SWALI: Kwanini sehemu kadha wa kadha wana wa Israeli walipoonekana wanakwenda kinyume na Torati hutumia kauli ya
“atakatiliwa mbali na watu wake”. Nini maana ya hii kauli?
Mambo ya Walawi 7:27
[27]Mtu ye yote alaye damu, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
JIBU: Ni kauli ya ujumla inayomaanisha huyo mtu atatengwa na kusanyiko la Israeli. Kutengwa huko kunaweza kuwa Kwa namna mbalimbali kutegemeana na aina ya kosa.
Hizi ndio aina kuu tatu za kukatiliwa mbali
Kifo kilihusika katika baadhi ya hukumu, ambazo Nyingine ni Mungu mwenyewe aliyezitekeleza (Walawi 20:3-6). Na nyingine Wanadamu. Kwamfano mtu yeyote aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa Mawe Mpaka kufa.
Vivyo hivyo katika kuihalifu sabato, adhabu ilikuwa ni hiyo soma;
Kutoka 31:14
[14]Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
Hii nayo ilikuwa ni aina nyingine ya kukatiliwa mbali, ambapo ulifutwa katika hesabu ya waisraeli, inayokufanya kupoteza haki ya kushiriki Ibada yoyote katika makusanyiko, au vipaumbele.
Hesabu 19:20
[20]Lakini mtu atakayekuwa najisi, naye hataki kujitakasa, mtu huyo atakatiliwa mbali katika mkutano, kwa sababu amepatia unajisi mahali patakatifu pa BWANA; hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake; yeye yu najisi.
Maana yake ni kuwa hauwi mshirika tena wa baraka za maagano ya Mungu, kama vile ulinzi na ahadi.
Mwanzo 17:14
[14]Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu.
Hata leo, katika agano jipya mambo mambo tunaweza kufanya yakatusababishia kukatiliwa mbali na rehema za Mungu.
Na adhabu hizo zinaweza kutekelezwa na wanadamu(watakatifu), na nyingine Mungu mwenyewe.
Kwamfano Biblia inatoa ruhusu kanisa kumtenga mtu ambaye anazoelea dhambi, (1Wakorintho 5:1-5)
Mungu mwenyewe anaweza kutekeleza hukumu hiyo, kwamfano tunaweza kuona kwa Anania na Safira, ambao walitumia njia ya hila katika mapatano ya Roho.(Matendo 5:1-11). Lakini pia kwa mtu ambaye anakusudia kuurudia ulimwengu baada ya kuipokea neema, hukumu kama hii huweza kumkuta. (Waebrania 10:26-27)
Kwahiyo jambo hili halikuwa tu kwa wana wa Israeli, lakini lipo hata sasa rohoni. Tusiwe watu wa kuzoelea dhambi tukidhani kuwa wakati wote Mungu ataturehemu. Usidanganyike ukishakatiliwa mbali si rahisi tena kumgeukia Mungu wako.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?
Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu
ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tofauti na nyaraka nyingi za mtume Paulo, ambazo aliziandika kwa Makanisa, waraka huu aliuelekeza kwa Timotheo ambaye alisimama sio tu kama msaidizi wake wa kihuduma bali pia kama mwanae Katika vifungo vya injili. Ni waraka wa kichungaji zaidi ya wa kimafundisho,
Katika waraka huu Paulo anamwagiza Timotheo namna ambavyo kanisa linapaswa likae katika utaratibu, Mungu alioukusudia.(1Timotheo 3:15)
Maudhui makuu ya Paulo kwa Timotheo yalikuwa ni haya;
Haya ni maelezo mafupi Kwa kila kipengele.
Paulo anamhiza Timotheo lengo kubwa la kumtaka abaki Efeso ni ili awazuie watu wasifundishe elimu nyingine.
1 Timotheo 1:3
[3]Kama vile nilivyokusihi ukae Efeso, nilipokuwa nikisafiri kwenda Makedonia, ili uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine;
Elimu hiyo potofu aliyoina iliegemea kuwazuia watu wasile aina ya vyakula, Wasioe, pamoja na kuhubiriwa Hadithi za kizee, na nasaba (1:4, 4:7)
Kwa urefu wa mafundisho Hayo bofya hapa >>> HADITHI ZA KIZEE.
