Title 2019

Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango?

JIBU: Biblia haijaeleza moja kwa moja kuhusu suala la uzazi wa mpango aidha utumike au la, kwasababu njia zinazotumika sasa hazikuwepo katikati ya watu wa kale, Lakini ni vizuri kufahamu lengo la kufanya hivyo ni nini, wapo wengine wanafanya hivyo kwasababu ya matatizo ya kiuchumi, wengine kwasababu ya mapungufu ya kimwili, wengine kwasababu ya kuzuia kuathiriwa kwa kazi yake Fulani, na pia wapo wengine ni kwasababu tu za kiasherati/zinaa n.k..

  Hivyo njia nyingi za sasa zitumiwazo kwa uzazi wa mpango zinachukuliwa kwa taswira ya kiasherati kwasababu iko wazi nyingi zinatumiwa hivyo. Lakini ikiwa ni kwa wana ndoa, na dhamira zao zikiwa ni safi mbele za Mungu, na malazi yao ni masafi siku zote, na wanazo sababu za muhimu zinazowalazimu kufanya hivyo labda kwasababu za uleaji wa watoto n.k. Si dhambi wanaweza kutumia. Kwasababu kumbuka pia maandiko yanasema Katika

1Timotheo 5: 8 “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini”.

  Unaona hapo? Uzaaji wa watoto usio na mpango, hususani pale usipokuwa na uwezo wa kuwalea, ni sawa na umeikana Imani. Hivyo ni vizuri kama wewe ni mwanandoa, ukae chini katika maombi na kumuuliza Mungu, na mapatano na mwenzako, na kisha zitumike.

Lakini mambo hayo hayamuhusu mtu asiye mwana-ndoa.

Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOANA?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

WATU WASIOJIZUIA.

MWANZI ULIOPONDEKA.


Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Kunena kwa lugha kukoje?

KUNENA KWA LUGHA. 

Kuna aina nyingi za lugha, zipo lugha za wanadamu na lugha za malaika, lugha za wanadamu ndio kama hizi tunazozifahamu na kuzizungumza; Kiswahili, kingereza, kiarabu, kizulu n.k..Na lugha za malaika nazo zipo nyingi, hatuwezi tukazielewa kwa upeo wetu wa kibinadamu.

 1Wakoritho 13: 1 “Nijaposema kwa LUGHA ZA WANADAMU na ZA MALAIKA, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao”.

 Sasa moja ya ishara kubwa kati ya nyingi ambayo Bwana aliichagua siku ile ya Pentekoste ijidhihirishe kama ushahidi kuwa Roho Mtakatifu amemwagwa juu ya watu wake ni ISHARA YA LUGHA. Kumbuka: angependa kutumia ishara nyingine pia angeweza, kama watu kutabiri, watu kung’aa nyuso zao kama Musa, n.k lakini yeye alipenda kutumia ishara ya lugha, kama tu alivyotumia ishara ya lugha kuwatapanya watu waliokuwa wanaujenga mnara wa Babeli. Sasa kilichotokea siku ile ya Pentekoste baada ya Roho Mtakatifu kushuka juu ya watu, watu kujikuta wanapata msukumo wa ajabu(au uwezo wa ajabu) kuzungumza lugha wasizozijua.

Na lugha hizo hazikuwa lugha za MALAIKA hapana! Bali zilikuwa ni lugha za WANADAMU. Ili tuelewe vizuri tujifunze kwa mfano ufuatao. Petro mwanafunzi wa Yesu alikuwa anaongea ki-galilaya lakini hawezi kuongea kiyunani, Roho aliposhuka juu yake siku ile ya Pentekoste, alisikia uwezo na msukumo wa ajabu ndani yake, na kujikuta anamtukuza Mungu kwa lugha nyingine pasipo kujua ile lugha anayoizungumza ni ya kiyunani. Na kadhalika Mathayo naye lugha yake ya asili ni ki-galilaya lakini nguvu ilipomjia akajikuta anamtukuza Mungu kwa lugha ya kiarabu, pasipo kujua kwamba anaongea kiarabu..na vivyo hivyo kwa wanafunzi wengine wote na wale wote waliokuwepo siku ile ya Pentekoste. 

