Title 2019

BWANA ailaze roho ya marehemu mahali pema PEPONI.

SWALI: Ni sahihi kwa Mkristo mtakatifu kumwambia BWANA ailaze roho ya mtu aliyekufa mahali pema PEPONI?


JIBU: Sio sahihi, kwasababu ameshakufa. Tumepewa amri ya kuombeana sisi kwa sisi, yaani tunapokuwa tunaishi hapa duniani, baada ya kufa hatujapewa amri ya kuombeana. Hakuna maombi yoyote yanayoweza kubadilisha hatima ya mtu aliyekufa, kilichobakia kwa mtu aliyekufa ni hukumu tu! (Waebrania 9:27).

Mazishi ya watu wasioamini ni tofauti na mazishi ya watu waliomwamini BWANA wetu Yesu Kristo, wasiomwamini wao hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na mambo yatakayofuata baada ya kifo, ndio maana wanasema maneno hayo, lakini sisi tulioamini ndio tunaoelewa kwamba kama ndugu yetu amekufa katika Bwana, basi tunalo tumaini la kukufuka tena kwasababu ni kama amelala tu!.. Lakini kama mtu amekufa katika dhambi na hakumpokea Kristo basi huyo hana tumaini la uzima wa milele, hivyo hawezi kuokolewa kwa maombi yoyote yale. Kwasababu Bwana Yesu alitupa maagizo ya kuenenda ulimwenguni kote kuihubiri injili, AAMINIYE NA KUBATIZWA ATAOKOKA, hakutupa agizo la kuenenda ulimwenguni kote kuwaombea wafu waokoke au walazwe mahali pema peponi.

Kwahiyo saa ya wokovu ni sasa katika maisha haya, baada ya maisha haya ni hukumu.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

WALE WATAKATIFU WALIOFUFUKA NA BWANA YESU KWAO JE! WALIKUWA PEPONI AU WAPI?

KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KUWEKA MSALABA MAKABURINI?

JE! NI SAHIHI KUWAOMBEA WAFU?

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO?

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

“Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

SWALI: Nini maana ya haya maandiko “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32)?.

JIBU: Tunaona wana wa Israeli baada ya kumkosa Mungu kule jangwani, Bwana aliwapiga kwa pigo la nyoka wa moto, na ndipo Musa akaambiwa atengeneze nyoka wa shaba na kumwinua juu ya nchi, ili kila amtazamaye apate kupona. Sasa Bwana wetu Yesu Kristo alifananishwa na yule nyoka wa shaba juu ya ule mti, kwamba na yeye aliinuliwa juu (Pale Kalvari) ili kila amtazamaye (kwa macho ya rohoni na kumwamini) apate uzima wa milele, na ndio maana alisema katika…

Yohana 3:14 ” Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.”

Kwahiyo hapo Bwana aliposema “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU” alimaanisha kuwa “baada ya kusulibiwa pale msalabani” kwa ajili ya dhambi ya ulimwengu, itaachiliwa nguvu kubwa ya watu wengi kuvutwa kwake, na ndio maana ukiendelea kusoma mstari unaofuata utaona ameweka wazi kuwa kuinuliwa kunahusu mauti ya mwili wake..

Yohana 12:32 “Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.
33 Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa”.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

MAJI YA UZIMA.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Kumbukumbu 23:24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako. 25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.

Kwa hio nikiingia katika shamba la jirani yangu, napaswa kula matunda na kushiba, bila, ila nisiweke katika kapu?


JIBU: Hapo unapaswa uelewe haizungumzii tu kuingia katika shamba la mtu mwingine wakati wowote unaojisikia wewe na kuanza kula kwasababu tu maandiko yamesema tule ila tusibebe chochote hapana!!.. Jambo kama hilo linakuja pale unapokuwa katika mazingira ambayo umeshikwa na njaa, na hauna chakula, na ukiangalia hauna chochote mfukoni kwa wakati huo, na mfano ukiendelea mbele katika hali hiyo unaweza ukazimia kwa njaa njiani…Sasa katika mazingira kama hayo hapo mbele za Mungu unaweza kuingia kwenye shamba la mwingine na kula pasipo kuhesabiwa hatia yoyote mbele za Mungu..isipokuwa usijifungashie mazao yake na kuondoka nayo.

