Title 2024

Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru.

Huwenda ukawa unajiuliza, Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema, Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru? . Je huko gizani ni wapi, na sirini ni wapi? Je yeye huwa anazungumza gizani.

Mathayo 10:26  “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.

27  Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”

JIBU: Ni vema tukaifahamu tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo, katika kufundisha jinsi ilivyokuwa alipokuwa anazungumza na watu mbalimbali. Yapo maneno au mafundisho au mafunuo aliyoyaweka wazi kwa watu wote, lakini yapo ambayo hakuyaweka wazi kwa kila mtu.

Mahubiri yake mengi aliyazungumza hadharani, lakini mengine haikuwa hivyo, kwamfano upo wakati alijitenga akapanda milimani, na wale waliomfuata ndio aliowafundisha (Mathayo 5:1), wakati mwingine aliingia nyumbani, hakutana kujulikana kwasababu alikuwa akitaka kuwafundisha wanafunzi wake tu, peke yao (Marko 9:29-31), wakati mwingine aliwaponya watu akawataka wasimdhihirishe, (Marko 1:44), wakati mwingine alijifunua utukufu  wake, kwa wale tu waliokwenda naye kuomba mlimani, uso wake ukawa unameta meta, kama jua, alipomaliza  akawakataza wasimwambie mtu, mpaka atakapofufuka (Mathayo 16).

Hayo ni mazingira mbalimbali, ambayo Yesu alisema nao bila kujulikana na kila mtu, Sasa mazingira hayo ndio aliyaita  “Gizani, au sirini”

Hii ni kufunua kuwa hata sasa Yesu anazungumza hadharani, lakini pia anazungumza sirini. Na yale ya sirini huwa ni makubwa zaidi na ndio maana haitaji yajulikane na kila mtu.

Watu wengi wanamsikia Yesu hadharani, lakini hawamsikii sirini. Hadharani, ni pale unaposikia mafundisho kanisani, mahubiri, semina, mkutano  n.k. Ni kweli Yesu atakufundisha mengi kupitia matumishi wake mbalimbali, na yatakujenga na ni muhimu ufanye hivyo.

Lakini lazima pia sirini pa Yesu uwe napo.

Je hapo ni wapi?

Ni eneo lako la utulivu la kimaombi na kutafakari”.

Ni muhimu sana kila mkristo, awe na wakati wake maalumu kila siku alioutenga wa kuzama uweponi, katika maombi, kusoma Neno na kutafakari shuhuda za Mungu maishani mwake. Ni muhimu sana.

Zaburi 91:1 AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

Mathayo 6:6  Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Hapa Yesu anataka uingie gharama, kidogo ili umsikie, au akuhudumie, au akufundishe. Ndio mfano wa wale waliomfata milimani. Vivyo hivyo na wewe, ingia gharama ya kudumu uweponi mwa Mungu. Ukiona mchana pana usumbufu, usiku ni muda mzuri sana, kuamka, tena masaa yako kadhaa kila siku,. Kumpa Bwana nafasi ya kukufundisha.

Ukiwa wa namna hii, hutamkosa Bwana popote pale. Kaa mahali pake pa siri. Kwasababu yupo pia sirini, akupe mambo mambo utayasema hadharani wakati fulani.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

AGIZO LA UTUME.

MKUU WA GIZA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya sulubu/ sulubisha?

Neno sulubu huzaa kusulibisha/kusulubisha,

Maana ya Sulubu, ni kuadhibisha kwa kuning’iniza kwenye mti wa msalaba, au nguzo iliyonyooka, kwa kufungwa au kugongelewa miguu na mikono, na kuacha hapo mpaka ufe.

Hii ni aina ya adhabu ya kifo, ambayo ilitumika zamani, kwenye falme zilizokuwa na nguvu na katili kama Rumi.

Watu walioshitakiwa kwa makosa makubwa ikiwemo uhaini, au uuaji, uvunjaji amani, hawakupewa adhabu ya kawaida ya kifo kama vile kukatwa kichwa na kufa mara moja,. Bali walipewa adhabu kali kama hii, lengo lake ni kumfanya Yule mshitakiwa kupitia mateso makali ya muda mrefu kabla ya kufa, kwasababu, baada ya kuning’inizwa kwake pale msalabani itamchukua siku tatu mpaka wakati mwingine wiki hadi kufa. Hivyo kipindi chote hicho unatakuwa unateseka tu pale mtini.

Hiyo ndio adhabu waliyoichagua kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye hakuwa na hatia yoyote, wala kosa, jambo ambalo hata mtawala yule Pilato alilishuhudia kuwa hakukuwa na uovu wowote ndani yake. (Luka 23:4). Lakini kwasababu ilipasa maandiko yatimie ili sisi tupate ukombozi mkamilifu, ndio maana ilimpasa Yesu aadhibiwe vikali, ili mimi na wewe tupokee ONDOLEO LA DHAMBI. Kwa kifo chake.

Gharama aliyoilipa ni kubwa sana, kusulubiwa uchi wa mnyama, bila nguo, kudhalilishwa na kupigwa, na kuharibiwa mwili wote. Ni kwasababu mimi na wewe tupokee msamaha wa dhambi, tuepushwe na hukumu ya milele ya jehanamu ya moto.

Ndio maana maandiko yanasema..

Waebrania 2:3  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako?

Ikiwa ni la! Basi waweza kufanya hivyo sasa, kwa kubofya hapa ili upate mwongozo wa sala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani

Print this post

SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.

