Category Archive Home

Je jina Eva na Hawa ni sawa?

Swali: Katika Mwanzo 3:20 na Mwanzo 4:1 mkewe Adamu ni Hawa. Nmekuwa nikisikia mkewe Adamu pia ni Eva. Je! jina Eva na Hawa ni sawa?

Jibu: Hawa na Eva ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti ni sawa na jina YESU na JESUS; ni jina moja isipokuwa katika lugha mbili tofauti, yaani ya kiingereza na ya  kiswahili.

Kadhalika na Eva (au Eve) ni kiingereza na HAWA ni kiswahili chake.

Sasa swali ni kwanini, tafsiri zake zionekane kama mbalimbali, yaani Kutoka Eve mpaka Hawa ni kama hazikaribiani?. Kwanini Eve isingetafsiriwa tu Eva kwa lugha ya kiswahili badala yake ikawa Hawa?

Jibu ni kwamba lugha ya kiswahili sehemu nyingi imeitafsiri herufi “V” kwa “W” katika majina ya watu au vitu. Kwamfano utaona jina “LAWI”, kwa lugha ya kiingereza ni “LEVI”.

Vilevile mji wa “Ninawi” kwa lugha ya kiingereza ni “NINEVEH”n.k

Kwahiyo hata Eva kiswahili chake ni lazima kirudi kwenye herufi “w” na kuwa “Hawa

Ni kama vile majina yote yanayoanza na herufi “J” yanavyobadilika na kuanza na herufi  “Y” yanapokuja katika lugha ya kiswahili…Kwamfano Jina Jesus-Yesu, Jonah-Yona, Joshua-Yoshua, Jezebel- Yezebeli n.k Ndivyo ilivyo kwa majina yote yenye herufi “V”, yalibadilika na kuwa “W” yanapoletwa katika lugha ya kiswahili.

Kwahiyo kwa hitimisho mtu anayetumia Jina Hawa na anayetumia Eva wote wapo sahihi, na wanamlenga mtu mmoja.

Je umempokea Yesu?..je umebatizwa?..je umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado unasubiri nini?. Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi.

Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya ELOHIMU?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

Rudi nyumbani

Print this post

Kipaku ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kipaku ni kipele kidogo kinachochipuka kwenye ngozi ya mwanadamu au mnyama. Kipele hichi kinaweza kusababishwa na mabadiliko ya mazingira, au aleji au magonjwa mbalimbali.

Hivyo Neno hili katika biblia linaonekana sehemu nyingi, hususani pale unapotajwa ugonjwa wa ukoma. Kwani ugonjwa huo kabla huujakolea kwenye mwili, huwa unaanza kwanza kama kipeleke kidogo king’aacho kekundu (ndio hicho kipaku). Hivyo katika hatua za awali ilikuwa ni ngumu kukitambua kama ni cha ukoma au cha ugonjwa mwingine wa kawaida. Hivyo ili kuepusha maambukizi zaidi kwa wengine, Mgonjwa Yule alitengwa kwa muda wa siku saba.

Na baada ya siku saba, kuhani huja na kuangalia, kama kipaku kile kimeenea zaidi kwenye mwili na kuzama kwenye ngozi basi ulikuwa ni ugonjwa wa ukoma. Hivyo mtu huyo alitengwa daima, kama hakutakasika.

Walawi 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,

2 Mtu atakapokuwa na kivimbe katika ngozi ya mwili wake, au kikoko, au kipaku king’aacho, nalo likawa pigo la ukoma katika ngozi ya mwili wake, ndipo atakapoletwa kwa Haruni kuhani, au kwa wanawe, makuhani mmojawapo;

3 na huyo kuhani ataliangalia hilo pigo lililo katika ngozi ya mwili; na kwamba malaika yaliyo katika hilo pigo yamegeuka kuwa meupe, na hilo pigo kuonekana kwake limeingia ndani kuliko ile ngozi ya mwili wake, ni pigo la ukoma hilo; na kuhani atamwangalia na kusema kuwa yu mwenye unajisi.

4 Na hicho kipaku king’aacho, kwamba ni cheupe katika ngozi ya mwili wake, na kuonekana kwake si shimo la kuingia ndani kuliko ngozi, na malaika hayakugeuka kuwa meupe, ndipo kuhani atamweka mahali muda wa siku saba huyo aliye na hilo pigo;

5 kisha kuhani atamwangalia siku ya saba; naye akiona ya kuwa pigo limeshangaa, na pigo halikwendelea mbele katika ngozi yake, ndipo kuhani atamweka mahali muda wa siku saba tena;

6 kisha siku ya saba kuhani atamwangalia tena; na tazama, ikiwa hilo pigo limeanza kufifia, wala pigo halikwendelea mbele katika ngozi yake, ndipo kuhani atasema kuwa yu safi; ni kikoko; naye atazifua nguo zake, kisha atakuwa yu safi”.

