Category Archive maswali na majibu

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Jibu: Tusome,


Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”

Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).


Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?


1) Mitume na Manabii:


Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.


Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.


2) Msingi


Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.


1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.


YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.


Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.


Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.


Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k


Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.


Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia inasema tujihadhari na “Mbwa” hawa mbwa ni akina nani? (Wafilipi 3:2)

Jibu: Tusome..

Wafilipi 3:2  “Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao”

Hapa kuna makundi matatu yaliyotajwa ambayo tunapaswa tujihadhari nayo, kundi la Kwanza ni “MBWA” kundi la Pili ni “WATU WAJIKATAO” na kundi la tatu ni “WATU WATENDAO MABAYA”.

Sasa kabla ya kwenda kuangalia Mbwa ni watu wa namna gani, kwanza tuyatazame haya makundi mawili ya mwisho, ambayo ni watu wajikatao na watenda mabaya..

Watu “watendao mabaya” wanaozungumziwa hapo, ni watu walio ndani ya imani lakini wanatenda mabaya.. watu hawa biblia imetuonya tujihadhari nao, yaani tusichangamane.. Mtume Paulo alizidi kuliweka hili vizuri katika kitabu cha 1Wakorintho 5:9-11.

1Wakorintho 5:9  “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10  Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11  Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye”.

Lengo la kutochangamana na makundi haya ya watu walio ndani ya kanisa lakini ni watenda mabaya, ni ili wajisikie aibu kwa wanayoyafanya na hatimaye wageuke na kutubu.

Kundi la Pili: Ni “Watu Wajikatao”.. kumbuka hapa anasema “watu wajikatao” na sio “watu wajikataao” kuna tofauti ya kujikata na kujikataa.. hapa wanazungumziwa watu wanaojikata!.. Sasa ni watu gani hao wanaojikata?.. si wengine bali walikuwa ni wayahudi ambao walikuwa wanashinikiza tohara, kuwa ndio dalili ya kukubaliwa na Mungu..

Lilikuwepo kundi la walioamini, ambao hata sasa lipo lililokuwa linasisitiza tohara kuwa ni jambo la lazima, na kwamba mtu asipotahiriwa hawezi kukubaliwa na Mungu. Watu hawa walikuwa kweli wamemwamini Yesu lakini sheria za torati bado zilikuwa zinawaendesha, ambazo kimsingi hizo haziwezi kumkamilisha mtu, bali Neema ya Yesu pekee… kushika mwezi, mwaka, siku, sabato haya yote hayafai katika kumkamilisha mtu.

1Wakorintho 7:19  “Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.

20  Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa”

Kwa maelezo mengine marefu kuhusiana na watu wajikatao unaweza kufungua hapa >>> WATU WAJIKATAO

Na kundi la Tatu na la Mwisho, ambalo biblia imetaja tujihadhari nalo ni kundi la “MBWA”.

 Sasa utajiuliza hawa “Mbwa” ni akina nani?

Bwana Yesu aliwataja wazi kabisa hawa Mbwa ni wakina nani.. Tusome..

Mathayo 7:15  “Jihadharini na MANABII WA UONGO, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni MBWA-MWITU WAKALI.

16  Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”

Umeona?… Kumbe Mbwa wanaozungumziwa hapo ni “Manabii wa Uongo” na tena hawajatwi kama Mbwa tu!, bali kama “Mbwa-Mwitu” tena wakali!.. maana yake wasiohurumia kundi.. Na hatutawatambua kwa mionekano yao, kwasababu kwa nje wamevaa mavazi ya kondoo, (wanafanana na watumishi wa kweli wa Mungu) lakini tutawatambua kwa matunda yao, maana yake kwa yale wanayoyafundisha na wanayoyaishi.

Na manabii wa uongo ni mjumuisho wa Mitume wa Uongo, wachungaji wa uongo, waalimu wa Uongo, pamoja na waimbaji wa Uongo. Kwaufupi watu wote wanaosimama kutangaza injili kwa wengine! Lakini maisha yao ya ndani si wakristo, ila kwa nje wanasifika kama watumishi wa Mungu.

Ikiwa mtu atasimama na kuhubiri injili nyingine tofauti na ile iliyoandikwa katika biblia, basi huyo kibiblia ni “Mbwa”, ikiwa mtu atahubiri injili isiyo ya wokovu, badala yake ya kumpoteza mtu au kumfanya afurahie dhambi..mtu huyo kibiblia ni Mbwa, na tumetahadharishwa kukaa mbali naye.

