Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Kama kitabu kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo Mtume kwa Waefeso”. Paulo ndiye aliyeuandika waraka huu.

Aliuandika akiwa kama mfungwa kule Rumi.

Waraka huu una sura sita(6), ambazo tunaweza kuzigawanya katika makundi mama mawili.

1) kundi la kwanza ni Sura ya 1-3,

Sura hizi zinaeleza asili ya Imani yetu iliyo katika Kristo Yesu jinsi ilivyo ya kipekee kwa nguvu na mamlaka, na ubora, na uweza na ukuu, na utajiri, na utukufu usiopimika, kwa akili za kibinadamu.(1:20-23).

2) Lakini kundi la pili ni Sura 4-6

Inaeleza juu ya mwenendo wetu, jinsi unavyopaswa uwe katika imani tuliyoipokea. Kwasababu ni vitu vinavyokwenda sambamba, haviwezi kutenganishwa, katika fundisho la ukristo.

Kwa ufupi; Katika Kundi la kwanza Yafuatayo ni mambo mama ambayo mwandishi ameyazungumzia juu ya mambo tunayoyapata ndani ya mwokozi wetu Yesu Kristo.

  1. Katika yeye tumebarikiwa katika baraka zote za rohoni (1:3). Akiwa na maana hakuna laana yoyote inayotukalia pindi tu tunapomwamini.
  2. Katika Kristo tunao ukombozi wetu ambao ni masamaha ya dhambi (1:7). Akiwa na maana dhambi zetu zote zimefutwa, wala kumbukumbu lake halipo.
  3. Katika yeye kwa njia ya masalaba wake kile kiambaza cha kati kimeondolewa, hivyo hakuna tofauti tena kati ya malaika walio mbinguni na sisi tuliopo duniani, mbele za Mungu (1:9-10), lakini si vya mbinguni na duniani tu, bali pia tofauti iliyokuwepo kati ya sisi na wayahudi imeondolewa kwa msalaba wake (3:5-11). Wote tunaitwa watoto wa Mungu (3:14)
  4. Katika Kristo tufahamu kuwa tulishachaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, hivyo tutambue si suala lililojitokeza tu ghafla, au kwa bahati (1:4), bali Mungu alituona tangu zamani.
  5. Katika Kristo tumepewa hakikisho(Arabuni) la ukombozi, ndio Roho wake tuliopewa ndani yetu. Ndio muhuri wetu mpaka siku ya ukombozi( 4:30). Hivyo tuwe na hakika ya ukombozi.
  6. Katika Kristo tumeokolewa kwa neema na si kwa matendo yetu (2:8-9). Akiwa na maana ile mizigo ya sheria kama ndio tiketi ya kuokolewa imewekwa chini, Yesu tayari ameshafanyika sheria yetu, kwa kumwamini tu yeye tumeokolewa.

Haya ni mambo ya muhimu sana, ambayo tunapaswa tuyafahamu juu ya Kristo tuliyempokea ndani yetu. Kulingana na mwandishi tukiyajua hayo itatufanya tusiwe watoto wachanga, wa kuchukuliwa na kila upepo wa elimu ya uongo, kwa hila za watu, na ujanja, na njia za udanganyifu (4:14).

Lakini katika kundi la pili ambalo ni sura ya 4-6;

Tunaelezwa wajibu wetu kimwenendo, baada ya kumwamini Kristo, jinsi unavyopaswa uwe, kwamba hatupaswi kuenenda kama mataifa waenendavyo, bali kinyume chake tukue mpaka kuufikia utimilifu wake.

Ambayo hiyo huja Kwa njia ya kuhudumiana kwa karama mbalimbali sisi kwa sisi katika kifungo cha umoja, kama kanisa la Kristo. (4:16)

Anaeleza pia yampasa kila mmoja binafsi auvue ule utu wa kale wa dhambi, na kuuvaa mpya mpya wa utakatifu na haki (4:20-24),

kwa kuuvua uongo, pia tusiruhusu hasira zitutawale, tusiwe wezi, vinywa vyetu visitoe maneno mabaya na matusi, tuwe wafadhili sisi kwa sisi, tusimzimishe Roho, upendo wetu udumu, uasherati usitajwe, wala aibu, wala ubishi.

Kwasababu watendao kama haya kulingana na Mungu hawana urithi katika ufalme wa Mungu.

Waefeso 5:5

[5]Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.

Halikadhalika Mwandishi anatoa pia agizo juu ya matendo ya giza kwamba tuyaonapo tuyakemee, vilevile tujiepushe walevi, bali tujazwe Roho wakati wote, kwa kumfanyia Mungu ibada.

