Title January 2024

Madirisha ya mbinguni ni nini/yapi?(Mwanzo 7:11)

Ni neno lenye maana zaidi ya moja, kwamfano katika vifungu hivyo, Lilimaanisha chemchemi za maji zilizokuwa juu ya anga, Mungu alizifungua, mvua ikaanza kunyesha bila kipimo au kiasi, usiku na mchana kwa  siku arobaini.

Mwanzo 7:11 Katika mwaka wa mia sita wa maisha ya Nuhu, mwezi wa pili, siku ya kumi na saba ya mwezi, siku ile chemchemi zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu, madirisha ya mbinguni yakafunguka.  12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku

Utakumbuka kuwa katika siku ile ya pili ya uumbaji, Mungu aliyatenga maji ya juu na ya chini (Mwanzo 1:6-7). Sasa yale ya juu, aliyaachia yote, yakawa yanashuka juu ya nchi na matokeo yake yakaifunika tena dunia. Hayo ndio madirisha ya mbinguni yaliyofunguliwa.

Ni neno pia linalomaanisha, Baraka za Mungu nyingi.

Kwamfano katika vifungu hivi, lilimaanisha hivyo;

Wafalme 7:2 Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.

Hichi ni kile kipindi, Israeli imepitia njaa kali kiasi cha watu kulana, lakini Elisha akatokea na kumwambia Yule mkuu wa mfalme, kwamba Bwana atawaletea Baraka nyingi siku hiyo, na chakula kitakuwa kama si kitu tena Israeli. Yeye akadhihaki na kusema hata kama Mungu akifungua milango yake yote ya mbinguni  (Baraka) hilo jambo haliwezekani ndani ya siku moja. Elisha akamwambia utaliona kwa macho yako, lakini hutakula chochote katika hivyo.

Vilevile katika vifungu hivi, utaona vikimaanisha Baraka pia;

Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Bwana anataka tumjaribu kiutoaji, ndipo atafanya muujiza wa kutufungulia Baraka zake nyingi ambazo hazitatosha hata mahali pa kuzihifadhia.

Hivyo Neno hili kibiblia lilimaanisha, hukumu ya Mungu iliyopitiliza, au Baraka za Mungu zilizopitiliza kufuata na tukio lenyewe lililoambatana nalo.

Bwana akubariki.

Je! Unatamani kushiriki Baraka zote za Mungu rohoni? Unatamani madirisha ya mbinguni yafunguliwe juu yako. Kama ni ndio basi sharti uokoke, umkabidhi Kristo maisha yako, kwa kutubu dhambi zako na kuwa tayari kumfuata Kristo, ili upate ondoleo la dhambi zako.

Ikiwa utapenda mwongozo wa sala ya kumpokea Kristo, baada ya toba yako ya kweli. Basi fungua hapa kwa sala hiyo>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NUHU WA SASA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”

JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuharimishwa ni nini, na kwanini Paulo aombe hivyo?(Warumi 9:2).

Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri tuanzia ule mstari wa kwanza, na tusome mpaka ule wa 5

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

3  Kwa maana ningeweza kuomba MIMI MWENYEWE NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO KWA AJILI YA NDUGU ZANGU, JAMAA ZANGU KWA JINSI YA MWILI;

4  ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;

5  ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina”

“Kuharimishwa” maana yake ni “kutengwa mbali na mtu/kitu (kwa ufupi kufanywa haramu)”.

Paulo aliomba kama ingewezekana Aharamishwe kwaajii ya ndugu zake katika mwili (yaani waisraeli), ili waokolewe.

Sasa kwanini aliomba vile, na je jambo hilo linawezekana?

Awali ya yote ili tuelewe vizuri hebu tuweke msingi kwanza kwa kuelewa agenda ya Wokovu ulioletwa na YESU KRISTO.

Wokovu kwamba ulianzia kwa Wayahudi, (soma Yohana 4:22) na baadaye ukahamia kwa watu wa mataifa.

Na kipindi Wokovu (injili) inahubiriwa kwa wayahudi, sisi watu wa mataifa tulikuwa tumeharimishwa, maana yake tulikuwa tumetengwa mbali na injili/neema, na kufanyika watu tusiostahili..

Waefeso 2:11 “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili, mnaoitwa Wasiotahiriwa na wale wanaoitwa Waliotahiriwa, yaani, tohara ya mwilini iliyofanyika kwa mikono;

12  kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, MMEFARAKANA NA JAMII YA ISRAELI, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. MLIKUWA HAMNA TUMAINI, HAMNA MUNGU DUNIANI”

Umeona?..kumbe kuna wakati sisi watu wa mataifa hatukuwa na Mungu (neema),Na wakati ulipofika waisraeli (wayahudi) walipomkataa Masihi YESU KRISTO, na kusema yeye siye yule aliyetabiriwa, Ndipo Ikafanya Neema iondoke kwao na kuja kwetu sisi watu wa mataifa, hivyo nao pia WAKAHARIMISHWA ili sisi tupate Neema..

Sasa Utauliza hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko..

