Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.
Waamuzi 16:13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. 14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande. 15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.
Waamuzi 16:13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo.
14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande.
15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.
Mtande ni kifaa maalumu kinachotumika kufumia nyuzi za nguo, kwa kuzisokota pamoja ili kuunda nguo. Tazama mfano wa picha.
Hivyo nyuzi za nguo zilipitishwa katikati ya kamba hizo ngumu za mtande, kisha kuvutwa na kukazwa na mfumaji.
Katika habari hiyo tunaona Delila kazi yake huwenda ilikuwa ni ya ufumaji. Kwasababu ya uwepo wa kifaa hicho katika nyumba yake. Lakini katika harakati zake za kutaka kujua asili ya nguvu za Samsoni, biblia inatuambia, Samsoni alimdanganya kwa kumwambia ikiwa atavifuma vishungi vyake saba vya nywele katika mtande ule, basi, hatakuwa na nguvu za kujinasua, mahali pale.
Delila kusikia vile akaamini ni kweli, kwasababu kwa kawaida mtu ukishikwa tu nywele zako, si rahisi kuleta vurugu kwasababu utakuwa unajiumiza mwenyewe. Delila akizingatia kuwa alijua pia namna ya kufuma nyuzi vizuri. Hivyo alijihakikishia kuwa hilo linawezekana. Na cha kuongezea akapigilia na msumari kabisa, ili atakapojaribu kuzivuta nyewe zake, kutoka pale ashindwe. Kisha wafilisti waje kumchukua.
Lakini bado tunaona hilo halikuwezekana. Samsoni aling’oa misumari ile na kuuvunja mtande ule, Delila alipomwamsha.
Ni nini Tunajifunza katika habari hiyo kama waaminio?
KATIKA USINGIZI MUNGU ANAUMBA, NA SHETANI NAYE ANANASA.
Jiulize kwanini majaribio hayo yote Delila aliyafanya wakati ambao Samsoni amelala?. Alijua kabisa wakati akiwa macho Samsoni hawezi kukubali. Lakini pia swali lingine watu wanalojiuliza, iweje Samsoni, asisikie lolote wakati anatendewa vitendo vile. Kwamfano mpaka Delila anachukua nywele zake na kuziingiza kwenye mtande na kuzibana na kuzipigia misumari, asisikie chochote, ni usingizi wa namna gani?
Ndugu Mitego ya shetani, si rahisi kuigundua, kwasababu anaoutashi wa kuiweka kiasi cha kukufanya wewe usiwe mwepesi kuitambua, au kuisikia. Utashutukia tu umeshanaswa. Hivyo kama mwaminio ni kukimbia usingizi wowote wa kiroho kwa hali zote. Kwa kumtazama na kumfuata Yesu wakati wote. Unapomtazama Yesu, na kumtii kwa kuyakimbia machafu ya dunia. Hapo hujalala kiroho.
Lakini Pia katika usingizi Mungu pia hufanya jambo, na hilo si lingine zaidi ya kuumba. Utalithibitisha hilo kipindi kile alipomuumba Adamu, Mungu anasema.
Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
Umeona? Ukitulia kwa Bwana, akapumzika kwa Bwana, ukalala kwake. Jiandae kuumbiwa jambo lako bora kuliko yote katika maisha yako. Kama vile Mungu alivyomuumbia Adamu, msaidizi bora kuliko wote.
Kulala kwa Bwana ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako, akupe ondoleo la dhambi. Kisha kuamua kuacha mambo yote ya kidunia na kumfuata yeye kwa uaminifu kwa kulitii Neno lake baada ya hapo. Na hapo ndipo unakuwa umelala kwake.
Hivyo chagua leo “Kuumbwa” badala ya “Kunaswa”. Mpokee Yesu sasa, ikiwa upo tayari kufanya hivyo. Basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KITENDAWILI CHA SAMSONI
JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?
Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?
Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)
Rudi nyumbani
Print this post
Mahali pekee ambapo maandiko yanaeleza kuchoka kwa Yesu, ni siku ile alipokuwa anatoka Uyahudi anakwenda Galilaya. Kwasababu safari yake ilikuwa ndefu, ya saa nyingi, ilibidi waweke kituo kwanza kwenye mji wa mmoja wa wasamaria, wapumzike. Yeye na wanafunzi wake kwenye kile kisima cha Yakobo.
Yohana 4: 5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe. 6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu AMECHOKA KWA SAFARI YAKE, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
Jua la mchana likiwa kali, anasikia mwili ni mchovu hautaki, kufanya kazi yoyote, njaa zinauma, mpaka mitume wakaondoka kwenda kutafuta chakula mjini. Lakini katika mazingira hayo hayo Analetewa na Mungu mtu mwenye dhambi amshuhudie habari za neema ya wokovu. Ndio Yule mwanamke msamaria.
Lakini Yesu hakuwa na udhuru kwa kusema, huu ni muda wangu wa kupumzika, ni muda wangu wa kulala, ni muda wangu wa lunch nile na wanafunzi wangu. Alitii vilevile katika uchovu wake, akaanza kuongea na Yule mwanamke habari za ukombozi, kwa kipindi kirefu kidogo.
Lakini mwisho wa mazungumzo yao haukuwa bure, Yule mwanamke aliondoka, lakini baada ya muda mfupi alirudi na jopo la watu, ili kuja kumsikiliza Bwana Yesu, maneno aliyoshuhudiwa na yeye (Yohana 4:1-42). Na baada ya hapo tena, Samaria yote ikamwamini, sehemu nyingine mpaka wakawa wanataka hata kumfanya mfalme.
