Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Neno la Mungu ambalo ndio mwanga wa njia zetu na taa ya miguu yetu. Zab 119:105..Leo tutajifunza kwa ufupi sana juu ya kulipa Zaka, Kimaandiko Zaka ni fungu la 10, yaani sehemu ya 10 ya mapato ya mtu anayatoa kwa Mungu. Kwahiyo zaka ni mojawapo ya aina ya sadaka.
Kabla hatujaenda kujifunza kuhusu umuhimu wa kulipa zaka, kama ina ulazima au la! Hebu tujifunze kidogo historia ya ZAKA.
Zaka kwa mara ya Kwanza ilianza kutolewa na mtu anayeitwa Ibrahimu, ambaye anajulikana kama Baba wa Imani.
Mwanzo 14:17 “Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme.
18 Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
19 Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
20 Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. ABRAMU AKAMPA FUNGU LA KUMI LA VITU VYOTE”.
Ibrahimu alimpa fungu la 10 huyu Melkizedeki, huyu Melkizedeki alikuwa ni Mungu aliyekuja katika Mwili wa kibinadamu… na pia anajulikana kama Kuhani Mkuu, mfano wa Mwana wa Mungu (Yesu Kristo) hana baba, wala mama, wala hana mwanzo wa siku wala mwisho wake. Kwahiyo alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyekuja katika mwili wa kibinadamu.
Sasa wakati Abramu ametoka kumwokoa ndugu yake Lutu ambaye alikuwa ametekwa yeye pamoja na wanawe, njiani wakati anarudi akakutana na Huyu Melkizedeki, na huyu Melkizedeki alikuwa amebeba Divai na Mkate, akampatia Abramu na kwasababu Abramu alimpenda sana Mungu, hakuona vyema kupokea bure bila kutoa chochote…zaidi ya yote Mungu amemwonekania na kumfanikisha katikati ya maadui zake na kuwashinda! Hivyo ndani yake kuna kitu cha kipekee kikamgusa akaona si vyema kutomrudishia chochote Mungu wake, hivyo akaamua mwenyewe pasipo kuambiwa na mtu yeyote kumtolea Mungu wake sehemu ya 10 ya vitu vyake!!! O huo ni moyo wa namna gani? Kumbuka hakuambiwa hata na Mungu afanye vile, ni yeye mwenyewe tu kuna kitu ndani yake kilimfanya ajisikie vibaya endapo angemwona Mungu wake anaondoka mikono mitupu, na hicho si kingine zaidi ya Roho Mtakatifu.
Sasa wakati huo kulikuwa hakuna sheria yoyote, wala amri 10 na Mungu hakuingia Agano na Ibrahimu kuhusu zaka, Miaka kama 400 hivi baadaye ndipo wana wa Israeli, walikuja kupewa sheria na Mungu! Na miongoni mwa hizo sheria ilikuwa ni pamoja na kulipa zaka!, ilikuwa ni lazima kulipa zaka, mtu asipolipa zaka ilikuwa inahesabika kwake kuwa ni dhambi!, na mbele za Mungu ni kama mwizi (Malaki 3:8-9).
Lakini sasa hatuishi kwa sheria bali kwa Imani, na Imani tunayoizungumzia ni Imani ile ile ya kwanza kama ya Ibrahimu, yaani Imani ya kufanya mambo bila ya kusukumwa sukumwa, na Imani hiyo ndio kama hiyo ya Ibrahimu, ya kumtolea Mungu fungu la 10 pasipo masharti!..Ibrahimu alitoa pasipo masharti, wala sheria, wala torati kwasababu Torati hata bado ilikuwa haijaja, wala kulazimishwa, wala kusukumwa wala kuombwa, wala kumwuliza Mungu, wala kuhubiriwa na mtu yeyote bali alitoa kwa Imani na kwa moyo, akitafakari kwamba vyote vimetoka kwa Mungu, na Mungu ndiye mpaji wangu (Yehova-YIRE), hivyo kama yeye amenipa sehemu kubwa ya vitu hivi, basi mimi nitamrudishia walau sehemu ya 10 ya vitu alivyonipa. Na akajiwekea hiyo kuwa ndio sheria yake daima! Kila sehemu ya 10 anayopata anamrudishia Mungu.
Ndugu, Ibrahimu alikutana na Melkizedeki, na hata sasa huyu Melkizedeki yupo naye si mwingine bali ni Bwana wetu Yesu Kristo, maandiko yanalithibitisha hilo katika…
Waebrania 6:20 “alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.
Waebrania 7:1 “Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
2 ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;
3 hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
4 Basi, angalieni jinsi mtu huyo alivyokuwa mkuu, ambaye Ibrahimu, baba yetu mkuu, alimpa sehemu ya kumi ya nyara”.
Waebrania 5:5 “Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.
6 kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki”.
Umeona Kristo amefananishwa na Melkizedeki, na kama Melkizedeki alipewa sehemu ya 10 na Ibrahimu, kadhalika Kristo naye anastahili sehemu ya 10, kwasababu yeye ndiye Melkizedeki wa Agano letu, na kama Melkizedekia alivyompigania Ibrahimu ndivyo Kristo anavyotupigania sisi sasa hivi,
Na kama Ibrahimu alimpa Melkizedeki fungu la 10 pasipo masharti, wala pasipo torati, wala pasipo sheria yoyote, wala pasipo kuhubiriwa na mtu, wala pasipo kushauriwa na mtu, wala pasipo kusukumwa na mtu yeyote ndivyo hivyo hivyo leo hii tunapaswa tumtolee YESU KRISTO fungu la 10 pasipo sheria yoyote, wala pasipo masharti yoyote, wala pasipo mahubiri yoyote, wala pasipo kusukumwa na mtu..Linapaswa liwe ni jambo linalotoka moyoni kwamba tunatambua uwepo wa Yesu Kristo katika maisha yetu na hivyo tunamheshimu kwa kumtolea fungu la 10, yeye hana shida na fedha! Lakini anaitazama mioyo yetu!. Na Bwana Yesu mwenyewe aliruhusu hilo katika (Mathayo 23:23).
Ukiona mtu anapinga kulipa ZAKA!(Na huku ameshaujua ukweli) Na anapinga kumtolea Mungu, Huo ni uthibitisho kuwa hana ROHO MTAKATIFU ndani yake! Ni moja ya uthibitisho wa mtu aliyekosa Roho Mtakatifu ndani yake!..Kwasababu ni wazi kuwa hampendi Mungu, kwasababu hawezi kumshukuru kwa kutoa hata sehemu ya 10 ya mali zake na kumrudishia yeye, ingawa anavuta pumzi bure, anakanyaga ardhi ambayo sio yake bure, anakula chakula ambacho hajui kimetengenezwaje tengenezwaje! Hathamini hata Kristo aliyeotoa uhai kwa ajili yake bure..Kwa ufupi ni mtu asiye na shukrani.