Waefeso 5:18-20

[18]Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;

[19]mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

[20]na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

Mwandishi anazidi kugusia mienendo yetu mpaka katika ngazi za kifamilia na kikazi.

kwamba wake wanapaswa wawatii waume zao, vilevile waume wawapende wake zao. Watoto wawaheshimu wazazi wao, na wazazi wasiwachokoze watoto wao, Watumwa wawatii bwana zao, na mabwana wasiwatishe watumwa wao.(5:22-6:9)

Anagusia pia eneo la vita vyetu. Kwamba rohoni tupo vitani dhidi ya adui yetu shetani na mapepo yake, yenye kazi ya kuwapofusha watu macho, lakini pia kurusha mishale ya moto kutuangamiza. Hivyo tunapashwa tuvae silaha zote za Mungu, ili tuweze kusimama. (6:10-20). Anaorodhesha silaha hizo. ambazo zinakamilishwa kwa sala na maombi ya daima.

Na mwisho anatoa salamu zake kwa watakatifu, akiwaambia pia habari zake nyingine watakazisikia kwa Tikiko, aliyempeleka kwao.

Kwa ufupisho.

Kitabu hichi kinatupa ufahamu kuhusu ubora wa imani tuliyoipokea lakini pia wajibu wetu baada ya hapo, kwasababu tusipothamini na kulegea adui yetu shetani na majeshi yake yatashambulia imani yetu na hatimaye, tukayakosa tuliyohakikishiwa.

Ukishaamini tembea katika utakatifu. Ukiwa unapiga hatua kila siku kwenda mbali na dhambi, basi fahamu kuwa ukombozi wako ni hakika. Kwasababu msalaba una nguvu ya kukusaidia madhaifu yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Rudi Nyumbani

Print this post

ANZA MAPAMBANO MWANZO WA MWAKA MPYA.

Jina la Mwokozi Mkuu, YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Kosa moja maarufu Mfalme Daudi alilolifanya katika maisha yake, (ingawa baadaye alikuja kusamehewa na Bwana), lilikuwa ni kumuua Uria na kumchukua Mke wake aliyeitwa Bathsheba.

Lakini tukifuatilia chanzo cha kosa, tunaona lilianzia katika MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati ambao Wafalme wanatoka kwenda vitani, ila yeye Daudi hakutoka kwenda vitani pamoja na wenzake badala yake akakaa nyumbani, na matokeo yake ni shetani kupata nafasi ya kumjaribu.

2Samweli 11:1 “Hata ikawa, MWANZO WA MWAKA MPYA, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Daudi akampeleka Yoabu, na watumishi wake pamoja naye, na Israeli wote; wakawaangamiza wana wa Amoni, wakauhusuru Raba. LAKINI DAUDI MWENYEWE AKAKAA YERUSALEMU.

2 Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.

3 Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?

4 Basi Daudi akapeleka wajumbe, akamtwaa; naye akaingia kwake; naye akalala naye; (maana yule mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake); kisha akarudi nyumbani kwake.

5 Yule mwanamke akachukua mimba; basi akapeleka na kumwambia Daudi, akasema, Ni mja-mzito”.

Laiti Mfalme Daudi angalisimama na kwenda vitani pamoja na wenzake, asingeingia kwenye jaribu kubwa kama lile, ambalo liliuharibu mwaka wake wote na kumchafulia heshima yake kwa vizazi vyote.

Yote hayo ni makosa aliyoyafanya MWANZO WA MWAKA, kumbe kuna kitu katika Mwanzo wa Mwaka, vile vile na katika Mwisho wa Mwaka,..Mwanzo wa Mwaka ni wakati wa kuanza mapambano, si wakati wakulala tena, ni wakati wa kukusanya nguvu ya pamoja na kuingia katika mapambano, ni wakati wa kukusanyika katika nyumba ya MUNGU kupambana kiroho na kuangusha ngome, ni wakati wa kuomba sana.

Bwana atusaidie tuwe na mipango mema katika mwanzo wa Mwaka.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Swali: Kwanini pale Edeni pawekwe MITI, isimamie uzima au Mauti na si kiti kingine kama JIWE?.


Jibu: Ijapokuwa zipo sifa nyingi za MITI zinazoipa vigezo vya kuweza kuwakilisha UZIMA au MAUTI…Lakini sifa kuu inayoweza kusimamia nafasi hiyo ni UREFU wa MAISHA.

Mti ndio kiumbe hai pekee kilichoumbwa na MWENYEZI MUNGU kinachoishi muda mrefu kuliko vyote.

