Title October 2024

Kama ni Mungu ndiye kaumba zao la Bangi kwanini tena iwe dhambi kuitumia??

Swali: Biblia inasema tumepewa mboga za majani kuwa chakula chetu, na Bangi pia ipo miongoni mwa zao la mboga za majani…sasa kwanini iwe dhambi kulitumia kama mboga au kiburudisho cha kusisimua (kuvuta) na ilihali ni Mungu mwenyewe ndio kaumba?


Jibu: Turejee..

Mwanzo 9:3 “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa MBOGA ZA MAJANI, kadhalika nawapeni hivi vyote”.

Ni kweli maandiko hayo yanathibitisha ulaji wa mboga, lakini si mboga zote!.. Tukisema kila mboga iliyopo kondeni tumepewa tule, tutakuwa hatujayaelewa vizuri maandiko kwasababu  kuna mboga nyingi sana ambazo sumu!, ambazo zinamwonekano mzuri lakini hazifai kwa chakula… na Mungu hawezi kumpa ruhusa Mtu wake aliyemuumba, ale SUMU!..

Zipo mboga kwaajili ya chakula cha wanadamu, nyingine kwaajili ya wanyama na hazifai kwa wanadamu… vile vile zipo mboga zisizofaa kwa chakula cha wanadamu na wanyama… Mboga hizo zinabaki tu kwa utukufu wa Mungu, au kwaajili ya urembo, mfano wa mboga hizo ni MAUA.

Kuna Maua ambayo yana mwonekano mzuri sana lakini ni SUMU kali sana, mfano wa hayo ni kama haya yanavyoonekana hapa chini.

maua sumu

Hayo ni mfano wa Mboga, lakini si kwaajili ya kula bali kwaajili ya urembo tu.. yameumbwa na Mungu kwa lengo hilo, hivyo mtu akila hayo anaweza kupata madhara makubwa ya kiafya au hata kifo.

Vile vile na Bangi, inaweza kuwepo katika kundi hilo la MAUA, kama itatumika kwa urembo si vibaya, lakini kwa matumizi mengine ya ndani ya mwili wa binadamu ni hatari.

Kwahiyo si kila kilicho halalishwa basi kinafaa kwa matumizi yote.. hapana!.. Mboga zimehalalishwa lakini si kwa matumizi ya chakula tu, ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Kwahiyo ulaji, au uvutaji wa Bangi ni dhambi kibiblia, vile vile matumizi ya tumbaku kula au kuvuta ni dhambi, kwani miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na tena maandiko yanasema mtu akiliharibu hekalu hilo Mungu naye atamharibu mtu huyo (Soma 1Wakoritho 3:16-17 na 1Wakorintho 6:19).

Na Bangi inaharibu ufahamu wa mtu, ambao ndani yake kunazalika hasira, kutokujali, vurugu, matukano, mauaji, uasherati na mambo yote mabaya..

Hivyo Bangi ni haramu, vile vile tumbaku na mazao mengine yaletayo matokeo kama hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

MTINI, WENYE MAJANI.

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Nini maana ya mmoja alikufa kwaajili ya wote hivyo walikufa wote? (2Wakorintho 5:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Nehemia 8:10

[10]Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.

Ni habari ya kutafakarisha, lakini zaidi sana ya kuwafariji watu wote wampendao Mungu. Tukisoma katika biblia ile habari ya Ezra na Nehemia, katika juhudi zao wa kuwarejesha Israeli katika ibada na njia za Mungu Yerusalemu.

Tunaona wakati ule ukuta wa Yerusalemu ulipomalizwa kujengwa baada ya kurudi kwao utumwani Babeli, Ezra hakuwaacha tu hivi hivi, wafurahie kukamilika kwa majengo, bali alitaka wakamilishwe na mioyo yao hivyo, alikichukua kitabu cha Torati na kuanza kuwasomea wayahudi wote tangu asubuhi mpaka adhuhiri, ili wajue ni nini Bwana anataka kwao (Nehemia 8).