Nyakati tunazoishi ni za hatari kubwa, zaidi hizo zinazokuja wakati si mwingi ndio za hatari mno. Watu wengi hawajui kuwa mwisho umekaribia sana, dunia imekwisha, na kwamba SIKU YA BWANA, ipo mlangoni.

Siku ya Bwana ni nini?

Siku ya Bwana ni kipindi fulani maalumu ambacho Mungu amekiandaa ili kuuharibu huu ulimwengu pamoja na watu wote waovu waliopo duniani, na mifumo yao mibovu. Na hiyo itakuja baada ya kanisa la Kristo kunyakuliwa 

Tukisoma katika kitabu cha Sefania tunaelezwa kwa urefu juu ya sifa kuu za siku hiyo itakavyokuja. 

Ametaja sifa zake sita (6), kwa kuziita “siku ya”..”siku ya”…”siku ya”

Tusome..

Sefania 1:14-16

[14]Hiyo siku ya BWANA iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya BWANA; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!

[15]Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

[16]Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

1) Anaanza kwa kusema ni Siku ya ghadhabu.

Ghadhabu ni zao la hasira, na hasira hufuatana na mapigo. ndio hapo tunaposoma kitabu cha ufunuo 16, tunaona kipindi hicho kikifika wale malaika saba watavimimina vile vibakuli vyao saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi. na kitakachofuata kwa tendo lile ni mapigo, ndio hapo utaona majipu mabovu, yanawatokea wanadamu, na tena jua linashushwa na kiwaunguza watu, mpaka wanafikia hatua ya kumtukana Mungu.

Ufunuo 16:8-9

[8]Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto. 

[9]Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu. .

2) Siku ya fadhaa na dhiki.

Dhiki na fadhaa ni taabu ambazo mtu anazipata hususani kutoka katika mazingira ya nje. Ukiendelea kusoma sura ile ya 16, utaona mito, chemchemi na bahari zote zinageuzwa kuwa damu, wanadamu wanakosa maji. hofu na mashaka ya mabadiliko ya nchi. Duniani hatakuwa ni mahali penye utulivu, tengeneza picha unaishi katika dunia ya namna hii, utastahimili vipi. Bwana anasema wanadamu watafuta kifo, lakini kifo kitawakimbia.

Ufunuo 16:3  Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.

4  Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu. 5  Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;

6  kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili

3) Siku ya uharibifu na ukiwa

Sio tu mapigo na dhiki, lakini pia kuharibiwa kwa huu ulimwengu na mifumo yake kutafuata, kwasababu biblia inasema siku hiyo kutatokea tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia kuumbwa, mpaka visiwa kuhama, inasema moto utatokea kuharibu huu ulimwengu, mfano wa sodoma na gomora na mfano wa kipindi cha gharika.

2 Petro 3:10-12

[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 

[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 

[12]mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? 

4) Siku ya giza na utusitusi.

Giza na utusitusi unaozungumziwa hapa ni ule wa rohoni. ni kipindi ambacho watu watautafuta uso wa Mungu lakini hawatauona, ndio maana Yesu alisema imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyetupeleka maadamu ni mchana, usiku waja asioweza mtu kufanya kazi. watu watamwita Mungu, lakini hakutakuwa na majibu yoyote.

Mithali 1:27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia.  28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.  29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.  30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote

5) Siku ya mawingu na giza kuu. 

Vilevile kwa jinsi dunia hii itakavyoharibiwa jua na mwezi na nyota vitazuiliwa.. duniani kutakuwa na giza ambalo halijawahi kutokea, na hayo ndio yatakuwa yale mapigo ya mwisho mwisho kabisa yatakayokuwa yanaukaribisha ujio wa pili wa Yesu duniani.

Vilevile wingu zito litatandaa angani, mawe mazito yatashuka duniani kama talanta, jiwe lenye uzito wa kg 34, hatujui itakuwa ni mvua ya namna gani, hiyo.

Ufunuo 16:18-21

[18]Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo. 

[19]Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake. 

[20]Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena. 

[21]Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.

6) Anasema pia ni siku ya tarumbeta na ya kamsa.

Kamsa ni kelele za vita. Maana yake katika kipindi hicho cha siku ya Bwana, vita vitakuwepo, ndio ile vita ya mwisho ijulikanayo kama Harmagedoni.Mataifa yote yatahusika. lakini Bwana awataua watu wengi sana. damu nyingi sana zitamwagika. ni nyakati ambayo hakutakuwa na shujaa, kila mtu ataomboleza mpaka mashujaa, wafalme na matajiri wote hao watalia sana, pesa zao hazitawasaidia wataomba milima iwaangukie wafe haraka, kuliko kushuhudia huo mfululizo wa mapigo ya Mungu mwenyezi.

Na ndio maana ukimalizia kusoma mistari inayofuata pale kwenye kitabu cha Sefania anasema

Sefania 1:17-18

[17]Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda BWANA dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi. 

[18]Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya BWANA; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha. 

Ndugu yangu, ikiwa unyakuo ukipita leo, fahamu haya utayashuhudia, wakati huu si wa kumbelelezewa wokovu, ni kuamka na kuikimbilia neema, nyakati mbaya zimekaribia, haya mambo ya duniani yatakufikisha wapi? uhai wako umefichwa wapi? Ukifa leo huko uendako utakuwa mgeni wa nani.Kwasababu huko nako kuna mateso makali vilevile kama hapa.

Embu dhamiria kutubu na kumgeukia Bwana Yesu leo, akupe msamaha wa dhambi bure. Hukumu ya Mungu inatisha. 

Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako. Na unatamani leo Yesu akutue hiyo mizigo ya dhambi. Basi waweza kusali sala hii kwa imani. Ukijua Kristo wakati wote yupo kutuokoa. Kumbuka kinachotangulia ni kuamini. Kisha ndipo kukiri.

Hivyo

Hapo ulipo piga magoti, kisha dhamiria moyoni mwako kuyasema maneno haya, na moja kwa moja leo, utapokea msamaha wa dhambi zako hapo hapo ulipo, 

Sema.

Ee Bwana Yesu asante kwa kuja kwako duniani, kutukomboa sisi wanadamu tuliokuwa tumepotea, kwa kifo chako pale msalabani na kufufuka kwako. Ninaamini kuwa wewe ndio Bwana na mwokozi, nami napokea neema uliyonipa bure ya ondoleo la dhambi, tangu leo ninakubali kufanyika mwana wako, na kugeuka kuacha njia mbaya za kale. Asante kwa kuwa unanipa nguvu hiyo na kuliandika leo jina langu katika kitabu cha uzima. Nami nafanyika kiumbe kipya. Asante kwa kunipokea, asante kwa kunisamehe, Asante kwa kunifanya mwana wako.  Ninaomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo Amen.

Basi ikiwa umesema sala hiyo toka moyoni kwa imani. Tayari umeshaupokea wokovu. Na hivyo hatua zilizobakia kwako ili kuitimiza haki yote, ni wewe kubatizwa. Tafuta mahali wabatizwapo kwa maji tele, na kwa jina la Yesu Kristo.  Ikiwa utahitaji msaada pia waweza kuwasiliana nasi kwa namba zetu chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani

Print this post

HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI.

(Mfululizo wa masomo yahusuyo Uhuru wa Roho na Utumwa wa sheria).

Jina la Bwana YESU, MKUU WA UZIMA libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).

Biblia inamfananisha HAJIRI, (yule aliyekuwa “kijakazi” wa Sara na Ibrahimu) na YERUSALEMU YA DUNIANI. Na tena inamfananisha “Ishmaeli” aliyekuwa mwana wa Hajiri na “wale wote walio chini ya utumwa wa sheria” waliopo pale katika mji wa YERUSALEMU uliopo Israeli.

Vile vile “Sara” aliye mwungwana (yaani huru) inamfananisha na YERUSALEMU YA MBINGUNI (mji wa kimbinguni) na mtoto wake “Isaka” inamfananisha na “watu wote wa kimbinguni” (yaani walio huru na utumwa wa sheria)..ndivyo maandiko yanavyosema..

Wagalatia 4:22 “Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana.

23  Lakini yule wa mjakazi alizaliwa KWA MWILI, yule wa mwungwana KWA AHADI.

24  Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri.

25  Maana HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto.

26  Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.”

Sasa maelezo marahisi ya maandiko haya ni kwamba Wana wa Israeli walipokea sheria kutoka kwa Musa alipopanda kule mlima Sinai/Horebu..na kuwaletea wana wa Israeli agano la sheria..ambalo watu wote waliokuwa chini ya hilo walikuwa ni “watumwa wa sheria”..na ndio wayahudi.

Sasa Agano hili la sheria wana wa Israeli walilolipokea kutoka Mlima SINAI,  lililowafunga na kuwafanya kuwa watumwa wa hiyo sheria na ndilo linalofananishwa na HAJIRI (aliyekuwa kijakazi wa Sara), kwasababu Hajiri alikuwa ni mtumwa na wala si Huru. Na mtoto wake Ishmaeli pamoja na wengine wote waliofuata (watoto wa Ishmaeli) bado walikuwa ni wana wa mjakazi tu vile vile.

Lakini Sara hakuwa mjakazi, bali alikuwa HURU pamoja na Mtoto wake Isaka, ikifunua agano la pili la UHURU ambalo ndilo la wale watu waliozaliwa kwa roho, ambao sheria imeandikwa ndani ya mioyo yao na si katika mawe, au makaratasi.

Na hawa ni watoto wa Sara kwa namna ya roho na ndio wana wa YERUSALEMU YA MBINGUNI, kwasababu wote wanaoishi kwa kuongozwa na roho ndio watakaoirithi YERUSALEMU MPYA na ndio wenyeji wao upo kule, lakini wanaoishi kwa sheria ambayo asili yake ni mlima Sinai, hao ni wa Yerusalemu ya duniani.

Na kama vile Hajiri alivyofukuzwa pamoja na mwanae, kwasababu si mwana wa ahadi…vile vile wote wanaoataka kuishi kwa sheria watatengwa na Kristo.

Wagalatia 5:4 “Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema”.

Biblia inatufundisha kuwa tunahesabiwa haki kwa Neema, kwa njia ya Imani na si kwa matendo ya sheria.

Warumi 3:9 “Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

10  Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.

11  Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa Imani”.

Sasa kujua kwa undani tofauti ya Matendo ya sheria na Matendo ya Imani fungua hapa >>NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

KATIKA MLIMA WA BWANA ITAPATIKANA.

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Rudi Nyumbani

Print this post

MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.

Mwimbaji mmoja wa tenzi za rohoni aliandika hivi “Kama alivyoonyeshwa Yakobo zamani, msalaba umekuwa ngazi ya mbinguni (Tenzi no. 81, ubeti wa 2)”.. akirejea wakati ule  Yakobo alipokuwa amelala pale Betheli na akaona maono, ngazi kubwa kutokea mbele yake, na malaika wakikwea na kushuka kutoka mbinguni.

