Category Archive maswali na majibu

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Jibu: Tusome,

Mithali 13:8 “Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”.

Dia ni Kiswahili kingine cha neno “Fidia”, Kwahiyo hapo biblia inaposema “Dia” ya nafsi ya mtu ni utajiri wake, na maskini hasikii ogofyo lolote, maana yake ni kwamba “Fidia ya mtu anapokutana na matatizo ni itatoka katika vitu alivyonavyo” ikiwa na maana kuwa mtu anapokutwa na tatizo labda kasababisha hasara Fulani au kafanya kosa Fulani katika jamii, lililomsababishia apigwe faini, au kakutana na watu na kaingiliwa na wahalifu katika nyumba yake, basi Mali alizo nazo zinaweza kuwa fidia kwaajili ya uhai wake, maana yake anaweza kuwapa wale watu sehemu ya mali zake na akaisalimisha roho yake.

Lakini mtu asiye na kitu kabisa (yaani Yule maskini kikweli kweli), huwa hawezi kupokea vitisho vyovyote, hakuna jambazi yeyote anayefikiria kwenda kuvunja nyumba ya maskini akiwa na mtutu ili amwibie mali zake.. Ikiwa na maana kuwa, maskini siku zote yupo huru!.. hafuatiliwi na mtu, wala hakuna mtu ana habari na maisha yake (hapokei ogofyo lolote).

Ni hekima gani tunaipata hapo? Au ni nini tunajifunza hapo?

Ili tuelewe ni nini tunajifunza hapo, hebu tuanzie kusoma kuanzia mstari wa 7

Mithali 13:7 “Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu; Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.

8 Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”

Hii ni hekima ambayo inaweza kutusaidia kuwa salama..sio lazima tuwapo na mali, tujionyeshe kuwa na mali kwa watu!, ndio maana hapo biblia inasema “kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.”.. Unapokuwa mtu wa kujionyesha mbele za watu mali ulizo nazo, unajiweka katika hatari ya kutoa DIA (Fidia) kwaajili ya uhai wako, kwasababu kila mtu atatamani hizo mali ulizo nazo, utavutia watu waovu na wasio waovu, utavutia majambazi, utavutia wenye mamlaka na watu  wapendao rushwa n.k

Hivyo hekima ni kujiweka katika maisha ya wastani, hata kama unazo mali nyingi, si lazima ujulikane wewe ni tajiri kuliko wote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya andiko hili  “Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.(Yohana 5:37)”

Jibu: Tusome,

Yohana 5:37  “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.

38  Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.”

Hapa Bwana Yesu hamaanishi kwa Wayahudi hawajawahi kuisikia sauti ya Mungu, wala kuliona umbile lake!. Hapana bali andiko hilo linamaansha kuwa Mungu alijidhihirisha kwao kimaumbile lakini hawakumwona na vile vile alijidhihirisha kwao kisauti lakini hawakumsikia.

Sawasawa kabisa na alivyosema katika Kitabu cha Isaya

Isaya 50:2 “Basi, NILIPOKUJA, MBONA HAPAKUWA NA MTU? NILIPOITA, MBONA HAPAKUWA NA MTU ALIYENIJIBU? Je! Mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? Au je! Mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu”.

Umeona hapo?.. kumbe kuna wakati Bwana anatujia kimaumbile lakini hatumwoni?… Sasa utauliza ni wakati gani anatujia hatumwoni, na ni wakati gani anapaza sauti yake hatuisikii??

Kupitia watumishi wake wa kweli, wanapotujia kama wageni na kutuletea habari njema, ujio wao unafananishwa kabisa na ujio wa Kristo kwetu kimaumbile, haihitaji yeye Mungu atutokee ndio ihesabike kuwa tumeliona umbile lake, bali watumishi wake tu kutujia tayari hao ni umbile lake…… utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko??

Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42  kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43  nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45  Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, KADIRI MSIVYOMTENDEA MMOJAWAPO WA HAO WALIO WADOGO, HAMKUNITENDEA MIMI.

46  Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

Umeona?.. Vile vile tusiposikiliza sauti za watumishi wake, ni sawa na hatujaisikiliza sauti yake!.. Ndio maana hapo katika Isaya 52:2 anasema “nilipoita mbona hamkuitika?”.. maana yake ni kwamba wenyewe walidhani sauti wanayoisikia ni ya mwanadamu kumbe ni ya Mungu.. vile vile walidhani umbile walionalo mbele yao ni la mwanadamu kumbe ndio umbile la Mungu, kwahiyo wakayadharau maneno ya Mungu aliyoyazungumza kupitia watumishi wake..