Na waliposikia waliona makosa yao mengi sana, na hukumu nyingi za Mungu, alizowatamkia kufuatana na makosa yao, yaliyowapelekea mpaka wakachukuliwa mateka. Ikumbukwe kuwa kitabu hicho cha torati hakikuwahi kusomwa tangu zamani walipochukuliwa utumwani, ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kukisoma baada ya miaka mingi kupita.

Hivyo wayahudi kusikia vile wakaanza kulia sana na kujuta na kuomboleza. Lakini tunaona kuna jambo lilifanyika la kitofauti.

Nehemia, alitambua wazo la Mungu…Hivyo akawazuia watu kulia na kuomboleza kwa ajili ya makosa yao. Kinyume chake akawaambia leo ni siku takatifu kwa Bwana, hivyo mle ,.mnywe, mtoe sadaka, mfurahi mbele za Mungu wenu kwasababu “furaha ya BWANA ni nguvu zenu” 

Hivyo watu wakasheherekea, badala ya kulia, Sio kwamba Nehemia alisheherekea makosa yao, hapana, bali alipewa kujua kwamba  furaha ya mtu kwa Mungu wake, ndio chanzo cha nguvu ya kumtumikia yeye. 

Ndio hapo baada ya wayahudi kujua makosa yaowakimfurahia Mungu, siku hiyo, na wakapokea nguvu nyingi za kuishika sheria ya Mungu. 

Yaani kwa namna nyingine, Mungu kuwakemea makosa yao,lengo lake lilikuwa sio awahukumu, au wainamishe vichwa vyao wakidhani kuwa wao ni kichefu-chefu kwake. Hapana..Bali anawapenda na hivyo anatarajia wajue nia ya makemeo yake.

Nehemia 8:10 Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.

11 Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike. 

12 Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa

 

Ni hata sasa, unaposoma biblia na kuona inakushitaki, inakuambia usiibe, usisengenye, amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji, wazinzi wote sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, inapokukemea maovu yako ya siri.. Usiinamishe kichwa na kusema “mimi sifahi mbele za Mungu, mimi ni mkosefu sistahili kuitwa mwana wake”..Ukaacha kukisoma kabisa, ukawa unalia tu, umenyong’onyea, na kujihisi wewe ni wajehanamu tu, Mungu hakupendi, ameshakuacha, ona sasa unamkosea kosea kila siku… Fahamu kuwa hilo sio kusudi la Mungu.

Kusudi la Mungu sio usome biblia, ujawe na hisia za Mungu kukuhukumu, au kukulaumu, au kukushitaki, bali kusudi la Mungu ni ujue  upendo wake uliozidi sana kwako, kiasi cha yeye kuonyesha hisia zake kwako namna ambavyo unapaswa uwe kama yeye.

Hivyo ukitoka kuonywa na kukemewa, unapaswa utoke kwa kufurahi moyoni  na kuruka-ruka, na hapo ndipo utapokea nguvu ya kuishinda hiyo dhambi. Lakini ukitoka kinyonge na mashaka utashindwa kwasababu furaha ya Bwana ndio chanzo cha nguvu zetu. Ukilipenda hilo katazo, utalitenda, usipolipenda kamwe huwezi litenda.

Mtunga Zaburi alisema,

Zaburi 119:52

[52]Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee BWANA, nikajifariji.

Bwana anataka tuone upendo wake kwetu katika makemeo yake, tufarijike tupokee nguvu ya kushinda. Pengine umetoka kufanya dhambi fulani ya makusudi na Roho Mtakatifu akakumbusha kuwa watu wa namna hii, huangukia katika mtego mbaya wa shetani bila kunasuka, Sasa hapo usianze kupoteza ladha na Mungu wako, au biblia, ukauchukia wokovu, kabisa,  maanisha kutubu, jifunze kutokana na makosa, kisha furahia mwambie Bwana asante kwa kunipenda,

hata wachezaji wa mpira, wafungwao kipindi cha kwanza, wanapotulia na kujihamasisha tena, hupokea nguvu ya kucheza vema kipindi cha pili, lakini wajilaumupo, hufanya vibaya zaidi

Na sisi pia tuiamshe furaha ya Bwana daima.Kila tusomapo Neno lake, tufurahi kwasababu ni barua ya upendo wa Mungu kwetu Ili tuweze kuwa na nguvu.