Na mtu wa namna hiyo atawezaye kumshukuru Mungu kwa kutoa sehemu ya 10 ya maisha yake kuhubiri Injili?, atawezaje kutoa kutoa hata uhai wake kwaajili ya Injili?, au atawezaje kuifia Imani? Kama tu sehemu ya 10 ya fedha yake hawezi kuitoa?. Huyo Mtu atawezaje hata kuacha vyote na kumfuata Kristo kama tu sehemu ya 10 kutoa ni vita?..Atawezaje kumtolea Mungu katika vyote alivyonavyo kama Yule mwanamke aliyetoa senti mbili na Bwana akamsifia? Tafakari tu!
Hivyo ZAKA sio kitu cha kukwepa kabisa! Hakitolewi kwa sheria wala kwa torati, wala kwa imeandikwa wapi kwenye biblia, bali kwa moyo kama vile Ibrahimu!..Kama huna kazi yoyote inayokupatia kipato hapo upo huru!, lakini chochote unachokipata tofauti na kazi kitolee sehemu ya 10 katika hicho na kumrudishia Mungu, huna kazi lakini umepewa zawadi kiasi Fulani cha fedha kitolee sehemu ya 10, na utoe kwa moyo pasipo kulazimishwa, kwasababu Mungu sio mkusanyaji mapato! Anataka tumtolee kwa Moyo na kwa furaha, huku tukielewa umuhimu wa kumtolea yeye kama Ibrahimu alivyofanya.
Kitakachompeleka mtu kuzimu sio kitendo cha kukiuka kulipa zaka au kuzini, au kuiba, au kutukana hapana kitakachompeleka mtu kuzimu ni kumkosa Kristo moyoni mwako, akaaye kama Roho Mtakatifu, ambapo sasa matokeo ya kutokuwa na Roho Mtakatifu ndio hayo sasa atakuwa mwizi, mwasherati, mtukanaji, atakuwa ni mtu asiyekuwa na Moyo wa Utoaji kabisa, likija suala la utoaji ni vita, anakuwa hawezi kuwasaidia wengine, na pia hawezi kuchangia chochote katika ufalme wa mbinguni katika utoaji wake, pia anakuwa mtu asiyesamehe Kwasababu Mtu aliye na Roho Mtakatifu hawezi kufanya mojawapo ya hayo mambo kwasababu Roho Mtakatifu atakuwa anaugua ndani yake kuhusu dhambi na atakuwa anaugua pia kuhusu ni kwanini hamtolei Mungu, hivyo hawezi kukwepa kulipa zaka kama vile asivyoweza kukwepa kuwasaidia wengine au kusali.
Upo usemi unaosema kwamba, mimi ni mkamilifu katika kila kitu! Isipokuwa ni zaka tu ndio sitoi!
Bwana akubariki jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
Kumbukumbu 22:8 “Utakapojenga nyumba mpya, fanya ukuta kando-kando ya dari lako, usije ukaleta damu juu ya nyumba yako, mtu akianguka huko”.
Bwana Yesu alisema, mtu yeyote anayeyasikia maneno yangu na kuyatenda anafananishwa na mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba…(Mathayo 7:24), Hii ikiwa na maana kuwa kumbe Maisha ya kila mtu aliyeokoka ni sawa na nyumba inayoijenga yeye mwenyewe,..Hivyo kila mtu anapaswa awe makini anapoijenga nyumba yake sio tu pale anapoujenga msingi wake bali pia mpaka pale anapomalizia…
Kwamfano tutaona hapa Bwana Yesu alikuwa anasisitiza juu ya msingi, ambao ndio mwanzo wa ujenzi wa maisha ya mtu, kwamba ukitaka nyumba yako(Maisha yako) yasiwe kazi bure basi zingatia ni ardhi gani unayoijengea nyumba yako, kama ni mwamba (ambao ndio maneno ya Yesu Kristo yenyewe) basi fahamu kuwa msingi wako nyumba yako utakuwa salama na nyumba yako itasimama imara milele lakini kama ni nje ya Kristo basi ujue Maisha yako unayoyaishi sasa hivi ni kazi bure kwasababu yatafikia mwisho yatakoma na utakuwa umepata hasara kubwa..
Lakini Sio tu kufanikiwa kuijenga nyumba yako juu ya mwamba imara, unapaswa pia uzingatie umaliziaji wa nyumba yako ili iwe katika ujenzi bora na salama..Kama tunavyosoma hapo juu enzi za agano la kale Mungu alitoa amri kwa waisraeli wote, pindi tu wanapomaliza kujenga nyumba zao, hawapasi kuzifunika tu kwa sakafu au matofali na kuziacha hivyo hivyo bila uzio wowote kama ujenzi mwingi unavyofanyika sikuhizi wa kuweka mabati, hapana bali Mungu aliwapa maagizo wahakikishe kuwa wanaweka ukuta kando-kando ya dari zao, ulionyanyuka, kusudi kwamba ikitokea mtu amepanda kule, na akateleza bahati mbaya, basi ule ukuta ulio kando kando ya dari umzuie asianguke mpaka chini, tofauti na ujenzi mwingi wa sasa hivi ulivyo, mtu akiteleza kwenye bati basi moja kwa moja ni mpaka chini, na pengine kumsababishia majeraha ya kudumu au mauti kabisa. Angalau baadhi ya magorofa marefu yana uzio huo kule juu kabsia, ingawa si yote.
Hivyo nyumba zote, na majengo yote ya kiyahudi ndivyo yalivyojengwa enzi zile. Na kama mtu asipofanya hivyo na ikatokea mtu akaanguka darini kwake, basi damu ya huyo mtu, Mungu ataitaka juu ya huyo mwenye nyumba.
Kama tulivyoona mkristo kweli anaweza akawa ameanza vizuri katika ujenzi wake, ameokoka, amemwamini Yesu Kristo, amepokea uzima wa milele, lakini hazingatii kuchukua tahadhari katika nyumba yake anayoijenga, haweki kuta, hajiwekei mipaka ya njia zake, hajui kuwa wapo watu wanamwangalia, wapo watu wanayatambelea Maisha yake kila siku, wanapanda mpaka juu ya dari lake, mahali ambao anadhania watu hawawezi kufika,Sasa kwa kutolijua hilo wale watu wanapofika, na kukutana na kikwazo kidogo tu, pengine wanamwona ni mvaaji wa vimini, unatembea nusu uchi barabarani halafu unasema umeokoka, ni rahisi wao kuanguka, na kusema kama wokovu ndio huu, ni heri niendelee kuwa kahaba milele…Hajui kuwa ameshamkosesha yule mtu na damu yake itatakwa juu yake.
