Sisi tuliookolewa pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo, tunafananishwa na mti mmoja alioupanda Mungu mwenyewe ulimwenguni. Na wote tunayo sehemu katika mti huo, na tumewekewa wajibu wa kufanya.
Bwana wetu Yesu Kristo anafananishwa na shina la mti, halafu sisi tunafananishwa na matawi.
Shina ni kuanzia kwenye mizizi, hadi mahali matawi yanapotokea. Hivyo Bwana wetu Yesu, ndiye anayechukua uhai wetu moja kwa moja kutoka kwa Mungu na kutuletea sisi. Lakini sisi ni kuanzia kwenye matawi mpaka kwenye matunda.
Yohana 15:1-2,5
[1]Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. [2]Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa…. [5]Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
[1]Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
[2]Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa….
[5]Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
Sasa wengi wetu tunachoona katika mashina ni matunda tu peke yake. lakini leo ni vema tuone jambo hili kwa ndani. Kwa kawaida tawi huundwa na vitu viwili, cha kwanza ni majani, na cha pili ni matunda.
na vyote viwili vinapaswa vionekane katika shina.
Hivyo mimi na wewe kama watakatifu, ni lazima tujiulize je majani yapo? na je matunda yake pia yapo?
Matunda ni nini?
Tafsiri ya awali ya matunda kama ilivyozungumziwa kwenye mfano ya mti, sio kuwavua watu kwa Kristo, kama inavyodhaniwa, hapana bali ni Kutoa tunda la wokovu wako. Yaani tunda la toba.
Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho alilifafanua vema..Tusome.
Mathayo 3:7-10
[7]Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? [8]Basi zaeni matunda yapasayo toba; [9]wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. [10]Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
[7]Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
[8]Basi zaeni matunda yapasayo toba;
[9]wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
[10]Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Aliwaona mafarisayo ambao walikiri kwa ujasiri wao ni wajumbe wa Yehova, uzao wa Ibrahimu, lakini mioyoni mwao, maovu na machafu ya kila namna yamewajaa. Hivyo wakaonekana ni miti isiyo na matunda.
Matunda ndio yale yanayojulikana kama tunda la Roho, ambayo kila mwamini anapaswa afanye bidii kuyatoa moyoni mwake katika maisha yake yote ya wokovu, awapo hapa duniani. Ambayo ni;
Wagalatia 5:22
[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu [23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu
[23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Mtu yeyote anayefanya bidii kuonyesha wokovu wake kimatendo, mtu huyo humzalia Mungu matunda, ambayo ndio chakula cha Roho wa Mungu. Na hivyo hufurahishwa sana na sisi..
Lakini kama tulivyosema shina huundwa na majani pamoja na matunda. Sasa majani, ni utumishi ambao kila mmoja wetu amepewa wa kuwavuta wengine kwa Kristo, kwa karama aliyopewa ndani yake.
Tuliagizwa na Bwana tuenende ulimwenguni kote, tukahubiri injili na kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake (Mathayo 28:19),
Unapowashuhudia wengine, ni kwamba majani yako yanawaponya mataifa, na hivyo unawaokoa. Kumbuka majani kimsingi hayana ladha, mara nyingi hutumika kama tiba. Ndicho Bwana anachokifanya kwa wenye dhambi kupitia sisi, tunapowashuhudia.
Ufunuo wa Yohana 22:1-2
[1]Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, [2]katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na MAJANI YA MTI HUO NI YA KUWAPONYA MATAIFA.
[1]Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
[2]katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na MAJANI YA MTI HUO NI YA KUWAPONYA MATAIFA.
Umeona? Kumbe majani yake, ni lengo la kuwaponya mataifa, watu wasiomjua Mungu. Tujiulize je na sisi tunayaponya mataifa kwa kuhubiri injili?
Wewe kama mkristo uliyemshirika wa mti wa uzima huna budi kuwa mhubiri wa injili usikae tu, hivi hivi ukasema tayari nimeokolewa inatosha, fanya jambo kwa Bwana. Waeleze wengine habari za Yesu, waponywe. Usijidharau ukasema siwezi, kumbuka aitendaye kazi hiyo ni Kristo ndani yako, wewe ni tawi tu. washuhudie wengine.