Kwasababu furaha ya Bwana ndio nguvu yetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

Furaha ni nini?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

 

Print this post

USI..USI..USI.

Usi!.. Usi!.. Usi! na sio Msi!… Msi!.. Msi!..

Amri za Mungu zinasema Usiue, Usizini, Usiibe … na sio Msiibe, Msiue, Msizini… Ikifunua kuwa Mungu anaongea na mtu mmoja mmoja… Anasema na Mimi kivyangu, lakini pia anasema na wewe kivyako… Na hatuambii wote kwa pamoja.

Kutoka 20:13 “Usiue. 

14 Usizini. 

15 Usiibe. 

16 Usimshuhudie jirani yako uongo. 

17 Usiitamani nyumba ya jirani yako…”

Siku ya Hukumu, hatutahukumiwa kwa pamoja, kila mtu atasimama peke yake, na kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe..

Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.

Na tena kila mtu atatoa habari zake mwenyewe na si pamoja na mwenzake..

Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”

Sasa kama ni hivyo kwanini Boss wako akukoseshe?..kwanini Rafiki akukoseshe, kwanini wanadamu wakukoseshe??… Na ilihali utasimama peke yako siku ile.

Kumbuka unapofanya uzinzi, siku ile hutakuwa na yule aliyefanya naye uzinzi, badala yake utasimama wewe kama wewe (kwasababu ile amri  inakuhusu wewe, na Mungu alikuwa anazungumza na wewe kivyako na si wewe pamoja na mwenzako)..

Kama unaiba, siku ile hutasimama na aliyekushawishi ukaibe, au uliyekuwa unashirikiana naye katika wizi.. wewe utakuwa peke yako, na yeye peke yake….kwasababu Amri ya Usiibe, uliambiwa wewe, nimeambiwa mimi na si wewe pamoja na mimi… Hivyo kila mtu atatoa habari zake mwenyewe.

Kama unaua, ni hivyo hivyo, kama uwaheshimu wazazi ni hivyo hivyo, na amri zote ni hivyo hivyo..

Hukumu ya Mungu inatisha!.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe;

CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.

Rudi Nyumbani

Print this post

KUWA MAKINI NA MATANGO MWITU, SIKU HIZI NI ZA MWISHO!

Kuna wakati Elisha alifika Gilgali na mahali pale palikuwa na njaa kali, na watu wengi (manabii) pia walikuwa  wamekusanyika kusikiliza mashauri ya mtu wa Mungu.

Hivyo akawaambia waweke sufuria motoni waandae chakula.

Lakini mmojawao akatoka akaenda mashambani kutafuta mboga. Na huko akafanikiwa kweli kukusanya zilizo bora, lakini kwasababu hakuwa na maarifa ya kutosha jinsi ya kutambua mboga sahihi ziwafaazo wanadamu akaona huko matango mwitu, na bila kujua, akidhani ni matango halisi, akayachuma na kuyaleta sufuriani. Matango yale yalikuwa ni sumu.

Lakini walipoonja kwa neema za Mungu walijua kuna kitu ambacho sio sahihi kimewekwa sufuriani, hivyo waacha wote kula. Ndipo Elisha akataarifiwa, juu ya jambo hilo, kama kimwagwe lakini kile chakula hakikumwagwa, bali aliwaagiza watie unga mule (kwa Neno la Bwana), na chakula kitaponyeka.  Wakafanya hivyo, kikawa sawa, wakala wakashiba.

2 Wafalme 4:38-41

[38]Elisha akafika Gilgali tena; na kulikuwa na njaa katika nchi; na hao wana wa manabii walikuwa wakikaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, Teleka sufuria kubwa, uwapikie wana wa manabii.

[39]Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtango-mwitu, akayachuma matango-mwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasua-pasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.

