SWALI: Mstari huu una maana gani? Je, ni kweli waandishi waliweza kubadilisha baadhi ya maneno ya torati, Na hivyo inaifanya biblia isiamike hadi sasa?
Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.
JIBU: Hii ni hoja inayotumiwa sana na wapinga-biblia, au wapinga-ukristo. Wakisimamia mstari huu, na kusema, unaona? Biblia ilichakachuliwa, zamani na waandishi wa kiyahudi kwa kuongeza baadhi ya maneno katika torati iliyoandikwa na mwenyezi Mungu,.. Kwahiyo hiyo inathibitisha kuwa biblia ni kitabu chenye kasoro..
Lakini je tukisoma vifungu hivyo, vinatuambia waliibadilisha torati?
Kabla ya kuendelea kusoma zaidi, embu tuitafakari tena hiyo kauli hapo mwishoni, anasema “kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo”. Ahaa Kumbe waandishi ndio wameifanya kuwa uongo..Lakini yenyewe kama yenyewe sio uongo.. Mfano nikikuambia, unanifanya kuwa mwongo mbele za ndugu zangu, haimaanishi kuwa mimi ni mwongo..maana yake ni kuwa, pengine ni kwasababu uliyawakilisha maneno yangu isivyopaswa, aidha kwa kuongeza chumvi au kupunguza, na kwasababu hiyo basi, mimi nikaonekana nimeongopa, lakini sivyo, mimi nilisema ukweli mwanzo, isipokuwa wewe ndio umeniwakilisha vibaya.
Ndivyo ilivyokuwa hapo, waandishi, ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kufundisha na kuwaelezea watu, walianza, kutoa tafsiri zisizo sawa za torati, na kuwafundisha watu na kuwaandikia, mfano Bwana Yesu alisema, waliipindua amri ya tano; inayosema waheshimu baba yako na mama yako, na kuwaambia watu, ikiwa kuna chochote umekiweka wakfu hupaswi kumsaidia mzazi wako, hata kama akiangamia kwa njaa ni sawa tu..Jambo ambalo Mungu hakuliagiza hata kidogo, ilikuwa ni wajibu wa kila mtu kumsaidia mzazi wake, awapo katika uhitaji (Soma Marko 7:7-13)
Umeona, sasa tukirudi kwenye ile habari ya mwanzo ili kuthibitisha hilo vizuri, ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata utaona Yeremia, anaeleza kwa undani jinsi kalamu za hao waandishi zilivyoweza kuipa torati tafsiri zisizo sahihi..
Yeremia 8:8 “Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi? Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo. 9 Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la Bwana, wana akili gani ndani yao? 10 Basi, kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao na mashamba yao nitawapa wale watakaowamiliki; MAANA KILA MMOJA WAO, TANGU ALIYE MDOGO HATA ALIYE MKUBWA, NI MTAMANIFU; TANGU NABII HATA KUHANI, KILA MMOJA HUTENDA MAMBO YA UDANGANYIFU. 11 KWA MAANA WAMEIPONYA JERAHA YA BINTI YA WATU WANGU KWA JUU-JUU TU, WAKISEMA, AMANI, AMANI, WALA HAPANA AMANI. 12 Je! Walitahayarika, walipokuwa wametenda machukizo? La! Hawakutahayarika, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi wataanguka miongoni mwao waangukao; wakati wa kujiliwa kwao wataangushwa chini, asema Bwana..
9 Wenye hekima wametahayari, wamefadhaika na kushikwa; tazama, wamelikataa neno la Bwana, wana akili gani ndani yao?
10 Basi, kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao na mashamba yao nitawapa wale watakaowamiliki; MAANA KILA MMOJA WAO, TANGU ALIYE MDOGO HATA ALIYE MKUBWA, NI MTAMANIFU; TANGU NABII HATA KUHANI, KILA MMOJA HUTENDA MAMBO YA UDANGANYIFU.
11 KWA MAANA WAMEIPONYA JERAHA YA BINTI YA WATU WANGU KWA JUU-JUU TU, WAKISEMA, AMANI, AMANI, WALA HAPANA AMANI.
12 Je! Walitahayarika, walipokuwa wametenda machukizo? La! Hawakutahayarika, wala hawakuweza kuona haya usoni; basi wataanguka miongoni mwao waangukao; wakati wa kujiliwa kwao wataangushwa chini, asema Bwana..
Umeona hapo? Anasema, hao waandishi na makuhani, wanawatabiria watu amani, amani, na kuwaambia mnaishi sawasawa na torati ya Mungu inavyosema, hivyo hamwezi kupatwa na madhara, ili hali ndani yao wanatamani, ni waovu, waabudu masanamu, wanakula rushwa n.k..
Wakati torati inakataza vikali vitu hivyo, wenyewe wanawatumainisha watu, Mungu anawapenda, ndio hapo anasema, wanawaponya jeraha zao kwa juu juu tu, mwisho wa siku wanaadhibiwa, halafu wanasema Mungu ni mwongo.. Mbona anatupiga bila sababu!.
Je! Waandishi wa namna hii wapo hadi sasa?
Jambo hili lipo hadi sasa katika kanisa la Mungu, Siku hizi za mwisho makristo na manabii wengi sana wa uongo wametokea, nao wanawaponya watu wa Mungu juu juu tu, hawawaelezi ukweli, mpaka inafikia hatua Mungu anaonekana mwongo, hasikii wala hajibu.
Wanawaambia, utafanikiwa, utabarikiwa, kesho yako ni ya kung’ara kama jua, wanawaambia watoe sadaka nyingi, watumie maji ya upako, mafuta na chumvi, wakati mwingine wafunge mwaka mzima, Mungu atawabariki.. Lakini wanasahau kuwa hao watu wana mizigo ya dhambi, ndiyo inayowafanya wasijibiwe maombi yao.. Kama vile maandiko yanavyosema..
Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”.
Isaya 59:1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”.
Hivyo hao watu wanataabika, januari mpaka disemba, lakini hawaona nuru yoyote, hawaona uzima wowote, ndio kwanza hali inakuwa mbaya, mwishoni wanakataa tamaa wanasema Mungu hajibu maombi, wanawageukia waganga wa kienyeji.
Ndugu, Neno la Mungu ni kweli kabisa, akisema atakuponya, atakuponya kweli, akisema atakubariki atakubariki kweli, lakini ni sharti ujue, anataka nini kwanza kwako ili hivyo vyote vikujie.. Anachotaka ni wewe uache dhambi, uache, rushwa, uache uzinzi, uache uongo, uache vimini, uache fashion za kidunia, anasa, uache ulevi, uwe mtakatifu. Ndipo hayo yote yatakapokujia..
Epuka injili zizisogusia dhambi katika maisha yako, ziepuke kama ukoma, hizo huwa zinakuja na maneno mazuri sana ya kushawishi na kufariji, lakini hazitakusaidia chochote, Mungu ni mtakatifu, kamwe hajibu maombi ya mwenye dhambi.
