Title 2024

Nardo ni nini? (Yohana 12:3)

Jibu: Turejee..

Yohana 12:3 “Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya NARDO SAFI yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.

4  Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema,

5  Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa DINARI MIA TATU, wakapewa maskini”

“Nardo” ni jamii ya mmea mdogo ujulikanao kama “Nardostachys”. Mmea huu hutoa maua madogo ya rangi ya “Pinki” (Tazama picha juu), na vijimatunda vidogo vyeusi ambavyo ndivyo chanzo cha mafuta aina ya “Nardo” yanayotumika kutengenezea madawa ya asili pamoja na marhamu (yaani Perfumes/pafyumu) iliyo ya gharama kubwa kuliko nyingine nyingi.

marhamu ya Nardo

Pafyumu iliyotengenezwa kwa “Nardo”, ilikuwa ni ya gharama kubwa na hata sasa ni ya gharama kubwa kutokana na upatikanani wa mimea hiyo.

Mimea ya Nardostachy, inapatikana katika safu za milima ya Himalaya, iliyopo nchini Nepali, na sehemu chache za “nchi ya India” pamoja na “Uchina”.  Na inamea kuanzia kwenye kimo cha Mita 3,000 mpaka mita 5,000 kutoka katika usawa wa bahari (Mita 5,000 ni karibia na kimo cha Mlima Kilimanjaro).. Hivyo upatikanaji wake ni mgumu sana, kutokana na sehemu chache unazomea na kimo unapopatikana!.

Kutokana na sababu hizo, ndizo zinazoifanya Marhamu ya Nardo kuwa ya gharama. Mpaka hapo tutakuwa tumeshafahamu kuwa ile Marhamu yule mwanamke aliyompaka Bwana iliagizwa kutoka mbali sana (maana yake nje ya Israeli) na ilikuwa ya gharama sana… Dinari 300 ni sawa na shilingi Milioni 6 za kitanzania.

Mistari mingine inayozungumzia Marhamu ya Nardo ni pamoja na Wimbo ulio bora 1:12, na 4:13-14

Sasa kufahamu kwa urefu ni nini tunajifunza kupitia tukio la mwanamke yule kukivunja kile kibweta fungua hapa >>AKAKIVUNJA KIBWETA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

GHARAMA YA UFALME WA MBINGUNI.

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).

Jibu: Turejee,

Wimbo 2:9 “Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani”.

“Kimiami” ni dirisha kubwa lililo katika “ghorofa”..

Madirisha makubwa yaliyo katika maghorofa tofauti na yale yaliyo katika nyumba za chini ndiyo yaliyoitwa “kimiami”.

Mfano wa dirisha la Kimiami ni lile ambalo mfalme Ahazia aliloanguka na kuugua..

2Wafalme 1:2 “Na Ahazia AKAANGUKA KATIKA DIRISHA la chumba chake orofani, katika Samaria, akaugua; akatuma wajumbe, akawaambia, Enendeni mkaulize kwa Baal-zebubu, mungu wa Ekroni, kwamba nitapona ugonjwa huu”.

Na lile ambalo Yezebeli alianguka, baada ya kuangushwa na wale matowashi..

2Wafalme 9:30 “Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani.

31 Hata Yehu alipoingia lango la mji, alisema, Je! Ni amani, Ewe Zimri, mwenye kumwua bwana wako?  32 AKAINUA USO WAKE KULIELEKEA DIRISHA, akasema, Aliye upande wangu ni nani? Matowashi wawili watatu wakachungulia.

33 Akasema, Mtupeni chini. Basi wakamtupa chini; na damu yake ikamwagika nyingine juu ya ukuta, na nyingine juu ya farasi, naye akamkanyaga-kanyaga”.

Tazama pia shubaka hapa >>>Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6) 

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA MATHAYO.

(Hotuba za Yesu)

Kitabu cha Mathayo ni moja ya vitabu vinne (4), vya injili. Yapo mambo mengi ya kujifunza ndani yake, lakini katika makala hii, tutaona mambo muhimu ya kufahamu ambayo yatakusaidia katika usomaji wako.

Tukiachia mbali matukio, na huduma mbalimbali ikiwemo za uponyaji alizozifanya Yesu. Tunafahamu kuwa Bwana “ALIFUNDISHA” pia. Na hapa ndipo kiini cha kujifunza kwetu.

