Ushindi wa kwanza wa vita vya kiroho unaanza na “kukataa”.. Na kukataa kunaanza katika “moyo”, na kunaishia katika “kinywa”.. Unapoukiri udhaifu ndivyo unavyopata Nguvu juu yako vile vile unapoukiri uzima ndivyo navyo unavyopata nguvu juu yako.
Vile vile unapoukataa Udhaifu wa adui, ndivyo unavyokosa nguvu juu yako…Ndivyo biblia inavyotufundisha kuwa Uzima na Mauti vimewekwa katika uwezo wa ndimi zetu,
Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”
Ndio maana hata wokovu tunaupata kwa kanuni hiyo, Kwanza “kuamini moyoni” pili “kukiri kinywani”
Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.
Kwahiyo daima katika maombi yako usisahau hilo kuwa “moyo na kinywa” vinashirikiana na vina nguvu..
Hivyo unapokuwa katika sala au hata nje ya sala… hakikisha siku zote unakataa moyoni mwako na katika kinywa chako Mahubiri yote ya shetani, na kazi zake anazozielekeza juu yako.
> Maana yake Unakataa “Dhambi juu ya maisha yako”.. na zenyewe zitaisha nguvu
> Unakataa “Hofu na mashaka kutoka kwa ibilisi”… na yenyewe yataisha nguvu.
> Unakataa “Magonjwa na maradhi ya ibilisi”…. na yataisha nguvu juu yako.
> Unakataa “shida na tabu za ibilisi”.. na zenyewe zitaisha nguvu..
> Unakataa “Maazimio yote ya ibilisi yaliyokusudiwa juu yako”… na yenyewe yataisha nguvu.
> Unakataa “Maneno na ratiba zote za adui juu yako”..nazo zitafutika kabisa..
> Unakataa “kuitwa majina yote ya kiMisri uliyokuwa unaitwa huko nyuma au unayoendelea kuitwa sasa”.. na yenyewe yataisha nguvu juu yako..
Kama zamani ulikuwa kahaba, basi sasa baada ya kuokoka unakataa hayo majina, kama ulikuwa unaitwa au unajiita jambazi, au mhuni fulani au mwizi, au jina lingine lolote la kihuni na lisilo na maana unakataa hayo majina kwamaana majina nayo yamebeba roho (soma 1Samweli 25:25).
Biblia inasema Musa alipokuwa mtu mzima alikataa kuitwa Mwana wa binti Farao.. Hivyo ushindi wake wa imani ulianzia hapo..
Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, AKAKATAA KUITWA MWANA WA BINTI FARAO
25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.”
Kwanini Musa alikataa kuendelea kuitwa “Mwana wa binti Farao”?.. Ni kwasababu wana wa binti za Farao walikuwa wanajulikana ni watu “kuabudiwa kama miungu” pia wàtu“wenye kiburi/majivuno/majigambo” na “wauaji wenye uwezo wa kufanya jambo lolote ovu na wasiulizwe na mtu”..
Na akajua endapo akiendelea kuitwa hivyo Mwana wa binti Farao, bado hizo tabia zao zitaendelea kukaa ndani yake na kumtumikisha, hivyo akakataa hicho cheo..na kujitoa katika ile nafasi.
Inasikitisha mtu baada ya kuokoka bado anaona ni sahihi kuitwa sistaduu, au brazameni, au bishoo, au Demu, au DJ, au jina lingine lolote la kihuni tu!.. Ni lazima uyakatae hayo majina kwa kinywa chako, na pia ubadilike ili kukataa kwako kuendane na mwenendo wako.. lakini kama utakataa kinywani lakini muonekano wako unasema wewe bado ni yule yule mtu wa kale, bado itakuwa haina maana!.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?
nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?
Swali: Je kuna roho ya kukataliwa katika biblia?.. na kama ipo je mtu anawezaje kufunguliwa kutoka katika hiyo roho?
Jibu: “Kukataliwa” kwa lugha nyingine ni ile hali ya “kukosa kibali”.
Mtu anaweza kukosa kibali “kwa Mungu” au “kwa wanadamu”.