Mwanzo 28:11 “Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.

12 Akaota ndoto; na tazama, NGAZI IMESIMAMISHWA JUU YA NCHI, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake…..

16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.  17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, NAPO NDIPO LANGO LA MBINGUNI”.

Na ufunuo wa ngazi hiyo ni MSALABA.. Hakika! Kupitia msalaba wa YESU tunafika mbinguni, kupitia ufunuo wa msalaba wa BWANA YESU maishani mwetu, na si shingoni mwetu, tutamwona MUNGU!..

Lakini nataka pia tuutafakari msalaba kwa jicho lingine, kama “ZANA YA KUJENGEA MAISHA”. Hebu turejee kisa kimoja katika biblia kilichomhusu Nabii Elisha pamoja na wana wa manabii na kisha tutauelewa Zaidi msalaba wa BWANA.

2Wafalme 6:1 “Kisha, wana wa manabii wakamwambia Elisha, Angalia basi, mahali tukaapo mbele yako ni padogo kwetu.

2 Basi twende mpaka Yordani, twakuomba, tutwae huko kila mtu mti mmoja, ili tujifanyie huko mahali pa kukaa. Akajibu, Haya! Nendeni.

3 Mmoja wao akasema, Uwe radhi, basi nakusihi, uende pamoja na watumishi wako. Akajibu, Nitakwenda.

4 Basi, akaenda pamoja nao. Nao walipofika Yordani, wakakata miti.

5 Lakini mmojawapo alipokuwa katika kukata boriti, chuma cha shoka kikaanguka majini; akalia, akasema, Ole wangu! Bwana wangu, kwani kiliazimiwa kile.

6 Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonyesha mahali. AKAKATA KIJITI, AKAKITUPA PALE PALE, CHUMA KIKAELEA.

7 Akasema, Kiokote. Basi akanyosha mkono, akakitwaa”

Nataka tuutafakari huo mstari wa sita..“AKAKATA KIJITI, AKAKITUPA PALE PALE, CHUMA KIKAELEA”.

Hiki kijiti ni NINI?, na Chuma ni nini?

Chuma ni zana ya ujenzi, kumbuka huyu mtu alikuwa anakata mti kwaajili ya ujenzi ya makazi, na kwa bahati mbaya kichwa cha shoka kikaangukia majini, na shoka halikuwa la kwake bali aliazima tu!. Hivyo kazi ya ujenzi wa makazi yake ikasimama, na vile vile akabaki na deni ya kulipia kile kifaa.

Huenda shoka lako likawa ni elimu uliyo nayo, ambayo pengine kupitia hiyo ndio umefikiri kujenga maisha yako, au kazi uliyo nayo ambayo kupitia hiyo ndio unafikiria kujenga maisha yako, na makazi yako..Huenda shoka lako ni kipawa au uwezo Fulani ulionao ambao kupitia huo unaamini kazi yako itaisha salama.

Nataka nikuambie wakati unafikiri Elimu yako ni chuma kigumu cha kujenga maisha, au kazi yako ndio chuma kigumu cha kujenga maisha yako, au utashi wako ndio chuma kigumu cha kuchonga maisha yako..usisahau kuwa yapo maji pembeni yako!!!, na hiko chuma saa yoyote kitazama..na kile ulichotazamia kukikamilisha kitasimama, na hata kupata hasara kubwa ya madeni.

Sasa kitu pekee kinachoweza kutoa chuma ndani ya maji, hata kielee, si winchi, au sumaku, au kifaa kingine chochote chenye uwezo…bali ni KIJITI KIDOGO TU!.. Na kijiti hiko si kingine Zaidi ya MSALABA BWANA YESU!!.

(Kumbuka msalaba wa Bwana YESU si Rozari shingoni, au sanamu madhahabuni, au mti wa msalaba juu ya kaburi, bali ni ufunuo wa Mauti ya YESU moyoni)…Maana yake wokovu unaopatikana kupitia uelewa wa mauti ya BWANA YESU…ambao huo unazaa mtu kujitwika msalaba wake na kumfuata yeye.

Marko 8:34  “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35  Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.

Je! msalaba wa KRISTO upo moyoni mwako??, Umeubeba msalaba wako na kumfuata yeye??.. Au unajitumainisha na chuma ulicho nacho!..ukiamini kuwa elimu yako itakuokoa, au kazi yako, au cheo chako.. Hivyo vyote ukiwa navyo na KRISTO HAYUPO MOYONI MWAKO, UNAFANYA KAZI BURE!!!.

Na tena ni heri ukose hivyo vyote, Ukose elimu, ukose kazi, ukose cheo, ukose kila kitu…lakini msalaba wa KRISTO upo moyoni mwako, kuliko kuwa na vyote hivyo halafu huna YESU moyoni!!…NI HASARA KUBWA!!!

Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa BWANA YESU leo, kama bado hujafanya hivyo, na BWANA ATAKUSAIDIA, Ikiwa utahitaji msaada huo wa kumpokea YESU, basi waweza wasiliana nasi na utapata msaada huo…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

NJIA YA MSALABA

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Shukrani ni nini kibiblia?

Shukrani au kushukuru ni ile hali ya kurudisha hisia chanya kwa mema au mabaya yaliyokufikia.

Kwa tafsiri ya kidunia, shukrani inatolewa pale mtu anapopokea mambo mema.. Kwamfano mtu atarudisha shukrani aidha ya maneno au matendo pale anapozawadiwa kitu, au anapofanyiwa jambo Fulani jema.