Lakini pia jambo la kukumbuka ni hili, sheria hizo walipewa wayahudi , hivyo utamaduni kama huo ulikuwa kwa wayahudi tu peke yao, kwasababu hiyo basi ilikuwa hata mtu akimwona mgeni kaingia katika shamba lake kwa dharura na kuanza kula, hamfanyi chochote kwasababu anajua agizo la Mungu juu ya masuala kama hayo. Lakini kwa mazingira ya watu wa mataifa kama sisi tuliyopo, huwezi tu kuingia katika shamba la mtu asiyemjua Mungu na kuanza kula mazao yake pasipo hata idhini yake, vinginevyo itakuwa ni kujitafutia tu matatizo..Ni rahisi kuingia katika shamba la mtu wa imani moja na wewe(Ndugu yako katika Kristo) kuliko la mtu asiyemjua Mungu,cha msingi ni kutumia hekima ya kwenda kuomba. Na ukikatazwa ondoka utafute pengine.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JE! NI VEMA KWA MKRISTO KWENDA HOSPITALI AU KUTUMIA MITI SHAMBA ANAPOUGUA?

KANUNI JUU YA KANUNI.

NAOMBA KUJUA WATAKAOENDA MBINGUNI JE! NI WENGI AU WACHACHE?

JE! KUNA DHAMBI KUBWA NA NDOGO?

JE! INAWEZEKANA MTU AKAWA ANAFANYA MIUJIZA NA KUTOA PEPO NA BADO ASINYAKULIWE?

JE! UNAMPENDA BWANA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je kuna andiko linalomruhusu mwanamke kuwa sister?

JIBU: Nadhani utakuwa unazungumzia ma-sisters mfano tunaowaona katika  dini ya Kikatoliki. Ni wazi kuwa hakuna andiko lolote au mahali popote kwenye biblia linasema hivyo. Lakini mwanamke anaweza akajizuia asiolewe kwa ajili ya ufalme wa mbinguni, biblia imesema hivyo katika

1Wakorintho 7: 34 “Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.
35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.
36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane”.

Hivyo mwanamke yeyote anayejizuia kuolewa kwa ajili ya ufalme wa mbinguni, hafanyi vibaya kulingana na maandiko lakini amaanishe kweli kufanya hivyo vinginevyo kama atakuwa anaishi kwa kulipuka tamaa, basi atakuwa anajitafutia mwenyewe hukumu..

Pia lipo andiko lingine linasema..

1 Timotheo 4 :1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wenginewatajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

3WAKIWAZUIA WATU WASIOE, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

Unaona hapo inasema “wakiwazuia”..ikiwa na maana kuwa wanahaja ya kuoa lakini wanalazimishwa kufanya hivyo kutokana labda na utaratibu wa dini zao au madhehebu yao..kwamba ili wapewe nafasi fulani inawapasa wawe hivyo…lakini haimaanishi kuwa mtu yeyote ambaye ametaka kumtumikia Mungu pasipo kuoa au kuolewa anakwenda kinyume na maandiko.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA.

MARIAMU

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

RABONI!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yohana mbatizaji alibatizwa na nani?

JIBU: Biblia haijaeleza mahali popote ni nani aliyembatiza Yohana mbatizaji, lakini kwa hekima tunaweza kufahamu kuwa yeye naye alibatizwa kama alivyokuwa anawabatiza wengine, kwasababu ni sharti kwanza uwe kielelezo wa jambo ambalo unalifanya ndipo uwafundishe na wengine vinginevyo utakuwa ni mnafki, huwezi kuwatangazia watu uhuru wakati wewe mwenyewe bado upo vifungoni…

Lakini sasa swali linakuja ni nani aliyembatiza Yohana?..Jibu ni kwamba miongoni mwa watu aliwahubiria suala la ubatizo na kuamini, mmojawapo kati yao ndiye aliyembatiza Yohana. Kumbuka suala la ubatizo, halimtilii mkazo sana mbatizaji kama linavyomtilia yule anayebatizwa, nikiwa na maana kuwa mbele za Mungu yule anayebatizwa ndiye mwenye uwezo wa kuufanya ule ubatizo kuwa batili au la, na sio mbatizaji..Na ndio maana tunakuja kumwona Bwana Yesu, yeye hakustahili kubatizwa na Yohana kwasababu yeye ndiye mwenye haki kuliko yeye, lakini yeye alimwambia fanya hivyo kwa sasa, ni kwasababu gani? Ni kwasababu hakukuwa na mwenye haki Zaidi yake atakayeweza kufanya vile…

Vivyo hivyo,na kwa Yohana kwa kuwa hakukuwa na mtu mwingine aliyeupokea ufunuo ule, pengine aliwaambia wale wafuasi wake, wafanye hivi kwa sasa (yaani wambatize), ili atimize haki yote.