Nabii wa Kweli wa Mungu atakuwa kama Musa!, Mpole kuliko wote, na mwenye kuwaelekeza watu kwa Mungu na si kwake wala kwa shetani.

Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

 2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

 3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye”

Je! Unaongozwa na nani?.. Manabii wa Uongo, Miujiza na Ishara au NENO LA MUNGU?.

Kumbukumbu 6:4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 

5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).

Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

Rudi nyumbani

Print this post

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 8 ili tuweze kuelewa vizuri..


Mathayo 22:8 “Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? NAYE AKATEKEWA”.


“Kutekewa” kunakozungumziwa hapo si Kutekewa maji au kinywaji fulani, hapana!…Bali maana yake Ni “KUKOSA MANENO”


Mtu anayekosa Neno la kujibu pale anapoulizwa, mtu huyo Ndio katekewa..
Katika habari hiyo Bwana Yesu anatoa mfano wa mtu aliyeishiwa maneno baada ya kukutwa hana vazi la harusi.


Hali itakayokuwa kwa wengi katika Ile siku ya mwisho. Maandiko yanaonyesha kuwa katika siku ya mwisho, Bwana atawakataa watu wengi, ambao hawakuwa na vazi la Harusi walipokuwa duniani.
Na vazi la harusi maandiko yameweka wazi kuwa Ni “Matendo ya haki ya watakatifu”.


Ufunuo 19:8 “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”


Katika siku ile wengi watadhani Ni dini zao zintakazowapa kibali Cha kuingia uzimani, wengine watadhani Ni Imani zao n.k. pasipo kujua kuwa bila utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu.


Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”


Na Utakatifu hatuupati kwa nguvu zetu, Bali kwa msaada wa Bwana.


Tunapotubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi Kama bado hatujabatizwa Basi Bwana anatupa Roho wake mtakatifu ambaye huyo ndiye atakayetusaidia sisi kuweza kuwa wakamilifu na watakatifu.


Hivyo tukiupata utakatifu katika maisha yetu, Basi katika Roho tutaonekana mbele zake tumevaa vazi la harusi na hivyo siku Ile hatutatekewa mbele zake, hatutaishiwa maneno.


Lakini tukiyakosa hayo, huku tukitumainia dini zetu, na madhehebu yetu, na theologia zetu… basi tujue kuwa tutakosa cha kujibu mbele zake siku Ile..


Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Rudi nyumbani

Print this post

Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.

Jibu:  Adhabu iliyompata Adamu na Hawa, haikutokana na hasira ya Mungu!.. bali ilikuwa ni matokeo ya walichokifanya.

Hebu tafakari mfano huu…. “unamwonya mtu asile kitu Fulani kwasababu unajua madhara ya hicho kitu kwamba endapo akikila basi kitamsababishia apofuke macho na hata kufa huko baadaye, kwasababu kina sumu mbaya ndani yake”.

Lakini huyo mtu ambaye ulimtahadharisha asifanye hivyo, hakukusikiliza wewe badala yake akaenda kula hicho kitu ambacho madhara yake ni kupofuka macho na hata kufa. Na siku alipokula wewe ukajua na kwa huzuni  ukaenda kumwuliza kwanini ulikula?..yeye akatoa sababu zake anazozijua yeye, kisha wewe ukamwambia kwamba.. “kwasababu umekula hicho kitu basi macho yako yatapofuka siku si nyingi  na pia utakufa!.

Sasa swali ni je!, kwa wewe kumwambia hivyo kwamba “atapofuka macho na kufa” je umemhukumu, au umemwambia tu mambo yatakayompata kutokana na kitu alichokifanya?.. Au je kwa wewe kumwambia hivyo, kuna uhusiano wowote wa wewe kumsamehe au kutomsamehe?.. Jibu ni la!, wewe umemwambia tu madhara ya alichokifanya na kuanzia pale utaanza kumhurumia na kumtafutia suluhisho ili ile sumu iliyoingia ndani yake iweze kutoka….

Ndicho kilichotokea pale Edeni, adhabu aliyoipata Adamu na Hawa ni kwasababu ya matokeo ya walichokifanya na si kwasababu ya hasira ya Mungu!!. Na Mungu kwa huruma zake, kuanzia pale ndio akaanza mpango wa kumponya mwanadamu kwa madhara aliyoyaingiza katika maisha yake.

