Title 2023

Ni kwa namna gani haki huinua taifa? (Mithali 14:34)

Swali: Maandiko yanasema “Haki huinua Taifa”.. Je hii imekaaje kiundani zaidi?

Jibu: Tusome,

Mithali 14:34 “HAKI HUINUA TAIFA; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote”.

Kwa tafsiri ya kawaida mtu mwenye haki ni yoyote yule anayefanya matendo ya haki bila kujali kile anachokiamini, lakini kibiblia ni tofauti kidogo…Kibiblia  mtu “mwenye haki” ni yule anayemcha Mungu na “asiye haki” ni yule asiyemcha Mungu.

Kwahiyo hata kama mtu atajitahidi kufanya matendo mazuri na yenye kukubalika katika jamii yake yote, lakini kama moyoni mwake hamwamini Mungu, huyo kibiblia ni mtu asiye haki hata kama ana sifa njema.

Kwahiyo wanapoongezeka watu wanaomcha Mungu wengi katika Taifa maana yake “Haki na yenyewe inazidi kuongezeka”. Na matokeo ya kuwepo Wenye haki wengi juu ya nchi kuliko wasio haki ni kunyanyuka kwa Taifa, na kinyume chake wanapokuwepo wasio haki wengi katika nchi kuliko wenye haki basi Taifa linakuwa hatiani kuanguka. Sasa utauliza ni kwa namna gani?.. Hebu tujikumbushe kidogo ile habari ya Ibrahimu na Elohimu wakati ule wa Maangamizi ya Sodoma na Gomora

Mwanzo 18:22 “Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana.

23 Ibrahimu akakaribia, akasema, JE! UTAHARIBU MWENYE HAKI PAMOJA NA MWOVU? 

24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, WALA HUTAUACHA MJI KWA AJILI YA HAO HAMSINI WENYE HAKI WALIOMO? 

25 Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki? 

26 BWANA AKASEMA, NIKIONA KATIKA SODOMA WENYE HAKI HAMSINI MJINI, NITAPAACHA MAHALI POTE KWA AJILI YAO. 

27 Ibrahimu akajibu, akasema, Basi, nimeshika kusema na Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu.

28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona humo arobaini na watano. 

29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini. 

30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini. 

31 Akasema, Tazama, nimeshika kusema na Bwana, huenda wakaonekana huko ishirini? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini. 

32 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi.

 33 Basi Bwana alipokwisha kuzungumza na Ibrahimu, akaenda zake; Ibrahimu naye akarudi mahali pake”.

Umeona? Kumbe Miji ya Sodoma na Gomora iliteketea kwasababu ya kukosekana wenye haki ndani yake, kumbe wangeonekana tu wenye haki 10, basi miji ile yote ingepona!…lakini walipokosekana ndipo miji ile ikaanguka na kuangamia.

Ikiwa na maana kuwa Amani ya Miji na Mataifa ni kwasababu ya wenye haki ndani yake, ni kwasababu ya watu wa Mungu kuwepo ndani yake, hao wakiondolewa Taifa au mji unaanguka na kuangamia.

Ndio maana maandiko yanazidi kutufundisha kuwa dhiki kuu haitaanza mpaka Kanisa (wenye haki) watakapoondolewa, ikimaanisha kuwa uwepo wa watu wa Mungu katika dunia ndio unaozuia mambo kuharibika.. lakini hao watakapoondolewa ndipo Mataifa yataanguka, na ulimwengu mzima kwa ujumla.

2Wathesalonike 2:6  “Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7  Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA.

8  Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake”

Je na wewe ni miongoni mwa wenye haki?