Na hapa Kristo anarudia tena maneno hayo hayo ya Isaya na kusema… “Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. SAUTI YAKE HAMKUISIKIA WAKATI WO WOTE, WALA SURA YAKE HAMKUIONA.”.. Maana yake Mungu alizungumza nao mara nyingi, na kuonekana kwao mara nyingi lakini hawakuwahi kumsikia wala kumwelewa wala kumfahamu hata mara moja, kwasababu mioyo yao ilikuwa mbali naye.

Na sisi tunajifunza kuwa sauti ya Mungu haiji kwetu kama sisi tunavyotaka au tunavyopanga, wala Mungu hatujii kimaumbile kama sisi tunavyotaka!..

Ni wengi sana wanafunga na kukesha ili kwamba Mungu awatokee, na waisikie sauti ya Mungu kama vile redio,..kama unafanya hivyo nataka nikuambie kuwa “unapoteza muda wako”.. kwasababu hiyo sio Njia ya MUNGU kuzungumza na sisi, hizo ni njia zetu sisi wanadamu za kuwasiliana..Mungu yeye anazo njia zake, ni lazima tuzijue hizo, tusilazimishe atumie zetu… “atafanya hivyo akipenda”, lakini si kanuni yake!.

Ukitaka kuisikia sauti ya Mungu vizuri, soma Neno na kulitafakari, Sikiliza mahubiri ya watumishi wa Mungu wa kweli, na ishi maisha matakatifu. Hapo utamwona Mungu sana katika maisha yako na utamsikia sana.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Swali: Kwanini Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri kwa miaka 400, Ni kosa gani kubwa walilolifanya mpaka Mungu kuwauza kwa Farao miaka yote hiyo?

Jibu: Hakuna kosa lolote walilolifanya mpaka kufikia hatua hiyo ya kupelekwa Misri katika nyumba ya utumwa. Bali Mungu aliruhusu iwe hivyo, kwa makusudi maalumu. Ni kama tu Yusufu alivyoenda kuuzwa kwa Misri kwa Potifa, maandiko hayaonyeshi kuwa Yusufu alifanya kosa lolote lililompelekea kwenda kuuzwa kama mtumwa kwa Potifa, lakini maandiko yanaonyesha kuwa Mungu alimpeleka Misri kwa lengo la kuwaokoa watu wengi siku za mbeleni, tunalisoma hilo katika Mwanzo 45:4-8

Mwanzo 45:4 “Yusufu akawaambia ndugu zake, Karibuni kwangu; basi, wakakaribia. Akasema, Mimi ni Yusufu, ndugu yenu, ambaye mliniuza kwenda Misri. 

5 Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi zenu, kwa kuniuza huku; MAANA MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUHIFADHI MAISHA YA WATU.

 6 MAANA MIAKA HII MIWILI NJAA IMEKUWA KATIKA NCHI, NA IKO TENA MIAKA MITANO ISIYO NA KULIMA WALA KUVUNA. 

7 MUNGU ALINIPELEKA MBELE YENU KUWAHIFADHIA MASAZO KATIKA NCHI, NA KUWAOKOA NINYI KWA WOKOVU MKUU

8 Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri”.

Hali kadhalika Mungu aliwapeleka wana wa Israeli Misri na kuwafanya kuwa watumwa, kwa malengo makuu mawili.. ambayo yanafanana na yale ya Yusufu.

1.MUNGU KUTANGAZA UKUU WAKE.

Kupitia wokovu wa Israeli kutoka Misri kwa mapigo yale 10 aliyompiga nayo Farao, na kwa kupitia ishara za ajabu alizozofanya jangwani kama kushusha Mana, kuleta Kware, kudhihirisha Nguzo ya Wingu na Moto n.k, ulimwengu umeweza kumjua Mungu wa Ibrahimu kuwa ni Mungu mkuu na wa haki na mwenye nguvu nyingi na maajabu mengi.

Kwahiyo ijapokuwa Israeli waliteswa Misri lakini maisha yao baadaye yalikuja kuwa mahubiri makubwa sana kwa ulimwengu kumjua Mungu wa kweli, pengine wasingepitia hiyo njia ya mateso tusingemjua Mungu kwa kiwango hicho.

