Title 2023

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

Ikiwa unafanya matendo mazuri yanayompendeza Mungu, basi mshukuru Mungu kwa hayo lakini USIJISIFU wala kujigamba hata kidogo kwa hayo. Kwasababu wakati unadhani kuwa umefanya 100 yanayompendeza Mungu kwa siku moja, yapo mengine 200 uliyoyafanya yasiyompendeza Mungu, kwa kutokujua.

Laiti tukifunguliwa macho na kuona makosa yetu yote tunayoyafanya bila sisi wenyewe kujua, tusingeendelea kujitamani hata kidogo, tusingeendelea kujivuna, tusingeendelea kujisifia vimema vichache vichache tunavyovitenda kwa siku!!!…Kwaufupi maisha yetu yamejaa makosa mengi kuliko mema!, hata kama tutajiona kama tuna mema mengi kuliko kasoro.. Lakini uhalisia utabakia pale pale kwamba makosa yetu yamezidi mema yetu..

Kwahiyo kama Mungu ni wa haki, basi ni haki yake atulipe mabaya mengi kuliko mema.

Kama ukimlazimisha Mungu akuhesabie haki ya kukubariki kwa sadaka yako uliyotoa  jumapili, vile vile anapaswa akuhesabie haki ya kuadhibiwa kwa mawazo yako ya kutamani na kwa hasira uliyomwonea ndugu yako siku hiyo hiyo ya jumapili. Na maandiko yanasema mtu amwoneaye ndugu yake hasira ni mwuaji, kwahiyo unapaswa uhukumiwe kama mwuaji..

Lakini kama hutaki Mungu atazame udhaifu wako huo na hutaki akuadhibu kwa makosa yako basi usilazimishe akulipe kwa matendo yako mazuri unayomfanyia. Bali kinyume chake nyenyekea!!!.. Fanya tu yakupasayo kufanya sawasawa na Luka 17:10.

Luka 17:10  “Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya”.

Na kama tukiingia mkataba huo na Mungu wa kupokea haki yetu kwa matendo yetu, basi tunazo sababu nyingi za kulipwa mabaya kuliko mema. Kwasababu Mungu siku zote ni  wa haki.

Lakini kama mara nyingi Mungu anatuvumilia kwa mabaya yetu tunayoyafanya sawasawa na Zaburi 130:3  “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama? Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe”…basi na sisi hatuna budi kutoyatumainia mema yetu tunayoyafanya!.

Ndio hapa sasa panazaliwa kitu kinachoitwa NEEMA!... Neema tafsiri yake ni upendeleo maalumu usiokuwa na sababu. Kwamba unapokea tu kitu kutoka kwa Mungu pasipo matendo yako.. Yaani Mungu anapenda tu kukupa si kwasababu wewe ni mtenda mema, au ni mwombaji sana, au ni mfungaji sana, au ni mhubiri mzuri… La!, bali anakutendea tu mema bila kwa upendo wake tu!, na huruma zake na kupenda kwake.

Ndio maana hatuna budi kila siku KUOMBA NEEMA YA MUNGU ije juu yetu. Kwasababu tukiipata hiyo tumepata kila kitu.

Usijivune, bali omba neema kwasababu Mungu huwapinga wenye kiburi na kuwapa wanyenyekevu Neema yake (1Petro 5:5).

Afya uliyonayo ni kwa neema tu, Uzima ulio nao ni kwa Neema tu, karama uliyo nayo ni kwa neema tu, zaidi sana hata Wokovu ulio nao ni kwa Neema tu na wala si kwa matendo yako.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9  wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”

Na zaidi ya yote pia Roho Mtakatifu tunampokea kwa Neema..

Wagalatia 3:2 “Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani”

Omba Neema!!.. omba Neema!, Omba Neema…usitumainie matendo yako..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

NEEMA YA MUNGU KWA MARIAMU.

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia, leo tujikumbushe historia fupi ya tafsiri ya biblia ya King James.