Kumbuka katika zama hizi tunahesabiwa haki mbele za Mungu kwa njia ya kumwamini Yesu Kristo… Na si kwa matendo yetu yasiyo na Imani yoyote…

Wagalatia 2:16 “hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 14:23 “Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu”


JIBU: Kitabu cha Mithali na Mhubiri ni vitabu vilivyobeba mafunzo mengi sio tu yale ya kiroho bali pia hata ya maisha ya kawaida. Mstari huo unaelezea uzito wa kitu kinachotendewa kazi zaidi ya kile kinachozungumzwa tu. Kwamfano hapo anaanza kwa kusema “katika KILA KAZI mna faida”.. Maana yake ni kuwa katika kazi yoyote (iliyonjema), inafaida nyuma yake,. Iwe ni ya kudharaulika au yenye heshima, iwe ni ngumu iwe ni rahisi, iwe ni ya kipato kikubwa au kidogo, maadamu kazi fulani inatendeka ni lazima faida tu itaonekana nyuma yake.

Lakini mtu akiwa ni wa mipango mikubwa, mikakati mingi, akili nyingi za kubuni namna ya kutenda kitu Fulani, vikao vingi,  halafu hakitendei kazi, Bwana anasema, badala ya faida kinyume chake ni hasara tu atapata..

Vivyo hivyo na katika roho. Bwana anataka tuwe watendaji wa Neno lake, Sio kusikia tu au kuomba tu peke yake. Unaweza ukaomba usiku kucha lakini kama sio mtendaji wa Neno lake uliombalo, ni unapoteza nguvu tu.

Kwamfano unaomba Bwana akusaidie uushinde uasherati, lakini bado unashikamana na vichocheo vyake vyote, una picha chafu kwenye simu yako, kinywa chako kinazungumza mambo ya kizinzi na vijana wenzako, unachati na watu wa jinsia tofauti muda wote, unatazama tamthilia zenye maudhui hayo, unasikiliza miziki ya kidunia, unaishi na boyfriend/girlfriend. Unategemea vipi tamaa zisikutawale? Utaomba usiku kucha na hutaona matokeo yoyote, kwasababu hukitendei kazi kile unachokiomba.

Bwana alisema kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa ndani yake.(Yakobo 2:17). Kukitendea kazi kile kimoja ukiombacho, kina nguvu sana kuliko maneno elfu unayoweza kumwomba Mungu mwaka mzima.

Yakobo 1:22  “Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. 23  Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. 24  Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

HATA WAKATI WENU WA MVI NITAWACHUKUENI. (Isaya 46:3)

Isaya 46:3 “Nisikilizeni, enyi wa nyumba ya Yakobo, ninyi mlio mabaki ya nyumba ya Israeli, mliochukuliwa nami tangu tumboni, mlioinuliwa tangu mimbani; 

4 na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa”.

Mstari huu wa faraja unatuonyesha fadhili za Mungu jinsi zilivyo nyingi kwa watu wake, Anaonyesha jinsi asivyoweza kuwaacha watu wake, tangu wakiwa tumboni mwa mama zao hadi kufikia uzee wao. Kila hatua ya maisha yupo nao, kila pito liwe rahisi au liwe gumu yupo nao, wakiwa watoto, wakafikia ujana, kisha nguvu zikaisha wakiwa wazee, Mungu yupo nao. Haleluya.

Daudi alilitambua hilo pindi alipoishiwa nguvu zake, akaandika…

Zaburi 37:25 “Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa Wala mzao wake akiomba chakula”.

Hivyo huna haja ya kuhofu kesho yako itakuwaje au uzee wako utaishaje, maadamu upo na Bwana, maadamu unamtumikia, siku hizo zikifika, atakuhifadhi Mungu wako. Mwingine anasema mpaka sasa sina mfuko wa mafao, na nguvu zangu zinakaribia kuisha, ni nani atakayenisaidia, ni nani atakayekuwa karibu na mimi? Jibu ni kuwa  Bwana ndiye atakayekuwa karibu na wewe. Kwasababu tangu zamani ulimtumainia. Lakini hata kama utakuwa na mali, huwezi kuwa na raha moyoni wakati huo endapo Kristo hayupo nafsini mwako sasa.

Hivyo wekeza maisha yako kwa Bwana sasa, ili kesho yako pia iwe na matumaini na raha tele. Ikiwa wewe ni kijana wakati huu uliopo, mtafute muumba wako, upokee WOKOVU kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu, mtumikie Mungu, kimbia kweli kweli tamaa za ujanani, kabla zile nyakati mbaya za hatari hazijafika, Kwasababu maandiko yanasema kuna siku-mbaya mbeleni zitawakumba watu ambao hawakumcha Mungu tangu zamani.