Lakini kibiblia, Shukrani inatolewa si tu baada ya kupokea mambo mazuri/mema bali pia kwa mambo yote (hata kwa yale mabaya).. Ndivyo biblia inavyotufundisha..

1Wathesalonike 5:18 “SHUKURUNI KWA KILA JAMBO; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

Soma pia Ayubu 2:10,

Maana yake ni lazima kumshukuru Mungu hata katika yale mambo ambayo tunaona hayajaenda kama tulivyotarajia, (Ikiwemo misiba, na hata wakati mwingine hasara)… kwasababu tunajua yote ni mapenzi ya Mungu kwetu maadamu tupo ndani ya KRISTO.

Lakini Zaidi sana ni vizuri kumshukuru MUNGU kwa mema anayokufanyia.

Moyo wa shukrani ni moyo unaompendeza MUNGU, na moyo usio na shukrani huondoa/hukausha mema yote na Baraka zote kwetu kutoka kwa Mungu.

Wengi wanajifungia milango yao ya Baraka baada ya kukaa kimya pale wanapotendewa jambo fulani na MUNGU, lakini wengine wanaendeleza milango ya Barakabaada ya kumshukuru Mungu kwa mambo waliyotendewa.

Shukrani ni jambo linalompendeza Mungu na linaloendeleza Baraka juu yetu.

Luka 17:12  “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13  wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14  Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

15  Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

16  akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17  Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18  Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

19  Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”.

JE SHUKRANI IPI NI BORA?..

Shukrani iliyo bora ni ile inayoambatana na Sadaka.. Hii ni shukrani bora na yenye nguvu sana zaidi ya ile ya midomo mitupu tu!.

Ifuatayo ni baadhi ya mistari ya shukrani katika biblia.

1Nyakati 16:8 “Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake”.

Ezra 13:11 “Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa”.

Zaburi 7:17 “Nitamshukuru Bwana kwa kadiri ya haki yake; Nitaliimbia jina la Bwana aliye juu”

Mistari mingine ni pamoja na Zaburi 9:1, Zaburi 28:7, Zaburi 33:2, Zaburi 92:1, Zaburi 136:1-3 na Isaya 12:4.

NI MAJIRA GANI SAHIHI YA KUMSHUKURU MUNGU.

Majira sahihi ya kumshukuru Mungu ni pale siku inapoanza, na inapoisha.. Inapoamka asubuhi na kuianza siku ni lazima kumshukuru Mungu kwa ulinzi wa usiku kucha na kwa kukupa siku mpya, vile vile unapoimaliza siku ni lazima umshukuru kwa kuimaliza salama na kwa ulinzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya Ayubu 31:10, “Mke wangu na asage kwa mwingine”?

Swali: Kusaga kunakozungumziwa katika Ayubu 31:10 ni kupi?..na maandiko hayo kwa ujumla yana maana gani?


Jibu: Turejee kuanzia mstari ule wa 9.

Ayubu 31:9 “Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;

10 Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake.

11 Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi”

Maneno haya ni ya Ayubu kwa rafiki zake watatu, ambapo alikuwa anajaribu kuwaambia ukamilifu wake kuwa hajawahi hata kumtazama mwanamke kwa kumtamani (Ayubu 31:1) wala hajawahi kumchukua mke wa jirani yake… Hivyo majaribu yaliyompata si kwasababu ya dhambi au makossa.

Na hapo mstari wa 9 anazidi kujithibitisha kuwa kama “moyo wake ulishawishwa kwa mwanamke, Na ameotea mlangoni pa jirani yake;  Ndipo hapo mke wake na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake”.

Akimaanisha kuwa kama yeye aliotea mlango kwa jirani yake, maana yake alisubiri mume wa mke wa jirani yake aondoke kisha aingia na kulala na mwanamke huyo.. basi na yeye pia mke wake na achukuliwe na akasage kwa nyumba ya mwanaume mwingine.

Sasa kusaga kunakozungumziwa hapo ni “kule kusaga nafaka”.. Kumbuka shughuli maarufu ya wanawake wa zamani katika nyumba zao zilikuwa ni kusaga nafaka kama ngano au mtama..

Ndio maana utaona katika lile tukio la unyakuo limefananishwa na wanawake wawili kukutwa wakisaga, na si wanaume..

Luka 17:34 “Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

35  Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

36  Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]

Kwahiyo kusagan ilikuwa ni shughuli ya siku zote ya wanawake wa nyumbani, Na walikuwa wanasaga kwa kutumia mawe maalumu yajulikanayo kama “Mawe ya kusagia”

Kwa maelezo ziadi kuhusiana na Jiwe/mawe ya kusagia fungua hapa >>>JIWE LA KUSAGIA

Kwahiyo Ayubu alimaanisha kama aliiba mke wa mtu mwingine, basi wake pia achukuliwe na kutumikia nyumba nyingine, (kwa shughuli hizo za kusaga na nyingine kama za mama wa nyumbani).. na si tu asage, bali pia na wengine wainame juu yake, (maana yake walale naye).

Lakini hayo yote Ayubu hayakumpata kwasababu alikuwa mkamilifu katika njia zake, na wala hakuwahi kulala na mke wa jirani yake, wala kudhulumu, wala kumnyima maskini mkate..njia zake zote zilikuwa ni kamilifu kama Bwana Mungu alivyomshuhudia..