King James au kwa Kiswahili “Mfalme Yakobo” wa Uingereza, alikuwa ni mmoja wa wafalme ambao hawakuwa maarufu sana kwa wakati wao. Lakini alikuja kufanya jambo la kishujaa ambalo mpaka leo yupo katika rekodi ya watu maarufu na wakihistoria waliowahi kutokea Uingereza.

Mwaka 1604 baadhi ya wanazuoni wa Kiprotestanti (Wapuriti) walipendekeza kuchapishwa kwa tafsiri mpya ya biblia, kuchukua nafasi ya ile iliyokuwepo ambayo ilijulikana kama tafsiri ya “Geneva”. Tafsiri ya Geneva ndio ilikuwa tafsiri ya kwanza kwa lugha ya kiingereza kuchapichwa huko Ulaya, iliyotumiwa na Waprotestanti.

Upungufu wa tafsiri hiyo ya Geneva, ni kwamba ilikuwa ina “maoni ya ziada” yaliyoongezwa ili kutilia mkazo kile kilichoelezwa katika biblia, na maoni hayo ya mkazo, yalilenga sana kuwakosoa viongozi wa kisiasa na kidini.

Hivyo baadhi ya waprotestanti hao, jamii ya Wapuriti, walitoa mapendekezo yao kuchapiswa biblia nyingine ambayo itaondoa hayo maoni ya watu na kuiacha yenyewe kama yenyewe, pasipo maoni ya watu. Na pia chapisho hilo litalenga pia kuitafsiri biblia nzima katika kingereza kizuri zaidi.

Wapuri hao baada ya kutoa hilo pendekezo, walilifikisha kwa Mfalme ambaye alikuwa anaitwa YAKOBO (King James).

Kikawaida wafalme wengi huwa hawajihusishi na masuala ya kiimani, zaidi sana huwa wanayapinga, lakini ikawa ni kinyume chake kwa huyu King James, badala ya kulipinga au kulikosoa wazo lao, yeye alikubali biblia mpya hiyo ichapishwe na tena akatoa sehemu kubwa ya hazina ya utajiri wake kusaidia zoezi zima la utafsiri mpya.

Tafsiri hiyo mpya ya Biblia hiyo mpya iliandaliwa kwa kipindi cha Miaka 7, na wanazuoni zaidi ya 47 kutoka kila mahali, Uingereza.  Walianza kuitafsiri biblia upya kutoka katika Lugha ya kigiriki kwa agano la kale, na kiaramu kwa agano jipya. Walipomaliza kuitafsiri biblia yote wakaiita biblia hiyo KING JAMES BIBLE, Yaani biblia ya Mfalme Yakobo.

Baada ya kumaliza kutafsiri, kazi ile ilionekana kama dhaifu sana, lakini muujiza ni kwamba ndani ya kipindi kifupi, tafsiri hiyo mpya ya King James, ilianza kupendwa na watu wengi, kwani haikuwa na mchanganyiko wa maoni ya watu, na ilikuwa na kiingereza kikamilifu na haikuongeza neno wala kupunguza Neno.

Kufikika Mwaka 1611, tafsiri ya King James ilikuwa imeshasambaa katika bara la Ulaya yote, na baadaye duniani kote. Na tangu mwaka huo wa 1611 mpaka leo karne ya 21 ndio kitabu kinachoongoza kwa kuuzwa kuliko vitabu vyote duniani, na kumfanya Mfalme James, kuendelea kushika nafasi za juu za watu maarufu waliowahi kutokea.

Ni nini tunajifunza katika Mfalme Yakobo (King James).

Ni Mfalme ambaye alikuwa na hofu ya Mungu, ingawa hakuwa mkamilifu sana, lakini alitii na kuheshimu pendekezo la watu wa Mungu, ambao walimshauri aridhie ombi la kukitakasa kitabu kitakatifu cha Bwana, kwa kuondoa maoni ya watu na kukiacha kisafi kama kilivyo.