2. KUTANGAZA NJIA YA WOKOVU

Lengo la pili la wana wa Israeli kupitia yale maisha ni kutangaza njia ya Wokovu. Maisha yao kuanzia Misri mpaka Kaanani, ni ufunuo kamili wa maisha ya Wokovu kutoka Dhambini(Misri), kueleka mbinguni (Kaanani) mji wa raha.

Tunapomwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zetu, katika roho ni kama tumetoka Misri..na hivyo Kristo anatuweka huru mbali na vifungo vyote vya dhambi, kwasababu maandiko yanasema “atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi (Yohana 8:34)”.

Hii inatufundisha nini?.. Si kila mateso tunayoyapitia yanatokana na makosa tuliyoyafanya?.. Yusufu hakuna kosa alilolifanya mpaka kufikia kuuzwa Misri kwa Potifa na hata kufungwa gerezani, vile vile wana wa Israeli hakuna kosa walilolifanya mpaka kufikia kuwa watumwa kwa muda ule, bali Mungu aliruhusu hayo yatokee ili mwisho wake aonyeshe utukufu wake!..

Kwahiyo hatutakiwi kukata tamaa tunapopitia shida, maadamu tuna uhakika tupo sawa na Mungu (yaani tunaishi maisha yanayompendeza yeye), vile vile tunapopitia magonjwa ya muda mrefu hatupaswi kukata tamaa wala kulaumu, bali tunapaswa kushukuru na kuendelea kuomba na kuishi maisha yanayompendeza, kwasababu Mungu anataka kufanya maisha yetu kuwa ushuhuda..

Hata Kristo maisha yake yalikuwa ni ya ushuhuda, alikuwa kama namna ya mtumwa (Wafilipi 2:7-8), lakini alijua mwisho wake utakavyokuja kuwa, na sisi hatuna budi kuwa watu wa namna hiyo hiyo, kwasababu mwisho wetu utakuwa mzuri hata kama mwanzo wetu umekuwa mbaya na wa kukatisha tamaa, maadamu tupo katika Neno lake na amri zake, basi hatuna haja ya kuwa na hofu, ni suala la muda tu.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

JIHADHARI NA MKUTANO WA WATU WALIOCHANGANYIKANA.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

Rudi nyumbani

Print this post

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 3

Wagalatia 2:3 “Lakini Tito aliyekuwa pamoja nami, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa.

4  BALI KWA AJILI YA NDUGU ZA UONGO WALIOINGIZWA KWA SIRI; AMBAO WALIINGIA KWA SIRI ILI KUUPELELEZA UHURU WETU TULIO NAO KATIKA KRISTO YESU, ILI WATUTIE UTUMWANI;

5  ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.”

Hapo kuna mambo matatu (3).. NDUGU WA UONGO, 2) WALIINGIA KWA SIRI, na 3) KUUPELELEZA UHURU.

1.NDUGU WA UONGO.

Watu waliookoka waliitwa NDUGU, na hata leo wanaitwa hivyo hivyo “Ndugu”, lakini wapo Ndugu wa Kweli na pia wapo wa “Uongo”. Ndugu wa kweli ni wale waliookoka kikweli kweli, ambao wapo katika kundi au kusanyiko katika Nia ya KRISTO na si kwaajili ya kutafuta mambo yao wenyewe (1Wakorintho 16:20 na Wagalatia 1:2).

Lakini “Ndugu wa Uongo” Hao ni watu ambao wanajiingiza katika kanisa, ikiwa Nia yao si kumtafuta Kristo wala kumtumikia bali kutafuta mambo yao mengine kama Fedha, au Fursa Fulani, na wengine kuupeleleza uhuru wa wakristo na wengine ni mawakala kabisa wa Ibilisi, wanajiunga kwa lengo la kuliharibu kundi na kulisambaratisha. Mfano wa hao ndio wale Paulo aliwaozungumzia katika waraka kwa Wafilipi..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”.

Makundi haya ya Ndugu wa Uongo, yamesambaa katika nafasi zote, kuanzia Wachungaji, Mitume, manabii, waimbaji, mpaka washirika/waumini.