Unakwenda disko, unatukana , na bado unasema umeokoka, unacheza kamari, una-bet na huku bado unasema umeokoka, wale watu wanaokutazama, wakiona mapungufu kama hayo, umewasababishia wao kuanguka mara mbili Zaidi. Ni heri ungesema sijaokoka wasingekuwa na la kujikwaa, na hiyo yote ni kwasababu hujiwekei kuta za kuilinda nyumba isiwe ya lawana.
Unasikiliza miziki ya kidunia, muda huo huo unamwimbia Mungu, wale watu wanaokuzunguka watakuonaje? Watasema kuna wokovu kweli hapo? unakula rushwa, unaongea matusi hivyo vyote ni vikwazo, unawasengenya wengine, hatujui kuwa sisi ni barua inayosomwa na watu wote. Ujenzi wetu wa mwisho unapaswa uthaminiwe kama ulivyokuwa ule wa kwanza.
Vinginevyo tutajikuta tunakwenda kulaumiwa kwa kuwakosesha wengine,. Na adhabu ya kuwakosesha wengine ni kubwa Zaidi, Bwana Yesu alitoa mfano wake na kusema ni heri mtu wa namna hiyo angefungiwa jiwe la kusagia na kutupwa baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hao.
Hivyo kama tumedhamiria kweli kumfuata Kristo, basi kila siku tujiangalie, tujiwekee mipaka, tuhakikishe ndani yetu hakuna mahali popote pa kumkwaza asiye amini..kuvaa vizuri ni mipaka!, kutokushiriki usengenyaji ni mipaka, kutoshiriki mazungumzo ya mizaha na kujiheshimu ni mipaka…Bwana atusaidie sote katika hilo.
Ubarikiwe. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.
HAMJAFAHAMU BADO?
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
NGUVU YA UPOTEVU.
http://wanatai.wingulamashahidi.org/
Ni muhimu kujifunza nini maana ya kukua kiroho,Namna ya kukua kiroho, faida za kukua kiroho. Na pia ni vizuri kujifunza mbinu za kukua kiroho.
Roho ni Utu wa Ndani wa Mtu ule unaozungumziwa katika kitabu cha Waefeso 3:16. Na utu huu wa ndani unakuwa si kwa kimo, bali kwa MAARIFA.
Mtu aliyemchanga kiroho anakuwa ana maarifa machache sana yamhusuyo Mungu. Haijalishi ana elimu nyingine yoyote nyingi kiasi gani, au ana elimu ya kidunia kiasi gani. Hivyo kukua kiroho maana yake kuongezeka maarifa katika kumjua Mungu.
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa hakuna mtu yeyote duniani ambaye ameshakuwa kiroho, na kufikia kiwango ambacho ndio mwisho. Hapana kila siku tunakuwa kiroho, haijalishi tuna maarifa kiasi gani kuhusu Mungu. Bado kila siku tunamsoma yeye kwasababu yeye hamaliziki.
Hivyo njia pekee ya kukua kiroho angalau kufikia kiwango fulani ambacho kitakupa ujasiri wa kuweza kuzidhibiti hila na mbinu za yule Adui. Ni kukaa chini kujifunza Neno la Mungu. Wengi wanaikwepa njia hii na kufikiri kuwa kuna njia nyingine ya mkato ya kukua kiroho, labda ya kuombewa, au kuwekewa mikono. Hakuna njia ya mkato zaidi ya hiyo ndugu!
Mbinu ya kukua kiroho inafananishwa sana na mbinu ya kukua kimaarifa shuleni, ili mwanafunzi afaulu vizuri njia pekee ni kusoma kwa bidii na kuzingaia yale waalimu wanayomfundisha..Kadhalika na sisi wakristo njia pekee ya kukua kiroho ni KULISOMA NENO KWA BIDII. Na kufuatilia kwa makini yale yanayofundishwa na watumishi wa Mungu walio wa kweli.
Na watumishi hao ni zile karama kuu tano, Mitume, Manabii, wainjilisti, waalimu na Wachungaji. Sio Mitume na Manabii na Waalimu unaowaona leo ambao Mungu wao ni tumbo kama biblia inavyosema..Bali Waalimu na wachungaji wanaofundisha kweli yote kama ilivyoandikwa katika Biblia Takatifu. Hao ndio wa kuwafuatilia kwa makini, kama vile mwanafunzi amfuatiliavyo mwalimu darasani..
Waefeso 4:11 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;
13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”.
Faida za kukua kiroho tunazipata katika mstari wa 13 na wa 14 unaosema…”
13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”
Lengo la kukua kiroho hata tutakapofikia cheo cha kimo cha Kristo. Ni ili tusichukuliwe chukuliwe na kila upepo wa elimu, kwa ujanja wa watu..Kwamfano utasikia watu wanakwambia mti fulani unasababisha kifo kwa wanafamilia. Au utasikia usikae baharini saa saba mchana kuna majini. au utasikia leo kimezuka hichi kanisani watu wanalishwa majani, wengine nyoka. Wengine wataambiwa ili wafunguliwe na matatizo yao watoe pesa kiasi fulani. Ili wafanikiwe wanunue mafuta haya au yale ya upako n.k
Hayo yote ndio yanayoitwa “upepo wa elimu” ambayo huwezi kuyashinda kama ni mchanga kiroho. Hivyo unapokuwa kiroho hizi Elimu zinakuwa hazikupelekeshi..Kunakuwa hakuna elimu yoyote inayozuka inataayoweza kukuchukua kwasababu una Elimu ya kutosha kuhusu Neno la Mungu. Haleluya.
Hivyo hizo ndio mbinu za kukua kiroho. Kwanza Soma Neno kwa bidii binafsi. Pili Jifunze kutoka kwa Watumishi wa Mungu, ambapo unaweza kusikiliza mahubiri kwa njia za semina, mitandano, kwenye vitabu n.k.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Utukufu wa Mungu ni nini?
Utukufu ni heshima fulani ya hali ya juu inayomfunika mtu au kitu. Wanadamu tuna utukufu wetu, Wanyama wanao utukufu wao kadhalika Mungu naye anao utukufu wake.
Sasa utukufu wa Mungu ni nini/ ni kitu gani?
Jibu: Utukufu wa Mungu ni UTAKATIFU! Ndio Heshima ya juu kabisa Mungu aliyo nayo..Yeye anatambulika kwa utakatifu wake, ambao ni ukamilifu, usafi na HAKI, Hilo ndilo vazi lake kuu, na kitambulisho chake na Heshima yake.
Kutoka 33:17 “Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako.
18 Akasema, Nakusihi unionyeshe utukufu wako.
19 Akasema, Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza jina la Bwana mbele yako; nami nitamfadhili yeye nitakayemfadhili; nitamrehemu yeye nitakayemrehemu.
20 Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.
21 Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;
22 kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;”
Kutoka 34:5″ Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana.
6 Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;
7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne”.
