Title April 2024

Nini maana ya  “manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana” (Mathayo 11:13)

Jibu:Turejee,

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

13  KWA MAANA MANABII WOTE NA TORATI WALITABIRI MPAKA WAKATI WA YOHANA”.

Mstari huo haumaanishi kuwa Torati yote na Manabii wote walimtabiri Yohana Mbatizaji.. kwamba atakuja kutokea na kuhubiri, na kwamba atakuwa nabii mkuu kuliko wote. Hapana, bali ilimaanisha kuwa Torati iliendelea kuwepo na kufanya kazi, na manabii waliendelea kutokea na kutoa unabii, mpaka wakati wa Yohana kutokea duniani.. na baada ya Yohana ndipo likaanza agano lingine jipya la ufalme wa Mungu kutangazwa na kila mtu kujiingiza kwa nguvu.

Maneno hayo yamewekwa katika Kiswahili kirahisi Zaidi katika kitabu cha Luka..

Luka 16:16  “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu”.

Sasa kufahamu nini maana ya Torati na Manabii fungua hapa >>>Nini maana ya “Torati na manabii”?

Lakini ni kwanini aseme tangu wakati wa Yohana ufalme wa Mungu unapatikana kwa nguvu na watu wanajiingiza kwa nguvu??..Ni kuonyesha kuwa hapo kwanza ilikuwa haiwezekani mtu kujiingiza katika ufalme wa Mungu..ilihitaji kuingizwa.. na waliokuwa wamesimama kama waingizaji wa watu katika ufalme wa Mungu ni Manabii na Torati..

Watu walisubiri maagizo ya Mungu kupitia Nabii au kuhani ndipo wapatanishwe na Mungu… lakini baada ya Bwana YESU kufa na kufufuka kiti cha rehema kimefunguliwa.. Watu hawahitaji tena manabii wala makuhani kumkaribia Mungu… (Maana yake kila mtu ana uwezo wa kumkaribia Mungu kupitia damu ya YESU).

Hatuhitaji tena kwenda Yerusalemu kwa makuhani ndipo tumsikie Mungu, hatuhitaji tena sanduku la agano, hatuhitaji tena nabii atokee ndipo atupe maagizo ya Mungu.. bali kupitia Roho Mtakatifu ndani yetu tunamkaribia yeye.

Kwa kadiri tunavyotia bidii ndivyo tunavyoukaribia na kuuteka ule ufalme..na wenye hekima na bidii ndio wanaoukaribia Zaidi ule ufalme.

Bwana atusaidie.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

MAJINA YA MANABII WANAWAKE

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je Bwana YESU alimjibu Pilato au hakumjibu? Je biblia inajichanganya?

Swali: Je biblia inajichanganya kwa habari ya Bwana YESU kumjibu Pilato? Maana katika (Yohana 18:33-34) inasema alimjibu lakini katika (Mathayo 27:13-14)..  inasema hakujibu chochote alipoulizwa? Je lipi ni sahihi?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote pale, isipokuwa kinachojichanganya ni tafakari zetu, na fahamu zetu… Lakini biblia ni kitabu kikamilifu na kilichovuviwa na Roho Mtakatifu wa Mungu, hivyo hakina kasoro yoyote.

Sasa tukirejea habari hiyo katika Yohana 18:33-37.

Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

35  Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

36  Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.

37  Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”

Hapa ni kweli tunasoma Bwana YESU alimjibu Pilato alipoulizwa kuhusu habari zake mwenyewe… Lakini tukirejea kitabu cha Mathayo ni kama tunasoma habari tofauti kidogo.

Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA.

12  Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.

13  Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?

14  Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”.

Hapa tunasoma Bwana YESU hamjibu Pilato.. Sasa swali je! Biblia inajichanganya??..Jibu ni la! Haijichanganyi.

Tukisoma vizuri habari hizo mbili zinaelezea kisa kimoja lakini katika mazingira manne tofauti..

  1. Mazingira ya Kwanza:

Wakati Bwana anafikishwa kwa Pilato, alitangulia liwali kumhoji Bwana YESU kama yeye ndiye mfalme wa Wayahudi hapo alijibu “wewe wasema (maana yake ndio mimi ndiye)” Huyo ni Liwali anahoji na anajibiwa na Bwana bila maficho yoyote.

Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA…”

  1. Mazingira ya pili:

Lakini wakati ambao Wazee wa makuhani wanamshitaki Bwana YESU kwa Pilato yeye hakujibu chochote..