Warumi 11:30 “ KWA MAANA KAMA NINYI ZAMANI MLIVYOMWASI MUNGU, LAKINI SASA MMEPATA REHEMA KWA KUASI KWAO”

31  KADHALIKA NA HAO WAMEASI SASA, ILI KWA KUPATA REHEMA KWENU WAO NAO WAPATE REHEMA.

Soma pia  Matendo 28:28 na Matendo 13:46,utaona jambo hilo Zaidi.

Sasa Mtume Paulo kwa kulijua hilo kwamba “Neema imewaondokea Wayahudi wengi” na imeenda kwa watu wa MATAIFA, kwa mantiki hiyo hiyo akatamani kama ingewezekana IONDOKE kwake (yaani aharimishwe), ili irudi tena kwa WAISRAELI ndugu zake wapate kuokolewa.

Na neema ikiondoka juu ya mtu/watu maana yake ile nguvu ya kumwamini KRISTO inakuwa haipo tena!, kila kitu kumhusu YESU ni upumbavu kwa mtu huyo au watu hao, (Mfano wa PAULO alivyokuwa kabla ya kuokoka..alikuwa anaona injili ni upuuzi na Zaidi sana alikuwa anawaua wafuasi wa BWANA YESU). (Hiyo yote ni kutokana na neema kutokuwepo juu yake).

Sasa swali ni je! Jambo hilo aliloliomba Paulo linawezekana?..yaani Mungu anaweza kumharimisha yeye ili ndugu zake wapone?

Jibu ni LA! Ni jambo ambalo haliwezekani,..Paulo alisema vile kutokana na huruma na upendo kwa ndugu zake!..Ni sawa na mtu aliye mzima, aone ndugu yake anateseka na ugonjwa mbaya..na aombe ahamishiwe yale maumivu kwake kutokana na kumhurumia yule mgonjwa, na ndivyo Paulo alichokuwa anakiomba.

Kadhalika Mungu hawezi kuihamisha Neema aliyokupa na kuipeleka kwa mtu mwingine kwa wewe kumwomba...(hawezi kukupokonya uzima wa milele ikiwa umestahili uzima wa milele) Neema huwa inaondoka kutoka kwa mtu kwa njia ya matendo yake(kama matendo yake yakiwa hayafai, lakini si kwa kumwomba Mungu aihamishe kutoka kwako.

Je umeokoka?..kama bado unasubiri nini?

Fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho na BWANA YESU yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Rudi nyumbani

Print this post

Yahu ni nani? (Wimbo 8:6).

Jibu: Turejee,

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni MIALI YA YAHU”.

“YAHU” ni jina lingine la “YAHWE” ambalo ndilo “YEHOVA”.

Kutoka 6:2 “Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao”.

Kwahiyo YAHU, YAHWE na YEHOVA ni jina Moja!

Lakini hapo katika Wimbo 8:6 maandiko yanasema kuwa “upendo una nguvu kama mauti”.. maana yake kama vile mauti ilivyo na nguvu kiasi kwamba wanaokufa ni ngumu kurudia uzima! Vile vile Upendo wa Mungu kwetu ni mkuu kiasi kwamba akitupenda ametupenda!, hakuna wakati atatuchukia, anaweza asipendezwe na sisi lakini si kutuchukia!.

Warumi 8:35 “Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?………

38  Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39  wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Lakini pia anasema wivu ni mkali kuliko Ahera..Ahera ni “Kaburi”, Kwa urefu Zaidi fungua hapa >>>Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Na miali yake ni miali ya YAHU. Maana yake ni kuwa Mungu ana upendo lakini pia anawivu, huwezi kamwe kutanganisha vitu hivi viwili, UPENDO na WIVU.

Kwahiyo kama Mungu ametupenda, basi hapendi kuona tunaabudu miungu mingine, tukifanya hivyo tunamtia yeye wivu, umbao unaweza kutupeleka kaburini (Ahera).

Kutoka 20:3 “Usiwe na miungu mingine ila mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, NI MUNGU MWENYE WIVU; NAWAPATILIZA WANA MAOVU YA BABA ZAO, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE CHA WANICHUKIAO, 

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

YAHU atusaidie tusimtie Wivu, lakini tumpende, na vile vile upendo wake utubidiishe katika kuyafanya mapenzi yake.

Maran atha.

Mafundisho Mengine:

Wivu ni nini na kuna aina ngapi za Wivu?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Rudi Nyumbani:

 

Print this post

JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.

Kuna vitu ambavyo Mungu amepanga, vitokee kwa njia ya asili, na vingine amepanga vitokee ndani ya wakati wake alioukusudia.  Kwamfano ikiwa amekusudia baada ya miaka kumi ndio uone majibu ya lile hitaji ulilomwomba, yeye mwenyewe ataanza kukuandalia njia sasa, na hatimaye ule wakati ukifika basi atafungua njia ya kukipata.

Lakini vipi kama utakihitaji kwa majira haya ya sasa. Na wakati huo huo iwe ni mapenzi ya Mungu na sio yako. Je hilo linawezekana? Maana yake ni kuwa  uivuruge mipango yake ili afanye sasa hivi kile unachokihitaji. Je! Mungu anaruhusu tuwe watu wa namna hiyo?

Jibu ni ndio.