1 Timotheo 4:1-3
[1]Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
[2]kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;
[3]wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Kwa wanaume: Paulo anatoa agizo la kwamba wao wanajukumu la kusalisha kila mahali, lakini bila hasira wala majadiliano, yaani wawe safi kiibada (2:8)
Kwa Wanawake: Paulo anatoa agizo kuwa hawana ruhusa ya kufundisha katika kanisa (2:12), halikadhalika wanawajibu wa kuvaa mavazi ya kujisitiri, mapambo yao yawe yale ya rohoni na sio ya mwilini (2:9-10).
Anaendelea kusema Wanawake ambao ni wajane waandikwe katika kanisa ili Wahudumiwe kimahitaji, lakini wale ambao si wajane kwelikweli hawapaswi kuandikwa (5:4-16)
Wazee, na vijana wafanyapo makosa wasikemewe, Bali Waonywe kwa upole Kulingana na marika yao(5:1), lakini pale wafanyapo dhambi. kwa kukusudia au kuzoelea wakemewe mbele ya wote. (5:20),
Watumwa wote wanawajibu wa kuwaheshimu mabwana zao, si tu kwa wale wasiamini bali pia kwa wale waaminio wawaheshimu wote. (6:1)
Kanisa lina wajibu wa kuwaombea watu wote, na watawala, ili liishi katika utulivu, na amani, katika utauwa wote.(2:1-4)
Sehemu hii Paulo anamwagiza Timotheo juu ya vigezo vya maaskofu, na Mashemasi namna wanavyopaswa wawe, kwamba wawe watu wasio laumika, wameshuhudiwa mema na watu wa nje, waume wa wake mmoja mmoja, si watu wa kupenda fedha,si walevi, si waongofu wapya, wanapaswa wawe wakaribishaji,, wastahivu, wenye kiasi, waaminifu, wawasimamiao watoto wao vema, na wake zao, (3:1-13).
Lakini pia anawahimiza wazee wanaotawala vema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima mara dufu (5:17).
Paulo anamwagiza Timotheo wajibu wake kama mwangalizi kuwa na upendo, Imani isiyo na unafki, na dhamiri njema, upole, saburi, na haki (1:5, 18-20, 6:11),
Anamwagiza afanye mambo yote bila upendeleo (1Timotheo 5:21).
Ajizoeshe kupata utauwa (4:8).
Awe kielelezo katika usemi na mwenendo (4:12)
Asiwaekee watu mikono kwa haraka,(5:22)
Akimbie tamaa ya fedha, na mashindano ya kidini (6:20).
Hitimisho.
Hivyo kwa ufupi, waraka huu ni wa kikanisa zaidi, na kwamba vigizo hivyo vikisimamiwa vema kanisa litakuwa imara, lenye heshima lisiloshitakiwa mabaya nje.
Ikiwa viongozi watachaguliwa hodari, na kila rika na jinsia likahudumu katika nafasi yake, yaani wanawake Kudumu katika upole, kujisitiri na kiasi na wanaume kuhudumu bila hasira wala majadiliano, huku waangalizi wakihakikisha mafundisho potofu hayapati nafasi. Ni ukweli kwamba kanisa hilo litakuwa imara sana.
Bwana akubariki
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mada nyingine:
Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)
Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?
Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)
JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE
Fahamu kanuni muhimu ya kufungua milango ya Baraka za rohoni na mwilini.
Neno la MUNGU linasema..
Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ALIYETUBARIKI KWA BARAKA ZOTE ZA ROHONI, KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, NDANI YAKE KRISTO”.
Ni lini tulibarikiwa na baraka zote za rohoni?..Je ni jana au leo??.. Nataka nikuambie kuwa si jana, wala juzi wala mwaka uliopita wala si siku ile ulipozaliwa…. bali ni tangu siku ile damu ya Mwokozi YESU ilipomwagika msalabani tayari tulishabarikiwa,
Na si kubarikiwa tu, bali pia tayari tulishaponywa tangu siku ile Kristo aliposulibiwa, tayari tulishashinda tangu siku ile Kristo aliposulibiwa..
Sasa swali ni hili, kama tayari Baraka na ushindi tulishapewa tangu siku ile ya pale Kalvari, kwanini sasa hatuzioni hizo Baraka zetu katika roho na katika mwili?
Hili ndilo swali la msingi kujiuliza.. kwanini hatuzioni hizo Baraka tulizobarikiwa miaka mingi iliyopita.
Sababu kuu ya sisi kutoshiriki Baraka zote za rohoni ambazo tayari zilishaachiliwa juu yetu, miaka elfu mbili (2) iliyopita pale Kalvari ni “shetani”.