Kumbuka hapa wazee wa makuhani hawakuwa wanamhoji kuhusiana na swali alilouliza Liwali kwamba kama yeye ni mfalme wa Wayahudi…LA! Bali wazee wa makuhani wenyewe walikuwa wanamshitaki kwa mambo mengine ikiwamo habari ya kulivunja hekalu pamoja na kujiita mwana wa Mungu.. Soma Mathayo 26:62-68..Na sasa wanataka wamsikie Bwana YESU akijitetea mbele ya Pilato. Lakini Bwana YESU hakujibu chochote.

Mathayo 27:12  “Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno”.

  1. Mazingira ya tatu:

Pilato aliposimama na kumwuliza Bwana YESU ajitetee, mbele ya wazee wa makuhani kuhusiana na mashtaka hayo (ya kulivunja hekalu na kujiita mwana wa Mungu).. yeye hakujibu chochote mpaka Liwali akashangaa!!..

Mathayo 27:13 “Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?

14  Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”

Na kwanini Bwana YESU hakumjibu hapa Pilato lolote?.. JIbu ni kwasababu Wazee wa Makuhani ambao waliokuwa ni wanafiki walikuwepo pale wakitafuta neno litokalo kinywani mwake ili waanze kuzusha maneno mengi juu yake..hivyo Bwana hakumjibu Pilato wala makuhani.

  1. Mazingira ya nne

Pilato alipoona hapati jibu lolote kuhusiana na mashtaka ya wayahudi juu ya Bwana.. alimchukua Bwana YESU ndani ya Praitorio na kumwoji akiwa peke yake swali lile lile aliloulizwa na Liwali! (Je wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?)..na Bwana YESU akampa jibu kama lile lile alilompa Liwali.

Yohana 18:33  “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?…”

Umeona?… Kwahiyo biblia haijichanganyi yenyewe.. Ni kwamba Bwana YESU hakujibu mashtaka ya Wazee wa Wayahudi lakini alijibu maswali ya Pilato na Liwali.

Na kwanini Bwana YESU asijibu mashtaka ya wazee wa makuhani? Na amjibu Liwali pamoja na Pilato peke yao?…ni kwasababu wale wazee walikuwa wamemkusanyikia kwa shari, wapate kumwongezea dhiki….

Maswali yao si ya lengo la kutaka kujua, bali kutafuta sababu za kumshitaki..kwani tayari alishawajibu huko nyuma lakini bado waliendelea kumtafuta kwa maswali mengine mengi (Mathayo 26:62-68).

Kwahiyo na sisi tunachoweza kujifunza ni utulivu na kunyamaza katika vipindi ambavyo adui anatumia vinywa vya watu kutujaribu.. Ukishajibu swali mara ya kwanza, na mtu haelewi badala yake anatafuta tu kasoro, basi kinachofuata baada ya hapo ni kukaa kimya.

Kwasababu yapo maswali ambayo ukijibu hayatamsaidia yule anayeuliza badala yake yatampa kila sababu za kukusumbua wewe ziaidi, kwasababu lengo lake si kutaka kujua bali ni kubishana au kukudhuru wewe au kukushambulia. Hivyo ni muhimu kuwa makini.

Tito 3:9  “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana.

10  Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini maandiko yanajichanganya yenyewe kwenye habari ya Paulo alipotokewa na Yesu alipokuwa anakwenda Dameski?

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

Liwali ni nani?

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Rudi Nyumbani

Print this post

JE NI YESU YUPI UNAYE? WA KIDINI AU WA UFUNUO!

Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRSTO libarikiwe daima!

Kuna tofauti ya kumjua YESU WA KIDINI na yule wa UFUNUO (Yaani Yesu aliyefunuliwa maishani mwako na yule uliyempokea kwa wazazi au kwa mhubiri fulani)  Utauliza kivipi?..Hebu tumwangalie mtu mmoja katika biblia ambaye hapo kwanza alimjua YESU wa kidini lakini baadaye akaja kumpokea wa KIUFUNUO, Na ikawa heri kwake!. Na mtu huyo si mwingine Zaidi ya Petro.

  1. YESU WA KIDINI.

Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.

41  Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, TUMEMWONA MASIHI (MAANA YAKE, KRISTO).

