Swali: Tunaona sehemu moja Bwana YESU akimshuhudia Yohana Mbatizaji kuwa yeye ndiye Eliya ajaye (Mathayo 11:14), lakini sehemu nyingine Yohana Mbatizaji anakataa jambo hilo kuwa yeye si Eliya, (Yohana 1:19-21) je ni yupi yupo sahihi, Bwana Yesu au Yohana Mbatizaji?.. au je biblia inajichanganya?
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 11:13 “Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana. 14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja”.
Mathayo 11:13 “Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
14 Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja”.
Ni kweli hapa Bwana YESU anasema “Yohana Mbatizaji ndiye Eliya ajaye”. Lakini kumbuka kuwa Bwana YESU hakumlenga Eliya kama Eliya, kwamba atarudi tena na kutokea duniani kuhubiri!.. La! Bali alimaanisha “roho ya Eliya/ huduma ya Eliya” ipo ndani ya Yohana Mbatizaji.
Ni sawa na kwenye ule mfano wa Lazaro na Tajiri Bwana YESU aliowaambia watu, pale Ibrahimu aliposema “Wanaye Musa na Manabii (Luka 16:29)” hakumaanisha Musa yupo sasahivi, bali alimaanisha kuwa watumishi wa Mungu wanaohubiri leo ndio akina Musa..
Hivyo Bwana YESU aliposema Yohana Mbatizaji ndiye Eliya alimaanisha ile roho iliyokuwa inatenda kazi ndani ya Eliya sasa ipo juu ya Yohana Mbatizaji. Sawasawa na ujumbe wa Malaika, aliompa Zakaria baba yake Yohana, kuwa mtoto atakayezaliwa atatangulia mbele za Bwana katika roho ya Eliya, lakini hatakuwa Eliya.
Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana. 14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake. 15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye. 16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao. 17 NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.”
Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.
14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.
16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.
17 NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.”
Hapo mstari wa 17 unasema, “Atatangulia katika roho ya Eliya”…na si kwamba atakuwa Eliya mwenyewe yule aliyepaa.. (Yule alishaondoka na hawezi kurudi tena).. Hivyo Yohana Mbatizaji, alijijua kuwa roho ya Eliya inatenda kazi ndani yake, lakini yeye si Eliya, na ndio maana walipomwuliza kama yeye ni Eliya akajibu siye.
Kwanini alijibu vile?..kwasababu ni kweli hakuwa Eliya, isipokuwa Huduma ya Eliya/roho iliyokuwa juu ya Eliya inatenda kazi ndani yake.
Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani? 20 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo. 21 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La”.
Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
20 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.
21 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Yohana Mbatizaji hakuwa Eliya aliyerudi… bali ni mtu ambaye roho ya Eliya ilikuwa inatenda kazi ndani yake. Hivyo biblia haijichanganyi mahali popote.
Je umeokoka?.. Kama bado basi fahamu kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu sana, na Kristo amekaribia kulichukua kanisa lake. Hivyo fanya uamuzi sahihi leo wa kumkabidhi Bwana YESU maisha yako kabla ya ule mwisho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).
ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?.
YOHANA MBATIZAJI
Rudi Nyumbani
Print this post
Swali: Je biblia inajichanganya kwa habari ya Bwana YESU kumjibu Pilato? Maana katika (Yohana 18:33-34) inasema alimjibu lakini katika (Mathayo 27:13-14).. inasema hakujibu chochote alipoulizwa? Je lipi ni sahihi?
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote pale, isipokuwa kinachojichanganya ni tafakari zetu, na fahamu zetu… Lakini biblia ni kitabu kikamilifu na kilichovuviwa na Roho Mtakatifu wa Mungu, hivyo hakina kasoro yoyote.
Sasa tukirejea habari hiyo katika Yohana 18:33-37.
Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi? 34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu? 35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini? 36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa. 37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”
Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?
34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?
35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?
36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.
37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”
Hapa ni kweli tunasoma Bwana YESU alimjibu Pilato alipoulizwa kuhusu habari zake mwenyewe… Lakini tukirejea kitabu cha Mathayo ni kama tunasoma habari tofauti kidogo.
Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA. 12 Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno. 13 Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia? 14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”.
Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA.
12 Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
13 Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”.
Hapa tunasoma Bwana YESU hamjibu Pilato.. Sasa swali je! Biblia inajichanganya??..Jibu ni la! Haijichanganyi.
Tukisoma vizuri habari hizo mbili zinaelezea kisa kimoja lakini katika mazingira manne tofauti..