Tembo ni kiumbe hai lakini miaka yake ya kuishi ni 80 tu, Kasuku ni miaka 90, kunguru ni miaka 90, kobe ni miaka 200 lakini MITI inafika mpaka miaka 2,000..

Ipo miti yenye miaka zaidi ya elfu chini ya Jua, na bado inaendelea kuzaa matunda yenye ubora ule ule, na zaidi ya yote MITI haisogei ipo palepale, lakini unaishi muda mrefu.

Tofauti na Jiwe, lenyewe Lipo kwa muda mrefu (hata miaka elfu) lakini haliishi (halina uhai), halizai wala haliongezeki liko vile vile siku zote…kama tu mifupa ya mfu iliyopo kaburini kwa mamia ya miaka.

Sasa kwa sifa hiyo ya MTI kuishi muda mrefu, ikiwa bado inaendelea kuzaa matunda yale yale na ikiwa bado ipo eneo lile lile moja..ndio inayoifanya ichukue sifa ya kusimamia UZIMA wa Daima au MAUTI ya daima.

Kwamba tunapotafakari maisha ya MTI (jinsi yalivyo marefu na usivyosogea). Hali kadhalika Mauti ya mtu aliye katika dhambi ni ya DAIMA, na hukumu yake ni ya Daima, vile vile UZIMA wa MTU aliye ndani ya MUNGU ni wa daima na usio badilika.

Sasa huu MTI wa uzima ni nini? Au upo wapi?..

MTI wa uzima ni YESU KRISTO, leo lifahamu hili, Nitakuhakikishia hilo kimaandiko.

Maandiko yanasema Kristo ndiye hekima ya MUNGU.

1 Wakorintho 1:23 “bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;

24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni KRISTO, nguvu ya Mungu, na HEKIMA YA MUNGU”.

Umeona hapo?..KRISTO ni HEKIMA ya MUNGU na kama Kristo ni Hekima ya MUNGU, basi yeye ni MTI wa UZIMA kama maandiko yasemavyo katika Mithali 3:18.

Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye HEKIMA, Na mtu yule apataye ufahamu……

18 Yeye ni MTI WA UZIMA kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”

Kumbe YESU KRISTO ni MTI wa UZIMA, na ana heri kila amshikaye!!!… naam si ajabu tuonapo anatajwa kama Mkuu wa Uzima (Matendo 3:15).

Si ajabu tusomapo kuwa hakuna mwingine mwenye Uzima zaidi yake yeye (Yohana 10:10) na yeye lpekee ndiye njia na Uzima (Yohana 14:6).

Si ajabu kusikia kuwa kila anayemkimbilia anapata uzima wa milele (Yohana 3:16, Yohana 6:47).

Kwaufupi hakuna UZIMA nje ya YESU KRISTO, aliyekufa na kufufuka na kupaa mbinguni, yeye ndiye MTI uishio Milele, na kwake yeye kuna Uzima.

Je unao uzima wa milele?…je umeupata huu Mti?..kama bado mkaribishe YESU maishani mwako na akufanye kiumbe kipya na ukabatizwe kwa maji tele na kwa jjina lake YESU.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

Uzima wa milele ni nini?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

CHAGUA UPANDE WA UZIMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini mke wa Ayubu hakupitia matatizo?

SWALI: Kwanini mke wa Ayubu hakupitia matatizo?


JIBU: Ni vema kufahamu kibiblia si kila tendo au jambo lililoandikwa lina umuhimu kulijengea hoja, kana kwamba usipolijua litakupunguzia sehemu  katika roho yako. Hapana, Kwamfano maswali kama Yohana alibatizwa na nani, Au mke wa Petro aliitwa nani au kaburi la Yesu lipo wapi kwasasa,  haya hayatusaidii sana kwasababu sio fundisho au agizo tuliloamuriwa tulishike.

Lakini ikiwa ni kutanua upana wa fikra zetu, basi tunaweza jifunza mambo kadhaa kuhusu matukio kama haya mfano wa hili la  mke wa Ayubu, kutohusishwa katika majaribu.

Ni swali ambalo watu huuliza, mbona watoto wote wa Ayubu, walikufa mifugo na mali pia viliondoka, lakini hatuoni mke wa Ayubu kuguswa.

Tukumbuke kuwa hakukuwa na agizo kwamba vyote alivyonavyo Ayubu ni LAZIMA viathiriwe…Hapana. Kwani tunaona hata miongoni mwa watumwa wake wapo walionusurika kifo. Na hao waliachwa wawe kama mashahidi wa yaliyotokea.