Lakini si kuhubiri tu, halafu maisha yako yapo kinyume na Kristo, hapana hilo nalo ni hatari, ukiwa na majani tu, halafu huna matunda ya wokovu moyoni mwako..Utalaaniwa.
[13]Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. [14]Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.
[13]Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.
[14]Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.
Umeona hawa ni watu, wanaodhani kumtumikia Mungu tu yatosha hakuna haja ya kuishi maisha matakatifu. wanakutwa na majani tu peke yake.
Tuhakikishe tuna majani, lakini vilevile tuna matunda kwasababu sisi ni shina, ndani ya mti wa uzima. Na neema ya Mungu itatusaidia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Rudi Nyumbani
Print this post
Swali: Je kazi ya udalali ni dhambi, na Mkristo anaruhusiwa kuifanya?
Jibu: Dalali ni yule mtu anayeuza kitu kwa niaba ya mwingine na kisha kuchukia asilimia fulani ya faida ya kile kilichouzwa.
Au pia dalali anaweza kuwa mtu mwenye kutafuta soko la bidhaa ya mtu mwingine na kisha kuchukua asilimia ya faida inayopatikana.
Kama hiyo ndio maana au tafsiri ya udalali, basi mtu akiifanya “SI DHAMBI”, Kwani hata ununuaji wa bidhaa kiwandani na uuzaji masokoni kwa namna moja au nyingine ni “Udalali”, kwani utanunua kwa gharama ndogo na kuuza kwa gharama kubwa na kisha kuichukua ile faida….Hapo tayari umeshakuwa dalali wa wenye kuitengeneza ile bidhaa..
Kwahiyo udalali si dhambi ikiwa tu haujahusisha mambo yafuatayo.
1. UONGO.
Labda umepewa kazi ya kutafuta mteja wa bidhaa husika, halafu ukampata na kumwekea kiwango cha juu sana nje na mapatano na yule aliyekupa bidhaa (lengo la kufanya hivyo ni ili wewe upate faida kubwa na ya haraka)…
Au mteja amehitaji bidhaa au nyumba na wewe ukamlaghai kwa uongo na kumpa kitu ambacho kiko chini ya viwango na huku ukijua kabisa kuwa kitu hiko hakistahili hiyo gharama, Huo wote ni Uongo na udalali huo ni haramu.
2.Dhuluma.(Utapeli).
Unapomdhulumu mtu fedha au bidhaa yake, aidha kwa kumlipa kisasi au kwasababu nyigine yoyote udalali huo ni haramu.
3. Haifanyiki ndani ya nyumba ya Mungu..
Udalali unaofanyika ndani ya Nyumba ya MUNGU ni haramu..
Utaona Bwana YESU aliwafukuza wale madalali wote waliokuwa wanabadili fedha ndani ya nyumba ya MUNGU.
Yohana 2:15 “Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;”
Vivyo hivyo kanisani si sehemu ya minada, na udalali, ni sehemu ya Ibada takatifu ya roho na kweli.
Swali lingine je?…Fedha ya udalali inaweza kutolewa sadaka ikiwemo Zaka?.
Jibu ni Ndio!.. kama udalali huo haujahusisha mambo hayo hapo juu, basi inaweza kutolewa sadaka ikiwemo Zaka(yaani fungu la Kumi), na ikakubalika mbele za Mungu.
Na je mkristo anaweza kufanya kazi ya udalali??..
Jibu ni Ndio! Anaweza kufanya, ikiwa hatatumia Uongo, au dhuluma, au rushwa, au kufanya ndani ya kanisa la Mungu.
KAMA MHUBIRI USIWE MFANO WA DIOTREFE.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
TUZIJARIBU HIZI ROHO.
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE
WhatsApp
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo, Tukijua kuwa ule mwisho unakaribia, hatuna budi siku baada ya siku tujichunguze je! Tumekamilika vema? ili siku ile tusionekane na mawaa mbele zake. Tulipokee taji timilifu tuliloandaliwa mbinguni na mwokozi wetu Yesu Kristo kwa neema zake.
Leo, napenda tufahamu juu ya wimbo mpya. Kama wewe ni msomaji mzuri wa kitabu cha Ufunuo. Utagundua zimetajwa nyimbo kuu tatu.