Na aliyetufundisha siri hiyo si mwingine zaidi ya Kiongozi wetu mkuu wa imani YESU KRISTO.

Embu tafakari haya maneno aliyoyasema.

Luka 18:1  Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. 2  Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3  Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu. 4  Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5  lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. 6  Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. 7  Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8  Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?

Katika vifungu hivyo ni wazi kuwa Bwana anajifananisha na huyo kadhi, ambaye hakuwa tayari kumsaidia Yule mwanamke mjane haja yake kwa wakati ule.  Lakini kutokana na hatua alizozichukua Yule mwanamke ilimbidi tu ampe kama alivyotaka.

Na ndivyo ilivyo kwa Mungu wako. Upo wakati unaweza kupata kile unachokitaka kwa wakati wako, na si kwa wakati wa Mungu? Zipo kanuni ambazo ukizitumia, zitakusaidia kuuvuta msaada wa Mungu kwa haraka zaidi.

Kanuni ya kwanza: Ni kuomba bila kukata tamaa.

Maombi ya kung’ang’ana yanaugusa sana moyo wa Mungu, zaidi ya sisi tunavyoweza kufikiri. Kwa bahati mbaya ni pale tunapoona Mungu amekaa kimya tunadhani, hasikii. Yeye mwenyewe anasema aliyeumba sikio utasemaje hasikii?? Tangu lini?. Mungu huwa anasikia, lakini anasubiri umakini wako wa kile unachokililia kwake, Kama alivyofanya huyo mwanamke. Kiwango chako cha kutokata tamaa, hupelekea majibu ya haraka ya maombi yako. Ukiomba leo hujaona kitu, unaendelea hivyo hivyo kesho, ikiwa kesho haipo, unaendelea kesho kutwa..hivyo hivyo hata kama ni kwa miaka 5, hakuna kusema, Mungu hatendi, au amenisusa. Omba bila ukomo, tena huku ukiamini asilimia mia kuwa  Bwana analishughulikia ,Usibahatishe kuomba. Utapokea kinyume na wakati.

Kanuni ya pili: Kustahimili vipingamizi.

Vipingamizi vinaweza kutokea kwa wanadamu, na wakati mwingine hata katika Neno la Mungu. Kwa wanadamu ni kama vile kuvunjishwa tamaa. Na kuambiwa Mungu hayupo na wewe, au umemkosea Mungu. Hilo unaweza kukumbana nalo sana. Lakini vilevile, Mungu anaweza kukuuliza, unataka upokee hili kwa sifa ipi uliyonayo? Wewe utamjibuje? Hilo nalo utakumbana nalo moyoni mwako.

Embu fuatilia kisa hiki.

Mathayo 15:22  Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23  Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. 24  Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25  Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie. 26  Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 27  Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28  Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Huyu mwanamke, alihitaji wokovu ambao wakati wake ulikuwa bado kwa watu wa mataifa, kwasababu Yesu alikuwa bado hajasulibiwa. Hivyo alipojaribu tendo ambalo lilikuwa ni gumu masikioni mwa watu. Moja kwa moja alikutana na vipingamizi. Cha kwanza ni kutoka kwa mitume walipoona Bwana hamjibu lolote, wakaanza kutaka afukuzwe, kwasababu anasumbua watu. Anapiga-piga kelele ovyo, anawavunjia wayahudi heshima, mpagani huyu. Lakini yeye hakujali yale maneno.

Baada ya hapo  akakumbana na Bwana mwenyewe, ambaye hapo mwanzo alimtazama wala hakumjibu neno lolote. Kumbuka, tabia hiyo ya kutojibu watu hakuionyesha kwa huyu mwanamke tu, bali kwa watu wengine pia, lakini huyu tu habari yake ndio imerekodiwa kwasababu ya kitu alichokifanya. Na alipoambiwa habari za mbwa, hakusijikia vibaya, akawa na hoja hapo hapo za kutetea, kwamba hata mbwa wanapata yale masalio yaangukayo kutoka mezani mwa bwana zake. Na mwisho wa siku akapokea alichokihitaji kinyume na taratibu.

Vilevile na wewe unachomwomba Bwana, atakuuliza una vigezo gani vya kupokea hiki. Hezekia alikuwa na hoja za kumpa Bwana na hatimaye akaongezewa maisha kwa kuponywa ugonjwa wake. Na wewe pia jiandae kwa hoja nzito, na majibu yako kwa Bwana daima yawe ni haya “Bwana sistahili kupokea, lakini Kristo tayari alikufa kwa ajili yangu msalabani, kunistahilisha mbele zako  ndilo linalonipa ujasiri huu wa kupokea chochote mbele zako kwa imani sawasawa (Waebrania 4:16)”. Ukifanya hivyo jiandae kupokea unachokihitaji.

Kanuni ya tatu: Tenda jambo la ziada:

Tendo la ziada, huvuruga mipango mingi ya Mungu. Kwamfano usipende kumwendea Mungu vilevile kwa desturi na mazoea ya sikuzote. Onyesha uhodari Fulani kwa Mungu, onyesha imani Fulani kubwa kwa Mungu. Mara nyingi Yesu alikuwa anafuatwa na Jeshi kubwa la makutano na kila mmoja alikuwa anahitaji ahudumiwe. Lakini utagundua wapo waliowahi kuhudumiwa kwasababu ya imani yao, na matendo yao ya kipekee kwake.