King James, aliruhusu pendekezo hilo pasipo kujua kuwa litaenda kuubadilisha ulimwengu. Mpaka Leo hii tafisiri bora ya kiingereza inayosomwa na wengi ni tafsiri hiyo ya King James. Na kwa kufanya hivyo Bwana akampa King James kumbukumbu la daima.

Ni wafalme wengi na mamalkia wengi wamekuja na kupita, wameandika vitabu lakini vitabu vyao vimepita, lakini kazi ya James mpaka leo inadumu na itaendelea kudumu hivyo mpaka Kristo anarudi.

Na sisi tukitaka tupate kumbukumbu la kudumu hatuna budi kumfikiri Mungu kwanza katika maisha yetu, haijalishi ngazi tuliyopo tuwe maskini, matajiri, tuwe wafalme tuwe watu wa kawaida.. tukimjali Bwana kwa mioyo yetu yote, na akili zetu zote na nguvu zetu zote, bali tuna kumbukumbu kubwa mbele zake si tu katika maisha haya, bali hata yale yajayo.

Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

 14 Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi? 

15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

 16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake.

 17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye”.

Bwana atubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

WHAT DOES IT MEAN TO BE A CHRISTIAN?

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

NI UTUKUFU WA MUNGU KUFICHA JAMBO.

Rudi nyumbani

Print this post

Haini ni mtu gani? Mithali 13:2

Tusome,

Mithali 13:2 “Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake; Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri”

Haini ni jina lingine la mtu ambaye ni “Msaliti”, mtu anayefanya usaliti juu ya mwingine ni sawa na kafanya “Uhaini”. Mtu anayeisaliti nchi yake mtu huyo ni Mhaini, vile vile  mtu anayeisaliti Imani yake yenye kumfikisha mbinguni, kwa kurudia mambo machafu mtu huyo anafanya uhaini kwa Mungu wake.

Zaburi 78:57 “Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa

 58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.

 59 Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.”.

Na maandiko yanazidi kuonyesha kuwa Wahaini wote wa imani watapata adhabu..

Zaburi 119:158 “Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako”.

Mithali 22:12 “Macho ya Bwana humhifadhi mwenye maarifa; Bali huyapindua maneno ya mtu haini.”

Soma pia Mithali 13:15 na Zaburi 25:3.

Kama tayari ulikuwa umeyakimbia machafu ya ulimwengu, na sasa umeyarudi nyuma fahamu kuwa huo unafanya uhaini mbele za Mungu, kimbia haraka sana msalabani ukatubu,  kama ulikuwa umeacha uzinzi na sasa umeurudia, tubu kwa machozi sana mbele za Bwana, leo hii ni nafasi yako ya kutubu na kumgeukia Mungu, usingoje kesho, na hakikisha unatubu kwa kumaanisha kabisa kutofanya hayo uliyoyafanya au unayoyafanya, na Bwana atakupokea lakini ukizidi kukawia upo hatarini sana…

 Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Sifa ni nini?

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Rudi nyumbani

Print this post

YESU KATIKA USINGIZI WAKE.

Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo.

Naamini kuwa ulishawahi kusoma katika maandiko kuwa kuna mahali Yesu alilala. Lakini ulishawahi kujiuliza ni kwanini habari ile iandikwe kulikuwa na umuhimu gani?

Kumbuka kila tukio lililoandikwa katika biblia limebeba somo kwetu sisi watakatifu.

Jambo pekee lililomfanya Yesu alale usingizi  mzito namna ile, sio kuchoka kama wengi wanavyodhani, kuna nyakati nyingi Yesu alikuwa anachoka kuliko hata hapa, lakini alikuwa halali, anapanda mlimani kuomba…lakini ni nini kilichompelekea alale?

Jambo lililompa Yesu usingizi mzito, ni ile DHORUBA iliyoanza kule baharini.

Marko 4:36-39

[36]Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.

