Title October 2024

VIGEZO VYA NEEMA YA MUNGU.

Tangu mwanzo mwanadamu alikuwa akijaribu kujiokoa kwa njia yake mwenyewe ikiwemo kuonyesha matendo yake mazuri, na mwenendo wake mkamilifu lakini hakuweza. Pengine aliweza kushinda wizi kikamilifu lakini uongo ukamshinda, aliweza kushinda uzinzi wote, lakini tamaa zikamtawala, aliweza kushinda ibada za sanamu na vinyago, lakini kusamehe kukamshinda. Alipoweza kushinda kimoja, nyuma yake kulikuwa na elfu vinavyo mhukumu.

 

Na hiyo ilimfanya asikidhi vigezo vya kuingia mbinguni, kwasababu watakaoiona mbingu na Mungu ni watakatifu asilimia mia wasio na doa lolote. Ndio maana maandiko yanasema wote wameoza,wamepotoka hakuna amtafutaye Mungu. Bali tunahesabiwa haki bure kwa neema ya Bwana Yesu Kristo.

 

Warumi 3:11  Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. 12  Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.

 

Ndio sababu ya Yesu kuja duniani, ili kwa kupitia kumwamini yeye tuipokee hiyo neema ya kuitwa watakatifu, bila kuonyesha kwanza kipimo chochote kwa Mungu. 

Maana yake ni kuwa mimi na wewe tunapomwamini Yesu Kristo, ni moja kwa moja tunaitwa watakatifu, tuliosamehewa dhambi zetu, na kuondolewa pia. 

 

Ikiwa umemwamini leo Yesu Kristo, moja kwa moja Mungu hakuhesabii tena dhambi yoyote kama mkosaji. Ijapokuwa utakuwa hujakamilika bado.  Hii ndio maana ya neema, yaani kukubaliwa kusikostahili. Ilikupasa kwanza uwe na matendo makamilifu asilimia 100 kama Bwana Yesu, ndio uitwe mtakatifu uliyestahili kumwona Mungu. Lakini sasa kwa kuupokea ukombozi wa Yesu Kristo, dhambi zako, zimefuta unaitwa mtakatifu, kabla hata ya ukamilifu wa utakatifu wenyewe kukufikia. Ndio maana sisi tulio ndani ya Kristo hatuna budi kuwa na amani, na furaha wakati wote. Kwasababu ule mzigo mzito wa kujitahidi sisi wenyewe kuingia mbinguni umeondolewa na Yesu Kristo Bwana wetu, kwa kifo chake pale msalabani.

 

 

Lakini sasa, katika nyakati hizi za mwisho suala hili la neema limetafsirika vibaya, kama tu nyakati zile za zamani, na hapo yatupasa  tuwe makini sana. Ni sawa na taifa litangaze neema kwa nchi yake na kusema, sasa huduma zote za maji ni bure, hakuna kulipia bili,matumizi ni kama unavyotaka. halafu uone watu wanatumia fursa hiyo kwenda kufungulia  mabomba yatiririshe maji kwenye mitaro na mabarabarani, kila mahali kuwe ni maji tu,  Bila shaka utasema hawa watu wamerukwa na akili, hawana sifa ya kupewa huduma hiyo tena.

 

Ndivyo ilivyo kwa jambo linaloitwa neema, tusijipojua kanuni zake, tutajikuta badala ya kupokea wokovu, tunapokea maangamizi. Badala ya kukazana kumpendeza Mungu, tunastarehe katika dhambi,  Na ndicho kinachoendelea sasa kwa sehemu kubwa miongoni watu na madhehebu.

 

Yafuatayo ni mambo ambayo ujiepushe nayo kwa nguvu zote, wewe uliyeipokea neema ya Mungu.

 

  1. Kuipokea neema bure,

2 Wakorintho 6:1

[1]Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

Ukisoma vifungu vichache vya nyuma anasema mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya.

 

Mtu ambaye hataki geuko, baada ya kusamehewa dhambi zake, huyo ni mtu ambaye ameipokea neema bure, haithamini, ameitwa mtakatifu, halafu hataki kuishi maisha matakatifu, anaendelea na maisha yake yale yale ya kale.. Mtu kama huyo asijidanganye neema hiyo ni batili. Mtu yeyote aliyeokoka  wakati huo huo una wajibu wa kuanza kupiga hatua za mabadiliko, na unapaswa uithamini sana hiyo zaidi ya vyote, kwasababu ni Mungu ndiye akutakasaye baada ya hapo.

 

Lakini pia mtu ambaye amekaa muda mrefu hamzalii Mungu matunda, anahesabika kama aliyeipokea neema ya Mungu bure, na hivyo mwisho wake unakuwa ni kukatwa.