Hivyo huo ndio utukufu wa Mungu, (Utakatifu na Ukamilifu), yeye ni mwenye rehema, mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu na si mwepesi wa hasira kwa ufupi ni “UTAKATIFU”..
Lakini pia pamoja na kwamba ni mwenye Huruma lakini bado pia hachukuliani na uchafu ndio maana anasema hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia..Hatamwesabia mwasherati, mzinzi, mwongo, mlevi, muuaji, msengenyaji kuwa hana hatia.
Ikimaanisha kuwa Utukufu wake alionao wa UTAKATIFU NA UKAMILIFU, Anataka na sisi tuwe nao.
Walawi 11:45 Kwa kuwa mimi ni Bwana niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili kwamba niwe Mungu wenu; basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu.
Je! Utukufu wa Mungu upo juu yako nawe pia?..Kumbuka utukufu wa Mungu ni utakatifu, na biblia inasema hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao…(Waebrania 12:14).
Kwahiyo matendo yote yasiyotokana na utakatifu ndio yanayoondoa utukufu juu ya mtu.
Warumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu”
Na huo Mtu huwezi kuupata ukiwa nje ya Kristo, hivyo ni lazima UOKOKE! Kwa kutubu na kumaanisha kuacha dhambi, kisha ubatizwe katika ubatizo sahihi kwa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kwaajili ya ondoleo la dhambi sawasawa na Matendo 2:38, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako,. Ambaye ndiye utukufu wa Mungu, atakayekusaidia kuwa Mtakatifu kama vile jina lake lilivyo na kukuongoza katika kweli yote ya Biblia.
Kumbuka anasema “basi mtakuwa watakatifu kwakuwa mimi Bwana ni Mtakatifu”
Bwana akuabariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:
SAYUNI ni nini?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?
Malimbuko maana yake “kitu cha kwanza kuja au kuzaliwa au zao la kwanza”, kwa lugha ya kiingereza “first fruits”…Katika Biblia agano la kale mtoto wa kwanza wa kiume kuzaliwa alikuwa ni malimbuko. Na huyo ni lazima awe malimbuko kwa Bwana.
Mwanzo 49:3 “Reubeni, u mzaliwa wangu wa kwanza, Nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu”.
Na sio tu watoto wa kwanza wa kiume, Bali hata wanyama wa kwanza na mazao ya kwanza ya nchi yote hayo yaliitwa malimbuko, na yalipaswa yatolewe pia kwa Bwana.
Mambo ya Walawi 23:9 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu;”
Bwana alituoa maagizo kwa wana wa Israeli wote kutoa malimbuko katika mazao yao, yaani kupeleka sehemu ya kwanza ya mavuno yao nyumbani kwa Mungu, kuonesha shukrani zao mbele za Mungu kwa kupewa mazao..
Kama Bwana asingewapa mvua basi wasingepata hata hicho kidogo, kwahiyo “walimrudishia Bwana sehemu ya kwanza kabisa ya mazao yao”, kuonesha kuwa Mungu ni wa Kwanza na mengine yatafuata.
Jibu ni ndio! ilikuwa na Baraka nyingi, kwasababu siku zote kitu cha Kwanza kumtolea Mungu kina nguvu kuliko cha Pili. Nguo mpya ambayo haijavaliwa na mtu ina thamani zaidi, na heshima zaidi kuliko ile ya Mtumba.
Raisi wa kwanza wa nchi, huwa anayoheshima kubwa Zaidi kuliko maraisi wengine wanaofuata. Kadhalika sadaka ya kwanza kabisa inayofika mbele za Mungu ina nguvu kubwa zaidi kuliko zinazofuata..Na sadaka hiyo ni ya “malimbuko”.
Kadhalika sadaka ya malimbuko ndiyo inayobariki kazi yote inayofuata, mshahara wa malimbuko ndio unaobariki mishahara mingine yote inayofuata. Tutakuja kuona hapo chini kidogo, ni kwa namna gani Kristo aliitwa limbuko lao waliolala, ikasababisha baraka kwa wote watakaolala kama yeye.
Jibu ni ndio! Kama tunalipa sadaka za Zaka, Malimbuko nayo ni lazima..Na baraka zake ni zile zile…Kwamba cha kwanza ni bora kuliko cha pili, haijalishi cha pili kitakuwa na wingi gani..lakini cha kwanza ni cha kwanza tu.
Na pia Roho Mtakatifu ndani yetu anatushuhudia, kwamba hiyo kazi kama Mungu asingeibariki basi tusingepata chochote, kwahiyo tunamheshimu Mungu na kumwonyesha kuwa yeye kwetu ni wa KWANZA kwa vitendo! kwahiyo tunampa Malimbuko yetu.
Kama umeajiriwa au umejiajiri, Mshahara wa Kwanza unaoupata unaupeleka kwa Bwana. Usiogope kupungukiwa, wala usiwaze waze utapata vipi fedha, yeye aliyekupa hiyo kazi anajua zaidi kuliko wewe, anasema maua haifanyi kazi na bado hayasokoti yanazidi kupendeza tu. kitu ambacho hata Sulemani katika fahari yake, hajawahi kuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo!. Kama Mungu anayavisha maua ya kondeni vizuri hivyo je si zaidi sisi?. (Mathayo 6:28)…hivyo usiangalie mazingira yanayokuzunguka mtolee Bwana sehemu ya kwanza.
Kadhalika Faida ya kwanza ya Biashara yoyote iliyo halali uliyojiajiri ni hivyo hivyo, sehemu ya kwanza ya mazao yako ya shambani, kama umevuna debe 10 mpelekee Bwana, mifugo yako imezaa wazaliwa wa kwanza mpelekee Bwana, au ibadilishe katika fedha, uipeleke nyumbani kwa Bwana.
Kumbuka kama umeshatoa mzaliwa wa kwanza wa mfugo wako, hao wengine hupaswi kutoa kama malimbuko. Hao utatoa tu kama sadaka na kwa jinsi Bwana atakavyokujalia. Na kwa jinsi utakavyopenda wewe kutoa, haina masharti!
Kumbuka pia kama umeacha kazi fulani na kwenda kuanza nyingine, ambayo inazalisha kwa namna nyingine, na ina mkataba mwingine wa kukuingizia kipato, hapo ni lazima utoe tena limbuko kwa hiyo kazi mpya ulioanza. Kwa ulinzi wa kazi yako.
Mtu wa Kwanza kufufuliwa alikuwa ni Kristo! Lazaro alifufuliwa lakini alikufa tena…Hivyo ufufuo wake haukuwa na nguvu ya umilele, lakini Yesu alifufuliwa na hawezi kufa tena yupo mpaka leo, kwahiyo yeye ndiye mzaliwa wa kwanza wa walio kufa, (LIMBUKO).