Lakini ni nini tunapaswa tujifunze katika habari hiyo? Wengi wetu hatujui kufanikiwa kwa huduma ile ya Yesu pale ndani ya mwanamke Yule zaidi ya wengine wengi, kulitokana na gharama ambazo Yesu aliingia. Yaani katika kipindi cha KUCHOKA kwake, alikuwa tayari kulitimiza kusudi la Mungu. Kitendo hicho rohoni huwa kinageuka na kuwa IMANI, kubwa sana mbele za Mungu.
Je! Na sisi, tunaweza kujifunza jambo hili kwa Bwana. Je! visingizio cha kuchoka, tumeshindwa kutimiza makusudi mangapi ya Mungu, yenye matokeo makubwa kama haya? Nimetoka kazini, nimefanya kazi wiki nzima, hivyo nimechoka siwezi kwenda kuomba. Weekend ni siku yangu ya kupumzika, siwezi kwenda kwenye ushuhudiaji?
Hatujui kuwa hapo ndipo Mungu anapathamini, tunataka siku ambayo tupo “free” tu.
Ukweli ni kwamba tukiwa watu wa kungojea siku ambazo tuna nafasi ya kutosha, au tuna afya, au tuna fursa, au tume-relax si rahisi kuzalisha vema kama wakati ambao tutajiona sisi ni dhaifu. Katika dunia hii ya masumbufu na mahangaiko ya maisha, utajikuta mpaka unamaliza maisha yako hujapata hata huo muda wa kupumzika vema. Hivyo tumia fursa hiyo sasa.
Isaya 40:29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. 30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; 31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Hubiri injili nyakati zote, omba nyakati zote, soma Neno nyakati zote. Kumbuka wakati wa kuchoka, ipo nguvu ya Mungu kukusaidia. Jenga ufalme wa Mungu. Na Bwana atakutia nguvu.
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.
NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Uweza na nguvu ni vyake milele na milele. Amen.
Kuna mambo ambayo Mungu aliyaweka wazi, lakini pia kuna mambo ambayo Mungu aliyaficha ndani ya Kristo mpaka utimilifu wa wakati wake mwenyewe utakapofika. Hivyo ni vema ukafahamu siri hizo alizozificha tangu mwanzo, na ngapi zimeshatimia, na ngapi zipo mbioni kutimia.
Siri hizo hazipo kwa mwingine zaidi ya Yesu Kristo.
Wakolosai 2:2 “..wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo;”
Na hivyo ndani ya Kristo ziliandikwa siri kuu Nne, ambazo leo tutaziona.
Yesu ndio yeye mwenyewe:
1Timotheo 3:16 Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Mungu alijificha sana, kiasi kwamba hakuna aliyemtambua kuwa ndiye yeye Yehova katika umbo la kibinadamu, na ndio maana maandiko yanasema, kama watu wa ulimwengu huu wangemtambua kuwa yeye ndiye tangu mwanzo, wasingelimsulibisha.
1Wakorintho 2:7 bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; 8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu;
Lakini bado tunaona ni jambo ambalo limejificha katika macho ya wengi hata sasa, lakini ashukuriwe Mungu tayari limeshafunuliwa hivyo hilo sio siri tena. Ni vizuri kuifahamu siri hii kwasababu wakati mwingine kushindwa kumtambua Kristo kama ndiye MUNGU mwenyewe. Hupunguza viwango vyako vya kutembea na yeye, na kumwelewa. Fahamu kuwa Yesu ni Mungu halisi Yehova mwenyewe kwenye umbile la kibinadamu ( Tito 2:13, Yohana 1:1, Wakolosai 2:9).
Mataifa nao ni warithi.
Waefeso 3:4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo. 5 Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho; 6 ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja, na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili;
Wale wapagani, walioitwa makafiri na wayahudi, wafilisti, waashuru, wamisri, wakaanani, n.k. hao Mungu anakuja kuwafanya kuwa warithi wa uzima wa milele. Jambo ambalo halikujulikana na wanadamu au wayahudi kwa kipindi kirefu, wakidhani Mungu ni wakwao tu. Lakini leo hii anaabudiwa katika dunia nzima. Ilikuwa ni SIRI, lakini sasa imedhihirishwa. Soma (Wakolosai 1:27)
Siri hii ukiifahamu itakufanya usibague mtu wa kumuhubiria injili, kitu mwanadamu chini ya jua anastahili kumjua Mungu katika Kristo Yesu. Hivyo usibague kama wewe ambavyo hukubaguliwa. Hubiri kwa watu wa dini zote, kabila zote na lugha zote.
Wayahudi watarudiwa tena.
Warumi 11:25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili. 26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake. 27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao. 28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
Tuwaonapo sasa wayahudi wapo mbali na injili ya Kristo, haitakuwa hivyo kwao milele. Mungu anasema “utimilifu wetu utakapowasili”. Yaani mpango wa Mungu wa wokovu kwetu utakapotimia. Basi na wao pia watarudiwa. Na Mungu atasimama nao, na kuwatetea. Na kuwaokoa (Zekaria 12:10-14). Na Mungu anasema kurudiwa kwao kutakuwa na utukufu mwingi zaidi.