Je! Umeokoka? Kweli kweli kwa kumaanisha kumfuata Kristo? Kama la! Basi huu ndio wakati wako sasa kuanza upya na Kristo. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi, waweza tupigia kwa namba uzionaza hapo chini.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA NA WASIO WAKRISTO (Sehemu ya kwanza).
Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?
Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?
Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)
KUONGOZWA SALA YA TOBA
Rudi nyumbani
Print this post
Unawaza nini juu ya kuipeleka injili mbele?..Je unafikiri nini juu ya hali ya kiroho ya wanao miaka kadhaa mbele?, endapo parapanda itakuwa haijalia miaka 20 ijayo, je hali ya kiroho ya wanao itakuwaje, ukilinganisha na kasi ya maadili kuporomoka?.. Je umewahi kufikiri kufanya chochote leo hii, ili miaka ya mbeleni watoto wako au Watoto wa wengine, wasikose chakula cha uzima?…
Kizazi tulichopo ni kizazi kinachoharibika kila siku, umewahi kufikiri hali itakuwaje miaka 10 mbeleni?..kama umewahi kufikiri kwamba hali utakuwa mbaya Zaidi kuliko sasa, basi pia jiulize leo hii unafanya nini ili wakati huo utakapofika, shetani asipate nafasi inayoiona mbeleni.
Kumbuka wewe usipotumia muda wako leo, au akili zako leo, au nguvu zako leo, kufikiri na kufanya jambo lolote juu ya ufalme wa Mbinguni, Bwana atafanya kupitia wengine, (kwasababu kazi yake ni lazima iende mbele) lakini wewe wewe utakuwa umejipunguzia thawabu zako mbele zake.
Hebu Leo tujifunze juu ya watu wawili katika biblia, ambao kupitia hao, tutapata hamasa na hekima katika kufikiri kuujenga ufalme wa mbinguni.
Mtu wa kwanza ni DANIELI, na wa pili ni YUSUFU. Watu hawa wawili wote walijaliwa uwezo wa kutafsiri ndoto, lakini kila mmoja kwa namna yake.
DANIELI:
Kuna wakati Mfalme Nebkadneza, (Mfalme wa Babeli) aliota Ndoto, lakini akawa ameisahau ile ndoto, na Danieli alipomwomba Bwana, aliweza kufunuliwa ndoto ile Pamoja na Tafsiri yake..na akaenda kumwambia mfalme, na ndoto ile na tafsiri yake vikathibitika..Na Mfalme akamtukuza sana Danieli, lakini si kama Yusufu.
YUSUFU:
Farao Mfalme wa Misri, naye aliota ndoto kama Nebukadneza…na ndoto ile alipoamka aliikumbuka…lakini cha ajabu ni kwamba hakuwaficha watafsiri wake ndoto ile, bali aliwahadithia alichokiota..yeye alichokuwa anahitaji tu ni maana ya ile ndoto..
Na alikuwa anajua kuwa watatokea waongo wengi, ambao watamwambia uongo..na kweli walitokea wengi wakampa tafsiri ya ndoto yake..lakini tafsiri zote hizo alizikataa..
Sasa ni Siri gani iliyofanya Tafsiri ya Yusufu ikubalike Zaidi ya zile nyingine zote??
Siri yenyewe ni mikakati baada ya kuielezea ile tafsiri..
Yusufu baada ya kusema kuna miaka 7 ya neema inakuja na 7 ya Njaa.. hakuishia hapo tu!.. lakini alitoa mikakati ni NINI CHA KUFANYA KATIKA HIYO MIAKA 7 YA NEEMA NA MIAKA 7 YA NJAA. Ndio utaona akamshauri Farao atafute mtu mwenye akili amweke juu ya kazi zake zote akusanye chakula cha kutosha katika miaka ya neema, ili itakapokuja miaka ya njaa basi hazina iwepo kubwa. (Hilo ndio wazo lililompandisha hadhi Yusufu, na wala si tu tafsiri)!..
Farao aliona hata kama tafsiri itakuwa ni ya UONGO, lakini wazo alilotoa YUSUFU NI LA HEKIMA NA AKILI…, hata kama Njaa haitakuja kama alivyotafsiri, lakini wazo tu la kuweka chakula akiba ni wazo kubwa sana na la akili sana, ambalo pengine katika utawala wake wote Farao hajawahi kushauriwa hivyo…
Tusome..
Mwanzo 41:28 “ Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.33 BASI, FARAO NA AJITAFUTIE MTU WA AKILI NA HEKIMA AMWEKE JUU YA NCHI YA MISRI.34 FARAO NA AFANYE HIVI, TENA AKAWEKE WASIMAMIZI JUU YA NCHI, NA KUTWAA SEHEMU YA TANO KATIKA NCHI YA MISRI, KATIKA MIAKA HII SABA YA KUSHIBA.35 NA WAKUSANYE CHAKULA CHOTE CHA MIAKA HII MYEMA IJAYO, WAKAWEKE AKIBA YA NAFAKA MKONONI MWA FARAO WAKAKILINDE KUWA CHAKULA KATIKA MIJI.36 NA HICHO CHAKULA KITAKUWA AKIBA YA NCHI KWA AJILI YA MIAKA HIYO SABA YA NJAA, ITAKAYOKUWA KATIKA NCHI YA MISRI, NCHI ISIHARIBIKE KWA NJAA.37 NENO HILO LIKAWA JEMA MACHONI PA FARAO, NA MACHONI PA WATUMWA WAKE WOTE.38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe”.
Mwanzo 41:28 “ Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.
29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.
30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.
31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.
32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.
33 BASI, FARAO NA AJITAFUTIE MTU WA AKILI NA HEKIMA AMWEKE JUU YA NCHI YA MISRI.
34 FARAO NA AFANYE HIVI, TENA AKAWEKE WASIMAMIZI JUU YA NCHI, NA KUTWAA SEHEMU YA TANO KATIKA NCHI YA MISRI, KATIKA MIAKA HII SABA YA KUSHIBA.
35 NA WAKUSANYE CHAKULA CHOTE CHA MIAKA HII MYEMA IJAYO, WAKAWEKE AKIBA YA NAFAKA MKONONI MWA FARAO WAKAKILINDE KUWA CHAKULA KATIKA MIJI.
36 NA HICHO CHAKULA KITAKUWA AKIBA YA NCHI KWA AJILI YA MIAKA HIYO SABA YA NJAA, ITAKAYOKUWA KATIKA NCHI YA MISRI, NCHI ISIHARIBIKE KWA NJAA.
37 NENO HILO LIKAWA JEMA MACHONI PA FARAO, NA MACHONI PA WATUMWA WAKE WOTE.
38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?
39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.
40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe”.