Na kutokana na Mungu kumtoa kaburini na kumleta juu kama Limbuko, amesababisha hata sisi tuliomwamini tutakaofuata kufa kama yeye, nasi pia tupate hiyo ofa ya bure ya kufufuliwa katika siku ile! haleluya!
Hivyo kama sio Mungu kumtoa Yesu kuwa limbuko, baraka ya kufufuliwa sisi wengine tusingekuwa nayo.
1Wakorintho 15:20 “Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.
21 Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu.
22 Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
23 Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja”.
Wakolosai 1:18 “Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.
Hiyo ndiyo faida ya “kutoa sadaka ya malimbuko”, Inakuwa inabariki mazao mengine yaliyosalia..Kama Bwana Yesu alivyotubariki sisi tutakaokufa katika yeye. Tunalotumaini la ufufuo, kwasababu yeye amefanyika kuwa mtangulizi wetu, Na wewe unalo tumaini la kufufuliwa kazi yako upya, au biashara yako, au kilimo chako endapo kitasuasua kama ulitoa limbuko(kama sadaka ya utangulizi)! siku ile ulipoianza hiyo kazi,
Lakini pamoja na hayo yote! haitakufaidia chochote, kama utatoa sadaka ya malimbuko na huku maisha yako yapo nje ya wokovu, huku bado ni mlevi, bado ni msengenyaji, bado ni mtukanaji, bado ni mfanyaji masturbation, na bado kahaba, bado mla rushwa..Mungu wetu hafanyi kazi ya ukusanyaji mapato kwetu,…Kwamba uwe mwovu au usiwe mwovu kodi ni lazima ulipe!.
Hapana Mungu wetu hayupo hivyo, yeye hakusanyi mapato kutoka kwetu kama wafanyavyo TRA kwasababu yeye ana kila kitu tayari, anataka tu! tujifunze kutoa kwa faida yetu wenyewe, kama yeye alivyo mtoaji, na hapendezwi na sadaka ya mtu mwovu, hivyo kama unatoa sadaka na bado mlevi, au kahaba..ni afadhali usitoe kabisa kwasababu ni machukizo mbele za Mungu. Hakuchukii wewe, bali unachotoa kinamchukiza, na anataka tufanye kilicho bora.
Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.
Hivyo kama hujampa Kristo maisha yako umechelewa sana, ni afadhali ufanye hivyo sasa kabla mlango wa Neema haujafungwa, unachotakiwa kufanya ni kutubu kwa kukusudia kuacha kufanya dhambi tena!!, Unaamua kwa vitendo! kuacha ulevi, anasa, uvaaji mbaya, rushwa, na mambo yote machafu kisha unaenda kubatizwa tena! kwasababu kama ulibatizwa na umerudia machafu ya ulimwengu huu, kiasi hata cha kufanya uzinzi na uasherati unapaswa ukabatizwe tena katika maji tele, na kwa jina la Yesu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako kulingana na Matendo 2:38,
kisha baada ya kufanya hivyo Roho Mtakatatifu ataingia ndani yako, na kukupa uwezo wa kushinda dhambi kwa namna ya kipekee.
Baada ya kufanya hivyo, utakuwa umeokoka na kufanyika kuwa mwana wa Mungu, hivyo tafuta kusanyiko la kikristo linalomhubiri Kristo, na maneno yake ya kwenye biblia yenye vitabu 66 na sio vitabu 666, ujiunge hapo!, ili usizimike kiroho. Na Bwana mwenyewe atakusaidia kufanya yaliyosalia, kwasababu Neno lake ni mwanga wa njia zetu.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?
Matendo 13:21 “ Hatimaye wakaomba kupewa mfalme; Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila ya Benyamini, kwa muda wa miaka arobaini.
22 Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, MTU ANAYEUPENDEZA MOYO WANGU, ATAKAYEFANYA MAPENZI YANGU YOTE”.
Japo Daudi hakuwa mkamilifu kwa viwango kama vya watumishi wengine wa Mungu waliomtangulia au waliomfuata mfano wa Musa, Samweli, Eliya au Danieli, lakini biblia inamshuhudia kuwa ni mtu aliyeupendeza moyo wa Mungu.(Daudi Aliupendeza moyo wa Mungu sana)..
Je! Alimpendezaje Mungu?
Embu tuangalie mambo baadhi yaliyomfanya Daudi awe vile, naamini yanaweza kutusaidia na sisi katika safari yetu ya kutafuta kumpendeza Mungu.
Jambo la kwanza: ni,Daudi alimwamini Mungu kwa moyo wake wote: Hakujali ukubwa wa tatizo lilolokuwa mbele yake, kwa jinsi tatizo lilivyoonekana kuwa kubwa ndivyo alivyomfanya Mungu wake kuwa mkubwa Zaidi ya hilo tatizo na hiyo ilimfanya asiogope chochote..
Zaburi 27:1 ‘Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?’
Wakati alipokuwa anapambana na Goliathi hakuogopa ukubwa wake na vitisho vyake ijapokuwa alikuwa hana silaha yoyote mkononi mwake lakini Daudi hakuogopa badala yake alimwambia maneno haya
1Samweli 17: 45 “Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.
46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.
Nasi tujiulize, majaribu makubwa yanaposimama mbele yetu je ndio tunamkimbia Mungu au ndio tunamwamini Mungu, na kumuacha ili aonyeshe yeye uweza wake?. Kumbuka Daudi hakufanya hivyo sio tu kwa Goliathi bali katika matatizo mengi yote aliyowahi kukumbana nayo alisema pia nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti sitaogopa mabaya kwa maana Bwana yupo pamoja nami, Gongo lake na limbo yake vyanifariji.(Zaburi 23).
Zaburi 119:47 ‘Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda.
48 Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako’.
Soma tena..
Zaburi 119:140 ‘Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda”.
Ukisoma sehemu nyingi katika Zaburi utaona Daudi akionyesha Upendo wake katika Neno la Mungu, na hiyo ilimfanya awe analitafakari sana, sio kulisoma tu kama gazeti hapana, bali alikuwa analitafakari sana mchana na usiku..
Na sisi je! Tunao moyo kama huo wa kulipenda Neno la Mungu, tunapoambiwa uzinzi ni dhambi, tunafurahia kusikia hivyo?, tunapoambiwa vimini ni dhambi tunafurahia kusikia hivyo?, tunapoambiwa usengenyaji ni dhambi Je tunazingatia kujirekebisha je, tunapoambiwa ulevi na uvutaji wa sigara ni dhambi tunasikiliza? tunalitafakari hilo usiku na mchanga..Kama ndio hivyo basi tujue kuwa tupo katika njia ya kuelekea kumpendeza Mungu..Daudi anasema hivi:
Zaburi ZABURI 1:1 “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2 Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, NA SHERIA YAKE HUITAFAKARI MCHANA NA USIKU
3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.”.