 

Tito 2:11  Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;12  nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 

 

Je! Umeitii neema hii inayokufundisha kukataa machafu ya duniani?. Leo yapo madhehebu yanayosema, ukiokoka umekoka milele, kazi yako imeisha, hata usipoonyesha  bidii nyingine yoyote kwa Mungu,huwezi potea. Ndugu yangu kuwa makini sana na imani hizi. Neema haipokelewi bure.

 

  1. Kuipungukia Neema

Epuke pia  kuipungukia neema.

 

Waebrania 12:15-17

[15]mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo. 

[16]Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja. 

[17]Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi.

Kuipungukie neema Ni tabia ya kuishusha thamani neema, na kuilazimisha  itende kazi hata katika kiwango ambacho si chake.

 

Hii hasa huja kwa watu ambao wanazoelea kufanya dhambi mara kwa mara wakiamini kuwa kwasababu Mungu hawahesabii makosa basi hata wakifanya kosa lolote hawawezi kupotea.

Ndugu, neema si kuhalalisha maisha ya dhambi. 

Biblia inasema..

Warumi 6:1  Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? 2  Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?

3  Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4  Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Usitende dhambi za mazoelea, ukadhani neema itakuwa sikuzote kukufunika. Ukiifanyia jeuri neema, itaondoka kwako.

 

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, 6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

 

  1. Kuibadili neema ya Mungu.

 

Yuda 1:4  Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.

 

Neema ya Mungu inaweza badilishwa ikamaanishwa kivingine kabisa. Kwamfano utaona leo hata mashoga, wanavyama vyao wakisema sisi tupo chini ya neema. Walevi nao, wenye dhambi nao wanasema neema ya Yesu ipo duniani sasa, kumwokoa kila mtu.

 

Hivyo watakuambia maneno kama usihukumu usije ukahukumiwa. Na wana amani na ujasiri katika hayo wanayoyafanya na wengine wanajiita maaskofu na wachungaji, wakihalalisha kila kitu kiovu kufanyika kwa kivuli cha neema.

 

Hao ndio waibadilishao neema ya Bwana Yesu kuwa ufisadi, hilo Neno ufisadi ni zaidi ya uasherati, Ni pamoja na matendo yote maovu kupita kiasi. Lakini neema ya Yesu,.haikuja kufunuki dhambi, bali ilikuja kuondoa dhambi ndani ya mtu. Usiwe mmojawapo aibadilishaye neema ya Mungu.

 

Hivyo kwa vifungu hivyo itoshe kusema kuwa NEEMA tunaipokea bure, lakini ili iweze kufanya kazi lazima tujue sifa zake,  kisha tuzikubali, vinginevyo tutajidanganya na kuangamia.  Ni sawa na mtu akupe gari bure, lakini usipoliweka mafuta, na kujua kuliendesha linakuwa halina tofauti na mdoli wa gari.

Lakini ukiithamini neema, itakutunza, itakuhifadhi na kuyaficha makosa yako yote, Hivyo utaendelea kuonekana mkamilifu asilimia mia mbele za Mungu, na hata ukifa, ni moja kwa moja mbinguni.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

Print this post

Neno Siuze linamaanisha nini kwenye biblia?

Siuze ni ‘Sembuse’, kwa uandishi mwingine.

Kwamfano mtu anaposema kauli hii

 “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji siuze mimi, kuzidi hapo?


.Ni sawa tu  na kusema “Kama Bwana Yesu alikuwa mwombaji sembuse mimi, kuzidi hapo?

Maana ya Neno hilo ni. “Si zaidi

‘Kama Bwana alikuwa mwombaji si zaidi mimi kuzidi hapo’.

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu ambavyo utalisoma neno hili kwenye biblia;

 

2 Mambo ya Nyakati 6:18

[18]Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga! 

 

2 Wakorintho 3:9

[9]Kwa maana ikiwa huduma ya adhabu ina utukufu, siuze huduma ya haki ina utukufu unaozidi. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Neno vuruvuru linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

Kuna Mbingu ngapi?

Rudi Nyumbani

Print this post

IFUATE KANUNI SAHIHI YA MUNGU

Zipo kanuni za ki-Mungu tunaweza kuzifuata na zikaleta matokeo kabisa halisi, lakini zisiwe na manufaa kwetu katika suala la wokovu.  Sasa kabla ya kuangalia ni kwa namna gani? 

chukulia mfano wa kawaida.

Mwanamke yeyote anaweza kubeba ujauzito katika mazingira mbalimbali, kwamfano anaweza akatwezwa nguvu (akabakwa), na akapata ujauzito, lakini pia anaweza kwenda kujiuza kama kahaba na bado akapata ujauzito, vilevile anaweza akasubiri aolewe kwanza katika ndoa halali ndipo apokee ujauzito na likafanikiwa vilevile tu, kuleta kiumbe duniani, kama angefanya hayo kabla ya ndoa, au atokapo nje ya ndoa yake.