Sasa wao pasipo kujua kwamba zile lugha wanazoziongea ni lugha halisi, wale watu wa nje ndio waliowasikia wanazungumza kwa lugha zao, labda tuseme kuliwepo na wayunani pale ghafla wanamsikia mtu akimtukuza Mungu huko ghorofani kwa lugha ya kiyunani, na hali anajua kabisa pale mjini wayunani wenzake ni wa kubahatisha, na Kadhalika kama palikuwepo na muarabu kafika pale mjini Yerusalemu kwa biashara yake, ghafla anamsikia mtu huko ghorofani anapaza sauti akimshukuru Mungu kwa lugha yake ya kiarabu, tena kiarabu kile cha ndani kabisa na hali anajua kabisa katika huo mji hakuna waarabu wenzake wengi, na cha ajabu akimtazama mtu anayenena hana hata dalili ya kufahamu tamaduni za kiarabu,ni wazi kabisa ataishia kuduwaa tu!. Sasa ndicho kilichotokea siku ya Pentekoste.

Ni mfano leo usafiri na kwenda Kijiji kimoja huko China, na wakati umefika huko, unamsikia mchina mmoja huko anaongea kichaga kile cha ndani kabisa, wakati unajiuliza hilo ni nini, unasikia mchina mwingine huko anamsifu Mungu kwa kimakonde! Bila shaka utashangaa na kujiuliza hawa wote si ni wachina! Imekuwaje basi mimi kuwasikia wakizungumza kwa lugha zetu za asili za kiafrika?. Sasa hiyo ishara ya lugha Bwana Yesu aliiachia siku ile ya Pentekoste ili watu wote wajue kwamba kuna kitu kipya kimemwagwa duniani (nacho si kingine Zaidi ya Roho Mtakatifu). Lakini Roho Mtakatifu mwenyewe sio lugha, kama tulivyosema hiyo ni ishara Roho Mtakatifu aliyoichagua tu kujidhihirisha yeye, anaweza akatumia ishara nyingine tofauti na hiyo, mtu akishindwa kuelewa hilo, atadhani kuwa asiponena kwa lugha basi hana Roho Mtakatifu ndani yake, Na ndio hapo inapelekea kulazimisha kufanya hivyo na asiponena mwisho wake anaishia kunena kwa akili zake tu, na sio kwa jinsi Roho anavyowajalia.

Kunena kwa lugha ni karama Roho wa Mungu anayoitoa kama yeye apendavyo na sio kila mtu anaweza kuwa nayo. Sasa nini kinatokea Roho Mtakatifu anapoingia ndani ya Mtu?Roho Mtakatifu anapoingia ndani ya mtu, hali atakayoisikia mtu yule kwa mara ya kwanza sio kunena kwa lugha, kwasababu lugha kazi yake ni ishara kwa watu wa nje wasioamini, kuwaonyesha kwamba kuna jambo jipya limeshuka juu ya huyo mtu, lakini kama Roho ameshuka juu ya mtu na yule mtu yupo peke yake, hakuna lugha hapo!.

 Jambo la kwanza atakalolisikia yule mtu ndani yake baada ya Roho Mtakatifu kushuka ni badiliko kubwa ndani ya moyo wake, atajisikia anaichukia dhambi, na maisha yake ya zamani, atajikuta anatamani na anakuwa na kiu ya KUWA MTAKATIFU, na huo ndio uthibitisho wa kwanza na sio kutamani kunena kwa lugha, au kuona maono, au kutabiri.Uthibitisho wa ROHO YA UASHERATI ndani ya mtu ni UASHERATI sio kuzungumza kingereza, vivyo hivyo uthibitisho wa ROHO YA MAUAJI ndani ya mtu ni MAUAJI anayoyafanya na sio elimu yake, huwezi kusema elimu ya mtu ndio uthibitisho wa Roho ya mauaji iliyopo ndani ya huyo mtu, Vivyo hivyo na ROHO MTAKATIFU kama jina lake lilivyo “MTAKATIFU” uthibitisho kwamba mtu yule anaye Roho Mtakatifu ndani yake ni UTAKATIFU ANAOUISHI, na sio lugha anazoziongea, Kwahiyo hizi lugha, ni ISHARA TU na Bwana anachagua nani wa kumpa hii na nani wa kumpa ile.