Zakayo hakufuata mkumbo, alibuni njia yake akapanda juu ya mkuyu Bwana akamwona. Yule mwanamke aliyetokwa na damu, hakufuata mkumbo, aliamini nikigusa tu pindo la vazi la Yesu nitapona. Yesu akaghahiri mwendo wake ili amtafute. Wale vipofu wawili Yeriko, waliposikia Yesu anapita, walipaza sauti zao kwa nguvu, wakisema Yesu turehemu. Yesu akawaponya

Vivyo hivyo na wewe, fanya jambo la ziada kwa Mungu wako. Kama ni kumsifu basi msifu zaidi ya kawaida ya sikuzote, uone kama hatafanya jambo kwako la ajabu. Kama ni kumtolea Mungu Mtolee zaidi ya kile kipimo cha kawaida. Fanya jambo kuu. Jimalize kwa ajili ya Bwana kwa kitu Fulani,  Utaamsha moyo wa Mungu akuhudumie kwa haraka sana.

Kanuni ya nne: Pia kuwa mfungaji.

Esta, aliweza kuuvuruga utaratibu wa mfalme. Siku ambapo alipanga kumwendea bila kualikwa. Utaona kuwa alifuata kanuni ya kufunga pamoja na watu wake kwa siku tatu. Ndipo akamkabili mfalme. Na mfalme akatii jambo lile. Kwasababu ilikuwa ni kifo kumfuata mfalme kama hajakualika.

Vivyo hivyo na wewe umwombapo Mungu jambo fulani, hakikisha unaambatanisha mifungo. Kwasababu hiyo hukuongozea umakini wako mbele za Mungu.

Ikiwa utafuata utaratu huo, basi uwezekano wa kupokea mahitaji yako kinyume na njia za kawaida ni mkubwa sana. Uombapo katika eneo lolote liwe gumu au jepesi Bwana atakumulikia nuru zake.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

IJUE KANUNI YA KUREJESHA NGUVU ZA KIROHO.

Rudi nyumbani

Print this post

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

Falaki ni nini katika biblia?

Jibu: Turejee,

Isaya 47:12 “Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda. 

13 Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na WASIMAME HAO WAJUAO FALAKI, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata”.

“Falaki” ni “elimu ya nyota na sayari na jua”.

Wanaofanya Falaki, wanaamini kuwa  “mpangilio wa nyota, mwezi na jua na sayari angani, unaathiri tabia ya nchi na tabia ya mtu/watu”. Jambo ambalo kwa sehemu moja ni kweli na sehemu nyingine uongo!.

Ni kweli Mpangilio wa Jua na mwezi, unaweza kuathiri tabia ya nchi, kama  vile vipindi vya mvua, kiangazi, au kipupwe….ipo miezi ambayo mvua inanyesha, na miezi ambayo mvua hainyeshi, ipo miezi ya kiangazi na miezi ya kipupwe…Majira ya mwezi wa 6 na 7 ni Kipindi ambacho jua linakuwa mbali na dunia na kweli nchi inaathirika na baridi kali, katika ukanda wa kusini wa dunia.

Vile vile tabia za mimea zinaathiriwa na majira na nyakati, yanayotokana na mpangilio wa mwezi na jua angani, mfano tabia za miembe kuzaa maembe zinaathiriwa na mwezi wa 12, kwamba yanapofika majira ya mwezi huo wa 12 mpaka wa 1 basi miti yote ya miembe inazaa sana, tofauti na kipindi kingine chote (kwahiyo kwa sehemu ni kweli).

Sasa kwa mantiki hiyo wana-falaki wanaamini kuwa kama mpangilio wa jua, mwezi na nyota angani unaweza kuathiri mazingira na hali ya hewa, basi vile vile mpangilio huo huo unaweza kuathiri tabia za watu, na hisia zao, na maamuzi yao na hata hatima yao!.

Kwamba kila tarehe na mwezi unabeba matukio yake kulingana na mtu na mtu, na pia kulingana na tarehe aliyozaliwa, vile vile mpangilio wa nyota na mwezi unaweza kuelezea ni kitu gani mtu atafanya, au atakitenda, au kitampata, vile vile ni bahati gani ipo mbele yake au hatari gani inamkabili.

Kwahiyo wote waliohitaji kujua mambo yatakayowapata mbeleni waliwatafuta hawa wana-Falaki, au kwa lugha nyingine wanajimu kujua hatima zao.

Lakini swali ni je! Elimu hii ina ukweli wowote na je wakristo ni sahihi kuitafuta, ili kujua hatima zetu kupitia falaki?

Jibu ni LA! Elimu hii haina ukweli wowote, mpangilio wa sayari na nyota, na mwezi hauwezi kuelezea tabia, hisia, maamuzi au hatima ya Mwanadamu!…mpangilio huo unaweza kufaa katika utabiri wa hali ya hewa na misimu ya kupanda na kuvuna (tena kwa sehemu ndogo) lakini hauwezi kutabiri maisha ya mtu.