Sasa unaweza jiuliza, katika njia zote hizo ambazo angepata ujauzito ni ipi iliyo halali inayokubalika mbele za Mungu na wanadamu. Bila shaka ni hiyo njia ya mwisho ambayo ni ya kuolewa kwanza, ndipo apokee ujauzito kutoka kwa mume wake mmoja wa halali. Na ndio mtoto huyo hujulikana kama halali sio haramu.

Lakini cha ajabu ni kuwa ijapokuwa njia halali ipo lakini feki pia huleta matokeo yaleyale mfano wa halali. Kwasababu gani? Kwasababu kanuni ya kupata mtoto, si kanuni ya uhalali. Hivyo ni vitu viwili tofauti, 

Hata Ibrahimu, alikuwa na watoto wengi, alitangulia Ishmaeli, kisha baadaye wakazaliwa na watoto wengine sita kwa suria mwingine, mbali na Isaka. Wote walikuwa wanadamu, viumbe wa Mungu, wenye akili na nguvu na baraka, wasio na hatia. Lakini lilipokuja suala la urithi, ndipo kubaguliwa  kulipokuja, Watoto wote wa masuria walifukuzwa wakapewa zawadi tu bali Isaka alipewa vyote.

Mwanzo 25:5-6

[5]Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo. 

[6]Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu. 

Hii ni kutufundisha nini hasaa katika maisha yetu ya wokovu.

Zipo kanuni nyingi sana za kiroho ambazo mtu yeyote, hata ambaye  hajamwamini Yesu anaweza zitumia na zikatoa matokeo yaleyale sawa tu na mtu ambaye ameokoka.

Kwamfano, kufanya miujuza na ishara kwa jina la Yesu. Watu hawajui kuwa jambo hili huhitaji imani tu, katika jina lake. Hivyo wale wafikiao kiwango hicho haijalishi ni mwizi, ni mpagani, anaweza pokea muujiza na akafanya pia muujiza sawa tu na yule aliyeokoka.

Kwasababu gani? kwasababu amefanikiwa kufuata kanuni ambayo ni Imani.

Akijua lile neno linalosema  ‘yote yawezekana kwake yeye aaminiye’’ (Marko 9:23). Ndio maana walikuwepo watu wengi wasiokuwa wayahudi kipindi kile cha Yesu walipokea miujiza mikubwa, zaidi ya wayahudi kwasababu tu ya ukubwa wa imani zao. Na sio haki zao.

Vivyo hivyo hata katika kuomba. Mtu yeyote aombaye hupokea. Ni kanuni ya asili ya rohoni, haijalishi ni nani.

Mathayo 7:8

[8]kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 

Watu hawajui hata kufanikiwa kwa shetani hutegemea maombi, na yeye pia huenda mbele za Mungu kuomba na hupewa..hajiamulii tu mambo yake ovyo ovyo bila idhini ya Mungu, kwasababu hii dunia si yake… utauliza kwa namna gani, ? unamkumbuka shetani kipindi cha Ayubu, yeye naye alikwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, ndipo akaleta uharibifu. Akapeka haja zake akasikiwa, dua zake na magoti yake.

Ayubu 1:6

[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. 

Watu wengi wanapoona wanamwomba Mungu wanajibiwa wanadhani, ndio wamekubaliwa na Mungu. Kumbe unaweza kuomba kama mwana-haramu usiyekuwa na urithi wa uzima wa milele, bali haki ya kupokea tu unachokiomba.

Unaweza ukafanya miujiza kama mwana-haramu. Lakini usiende mbinguni.

Mathayo 7:22-23

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. 

 Unaweza ukamwamini Yesu, na kumuhofu,  lakini ukaamini kama mashetani.

Yakobo 2:19

[19]Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. 

unaweza ukawavuta watu kwa Kristo na wakaokoka, lakini ukawa mtu wa kukataliwa kama tu Paulo alivyosema katika; 

1 Wakorintho 9:27

[27]bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa. 

Sasa kanuni sahihi ya Mungu ni ipi ili tuonekane kamili na halali?

Kanuni Mungu anayoitazama kwetu ni Wokovu uliokamilishwa kwa matendo yake.

Angalia mwishoni pale kwenye Mathayo 7:23 Bwana Yesu alichokisema;

“ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona je unaishi maisha gani?. hicho ndio kipimo cha ki-Mungu, 

Alisema pia.

Yakobo 2:24

[24]Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 

Hakikisha maisha yako yanaendana na ukiri wako, wa imani yako, usiishi tu kama mtu ambaye hajaamini ukijitumainisha, kuona maombi yako yanajibiwa, karama yako inafanya kazi, imani yako inatenda kazi..hizo ni kanuni za kupokea lakini sio kanuni za uhalali wa kuurithi uzima wa milele. Ishi kama mtu ampendezaye Bwana wake kimwenendo, ndipo hayo mengine yakifuata huna hasara.