Swali ni je! Hizi nyimbo ni zipi na zinatimiaje?
Wimbo wa Musa na wa mwanakondoo tunazisoma, katika Ufunuo 15:2-3
Ufunuo 15:2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu. 3 Nao WAUIMBA WIMBO WA MUSA, MTUMWA WA MUNGU, NA WIMBO WA MWANA-KONDOO, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa
Ufunuo 15:2 Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.
3 Nao WAUIMBA WIMBO WA MUSA, MTUMWA WA MUNGU, NA WIMBO WA MWANA-KONDOO, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa
Wimbo wa Musa, ni injili ya Musa, ambayo iliwafanya watu wa kale, kutembea katika hiyo ili wamkaribie Mungu, ndiyo ile torati, ambayo wale waliokuwa katika agano la Ibrahimu kwa uzao, walirithi neema hiyo. Hivyo wana wa Israeli wote walikuwa wanauimba wimbo wa Musa. Yoyote ambaye hakuwa hana wimbo huo, basi wokovu au kumkaribia Mungu hakukuwezekana kwake.
Lakini wimbo wa Musa haukuwa na ukamilifu wote kwasababu ulikuwa ni wa mwilini, na wa kutarajia ahadi ya mwokozi mbeleni. Hivyo Mungu akaleta wimbo mwingine mpya kwa wanadamu wote. Ndio huo wimbo wa mwana-kondoo.
Ambayo ni injili ya neema iliyoletwa na Bwana wetu Yesu Kristo na kuhubiriwa na mitume wake. Kwa ufupi sisi wote tuliomwamini Yesu Kristo katika agano hili jipya, kwa pamoja tunauimba wimbo wa mwana-kondoo. Ndio maana kiini cha imani, na wokovu wetu ni Yesu Kristo. Mtu yeyote ambaye hajaoshwa dhambi zake kwa damu ya Yesu, hawezi kumwona Mungu, wala kamwe hataweza kumwelewa, haijalishi ataonyesha bidii zake nyingi kiasi gani. Kwasababu ndio utimilifu wote.
Lakini upo wimbo mwingine wa Tatu ndio huo wimbo mpya.
Wimbo huu, si wote watakaoweza kuuimba, lakini watakaoweza kuuimba watakuwa karibu sana na mwana-kondoo (Yesu Kristo), baada ya maisha haya. Ndio wale washindao, Ndio wale Yesu aliosema atawakiri mbele ya Baba na malaika zake, ndio wale watakaoketi pamoja naye katika viti vya enzi, ndio wale watakaotoka mashariki, magharibi, kaskazini na kusini, kula mkate naye mezani pake. Na vigezo amevianisha pale. Anasema..
Ufunuo 14:1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao. 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao; 3 na KUIMBA WIMBO MPYA mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; WALA HAPANA MTU ALIYEWEZA KUJIFUNZA WIMBO ULE, ila wale mia na arobaini na nne elfu, WALIONUNULIWA KATIKA NCHI. 4 HAWA NDIO WASIOTIWA UNAJISI PAMOJA NA WANAWAKE, KWA MAANA NI BIKIRA. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 5 NA KATIKA VINYWA VYAO HAUKUONEKANA UONGO. MAANA HAWANA MAWAA
Ufunuo 14:1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni, kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi kuu. Na hiyo sauti niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi, wakivipiga vinubi vyao;
3 na KUIMBA WIMBO MPYA mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; WALA HAPANA MTU ALIYEWEZA KUJIFUNZA WIMBO ULE, ila wale mia na arobaini na nne elfu, WALIONUNULIWA KATIKA NCHI.
4 HAWA NDIO WASIOTIWA UNAJISI PAMOJA NA WANAWAKE, KWA MAANA NI BIKIRA. Hawa ndio wamfuatao Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
5 NA KATIKA VINYWA VYAO HAUKUONEKANA UONGO. MAANA HAWANA MAWAA
Kama tunavyoweza kuona hapo tabia za wale walioweza kuuimba wimbo huo ni mbili;
Hapo hamaanishi kuwa hawakuwa wazinzi, hapana, (ni kweli uzinzi sio jambo lao) bali anamaanisha hasaa uzinzi wa rohoni, yaani Kumwabudu Mungu pamoja na sanamu. Na sanamu kwa wakati wetu si tu vile vinyago vya kuchonga tu, bali pia ni kitu chochote kinachochukua nafasi ya Mungu wako moyoni. Wengine mali, wengine tv, wengine mipira, wengine elimu, wengine ma-magemu, wengine ushirikina, wengine udhehebu. Hizo ni sanamu, unapozidhibiti wewe kama mkristo hiyo ni hatua mojawapo ya kuweza kuuimba wimbo huo mpya.