[40]Basi wakawapakulia hao watu ili wale. Ikawa, walipokuwa katika kula chakula, wakapiga kelele, wakasema, Mauti imo sufuriani, Ee mtu wa Mungu. Wala hawakuweza kula.

[41]Lakini yeye akasema, Leteni unga. Naye akautupa ndani ya sufuria; akasema, Wapakulie watu, ili wale. Wala hakikuwamo kitu kibaya sufuriani.

Habari hiyo inafunua nini?

Inatueleza hali ya kiroho ya watu iliyopo sasa.

Palipo na njaa ni rahisi mtu kula kila kitu, ilimradi tu asife. si rahisi akae chini na kufikiria ubora wa kile anachokula. Leo hii njaa ya Neno la kweli la Mungu ni kubwa, hivyo kila mtu anaenda kondeni kuokota kitu kimfaacho, huko huko tunakutana na vizuri lakini pia tunakutana na vibaya..

shida ipo hapo, je tunaweza kupambanua?

Kwasababu ukila sumu, ile sumu haitakuambia ngoja nisikuletee madhara kwasababu hukukusudia kunila, au hukujua kuwa mimi ni sumu, utakufa tu  sawasawa na yule anayejua anachokifanya.Kumbe ujinga una gharama kubwa.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 7:15

[15]Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

Mafundisho yasiyomhubiri Kristo na utakatifu, ni kuwa makini nayo, ni heri usiyasikilize kabisa kwa usalama wako wa kiroho. Yanayokuambia tunaokolewa kwa neema tu, hivyo matendo yako ni kazi bure mbele za Mungu, ukiokolewa umeokolewa milele, hata ukiwa unatenda dhambi vipi huwezi potea, yapime sana hayo mafundisho.

Mafundisho ya kuzimu-kuzimu tu na majini na wachawi epukana nayo, Mafundisho ya sanamu ibadani, ni mauti chunguni. Mafundisho yanayopinga habari za mwisho wa dunia, ambayo hayana habari na unyakuo au kumfanya mtu atazame kurudi kwa pili kwa Kristo, kinyume chake ni kukuweka kidunia, ufikirie mafanikio ya mwilini ni matango mwitu.

Manabii wa uongo ni wengi, wapo wanaotenda kazi kwa uwazi, lakini  wapo wanaotenda kazi kwa siri.

Jifunze kusoma biblia, jinsi usomavyo Neno la Mungu utagundua kuwa mtu uliyeokoka  kwa wakati uwapo hapa duniani Bwana anakutana Utembee katika utakatifu (Waebrania 12:14). Lakini pia uelekeze macho yako mbinguni kwa yale mambo yajayo, ya mbingu mpya na nchi mpya.

Luka 12:35-36

[35] Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; [36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

Jihadhari na matango mwitu.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii  >>>> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Kusanyiko la makini/ mkutano wa makini ni upi?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

 

Print this post

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Swali: Kulikuwa na ubaya gani wa Adamu na Hawa kula matunda ya mti wa Uzima, ili wapate tena uzima wa milele baada ya kuupoteza? (Mwanzo 3:22-24).


Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mwanzo 3:22 “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, AKALA, AKAISHI MILELE;

23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa”.

Sababu pekee ya Bwana MUNGU kuwazuia wazazi wetu wa kwanza (Adamu na Hawa) kula yale matunda ya Mti wa Uzima, si kwamba Mungu alikuwa hataki waishi milele!. La!.. kinyume chake ni mpango wake mkamilifu wa Mungu kwamba mwadamu aishi milele.

Tito 1:2 “katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele”

Soma pia 1Yohana 2:25 utaona jambo hilo hilo…

Lakini kwasababu tayari mwanadamu alikuwa ameshaiingiza dhambi ndani yake na katika kizazi chake, hivyo asingeweza kuishi milele katika dhambi, hivyo ni lazima dhambi iondoke kwanza ndani yake ndipo aishi milele, kwasababu kama akiishi milele na dhambi imetawala maisha yao, ni uharibifu mkubwa utaendelea na maisha yatakuwa nje na mpango wa Mungu, kwasababu yeye Mungu ni mkamilifu, hivyo kanuni ya maisha ya milele, ni sharti yasiwe na dhambi.