Hivyo katika kufundisha kwake, kuligawanyika mara mbili. Kuna taarifa ambazo alizotoa bila kutolea maelezo mengi, lakini pia kuna taarifa alizitoa kama hotuba.

Sasa tutaangazia hizo HOTUBA, ambazo zimerekodiwa kwenye kitabu hichi.

Zipo tano (5), Nazo ni

  1. Hotuba ya Mlimani. (Mathayo 5-7)
  2. Hotuba ya utume (Mathayo 10)
  3. Hotuba ya ufalme wa mbinguni (Mathayo 13)
  4. Hotuba ya kanisa (Mathayo 18)
  5. Hotuba ya siku za mwisho (Mathayo 24)

Kabla ya kuziangalia kwa upana kidogo. Tufahamu kwanza hapo tusemapo “hotuba” tunamaanisha nini.

Hotuba ni mahubiri/mafundisho aliyoyasema Yesu kwa upana, yaliyolenga mada Fulani maalumu.

Ni mazungumzo marefu ya Bwana Yesu. kukazia jambo lile lile moja. Sasa embu Tuangalie kiini cha kila hotuba.

1) Hotuba ya mlimani. (Mwenendo wa Mkristo)

Hii tunaisoma katika sura ile ya 5,6,7. Ni wakati ambapo Bwana Yesu alipanda mlimani, kisha wanafunzi wake wakamfuata, akaanza kuwafundisha mambo mengi. Sasa kiini cha hotuba hii, kilikuwa ni kuwafundisha mwenendo sahihi wa Mkristo, unaokubaliwa na Mungu.

Anaanza kwa kusema HERI, HERI, HERI, maskini wa roho, wapole, wenye rehema, wapatanishi, wenye moyo safi, wenye kiu na njaa ya haki, n.k. anaendelea jinsi tunapavyopaswa tuwapende maadui, tusamehe, tusilipize kisasi, akafundisha usahihi wa kuomba, kufunga, kutoa sadaka, usafi wa moyo, na upendo, na mambo mengine kadha wa kadha.

Ni maneno ambayo kama wewe ni mwamini basi unapaswa uyasome na kuyatafakari kila inapoitwa leo. Kwasababu Huu ndio uliokuwa mwenendo wa Yesu duniani. Akahesabiwa kumpendeza Mungu kabla hata hajaanza huduma yake ya kuhubiri, kwasababu aliishi aliyokuwa anayasema. Hivyo siri iliyopo hapa ni kwamba alikuwa anasema mwenendo wa maisha yake yalivyokuwa.

Na sisi pia tukitaka tufanane, na Kristo kimwenendo na tabia, basi tuzingatie sana, kuyaaishi haya tunayoyasoma katika sura hizi tatu yaani 5,6,7, Ni muhimu sana, sio kuimba “natamani kufanana na wewe”, lakini hatujui tunafananaje na yeye.

2) Hotuba ya Utume (Mathayo 10)

Katika mahubiri haya, Bwana Yesu aliwaita wanafunzi wake na kuanza, kuwapa maelezo ya namna ya kuhubiri kule atakapowatuma. Akawaeleza kwa upana jinsi mazingira ya kuhubiri yalivyo, kwamba kuna mahali pia hawatakubalika, akawafundisha pia jinsi ya kuhubiri, akawaondoa hofu ya wanadamu, na hofu ya kusumbukia mahitaji kwamba huko huko mbele ya safari Bwana atakuwa nao, akawafundisha pia mahali pa kuanzia kuhubiri, akawafundisha hekima ya kuhubiri, na kuponya watu. Na mambo mengine kadha wa kadha.

Kiasi kwamba, wewe kama mtendakazi katika shamba la Bwana ukisoma habari hizi, zitakusaidia katika ustahimilivu wako shambani mwa Bwana, tukikumbuka kuwa kila mmoja wetu ameitwa na Bwana kwenda kuwafanya wengine kuwa wanafunzi. Hivyo, Usomapo habari hii ya kitume, itakusaidia kunoa vema utumishi wako, katika eneo la upelekaji kazi ya Mungu mbali. Pata nafasi pitia wewe mwenyewe kwa utulivu sura yote ya kumi. Bwana atakupa kuelewa mengi ndani yake. Na hivyo utakuwa mtume, kama mitume wako walivyokuwa.