Na ndipo akapata mpango bora, ambao huo utaondoa moja kwa moja madhara yaliyoingia ndani ya Mwanadamu, na mpango huo si mwingine zaidi ya ule wa kumtoa Mwanawe wa pekee YESU KRISTO, aje kufa kwa ajili ya dhambi zetu, na kutukomboa, kuanzia hapo Mungu akamtoa Adamu pale Edeni ili amweke katika mpango mpya na ulio kamili, utakaomkamilisha.

Yesu Kristo pekee ndiye tiba ya KIFO  ambacho kilikuwa kimeingia katika maisha yetu tangu siku ile wazazi wetu, Adamu na Hawa walipoasi.

Yohana 11:25  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”

Yesu Kristo ndiye tiba ya mambo yote, ndiye suluhisho la matatizo yote ya maisha, na pasipo yeye sisi hatuwezi kufanya lolote.

Yohana 15:5  “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”.

Na nje ya Yesu Kristo hapana wokovu..

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

Je! Umempokea Yesu katika maisha yako?.. je umebatizwa katika ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu wa kweli?. Kama bado unasubiri nini?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

JINA LAKO NI LA NANI?

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Yesu ni Mungu au Nabii?

Maandiko yanaonyesha kuwa YESU ni Mungu na pia ni NABII.  Ni sawa na mkuu wa nchi anaweza kuwa RAISI kwa wananchi, lakini pia anaweza kuwa BABA au MAMA kwa watoto wake. Hivyo mtu mmoja anaweza kuwa na vyeo zaidi ya kimoja kufuatana na mazingira aliyopo. Raisi akiwa ofisini ataitwa Raisi, akiwa nyumbani kwake na watoto wake ataitwa Baba/mama.

Vile vile Kristo akiwa mbinguni ni Mungu, akiwa duniani ni Mwana wa Adamu na Nabii na Mwokozi, na akiwa ndani yetu ni Roho Mtakatifu.

Sasa ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa ni Nabii?

Luka 24:19  “Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, ALIYEKUWA MTU NABII, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote”

Kumbukumbu 18:15 “Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”.

Vile vile ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu?

Mathayo 16:15  “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16  Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”

Na ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa YESU alikuwa Mungu?

Tito 2:13  “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”

Soma pia 1Timotheo 3:16 na Yohana 1:1.

Kwahiyo Yesu ni yote katika vyote, na ndio Mwokozi wa Ulimwengu, na ndiye Njia ya kufika mbinguni. Hakuna mwanadamu yeyote atakayefika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.

Je umempokea Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kalibu maana yake nini? (Mathayo 6:30).

Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?”

Neno hili “kalibu” limerudiwa pia kutajwa katika Luka 12:28, na maana ya neno hili ni “TANURU LA MOTO”. Kwa kawaida baada ya kusafisha mazingira, kwa kuondoa Nyasi au takataka huwa zinatupwa katika tanuru la moto, sasa tanuru hilo ndilo linaloitwa “Kalibu”, Na Bwana Yesu alitoa mfano huo kuonyesha maisha yetu jinsi yalivyo na thamani mara nyingi zaidi kuliko maua ya kondeni.

Kwani kama Mungu anavyoyavika utukufu maua ya kondeni, kwa rangi rangi zake za kuvutia, basi sisi ni zaidi sana mbele zake kuliko hayo MAUA ya kondeni, ambayo leo yapo lakini kesho yanatupwa motoni.. Sisi tuna thamani mbele zake kuliko maua, maana yake sisi atatuvisha zaidi kuliko Maua, atatulisha zaidi kuliko ndege, atatubariki kuliko viumbe vyote vya asili. Huo ni upendeleo wa kipekee sana.

Tunachopaswa kufanya ni kuutafuta tu ufalme wake na haki yake, halafu hayo  mengine ya chakula, mavazi tumwachie yeye, kasema atatuzidishia, na yeye kamwe hawezi kusema uongo.

Luka 12:29 “Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,

30  kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.

31  Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.

32  Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Nyinyoro ni nini?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

Jibu: Tusome,

Waamuzi 18:2 “Basi wana wa Dani wakatuma watu wa jamaa zao, watu watano katika hesabu yao yote, watu mashujaa, kutoka Sora, na kutoka Eshtaoli, ili kuipeleleza hiyo nchi, KUIAUA; wakawaambia, Haya, endeni mkaikague nchi hii; basi wakaifikilia nchi ya vilima vilima ya Efraimu, hata nyumba ya huyo Mika, Wakalala huko”

Kuiaua nchi maana yake ni KUITEMBELEA NCHI au KUIZURU. Kwahiyo watu wanaozunguka zunguka ndani ya nchi kwa lengo la kuipeleleza au kwa lengo la utalii, maana yake ni WAMEIAUA HIYO NCHI.