Hivyo jambo la kwanza mtu akipokea Roho Mtakatifu ni kuanza kuona ile kiu ya kupenda dhambi inakufa, anaanza kupenda kuwa MTAKATIFU na kuishi maisha ya kumcha Mungu, Sasa vya ziada ndio hizo ishara nyingine zinafuatana naye, labda anaona MAONO, lakini haneni kwa lugha, sasa mtu kama huyo anaweza akadhani hajapokea Roho Mtakatifu kwasababu tu hajanena kwa lugha, hajui kwamba Roho Mtakatifu yupo ndani yake, na amemchagulia ishara ya Maono iambatane naye badala ya ishara ya lugha.

Mwingine katubu dhambi na ghafla anaona kiu ya kupenda dhambi inakufa anatamani na anaanza kuishi maisha ya UTAKATIFU, lakini anajigundua kila anapolala anaota ndoto na zile ndoto zinakuja kutokea kama zilivyo, lakini hajanena kwa lugha, naye huyo Roho kapenda kumpa kipawa cha NDOTO badala ya lugha, Vivyo hivyo na wengine watapewa, karama za uponyaji badala ya LUGHA, wengine watapewa karama za unabii badala ya lugha, wengine watapewa karama neno la faraja, wengine karama za neno la maarifa, wengine watapewa uinjilisti badala ya lugha, wengine watapewa lugha badala ya uinjilisti, na maono, wengine waalimu, wengine wachungaji, N.k na wengine watapewa karama mbili mbili, wengine tatu tatu, wengine moja tu n.k Lakini wote hawatenena kwa lugha wala wote hawatakuwa manabii n.k na ndio maana Mtume Paulo ililisema hilo katika.. 

1Wakoritho 12: 28 “ Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? WOTE WANENA KWA LUGHA? Wote wafasiri?”

Umeona hapo? Sio wote watanena kwa lugha. Hivyo usikazane kutafuta kunena kwa lugha, kama hiyo karama haipo ndani yako,[sisemi kama ukimwomba Mungu hatakupa,] lakini ikiwa haipo ndani yako zidi kujaa Roho Mtakatifu, na baki katika nafasi uliyoitiwa. 

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Print this post

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

JIBU: Kama tukisoma Marko 2: 17 tunaweza kuona Bwana Yesu aliwaambia watoza ushuru na Mafarisayo maneno haya, “…WENYE AFYA HAWAHITAJI TABIBU, BALI WALIO HAWAWEZI; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.” Bwana alitumia mfano huo wa kidunia kueleza mambo ya rohoni, akimaanisha kuwa ni jambo la kawaida kwa mtu aliye mgonjwa kumtafuta daktari amuhudumie afya yake. Kwasasa tunaweza kusema kwenda hospitali. Hivyo mkristo kuumwa na kwenda hospitali hafanyi kosa lolote, maadamu anafanya tendo ambalo halimwathiri Imani yake.  

Kadhalika pia anaweza kutumia aina zozote za mimea ambazo anaweza kuona zitamsaidia kuimarisha afya ya mwili wake, mwingine anaona kutumia mwarobaini, au alovera ni nafuu zaidi kwake kuliko dawa za hospitalini kwasababu pia dawa nyingi za hospitalini zinatengenezwa kutoka kwenye hiyohiyo mimea ya asili. Lakini la kuzingatia mkristo anapotumia dawa hizo, hapaswi kuzihusisha na ibada zozote za Kiroho isipokuwa kwa Mungu wake.  