3) Hotuba ya ufalme wa mbinguni (Mathayo 13)

Hii ni hotuba, iliyohusu siri za ufalme wa Mbingu. Ambapo Bwana Yesu alitumia mifano (mafumbo), kuulezea. Biblia inaposema ufalme wa mbinguni, inamlenga YESU mwenyewe, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani (Luka 4:18-19).

Katika sura hii ya 13, alieleza mifano mikuu saba (7), japokuwa kulikuwa na mengine aliyokuwa iliyohusu ufalme wa mbinguni isipokuwa haijarekodiwa katika kitabu hichi. Mfano wa kwanza ulikuwa ni wa mpanzi, kisha magugu na ngano, kisha chembe ya haradali, kisha chachu katika unga, kisha hazina iliyositirika katika shamba, kisha mfano wa mfanyabiashara na lulu, na juya lililotupwa baharini.

Katika mifano hii yote, maudhui ni kuonyesha ukubwa ulio ndani ya Kristo Yesu, pale mtu anapomwamini na kustahimili kumfuata ukweli ni kwamba ataanza kama chenye ya haradali, lakini ataishia mti mkubwa, ni kama aliyepata hazina na lulu kubwa sana, akaenda kuuza akawa tajiri,.

Hivyo usomapo kwa makini mifano hii, utakuwa na kila sababu ya kuutafuta sana ufalme wa Mungu (yaani Kumuhufadhi Kristo sana moyoni mwako). Kwasababu unajua ulichokitapata ni zaidi ya vitu vyote duniani. Ambavyo utakuja kuvifurahia vema uendapo kule ng’ambo mbinguni.

4) Hotuba ya kanisa (Mathayo 18)

Hotuba hii inalenga, namna ya kuchukuliana sisi kwa sisi (Kanisa), tuliomwamini Yesu katika eneo la kujishusha na kunyenyekeana, kutokwazana, kutokupuuziana, lakini pia kuwa tayari kuwatafuta wale waliopotea na kuwarudisha kundini, ni muhimu sana, akatoa mfano wa mtu aliyeacha kondoo wake tisini na tisa, na kwenda kumtafuta Yule mmoja aliyepotea. Na sisi yatupaswa tuwe na moyo huo wa kichungaji.

Vilevile kusameheana sisi kwa sisi hata saba mara sabini akatoa mfano wa Yule mtu aliyesamehewa talanta elfu kumi, lakini yeye hakuwa tayari kumsamehe aliyemdai dinari mia, pia alifundisha njia nzuri ya kuonyana kingazi kufatana na utaratibu kwa kikanisa.

Hivyo usomapo hotuba hii, utafahamu namna ambavyo Bwana anataka sisi tuishi kama ndugu tuwapo pamoja kama kanisa lake.

5) Hotuba ya siku za mwisho (Mathayo 24)

Hii ni hotuba inayohusu, matukio yote ya siku za mwisho wa dunia, na kurudi kwa Yesu kutakavyokuwa, anaeleza kwa urefu dalili zake, mabadiliko ya kimwenendo ya watu, yatakavyokuwa, majanga ya asili, na vita vitakavyofuata baadaye, anatoa tahadhari ya manabii wa uongo, unyakuo wa kanisa, dhiki kuu na mapigo ya Mungu, Na mwisho anatoa angalizo ni nini tunapaswa tufanye. Kwamba “Tukeshe”, kwasababu hatujui siku wala saa.

Hotuba hii ni vizuri ukaisoma kwa urefu, na kuelewa kwa undani, kwasababu nyakati tulizopo sasa, tupo katika “mwisho wa siku za mwisho.” Dalili nyingi zilizotabiriwa zilishatimia. Jiulize umejiandaaje kwa yaliyo mbele yetu?

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, ufahamupo Mahubiri hayo (Hotuba), utapata uelewa wa undani kimaudhui ndani ya kitabu cha Mathayo, Jifunze kusoma sana, na kurudia rudia, hotuba hizi, kulikuwa na sababu kwanini Bwana atoe habari zake kwa urefu, kwasababu ndio “Fundisho” la mwamini. Zingatia hayo na Bwana akubariki.

Tutakuwa na uchambuzi wa vitabu vingine..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwa namna gani mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pake? (Zaburi 116:15).

Swali: Je ni kwamba Mungu anafurahia Mauti ya watu wake mpaka aseme hivyo?