Hivyo kuifahamu siri hii, itakuwasadia wewe ambaye umepata neema hii bure kutoichezea, bali kuithamini sana, kwasababu ikiwa wale waliipoteza, vivyo hivyo na sisi tunaweza ipoteza kwa kutokuamini kwetu. Na ndivyo itakavyokuja kuwa baadaye. Israeli watakaporudiwa kwa kipindi kifupi, sisi tutakuwa tumekwenda kwenye unyakuo, watakaobaki watalia na kuomboleza. Hivyo ni muhimu kuutimiza wokovu wako kwa kugopa na kutetemeka, kama maandiko yanavyotuambia (Wafilipi 2:12). Ithamini neema ya Kristo.
Kurudi kwa Bwana.
Kipindi kile Bwana alipokuwa duniani, wanafunzi walimuuliza kuhusiana na siku ya kurudi kwake, ndipo akawaeleza wazi kuwa hakuna mtu aijuaye, isipokuwa Baba tu (Mathayo 24:36). Lakini Kristo alipopaa juu alipokea ufalme na enzi na nguvu, maana yake pia alitambua mpango wote alipowekewa na Baba yake, tunalithibitisha hilo katika kuvunjwa kwa ile mihuri saba (Ufunuo 6).
Na baadaye tunaona biblia inasema..
Ufunuo 10:7 isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari kupiga baragumu; hapo ndipo SIRI YA MUNGU ITAKAPOTIMIZWA, kama alivyowahubiri watumishi wake hao manabii.
Hii siri ya Mungu itakayotimizwa ndio hiyo inayohusiana na kutambua wakati husika wa Bwana kurudi. Na ndio maana ukisoma katika vifungu vya juu kidogo utaona yapo mambo ambayo Yohana aliyasikia lakini akakatazwa kuyaandika. Kuonyesha kuwa ipo sehemu ya Neno la Mungu, ambayo haijafunuliwa kwetu sisi, Mungu atakuja kufanya hivyo baadaye.
Ufunuo 10:3 Naye akalia kwa sauti kuu, kama simba angurumavyo. Na alipolia, zile ngurumo saba zikatoa sauti zao. 4 Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika. Nami nalisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Yatie muhuri maneno hayo yaliyonenwa na hizo ngurumo saba, usiyaandike.
Hivyo hii ndio siri moja tu, ambayo ipo ndani ya Kristo hatujafunuliwa bado. Lakini wakati u karibu.
Je! Unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho, umejiandaaje na karamu ya mwana-kondoo mbinguni kwa tukio la unyakuo. Tubu dhambi zao, umegukie Kristo akupe ondoleo la dhambi zako bure. Ikiwa upo tayari leo kumpokea Yesu maishani mwako, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>
Bwana akubariki.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
Karama tisa (9) za Roho mtakatifu tunazisoma katika kitabu cha 1Wakorintho 12.
Tusome,
1Wakorintho 12:4 “Basi pana tofauti za KARAMA; bali Roho ni yeye yule. 5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. 6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. 7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa NENO LA HEKIMA; na mwingine NENO LA MAARIFA, apendavyo Roho yeye yule; 9 mwingine IMANI katika Roho yeye yule; na mwingine KARAMA ZA KUPONYA katika Roho yule mmoja; 10 na mwingine MATENDO YA MIUJIZA; na mwingine UNABII; na mwingine KUPAMBANUA ROHO; mwingine AINA ZA LUGHA; na mwingine TAFSIRI ZA LUGHA; 11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye”.
1Wakorintho 12:4 “Basi pana tofauti za KARAMA; bali Roho ni yeye yule.
5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa NENO LA HEKIMA; na mwingine NENO LA MAARIFA, apendavyo Roho yeye yule;
9 mwingine IMANI katika Roho yeye yule; na mwingine KARAMA ZA KUPONYA katika Roho yule mmoja;
10 na mwingine MATENDO YA MIUJIZA; na mwingine UNABII; na mwingine KUPAMBANUA ROHO; mwingine AINA ZA LUGHA; na mwingine TAFSIRI ZA LUGHA;
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye”.
Tuangalie utendaji kazi wa moja baada ya nyingine.
1. NENO LA HEKIMA.
Hii ni karama ya upambanuzi wa jambo lililo gumu kutatulika.. Kwamfano kunaweza kutokea jambo katika kanisa ambalo ni gumu sana kutatulika au kufahamika, (fumbo kubwa)..sasa mtu mwenye karama hii ya Neno la Hekima anaweza kulijua jambo hilo na kulitatua, au kutoa mapendekezo ya kulitatua kwa njia ya mafundisho au matendo..
Mfano wa mtu aliyekuwa na karama hii ni Sulemani..
Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa, basi ndoa nyingi zitasimama, na wizi na mambo ya kando kando hayataweza kupata nafasi kwasababu yatawekwa wazi.
2. NENO LA MAARIFA.
Hii ni karama ya MAARIFA kama jina lake lilivyo.. Mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo mkubwa wa kujua mambo mengi..ya kidunia na kibiblia.. (Maarifa aliyonayo kuhusu biblia yanamtofautisha na mtu mwingine).. Vile vile maarifa anayokuwa nayo juu ya mambo mengine ya ulimwengu yanamtofuatisha na mkristo mwingine.
Watu wenye karama hii wakiwemo ndano ya kanisa, mafundisho ya manabii wa uongo ni ngumu kupata nafasi, (kwasababu manabii wa uongo wanawadanganya watu wasio na maarifa ya kutosha) sasa wakiwepo watu wenye karama hii ya maarifa, basi wanaweza kulifundisha kundi au kulielekeza mambo mengi kiusahihi kabisa.