Anachokifanya adui ni kuzuia kupokea zile Baraka, na si kuzuia zisitoke!.. Tayari Mungu alishatubariki..wala hatuwezi kumwomba tena atubariki, ni sisi kupambania kilicho chetu.
Sasa ili tuweze kupokea kilicho chetu, ni lazima tupambane vita, na vita hivyo ni vile vya kiroho, kwani shetani na majeshi yake yamesimama kuhakikisha hatupokei kilicho chetu.. shetani hamzii MUNGU kutoa, bali anatuzuia sisi kupokea… Na MUNGU tayari alishatoa, ila shetani anazuia tusipokee..
Ni sawa na mzazi aliyemtumia mwanae aliyeko shuleni fedha za matumizi kupitia anwani ya shule, halafu mwalimu mmoja azifiche zile fedha zisimfikie mtoto, hapo mtoto mwenye busara akishajua katumiwa fedha ana wajibu wa kuzifuatilia, na kuulizia na kama kuna shida kwa mwalimu, na kama akiona kuna shida basi aweza kushitaki ili tatizo litatuke, kwasababu atajua shida si mzazi bali ni mwalimu (sasa huu ni mfano tu).
Na mambo ya rohoni ni hivyo hivyo, BWANA MUNGU wetu alishatubariki kwa Baraka zote za rohoni.. kazi tuliyobakiwa nayo ni kushughulika na vizuizi vya sisi kupokea hizo Baraka.
Na silaha zifuatazo ndizo zinazoweza kuvunja vizuizi vyote na kuachia kilicho chetu.
1. MAOMBI
Maombi (hususani yanayohusisha mfungo) ni silaha ya kwanza ya kuzipinga hila za adui zinazozuia Baraka zetu.. Mtu aliyejizoeza kuomba ni rahisi kupokea Baraka zote zilizoahidiwa na MUNGU, na mtu anayepungukiwa maombi ni kinyume chake.
2. KUSOMA NENO.
Maombi bila Neno la Mungu ni sawa na bendera iliyokosa mlingoti… Mtu aombaye huku Neno la Mungu limejaa ndani yake, ni rahisi sana kuteka Baraka zake tofauti na yule asiyekuwa msomaji wa NENO, na kusoma Neno kunakozungumziwa hapa si kushika vifungu vya biblia, La!.. Unaweza kuwa umeshika vifungu elfu vya biblia na bado usiwe umelijua Neno.
Bali kusoma Neno kunakozungumziwa hapa ni kule kujifunza kitabu baada ya kitabu na kujua maudhui ya kila kitabu katika ufunuo wa Roho.
3. UTAKATIFU
Utakatifu wa mwilini na rohoni ni mkuki wa kumpiga yule mwovu aachie vinavyotuhusu.. kinyume chake uchafu na maisha ya dhambi ni kifungo kinachozuia Baraka zetu.
Sasa utauliza Baraka za rohoni na mwilini ni zipi?
Mfano wa Baraka za rohoni ni Amani, furaha, upendo, uvumilivu, upole, utu wema na mambo mengine yote mema yanayofanana na hayo, kwa ufupi ni Roho Mtakatifu na matunda yake (Wagalatia 5:22).
Na baraka za mwilini hamna haja ya kuziandika maana zinajulikana, ambazo ni zile zote zinazohusu mahitaji ya mwilini.
Je umepungukiwa na Baraka?…fahamu kuwa Maombi, Neno na Utakatifu ndio dawa ya kutibu hilo tatizo, wala usimnung’unikie MUNGU kwanini hakubariki.. yeye tayari alishatubariki, ni sisi kupambana kupata vilivyo vyetu..Anza mapambano hayo kuanzia sasa ikiwa tayari umeshampokea Bwana YESU.
Na kumbuka mapambano haya hamna siku yatapoa, hata baada ya kuwa mtumishi.. ni jambo endelevu daima mpaka safari ya maisha inaisha, kwani pia kuna kupokonywa na yule aliyetuzuia tusipokee, ikiwa hatutasimama katika mambo hayo makuu matatu, na mengine yanayofanana na hayo.
Hivyo ukristo ni mapambano, ni vita, lakini vyenye nafasi kubwa ya kushinda Zaidi ya kushindwa kwa msaada wa Roho Mtakatifu.
Warumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote TUNASHINDA, NA ZAIDI YA KUSHINDA, kwa yeye aliyetupenda”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.
MILANGO YA KUZIMU.
NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?
CHAKULA CHA ROHONI.
MILANGO YA KUZIMU.
SWALI: Je! watu wanapaswa wakemewe au wasikemewe pale wanapofanya dhambi kulingana na 1Timotheo 5:1 na 20?