Zaburi 119:140 ‘Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda’
Tatu: Daudi alikuwa ni mtu aliyekubali na kuyakiri makosa yake haraka sana, na kutubu. Alipozini na mke wa Uria, baada ya kuletewa habari hizo na nabii Nathani ukisoma 2 Samweli 12: 13 utaona hilo, saa ile ile Daudi alikiri kuwa kweli ametenda dhambi…Lakini sisi ni mara ngapi tunamficha Mungu dhambi zetu, hata kama uthibitisho wote unaonekana, tutajaribu kutengeneza mazingira na kusema ni kwasababu ya hiki au kile ndio maana nimetenda hivi au vile kama tu vile walivyofanya Adam na Hawa pale bustanini..
Ukisoma Zaburi 51, utaona jinsi Daudi alivyoungama dhambi zake zote..Vivyo hivyo na sisi Mungu atusaidie tuwe na moyo huo huo, wa kukiri makosa yetu na hivyo kutubu, kwa kumaanisha kabisa kuacha.
Nne: Daudi alikuwa ni mtu wa kuustaajibu uweza wa Mungu, na hivyo hakuona aibu kuutangaza uweza huo kwa kila mtu:
Zaburi 119: 46 ‘Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu’.
Daudi alikuwa yupo radhi kumtukuza Mungu hadi nguo zinamtoka bila kujali yeye ni mfalme, (Daudi alicheza mpaka nguo zikaanguka)alimtukuza Mungu dunia nzima ilijua kuwa yeye kweli ni mtumishi wa Yehova. Ukisoma Zaburi sehemu kubwa utaona Daudi anavyoibiri kazi ya Mungu na uweza wake na utukufu wake duniani kote..
Mtume Paulo aliandika katika Warumi 1:16 ‘Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia’.
Hivyo na sisi Tunapaswa kuitangaza injili kwa nguvu zetu zote Mungu alizotupa, ili na sisi tumpendeze Mungu.
Bwana atusaidie sote katika hayo. Naamini tutachukua hatua nyingine katika kuyarekebisha hayo machache, Mungu akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine.
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?
SWALI: Nini maana ya huu mstari?
1Wakorintho 13:8 “Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”…Nini maana ya ukiwapo unabii utabatilika?
JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu karama iliyo kuu kuliko zote ni upendo..(1Wakorintho 12:31)..Hii Ndio karama yenye nguvu kuliko karama nyingine zote (hakuna kitu chenye nguvu kuliko upendo)…Na karama hii ni tofauti na zile karama 9 ambazo mtu anakuwa na kipawa cha kipekee kutoka kwa Mungu, ambacho kinamtofautisha yeye na wengine katika kanisa…Karama ya Upendo ni karama ambayo Mungu anampa kila mtu pindi tu anapojiweka tayari kutaka kuwa na huo upendo.
Upendo unapokuwepo mahali hata unabii unakuwa hauna nguvu..Kwamfano Adamu na Hawa walipoasi tayari walikuwa wameshajitenga na uwepo wa Mungu milele, wao (pamoja na sisi wote maana wote tumetoka kwa Adamu)..kitendo tu cha kula lile tunda, basi mwanadamu alitoka katika nafasi ya kuwa mwana wa Mungu (kuishi milele) na kubakia kuwa tu kiumbe cha Mwenyezi Mungu tu!…. Muunganiko wa Mungu na mwanadamu ulikatikia pale Edeni kutokana na Adamu na Hawa kula lile tunda.
Lakini kutokana na Upendo Mungu aliotupendea alighairi mpango huo wa kumtenga mwanadamu milele na kumrudishia tena uzima wa Milele..
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.
Upendo umeutangua ule unabii wa sisi kutengwa na Mungu milele, ndio maana biblia inasema hapo juu “ukiwapo unabii utabatilika”..Upendo umebadilisha mawazo ya Mungu juu yetu moja moja…Tulikuwa tumetabiriwa kupotea milele, sasa kinyume chake kwasababu ya Upendo wake kwetu tumepokea Uzima wa Milele kupitia Yesu Kristo mwanawe.
Ndio maana Biblia inazidi kutuambia hata mambo yajayo (yaani Unabii) hayawezi kututenga sisi na upendo wa Mungu ulio katika Kristo, hata malaika, hata mbingu haziwezi kututenga sisi na Upendo wa Kristo kwetu..Tumependwa tumependwa! Hakuna kinachoweza kubadilisha hilo..
Warumi 8:33 “Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
35 NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?………. 38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”
Hivyo ni muhimu kulipata hili pendo la Kristo, ambalo linaweza kutangua hata unabii, upendo huo tukiupata tunaweza na sisi tukawapenda ndugu zetu hata kama wametufanyia mabaya kiasi gani, hata kama tulikuwa tumewatabiria kuwalipiza kisasi, upendo huo unayafuta hayo na kuwapenda ndugu pasipo masharti.
Vilevile unabii pia unatabia ya kuisha muda wake pale unapotimia, unao ukomo wake, lakini Upendo unaotoka kwa Mungu hauna mwisho, na sio Unabii tu peke yake wenye ukomo bali hata lugha, na maarifa yoyote ya kimbinguni au ya kiduniani vina ukomo haviwezi kuushinda upendo. Upendo una nguvu kuliko kitu kingine chote..Ndio maana amri iliyo kuu na kubwa kuliko zote ni UPENDO!
1Wakorintho 13: 1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika”.
Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?
Kuna aina tatu za Imani zilizoonekana katikati ya kundi lililokuwa likumfuata Yesu waponywe.
Kundi la Kwanza: Ni lile lililohakikisha kuwa linamwona Yesu uso kwa uso, na kuzungumza naye, na kumwomba Bwana Yesu awaponye au kama mgonjwa wao hayupo hapo basi litahakikisha Bwana Yesu anaambata nao hadi makwao ili waombewe, Kundi hili linatabia ya kumwachia Yesu afanye shughuli zote.
Kundi hili ndio lililokuwa kubwa kushinda yote, na hata leo lipo na ni kubwa pia, hawa ndio wale watu ambao ni ili waponywe au wafanyiwe haja zao ni lazima wawatafute watumishi wa Mungu mahali popote walipo kwa gharama zozote zile, wapo radhi kwenda mpaka Nigeria, china bila kujali gharama za fedha wanazoingia ilimradi tu waonane na watumishi wa Mungu wawaombee.
Ni lile ambalo, lilipata ufunuo wa Zaidi wa kutambua uweza wa Yesu, Hivyo halikuhitaji mpaka Yesu afike nyumbani kwao ndipo waponywe. Mfano wa hili ni yule Akida aliyemfuata Yesu..
Tusome..
Mathayo 8:5 “Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,
6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.
7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.
8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona.
9 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli”.