[37]Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.

[38]Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?

[39]Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.

[40]Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado?

Umeona hapo, hakuna mahali popote biblia inarekodi Yesu alipitiwa na usingizi,  isipokuwa hapo kwenye dhoruba kuu.

Wakati wengine wanahangaika na matatizo, hawapati usingizi, wanapambana na changamoto zao..upande wa pili wa Yesu mambo ni tofauti,kule kuyumba kwa chombo kumbe ndio kulikuwa kunavuta usingizi vizuri.

Lakini ni nini Bwana anataka tujifunze juu ya tabia hii ya Kristo?

Ni kwamba hata yeye akiwa amejaa vizuri ndani yetu, tutadhihirisha tabia kama zake.

Ni kwanini leo hii tuna hofu ya maisha, tuna hofu ya kesho, tutaishije, tutakula nini, tutavaa nini? tuna hofu ya wezi, tuna hofu na kufukuzwa kazi, tuna hofu ya magonjwa?

Ni kwasababu Kristo hajajaa ndani yetu vizuri, ni kwasababu hatujapokea uhakika wa kuwa salama daima.

Wakristo wengi, wakiwa kwenye matatizo, mbalimbali hawana raha, wanapoteza utulivu..wanahangaika huku na kule kama wakina Petro. Hii ni hali ya kawaida ya kibinadamu. Lakini Yesu anaweza kukupa usingizi katikati ya tufani na dhoruba..endapo atajaa ndani yako vizuri.

Unachopaswa kufanya ni jiachie tu kwa Yesu, mwache yeye ahangaike na hiyo tufani, itaisha tu yenyewe, haitadumu muda mrefu, atakufungulia mlango wa kutoka katika hilo jaribu, haijalishi ni kubwa kiasi gani.

Jiachie tu kwa Yesu mtafakari yeye muda wote, muwaze yeye na uweza wake, Kama hujaokoka, hakikisha unafanya hivyo sasa, hivyo kwa jinsi utakavyokuwa unaendelea kumsogelea yeye ndivyo atakavyokupa wepesi kwa kukabiliana na mambo yote, na changamoto zote unazokutana nazo..Na hatimaye zitaisha tu bila hata kusumbuka kwasababu yeye yupo kazini.

Mkaribie Yesu sasa acha kuzitegemea akili zako mwenyewe..Naye atakusaidia, yeye mwenyewe anasema;

Mathayo 11:28-29

[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

[29]Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu

Anasema pia..

Mathayo 6:31-34

[31]Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

[32]Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

[33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

[34]Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.

Mkaribie Yesu, Akutue mizigo. Akupe uzingizi, akupe raha.

Zaburi 127:2 “Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Dia ni nini katika biblia? (Mithali 13:8)

Jibu: Tusome,

Mithali 13:8 “Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”.

Dia ni Kiswahili kingine cha neno “Fidia”, Kwahiyo hapo biblia inaposema “Dia” ya nafsi ya mtu ni utajiri wake, na maskini hasikii ogofyo lolote, maana yake ni kwamba “Fidia ya mtu anapokutana na matatizo ni itatoka katika vitu alivyonavyo” ikiwa na maana kuwa mtu anapokutwa na tatizo labda kasababisha hasara Fulani au kafanya kosa Fulani katika jamii, lililomsababishia apigwe faini, au kakutana na watu na kaingiliwa na wahalifu katika nyumba yake, basi Mali alizo nazo zinaweza kuwa fidia kwaajili ya uhai wake, maana yake anaweza kuwapa wale watu sehemu ya mali zake na akaisalimisha roho yake.

Lakini mtu asiye na kitu kabisa (yaani Yule maskini kikweli kweli), huwa hawezi kupokea vitisho vyovyote, hakuna jambazi yeyote anayefikiria kwenda kuvunja nyumba ya maskini akiwa na mtutu ili amwibie mali zake.. Ikiwa na maana kuwa, maskini siku zote yupo huru!.. hafuatiliwi na mtu, wala hakuna mtu ana habari na maisha yake (hapokei ogofyo lolote).