Lakini anasema..
Ni watu walionena kweli yote ya Mungu (injili ya Kristo), wala hawakuibatilisha kwa ajili ya fedha, au maslahi, au cheo, au unafki au wafuasi. Bali waliitetea kweli yote ya Mungu na kuiishi pia, . Maana yake mimi na wewe tukiinena kweli ya Kristo na kuiishi, basi vinywani mwetu tunakuwa hatuna uongo.
Na matokeo ya mtu wa jinsi hii, ni kwamba anakuwa na nafasi maalumu sana mbinguni (Ufunuo 5:8-9), Ni sawa na leo unajisikiaje unapoitwa uishi ikulu na raisi wako? Unajisikiaje kila mahali aendapo na msafara wake wewe upo pamoja naye. Anapopokea heshimu, na wewe unapokea naye.
Hivyo bidii ina malipo. Nyakati tulizonazo sio kusema nimeokoka hiyo inatosha!.. Ni nyakati za kujifunza wimbo huu mpya kwa bidii. Kutijahidi kumpendeza Bwana. Na yeye mwenyewe ameahidi neema yake itatusaidia.
KARAMU YA MWANA-KONDOO.
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?
Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule(Kutoka 12:4)
Huu ni mwongozo wa maombi maalumu kwa ajili ya familia yako. Kama watakatifu, ni wajibu wetu kuziombea familia, Lakini sio kuziombea tu, bali kufahamu maeneo muhimu ya kugusia kwenye maombi hayo. Huu ni mwongozo maalumu wa maombi ya familia. Bofya juu ufungue chapisho hilo (pdf)
Pia Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
MISTARI YA KUOMBEA AMANI YA FAMILIA.
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
(Masomo maalumu kwaajili ya watumishi).
Kama Mhubiri au Mtumishi wa Mungu, usiupende ulimwengu wala usiikimbia sauti ya Mungu.
Bwana YESU alimwambia Petro maneno haya…
Luka 5:10 “na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, TANGU SASA UTAKUWA UKIVUA WATU”.
Hapa tunaona Bwana YESU anawafananisha “watu” na “samaki”…na “dunia” anaifananisha na “bahari”…
Tena anazidi kulithibitisha hili katika Mathayo 13:47- 49..
Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna; 48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa 49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,”
Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa
49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,”
Kama samaki wanawakilisha watu waliopo duniani, basi Injili ya BWANA YESU ndio NYAVU na Bwana amekusudia tuwavue watu (samaki) kutoka katika dunia, na si samaki watuvue sisi na kutushusha baharini. Maana yake samaki wanatakiwa watolewe kwenye maji, na si samaki watuvute sisi majini.
Utauliza je! MHUBIRI anaweza kuvuliwa na samaki?.. jibu ni NDIO!
Utakumbuka kisa cha YONA? Alipoikimbia sauti ya BWANA, ni nini kilitokea?, biblia inasema ALIMEZWA na samaki na akakaa tumboni mwa samaki siku tatu.
Yona 1:17 “Bwana akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku”
Vile vile, na mtumishi/mhubiri anayeikimbia sauti ya Mungu, kitakachofuata ni KUMEZWA NA WATU WA ULIMWENGU, (Mtu huyu anawekwa mikononi mwa watu wakuu wa ulimwengu) ambao hawana huruma, wenye nguvu kuliko yeye.
Tumbo la samaki ni vifungo vyote vya mateso vya watu wa kidunia,
Je wewe ni Mhubiri??…Isikie sauti ya Mungu, simama hubiri Neno la Mungu, usiende njia ya bahari (ya ulimwengu)…Ukienda njia ya ulimwengu ya bahari) iwe kwa lengo la kuhubiri sio kwa kufuata mambo yako, kwani bahari ina hatari nyingi.