Lakini wakikosekana ndio linatimia lile Neno “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa (Hosea 4:6)”
3. IMANI
Hii ni karama ya kutenda matendo ya Imani.. Watu wenye karama hii katika kanisa ni wale wenye kutenda au kuhamasisha watu katika kanisa kufanya matendo ya Imani. Na maisha yao yote yakijaa matendo ya Imani.
Huwa hawaogopi magonjwa, changamoto, wala dhoruba yoyote.. Kukitokea hofu wamesimama imara!, kanisa likiishiwa nguvu, watu wenye hii karama wanalitia nguvu na kulihamasisha..
Watu kama hawa wakiwepo katika kanisa basi kanisa hilo haliwezi kupungua nguvu ya kuendelea mbele, wala watu wake hawawezi kukata tamaa daima.
4. KARAMA ZA KUPONYA.
Zinaitwa “Karama za kuponya” na si “Karama ya kuponya”… Maana yake ni Karama hii inafanya kazi ya kuponya vitu vingi, ikiwemo magonjwa, maisha, roho, nafsi na vitu vingine vilivyoharibika.
Mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo wa kumwombea mtu na akapona kirahisi, au kumfundisha mtu na akapokea uponyaji kirahisi.. Vile vile ana uwezo wa kumwekea mtu mikono akapokea uponyaji kirahisi ikiwa ana ugonjwa au maisha yake yameharibika.
Vile vile anaweza kumfundisha mtu na mtu yule akaponyeka roho yake na majeraha ya adui.
Vile vile kama kazi ya mtu au maisha yake yameharibika mtu mwenye karama hii anaweza kumjenga upya kwa kumfundisha au kumwombea na mtu yule akaponyeka kabisa kabisa dhidi ya mapigo yote ya yule adui.
Watu kama wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa, basi kanisa hilo litakuwa na watu wanaosimama kila siku na hakuna atakayekuwa anaanguka.
5. MATENDO YA MIUJIZA.
Hii ni karama ya Ishara ndani ya kanisa. Watu wenye karama hii ni wale ambao maisha yao yamejaa miujiza na ishara.. Wakiwemo ndani ya kanisa basi ni lazima kuna miujiza itaonekana ambayo itawashangaza wengi na kuwafanya waaamini mahali pale kuna Mungu.
Kuna watu wakiingia mahali au wakienda mahali lazima kuna tukio la ajabu litatokea pasipo hata kupanga au kusema (ni ishara ambazo zinafuatana nao).
Kunatokea ajali ghafla anatoka mzima bila dhara lolote.. hajala wiki 2 lakini bado anaonekana ana nguvu zile zile.. Anafika mahali kivuli chake kinaponya watu.. anaimba tu au anaongea!, watu wanajazwa Roho Mtakatifu n.k
Watu wa namna hii kwa ufupi, wanakuwa wanafanya vitu vya ajabu, na kuwa na matukio mengi ya kushangaza shangaza na wengi wenye karama hii wanakuwa na vipindi vya kukutana/kutokewa na malaika. Yote ni kwa lengo la kuthibitisha uwepo wa Mungu katika kanisa.
6. UNABII
Hii ni karama inayohusika na kutabiri mambo yajayo au yanayoendelea sasa, au kuelezea yaliyopita.
Watu wenye karama hii wanakuwa na uwezo wa kuona mambo yajayo ya Mtu, Watu, kanisa au Taifa. Na nabii zao zinaegemea biblia. Na Mungu anawafunulia kwa njia aidha ya Ndoto, Neno au Maono.
Pia wana uwezo wa kumfundisha na kumwombea mtu au kumshauri kuhusiana na kile walichooneshwa! (kilichopita, kinachooendelea au kijacho).
Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa basi kanisa litasimama na kuendelea.
7. KUPAMBANUA ROHO.
Hii ni karama ya kupambanua au kuzijaribu roho. Mtu mwenye karama hii anakuwa mwepesi wa kuzitambua roho (kama ni roho wa Mungu au roho nyingine).
Kama kuna roho ya uchawi inaingia basi anakuwa na uwezo wa kupambanua, kama ni roho ya uzinzi, wizi, uadui, fitina, n.k anakuwa na uwezo wa kuiona kabla ya wengine na hivyo kutoa mashauri au kuomba iondoke.
Vile vile mtu mwenye karama hii anakuwa na uwezo wa kujua utendaji kazi wa Roho Mtakatifu, ni rahisi kujua karama za watu katika migawanyo yake..(kwamba huyu ana karama hii na yule ile).. Na pia anakuwa na uwezo mkubwa wa kufundisha juu ya karama za roho.
Watu wenye karama hii wakiwemo ndani ya kanisa.. ni ngumu sana kanisa hilo kushambuliwa na roho nyingine..
8. AINA ZA LUGHA.
Hii ni karama ya ishara ndani ya kanisa, ambayo madhumuni yake ni kama yale ya karama ya MIUJIZA.
Mtu mwenye karama ya lugha, anakuwa na uwezo wa kuzungumza lugha nyingi kimiujiza, (lugha za rohoni na za mwilini).. Lugha za rohoni ambazo (maarufu kama kunena kwa lugha).. mtu anakuwa na uwezo wa kuzinena na wakati mwingine kutoa tafsiri zake.
