Category Archive Home

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

Haki ni Nini katika biblia. Haki ya Mungu ni ipi?

Haki maana yake ni kitu ambacho mtu anastahili kukipata. Kwamfano kuishi ni haki ya Kila mwanadamu, Hakuna mtu anayepaswa kumzuia mwingine kuishi, kisa ni mwanamke au ni mfupi, au ni kichaa, au mlemavu. Maadamu tu amekuwa mwanadamu tayari anayo haki ya kuishi.

Mfano mwingine wa haki, ni mtu aliyesoma  ukahitimu katika shahada Fulani labda tuseme ya utatibu, mtu kama huyo tunasema ana haki ya kuitwa daktari kwasababu amesomea jambo Hilo.

Vivyo hivyo katika Roho. Mungu naye anayo haki yake, katika kutoa vitu vyake.

Mwanzoni ilikuwa Ili kumkaribia Mungu na kupata kibali kwake na mema yote na baraka zote ilikupasa kwanza uishike Sheria yake yote. Hivyo yoyote aliyeweza kufanya hivyo alipatiwa haki hiyo. Soma Kumbukumbu 28

Lakini Kwa bahati mbaya hakukuwa na mtu aliyestahili kumkaribia Mungu kwasababu Hakuna mwanadamu aliyekwenda katika maagizo yote ya Mungu Kwa ukamilifu wote, bila kosa. Kwahiyo tangu zamani hakukuwa na mwanadamu hata mmoja aliyefanikiwa kumkaribia Mungu. Wote walitenda dhambi (Zaburi 14:3)

Hivyo Mungu akabuni mpango mwingine wa kumwokoa mwanadamu ili awe amestahili kupokea mambo yote ya rohoni ya Mungu, ikiwemo uzima wa milele na kumkaribia yeye.

Ndipo akamleta Yesu duniani, Ili Kila amwaminiye asipotee Bali apokee kuhesabiwa haki bure, bila kutegemea Tena matendo ya Sheria. Kwasababu Kwa matendo ya Sheria hakukuonekana aliyestahili.

Hivyo Mimi na wewe tunapomwamini Kristo kama ndiye Bwana na mwokozi pekee wa maisha yetu na kuukubali msamaha wake wa dhambi, basi tunahesabiwa tumestahili kuitwa watakatifu, na hivyo tunamkaribia Mungu katika ukamilifu wote, kumwomba yeye na kupokea vyote kutoka kwake bila sharti. Haleluya!

Warumi 3:21-24

[21]Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; 

[22]ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 

[24]wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 

Hivyo ikiwa umekombolewa na Yesu Kristo, basi unapaswa uwe na ujasiri wote kumkaribia Mungu, bila kutegemea ukamilifu wako,Bali Kristo tu, na hivyo utapokea mema, yote kutoka Kwa Mungu.

Waebrania 4:16

[16]Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. 

Hiyo Ndio inaitwa “HAKI itokayo Kwa Mungu” ambayo tunaipata kwa kupitia Yesu Kristo tu peke yake.

Kwa Yesu tunapokea uzima wa milele bure. Kwa Yesu Tunapokea majibu ya mahitaji yetu yote bure. Kwa Yesu tunaitwa watakatifu.

Lakini Swali ni je! Umemwamini Kristo? Kumbuka kamwe huwezi kumpendeza Mungu Kwa matendo yako pekee, Kila mwanadamu chini ya jua anamuhitaji Kristo.

Ikiwa Bado hajaokoka basi mlango upo wazi Leo. Tubu mgeukie Bwana akuponye. Ikiwa upo tayari kupokea msamaha wa dhambi Leo, na kufanywa kiumbe kipya, basi fungua hapa Kwa Mwongozo huo. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Mafundisho mengine

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Jibu: Turejee,

Mathayo 24:35  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Ili tuelewe vizuri, tutafakari kwanza mstari ufuatao…

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Mpaka maandiko yaseme kuwa “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”… Maana yake kuna watu, au vitu ambavyo haviwezi kuwa vile vile jana, leo na hata milele.

Kwa mfano mtu hawezi kuwa na tabia ile ile, au msimamo ule ule jana na leo na hata milele,..ni lazima tu utafika wakati tabia yake itabadilika, mtazamo wake utabadilika, utendaji wake utabadilika au hata msimamo wake!…. lakini KRISTO YESU yeye ni yule yule, kitabia, na kiutendaji, hajawahi kusema jambo halafu akajikosoa.. ni yeye yule na ataendelea kuwa vile vile Milele.