Kwahiyo BWANA MUNGU akaweka mpango kwanza wa kuiondoa dhambi ndani ya mtu, na mzizi wake, kisha yule mtu apate tena uzima wa milele.

Na mpango wa Mungu wa kuondoa dhambi ndani ya Mtu na kumrejeshea Uzima wa milele, ameushona ndani ya Mwanae YESU KRISTO, kwamba kwa kupitia njia ya kumwamini yeye, na kutubu basi tunaoshwa dhambi zetu na kupata uzima wa milele.

Warumi 5:21 “ili kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala katika mauti, vivyo hivyo kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu”.

17  Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye”.

Hivyo kamwe hatuwezi kupata uzima wa milele, tukiwa katika dhambi..ni lazima kutubu kwanza na kumwamini Bwana YESU ndipo tupate uzima wa milele.

Na hiyo ndio sababu ya Bwana MUNGU kuifunga ile njia ya MTI WA UZIMA pale Edeni, ilikuwa ni sharti kwanza ADAMU na HAWA watakaswe ndambi zao kwa damu ya Mwanakondoo… Na majira yalipofika Mungu alimtuma mwanae ili afe kwaajili ya wote walio hai, na waliokwisha kutangulia, waliokufa katika haki, ili kwamba wote tutakaswe na kupata uzima wa milele.

Na hili ni la kujua siku zote, kwamba hakuna uzima wa milele kwa mwingine yeyote Zaidi ya YESU KRISTO.

Yohana 3:35 “Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.

36  Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Mistari ifuatayo inazungumzia uzima wa milele ndani ya YESU KRISTO (1Yohana 5:11-13, Yohana 3:16, Yohana 5:24,  Yohana 6:54,  Yohana 12:50, Yohana 17:2, na Warumi 6:23)  .

Je umempokea BWANA YESU?… kama bado unangoja nini?..Fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, majira yameenda sana na ule mwisho umekaribia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. 

SWALI: Nini maana ya Waefeso 6:24, pale inaposema “katika hali ya kutoharibika”?

[24]Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.


JIBU: Mtume Paulo alipokuwa anahitimisha ujumbe wa waraka wake kwa waefeso, alimalizia kwa kuwatamkia neno la heri watu watu wale akiwaambia ‘NEEMA  ikae pamoja nao.

Lakini tunaona hapo hakukusudia tamko hilo kwa watu wote,  bali anasema ikae kwa wale wampendao Bwana, lakini bado sio tu kwa  wampendao Bwana.. Bali wampendao katika “hali ya kutokuharibika”.

Yaani kwa ufupi upendo usio poa.. Ndio upendo usio haribika.

Ndio ule unaozungumziwa kwenye 1Wakoritho 13. Kwamba hustahimili yote, huvumilia yote, huamini yote, haupungui Neno wakati wowote.

Ni kuonyesha kuwa Bwana wetu Yesu Kristo anastahili kupendwa daima, zaidi ya vitu vyote, kwasababu ya upendo wake mkuu aliotuonyesha sisi wa kuacha vyote mbinguni kwa ajili yetu, ili tukombolewe. Na kwa rehema zake akatupa na vipawa kabisa, na uwezo wa kuitwa wana wa Mungu, kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu aliyetupa . Hakika anastahili kupendwa  sana bila ukomo.

Zingatia: Waraka huu sio wa waefeso tu, bali ni wetu pia sote tumeandikiwa. Hivyo tutaongezewa neema ikiwa tutampenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usio haribika. Sio njaa itufanye tumwache, au ufukara, au mke, au kazi, au uzuri, au ubaya, au ndugu, au mali, au afya, au ugonjwa.. au kitu chochote, Bali kila wakati sisi shauku yetu kwa Kristo iwe ni ile ile. Kuomba ni kule-kule, kumtafuta Mungu ni kule-kule. Amen

Neema ya Bwana iwe nasi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Rudi Nyumbani

Print this post

NYWELE ZAKO ZIKUFUNDISHE, SAUTI YA MUNGU.