JIBU: Tusome,
1 Timotheo 5:1-2
[1]Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;
[2]wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.
Na,
1 Timotheo 5:20
[20]Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.
Mwandishi anatoa maelezo katika mazingira mawili tofauti. Mazingira ya kwanza ni katika eneo la marekebisho na mazingira ya pili ni katika eneo la makosa ya makusudi.
Kwamfano katika vifungu hivyo vya kwanza, anavyosema Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;analenga hasaa katika makosa ambayo yanajitokeza katikati ya huduma au maisha ya kikristo, kwamfano pengine mtu katika kuhudumu kwake kaonyesha uvunjifu fulani wa nidhani ya kimadhabahu, au kasema lugha isiyo ya staha, au kavaa vazi lisilo na heshima, au kabagua wengine, au kawadhulumu wengine, n.k. ambayo imesababishwa na uchanga wa kiroho au madhaifu ya kibinadamu.
Katika mazingira kama hayo Paulo anamhimiza Timotheo, kulingana na marika yao asitumie kukemea bali awaeleze kwa upole, nao watajirekebisha, akitambua kuwa wapo katika hatua za kuutafuta ukamilifu.
Lakini katika hivyo vifungu vya pili. Analenga Zaidi kwa wale wanaodumu kutenda dhambi. Wanaojua kabisa wanachokifanya sio sahihi, lakini wanaendelea kudumu kufanya hivyo, Paulo anasema hawapaswi kuvumiliwa bali kukemewa mbele ya watu wote.
Kwamfano mtu ni mzinzi, na tabia hiyo anaendelea nayo kanisani, au ni mlevi, au mchonganishi, sasa hawa wanapaswa wakemewe hadharani bila kujali marika yao, ili wengine wasiige Tabia hizo. Kwasababu wakiachwa wataendelea kulichachusha kanisa.
Makanisa mengi leo hii yamekumbwa na matatizo makubwa mpaka kusababisha jina la Kristo kutukanwa Nje, ni kutokana na kuvumiliwa kwa watu wa namna hii wanaodumu katika kutenda dhambi.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kuna hukumu za aina ngapi?
Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).
USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.
Swali: Madongoa kama inavyosomeka katika Ayubu 7:5, ni kitu gani, na ina ujumbe gani kiroho?.
Jibu: Turejee..
Ayubu 7:5 “Mwili wangu unavikwa mabuu na MADONGOA YA UDONGO; Ngozi yangu hufumba, kisha ikatumbuka tena”.
Madongoa ni udongo ulioshikamana pamoja, sawasawa na Ayubu 38:38..
Ayubu 38:38 “Wakati mavumbi yagandamanapo, Na madongoa kushikamana pamoja?”
Kikawaida ardhi yenye Madongoa haifai kwa kilimo, bali mpaka madongoa hayo yatakapovunjwa na kulainishwa, ndipo mbegu ziweze kupandwa…
Isaya 29:23 “Tegeni masikio, sikieni sauti yangu, sikilizeni mkasikie neno langu.
24 Je! Mwenye kulima alima daima, ili apande? Afunua daima MADONGOA YA NCHI YAKE, na kuyavunja?
25 Akiisha kuulainisha uso wa nchi yake, je! Hamwagi huko na huko kunde, na kutupa-tupa jira, na kuitia ngano safu safu, na shayiri mahali pake palipochaguliwa, na kusemethi karibu na mipaka yake?
26 Kwa maana Mungu wake anamwagiza vizuri na kumfundisha”.
Neno hili pia tunaweza kulisoma katika kile kitabu cha Hosea 10:11..
Ni ni nini tunachoweza kujifunza??
Kama vile ardhi yenye madongo ilivyokuwa ngumu kwa kilimo, hali kadhalika mioyo yetu inafananishwa na shamba sawasawa na ule mfano wa Mpanzi (Mathayo 13:18-23), na kama mioyo yetu ni migumu kwa namna hiyo basi ni ngumu pia kumzalia MUNGU matunda.
Mfano wa moyo wenye madongoa ni ule ulio mgumu kusikia Neno, mtu mwenye moyo wa kupuuzia, na kutokujali pale asikiapo Neno la MUNGU, mtu wa namna hii anahitaji sana kusaidiwa.
Je ni wewe mtu huyo?. Kama ndio basi mkimbilie YESU leo kwa kumaanisha kabisa naye ataufanya maoyo wako kuwa mlaini, na utayaona matunda ya BWANA.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tufanyaje ili tuonekane tunampenda Mungu?
KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?
Swali: Je Mungu ni mkaidi kulingana na Zaburi 18:26, au kwanini Mungu aseme maneno hayo?
Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 24, ili tupate maana kamili..
Zaburi 18:24 “Mradi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
25 Kwa mtu mwenye fadhili UTAKUWA MWENYE FADHILI; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
26 KWAKE AJITAKASAYE UTAJIONYESHA KUWA MTAKATIFU; Na KWA MPOTOVU UTAJIONYESHA KUWA MKAIDI”
Hapo anasema kwa mtu mwenye fadhili Bwana atajionyesha mwenye fadhili kwake, na kwa ajitakasaye Bwana atajionyesha ni mtakatifu kwake, vile vile na kwa mpotovu atajionyesha mkaidi.
Sasa kwa maneno hayo haimaanishi kuwa Bwana ni MKAIDI..La! yeye ni mwema siku zote na hawezi kufananishwa na sisi wanadamu…Lakini sasa swali ni kwanini aseme hivyo?
Ili tuelewe vizuri tafakari mfano huu; Unaye mtoto halafu ukaanza kuona anaonyesha tabia za kukosa nidhamu, na anafanya mabaya mengi, na ulipomwonya haonyeki, kisha ukaamua kumwambia kuwa endapo akiendelea kuwa na tabia hiyo, utakuwa mbaya kwake!..na akibadilika kuwa mzuri basi utakuwa mzuri kwake…
Je kwa kauli hiyo utakuwa umemaanisha kuwa wewe ni ni MTU MBAYA na MWOVU?.. bila shaka hutakuwa umemaanisha hivyo, bali utakuwa umemaanisha kuwa endapo akiendelea kufanya mabaya, basi utambadilikia na kumwadhibu, jambo ambalo ni baya machoni pa huyo mtoto, na ndicho Bwana Mungu alichomaanisha hapo kuwa kwa “mtu mpotovu atajionyesha kuwa Mkaidi”… Na si kwamba MUNGU ni Mkaidi.
Kwamba kwa mtu anayefanya mabaya Bwana na maovu na hakubali kuonyeka basi atapata mabaya kutoka kwa Mungu, kwani BWANA atamwadhibu,…Na adhabu za Bwana ni za lengo la kuonya, na kumfanya mtu aache njia mbaya, na si za kumpoteza mtu.
Waebrania 12:10 “Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.
11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
12 Kwa hiyo inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza,
13 mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe.
14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”
Na kinyume chake ni kweli, kwa mtu ajitakasaye, yeye Bwana atajionyesha mtakatifu kwake, Maana yake ataona mema mengi kutoka kwa Bwana..
Hivyo hiyo ni tahadhari kwetu na pia ni faraja kwetu, kwamba tukae katika usafi na utakatifu, ili tuuone wema wa Mungu, na tusikae katika upotovu, tusije tukauona ukaidi wa MUNGU, kwani Bwana atajionyesha kwa kila mtu sawasawasa na matendo yake.
Zaburi 18:24 “Mradi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
25 Kwa mtu mwenye fadhili UTAKUWA MWENYE FADHILI; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
26 KWAKE AJITAKASAYE UTAJIONYESHA KUWA MTAKATIFU; Na KWA MPOTOVU UTAJIONYESHA KUWA MKAIDI”
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?
TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa pili (2Wakorintho)
Kama kitabu kinavyojitambulisha, “Waraka wa pili wa Petro kwa watu wote”
Petro ndiye mwandishi. Ni waraka mfupi, aliouelekeza kwa watakatifu wote duniani.
Na haya ndio maudhui yake makuu;
Haya ndio maelezo ya kila kipengele kwa ufupi;
Petro anawahimiza watakatifu wasikwamwe kiroho bali waendelee kukua, mpaka kufikia utimilifu wao ambao ni upendo, Na kwamba mtu asipojitahidi kufanya hivyo matokeo yake ni kuwa atakuwa mvivu, na hatimaye atajikwaa.
2 Petro 1:3-8
[3]Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
[4]Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.
[5]Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,
[6]na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,
[7]na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.
[8]Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
Mtume Petro anatoa hakikisho la ushuhuda wao juu ya ujio wa Kristo, kwamba hawakuupokea katika hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali walishuhudia wao wenyewe kwa macho, walipotokewa na Musa na Eliya juu ya mlima ule mrefu na kuisikia sauti ya Mungu mbinguni moja kwa moja ikimshuhudia Yesu kuwa ndiye mwana wa Mungu, aliyependwa naye.