Ni hekima gani tunaipata hapo? Au ni nini tunajifunza hapo?

Ili tuelewe ni nini tunajifunza hapo, hebu tuanzie kusoma kuanzia mstari wa 7

Mithali 13:7 “Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu; Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.

8 Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote”

Hii ni hekima ambayo inaweza kutusaidia kuwa salama..sio lazima tuwapo na mali, tujionyeshe kuwa na mali kwa watu!, ndio maana hapo biblia inasema “kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.”.. Unapokuwa mtu wa kujionyesha mbele za watu mali ulizo nazo, unajiweka katika hatari ya kutoa DIA (Fidia) kwaajili ya uhai wako, kwasababu kila mtu atatamani hizo mali ulizo nazo, utavutia watu waovu na wasio waovu, utavutia majambazi, utavutia wenye mamlaka na watu  wapendao rushwa n.k

Hivyo hekima ni kujiweka katika maisha ya wastani, hata kama unazo mali nyingi, si lazima ujulikane wewe ni tajiri kuliko wote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je watu wa kale walitumia vifaa gani kuandikia?

Watu wa kale walitumia wino, na kalamu pamoja na karasati kuweka kumbukumbu zao kama tunavyofanya sasa..

Isipokuwa wino wao, kalamu zao na karatasi zao zilikuwa tofauti na hizi tunazotumia sasa..

Mtume Yohana katika nyaraka zake aliandika hivi; 

3 Yohana 1:13

[13]Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu. 

Kuonyesha kuwa unandishi wao ulitegemea wino na kalamu, kama tu huu wetu.

Je! Wino wa kale ulitengenezwaje?

Tofauti na huu wa kwetu unaotengenezwa na kemikali mbalimbali..wino wa zamani ulikuwa unatengenezwa na MASINZI. Masinzi hayo yalikuwa yanavunwa aidha kutoka  katika mafuta yaliyochomwa au kuni pale yanapoganda katika chombo kama sufuria kwa pembeni.

Wino wa kale

Sasa yalipokusanywa kama poda, baadaye yanachanganywa na gundi inayotoka katika mmea wa mpira..lengo la kufanya hivyo ni kuufanya wino huo ushikamane vizuri ili  wakati wa uandishi wino usitapakae ovyo.

Hivyo mwandishi anapoununua wino huo anachofanya ni kuchanganya na maji, kisha kutumia kalamu yake kuchovya na kuandika katika hilo karatasi lao.

Je! Kalamu zao ziliundwaje

Tofauti na kalamu zetu hizi, ambazo zinatengenezwa kwa mirija ya pastiki na chuma. Kalamu za zamani ziliundwa na mmea ujulikanao kama MWANZI ambayo hata huku sehemu kadhaa hutumika.. Mianzi hii ilichongwa kwa pembeni kuacha ncha. Ili kuruhusu wembamba wa uandishi katika karatasi  kama tu kalamu zetu za kisasa zilivyo.Tazama picha.

Kalamu za kale

Je karatasi za kale zilikuwaje?

Karatasi za zamani zilifanana hizi isipokuwa zenyewe zilikuwa ni nene, ziliundwa na mmea ujulikanao kama mafunjo(Ayubu 8:11).

Mmea huu ulichongwa kulingana na ukubwa wa karatasi, kisha kuchanjwa chanjwa katika vipisi vidogo, ambavyo baaadaye vililowekwa katika maji ili vilainike..kisha vinawekwa katika ubao ulionyooka, kisha vinalazwa kipisi kimoja baada ya kingine, na vingine kupita kwa kukatiza..kisha panawekwa ngozi ya mnyama kwa juu , na baada ya hapo kukandamizwa, ili vipisi hivyo vishikane,

Na kuachwa siku kadhaa, baadaye wakitoa, tayari karatasi hiyo nene hutokea… ngumu na imara kuliko hata hizi tulizonazo sasa. Ndizo walizotumia watu wa kale kuandikia.

karatasi za kale

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu? Umejiandaaje? Ikiwa bado hujafanya hivyo na unahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Yerusalemu ni nini?