Maisha ya mtu hayatabiriwi wala kusomwa kwa kutazama jua, au mwezi au nyota au sayari, kama ndivyo kulikuwa hakuna haja ya Kristo kuja, au hata kama angekuja basi angetuhubiria sana hiyo elimu, bali maisha ya mtu yanatabiriwa kwa KULITAZAMA NENO LA MUNGU peke yake!.

Ukitaka kujua kesho yako itakuwaje, isome biblia, itakuambia sio tu kesho utakuwa wapi, bali MILELE UTAKUWA WAPI!!!.

Utauliza vipi wale Mamajusi, mbona walioiona nyota ya Bwana YESU kutoka mashariki?.

Mungu alipenda kutumia ishara ya nyota kuelekeza utukufu wa mwanae alipozaliwa, lakini hakuwa anahubiri elimu ya nyota pale!, ni sawa na alivyotumia ishara ya Nguzo ya wingu au nguzo ya moto juu ya wana wa Israeli walipokuwa jangwani,.. ilikuwa ni kwa lengo la kuelekeza utukufu wa wana wake mahali walipo, lakini hakuwa anahubiri elimu za mawingu na moto, kwamba zikasomwe kwa bidii ili kuelezea utukufu juu ya mtu/watu.

Vile vile leo hii shetani anapenyeza elimu hii ya Nyota(Falaki) ndani ya kanisa kwa kasi sana!. Elimu hii inatoka kwa waganga na inahamia kanisani kwa kasi sana..Watu hawasomi tena biblia wanatafuta kusomewa nyota zao! Hawaombi tena kulingana na Neno wanaombea nyota kwa kurejea elimu ya falaki.

Ndugu usidanganyike!..Elimu ya nyota (Falaki) ni elimu ya shetani asilimia mia.

Kama unataka kusafisha hatima yako itii biblia, wala usitafute maombi ya kutakasiwa nyota!, hiyo ni elimu nyingine!… Vile vile ukitaka kujua kesho yako itakuwaje kasome biblia, usitafute utabiri wa kusomewa nyota kutoka kwa yoyote yule iwe mganga au anayejiita mtumishi wa Mungu.. Biblia pekee ndiyo itakayokuonyesha tabia yako na kukupa utabiri sahihi wa maisha yako ya kesho na ya milele.

Je umemwamini Yesu?, je umebatizwa ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu?.

Bwana Yesu anarudi.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MSHIKE SANA ELIMU.

NYOTA ZIPOTEAZO.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

Haki ni Nini katika biblia. Haki ya Mungu ni ipi?

Haki maana yake ni kitu ambacho mtu anastahili kukipata. Kwamfano kuishi ni haki ya Kila mwanadamu, Hakuna mtu anayepaswa kumzuia mwingine kuishi, kisa ni mwanamke au ni mfupi, au ni kichaa, au mlemavu. Maadamu tu amekuwa mwanadamu tayari anayo haki ya kuishi.

Mfano mwingine wa haki, ni mtu aliyesoma  ukahitimu katika shahada Fulani labda tuseme ya utatibu, mtu kama huyo tunasema ana haki ya kuitwa daktari kwasababu amesomea jambo Hilo.

Vivyo hivyo katika Roho. Mungu naye anayo haki yake, katika kutoa vitu vyake.

Mwanzoni ilikuwa Ili kumkaribia Mungu na kupata kibali kwake na mema yote na baraka zote ilikupasa kwanza uishike Sheria yake yote. Hivyo yoyote aliyeweza kufanya hivyo alipatiwa haki hiyo. Soma Kumbukumbu 28

Lakini Kwa bahati mbaya hakukuwa na mtu aliyestahili kumkaribia Mungu kwasababu Hakuna mwanadamu aliyekwenda katika maagizo yote ya Mungu Kwa ukamilifu wote, bila kosa. Kwahiyo tangu zamani hakukuwa na mwanadamu hata mmoja aliyefanikiwa kumkaribia Mungu. Wote walitenda dhambi (Zaburi 14:3)

Hivyo Mungu akabuni mpango mwingine wa kumwokoa mwanadamu ili awe amestahili kupokea mambo yote ya rohoni ya Mungu, ikiwemo uzima wa milele na kumkaribia yeye.

Ndipo akamleta Yesu duniani, Ili Kila amwaminiye asipotee Bali apokee kuhesabiwa haki bure, bila kutegemea Tena matendo ya Sheria. Kwasababu Kwa matendo ya Sheria hakukuonekana aliyestahili.

Hivyo Mimi na wewe tunapomwamini Kristo kama ndiye Bwana na mwokozi pekee wa maisha yetu na kuukubali msamaha wake wa dhambi, basi tunahesabiwa tumestahili kuitwa watakatifu, na hivyo tunamkaribia Mungu katika ukamilifu wote, kumwomba yeye na kupokea vyote kutoka kwake bila sharti. Haleluya!

Warumi 3:21-24

[21]Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; 

[22]ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 

[24]wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 

Hivyo ikiwa umekombolewa na Yesu Kristo, basi unapaswa uwe na ujasiri wote kumkaribia Mungu, bila kutegemea ukamilifu wako,Bali Kristo tu, na hivyo utapokea mema, yote kutoka Kwa Mungu.