Umeona?.. watafsiri wengine walikuwa wanakuja na tafsiri zao lakini mwisho wa siku wanamshauri Farao mambo yasiyo na hekima, wala yasiyojenga, wala yasiyo na manufaa..ndio maana hata tafsiri zao Mfalme alizikataa.. Lakini Yusufu alipotoa tafsiri na mikakati bora baada ya ile tafsiri ndipo hata tafsiri yake ikathibitika.
Na utaona Yusufu alipokea kibali sana mbele ya Farao, Zaidi hata ya Danieli alivyotukuzwa na Nebukadreza.
Je na wewe unataka kibali leo mbele za Mungu? Kama Yusufu alivyopata mbele ya Farao??..kama ndio! basi anza kufikiri kuhusu Injili ya Kristo, katika siku za mbeleni, na anza kufanya kitu kuanzia sasa. Kama ni mhubiri basi weka hazina kwa vizazi vinavyokuja… Kama ni mtu wa kukirimu, basi changia injili kwa mali zako kwa kadiri uwezavyo, ili kusudi Watoto wanaochipukia wasikue na kukuta idadi ya disco na bar zimezidi makanisa, wasije wakakuta idada ya vikundi vya wahuni vimezidi vya watu wema, wasije wakakutana na ugumu wa kuitafuta injili ya kweli, Zaidi ya huu tulionao sisi katika kizazi chetu..
shetani anayo mikakati sasahivi ya kuharibu kizazi hata cha tano kijacho..na hata sasa kashaanza kufanya juhudi hizo, inatupasaje sisi, tunaosema tumeokoka sasa? Kama wewe umeipata injili ya kweli, kiurahisi, basi rahisisha pia kwa wanaokuja, ambao kwa ambao hawajasikia..ndivyo Mungu atakavyokupa kibali.
Mithali 13:22 “Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi”
Tujifunze kwa Yusufu, ili na sisi tupate kibali mbele za Mungu.
Maran atha!
FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.
Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?
Kwanini vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.
Swali: Deuterokanoni ni nini? na je vitabu vya Deutorokanoni ni vitabu vya kiMungu? (ambavyo vimevuviwa na Roho Mtakatifu) na vyenye kufaa kwa mafundisho.?
Jibu: Deuterokanoni ni vitabu vingine saba (7) ambavyo vimeongezwa na kanisa Katoliki juu ya vitabu 66 vya Biblia takatifu, na hivyo kufanya jumla ya vitabu 73 katika biblia ya kikatoliki. Maana ya neno “Deuterokanoni” ni “Orodha ya pili” ambayo imekuja baada ya orodha ya kwanza yenye vitabu 66
Na ordha hiyo ya vitabu vya Deuterokanoni ni..
1. Tobiti
2. Yudith
3. Wamakabayo I
4. Wamakabayo II
5. Hekima
6. Yoshua bin Sira
7. Kitabu cha Baruk.
Vitabu vya Deuterokanoni, viliandikwa baada ya nabii wa Mwisho (Nabii Malaki) kupita!.. Na vitabu hivi hapo kabla havikuhesabiwa kuwa vitabu vitakatifu na pia wakristo!!..na wala havikuwekwa katika orodha ya vitabu vitakatifu au vya mafundisho ya kiMungu.
Vilikuja kuongezwa katika orodha ya vitabu vitakatifu na Papa Damasus 1 katika karne ya 4.
Lakini swali ni je!.. Vitabu hivi ni vitabu vitakatifu? Na kama sio kwanini?
Jibu ni kwamba vitabu hivi si vitabu vitakatifu wala vilivyovuviwa na Roho Mtakatifu, kwasababu zifuatazo.
Vinakinzana na vitabu vingine vitakatifu.
Kamwe Mungu hajichanganyi, na wala Neno lake halijichanganyi..lakini vitabu hivi vina mafundisho ambayo yanakinzana na mafundisho ya kweli ya Roho mtakatifu yaliyopo ndani ya vitabu 66. (Vitabu 66 havipingani hata kimoja, bali vyote vinakubaliana katika jambo moja, kwasababu vimevuviwa na Roho huyo huyo mmoja), lakini vitabu vya Deuterokanoni vinapingana na vitabu hivi vingine 66.
Kwamfano kitabu cha 2 Wamakabayo 12:43-45 kinafundisha Maombi kwa Wafu, na mafundisho ya toharani, jambo ambalo halionekani katika vitabu vingine 66 vya biblia.
Hakuna mahali popote katika biblia, panaonyesha kuwa wafu waliombewa au wanaombewa.. Zaidi sana biblia inasema katika Waebrania 9:27 “ kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu”.
Kwahiyo kitabu hiki si cha kiMungu, kwasababu Mungu kamwe hawezi kujichanganya..huku aseme hivi, na kule aseme vingine..
Na pia vitabu hivi, kuna sura zinazofundisha “Ulevi”, “Uchawi” na “Mazungumzo ya uongo”. Kwahiyo kwa ufupi si vitabu vya kiMungu, bali ni vya adui, shetani..ambavyo lengo lake ni kuwapeleka watu mbali na Mungu.
Biblia yenye vitabu 66, ndio biblia pekee ambayo mwanzo wake hadi mwisho wake imevuviwa na Roho Mtakatifu, na Ndio Neno la Mungu pekee, lakini hiyo yenye vitabu vya Deuterokanoni na nyingine yoyote yenye vitabu Zaidi ya hivyo ni ya kishetani, na si ya kuisoma wala kusikiliza mahubiri yanayotumia vitabu hivyo.
1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”
Bwana Yesu akubariki.
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
Biblia ina vitabu vingapi?
KITABU CHA UZIMA
Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Atukuzwe Yesu Kristo Bwana wetu milele na milele. Sifa na utukufu ni vyake yeye sikuzote..
Biblia inatuambia, mambo yote yaliyoandikwa katika agano la kale, yalikuwa ni kivuli cha agano jipya la rohoni. Hivyo maagizo mengi ya mwilini, unayoyasoma kule, yalikuwa ni muhtasari wa agano jipya lili bora Zaidi.
Ni sawa na mwanafunzi anayeanza chekechea, ukitaka kumfundisha Hesabu za KUJUMLISHA na KUTOA, huwezi moja kwa moja ukamwandikia 5-3=2. Ukadhani ataelewa, ni kweli kwa upande wako ni rahisi kwasababu tayari upeo wako ulishatanuka, lakini kwa mtoto, huna budi kutumia njia ya vitendo kwa mwanzoni..
Ndipo itabidi umwekee vijiti, au mawe, ahesabu kimoja mpaka cha tano, kisha aondoe hapo vitatu, ndipo vile viwili vinavyosalia, viwe jibu. Hivyo akilini mwake anajua hesabu ni vijiti na mawe, lakini kihalisia sio hivyo.. Atakapokomaa akili, ndipo atakuwa hana haja ya vijiti, au vidole, au mawe tena.
Vivyo hivyo katika biblia, agano la kale la mwilini lilikuwa ni hatua za awali za kulielewa agano lilibora la rohoni..(Waebrania 10:1, Wakolosai 2:16-17).