Jibu: Turejee mstari huo…

Zaburi 116:15 “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake

Sasa ili tupate vizuri maana ya huu mstari hebu tuweke msingi kwa kusoma tena mstari ufuatao…

Ezekieli 33:11 “Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, SIKUFURAHII KUFA KWAKE MTU MWOVU; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?”

Kama Bwana hakufurahii kufa kwake MTU MWOVU, basi kinyume chake ni kweli!! kuwa “KUFA KWAKE MTU MWENYE HAKI ikiwa amemaliza kusudi lake duniani NI JAMBO LINALOMPENDEZA MUNGU”… Na Ndio hapo kwenye Zaburi 116:15 anasema “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake”.

Sasa kwanini MAUTI YA WENYE HAKI NI YA THAMANI MACHONI PA MUNGU?

1. DUNIANI NI MAHALI PA DHIKI.

Hii ndio sababu KUU..Duniani si mahali pa raha kwa “Wanaomcha Mungu”.. Kwa wengine wasiomcha Mungu panaweza kuwa mahali pao kwa raha ya kitambo..lakini kwa wacha Mungu si sehemu ya faraja hata kidogo..

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. ULIMWENGUNI MNAYO DHIKI; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Kutokana na kwamba ulimwenguni ni mahali pa dhiki, na tena pa mapito, ni mahali pa kutaabika kupambana na dhambi na kutaabika kuhubiri injili.. hivyo  MAUTI ni sehemu ya  mapumziko kwa wanaomcha Mungu kutokana na taabu hizo za ulimwengu…ndivyo maandiko yanavyosema..

Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA TANGU SASA. NAAM, ASEMA ROHO, WAPATE KUPUMZIKA BAADA YA TAABU ZAO; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

Hiyo ndiyo sababu kwanini KIFO ni sehemu bora kwa WANAOMCHA MUNGU KULIKO KUENDELEA KUSHI DUNIANI. Na Mkristo yeyote yule wa kweli, ni lazima atamani kuondoka katika haya maisha kuliko kuendelea kubaki hapa!!, ni lazima atamani kila siku ile siku ya unyakuo ifike, au siku ya kulala kwake (kufa) ifike akamwone Bwana.

Kitu pekee ambacho kinapaswa kutufanya tuendelee kutaka kubaki duniani ni “kuimaliza kazi yake”, (maana yake tusiondoke kabla ya kuimaliza kazi yake aliyotuitia, kwani kuna hatari ya kufa bila kuifanya kazi yake au kuimaliza).. na hakuna sababu nyingine tofauti na hiyo…

Ukiona unatamani uendelee kubaki duniani, ili uwe milionea, au ili uendeshe na kumiliki magari, au utengeneze majumba kwa fahari yako, kuna shida katika Imani yako!..(Ni muhimu kujipambanua upya).. wewe utakuwa wenyeji wako ni hapa duniani, sio mbinguni.

Walio wa mbinguni wanatamani ya mbinguni, na walio waduniani wanatamani, na kuwekeza, na kusifia vya duniani…

Wafilipi 3:20 “Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”

Soma pia 1 Petro 2:11 utaona jambo hilo, hivyo jihakiki ni nini kinakupa sababu ya wewe kuendelea kubaki hapa duniani?..ni vitu vya dunia hii au vile vijavyo?.

Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho aliandikia kuwa “kuishi kwake ni Kristo na kufa ni faida”,..Maana yake kusudi lake kuu la kuendelea kubaki duniani ni Kristo (yaani kufanya kazi Kristo aliyomuitia na kuimaliza)..Nje na hapo kufa ni FAIDA KUU!

Wafilipi 1:21 “Kwa maana kwangu mimi kuishi ni KRISTO, NA KUFA NI FAIDA.

22  Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.

23  Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana;

24  bali kudumu katika mwili kwahitajiwa zaidi kwa ajili yenu”.

Hapo anasema kudumu katika mwili (yaani kuendelea kuishi) kwahitajika kwaajili yao, na si kwaajili yake (maana yake kwaajili ya kuwahubiria wao injili).

Je mimi na wewe kubaki kwetu katika mwili kwahitajika kwaajili ya nini??…je ni kwaajili ya matumbo yetu, na tamaa, na anasa au kwaajili ya Bwana?..

Kumbuka pia, ni hasara kubwa sana kufa katika dhambi!.. na hakuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kutoka katika mateso ya moto wa jehanamu na kumingiza paradiso. (Hayo maombi hayapo usidanganyike).