Ni fundisho gani lipo nyuma ya pigo hili la ukoma?

Zamani za agano la kale ukoma uliwakilisha pigo kutoka kwa Mungu,. Na sikuzote Mungu kabla hajaleta mapigo hutanguliza kwanza ishara na dalili, Kama vile KIPAKU tu kidogo.. Lakini baada ya siku SABA, huenea mwili wote.

Kufunua nini?

Yesu alipokuwa duniani alisema tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia, akasema pia kabla ya ule mwisho wa dunia kufika ambapo Mungu ataleta mapigo makubwa sana juu ya ulimwengu huu wa dhambi..Zitatangulia kwanza dalili na ishara, ambazo yeye aliziita ‘mwanzo wa utungu’..Ndio haya matetemeko, majanga, magonjwa, tetesi za vita, n.k.  tuliyoyana tangu enzi za Bwana hadi sasa, (Ndio kipaku chenyewe rohoni, ila ukoma wenyewe kuenea bado).

Lakini aliruhusu kipindi cha neema cha NYAKATI SABA kipite kwanza, ili watu watengeneze mambo yao, watubu dhambi zao, Bwana awaepushe na uharibifu huo. Ndio hii miaka 2000, sasa ambapo ndani yake nyakati saba za kanisa zinapita, na sisi watu wa kizazi hiki ndio tupo katika kanisa la mwisho kabisa la saba, lijulikanalo kama LAODIKIA (Ufunuo 3:14-22).

Hivyo ni kama dalili za ukoma tu, mwisho wa siku saba, uhakika unapatikana. Na ndivyo ilivyosasa, hivi karibuni Unyakuo utapita, Bwana atawaondoa kwanza watu wake ulimwenguni.  Na baada ya hapo atatusha laana yake ya mwisho juu ya huu ulimwengu, ndio vile vitasa saba vinavyozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo 16.

Jiulize ndugu yangu, je huu ukoma ulioanza ndani yako, kama kipaku, je umeshaupatia tiba? Kumbuka tiba ni Bwana Yesu, usisubiri unyakuo ukupite, au ufe katika dhambi zako, mguekie Masihi akuoshe na kukusafisha.

Maandiko yanasema kipindi cha Elisha, kulikuwa na wakoma wengi, Israeli, lakini hakutumwa kwa mmojawapo wao, ila Naamani mtu wa shamu (Luka 4:27). Kwasababu gani? Kwasababu alikubali kutii maagizo aliyopewa na Elisha kwenda kujichovya mtoni mara saba..Leo hii watu hatutaki kusoma kitabu cha Ufunuo, ambapo ndani yake tutakutana na ujumbe wa makanisa saba na nyakati zao. Ambazo kwa kuzielewa hizo tutaweza kuepukana na ukoma huu wa rohoni ambao Mungu anawapiga watu sasa.. Badala yake tunapenda kusikia habari ya kutabiriwa, na mafanikio ya mwilini.. Hii ni hatari kwasababu tunaweza kujikuta tunaachwa katika unyakuo, kama sio kufa katika dhambi.

Bwana atusaidie tulipende Neno lake.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Je mke wa Musa alikuwa ni Mweusi?

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi nyumbani

Print this post

MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.

Yakobo 1:13 “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu”

Hapo Neno linasema kuwa Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, kinyume chake ni kweli kwamba yeye anajaribiwa na MEMA tu!. Maana yake tunapofanya mema hapo tunakuwa tunamweka Mungu kwenye jaribu la kutubariki.. Na hivyo ni lazima aachie baraka kwetu.

Lakini tukienda kinyume na Neno lake na huku tunataka atubariki, hapo maana yake tunamjaribu yeye kwa Maovu.. Mfano wa watu waliomjaribu Mungu kwa maovu ni Wana wa Israeli kipindi wapo jangwani, Walitaka Bwana awashushie chakula kile cha kimiujiza, huku mioyoni mwao wamemwacha Mungu, ni watu wenye viburi, ni watu wa kunung’unika, ni watu wasio na heshima wala staha kwa Mungu na mwishowe wakaangukia hukumu.

Waebrania 3:7 “Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake,

8  Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa,

9  Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini.

10  Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu;

11  Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu”.

Na maandiko yanasema Mungu ni yeye Yule jana na leo na hata milele, alilolikataza miaka elfu 2 iliyopita analitakata hata leo.. Akisema “yeye hajaribiwi na Movu, ni kweli hajaribiwi na hayo”.. Lakini kinyume chake anajaribiwa na Mema yaliyoandikwa katika Neno lake.