Nyakati hizi za mwisho, adui anaweka uzito kwenye mioyo ya watu wasipende kutafuta maisha matakatifu, kinyume chake wabakie tu kwenye miujiza, uponyaji, utabiri…Siku ile hivyo vitu havitafuata na wewe ndugu, bali matendo yako.

Ufunuo wa Yohana 14:13

[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao. 

Tuanze sasa kujipima mienendo yetu. Kisha tutumie nguvu nyingi hapo kujirekebisha, sawasawa na imani tuliyoipokea, ili tuwe wana halali waliozaliwa kweli ndani ya Kristo, watakaorithi uzima wa milele.

Wokovu wa kweli hufunuliwa kwa mwenendo mzuri. Tuitazame sana kanuni hii.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANUNI JUU YA KANUNI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Print this post

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

SWALI: Naomba kufahamu ujumbe ulio katika Mithali 29:5

‘Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake’.

JIBU: Mithali hii inazungumzia madhara yanayoibuka katika tabia ya kujipendekeza.

Kujipendekeza ni kitendo cha mtu kumthaminisha mtu, hata kama alikuwa hastahili sifa hizo, ili tu upate kitu Fulani kutoka kwake. Kumthaminisha kunaweza kuwa kumsifia, au kumpongeza, au kumzungumzia mema yake kupita kiasi, au kueleza mabaya ya wengine kwa huyo mtu, n.k.

 Na yote hayo hayawi kwa lengo la kuuthamini kweli uzuri wa Yule mtu, hapana bali  ni aidha upate kupendwa wewe zaidi ya wengine, au usaidiwe, au upewe cheo,  au kipaumbele Fulani. Hata kama utaona mabaya yake huwezi kumwambia kwasababu, huna lengo la kusaidia bali upate matakwa yako tu.

Sasa  hilo ni kosa, matokeo ya hilo biblia inatuambia “unamtandikia wavu ili kuitega miguu yake”. Yaana unampeleka kwenye mtego au aungamivu wake kabisa.  Hii ni kweli, tunaona hata viongozi wengi wa nchi wameponzwa na wasaidizi wao wa karibu,na matokeo yake wakaiharibu  nchi, kwasababu tu ya kupokea sifa za uongo kutoka kwao, kwamba wanafanya vema, wanawajibiki vizuri n.k..  Kama ilivyokuwa kipindi kile cha Mfalme Sedekia na wale manabii wa uongo wajipendekezao, walimtabiria uongo, lakini Yeremia alimweleza mfalme ukweli  hawakutaka kumsikiliza. Matokeo yake Mfalme Sedekia akaingia katika matatizo makubwa ya kutobolewa macho na kupelekwa utumwani, hiyo yote ni kwasababu alikaa na manabii wajipendekezao (Yeremia 34-41), kama tu ilivyokuwa Kwa Mfalme Ahabu naye na manabii wake mia nne wa uongo.

Hii ni kutufundisha nini?

Hasaa biblia hailengi, tuwe makini na watu wajipendekezao. Hapana, kwasababu wakati mwingine si rahisi kuwatambua, inahitaji neema ya Mungu. Lakini inalenga hasaa katika upande wetu , kwamba sisi tujiepushe na ‘tabia ya kujipendekeza”. Kwasababu tunaweza kudhani tunatafuta faidi yetu tu wenyewe, lakini kumbe tunamsababishia madhara Yule mtu ambaye tunajipendekeza kwake. Tunategea wavu mbaya sana, aanguke na kupotea kabisa, na huo si upendo.

Itakusaidia nini akutendee mema, halafu yeye aangamie?

Hivyo, pastahilipo kweli kusifia tusifie, lakini si kwa lengo la kujipendekeza, kwasababu tukienda huko, tunatenda dhambi kubwa zaidi. Hiyo ndio maana ya hivyo vifungu, tufikiriapo kujipendekeza, tuone kwamba ni watu wasio na hatia tunawategea wavu waangamie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kama ni Mungu ndiye kaumba zao la Bangi kwanini tena iwe dhambi kuitumia??

Swali: Biblia inasema tumepewa mboga za majani kuwa chakula chetu, na Bangi pia ipo miongoni mwa zao la mboga za majani…sasa kwanini iwe dhambi kulitumia kama mboga au kiburudisho cha kusisimua (kuvuta) na ilihali ni Mungu mwenyewe ndio kaumba?


Jibu: Turejee..

Mwanzo 9:3 “Kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa MBOGA ZA MAJANI, kadhalika nawapeni hivi vyote”.

Ni kweli maandiko hayo yanathibitisha ulaji wa mboga, lakini si mboga zote!.. Tukisema kila mboga iliyopo kondeni tumepewa tule, tutakuwa hatujayaelewa vizuri maandiko kwasababu  kuna mboga nyingi sana ambazo sumu!, ambazo zinamwonekano mzuri lakini hazifai kwa chakula… na Mungu hawezi kumpa ruhusa Mtu wake aliyemuumba, ale SUMU!..