Sasa tukirudi katika kichwa cha somo letu. Tufanye nini ili tuonekane safi mbele za Mungu?.
Kumbuka, katika torati Mungu aliwaatenga Wanyama wote katika makundi mawili makuu.
Sasa ili mnyama aitwe safi, ilikuwa ni sharti, akidhi vigezo maalumu Mungu alivyovioanisha.. Na vigezo vyenyewe zipo vitatu ambavyo ni hivi;
Ikiwa na maana kama hatokidhi vigezo vyote vitatu, basi huyo mnyama ni najisi, haijalishi atakuwa na kimoja au viwili kati ya hivyo. Hakuruhusiwa, kuliwa, na wengine kufugwa au kuguswa mizoga yao.
Walawi 11:2 “Neneni na wana wa Israeli, mkiwaambia, Wanyama hawa ndio wanyama wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote walio juu ya nchi.3 Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.6 Na sungura, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.8 Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu.
Walawi 11:2 “Neneni na wana wa Israeli, mkiwaambia, Wanyama hawa ndio wanyama wenye uhai mtakaowala, katika hayawani wote walio juu ya nchi.
3 Kila mnyama mwenye kwato katika miguu yake, mwenye miguu ya kupasuka kati, mwenye kucheua, katika hayawani, hao ndio mtakaowala.
4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; ngamia, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
5 Na wibari, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
6 Na sungura, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.
8 Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu.
Sio kwamba aliwaona wana sumu kali, au wana madhara wakiliwa, kama wengi wanavyodhani hapana, kwasababu wengi wao wanaliwa hadi sasa, na hakuna madhara yoyote yanayowapata bali alikuwa anatufundisha jambo la rohoni, ili tutakapoingia katika agano jipya tuelewe vema, Mungu anapozungumzia unajisi anamaanisha nini.
Kwamfano, anaposema,
Kucheua ni nini? Ni ile hali ya mnyama kuwa na uwezo wa kukirejesha tena kile chakula alichokimeza na kukitafuta tena, kwa kawaida Wanyama kama ng’ombe, twiga, ngamia, hawa wanakuwa na tumbo la ziada, ambalo linawasaidia kurejesha na kutafuna tena kile walichokila.
Hii inafunua nini sasa katika agano jipya?. Ukiwa si mtu wa kutafakari na kukitendea kazi kile unacholishwa (Neno la Mungu), wewe ni kusikia tu kilasiku, lakini hakuna tendo lolote la ziada unalolionyesha kwa kile ulichofundishwa, huzalishi chochote, mbele za Mungu ni kama mnyama najisi, asiyeweza kucheua, Na kamwe hutoweza kuingia mbinguni (patakatifu pa Mungu), siku ukifa. Mungu anataka tutendee kazi Neno lake, pia tujifunze kuzikumbuka Fadhili zake alizotutendea huko nyuma, tusiwe hasahaulifu. Usahaulifu ni tabia ya unajisi.
Hivyo jiangalie ndani yako je! Wewe ni mtu wa kulitendea kazi Neno la Mungu? Tangu uliopoanza kusikia ni mangapi umeyatendea kazi, Kama sio, basi bado hujawa safi.
2) Awe na Kwato:
Kucheua tu haitoshi, walikuwepo Wanyama wenye uwezo huo kama ngamia, lakini walikosa kwato.. yaani ni kama nyama tu imeshuka mpaka chini, ni sawa na kusema hawana kiatu.
Hivyo, ni dhaifu kwa upande mmoja, kwasababu wamekosa ulinzi miguuni, ukipita msumari mrefu, basi safari yao imekwisha, hawawezi kutembea kila mahali, penye miiba, hawawezi kuruka, kwasababu miguuni ni wadhaifu.
Tofauti na mnyama farasi,au swala, yeye ana kwato ndio maana ni mwepesi kutembea popote, ngombe anakwato, ndio maana anaweza kulima hata kwenye mashamba n.k.
Hii inatupa tafsiri gani rohoni?
Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”;
Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani”;
Hapo anasema, ukiwa askari wa Kristo ni lazima ujifunze kusimama ukiwa umejifungia utayari miguuni.. utayari wa nini? Utayari wa kumtumikia Mungu kwa hali zote. Na je utayari huo unatokea wapi? Unatokea kwenye kuisikia injili ya Yesu Kristo, kwa kupitia hiyo tunapokea hamasa, na nguvu na uweza wa kumtumikia yeye.
Wanajeshi, kwa kawaida ni lazima wavae viatu vigumu miguuni waendapo vitani, ili kuwasaidia kukatisha katika mazingira yoyote magumu, vinginevyo wakienda peku peku, hawataweza kwenda mbali
Halikadhalika na wewe, ukiwa umejivika UTAYARI huo wa kumtumikia Bwana katika mazingira yoyote, rohoni unaonekana kama ni mnyama mwenye kwato. Unafaa kwa kazi,
3) Mwisho, kwato ziwe zimegawanyika.
Wapo Wanyama ambao walikuwa wanacheua, walikuwa wana kwato, lakini kwato zao zilikuwa hazijagawanyika mara mbili. Hapo bado walikuwa ni najisi.
Ni kwanini, Bwana alitaka kwato za mnyama zigawanyike mara mbili, ili waonekane safi? Ni siri gani ipo nyuma yake?
Kama tulivyotangulia, kuona kwato, Ni utayari tuupatao katika injili…
Lakini lazima tujifunze kuligawanya Neno la Mungu. Ndio maana biblia inayo agano la kale na jipya. Ili tuweze kuwa askari kamili ya Kristo, hatuna budi kufahamu kuweka injili ya Kristo kama atakavyo yeye, kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.
Kwa kukosa, kuelewa ufunuo uliokatika agano lake, ndio inayopelekea, watu kufundisha kuwa vyakula ni najisi kwasasa..
1 Timotheo 4 : 1-5
1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;
3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.
4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;
5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
Wengine wanaona Ibrahimu, Daudi, wameoa wake wengi, anadhani ndio hata sasa ndivyo ilivyo, na Mungu anapendezwa navyo. Hawajui ni ufunuo gani ulikuwa nyuma yake.
Hivyo biblia inatutaka sana tujifunze kuligawanya vema Neno la Mungu. (2Timotheo 2:15).
Ni muhimu sana. Na hiyo inamuhitaji Roho Mtakatifu.
Hivyo kwa kukidhi vigezo hivi vitatu; 1) Kutendea kazi Neno la Mungu 2) Kumtumika kwa Bwana 3) Kuwa na maarifa ya Neno la Mungu. Basi utakuwa mnyama safi mbele za Mungu.
Na hivyo tutamkaribia Mungu.
Lumbwi ni nini katika biblia?
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Bwana alimaanisha nini aliposema enendeni mkaihubiri injili kwa kila kiumbe?
Maji ya Farakano ni nini katika biblia?