Kwamfano unapomtolea Mungu sadaka isiyo na kasoro (Maana yake iliyo sawasawa na Neno lake, na kwa nia njema) Hilo ni jaribu kwa Mungu kukubariki wewe, na hapo utakuwa umemjaribu kwa Mema.

Malaki 3:8 “Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu.

 9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.

 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi”.

Na mambo mengine yote mema, ambayo tunayafanya yaliyo sawasawa na Neno la Mungu, mambo hayo ni TANZI kwa Mungu, kutumwagia Baraka zake, au kuzungumza na sisi.

Lakini kama moyoni mwako umemwacha Bwana, halafu unatafuta kuisikia sauti yake, unaenda kwa nabii ili usikie Mungu anasema nini kuhusu wewe, hapo unamjaribu Mungu kwa mabaya na hivyo unajitafutia laana badala ya Baraka.

Ezekieli 14:4 “Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;

  5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao.

  6 Kwa sababu hiyo uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Rudini ninyi, mkageuke na kuviacha vinyago vyenu; mkageuze nyuso zenu zisielekee machukizo yenu yote. 

7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe

8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.”

Bwana Yesu atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

KWANINI MIMI?

Rudi nyumbani

Print this post

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Jibu: Tusome..

Walawi 22:21 “Na mtu awaye yote atakayemtolea BWANA dhabihu katika sadaka za amani, ili kuondoa nadhiri, au SADAKA YA MOYO WA KUPENDA, katika ng’ombe, au katika kondoo, atakuwa mkamilifu, apate kukubaliwa; pasiwe na kilema ndani yake cho chote”.

Sadaka ya Moyo wa kupenda, ni sadaka ambayo wana wa Israeli walimtolea Mungu wao wenyewe kwa kupenda (yaani pasipo kuagizwa wala masharti).

Zilikuwepo sadaka zilizokuwa na sababu, kwa mfano sadaka ya Shukrani, tayari sadaka hiyo inatolewa kwa lengo la kushukuru, kutokana na mambo fulani ambayo mtu kafanyiwa na Mungu.

Lakini sadaka ya Moyo wa kupenda, haikuwa na sababu yoyote nyuma yake… ni mtu tu anapenda  kumtolea Mungu kwasababu amependa tu kufanya hivyo..na wala si kwasababu Mungu kaagiza.

Mfano wa sadaka hiyo ni ile ambayo baadhi ya wana wa Israeli waliipeleka mbele za Bwana wakati wa ujenzi wa Maskani ya Bwana.

Wakati huo Mungu hakuwaagiza wana wa Israeli wachangie gharama za ujenzi huo wa maskani ya Mungu…lakini baadhi ya watu waliguswa na kumtafuta Musa na  kudhamiria kubeba gharama za  kazi hiyo kwa mapenzi yao wenyewe…

 Kutoka 35:29 “Wana wa Israeli WAKALETA SADAKA ZA KUMPA BWANA KWA MOYO WA KUPENDA; wote, waume kwa wake, AMBAO MIOYO YAO ILIWAFANYA KUWA WAPENDA KULETA KWA HIYO KAZI, ambayo BWANA aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa”.

Kutoka 35:21 “Wakaja kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza, na kila mtu ambaye roho yake ilimfanya kuwa apenda, nao wakaleta sadaka za kumpa BWANA, kwa kazi ya hema ya kukutania, na kwa utumishi wake, na kwa hayo mavazi matakatifu”.

Soma pia Kutoka 25:2 na 2Nyakati 29:31.

Swali ni je! katika Agano jipya bado tunazo sadaka kama hizi?..

Jibu ni Ndio! Bado Zipo na ndizo zinazompendeza Bwana, na tunazopaswa kutoa.

Utauliza katika agano jipya tunasoma wapi hayo…??.

2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu”.

Umeona sadaka ya Moyo wa kupenda ni sadaka Bwana anayoikubali.

Je na wewe unayo desturi ya kumtolea Bwana kwa moyo wa kupenda au kwa sababu tu ya shinikizo fulani?.

Kamwe usiache kumtolea Mungu, lakini katika kumtolea hakikisha unamtolea kwa Moyo.

Sadaka ya namna hii ni sadaka bora na inayompendeza Mungu

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI WATU WANAVYOIUNDA SANAMU YA NDAMA MIOYONI MWAO.

Mambo yaleyale waliyokuwa wanayafanya wana wa Israeli walipokuwa jangwani, yanafanywa sasa na wana wa Mungu. Ni vizuri tukafahamu asili ya ile ndani jinsi ilivyoundwa, ili tuelewe kwa undani, inavyoundwa sasa mioyoni mwa watu.

