Kerubi au Makerubi ni Malaika wa Mungu,..Moja ya makundi ya malaika walioko mbinguni ambao kazi yao hasaa ni kuilinda enzi ya Mungu, na kumtukuza..Shetani naye alikuwa ni kerubi kabla hajaasi, lakini sasa sio kerubi tena,..
Ezekieli 28:14 “Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.
15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako.
16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto”.
Makerubi utaona wakitajwa katika kitabu cha Mwanzo mara baada ya Adamu na Hawa kufukuzwa katika bustani ya Edeni wakawekwa ili kuilinda njia ya mti wa Uzima wasiifikie (Mwanzo 3:24), Utaona pia Musa alipoagizwa atengeneze sanduku la Agano ndani ya Hema ya kukutania alipewa masharti afanye makerubi wawili juu ya sanduku lile ili kukifunika kiti cha rehema..(Kutoka 25:17-22), vile vile hata katika hekalu maagizo hayo yalitolewa.
2Nyakati 3:10 “Na ndani ya nyumba ya patakatifu pa patakatifu akafanyiza makerubi mawili ya kuchonga; wakayafunikiza kwa dhahabu.
11 Na mabawa ya makerubi hayo urefu wake ulikuwa mikono ishirini; bawa moja mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la pili.
12 Na bawa la kerubi la pili lilikuwa mikono mitano, likiufikilia ukuta wa nyumba; na bawa la pili mikono mitano, likishikana na bawa la kerubi la kwanza.
13 Yakaenea mabawa ya makerubi hayo mikono ishirini; yakasimama juu ya miguu yao, na nyuso zao ziliielekea nyumba”.
Tunawasoma pia katika kitabu cha Ezekieli makerubi ni malaika wenye sifa ya kuwa na mabawa manne, mawili walitumia kupaa, na mawili walitumia kufunika miili yao, na kila mmoja mwenye nyuso nne, (Ezekieli 10)..wanafananishwa na wale wenye uhai wanne tunaowasoma katika kitabu cha Ufunuo 4
Hivyo kwa ufupi makerubi na malaika wanaoonekana kuwa karibu sana na kiti cha enzi cha Mungu kuliko malaika wengine wote, wakimsifu na kuuhubiri ukuu wake usiku na mchana (Soma Ufunuo 4:6-9).
Nasi tunapokuwa katika hali ya kumsifu Mungu na kumwimbia kwa nguvu zetu zote, basi kundi hili la malaika linakuwa karibu sana na sisi, tufauti na tunaposali au kuhubiri.
Ubarikiwe.
Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba
+225693036618/ +225789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.
MALAIKA WA MAJI NI YUPI? NA JE KUNA MALAIKA WA AINA NGAPI?
JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?
About the author