Mungu wetu anaiaua dunia hii tunayoishi, kutafuta watu wanaomcha yeye, kuwatia nguvu na kuonyesha uweza wake juu yao.

2Nyakati 16:9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake…”

Lakini pia adui yetu shetani ANAIAUA dunia nzima kutafuta mwenye haki mmoja amwangushe..

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 

7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

 8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”

Hivyo hatuna budi kuutunza ukamilifu wetu ili tusije tukanaswa katika mitego ya shetani na hatimaye kuanguka kabisa.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.

Rudi nyumbani

Print this post

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Jibu: Tusome,

1Samweli 28:24 “Naye yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona nyumbani; akafanya haraka kumchinja; akatwaa na unga, akaukanda, akafanya MKATE WA MOFA kwa unga huo”.

Mkate wa Mofa ni mkate uliotengenezwa bila kuwekwa “Hamira”.  Hamira kwa lugha ya kibiblia inaitwa “Chachu” kazi yake ni kuchachusha au kuumua unga uliokandwa, kama biblia inavyosema katika..

Mathayo 13:33  “Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia”

Na tena biblia inasema.. “Chachu kidogo huchachua donge zima (Wagalatia 5:9)”

Kwahiyo Mikate ya Mofa ni mikate iliyotengenezwa bila kuwekwa hamira, mfano wa chapati. Kwa  wayahudi baada ya sikukuu ya pasaka kupita, sikukuu iliyokuwa inafuata ilikuwa ni sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu (yaani Mofa),  Ndani ya siku 7 Wana wa Israeli waliambiwa wale mikate ya Mofa, na mtu yeyote ambaye alionekana anakula mikate mingine zaidi ya hiyo, aliuawa kulingana na sheria ya torati.

Na ndani ya kipindi hicho pia mtu yeyote akionekana na Viungo vya Hamira ndani kwake, hata kama atakuwa hajaviweka kwenye unga, kitendo tu cha kuiweka ndani ilikuwa pia adhabu yake ni kifo

Kutoka 12: 15 “Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba; siku hiyo ya kwanza mtaondoa chachu yote isiwe katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula mkate uliochachwa tangu siku hiyo ya kwanza hata siku ya saba, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na Israeli”.

Soma pia Walawi 23:5-6.

Lakini je! Mkate wa Mofa unawakilisha nini kiroho?

Mkate wa Mofa unawakilisha Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo,  Na ndio uliotumika na wakristo wa kanisa la kwanza katika kushiriki Meza ya Bwana, na ndio unapaswa utumike hata sasa katika kushiriki meza ya Bwana, na si biskuti au maandazi!.

Luka 22:19  “Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu”.

Sasa kwanini Bwana Yesu achague mkate wa Mofa, kuwakilisha Mwili wake?

Ni kwasababu Mwili wa Bwana Yesu haubadiliki wala hauwezi kubadilishwa maumbile. Hamira/chachu kazi yake ni kubadilisha maumbile ya vitu, ndio maana inapowekwa kwenye unga uliokandwa baada ya muda Fulani utakuta ule unga umeumuka!

  Sasa mwili wa Kristo hauumushwi, wala hauwezi kubadilishwa kimaumbile..bali siku zote ni ule ule!(Waebrania 13:8).. Maana yake kanuni za Bwana Yesu ni zile zile, hazibadilishwi na mazingira wala na mtu, Neno lake ni lile lile jana na leo na hata milele.

Hatuwezi kutia hamira Neno la Mungu, Neno la Mungu likisema ulevi ni dhambi!, hatuwezi kuliwekea hamira hapo na kusema ulevi sio dhambi!..likisema “mtu anapaswa avae mavazi ya kujisitiri” hatuwezi kulitia hamira kwa kusema “Mungu haangalii roho bali anaangalia mwili (1Timotheo 2:9)”

Na mambo mengine yote, biblia iliyoyataja ni lazima tuyazingatie yabaki kama yalivyo bila kuumuliwa na hamira za mafundisho ya uongo.

Bwana Yesu atusaidie katika hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Nini tofauti kati ya Bustani ya Edeni (Mwanzo 2:8) na bustani ya Adeni (Ezekieli 28:13 na  Yoeli 2:3)

Jibu:Tusome

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa EDENI, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya”.