Maandiko yanatuonyesha, hawakuwa na rasilimali zozote za kuitengeneza, vilevile hawakuwa na urahisi wowote wa kuifanyia karamu yake, kwasababu pale palikuwa ni jangwani, hakuna namna wataweza kupika vyakula vizuri, pamoja na kupata pombe za kuifurahisha ibada yao.

Lakini cha ajabu ni kuwa, japokuwa changamoto hizo zilikuwepo, lakini vyote hivyo vilipatikana, na mambo yakaenda vizuri kabisa bila shida. Ndama akatengenezwa tena sio wa mawe bali wa dhahabu, vilevile Vinywaji vilipatikana(pombe zote) pamoja na vyakula vya kila namna? Na disco la miziki na vinanda juu vikawekwa.

Kutoka 32:2 “Haruni akawaambia, Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.  3 Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni.  4 Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; nao wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.  5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Haruni akatangaza akasema, Kesho itakuwa sikukuu kwa Bwana.  6 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze”.

Utajiuliza vilipatikanaje?

Hii ni kuthibitisha kuwa nafsi ya mtu ikidhamiria kutafuta jambo Fulani, ni lazima itapata tu haijalishi mazingira iliyopo.

Ndicho walichokifanya hawa.. Walipohitaji dhahabu, wakakumbuka kuwa wake zao, wanazo kwenye masikio yao, wanazo kwenye shingo zao.. Hivyo wakazitumia hizo hizo na kuzikusanya, zikawa nyingi, mno, wakampa Haruni akaziyeyusha na matokeo yake ikatokea ndama kubwa iliyong’aa sana.

Biblia haijatuambia pombe na vyakula vizuri walivitolea wapi, lakini ni wazi kuwa, waliagiza watu, waende nje ya jangwa kununua vyakula hivyo na pombe, katika miji ya kandokando huwenda muasisi alikuwa ni Kora au mwingine.. Au pengine wakatoa baadhi ya hizo dhahabu wakanunua. Lakini kwa vyovyote vile, na kwa njia yoyote ile, shughuli ilikamilika.

karamu ilikuwepo, watu walikula, walikunywa walisaza..na zaidi sana Sanamu yenye utukufu ilitengenezwa. Akili hizo hawakuwahi hata sikumoja kuzielekeza kwa Mungu wao aliyewaokoa kwa gharama kubwa sana kutoka kwa watesi wao wamisri, hawakuwahi kufikiria kumfanyia Mungu karama ya shukrani kama hiyo wale na wanywe mbele ya Yehova kwa matendo makuu aliyowatendea..

Hata kufikiria kutengeneza kibanda kidogo tu cha udongo kwa ajili ya Mungu wao kukutana nao, kuliko Musa kupanda huko milimani, na kutoweka muda mrefu,hawakuwahi kufikiri hivyo, wanakuwa wepesi kuwaza kuunda miungu ya dhahabu ambayo haijawahi kuwasaidia kwa chochote..Unadhani Kwa namna hiyo wangeachaje kumtia Mungu wivu?

Mambo kama haya yanaendelea sasa miongoni mwa wakristo..

Tukisikia harusi Fulani inafungwa, tunakuwa wepesi kubuni kila namna ya kuifanya ipendeze, tunaweza kutoa hata michango ya milioni moja, na kutengeneza kamati nzuri za maandalizi, tunatoa mapendekezo haya au yale, mpaka inatokea na kuvutia, hata kama ilikuwa ni ya bajeti ndogo lakini itafanikiwa tu mwisho wa siku..Lakini kwa Mungu aliyetukomboa, aliyetufia msalabani, ambaye kila siku anatupigania usiku na mchana, anatupa pumzi yake bure, hatuna muda naye..Zaidi tunaitazama nyumba yake, au kazi yake, tunaona kabisa ipo katika hali ya unyonge, lakini tunapita tu,kama vipofu, tunasema Mungu mwenyewe atatenda..

Tukiangalia tulivyovichangia katika mambo yasiyo ya msingi ni vingi kuliko tulivyovipeleka kwa Mungu. Ndugu tukiwa watu wa namna hii hapo tuwe na uhakika kuwa tumeunda sanamu za ndama nyingi, na tunaziabudu bila kujua. Na zimemtia sana Mungu wetu wivu sana.

Kukitokea party, au birthday, au tafrija Fulani, ni wepesi sana kuutikia, lakini kwa Mungu ni mpaka tukumbushwe kumbushwe, tuvutwe vutwe.. Hii inasikitisha sana.

Embu hii Ndama ya dhabahu tuivunje.. Hii miungu tuiondoe ndani yetu, mioyo yetu itusute.. Tumpe Mungu kipaumbele cha kwanza, kwasababu yeye ndio anayestahili kuliko hao wengine. Tusiwaone wale ni wajinga sana kuliko sisi. Huwenda wale wanao unafuu mkubwa zaidi ya sisi ambao tumeshaona mifano lakini tunarudia mambo yaleyale.