Lakini Zaidi sana anakuwa na uwezo wa kunena lugha nyingine za jamii nyingine.. Pindi anapojaa Roho Mtakatifu anajikuta anauwezo wa kunena lugha ya taifa lingine au kabila lingine ambalo sio lake, tena anazungumza vizuri sana.
Na watu wa wanapoona huyu mtu hajasoma kabisa lakini anaongea kiingereza kizuri namna hiyo, basi wanamshangaa Mungu na kumtukuza na kumwamini, na baadaye yule mtu akimaliza kunena basi anarudi katika hali yake ya kawaida ya kuongea lugha yake ya asili.
Watu wenye karama hii wakiwepo ndani ya kanisa..basi hofu ya Mungu inaongezeka na kuthibitisha kuwa Mungu yupo katikati ya kanisa lake.
9. TAFSIRI ZA LUGHA.
Hii ni karama ya 9 na ya mwisho iliyotajwa katika orodha hii.. Karama hii inahusiana pakubwa sana na ile ya “Aina za lugha”.. Kwani mwenye karama ya Aina za lugha, mara nyingine atamwitaji huyu mwenye Tafsiri za lugha ili aweze kutafsiri kinachozungumzwa.. ili kanisa lisiingie katika machafuko. (Soma 1Wakorintho 14:27).
Hizi ndizo karama 9 maarufu katika biblia. Zipo karama nyingine kama za kukirimu, au Uimbaji hizo zinaangukia katika kundi la huduma ya UINJILISTI, Mtu anayeimba anafanya uinjilisti, hivyo ni mwinjilisti!.
Na mtu anaweza kuwa na karama Zaidi ya moja, (Maana yake mtu anaweza kuwa na karama ya Imani na pia ya kinabii au ya Aina za Lugha, na Tafsiri za lugha hapo hapo) ingawa jambo hilo linakuwa ni nadra sana!…. Lakini Roho Mtakatifu ndiye anayemgawia mtu na si mtu anajipachikia!.
Na kumbuka!. Karama za Roho Mtakatifu ni kwa lengo la kufaidiana na si kuonyeshana au biashara.. Karama nyingi shetani kaziua kwa njia hiyo (anawapachikia watu kiburi, au kupenda sifa na utukufu na fedha).. mwisho wa siku kile kipawa kinazima!.
Ili kufufua karama iliyozima, njia ni kujishusha, kuwa mnyenyekevu, vile vile uwe na nia ya Kristo ya kulijenga kanisa, na pia ukubali na uheshimu kujengwa na karama nyingine, lakini ukijiona wewe ni wewe huhitaji wengine, fahamu kuwa hata cha kwako hakitaweza kufanya kazi.
Kanisa la siku za mwisho, tuna tatizo kubwa sana wa kuruhusu utendaji kazi wa Roho Mtakatifu kupitia karama zilizowekwa ndani yetu.. Na tatizo kubwa lipo kwa “viongozi” na “wasio viongozi (washirika)”.
Viongozi wengi hawaruhusu vipawa hivi vitende kazi aidha kutokana na wivu, au kutokuwa na maarifa ya kutosha kuhusiana na vipawa hivyo…
Lakini pia na watu wengine ndani ya kanisa (washirika) wanaoujenga mwili wa Kristo. Wanapokataa kujishughulisha vya kutosha na mwili wa Kristo, basi vile vipawa vilivyopo ndani yao vinazima, na hivyo kanisa linabaki na karama moja au mbili zinazofanya kazi.
Fahamu kuwa unapoenda kanisani, unacho kitu cha kiroho kwaajili ya ule mwili.. Ni wajibu wako kupambana mpaka kitokee, na kionekanane na kifanye kazi…usinyooshee tu kidole, wala usilaumu tu, na wakati huo wewe mwenyewe karama imekufa ndani yako (hujijui wewe ni nani/wala nafasi yako ni ipi), kanisani unaenda tu kama mtu anayeangalia Tv asiyehusika na mambo yanayoendelea kule (Hiyo haifai kabisa kwa mkristo aliyeokoka).
Ukiambiwa uombe huombi!! Karama yako itatendaje kazi ndani yako??,..ukiambiwa ufunge hufungi!! kuhudhuria tu kwenye ibada ni lazima ukumbushwe kumbushwe!..na bado unalaumu kanisani hakuna karama?..hiyo karama ipo kwa nani kama si ndani yako, na wewe umeiua kwa ukaidi wako???
Katika nyumba ya Mungu kila mtu lazima awe kiungo, ndipo udhihirisho mkamilifu wa Roho utaonekana.
Bwana akubariki na atusaidie.
NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.
JE! KARAMA NI UTHIBITISHO WA KUWA NA MUNGU?
USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.
Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?
JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?
WhatsApp
Mstari huu unaeleza uhalisia wa mambo kwa ujumla wake katika maisha ya wanadamu hapa duniani.
Tunafahamu kwamba maskini wengi hutumia maombi kupata kitu, huwa wanyenyekevu pale wanapotaka kupewa kitu, kwasababu hawana.
Lakini matajiri hawawezi kujishusha (japo si wote) kauli zao huwa ni za lazima na zenye amri. Kwani mali zake humpa kiburi. Hivyo waombe ya nini?
Sasa biblia haitufundishi tuwe matajiri ili tuwe wakali (wenye sauti) hapana, bali inatutahadharisha matokeo ya mafanikio yoyote. Jinsi yanavyoweza kumpotezea mtu unyenyekevu wake.