Zipo mboga kwaajili ya chakula cha wanadamu, nyingine kwaajili ya wanyama na hazifai kwa wanadamu… vile vile zipo mboga zisizofaa kwa chakula cha wanadamu na wanyama… Mboga hizo zinabaki tu kwa utukufu wa Mungu, au kwaajili ya urembo, mfano wa mboga hizo ni MAUA.

Kuna Maua ambayo yana mwonekano mzuri sana lakini ni SUMU kali sana, mfano wa hayo ni kama haya yanavyoonekana hapa chini.

maua sumu

Hayo ni mfano wa Mboga, lakini si kwaajili ya kula bali kwaajili ya urembo tu.. yameumbwa na Mungu kwa lengo hilo, hivyo mtu akila hayo anaweza kupata madhara makubwa ya kiafya au hata kifo.

Vile vile na Bangi, inaweza kuwepo katika kundi hilo la MAUA, kama itatumika kwa urembo si vibaya, lakini kwa matumizi mengine ya ndani ya mwili wa binadamu ni hatari.

Kwahiyo si kila kilicho halalishwa basi kinafaa kwa matumizi yote.. hapana!.. Mboga zimehalalishwa lakini si kwa matumizi ya chakula tu, ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 10:23  “Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo”.

Kwahiyo ulaji, au uvutaji wa Bangi ni dhambi kibiblia, vile vile matumizi ya tumbaku kula au kuvuta ni dhambi, kwani miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na tena maandiko yanasema mtu akiliharibu hekalu hilo Mungu naye atamharibu mtu huyo (Soma 1Wakoritho 3:16-17 na 1Wakorintho 6:19).

Na Bangi inaharibu ufahamu wa mtu, ambao ndani yake kunazalika hasira, kutokujali, vurugu, matukano, mauaji, uasherati na mambo yote mabaya..

Hivyo Bangi ni haramu, vile vile tumbaku na mazao mengine yaletayo matokeo kama hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

MTINI, WENYE MAJANI.

JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Nini maana ya mmoja alikufa kwaajili ya wote hivyo walikufa wote? (2Wakorintho 5:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Nehemia 8:10

[10]Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.

Ni habari ya kutafakarisha, lakini zaidi sana ya kuwafariji watu wote wampendao Mungu. Tukisoma katika biblia ile habari ya Ezra na Nehemia, katika juhudi zao wa kuwarejesha Israeli katika ibada na njia za Mungu Yerusalemu.

Tunaona wakati ule ukuta wa Yerusalemu ulipomalizwa kujengwa baada ya kurudi kwao utumwani Babeli, Ezra hakuwaacha tu hivi hivi, wafurahie kukamilika kwa majengo, bali alitaka wakamilishwe na mioyo yao hivyo, alikichukua kitabu cha Torati na kuanza kuwasomea wayahudi wote tangu asubuhi mpaka adhuhiri, ili wajue ni nini Bwana anataka kwao (Nehemia 8).

Na waliposikia waliona makosa yao mengi sana, na hukumu nyingi za Mungu, alizowatamkia kufuatana na makosa yao, yaliyowapelekea mpaka wakachukuliwa mateka. Ikumbukwe kuwa kitabu hicho cha torati hakikuwahi kusomwa tangu zamani walipochukuliwa utumwani, ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kukisoma baada ya miaka mingi kupita.

Hivyo wayahudi kusikia vile wakaanza kulia sana na kujuta na kuomboleza. Lakini tunaona kuna jambo lilifanyika la kitofauti.

Nehemia, alitambua wazo la Mungu…Hivyo akawazuia watu kulia na kuomboleza kwa ajili ya makosa yao. Kinyume chake akawaambia leo ni siku takatifu kwa Bwana, hivyo mle ,.mnywe, mtoe sadaka, mfurahi mbele za Mungu wenu kwasababu “furaha ya BWANA ni nguvu zenu” 

Hivyo watu wakasheherekea, badala ya kulia, Sio kwamba Nehemia alisheherekea makosa yao, hapana, bali alipewa kujua kwamba  furaha ya mtu kwa Mungu wake, ndio chanzo cha nguvu ya kumtumikia yeye. 

Ndio hapo baada ya wayahudi kujua makosa yaowakimfurahia Mungu, siku hiyo, na wakapokea nguvu nyingi za kuishika sheria ya Mungu. 

Yaani kwa namna nyingine, Mungu kuwakemea makosa yao,lengo lake lilikuwa sio awahukumu, au wainamishe vichwa vyao wakidhani kuwa wao ni kichefu-chefu kwake. Hapana..Bali anawapenda na hivyo anatarajia wajue nia ya makemeo yake.

Nehemia 8:10 Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.

11 Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike. 