Hali kadhalika, vitu tunavyoviona katika mbingu kama jua, mwezi  na nyota, ijapokuwa tunaona vimedumu kuwa vilevile kwa maelfu ya miaka, lakini biblia inatabiri kuwa siku moja vitatoweshwa vyote…

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13  na NYOTA ZIKAANGUKA juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14  MBINGU ZIKAONDOLEWA KAMA UKURASA ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.

Vile vile vitu tunavyoviona katika “NCHI” kama vile milima, na habari ambavyo tunaviona kama zimedumu kwa maelfu ya miaka, lakini bado biblia inatabiri kuwa siku moja vitafutika..

Ufunuo 16:20  “Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena”

Soma pia Ufunuo 21:1..

Lakini wakati ambapo vitu vyote hivi vinaondolewa (maana yake VINAPITA) Bado Kristo atabaki kuwa yeye yule, na maneno yake yatabaki kuwa yale yale, na yana nguvu ile ile katika umilele wote.

Kwamfano maneno ya Yesu anayosema yeye ni ALFA na OMEGA, yaani Mwanzo na Mwisho (katika Ufunuo 21:6 na Ufunuo 22:13) yataendelea kuwa hivyo hivyo Milele, hakuna wakati utafika Kristo ataacha kuwa Alfa na Omega…jua na mwezi na nyota na wanadamu watapita, lakini maneno hayo yataeendelea kuwa halisi hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile maneno yake aliyosema kuwa “Yeye ndio Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6)” yataendelea kuwa hivyo milele na milele, hakuna wakati utafika ambao Kristo ataacha kuwa Njia, au ataacha kuwa  Kweli au ataacha kuwa Uzima..Kristo YESU sasa ni Uzima, na ataendelea kuwa UZIMA hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile aliposema kuwa yeye ni “Nuru ya Ulimwengu (Yohana 8:12)”…Maneno hayo hautafika wakati ambao yata-expire… Jua na mwezi kuna wakati vitaisha muda wake wa matumizi, jua litaondolewa halitamulika tena, na mwezi utaondolewa hautaangaza tena.. lakini Kristo ataendelea kuwa NURU hata kipindi ambacho jua na mwezi havipo..

Ufunuo 21:23  “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, KWA MAANA UTUKUFU WA MUNGU HUUTIA NURU, NA TAA YAKE NI MWANA-KONDOO”.

> Vile vile maneno yake mengine yanamtaja yeye kama “Mwaminifu na wa Kweli (katika Ufunuo 3:14, na Ufunuo 19:11)”. Yeye atabaki kuwa hivyo Milele na milele, hakuna wakati ambao atabadilika na kukosa uaminifu!… Sisi wanadamu tunaoishi chini ya jua na juu ya nchi, tutakuwa waaminifu tu kwa kitambo Fulani lakini si milele. Lakini yeye ataendelea kuwa mwaminifu milele na milele hata wakati ambao mbingu zitafutwa, na kuletwa mbingu mpya na nchi mpya, bado ataendelea kuwa mwaminifu.

> Pia alisema wote wamwaminio yeye watakuwa na uzima wa milele, hakuna wakati hilo Neno litabadilika, kwamba awanyime uzima wa milele wale wote waliomwamini na kuishi kwa kuzifuata amri zake.. Majira yatabadilika, vipindi vitabadilika lakini milele na milele hawezi kujisahihisha maneno yake hayo. AKIAHIDI AMEAHIDI!!.. Na milele habadiliki.

Na maneno mengine yote yaliyosalia aliyoyasema BWANA YESU hakuna hata moja litapita!!! , yote yatabaki kuwa vile vile

Je umemwamini huyu Mkuu wa UZIMA asiyeweza KUBADILIKA?, Au Unawatumainia wanadamu ambao leo wapo na kesho hawapo, leo wanaahidi na kesho wamebadilika, leo wanakupenda kesho wanakuchukia.. Ni heri ukaanza kumtumainia yeye asiyeweza kubadilika, YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA.

Mungu akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Mafundisho Mengine

Mbinguni ni sehemu gani?

Kuna Mbingu ngapi?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA ANASAMEHE.

Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRISTO lihimidiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai, ambalo ndilo taa na mwanga wa njia yetu ya kwenda mbinguni (Zab.119:105).

Moja ya hubiri kubwa na kongwe la shetani, ni kuwahubiria watu kuwa “MUNGU HASAMEHI na ANACHUKIA WATU”.