Ayubu 1:1 “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu”

Ni mambo gani tunajifunza kwa maisha ya Ayubu?

Jambo la kwanza: ni roho ya kumcha Mungu na kuepukana na Uovu.. Watu wanaomcha Mungu na kuepukana na uovu ndio wanaosifiwa naye..

pili: ni Uvumilivu wa Ayubu…Pamoja na majaribu yote yale, alimngoja BWANA, wala hakumwazia Mungu kwa upumbavu (Ayubu 1:22), na mwisho wa siku Bwana alimwokoa na majaribu yale yote.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

Je umempokea YESU?..kama bado unasubiri nini?.. Fahamu kuwa mlango wa wokovu hautakuwa wazi siku zote, ipo siku utafungwa, na siku hiyo imekaribia sana, huwenda ikawa leo?..Je parapanda ikilia na ikikukuta ukiwa katika hali hiyo, utakuwa mgeni wa nani?..au ukifa katika hali hiyo kule uendako utakuwa mgeni wa nani?.. Tafakari sana na ufanye maamuzi, kama bado hujaokoka.

Bwana YESU ANARUDI.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

Biblia inamaana gani inaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kuba ni nini (Ayubu 22:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu,

Ni swali ambalo linaulizwa na wengi, je ni kweli mtu anaweza kuzishinda tamaa za mwili? Au vishawishi vyake?  Anaweza kweli kuacha dhambi ya uzinzi, au kujichua,au kutazama picha za ngono, au ulevi, au miziki, n.k.?

Jibu la kibinadamu ni hapana! Na ndivyo ilivyo.. Lakini jibu la Mungu ni ndio, kwasababu alisema kwake yote yanawezakana.(Mathayo 19:26).

Akili yako itakuambia haiwezekani, kwasababu hujajua kanuni ya kuwezekana. Mimi niliwahi pia kufikiri hivyo hapo nyuma. Lakini nikathibitisha kile maandiko yanasema, kuwa hilo jambo linawezakana, Mungu hasemi uongo. Sasa utauliza ni kwa namna gani?

Awali ya yote ni vema ukafahamu kuwa hakuna mwanadamu yoyote aliyeumbwa na uwezo wa kuzishinda tamaa za mwili.  Hayupo. Vilevile anayejaribu kufanya hivyo kwa akili zake, na kwa nguvu zake peke yake, pia anajidanganya mwenyewe kwasababu, utafika wakati atayarudia yaleyale tu. Ikiwa wewe ni mmojawapo unayejaribu kupambana kwa nguvu zako, utavunjika moyo ni heri leo ujue kanuni sahihi ya kuitumia.

Sasa ni kwa namna gani tutaweza kushinda hali hizo za mwili?

Kanuni imetolewa kwenye mistari huu.

Wagalatia 5:16  BASI NASEMA, ENENDENI KWA ROHO, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. 17  Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

Anasema “Enendeni kwa Roho”, biblia ya kiingereza inatumia neno “Walk in spirit” akiwa na maana “Tembeeni katika Roho”

Wakristo wengi, wanampokea kweli Roho Mtakatifu, wanajazwa Roho kabisa, lakini ni wachache sana “wanaotembea katika Roho Mtakatifu”.

Ni sawa, na mgeni unayemkaribisha nyumbani mwako. Halafu unapokwenda kazini, au matembezini unamwacha nyumbani, hajui kingine chochote kuhusu wewe zaidi ya maisha ya palepale unayokutana naye nyumbani. Ndivyo anavyofanywa Roho Mtakatifu na waamini wengi.

Tunamtambua Roho tu, pale tunapokuwa ibadani, lakini maisha nje ya ibada, sisi ni watu wengine kabisa. Na hapo ndipo linapokuja tatizo kwanini vishawishi na tamaa zinatushinda. Kwasababu hatutembei na  Roho Mtakatifu.

Ukweli ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye anayekusaidia wewe kuua nguvu ya tamaa ndani yako. Na hivyo anahitaji uwepo wake uwe nawe wakati wote, ili hilo liwezekane.  Ni sawa na GANZI, anayopigwa mgonjwa, wakati ganzi, ipo mwilini hawezi kusikia maumivu, lakini inapoisha maumivu yanamrudia kwa kasi, hivyo anahitaji kuongezewa ganzi nyingine, ili aendelee tena kukaa bila maumivu.

Ndivyo alivyo Roho Mtakatifu, huna budi kufahamu ni namna gani atakupiga ganzi, ili uweze kuishi maisha ya ushindi hapa duniani. Na kanuni si nyingine zaidi ya Kuenenda katika Roho. Kuanzia leo acha kupambana na hizo tamaa kivyako, hutazishinda, pambania kujawa na Roho lakini pia kutembea naye maishani mwako.

Sasa Tunatembeaje katika Roho?

Kwa kuzingatia mambo makuu matatu.

1). KWA KUWA WAOMBAJI WA DAIMA:

Watu wengi wanapofikiria maombi akili zao zinakwenda moja kwa moja kudhani ni wasaa kwa  kuwasilisha mahitaji yao. Lakini maombi si mahali tu pa mahitaji, bali ni mahali pa kujazwa Roho. Hivyo kama mtoto wa Mungu uingiapo kwenye maombi yako kila siku tumia nafasi ya kuomba ujazwe Roho Mtakatifu, akuongoze, akupe nguvu, akujenge nafsi yako, uimarike. Hivyo yakupasa uingie katika maombi ya ndani kabisa sio juu juu ya kutimiza ratiba, bali ya kuweka mawazo yako yote kwa Roho Mtakatifu, akujawe ndani yako, hili ni muhimu sana, kwasababu yeye ndio atakayekusaidia.