Kwamfano mtu anapewa dawa za miti shamba labda mwarobaini, halafu anaambiwa achinje kuku, au aweke uvunguni, au aseme maneno Fulani au afanye kafara kisha ndio anywe, sasa hizo tayari ni ibada za sanamu ambazo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini mtu akiwa na mwarobaini wake nyumbani, akatengeneza akanywa kwa jina la YESU hakuna tatizo lolote. Akizingatia tu lile Neno katika

Wakolosai 3: 17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO au KWA TENDO, fanyeni yote KATIKA JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Lakini pia kuna mwingine kwa Imani yake anaamini kuwa Mungu ndiye mponyaji wake kwa asilimia zote pasipo kupitia nyenzo yeyote, hivyo anaposikia kuumwa anaamini kuwa Mungu atamponya pasipo kwenda hospitali, akiliamini lile Neno (Mathayo 8:17 “…Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.” )

hivyo mtu wa namna hii pia hafanyi kosa, Kwasababu Mungu ni yule yule anayeweza kumponya mtu kwa kupitia daktari au pasipo daktari..Hapo ni kulingana na Imani ya mtu kwa Mungu wake.  

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

YESU MPONYAJI.

HADITHI ZA KIZEE.

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

MKUU WA GIZA.

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni sahihi kulima mazao, ambayo hutumiwa kutengenezea pombe?

SWALI: Kwamfano tunajua kuna pombe zinazotengenezwa na mtama Je! ni sawa kwa mkristo wa kweli kulima mtama na kuuza na hata hiyo hela kuitumia kutolea sadaka?


JIBU: Hakuna zao lolote lililoumbwa na Mungu lenye ubaya wowote ndani yake, zao linafanyika kuwa baya pale tu linapotumiwa kwa matumizi yasiyo sahihi, kwamfano mtama ni zao la chakula, wengine wanatumia kama ugali, lakini baadhi ya watu wanatumia fursa ya zao hilo ili kuunda pombe. Hivyo mtu anayeligeuza zao kuwa hivyo , au kupanda kwa ajili hiyo, atakuwa na hatia mbele za Mungu.

Lakini zao lenyewe kama zao halina shida kama mtu akilipanda kwa ajili ya matumizi ya asili, kwasababu yapo mazao mengine mengi tu kwamfano zao kama miwa, ambayo ingetumiwa kutengenezea sukari wengine wanaundia pombe, minazi ambayo ingetumika kuzalisha nazi na mafuta wengine wanaigema kutolea pombe, ulezi na ndizi ambazo zingetumika kama chakula wengine wanatumia kutengeneza pombe n.k. Lakini biblia ilishasema katika, 

Isaya 5:20 Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu; watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza; WATIAO UCHUNGU BADALA YA UTAMU, NA UTAMU BADALA YA UCHUNGU!.

Unaona hapo? Biblia imetoa onyo kali kwa wale wote wanaopenda kupundia, vitu ambavyo Mungu aliviumba vitumike ipasavyo katika uhalisia wake, Kuzalisha mtama kwa ajili ya kutengenezea pombe ni sawa na kutia uchungu katikati ya jamii badala ya utamu. Kuzalisha ulezi na ndizi kwa dhumuni la kuviuzia viwanda vya utengenezaji pombe, ni sawa na kutia uchungu katikati ya jamii badala ya utamu. Kadhalika na mambo mengine yote ambayo yangepaswa yatumike kwa matumizi ya asili lakini watu wanayageuza, kwamfano wanaume kwa wanaume, na wanawake kwa wanawake ni sawa na kutia nuru badala ya giza..Bwana alishasema OLE WAO wafanyao hivyo. 

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JE! TUNARUHUSIWA KUNYWA MVINYO KIDOGO KWA AJILI YA TUMBO KAMA PAULO ALIVYOMWAMBIA TIMOTHEO?