Fundisho hili ni silaha kubwa sana ya kumfanya mtu asijaribu kumtafuta Mungu, au hata kama alikuwa ameshaanza hatua za kuutafuta uso wa Mungu, basi akate tamaa njiani. Anajua mtu akifahamu kuwa anaweza kusamehewa na Mungu basi hatampata tena, na yeye anataka watu waendelee kudumu katika dhambi ili hatimaye waukose uzima wa milele kama yeye alivyoukosa.

Sasa sifa moja kuu ya MUNGU aliyeumba mbingu na nchi, ni MSAMAHA. Maana yake “anatoa msamaha hata kwa mtu asiyestahili kusamehewa”.. Na hii ndio sifa ya kwanza inayomfanya yeye (MUNGU) kutisha!..na wala si tu yale matendo ya miujiza aliyoyafanya kule Misri, au anayoendelea kuifanya hata sasa, ambayo kimsingi tunadhani hayo ndiyo yanayomfanya Mungu atishe.

Muujiza Mkuu na wa kwanza unaomfanya Mungu kutisha, ni KUSAMEHE NDAMBI, na KUZIONDOA KABISA NDANI YA MTU.

Zaburi 130:3 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, ILI WEWE UOGOPWE”.

Je! Unajihisi wewe ni mwenye dhambi, na unahisi dhambi yako haifutiki??…fahamu kuwa MUNGU kuna msamaha, na sio tu msamaha bali pia na ondoleo la dhambi, kiasi kwamba baada ya kusamehewa Mungu anaondoa mpaka msingi wa hiyo dhambi, kiasi kwamba wakati mwingine haitakuwa na nguvu juu yako.

Je unahisi mauaji uliyoyafanya hayawezi kusameheka?, je unahisi mawazo uliyowaza au unayowaza hayana msamaha?, je unahisi tendo ulilolifanya na tena umelirudia mara nyingi nyingi halina msamaha?..kama hayo mawazo yapo ndani yako basi fahamu kuwa ni adui ndiye anayekuambia hivyo.

Yote uliyoyafanya yanasameheka ikiwa utataka Bwana akusamehe!. Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha kuacha hayo unayoyafanya, Ikiwa utatubu kweli kwa kumaanisha, basi kwa IMANI amini kuwa Mungu kashakusamehe, hauhitaji kutokewa na Malaika na akamwambie kwamba umesamehewa, wewe Amini tu, kwasababu ndivyo biblia inavyotufundisha kwamba “tuenende kwa Imani na si kwa kuona” (2Wakorintho 5:7).

Na ukishaamini namna hiyo, basi Mungu kashakusamehe lile kosa au yale makosa uliyoyafanya hata kama uliyafanya kwa kurudia rudia mara 100, tayari atakusamehe deni yako yote. Lakini kumbuka msamaha si ondoleo!.. Mtu anaweza kukusamehe tusi ulilomtukana, lakini kama ile roho ya kutukana haijaondoka ndani yako basi unaweza kurudia tena kesho na kesho kutwa kumtukana matusi yale yale.

Kwahiyo ili lile kosa lisijirudie rudie tena katika maisha yako, linahitaji kuondolewa kwa mizizi yake ndani yako. Sasa kanuni ya kuondoa mzizi wa dhambi ndio shetani amewafumba watu macho wasiione.

Lakini ashukuriwe Mungu kwasababu ipo wazi katika maandiko.

Tusome,

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Hapa Petro anawaonyesha hawa Makutano, kanuni ya KUONDOA MZIZI wa dhambi ndani yao, baada ya wao KUTUBU dhambi,  kwamba WAKABATIZWE KWA JINA LAKE YESU KRISTO. Kama ishara ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu upya, na kwa ishara hiyo ya maji basi ule mzizi wa dhambi utaondoka ndani yao, zile dhambi za kujirudia rudia zitakoma, kwahiyo mtu wa Mungu anabaki huru mbali na dhambi.

Na tena Mungu wetu kwa upendo wake anatuongezea na zawadi ya Roho Mtakatifu, ndani yetu kama Muhuri wa Mungu kwa kile tulichokitubia.

Je bado umezishikilia dhambi zako? Kwanini usiungame leo kwa kutubu na kubatizwa?. Na kumbuka ungamo sahihi ni lile la kutubu kwa kumaanisha, na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, Kutubu kusikotoka moyoni, na ubatizo usio sahihi haviwezi kuleta matokeo yoyote kwa mtu.

Bwana akubariki.