Unaona mtu huyu alitafakari kwa ukaribu sana akaangalia na kazi yake anayoifanya kila siku ya Uakida akasema moyoni mwake kama mimi nikitoa tu amri kwamba kitu fulani kifanyike , huwa kinatendeka haraka sana hata kama mimi sipo huko..Sasa si Zaidi huyu ambaye ni Masihi mwenyewe, mkuu wa ufalme wa mbinguni, anao uwezo pia wa kunitamkia tu uponyaji mahali nilipo na malaika zake wakalishughulika na hilo mara moja na mambo yote yakawa sawa..
Hivyo kwa ufunuo huo huo akamwambia Bwana huna haja ya wewe kuja nyumbani kwangu, ya nini kujichosha, wakati unalo jeshi la malaika chini yako?..SEMA NENO TU! Na mtumishi wangu atakuwa mzima..
Bwana alistaajabia sana, kwasababu kundi la watu wenye hiyo haikuiona kabisa, anasema hata katika Israeli nzima, ikiashiria kuwa watu wenye Imani ya namna hiyo iliyojaa ufunuo wa kumchukulia Yesu kama ni Zaidi ya wanavyomfikiria walikuwa nao wachache.
Watu wa namna hii pia leo wapo isipokuwa ni wachache sana, watu wenye Imani na YESU aliye ndani ya mioyo yao, watu ambao hawategemei watumishi wa Mungu kuwaombea, watu ambao hawahangaiki huku na kule kutafuta maombezi, Ni kwasababu wamepata ufunuo wa uweza wa nguvu za YESU, Mungu anapendezwa nao sana, hawa wakiwa na haja wanapiga magoti wenyewe wanamwomba YESU aliye ndani yao..Na mwisho wa siku wanapokea miujiza yao..Na kundi hili huwa ni rahisi Zaidi kupokea kuliko lile la kwanza.
Ni kundi ambalo halikuhitaji ruhusu yoyote ya YESU ili kupokea kitu kutoka kwake ..Halikuhitaji kumwita Yesu aje manyumbani kwao, wala halikuhitaji YESU awatamkie Neno lolote wala halikumuhitaji Yesu afahamu jambo lolote,..Lilifanya kimya kimya lakini matokeo yake yalikuwa ni makubwa na ya papo kwa papo..Mfano wa kundi hili tunaona ni yule mwanamke aliyetokwa na damu miaka 12, tusome:
Luka 8:43 “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,
44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.
45 Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.
46 Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.
47 Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.
48 Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani”.
Hapa ndipo Bwana Yesu anapotaka kila mmoja wetu afikie, mahali ambapo Yesu anakutafuta wewe, na sio wewe unamtafuta Yesu..kwamba tuwe na mamlaka kamili ya kuweza kutumia nguvu zake bila kipimo chochote. Na hatua hii ikikomaa vizuri ndani ya mtu ndio ile inakuja kuitwa IMANI TIMILIFU, (Wakorintho 13:2) ambayo mtu akiwa nayo anakuwa na uwezo wa kikiambia kitu hichi kwa jina la YESU ondoka nenda kule, nacho kikatii, Anao uwezo wa kuamrisha milima na kufanya jambo lolote kwa jinsi atakavyo yeye, hapo si kwamba anaomba kwa Mungu hapana, bali anafanya kwa amri yake mwenyewe kwa jina la Yesu nacho kinatokea..
Na njia pekee ya kufikia huko ni kuwa na maarifa ya kutosha, ya YESU KRISTO, tunahitaji kumjua sana Yesu KRISTO kwa mapana na marefu, kiasi kwamba ile Imani ya kufanya chochote kwa jina lake ijengeke yenyewe ndani yetu.
Bwana atujalie tufike huko, katika tumtafakari sana Bwana YESU, Mfalme wa Wafalme, kama ipasavyo ambaye biblia inatuambia “ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika”(Wakolosai 2:3).
Bwana akubariki sana, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Jina la Mfalme Mkuu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze maneno yake ambayo ni mwanga wa njia zetu, na taa iongozayo miguu yetu (Zab. 119:105)
Leo tutajifunza kwa ufupi, umuhimu wa kutubu dhambi kabla ya kumaliza haya maisha, yapo mafundisho mengi yanayohubiri kuwepo kwa nafasi ya pili ya kusamehewa moto wa milele baada ya kufa…Miongoni mwa mafundisho hayo ni mafundisho ya kupitia Toharani. Lengo kuu la mafundisho haya ni kuwapa watu wanaoishi katika dhambi matumaini kwamba hata wakifa katika dhambi zao bado watakuwa na nafasi ya kutolewa kwenye mateso hayo ya milele na kuingia paradiso, na maombi ya watakatifu waliopo duniani yanaweza kupunguza mateso ya kule.
Haya ni moja ya mafundisho ya shetani yaliyobuniwa kuzimu kwa ujuzi wa hali ya juu yanayowapa watu matumaini na faraja za uongo…shetani anajua watu wanapenda faraja….Alijua Hawa anapenda faraja ndio maana uongo wa kwanza alioutumia ni uongo wa faraja…alimwambia Hawa kwamba “hakika hamtakufa” wakati Bwana alishawaambia wakila tu “watakufa”
Hivyo shetani ni Yule Yule aliyoyatumia Edeni kuwaangusha watu wa kwanza kuumbwa (Adamu na Hawa) ndio hayo hayo anayoyatumia kuwaangusha watu siku za mwisho (yaani mimi na wewe) hivyo tusipokuwa makini kidogo tu! Ni rahisi kwenda na maji!
Mahubiri ya Toharani yatawafanya watu wengi sana wajute siku ile, watakapokwenda huko na kugundua kuwa hakuna kitu kama hicho cha kupata nafasi ya pili. Walidanganywa!
Hebu chukua muda kutafakari kwa Makini sana mstari ufuatao ambao Bwana Yesu aliusema kisha useme mwenyewe kama kweli kutakuwa na nafasi ya pili..
Yohana 8:24 “Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu”.
Itafakari hiyo sentensi kwa makini, usiisome tu juu juu kwa mazoea, kwamba ulishawahi kuusoma huo mstari na hivyo huwezi kuurudia tena, hebu ingia ndani zaidi kuutafakari!…Bwana Yesu anasema msiposadiki kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu…Ikiwa na maana kuwa kuna tatizo “katika kufa ukiwa na dhambi”…Hiyo ndiyo maana yake!…Na madhara hayo ni baada ya kifo! Kwamba mtu akifa mifupa itakwenda kuchimbiwa kaburini, nguo zitachimbiwa, ardhini nyama ya mwili wake itachimbiwa na kuoza lakini dhambi zake alizonazo atavuka nazo upande wa pili…Na hivyo hiyo dhambi inapaswa ichujwe kabla ya kifo, iachwe hapa hapa duniani..kwasababu ukivuka nayo kule hakuna nafasi tena ya kuitua.