Tumpende Mungu, tuuthamini na wokovu wake, tuithamini pia na kazi yake.

EFATHA.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Baali alikuwa nani?

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Kusubu ni nini? Miungu ya kusubu ni ipi?

Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Rudi nyumbani

Print this post

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

Jibu: Tusome kuanzia ule wa 2 ili tuweze kuelewa vizuri.

Ayubu 24:2 “Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

3 Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.”.

Hapa Ayubu anazungumzia juu ya kundi la watu wabaya ambao wanawaonea Mayatima na kuwadhulumu wajane.

Ndio hapo anasema wapo (watu duniani) ambao.

1. Wanaondoa alama za Mipaka, na kuyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

Maana yake wanawadhulumu watu mashamba/ardhi kwa kuondoa mipaka iliyokuwepo na kuweka mipaka ya uongo!,..na baada ya kumiliki ardhi kwa dhuluma namna hiyo bado wanalisha mifugo yao juu ya hizo ardhi za dhuluma.

2. Humfukuza punda wake asiye baba,

Maana yake humfukuza Punda wa Yatima, (mtoto asiye na Baba). Punda wake anapoingia mahali kula vichache vilivyosalia katika  mashamba yao, wao humfukuza punda Yule, pasipo kuzingatia kuwa Yule ni yatima asiye na uwezo wa kujimudu mwenyewe, asiye na uwezo wa kununulia chakula punda wake, lakini wao hawajali hayo yote, bali wanazifukuza punda zake.

3. Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.

Hawa watu pia wanachukua Ng’ombe za wanawake wajane, ambao wamefiwa na waume zao, na hata nguvu za kufanya kazi tena hawana!.. wanachukua Ng’ombe zao na kuwaweka Rehani, kutokana na mikopo wanawake hao waliyoichukua.. Jambo ambalo ambalo si jema machoni pa Mungu..Wangepaswa wawahurumie na kuwapa mikopo bila kuwawekea rehani chochote kwasababu wao hawana tumaini msaada wowote wapo wao kama wao, na umri wao umeshakwenda..

 Kumbukumbu 24:17 “Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani; 

18 bali kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika Misri, Bwana, Mungu wako, akakukomboa huko; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili”

Hivyo watu wa namna hii ambao wanawatesa Wajane na Mayatima, Bwana Mungu alitaja hukumu yao katika kitabu cha Kutoka 22:22

Kutoka 22: 22 “Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima.

 23 Ukiwatesa watu hao katika neno lo lote, nao wakanililia mimi, hakika yangu nitasikia kilio chao, 

24 na hasira yangu itawaka moto, nami nitawaua ninyi kwa upanga; na wake wenu watakuwa wajane, na watoto wenu mayatima”.

Hivyo na sisi hatuna budi kuwatendea Mema watu hawa, na kuwapenda ili na Bwana atubariki

Shalom

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mtu asiye na akili ni nani kibiblia?

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NA TAA YA MUNGU ILIKUWA BADO HAIJAZIMIKA

Jina la Bwana na Mwokozi, Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo lihimidiwe!..karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu.

Upo wakati ambao TAA ya Mungu itazima!.. Tuitikie wito wa Mungu, kabla ya huo wakati kufika..

1Samweli 3:2 “Ikawa wakati huo, Eli alipokuwa amelala mahali pake (tena macho yake yalikuwa yameanza kupofuka, hata asiweze kuona), 

3 NA TAA YA MUNGU ILIKUWA HAIJAZIMIKA BADO, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu la Bwana, palipokuwa na sanduku la Mungu;

 4 basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.”

Sasa ili kuelewa vizuri Taa ya Mungu ni kitu gani, na ilikuwa inazimika wakati gani..hebu turejee ile Hema ambayo Musa aliagizwa aitengeneze, tunasoma Ilikuwa imegawanyika katika Sehemu kuu tatu, Ua wa Ndani, Patakatifu na Patakatifu pa patakatifu.

Na ndani katika Patakatifu, palikuwa na madhabahu ya uvumba, Meza ya mikate ya wonyesho pamoja na KINARA CHA TAA, ambacho kilikuwa na Mirija saba. (Tazama picha juu).

Hiki kinara cha Taa kazi yake ilikuwa ni kutia Nuru ile hema wakati wa USIKU. Kwamba Nyakati zote za usiku ni sharti ndani ya Hema kuwe na Nuru, na amri hiyo ilikuwa ni ya Daima, maana yake ya kila siku!.. haikupaswa hata Usiku mmoja upite bila Kinara hicho kuwashwa ndani ya Hema.

Kutoka 27: 20 “Nawe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima. 

