KAFIRI NI NANI?
Kafiri ni Mtu yeyote asiyeamini IMANI fulani…kafiri Katika Biblia ni mtu yeyote asiyeuamini Ukristo, Ukafiri hauna tofauti sana na upagani, Mtu yeyote asiyemwamini Bwana Yesu Kristo kwamba alikuja, na kufa kwaajili ya dhambi za ulimwengu mtu huyo ni kafiri.
Mtu yeyote asiyeshika njia za Bwana Yesu Kristo na kumkana mtu huyo kafiri.
Yuda 1:14 “Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo”
Kwahiyo kafiri ni nani?…Jibu: Ni mtu yeyote asiyempenda Bwana YESU huyo ni kafiri, na tena Biblia inasema Amelaaniwa
2Wakorintho 16:22 “Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha”.
Kwahiyo mtu yeyote akitaka asiwe kafiri, ni sharti amkiri Yesu Kristo, na kumwamini, na kumpa Maisha yake na kudhamiria kuacha dhambi.
Na makafiri wote hawataurithi uzima wa milele. kwasababu hawajamwamini Mwana pekee wa Mungu (Yesu Kristo)
Yohana 3:18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu. 19 Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. 20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.
Yohana 3:18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.
20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.
Ubarikiwe sana.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MPAGANI NI NANI?
WAPUNGA PEPO NI WATU WA NAMNA GANI?
NINI MAANA YA KIPAIMARA?..NA JE! NI JAMBO LA KIMAANDIKO?
JE! MTU KUSIKIA SAUTI ZA WATU WALIO MBALI, KUNAWEZA TOKANA NA MUNGU?
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Tofauti na sisi wanadamu tulivyo, tukiunda kitu au tukiumba kitu Fulani ni kwa lengo moja tu ni ili kutusaidie sisi kufanya jambo fulani au kitunufaishe kwa namna moja au nyingine. Kwamfano mtu anaunda gari ni ili limsafirishe, anaunda meli ni ili imsaidie kutembea juu ya maji n.k. lakini kwa Mungu haiko hivyo yeye alituumba sisi kwa mapenzi yake/raha yake/furaha yake tu basi, (his pleasure).
Hakupungukiwa na kitu Fulani na hivyo akatuumba sisi ili kwa kupitia sisi akipate hapana, wengine wanasema Mungu alituumba ili tumwabudu, kusema hivyo sio sahihi , ukweli ni kwamba tunamwabudu Mungu kwasababu alituumba, lakini sio alituumba ili tumwabudu, Mungu hajaishiwa sifa biblia inasema vyote vinatoka kwake..(Zaburi 139)
Wakolosai 1:16 “Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake”.
Hivyo fahamu tu kuwepo kwako wewe duniani ni furaha yake, anafurahi kukuona wewe upo kama ulivyo, anafurahia kukuona unafanya mambo mazuri kama yeye anayoyafanya, anafurahia kukuona wewe unayo amani kama yeye aliyonayo, unayo furaha, unao upendo kama yeye alionao, ..hakukuumba ili akutese, au akutumikishe hapana..Lakini ni kwasababu amekupenda tu na ametaka wewe uwepo…
Ni kwa vile tu tulizama katika dhambi, tukajiharibia maisha wenyewe lakini mapenzi ya Mungu halisi yalikuwa ni milele tuishi ndani ya PENDO lake, lakini pamoja na hayo Pendo hilo limerejeshwa na YESU KRISTO, Kwa kupitia yeye huyo ndio tunaona ni jinsi gani alivyokuwa amtupenda tokea mwanzo….Jaribu kufikiria jinsi alivyomtuma mwanawe wa pekee, kutuokoa sisi tuliokuwa tumepotea, alichukua dhambi zetu, alichukua magonjwa yetu, alichukua masumbuko yetu…
Hata na wewe ukikaa ndani yake basi Pendo hilo nalo litakuja ndani yako..Nawe utamfarahia Mungu wako kama vile yeye anavyokufarahia, utampa sifa wa jinsi alivyokuumbwa kwa utashi wa hali ya juu namna hiyo, utamwabudu kwa uumbaji wake wote ulivyo mkuu, utamtukuza kwa jinsi anavyokulisha na kukupa riziki zako za kila siku..
Zaburi ZABURI 150 1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake. 2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. 3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi; 4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi; 5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana. 6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana.
Zaburi ZABURI 150
1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana.
Haleluya.
YESU NI NANI?
BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA.
JE! KUBET NI DHAMBI?
NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?
UNYAKUO.
JINSI EDENI ILIVYOKUWA.
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Kuna Roho inayofuatana na Majina, katika Maandiko tunaona watu wengi sana walibadilishwa majina yao, wengine wakati wa kuanza huduma au kabla ya kuanza huduma. Ibrahimu hapo kwanza aliitwa Abramu (Mwanzo 17:5), Sarai jina lake lilibadilishwa na kuitwa Sara, Yakobo jina lake lilibadilishwa na kuitwa ISRAELI. nk Kwahiyo ni Muhimu kujua maana ya majina kabla ya kumpa mtoto jina au kabla hujajipa jina.