Kaniki ni nini katika biblia? (Yeremia 8:21).

Karismatiki ni nini?

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Rudi nyumbani

Print this post

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

Zaburi 147:3 Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao.  4 Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.  5 Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.

Ukitazama juu unaona nyota nyingi sana zisizo na idadi, mbali na hizo zilizo ndani ya upeo wa macho yetu, lakini pia zipo nyingine tusizoziona ambazo idadi yake ni mabilioni kwa mabilioni, matrilioni kwa matrilioni,..

Lakini hapa Mungu anatupa siri ya uweza wake, anasema zote hizo amezihesabu na kuzipa majina,..

Sasa Kwanini atuambie jambo kama hilo?

Ni kutuaminisha kuwa ikiwa anazifahamu  nyota zote zilizo mbali, nje-ndani, atashindwaje kutufahamu sisi? Atashindwaje kuziona taabu zetu na shida zetu, atashindwaje kuyaona mateso yetu na majeraha yetu?

Hivyo hapo anaposema ‘Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao’. Anamaanisha, huweza kutufanya upya, endapo tutamkaribia.

1Petro 5:7  ‘huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu’.

Mkaribie Kristo akuponye kwasababu yeye yupo karibu sana na wewe zaidi ya nyota za angani.

Utukufu na uweza vina yeye milele na milele amina.

Maombi Yangu:

“Baba mwema, tumeona uweza wako, juu ya ulimwengu wako uliouumba, kwamba hakuna lolote usilolijua,wala usiloliweza, na sasa ninakukaribia Baba wa Upendo, kama ulivyoahidi kwenye Neno lako kwamba utaziganga jeraha zangu, Naomba sasa niponye moyo wangu, na mwili wangu, nifanye upya tena, nisimame mbele zako, nikutumikie. Ni katika jina la Yesu naomba nikuamini. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NYOTA ZIPOTEAZO.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

Agano ni nini? na kuna aina ngapi za maagano?

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kosa gani alilolifanya Eli, ilihali aliwaonya watoto wake?

SWALI: Kwanini Mungu alimuadhibu Eli kwa kosa la kutowaonya watoto wake, angali tunasoma katika maandiko aliwaonya hapo kabla?

Tusome;

1Samweli 2:22 Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania. 

23 Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote.  24 Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa Bwana. 

25 Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa Bwana, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu Bwana amekusudia kuwaua.

Lakini Hapa Mungu anasema…

1Samweli 3:12 Siku hiyo nitayatimiza maneno yale yote niliyoyasema juu ya Eli katika habari za nyumba yake, tangu mwanzo hata mwisho. 

13 Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye HAKUWAZUIA. 

14 Na kwa hiyo nimeapa juu ya nyumba ya Eli, ya kwamba uovu wa nyumba ya Eli hautasafika kwa dhabihu wala kwa sadaka hata milele.


JIBU: Kibiblia “Kuonya” sio tu kusema kwa mdomo, bali pia kuchukua hatua stahiki, endapo maonyo hayatatekelezwa. Eli ni kweli aliwaonya watoto wake, kwa dhambi walizokuwa wanazifanya madhabahuni pa Mungu, lakini aliendelea kuwaangalia, wakifanya mambo yao maovu bila kuwaondoa katika nafasi zao. Ndio maana hapo kwenye 2Samweli3:13 Mungu anamwambia Samweli, kwamba HAKUWAZUIA. Hakuwaondoa katika kazi ya utumishi, Pengine kwasababu ni watoto wake, warithi wake, akawastahi zaidi ya  Mungu. Hivyo wakati wa adhabu ulipofika yeye naye alishiriki adhabu ile.