Bwana akunyanyuapo, ndio uwe wakati wako wa kujishusha. Kwasababu mali, fedha, mafanikio visipowekewa mipaka yake vinaweza kuyaharibu maisha ya mwaminio kwa sehemu kubwa. (1Timotheo 16:10)
Lakini pia katika eneo la kiroho. Kuna maneno haya Bwana Yesu aliyasema.
Mathayo 5:3
[3]Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Ikiwa na maana watu walio maskini rohoni, ni wale wanaojiona kila siku wana haja na Mungu, bado hawajafika. Na hivyo humlilia Mungu sikuzote kwa unyenyekevu ili Bwana ayaongoze maisha yao.
Lakini wale wanaojiona wamefika wanajua kila kitu hawawezi kufanya hivyo. Ndio wale mafarisayo enzi za Bwana Yesu ambao hata kuomba kwao kulikuwa ni kwa majivuno (Luka 18:9-14). Hawawezi kujishusha, maneno yao ni ya ukali, wala hawaoni shida kumwita hata Bwana wao Beelzebuli.
Hata kama tutakuwa tumepiga hatua kubwa kiasi gani rohoni, Bwana hataki tujidhani kuwa sisi tumefika, sisi ni matajiri, bali tumtegemee yeye sikuzote haijalishi wewe ni mtumishi mkubwa au uliyeokoka leo.
Unyenyekevu kwa Bwana unapaswa uwe ni uleule. Usiende mbele za Mungu kama mtumishi wa Mungu, nenda kama mtoto wa Mungu mfano tu wa yule ambaye kaokoka leo. Jinyenyekeze kama vile ndio umeokoka leo. Kwasababu kumjua Bwana itatuchukua milele.
Lakini tukijiona ni matajiri tutaishia katika anguko hili alilolisema katika..
Ufunuo 3:17-19
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. [18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. [19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Hivyo katika utajri wowote (wa kiroho /kimwili). Bwana atupe unyenyekevu kama wa maskini. Ndio kiini cha mstari huo.
Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.
ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?
SWALI: Nini maana ya Mithali 25:13
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.
JIBU: Kwa wanaoishi maeneo ambayo kuna misimu ya theluji, wanafahamu kuwa vipindi hivyo vya baridi vinapofika, huwa kunakuwa na upepo-baridi unaovuma.
Sasa kwa mujibu wa vifungu hivyo, anasema, Kama upepo huo ukivuma kipindi cha mavuno, ambacho kimsingi ni wakati wa kiangazi,na sio baridi, kingekuwa ni shangwe kubwa sana kwa wavunaji.
Kwa namna gani?
Kazi ya uvunaji inafanyika wakati wa jua kali, kwasababu mazao pia wakati huo yanakuwa yamekauka. Lakini pia mfano jua lile likapoozwa na upepo wa baridi, huuburudisha sana moyo wa mvunaji.
Vivyo hivyo anafananisha na wajumbe waaminifu wanaotumwa kupeleka habari fulani anasema;
“Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao”.
Mjumbe wa kwanza mwaminifu aliyetumwa ni Bwana wetu Yesu Kristo. Alimburudisha Baba moyo wake, kwasababu yote, na kusudi alilopewa kulifanya la kutukomboa sisi alilitimiza lote.
Vivyo hivyo na sisi, tumewekwa kuwa wajumbe wa Bwana, wa kuenenda kuihubiri injili ya Kristo kwa kila kiumbe, ulimwenguni kote. Yatupasa tuwe waaminifu, mfano wa Bwana na mitume wake, ili moyo wa Kristo wetu ufurahi.
Na thawabu ya kuuburudisha moyo wa Bwana ni sisi kupewa mamlaka kubwa kule ng’ambo tufikapo, kwa mfano ambao Bwana Yesu aliutoa katika vifungu hivi;
Luka 19:12-26
[12]Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi. [13]Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja. [14]Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale. [15]Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake. [16]Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi. [17]Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi. [18]Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida. [19]Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano. [20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. [21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. [22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; [23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? [24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. [25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. [26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho.
[12]Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.
[13]Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.
[14]Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.
[15]Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
[16]Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
[17]Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
[18]Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
[19]Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
[20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
[21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
[22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
[23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
[24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
[25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
[26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho.
Je na sisi tunaweza kuwa mbele za Bwana Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; ?
Bwana atusaidie.
Je! Umeokoka?
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)
Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?
WALIYATWAA MAVAZI YAKE, WAKAFANYA MAFUNGU MANNE,
Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?
AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.
(Masomo maamulu kwa watumishi wa Mungu).
Je wewe ni mtumishi wa MUNGU?..Basi fuatilia mfululizo wa masomo haya katika tovuti yetu hii (www.wingulamashahidi.org).
Kama mtumishi wa Mungu kuna Anwani au nembo au Lebo ambayo inapaswa iambatane na kila fundisho unalolitoa kwa wahusika. Na Anwani/lebo hiyo/nembo hiyo si nyingine Zaidi ya “TOBA”. Hakikisha mahubiri yako yanalenga Toba, au kuwakumbusha watu umuhimu wa kujitakasa.
Kwanini iko hivyo?
Hebu tujifunze kwa mmoja ambaye ni mjumbe wa Agano, tena ndiye Mwalimu wetu MKUU na Mwinjilisti MKUU YESU KRISTO.