Hakuna maombi yoyote ya Mchungaji, au Askofu, au Nabii, au Mtume, au Papa, au Padre, au Kadinali, au Mwalimu, au Rabi, au Mwinjilisti, au Kuhani au Malaika wa mbinguni…. yatakayomtoa mtu kwenye mateso ya moto wa jehanamu na kumwamisha kumwingiza peponi, Mtu akifa katika dhambi!, habari yake ndio imeishia hapo..

Bwana YESU Kwa kinywa chake mwenyewe ametupa tahadhari hiyo katika kitabu cha Yohana..

Yohana 8:24 “Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

Mistari ya biblia kuhusu kibali.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni kelele gani zinazozungumziwa hapo katika Waefeso 4:31.

Waefeso 4:31 “Uchungu wote na ghadhabu na hasira NA KELELE na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya”.

Kelele zinazozungumziwa hapo ni kelele za  “Maneno” , kelele za “Maombi” na kelele za “Nyimbo”

1.KELELE ZA MANENO.

Hizo ni zile kelele zinazotokana na malumbano yasiyo na msingi wa kiroho, au mashindano ya maneno. Watu wagomvi huwa wana kelele, watu wabishi huwa wana kelele, watu wakorofi huwa wana kelele, na yote ni matunda ya dhambi ambayo hayapaswi kuwa ndani ya mtu aliyeokoka.

2. KELELE ZA MAOMBI

Kuna mambo ambayo mtu akiomba ni kelele mbele za Mungu, na mfano wa hayo ni yale yasiyotokana na Neno, maana yake mtu anaomba kitu kwa tamaa zake na ambacho si mapenzi ya Mungu, na tena anatumia sauti kubwa, (maombi kama haya ni kelele mbele za Mungu na pia hayana majibu.)

Yakobo 4:3 “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

3. KELELE ZA NYIMBO.

Amosi 5:23 “NIONDOLEENI KELELE za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu”.

Si nyimbo zote ni kelele mbele za Mungu, zipo zinazomtukuza Mungu na wanaoimba pia wanamtukuza Mungu.. Lakini zipo nyimbo ambazo hazimtukuzi Mungu ingawa zina majina na sifa za kumtukuza Mungu,

Vile vile zipo nyimbo ambazo zina maneno mazuri ya kumtukuza Mungu, lakini wanaoimba ni watu wasio na mahusiano yoyote na MUNGU, nyimbo za namna hiyo ni KELELE mbele za MUNGU.

Vile vile nyimbo zenye midundo ya kidunia, lakini zina maneno ya kibiblia, hizo nazo ni kelele, na si kelele tu bali pia ni machukizo.

Jihadhari na kelele.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Rudi Nyumbani

Print this post

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

Amosi 5:23 “Niondoleeni KELELE ZA NYIMBO ZENU; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu”.

Je ni kwamba Mungu wetu hapendezwi na nyimbo tunazomwimbia??

Jibu ni la! Yeye anapendezwa na nyimbo na tena anaketi katika SIFA.

Zaburi 22:3 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli”.

Lakini kwanini aseme “niondoleeni kelele za nyimbo zenu?”… Ni wazi kuwa kuna nyimbo ambazo kwa Mungu ni kama kelele.

Sasa ni aina gani za nyimbo ambazo kwa Mungu ni kelele?.

1. NYIMBO ZA UNAFIKI.

Nyimbo za kinafiki ni zile mtu anazoimba kwa kupaza sauti, lakini maisha yake hayaendani na kile anachokiimba, kuanzia, uzungumzaji, uvaaji, utendaji na maisha yake yake siri. Mtu mwenye tabia hiyo halafu akasimama na kuimba nyimbo za kumtukuza Mungu, iwe ni nyimbo alizozitunga yeye, au za mwingine, mtu huyo anapiga kelele mbele za Mungu na hivyo anafanya dhambi.

2. NYIMBO ZENYE MIDUNDO YA KIDUNIA.

Kuna nyimbo ambazo zinafanana sana na za kidunia, kiasi kwamba mtu akisikiliza anafananisha na nyimbo Fulani ya kidunia ambayo alishawahi kuisikia mahali fulani. Nyimbo za namna hiyo ni kelele, na si kelele tu, bali pia ni machukizo… mfano wa hizo ni nyimbo aina ya rege, rap, pop, taarabu na nyingine zinazofanana na hizo, Nyimbo za namna hii zinajulikana kama nyimbo za upuuzi (Amosi 6:5). Hivyo wakristo hatupaswi kutumia midundo hiyo kumwimbia MUNGU.