2. WANAJIINGIZA KWA SIRI

Kundi hili la Ndugu wa Uongo, huwa hawajiingizi kwa wazi bali kwa siri, maana yake ni kwamba wanajigeuza na kufanana na Ndugu wa kweli.. lakini ndani yao wanajua ni nini wanatafuta sawasawa na maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 11:13  “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.

14  Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

15  Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”

3. KUUPELELEZA UHURU.

Sasa ni Uhuru gani ambao Wakristo wanao?.. Jibu: Ni uhuru unaotuweka mbali na utumwa wa Sheria… Katika Ukristo hatuna sheria za kutahiriwa, kwamba ni lazima mtu atahiriwe au asitahiriwe ndipo akubaliwe na Mungu, vile vile na sheria nyingine zote kama kushika sabato na kushika miezi na sikukuu, kuna aina fulani tu ya chakula n.k hizo zote maandiko yanasema tumewekwa huru nazo..

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo……………………..

20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21  Msishike, msionje, msiguse;

22  (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23  Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili”.

Sasa walikuwepo wayahudi ambao wanajiingiza katika kanisa la Kweli la Kristo, si kwa lengo la kumtumikia Bwana, bali kwa lengo la kuwatwika watu mzigo wa kushika sabato, na mwandamo wa mwezi na sikukuu za kiyahudi.

Hata sasa wapo watu baadhi ambao wengine wanatenda mfano wa hayo kwa kujua au kwa kutokujua, mfano mapokeo ya kushika sabato yanauua uhuru wetu katika Kristo, mapokeo ya kutahiriwa yanaua uhuru wetu katika Kristo n.k

Hivyo hatuna budi kuzipima roho, si kila pokeo ni la kupokea.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx

Mada Nyinginezo:

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Rudi nyumbani

Print this post

Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.

Jibu: Ni kweli Kristo alizichukua dhambi zetu kama biblia inavyosema katika kitabu cha Petro..

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeshakamilika asilimia mia kwamba hatutakuwa na kasoro zozote kuanzia hapo na kuendelea…Kasoro chache chache na madhaifu machache chache bado tutaendelea kuwa nayo mpaka siku tutakapopata ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).

Wakati parapanda ya mwisho itakapolia hapo ndipo tutapata ukombozi wa miili yetu, na tutakuwa wakamilifu asilimia zote kwasababu tutapewa miili mingine isiyo na kasoro wala madhaifu.. lakini sasa ulimwenguni bado tupo katika mapambano, bado tupo vitani, bado ibilisi yupo, bado tutapitia vipindi vya kukosea vidogo vidogo, lakini si vya kutuangusha kabisa!!.. Kama kile Petro alichopitia wakati anakutana na Paulo kule Antiokia (Soma Wagalatia 2:11-14).

Vile vile tutapitia vipindi vya kuudhiwa, na kupata hasira, tutapitia vipindi vya kukosea kuongea, kukosea kutenda, tutapitia vipindi pia vya kuwakosa wengine pasipo kujua au kwa kujua, tutapitia vipindi vya kumkosa Mungu kwa kujua au kwa kutokujua n.k.. sasa kwa kasoro hizo zote tunazozibeba ni lazima tuwe watu wa kuomba rehema na toba mara kwa mara ili muda wote tudumu katika usafi na pia Bwana anyooshe mapito yetu..

Hiyo ndiyo sababu pia Bwana Yesu akatufundisha kuomba toba na rehema kila mara..

Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2  Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]……………….

4 UTUSAMEHE DHAMBI ZETU, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.

Kwahiyo ni lazima kuomba rehema na toba kila siku, kwasababu bado tupo katika mwili, na pia ni ishara ya unyenyekevu kwa Mungu.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Fahamu Namna ya Kuomba.

JIRANI YANGU NI NANI?

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?


Jibu: Tusome,


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Mstari huo tukiusoma kama ulivyo ni rahisi kutafsiri kuwa “Biblia imekataza kuchinja wanyama na kula nyama”…lakini kiuhalisia hiyo sio maana yake kabisa…kwasababu kama hiyo ingekuwa ndio maana yake basi pia hapo imekataza matoleo… na tunajua matoleo ni jambo linalokubalika mbele za Mungu (Warumi 25:26).


Sasa tukisoma kuanzia ule mstari wa kwanza utaona Mungu anawakemea au kuwaonya wale watu ambao wanakusanya vingi na vikubwa na kwenda kumtolea Mungu, wakidhani kuwa Mungu anapendezwa na sadaka zao hizo kubwa na nyingi na huku mioyoni wapo mbali na Mungu.