Ikiwa utahitaji msaada katika kuongozwa sala ya Toba, au ubatizo basi waweza wasiliana nasi na tutakusaidia katika hilo.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUTUBU

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

BABA UWASAMEHE

UMEONDOLEWA DHAMBI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

Je Imani yako imefifia?, je upendo wako umepoa?, je Amani yako imepungua?, na haki yako imepoa?.. Na hujui cha kufanya na ndani bado una haja sana ya kuwa na mambo hayo?.. Basi suluhisho lipo ndani ya biblia.

Ifuatayo ni kanuni moja nyepesi ya kurejesha joto la ROHO MTAKATIFU ndani yako. Kumbuka mtu aliyejaa Roho Mtakatifu ataonyesha matunda yafuatayo…

Wagalatia 5:22  “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23  upole, kiasi;…”.

Ikiwa mambo haya yalikuwa ndani yako lakini sasa huyaoni tena, au ikiwa hauna kabisa, basi tumia kanuni ifuatayo kuyarejesha/kuyajenga ndani yako.

KAA KARIBU NA WATU WATU WANAOMWITA BWANA.

Watu wanaomwita Bwana, kwa lugha nyingine ni watu waliookoka kikweli kweli,…Utauliza kwa namna gani?…Tusome maandiko yafuatayo..

2Timotheo 2:22  “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, PAMOJA NA WALE WAMWITAO BWANA KWA MOYO SAFI”.

Hapo mwisho anasema, ukatafute haki, Imani na upendo na amani “pamoja na wale wote wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Kumbe! Haki inapatikana kwa watu wanaomwita Bwana kwa dhamiri safi, kumbe tukikaa na watu waliomaanisha kumwita Bwana na kumtafuta basi Amani tutaipata, na upendo na Imani.

Kama maandiko yasemavyo kwamba “chuma hunoa chuma, Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake” (Mithali 27:17). Vivyo hivyo na sisi tunapokaa na watu wenye kumaanisha kumtafuta Mungu basi ule moto ulio ndani yao atahamia na kwetu pia.

Lakini tukijitenga na kubaki wenyewe, au tukijumuika na watu wengine wasio na nia ya dhati kumtafuta Bwana, ni ngumu kuuwasha ule moto wa Roho ndani yetu!, tutabaki kama tulivyo!.. Kanuni ni kukaa pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi!…Vile vile tunapojitenga na kuamua kukaa peke yetu kwa muda mrefu ni pia ni hatari!!.. Imani, amani, upendo na haki yako vinaweza kuathirika pakubwa.

Sasa tunawapatia wapi watu wamwitao Bwana kwa moyo safi?.

1.Katika kanisa lililo hai.

Hii ni sehemu pekee ambayo utawapata watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, jiunge na kanisa la kiroho lililo karibu nawe, au hata lililo mbali ikiwa lililo karibu nawe halina utakatifu. Jumuika na watu hao, katika utii na unyenyekevu, na katika ibada zote, na hapo Roho Mtakatifu atakujenga ndani yako na kukujaza nguvu zake, utaona Imani yako inapata nguvu, upendo wako uliopoa unawaka tena, haki yako iliyopotea inarudi na Amani yako pia inahuika upya, na ifanye hiyo iwe desturi yako daima.

Waebrania 10:25 “wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine;..”.

Na utajuaje kanisa hilo, ni la kiroho?.

Kigezo cha kwanza ni mwonekano wa nje wa waabuduo wa mahali hapo!, ukiona mwonekano na mazungumzo ya waabuduo si ya kiMungu, kwamba wanazungumza kidunia na wanavaa kidunia, kiasi kwamba hauoni tofauti na mtu anayeenda disko na anayeshiriki mahali hapo, basi tuchukua tahadhari hapo si sehemu salama!.

Vile vile mafundisho yanayofundishwa mahali pale kama hayalengi TOBA, na UJIO wa PILI wa BWANA YESU, na UTAKATIFU wa MWILINI na ROHONI, pia hapo si sehemu salama, lakini kama kanisa lina vigezo hivyo vya Utakatifu wa kimafundisho na kimwonekano, basi ndani yake watakuwepo watu wamwitao Bwana kwa moyo safi, kaa hapo na utaona mabadiliko makubwa ya kiroho ndani yako.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

KAMA WEWE NI KIJANA, BASI FAHAMU YAFUATAYO NA UCHUKUE TAHADHARI!

Ikiwa wewe ni kijana basi fahamu basi fahamu mambo yafuatayo.

1.MAWAZO MABAYA YANAANZIA UJANANI.

Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni, Sitailaani nchi tena baada ya hayo kwa sababu ya wanadamu, MAANA MAWAZO YA MOYO WA MWANADAMU NI MABAYA TANGU UJANA WAKE; wala sitapiga tena baada ya hayo kila kilicho hai kama nilivyofanya”.