2 Petro 1:16-17
[16]Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake.
[17]Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.
[18]Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu.
Lakini pia anawahimiza kujiepusha na manabii wa uongo, ili wasije wakachukuliwa na makosa Yao, wakaangamia tena. Ambao sifa zake nyingi ameziorodhesha pale (kwenye sura yote ya pili), Sifa zao ni pamoja na tamaa na uzinzi, akiwataja kama watu wasiokoma kutenda dhambi, wasaliti wa Bwana, wenye uhodari wa kutunga maneno wenye werevu, ili wawavute watu kwao, wenye kupenda ujira wa udhalimu kama Balaamu, watoao maneno ya makufuru, watu wa kujikinai, wasio na hofu ya Mungu, watu wa anasa, wa kuhadaa watu waliosimama imara, ili wawaaungushe.
2 Petro 3:17
[17]Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu.
Petro pia anawahimiza watakatifu wawe na tumaini juu ya uthabiti wa kurudi kwa Bwana,
akiwatahadharisha juu ya kuibuka kwa kundi la watu wenye kudhihaki, wanaosema iko wapi ile ahadi,mbona muda mrefu umepita? lakini Petro analirekebisha kwa kulitolea maelezo kuwa Mungu hakawii kutimiza ahadi yake bali anavumilia ili watu wote wafikie toba. Lakini siku hiyo itakuja kama mwizi, na ulimwengu ukaliwao na waovu utaharibiwa.
2 Petro 3:9-13
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[12]mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?
[13]Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.
Mwisho, mtume Petro anaeleza uthabiti wa yale anayowaeleza, akiwatolea mfano kwa kurejea pia nyaraka za mitume wengine (akimtaja Paulo).Kama pia anayaeleza mambo hayo hayo ayasemayo katika nyaraka zake.
Petro 3:15-16
15 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi
Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika
nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu,
wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao
wenyewe.
Hivyo kwa ujumla maudhui ya waraka huu ni kuwahimiza watakatifu kufanya bidii katika ukamilifu na kujiepusha na manabii wa uongo, na kuchoka kungojea ahadi za Mungu. Bali waendelee mbele kutibitika katika ukamilifu bila wala wala hila hadi siku ya kutokea kwake Bwana Yesu mara ya pili.
Je wewe kama mkristo unayemngojea Bwana. Unafanya imara wito wako na uteule wako, kwa kukua kila siku katika neema kiasi cha kukufanya ujione huna mawaa wala aibu, katika siku ile ya Bwana?
Kama sio, basi wakati ndio huu, Maanisha kugeukia kumfuata Kristo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)
Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Rudi Nyumbani
SWALI: Konstantino mkuu ni nani, na je umuhimu wake katika ukristo ni upi?
JIBU: Konstantino mkuu ni Mmoja wa wafalme waliotawala chini ya dola ya Rumi, Kuanzia mwaka wa 306BK mpaka 337BK.
Dola hii ya Rumi ndiyo dola iliyokuwa na nguvu sana, zaidi ya zote zilizowahi kutokea katika historia, ilifanikiwa kutawala kikamilifu katika nyanja karibia zote, za kijeshi, kisiasi hadi kiuchumi, na ndio ngome iliyodumu kwa muda mrefu kuliko zote.
Itakumbukwa kuwa hata wakati Kristo anakuja duniani, dola hii ndio ilikuwa inatawala ulimwenguni kote na Kaisari ndiye aliyekuwa mfalme. Israeli wakati huo halikuwa taifa huru kama tunavyoliona sasa, bali ilikuwa koloni la Rumi, na watalawa na maliwali wake wote akiwemo, Pilato na Herode walikuwa ni Warumi.
Utawala huu ndio uliomsulubisha Kristo kwa shinikizo la wayahudi. Lakini tunaona katika historia, injili ilipoanza kuhubiriwa na jamii kubwa ya watu kugeuzwa kuwa wakristo duniani kote, Utawala huu ulianza kulitesa kanisa, na hata baadhi ya wafalme wao waovu waliotokea walitunga sheria kwamba ikionekana mtu yeyote anajiita mkristo, basi adhabu yake ilikuwa ni kifungo kama sio kifo.