Wakati Bwana anafikishwa kwa Pilato, alitangulia liwali kumhoji Bwana YESU kama yeye ndiye mfalme wa Wayahudi hapo alijibu “wewe wasema (maana yake ndio mimi ndiye)” Huyo ni Liwali anahoji na anajibiwa na Bwana bila maficho yoyote.
Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA…”
Lakini wakati ambao Wazee wa makuhani wanamshitaki Bwana YESU kwa Pilato yeye hakujibu chochote..
Kumbuka hapa wazee wa makuhani hawakuwa wanamhoji kuhusiana na swali alilouliza Liwali kwamba kama yeye ni mfalme wa Wayahudi…LA! Bali wazee wa makuhani wenyewe walikuwa wanamshitaki kwa mambo mengine ikiwamo habari ya kulivunja hekalu pamoja na kujiita mwana wa Mungu.. Soma Mathayo 26:62-68..Na sasa wanataka wamsikie Bwana YESU akijitetea mbele ya Pilato. Lakini Bwana YESU hakujibu chochote.
Mathayo 27:12 “Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno”.
Pilato aliposimama na kumwuliza Bwana YESU ajitetee, mbele ya wazee wa makuhani kuhusiana na mashtaka hayo (ya kulivunja hekalu na kujiita mwana wa Mungu).. yeye hakujibu chochote mpaka Liwali akashangaa!!..
Mathayo 27:13 “Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia? 14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”
Mathayo 27:13 “Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”
Na kwanini Bwana YESU hakumjibu hapa Pilato lolote?.. JIbu ni kwasababu Wazee wa Makuhani ambao waliokuwa ni wanafiki walikuwepo pale wakitafuta neno litokalo kinywani mwake ili waanze kuzusha maneno mengi juu yake..hivyo Bwana hakumjibu Pilato wala makuhani.
Pilato alipoona hapati jibu lolote kuhusiana na mashtaka ya wayahudi juu ya Bwana.. alimchukua Bwana YESU ndani ya Praitorio na kumwoji akiwa peke yake swali lile lile aliloulizwa na Liwali! (Je wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?)..na Bwana YESU akampa jibu kama lile lile alilompa Liwali.
Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi? 34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?…”
34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?…”
Umeona?… Kwahiyo biblia haijichanganyi yenyewe.. Ni kwamba Bwana YESU hakujibu mashtaka ya Wazee wa Wayahudi lakini alijibu maswali ya Pilato na Liwali.
Na kwanini Bwana YESU asijibu mashtaka ya wazee wa makuhani? Na amjibu Liwali pamoja na Pilato peke yao?…ni kwasababu wale wazee walikuwa wamemkusanyikia kwa shari, wapate kumwongezea dhiki….
Maswali yao si ya lengo la kutaka kujua, bali kutafuta sababu za kumshitaki..kwani tayari alishawajibu huko nyuma lakini bado waliendelea kumtafuta kwa maswali mengine mengi (Mathayo 26:62-68).
Kwahiyo na sisi tunachoweza kujifunza ni utulivu na kunyamaza katika vipindi ambavyo adui anatumia vinywa vya watu kutujaribu.. Ukishajibu swali mara ya kwanza, na mtu haelewi badala yake anatafuta tu kasoro, basi kinachofuata baada ya hapo ni kukaa kimya.
Kwasababu yapo maswali ambayo ukijibu hayatamsaidia yule anayeuliza badala yake yatampa kila sababu za kukusumbua wewe ziaidi, kwasababu lengo lake si kutaka kujua bali ni kubishana au kukudhuru wewe au kukushambulia. Hivyo ni muhimu kuwa makini.
Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana. 10 Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae”
Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana.
10 Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae”
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwanini maandiko yanajichanganya yenyewe kwenye habari ya Paulo alipotokewa na Yesu alipokuwa anakwenda Dameski?
Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?
NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.
Liwali ni nani?
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
WhatsApp
Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRSTO libarikiwe daima!
Kuna tofauti ya kumjua YESU WA KIDINI na yule wa UFUNUO (Yaani Yesu aliyefunuliwa maishani mwako na yule uliyempokea kwa wazazi au kwa mhubiri fulani) Utauliza kivipi?..Hebu tumwangalie mtu mmoja katika biblia ambaye hapo kwanza alimjua YESU wa kidini lakini baadaye akaja kumpokea wa KIUFUNUO, Na ikawa heri kwake!. Na mtu huyo si mwingine Zaidi ya Petro.
Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu. 41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, TUMEMWONA MASIHI (MAANA YAKE, KRISTO). 42 Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”
Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.
41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, TUMEMWONA MASIHI (MAANA YAKE, KRISTO).
42 Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”
Hapa Petro anamjua na kumpokea YESU kwa kuambiwa TU!!!…Anaambiwa na Adrea kaka yake habari za YESU, hivyo Petro anaamini na akampokea YESU wa kidini, akawaa mfuasi wa YESU tu, lakini bado hajafunuliwa ndani yake!. Akamjua tu kulingana na dini ya kiyahudi kuwa atakuja Masihi na hivyo amemwona! Na si Zaidi.
Baada ya kipindi kirefu kupita, Petro ampokea YESU wa ufunuo na hapo inakuwa heri kwake.
Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. 15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? 16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI. 17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo?… Petro amemjua YESU KIUFUNUO!.. aliyefunuliwa na Baba wa mbinguni, na si yule aliyeambiwa na kaka yake Andrea.
Kumbuka tayari alikuwa ameshajua kuwa YESU ndiye Kristo, kwani Andrea alishamwambia… Lakini ni kidini tu!..alipotulia na kumruhusu Roho Mtakatifu afanye kazi ndani yake ndipo akajua huyu wa kidini hatoshi, na kumbe YESU NA ZAIDI NA ALIVYOKUWA ANAMFIKIRIA..
Na utaona baada ya hapo ndipo Bwana anampa Petro funguo za Ufalme wa Mungu, baada tu ya kumpata YESU WA UFUNUO.
Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni 18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 19 NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI”
Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
19 NAMI NITAKUPA WEWE FUNGUO ZA UFALME WA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGWA MBINGUNI; NA LO LOTE UTAKALOLIFUNGUA DUNIANI, LITAKUWA LIMEFUNGULIWA MBINGUNI”
Ni Kwanini leo hii, wengi funguo za ufalme wa Mungu hawana???… Sababu kuu ni YESU WALIYE NAYE MAISHANI MWAO si wa ufunuo bali wa kidini… Kama ni wa kidini huyo hawezi kufungua lolote ndani yao, lakini kama ni yule wa UFUNUO huyo anafungua mbingu na nchi!.
Sasa swali tunampataje YESU WA UFUNUO.
Tunampata YESU wa ufunuo kwanza kwa kuweka mbali mapokeo, na udini, na udhehebu na ujuaji na kumruhusu ROHO MTAKATIFU afanye ndani yako kwa unyenyekevu wote..huku ukiwa umejikana nafsi yako na kujitwika msalaba wako… Kidogo kidogo utaanza kumwona YESU kwa UFAHAMU MWINGINE, Na utayagundua mengi kumhusu yeye, na hayo mambo mapya utakayoyapata kumhusu YESU ndiyo mafunuo.
NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?
Petro na Adrea waliitwa na Bwana wakati gani?
HERI, WALE MUNGU ASIOWAHESABIA MAKOSA YAO.
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?
Ushindi wa kwanza wa vita vya kiroho unaanza na “kukataa”.. Na kukataa kunaanza katika “moyo”, na kunaishia katika “kinywa”.. Unapoukiri udhaifu ndivyo unavyopata Nguvu juu yako vile vile unapoukiri uzima ndivyo navyo unavyopata nguvu juu yako.
Vile vile unapoukataa Udhaifu wa adui, ndivyo unavyokosa nguvu juu yako…Ndivyo biblia inavyotufundisha kuwa Uzima na Mauti vimewekwa katika uwezo wa ndimi zetu,
Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”
Ndio maana hata wokovu tunaupata kwa kanuni hiyo, Kwanza “kuamini moyoni” pili “kukiri kinywani”
Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.
Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.
Kwahiyo daima katika maombi yako usisahau hilo kuwa “moyo na kinywa” vinashirikiana na vina nguvu..
Hivyo unapokuwa katika sala au hata nje ya sala… hakikisha siku zote unakataa moyoni mwako na katika kinywa chako Mahubiri yote ya shetani, na kazi zake anazozielekeza juu yako.
> Maana yake Unakataa “Dhambi juu ya maisha yako”.. na zenyewe zitaisha nguvu
> Unakataa “Hofu na mashaka kutoka kwa ibilisi”… na yenyewe yataisha nguvu.
> Unakataa “Magonjwa na maradhi ya ibilisi”…. na yataisha nguvu juu yako.
> Unakataa “shida na tabu za ibilisi”.. na zenyewe zitaisha nguvu..