Mawazo ya kuidharau injili, mawazo ya ukaidi wa moyo na kiburi cha uzima yanaanzia ujanani.

Yeremia 22: 21 “Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako TANGU UJANA WAKO, KUTOKUITII SAUTI YANGU”.

   2. MUNGU ANATAFUTWA UJANANI NA SI UZEENI!.

Mhubiri 12: 1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo”.

Maana yake katika uzee “haitawezekana kabisa” kumtafuta Mungu kama utapuuzia wito wa Mungu katika ujana wako!!!. Wakati wa Ujana ndio wakati wa kujifunga NIRA YA MUNGU iliyotajwa na BWANA YESU katika Mathayo 11:29.

Maombolezo 3:27 “Ni vema mwanadamu aichukue NIRA WAKATI WA UJANA WAKE.

28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake”.

   3. KAMA UTACHAGUA ANASA, BASI FAHAMU KUWA SIKU YA MWISHO UTASIMAMA HUKUMUNI.

Mhubiri 11:9 “Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya KWAMBA KWA AJILI YA HAYO YOTE MUNGU ATAKULETA HUKUMUNI”

Maana yake kama utachagua uzinzi katika ujana wako, au ulevi, au anasa nyingine yeyote basi pia jiweke tayari kusimama mbele ya kiti cha hukumu siku ile ya mwisho, ambapo maandiko yanasema kila mtu atatoa habari zake mwenyewe (Warumi 14:12), na tena kila neno la upuuzi litatolewa hesabu yake siku ile ya hukumu (Mathayo 12:36).

  4. NEEMA YA WOKOVU HAIKUBEMBELEZI.

Ufunuo 22:10 “ Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  MWENYE KUDHULUMU NA AZIDI KUDHULUMU; NA MWENYE UCHAFU NA AZIDI KUWA MCHAFU; NA MWENYE HAKI NA AZIDI KUFANYA HAKI; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”.

Ikiwa umechagua uchafu!, basi usiufanye kidogo!..ufanya sana, lakini kama umechagua USAFI, basi JITAKASE SANA, usiwe hapo katikati (vuguvugu!)..

   5. UTAKAPOKUWA MZEE UTAPELEKWA USIKOTAKA.

Yohana 21:18  “Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka”.

Uhuru ulionao si wa Daima, ipo siku utaisha, na wengine watakuwa na mamlaka juu yako…….

Je wewe kama kijana sasa umejipangaje?..je unawaza nini katika ujana wako huu? au unafikiri nini?…Kwanini usiamua kumgeukia Muumba wako leo!, na kuachana na udunia, na tamaa za ujanani, ambazo hazina faida yoyote Zaidi sana zina hasara nyingi?

2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”.

Bwana Yesu akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Ikiwa unahitaji msaada wa kuokoka na ubatizo basi wasiliana nasi kwa namba zetu tajwa hapo chini.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Mke wa ujana wako ni yupi kibiblia?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

Jibu: Turejee,

Yohana 4:19  “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21  Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Maana ya kumwabudu Baba katika roho na kweli, ni KUMFANYIA MUNGU IBADA, KATIKA ROHO MTAKATIFU NA KATIKA KWELI YA NENO LAKE.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE…”

Sasa BWANA YESU aliposema kuwa “SAA INAKUJA”, alimaanisha kuwa kuna kipindi kinakuja  mbeleni, ambacho waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli, na wakati huo si mwingine Zaidi ya ule wa Pentekoste. Kipindi ambacho Roho Mtakatifu atamwagwa juu ya kanisa kwa mara ya kwanza, baada ya BWANA YESU kuondoka!.

Huo ndio uliokuwa mwanzo wa watu kumwabudu Baba katika roho na kweli. (Matendo 2:1-15)

Lakini pia aliposema kuwa..“NA SASA IPO”…. maana yake hata huo wakati tayari Baba ameshaanza kuabudiwa katika roho na kweli. Na aliyekuwa anamwabudu baba katika ROHO NA KWELI ni yeye mwenyewe BWANA YESU KRISTO. Kwasababu tayari alikuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, ambaye alipoondoka ndipo akammwaga juu ya kanisa.

Yohana 16:7 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na hata sasa tupo kipindi ambacho Neema ya Roho Mtakatifu bado ipo duniani kwa kila anayemwitaji sawasawa na Matendo 2:38, Na kumbuka Roho Mtakatifu pekee ndiye funguo za mtu kumwabudu Mungu katika roho na kweli, na pasipo yeye haiwezekani kumwabudu Mungu katika roho.