Mfano huo huo pia tunaweza kujifunza kwa Ibrahimu, Mungu alipompa ufunuo wa TOHARA kwa uzao wake wote, na Mungu akamwambia awatahiri watoto wake na watu wa nyumbani mwake,. Tunaona pia yeye naye hakujitenga kana kwamba haumuhusu hapana, bali yeye baada ya kuwatahiri watu wake, kadhalika yeye naye akatahiriwa na wao. soma

Mwanzo 17: 23 “Ibrahimu akamtwaa Ishmaeli mwanawe, na wote waliozaliwa nyumbani mwake, na wote walionunuliwa kwa fedha yake, wanaume wote wa watu wa nyumba ya Ibrahimu, akawatahiri nyama ya magovi yao siku ile ile, kama Mungu alivyomwambia.
24 Naye Ibrahimu alikuwa mwenye umri wa miaka tisini na kenda alipotahiriwa nyama ya govi lake.
25 Na Ishmaeli mwanawe alikuwa mtu wa miaka kumi na mitatu, alipotahiriwa nyama ya govi lake.
26 Siku ile ile akatahiriwa Ibrahimu na Ishmaeli mwanawe”.

Unaona hapo sasa kwa mifano hiyo hiyo tunaweza kufahamu kuwa Yohana naye baada ya kumbatiza mmoja wa wafuasi wake, yeye naye akabatizwa na wao, ili haki yote itimizwe, Amen.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Usiku huu wa leo wanataka roho yako!” Ni wakina nani hawa?

SWALI: Luka 12:20 inasema “USIKU HUU WA LEO WANATAKA roho yako!” Ni wakina nani hawa wanaoitaka roho yake?

Luka 12:13 Mtu mmoja katika mkutano akamwambia, Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie urithi wetu.
14 Akamwambia, Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu?
15 Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.
16 Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.
18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.

JIBU: Tunaona huyu mtu mawazo yake yote yalikuwa kwenye Mali tu, akijitumainisha katika mali za dunia hii, asijitajirishe kwa MUNGU, alifahamu kwa wingi wa mali zake hata akiumwa anao madaktari wataalamu wa kumuhudumia. Lakini biblia inasema “Usiku wa leo WANAITAKA roho yako!”…Kumbuka haijasema ANAITAKA roho yako, hapana bali WANAITAKA, ikiwa na maana kuwa ni Zaidi ya mmoja.

Pengine wakati amestarehe usiku na familia yake, kulikuwa na majambazi mahali Fulani, tayari wamejiandaa kuja kumvamia na kumuua ili wachukue mali zake, na yeye hapo hajui chochote, au pengine wachawi walimwonea wivu kwa mafanikio yake, sasa wakati huo huo usiku walikuwa vilingeni wakimpangia mikakati ya kumuua kichawi .Au Pengine maadui zake, walimpangia tukio baya usiku huo huo la kumwangamiza, n.k. Sasa hawa wote kwa ujumla ndo hao WANAOITAKA roho yake kama biblia inavyosema. Laiti mtu huyo angekuwa amejitajirisha kwa Mungu, Mungu angemwepusha na hizo hatari zote,lakini yeye aliona Mungu sio kitu cha maana sana kwake kulinganisha na Mali, aliona mali kwake ni ulinzi Zaidi ya Mungu.

Vivyo hivyo na sisi tunazungukwa na hatari nyingi sana pasipo kujua. Tunapotumainia mali au wanadamu kama kinga zetu,badala ya YESU KRISTO na kuudharau WOKOVU unaopatikana kwa njia ya msalaba, na kuona ni kitu kisichokuwa na maana, kama huyu tajiri na ulinzi wake wote, hakupona mikononi mwa shetani..biblia inasema Waebrania 2: 3 “sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia;”

Na pia inasema.

Zaburi 127: 1 “Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure”.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

MTI UANGUKAPO, PAPO HAPO UTALALA.

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE:

UNYAKUO.

NGURUMO SABA

MIHURI SABA

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno;” maana yake nini?