> Unakataa “Maazimio yote ya ibilisi yaliyokusudiwa juu yako”… na yenyewe yataisha nguvu.
> Unakataa “Maneno na ratiba zote za adui juu yako”..nazo zitafutika kabisa..
> Unakataa “kuitwa majina yote ya kiMisri uliyokuwa unaitwa huko nyuma au unayoendelea kuitwa sasa”.. na yenyewe yataisha nguvu juu yako..
Kama zamani ulikuwa kahaba, basi sasa baada ya kuokoka unakataa hayo majina, kama ulikuwa unaitwa au unajiita jambazi, au mhuni fulani au mwizi, au jina lingine lolote la kihuni na lisilo na maana unakataa hayo majina kwamaana majina nayo yamebeba roho (soma 1Samweli 25:25).
Biblia inasema Musa alipokuwa mtu mzima alikataa kuitwa Mwana wa binti Farao.. Hivyo ushindi wake wa imani ulianzia hapo..
Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, AKAKATAA KUITWA MWANA WA BINTI FARAO 25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo; 26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.”
Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, AKAKATAA KUITWA MWANA WA BINTI FARAO
25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.”
Kwanini Musa alikataa kuendelea kuitwa “Mwana wa binti Farao”?.. Ni kwasababu wana wa binti za Farao walikuwa wanajulikana ni watu “kuabudiwa kama miungu” pia wàtu“wenye kiburi/majivuno/majigambo” na “wauaji wenye uwezo wa kufanya jambo lolote ovu na wasiulizwe na mtu”..
Na akajua endapo akiendelea kuitwa hivyo Mwana wa binti Farao, bado hizo tabia zao zitaendelea kukaa ndani yake na kumtumikisha, hivyo akakataa hicho cheo..na kujitoa katika ile nafasi.
Inasikitisha mtu baada ya kuokoka bado anaona ni sahihi kuitwa sistaduu, au brazameni, au bishoo, au Demu, au DJ, au jina lingine lolote la kihuni tu!.. Ni lazima uyakatae hayo majina kwa kinywa chako, na pia ubadilike ili kukataa kwako kuendane na mwenendo wako.. lakini kama utakataa kinywani lakini muonekano wako unasema wewe bado ni yule yule mtu wa kale, bado itakuwa haina maana!.
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?
HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.
MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.
Swali: Je kuna roho ya kukataliwa katika biblia?.. na kama ipo je mtu anawezaje kufunguliwa kutoka katika hiyo roho?
Jibu: “Kukataliwa” kwa lugha nyingine ni ile hali ya “kukosa kibali”.
Mtu anaweza kukosa kibali “kwa Mungu” au “kwa wanadamu”.
1. KUKOSA KIBALI KWA MUNGU.
Sababu kuu ya Mtu kupoteza kibali (kukataliwa) na Mungu ni “DHAMBI/MAOVU”. Dhambi inapoweka mizizi katika maisha ya mtu inampotezea kibali kwa Mungu.. Mtu huyu anaweza kumwomba Mungu na asione majibu anayoyategemea…anaweza kupambana na asione matokeo ya kile anachokipambania.
Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, HATA HATAKI KUSIKIA”.
Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, HATA HATAKI KUSIKIA”.
Mfano wa mtu aliyepoteza kibali mbele za Mungu na kuwa mtu wa kukataliwa mbele zake ni Mfalme Sauli (1Samweli 16:1) na pamoja na Kaini (Mwanzo 4:10-12).
Sasa mtu anapopoteza kibali cha kiMungu vilevile hawezi kupata kibali kwa watu, hivyo atakuwa mtu wa kukataliwa na watu sahihi (lakini anaweza kukubalika na watu wasio sahihi, jambo ambalo ni hatari kubwa). Mfano wa watu hao katika biblia ni Kaini..
Mwanzo 4:10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. 11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; 12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. 13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. 14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; HATA ITAKUWA KILA ANIONAYE ATANIUA”
Mwanzo 4:10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; HATA ITAKUWA KILA ANIONAYE ATANIUA”
Umeona hapo?..Kaini alijua madhara ya “kukataliwa na Mungu” ni “kukataliwa na watu pia”… ndio maana anasema “watu watakapomwona watamwua”.
Kwahiyo DHAMBI au MAASI ndio msingi mkubwa wa mtu kupoteza kibali. Na kwasababu dhambi zote zinaasisiwa/kuchochewa na roho ya Ibilisi na mapepo yake, hivyo basi ni sahihi kabisa kusema kukataliwa ni roho..