Kwanini Mungu akuumbe hivyo ulivyo? Kwanini asingeweka pembe kichwani kwako, au kwanini asingekuwekea  vilemba vya nyama kama vile vya kuku kichwani, au antena mbili kama zile za konokono au mdudu, bali amekuwekea nywele kichwani pako.

Sauti ya Mungu ipo katika maumbile yetu. Sisi kujikuta hivi tulivyo sio kwamba, ndio umbile bora zaidi ya yote Mungu aliloona linamfaa mtu, hapana,  tungeweza kuumbwa vizuri zaidi hata ya mwonekano huo tulionao, lakini tumebuniwa hivi, kwa kusudi la kipekee ambalo tunapaswa tulijue, na sio kwa kusudi la urembo.

Kwamfano usipoweza kuelewa utendaji kazi wa mwili wako jinsi viungo vinavyoshirikiana huwezi kuelewa jinsi kanisa la Kristo linavyopaswa kufanya kazi likutanikapo, kwasababu sisi tunaitwa viungo mbalimbali ndani ya mwili wa Kristo.Umeona? Bwana akasema kiungo kimoja kikiumia, vyote vimeumia.

Hivyo tumeumbwa, kimalengo sio kimwonekano bora au kiuzuri,. Ni sawa na mtu aulizwe kati ya jiko, na maua kipi kina umuhimu zaidi kuwepo ndani mwako. Ni wazi kuwa atasema jiko,kwasababu litamsaidia kupika. Hakulichagua kwasababu lina mwonekano bora, lakini kwasababu lina matumizi muhimu zaidi ya vingine.

Vivyo hivyo na wewe ujitazamapo mwili wako, usijitazame kiuzuri kuliko  viumbe vingine, au wanadamu wenzako, bali fikiria tu katika picha ya matumizi ya kila kiungo ulichopewa, kinakufundisha nini kuhusu muumba wako au kinatimiza kusudi gani kwa Mungu wako. Hilo ndio lengo hasaa la wewe kubuniwa hivyo ulivyo.

Leo tutaanza na NYWELE, kisha wakati mwingine tutatazama na viungo vingine;

Utazamapo nywele zako Bwana anataka ujue yafuatayo;

  1. Mambo yako yote, yapo katika hesabu za Mungu.

Mathayo 10:30  lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. 31  Msiogope basi; bora ninyi kuliko mashomoro wengi

Ni kawaida  kudhani kuwa Mungu hathamini, au hajui kila kitu, au anasahau sahau. Lakini sivyo, ukimfuata Mungu, vitu vyako vyote vinavyotoka na kuingia vipo kimahesabu, hakuna kitu kinachotokea kwa ghafla tu, bila yeye kujua au kuruhusu, Hivyo mashaka yakija, kumbuka nywele zako zilivyo nyingi lakini zimehesabiwa, vivyo hivyo mambo yako yote yamehesabiwa.

  1. Huwezi epukana na maadui.

Zaburi 69:4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua

Jinsi nywele zako zilivyo nyingi, maadui nao vivyo hivyo. Na maadui zetu sio wanadamu bali ni mapepo ambayo mara nyingine huweza pia yavaa wanadamu, kutudhuru. Hivyo usiwe mtu wa kunung’unika au kulamimika, ujue kila mwanadamu yupo vitani. Kama Bwana wetu Yesu Kristo hakuwa na dhambi hata mmoja lakini alikuwa na jopo la maadui kwanini wewe usiwe nao. Hivyo kuwashinda ni kuwa mwombaji daima, na kutembea katika njia za Bwana sikuzote. Ukikumbuka kuwa maadui ni jambo la kawaida, kama tu nywele zako zilipo hapo kichwani.

  1. Si kila kitu unaweza kufanya. hivyo kuwa na kiasi.

Mathayo 5:36  Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.