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Ikiwa upo tayari kutubu dhambi zako leo , na kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, basi bofya hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

UFANYE WEMA WAKO KATIKA MAARIFA.

ANGALIENI MWITO WENU.

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya’Shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo’Ayubu 20:4

Ayubu 20:4 Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi, 

5 Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo, Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu? 

6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni; 

7 Hata hivyo ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe; Hao waliomwona watasema, Yuko wapi?

Waovu wanayo  ‘shangwe’ maandiko yanasema hivyo,  lakini shangwe yao ni ya muda mfupi tu. Usishangae kuona mtu ni tapeli na muuaji lakini anaishi maisha ya raha, yenye afya, watoto wake wanafanikiwa sana, uso wake unang’aa kila wakati, na biashara zake zinachanua. Ndio! hilo jambo lisikushtushe, kwasababu maandiko hayatuahidi kuwa waovu watapitia shida wakati wote duniani. Hapana.

Tena anasema wataweza kufikia kuwa na ukuu usio wa kawaida mfano wa kuifikia mbingu, ikiwa na maana wanaweza kuonekana hata ni miungu duniani. Lakini hiyo yote ni kwa muda tu, siku watakapokufa habari yao itakuwa imeishia hapo, Biblia inatumia mfano wa ‘Mavi’ jinsi yapoteavyo, ndivyo watakavyopotea watu hao milele.

Hakuna mtu anaweza kukitafuta kinyesi chake alichojisaidia mwaka jana au mwezi uliopita,. Ni wazi kabisa alishakisahau, na tayari kilipofika chooni kiliyeyuka na kuingia katika mfumo wa chemba ya maji machafu, kikatowekea huko. Sasa ndivyo itakavyokuwa kwa mtu Yule ambaye anashindania raha ya dunia hii anaacha kutafuta raha ya kudumu inayotoka kwa Yesu Kristo peke yake.

Zaburi 92:7 Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele;

Yesu alisema itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako, au utatoa nini badala ya nafsi yako? Ujue kuwa kusudi la wewe kuwepo duniani sio kula na kunywa, au kupanda na kujenga au kuwa milionea au kuwa maarufu. Bali ni kuyatenda mapenzi ya Mungu kwanza kisha hayo mengine yafuate baadaye.

Kubali kubadilika leo Yesu ayaponye maisha yako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo basi fungua hapa kwa mwongozo wa kumpokea Yesu maishani mwako >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

Beelzebuli ni nani? (Mathayo 12:24).

SHUGHULIKA SANA NA DHAMBI YA KUSAHAU.

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Rudi nyumbani

Print this post

Maana ya ‘taabu haitoki mchangani, Wala mashaka hayachipuki katika nchi’ ni nini?

Ayubu 5:6 “Kwani taabu haitoki mchangani, Wala mashaka hayachipuki katika nchi;”

Watu wengi tumekuwa tukilaumu mazingira, tukilaumu wanyama, tukilaumu ardhi, na vitu vingine vya asili kuwa ndio chanzo cha matatizo yetu, chanzo ya shida zetu na mashaka yetu rohoni. Lakini maandiko yanatupa uhalisia kwamba taabu na mashaka havichupuki ardhini, kama vile mchicha umeavyo, bali vinatoka ndani yetu wenyewe.

Makosa  yetu ndio zao la kila aina ya matatizo yetu. Asili ya migogoro katika ndoa, sio ule m-buyu uliokaribu na nyumba zetu. Unaweza kuhama hata nchi ukakaa chini ya mizeituni na mizabibu mizuri, na maua, lakini bado ndoa yako ikaendelea kuwa na matatizo tena makubwa zaidi  hata yale ya mwanzo.

Sababu ya kuteswa na mapepo, sio Yule paka mweusi wa jirani anayekuja kulala batini kwako kila siku usiku. Bali ni kwasababu Kristo hayupo ndani yako.