Kwahiyo mtu anapojigundua kuwa kila mahali hakubaliki, anakataliwa na kila mtu, na hata wakati mwingine hajui sababu… ni muhimu kulitafakari hilo kwa jicho la pili, kwasababu ni roho ipo nyuma yake inayopalilia dhambi juu ya maisha yake, ambayo matokeo yake huyo mtu ni kukatalika kwa kila anayemwona, au kila anachokipanga..
Hivyo suluhisho pekee la kuiondoa hiyo roho ya kukataliwa ndani ya mtu ni KUOKOKA KIKWELI KWELI.. Na maana ya kuokoka ni KUACHA DHAMBI!!!.. Mtu anayetaka kuokoka lakini hataki Kuziacha dhambi zake, hataki kuacha uzinzi, ulevi, wizi, usengenyaji, matukano, kutokusamehe, chuki, wivu, usengenyaji, fitina n.k hawezi kupokea wokovu mkamilifu. Lakini anayetubu kwa kudhamiria kuziacha dhambi zake ndiye anayepokea wokovu mkamilifu.
Na matokeo ya kupokea wokovu mkamilifu ni kuondoa roho ya kukataliwa ndani yako, na si tu roho ya kukataliwa bali na roho nyingine zote ambazo zimekaa ndani yako zinazochochea tabia na mienendo mingine isiyofaa.
Je umeokoka?
Kama bado na unatamani kufanya hivyo basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu kwa msaada Zaidi au ukafuatiliza sala hii >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Mistari ya biblia kuhusu kibali.
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
TENDA JAMBO LA ZIADA.
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
NUHU WA SASA.
Unaweza kuuliza je! Mwamini anaweza kufungwa na adui?. Jibu ni ndio anaweza kufungwa. Utauliza tena, kama anafungwa sasa kazi ya Yesu msalabani ilikuwa ni nini ikiwa hajawekwa huru kweli kweli.
Jibu ni kwamba mwamini yeyote, hawezi kuwa na kifungo katika roho yake, yaani hawezi kufungwa roho aidha na mapepo, au wanadamu au chochote kile. Hawezi kuwa na laana yoyote ndani yake, aidha ya ukoo au ya mabibi. Kwasababu yeye ni mbarikiwa amewekwa huru na Yesu, na ndio kazi Yesu aliyokuja kuifanya kuwaweka huru walioonewa na ibilisi.Hivyo mtu yeyote aliyemwamini Yesu kwa ‘TOBA’, ubatizo na kupokea Roho. Huyo hana kifungo chochote kwasababu uhai wake unakuwa umefichwa ndani ya Kristo.
Lakini Shetani anauwezo wa kumzuia, katika mambo mengi, asipojua ni nini anapaswa afanye. Na hicho ndicho kifungo cha nje akifanyacho adui. Kukuzuia wewe mwamini, ndicho alichokifanya kwa Paulo wakati Fulani alipotaka kwenda kuhubiri injili kwa Wathesalonike akasema shetani alinizuia (1Wathesalonike 2:8).
Lakini pia tunamwona Mtume mwingine aliyeitwa Petro.
sasa hebu tuangalie kisa hiki kwenye maandiko Kilichomhusu yeye, tuone ni maeneo gani huwa adui analenga mahususi.
Matendo 12:4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. 5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. 6 Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakalilinda gereza. 7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika kule chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. MINYORORO YAKE IKAMWANGUKA MIKONONI. 8 Malaika akamwambia, Jifunge, KAVAE VIATU VYAKO. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, JIVIKE NGUO YAKO, ukanifuate. 9 Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.
Matendo 12:4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.
5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
6 Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakalilinda gereza.
7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika kule chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. MINYORORO YAKE IKAMWANGUKA MIKONONI.
8 Malaika akamwambia, Jifunge, KAVAE VIATU VYAKO. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, JIVIKE NGUO YAKO, ukanifuate.
9 Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.
Umeona maeneo aliyofungwa Petro?
Wafungwa wa zamani, ilikuwa ili aitwe mfungwa, ni lazima mambo hayo matatu yakamilishwe juu yake; nayo ni.
1) Kufungwa, Minyororo mikononi
2)Kuondolewa Mavazi, na kupewa mengine ya gerezani.
3)Kuondolewa viatu miguuni
Na hiki ndicho kitu anachokifanya pia adui kwa mwamini. Anaanza kwa kukufunga mikono yako rohoni, kisha kuyaondoa mavazi yako, na mwisho viatu vyako miguuni. Baada ya hapo unakuwa tayari huna nguvu ya kumshinda.