Angalizo: Ukimpa Mtoto jina hata kama liwe zuri au lina tafsiri nzuri kiasi gani, kama mtoto huyo hatakuzwa katika malezi ya kumcha Mungu bado atakuwa mbaya tu, na akifa ataenda Jehanamu ya moto..
Kadhalika, mtoto anaweza akawa na jina lenye tafsiri isiyo njema, lakini kama atakuzwa katika Njia sahihi, hiyo haimzuii Mungu kumtumia, na jina lake kuwepo katika kitabu cha Uzima
Kwasababu majina yaliyopo katika kile kitabu cha uzima hayajaandikwa kulingana na tafsiri, bali kulingana na matendo!! Watakuwepo wengi wenye majina mazuri katika ziwa la Moto, na watakuwepo pia wengi wasio na majina mazuri Mbinguni Kwahiyo Jina pekee halimfanyi mtu au mtoto kuwa mzuri bali malezi pia ya kumcha Mungu….Na malezi sio tu kumpeleka kanisani kila jumapili, bali pia na kumfundisha Njia za Bwana kila siku hata akiwa nyumbani! huku mzazi ukionesha kielelezo cha kumcha Mungu.
Lakini yote katika yote ni vizuri kumpatia mtoto jina lililo zuri na lenye tafsiri bora!
Hili ndio jina lenye “nguvu” kuliko majina yote, hakuna lililo juu ya hili, kwa vizazi vyote mpaka mwisho wa dunia, halitakuwepo lililo kuu zaidi ya hili maana ya jina hilo ni YEHOVA MWOKOZI, Hivyo Yesu ndiye mwokozi wa Ulimwengu. (Tafadhali; Usimpe mwanao, wala usijipe mwenyewe hili jina, kwasababu ni jina tukufu la Mwana wa Mungu)
Maana yake ni “Yehova ni mwenye Neema”..Asili ya hili jina ni kiyahudi, Yohana Mbatizaji aliitwa hili jina pamoja na Yohana Mwanafunzi wa Yesu, ambaye ni ndugu yake Andrea.
Maana yake ni “Mlukania” Lukania ni mahali palipokuwa kusini mwa Italy..ambapo tafsiri yake haijajulikana mpaka leo.
Tafsiri yake ni “Zawadi ya YEHOVA” Asili yake ni lugha ya Kiebrania
Maana yake ni “Mnyenyekevu”
Maana yake ni “Yehova atapandisha au atanyanyua”..Asili ya jina hili ni lugha ya kiebrania.
Maana yake. Ni “Anayechukizwa au anayeonewa” asili yake ni lugha ya kiebrania.
Maana yake “Mungu amesikia” asili yake ni lugha ya kiebrania.
Tafsiri yake ni jiwe dogo, kama la kurusha, asili ya jina hili ni lugha ya kigiriki.
Maana ya Neema, ni upendeleo wa kipekee ambao mtu au kitu kinaweza kupata, upendeleo huo hauna chanzo/sababu maalumu. Mungu pekee ndiye anayetoa Neema.
Tafsiri yake ni “Aliye Imara, Thabiti” Asili ya jina hili ni lugha ya Kiebrania, katika Biblia alionekana Ethan mtu wa hekima katika Zaburi ya 89
Ivan na Yohana ni jina moja, isipokuwa kwa Ivan limewekwa kwa lugha ya kirusi ya sasa, lakini ni hilo hilo Yohana, ambalo tafsiri yake ni “Yehova ni mwenye Neema”
Jina Charles limetokana na neno la kijerumani “karl” lenye tafsiri ya “mwanamume”.
Jina Irene limetokana na neno la kigiriki “Eirene”…lenye maana ya “AMANI”
Jina Carolina au Caroline tafsiri yake ni “Mwanamke kwa kiingereza woman”. kwa jinsia ya kiume ni Carlos, au Charles
Jina Careen ni mchanganyiko wa majina mawili (CAROLINA na IREEN). Maana ya Irene ni “Amani”, na Caroline ni “Mwanamke”. Kwahiyo tafsiri yake ni “Mwanamke wa Amani”
JINA LAKO NI LA NANI?
JINA LA MUNGU NI LIPI?
USILITAJE BURE JINA LA BWANA!
Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?
KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?
[embedyt] https://www.youtube.com/embed?listType=playlist&list=PLIIhnDzXkeEcXSNPlq09Q5yonU3MOLI0h&v=DWFSX1GfuC8&layout=gallery[/embedyt]
Unaweza ukawa umezunguka huku na huko, umejaribu hiki na kile kwa bidii zako ili kuacha kuvuta sigara lakini imeshindikana, ni uwazi usiopingika kwamba vitu vyote vyenye addiction (yaani ulevi ndani yake) ni ngumu sana kuviacha, sio pombe, sio ugoro, sio bangi, sio madawa ya kulevya sio sigara, sio mirungi vyote hivyo kwa bidii za mtu binafsi ni ngumu leo anaweza akaacha kwa muda tu lakini kikipita kipindi Fulani kifupi ile hamu ikimzidia anarudia tena , Ni utumwa mgumu sana ambao kwa bidii za kibinadamu ni kama haiwezekani, ..Lakini nataka leo nikupe habari njema nazo ni hizi:
Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.(Yohana 8:36).