Sababu ya kutokupiga hatua kiroho, sio hiyo ardhi unayoishi, au unayoimiliki, usihangaike na maombi ya kufungua/ kukomboa ardhi, hangaika na vifungo vilivyomo ndani yako. Ambavyo vinatokana na aidha kutolielewa Neno la Mungu, au kuwa nje ya wokovu.

Biblia inasema..

Yohana 8:36  Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.

Na tena inasema…

Yohana 8:32  “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Rekebisha mwenendo wako, pokea wokovu wa kweli, kisha liishi Neno la Kristo kila siku. Hakika utaona jinsi tatizo lako linavyotalika kirahisi, ndipo utaacha kuyalaumu mazingira ya nje.

Ayubu 5:6 “Kwani taabu haitoki mchangani, Wala mashaka hayachipuki katika nchi;”

Je! Umeokoka?  Kama bado unasubiri nini? Je! Unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi, tunaishi katika muda wa nyongeza tu, siku yoyote unyakuo wa kanisa unapita, watakatifu kuchukuliwa mbinguni na wenye dhambi kwenda motoni?. Fanya uamuzi sahihi sasa, ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi fungua hapa kwa mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MTU MWENYE KUSITA-SITA KATIKA MAWAZO MAWILI.

LAKINI WAKATI WA TAABU WATASEMA, SIMAMA UKATUOKOE.

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona anamaana gani?

SWALI: Mhubiri anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona bali mwanamke mmoja miongoni mwa wote mimi sikumwona, anamaana gani,?


JIBU: Tusome,

Mhubiri 7:27 Tazama, asema Mhubiri, mimi nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili, ili kuitafuta jumla;  28 ambayo bado nafsi yangu nikali nikiitafuta, nisiione; mwanamume mmoja katika elfu nimemwona; bali mwanamke mmoja miongoni mwa wote mimi sikumwona.

Ukichunguza hapo utaona Sulemani hajaenda moja kwa moja kutaja mtu aliyemwona Kwamba ni mtu ‘mkalimifu’ au ‘ mtu anayeelekea ukamilifu’.

Katika maisha yake ya kuchunguza na kulinganisha mambo kwa hekima ya ki-Mungu, aliona kuna vitu Fulani vipo katika jinsia fulani na kuna vitu Fulani havipo katika jinsia husika,. Kumbuka Sulemani alikuwa na uzoefu wa kuishi na wanawake wengi, alikuwa na wake mia saba na masuria mia tatu, bado na wakwe zake kama angependa kuwahesabu, jumla yao ingekuwa ni kubwa sana. Hivyo alipokuwa anayasema maneno hayo, hakuwa anabahatisha mawazo yake, au anaonyesha udhaifu kwa wanawake hapana..

Sulemani aliona katika jambo la juhudi ya kuulekea ukamilifu wote aliouhitaji Mungu, halikuwa kwa jinsia zote, bali kwa jinsia ya kiume tu, na tena kati ya hao ni wachache sana aliowaona, yaani mmoja kati ya elfu, lakini kwa wanawake hakuwahi kuona hata kwa mmoja,. Lakini hakumaanisha kwamba mtu huyo aliyemwona tayari alikuwa ni “Mkamilifu”..Kwasababu kipindi chote kile alichokuwepo, hakukuwahi kutokea mwanamume aliyempendeza Mungu kwa utimilifu wake wote, isipokuwa wapo waliojitahidi kusogelea hatua hizo lakini hawakufikia,  mfano wa hao ni kama Ayubu, na Henoko. N.k. Lakini hao wote bado hawakuwa wakamilifu kwa viwango Mungu alivyovitaka, japo kulikuwa na vimelea hivyo, tofauti na katika ile jinsia nyingine.

Lakini maono yake yalikuja kutimia kwa mwokozi wetu YESU KRISTO, yeye ndiye aliyeishi asilimia mia maisha ya ukamilifu ya kumpendeza Mungu bila kutenda dhambi yoyote,ambaye alijaribiwa kama sisi tulivyojaribiwa bila kumkosea Mungu. Na ndio maana kwanini Masihi hakuja katika jinsia ya kike, kuukomboa ulimwengu bali jinsia ya kiume.