Sasa kwa jinsi unavyoomba kwa muda mrefu, na kwa mara kwa mara, ndivyo unavyozidi kumpa nafasi Roho wa Mungu kukujaza nguvu, na mwisho unaona vitu kama tamaa ni vidogo sana, kwasababu ganzi imeshaingia vya kutosha ndani yako.

Jambo hili linatakiwa liwe ni la kila siku(Waefeso 6:18). Kama wewe sio mwombaji, kiwango cha Roho kitakuwa kidogo ndani yako, mwili utakulemea tu, haijalishi upo kwenye wokovu kwa miaka 50, utasumbuliwa tu na tabia za mwilini, Ndio maana tunasisitizwa tuombe kila wakati. Maombi ni kila wakati, kila saa, omba kwa akili, pia omba wa kunena kwa lugha kwa jinsi Bwana atakavyokujalia. Lakini elekeza mawazo yako katika kujazwa na yeye, ukiwa ni mwombaji wa wiki mara moja uendapo kanisani jumapili, au mwezi mara moja, hapo unapoteza muda, hutembei katika Roho. Uthibitisho wa anayetembea kwa Roho ni Yule ambaye ni mwombaji wa kila siku.

2) LIWEKE NENO LA MUNGU AKILINI MWAKO WAKATI WOTE.

Neno la Mungu, husisimua roho zetu wakati wote. Na adui anachohakikisha ni kutufanya sisi tulisahau, hivyo mambo mengine yatawale akili zetu. Anajua akili yako ikiwa inatafakari habari na maonyo katika biblia, itakaa mbali na njia mbovu.

Pale adui anapotaka kukujaribu ukifiria wema Mungu aliomtendea Yusufu, kwa kuukimbia uzinzi, anajua utapata nguvu, pale Mungu alipomtukuza Ayubu kwa kukaa mbali na maovu, utapata nguvu, jinsi Danieli alivyokuwa mwaminifu, Mungu akamwinua anajua utaendelea katika uaminifu wako . Hivyo hapendi, wewe utawaliwe na Neno kichwani, anataka utawaliwe, na movie, utawaliwe na mipira, utawaliwe na siasa, na  mambo ya mitaani, basi. Akili yako izunguke hapo, lakini isizunguke kwenye BIBLIA.

Ukijizoesha kilizungusha Neno la Mungu, na ahadi za Mungu kichwani mwako. Tafsiri yake ni kuwa unamzungusha Roho Mtakatifu, katika ulimwengu wako wa maisha. Na ni nini atakachokifanya kwako kama sio kukusimua roho yako, kwa Neno lile. Hivyo unayashinda yote kirahisi. Watu hawajui Neno la Mungu ndio Roho Mtakatifu mwenyewe wanasema nao.

Yohana 6:63  Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; MANENO HAYO NILIYOWAAMBIA NI ROHO, TENA NI UZIMA.

Soma sana Neno, lakini zaidi, lidumu kichwani pako, kutwa nzima. Huu ni ulinzi kamili, na silaha madhubuti ya mambo yote ya mwilini.

3) FANYA MAAMUZI YA GEUKO LA KWELI.

Maamuzi ni kutii. Ukiwa mtu wa nia nia mbili, unataka kumfuata Yesu, na wakati huo huo hutaki ulimwengu ukuache nyuma. Hapo napo unamzuia Roho wa Mungu kufanya kazi yake vema ndani yako. Unaweza ukawa ni mwombaji kweli lakini kama moyoni mwako hujaamua kufanya maamuzi, bado ni kazi bure.

1Yohana 2:15  Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16  Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17  Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele

Ukiamua kumfuata Yesu, fahamu kuwa hii dunia sio fungu lako tena, anasa sio rafiki tena kwako. sio tu na ulimwengu lakini pia na nafsi yako.Ndipo hapo unachukua hatua za dhahiri kabisa katika  imani yako, kama ulikuwa na vichocheo vyote vinavyokusababishia utende dhambi, ndio hapo Yesu anakuambia ukate, usione huruma kutupa hizo nguo za kizinzi ulizozoea kuzivaa, kuachana na huyo girlfriend, kuacha hizo muvi za kizinzi, unazoangalia, usione shida kuacha kampani zako za walevu, usijihurumie hata kidogo, huku ukiwa na mawazo kuwa unafanya hivyo kwasababu ya Kristo ndiye atakayekupa neema ya kushinda.

Ijapokuwa mwanzoni utaona shida kwasababu unafanya kimwili, kwa utiifu wako huo baadaye Roho wa Mungu atakunasa, kwasababu umempa umiliki wote wa maisha yako. Ganzi kubwa sana itaingia ndani yako,.

Ukizingatia mambo hayo matatu, kila siku katika maisha yako. Basi wewe unaenenda kwa Roho. Hakuna litakalokuwa gumu kwako. Kwasababu si kwa nguvu zako bali kwa nguvu za aliye ndani yako, unayashinda hayo.

Wagalatia 5:25  Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.26  Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

Kamwe hatuwezi kuitenganisha nyumba ya MUNGU na JINA LAKE.. Vitu hivi viwili vinakwenda pamoja DAIMA!!!..