1. KUKOSA KIBALI KWA MUNGU.
Sababu kuu ya Mtu kupoteza kibali (kukataliwa) na Mungu ni “DHAMBI/MAOVU”. Dhambi inapoweka mizizi katika maisha ya mtu inampotezea kibali kwa Mungu.. Mtu huyu anaweza kumwomba Mungu na asione majibu anayoyategemea…anaweza kupambana na asione matokeo ya kile anachokipambania.
Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, HATA HATAKI KUSIKIA”.
Mfano wa mtu aliyepoteza kibali mbele za Mungu na kuwa mtu wa kukataliwa mbele zake ni Mfalme Sauli (1Samweli 16:1) na pamoja na Kaini (Mwanzo 4:10-12).
Sasa mtu anapopoteza kibali cha kiMungu vilevile hawezi kupata kibali kwa watu, hivyo atakuwa mtu wa kukataliwa na watu sahihi (lakini anaweza kukubalika na watu wasio sahihi, jambo ambalo ni hatari kubwa). Mfano wa watu hao katika biblia ni Kaini..
Mwanzo 4:10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; HATA ITAKUWA KILA ANIONAYE ATANIUA”
Umeona hapo?..Kaini alijua madhara ya “kukataliwa na Mungu” ni “kukataliwa na watu pia”… ndio maana anasema “watu watakapomwona watamwua”.
Kwahiyo DHAMBI au MAASI ndio msingi mkubwa wa mtu kupoteza kibali. Na kwasababu dhambi zote zinaasisiwa/kuchochewa na roho ya Ibilisi na mapepo yake, hivyo basi ni sahihi kabisa kusema kukataliwa ni roho..
Kwahiyo mtu anapojigundua kuwa kila mahali hakubaliki, anakataliwa na kila mtu, na hata wakati mwingine hajui sababu… ni muhimu kulitafakari hilo kwa jicho la pili, kwasababu ni roho ipo nyuma yake inayopalilia dhambi juu ya maisha yake, ambayo matokeo yake huyo mtu ni kukatalika kwa kila anayemwona, au kila anachokipanga..
Hivyo suluhisho pekee la kuiondoa hiyo roho ya kukataliwa ndani ya mtu ni KUOKOKA KIKWELI KWELI.. Na maana ya kuokoka ni KUACHA DHAMBI!!!.. Mtu anayetaka kuokoka lakini hataki Kuziacha dhambi zake, hataki kuacha uzinzi, ulevi, wizi, usengenyaji, matukano, kutokusamehe, chuki, wivu, usengenyaji, fitina n.k hawezi kupokea wokovu mkamilifu. Lakini anayetubu kwa kudhamiria kuziacha dhambi zake ndiye anayepokea wokovu mkamilifu.
Na matokeo ya kupokea wokovu mkamilifu ni kuondoa roho ya kukataliwa ndani yako, na si tu roho ya kukataliwa bali na roho nyingine zote ambazo zimekaa ndani yako zinazochochea tabia na mienendo mingine isiyofaa.
Je umeokoka?
Kama bado na unatamani kufanya hivyo basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu kwa msaada Zaidi au ukafuatiliza sala hii >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mistari ya biblia kuhusu kibali.
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
JIBU: Yesu ni mtu ambaye alizungukwa na makutano mengi, hivyo isingekuwa rahisi kwao kumkamata wakati wa mchana, kwasababu walijua watakutana na upinzani mkubwa wa makutano.. kama maandiko yanavyosema katika vifungu hivi;
Mathayo 21:45-46
[45]Wakuu wa makuhani na Mafarisayo, waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao.
[46]Nao walipotafuta kumkamata, waliwaogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii.
Hivyo njia pekee, ilikuwa ni usiku. Tena wakamwendea na marungu na mapanga kujidai kuwa wanakwenda kumtafuta mwizi, huku mioyoni mwao wakijua kabisa wanayekwenda kumfuata ni mtu wa haki.
Na hiyo ni kuthibitisha kwamba walikuwa hawajiamini kwa matendo yao, kwasababu waliyajua ni maovu ndio maana waliyafanya gizani.