Hivyo huyo mwanaume pekee aliyefikia ukamilifu ni Yesu tu, Sisi wengine wote tumepungukiwa na utukufu wa Mungu, iwe ni wa jinsia ya kike au ya kiume. Na wote tunaokolewa kwa neema yake tu pindi tunapomwamini yeye. Hiyo ikiwa wewe bado hujaupokea wokovu, na unatamani kufanya hivyo sasa, basi bofya hapa ili uweze kupata mwongozo huo wa kumruhusu Kristo aingie maishani mwako akuokoe.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Biblia ilimaanisha nini iliposema “Mwanamke atamlinda mwanamume” Yeremia 31:22?

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

Biblia inasemaje kuhusu Nywele?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

(Masomo yahusuyo malaika na uwezo wao)

Swali: Je watu wa Mungu wanaweza kuwaamuru Malaika watende jambo Fulani au watoke na kwenda mahali Fulani kama vile mapepo yanavyoamrishwa kwa jina la Yesu?.

Jibu ni hapana!!. Hatujapewa mamlaka yoyote ya kuwaamrisha Malaika, iwe kwa mapenzi yetu wenyewe au kwa jina la Yesu!. Malaika ni viumbe wanaotii na kufuata maagizo ya Mungu tu! si maagizo yetu, na hakuna mahali popote katika maandiko panapoonyesha au kufundisha wanadamu kuwapa malaika maagizo. Zaidi sana sisi (wanadamu) ndio tuliowekwa chini ya uwezo wa Malaika.

Utaona wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, maandiko yanasema Mungu aliwapelekea malaika ambaye aliwaongoza katika njia yao yote, na umati mzima wa Israeli ulionywa na Mungu kumsikiliza Malaika yule kwani Mungu ameweka Neno lake ndani yake, na Zaidi sana Mungu aliwaonya kuwa wasimposikiliza yule malaika hatawasamehe, kinyume chake atawadhuru!.

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

 21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake.

 22 Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao. 

23 Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwenye Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawakatilia mbali”.

Kwahiyo elimu ya kuwaamrisha malaika au kuwapa maelekezo haipo kibiblia, huenda uwezo huo tutakuwa nao baada ya kumaliza maisha haya tutakapofika mbinguni lakini kwa wakati huu hatujapewa hayo mamlaka, kwasababu hata Bwana wetu Yesu alipokuwa duniani alijishusha akawa mdogo kuliko Malaika wote..si Zaidi sisi?

Waebrania 2:9  “ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu”.

Sasa kama ni hivyo ni njia zipi tunaweza kuzitumia ili Malaika wafanya yale tunayoyataka sisi.

1.KWA KUMWOMBA BABA

Tukitaka kuona Malaika wanafanya yale tunayoyataka, njia ya kwanza ni sisi kumwomba Baba yetu yetu wa Mbinguni, (tunaomba kwamba atupelekee malaika zake watufanyie hiki au kile) na kama jambo hilo tuliombalo ni mapenzi ya Mungu basi Baba yetu wa mbinguni  anawapa amri Malaika wake kutekeleza kile tulichokiomba, au tukitakacho (hapo amri inakuwa imetoka kwa Mungu moja kwa moja na si kwetu). Kama Bwana Yesu alivyomwambia Petro wakati ule alipomkata mtumwa wa kuhani mkuu sikio.

Mathayo 26:51  “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.

52  Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.

53  Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, NAYE ATANILETEA SASA HIVI ZAIDI YA MAJESHI KUMI NA MAWILI YA MALAIKA?”.

2. KWA KULITENDA NENO.

Njia ya pili ni kwa kuliishi na kuliltenda Neno la Mungu. Malaika wa Mungu walishapewa maagizo ya kutekeleza yale yote yaliyoagizwa kwenye Neno la Mungu. Kwamfano Neno la Mungu linasema “

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20  na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”.