MATUMIZI YA DIVAI.

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

JE! MABALASI BWANA YESU ALIYOYATUMIA KUGEUZIA MAJI KUWA DIVAI, YALITUMIKA KWA KAZI HIYO TU?

JE! MTU ANAPOFUNGA KWA MUDA WA SAA 24,ANAPASWA KUNYWA MAJI AU KITU CHOCHOTE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?

SWALI: Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini katika hivi vifungu?

Luka14:26 “kama mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake,na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; na naam, na hata nafsi yake mwenyewe , hawezi kuwa mwanafunzi wangu ”.


JIBU: Bwana Yesu aliposema yeye “asiyemchukia” baba yake na mama yake, hakumaanisha, kumdharau, au kuweka uadui naye, hapana kwasababu Bwana Yesu hawezi kufundisha upande mmoja upendo na mwingine chuki, bali pale alimanisha kupenda mapenzi ya wazazi au ya mtu binafsi Zaidi ya mapenzi ya Mungu, mtu wa namna hiyo hawezi kuwa mwanafunzi wake.

Leo hii mtu atafahamu kabisa kuwa mlevi au kufanya matambiko ya kimila ni dhambi sawa sawa na Neno lake katika

Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.

lakini kwasababu mzazi wake anamshurutisha afanye vile kwasababu wazee wa ukoo wameagiza ,na asipofanywa hivyo atatengwa na ukoo, yeye anaamua awe mlevi, au apige ramli ili tu kuwaridhisha wazazi wake. Mtu wa namna hiyo biblia inasema hawezi kuwa mwanafunzi wa YESU.

Kadhalika Bwana anasema mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho hawezi kuuona ufalme wa mbinguni, lakini mtu kwasababu dini ya wazazi wake haiamini hivyo, anaona vema abaki hivyo hivyo tu, angali akijua kabisa ubatizo sahihi ule wa kuzamishwa katika maji tele tena katika Jina la YESU KRISTO ndio Bwana anaouhitaji kwa mtu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zake, lakini yeye hataki kutii akiwaogopa wazazi au ndugu zake..Sasa mtu kama huyu hawezi kuwa mwanafunzi wa YESU.

Na maagizo mengine yote Bwana aliyotupa, hatupaswi tutazame kwanza wanadamu wanatoa maoni gani kuhusu hayo.Kama ni Bwana kasema moja kwa moja tunatii pasipo kuwatazama wanadamu wanasema nini.

Ili kufanyika wanafunzi kweli kweli wa Kristo hatuna budi kuingia gharama, Hivyo Bwana atupe rehema tuweze kuzishinda hatua zote.

Amen.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada zinazoendana:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

UBATILI.

WANA WA MAJOKA.

RACA


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

SWALI: Tumeambiwa sisi (Watakatifu) tutahukumu, Je! baada ya kuhukumu tutaweza kuwaamurisha malaika wawachukue wale tuliowahukumu na kuwatupa kwenye ziwa la moto?


JIBU: Ubarikiwe kwa swali zuri, lakini kuna jambo la kujifunza zaidi hapo, siku ile tutakapoketi na Bwana kuhukumu, sisi ndio tutafanana na yeye lakini hukumu ya mwisho atatoa yeye peke yake YESU KRISTO. Sisi tutakuwa kama mawakili. Kwa mfano siku ile atasimamishwa mtu aliyekuwa anafanya uasherati, na huku anasema ameokoka, na Bwana atamwuliza kwanini ulikuwa unafanya vile, labda atasema kwasababu kizazi chetu kilikuwa na simu zenye internet hivyo ilikuwa ni ngumu kujizuia, sasa utaitwa wewe Michael ambaye saa hiyo utakuwa pembezoni mwa Bwana, na Bwana atakuuliza ilikuwaje wewe uliushinda uasherati katika kizazi cha internet, utatoa sababu pale, sasa zile sababu zako utakazozitoa wewe mtakatifu ndizo zitakazo muhukumu yule mkosaji Unakumbuka yale maneno Bwana Yesu aliyoyasema katika..