Mfano wa watawala hawa alikuwa Nero, trajan, na Domitian, Na hiyo ilipelekea jamii kubwa sana ya wakristo kuuawa kikatili, wengine kuchomwa moto, wengine kusulubiwa, wengine kuwekwa katika viwanja vya mauaji na kuachiwa wanyama wakali wawaue, idadi ya mamilioni ya wakristo walipoteza maisha kwa njia hii. Historia hiyo utaipata vema katika kitabu maarufu kijulikanacho kama (Foxes book of martyrs). Kumbuka utawala uliohusika ulikuwa ni huu wa Rumi, chini ya watawala wao mbalimbali.
Hivyo kwa wakati wote huo ukristo ulionekana kama imani ya vikundi fulani vya wavuruga amani..
Wakati huo Rumi lilikuwa ni taifa la kipagani likiongozwa kisiasa, chini ya dini zao za miungu mingi.
Lakini alipokuja kutokea huyu mtawala mpya aliyeitwa Kostantino baada ya watawala 59 kupita nyuma yake,
Kwa mujibu wa ushuhuda wake anasema wakati anakwenda kupigana vita mojawapo kuu iliyomkabili, katika maono aliona..msalaba angani, akaambiwa kwa ishara hii utashinda. Hivyo Konstantino akaichukua nembo ya ukristo na kuipachika katika ngao za jeshi lake, na hivyo akashinda vita ile iliyokuwa inamkabili, ushindi huo ulimuimarishia sana ufalme wake.
Huo ndio ukawa mwanzo wake wa kuwa mkristo. Aliendelea kuupa sana kipaumbele ukristo, Kuanzia huo wakati ndio ukawa mwisho wa mauaji ya watakatifu. Na mwanzo wa dini ya Kikatoliki.
Lakini historia inaonyesha Konstantini hakuwa ameupokea ukristo katika ukamilifu wote, kama madhehebu baadhi yanavyoamini. Bali ukristo wake ulikuwa na msukumo wa kisiasi pia nyuma yake, ambao ulilenga kuwaunganisha wakristo na warumi wakipagani, kwasababu hakuacha pia kuabudu miungu yake ya kirumi. Ndio maana ibada gheni za miungu zilichanganywa na imani ya mitume, kwa kuzaliwa kanisa katoliki na kulipelekea kanisa kuingia katika kipindi kirefu sana cha ukimya kijulikanacho kama kipindi cha giza.
Pamoja na hayo ni kweli alifanikiwa kukomesha mateso kwa wakristo, na kuuthaminisha ukristo, na wakati mwingine kuruhusu mabaraza ya Wakristo, kuthibitisha vipengele kadha wa kadha vya imani, vilivyoleta msaada mwingi.
Lakini pia hakuuingiza Ukristo Katika misingi yake yote, ndio maana kanisa liliongia katika kipindi cha giza.
Hata hivyo kwa sehemu yake alisimama kuanzisha Imani ijapokuwa hakufanya katika utimilifu wote. Ilikuwa ni wajibu wa mabaraza Na wazee na watakatifu, Kuyatengeneza yaliyosalia, lakini hawakupiga hatua yoyote zaidi ya pale kwa miaka mingi.
Lakini ashukuriwe Mungu wakati wa matengenezo ulipofika (Karne ya 15)..Bwana aliwanyanyua watu wake mbalimbal8 mfano wa Martin Luther, Zwingli, Calvin na wengineo kulitengeneza upya kanisa kutoka katika misingi mibovu Mpaka wakati wa Pentekoste, ambapo kanuni zote za Kibiblia zilirejeshwa. Na mpaka sasa Kanisa linazidi kupanda katika utumilifu wake wote.
Hivyo ni wajibu wetu, sote kusoma biblia na kuifahamu kwa kina kwa mwongozo wa Roho Mtakatifu, lakini pia kuhubiri injili kwasababu kwa njia hiyo ndivyo tutakavyoujenga ufalme Wa Kristo Na kuufanya uenee duniani kote, kiufasaha.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Naliupata wenyeji huu kwa mali nyingi, maana yake nini (Matendo 22:28)
Kichwa cha kitabu hichi kinasema “Waraka wa kwanza wa Petro kwa watu wote” Kutuonyesha kuwa Petro Ndiye mwandishi.
Waraka huu mfupi aliuelekeza kwa watakatifu wote waliotawanyika, na kuishi kama wageni maeneo ya Asia ndogo ambayo kwasasa ni nchi ya Uturuki.
Maudhui makuu ya waraka huu tunaweza kuyagawanya katika sehemu kuu nne(4):
1) Ni kuwafariji watakatifu kwa kuwaeleza juu ya utukufu walioandaliwa mbinguni utakaofunuliwa siku ya mwisho. Na kwamba kwa kulitambua hilo basi wafurahi Katika majaribu mbalimbali ya imani, yaliyo ya kitambo tu.