42  Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”

Hapa Petro anamjua  na kumpokea YESU kwa kuambiwa TU!!!…Anaambiwa na Adrea kaka yake habari za YESU, hivyo Petro anaamini na akampokea YESU wa kidini, akawaa mfuasi wa YESU tu,  lakini bado hajafunuliwa ndani yake!. Akamjua tu kulingana na dini ya kiyahudi kuwa atakuja Masihi na hivyo amemwona! Na si Zaidi.

  1. YESU WA UFUNUO.

Baada ya kipindi kirefu kupita, Petro ampokea YESU wa ufunuo na hapo inakuwa heri kwake.

Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?

14  Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

15  Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.

Umeona hapo?… Petro amemjua YESU KIUFUNUO!.. aliyefunuliwa na Baba wa mbinguni, na si yule aliyeambiwa na kaka yake Andrea.

Kumbuka tayari alikuwa ameshajua kuwa YESU ndiye Kristo, kwani Andrea alishamwambia… Lakini ni kidini tu!..alipotulia na kumruhusu Roho Mtakatifu afanye kazi ndani yake ndipo akajua huyu wa kidini hatoshi, na kumbe YESU NA ZAIDI NA ALIVYOKUWA ANAMFIKIRIA..

Na utaona baada ya hapo ndipo Bwana anampa Petro funguo za Ufalme wa Mungu, baada tu ya kumpata YESU WA UFUNUO.

Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni

18  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

19  NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI”

Ni Kwanini leo hii, wengi funguo za ufalme wa Mungu hawana???… Sababu kuu ni YESU WALIYE NAYE MAISHANI MWAO si wa ufunuo bali wa kidini… Kama ni wa kidini huyo hawezi kufungua lolote ndani yao, lakini kama ni yule wa UFUNUO huyo anafungua mbingu na nchi!.

Sasa swali tunampataje YESU WA UFUNUO.

Tunampata YESU wa ufunuo kwanza kwa kuweka mbali mapokeo, na udini, na udhehebu na ujuaji na kumruhusu ROHO MTAKATIFU afanye ndani yako kwa unyenyekevu wote..huku ukiwa umejikana nafsi yako na kujitwika msalaba wako… Kidogo kidogo utaanza kumwona YESU kwa UFAHAMU MWINGINE, Na utayagundua mengi kumhusu yeye, na hayo mambo mapya utakayoyapata kumhusu YESU ndiyo mafunuo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

Petro na Adrea waliitwa na Bwana wakati gani?

HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Isaya 24:16-18 Kukonda kwangu!

SWALI: Nini Maana ya Isaya  24:16-18, inapomzungumzia mwenye haki, na anaposema Kukonda kwangu!

Isaya 24:16 Toka pande za mwisho wa dunia tumesikia nyimbo, Atukuzwe mwenye haki. Ndipo niliposema, Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu! Watenda hila wametenda hila, naam, watendao hila wametenda hila sana. 

17 Hofu, na shimo, na mtego, vi juu yako, Ee mwenye kukaa duniani. 

18 Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika


JIBU: Vifungu hivyo vinazungumzia unabii wa Masihi (Yesu Kristo) mwokozi wetu.

Katika mstari wa 16, nabii Isaya anaonyeshwa maono, ya nyimbo za “mwenye haki” ambaye si mwingine zaidi ya Kristo, Kwamba atukuzwe. Jambo ambalo ni la furaha, Kristo kuja duniani, ni tendo ambalo lilishangaliwa sio tu na malaika (Luka 2:8-14), lakini pia na wanadamu (Yohana 12:12-13).

Lakini tunaona katika sentensi inayofuata nabii Isaya, anaonyesha masikitiko yake, kwa kusema Kukonda kwangu! Kukonda kwangu!  Ole wangu, watenda hila wametenda hila.  Akifunua kimifano hali ya taabu na huzuni inayompelekea hata kupoteza afya kwasababu ya mienendo ya watu waovu baada ya pale. Yaani badala wampokee mwokozi, wengi walimpinga na kumkataa, wakamsulubisha, na kuukata wokovu, ulioletwa na huyo mwenye haki.

Hivyo katika vifungu vinavyofuata 17-18, Anaeleza hukumu itakayowapata waliopo duniani, kwa kosa la kumkataa masihi, akilenga hasaa siku ile kuu ya Bwana, siku ya mwisho ya ghadhabu ya Mungu ambayo hii dunia itaharibiwa kabisa pamoja na watu waovu. Ambapo kwa urefu wake, inaelezwa pia katika vifungu vinavyofuata.