Ayubu 1:16

[16]Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. 

Vivyo hivyo hata katika eneo la familia ya Ayubu hwenda ilipasa  abakie shahidi wa kueleza hali ya moyoni iliyokuwa inaendelea katika nyumba hiyo.

Mke wa Ayubu anatufunulia machungu yaliyowapata kiasi cha mwanadamu wa kawaida kushindwa kuvumilia, isipokuwa tu kumkufuru Mungu. Kikawaida mpaka mtu kufikia hatua ya kutoa maneno ya matusi, na kufuru kwa muumba wake, ujue kabisa jambo lililomkuta limeijeruhi sana nafsi yake mpaka kushindwa kuvumilia.

Ni Ayubu tu peke yake ndiye aliyeweza kustahimili hivyo, hata mke wake alipomshauri alikataa. Hii ni kutuonyesha jinsi gani mtu huyu alivyo mwogopa Mungu, zaidi ya matatizo yake. Kama tusingesikia aliyoyafanya mkewe, hakika tusingejua-fika hali waliyokuwa nayo Ayubu, na nguvu aliyojaliwa hata kutoa majibu kinyume na uhalisia wa kibinadamu.

habari ya Ayubu hutupa sisi funzo kubwa la uvumilivu katika Imani. Kwasababu tunapostahimili, sikuzote mwisho wake Mungu huwa anatupa faraja kubwa zaidi ya mwanzo.

Yakobo 5:11

[11]Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kuguguna maana yake nini? (Ayubu 30:3 )

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Kama kinavyoanza kwa utambulisho wake, ‘Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai’.

Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu.

Madhumuni makuu ya waraka huu ulikuwa ni kuwasisitiza Wakolosai  jinsi Yesu alivyo UTOSHELEVU WOTE, ambaye kwa kupitia yeye Uumbaji wote umekamilishwa ndani yake, lakini si hilo tu bali na  utimilifu  wote wa ki-Mungu unapatikana ndani yake, pamoja na hazina zote za hekima na maarifa.

Akiwa na maana kuwa mtu akimpata Kristo, hahitaji kitu kingine cha pembeni kumkamilisha yeye, Utoshelevu wote upo kwake.

Hivi ni vifungu mama,

1:15-17

“15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.

2:3

ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

 

2:9

 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Lakini Sababu ya kusisitiza jambo ni ipi?

Anaeleza kwa undani katika sura ile ya pili, kwamba ni kutokana na uwepo wa watu waliolivamia kanisa na kuwadanganya kwa maneno ya ushawishi, nia zao ni kuwafanya mateka kwa elimu isiyo na matunda, ya mapokeo ya kibinadamu, yasiyo ya Kristo (2:8). Kwamba mtu akishika hayo, ndio utimilifu wote unapatikana.

Vilevile kuonekana kwa baadhi ya desturi za kiyahudi ndani ya kanisa, kama vile kushika sikukuu, tohara,  sabato, na mwandamo wa mwezi. Vikidhaniwa kuwa vitu hivyo vinaweza kuleta ukamilifu wote pamoja na Kristo (2:11-23)

Na pia kuzuka kwa ibada bandia za kuabudu viumbe vya rohoni (malaika), kwa mawazo kuwa mtu ataupokea ukamilifu.(2:18)

Paulo anaeleza yote hayo hayana wokovu, isipokuwa kwa njia ya haki tuliyoipokea kwa msalaba wake uliofuta hati ya mashtaka yetu, kwa mateso yake pale msalabani ambayo kwa kupitia njia hiyo tumepokea msamaha wa dhambi, pale tu tunapoamini na kubatizwa (2:12-17)

Maisha mapya ndani ya Kristo.

Sehemu ya tatu Paulo anaeleza kwamba kuamini ni pamoja na kuuvaa utu upya wa Kristo. Hivyo huyu mtu hatarajiwi kuendelea kuishi hivi hivi tu, kisa Kristo amemkamilisha kwa kila kitu, bali anapaswa aenende kwa Kristo mwenyewe, ayafikiri yaliyo juu, (3:1-17),

Kwa namna gani?

Kwa kuzifisha tabia za mwilini, kama uasherati, uchafu, kutamani, mawazo mabaya, ghadhabu, matusi. Lakini pia kujivika utu wema, moyo wa rehema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, kusameheana, upendo, ibada. Vilevile si tu katika mambo ya rohoni , bali mpaka kwenye ngazi za kifamilia, kwamba wake kuwatii waume zao, na waume kuwapenda wake zao, na watoto kuwatii wazazi. Hizo ndio tabia za utu mpya.