Kwa somo refu lihusuyo jinsi ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli fungua hapa >>Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

UWEZO WA KIPEKEE.

Rudi nyumbani

Print this post

MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.

Kama mwanamke uliyeokoka. Fahamu kuwa una wajibu wa kujiombea wewe, kuombea jinsia yako, na kuliombea Kanisa la Kristo kwa ujumla. Huu ni mwongozo wa kipengele muhimu vitakavyokusaidia katika maombi yako. ambavyo kama utakuwa ni mwombaji wa mara kwa mara katika maeneo hayo, basi unajijengea mazingira ya kuwa  mwanamke bora, mama bora, na zaidi sana mtumishi bora wa Bwana katika mwili wa Kristo.

Mwongozo huu unaweza kuutumia pia muwapo wanawake wawili au watatu katika kikundi chenu cha maombi, au kanisani. Na hivyo kila kipengele tenga muda wa kutosha kuomba.

  • Omba Bwana akufanye kuwa shujaa wa injili, pia omba Bwana anyanyue jeshi la wanawake watetea injili, watumike vema katika nafasi zao kanisani,na nje ya Kanisa, kuwaokoa wenye dhambi. Katika maandiko Mfano wa Hawa ni Prisila Matendo 18:18, 26. 

NANGA: Zaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;”

  • Omba Bwana akupe uwezo wa kuirithisha imani kwa vizazi vijavyo, Pia awanyanyue wanamwake  vijana/wazee wengi wa namna hiyo, wenye uwezo wa kuirithisha imani ya Kristo kwa vizazi vingi mbeleni. Imani isiishie kwao tu, bali hata kwa vijukuu na vitukuu vyao.

Mfano wa wanawake  hawa alikuwa ni Loisi.

NANGA: 2Timotheo 1:5  nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo

  • Omba Bwana aamshe kwako na kwa wanawake wote Roho ya uombolezaji(kuugua ndani) mtakaosimama katika mahali palipo bomoka kwa ajili ya kulinyanyua kanisa na wenye dhambi.

NANGA: Yeremia 9:17 Bwana wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje;  18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji.  19 Maana sauti ya maombolezo imesikiwa toka Sayuni, Jinsi tulivyotekwa! tulivyofadhaika sana! Kwa sababu tumeiacha nchi, kwa kuwa wameangusha makao yetu.

  • Omba Bwana aamshe Kiu ya kupenda kujifunza Neno, ndani yako na kwa wanawake wengine wote wamchao Mungu. Mfano wa Hawa alikuwa ni Mariamu Dada yake Martha.

NANGA:  Luka 10:39  Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.

  • Omba Bwana akupe Roho ya upole na utulivu; Sio ya vurugu au  kutanga-tanga huku na huko kiroho, au kimwili. Sawasawa na Agizo Mtume Petro aliloliandika kwa kanisa (1Petro 3:1-6).

NANGA: 1Petro 3:4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

  • Bwana aweke Roho ya utii, wewe na kwa Wanawake wote wamchao Bwana ndani ya Kanisa. Mfano wa ile iliyokuwa ndani ya Sara, ambayo aliweza kumtii Mungu, lakini pia mume wake.

NANGA:  1Petro 3:6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote

  • Bwana akupe Roho ya kupenda kujisitiri, na kuvaa mavazi ya jinsia yako, vilevile awape na wanawake wote watakatifu moyo huo.  (Kumbu 22:5)

NANGA:  1Timotheo 2:9  Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani

  • Bwana akuumbie Roho ya kujitoa kwake Bwana, kwa mali zako, na kwa nguvu zako. ( Mfano wa hawa alikuwa ni Mariamu magdalena, Mshunami (Yohana 12:3, 2Wafalme 4:8-18))

NANGA: Luka 8:3  na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao

  • Bwana aiamshe Roho ya ‘usaidizi’ katika huduma, pia iumbike katikati ya wanawake. Kumbuka wewe kama mwanamke umepewa karamu kubwa sana ya usaidizi tangu kuumbwa kwako. Ombea itende kazi vema ili iifaidie kanisa na familia.

NANGA:  Mwanzo 2:18  Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye

  • Bwana akuumbie Roho ya uaminifu hata pale ambapo hujapata kitu chochote. Usimwache Bwana.

NANGA: Luka 1:6  Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiendelea katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama. 7  Nao walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili ni wazee sana

  • Akupe Roho ya kumwimbia Mungu kwa moyo wote wa furaha na kuchangamka Mfano wa wanawake mashujaa waliomcha Mungu zamani, ambao hawakuona aibu kumwimbia Bwana kwa mioyo yao yote.