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.

42 Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani”.

Kwa namna hiyo ya malkia wa sheba atakavyokihukumu kizazi kile, ndivyo na sisi tutakavyokihukumu kizazi hichi.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JE NI KWELI TUTAWAHUKUMU MALAIKA? SAWASAWA NA 1WAKORINTHO 6:2

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

JE! BAADA YA ULIMWENGU HUU KUISHA MALAIKA WATAKUWA NA KAZI GANI TENA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

SWALI: Yesu alikuwa na maana gani alipomwambia yule Mama kwamba chakula cha watoto hawapewi mbwa?

JIBU: Tusome,

Mathayo 15: 21 “Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.
22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Kumbuka Bwana Yesu alipokuja duniani, hakutumwa kwanza kwa watu wa mataifa, hapana kwasababu wao hawakuwa wanamtazamia mwokozi yeyote, kadhalika watu wa mataifa walikuwa ni watu wasiokuwa ni dini, wapagani, wasiomjua Mungu, walikuwa wanaabudu miungu,na ndio maana Bwana akawafananisha na mbwa katika mfano huo…

Lakini wayahudi ni watu wa Mungu tangu zamani uzao wa Ibrahimu, pamoja na hayo kwa miaka mingi walikuwa wanalitazamia taraja la wokovu wao ambalo lingeletwa tu na MASIHI mwenyewe atakayeshuka kutoka mbinguni, Hivyo kwa kuwa wale ni uzao wa Mungu, uzao wa Ibrahimu, sasa ulipofika wakati wa Mungu kuwatimizia haja yao waliyokuwa wanaisubiria kwa muda mrefu, ndio akamleta Bwana Yesu duniani aje kuwakomboa..

Na ndio maana sasa tunamwona Bwana Yesu alipokuwa duniani, hakuhubiri katika nchi yoyote ya mataifa, kadhalika hakuwatuma hata wanafunzi wake katika mji au kijiji chochote cha mataifa, kwasababu hakutumwa kwao, bali kwa wale waliomtazamia (yaani wayahudi).

Lakini hapa tunamwona huyu mwanamke ambaye ni mtu wa Tiro, (mwanamke aliyekuwa wa kimataifa), asiyekuwa na dini wala Imani katika Mungu wa kweli, alipomwona Bwana akipita kando kando ya miji yao, akamfuata ili ahudumiwe naye, lakini Bwana hakuonyesha kumjali kwa namna yoyote ile, lakini kwa vile alivyokuwa akimsumbua sumbua, ndipo Bwana akamwambia sikutumwa [kwa watu wa mataifa] ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli (yaani wayahudi)..lakini alipozidi kumsumbua sumbua, aliongezea na kumwambia “si vema kutwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa”..yaani akiwa na maana kuwa si vizuri kuiondoa ile neema ya wokovu kwa wale waliostahili kuipokea(yaani wayahudi) na kuwapatia watu ambao hawakustahili kuipokea au kuitazamia(watu wa mataifa).

Lakini pamoja na hayo tunakuja kuona baadaye, ile neema ililetwa kwetu sisi mataifa, baada ya wale ambao waliostahili kuipokea kuikataa, hivyo sisi sasa sio mbwa tena bali tumefanywa kuwa wana wa Mungu kwa damu ya Yesu Kristo.

Hiyo ndio siri iliyokuwa imefichwa tangu zamani kwamba sisi watu wa mataifa tumehesabiwa kuwa warithi wa wokovu sawa na wayahudi kwa njia ya Yesu Kristo. Haleluya. Hivyo ndio maana Mtume Paulo akasema katika..