Mikono ni nini?
Ni “maombi na mifungo”
Mikono ni viungo mama katika mwili. Husaidia viungo vingi kufanya shughuli zake. Silaha hushikwa na mikono, hata ngumi hurushwa kwa mikono. Hivyo adui anajua akizuia mikono yako. Huwezi kufanya lolote. Mikono ya mwamini, ni “maombi na mifungo”.
Mtu ambaye ni mwombaji, kiwango cha Roho ndani yake huwa ni kikubwa, na hivyo hakuna mnyororo wowote, unaoweza kumshika. Ndio maana utaona baada ya kanisa kumwombea Petro kwa juhudi, akafunguliwa. Vilevile Paulo na Sila walipokuwa wamefungwa kipindi kile, hawakulala tu, bali usiku wa manane walikuwa wakiomba, na matokeo yake vifungo vikawaachia.
Matendo 16:25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26 Ghafla pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.
Umeona, maombi, huondoa minyororo mikononi. Kuwa mwombaji, uzishinde nguvu za mwovu. Shetani anawaogopa waombaji
Mavazi ni nini?
Ufunuo 19:8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu
Mavazi, ni matendo mema. Ukikosa matendo mema,(Utakatifu), si rahisi kumshinda adui, utakuwa mwamini asiye na matunda yoyote, itaishi tu kama mwanadamu ambaye anamapungufu ya akili rohoni, hutaweza kufanya lolote.Ndani una makunyanzi, mawaa, ambazo katika hizo shetani anakuwa na haki ya kukulaumu.
Ishi kama mkristo, ukiwa rafiki wa dunia, fahamu kuwa unajifanya adui kwa Mungu moja kwa moja. Nuru yako isipoangaza nje, huwezi mshinda shetani. Ni lazima uwe kikombe safi, nje na ndani. Huwezi kusema umeokoka halafu matendo yako hayaendani na imani yako.Unajidanganya, bado hujaifahamu neema ya Mungu.
Miguu ni nini?
Waefeso 6:14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani.
Miguu ni utayari, wa kuhubiri. Adui anapenda kukawiisha nia za watu, kwa kuwavuta katika mambo yao mengine, na kusahau yaliyo ya msingi kwao, ndio hapo atawasonga kwa anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu. Na mwisho wa hapo wanabakia kuwa hawana matunda.
Hivyo ndugu uliyeokoka, usiruhusu adui kukuzuia popote. Jijengee desturi ya kuwa mwombaji wa kila siku. Mikono yako isifungwe. Penda kuishi maisha matakatifu, vazi lako lisibadilishwe, kuwa tayari kuhubiri injili wakati wowote, ukifaao na usiokufaa, epuka udhuru wa mwili au kazi, pinga sana hapo jiwekee ratiba yako, ili upate sehemu ya kuwaeleza wengine habari za Yesu Kristo anayewaokoa wanadamu.
Tukizingatia hayo. Tutakuwa tumemshinda shetani ndani na nje. Hatujafungwa ndani wala nje.
Bwana akubariki
Shalom.
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)
VITA DHIDI YA MAADUI
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.
Swali: Muujiza wa kwanza wa Bwana YESU ulikuwa ni upi?
Jibu: Mwujiza wa kwanza wa Bwana YESU ni ule wa Kana ya Galilaya, ambapo aligeuza maji kuwa Divai.
Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. 2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. 3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. 5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. 6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. 7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. 8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. 9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, 10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa. 11 MWANZO HUO WA ISHARA YESU ALIUFANYA HUKO KANA YA GALILAYA, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”.
Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.
7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.
8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.
9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,
10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.
11 MWANZO HUO WA ISHARA YESU ALIUFANYA HUKO KANA YA GALILAYA, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”.
Mstari huo wa 11 unatudhihirishia wazi kuwa hiyo ndio iliyokuwa ishara ya kwanza kufanywa na BWANA YESU mbele ya wanafunzi wake.
Sasa kujua kwa mapana ujumbe uliopo nyuma ya muujiza wa kwanza wa Bwana YESU wa Kana ya Galilaya fungua hapa >>Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?
NI NINI BWANA ANATAKA KUTOKA KATIKA MUUJIZA ALIOKUFANYIA?
JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?
Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)
SIRI KUU NNE (4), UNAZOPASWA UZIFAHAMU NDANI YA KRISTO.