Lakini nyumba ya Mungu inapogeuzwa na kuwa  nyumba ya Jina la Mchungaji, au jina la Nabii, au inakuwa nyumba ya Maji ya Upako, au mafuta ya Upako, au chumvi ya Upako..nyumba  hiyo inakuwa si nyumba tena ya Mungu bali inakuwa ni pango la wanyang’anyi kulingana na biblia.

Yeremia 7:11 “Je! Nyumba hii, IITWAYO KWA JINA LANGU, imekuwa pango la wanyang’anyi machoni penu? Angalieni, mimi, naam, mimi, nimeliona jambo hili, asema Bwana”.

Tunapoacha kulinyanyua jina la BWANA YESU ndani ya nyumba yake, na badala yake tunalinyanyua jina la Nabii, au Mchungaji, au Mtume, au mtu Fulani ndani ya kanisa, hapo MUNGU tunayemtamani hayupo!.

Tunapoliondoa jina la BWANA YESU ndani ya Kanisa, na kuanza kutumia mafuta ya upako kila wakati kama njia mbadala!…hapo tumemwondoa MUNGU kabisa na tumemweka mungu mwingine ambaye ni shetani..tunapoliondoa jina la YESU na kutumia chumvi au udongo kama mbadala wake, kwa kila changamoto inayouja mbele yetu…hapo MUNGU hayupo, bali tupo wenyewe!!.

Tunapoacha kuomba kwa jina la BWANA YESU na kuanza kuziomba sanamu..hayo ni machukizo makubwa..

Yeremia 7:30 “Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao NDANI YA NYUMBA HIYO, IITWAYO KWA JINA LANGU, hata kuitia unajisi”.

Kama Mkristo au Mhubiri kamwe usilitenganishe jina la BWANA YESU na NYUMBA YAKE!.. Nyumba yake imekusudiwa kukaa jina lake humo MILELE.. Hakuna wakati ambapo JINA LA YESU, Litaisha muda wa matumizi yake ndani ya KANISA.. Hicho kipindi hakipo!.

Zama hizi za siku za mwisho shetani amenyanyua uongo mkubwa sana, kuwa ZAMA ZA JINA LA YESU ZIMEPITA! Hivyo sasa jina la YESU halina nguvu tena wala hatulitumii tena.. Ndugu fahamu kuwa huo ni uongo wa adui asilimia zote, jina la YESU limekusudiwa kutajwa na kutumika ndani ya NYUMBA YAKE DAIMA..

2Nyakati 7:16 “Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa, ILI KWAMBA JINA LANGU LIPATE KUWAKO HUKO MILELE; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima”

Na tena Macho ya Mungu na Moyo wake upo katika Nyumba ile ambayo ndani yake LINAKAA JINA LAKE na si jina la Mtu au kitu. Na tena maandiko yanasema hakuna jina lingine tulilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa hilo jina la YESU.

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”.

Na zaidi sana yanasema,  lolote lile tufanyalo liwe kwa tendo au kwa Neno tufanye yote kwa jina la BWANA YESU.

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa JINA LA YESU ndio MSINGI WA KANISA la kweli la MUNGU.. Mahali pasipotajwa wala kutumika jina hilo, mahali hapo hapana MUNGU wa mbingu na nchi bali pana roho nyingine, ambayo ni ya Adui shetani.

Mistari mingine inayozidi kuthibitisha kuwa nyumba ya MUNGU imekusudiwa kuwekwa jina lake milele ni kama ifuatayo.. 2Samweli 7:13, 1Wafalme 5:5, 1Wafalme 8:18-19, 1Wafalme 9:7, Yeremia 7:10-14, Yeremia 32:34 na Yeremia 34:15.

Je! Umempokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho za kurudi kwake mwana wa Adamu, na hukumu ya mwisho ipo karibu.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

ORODHA YA MITUME.

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kigutu ni nani? (Marko 9:43)

Swali: “Kigutu” ni mtu wa namna gani kama tunavyosoma katika Marko 9:43?


Jibu: Turejee,

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima U KIGUTU, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

“Kigutu” ni mtu aliyekatwa mkono au aliyekatika mkono, tazama picha juu.

Biblia inatufundisha kuwa kiungo chetu kimoja kikitukosesha tukiondoa ili kisitupeleke katika jehanamu ya moto.

Sasa ni kweli kiungo kinaweza kuwa tabia, au marafiki, au vitu vya kimwili ambavyo vimejiungamanisha na mtu kiasi kwamba vinamkosesha katika Imani. Lakini pia biblia iliposema kiungo, imemaanisha pia kiungo kama kiungo, ikiwa na maana kwamba kama ni mkono ndio unakukosesha basi uondoe!, kama mkono wako umezoea kuiba, baada ya kutubu!, basi uondoe! Na hautaiba tena.

Kama ni jicho pia liondoe, na viungo vingine vyote… Na sababu ya Bwana kusema hivyo ni ili mtu aokoke na ziwa la moto, ambao kule kuna funza wasiokufa!, na moto wa kule hauzimiki, na wote wanaoshuka huko moshi wa maumivu yao unapanda juu milele na milele.

Ufunuo 14:10 “yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; NAYE ATATESWA KWA MOTO NA KIBERITI MBELE YA MALAIKA WATAKATIFU, NA MBELE ZA MWANA-KONDOO

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake”.

Kwa upana juu ya viungo vinavyokosesha fungua hapa >>YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini tofauti kati ya moyo na roho?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Kulingana na 1Wakorintho 3:10-15, kama inavyosema..ni kwa namna gani kazi ya mtu itateketea, na kupimwa kwa moto?”

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.

Rudi nyumbani

Print this post