 NANGA: Kutoka 15:20 Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.  21 Miriamu akawaitikia,Mwimbieni Bwana ,kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini

  • Omba Bwana akuumbie Nguvu ya “maombi ya kung’ang’ania” mpaka ipatikane ichipushwe pia miongoni mwa kundi Mfano wa Hawa alikuwa ni Rispa binti aya ambaye aliweza kukesha milimani kufunga na kuombeleza kwa miezi mingi mpaka mfalme akasikia habari zake, akatoa agizo juu yake

NANGA: Soma – 2Samweli 21, yote

  • Bwana akupe Roho ya Uwazi na kusaidiana kwa umoja na wanawake wenzako wacha Mungu ndani ya kanisa na pia iwepo  kwa wanawake wote.

NANGA: Luka 24:22  tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, 23  wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai

PIA OMBA…

  • Bwana akuumbie Roho ya uangalizi na ulezi kwa watoto, na vijana katika maadili ya kumcha Bwana

NANGA: 2Yohana 1:1  Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli;

  • Upewe Roho ya huruma na ya kutunza uhai. Mfano wa hawa ni  (yehosheba). Aliuhifadhi uzao wa kifalme katika  Israeli kwa kumficha mtoto asiuawe.  (2Wafalme 11:2). Ilikuwa pia kwa mama yake Musa, lakini pia kwa Shifra na Pua wazalisha wa kiebrania

NANGA:  (Soma Kutoka 1:15-19)

  • Roho ya unyenyekevu na ya kujiachilia kwa Bwana moja kwa moja, bila kigugumizi chochote cha rohoni. Mfano wa Ruthu kwa Naomi, ambaye alijitoa kwa mkwewe katika hali zote bila kujali ujana wake, au umaskini wa mkwewe.

NANGA: Ruthu 1:16 Naye Ruthuu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;  17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe name

  • Akupe Moyo wa ujakazi mwema wenye manufaa, utakaowaleta wengine kwa Kristo ikiwa wewe ni mwajiriwa mahali fulani (Mfano wa hawa alikuwa ni Roda, &  Yule kijakazi wa Naamani) – 2 Wafalme 5:1-19, Matendo 12:13
  • Bwana akupe moyo wa kupenda kudumu hekaluni mwa Bwana. Vivyo hivyo na wanawake wote kanisani. Mfano ni Ana binti Fanueli.

NANGA: Luka 2:36  Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. 2.37  Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba

  • Bwana akupe ufahamu wa kuyatunza Maneno ya Mungu moyoni wako. Usiwe wa kutokuzingatia kile Mungu anachosema na wewe. Mfano bora ni  (Mariamu mamaye Yesu)

NANGA: Luka 2:51  Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. 51  Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake

  • Roho ya kupenda kujitaabisha kwa Bwana katika hekima yote ya ki-Mungu itokee ndani yako na kwa wanawake wengine. (Martha)-

NANGA: Luka 10:40  “Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi;..”

  • Bwana akujalie wewe na wanawake wote Roho ya nguvu na ya ujasiri ya kuweza hata kuliamua taifa. Mfano wa Debora, katika nafasi yako kama mama.

NANGA: Waamuzi 4:4 Basi Debora, nabii mke, mkewe Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule.  5 Naye alikaa chini ya mtende wa Debora, kati ya Rama na Betheli, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu; wana wa Israeli wakakwea kwake, awaamue

  • Roho ya kuthamini, Bwana alivyoviweka mkononi mwako, kuvilinda na kuvitafuta pindi vipoteapo.

NANGA: Luka 15:8  Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? 15.9  Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.

  • Bwana akupe Roho ya kuridhika na hali, na mwonekano wako, kutoongeza mapambo mwilini. Usiwe kama Yezebeli-2Wafalme 9:30
  • Bwana awajalie wanawake wote wakue kiroho, ili wasichukuliwe mateka na watu wadanganyifu (2Timotheo 3:6)
  • Bwana awafariji wajane wote, lakini pia awape moyo wa kupenda kutoa na kutumika (Mfano wa Yule aliyetoa senti mbili, Yule aliyetembelewa na Eliya)-

NANGA: Soma (Marko 12:42, 1Wafalme 17:12, Luka 7:11)