Isaya 51:3 “Maana Bwana ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama BUSTANI YA EDENI, na nyika yake kama bustani ya Bwana; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba”. 

Hapa tunaona ikitajwa bustani ya “Edeni” lakini tukisoma mahali pengine tunaona ikitajwa bustani nyingine ya “Adeni”

Ezekieli 28:13 “Ulikuwa ndani ya ADENI, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari”

Yoeli 2:3 “Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na BUSTANI YA ADENI mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao”.

Na pia katika Ezekieli 31:9, Ezekieli 31:16-18, na  Ezekieli 36:35 utaona ikitajwa Adeni na si Edeni, swali je kuna utofauti wowote?

 Jibu ni la! hakuna utofauti wowote iliyopo kati kati ya “Adeni” na “Edeni”, hayo ni maneno mawili yenye maana moja, sehemu moja biblia imetaja Edeni, sehemu nyingine Adeni lakini maana ni ile ile..Na maana ya neno Edeni au Adeni ni “paradiso ya raha”.

Mungu alipoiumba dunia, alimweka mwanadamu wa kwanza katika bustani ya Edeni, na alikusudia mahali pale pawe Paradiso yake ya milele. Dunia yote ilikuwa ni nzuri, lakini pale Edeni palikuwa ndio kitovu cha utukufu wa mwanadamu.

Lakini baada ya shetani kumdanganya Hawa, ndipo Uovu ukaingia na kusababisha mwanadamu kuondolewa katika bustani ile, na Mungu kuitowesha kabisa!

Lakini Bwana ameahidi kuumba Mbingu Mpya na Nchi mpya (Isaya 65:17), ambayo itakuja baada ya utawala wa miaka elfu kuisha hapa duniani. Katika mbingu mpya na nchi mpya, Bwana ametuandalia mambo mazuri kuliko yaliyokuwepo Edeni, maandiko yanasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia mambo ambayo Mungu kawaandalia wale wampendao..(1Wakorintho 2:9).

Lakini ahadi hiyo kulingana na Neno lake ni kwa wale waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake.

Je umempokea Yesu?..kama bado unasubiri nini?. Mwamini leo na ukabatizwe katika ubatizo na ujazwe Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

EDENI YA SHETANI:

Je! Ni kweli Yesu alirejesha kila kitu kama pale Edeni?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kukaramkia ni kufanya nini? (2Wakorintho 7:2)

Swali: Kukaramkia ni nini?

Jibu: Tusome,

2Wakorintho 7:2  “Tupeni nafasi mioyoni mwenu. Hatukumdhulumu mtu ye yote, wala kumharibu mtu, wala kumkaramkia mtu.

3  Sisemi neno hilo ili niwahukumu ninyi kuwa na hatia; kwa maana nimetangulia kusema, ya kwamba ninyi mmo mioyoni mwetu hata kwa kufa pamoja, na kuishi pamoja”

“Kukaramkia” ni Kiswahili kingine cha neno “Utapeli” (ambao unahusisha kuchukua fedha kutoka kwa mtu kwa njia ya ulaghai wa maneno). Mfano wa watu wanaokaramkia watu ni manabii wa uongo, na makristo wa uongo!, ambao wanaweza kutumia chochote kile kudanganya nacho watu, ili lengo lao wapate fedha kutoka kwao. ( Na fedha hizo ndizo zijulikanazo Kama mapato ya aibu, ambayo yanatajwa katika kitabu Cha Tito 1:7)

Katika siku hizi za mwisho manabii wa uongo wanatumia maji, mafuta, udongo na vyote vijulikanavyo kama visaidizi vya upako kulaghai watu, hivyo wanawakaramkia watu na kuchukua fedha zao na mali zao, huku wakiwaaminisha kuwa matatizo yao yameondoka.

Watumishi hawa wa uongo, maandiko yanasema kuwa mungu wao ni tumbo!!..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”

Mitume wa kanisa la kwanza hawakumkaramkia mtu yeyote, ili kupata faida.. Zaidi walihubiri injili kamili yenye kumgeuza mtu kutoka katika dhambi kuingia katika haki kupitia Yesu Kristo.

Na sisi hatuna budi kuwa kama hao, tuifanye kazi ya Mungu bila kumkaramkia mtu yeyote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

Je jina Eva na Hawa ni sawa?

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

JIHADHARI NA DHAMBI YA WIVU/HUSUDA.

Rudi nyumbani

Print this post