Wakati mwingine, tunajiaminisha na kujihakikishia mambo na kuweka na viapo juu yake kana kwamba mambo yote yapo ndani ya uwezo wetu. Kauli kama, “leo nife,kama sitakupa hiyo fedha” au “Mungu anipige hapa hapa kama ninalokuambia ni uongo” Kauli  kama hizi, za kuongezea hakikisho lingine juu, hazitokani na Mungu, maneno yetu tumeambiwa yawe ndio ndio, au sio sio, zaidi ya hapo yanatokana na Yule mwovu. Kwahiyo popote unapojiona unakaribia kuzidi mipaka kumbuka hizo nywele zilizo juu yako hujawahi kuzifanya ziwe hivyo ulivyo, Bwana ndiye azibadilishaye, hivyo jiwekee mipaka.

  1. Zithamini nguvu zako za rohoni.

Nywele zako hufunua nguvu zako za rohoni. Wanadhiri wote wa Mungu hawakuruhusiwa kukatwa nywele, Samsoni alipewa nguvu, kwa agano la kutokatwa nywele, kufunua kuwa watakatifu wote nywele zao za rohoni ndio nguvu zao. Lakini unapoacha mpango wa Mungu adui anazikata, kama ilivyokuwa kwa Samsoni. Lakini baadaye alipojua amefanya makosa ziliota tena lakini katika gharama za ‘kutoona’ tena.

Waamuzi 16:22 Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake.

Tunza nguvu zako, usiruhusu kiwembe chochote cha mwovu kikupitie. Kwasababu hata zikirejea tena, hutakuwa kama hapo mwanzo.

  1. Uwe na nyakati za maombolezo.

Yeremia 7: 29 Zikate nywele zako, Ee Yerusalemu, uzitupe, Ukafanye maombolezo juu ya vilele vya milima; Kwa maana Bwana amekikataa na kukitupa Kizazi cha ghadhabu yake.

Zamani, kukatwa nywele zote kuisha kabisa ilikuwa ni ishara ya kuingia kwenye maombolezo, kwasababu utukufu wako umeuvua.

Maombolezo, kwa agano jipya sio kulia kama msiba, hapana bali kuingia kwenye maombi ya ndani kabisa, ya kuutafuta uso wa Mungu, ambayo huambatana na mifungo. Na leo, ni kila mara tunakwenda saluni kukata nywele zetu. Tujue Bwana anatutaka kama vile tukatavyo nywele zetu mara kwa mara ndivyo tukumbuke maombi ya kujimimina sana mbele zake.

Je! Somo hilo unajifunza mwilini mwako?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

ILI TUONEKANE WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU.

MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kusujudu ni nini, na je tuna sharti la kusujudu kwa Mungu?

Swali: Je kusujudu ni nini, na sisi wakristo tunayo amri ya kusujudu mbele za Mungu?


Kusujudu ni kitendo cha kuinama kwa kuelekeza kichwa chini kama ishara ya kuabudu au kutoa heshima kwa Mungu, mtu au shetani.. Zaidi ya kuinama tu, kusujudu pia kunaweza kuhusisha kupiga magoti na kuinamisha kichwa chini mpaka kufikia kugusa ardhi (soma 2Nyakati 7:3).

Maandiko yanatuonyesha mara kadha wa kadhaa watu wakimsujudia Mungu, na watu wakiwasujudia wanadamu na vile vile wakimsujudia shetani.

     1.Watu kumsujudia Mungu

Mfano wa watu waliosujudu mbele za Mungu ni yule Mtumwa, Ibrahimu aliyemtuma kwenda kumtafutia mwanae Isaka, mke.. Maandiko yanasema alipokutana tu na Rebeka na kupata uhakika kuwa ndiye binti aliyechaguliwa na Bwana, basi yule mtumwa alisujudu mbele za Bwana mpaka chini..

Mwanzo 4:24 “Akasema, Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, aliyemzalia Nahori.