Marko 14:48-49
[48]Yesu akajibu, akawaambia, Je! Ni kama juu ya mnyang’anyi mmetoka wenye panga na marungu, kunitwaa mimi? [49]Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia.
Hiyo ndio sababu kwanini wamfuate usiku, lakini hawakujua ndio walikuwa wanairahisisha njia ya wokovu. Kufunua kuwa giza kamwe haliwezi kuishinda nuru.
Yohana 1:4-5
[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
Mwamini Kristo, Nuru yake ikuangazie moyoni mwako.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?
Yesu kuvishwa taji la miiba kichwani, kulifunua nini?
Kwa kiyahudi huitwa ‘Tevat’, ni chombo cha majini kilichotumika mahususi kwa ukombozi. Ni mfano wa meli iliyotumika kuokoa watu/wanyama kutoka katika maangamizi fulani. Kwamfano katika biblia tunaona Nuhu aliagizwa atengeneze safina, ambayo ataingia yeye pamoja na familia yake, na wanyama wa nchi.
Ukisoma Mwanzo 6-8, utapata kufahamu vipimo vya safina hiyo vilivyokuwa na vigezo vyake, japokuwa biblia haijatueleza mahususi umbo la chombo kile kilivyokuwa.
Lakini pia wakati Musa anazaliwa, tunaona wazazi wake walimtengeneze a naye kisafina kidogo, akafichwa ndani yake, ili kunusuriwa na maangamizi ya Farao.
Kutoka 2:1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi.
2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu.
3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto.
Jambo la muhimu kufahamu ni kuwa safina hizo ilikuwa ni lazima zipakwe LAMI ndani na nje. Lami hizo ni mfano wa gundi nzito zilizopakwa, lengo lake likiwa ni kuzuia maji yasiweze kupenya sehemu yoyote ndani ya Safina, (Mwanzo 6:14, Kutoka 2:3). Safina zilikuwa na sifa kama za “nyambizi” tulizonazo sasa, ambazo hazihathiriwi na maji mahali popote ziwapo juu au chini ya maji.
Ni Kristo Yesu, yeye ndiye mwokozi wetu dhidi ya ghadhabu ya Mungu juu ya ulimwengu huu kwa wenye dhambi. Na DAMU yake ndiyo ile LAMI. Inayonyunyizwa kwetu sisi. Mtu yeyote ambaye hajamwamini Yesu, ni dhahiri kuwa ghadhabu ya Mungu ipo juu yake, hawezi kuiepuka. Kwasababu amekataa msamaha wa dhambi, tuliopewa bure kwa kifo chake pale msalabani.
Je! Unaichezea neema? Kumbuka ulimwengu huu unafikia mwisho. Kristo amekaribia kurudi, kuwanyakua watu wake. Je! Bado upo kwenye dhambi? Ikiwa utataka kuupokea wokovu leo bure, basi uamuzi huo ni bora kwako, Hivyo waweza, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala hiyo ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)
Unaweza kuuliza je! Mwamini anaweza kufungwa na adui?. Jibu ni ndio anaweza kufungwa. Utauliza tena, kama anafungwa sasa kazi ya Yesu msalabani ilikuwa ni nini ikiwa hajawekwa huru kweli kweli.
Jibu ni kwamba mwamini yeyote, hawezi kuwa na kifungo katika roho yake, yaani hawezi kufungwa roho aidha na mapepo, au wanadamu au chochote kile. Hawezi kuwa na laana yoyote ndani yake, aidha ya ukoo au ya mabibi. Kwasababu yeye ni mbarikiwa amewekwa huru na Yesu, na ndio kazi Yesu aliyokuja kuifanya kuwaweka huru walioonewa na ibilisi.Hivyo mtu yeyote aliyemwamini Yesu kwa ‘TOBA’, ubatizo na kupokea Roho. Huyo hana kifungo chochote kwasababu uhai wake unakuwa umefichwa ndani ya Kristo.
Lakini Shetani anauwezo wa kumzuia, katika mambo mengi, asipojua ni nini anapaswa afanye. Na hicho ndicho kifungo cha nje akifanyacho adui. Kukuzuia wewe mwamini, ndicho alichokifanya kwa Paulo wakati Fulani alipotaka kwenda kuhubiri injili kwa Wathesalonike akasema shetani alinizuia (1Wathesalonike 2:8).