Mamia kwa mamia kama sio maelfu kwa maelfu ya watu duniani wanaacha kuvuta sigara, kwa kumruhusu tu YESU atende kazi maishani mwao. Sio tu kwa wavuta sigara bali pia hata na kwako wewe mnywaji pombe na mtumiaji wa ugoro na madawa ya kulevya, Kwasababu kwake yeye hakuna linaloshindikana, akikufungua habakishi hata chembe moja ndani yako, haijalishi wewe ni mtumwa wa hicho kitu kwa kiwango gani, hakuna utumwa ulio mkubwa zaidi ya utumwa wa DHAMBI lakini huo aliukomesha pale msalabani, si zaidi sigara ambayo ni kitawi kidogo sana cha dhambi yenyewe?.
Ikiwa umekusudia kweli na unataka kuacha leo basi, tiba ipo kwa YESU, Hatuhitaji kusema maneno mengi Unachopaswa kufanya ni kuanzia sasa umgeukie tu yeye..Utubu dhambi zako kwanza kwa kumaanisha kuziacha, na kisha yeye mwenyewe atakuvika huo uwezo wa kuacha kuvuta sigara, ataiondoa hiyo kiu ya sigara ndani yako moja kwa moja..Lakini Ikiwa tu umemaanisha kuwa kiumbe kipya. Kama upo tayari basi nataka ufuatishe sala hii, lakini tafuta kwanza mahali pa utulivu kisha fuatisha sala hii kwa IMANI..Kwasababu yeye yupo hapo hapo ulipo kukuhudumia hauhitaji mchungaji, au mhubiri aje kukuombea, wewe mwenyewe hapo ulipo anakusikia, kwasababu sio mchungaji anayekuponya au mhubiri bali ni yeye huyo YESU MWOKOZI ndiye anayekwenda kushughulika na shida yako…
Sema maneno haya kwa sauti:
EE! BWANA YESU, NAJA MBELE ZAKO, NINAJIJUA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NIMEKUKOSEA KWA MAMBO MENGI, NA MOJAWAPO NDIO HILI LA KULIHARIBU HEKALU LAKO KWA KULIVUTISHA SIGARA, LEO HII NINAJUTA NA NINATUBU MBELE ZAKO KWA KUMAANISHA KABISA KUWA SITAKI KUVUTA SIGARA TENA, NA NIMEMAANISHA KUACHANA NA MAISHA YA DHAMBI. NJOO NDANI YANGU BWANA YESU, UNIBADILISHE UNIFANYE KUWA UPYA NIFANANE NA WEWE, MIMI KWA NGUVU ZANGU NIMESHINDWA KUACHA SIGARA LAKINI WEWE ULISEMA KATIKA MATHAYO 11:28 KWAMBA TUJE KWAKO SISI WOTE TUNAOSUMBUKA NA KULEMEWA NA MIZIGO YA DHAMBI, NAWE UTATUPUMZISHA, NAWE UTATUPA RAHA NAFSINI MWETU NA LEO HII KWA UNYENYEKEVU WOTE NIMEKUJA KWAKO BWANA YESU ILI UNIFUNGUE KATIKA VIFUNGO HIVI VYA DHAMBI NA MAUTI. NINAKIRI KUWA WEWE NDIO BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NA KWAMBA ULIKUFA NA UKAFUFUKA, NA SASA UPO HAI KUNISIKIA, HIVYO KUANZIA LEO NAAHIDI KUKUTUMIKIA NA KUKUISHIA WEWE DAIMA.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE NA KUNIPONYA NA SHIDA YANGU YOTE AMEN.
Ikiwa umesali sala hii kwa imani, basi fahamu kuwa Mungu amekusikia na kukusamehe dhambi zako zote sio hiyo ya sigara tu bali na nyingine zote, , hivyo unachopaswa kufanya ni kutupa sigara zote ziweke mbali nawe wakati Bwana YESU anaendelea kushughulika na hiyo kiu ya sigara ndani yako, Hivyo hakikisha, unatafuta kanisa la kiroho, lililokaribu nawe ili kukusaidia kukua kiroho, au wasiliana nasi kwa namba hizi 0789001312 ikiwa utahitaji msaada wetu.
Bwana akubariki.
WEWE NI HEKALU LA MUNGU.
FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.
NI KWASABABU YA YESU KRISTO.
Ni Muhimu kufahamu kama Je kujipamba ni dhambi? au kujichubua ngozi ni dhambi? kama kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi na kama kupaka wanja ni dhambi?
Kiuhalisia Kujipamba kunahusisha kupaka rangi uso, kujichubua ngozi, kuchonga nyusi, kupaka lipstick, kupaka wanja, kupaka hina,kusuka nywele, kuvaa hereni, bangili, na mikufu, kuweka kucha za bandia, kuweka nywele za bandia (wigi), kujipulizia marashi makali.
Watu wengi hususani wanawake hawapendi kuambiwa ukweli, kutokana na kwamba wanahofia wataonekana wamepitwa na wakati. Lakini ukweli ni kwamba kujipamba ni DHAMBI, Tena ni dhambi ambayo inawapeleka wanawake wengi kuzimu, na wanaume baadhi wanaofanya hayo..