21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE YA BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israel”

Tusome tena..

Walawi 24:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 

2 Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima. 

3 Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza TANGU JIONI HATA ASUBUHI MBELE ZA BWANA DAIMA; ni amri ya milele katika vizazi vyenu”

Hapo mstari wa 3, unasema ataitengeneza “tangu jioni hata asubuhi” maana yake wataiwasha tangu jioni mpaka asubuhi, na kukiisha pambazuka basi taa ile inazimwa, kwasababu kulikuwa na Nuru ya mwanga wa Nje wa jua iliyokuwa inaingia ndani ya Hema.

Sasa tukirudi katika habari hiyo ya Samweli,  maandiko yanasema Samweli alikuwa analala katika Hema karibu na sanduku la BWANA, na wakati ambapo Taa ya Mungu bado haijazimika..Maana yake bado hakujapambazuka, (kwasababu kukisha pambazuka tu, tayari ile taa ilikuwa inazimwa).

Wakati huo ndipo Samweli aliisikia Sauti ya Mungu ikimwita mara 4, na Samweli akaitikia wito wa Mungu.

Lakini ni nini tunajifunza katika hiyo habari?

Upo wakati ambao sauti ya Mungu inaita juu ya Mtu..na wakati huo ni wakati wa giza Nene juu ya maisha ya mtu.. Huo ndio wakati ambapo Mungu anamwita mtu, na anamwita kwa sauti ambayo inakuwa inayofanana na ya watu wa Mungu.. kiasi kwamba mtu anaweza kudhani ni mtu anayemwita/kumshawishi kumbe ni Mungu, ndio maana Samweli alipoitwa alikimbilia kwa Eli akidhani ni Eli anayemwita kumbe ni MUNGU.

Vile vile Mungu anawaita leo watu kutoka katika dhambi, na uvuguvugu lakini watu wanadhani ni wachungaji wao ndio wanaowaita, wengine wanadhani ni wahubiri ndio wanaowatafuta wawe washirika wao, pasipo kujua kuwa ni sauti ya Mungu ndio inayowaita na si watu.

Sasa endapo Samweli asingeitikia ule wito wakati ule ambapo TAA BADO HAIJAZIMIKA, huenda ile sauti ya Mungu asingeisikia tena kwa wakati ule mpaka labda kipindi kingine ambapo Taa hiyo itakuwa inawaka.

Ndugu TAA ya Mungu leo ni NEEMA,  Hii Neema kuna wakati itasimama!, na hakutakuwa tena na nafasi ya kumkaribia Mungu, wakati ambao unyakuo wa kanisa utapita, ndio wakati ambao TAA itakuwa imezima, vile vile wakati ambao utaondoka katika haya maisha huo ndio wakati ambao Taa ya Mungu itakuwa imezimika juu yako.

Je umemkabidhi Yesu maisha yako?.. Umebatizwa katika ubatizo sahihi? Umeokoka?.. Kama bado ni vyema ukafanya hivyo sasa kabla Taa haijazimika.

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

Maran atha!

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

NYAKATI AMBAZO NI LAZIMA TUKUTANE NAZO TU:

Rudi nyumbani

Print this post

Thenashara ni nini? (Marko3:16)

Thenashara ni neno la kiebrania linalomaanisha namba “kumi na mbili” (12). Kwahiyo badala ya kusema watu 12, ni sahihi kabisa kusema “watu Thenashara”, au badala ya kusema “miezi 12” ni sahihi kusema “miezi Thenashara”…badala ya kusema makabila 12 ni sawa na kusema “Makabila thenashara” n.k

Biblia imelitumia Neno hilo Thenashara kuwakilisha wale Wanafunzi 12 wa Bwana Yesu, ambao baadaye waliitwa Mitume.

Marko 3:16  “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17  na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;

18  na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,

19  na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani”

Na ni kwanini wanafunzi hawa 12, watenganishwe kwa kuitwa hivyo Thenashara?.. Ni kwasababu Bwana Yesu alikuwa anao wanafunzi wengine wengi zaidi ya 70,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.”

 hivyo ili kuwatofautisha hawa wanafunzi 70 na wale 12 aliowateua kwanza kndio likatumika hilo neno “Thenashara”

Unaweza kulisoma neno hilo pia katika Mathayo 26:14-16, Marko 4:10, Marko 9:35, na Yohana 20:24

Je umefanyika kuwa Mwanafunzi wa Yesu? kwa kutubu dhambi zako zote, na kumaanisha kuziacha na vile vile kuchukua msalaba wako na kumfuata yeye?

Luka 14:27  “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Wahuni ni watu gani katika biblia?

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

Hesabu 11:6 “lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu”

Nakusalimu  katika jina lenye uweza la YESU KRISTO mwokozi wetu. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuifikia hivyo, nakukaribisha tuyatafakari pamoja maneno yake.