Na utaona Bwana anazidi kusema.. “Mbingu na dunia ni mali yake, hakuna chochote tutakachoweza kumpa yeye ambacho kitakuwa cha kipekee”…ikifunua kuwa Mungu hana haja na vitu bali mioyo yetu, kwasababu kila kitu ni chake.


Isaya 66:1 “BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?


2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.


Umeona?..Mtu mnyonge ndiye atakayemwangalia Bwana, mtu mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno lake…Maana yake mtu wa namna hii atakapoleta sadaka yake ndio Mungu atakayoikubali, lakini mtu mwovu na mwenye kiburi Mungu haitaki sadaka yake.


Sasa endapo mtu mwovu anayemkataa Mungu analeta sadaka yake mbele za Mungu, sadaka yake hiyo inaonekana kama ni sadaka ya hatia.


Kama akileta Ng’ombe na kumpeleka kwa Kuhani kama sadaka ya kuteketezwa, Bwana ataiona sadaka hiyo kama ni kafara ya Mtu sio ya ng’ombe, hivyo atajitafutia laana badala ya baraka.


Utaona maandiko yanazidi kulisisitiza hilo katika Mithali 15:8

.
Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA…”

Ndio maana katika Isaya 66, Bwana anasema..


Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.


Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kuwa, Bwana hapendezwi na matoleo mabaya, yeye alisema kulitii Neno lake ni bora kuliko dhabihu Soma (1Samweli 15:22).


Hivyo usipeleke madhabahuni fedha haramu, fedha iliyopatikana kwa rushwa, kwa wizi, kwa uuuzaji wa vitu haramu kama bangi, pombe, sigara au hata kwa uuzaji wa mwili.


Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya BWANA, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako, yote mawili”


Vile vile hatupaswi kumtolea Mungu dhabihu huku hatuna mapatano sisi kwa sisi..


Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”


Bwana Yesu atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Jibu: Tusome,

Yohana 11:14  “Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.

16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye”

Kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Tomaso alitaka na yeye kwenda kufa pamoja na Lazaro, lakini kiuhalisia sio hivyo!.

Tomaso hakutaka kwenda kufa pamoja na Lazaro, bali hapo alimaanisha “kwenda kufa pamoja na Bwana Yesu”.

Ili tuelewe vizuri tuanze kusoma kisa hicho kuanzia juu mstari ule wa tano..(Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa).

Yohana 11:5  “ Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.

6  Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.

7  Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, TWENDENI UYAHUDI TENA.

8  Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, JUZIJUZI TU WAYAHUDI WALIKUWA WAKITAFUTA KUKUPIGA KWA MAWE, NAWE UNAKWENDA HUKO TENA?

9  Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.

10  Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.

11  Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

12  Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.

13  Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.

14  Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.

15  Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16  Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, TWENDENI NA SISI, ILI TUFE PAMOJA NAYE”

Katika kisa hiki tunaona Bwana Yesu anawapa taarifa wanafunzi wake ya kurejea tena kule Uyahudi ambapo walitaka kumpiga mawe mpaka afe!.. na taarifa hiyo ikawashitusha wanafunzi inakuwaje anataka kurudi tena huko kwenye hatari! (Maana yake si ndo anaenda kufa sasa!)

Lakini  Tomaso aliposikia wanafunzi wenzake wakimhoji hivyo, ndipo na yeye akawashauri kwamba wasimwache aende pake yake huko uyahudi, bali nao pia waende pamoja naye, ili kama ikitokea kauawa basi na wao wafe pamoja naye!.

Ni moyo mzuri aliokuwa nao Tomaso, lakini hakujua kuwa kufa kwaajili ya Kristo ni Neema na si jambo la kujiamulia tu au kujivunia kwamba linaweza kutendeka kwa uwezo wa mtu.

Mtume Petro alijaribu hilo zoezi kama la Tomaso likamshinda, kwasababu alidhani anaweza kufa ajili ya Kristo kwa nguvu zake..

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32  lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

33  Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani AU HATA KIFONI.

34  Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui”.

