (Zerubabeli na Yoshua), ambayo yanapokea mafuta na kutoa kuelekea kwenye mirija. Lakini hayahusiki katika kutengeneza mafuta au  kuwasha taa yoyote.

Na ndivyo ilivyokuwa kwao ujenzi huo ulienda ukakamilika bila taabu zao wenyewe walizozitarajia, bali Mungu alihakikisha anawapatia kibali, pamoja na vitendeakazi vyote(Mali) kiasi kwamba utukufu wa hekalu hilo la pili ukawa mkubwa sana kuliko ule wa kwanza, pamoja na udhaifu wao.

Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tufahamu kuwa jambo lolote kuu tunalotamani kumfanyia Mungu, aidha kujenga nyumba yake, kusapoti injili, kuhubiri injili sehemu za taabu na nguvu n.k. Tusifirie sana hali zetu, bali tumfikirie Roho Mtakatifu, kwasababu yeye mwenyewe aliahidi kuwa atatupa nguvu ya kuyatenda hayo yote, na kuyatimiliza.(Matendo 1:8), ili utukufu wote umrudie yeye.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

Mafuta mabichi ni mafuta ya aina gani? (Zaburi 92:10)

Rudi Nyumbani

Print this post

Aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye maana yake nini?.

Swali: Neno la Mungu limemaanisha nini kusema aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye? (1Wakorintho 6:17).


Jibu: Turejee…

1 Wakorintho 6:17 “Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye”.

Maana ya kuwa roho moja na Bwana ni kama maandiko yafuatayo yanavyoeleza..

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema Njoo!…..”.

Hapa anasema Roho (yaani wa Roho wa Mungu) na bibi-arusi (yaani kanisa la Mungu)…Wasema Njoo!!…

Maana yake hawa wawili (Roho pamoja na bibi arusi) wote wanatoa Kauli moja!.. ya Njoo!..

Maana yake Bibi arusi akisema ni Roho wa Mungu kasema na Roho wa Mungu akisema ni  Bibi arusi kasema…kwanini?…kwasababu wameungwa pamoja.

Ndio sababu Bwana YESU alisema, tukiwapokea waliotumwa na yeye, tumempokea yeye, na tukiwakataa waliotumwa na yeye, tumemkataa yeye kwasababu wameungwa na yeye.

Mathayo 10:40 “Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma”.

Je umemwamini Bwana YESU?. Je unasubiri Bwana YESU mwenyewe akutokee ndio uamini?..

Kama ndicho unachosubiri basi upo hatarini, kwasababu YESU yupo anafanya kazi ndani ya watu wake, mtumishi wa MUNGU wa kweli kukujia na kukupa habari za uzima wa milele, tayari YESU ameshakutokea kwasababu maneno akuambiayo si yake bali ya Roho wa Mungu.

Na anapokuita uingie kwenye imani/wokovu si yeye bali ni Roho wa MUNGU ndani yake..

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Rudi Nyumbani

Print this post