Wana wa Israeli walipofika jangwani hawakujua kuwa watalishwa chakula cha aina moja tu, Mwanzoni waliifurahia ile mana, jinsi ilivyokuwa nzuri na tamu, lakini siku zilivyozidi kwenda, hamu ya mana ile ikaanza kupungua ndani yao, wakaanza kutamani na vyakula vingine..Walipoona asubuhi kifungua kinywa ni mana, mchana ni mana, chakula cha jioni ni mana.. wakasema haya mambo yataendelea mpaka lini?..wakaikinai, Wakaanza kufikiria ni wapi watapata chakula cha aina nyingine walau wabadili ladha. Ni wapi watapata nyama, watapata kuku, watapata pilau, na pizza, na Baga.

Hesabu 11:4 “Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule?  5 Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu;  6 lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu.  7 Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtama na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola”

Wana wa Israeli wakasau kuwa vyakula hivyo ndivyo vilivyokuwa vinawaletea magonjwa makali kule Misri, ndivyo vilivyokuwa vinafubaza miili yao. Tofauti na mana, ambayo walipoila hawakuumwa, wala kudhoofika maandiko yanasema hivyo (Kumbukumbu 8:3-4), japokuwa kilikuwa ni chakula cha aina moja tu, lakini ni salama.. Wao  wakaidharau.

Ndugu yangu Mana inafananishwa na “Neno la Mungu”. Tunapookoka, tujue kuwa tutapewa chakula cha aina moja tu, nacho ni Neno la Mungu [Hilo usiliondoe akilini].. tutaamka nalo, tutatembea nalo, tutalala nalo. Ndio chakula cha Roho zetu pekee, kitufaacho kwa wakati wote hakuna kingine..Hatutalishushia na jbo lingine lolote…Hatujapewa biblia, pamoja na kitabu cha saikolojia, kitufariji Hatujapewa biblia na vilabu vya mipira (FIFA) vituburudishe ,  tunalimeza hivyo hivyo, bila kugoshiwa.

Lakini kwasababu ya tamaa ya mambo ya ulimwengu na mengineyo. Inasikitisha kuona wakristo wengi tunavyolikinai Neno la Mungu kwa haraka sana.. Utakuta mwanzoni mwa wokovu wetu, tulikuwa tunapenda sana kusikiliza Neno, tupo tayari kushinda muda wote kusikiliza mahubiri na mafundisho, tulikuwa tupo tayari kusoma mstari baada ya mstari, , kitabu baada ya kitabu, kudumu muda mrefu kwenye Neno la Mungu.Tukielezwa  habari za mambo mengine, tuliona kama ni takataka..

Lakini ulipofika wakati tumekula tumeshiba, tunaona sasa kama hivyo vingine vya nje vinatupita.. Tunapoona biblia ni ile ile, haina matoleo mapya, maagizo ni yaleyale, yanayotutaka tuwe watakatifu na wenye imani, na tujiepushe na mambo ya ulimwengu huu.. Tunaona kama ni habari zile zile za kale za kujitesa.

Ndio hapo utamwona Mkristo anapoa  anaanza, kufuatilia na miziki ya kidunia, anaanza kuwa mshabiki wa mipira na thamthilia za kidunia, tena anazichambua kwa undani kama vile tu anavyochambua Biblia, ili tu aipe nafsi yake ladha nyingine..mwingine anachanganyia na miziki ya kidunia humo humo..Mpaka Neno la Mungu linakuwa sio chakula kikuu kwake, bali sehemu ya vyakula vyake. Kama wana wa Israeli walivyoifanya mana, kuwa sehemu mojawapo ya vyakula vyao..

Lakini viliwatokea puani, wakaanza kufa, na kupata mapigo mengi sana, kutoka kwa Mungu. (Soma Hesabu 11:33).

Ndugu tunapoamua kumfuata Kristo tusitegemee tutapewa chakula kingine zaidi ya NENO LAKE. Na kama tukilikinai mapema sana, hatutamaliza mwendo wetu salama. Si ajabu tunakutwa na majaribu mengi, na mapigo mengi, kwasababu tu ya tamaa ya mambo mengine zaidi ya Neno la Mungu.

Tukijifunza kuishi sawasawa na biblia,tuitegemee hiyo tu, hata kama tutakosa vingi, hatutafaidi na vingi vya ulimwengu huu, lakini roho zetu na nafsi zetu zipo salama. Hivyo tujifunze, kukifurahia chakula hiki hiki kimoja, Mungu anatambua kuwa hatutadhoofika, kinyume chake ndio tutaimarika na kubarikiwa.