Lakini pia tunamwona Mtume mwingine aliyeitwa Petro.
sasa hebu tuangalie kisa hiki kwenye maandiko Kilichomhusu yeye, tuone ni maeneo gani huwa adui analenga mahususi.
Matendo 12:4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.
5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
6 Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakalilinda gereza.
7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika kule chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. MINYORORO YAKE IKAMWANGUKA MIKONONI.
8 Malaika akamwambia, Jifunge, KAVAE VIATU VYAKO. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, JIVIKE NGUO YAKO, ukanifuate.
9 Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.
Umeona maeneo aliyofungwa Petro?
Wafungwa wa zamani, ilikuwa ili aitwe mfungwa, ni lazima mambo hayo matatu yakamilishwe juu yake; nayo ni.
1) Kufungwa, Minyororo mikononi
2)Kuondolewa Mavazi, na kupewa mengine ya gerezani.
3)Kuondolewa viatu miguuni
Na hiki ndicho kitu anachokifanya pia adui kwa mwamini. Anaanza kwa kukufunga mikono yako rohoni, kisha kuyaondoa mavazi yako, na mwisho viatu vyako miguuni. Baada ya hapo unakuwa tayari huna nguvu ya kumshinda.
Mikono ni nini?
Ni “maombi na mifungo”
Mikono ni viungo mama katika mwili. Husaidia viungo vingi kufanya shughuli zake. Silaha hushikwa na mikono, hata ngumi hurushwa kwa mikono. Hivyo adui anajua akizuia mikono yako. Huwezi kufanya lolote. Mikono ya mwamini, ni “maombi na mifungo”.
Mtu ambaye ni mwombaji, kiwango cha Roho ndani yake huwa ni kikubwa, na hivyo hakuna mnyororo wowote, unaoweza kumshika. Ndio maana utaona baada ya kanisa kumwombea Petro kwa juhudi, akafunguliwa. Vilevile Paulo na Sila walipokuwa wamefungwa kipindi kile, hawakulala tu, bali usiku wa manane walikuwa wakiomba, na matokeo yake vifungo vikawaachia.
Matendo 16:25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26 Ghafla pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.
Umeona, maombi, huondoa minyororo mikononi. Kuwa mwombaji, uzishinde nguvu za mwovu. Shetani anawaogopa waombaji
Mavazi ni nini?
Ufunuo 19:8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu
Mavazi, ni matendo mema. Ukikosa matendo mema,(Utakatifu), si rahisi kumshinda adui, utakuwa mwamini asiye na matunda yoyote, itaishi tu kama mwanadamu ambaye anamapungufu ya akili rohoni, hutaweza kufanya lolote.Ndani una makunyanzi, mawaa, ambazo katika hizo shetani anakuwa na haki ya kukulaumu.
Ishi kama mkristo, ukiwa rafiki wa dunia, fahamu kuwa unajifanya adui kwa Mungu moja kwa moja. Nuru yako isipoangaza nje, huwezi mshinda shetani. Ni lazima uwe kikombe safi, nje na ndani. Huwezi kusema umeokoka halafu matendo yako hayaendani na imani yako.Unajidanganya, bado hujaifahamu neema ya Mungu.
Miguu ni nini?
Waefeso 6:14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani.
Miguu ni utayari, wa kuhubiri. Adui anapenda kukawiisha nia za watu, kwa kuwavuta katika mambo yao mengine, na kusahau yaliyo ya msingi kwao, ndio hapo atawasonga kwa anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu. Na mwisho wa hapo wanabakia kuwa hawana matunda.
Hivyo ndugu uliyeokoka, usiruhusu adui kukuzuia popote. Jijengee desturi ya kuwa mwombaji wa kila siku. Mikono yako isifungwe. Penda kuishi maisha matakatifu, vazi lako lisibadilishwe, kuwa tayari kuhubiri injili wakati wowote, ukifaao na usiokufaa, epuka udhuru wa mwili au kazi, pinga sana hapo jiwekee ratiba yako, ili upate sehemu ya kuwaeleza wengine habari za Yesu Kristo anayewaokoa wanadamu.