Usiwe kama Nabii Yona ambaye aliikimbia sauti ya Mungu na kwenda njia ya bahari, na akapata ajali ile.
Bwana atusaidie sana.
UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?
Makasia ni nini? (Yona 1:13).
MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.
TWEKA MPAKA VILINDINI.
NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?
Jibu: Jibu la swali hili tutalipata katika ule mstari wa 22, sura ya 7 ya kitabu cha Mwanzo…
Mwanzo 7:22 “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu”.
Hapo yanatajwa mambo mawili,
1. Kila chenye roho ya uhai puani kikafa.
Kufuatia andiko hili, ni wazi kuwa samaki hawapumui kupitia pua kwasababu wao wapo chini ya maji..
2. Pia Kila kilichokuwako katika nchi kavu.
Kupitia maneno haya ni wazi kuwa gharika haikuwahusu viumbe wa majini au baharini, kwasababu hao hawaishi nchi kavu.
Vile vile hatusomi popote kuwa Nuhu aliingiza nyangumi, au kambale ndani ya safina, badala yake tunaona ni wanyama tu peke yao, na tena walimfuata Nuhu mwenyewe na wala Nuhu hakwenda kuwatafuta, sasa kwa mantiki hiyo nyangumi wangemfuataje Nuhu safinani?.
Kwahiyo ni wazi kuwa gharika ile ilihusu viumbe waliooishi nchi kavu, ambao ni wanadamu ndege, wanyama na wadudu.
Mwanzo 7:20 “Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano. 21 Wakafa wote wenye mwili waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu”
Mwanzo 7:20 “Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano.
21 Wakafa wote wenye mwili waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu”
Sasa kama ni hivyo, basi samaki walihifadhiwa wapi wakati wa gharika?
Jibu ni kwamba samaki waliendelea kubaki majini wakati wa gharika.
Lakini pamoja na hayo biblia inatabiri ujio wa gharika nyingine ambayo si ya maji tena bali ya moto, ambapo viumbe vyote vitafumuliwa na hakuna kitakachosalia..
2 Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia. 7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu. 8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja. 9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa”.
2 Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu.
8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa”.
Bwana atusaidie tukae katika mwenendo wa UTAKATIFU na UTAUWA.
Maran atha.
NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.
NUHU WA SASA.
KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?
Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri, turejee mistari hiyo (kuanzia ule mstari wa 16 -22).
Mathayo 23:16 “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga. 17 Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu? 18 Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga. 19 Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka? 20 Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake. 21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake. 22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.
Mathayo 23:16 “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.
17 Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?
18 Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.
19 Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?
20 Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.
21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.
22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.
Shabaha kubwa ya Bwana YESU hapo si kuhalalisha VIAPO, Kwamba ni halali Mtu kuapa kwa Hekalu au kwa maadhahabu!.. La! Hiyo haikuwa shabaha yake kwani tayari alishaonya kuhusu viapo katika Mathayo 5:33-37.
Mathayo 5:33 “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34 lakini mimi nawaambia, USIAPE KABISA; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; 35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu. 36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu”.
Mathayo 5:33 “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;
34 lakini mimi nawaambia, USIAPE KABISA; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;
35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.
36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu”.
Na Pia Mtume Yakobo akaliandika jambo hilo hilo katika Yakobo 5:12.
Kwahiyo lengo la Bwana YESU halikuwa kuhalalisha viapo, bali ni kuonyesha UOVU na UNAFIKI wa viongozi hao wa kiyahudi (Mafarisayo na Masadukayo na waandishi) kupitia viapo vyao!. Kwamba wanavipa nguvu viapo vya sadaka Zaidi ya viapo vya Hekalu ambalo ndani yake lina Mungu na sadaka pia…Lakini wenyewe wanatazama sadaka tu!.
Maana yake ni kwamba kama Mtu ameapa kutoa sadaka (dhahabu au kitu kingine chochote) basi amejifunga (maana yake ni lazima atimize kiapo chake hicho, na asipotimiza ni dhambi kubwa)..lakini kama ameapa tu kwa kwa hekalu (labda kuabudu siku hiyo hekaluni, na asiabudu), basi sio kosa kubwa sana!!..