UFUNUO: Mlango wa 3 part 3
MIMI NIKO AMBAYE NIKO
Swali: Kuna nini katika Divai mpaka Bwana YESU ayageuze maji kuwa Divai?
Jibu: Hakukuwa na chochote maalumu au cha kipekee katika Divai.
Sababu ya Bwana YESU kuyageuza maji kuwa Divai na si kinywaji kingine ni kwasababu ndicho kinywaji kilichokuwa kimepunguka pale! (Kulingana na zile taarifa alizoletewa na mama yake).. Endapo kama ingekuwa ni chakula ndicho kilichopunguka basi Bwana YESU angefanya muujiza wa chakula kuongezeka cha kuutosha ule umati wote, huenda angefanya muujiza kama ile ya Mikate na Samaki, alipolisha maelfu ya watu. (Marko 6:38-44 na Luka 9:13-17).
Sasa kabla ya kuangalia ni ujumbe gani tunapata kwa mwujiza ule, hebu kwanza tuangalie matokeo ya kukosa Divai katika ile Harusi.
Kufahamu kwa kina matumizi ya Divai katika biblia fungua hapa >>MATUMIZI YA DIVAI.
Kulingana na Desturi za kiyahudi ilikuwa ni aibu kubwa sana arusi ikose Divai, au chakula…Hivyo ni aibu kubwa sana kwa wanafamilia, sawasawa tu sasa sherehe ikipungukiwa na chakula inakuwa ni aibu kubwa kwa walioandaa na huzuni na karaha!..
Sasa kitendo cha Bwana YESU kubadili yale maji na kuwa Divai, tena yenye kuwatosha watu wote ni kitendo KILICHOWAONDOLEWA AIBU WANA ARUSI NA WAZAZI.. vile vile ni kitendo kilichowaondolewa huzuni, na masononeko na fadhaa.. na ni kitendo kilichowapa heshima. Ndio maana utaona yule mkuu wa Meza alimfuata Bwana arusi kumsifu badala ya Bwana YESU.
Sasa ni ujumbe gani mkuu tunaupata hapo?
Ujumbe mkuu si upekee wa Divai.. bali ni Faida ya BWANA YESU ndani yetu au katikati yetu. Kuwa yeye anapoingia ndani yetu anazichukua aibu zetu, na fadhaa zetu na masikitiko yetu, na kutuheshimisha na kutuondolea aibu zetu..
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Unauona upendo wa YESU kwetu pale tunapomkaribisha na kumtwika fadhaa zetu?.. Wale wanaharusi waliona thamani ya YESU na kumwalika katika sherehe yao, na pale walipopungukiwa ndipo Kristo alipozuchukua fadhaa zao na aibu yao..
Wenye harusi , (wao hawakumwalika Bwana kwasababu walijua divai itaisha ili baadaye wamwite awageuzie maji kuwa Divai).. La! Ile ilitokea tu kama dharura na ndipo Bwana akafanya miujiza.. Wao lengo lao kubwa lilikuwa ni kumwitaji YESU ndani ya harusi yao, na si wamtumie.
Na sisi leo hatupaswi kumfuata BWANA YESU kwasababu tu tunataka uponyaji, au heshima au kuinuliwa kimaisha (watu wote waliomfuata Bwana YESU kwa haja kama hizo aliwakimbia Soma Yohana 6:25-26)..Lakini tumfuate Bwana YESU kwasababu tunataka uzima kwanza, na kuyafanya mapenzi yake na hayo mengine yawe ni dharura tu, kama wale waliomwalika.
Ukishahikiki kwamba uzima upo ndani yako, ndipo tumtwike hayo mengine..
1Petro 5:7 “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu”.
Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.
Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.
WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.
BUSTANI YA NEEMA.
MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.
Bwana YESU KRISTO alizaliwa katika Nchi/Taifa la ISRAELI, lililopo mashariki ya kati. Na mji aliozaliwa ni Bethlehemu ambao ulikuwa katika urithi wa kabila la YUDA.
Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.
Pamoja na kwamba Bwana YESU alizaliwa Bethlehemu kulingana na unabii huo wa Mika, lakini hakulelewa katika huo mji wa Bethlehemu badala yake wazazi wake waliishi mahali palipojulikana kama NAZARETI, Mji mdogo sana uliopo kaskazini mwa Taifa hilo la Israeli, na huko ndiko Kristo alikokulia, ndio maana mahali pengine anajulikana kama Mnazorayo (yaani mtu wa Nazareti).
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.