Waefeso 3: 4 “Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo.
5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;
6 ya kwamba MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;”

Hivyo somo la kujifunza, hapo ni lipi?. Tumwendeapo Mungu, kwa haja ihusuyo wokovu wetu, hata kama ni kweli tutakuwa hatustahili mbele za Mungu, pengine njia zetu zimekuwa mbaya sana, na tumeomba mara ya kwanza, na ya pili na ya tatu hatujajibiwa…Hatupaswi kukataa tamaa, tuzidi kuomba tuzidi kuomba kama yule mwanamke..Kwasababu Bwana Yesu alishatupa mfano unaofanana na huo, juu ya yule kadhi dhalimu, aliyekuwa hamchi Mungu, lakini yule mwanamke mjane alivyomwendea mara ya kwanza hakupewa haki yake, lakini kwa jinsi alivyokuwa akimwendea endea mara kwa mara, alimpatia haki yake, japo hamchi Mungu, ili asije akamsumbua daima…(Luka 18:1-8)

Vivyo hivyo na sisi tusiache kumwomba Mungu neema ya wokovu, neema ya uponyaji, mahitaji binafsi, hata kama hatutaona dalili zozote za kujibiwa maombi yetu. Kwasababu Mungu anapendezwa na mtu aombaye kwa bidii.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

MADHARA YA KUUPIZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?

CHANZO CHA MAMBO.

MAVAZI YAPASAYO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Warumi 8:3 “Maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili”;


JIBU: Sheria peke yake haiwezi kuondoa dhambi ndani ya mtu, kwamfano Mungu alipotoa amri usizini, Ni kweli wengi waliijitahidi kuishika kwa kutokuzini kabisa maisha yao yote mpaka kifo, lakini ukweli ni kwamba ile tamaa ya kutamani kuzini ilikuwepo ndani yao. Walijizuia vile ni kwasababu sheria ilisema hivyo, lakini sio kwamba ilitoka moyoni mwao kabisa kuchukia uasherati, Na ndio maana sheria hapo inaonekana kuwa dhaifu, kwasababu yenyewe kama yenyewe haiwezi kuondoa dhambi, bali ni kama inazuia tu kwa muda… wanaitumikisha miili kwa nguvu hata hivyo haisaidii kuondoa tamaa za mwili.

Lakini sheria ya Roho wa Mungu huondoa dhambi ndani ya moyo wa mtu kabisa, pale mtu anapozaliwa mara ya pili, ile kiu ya kutamani dhambi Mungu anaiua mwenyewe ndani ya mtu, hivyo mtu wa namna hiyo hata kama Mungu asingesema usizini, yeye mwenyewe kwa kuwa mafuta ya Roho wa Mungu yanakaa ndani yake, ataona kuwa kile kitendo ni kibaya, kadhalika kutamani nako ataona ni kubaya, kumchukia ndugu ni kubaya n.k….unaona hapo, utagundua kuwa zile sheria zote za Mungu zinatimilika zenyewe ndani ya moyo wa Mungu bila hata shuruti.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema, mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. Mtu hawezi kushinda dhambi kwa nguvu zake mwenyewe, nje ya Roho Mtakatifu. Wapo wanasema zishike amri kumi tu, basi inatosha kumpendeza Mungu…Lakini hawajui kuwa wapo wayahudi waliozikisha vizuri Zaidi ya wao lakini bado wakawa wanajiona kuwa hawana uzima ndani yao. Ni kwasababu gani?. Kwasababu sheria wanaishika kwa njia ya mwili lakini sio kwa njia ya Roho.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

UTIMILIFU WA TORATI.

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

FUVU LA KICHWA.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?

SWALI: Je! Mungu anasababisha ajali au majanga, kwamfano ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuzama?


JIBU: Mungu hasababishi ajali yoyote ile, japo Mungu anaweza akamwadhibu mtu kwa makosa yake. Shetani ndiye mwenye lengo siku zote la kuangamiza hata wakati ambapo mtu hana makosa, kama alivyofanya kwa Ayubu, kwasababu biblia inasema yeye alikuwa ni muuaji tangu mwanzo.(Yohana 8:44).