Sasa mtu anapolitii hili Neno na kutoka kwenda kuhubiria wengine habari njema, hapo bila hata kuomba kwamba Malaika wa Mungu waende na yeye, tayari wataenda tu na yeye!.. kwasababu tayari Mungu kasema “atakuwa na wale wote wanaotoka kwenda kuhubiri”, hivyo Malaika wa MUNGU wataambatana na mtu huyo kuhakikisha kuwa watu wanapokea wokovu na ishara zinatendeka!.

Hizi ndio njia kuu mbili, zitakazowafanya Malaika wa Mungu, wafanye yale tunayoyataka au tunayofikiri, lakini si kwa kuwapa Amri, au kuwaamuru, wao wanafuata amri kutoka kwa Mungu na si kutoka kwetu. Sisi mamlaka tuliyopewa ni  juu ya mapepo na falme zote za giza, kuziamrisha ziti chini yetu kwa jina la Yesu (Luka 10:19).

Kwa elimu Zaidi juu ya Malaika, wasiliana nasi inbox.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Yohana mbatizaji alibatizwa na nani?

Je! baada ya ulimwengu huu kuisha malaika watakuwa na kazi gani tena?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

Rudi nyumbani

Print this post

Beelzebuli ni nani? (Mathayo 12:24).

Swali: Katika biblia Beelzebuli alikuwa ni nani?, na kwanini Mafarisayo wamwite Bwana Yesu Belzebuli/.

Jibu: Jina Beelzebuli ni mwunganiko wa maneno matatu (3), Beel-ze-buli.. “Beel” maana yake ni
“bwana au mkuu”“Ze”  ni kiunganishi chenye maana ya “wa”  na “Buli” ni pepo wachafu mfano wa inzi.

Kwahiyo ukiunganisha maneno hayo  matatu linakuja neno  “Mkuu/bwana wa pepo”.. sawasawa na biblia ilivyotafsiri katika Mathayo 12:24.

Mathayo 12:22  “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.

23  Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi?

24  Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa BEELZEBULI MKUU WA PEPO”.

Sasa huyu Beelzebuli mkuu wa pepo ni nani?

Si mwingine Zaidi ya “shetani mwenyewe”. Biblia inamtaja shetani kuwa ndiye mkuu wa ufalme wa giza, na ndiye mkuu wa pepo wote walioasi (Ufunuo 12:9).

Kwahiyo Mafarisayo walipoona Bwana anatoa mapepo kwa uweza wa Mungu na wenyewe hawawezi, wakaingiwa na wivu, na kuamua kuzusha kuwa anatoa pepo kwa uwezo wa shetani (beelzebuli) na si kwa uwezo wa kiMungu. Lakini jibu la Bwana lilikuwa “shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake, vinginevyo ufalme wake hautasimama”.

Mathayo 12:26 “NA SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; BASI UFALME WAKE UTASIMAMAJE?

27  Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu.

28  Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajili”

Hii ikifundisha kuwa uweza wa Mungu pekee ndio unaoweza kutoa pepo!. Shetani kwamwe hawezi kutoa pepo kwani mapepo yake yote yanafanya kazi yake..anachokifanya ni kubadilisha tu tatizo ndani ya mtu, au kuongeza tatizo ndani ya mtu.

Watu wanaoenda kwa waganga na kusema wameaguliwa na kupona, kiuhalisia hawajapona bali wamebadilishiwa tatizo au wameongezewa pepo lingine juu ya lile lililokuwepo ili kutuliza tu maumivu, lakini baada ya muda lile tatizo litajirudia na lingine kubwa Zaidi ya hilo (kwasababu kamwe shetani hawezi kulitoa pepo lake ndani ya mtu, kwasababu yeye ndiye kaliweka humo, sasa akilitoa si atakuwa anafanya kazi ya Mungu, na yeye kamwe hawezi kufanya hivyo, kwasababu hana mapenzi na wanadamu, yeye anachokitafuta ni kuwaangamiza wadamu na si kuwaweka huru).