Unabii ambao ni kweli kabisa, unapompinga Kristo leo, aliye mwenye haki, aliyekuja kukuondolea dhambi zako, huwezi kuikwepa jehanamu ya moto, kwasababu matendo yako pekee hayawezi kukufanya mkamilifu, vilevile katika siku za mwisho ikiwa utakuwepo duniani, huwezi kuyakwepa mapigo ya Mungu juu yako.

Hivyo mpendwa ni heri ukampokea Yesu leo, akusamehe dhambi zako. Jina lako liandikwe kwenye kitabu cha uzima. Mwisho umekaribia sana, Jiulize ukifa leo katika hali ya dhambi utaenda kuwa mgeni wa nani huko ng’ambo ufikapo?

Ikiwa upo tayari kuupokea wokovu leo, upate msamaha wa dhambi zako basi fungua hapa kwa mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

“Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

Rudi Nyumbani

Print this post

NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO

Ushindi wa kwanza wa vita vya kiroho unaanza na “kukataa”.. Na kukataa kunaanza katika “moyo”, na kunaishia katika “kinywa”.. Unapoukiri udhaifu ndivyo unavyopata Nguvu juu yako vile vile unapoukiri uzima ndivyo navyo unavyopata nguvu juu yako.

Vile vile unapoukataa Udhaifu wa adui, ndivyo unavyokosa nguvu juu yako…Ndivyo biblia inavyotufundisha kuwa Uzima na Mauti vimewekwa katika uwezo wa ndimi zetu,

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”

Ndio maana hata wokovu tunaupata kwa kanuni hiyo, Kwanza “kuamini moyoni” pili “kukiri kinywani”

Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.

Kwahiyo daima katika maombi yako usisahau hilo kuwa “moyo na kinywa” vinashirikiana na vina nguvu..

Hivyo unapokuwa katika sala au hata nje ya sala… hakikisha siku zote unakataa moyoni mwako na katika kinywa chako Mahubiri yote ya shetani, na kazi zake anazozielekeza juu yako.

> Maana yake Unakataa “Dhambi juu ya maisha yako”.. na zenyewe zitaisha nguvu

> Unakataa “Hofu na mashaka kutoka kwa ibilisi”… na yenyewe yataisha nguvu.

> Unakataa “Unyonge na wasiwasi wa ibilisi”.. na vitaondoka katika maisha yako.

> Unakataa “Magonjwa na maradhi ya ibilisi”…. na yataisha nguvu juu yako.

> Unakataa “shida na tabu za ibilisi”.. na zenyewe zitaisha nguvu..

> Unakataa “Maazimio yote ya ibilisi yaliyokusudiwa juu yako”… na yenyewe yataisha nguvu.

> Unakataa “Maneno na ratiba zote za adui juu yako”..nazo zitafutika kabisa..

> Unakataa “kuitwa majina yote ya kiMisri uliyokuwa unaitwa huko nyuma au unayoendelea kuitwa sasa”.. na yenyewe yataisha nguvu juu yako..

Kama zamani ulikuwa kahaba, basi sasa baada ya kuokoka unakataa hayo majina, kama ulikuwa unaitwa au unajiita jambazi, au mhuni fulani au mwizi, au jina lingine lolote la kihuni na lisilo na maana unakataa hayo majina kwamaana majina nayo yamebeba roho (soma 1Samweli 25:25).

Biblia inasema Musa alipokuwa mtu mzima alikataa kuitwa Mwana wa binti Farao.. Hivyo ushindi wake wa imani ulianzia hapo..

Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, AKAKATAA KUITWA MWANA WA BINTI FARAO

25  akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;

26  akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.”

Kwanini Musa alikataa kuendelea kuitwa “Mwana wa binti Farao”?.. Ni kwasababu wana wa binti za Farao walikuwa wanajulikana ni watu “kuabudiwa kama miungu” pia wàtu“wenye kiburi/majivuno/majigambo” na “wauaji wenye uwezo wa kufanya jambo lolote ovu na wasiulizwe na mtu”..

Na akajua endapo akiendelea kuitwa hivyo Mwana wa binti Farao, bado hizo tabia zao zitaendelea kukaa ndani yake na kumtumikisha, hivyo akakataa hicho cheo..na kujitoa katika ile nafasi.