Katika Biblia kulikuwepo na mwanamke mmoja tu ambaye alikuwa anajipamba…Na huyo si mwingine zaidi ya mwanamke Yezebeli..
2Wafalme 9:30 “Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani”.
Mwanamke huyu biblia inasema alikuwa mchawi…na aliwakosesha sana wana wa Israeli na alimsumbua sana Nabii Eliya. Na alienda kuzimu! kwasababu anaonekana tena katika kitabu cha Ufunuo kutajwa kama Nabii wa Uongo, na Manaabii wa Uongo pamoja na wachawi, na waabudu sanamu wote biblia imesema sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Kasome (Ufunuo 2:20)
Na biblia inasema miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, hivyo hatuwezi kulifanya hekalu la Mungu kuwa nyumba inayofanana na nyumba za makahaba. Na Neno linasema mtu akiliharibu hekalu la Roho Mtakatifu, Mungu naye atamharibu mtu huyo.
1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”.
1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”.
Hivyo kujipamba kwa aina yoyote ile ni dhambi.. kusuka nywele ni dhambi, kujichubua ngozi ni dhambi, kuchonga nyusi ni dhambi, kupaka lipstick ni dhambi, kupaka wanja ni dhambi nk Mwanamke anapaswa ajiweke katika hali yake ya asili, kadhalika na wanamume pia..Ni wajibu wetu wote kujiweka safi na nadhifu, lakini si kuharibu uhalisia.
Mungu akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU SAWASAWA NA KUTOKA 20:5-6?
AMPOKEAYE NABII KWA KUWA NI NABII, ATAPATA THAWABU YA NABII; MSTARI HUU UNAMAANA GANI?.
SHETANI ANATOLEA WAPI FEDHA, ANGALI TUNAJUA FEDHA NA DHAHABU NI MALI YA BWANA?
ASKOFU MKUU NA MCHUNGAJI MKUU NI NANI?
WhatsApp
Tunasoma mara baada ya Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake wengine 70 wawili wawili wamtangulie kila mahali alipotaka kwenda, na kuwapa amri ya kufanya ishara zote alizokuwa anafanya yeye, walipotii na kwenda kuhubiri kwa furaha na kurudi kumpa Bwana ripoti ya mambo yote yaliyotendeka huko…Wao Hawakujua ni kitu gani Bwana Yesu alikuwa anaona huku nyuma, pengine wao kwa nje walikuwa wanaona ni jambo la kawaida tu, wanatimiza wajibu wao uwapasao kufanya, lakini Bwana Yesu aliwafumbulia alichokuwa anakiona aliwaambia maneno haya:
Luka 10:17 “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. 19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.
Luka 10:17 “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.
18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.
Unaona yaani kwa jinsi walivyokuwa wanalisambaza lile Neno la Mungu na kuiangaza nuru ya injili kila mahali, huku Nyuma shetani alikuwa anaanguka kwa kasi ya ajabu sana mfano wa Umeme/radi, hakuna kitu kinachosafiri kwa kasi zaidi ya umeme, hivyo hapo Bwana alipokuwa anasema nilimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme, alimaanisha ni anguko ambalo halikuwa na kipingamizi chochote kile (flawless). Leo hii shetani anaweza kuleta vipingamizi katika maombi, anaweza ukaomba lakini bado shetani akabakia pale pale ameshikilia..Lakini kwa pamoja tunapoamka na kwenda kuhubiri injili ya Kristo kila mahali, anajua hawezi kubaki pale pale, ni lazima aanguke tu, na ndio maana jambo kubwa ambalo shetani analipiga vita kuhubiri injili.
Kumbuka kibiblia mbinguni sio tu, kule Mungu alipo, mbinguni inaweza ikawa nafasi ya juu sana, ambayo kimsingi ndio inayompasa Mungu peke yake aikalie, lakini wanadamu au shetani wanaweza kutafuta nafasi hiyo kwa nguvu na kuketi hapo, na hivyo rohoni wakaonekana kama wamefika mbinguni. Soma Danieli 4:9-37, soma pia:
Isaya 14:13 “Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. 14Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. 15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. 16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; 17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? 18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;”
Isaya 14:13 “Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.
14Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.
15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.
16 Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme;
17 Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?
18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima, Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;”
Ikiwa wewe umeokoka na umekaa katika hali hiyo kwa miezi sasa, au miaka, na hutaki kuangaza nuru ya injili kwa wengine ili na wenyewe waokoke kama wewe, hutaki kuitumia karama Mungu aliyoiweka ndani yako kumtangaza yeye na huku unamwomba Mungu watu waokolewe nataka nikuambie shetani atendelea kuwatesa tu..Usitegemee kuwa shetani ataondoka kwenye jamii unayoishi, usitegemee huyo mkuu wa giza ataacha aliye katika eneo lako ataacha kuwapufusha watu macho wasiiamini Injili..Ataendelea sana kuziangusha roho za wengi…
Unadhani mapepo hayo yatadondoka kwa maombi tu?…Bwana Yesu hakuwaambia kauli ile walipotoka kusali, lakini aliwaambia kauli ile walipotoka kuhubiri..Vivyo hivyo na wewe, leo hii usipozaa matunda utafika wakati Bwana atakukata, unaposikia injili Mungu anatazamia na wengine waisikie hiyo hiyo uliyoisikia kwa kupitia wewe..Lakini kama wewe utakuwa ni kupokea tu hutaki kutoa ili na wengine waokolewe, wakati utafiki utakatwa.