Katika sura ya 4.

Bado Paulo aendelea kueleza huo mwenendo ndani ya Kristo, unapaswa uonekane mpaka kwa mabwana, kwa watumwa wao. Kwamba mabwana wawape watumwa haki zao, Lakini pia watakatifu wote, wanapaswa kudumu katika maombi, na kuenenda kwa hekima kwa watu wasioamini, katika usemi bora, na kujifunza kuukomboa wakati.

Na mwisho.

Paulo anawasilisha salamu za washirika wenzake wa injili, kwa Wakolosai ikiwemo, Epafra, Luka, Dema, marko, Aristarko, Yusto.

Hitimisho.

Kwa ufupi waraka huu, hueleza kwamba utoshelevu wote upo ndani ya Kristo tu na sio zaidi ya hapo, hatuhitaji kitu kingine cha pembeni kutukamilisha sisi, Lakini ni wajibu wa huyu mkristo kutembea katika maisha mapya ndani yake. Kwasababu mambo yote mawili yanakwenda sambamba hayatengani. Kristo huokoa na kutakasa wakati huo huo. Unapookolewa, saa hiyo hiyo umevikwa utu upya. Huwezi kuendelea katika dhambi.

Ni kipi cha ziada tunachoweza kujifunza katika waraka huu?.

Maombi ya Paulo na Eprafa yasiyokoma kwa kanisa hili(1:3, 9, 4:12):

Hatuna budi kujijengea desturi ya sikuzote kuliombea kanisa la Bwana, hususani mahali tulipo, pamoja na watakatifu wengine tuwajuao. Kwasababu kusimama kwa kanisa hutegemea sana maombi yasiyokoma.

                                        Bwana akubariki.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     ||kiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii. Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Jibu: Turejee…

1 Nyakati 17:11-12 “Hata itakuwa, siku zako zitakapotimia, uende na babazo, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayekuwa wa wana wako; nami nitaufanya imara ufalme wake.

12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba, nami nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake milele”.

Unabii huu unamuhusu BWANA YESU KRISTO, na si SULEMANI. yeye (YESU) ndiye atakayetokea na kuijenga nyumba ya MUNGU (Hekalu) lililo kamilifu na takatifu,  na nyumba hiyo ni MWILI wake (Yohana 2:19-22).

Lakini pamoja na hayo pia Hekalu la damu na Nyama, Mungu alimzuia Daudi asilijenge KWASABABU alimwaga damu nyingi za hatia na zisizo za hatia, na kwasababu hiyo Mungu hakumruhusu aijenge nyumba ile bali mwanae Sulemani.

1  Nyakati 28:3 “Lakini Mungu akaniambia, Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umekuwa mtu wa vita, nawe umemwaga damu ………………

5 tena katika wana wangu wote (kwani BWANA amenipa wana wengi), amemchagua Sulemani mwanangu ili aketi juu ya kiti cha enzi cha ufalme wa BWANA, juu ya Israeli.

6 Akaniambia, Sulemani, mwanao, ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu; kwa kuwa nimemchagua awe mwanangu, nami nitakuwa babaye”

Na ni damu za akina na Daudi alizozimwaga?.

   1.DAMU ZA MAADUI.

Daudi alikuwa ni mtu wa vita tangu ujana wake, yeye pamoja na mashujaa wake walikuwa ni watu wa kuua maadui zao kwa upanga, hilo likawa kizuizi kwa Daudi kuijenga nyumba ya Bwana.

   2. DAMU YA URIA.

Damu ya Uria, jemedari aliyoimwaga Daudi, ilikuwa ni kikwazo kikubwa cha Daudi kupata ruhusu ya kuijenga nyumba takatifu ya Mungu atakayokaa..

Kwani laiti Daudi angeijenga nyumba ile pamoja na tendo lake hilo alilolitenda la kumuua Uria na kumchukua mke wake, basi maadui wa Bwana wangeiona hiyo nyumba aliyoijenga na kukumbuka Daudi aliyoyafanya, wangepata sababu ya kukufuru na kukashifu ile nyumba sawasawa na maneno ya Bwana.

2 Samweli 12:13 “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.

14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umewapa adui za BWANA nafasi kubwa ya kukufuru, mtoto atakayezaliwa kwako hakika yake atakufa”.

Ni lipi tunaloweza kujifunza hapo?

Bwana hakuwahi kupendezwa na mauaji tangu mwanzo, watu wa kale waliruhusiwa kuua kwasababu ya ugumu wa mioyo yao, lakini tangu mwanzo Bwana alikataza mauaji Soma Kutoka 20:13.