Ila kwa upande wa dhahabu (sadaka), ni kosa kubwa! Pasipo kuona kuwa Hekalu/Madhabahu ni kuu kuliko sadaka! Kwamba aliyeapa kwa Hekalu kaapa jambo kubwa sana kuliko yule aliyeapa kwa sadaka (dhahabu) peke yake itolewayo Hekaluni… kwasababu ndani ya Hekalu ndiko kwenye taratibu zote za matoleo, na si ndani ya matoleo ndio kwenye Hekalu…Ila Mafarisayo walikuwa hawalioni hilo, na ndio maana Bwana YESU anawaita vipofu.
Na kwanini walikuwa wamevipa hadhi kubwa viapo vya sadaka kuliko vya Hekalu??… Hakuna sababu nyingine Zaidi ya kwamba walikuwa wanapenda fedha!!!, walijua ya kwamba wakiwabana watu katika matoleo basi watanufaika Zaidi, hivyo walijali matoleo kuliko Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu yake..
Na jambo hilo hilo utaona Bwana YESU alilirudia juu ya “vile vipasavyo kuwasaidia wazazi”..ambapo Mafarisayo walisema endapo mtu akipata chochote na kile anaweza kukifanya chote wakfu (yaani Korbani) na wala asiwape chochote wazazi, na isiwe dhambi!… jambo ambalo ni baya sana! (soma Marko 7:11).. na kwa maelezo marefu juu ya habari hiyo ya Korbani fungua hapa >>>>Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)
Mfano kamili wa baadhi ya viongozi wa kiimani wa leo??…. Utaona wanathamini Matoleo Zaidi ya Hekalu la Mungu na taratibu zake. Utaona mtu akiahidi kuja kanisani na asije, haiwi shida….lakini hebu mtu aahidi kutoa halafu asitoe!, inakuwa ni vita vikali na ni laana kubwa!…pasipo kujua kuwa nyumba ya Mungu ni kuu kuliko sadaka, kwasababu ndani ya nyumba ya Mungu kuna matoleo!.. (Na mtu akiiheshimu nyumba ya Mungu ataheshimu pia matoleo).
Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?
WEWE NI HEKALU LA MUNGU.
JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?
UJIO WA BWANA YESU.
CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.
Jibu: Turejee…
Wimbo 3:7 “Tazama, ni MACHELA yake Sulemani; Mashujaa sitini waizunguka, Wa mashujaa wa Israeli”
“Machela” yanayozungumziwa hapo si vile vitanda vinavyotumika zama hizi kwaajili ya kubebea wagonjwa walio mahutihuti!..Bali vilikuwa ni vitanda maalumu vilivyotumika kubebea Wafalme na Mamalkia enzi za zamani, walipotembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine (umbali mfupi).
Kutokana na zama kubadilika, matumizi ya Machela kubebea wakuu wa nchi hayapo tena, bali sasa yanatumika magari ya kimakenika, na Machela yamebaki kuwa na matumizi ya kubebea wagonjwa wa dharura walio katika hali ya umahutihuti,..na zaidi sana Machela za zama hizi yana magurudumu na hayabebwi tena kwa mikono kama yale ya zamani.
Kasoro moja ya Machela ya zama za zamani ambayo yaliwabeba wafalme ni kwamba hayakuwa na uimara wa kutosha, kiasi kwamba ikitokea ajali kwa waliombeba bali yule aliyebebwa anaweza kuanguka, na pia kwasababu mwendo wa wanadamu unatofuatiana, hivyo basi hata aliyebebwa wakati wa safari atahisi hali ya kupanda na kushuka, au kurushwa rushwa, na kupepesuka na hivyo yupo hatarini saa yoyote kuanguka..
Na vivyo hivyo, dunia imefananishwa na mfalme aliyebebwa kwenye machela, anawaya-waya, anapepesuka wakati wowote yupo hatarini kuanguka (yupo katika wasiwasi).
Isaya 24:19 “Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana. 20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, NAYO INAWAYA-WAYA KAMA MACHELA; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena. 21 Tena itakuwa katika siku hiyo, Bwana ataliadhibu jeshi la mahali palipo juu katika mahali palipo juu, na wafalme wa dunia katika dunia”
Isaya 24:19 “Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana.