Inasikitisha mtu baada ya kuokoka bado anaona ni sahihi kuitwa sistaduu, au brazameni, au bishoo, au Demu, au DJ, au jina lingine lolote la kihuni tu!.. Ni lazima uyakatae hayo majina kwa kinywa chako, na pia ubadilike ili kukataa kwako kuendane na mwenendo wako.. lakini kama utakataa kinywani lakini muonekano wako unasema wewe bado ni yule yule mtu wa kale, bado itakuwa haina maana!.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Roho ya kukataliwa ni nini?

Swali: Je kuna roho ya kukataliwa katika biblia?.. na kama ipo je mtu anawezaje kufunguliwa kutoka katika hiyo roho?


Jibu: “Kukataliwa” kwa lugha nyingine ni ile hali ya “kukosa kibali”.

Mtu anaweza kukosa kibali “kwa Mungu” au “kwa wanadamu”.

  1. KUKOSA KIBALI KWA MUNGU.

Sababu kuu ya Mtu kupoteza kibali (kukataliwa) na Mungu ni “DHAMBI/MAOVU”. Dhambi inapoweka mizizi katika maisha ya mtu inampotezea kibali kwa Mungu.. Mtu huyu anaweza kumwomba Mungu na asione majibu anayoyategemea…anaweza kupambana na asione matokeo ya kile anachokipambania.

Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, HATA HATAKI KUSIKIA”.

Mfano wa mtu aliyepoteza kibali mbele za Mungu na kuwa mtu wa kukataliwa mbele zake ni Mfalme Sauli (1Samweli 16:1) na pamoja na Kaini (Mwanzo 4:10-12).

Sasa mtu anapopoteza kibali cha kiMungu vilevile hawezi kupata kibali kwa watu, hivyo atakuwa mtu wa kukataliwa na watu sahihi (lakini anaweza kukubalika na watu wasio sahihi, jambo ambalo ni hatari kubwa). Mfano wa watu hao katika biblia ni Kaini..

Mwanzo 4:10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.

11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;

12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.

13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; HATA ITAKUWA KILA ANIONAYE ATANIUA”

Umeona hapo?..Kaini alijua madhara ya “kukataliwa na Mungu” ni “kukataliwa na watu pia”… ndio maana anasema “watu watakapomwona watamwua”.

Kwahiyo DHAMBI au MAASI ndio msingi mkubwa wa mtu kupoteza kibali. Na kwasababu dhambi zote zinaasisiwa/kuchochewa na roho ya Ibilisi na mapepo yake, hivyo basi ni sahihi kabisa kusema kukataliwa ni roho..

Kwahiyo mtu anapojigundua kuwa kila mahali hakubaliki, anakataliwa na kila mtu, na hata wakati mwingine hajui sababu… ni muhimu kulitafakari hilo kwa jicho la pili, kwasababu ni roho ipo nyuma yake inayopalilia dhambi juu ya maisha yake, ambayo matokeo yake huyo mtu ni kukatalika kwa kila anayemwona, au kila anachokipanga..

Hivyo suluhisho pekee la kuiondoa hiyo roho ya kukataliwa ndani ya mtu ni KUOKOKA KIKWELI KWELI.. Na maana ya kuokoka ni KUACHA DHAMBI!!!.. Mtu anayetaka kuokoka lakini hataki Kuziacha dhambi zake, hataki kuacha uzinzi, ulevi, wizi, usengenyaji, matukano, kutokusamehe, chuki, wivu, usengenyaji, fitina n.k hawezi kupokea wokovu mkamilifu. Lakini anayetubu kwa kudhamiria kuziacha dhambi zake ndiye anayepokea wokovu mkamilifu.

Na matokeo ya kupokea wokovu mkamilifu ni kuondoa roho ya kukataliwa ndani yako, na si tu roho ya kukataliwa bali na roho nyingine zote ambazo zimekaa ndani yako zinazochochea tabia na mienendo mingine isiyofaa.

Je umeokoka?

Kama bado na unatamani kufanya hivyo basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu kwa msaada Zaidi au ukafuatiliza sala hii >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mistari ya biblia kuhusu kibali.

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

TENDA JAMBO LA ZIADA.

MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.

NUHU WA SASA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Yesu alikamatwa usiku, hawakuyafanya yale mchana?

JIBU: Yesu ni mtu ambaye alizungukwa na makutano mengi, hivyo isingekuwa rahisi kwao kumkamata wakati wa mchana, kwasababu walijua watakutana na upinzani mkubwa wa makutano.. kama maandiko yanavyosema katika vifungu hivi; 

Mathayo 21:45-46

[45]Wakuu wa makuhani na Mafarisayo, waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao.