Hivyo hatuwezi kuishi sasa kwa kuyaangalia matendo ya Daudi, kama Daudi aliua basi na sisi ndio tuue, kama Daudi alioa wake wengi basi na sisi ndio tuoe wake wengi n.k.

Bali tunamtazama YESU KRISTO sasa aliye Ukamilifu na Utimilifu wa sheria, yeye anasema…

Mathayo 5:38 “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.

40 Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.

41 Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

SWALI: Biblia humaanisha nini kwenye vifungu hivi?

Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita; Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.


JIBU: Ni vema kwanza kufahamu kwanini watu wanapigana vita?

Zipo sababu nyingi,baadhi ya hizo ni hizi,

Kujilinda, kutoelewana, kulipiza visasi, kutofautiana kiitikadi, au kutanua ngome.

Hivyo ili watu kufikia malengo hayo, njia pekee waionayo ni kutumia silaha, kuuana. Lakini biblia inashauri njia iliyo bora zaidi ambayo inaweza kutumiwa na hatimaye yote hayo yakatatulika. Na njia hiyo ni hekima.

Hekima ni nini?

Hekima ni uwezo wa kipekee utokao kwa Mungu, unaomsaidia mtu kuweza kupambanua, au kutatua, au kuamua jambo Fulani vema. Hivyo kupitia hekima mtu anaweza kuponya vitu vingi pasipo uharibifu wowote, na kuunda mfumo bora.

Sulemani ambaye ndiye aliyeyaandika maneno hayo alijaliwa amani katika ufalme wake, sio kwamba hakuwa na maadui wanaomzunguka hapana, bali alipewa hekima ya kuishi nao, na kuzungumza nao, na kukubaliana nao, hivyo Israeli hakukuwa na kumwagika damu kama ilivyokuwa kwa baba yake Daudi, ambaye yeye kutwa kuchwa alikuwa vitani. Kilichoweza kumsaidia ni hekima ya Mungu ndani yake.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anasema;

Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi’.  Akiwa na maana mkosaji mmoja (wa hekima), jinsi anavyoweza kuharibu mipango mingi mizuri ambayo huwenda ilikuwa tayari imeshaleta matokeo mema. Na kweli hili angalia mahali penye viongozi wabovu, huathiri jamii nzima, hata Israeli, Wafalme wa kule ndio waliisababishia Israeli kunajisika kwa muda mrefu hadi kupelekea kwenda utumwani Babeli mfano wa hao walikuwa ni Yeroboamu na Ahabu.

Kwa ufupi vifungu hivi vinatueleza uzuri wa hekima, lakini pia madhara yasababishwayo pale hekima inapokosekana, hata kwa udogo tu.

Je! Mtu anawezaje kupata hekima?

Hekima chanzo chake ni kumcha Mungu. (Mithali 9:10). Ambapo panaanzia kwenye wokovu, kisha kuendelea kuishi maisha ya utii kwa Kristo baada ya hapo.

Mtu wa namna hii, huvikwa, ujuzi huo wa ki-Mungu, na hivyo anakuwa na uwezo wa  kuutibu ulimwengu kwa namna zote. Mioyo, Ndoa,kanisa, jamii, taifa, vyote huponywa kwa hekima msingi huu wa hekima ya ki-Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Jibu: Turejee..

1Nyakati 28:17 “na nyuma, na mabakuli, na vikombe vya dhahabu safi; na kwa MATASA ya dhahabu, kwa uzani kwa kila TASA; na kwa matasa ya fedha, kwa uzani kwa kila tasa”.

Ukisoma kuanzia juu utaona kuwa hivyo ni vyombo ambavyo vingepaswa viwepo ndani ya MUNGU aliyokusudia kuijenga Mfalme Daudi.

Lakini kwasababu haikuwa mapenzi ya MUNGU mfalme Daudi aijenge ile nyumba bali mwanae (Sulemani)…hivyo ilimbidi Mfalme Daudi ampe maelekezo ya namna ya kuijenga ile nyumba na viwango vyake.

Moja ya maagizo aliyompa kulingana na alivyooneshwa na Bwana ni uwepo wa MATASA ndani ya nyumba hiyo..(kwamba atakapoijenga basi aweke Matasa ya dhahahu ndani yake).

Sasa Matasa yalikuwa ni nini?

Matasa yalikuwa ni “Makarai/mabeseni” ya dhahabu yaliyowekwa ndani ya Hekalu kwa kusudi la kutawadha (kunawa).