Hili ni funzo, pia kwa viongozi wote wa imani, nyakati hizi tunazoishi, kanisa limegeuzwa kama mahali pa kila mtu kujiamulia jambo lake, na viongozi wanaona wanafumbia macho. Utakuta mchungaji ni mzinzi, lakini askofu akipata taarifa, badala wamwondoe katika ofisi ile, wanamwonya tu, kisha wanamuhamisha dayosisi, wanamstahi, na akifika kule anaendelea na maovu yake, anahamishwa tena dayosisi.

Utakuta watoto wa wachungaji, ni walevi, hawana maadili, lakini wanaendelea kubaki katika nafasi za wazee wa kanisa au waimbaji kwaya. Mchungaji akiambiwa, anachokifanya ni kuwaonya tu, lakini bado wanaendelea kushika nafasi hizo za madhabahuni. Hii ni hatari. Mungu anataka hatua stahiki zifuatane na maonyo kama hakuna mabadiliko.

Hivyo kama wewe ni kiongozi, kumbuka maonyo yako ni lazima yaambatane na vitendo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo?

IKABODI MAANA YAKE NI NINI?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Baraka ni karama ya Mungu, na kila mmoja wetu aliyekombolewa na Yesu, ahadi hiyo ni yake. Baraka zimegawanyika mara mbili, zipo baraka za mwilini, na baraka za rohoni. Lakini kubwa zaidi ni zile za rohoni. Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyoeleza Baraka za Mungu. Lakini pia ikiwa utapenda kupata vifungu mbalimbali, pamoja na mafundisho mazuri ya Neno la Mungu, bofya link hii uweze kujiunga na kundi letu la Whatsapp>>> WHATSAPP GROUP

Wafilipi 4:19  “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu”

Yakobo 1:17  “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”.

Hesabu 6: 24 “Bwana akubarikie, na kukulinda;  25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;  26 Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”

3Yohana 1:2  “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”

2Wakorintho 9:8  “Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;”

Kumbukumbu 28:2 “na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.  3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.  4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.  5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.  6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo”.

Waefeso 1:3 ” Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;”

Mathayo 6:30 ” Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? 31  Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32  Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33  Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34  Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”

Malaki  3:10 “Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Zaburi 20:4 “Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote”.

Mathayo 5:6  “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.

Mithali 16:3 “Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika”

Yeremia 17:7 “Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”

Pia Kwa wokovu/ maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU KIFO.

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

MISTARI YA BIBLIA YA UPONYAJI.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Huu ni mfululizo wa masomo maalumu kwa ajili ya wanawake: Ikiwa hukupata chambuzi nyingine za nyuma basi fungua link hii  uweze kuzipitia >>>   MAFUNDISHO KWA WANAWAKE

Mwanzo 34:1-3 Inasema..

“Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, AKATOKA KUWAONA BINTI ZA NCHI.  2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri.  3 Moyo wake ukaambatana na Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana, akasema na huyu msichana kwa maneno mazuri”

Dina alikuwa ni binti wa Yakobo, aliyejitunza na kujiheshimu, alikaa chini ya Mama zake akifundishwa desturi za uzao wa Ibrahimu unavyopaswa uwe. Akafahamu kuwa uzao wao haupaswi kuchanganywa na uzao wa ukoo mwingine, Ili Baraka ya Ibrahimu aliyoahidiwa kwa uzao wake isiingiliwe na doa.

Lakini Tunaona, jambo moja alilolifanya Dina, ambalo pengine hakujua mwisho wake utampelekea pabaya. Na jambo lenyewe “ni yeye kutoka na kwenda kuonana na mabinti wa nchi”. Kama msichana alipoona mabinti wa mataifa mengine, wanaishi maisha ya kidunia, maisha ya anasa, maisha ya ukisasa. Na yeye naye akatamani kwenda kuunga urafiki nao, bila kujua mwisho wake utakuwaje.