Ingekuwa hakuna tatizo katika kufa ukiwa na dhambi na kwamba kuna nafasi nyingine ya kuokoka ukiwa kule…Bwana Yesu asingesema hivyo…jiulize sana kwanini ahusishe “kifo” na “dhambi” maana yake ukishakufa na dhambi ndio basi tena…ndio maana alikuwa anakazana kuwaambia watubu kabla ya kufa! Kwasababu hakuna tena toba, wala injili baada ya kifo..kinachofuata baada ya hapo ni hukumu..
Ndugu Kama ulikuwa unaamini hivyo kwamba kuna nafasi ya pili ya kuokoka baada ya kifo, ambayo mafundisho haya yanafundishwa sana katika kanisa Katoliki au pengine ulisikia kwa mchungaji wako au kiongozi wako wa dini..fahamu kuwa ulidanganywa! Kama tu Hawa alivyodanganywa kwamba hatakufa!…Umesoma mwenyewe maneno ya Bwana Yesu hapo juu, jinsi alivyokuwa anakazana kuwafanya watu wamwamini kabla ya kufa… na wewe kama hutatubu leo na kumwamini Bwana Yesu utakufa katika dhambi zako..Na baada ya kifo ni hukumu!, kama ni mlevi, mwasherati, mtukanaji, mfanyaji masturbation, mtazamaji wa picha za uchafu, mlawiti, msagaji, msengenyaji, mtoaji mimba, mvaaji mavazi ya kikahaba n.k ukifa leo bila kutubu…utakwenda jehanamu! Hakuna nafasi ya pili…
Bwana anatuonya hapo juu! Kwamba tusipomwamini tutakufa katika dhambi zetu! Je! Na wewe unataka kufa katika dhambi zako? Kama sio basi ni vema ukakata shauri leo la kumgeukia Bwana Yesu, akusafishe dhambi zako na akuoshe kabisa…unachotakiwa kufanya ni kutii msukumo uliopo ndani yako unaokusukuma kuacha dhambi na kumgeukia mwokozi, ujumbe huu unaweza ukawa ni wa kwako kukubadilisha ..
Hivyo unautii huo wito kwa kuamua kwa dhati kwamba kuanzia leo mimi na dhambi basiii, disko ndio mwisho leo, kuchat chat ovyo katika mitandao kwenye vitu visivyo na maana ndio mwisho, kutukana ndio mwisho, kusikiliza miziki ya kidunia ndio mwisho, na unaifuta yote sasahivi bila kuacha wimbo hata mmoja, na unakata kila mnyororo, unasema mimi na uasherati basi, na wale wanawake au wanaume unaotembea nao sasa inatosha, unawapigia simu na kuwaeleza maamuzi yako, na unawaacha kabisa…na unachukua msalaba wako unamfuata Yesu wewe kama wewe..
Baada ya hapo ile nguvu ya Roho itakuvaa itakayokuwezesha kutokutamani hayo mambo tena…utakuwa hujilazimishi kujizua kutukana, au kuiba, au kuzini, n.k itakuwa ni kitu kinachotoka ndani chenyewe (kama vile usivyotumia nguvu yoyote kusukuma damu kwenye moyo wako)…na utaona amani Fulani ya ajabu imekuingia Ukiona hali kama hiyo imekuja ndani yako fahamu kuwa ni Roho Mtakatifu huyo..Lakini ukikaidi sauti yake na kuendelea na ulimwengu huu wa kitambo utakufa katika dhambi zako na hakutakuwa na nafasi ya pili tena huko uendako. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Bwana akubariki sana, Tafadhali share na wengine
Mada Nyinginezo:
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
SWALI: BWANA YESU ASIFIWE SANA ndugu zangu..naswali naomba kujua BWANA alikuwa anamaana gani kusema haya maneno…Mathayo 5:13 ‘Ninyi ni chumvi ya dunia;lakini chumvi IKIWA IMEHARIBIKA ITATIWA NINI HATA IKOLEE?….’
JIBU: Bwana Yesu alitumia mfano wa chumvi kuonyesha jinsi watakatifu wanavyopaswa wawe waangalifu hapa duniani..Chumvi ni kama sukari, hata siku moja hujawahi kuweka sukari kwenye chai na ukakutana na kipande cha jiwe ndani yake, tofauti na vitu vingine kama vile mchele, au maharage ambavyo utakutana navyo sana, vivyo hivyo na chumvi nayo inapotengezwa, huwa inatengenezwa kwa umakini wa hali ya juu sana, kuhakikisha kuwa hakuna uchafu wowote unajipenyeza ndani ya chumvi ile..
Kwasababu wanafahamu chumvi ni tofauti na nafaka, ikiingia uchafu kidogo tu, basi haifai tena ni ya kutupa, ni kitu ambacho kisichoweza kuchambulika kama vile mchele, huwezi ukatoa punje moja moja ya chumvi uitenganishe na uchafu, hiyo haiwezekani, ikiingia uchafu kidogo tu, basi hiyo haifai tena, hata kamaa ukijaribu kuiweka katika mboga haiwezi kukolea kwa namna yoyote ile.
Vivyo hivyo na sisi tuliookoka, Bwana anasema ni chumvi, hatupaswi kutiwa unajisi na kitu chochote kichafu, kwasababu ulimwengu unatuangalia sisi kama viungo vya kipekee sana, na ndio maana hata leo ukisikia watu wawili wamefumaniwa katika uzinzi na mmojawapo ni mchungaji, utaona watu wote wanaacha kumfuatilia yule mwingine, na kuanza kufuatilia habari za yule mchungaji,..
ni kwasababu yeye alikuwa ni chumvi, lakini sasa ameshatiwa doa, unadhani mtu kama huyo hata kama akitubu kwa dhati kabisa, na Mungu kweli akamsamehe, Unadhani ile jamii inayomzunguza bado itamwelewa?, haiwezekani tena, utumishi wake ndio tayari umeshaharibika hivyo..
Na ndio maana Bwana anasema “chumvi ikiwa imeharibikaitatiwa nini hata ikolee?”, Wewe unasema umeokoka halafu bado unaonekana unatukana ovyo, utumishi wako utaaminikaje mbele za watu?, Unakwenda Disco, au muda wote wewe ni kusengenya watu, unadhani wale watu wanaokuzunguka watakuaminije hata kama utawapelekea habari za Mungu..
Waefeso 5:25 “……….kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa”.
Hivyo hapo Bwana alikuwa anatuonya tuwe waangalifu, sisi ni chumvi, tuliotakaswa siku ile tulipookoka tusio na hila wala waa wala, kunyanzi lolote, na sio mchele ambao hata ukiingia uchafu unaweza kuchambulika.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?
https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/je-ni-vema-kwa-mkristo-kwenda-hospitali-au-kutumia-miti-shamba-anapougua/
FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?
Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?