Popote pale ulipo unaweza kuwahubiria wengine injili, iwe ni kazini, iwe ni shuleni, iwe ni mtaani, iwe ni nyumbani, iwe ni mitandaoni, iwe ni safarini, iwe barabarani..Kwa karama Mungu aliyokupa na mlango aliokufungulia itumie hiyo hiyo kumletea Kristo faida..Tukishirikiana kwa pamoja, hakuna nguvu yoyote ya shetani itakayoweza kuzuia watu wasimjue Mungu, yeye kazi yake itakuwa ni moja tu, kila sekunde ni kuanguka huko aliko kwa kasi ya umeme. Kuhubiri Injili ni moja ya zile silaha zilizotajwa katika..
Waefeso 6: 13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani” Unapowahubiria wengine wokovu, unammaliza shetani na upande wa pili.
Waefeso 6: 13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”
Unapowahubiria wengine wokovu, unammaliza shetani na upande wa pili.
Ni maombi yangu utafanya hivyo kuanzia huu wakati. Bwana akubariki…
TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.
ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:
INJILI YA MILELE.
Luka 14: 25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, 26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? 29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, 30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. 31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? 32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. 33 Basi, KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”
Luka 14: 25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,
26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?
29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.
31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.
33 Basi, KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”
Bwana Yesu alisema katika mstari wa 26 kuwa asiyemchukia Baba yake na Mama yake, mke wake, mwanawe, na ndugu zake wakiume na wake hawezi kuwa mwanafunzi wake..
Chuki inayozungumziwa hapo sio chuki ile ya dhambi, kwamba umchukie Baba yako au mama yako kwa nia ya kumdhuru, au kumdharau, au kumshushia heshima hapana! Bali chuki inayozungumziwa hapo ni “kuyachukia mapenzi yake ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu”…Baba anakuambia mwanangu tunapaswa tuende kwa waganga na wewe hali unajua kuwa hayo ni machukizo kwa Mungu, hapo unapaswa uyachukie hayo mapenzi ya Baba yako na kumwambia wazi kwa ujasiri kuwa “Baba mimi siwezi kwenda huko, kwasababu ni Mkristo, namwabudu Mungu aliye mbinguni”..
Mama yako anakwambia ukajiuze tupate pesa, wewe unatakiwa umwambie wazi kuwa “mimi siwezi kufanya hivyo kwasababu ni Mkristo”..Mume wako anakuambia ufanye mambo machafu ambayo ni machukizo kwa Mungu, na anakulazimisha, kutenda dhambi.. hapo unapaswa kumweleza wazi msimamo wako kwamba wewe ni Mkristo, na kama hataki kuishi na wewe, basi anayoruhusa ya kuondoka!…Biblia imeruhusu matengano Katika mazingira kama hayo (soma 1Wakorintho 7:15).
Kuna mtu mmoja alikuwa anazungumza na mimi anasema alikuwa ameokoka tu vizuri yeye na mchumba wake, tena walikuwa wamesimama ipasavyo katika imani, lakini siku ya kwenda kutambulishwa kwao, mama yake Yule mwanamume akamwambia kama hutaacha huo wokovu wako, mimi sio mama yako, na nitakuachia laana..Sasa Yule mwanamume kwa kuwa alikuwa anampenda mama yake zaidi ya Kristo, akaamua kuacha wokovu anakamshawishi na mke wake wote wakaucha wokovu, wakaanza kuwa watu wa ajabu, Yule mwanamume akawa mzinzi na mtu wa kidunia kishinda hata walipokuwa hapo mwanzo..Sasa watu wa namna hiyo Kristo anasema hawafai kwake, na aliposema hawafai alimaanisha kusema kweli hawafai..
Na jambo lingine Bwana alilolisema ni kwamba 33…KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”
Pia mtu asiyeacha vyote alivyonavyo…Maana ya kuacha vyote ulivyo navyo ni kuvitoa vile vitu ndani ya moyo wako…kila mtu anafahamu namna ya kukitoa kitu moyoni, hakuna haja ya kuelezea… “unapotoa kitu moyoni, unakuwa unakifuta ndani yako, kinakuwa sio kitu tena kinachokupa raha, kiwepo kisiwepo ni sawa tu” Wakati mwingine hiyo hali inaweza kuambatana na kuviacha vitu kwa nje kabisa wazi wazi…
Ulikuwa ni Tajiri unauacha utajiri wako unamfuata Yesu, maana yake…Hata mali zote zikipukutika katika safari yako ya kumfuata YESU hilo hujali, kwasababu hazipo tena moyoni mwako, Unamhisi Yesu moyoni kuliko utajiri ulionao…Na pia unakuwa humfuati Yesu ili akupe mali au azilinde mali zako, unamfuata kwasababu Moyoni mwako unaona una haja naye…Kuna upendo fulani ambao unamiminika ndani yako ambao hauwezi kuuelezea, Unajikuta tu unampenda tu Yesu bila sababu kama yeye anavyokupenda wewe bila sababu yoyote.