Yeye katika mahubiri yake yote alihubiri “Toba”.. Huenda unaweza kusoma mahali akiwa anafundisha na usione likitajwa neno Toba, lakini fahamu kuwa alikuwa anahubiri Toba kila siku katika mafundisho yake yote… Kwani biblia inasema kama yote aliyoyafanya BWANA YESU kama yangeandikwa basi dunia isingetosha kwa wingi wa vitabu.
Yohana 21:25 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”
Kwahiyo Mahubiri ya BWANA WETU YESU yote Yalikuwa yamejaa toba.. sasa tunazidi kulithibitishaje hilo?.. hebu tusome maandiko yafuatayo..
Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”
Nataka tuutafakari kwa undani huu mstari… anasema “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”…. Zingatia hilo neno “TOKEA WAKATI HUO….TOKEA WAKATI HUO…TOKEA WAKATI HUO”.. Maana yake “kilikuwa ni kitu endelevu”, sio kitu cha kusema mara moja na kuacha, (hiyo ndiyo ilikuwa lebo ya mafundisho yake daima).. Kila alipohubiri lazima aliwahubiria pia watu watubu.
Umeona?. Je na wewe Mchungaji, na wewe Mwalimu wa injili, na Wewe nabii, na wewe Mtume, na wewe Mwimbaji wa injili.. LEBO YA MAHUBIRI YAKO NI IPI????.
Je! injili yako unayohubiri ni ya TOBA, au ya kuwafariji watu katika dhambi zao??.. Je unazunguka huku na kule kuhubiri injili ya namna gani?..Je ni injili ya Toba au ya Mali tu!.
Luka 24:45 “Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. 46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; 47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. 48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya”
Luka 24:45 “Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya”
Hakuna furaha, hakuna mafanikio, hakuna Amani ikiwa mtu yupo katika maisha ya dhambi.. utamhubiria afanikiwe lakini hata akiyapata hayo mafanikio basi dhambi itamuua tu na kumkosesha raha.. Raha pekee na Amani mtu ataipata baada ya kutubu, ndivyo maandiko yasemavyo..
Matendo 3:19 “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana”
Toba ni nini?
VYA MUNGU MPENI MUNGU.
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?
WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.
Tunapokisoma kisa cha Daudi, cha kumwiba mke wa shujaa wake (Uria), na kumlazimisha kuzini naye kwa siri, na baadaye kumuua mumewe , (2Samweli 11) tunaishia kuona picha mbaya sana ya Daudi. Na kumshutumu, na wengi wetu kusema Daudi ni mzinzi sana, iweje apendwe na Mungu namna ile, tena awe kipenzi cha Mungu?
Ni kweli kabisa alichokifanya Daudi hakistahili kufanywa na mtu yeyote, ambaye anamjua Mungu, mfano wa Daudi. Lakini kuna funzo kubwa sana ambalo wengi wetu hatulioni nyuma ya maisha ya Daudi baada ya pale.
Daudi alipozama katika dhambi ile, na kugundua makosa yake. Alikuwa na badiliko lisilo kuwa la kawaida. Sio kule alikokuwa anaomboleza usiku kucha, Hapana, lile lingekuwa la “kufoji” tu, ambalo yoyote anaweza kulifanya hata leo. Kinyume chake Daudi alikuwa na badiliko la kimatendo. Na hilo ndilo lililomfanya apendwe sana na Mungu.
Sasa angalia Daudi Yule Yule ambaye alikuwa ni mzinzi, mwenye tamaa ya hali ya juu,akiona tu mwanamke mzuri hajali, huyu ni mke wa mtu au la yeye alimwiba na kuzini naye. Lakini Dakika zake za mwisho hazikuwa hivyo. Alibadilika kwelikweli baada ya dhambi ile.
Utakumbuka hata alipokuwa mzee, Wakuu wa Israeli walikwenda kumtafutia Binti mzuri bikira katika taifa lote la Israeli, ili amlalie Daudi ampe joto kwasababu nguo za joto hazikutosha. Lakini biblia inasema Daudi alipolala naye ‘hakumjua’.
Kwa jinsi ya kibinadamu, binti alale, na mtu mwenye sifa ya tamaa kama Daudi, halafu asimwingilie. Lazima kutakuwa kuna jambo lingine limetendeka ndani ya maisha ya huyo mtu.
Tusome;
1 Mfalme 1:1
“Daudi alikuwa mzee, mkongwe katika siku zake, nao wakamfunika nguo, lakini asipate moto. 2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, Bwana wangu mfalme na atafutiwe kijana mwanamwali; naye asimame mbele ya mfalme, amtunze; alale kifuani mwako, ili bwana wangu mfalme apate moto. 3 Basi wakatafuta kijana mzuri mipakani mwote mwa Israeli, wakamwona Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme. 4 Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua”
“Daudi alikuwa mzee, mkongwe katika siku zake, nao wakamfunika nguo, lakini asipate moto.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, Bwana wangu mfalme na atafutiwe kijana mwanamwali; naye asimame mbele ya mfalme, amtunze; alale kifuani mwako, ili bwana wangu mfalme apate moto.
3 Basi wakatafuta kijana mzuri mipakani mwote mwa Israeli, wakamwona Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
4 Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua”
Ni wazi kuwa habari hiyo ilijulikana Israeli nzima, Daudi amelala na binti bikira mrembo miaka kadhaa lakini hajamwingilia. Ni shujaa kiasi gani. Hawakujua kuwa anawathibitishia Israeli kuwa yeye sio Yule wa zamani, sio Yule mzinzi mliyemzoea, ameshabadilika. Si mtu wa kulipuka lipuka tamaa ovyo kama alivyokuwa hapo mwanzo.