Lakini pia Mji huo wa Nazareti ulikuwa ndani ya Wilaya iitwayo Galilaya, wakati mji wa Bethlehemu aliozaliwa Bwana YESU ulikuwa katika Wilaya iliyoitwa Yudea au Uyahudi.
Wilaya ya Galilaya ndio uliyojumuisha miji mingine midogo midogo kama Kapernaumu na Korazini na Bethsaida, ambapo wanafunzi wengi wa Bwana YESU walitokea katika hiyo miji, na ndio miji ambayo iliona miujiza mingi ya Bwana YESU lakini haikutubu (Mathayo 11:21)…. Wakati Wilaya ya Uyahudi ndio iliyobeba miji ya Bethlehemu pamoja na Yerusalemu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba BWANA YESU alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi na kulelewa Nazareti ya Galilaya, na alifia YERUSALEMU na kuzikiwa hapohapo, na kufufuka hapo hapo YERUSALEMU. Na sasa yupo hai na atarudi tena mara ya pili na siku hizo zimekaribia kulingana na unabii wa biblia.
Bwana YESU ANARUDI.
Kama unatamani kuokoka basi fuatiliza sala hii >>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?
Raheli aliwalilia vipi watoto wake?
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA
Yerusalemu ni nini?
AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.
Huwenda ukawa unajiuliza, Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema, Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru? . Je huko gizani ni wapi, na sirini ni wapi? Je yeye huwa anazungumza gizani.
Mathayo 10:26 “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. 27 Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”
Mathayo 10:26 “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.
27 Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”
JIBU: Ni vema tukaifahamu tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo, katika kufundisha jinsi ilivyokuwa alipokuwa anazungumza na watu mbalimbali. Yapo maneno au mafundisho au mafunuo aliyoyaweka wazi kwa watu wote, lakini yapo ambayo hakuyaweka wazi kwa kila mtu.
Mahubiri yake mengi aliyazungumza hadharani, lakini mengine haikuwa hivyo, kwamfano upo wakati alijitenga akapanda milimani, na wale waliomfuata ndio aliowafundisha (Mathayo 5:1), wakati mwingine aliingia nyumbani, hakutana kujulikana kwasababu alikuwa akitaka kuwafundisha wanafunzi wake tu, peke yao (Marko 9:29-31), wakati mwingine aliwaponya watu akawataka wasimdhihirishe, (Marko 1:44), wakati mwingine alijifunua utukufu wake, kwa wale tu waliokwenda naye kuomba mlimani, uso wake ukawa unameta meta, kama jua, alipomaliza akawakataza wasimwambie mtu, mpaka atakapofufuka (Mathayo 16).
Hayo ni mazingira mbalimbali, ambayo Yesu alisema nao bila kujulikana na kila mtu, Sasa mazingira hayo ndio aliyaita “Gizani, au sirini”
Hii ni kufunua kuwa hata sasa Yesu anazungumza hadharani, lakini pia anazungumza sirini. Na yale ya sirini huwa ni makubwa zaidi na ndio maana haitaji yajulikane na kila mtu.
Watu wengi wanamsikia Yesu hadharani, lakini hawamsikii sirini. Hadharani, ni pale unaposikia mafundisho kanisani, mahubiri, semina, mkutano n.k. Ni kweli Yesu atakufundisha mengi kupitia matumishi wake mbalimbali, na yatakujenga na ni muhimu ufanye hivyo.
Lakini lazima pia sirini pa Yesu uwe napo.
Je hapo ni wapi?
“Ni eneo lako la utulivu la kimaombi na kutafakari”.
Ni muhimu sana kila mkristo, awe na wakati wake maalumu kila siku alioutenga wa kuzama uweponi, katika maombi, kusoma Neno na kutafakari shuhuda za Mungu maishani mwake. Ni muhimu sana.
Zaburi 91:1 AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
Mathayo 6:6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Hapa Yesu anataka uingie gharama, kidogo ili umsikie, au akuhudumie, au akufundishe. Ndio mfano wa wale waliomfata milimani. Vivyo hivyo na wewe, ingia gharama ya kudumu uweponi mwa Mungu. Ukiona mchana pana usumbufu, usiku ni muda mzuri sana, kuamka, tena masaa yako kadhaa kila siku,. Kumpa Bwana nafasi ya kukufundisha.
Ukiwa wa namna hii, hutamkosa Bwana popote pale. Kaa mahali pake pa siri. Kwasababu yupo pia sirini, akupe mambo mambo utayasema hadharani wakati fulani.
Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)
UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?
AGIZO LA UTUME.
MKUU WA GIZA.