Zaidi sana huyu Tomaso ambaye alitaka kwenda kufa pamoja na Bwana, siku Bwana anakamatwa alimkimbia, hakuonekana!..(huenda ndo alikuwa Yule kijana aliyekimbia uchi, Marko 14:52)…na zaidi sana hata baada ya kufufuka kwake bado ilikuwa ni ngumu kuamini mpaka alipotokewa na Bwana Yesu..(huyo ndio mtu aliyetaka kwenda kufa na Yesu Yerusalemu)

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Tomaso hakutaka kwenda kufa na Lazaro, vinginevyo ingekuwa haina maana… lakini kinyume chake alitamani kwenda kufa pamoja na Bwana kwasababu aliamini huo ni ushujaa mkuu wa Imani.

Jambo tunaloweza kujifunza ni kuwa, hatupaswi kuzitumainia nguvu zetu, hatuwezi kusema tutamtumikia Mungu kwa nguvu zetu, hatuwezi kujivuna kuwa tutafanya hiki au kile kwa nguvu zetu, bali siku zote hatuna budi kuwa katika hali ya unyenyekevu, na kujishusha mbele za Bwana, kama tunatamani kufa kwaajili ya Bwana kifo cha kishujaa, basi tumalizie kwa kusema, BWANA TUSAIDIE

Na chochote kile tukifanyacho au tukikusudiacho ni lazima kumalizia kwa kusema “KWA MSAADA WA BWANA KITAFANIKIWA”.. Lakini tukijivuna kuwa tunaweza hiki au kile, tutaishia kumkana na hata kumsaliti.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

Swali: Je mapepo yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai kama mawe, milima, bahari, maji au nyumba, na hata kubadilisha maumbile ya hivyo vitu?

Jibu ni LA! Mapepo hayawezi kuviingia vitu visivyo na uhai bali yanaweza kuvitumia vitu visivyo na uhai.. mapepo hayawezi kuyaingia mawe au maji au mchanga au maji kama vile yanavyoingia ndani ya mtu, na kuviendesha vitu hivyo kama yanavyowaendesha wanadamu… Sehemu pekee ambayo mapepo yanaweza kuingia ni ndani ya viumbe hai kama wanadamu na wanyama, basi!

Biblia imerekodi mara kadhaa mapepo kuingia ndani ya watu (Luka 8:27) na pia ndani ya wanyama soma Marko 5:12-13. Lakini hakuna mahali popote panapoonyesha mapepo yamewahi kuingia ndani ya mawe au katika maji au katika mchanga, au katika matofali au katika gari la farasi au katika chakula..

Mapepo yanachoweza kufanya ni kuvitumia tu vitu vya asili, kwamfano yanaweza kuvumisha upepo lakini si kuingia ndani ya upepo, vile vile yanaweza kutetemesha ardhi lakini si kuiingia ardhi, yanaweza kuitikisa bahari lakini si kuiingia bahari… uwezo ambao hata sisi wanadamu tunao, sisi tunaweza kuvumisha upepo tukiwa na kifaa kinachoitwa feni, lakini si kuuingia upepo, vile vile tunaweza kutengeneza mawimbi ya bahari kwa vyombo maalumu n.k, lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeiingia bahari na kuiendesha bahari kama vile tunavyoiendesha mikono yetu au miguu yetu.

Na mapepo ni hivyo hivyo, hayana uwezo wa kuviingia vitu visivyo na uhai.

Kwahiyo tunachopaswa kufanya ili roho za mapepo zisiweze kutumia vitu vya asili kutuletea matatizo ni sisi kudumu katika usafi na utakatifu pamoja na kuomba… tukifanya hivyo shetani na mapepo yake hawawezi kutumia vitu vinavyotuzunguka kutuletea madhara, hawawezi kuzitumia nyumba zetu kama vituo vyao vya mikutano.

Lakini tusipojisogeza karibu na Mungu, basi shetani atatumia vitu vyote kutudhuru, atatumia ardhi, bahari, mabonde, na magari na hata nyumba kutuletea matatizo…

Isaya 13:21 “Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

MAJINI WAZURI WAPO?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Jibu: Tusome,


Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”

Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).


Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?


1) Mitume na Manabii:


Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.


Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.


2) Msingi


Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.


1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.


YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.


Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.


Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.


Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k


Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.


Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

Jibu: Tusome..

Wafilipi 3:2  “Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao”

Hapa kuna makundi matatu yaliyotajwa ambayo tunapaswa tujihadhari nayo, kundi la Kwanza ni “MBWA” kundi la Pili ni “WATU WAJIKATAO” na kundi la tatu ni “WATU WATENDAO MABAYA”.