20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, NAYO INAWAYA-WAYA KAMA MACHELA; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena.
21 Tena itakuwa katika siku hiyo, Bwana ataliadhibu jeshi la mahali palipo juu katika mahali palipo juu, na wafalme wa dunia katika dunia”
Kama dunia inawaya-waya, ya nini kuitumainia??.. Na kwanini inawaya-waya?..ni kwasababu imekaribia mwisho wake, wakati wowote inaisha…na kinachoifanya iwayewaye si kingine Zaidi ya Dhambi, iliyojaa ndani yake.
Kwa urefu zaidi kuhusu kuwaya-waya kwa dunia fungua hapa >>> Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.
Je umempokea YESU maishani mwako?..au na wewe unawaya-waya na dunia?…anasa zimekutawala, udunia umekushika..ni wakati sasa wa kuikimbia dunia na mambo yake na kumfanya BWANA YESU kuwa msingi wa maisha yako.
TOA HUDUMA ILIYO BORA.
Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?
KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.
Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.
SWALI: Naomba kufahamu tafsiri ya Yakobo 1:13-17, hususani pale anaposema “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu”
Yakobo 1:13-17,
[13]Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. [14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. [15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. [16]Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. [17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
[13]Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
[15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
[16]Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike.
[17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
JIBU: Katika hiyo mistari ya juu kabisa, tunasoma mtume Yakobo akitoa ufafanuzi wa mawazo ya watu kuhusu Mungu ambayo sio sahihi. Wakidhani kuwa majaribu yampatayo mtu hutolewa na Mungu, kwasababu chanzo chake ni Mungu.
Chukulia mfano labda mpendwa kabarikiwa na Mungu kwa shamba la mizabibu, likawa linasitawi sana, hata kumfanya afungue kiwanda chake cha juisi na kuuza na kupata faida nyingi..Sasa baada muda fulani watu wakamfuata na kuulizia bidhaa ya mvinyo, mwanzoni alikataa, lakini baadaye alipopiga hesabu na kuona faida itakuja mara nne,.akaingiwa na tamaa akaanza kutengeneza divai akauza na yeye mwenyewe akaanza kuwa mlevi, hatimaye maisha yake ya wokovu yakaporomoka akawa amekufa kabisa kiroho. Mwishowe akaanza kumlaumu Mungu amemletea jaribu la kumpa shamba la mzabibu na kumbariki sana, ndio maana akawa mlevu. Sasa mtu wa jinsi hii Mtume Yakobo anasema asiseme amejaribiwa na Mungu.
Ni sawa na tamaa za mwili,.Mungu aliziweka mahususi kwa ajili ya furaha ya wanandoa lakini imebadilika na kuwa uzinzi, na watu hutumia kisingizio kuwa Mungu ameziweka kama jaribu kwao. kumbe Mungu alichowapa ni chema isipokuwa wao wenyewe wamekigeuza kuwa uovu.
ndo maana sasa ya vifungu vinavyofuata vinasema. “kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu. Kwa lugha rahisi anamaanisha chochote kitolewacho kilicho chema hutoka kwa Mungu, lakini tu sio kilicho chema bali pia chochote kilicho kikamilifu, hutoka juu kwa Baba yetu.
Mungu sikuzote hutupa sisi vitu vizuri. Na si vizuri tu bali pia vilivyo vikamilifu hutoka kwake. tujengwe na tufurahie, isipokuwa sisi huvipindua na kuvitumia kwa tamaa zetu.
Pesa ni kitu kizuri, chakula ni kitu kizuri, usingizi ni kitu kizuri, ndoa ni kitu kizuri, kazi ni kitu kizuri, muziki ni kitu chema.
Lakini watu wanapovitumia kinyume ndio huzaa uzinzi, anasa, ulevi, uvivu, ufisadi.n.k.
Vitu vyote vyema vimetoka kwa Mungu na hajatupa ili kutujaribu..anaendelea kusema..
“hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.
Baba wa mianga, akijifananisha na jua ambalo huangaza kotekote, isipokuwa yeye amelizidi jua, hana misimu wala majira ya kuangaza, yeye wakati wote hutoa vilivyo vyema, hifadhili majira yote kwa watu wake.