3. NYIMBO ZINAZOSHIRIKISHA WASANII WA KIDUNIA.

Wasanii wa kidunia ni watu wanaoimba nyimbo za zinazotukuza na kusifia mambo ya ulimwengu huu, na ulimwengu upo chini ya shetani, sasa mtu anayewashirikisha waimbaji hao wa kidunia, waliozoea kumwimbia shetani, kisha wakapewa mashairi ya kumsifu Mungu pamoja na watu wa kiMungu, hizo ni kelele na machukizo mbele za Mungu, haijalishi nyimbo hiyo itakuwa na beti nzuri kiasi gani na ujumbe mzuri kiasi gani, au zenye kumsifia MUNGU kwa kiasi gani,  bado ni kelele mbele za Mungu na hazina matunda yoyote.

Nyimbo zenye kumtukuza Mungu ni zile zilizobeba ushuhuda wa Neno kuanzia kwa MWIMBAJI, beti na mdundo. Na zinapoimbwa zinamtukuza Mungu na kuwabariki wasikiao.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAONO YA NABII AMOSI.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?

Kuna wakati wa kukokotwa-kokotwa, lakini kuna majira ya  kuachwa ufanye maamuzi mwenyewe, na usipofanya unakufa. Mtu aliye mchanga kiroho, ni rahisi Mungu kuchukuliana naye katika mambo yasiyofaa kutokana na uchanga wake kwa siku zile za awali, lakini haiwezi kuwa hivyo siku zote, kwa jinsi siku zinavyokwenda, kusukumwa sukumwa hakutakuwepo, ni kuwa makini sana!.

Ukitafakari habari ya Mke wa Lutu, unaweza kupata picha halisi jambo hili lilivyo, yeye alidhani ataendelea kuvutwa-vutwa tu nyakati zote, lakini walipofikishwa mahali Fulani, nje kidogo ya mji wameshaijua njia, waliambiwa wajiponye wenyewe nafsi zao, lakini yeye akageuka nyuma, na wakati ule ule akawa jiwe la chumvi.

Mwanzo 19:15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 

16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, KWA JINSI BWANA ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji. 

17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, JIPONYE NAFSI YAKO USITAZAME NYUMA, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.

Hatari tuliyonayo sisi tuliopo katika siku hizi za mwisho, katika kanisa hili la Laodikia (Ufunuo 3:14-21), ni kwamba tunafahamu mambo mengi, na tumeshaona mifano mingi kwenye maandiko na kwenye historia, lakini geuko la dhati ndani ya wengi halipo, tukifikiri  tutalinganishwa na wale watu wa zamani. Neema kwako wewe haifanyi kazi katika kukokotwa tena, bali katika kukimbia. Ilifika wakati Yesu hakuwaambia tena wanafunzi wake “nifuate”, aliwaambia na “ninyi mnataka kuondoka?”

Halikadhali, kama umeshaokoka, jichunge sana, dhambi usiifanye rafiki kwako, ukidhani kila kosa tu utakalolifanya upo msamaha, acha hayo mawazo, unajitafutia kuwa mke wa lutu. Neno la Mungu linasema;

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

Ni kusimama imara, sio tena kumbelezewa injili, sio tena kukumbushwa-kumbushwa wajibu wako wewe kama mkristo, na kuambiwa kaombe, nenda ibadani, mtafute Mungu, acha anasa, soma biblia. Ni wakati wa kujitambua kuwa sasa umeshatolewa nje ya mji, changamka, zama ndani ya Kristo. Acha kuwa vuguvugu utatapikwa, zama hizi ni zama za uovu. Wokovu wa mawazo mawili sio sasa, neema hiyo haipo kwetu mimi na wewe siku hizi za mwisho. Injili ya maneno laini, isikupumbaze, fanya Imara uteule wako na wito wako.

Ufunuo 22:10  Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa

12  Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Kimbia, usiangalie nyuma.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! “majira na sheria” mpinga-kristo atakayokuja kubalisha ni kupindua siku ya sabato na kuwa jumapili?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

Jibu: Turejee,

Wagalatia 5:19  “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, UCHAFU, ufisadi,

20  ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21  husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Dhambi zote ni “uchafu” lakini zipo dhambi ambazo ni “chafu Zaidi”, hizo ndizo zinazoitwa “Uchafu” Mfano wa hizo ni zile zilizotajwa katika Mambo ya Walawi 18 na 20(Dhambi za kulala na mnyama na ndugu wa karibu).