12 Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa

 

Ni hata sasa, unaposoma biblia na kuona inakushitaki, inakuambia usiibe, usisengenye, amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji, wazinzi wote sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, inapokukemea maovu yako ya siri.. Usiinamishe kichwa na kusema “mimi sifahi mbele za Mungu, mimi ni mkosefu sistahili kuitwa mwana wake”..Ukaacha kukisoma kabisa, ukawa unalia tu, umenyong’onyea, na kujihisi wewe ni wajehanamu tu, Mungu hakupendi, ameshakuacha, ona sasa unamkosea kosea kila siku… Fahamu kuwa hilo sio kusudi la Mungu.

Kusudi la Mungu sio usome biblia, ujawe na hisia za Mungu kukuhukumu, au kukulaumu, au kukushitaki, bali kusudi la Mungu ni ujue  upendo wake uliozidi sana kwako, kiasi cha yeye kuonyesha hisia zake kwako namna ambavyo unapaswa uwe kama yeye.

Hivyo ukitoka kuonywa na kukemewa, unapaswa utoke kwa kufurahi moyoni  na kuruka-ruka, na hapo ndipo utapokea nguvu ya kuishinda hiyo dhambi. Lakini ukitoka kinyonge na mashaka utashindwa kwasababu furaha ya Bwana ndio chanzo cha nguvu zetu. Ukilipenda hilo katazo, utalitenda, usipolipenda kamwe huwezi litenda.

Mtunga Zaburi alisema,

Zaburi 119:52

[52]Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee BWANA, nikajifariji.

Bwana anataka tuone upendo wake kwetu katika makemeo yake, tufarijike tupokee nguvu ya kushinda. Pengine umetoka kufanya dhambi fulani ya makusudi na Roho Mtakatifu akakumbusha kuwa watu wa namna hii, huangukia katika mtego mbaya wa shetani bila kunasuka, Sasa hapo usianze kupoteza ladha na Mungu wako, au biblia, ukauchukia wokovu, kabisa,  maanisha kutubu, jifunze kutokana na makosa, kisha furahia mwambie Bwana asante kwa kunipenda,

hata wachezaji wa mpira, wafungwao kipindi cha kwanza, wanapotulia na kujihamasisha tena, hupokea nguvu ya kucheza vema kipindi cha pili, lakini wajilaumupo, hufanya vibaya zaidi

Na sisi pia tuiamshe furaha ya Bwana daima.Kila tusomapo Neno lake, tufurahi kwasababu ni barua ya upendo wa Mungu kwetu Ili tuweze kuwa na nguvu.

Kwasababu furaha ya Bwana ndio nguvu yetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

Furaha ni nini?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

 

Print this post

USI..USI..USI.

Usi!.. Usi!.. Usi! na sio Msi!… Msi!.. Msi!..

Amri za Mungu zinasema Usiue, Usizini, Usiibe … na sio Msiibe, Msiue, Msizini… Ikifunua kuwa Mungu anaongea na mtu mmoja mmoja… Anasema na Mimi kivyangu, lakini pia anasema na wewe kivyako… Na hatuambii wote kwa pamoja.

Kutoka 20:13 “Usiue. 

14 Usizini. 

15 Usiibe. 

16 Usimshuhudie jirani yako uongo. 

17 Usiitamani nyumba ya jirani yako…”

Siku ya Hukumu, hatutahukumiwa kwa pamoja, kila mtu atasimama peke yake, na kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe..

Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.

Na tena kila mtu atatoa habari zake mwenyewe na si pamoja na mwenzake..

Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”

Sasa kama ni hivyo kwanini Boss wako akukoseshe?..kwanini Rafiki akukoseshe, kwanini wanadamu wakukoseshe??… Na ilihali utasimama peke yako siku ile.

Kumbuka unapofanya uzinzi, siku ile hutakuwa na yule aliyefanya naye uzinzi, badala yake utasimama wewe kama wewe (kwasababu ile amri  inakuhusu wewe, na Mungu alikuwa anazungumza na wewe kivyako na si wewe pamoja na mwenzako)..

Kama unaiba, siku ile hutasimama na aliyekushawishi ukaibe, au uliyekuwa unashirikiana naye katika wizi.. wewe utakuwa peke yako, na yeye peke yake….kwasababu Amri ya Usiibe, uliambiwa wewe, nimeambiwa mimi na si wewe pamoja na mimi… Hivyo kila mtu atatoa habari zake mwenyewe.

Kama unaua, ni hivyo hivyo, kama uwaheshimu wazazi ni hivyo hivyo, na amri zote ni hivyo hivyo..

Hukumu ya Mungu inatisha!.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?

Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe;

CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.

Rudi Nyumbani

Print this post

KUWA MAKINI NA MATANGO MWITU, SIKU HIZI NI ZA MWISHO!