Kadhalika Ulikuwa ni MASKINI, unauacha Umaskini wako unamfuata YESU. Unauondoa umaskini moyoni mwako….Usimfuate Yesu kwasababu hauna gari! Au kwasababu umaskini unakutesa na kukuumiza… Hapo hujajikana nafsi ndugu! Usimfuate Yesu kwasababu unataka utajiri, au unataka heshima katika jamii, au kwasababu unataka kuwakomesha maadui..Unatakiwa Uuache umaskini wako ndipo unamfuata Yesu kiasi kwamba hata katika safari yako ya Imani, ukiongezekewa na kuwa Tajiri wa mambo ya kimwili, hilo kwako halina maana sana!…mali zikiongezeka ni kama vile moyoni mwako hakuna kilichoongezeka…lakini uhusiano wako na Yesu unapoimarika ndipo unajihisi uchangamfu wa Ajabu unakuvaa….Inafikia mahali umasikini na Utajiri kwako ni sawasawa tu! Kama Ayubu, ilifika wakati hata mali zilipoongezeka hakufurahia (Soma Ayubu 31:25)..
Wapo watu ni maskini lakini hata katika huo umaskini wao, hawajawahi kumwomba Mungu katika sala zao utajiri, wameridhika na wana amani ya Ajabu mioyoni mwao..wawe nacho wasiwe nacho, hilo kwao halijalishi maadamu wanaye Yesu, hilo kwao ndio linalojalisha, huo ndio utajiri mkubwa kwao. Hivyo ni lazima kabla ya kumfuata Yesu kuuacha umaskini! Na kumfuata yeye wewe kama wewe.
Na pia baada ya kuacha vyote namna hiyo, kitakachofuatia ni kuchukiwa, kutengwa, kuonekana umerukwa na Akili, kuonekana mjinga katika jamii na kuonekana hufai…Na hivyo pia unapaswa uwe navyo tayari! Bwana Yesu hakutuficha kabisa alituambia ili tukikutana nayo tusiseme mbona hivi mbona vile..Upige gharama kabisa kabla ya kuanza kujenga Mnara! Usije ukafika katikati ukashindwa kumalizia…
Ndivyo ilivyo kwa Bwana Yesu kabla ya kumfuata, piga hesabu kuwa kuna kuchekwa huko mbele, kuna kudharaulika, kuna kupungukiwa wakati mwingine hata kwa kipindi kirefu sana, wakati mwingine hata miaka kadhaa, hata miaka 5, au 10, hata 15, lakini haitadumu hivyo hata milele, kuna kutengwa na kuonekana mjinga, hata kwa miaka kadhaa…piga gharama zote hizo..Kama haupo tayari! Kuonekana mshamba kwa muda mrefu hivyo, au kuonekana mjinga kwa miaka kadhaa, au kudharaulika kwa miaka kadhaa, au kama haupo tayari kukosana na mama yako kuhusiana na Imani yako, au kukosana na Baba yako, au Watoto wako, au mke wako..kama unajua yatakushinda huko mbeleni…Biblia inasema tafuta sharti ya Amani mapema!…Usijiingize mahali ambapo hujajua yatakayokupata mbeleni, ukaja ukakutana na ambayo hukutegemea ukaanza kujuta na kulalamika.
Kwasababu Bwana Yesu anasema:
Luka 12: 51 “Je! Mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia, La, sivyo, bali mafarakano. 52 Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu kwa wawili, wawili kwa watatu. 53 Watafarakana baba na mwanawe, na mwana na babaye; mama na binti yake, na binti na mamaye; mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu”.
Luka 12: 51 “Je! Mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia, La, sivyo, bali mafarakano.
52 Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu kwa wawili, wawili kwa watatu.
53 Watafarakana baba na mwanawe, na mwana na babaye; mama na binti yake, na binti na mamaye; mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu”.
Je! Umejikana nafsi?..Umejitwika msalaba wako na kumfuata Yesu? Fahamu kubwa mtu yeyote anayeingia gharama kubwa kama hizo, Sio bure bure tu, Huyo anapelekwa katika viwango vya juu zaidi vya kuwa karibu na Kristo zaidi ya watu wengine wote, anafanyika kuwa mwanafunzi wake, na zaidi ya yote Bwana atakuja kumpa mara mia, na siku ile ataketi pamoja naye katika kiti chake cha enzi akiwahukumu mataifa..(Mathayo 19:27-30)
NJIA YA MSALABA.
BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?(MATHAYO 6:24)
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
JE? NI HATUA ZIPI MUHIMU ZA KUFUATA BAADA YA KUBATIZWA?
MTI WA MLOZI ALIOONYESHWA NABII YEREMIA 1:12 TAFSIRI YAKE NI NINI?
Hesabu 19:1 “Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
2 Hii ndiyo amri ya sheria Bwana aliyoagiza, akisema, Waambie wana wa Israeli wakuletee ng’ombe mke mwekundu asiye na kipaku, mkamilifu, ambaye hajatiwa nira bado;
3 nanyi mtamleta kwa Eleazari kuhani, naye atakwenda naye nje ya kambi, na mtu mmoja atamchinja mbele yake”;
Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
13 Naye amevikwa VAZI LILILOCHOVYWA KATIKA DAMU, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.”
WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.
AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.
SIKU YA TAABU YA YAKOBO.
NOTI YA UFALME WA MBINGUNI.
SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
Sasa Roho Mtakatifu anajua kabisa hatuwezi kumtumikia Mungu katika hali hiyo ya utumwa wa Kesho itakuwaje! Kwasababu hiyo basi ni lazima ampitishe katika kipindi fulani cha madarasa, kuipunguza hiyo hofu ndani ya Mtu ili aweze kuishi kwa furaha akiwa ndani ya Yesu.
Hebu fikiria mwanao, anakaa nyumbani mwako, halafu anakwenda shule huku anamashaka kwamba Kesho anaweza asipate chakula nyumbani, au akiwa na mashaka kwamba atakosa ada! Je! Huyo mtoto atasoma kweli, au atafanya vizuri darasani? Ni wazi kuwa hatasoma bali atakuwa ni mtu tu wa mawazo siku zote! Na itamsababishia kufeli, na hivyo hivyo Mawazo ya Maisha haya na mawazo ya Kesho itakuwaje! Itatusababishia tusimwelewe Mungu na kutusababisha tufeli mitihani mingi ya Maisha yetu ya kikristo.
Kulitatua hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake masomo kadhaa, ya kutohofia Kesho, na hivyo kwa masomo hayo pia anatufundisha na sisi…Embu tusome tukio hili moja..
Mathayo 16:5 “Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate. 6 Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo. 7 Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate. 8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate? 9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota? 10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nne, na makanda mangapi mliyoyaokota? 11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mkate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo. 12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mkate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo”
Mathayo 16:5 “Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate.
6 Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.
7 Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate.
8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate?
9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota?
10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nne, na makanda mangapi mliyoyaokota?
11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mkate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.
12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mkate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo”
Somo hilo Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi baada ya Wanafunzi wake kusahau kubeba mikate ya safari yao..Hivyo walipofika njiani, Bwana Yesu akawaambia wajihadhari na chachu ya mafarisayo, wenyewe wakadhani anawashutumu kwanini hawakubeba mikate katika safari yao..na hivyo hawana kitu cha kula, kwamba Bwana kawakataza wasile chachu ya mafarisayo…(kumbuka chachu ni hamira, na chachu ilikuwa inawekwa kwenye mikate, hivyo mtu akizungumzia chachu ilikuwa inajulikana kwamba anazungumzia mikate yenye Hamira)..
Hivyo wanafunzi wakahuzunika sana, kwasababu watakwenda kukaa na njaa bila chakula huko wanakokwenda…Lakini Bwana Yesu aliwakemea na kuwaambia wana Imani chache…kwasababu wameshasahau jinsi gani Bwana alifanya miujiza ya kutokeza maelfu ya mikate kutoka katika mitano tu na maelfu ya watu wakala na kusaza na kukusanya mabaki mengi tena mara mbili… kama Mungu aliweza kufanya hivyo huko nyuma kwanini asiwafanyie tena hivyo huko mnakokwenda?? Huo ndio ulikuwa ujumbe wa Bwana! Wasianze kutafakari tafakari Kesho wakula nini? Kesho kutwa watavaa nini…wao kazi yao ni kuangalia mbele kuitenda kazi ya Mungu na hayo mengine watazidishiwa…
Tunaona tena mahali pengine Bwana Yesu alizidi kulitilia mkazo jambo hilo katika Mathayo Mlango wa 6
Mathayo 6: 24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali. 25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi? 26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao? 27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja? 28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti 29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo. 30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? 31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”
Mathayo 6: 24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?
27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti
29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.
30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?
31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”
Unaona! Bwana anatufundisha ni jinsi gani, Kesho yetu ipo mikononi mwake, kwamba haijalishi leo sina chochote lakini Kesho nitakuwa na kitu..Bwana hawezi kutupungukia kabisa ikiwa tu tupo katika kusudi lake, anasema hivyo katika Neno lake (Waebrania 13:5), anajua tuna haja ya chakula, mavazi, malazi, makazi n.k lakini anachotutaka ni sisi kumtafuta kwanza yeye..Tusiwe na hofu ya Kesho..Kwasababu Hofu ni utumwa, hakuna mtu yeyote mwenye hofu, akapiga hatua yoyote mbele, hakuna.
Tatizo lililopo tunataka pindi tu tunapomkaribisha Yesu Maishani mwetu, basi atupe ratiba ya leo, Kesho na miaka mitano au kumi mbele itakuwaje! Tunataka tuone Kesho tutakuwa na shilingi ngapi mifukoni mwetu, uhakika wa kila kitu…Mungu si wakati wote anatenda kazi hivyo, wakati mwingine unaweza kukupitisha katika ukame leo, na huku hujui Kesho utakuwaje na ghafla ukashangaa kafungua mlango Kesho ukapata unayohitaji tena na zaidi ya matarajio yako…
Hivyo yeye anataka tu tumwamini kwamba hatatuacha kabisa! Anafahamu tunayohitaji!