25 Tena akamwambia, Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha, na mahali pa kukaa wageni.

26 YULE MTU AKAINAMA AKAMSUJUDU BWANA. 

27 Akasema, Na atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, ambaye hakuacha rehema zake na kweli yake kwa bwana wangu. Bwana akaniongoza mimi nami njiani hata nyumba ya nduguze bwana wangu”.

Wengine waliosujudu mbele za Bwana katika biblia ni Musa (soma Kutoka 34:8-9) na Wana wa Israeli kipindi utukufu umeshuka juu ya Nyumba ya Mungu (2Nyakati 7:3)…pamoja na mwandishi Ezra na wenzake katika Nehemia 8:6.

    2. Watu kusujudia Malaika.

Mfano wa watu waliowasujudia Malaika ni Yohana, Mtume wa Bwana YESU.

Ufunuo 22:8  “Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili NISUJUDU mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.

9  Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. MSUJUDIE MUNGU”.

Mwingine aliyejaribu kumsujudia Malaika ni Yoshua (soma Yoshua 5:14)

    3. Watu kuwasujudia wanadamu.

Mfano wa watu waliomsujudia mwanadamu katika biblia ni wale wana 11 wa Yakobo, ambao walisujudu mbele ya ndugu ya Yusufu, walipofika nchi ya Misri.

Mwanzo 43:27 “Akawaulizia hali yao, akasema, Je! Baba yenu, yule mzee mliyemnena, hajambo? Angali hai?

28 Wakasema, Mtumwa wako baba yetu hajambo, angali hai; WAKAINAMA, WAKASUJUDU”.

Mwingine aliyemsujudia mwanadamu ni Jemedari Yoabu (2Samweli 14:22), mwengine tena ni Arauna (2Samweli 24:20) na yule mwanamke wa Tekoa (2Samweli 14:4).., Hamani aliyesujudiwa na watu (Esta 3:2)

     4. Watu kumsujudia shetani na jeshi lake.

Mfano wa watu waliomsujudia shetani na majeshi yake ni Wana wa Israeli, kipindi wanakatiza Moabu, ambapo waliisujudia miungu ya Moabu, na kufanya dhambi kubwa mbele za Mungu..

Hesabu 25: 1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;

2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, WAKAISUJUDU HIYO MIUNGU YAO. 

3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli”.

Mwingine aliyesujudia mashetani ni Mfalme Yeroboamu (1Wafalme 16:31)

Swali ni je! Watu waliozaliwa mara ya pili (wa agano jipya) ni sahihi KUSUJUDU??

Jibu ni NDIO!.. Lakini anayepaswa na kustahili kusujudiwa ni MUNGU PEKE YAKE!… Wengine waliosalia ambao ni wanadamu au malaika hatupaswi kuwasujudia hata kidogo.. Maandiko kwa kupitia kinywa cha Bwana wetu YESU KRISTO yanatufundisha hilo moja kwa moja..

Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,

9  akamwambia, Haya yote nitakupa, UKIANGUKA KUNISUJUDIA.

10  Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, MSUJUDIE BWANA MUNGU WAKO, UMWABUDU YEYE PEKE YAKE.

11  Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”

Hivyo anayestahili KUSUJUDIWA ni Mungu peke yake sawasawa na maandiko hayo..

Lakini pia kusujudu na kuabudu ni lazima kufanyike katika roho na kweli ndivyo biblia inavyotufundisha, Kusujudu (kwa kuanguka chini) kunafaa sana kwa maombi ya Rehema na Toba, vile vile kwafaa sana kwa maombi ya maombi ya kupeleka mahitaji, kwani ni ishara ya unyenyekevu na kujishusha mbele za Mungu.

Na kusujudu si kanuni ya maombi, kwamba kila maombi ni lazima yaambatane na kusujudu, na kwamba usiposujudu basi maombi yako hayatasikiwa wala kukubalika,… bali ni tendo linaloambatana na msukumo wa kiungu na mzigo wa Roho Mtakatifu ndani.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAIDA ZA MAOMBI.

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Rudi Nyumbani

Print this post