Kuna wakati Elisha alifika Gilgali na mahali pale palikuwa na njaa kali, na watu wengi (manabii) pia walikuwa  wamekusanyika kusikiliza mashauri ya mtu wa Mungu.

Hivyo akawaambia waweke sufuria motoni waandae chakula.

Lakini mmojawao akatoka akaenda mashambani kutafuta mboga. Na huko akafanikiwa kweli kukusanya zilizo bora, lakini kwasababu hakuwa na maarifa ya kutosha jinsi ya kutambua mboga sahihi ziwafaazo wanadamu akaona huko matango mwitu, na bila kujua, akidhani ni matango halisi, akayachuma na kuyaleta sufuriani. Matango yale yalikuwa ni sumu.

Lakini walipoonja kwa neema za Mungu walijua kuna kitu ambacho sio sahihi kimewekwa sufuriani, hivyo waacha wote kula. Ndipo Elisha akataarifiwa, juu ya jambo hilo, kama kimwagwe lakini kile chakula hakikumwagwa, bali aliwaagiza watie unga mule (kwa Neno la Bwana), na chakula kitaponyeka.  Wakafanya hivyo, kikawa sawa, wakala wakashiba.

2 Wafalme 4:38-41

[38]Elisha akafika Gilgali tena; na kulikuwa na njaa katika nchi; na hao wana wa manabii walikuwa wakikaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, Teleka sufuria kubwa, uwapikie wana wa manabii.

[39]Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtango-mwitu, akayachuma matango-mwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasua-pasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.

[40]Basi wakawapakulia hao watu ili wale. Ikawa, walipokuwa katika kula chakula, wakapiga kelele, wakasema, Mauti imo sufuriani, Ee mtu wa Mungu. Wala hawakuweza kula.

[41]Lakini yeye akasema, Leteni unga. Naye akautupa ndani ya sufuria; akasema, Wapakulie watu, ili wale. Wala hakikuwamo kitu kibaya sufuriani.

Habari hiyo inafunua nini?

Inatueleza hali ya kiroho ya watu iliyopo sasa.

Palipo na njaa ni rahisi mtu kula kila kitu, ilimradi tu asife. si rahisi akae chini na kufikiria ubora wa kile anachokula. Leo hii njaa ya Neno la kweli la Mungu ni kubwa, hivyo kila mtu anaenda kondeni kuokota kitu kimfaacho, huko huko tunakutana na vizuri lakini pia tunakutana na vibaya..

shida ipo hapo, je tunaweza kupambanua?

Kwasababu ukila sumu, ile sumu haitakuambia ngoja nisikuletee madhara kwasababu hukukusudia kunila, au hukujua kuwa mimi ni sumu, utakufa tu  sawasawa na yule anayejua anachokifanya.Kumbe ujinga una gharama kubwa.

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 7:15

[15]Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

Mafundisho yasiyomhubiri Kristo na utakatifu, ni kuwa makini nayo, ni heri usiyasikilize kabisa kwa usalama wako wa kiroho. Yanayokuambia tunaokolewa kwa neema tu, hivyo matendo yako ni kazi bure mbele za Mungu, ukiokolewa umeokolewa milele, hata ukiwa unatenda dhambi vipi huwezi potea, yapime sana hayo mafundisho.

Mafundisho ya kuzimu-kuzimu tu na majini na wachawi epukana nayo, Mafundisho ya sanamu ibadani, ni mauti chunguni. Mafundisho yanayopinga habari za mwisho wa dunia, ambayo hayana habari na unyakuo au kumfanya mtu atazame kurudi kwa pili kwa Kristo, kinyume chake ni kukuweka kidunia, ufikirie mafanikio ya mwilini ni matango mwitu.

Manabii wa uongo ni wengi, wapo wanaotenda kazi kwa uwazi, lakini  wapo wanaotenda kazi kwa siri.

Jifunze kusoma biblia, jinsi usomavyo Neno la Mungu utagundua kuwa mtu uliyeokoka  kwa wakati uwapo hapa duniani Bwana anakutana Utembee katika utakatifu (Waebrania 12:14). Lakini pia uelekeze macho yako mbinguni kwa yale mambo yajayo, ya mbingu mpya na nchi mpya.

Luka 12:35-36

[35] Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; [36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

Jihadhari na matango mwitu.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii  >>>> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Kusanyiko la makini/ mkutano wa makini ni upi?

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

 

Print this post

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Swali: Kulikuwa na ubaya gani wa Adamu na Hawa kula matunda ya mti wa Uzima, ili wapate tena uzima wa milele baada ya kuupoteza? (Mwanzo 3:22-24).


Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mwanzo 3:22 “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, AKALA, AKAISHI MILELE;

23 kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa”.

Sababu pekee ya Bwana MUNGU kuwazuia wazazi wetu wa kwanza (Adamu na Hawa) kula yale matunda ya Mti wa Uzima, si kwamba Mungu alikuwa hataki waishi milele!. La!.. kinyume chake ni mpango wake mkamilifu wa Mungu kwamba mwadamu aishi milele.