Asilimia kubwa ya ajali na majanga yanaletwa na shetani. Na pia biblia inasema yapo majanga mengine yanaletwa na Mungu mwenyewe, na mpaka imefikia hivyo ujue ni adhabu kutokana na makosa ya watu wenyewe, na pia Bwana anasema huwa hafanyi jambo lolote bila kuwafunuliwa hao watumishi wake manabii, kuwaonya kama tunavyoona alivyofanya kwa watu wa Ninawi.

Leo hii mtu anamuudhi Mungu labda ni muuaji, lakini kabla Mungu hajamwadhibu atamwonya pengine kwa kumtumia Mtumishi wa Mungu au kwa kusikia mahubiri, na akajua kabisa Mungu anamwonya atubu utakuta pengine alisikia Neno likisema “Uaye kwa upanga, atauawa kwa upanga”..

Lakini yeye akapuuzia na kuendelea na tabia yake ya kuuiba na kuua watu pasipo hatia.. Sasa mtu kama huyo inatokea mazingira labda siku moja amekutana na kundi la wanyang’anyi usiku, na kwa bahati mbaya wakamvamia na kumchoma kisu, kisha na kufa..Sasa kwa nje unaweza ukasema ni shetani lakini sio shetani bali ni Mungu mwenyewe kamlipizia kisasi juu yake.

Hivyo zipo ajali zinazotoka kwa Mungu mwenyewe. Kadhalika zipo pia zinazotengenezwa na shetani, ambazo hizo ndio nyingi kuliko zile zinazotoka kwa Mungu.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

NI NANI ANAYETAWALA DUNIA KATI YA MUNGU NA SHETANI?

KWANINI MUNGU ANARUHUSU WATU WAPITIE SHIDA?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Jehanamu ni nini?

RAHABU.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Paulo hakumsamehe Marko, pindi walipotaka kwenda tena kazini?

Matendo 15:37 ″Barnaba akaazimu kumchukua Yohana aliyeitwa Marko pamoja nao.

38 Bali Paulo HAKUONA VEMA kumchukua huyo aliyewaacha huko pamfilia,asiende nao kazini.

39 Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana….”

JIBU: Ukisoma kitabu cha Matendo 13:13 utaona Yohana, aliwaacha wakina Paulo na Barnaba huko Pamfilia, inaonekana aliogopa dhiki itakayokwenda kuwakuta mbeleni, kwasababu Paulo bado mzigo wa kupeleka injili duniani kote alikuwa nao, hivyo walipomsihi waende pamoja alikataa, lakini sasa baadaye tunakuja kumwona tena akikutana na mtume Paulo na Barnaba na kutaka kujumuika nao katika kwenda kuipeleka injili, na ndio hapo tunaona mtume Paulo hakukubali jambo hilo kwasababu kama alishindwa kuandamana nao wakati wa tabu za awali,

kadhalika hataweza kushikamana nao katika dhiki zinazofuata, hivyo sio kwamba Paulo hakumsamehe, alimsamehe lakini hakutaka kuambatana naye tena ili asiwe kikwazo cha injili kwenda mbele.

Ni mfano tunaopaswa tujifunze na sisi [watumishi wa Mungu], kazi ya Mungu si ya kuifanya kirafiki tu, hapana bali wale watakaoitenda kazi kiuaminifu ndio tuambatane nao na kuwatambua hata kama watakuwa si watu wetu wa karibu sana. Lakini ikiwa ni ndugu halafu anaipuuzia kazi ya Mungu, hapo ni kumweka kando, Biblia ilishasema

Wafilipi 2:12 “…utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu”

Mungu akubariki.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada zinazoendana:

Paulo alikuwa na maana gani aliposema “nimeaminiwa uwakili”

DHAMBI YA MAUTI

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

KWANINI PALE BWANA ALICHUKUA HATUA YA KUMSAMEHE DHAMBI KWANZA KABLA YA KUMPONYA YULE MTU MWENYE KUPOOZA?.

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

AGIZO LA UTUME.

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!


Rudi Nyumbani:

Print this post