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
Swali: Mti wa Mshita uliotengenezea sanduku la Agano ndio upi kwasasa?(Kutoka 25:10)
Jibu: Tusome
Kutoka 25:10 “Nao na wafanye sanduku la MTI WA MSHITA; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.11 Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote”.
Kutoka 25:10 “Nao na wafanye sanduku la MTI WA MSHITA; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.
11 Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote”.
Mshita ni jamii ya miti ambayo hata sasa ipo, na inapatikana katika sehemu nyingi za dunia, ikiwemo katika bara letu la Afrika, na hata katika Afrika mashariki. (Tazama picha juu). Mti wa Mshita ni mti unaostahimili ukame zaidi ya miti mingi.
Tabia za mti wa mshita, ni kwamba ni moja ya miti migumu, na vile vile ni mti ambao hauharibiwi na wadudu wala maji, wala hauingiaa fangasi kirahisi, jambo linaloifanya mbao ya mti huo iweze kutumika kutengenezea baadhi ya vyombo vya kuhifadhia vyakula, na sifa nyingine ya mbao ya mti wa Mshita ni rahisi kupakika rangi, kwasababu uso wake ni mwororo.
Sasa Kwanini Sanduku la Agano lilitengenezwa kwa mti wa Mshita?
Jibu, ni kwasababu ya tabia au sifa za mti huo.
Ndani ya Sanduku la Agano kulihifadhiwa chakula (yaani ile pishi ya mana) kwaajili ya ukumbusho wa vizazi vijavyo vya wana wa Israeli..Hivyo ni lazima chakula hicho kihifadhiwe ndani ya sanduku lililo imara lisiloingia fangasi wala wadudu waharibifu. Mbao nyingine zaidi ya Mshita, hazina sifa hizo!
Vile vile ndani ya Sanduku kulikuwa na zile mbao mbili, ambazo Musa aliambiwa azitengeneze, zilizoandikwa Amri kumi na chanda cha Mungu mwenywe, Mbao hizo ziliwekwa ndani ya Sanduku kuwa ukumbusho wa daima, hivyo ni lazima zihifadhiwe katika Sanduku lililo gumu ambalo haliharibiki haraka..
Na vile vile kulikuwa na ile fimbo ya Haruni iliyochipuka, ambayo ilihifadhiwa nayo pia kama ukumbusho wa utumishi wa kikuhani wa nyumba ya Lawi.. Fimbo hiyo nayo ilipaswa ihifadhiwe ndani ya sanduku imara lisiloruhusu unyevunyevu au maji kuingia.
Na sanduku la Agano linafananishwa na mioyo yetu.. Katika kitabu cha Yeremia 31:31, Biblia ilitabiri kuwa katika Agano jipya tulilopo sisi, sheria za Mungu zimeandikwa mioyoni mwetu.. Mioyo yetu kwa Bwana ni kama mti wa Mshita, Hivyo hatuna budi kuzidi kuiimarisha mioyo yetu, kwa kukaa mbali na dhambi ili tuzidi kuzidumisha sheria za Mungu katika mioyo yetu.
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
Mwerezi ni nini?
FANYA BIDII ZOTE ULE MATUNDA YA UZIMA.
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?
Rudi Nyumbani:
Swali: Katika biblia tunasoma sehemu kadha wa kadha zikiwataja “wana wa manabii”.. Je! Hawa wana wa manabii walikuwa ni watu gani?, na kazi yao ilikuwa ni ipi? Na kwanini waliitwa hivyo?.. Na je hata leo kuna wana wa manabii?
Jibu: Ni kweli Katika Agano la kale lilikuwepo kundi la watu waliojulikana kama Wana wa Manabii. (Soma 1Wafalme 20:35, 2Wafalme 6:1, 2Wafalme 4:1, na 2Wafalme 2:5).
Watu hawa walikuwa ni “manabii wa Mungu”, ambao walijitia katika kifungo cha kujifunza juu ya Nabii zilizotangulia kabla yao..
Kumbuka sio kujifunza jinsi manabii wanavyoishi au wanavyokula au wanavyoona maono!… La! Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumfundisha mtu mwingine namna ya kuona maono!…hivyo ni vipawa vya Mungu ambayo ni Mungu mwenyewe anaviweka ndani ya mtu, na hatujifunzi wala hatufundishwi.. Ni sawa na ndoto…
Hakuna mtu anayeweza kumfundisha mwenzake jinsi ya kuota!.. Ndoto zinakuja zenyewe, kwasababu ni vipawa vya asili ambavyo Mungu kaviweka kwetu sote.. Na nabii za Mungu, zinawajia watu maalumu ambao Bwana kawachagua, na si kupitia kujifunza!.
Kwahiyo hawa wana wa manabii, au kwa lugha nyingine “Wanafunzi wa manabii” walikuwa ni watu waliojikita kujifunza Nyakati na Majira, Pamoja na Nabii zilizotangulia kutolewa na manabii wengine waliowatangulia..(kumbuka walikuwa wanajulikana kama wana wa manabii, na sio wana wa NABII!)..
Na lengo la kufanya hivyo (yaani kupokea maarifa hayo) ni ili wawe salama, na wawe na uhakika wa Nabii watakazozitoa isije wakapotoka na kutoa unabii wa uongo.
Kwa mfano Nabii anaweza kuona maono au kupata ujumbe kuhusu Taifa la Israeli, sasa ili authibitishe ujumbe ule au ono lile kama kweli ni kutoka kwa Bwana, ni sharti awe na Nabii nyingine za kutosha, za waliomtangulia zinazosapoti ono lake hilo jipya!.. Na akija kugundua kuwa Nabii mwingine, mkuu aliyetangulia alishatabiri jambo kama hilo au linalokaribiana na hilo… basi ndipo Ono lake hilo linathibitika… lakini akija kukuta ono lake linakinzana na maono ambayo manabii wakuu waliyatoa, ndipo analiacha, kwasababu sio kutoka kwa Bwana… (kwasababu kamwe Bwana hawezi kujipinga katika maneno yake).
Hivyo ndio maana ilihitajika shule ya manabii, ambayo lengo lake ni kujifunza kujua Nabii zilizotangulia juu ya watu, na mataifa…
Ili tuzidi kuelewa vizuri, utakumbuka kipindi cha Nabii Yeremia wakati anatabiri kwamba Israeli watachukuliwa utumwani kwenda Babeli.. utaona Yeremia alikuwa ni mtu mwenye elimu ya kutosha kuhusu Nabii zilizotangulia, alihakiki jumbe anazozipokea katika maono, kwa nabii za waliomtangulia kama wakina Isaya, na wengineo..
Na jambo moja utaona alilojifunza ni kuwa “Manabii karibia wote, hawakuwahi kutabiri juu ya amani kwa mataifa, manabii wengi walikuwa wanatabiri juu ya Vita na Mabaya na Tauni”.. Na Yeremia alijua Mungu hawezi kujipinga.. Hivyo maono yake aliyahakiki kwa namna hiyo..