Walawi 18:23 “Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; NI UCHAFUKO”.

Walawi 20:12 “Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo UCHAFUKO; damu yao itakuwa juu yao”.

Utaona dhambi nyingine zimetajwa tu kama ni “Machukizo” lakini hizi zimetajwa kama “Uchafuko” maana yake zimezidi machukizo.. Ni uchafu mkuu mbele za Mungu.

Kulala na Mnyama, ni uchafu, vile vile kulala na mama mkwe au baba mkwe ni uchafu..na wachafu wote hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Rudi Nyumbani

Print this post

Tirano alikuwa nani na darasa lake lilikuwaje? (Matendo 19:9)

Swali: Huyu Tirano tunayemsoma katika Matendo 19:9 alikuwa ni nani, na darasa lake lilikuwaje?


Jibu: Tuanzie kusoma mstari ule wa 8 hadi ule wa 11 ili  tuweze kuelewe vizuri..

Matendo 19:8  “Akaingia ndani ya sinagogi, akanena kwa ushujaa kwa MUDA WA MIEZI MITATU, akihojiana na watu, na kuwavuta katika mambo ya ufalme wa Mungu.

9  Lakini wengine walikaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia mbele ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi, akahojiana na watu kila siku katika DARASA YA MTU MMOJA, JINA LAKE TIRANO.

10  Mambo haya yakaendelea kwa MUDA WA MIAKA MIWILI, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.

11  Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida”.

Baada ya Paulo kuingia Efeso, aliingia katika sinagogi moja la wayahudi ili kuhubiri habari za BWANA YESU, na wachache waliamini na kuitii injili, lakini wengi walikaidi na hata kuitukana kabisa injili mbele ya watu wote..

Mtume Paulo alipoona kuwa wameikataa injili, aliliacha sinagogi hilo (la wayahudi) ambalo pengine lingekuwa ndio sehemu bora kwa watu kujifunzia habari za Bwana YESU, lakini kutokana na ubishi na ugumu wa watu wa sinagogi (wayahudi).. Paulo aliondoka pamoja na wale wachache walioamini (wanafunzi)..na kuhamia kwenye darasa lingine la mtu mmoja wa mataifa aliyeitwa TIRANO. (na kipindi ambacho Paulo alihudumu katika Sinagogi la wayahudi mpaka alipoondoka na kuhamia kwenye darasa la Tirano ni muda wa miezi 3)

Kumbuka hapo biblia inaposema “darasa la Tirano” inamaanisha “jengo” lililokuwa maalumu kwaajili ya kufundishia la mtu aliyeitwa Tirano.

Sasa swali huyu Tirano alikuwa nani?

Biblia haijaeleza kwa kina huyu Tirano alikuwa ni nani, lakini ni wazi kuwa alikuwa ni mmoja wa wayunani aliyeamini injili na hivyo akatoa darasa lake hilo liweze kutumika kama mahali pa kufundishia watu injili.. Kama tu Petro alivyoalikwa nyumbani kwa Simoni mtengeneza ngozi kule Kaisaria (Matendo 9:43).

Na mpaka atoe darasa hilo, maana yake hapo kwanza inawezekana alikuwa ni mwalimu wa Falsafa za Kiyunani (kwani wayunani walikuwa ni watu wasomi na wenye kutafuta elimu sana).

Na baada ya Paulo kuhama kutoka kwenye lile Sinagogi na kuhamia kwenye darasa hilo la Tirano, injili ilipata mafanikio makubwa sana, kwani baada ya miaka miwili tu, Watu wote wa Asia waliisikia injili na kuitii..

Matendo 19:10 “Mambo haya yakaendelea kwa MUDA WA MIAKA MIWILI, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.

11  Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida”.

Ikifunua kuwa kuna mambo au mifumo ndani ya masinagogi (au madhehebu) ambayo inazuia kutembea kwa Roho Mtakatifu, zipo tabia ambazo zinazuia injili kusambaa, ipo mienendo inayokinzana na nguvu za Roho Mtakatifu kutembea.. na mojawapo ya hiyo ni tabia ya kupingana na Neno la Mungu (kama ilivyokuwa kwa hawa wayahudi ndani ya Sinagogi)..walikuwa wanashindana na Paulo kutwa kuchwa.