SWALI: Nini maana ya huu mstari? “Mathayo 13:30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu. ”


JIBU: Mfano huu Bwana alioutoa unahusu siku za mwisho, na kumbuka siku za mwisho ndio hizi tunazoishi sasa mimi na wewe, kwamba Bwana atatuma wavunaji watakaovuna watu, sasa ili kuelewa hawa wavunaji ni wakina nani hebu tusome mstari ufuatao..

Mathayo 9:37 “ Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.
38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”

Unaona hapo, siku hizi za mwisho, wahubiri ndio wavunaji, na siku hizi za mwisho Bwana amesema atawatuma wengi,wa ukweli na wauongo, ambao watawavuna watu wote walioko ulimwenguni (waovu na wema), wale walio waovu (wanaofananishwa na magugu) watafungwa matita matita (yaani watafungwa katika madhehebu mbali mbali) na watasubiria kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti, kwasababu ni magugu.

Kama unapenda uasherati, utapata muhubiri atakayekufariji katika uasherati wako, vivyo hivyo na mambo mengine maovu, utapata wahubiri na waalimu na makanisa yanayochukuliana na hayo mambo.

Lakini wale walio wema(yaani zile ngano njema) zitakusanywa pamoja na kuhifadhiwa ghalani (na ghalani ni mbinguni), wale walio tayari kufumbua macho yao waone, kufumbua masikio yao wasikie, Bwana anawakusanya katika siku hizi za mwisho kupitia wahubiri wake waaminifu na wa kweli na kuwaweka tayari kwa ajili ya unyakuo.

Je! Na wewe umejiandaaje? Huu ni wakati wa kukusanywa,Unakusanywa wapi leo? Kwenye dhehebu lako? au katika Neno la Mungu?.

Kanisa/muhubiri asiyekuhubiria kwamba Ibada za sanamu,ulevi,ulavi,ulawiti,uongo,rushwa,wizi,masturbation, chuki,usengenyaji,uvaaji vibaya, ni tiketi ya kwenda motoni, basi huyo ni mvunaji ametumwa kukufunga katika tita lake, na kukupeleka motoni, Biblia inasema mtu asipozaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho hawezi kuuona ufalme wa mbinguni na pasipo huo UTAKATIFU hakuna mtu atakayemwona Mungu.

Ubarikiwe!

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA.

LULU YA THAMANI.

MSHIKE SANA ELIMU.

MAISHA YETU NI MILKI YA YESU KRISTO.

TUZIJARIBU HIZI ROHO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

Mathayo 5:29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.


JIBU: Hapo ni kama inavyojieleza, kiungo kinaweza kikawa kiungo kama kiungo cha mwilini, hususani viungo vya uzazi hivyo ndivyo vinavyowakosesha wengi,…lakini pia kinaweza kikawa kiungo cha nafsi yako, mfano ndugu, marafiki, jamii, kazi, fani, n.k….Yaani kwa ujumla chochote kile kinachoweza kukufanya usiwe na uhusiano mzuri na Mungu, unapaswa ukiweke kando, mana ni heri kufanya hivyo uokoke kuliko kuwa nacho kisha ukaishia kuzimu.

Kwasababu Bwana Yesu alishasema katika,

Mathayo 16: 25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?.

Ubarikiwe!

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

LULU YA THAMANI.

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.


JIBU: Hiyo ni hekima ya kidunia Sulemani aliiona ambayo pia inafananishwa na mambo ya rohoni. Ni wazi kuwa zizi lisilokuwa na ng’ombe au mfugo wowote, huwa ni safi ikiwa na maana kuwa hakuna mnyama atakayeweza kulichafua kwa kinyesi, au mikojo, au majani, hivyo kama ni mtu analimiliki hatateseka kwa namna yoyote ile kuligharamia, hatapoteza muda wake mwingi kulitunza, yeye atalifunga tu kwasababu litaendelea kuwa safi daima na kukaa pasipo na taabu yoyote, lakini mtu kama huyo kipo kitu atakikosa..