Tuache kutanga tanga na tamaa..Tii kile biblia inasema, vingine tuwaachie mataifa, Ili tuweze kufanikiwa na kuishi maisha mema katika hii dunia Mungu aliyotuweka, ndani yake.

Kumbuka shetani alilijua hilo, ndio maana alipomjaribu Bwana kule jangwani, kwa kumletea vyakula vyake vya vigeni, wakati ananjaa. Yesu alimwambia, imeandikwa mtu hataishi kwa mkate bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu” (Mathayo 4:1-4).

Akamfukuza, na wewe usimvulie shetani na mambo yake maovu.

Bwana atusaidie.

Ubarikiwe daima.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia ni nini?

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Ni nani atakayeigeuza mioyo ya watoto iwaelekee mababa?

Wale mamajusi walikuwa ni wakina nani?

Rudi nyumbani

Print this post

Mtu akizaa watoto mia, lakini nafsi yake haikushiba mema;

SWALI: Naomba kujua Mstari huu unamaana gani?

Mhubiri 6:3 ‘Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;’


JIBU: Biblia inatuonyesha yapo makundi mawili ya watu   “Ambao wakiwa hapa duniani hawatapenda maisha yao hata kufa”

Kundi la kwanza:  Ni la watakatifu waliojikana nafsi, mfano wa hawa ni Ibrahimu ambaye ijapokuwa alikuwa ni tajiri, mwenye mali nyingi, lakini aliishi kama mpitaji hapa duniani, akaka katika mahema, akijua kuwa wenyewe wake ni kule mbinguni, hakufurahishwa na anasa zozote za ulimwengu huu kama Lutu.

Waebrania 11:9-10

[9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.

[10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.

Mfano wa hawa pia ni akina Musa, Yohana mbatizaji, pamoja na mitume na manabii wote tunaowasoma katika biblia..(Soma Waebrania 11:23-40 )

Hawa hawakuyafurahia maisha ya duniani, walijitesa nafsi zao, wasile raha yoyote ya duniani mpaka kufa kwao . Hivyo Wana heri kwasababu katika ulimwengu ujao walioungojea watatukuzwa sana na Kristo. Na sisi pia kama wana wa manabii na mitume tunapaswa tuwe kama hawa. Akili zetu na fikra zetu tuzielekeze katika ulimwengu ule na sio hapa.

Lakini kundi la Pili: Ndio kama hilo linalozungumziwa hapo..Ambalo pia linafanikishwa duniani, linapewa uzao mkubwa, watoto wengi, linajilimbikizia mali na heshima,…lakini halinufaiki na chochote katika vitu vyake, mpaka linakufa linakuwa bado halijaridhika. Huwenda linafanyakazi miaka yote usiku na mchana hadi uzeeni, na  kufanikiwa kuhifadhi fedha nyingi kwenye akaunti. Halafu linakufa bila kuonja chochote..tena linakosa maziko.

Sasa Mhubiri anasema ni heri mimba iliyoharibika..kuliko hao..kwasababu halijafaidi hapa duniani wala kule mbinguni halitaonja chochote..

Afadhali yule atuamiaye/ alaye akiba yake, hata kama hatakwenda popote lakini  jasho lake limemrudishia malipo kuliko hili, ambalo lilikuwa linasubiri siku moja lijifurahishe lakini hiyo siku haijafika.

Mstari huo unafanana na ule wa juu yake unaosema..

Mhubiri 6:2

[2]mtu aliyepewa na Mungu mali, ukwasi, na heshima, hata asipungukiwe na kitu cho chote kwa nafsi yake, katika yote anayoyatamani walakini Mungu hamwezeshi kula katika hizo; bali mgeni hula. Hayo ndiyo ubatili hasa, nayo ni ugonjwa mbaya.

Bwana atusaidie tuwe watu wa kujiwekea hazina mbinguni. Ikiwa umebarikiwa chochote ni vema ukiwekeze kwa Mungu, kubali kuwa kama mpitaji duniani, ili utajiri wako uwe ni kule na sio hapa. Bwana Yesu alisema hazina ya duniani hupotea, na haidumu lakini ile ya mbinguni hudumu milele.

 Kumbuka hazina inayozungumziwa hapa si ile ya kujitunzia akiba yako ya miezi mwili/mwaka mmoja mbele, kwa matumizi ya msingi hapana..lakini ni ile ya kujihakikishia maisha kana kwamba utaishi milele duniani, hiyo ndio inayozaa uchoyo, ubinafsi, na kutoridhika, na kuwa mtumwa wa mali  n.k. Hii, Ina hatari kubwa sana, sisi kama watakatifu kesho yetu yapaswa iwe mikononi mwa Mungu, sio katika akiba zetu, kama watu wa ulimwengu huu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

Rudi nyumbani

Print this post