Walikuwa wanaikejeli injili, hata kama wanaona kinachohubiriwa ni kweli kabisa..

Na hata katika madhehebu na makanisa leo ni hivyo hivyo, utakuta mtu au kiongozi anaweza kuiona kweli lakini bado akashindana nayo na kuipinga!..Kiongozi anaweza kuona jambo Fulani sio sawa lakini bado akalipalilia, na kushindana na ile kweli, watu wanaweza kufunuliwa maandiko lakini bado wakawa hawabadiliki wapo vile vile, bado maisha yao ni yale yale NA KWA MATENDO YAO WANAITUKANA INJILI (ingawa midomo yao inakiri).. mambo hayo yanazuia injili kusambaa na kutembea kwa Roho Mtakatifu.

Bwana atusaidie tuzidi kutembea katika kweli yake.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Sinagogi kufumakana maana yake nini? (Matendo 13:43).

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Rudi Nyumbani

Print this post

UTAJUAJE UFAHAMU WAKO UMECHUKULIWA?

Swali: Utajuaje ufahamu wako umetekwa au ni viashiria gani vitakavyotambulisha kuwa ufahamu umetekwa na adui?


Jina la Bwana YESU libarikiwe.

Kabla ya kujipima kama ufahamu umechukuliwa au la!..Ni vizuri kwanza tukajua kibiblia mtu mwenye ufahamu anatafsiriwaje?

Turejee kile kitabu cha Ayubu 28:28.

Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU

Kwahiyo kumbe Mtu anayeweza kujitenga na Uovu ndiye mwenye ufahamu…maana yake kinyume chake yule asiyeweza kujitenga na uovu hana Ufahamu…au kwa lugha nyingine “UFAHAMU WAKE UMETEKWA”.

Na hapo neno linasema “kujitenga na uovu” na sio  “kujizuia na uovu”… maana yake “unakaa nao mbali”... Kama ni ulevi mtu anakaa nao mbali, kuanzia mazingira ya kulewa mpaka makundi ya walevi (wote anajitenga nao).

Kama ni uasherati na uzinzi, mtu anakaa nao mbali kuanzia mawasiliano, mavazi, makundi…vile vile anajitenga na mazingira yote yanayochochea hiyo dhambi ikiwemo mazungumzo na mitandao.

Kama ni usengenyaji, mtu anajitenga na mazingira hayo na makundi yote..

Kama ni utukanaji vivyo hivyo, Kama ni wizi/ufisadi au utukanaji na hasira ni hivyo hivyo..

Lakini kinyume chake mtu asiyeweza kujitenga na hayo yote basi UFAHAMU WAKE UMECHUKULIWA (UMETEKWA)!!...Upo chini ya Milki ya mkuu wa giza. Anatumikishwa na mamlaka za giza.

Haijalishi kama ni mchungaji, au askofu, au Nabii, au Mtume, au mwimbaji wa kwaya, au Papa, au Raisi wa nchi, au mtu mwingine yoyote mwenye kuheshimika katika jamii au kanisa.

Mtu asiyeweza kujiepusha na UOVU  ufahamu wake haupo (Umefungwa na kamba za kuzimu)., haijalishi ana uwezo mkubwa kiasi gani wa kupambanua mambo ya kimwili, haijalishi ana elimu kubwa kiasi gani na anategemewa na watu wengi kiasi gani katika kutatua mambo…bado ufahamu wake haupo!.

UTAURUDISHAJE UFAHAMU WAKO?.

Hakuna mtu ambaye kwa nguvu zake ana uwezo wa kuurudisha ufahamu wake!… Isipokuwa kwa msaada wa Mungu tu…Na msaada huu unaanza pale tunapoamua kufanya mageuzi katika maisha yetu kwa kutubia dhambi zetu na kumkiri Mwokozi YESU.

Ambapo kama tutatubu kwa kumaanisha kweli basi atatupa kipawa cha Roho wake mtakatifu ambaye kupitia huyo basi ataurejesha ufahamu uliochukuliwa na ile nguvu ya kuushinda uovu na kujitenga nao itakuwa juu yetu.

Faida ya kwanza ya ufahamu wa mtu kurudi ndani yake ni UZIMA WA MILELE lakini pia UZIMA WA MAISHA ya duniani, kwani ufahamu wa roho ndio unaofungua kufahamu mambo mengine yote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post