Hata leo, uonapo Mungu amekupa kitu chema, halafu baadaye kikakuletea matatizo makubwa.. Tafakari hapo kuna mahali ulimpa nafasi shetani kukujaribu. Kwasababu Mungu hawezi kumpa mtu jiwe aliyemwomba mkate.
“kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu.
Ubarikiwe.
YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.
EPUKA KUTOA UDHURU.
SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.
Jibu: Turejee..
1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu. 4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake. 5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, YUAAIBISHA KICHWA CHAKE; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa”.
1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.
4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.
5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, YUAAIBISHA KICHWA CHAKE; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa”.
Kuhusiana na maelezo marefu juu ya agizo la wanawake kufunika vichwa wawapo ibadani fungua hapa >>>Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?
Lakini matokeo ya Mwanamke kutofunika kichwa awapo ibadani ni “kuabisha kichwa chake”. Na kichwa kinachozungumziwa hapo (kinachoaibika) si kile chenye nywele bali ni kile cha “UONGOZI”
Kwahiyo mwanamke asipofunika kichwa chake awapo ibadani, kulingana na biblia anaaibisha Uongozi aliowekwa chini yake na Roho Mtakatifu!, Na uongozi huo si mwingine Zaidi ya ule wa zile huduma tano zinazotajwa katika Waefeso 4:11 (Mitume, Manabii, Waalimu, Wachungaji, na wainjilisti)…ambazo ni huduma za wanaume tu!. (Kumbuka tena, si agizo la biblia mwanamke kuwa mchungaji!, rejea Zaidi 1Wakorintho 14:34, na 1Timotheo 2:11-12.
Na matokeo ya kuuabisha huo uongozi wa Roho Mtakatifu ni kumwaibisha KRISTO mwenyewe kwasababu pia Kichwa cha kila mwanaume (yaani uongozi wa kila mwanaume anayemtumikia Mungu) ni KRISTO (sawasawa na hiyo 1Wakorintho 11:3). Hivyo mwanamke ni lazima afunike kichwa chake awapo ibadani, kama dalili ya kuongozwa (kumilikiwa).
Sasa swali lingine ni hili, Je Mwanaume naye anapaswa afunike ili asimwaibishe Kristo?…Jibu ni la!.. Mwanaume hapaswi kufunika kichwa awapo kanisani, Kwasababu yeye ni mfano wa Utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa Mwanaume..
1Wakorintho 11:7 “Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume”.
Anaposema mfano wa Utukufu wa Mungu, maana yake “yeye anasimama kumwakilisha KRISTO” amepewa hiyo nafasi ya kuwa mwakilishi wa KRISTO kwa neema, (Ingekuwa hajapewa hiyo nafasi, basi na yeye pia ingempasa afunike kichwa) lakini kwasababu kapewa nafasi ya kumwakilisha KRISTO, basi hapaswi kufunika kichwa, bali anapaswa awe kama KRISTO,
Maana yake kama Kristo alivyo Mchungaji, naye pia atakuwa mchungaji, kama Kristo alivyo mwalimu, naye pia atakuwa mwalimu, n.k. Lakini mwanamke hajapewa hiyo nafasi ya kumwakilisha KRISTO kwasababu hajaumbwa kwa mfano wa utukufu wa Mungu, bali kwa utukufu wa Mtu (mwanaume).
Kwahiyo kama wewe ni Mama, au dada, basi fuata agizo hilo la Bwana YESU wala usikubali kiburi cha kidunia kikuvae, kwa kufikiri hayo ni maagizo ya wanadamu au ni sheria ya torati..hiyo sio sheria bali ni agizo la Bwana tena lipo katika agano jipya.. na Zaidi sana Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho Mtakatifu alijua fitina zitazuka kushindana na agizo hilo siku za mwisho..
1Wakorintho 11:16 “Lakini mtu ye yote akitaka kuleta fitina, sisi hatuna desturi kama hiyo, wala makanisa ya Mungu”.
Bwana atusaidie.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
FUVU LA KICHWA.
LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.
Biblia inasemaje kuhusu Nywele?
MAJINA YA MANABII WANAWAKE