[46]Nao walipotafuta kumkamata, waliwaogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii. 

Hivyo njia pekee, ilikuwa ni usiku. Tena wakamwendea na marungu na mapanga kujidai kuwa wanakwenda kumtafuta mwizi, huku mioyoni mwao wakijua kabisa wanayekwenda kumfuata ni mtu wa haki.

Na hiyo ni kuthibitisha kwamba walikuwa hawajiamini kwa matendo yao, kwasababu waliyajua ni maovu ndio maana waliyafanya gizani.

Marko 14:48-49

[48]Yesu akajibu, akawaambia, Je! Ni kama juu ya mnyang’anyi mmetoka wenye panga na marungu, kunitwaa mimi? [49]Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia. 

Hiyo ndio sababu kwanini wamfuate usiku, lakini hawakujua ndio walikuwa wanairahisisha njia ya wokovu. Kufunua kuwa giza kamwe haliwezi kuishinda nuru.

Yohana 1:4-5

[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. 

Mwamini Kristo, Nuru yake ikuangazie moyoni mwako.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Yesu kuvishwa taji la miiba kichwani, kulifunua nini?

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Rudi Nyumbani

Print this post

SAFINA NI NINI?

Kwa kiyahudi huitwa ‘Tevat’, ni chombo cha majini kilichotumika mahususi kwa ukombozi. Ni mfano wa meli iliyotumika kuokoa watu/wanyama kutoka katika maangamizi fulani. Kwamfano katika biblia tunaona Nuhu aliagizwa atengeneze safina, ambayo ataingia yeye pamoja na familia yake, na wanyama wa nchi.

Ukisoma Mwanzo 6-8, utapata kufahamu vipimo vya safina hiyo vilivyokuwa na vigezo vyake, japokuwa biblia haijatueleza mahususi umbo la chombo kile kilivyokuwa.

Lakini pia wakati Musa anazaliwa, tunaona wazazi wake walimtengeneze a naye kisafina kidogo, akafichwa ndani yake, ili kunusuriwa na maangamizi ya Farao.

Kutoka 2:1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi. 

2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu. 

3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto.

Jambo la muhimu kufahamu ni kuwa safina hizo ilikuwa ni lazima zipakwe LAMI ndani na nje. Lami hizo ni mfano wa gundi nzito zilizopakwa, lengo lake likiwa ni kuzuia maji yasiweze kupenya sehemu yoyote ndani ya Safina, (Mwanzo 6:14, Kutoka 2:3). Safina zilikuwa na sifa kama za “nyambizi” tulizonazo sasa, ambazo hazihathiriwi na maji mahali popote ziwapo juu au chini ya maji.

Safina inamwakilisha nani ?

Ni Kristo Yesu, yeye ndiye mwokozi wetu dhidi ya ghadhabu ya Mungu juu ya ulimwengu huu kwa wenye dhambi. Na DAMU yake ndiyo ile LAMI. Inayonyunyizwa kwetu sisi. Mtu yeyote ambaye hajamwamini Yesu, ni dhahiri kuwa ghadhabu ya Mungu ipo juu yake, hawezi kuiepuka. Kwasababu amekataa msamaha wa dhambi, tuliopewa bure kwa kifo chake pale msalabani.

Je! Unaichezea neema? Kumbuka ulimwengu huu unafikia mwisho. Kristo amekaribia kurudi, kuwanyakua watu wake. Je! Bado upo kwenye dhambi? Ikiwa utataka kuupokea wokovu leo bure, basi uamuzi huo ni bora kwako, Hivyo waweza, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala hiyo ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE

Rudi Nyumbani

Print this post

KIFUNGO CHA MWAMINI KIPO WAPI?

Unaweza kuuliza je! Mwamini anaweza kufungwa na adui?. Jibu ni ndio anaweza kufungwa. Utauliza tena, kama anafungwa sasa kazi ya Yesu msalabani ilikuwa ni nini ikiwa hajawekwa huru kweli kweli.

Jibu ni kwamba mwamini yeyote, hawezi kuwa na kifungo katika roho yake, yaani hawezi kufungwa roho aidha na mapepo, au wanadamu au chochote kile. Hawezi kuwa na laana yoyote ndani yake, aidha ya ukoo au ya mabibi. Kwasababu yeye ni mbarikiwa amewekwa huru na Yesu, na ndio kazi Yesu aliyokuja kuifanya kuwaweka huru walioonewa na ibilisi.Hivyo mtu yeyote aliyemwamini Yesu kwa ‘TOBA’, ubatizo na kupokea Roho. Huyo hana kifungo chochote kwasababu uhai wake unakuwa umefichwa ndani ya Kristo.