OMBA PIA…

  • Roho ya kuwajibika kwa wanawake, Bwana aiamshe kwako na  katika kanisa (kupenda kushughulika Mithali 31:10-31
  • Bwana awajalie wanawake wote Wajawazito kujifungua salama.(Kutoka 1:15-17, Isaya 66:9)
  • Mabinti/ wanawake katika kanisa wanaotaka kuolewa, Bwana awape wenzi sahihi (Abigaili aliolewa na Nabali mume asiyestahili. -1Samweli  25)  Jambo hilo lisitokee ndani ya kanisa.
  • Magonjwa yanayoishambulia jinsia ya kike. Bwana ayafute mbali na wewe na ndani ya kanisa la Mungu (Marko 5:25-34)

PIA OMBA HIZI TABIA ZIONDOKE NDANI YAKO NA WANAWAKE WOTE…

  • Roho ya kujichanganya na makundi yasiyofaa/ kutokuwa na mipaka, itoweshwe (Dina hakuwa na mipaka,  akahadaiwa na watu wa kidunia – Mwanzo 34:1).
  • Roho ya utoaji mimba, ipotelee mbali kwa wanawake wacha Mungu na kwa jamii yetu (Kutoka 20:13, Ayubu 3:3-12).
  • Bwana aifutilie mbali tabia ya kupuuzia maono: Mke wa Herode alisemeshwa kwa ajili ya haki ya Yesu lakini hakuchukua hatua stahiki, kama Bwana alivyotaka (Mathayo 27:19)
  • Wanawake wa kikristo wanaonyanyaswa kijinsi agh. Kulazimishwa kuolewa, kukeketwa, kubakwa, kupigwa, kunyimwa haki za elimu, na kumcha Mungu n.k. Bwana afutilie mbali hiyo roho; > Mfano ni Kisa cha Tamari na amnoni (2Samweli 13)
  • Nguvu za giza zinazowavaa wanawake kiwepesi, zisipate nafasi ndani ya kanisa la Kristo.( Marko 16:9)
  • Roho ya udanganyifu wa nyoka, (kushawishwa) Bwana aifukuzie mbali na kanisa lake takatifu (Mwanzo 3:1)
  • Roho ya uuaji ya Yezebeli na Athalia, na herodia  isipate nafasi ndani ya Kanisa la Bwana –, (2Wafalme 11:1, Mathayo 14:8)
  • Roho ya kiburi isitokee miongoni mwa kundi (Vashti –Esta 1:12)
  • Roho ya masengenyo, na udadisi ifutwe katikati ya kundi la Kristo (1Timotheo 5:13)
  • Roho za ndoa kuvunjika, na magomvi zisitoe mzizi ndani ya kanisani.  (Waefeso 5:33)
  • Roho ya kukufuru kama ya Mke wa Ayubu Bwana aifutilie mbali. (Ayubu 2:9)
  • Roho ya kupenda ulimwengu na mambo ya kidunia, iondoshwe (Mke wa Lutu) –Mawnzo 19:26
  • Roho ya tamaa ya kuiba vya Mungu, isichipuke ndani ya kundi la wanawake ( mkewe Safira) Matendo 5:1
  • Roho ya uzinzi ife iyeyushwe kabisa (mke wa potifa)- Mwanzo 39:7
  • Roho ya ushirikina na uchawi isipate nafasi miongoni mwa wanawake (mganga wa Sauli)-Samweli 28:11
  • Roho ya mashindano itoweke miongoni mwa wanawake (Lea na Raheli, wanawake hao)-Mwanzo 29:30
  • Roho ya kuzira/ kukwazika mapema hata kutaka kuacha kutumika ifitwe miongoni mwa wanawake (Hajira- Mwanzo 16:9)
  • Roho ya kutumiwa na adui (u-agent), ili kuliangusha kundi ifutwe (Delila –Waamuzi 16)
  • Roho ya kusema uongo/  kutumia hila,  isionekane ndani ya kundi (Mama yake Yakobo – Rebeka- Mwanzo 27:6)
  • Roho ya uchungu usiokoma moyoni, vinyongo, visasa, kutokuachilia, kutokusamehe, iyeyuke ndani ya wanawake.(Yakobo 3:14)
  • Roho ya matabaka, ndani ya Kanisa ipotelee mbali(Wafilipi 4:2). Sintike na Euodia
  • Roho ya udhuru isisimame ndani ya kundi la wanawake kanisani. – (Matendo 1:14)
  • Roho ya kudharau, watu wa Mungu, au kazi ya Mungu, isiwe na sehemu miongoni mwa wanawake( Mfano wa Mikali, binti Sauli. 2Samweli 6:16

Kwa ushauri/ Msaada/ Maombezi /Ratiba za ibada, wasiliana nasi kwa mawasiliano haya;

Na, Mwl Denis & Devis Julius

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post