Lakini utaona alitokea mtu anaitwa Hanania, ambaye alijitokeza na kuanza kutabiri juu ya Amani kwa Israeli kwamba hawataenda utumwani, watakuwa salama, ni ilihali Taifa zima limemwacha Mungu..jambo ambalo linakinzana na Nabii Mungu alizozitoa kupitia manabii wakuu waliotangulia… Na Yeremia kuliona hilo akamwambia Hanania maneno yafuatayo…
Yeremia 28:7 “Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote,
8 MANABII WALIOKUWAKO KABLA YA ZAMANI ZANGU, NA ZAMANI ZAKO, WALITABIRI JUU YA NCHI NYINGI, NA JUU YA FALME KUBWA, HABARI YA VITA, NA YA MABAYA, NA YA TAUNI”.
Umeona jambo Yeremia alilomwambia huyu Hanania?…
Yeremia alikuwa ni Mwana wa manabii, lakini Hanania alikuwa ni mtu tu aliyejizukia na kujiita Nabii, hana elimu yoyote ya Nabii za Mungu.. na akaanza kuwafariji watu kwa maneno ya uongo!..Jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na hata kumwua Hanania.
Yeremia 28:15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo. 16 BASI BWANA ASEMA HIVI, TAZAMA, NAKUTUMA UENDE ZAKO TOKA JUU YA USO WA NCHI; MWAKA HUU UTAKUFA, KWA SABABU UMENENA MANENO YA UASI JUU YA BWANA.17 BASI NABII HANANIA AKAFA, MWAKA UO HUO, MWEZI WA SABA”.
Yeremia 28:15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo.
16 BASI BWANA ASEMA HIVI, TAZAMA, NAKUTUMA UENDE ZAKO TOKA JUU YA USO WA NCHI; MWAKA HUU UTAKUFA, KWA SABABU UMENENA MANENO YA UASI JUU YA BWANA.
17 BASI NABII HANANIA AKAFA, MWAKA UO HUO, MWEZI WA SABA”.
Lakini leo hii shetani kaligeuza hili Neno “Wana wa Manabii”. Leo hii kuna watu wamefungua vyuo vyao, wakiwa wenyewe wanajiita Manabii wakuu, na vijana wao wanawaita “wana wao (yaani wana wa manabii)”.. Lakini ukiingia katika madara yao na kusikia wanachofundishwa, ni huzuni tupu!.
Utasikia wanachofundishwa ni jinsi ya kuona maono, jinsi ya kutumia na kutengeneza mafuta na chumvi na mengineyo, utaona wanafundishwa mtindo wa maisha na mtindo wa kuongea, na kuvaa kama nabii mkuu wao, na jinsi ya kumwogopa na kumtukuza baba yao, nabii mkuu..
Na watasomea hata miaka 5 na wakitoka hapo wanapewa na vyeti, tayari wakufunzi!!!..
Ndugu! Huo ni uongo wa shetani…
Wana wa manabii katika Agano la kale, hawakufundishwa wala hawakuwa wanajifunza mitindo ya kuongea ya manabii waliowatangulia…wala walikuwa hawajifunzi jinsi ya kuona maono! (kwasababu tayari walikuwa na hiyo karama, ndio maana wakaitwa manabii)..Walichokuwa wanajifunza ni Nabii zilizotangulia zinazohusu wakati waliopo wao, na za mataifa mengine, kuanzia zilizoandikwa katika Torati ya Nabii Musa, mpaka wakati waliopo wao, ili kusudi wasije wakapotoka na maono waliyokuwa wanayapokea.
Na sisi leo hii wote ni wana wa Manabii.. ambao manabii wetu si baba zetu wa kiroho!!! Wala si maaskofu wetu, bali ni MITUME WA KWENYE BIBLIA, na MANABII WA KWENYE BIBLIA!!!...Tunatembea katika Nabii walizozitoa hao, wakina Musa, Isaya, Yeremia, Habakuki, na mitume wakina Petro, Yohana, Paulo n.k.. (Na nabii zao hazijawahi kukinzana),Kwasababu walikuwa na Roho mmoja.
Kwamfano Nabii Isaya alitoa unabii ufuatao..
Isaya 13:6 “Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu”.
Nabii Yoeli naye alitoa unabii kama huo huo katika Yoeli 3:14, na manabii wengine wote walitabiri hayo hayo…
Kwahiyo ili sisi tuhesabike kuwa “Wana wa manabii” ni lazima maono yetu tunayoyaona katika ndoto, au kwa wazi, ni lazima yapatane na huo unabii wa Isaya, na Yoeli na wengineo katika biblia!… usipopatana na huo unabii wa Isaya basi hilo Ono au huo Unabii ni wa UONGO!!! Ni kutoka Kuzimu!!!...
Tukiota au tukiona maono ambayo yanatuonyesha au kutuambia kuwa “Tufurahi, tupige kelele za shangwe, kwasababu siku ya Bwana bado sana”..basi hilo ni Ono kutoka kuzimu!!!..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba wana wa manabii, ni manabii ambao walikuwa wamejikita katika kusoma Nabii za manabii wa Mungu waliowatangulia, ili wasifanye makosa katika kutoa nabii zao.
Na sisi ni lazima tuwe wanafunzi wa biblia, turejee biblia katika kuhakiki kila kitu, na hatupaswi kuamini tu kila jambo ambalo tunalipokea katika ndoto au maono.
Bwana Yesu na atusaidie sana.
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.
Marko 5:12 “Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; NALO KUNDI LOTE LIKATELEMKA KWA KASI GENGENI, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini”.
Marko 5:12 “Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.
13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; NALO KUNDI LOTE LIKATELEMKA KWA KASI GENGENI, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini”.
“Genge” linalozungumziwa hapo sio lile linalotengenezwa kwaajili ya biashara za mboga mboga, au matunda..Bali Neno “genge” ni Kiswahili kingine cha “Mteremko wa mwamba”..Ipo miteremko ambayo chini ni udongo, lakini pia ipo miteremko ambayo chini ni mwamba…sasa hiyo ambayo chini ni mwamba, ndiyo inayoitwa “Genge”
Kwahiyo hapo biblia iliposema kuwa wale Nguruwe waliteremkia kwa kasi gengeni, ilimaanisha walishuka kwa kasi katika mteremko huo unaoelekea ziwani.. Na tofauti na miteremko ya kawaida na ile ya miamba..ni kwamba miteremko ya miamba INAKUWA INATELEZA!, kiasi kwamba mnyama au mtu au kitu kikianza safari ya kuelekea huko basi kwa haraka sana kitakuwa kimefika hitimisho…Ndio maana hao nguruwe biblia inataja WALISHUKA KWA KASI…
Kufunua ni jinsi gani mapepo yanavyowapeleka watu mahali ambapo si sahihi, na tena kwa haraka sana…Leo hii mtu akiingiwa na mapepo basi, hitimisho lake litakuwa ni KIFO, kama hayatamtoka. Na hakuna pepo lolote lisilotoka endapo mtu akimaanisha kuamua limtoke. Kwasababu hakuna lililo kubwa kwa Mkuu wa Uzima Yesu, na zaidi sana miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu na si mapepo. Kwahiyo tunazo haki zote za kudai uzima na haki zote za kumpokea Roho Mtakatifu endapo tutamhitaji..