Lakini Shetani anauwezo wa kumzuia, katika mambo mengi, asipojua ni nini anapaswa afanye. Na hicho ndicho kifungo cha nje akifanyacho adui. Kukuzuia wewe mwamini, ndicho alichokifanya kwa Paulo wakati Fulani alipotaka kwenda kuhubiri  injili kwa Wathesalonike akasema shetani alinizuia (1Wathesalonike 2:8).

Lakini pia tunamwona Mtume mwingine aliyeitwa Petro.

sasa hebu tuangalie kisa hiki kwenye maandiko Kilichomhusu yeye, tuone ni maeneo gani huwa adui analenga mahususi.

Matendo 12:4  Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.

5  Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.

6  Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakalilinda gereza.

7  Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika kule chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. MINYORORO YAKE IKAMWANGUKA MIKONONI.

8  Malaika akamwambia, Jifunge, KAVAE VIATU VYAKO. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, JIVIKE NGUO YAKO, ukanifuate.

9  Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.

Umeona maeneo aliyofungwa Petro?

Wafungwa wa zamani, ilikuwa ili aitwe mfungwa, ni lazima mambo hayo matatu  yakamilishwe juu yake; nayo ni.

1) Kufungwa, Minyororo mikononi

2)Kuondolewa Mavazi, na kupewa mengine ya gerezani.

3)Kuondolewa viatu miguuni

Na hiki ndicho kitu anachokifanya  pia adui kwa mwamini. Anaanza kwa kukufunga mikono yako rohoni, kisha kuyaondoa mavazi yako, na mwisho viatu vyako miguuni. Baada ya hapo unakuwa tayari huna nguvu ya kumshinda.

Mikono ni nini?

Ni “maombi na mifungo”

Mikono ni viungo mama katika mwili. Husaidia viungo vingi kufanya shughuli zake. Silaha hushikwa na mikono,  hata ngumi hurushwa kwa mikono. Hivyo adui anajua akizuia mikono yako. Huwezi kufanya lolote. Mikono ya mwamini, ni “maombi na mifungo”.

Mtu ambaye ni mwombaji, kiwango cha Roho ndani yake huwa ni kikubwa, na hivyo hakuna mnyororo wowote, unaoweza kumshika. Ndio maana utaona baada ya kanisa kumwombea Petro kwa juhudi, akafunguliwa. Vilevile Paulo na Sila walipokuwa wamefungwa kipindi kile, hawakulala tu, bali usiku wa manane walikuwa wakiomba, na matokeo yake vifungo vikawaachia.

Matendo 16:25  Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26  Ghafla pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.

Umeona, maombi, huondoa minyororo mikononi. Kuwa mwombaji, uzishinde nguvu za mwovu. Shetani anawaogopa waombaji

Mavazi ni nini?

Ufunuo 19:8  Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu

Mavazi, ni matendo mema. Ukikosa matendo mema,(Utakatifu), si rahisi kumshinda adui, utakuwa mwamini asiye na matunda yoyote, itaishi tu kama mwanadamu ambaye anamapungufu ya akili rohoni, hutaweza kufanya lolote.Ndani una makunyanzi, mawaa, ambazo katika hizo shetani anakuwa na haki ya kukulaumu.

Ishi kama mkristo, ukiwa rafiki wa dunia, fahamu kuwa unajifanya adui kwa Mungu moja kwa moja. Nuru yako isipoangaza nje, huwezi mshinda shetani. Ni lazima uwe kikombe safi, nje na ndani. Huwezi kusema umeokoka halafu matendo yako hayaendani na imani yako.Unajidanganya, bado hujaifahamu neema ya Mungu.

Miguu ni nini?

Waefeso 6:14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani.

Miguu ni utayari, wa kuhubiri. Adui anapenda kukawiisha nia za watu, kwa kuwavuta katika mambo yao mengine, na kusahau yaliyo ya msingi kwao, ndio hapo atawasonga kwa anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu. Na mwisho wa hapo wanabakia kuwa hawana matunda.