Waebrania 4:16

[16]Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. 

Hiyo Ndio inaitwa “HAKI itokayo Kwa Mungu” ambayo tunaipata kwa kupitia Yesu Kristo tu peke yake.

Kwa Yesu tunapokea uzima wa milele bure. Kwa Yesu Tunapokea majibu ya mahitaji yetu yote bure. Kwa Yesu tunaitwa watakatifu.

Lakini Swali ni je! Umemwamini Kristo? Kumbuka kamwe huwezi kumpendeza Mungu Kwa matendo yako pekee, Kila mwanadamu chini ya jua anamuhitaji Kristo.

Ikiwa Bado hajaokoka basi mlango upo wazi Leo. Tubu mgeukie Bwana akuponye. Ikiwa upo tayari kupokea msamaha wa dhambi Leo, na kufanywa kiumbe kipya, basi fungua hapa Kwa Mwongozo huo. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

SWALI: Nini maana ya Mithali 16:30

Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;  Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya. 

JIBU: Mstari huo haumaanishi mtu anayefumba macho yake, Huwa anaishia kuwaza mawazo mabaya, hapana kama ni hivyo basi,  tungekuwa tunafanya makosa kufumba macho tunapoomba.

Zaidi sana mtu mwenye hekima huwa anapoona jambo la kutisha ovu, au lenye aibu Ndio anayekuwa wa kwanza kufumba macho yake asiruhusu kuona kinachoendelea.. kama vile walivyofanya watoto wa Nuhu.(Mwanzo 9:23)

Hali kadhalika anaposema mtu aikazaye (aifumbaye), midomo yake. Haimaanishi mtu asiyezungumza-zungumza, Huwa anaishia kuyazungumza maneno yasiyofaa. Kama ni hivyo biblia isingesema;

Mithali 21:23

[23]Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu. 

Lakini je? Vifungu hivyo vilimaanisha Nini?

Hapo anaposema afumbaye macho yake ni kuwaza yaliyopotoka,..alimaanisha afumbaye macho asitazame kweli (ambayo ni Neno la Mungu), linapomfundisha au kumwonya. Mtu huyo lengo lake ni kuendelea katika mawazo yake mabaya ya dhambi. Mfano aambiwapo kuishi na mke ambaye si wako ni uzinzi, na wazinzi sehemu Yao ni Katika ziwa la moto, lakini hataki kuliona au kulisikia Hilo andiko, jibu lake ni kuwa anataka kuendelea katika matendo yake ya giza.

Ndicho kilichokuwa Kwa waliompinga Yesu., Ndio maana akasema  maneno haya; 

Mathayo 13:15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, 

Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 

Vilevile anaposema “Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya”

Anamaanisha, aizuiaye midomo yake kusema maneno ya uzima, ya staha, ya kujenga, ya adabu, ya maarifa, ya busara n.k.. Mwisho wake utakuwa ni kunena maneno mabaya tu.

Bwana alisema..

Luka 6:45

[45]Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake. 

Vivyo na hivyo na sisi, hatuna budi tujipime na kujichunguza…macho yetu hutazama Nini, vinywa vyetu vimejawa na maneno gani.? Lakini fahamu kuwa huwezi kushinda jicho lako, au ulimi wako ikiwa Kristo hajaumbika ndani yako.

Je! Unataka msaada Kwa Yesu Kristo? Kama jibu ni Ndio, basi unachopaswa kufanya cha kwanza ni kuyaachilia maisha yako kwake. Ili akusamehe dhambi zako. Ndipo akupe nguvu ya kushinda dhambi.

Hivyo bofya hapa Kwa ajili ya Mwongozo wa Sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Jibu: Turejee,

Mathayo 24:35  “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”

Ili tuelewe vizuri, tutafakari kwanza mstari ufuatao…

Waebrania 13:8 “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”.

Mpaka maandiko yaseme kuwa “Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele”… Maana yake kuna watu, au vitu ambavyo haviwezi kuwa vile vile jana, leo na hata milele.

Kwa mfano mtu hawezi kuwa na tabia ile ile, au msimamo ule ule jana na leo na hata milele,..ni lazima tu utafika wakati tabia yake itabadilika, mtazamo wake utabadilika, utendaji wake utabadilika au hata msimamo wake!…. lakini KRISTO YESU yeye ni yule yule, kitabia, na kiutendaji, hajawahi kusema jambo halafu akajikosoa.. ni yeye yule na ataendelea kuwa vile vile Milele.

Hali kadhalika, vitu tunavyoviona katika mbingu kama jua, mwezi  na nyota, ijapokuwa tunaona vimedumu kuwa vilevile kwa maelfu ya miaka, lakini biblia inatabiri kuwa siku moja vitatoweshwa vyote…

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13  na NYOTA ZIKAANGUKA juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14  MBINGU ZIKAONDOLEWA KAMA UKURASA ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake”.

Vile vile vitu tunavyoviona katika “NCHI” kama vile milima, na habari ambavyo tunaviona kama zimedumu kwa maelfu ya miaka, lakini bado biblia inatabiri kuwa siku moja vitafutika..