Kwasababu ndani ya Hekalu kulikuwa na makuhani wengi waliokuwa wanafanya kazi mbalimbali na kwa zamu, na kulingana na desturi za wayahudi ilikuwa ni lazima kila Kuhani anawe

(atawadhe) kabla ya kuanza kazi ya kikuhani na hata baada ya kumaliza.

Hivyo vyombo hivyo (MATASA) vilitumika kuhifadhia maji kwaajili ya shughuli hiyo.

Na pia vilikuwepo VITASA hivi vilikuwa ni vibaluli vidogo vya kuweza kushikwa kwa mkono, tofauti na Matasa ambayo yalikuwa yanabeba ujazo mkubwa wa maji, na vitasa ndio vile vinavyotajwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana  mlango wa 15 na 16.

Ufunuo 15:5 “Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;

6 na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu

7 Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba VITASA SABA vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele”.

Ni nini tunajifunza katika hayo?

Tunachoweza kujifunza ni kuwa matasa ya Hekalu la duniani yalijaa maji ya kuoshea makuhani lakini vile VITASA vya Hekalu la mbinguni vimejaa hasira na hukumu ya MUNGU kwa wanadamu wasiomcha yeye.

Bwana atusaidie tumtafute, tusipotee wala kuangukia katika hukumu yake.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

YAKINI NA BOAZI.

Je wakati Bwana YESU anazaliwa shetani alikuwa amefungwa?

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini biblia iwasifu wenye kutumia shoto zaidi ya wanaotumia kulia? (Waamuzi 20:16).

Kwanini biblia iwasifu wenye kutumia shoto zaidi ya wanaotumia kulia? (Waamuzi 20:16).


Swali: Je kuna jambo gani la ziada katika mkono wa kushoto hata watajwe kama mahodari katika vita?.

Jibu: Turejee…

Waamuzi 20:16 “Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.

Ni kweli zipo tafiti zinazoonyesha kuwa mkono wa kushoto una nguvu (uwezo) kuliko ule wa kuume (kulia).

Lakini hiyo si sababu biblia iliyoitumia kuusifiia mkono huo(wa kushoto) zaidi ya ule wa kulia…kwasababu pia walikuwepo mahodari waliotumia mikono yote miwili na walionekana sawa tu..

1Nyakati 12:2 “Walikuwa wenye kupinda upinde, nao walikuwa hodari wa kutumia mkono wa kuume na wa kushoto, kwa kutupa mawe ya teo, na kwa kupiga mishale ya upinde; walikuwa wa nduguze Sauli, wa Benyamini”.

Sasa ni sababu gani inayowafanya wanaotumia shoto kuonekana mashujaa zaidi?.

Jibu, Sababu kuu ni mbinu za upiganaji.

 Kawaida ni kuwa idadi ya askari wanaotumia mkono wa kulia (kuume)…ni kubwa kuliko ile ya wanaotumoa shoto.

Sasa kikawaida inakuwa ni ngumu sana kupambana na mtu anayetumia mfumo mwingine tofauti na wa kwako, lakini mfumo unaofanana na wewe ni rahisi kumsoma, na kumwingia.

Ni rahisi sana mashoto kupambana na mashoto wenzake na kulia kupambana na kulia mwenzake..lakini inapotokea kinyume na hapo, basi vita vinakuwa vigumu kwasababu ni mifumo miwili tofauti.

Na kwasababu mashoto ni wachache na wengi wanaokutana nao wakati wa vita ni watu wanaotumia mkono wa kuume (kulia), basi wanapata mzoefu mkubwa wa kupambana na watu wa tofauti na mikono yao, na kuwafanya kuwa hodari zaidi..

Lakini wale wanaotumia kulia, wanakuwa na uhodari hafifu kwasababu ni mara chache sana wanakutana na wasiotumia mashoto, hiyo inawafanya uzoefu wa kupigana na jamii hiyo ya watu kuwa mdogo, na kuwafanya kuanguka (kupigwa) wanapokutana na watu wanaotumia mashoto, hiyo ndio sababu kuu…

Na sababu nyingine inayowafanya watu wanaotumia mashoto kuwa hodari zaidi katika biblia, ni uwezo wa kuficha jambo bila kujulikana..

Kikaiwaida askari anajulikana kwa kuhifadhi upanga wake upande wa paja lake la kushoto, lakini wale wanaotumia mashoto huficha panga zao upande wa kuume, jambo linalowafanya wasifahamike kwa haraka kama ni maaskari..