Kama unafanya shughuli yoyote ambayo inakupatia kipato, na ikatokea ukapungukiwa kabisa, anatakiwa umwamini kuwa hajakuacha, na wala hana mpango wa kukuacha!..kumbuka wakati fulani nyuma ambapo ulipitia kupungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza…ukumbuke huo muujiza, na usikie sauti yake leo moyoni mwako ikikuambia…HUJAFAHAMU TU?..Haujafahamu bado?..Siku ile ulipopungukiwa na akakufungulia mlango kimiujiza?..Yatafakari matendo yake ya nyuma kisha Uinyanyue Imani yako kwake..na siku zote utaishi Maisha ya furaha na yasiyo na hofu, ukijua kuwa Baba yako wa Mbinguni, sio Baba wa kambo, ni Baba wa damu kabisa ambaye hapendi kuona utakufa njaa wala kuteseka.
Maombolezo 3:36 “Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa”.
Mada nyinginezo:
CHAKULA CHA ROHONI.
USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.
YAKUMBUKE YA NYUMA.
SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)
MUNGU WANGU,MBONA UMENIACHA?.
LAANA YA YERIKO.
Hii ni moja ya ndoto inayootwa na watu wengi, ikiwa na wewe ni mmojawapo na inajirudia rudia mara kwa mara basi fahamu kuwa lipo jambo ambalo Mungu anataka kukukumbusha, Sikuzote meno yanafanya kazi mbili kuu, ya kwanza ni kumeng’enya na ya pili ni kung’ata,..asilimia kubwa ya viumbe vyote vinatumia meno kwa kazi mojawapo ya hizo, isipokuwa tu mwanadamu inaongezeka nyingine hapo, ambayo ni kuzungumza, mtu usipokuwa na meno huwezi kuzungumza, atatoa sauti tu zisizoeleweka…
Vilevile Mtu Ukipoteza meno huwezi kula vitu vigumu, wala huwezi kung’ata kitu chochote Na ndio maana mtu unapoota meno yake aidha ya juu au ya chini au magego yanang’oka halafu ghafla ukashtuka saa hiyo hiyo na kujiona yupo salama huwa anashukuru kweli, anasema afadhali imekuwa ndoto, ni kwasababu unajua thamani iliyo katika meno yake.
Sasa ukiota meno yanatoka Hapo ni Mungu anakukumbusha, kuwa unakaribia kupoteza Meno yako ya rohoni, yenye thamani kubwa zaidi ya haya ya mwilini, ikiwa hujaokoka basi nakushauri utubu haraka sana, umegukie Mungu wako, kwasababu mara kikipotea hicho basi fahamu kuwa kitapotea milele…Ukishaondolewa uwezo wako wa kupambanua na kuyaelewa mambo ya rohoni basi hutakaa uwe nao tena, ukishaondolewa uwezo wako wa kung’ata maadui zako wa rohoni kwa meno makali Mungu aliyokupa basi fahamu utabakia hivyo milele, Vilevile Ukishaondolewa uwezo wa kuzungumza na Mungu wako rohoni basi ndio utabakia hivyo milele na milele hatakaa akuelewe wewe, hiyo inamaanisha hata ukiomba dua yao hawezi kukusikia…Na hiyo yote ni kwasababu ya dhambi zako unazozitenda sasa hivi.
Zaburi 58:3 “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo. 4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake. 5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi. 6 Ee Mungu, UYAVUNJE MENO YAO VINYWANI MWAO; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba. 7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu”.
Zaburi 58:3 “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.
4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.
5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.
6 Ee Mungu, UYAVUNJE MENO YAO VINYWANI MWAO; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.
7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu”.
Ndugu Usiipuuzie Injili ya msalaba hata kidogo, inapohubiriwa mbele zako, Mungu ameona jambo hilo kwako na hivyo anakuonya kwasababu anakupenda, mgeukie muumba wako, anza kuzingatia Neno lake kile anachokuambia tii na yeye mwenyewe atakuokoa na kukulinda na kukuongoza hadi unyakuo.
Aidha kama wewe tayari upo ndani ya Kristo, na unaota ndoto za namna hiyo hapo Mungu anakuonyesha pia ni jinsi gani unaelekea kupoteza ule uwezo wako wa thamani uliokuwa nao wa kupambanua mambo ya rohoni na ukali wako, hivyo simama imara kama ulikuwa umeshaanza kuyumba yumba, au kupoa simama imara ili usije ukabakia kuwa mbwa bubu tu asiyeweza hata kubweka rohoni (kukemea dhambi )kwa kukosa meno.
Isaya 56:10 “Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi. 11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. 12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi”.
Isaya 56:10 “Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi.
11 Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
12 Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa kama leo, Sikukuu kupita kiasi”.
Zingatia hayo na Bwana hakika atakuwa na wewe katika kila hatua moja unayopiga kwake…Hizi ni siku za mwisho na Unyakuo wa kanisa upo karibuni, tengeneza mambo yako.
Ubarikiwe.
KUOTA UNAENDESHA GARI.
KUOTA UPO UCHI.
KUOTA UNAFANYA MTIHANI.
JE! NI KWELI KUNA VIUMBE VINAVYOISHI SAYARI NYINGINE (ALIENS)?
UBATILI.