Kwahiyo wanaoenda kwa waganga ili kupata tiba, hakuna tiba yoyote wanayoipata Zaidi ya kuongeza matatizo..Suluhisho la tabu na matatizo yote ni Yesu tu!, huyo ndiye maandiko yanasema kuwa akikuweka huru unakuwa huru kweli kweli (Yohana 8:36), na si waganga wala wachawi wala watabiri.

Kama umewaza kwenda kwa waganga kwasababu ya tatizo ulilokuwa nalo, leo hii badilisha fikra zako, kule unaenda kuongeza matatizo na si kupunguza. Mkimbilie Yesu, huyo peke yake ndiye Suluhisho na ndiye mwenye upendo wa kweli.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je ni kweli hakuna aliyepaa mbinguni zaidi ya Mwana wa Adamu? (Yohana 3:13)

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

Rudi nyumbani

Print this post

Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)

Swali: Mti wa Mvinje uliotumika kutengenezea safina kulingana na Mwanzo 6:14 ndio mti gani kwasasa?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 6:13 “Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia. 

14 Ujifanyie safina ya MTI WA MVINJE; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami”.

Mti wa Mvinje ni jamii ya miti inayoota karibia sehemu kubwa ya dunia, ikiwemo barani Afrika (Tazama picha juu).

Sifa ya miti hii ni migumu sana na Imara, lakini iliyo kuu kuliko zote ni uwezo iliyonayo ya kutoathiriwa na maji.

Tofauti na miti mingine, ambayo adui wake wa kwanza ni maji, (inapogusa maji basi inaoza), lakini Mti wa Mvinje wenyewe hauathiriwi na maji, hivyo kufanya mbao ya mti huo itumike kwa matumizi ya kutengeneza boti ndogo ndogo na hata kubwa (boti za wavivu na baadhi ya za abiria zinatengenezwa kwa kutumia miti hii), vile vile mbao ya mti wa Mvinje inatumika kutengenezea viti vya viwanja vya michezo na sehemu za Uma, na vile vile inatumika kutengenezea viungio vya barabara za treni (Reli), na matumizi mengine ya samani za ndani kama vile milango na makabati.

Kwa sifa miti hiyo iliyoibeba ndiyo ikawa sababu ya Mungu kumwambia Nuhu ajenge safina kwa kutumia miti hiyo, kwani ingetumika miti mingine huenda isingeweza kuvumilia kudumu juu ya maji kwa miezi yote ile mitano, kwani maandiko yanasema mvua ilinyesha siku 40 usiku na mchana, na maji yalidumu juu ya uso wa nchi siku 150 (Miezi 5) soma Mwanzo 7:4,24.

Maandiko mengine katika biblia yanayohusu mti wa mvinje ni pamoja na Isaya 6:13 na Isaya 44:14.

Lakini leo hii mvinje wetu ni nini?

Mti wa Mvinje leo hii si mwingine Zaidi ya msalaba utuokoao sisi na dhambi zetu, na safina yetu ni Bwana Yesu Kristo, tuwapo ndani ya Kristo basi gharika ya ghadhabu ya Mungu ambayo imekusudiwa kumwagwa katika siku hizi za mwisho haitatupata.

Je umeokoka? Kama bado unasubiri nini? Kumbuka dunia hii inaenda kuisha, tupo nyakati za majeruhi na unyakuo umekaribia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mretemu ni mti gani?

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Mwerezi ni nini?

FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Rudi nyumbani

Print this post

Praitorio ni nini? Na Kwanini ilikuwa ni najisi kwa wayahudi kuingia humo? (Yohana 18:28)

Jibu: Turejee,

Yohana 18:28  “Kisha wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa mpaka Praitorio, nayo ikawa alfajiri; lakini wao wenyewe hawakuingia ndani ya ile praitorio,wasije wakanajisika,bali wapate kuila Pasaka”.

Praitoria ni “ukumbi wa hukumu” ambao unakuwepo ndani ya majumba ya wafalme. Wahalifu ambao ilibidi kesi zao ziamuliwe na mfalme au liwaji wa mji, basi walipelekwa katika ukumbi huo na kukutana na mkuu huyo na kuhojiwa na moja kwa moja kutolewa hukumu.