Ufunuo 16:20  “Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena”

Soma pia Ufunuo 21:1..

Lakini wakati ambapo vitu vyote hivi vinaondolewa (maana yake VINAPITA) Bado Kristo atabaki kuwa yeye yule, na maneno yake yatabaki kuwa yale yale, na yana nguvu ile ile katika umilele wote.

Kwamfano maneno ya Yesu anayosema yeye ni ALFA na OMEGA, yaani Mwanzo na Mwisho (katika Ufunuo 21:6 na Ufunuo 22:13) yataendelea kuwa hivyo hivyo Milele, hakuna wakati utafika Kristo ataacha kuwa Alfa na Omega…jua na mwezi na nyota na wanadamu watapita, lakini maneno hayo yataeendelea kuwa halisi hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile maneno yake aliyosema kuwa “Yeye ndio Njia, Kweli na Uzima (Yohana 14:6)” yataendelea kuwa hivyo milele na milele, hakuna wakati utafika ambao Kristo ataacha kuwa Njia, au ataacha kuwa  Kweli au ataacha kuwa Uzima..Kristo YESU sasa ni Uzima, na ataendelea kuwa UZIMA hivyo hivyo milele na milele.

>Vile vile aliposema kuwa yeye ni “Nuru ya Ulimwengu (Yohana 8:12)”…Maneno hayo hautafika wakati ambao yata-expire… Jua na mwezi kuna wakati vitaisha muda wake wa matumizi, jua litaondolewa halitamulika tena, na mwezi utaondolewa hautaangaza tena.. lakini Kristo ataendelea kuwa NURU hata kipindi ambacho jua na mwezi havipo..

Ufunuo 21:23  “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, KWA MAANA UTUKUFU WA MUNGU HUUTIA NURU, NA TAA YAKE NI MWANA-KONDOO”.

> Vile vile maneno yake mengine yanamtaja yeye kama “Mwaminifu na wa Kweli (katika Ufunuo 3:14, na Ufunuo 19:11)”. Yeye atabaki kuwa hivyo Milele na milele, hakuna wakati ambao atabadilika na kukosa uaminifu!… Sisi wanadamu tunaoishi chini ya jua na juu ya nchi, tutakuwa waaminifu tu kwa kitambo Fulani lakini si milele. Lakini yeye ataendelea kuwa mwaminifu milele na milele hata wakati ambao mbingu zitafutwa, na kuletwa mbingu mpya na nchi mpya, bado ataendelea kuwa mwaminifu.

> Pia alisema wote wamwaminio yeye watakuwa na uzima wa milele, hakuna wakati hilo Neno litabadilika, kwamba awanyime uzima wa milele wale wote waliomwamini na kuishi kwa kuzifuata amri zake.. Majira yatabadilika, vipindi vitabadilika lakini milele na milele hawezi kujisahihisha maneno yake hayo. AKIAHIDI AMEAHIDI!!.. Na milele habadiliki.

Na maneno mengine yote yaliyosalia aliyoyasema BWANA YESU hakuna hata moja litapita!!! , yote yatabaki kuwa vile vile

Je umemwamini huyu Mkuu wa UZIMA asiyeweza KUBADILIKA?, Au Unawatumainia wanadamu ambao leo wapo na kesho hawapo, leo wanaahidi na kesho wamebadilika, leo wanakupenda kesho wanakuchukia.. Ni heri ukaanza kumtumainia yeye asiyeweza kubadilika, YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA.

Mungu akubariki.

Mafundisho Mengine

Mbinguni ni sehemu gani?

Kuna Mbingu ngapi?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

Je! Sulemani alienda mbinguni?

Rudi Nyumbani:

 

 

Print this post

Gudulia ni nini? (1Samweli 26:11).

Jibu: Tusome,

1Samweli 26:11 “Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi

12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile GUDULIA LA MAJI, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia”.

Gudulia ni chombo maalumu kilivyotengenezwa kwa lengo la kuhifadhia maji ya kunywa ya watu wachache, kwa lugha ya sasa hivi tunayaita “majagi”

Magudulia/majagi ya zamani yalitengenezwa kwa malighafi tofauti na ya zama hizi. Zamani majagi/magudulia waliyatengeneza kwa kutumia udongo wa (mfinyanzi tazama picha juu), lakini sasa yanayotumika mengi yao yametengenezwa kwa glasi au plastiki.(tazama picha chini).

Gudulia ni nini?

Mistari mingine inayotaja chombo hiki (gudulia) ni pamoja na 1Wafalme 19:6, Yeremia 19:1 na Yeremia 19:10.

Je umemwamini Bwana Yesu?, je unajua kuwa tunaishi katika majira ya kurudi kwa YESU mara ya pili, na wakati wowote unyakuo wa kanisa utatokea?.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Shilo ni wapi?

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALA HAKUACHA MTU ACHUKUE CHOMBO KATI YA HEKALU.

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

JINSI YA KUISHINDA HALI YA MSONGO WA MAWAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA ANASAMEHE.