2) Lakini pia unalenga kuwahimiza kuishi maisha ya utakatifu ya kumpendeza Mungu katika wakati wao wa kuishi hapa duniani.
3) Vilevile wajibu wakuishi maisha ya nidhamu katika Jamii ya wasioamini inayowazunguka.
4) Halikadhalika wajibu wa viongozi kulichunga kundi la Kristo kwa uaminifu wotena wajibu wa kanisa lote kumpinga shetani.
Haya ni maelezo mafupi juu ya kila kipengele:
Petro anawahimiza watakatifu kwamba wafurahi katika majaribu mbalimbali (kuliko kuhuzunika) kwa sababu ya uthamani mkuu wa imani yao itakayolipwa siku ile ya mwisho ambayo Yesu atafunuliwa kwetu.
1 Petro 1:6-7
[6]Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;
[7]ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.
> Petro Anahimiza kuiga kielelezo cha Kristo ambaye yeye alikubali kuteswa ijapokuwa hakutenda Dhambi, hata alipotukanwa hakurudisha majibu. Vivyo hivyo na sisi tukubali teso lolote kwa ajili yake katika upole wote, uvumilivu na ustahimilivu.
1 Petro 2:19-21
[19]Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.
[20]Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
[21]Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.
1 Petro 4:12-16
[12]Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
[13]Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
[14]Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.
[15]Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.
[16]Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
Sehemu hii ya pili Mtume Petro anawahimiza watakatifu, kuwa kwasababu wanatazamia neema itakayofunuliwa siku ya mwisho ya kuja kwake Yesu Kristo (1:13), hivyo hawana budi kuishi maisha ya kiasi na utakatifu hapa duniani.
1 Petro 1:13-16
[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
[14]Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;
[15]bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
1 Petro 2:1-2
[1]Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.
[2]Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;
> Petro anaendelea kuwasihi watakatifu waishi kama wapitaji duniani, kwa kuziepuka tamaa za mwili.
1 Petro 2:11
[11]Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.
1 Petro 4:2-3
[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
> Anaeleza pia Wajibu wa kupendana kuhurumiana, kunyenyekeana, tuwe watu wasiolipa baya kwa baya, bali wenye kubariki(3:8-12, 4:7)
> Kadhalika pia anaeleza wajibu wa wanandoa. Kwamba wake wawatii Waume zao, na kujipamba kwao kunapaswa kuwe kwa mapambo ya rohoni, Lakini pia waume kuishi na wake zao kwa akili. (3:1-7)
Katika sehemu hii ya tatu anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaopasa kwa watu wasioamini, ili wakose nafasi ya kutushitaki au kutulaumu kwa lolote.
> Anagusia katika eneo la watumwa Kwamba wawatii bwana zao, si wale tu wapole bali pia wale wakali.(2:18)
> Lakini pia Watakatifu waitii kila kilichoamriwa na mamlaka.
1 Petro 2:13-15
[13]Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;
[14]ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.
[15]Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;
> Lakini pia anahimiza watakatifu wawaheshimu watu wote(2:17)
Mwishoni Petro anatoa wito wa waangalizi wa kanisa la Mungu (wazee), kwamba walichunge kundi kwa hiari, sio kwa kulazimishwa au kutazamia malipo ya kifedha, bali kwa moyo.
1 Petro 5:1-3
[1]Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;
[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.
[3]Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.
> Pamoja na hayo anasisitiza watakatifu wote wawe na kiasi na kukesha, kwasababu adui yetu ibilisi ni mfano wa simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo wana wajibu wa kumpinga sikuzote.(5:8-9)
Hitimisho:
Hivyo kwa maelezo machache ni kwamba Petro analihimiza kanisa kutembea katika uvumilivu wote na uthabiti Wa imani, pamoja na utakatifu, na kutimiza wajibu wao katika utakatifu na adabu kwa wanadamu wote, katika wakati ambao kanisa linasubiria neema kuu itakayofunuliwa siku ya mwisho Yesu atakaporudi.
Na ndivyo ambavyo sote tunapaswa tuishi hivyo sasa.
Kama mkristo je unaendelea kufurahi katika majaribu? Unaishi maisha matakatifu? Unaishi vema na jamii yako? unaifanya kazi ya Mungu? Unampinga shetani kwa kudumu katika sala?
Ikiwa hayo, unayazingatia basi, wewe ni mshirika wa neema hiyo kuu ya Mungu itakayofunuliwa siku ya mwisho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)