Kipindi Wakuu wa makuhani wamemkamata Bwana Yesu, hawakuweza wao wenyewe kumhukumu kwasababu nchi ya Israeli yote ilikuwa chini ya utawala wa Warumi (kwaufupi ilikuwa ni koloni la Warumi), waliokuwa wanaiongoza serikali yote ni Warumi, na ndio waliokuwa wananatoa hukumu ya mwisho, ndio maana ikawabidi wakuu wa makuhani wampeleka Bwana Yesu kwa Pilato ambaye ndiye aliyekuwa liwali wa Uyahudi, na ndiye mwenye kutoa maamuzi ya mwisho (Mathayo 27:2).

Sasa kwasababu sheria za Wayahudi hazikuwawaruhusu wao kuchangamana na watu wa mataifa, wala kuingia katika nyumba zao tena hususani wakati wa sikukuu, hiyo ikawafanya wale wakuu wa makuhani wabaki nje wakati Kristo anaingizwa ndani ya Praitorio kuzungumza na Pilato.

Wayahudi hawakuingia katika nyumba za watu wa mataifa, kwasababu katika nyumba hizo kulikuwa na vitu najisi vilivyo kinyume na sheria za Musa, mfano wa vitu hivyo ni sanamu, utakuta hata kikombe tu cha kunywea maji kimetengenezwa kwa taswira ya miungu yao, na Zaidi sana vyakula vya watu wa mataifa vingi vilikuwa ni najisi kulingana na sheria za kiyahudi. Kwahiyo endapo Myahudi akiingia katika nyumba hizo na kushiriki vitu vyao hivyo hata kwa bahati mbaya au kwa kutokujua, basi tayari anakuwa amejitia unajisi, na mtu akiwa najisi anakuwa hastahili kushiriki sikukuu yoyote ya kiyahudi, (anatengwa kwa muda Fulani mpaka unajisi wake utakapoisha).

Ndio maana ikawepo sheria ya wao kutochangamana na watu wa mataifa wala kuingia katika nyumba zao..utazidi kulithibitisha hilo zaidi kipindi kile Mtume Petro ameenda nyumbani kwa Kornelio..

Matendo 10:26 “Lakini Petro akamwinua, akasema, Simama, mimi nami ni mwanadamu.

27  Na katika kusema naye akaingia ndani, akaona watu wengi wamekusanyika.

28  Akawaambia, NINYI MNAJUA YA KUWA SI HALALI MTU ALIYE MYAHUDI ASHIKAMANE NA MTU ALIYE WA TAIFA LINGINE WALA KUMWENDEA, lakini Mungu amenionya, nisimwite mtu awaye yote mchafu wala najisi.

29  Kwa sababu hiyo nalikuja nilipoitwa, nisikatae; basi nawauliza, ni neno gani mliloniitia?”

Lakini swali ni je! Hiyo sheria ya wayahudi kutochangamana na watu wa mataifa mpaka leo hii ni agizo la Mungu?..Kwamba watu wa mataifa ni najisi mpaka leo??

Jibu ni La!.. Kupitia msalaba wa Yesu Kristo umetufanya wote wawili kuwa mamoja.. Hakuna Myahudi wala Myunani, kwa kumwamini Yesu Kristo sote tunakuwa safi, na kitu kimoja mbele za Mungu, wala hakuna aliye bora kuliko mwingine..yeye Kristo ndiye aliyekibomoa hicho kiambaza cha kati kilichotutenganisha.

Waefeso 2:11  “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;

12  kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.

13  Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.

14  Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga.

15  Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani.

16  Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.

17  Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu.

18  Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Roho mmoja”.

Tunakuwa Najisi tu tunapokuwa nje ya Yesu Kristo, na kinachotufanya kuwa najisi si kitu kingine Zaidi ya dhambi ndani ya maisha yetu, kama Bwana Yesu alivyosema katika Mathayo 15:17-20.

Je! umeokoka?, kama bado unasubiri nini?..Hizi ni siku za mwisho, na Bwana yupo mlangoni.

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIMPE NGUVU SHETANI.

Lumbwi ni nini katika biblia?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post