Jina la Bwana na Mwokozi Mkuu YESU KRISTO lihimidiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu lililo hai, ambalo ndilo taa na mwanga wa njia yetu ya kwenda mbinguni (Zab.119:105).

Moja ya hubiri kubwa na kongwe la shetani, ni kuwahubiria watu kuwa “MUNGU HASAMEHI na ANACHUKIA WATU”.

Fundisho hili ni silaha kubwa sana ya kumfanya mtu asijaribu kumtafuta Mungu, au hata kama alikuwa ameshaanza hatua za kuutafuta uso wa Mungu, basi akate tamaa njiani. Anajua mtu akifahamu kuwa anaweza kusamehewa na Mungu basi hatampata tena, na yeye anataka watu waendelee kudumu katika dhambi ili hatimaye waukose uzima wa milele kama yeye alivyoukosa.

Sasa sifa moja kuu ya MUNGU aliyeumba mbingu na nchi, ni MSAMAHA. Maana yake “anatoa msamaha hata kwa mtu asiyestahili kusamehewa”.. Na hii ndio sifa ya kwanza inayomfanya yeye (MUNGU) kutisha!..na wala si tu yale matendo ya miujiza aliyoyafanya kule Misri, au anayoendelea kuifanya hata sasa, ambayo kimsingi tunadhani hayo ndiyo yanayomfanya Mungu atishe.

Muujiza Mkuu na wa kwanza unaomfanya Mungu kutisha, ni KUSAMEHE NDAMBI, na KUZIONDOA KABISA NDANI YA MTU.

Zaburi 130:3 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, ILI WEWE UOGOPWE”.

Je! Unajihisi wewe ni mwenye dhambi, na unahisi dhambi yako haifutiki??…fahamu kuwa MUNGU kuna msamaha, na sio tu msamaha bali pia na ondoleo la dhambi, kiasi kwamba baada ya kusamehewa Mungu anaondoa mpaka msingi wa hiyo dhambi, kiasi kwamba wakati mwingine haitakuwa na nguvu juu yako.

Je unahisi mauaji uliyoyafanya hayawezi kusameheka?, je unahisi mawazo uliyowaza au unayowaza hayana msamaha?, je unahisi tendo ulilolifanya na tena umelirudia mara nyingi nyingi halina msamaha?..kama hayo mawazo yapo ndani yako basi fahamu kuwa ni adui ndiye anayekuambia hivyo.

Yote uliyoyafanya yanasameheka ikiwa utataka Bwana akusamehe!. Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha kuacha hayo unayoyafanya, Ikiwa utatubu kweli kwa kumaanisha, basi kwa IMANI amini kuwa Mungu kashakusamehe, hauhitaji kutokewa na Malaika na akamwambie kwamba umesamehewa, wewe Amini tu, kwasababu ndivyo biblia inavyotufundisha kwamba “tuenende kwa Imani na si kwa kuona” (2Wakorintho 5:7).

Na ukishaamini namna hiyo, basi Mungu kashakusamehe lile kosa au yale makosa uliyoyafanya hata kama uliyafanya kwa kurudia rudia mara 100, tayari atakusamehe deni yako yote. Lakini kumbuka msamaha si ondoleo!.. Mtu anaweza kukusamehe tusi ulilomtukana, lakini kama ile roho ya kutukana haijaondoka ndani yako basi unaweza kurudia tena kesho na kesho kutwa kumtukana matusi yale yale.

Kwahiyo ili lile kosa lisijirudie rudie tena katika maisha yako, linahitaji kuondolewa kwa mizizi yake ndani yako. Sasa kanuni ya kuondoa mzizi wa dhambi ndio shetani amewafumba watu macho wasiione.

Lakini ashukuriwe Mungu kwasababu ipo wazi katika maandiko.

Tusome,

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Hapa Petro anawaonyesha hawa Makutano, kanuni ya KUONDOA MZIZI wa dhambi ndani yao, baada ya wao KUTUBU dhambi,  kwamba WAKABATIZWE KWA JINA LAKE YESU KRISTO. Kama ishara ya kuuvua utu wa kale na kuuvaa utu upya, na kwa ishara hiyo ya maji basi ule mzizi wa dhambi utaondoka ndani yao, zile dhambi za kujirudia rudia zitakoma, kwahiyo mtu wa Mungu anabaki huru mbali na dhambi.

Na tena Mungu wetu kwa upendo wake anatuongezea na zawadi ya Roho Mtakatifu, ndani yetu kama Muhuri wa Mungu kwa kile tulichokitubia.

Je bado umezishikilia dhambi zako? Kwanini usiungame leo kwa kutubu na kubatizwa?. Na kumbuka ungamo sahihi ni lile la kutubu kwa kumaanisha, na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO, Kutubu kusikotoka moyoni, na ubatizo usio sahihi haviwezi kuleta matokeo yoyote kwa mtu.

Bwana akubariki.

Ikiwa utahitaji msaada katika kuongozwa sala ya Toba, au ubatizo basi waweza wasiliana nasi na tutakusaidia katika hilo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUTUBU

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

BABA UWASAMEHE

UMEONDOLEWA DHAMBI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi nyumbani

Print this post