Tukizingatia hayo. Tutakuwa tumemshinda shetani ndani na nje. Hatujafungwa ndani wala nje.
Bwana akubariki
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)
Swali: Njia ya msalaba ni nini na Ipi historia ya njia ya msalaba?
JIBU..
Njia ya Msalaba ni Desturi iliyoanzishwa na kanisa Katoliki ambapo waumini wanapita katika mitaa ile Bwana YESU aliyosulubiwa, kuanzia alipotoka kwa Pilato mpaka mwili wake ulipowekwa kaburini.
Kulingana na kanisa Katoliki, kuna vituo 14 ambavyo Bwana YESU alipitia, ambapo kila inapofika Ijumaa kuu (ile ya pasaka) wakatoliki hupita katika vituo hivyo huko YERUSALEMU kuanzia mahali pajulikanapo kama “ngome ya Antonia” mpaka “kanisa la Roma la ufufuo” (karibia na mahali ambapo Kaburi la Bwana YESU lilikuwepo)..matembezi hayo ni ya mita 600.
Na wale wasiokuwepo Israeli basi watapita karibu na picha kumi na nne (14) zilizochorwa katika kuta za makanisa hayo ya Roma na kusema baadhi ya sala.
Vifuatavyo ni vituo hivyo kulingana na kanisa katoliki.
1. Yesu anahukumiwa kuuawa.
2. Yesu anapewa msalaba na maaskari wa kiroma
3. Yesu anaanguka chini kwa mara ya kwanza.
4. Yesu anakutana na mama yake (Mariamu)
5. Simoni Mkirene anashurutishwa kuubeba msalaba wa Yesu.
6. Veronika anapangusa damu katika uso wa Bwana Yesu.
7. Yesu anaanguka kwa mara ya pili.
8. Yesu akutana na wanawake wa Yerusalemu.
9. Yesu anaanguka mara ya tatu
10. Yesu anavuliwa mavazi yake
11. Bwana Yesu anagongomelewa msalabani
12. Yesu anaisalimu roho yake
13. Mwili wa Bwana Yesu unaondolewa msalabani.
14. Mwili wa Bwana Yesu wawekwa kaburini.
Hivyo ndivyo vituo 14, Bwana Yesu alivyovipitia kulingana na kanisa katoliki.
Lakini vituo baadhi hapo hatuvioni katika maandiko, kwamfano kituo cha 3,7 na 9 cha Bwana YESU kuanguka chini mara ya kwanza, na ya pili na ya tatu havipo katika maandiko..
Vile vile kituo cha 6 kinachomtaja Veronika kufuta damu katika uso wa Bwana YESU hakipo katika biblia..na hata kituo cha 4 cha Bwana YESU kukutana na mama yake hakipo katika biblia!.
Hivyo kama habari hizo hazipo katika biblia hatupaswi kuziamini wala kuzishika kwani huenda ni habari za kutungwa! au zimetolewa katika vyanzo visivyo sahihi, ambavyo havijahakikiwa na Roho Mtakatifu.
Kitabu cha biblia chenye vitabu 66, hiyo ndiyo iliyohakikiwa na Roho Mtakatifu lakini vitabu vingine nje na hivyo vya kwenye biblia ni potofu na vina udanganyifu.
Na Zaidi hatujapewa amri ya kuadhimisha vituo vya Bwana YESU alivyopitia, ndio! Tunaweza kutafakari lakini si kufanyia ibada,..sala za namna hiyo ni ibada za sanamu, kwani zinamfanya mtu aanguke katika zile picha au katika ile mitaa huko Yerusalemu, jambo ambalo ni machukizo.
Kufahamu njia ya Msalaba hasa kibiblia ni ipi fungua hapa >>> NJIA YA MSALABA
Shalom..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.
Matuoni ni nini katika biblia?
MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.
UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.
Swali: Muujiza wa kwanza wa Bwana YESU ulikuwa ni upi?
Jibu: Mwujiza wa kwanza wa Bwana YESU ni ule wa Kana ya Galilaya, ambapo aligeuza maji kuwa Divai.
Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.
7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.
8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.
9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,
10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.
11 MWANZO HUO WA ISHARA YESU ALIUFANYA HUKO KANA YA GALILAYA, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”.
Mstari huo wa 11 unatudhihirishia wazi kuwa hiyo ndio iliyokuwa ishara ya kwanza kufanywa na BWANA YESU mbele ya wanafunzi wake.
Sasa kujua kwa mapana ujumbe uliopo nyuma ya muujiza wa kwanza wa Bwana YESU wa Kana ya Galilaya fungua hapa >>Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI NINI BWANA ANATAKA KUTOKA KATIKA MUUJIZA ALIOKUFANYIA?
JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?
Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)
Swali: Kuna nini katika Divai mpaka Bwana YESU ayageuze maji kuwa Divai?
Jibu: Hakukuwa na chochote maalumu au cha kipekee katika Divai.
Sababu ya Bwana YESU kuyageuza maji kuwa Divai na si kinywaji kingine ni kwasababu ndicho kinywaji kilichokuwa kimepunguka pale! (Kulingana na zile taarifa alizoletewa na mama yake).. Endapo kama ingekuwa ni chakula ndicho kilichopunguka basi Bwana YESU angefanya muujiza wa chakula kuongezeka cha kuutosha ule umati wote, huenda angefanya muujiza kama ile ya Mikate na Samaki, alipolisha maelfu ya watu. (Marko 6:38-44 na Luka 9:13-17).
Sasa kabla ya kuangalia ni ujumbe gani tunapata kwa mwujiza ule, hebu kwanza tuangalie matokeo ya kukosa Divai katika ile Harusi.
Kufahamu kwa kina matumizi ya Divai katika biblia fungua hapa >>MATUMIZI YA DIVAI.
Kulingana na Desturi za kiyahudi ilikuwa ni aibu kubwa sana arusi ikose Divai, au chakula…Hivyo ni aibu kubwa sana kwa wanafamilia, sawasawa tu sasa sherehe ikipungukiwa na chakula inakuwa ni aibu kubwa kwa walioandaa na huzuni na karaha!..
Sasa kitendo cha Bwana YESU kubadili yale maji na kuwa Divai, tena yenye kuwatosha watu wote ni kitendo KILICHOWAONDOLEWA AIBU WANA ARUSI NA WAZAZI.. vile vile ni kitendo kilichowaondolewa huzuni, na masononeko na fadhaa.. na ni kitendo kilichowapa heshima. Ndio maana utaona yule mkuu wa Meza alimfuata Bwana arusi kumsifu badala ya Bwana YESU.
Sasa ni ujumbe gani mkuu tunaupata hapo?
Ujumbe mkuu si upekee wa Divai.. bali ni Faida ya BWANA YESU ndani yetu au katikati yetu. Kuwa yeye anapoingia ndani yetu anazichukua aibu zetu, na fadhaa zetu na masikitiko yetu, na kutuheshimisha na kutuondolea aibu zetu..
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Unauona upendo wa YESU kwetu pale tunapomkaribisha na kumtwika fadhaa zetu?.. Wale wanaharusi waliona thamani ya YESU na kumwalika katika sherehe yao, na pale walipopungukiwa ndipo Kristo alipozuchukua fadhaa zao na aibu yao..
Wenye harusi , (wao hawakumwalika Bwana kwasababu walijua divai itaisha ili baadaye wamwite awageuzie maji kuwa Divai).. La! Ile ilitokea tu kama dharura na ndipo Bwana akafanya miujiza.. Wao lengo lao kubwa lilikuwa ni kumwitaji YESU ndani ya harusi yao, na si wamtumie.
Na sisi leo hatupaswi kumfuata BWANA YESU kwasababu tu tunataka uponyaji, au heshima au kuinuliwa kimaisha (watu wote waliomfuata Bwana YESU kwa haja kama hizo aliwakimbia Soma Yohana 6:25-26)..Lakini tumfuate Bwana YESU kwasababu tunataka uzima kwanza, na kuyafanya mapenzi yake na hayo mengine yawe ni dharura tu, kama wale waliomwalika.