Hiyo ndio sababu Mungu alimpenda Daudi. Kwasababu alikuwa na badiliko la dhati Kwa Mungu wake. Je! Na sisi, tunaweza kusema tumeuacha ulimwengu kweli kweli pale tunapomgeukia Mungu, au tutakuwa na vimelea vya kidunia ndani yetu, pale tunapokutana na majaribu kama yale yale ya mwanzo. Tulipokuwa wazinzi na sasa tumeokoka, Je! Tuna ujasiri wa kuishi maisha ya mbali zinaa, au bado tupo nusu nusu.
Tuwe na badiliko la dhati, leo tumeanguka katika dhambi Fulani mbaya, sasa tumetubu, tusiwe tena walewale wa kuanza kuangalia angalia nyuma kama mke wa Lutu. Mungu atakuchukizwa na sisi na mwisho wa siku tutakuwa jiwe la chumvi kama sio kutapikwa mfano wa kanisa la Laodikia.
Tumaanishe kwelikweli kuacha mambo maovu tuliyoyazoelea. Jifunze kwa Daudi. Yule sio mzinzi kama wewe unayejitumaisha kwa visa vyake vya zamani, ukadhani kuwa utanusurika hukumu ikiendelea na tabia hiyo.
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?(Opens in a new browser tab)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4
Kwanini Daudi achukue mawe matano, na malaini na sio vinginevyo?
(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)MADHIHIRISHO MATATU YA MUNGU.(Opens in a new browser tab)
Masomo maalumu yahusuyo (Wanawake na mabinti).
Alamothi ni nini? Na nini ufunuo wake? (1Nyakati 15:20)
Jibu: Tusome,
1Nyakati 15:19 “Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu; 20 na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya SAUTI YA ALAMOTHI”
1Nyakati 15:19 “Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu;
20 na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya SAUTI YA ALAMOTHI”
“Alamothi” maana yake ni “wanawake vijana”… Hivyo hapo anaposema vinanda vya sauti ya Alamothi, maana yake ni vinanda vya sauti za “wanawake vijana”.
Hiki ni kipindi ambacho Mfalme Daudi alikuwa analitoa sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumbani kwa Ben-edomu na kulipandisha Yerusalemu.
Na wakati wanalipandisha Daudi aliwaandaa wana wa Asafu (watu walio hodari wa kuimba) wenye matoazi pamoja na kundi lingine la watu nane (8) viongozi wa sifa, wenye vinanda vitakavyotoa sauti kuwafuatiliza wanawake vijana waimbaji (Alamothi).
Ni nini tunajifunza?
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni jinsi “wanawake walivyo na nafasi kubwa katika kumwimbia Mungu”. Daudi aliona, wana wa Asafu pekee haitoshi (ambao ni wanaume) …..zinahitajika pia sauti za wanawake vijana, katika kumwimbia Mungu. Na utaona jambo hilo Mungu alilikubali sana na likawa Baraka sana kwa Mfalme Daudi.
Na Mungu ni yule yule hajabadilika, kama alizikubali sifa za Daudi na kundi lake, atafanya hivyo hata leo, ikiwa tutasimama vyema katika nafasi zetu.
Ikiwa wewe ni mwanamke au binti.. fahamu kuwa sauti yako ni ya thamani sana katika kumwimbia Mungu, (ndio maana si nzito kama ya mwanaume). Hivyo chukua nafasi hiyo katika kulitimiza kusudi la Mungu ndani yako. Tafuta namna yoyote umwimbie Mungu na Bwana atakubariki.
Zaburi ya 46 ambayo iliandikwa na wana wa Kora, ni Zaburi maalumu kwa ALAMOTHI. Ni nyimbo iliyokusudiwa iimbwe na Maalamothi, yenye kumtukuza Mungu kuhubiri uweza wake.
Zaburi 46:1 “Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. 2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. 3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake. 4 Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye juu. 5 Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema. 6 Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki; Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka. 7 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. 8 Njoni myatazame matendo ya Bwana, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. 9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari. 10 Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. 11 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu”
Zaburi 46:1 “Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.
4 Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye juu.
5 Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki; Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka.
7 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njoni myatazame matendo ya Bwana, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.
10 Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.
11 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu”
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?
Ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda.
TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.
Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
AGANO LA KALE
Vitabu vya Agano la Kale vimegawanyika katika makundi makuu manne (4)
1. VITABU VYA SHERIA. (Tazama jedwali chini).
2. VITABU VYA HISTORIA (Tazama Jedwali chini).
3. VITABU VYA MASHAIRI (Tazama Jedwali chini).
4. VITABU VYA MANABII WAKUBWA (Tazama Jedwali chini).
5. VITABU VYA MANABII WADOGO (Tazama jedwali chini).
AGANO JIPYA
Vitabu vya Agano jipya vimegawanyika katika makundi makuu matano (5)
1. VITABU VYA INJILI (Tazama jedwali chini)
2. KITABU CHA HISTORIA (Tazama jedwali chini)
3. VITABU VYA NYARAKA ZA PAULO MTUME (Tazama jedwali chini)
4. VITABU VYA NYARAKA KWA WATU WOTE (Tazama jedwali chini)
5. KITABU CHA UNABII (Tazama jedwali chini)
MAJINA YA MANABII WANAWAKE
MANABII WA BIBLIA (Wanaume)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).
MAJINA YA MITUME WA BWANA YESU