Hivyo ndugu uliyeokoka, usiruhusu adui kukuzuia popote. Jijengee desturi ya kuwa mwombaji wa kila siku. Mikono yako isifungwe. Penda kuishi maisha matakatifu, vazi lako lisibadilishwe, kuwa tayari kuhubiri injili wakati wowote, ukifaao na usiokufaa, epuka udhuru wa mwili au kazi, pinga sana hapo jiwekee ratiba yako, ili upate sehemu ya kuwaeleza wengine habari za Yesu Kristo anayewaokoa wanadamu.

Tukizingatia hayo. Tutakuwa tumemshinda shetani ndani na nje. Hatujafungwa ndani wala nje.

Bwana akubariki

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

VITA DHIDI YA MAADUI

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Njia ya Msalaba ni nini, na Je ipo kibiblia?

Swali: Njia ya msalaba ni nini na Ipi historia ya njia ya msalaba?

JIBU..

Njia ya Msalaba ni Desturi iliyoanzishwa na kanisa Katoliki ambapo waumini wanapita katika mitaa ile Bwana YESU aliyosulubiwa, kuanzia alipotoka kwa Pilato mpaka mwili wake ulipowekwa kaburini.

Kulingana na kanisa Katoliki, kuna vituo 14 ambavyo Bwana YESU alipitia, ambapo  kila inapofika Ijumaa kuu (ile ya pasaka) wakatoliki hupita katika vituo hivyo huko YERUSALEMU kuanzia mahali pajulikanapo kama “ngome ya Antonia” mpaka “kanisa la Roma la ufufuo” (karibia na mahali ambapo Kaburi la Bwana YESU lilikuwepo)..matembezi hayo ni ya mita 600.

Na wale wasiokuwepo Israeli basi watapita karibu na picha kumi na nne (14) zilizochorwa katika kuta za makanisa hayo ya Roma na kusema baadhi ya sala.

Vifuatavyo ni vituo hivyo kulingana na kanisa katoliki.

1. Yesu anahukumiwa kuuawa.

2. Yesu anapewa msalaba na maaskari wa kiroma

3. Yesu anaanguka chini kwa mara ya kwanza.

4. Yesu anakutana na mama yake (Mariamu)

5. Simoni Mkirene anashurutishwa kuubeba msalaba wa Yesu.

6. Veronika anapangusa damu katika uso wa Bwana Yesu.

7. Yesu anaanguka kwa mara ya pili.

8. Yesu akutana na wanawake wa Yerusalemu.

9. Yesu anaanguka mara ya tatu

10. Yesu anavuliwa mavazi yake

11. Bwana Yesu anagongomelewa msalabani

12. Yesu anaisalimu roho yake

13. Mwili wa Bwana Yesu unaondolewa msalabani.

14. Mwili wa Bwana Yesu wawekwa kaburini.

Hivyo ndivyo vituo 14, Bwana Yesu alivyovipitia kulingana na kanisa katoliki.

Lakini vituo baadhi hapo hatuvioni katika maandiko, kwamfano kituo cha 3,7 na 9 cha Bwana YESU kuanguka chini mara ya kwanza, na ya pili na ya tatu havipo katika maandiko..

Vile vile kituo cha 6 kinachomtaja Veronika kufuta damu katika uso wa Bwana YESU hakipo katika biblia..na hata kituo cha 4 cha Bwana YESU kukutana na mama yake hakipo katika biblia!.

Hivyo kama habari hizo hazipo katika biblia hatupaswi kuziamini wala kuzishika kwani huenda ni habari za kutungwa! au zimetolewa katika vyanzo visivyo sahihi, ambavyo havijahakikiwa na Roho Mtakatifu.

Kitabu cha biblia chenye vitabu 66, hiyo ndiyo iliyohakikiwa na Roho Mtakatifu lakini vitabu vingine nje na hivyo vya kwenye biblia ni potofu na vina udanganyifu.

Na Zaidi hatujapewa amri ya kuadhimisha vituo vya Bwana YESU alivyopitia, ndio! Tunaweza kutafakari lakini si kufanyia ibada,..sala za namna hiyo ni ibada za sanamu, kwani zinamfanya mtu aanguke katika zile picha au katika ile mitaa huko Yerusalemu, jambo ambalo ni machukizo.

Kufahamu njia ya Msalaba hasa kibiblia ni ipi fungua hapa >>> NJIA YA MSALABA

Shalom..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Matuoni ni nini katika biblia?

MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.

UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Rudi Nyumbani

Print this post