Sasa kabla ya kwenda kuangalia Mbwa ni watu wa namna gani, kwanza tuyatazame haya makundi mawili ya mwisho, ambayo ni watu wajikatao na watenda mabaya..

Watu “watendao mabaya” wanaozungumziwa hapo, ni watu walio ndani ya imani lakini wanatenda mabaya.. watu hawa biblia imetuonya tujihadhari nao, yaani tusichangamane.. Mtume Paulo alizidi kuliweka hili vizuri katika kitabu cha 1Wakorintho 5:9-11.

1Wakorintho 5:9  “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10  Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11  Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye”.

Lengo la kutochangamana na makundi haya ya watu walio ndani ya kanisa lakini ni watenda mabaya, ni ili wajisikie aibu kwa wanayoyafanya na hatimaye wageuke na kutubu.

Kundi la Pili: Ni “Watu Wajikatao”.. kumbuka hapa anasema “watu wajikatao” na sio “watu wajikataao” kuna tofauti ya kujikata na kujikataa.. hapa wanazungumziwa watu wanaojikata!.. Sasa ni watu gani hao wanaojikata?.. si wengine bali walikuwa ni wayahudi ambao walikuwa wanashinikiza tohara, kuwa ndio dalili ya kukubaliwa na Mungu..

Lilikuwepo kundi la walioamini, ambao hata sasa lipo lililokuwa linasisitiza tohara kuwa ni jambo la lazima, na kwamba mtu asipotahiriwa hawezi kukubaliwa na Mungu. Watu hawa walikuwa kweli wamemwamini Yesu lakini sheria za torati bado zilikuwa zinawaendesha, ambazo kimsingi hizo haziwezi kumkamilisha mtu, bali Neema ya Yesu pekee… kushika mwezi, mwaka, siku, sabato haya yote hayafai katika kumkamilisha mtu.

1Wakorintho 7:19  “Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.

20  Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa”

Kwa maelezo mengine marefu kuhusiana na watu wajikatao unaweza kufungua hapa >>> WATU WAJIKATAO

Na kundi la Tatu na la Mwisho, ambalo biblia imetaja tujihadhari nalo ni kundi la “MBWA”.

 Sasa utajiuliza hawa “Mbwa” ni akina nani?

Bwana Yesu aliwataja wazi kabisa hawa Mbwa ni wakina nani.. Tusome..

Mathayo 7:15  “Jihadharini na MANABII WA UONGO, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni MBWA-MWITU WAKALI.

16  Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”

Umeona?… Kumbe Mbwa wanaozungumziwa hapo ni “Manabii wa Uongo” na tena hawajatwi kama Mbwa tu!, bali kama “Mbwa-Mwitu” tena wakali!.. maana yake wasiohurumia kundi.. Na hatutawatambua kwa mionekano yao, kwasababu kwa nje wamevaa mavazi ya kondoo, (wanafanana na watumishi wa kweli wa Mungu) lakini tutawatambua kwa matunda yao, maana yake kwa yale wanayoyafundisha na wanayoyaishi.

Na manabii wa uongo ni mjumuisho wa Mitume wa Uongo, wachungaji wa uongo, waalimu wa Uongo, pamoja na waimbaji wa Uongo. Kwaufupi watu wote wanaosimama kutangaza injili kwa wengine! Lakini maisha yao ya ndani si wakristo, ila kwa nje wanasifika kama watumishi wa Mungu.

Ikiwa mtu atasimama na kuhubiri injili nyingine tofauti na ile iliyoandikwa katika biblia, basi huyo kibiblia ni “Mbwa”, ikiwa mtu atahubiri injili isiyo ya wokovu, badala yake ya kumpoteza mtu au kumfanya afurahie dhambi..mtu huyo kibiblia ni Mbwa, na tumetahadharishwa kukaa mbali naye.

Nabii wa Kweli wa Mungu atakuwa kama Musa!, Mpole kuliko wote, na mwenye kuwaelekeza watu kwa Mungu na si kwake wala kwa shetani.

Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

 2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

 3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye”

Je! Unaongozwa na nani?.. Manabii wa Uongo, Miujiza na Ishara au NENO LA MUNGU?.

Kumbukumbu 6:4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 

5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

Rudi nyumbani

Print this post