Ukishahikiki kwamba uzima upo ndani yako, ndipo tumtwike hayo mengine..
1Petro 5:7 “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.
Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.
WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.
Bwana YESU KRISTO alizaliwa katika Nchi/Taifa la ISRAELI, lililopo mashariki ya kati. Na mji aliozaliwa ni Bethlehemu ambao ulikuwa katika urithi wa kabila la YUDA.
Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.
Pamoja na kwamba Bwana YESU alizaliwa Bethlehemu kulingana na unabii huo wa Mika, lakini hakulelewa katika huo mji wa Bethlehemu badala yake wazazi wake waliishi mahali palipojulikana kama NAZARETI, Mji mdogo sana uliopo kaskazini mwa Taifa hilo la Israeli, na huko ndiko Kristo alikokulia, ndio maana mahali pengine anajulikana kama Mnazorayo (yaani mtu wa Nazareti).
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.
Lakini pia Mji huo wa Nazareti ulikuwa ndani ya Wilaya iitwayo Galilaya, wakati mji wa Bethlehemu aliozaliwa Bwana YESU ulikuwa katika Wilaya iliyoitwa Yudea au Uyahudi.
Wilaya ya Galilaya ndio uliyojumuisha miji mingine midogo midogo kama Kapernaumu na Korazini na Bethsaida, ambapo wanafunzi wengi wa Bwana YESU walitokea katika hiyo miji, na ndio miji ambayo iliona miujiza mingi ya Bwana YESU lakini haikutubu (Mathayo 11:21)…. Wakati Wilaya ya Uyahudi ndio iliyobeba miji ya Bethlehemu pamoja na Yerusalemu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba BWANA YESU alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi na kulelewa Nazareti ya Galilaya, na alifia YERUSALEMU na kuzikiwa hapohapo, na kufufuka hapo hapo YERUSALEMU. Na sasa yupo hai na atarudi tena mara ya pili na siku hizo zimekaribia kulingana na unabii wa biblia.
Je umeokoka?
Bwana YESU ANARUDI.
Kama unatamani kuokoka basi fuatiliza sala hii >>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?
Raheli aliwalilia vipi watoto wake?
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA
Jibu: Turejee,
Walawi 19:32 “Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana”.
Maana ya kumwondokea ni “kumsogelea au kumkaribia ili kumsikiliza”. Hivyo biblia iliposema mwondokeeni mtu mwenye mvi, maana yake “tumsogeleeni mtu mwenye mvi na kumsikiliza”..
Na kwanini tumsogelee mtu/watu wenye mvi?..Ni kwasababu “kuna hekima katika wazee, kwani wameishi muda mrefu na kukutana na mengi na kujifunza mengi”. (wazee walio ndani ya KRISTO).
Ayubu 12:12 “Wazee ndio walio na hekima, Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu”.
Soma pia Ayubu 32:6-7 na Mithali 23:22.
Hivyo ukitaka mashauri sahihi kuhusu maisha basi watafute walio na mvi, (yaani wazee) walio ndani ya Kristo, watakuambia au ukutahadharisha na mengi…
> Vile vile ukitaka maarifa na ushauri sahihi kuhusu ndoa, kazi au elimu watafute wenye mvi walio ndani ya KRISTO watakushauri na kukutahadharisha mambo yaliyo sahihi na yale yasio sahihi.
> Vile vile ukitaka mashauri sahihi ya kiroho watafute wenye mvi za kiroho watakushauri mambo sahihi.
Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo, wenye mvi wanafahamu Zaidi kuliko vijana.
Lakini hasemi tu! Kumwondokea mwenye mvi… bali pia anasema “heshimuni uso wa mzee”. Maana yake mzee/wazee wanapaswa kuheshimiwa sana…. ni kosa kumvunjia mzee heshima, hata kama kafanya jambo lisilo sahihi mbele ya macho yako. Si ruhusa kumkemea mzee kama wanavyokemewa vijana au watoto.
1Timotheo 5:1 “Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;
2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.
HATA WAKATI WENU WA MVI NITAWACHUKUENI. (Isaya 46:3)
UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?