Jambo hilo tunaliona kwa Ehudi aliyekuwa mwamuzi wa Israeli.

Waamuzi 3:14 “Wana wa Israeli walimtumikia Egloni mfalme wa Moabu muda wa miaka kumi na minane.

15 Lakini wana wa Israeli walipomlilia BWANA, BWANA akawainulia mwokozi, Ehudi, mwana wa Gera, Mbenyamini, mtu aliyekuwa mwenye shoto; nao wana wa Israeli walimpelekea Egloni mfalme wa Moabu tunu mkononi mwa huyo Ehudi.

16 Ehudi alijifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wake ulipata dhiraa moja; akaufunga huo upanga ndani ya nguo yake katika paja lake la MKONO WA KUUME…………

20 Basi Ehudi akamwendea; naye alikuwa anaketi peke yake katika chumba chake cha baridi. Ehudi akasema, Mimi nina ujumbe utokao kwa Mungu kwako wewe. Basi akainuka katika kiti chake.

21 Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;

22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”

Bwana atupe kutumia mashoto mbele ya adui wetu ibilisi, tupiganapo vita vya kiroho.

Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani……..

17 tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu”

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

TUTAMPIGA KWA NDIMI ZETU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)

Swali: Ni ipi sababu ya Nabii Eliya kufunga mbingu, mvua isinyeshe kwa miaka mitatu na nusu?


Jibu: Turejee..

1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu”.

Sababu kuu ya Mungu kufunga Mbingu kwa muda wa miaka mitatu na nusu kupitia kinywa cha Eliya nabii, ni MAOVU ya wana wa Israeli pamoja na mfalme wao aliyeitwa Ahabu.

kwani mfalme Ahabu wa Israeli alimwoa YEZEBELI, mwanamke wa nchi ya Lebanoni  aliyekuwa Mchawi na kahaba na mwenye kumwabudu mungu baali (2Wafalme 9:27), na hivyo akawakosesha Israeli wote, na kuwafanya wamwambudu mungu baali badala ya MUNGU WA MBINGU NA NCHI.

Sasa kitendo cha Taifa zima kumwacha Mungu wa Israeli na kwenda kuabudu miungu mingine, ni Kosa kubwa sana na lenye matokeo makubwa sana kwa Taifa..

Sasa kwa kosa hilo la Mfalme, na malkia wake na Watu karibia wote wa Israeli kumwabudu baali, ndio ikapelekea MUNGU kuadhibu nchi nzima kwa kufunga mbingu mpaka mioyo yao ilipofunguka na kumgeukia Bwana.

Na utaona MUNGU alishatangulia kuwatahadharisha wana wa Israeli kupitia kinywa cha Nabii Musa, kuhusiana na makosa ya kuabudu miungu mingine na matokeo yake, KUWA MBINGU ZITAFUNGWA..

Kumbukumbu 11:16 “Jitunzeni nafsi zenu, mioyo yenu isije ikadanganywa, mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu;

17 hasira za Bwana zikawaka juu yenu, NAYE AKAFUNGA MBINGU KUSIWE NA MVUA, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana”.

Na utaona pia Maombi ya Mfalme Sulemani, wakati analiweka wakfu lile Hekalu yalilenga hayo hayo…

1Wafalme 8:35 “Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa;

36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao”.

Hivyo hiyo ndio sababu ya mbingu kufungwa wakati wa Eliya, (maovu ya kumwabudu baali), na ndio maana utaona pale walipojinyenyekeza tu na kutubia, basi Eliya aliomba na mbingu zikafunguka.

1Wafalme 18:38 “Ndipo moto wa Bwana ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji.

39 Na watu wote walipoona, wakaanguka kifudifudi; wakasema, Bwana ndiye Mungu, Bwana ndiye Mungu.

40 Eliya akawaambia, Wakamateni hao manabii wa Baali, asiokoke hata mmoja. Wakawakamata; na Eliya akawachukua mpaka kijito cha Kishoni, akawaua huko.

41 Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele”.

Na jambo kama hili bado linaendelea kiroho na kimwili, kama tukimtumikia Bwana basi Bwana atatunyeshea mvua yake ya Baraka, lakini kama tutamwacha basi mbingu za Baraka zitafungwa, hivyo huu si wakati wa kusita sita katika mawazo mawili, bali ni wakati wa kufanya maamuzi thabiti ya kusimama na Bwana.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baali alikuwa nani?

YEZEBELI ALIKUWA NANI

RUHUSU TOHARA IPITE JUU YA KARAMA YAKO.

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Rahabu kwenye biblia.

Rudi Nyumbani

Print this post