Na kanuni za kupokea Roho Mtakatifu ni hii..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
Je umetubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu?
JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?
Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?
Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”
MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.
RAFIKI WA KWELI NI YUPI?
Rudi Nyumbani
Kombeo ndio hiyo hiyo teo, ni moja ya silaha ya kurusha iliyotumika zamani katika vita.
Kombeo/teo ilitengenezwa kwa Ngozi au Kamba, na jiwe lilikuwa likiwekwa katikati yake na kurushwa kumwelekea adui. Kwa ulimwengu wa sasa Silaha ya manati ndio inayotumika kama mbadala ya teo.
Hivi ni vifungu ambavyo utakutana na neno hilo;
Waamuzi 20:16 “Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.
Maana yake ni kuwa jeshi la Benyamini, lilikuwa na watu mia saba ambao wakuwa na shabaha ya hali ya juu sana ya kuweza kurusha mawe kwa kombeo/teo bila kukosea.. Biblia imetumia mfano wa ‘kulengwa kwa unywele’, jinsi ulivyo mdogo, kuonyesha kiwango cha shabaha cha hawa watu kilivyokuwa cha juu sana.
Utasoma pia andiko hilo katika vifungu hivi;
1Nyakati 12:2 “Walikuwa wenye kupinda upinde, nao walikuwa hodari wa kutumia mkono wa kuume na wa kushoto, kwa kutupa mawe ya teo, na kwa kupiga mishale ya upinde; walikuwa wa nduguze Sauli, wa Benyamini”.
2Wafalme 3:25 “Wakaibomoa ile miji; wakatupa katika kila mahali palipo pema kila mtu jiwe lake, wakapajaza; wakaziziba chemchemi zote za maji, wakaikata miti yote iliyo mizuri; mpaka katika Kir-haresethi tu wakayasaza mawe yake; ila wenye kombeo wakauzunguka wakaupiga”.
Lakini pia katika biblia tunaona, hii ilikuwa ni silaha maarufu aliyoitumia Daudi kumwangusha adui yake Goliathi..
1Samweli 17:40 “Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti…49 Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi”.
1Samweli 17:40 “Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti…
49 Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi”.
Tunaona Daudi alipopewa, mikuki, na mapanga, na mishale, Silaha zenye ufanisi wa hali ya juu wa kivita, yeye hakutaka, bali alichagua kombeo lake na mawe matano. Alikubali kutumia silaha dhaifu, ili tumaini lake lisiwe katika silaha alizonazo bali katika Bwana ndio maana akasema..
1Samweli 17:45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana. 46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.48 Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti.
1Samweli 17:45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana. 46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.
48 Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti.
Hata sasa, hatupaswi kutegemea nguvu zetu, kushindana au kupambana na hali au majaribu mazito yanayotukabili mbele yetu.. Wengi wakiona hali imekuwa ngumu, wanachowaza ni moja kwa moja kutafuta fedha nyingi ili waweza kukabiliana na shida zao, ndugu ni heri umtegemee Bwana, amini katika hicho hicho kidogo ulichonacho, kwamba Bwana anaweza kukitumia hicho kukupa ushindi mkuu.
Mwingine atakuambia ukikosa elimu, hutoweza kufanikiwa, au kumtumikia Mungu. Ni kweli elimu ni nyenzo nzuri ya kukufikisha mahali Fulani pazuri, lakini isipokuwa na Mungu nyuma yake ni bure. Wewe usiyekuwa na elimu ya kutosha ukimtumikia Bwana kwa uaminifu, utafanikiwa hata Zaidi ya wale wenye elimu kubwa.
Kombeo hilo Bwana alilokupa lielekeze tu kwa Bwana, na yeye mwenyewe atakuonyesha maajabu.
Zaburi 20:7 “Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu”.
Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Kibanzi na Boriti ni nini kama tunavyosoma kwenye biblia?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.
SIFONGO NA SIKI NI NINI?
Jehanamu ni nini?
Luka 8:26 “Wakafika pwani ya nchi ya Wagerasi, inayoelekea Galilaya.27 Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini.28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese”.
Luka 8:26 “Wakafika pwani ya nchi ya Wagerasi, inayoelekea Galilaya.
27 Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini.
28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese”.
Tabia mojawapo ya mtu mwenye pepo ni KUTOKUVAA NGUO KABISA, au KUVAA NUSU UCHI!.
Ukiona unapenda kuviweka wazi viungo vya mwili wako, na hata hujisikii vibaya…fahamu kuwa hiyo ni dalili ya kuwa na Pepo ndani yako!..Na tabia nyingine ya mtu mwenye pepo ni kuwa “Anakuwa Mkali sana”..pindi anapotaka kusaidiwa..
Mathayo 8:28 “Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, WAKALI MNO, hata mtu asiweze kuipitia njia ile”.
Ukiona unachukia sana, unapoambiwa kwamba mavazi unayovaa si ya kujisitiri, basi hiyo ni dalili ya kwamba unalo pepo ndani yako!, ambalo linapaswa litoke.
Ukiona unakasirika au unakuwa mkali unapoambiwa kuwa vimini unavyovivaa, au suruali unazozivaa(mwanamke) ni dhambi, basi tafuta msaada wa haraka ili kusudi hayo mapepo yaweze kukutoka, kwasababu katika hali ya kawaida, mtu mwenye akili timamu hawezi kukaa nusu tupu na akatembea hivyo barabarani na akajiona yupo sawa…
Ishara ya kwanza ya Yule mtu kutokwa na mapepo ni yeye kuvaa nguo, na kuwa akili zake timamu.
Marko 5:15 “Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, AMEVAA NGUO, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa”.
Je wewe mwanamke/mwanaume hapo kazini ulipoketi, au hapo shuleni ulipo sasa, au hapo kanisani unaposhiriki sasa je umevaa Nguo?..umejisitiri?, je kifua chako kimefunikwa au kipo wazi?..je mgongo wako umefunikwa au upo wazi?.. Je mapaja yako yamefunikwa au yapo wazi?, je tumbo lako limefunikwa au lipo wazi?.. Kama mwili wako haujasitirika! Basi ni ishara kuwa unayo mapepo na huna akili timamu (mapepo yameondoa ufahamu wako).