Lakini zizi ambalo lina mifugo, kama ng’ombe n.k. tunafahamu zizi kama hilo haliwezi kuwa safi kwasababu ng’ombe watakuwa wanajisaidia huko kila saa, mikojo itakuwa inafagiliwa mara kwa mara, kadhalika zizi nalo litapaswa liwe linapigwa dawa za kuuwa wadudu kila wakati vinginevyo mifugo haitaweza kukaa, zizi pia ni lazima liwe na majani ya kutosha, kama tunavyofahamu Ng’ombe ni mnyama anayekula sana hivyo mmiliki itampasa awe maporini muda mwingi kutafuta majani ya mifugo…Hivyo mmliki wa zizi hilo atapata dhiki na taabu nyingi zaidi ya yule ambaye zizi lake halina mfugo wowote isipokuwa huyu taabu yake haitakuwa ya bure, kuna wakati ataona taabu ya kuhangaika kwake.

Na ndio hapo tukirudi kwenye mithali anatumbia “bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi”…Hii Inamaana gani?.


Inamaana kuwa yule ng’ombe atakwenda KUMLIMISHA katika shamba lake, na kumletea faida nyingi kwa nguvu zake, tofuati na yule aliyeona ni taabu kumlea ng’ombe, siku ya ukulima wake itampasa sasa yeye mwenyewe akalime au aajiri kibarua.

Kadhalika katika roho, wengi wanapenda kuwa na mavuno mengi kwa Bwana, lakini hawapendi kuingia gharama za kuyafikia. Bwana Yesu aliwaambia makutano waliokuwa wanamfuata, wale waliopendezwa na njia ya Bwana lakini hawakuwa tayari kuingia gharama..soma

Luka 14: 25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.
27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?
29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.
31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.
33 Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Hivyo na sisi pia tunapashwa ili tuwe na mavuno mengi Bwana anatuagiza tuwe tayari kuingia gharama za kuyapata mavuno hayo..Na gharama zenyewe ndio hizo Bwana alizozitoa hapo juu.


Amen.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

TWEKA MPAKA VILINDINI.

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

NJIA YA BWANA INATENGENEZWA WAPI?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

JINA LAKO NI LA NANI?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

JIBU: ZAKA/FUNGU LA KUMI Ni moja ya kumi au sehemu ya kumi ya mapato yako yote, hicho huwa kinakwenda kwa Bwana na ni wajibu kwa kila mkristo mwenye shughuli ya kujipatia kipato kumtolea MUNGU sehemu hiyo ya mapato yake..

Walawi 27: 30 “Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.”

Malaki 3: 8 Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.

9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.

10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi.

Sasa fungu la kumi au zaka ni tofauti na ‘sadaka/matoleo’. SADAKA yenyewe ni kile ulichonacho juu ya fungu la kumi, kile ulichokirimiwa pasipo sharti lolote la utoaji unampelekea Mungu, sasa zipo sadaka za aina tofauti tofauti kulingana na mahali au mtu mwenyewe, kwa mfano zipo.

1) sadaka za shukrani, hizi huwa mtu anatoa baada ya Mungu kumtendea au kumfanikisha katika jambo Fulani, aidha, afya, ulinzi, masomo, biashara, kazi, familia, n.k. Huwa anaambatanisha sadaka yake ya shukrani mahali Bwana anapolia kiroho ni tofauti na fungu la kumi.

2) Zipo sadaka nyingine za michango: Hizo zipo nyingi kulingana na uhitaji wa kanisa, mfano jengo, uenezaji injili, vyombo vya nyumba ya MUNGU, mahitaji n.k. Hivyo sadaka/matoleo yapo ya aina nyingi, na pia Mungu hajaweka sharti lolote la utoaji ni jinsi mtu atakavyoguswa moyo na Mungu wake, ndicho atakachotoa.

Kutoka 35:5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;

Kwahiyo jambo la kukumbuka pia katika agano jipya, ni kwamba Mungu hajamwekea mtu sheria au tanzi yoyote katika kutoa ZAKA hata kama hajisikii tu atoe , hapana hiyo haipo katika Ukristo kwasababu Mungu hapendezwi na mtu atoaye kwa moyo wa huzuni au wa kulazimishwa. Lakini ni vizuri pia ikumbukwe kuwa ni wajibu wa kila mkristo yoyote kumtolea MUNGU wake aliyemuokoa. Ni ngumu kwa mtu yeyote kusema amejazwa Roho halafu suala la utoaji kwake ni mzigo.

2Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

9 kama ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele.”

Ubarikiwe ndugu.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

UDHAIFU WA SADAKA!

CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!

NUHU WA SASA.

UTIMILIFU WA TORATI.

UPEPO WA ROHO.


Rudi Nyumbani:

Print this post