Hivyo kidogo kidogo, akaanza kuchukuliwa na desturi za wanawake wa kidunia, akaanza kujichanganya, siku ya kwanza, siku ya pili, wiki ya kwanza wiki ya pili, mwezi wa kwanza, mwezi wa pili. Kidogo kidogo wale mabinti wa kidunia waanza kumfundisha tabia mbaya..Pengine wakaanza kumwambia “Mbona wewe ni mrembo, hadi sasa huna boyfriend”..Mbona una shepu zuri, embu vaa hizi nguo fupi uonekane na wanaume..Embu twende leo disco, tukakutane na vijana wenzetu, tule maisha, ujana maji ya moto..

Akawa anawasikiliza, na huko ndipo akakutana na huyo Shekemu, akamlaghai, kisha akambikiri..Taarifa zikawafikia ndugu zake, wakakasirika sana Simeoni na Lawi, hadi kufikia kitendo cha kwenda kuwaua watu wote wa huo ukoo. Kwasababu waliona tendo alilofanya Dina, ni chukizo kubwa sana kwa jamii yao. Kuuchafua uzao uliobarikiwa, kuvunja maagano ya Mungu.

Nini Bwana anataka mabinti na wanawake wajifunze?

Kabla ya kuanguka katika dhambi, ushawihi huwa unaanza kwanza kwa marafiki wanaokuzunguka.  Angalia ni watu wa namna gani uliozoena nao, au uliounga urafiki nao, au unaokaa nao muda mrefu. Mabinti wengi waliookoka, hawajafundishwa kuvaa vibaya na wanaume wazinzi, bali na mabinti wenzao, hawajafundishwa kwenda disco au kunywa pombe na wanaume, bali mabinti wenzao. Hawajafundishwa kwenda kwa waganga na kaka zao, bali wanawake wenzao, hawajafundishwa kusengenya na jamii, bali ni wanawake wenzao wanaokutana nao masaluni na mabarazani.

Hawa ndio maadui wa kwanza. Dina hakutoka kwenda kumtafuta Shekemu, alitoka kuwatazama mabinti  tu wa kidunia na huko huko wakamuunganishia Shekemu. Laiti angetulia nyumbani akakaa na wale wabinti wenzake wa ukoo mmoja hata kama ni washamba, angekuwa salama.

Wewe kama mwanamke usipende kuunga urafiki na wanawake ambao hawajaokoka, ambao hawana habari na Mambo ya ufalme wa mbinguni, upo chuo, upo shuleni, upo kazini, ni heri ubaki kivyako vyako, kuliko kujiingiza hatarini. Siku zote uangamivu unavyokuja huwa unaanzia mbali sana, hivyo kuwa makini, tafuta watu waliodhamiria kuishi maisha matakatifu, hao ndio wawe marafiki zako wa karibu, washauri wako, uige tabia zao, kataa kampani za kipepo, acha wakuone mshamba, lakini roho yako ipo salama, acha upitwe na fashion, acha upitwe na uzuri lakini jina lako lipo katika kitabu cha uzima.

Majira tunayoishi ni ya kung’ang’ania kwa nguvu wokovu tuliopewa, ni kuwa siriazi kweli kweli, kwasababu maelfu kwa maelfu ya watu wanaangamia, wanashindwa kumaliza mwendo wao salama hapa duniani wanaponzwa na marafiki, Unadhani na sisi tukiwa walegevu, tunadhiria kila kitu tu kinachokuja mbele yetu, tutawezaje kupona. Njia imesonga, mlango ni mwembamba, tunajiingiza kwa nguvu, isitoshe muda tuliobakiwa nao ni mchache. Hivyo hatupaswi kuwapa nafasi watu wakidunia katika maisha yetu.

Tujifunze kwa Dina. Tuwe salama. Kataa, kampani za kipepo!

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO KWA WANAWAKE

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

MAZUNGUMZO MABAYA HUHARIBU TABIA NJEMA.

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; (Mithali 11:16)

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post