Lakini kama sehemu za juu za mikono yako zipo wazi, au kifua chako au mapaja yako, au umevaa nguo lakini inachora maungo yako, kiasi kwamba hauna tofauti na mtu aliye uchi kabisa, basi fahamu kuwa UNAYO MAPEPO NA PIA HUNA AKILI TIMAMU, na zaidi sana ukiona unakasirika unapoyasikia haya maneno, basi ndio uthibitisho wa mwisho kuwa Mapepo yapo ndani yako!.. na hivyo unahitaji msaada.
Na habari njema ni kwamba, msaada huo unaweza kuanza kuupata hapo hapo ulipo.
Unachopaswa kufanya sasahivi ni kudhamiria KUTAKA MSAADA WA KUTOKANA NA HAYO MAPEPO!... Na unadhamiria kwa Kumpokea Bwana Yesu maishani mwako..(Usiseme tayari nilikuwa nimeshampokea!)…Ulikuwa bado hujampokea ndio maana ulikuwa unaona upo sawa kukaa nusu uchi!!.. Bwana Yesu angekuwa ndani yako, usingekuwa hivyo ulivyo sasa!!… Wewe sasahivi ndani yako yapo mapepo ambayo yanakufanya UKAE UCHI!!.
Kwahiyo unapaswa pale ulipo ujitenge wewe binafsi, uombe toba!, kwa kudhamiria kuacha njia mbaya…kutubu dhambi maana yake ni pamoja na kuacha vyote ulivyokuwa unavifanya, maana yake leo leo nenda kachome vimini vile, na suruali zile unazozivaa, na anza kuvaa nguo kamili, kwa kufanya hivyo utakuwa umeonyesha kwa vitendo kwamba hutaki tena mapepo ndani yako, na akili itakurudia, na utaona kweli ulikuwa vifungoni.
Baada ya kufanya hivyo nenda katafute ubatizo sahihi, ubatizwe upya, na ubatizo wa kibiblia ni ule wa jina la Yesu na wa maji mengi, baada ya hapo Roho Mtakatifu atashuka juu yako na kukusafisha kabisa..
SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ni Mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu! (Zab 119:105).
Si watu wote waliokuwa wanamfuata Bwana au waliokuwa wanamjua Bwana walikuwa wanafunguliwa au kuponywa magonjwa yao!.. Wengi walikuwa hawafunguliwi..Na hiyo ni kwasababu walikuwa hawana HAJA YA KUPONYWA!.. aidha kutokana na kwamba hawamwamini, au walimdharau!.
Luka 9:11 “Na makutano walipojua walimfuata; akawakaribisha, akawa akisema nao habari za ufalme wa Mungu, AKAWAPONYA WALE WENYE HAJA YA KUPONYWA”.
Utaona pia kipindi Bwana Yesu anaenda Galilaya, hakufanya miujiza mingi huko kutokana na kwamba watu hawakumwamini..
Mathayo 13:53 “Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake.54 Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?56 Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?57 Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe.58 WALA HAKUFANYA MIUJIZA MINGI HUKO, KWA SABABU YA KUTOKUAMINI KWAO”.
Mathayo 13:53 “Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake.
54 Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?
55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?
56 Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?
57 Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe.
58 WALA HAKUFANYA MIUJIZA MINGI HUKO, KWA SABABU YA KUTOKUAMINI KWAO”.
Umeona hapo?..hakufanya miujiza mingi, kwasababu moja tu!..walimdharau na hawakumwamini!
Vile vile utakumbuka kipindi Bwana Yesu ameingia katika lile eneo lenye birika la Bethzatha..ijapokuwa mule ndani kulikuwa na idadi kubwa ya wagonjwa ambao walihitaji kupona…lakini wengi wao hawakuwa na haja ya kuponywa na Bwana Yesu…wenyewe akili zao na tumaini lao lilikuwa katika yale maji yaliyoaminika kwa wakati huo kama MAJI YA UPAKO!!.
Bwana akawa anapita katikati ya wagonjwa hao…pengine akakutana na baadhi na kuwauliza kama wanataka kuponywa na pengine hata hawakumjibu neno, au walimdharau na kumfukuza..lakini alipokutana na mmoja na kumwuliza kama anataka kuwa mzima, akakiri kuwa anataka kupona lakini hakuna mtu wa kumtia birikini..Na Bwana Yesu akamwambia asimame ajitwike godoro lake aende..na alipotii na kuamini Neno hilo akawa mzima!.. Lakini wale wengine waliendelea kusubiri Maji yale yachemke..
“1 Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu.2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano.3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.4 Kwa maana kuna wakati ambapo malaika hushuka, akaingia katika ile birika, akayatibua maji. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wote uliokuwa umempata.]5 Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini na minane.6 Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, ALIMWAMBIA, WATAKA KUWA MZIMA?7 Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.8 YESU AKAMWAMBIA, SIMAMA, JITWIKE GODORO LAKO, UENDE.9 Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda. Nayo ilikuwa ni sabato siku hiyo”.
“1 Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu.
2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano.
3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.
4 Kwa maana kuna wakati ambapo malaika hushuka, akaingia katika ile birika, akayatibua maji. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wote uliokuwa umempata.]
5 Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini na minane.
6 Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, ALIMWAMBIA, WATAKA KUWA MZIMA?
7 Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.
8 YESU AKAMWAMBIA, SIMAMA, JITWIKE GODORO LAKO, UENDE.
9 Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda. Nayo ilikuwa ni sabato siku hiyo”.
Je na wewe una haja ya kuponywa roho yako na mwili wako leo?. Basi usijitumainishe katika maji wanayoyaita ya upako, au chumvi wanayoiita ya upako, au mafuta wanayoyaita ya upako.. Mwamini Bwana Yesu leo na maneno yake na pia chukua hatua ya kusimama.
Huenda umeshatumia hayo maji sana, au mafuta kwa muda mrefu lakini hujaona matokeo yoyote…leo hii yageukie maneno ya Bwana YESU katika biblia, yanayosema.. “KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA (ISAYA 53:5)” Wala usiuangalie umati..ukiona mahali pana umati mkubwa wa wagonjwa, ambao hawajapona matatizo yao lakini wanatumainia vitu kama maji, kuwaponya!..fahamu kuwa hapo ni Bethzatha kiroho!.. Uponyaji kutokea ni bahati sana (tena ni kwasababu tu ya huruma za Mungu, na wala si kwasababu vitendea kazi hivyo vina upako)…ndio maana utaona sehemu kama hizo zina msururu wa wagonjwa ambao hawajafunguliwa, lakini wenye matumaini ya kufunguliwa siku moja.. Mahali ambapo Bwana Yesu yupo, hakuna mlundikano wa wagonjwa… kwasababu yeye ni mponyaji na sio daktari!.
Leo hii kwa imani tupa hayo mafuta, tupa hayo maji, halafu liamini hili Neno la Bwana Yesu..halafu subiria uuone muujiza kwa macho yako!. Utashangaa huko kwenye maji ulikuwa unafanya nini siku zote!..
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.
NUNUA MAJI YA UZIMA.
BIRIKA LA SILOAMU.