Tito 1:2 “katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele”

Soma pia 1Yohana 2:25 utaona jambo hilo hilo…

Lakini kwasababu tayari mwanadamu alikuwa ameshaiingiza dhambi ndani yake na katika kizazi chake, hivyo asingeweza kuishi milele katika dhambi, hivyo ni lazima dhambi iondoke kwanza ndani yake ndipo aishi milele, kwasababu kama akiishi milele na dhambi imetawala maisha yao, ni uharibifu mkubwa utaendelea na maisha yatakuwa nje na mpango wa Mungu, kwasababu yeye Mungu ni mkamilifu, hivyo kanuni ya maisha ya milele, ni sharti yasiwe na dhambi.

Kwahiyo BWANA MUNGU akaweka mpango kwanza wa kuiondoa dhambi ndani ya mtu, na mzizi wake, kisha yule mtu apate tena uzima wa milele.

Na mpango wa Mungu wa kuondoa dhambi ndani ya Mtu na kumrejeshea Uzima wa milele, ameushona ndani ya Mwanae YESU KRISTO, kwamba kwa kupitia njia ya kumwamini yeye, na kutubu basi tunaoshwa dhambi zetu na kupata uzima wa milele.

Warumi 5:21 “ili kwamba, kama vile dhambi ilivyotawala katika mauti, vivyo hivyo kwa njia ya haki neema itawale hata uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu”.

17  Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye”.

Hivyo kamwe hatuwezi kupata uzima wa milele, tukiwa katika dhambi..ni lazima kutubu kwanza na kumwamini Bwana YESU ndipo tupate uzima wa milele.

Na hiyo ndio sababu ya Bwana MUNGU kuifunga ile njia ya MTI WA UZIMA pale Edeni, ilikuwa ni sharti kwanza ADAMU na HAWA watakaswe ndambi zao kwa damu ya Mwanakondoo… Na majira yalipofika Mungu alimtuma mwanae ili afe kwaajili ya wote walio hai, na waliokwisha kutangulia, waliokufa katika haki, ili kwamba wote tutakaswe na kupata uzima wa milele.

Na hili ni la kujua siku zote, kwamba hakuna uzima wa milele kwa mwingine yeyote Zaidi ya YESU KRISTO.

Yohana 3:35 “Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.

36  Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Mistari ifuatayo inazungumzia uzima wa milele ndani ya YESU KRISTO (1Yohana 5:11-13, Yohana 3:16, Yohana 5:24,  Yohana 6:54,  Yohana 12:50, Yohana 17:2, na Warumi 6:23)  .

Je umempokea BWANA YESU?… kama bado unangoja nini?..Fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, majira yameenda sana na ule mwisho umekaribia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

MJUE SANA YESU KRISTO.

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. 

SWALI: Nini maana ya Waefeso 6:24, pale inaposema “katika hali ya kutoharibika”?

[24]Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.


JIBU: Mtume Paulo alipokuwa anahitimisha ujumbe wa waraka wake kwa waefeso, alimalizia kwa kuwatamkia neno la heri watu watu wale akiwaambia ‘NEEMA  ikae pamoja nao.

Lakini tunaona hapo hakukusudia tamko hilo kwa watu wote,  bali anasema ikae kwa wale wampendao Bwana, lakini bado sio tu kwa  wampendao Bwana.. Bali wampendao katika “hali ya kutokuharibika”.

Yaani kwa ufupi upendo usio poa.. Ndio upendo usio haribika.

Ndio ule unaozungumziwa kwenye 1Wakoritho 13. Kwamba hustahimili yote, huvumilia yote, huamini yote, haupungui Neno wakati wowote.

Ni kuonyesha kuwa Bwana wetu Yesu Kristo anastahili kupendwa daima, zaidi ya vitu vyote, kwasababu ya upendo wake mkuu aliotuonyesha sisi wa kuacha vyote mbinguni kwa ajili yetu, ili tukombolewe. Na kwa rehema zake akatupa na vipawa kabisa, na uwezo wa kuitwa wana wa Mungu, kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu aliyetupa . Hakika anastahili kupendwa  sana bila ukomo.

Zingatia: Waraka huu sio wa waefeso tu, bali ni wetu pia sote tumeandikiwa. Hivyo tutaongezewa neema ikiwa tutampenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usio haribika. Sio njaa itufanye tumwache, au ufukara, au mke, au kazi, au uzuri, au ubaya, au ndugu, au mali, au afya, au ugonjwa.. au kitu chochote, Bali kila wakati sisi shauku yetu kwa Kristo iwe ni ile ile. Kuomba ni kule-kule, kumtafuta Mungu ni kule-kule. Amen

Neema ya Bwana iwe nasi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Rudi Nyumbani

Print this post