Category Archive Home

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Taji ya miiba juu ya kichwa cha Bwana Yesu, iliashiria nini kiroho?..

Tusome,

Mathayo 27:27 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28 WAKAMVUA NGUO, WAKAMVIKA VAZI JEKUNDU.

29 WAKASOKOTA TAJI YA MIIBA, WAKAIWEKA JUU YA KICHWA CHAKE, NA MWANZI KATIKA MKONO WAKE WA KUUME; WAKAPIGA MAGOTI MBELE YAKE, WAKAMDHIHAKI, WAKISEMA, SALAMU, MFALME WA WAYAHUDI!

30 Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.

31 Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha”.

Kumbuka Pilato alipomuuliza Bwana Yesu kama yeye ni mfalme wa Wayahudi, Bwana hakukanusha… alimwambia “wewe wasema” maana yake “mimi ndiye”.

Hivyo wale Askari waliposikia Bwana Yesu kakiri kuwa ndiye  mfalme wa wayahudi, walicheka sana.. na kwasababu askari wa kirumi walikuwa wanawadharau wayahudi.. Hivyo ili kuwadhalilisha wayahudi.. ndio wakamvua zile nguo za thamani Bwana Yesu na kumvika vazi la jekundu, na kisha kumpa mwanzi (yaani fimbo)..na kumvika taji ya miiba…na mwisho kuinama kama vile wanamsujudia..

Lengo la kufanya vile ni kumweka katika mazingira kama ya kifalme… kwasababu kikawaida Mfalme anakuwa anavaa mavazi mekundu, pia anakuwa ameshika/anatembea na mwanzi wa thamani, na vile vile kichwani anakuwa na taji la thamani sana.. Lakini kwasababu hawa askari lengo lao lilikuwa ni kufanya dhihaka kwa wayahudi…ndio wakafanya hayo kwa Bwana Yesu, ili aonekane kama mfalme lakini asiye na utukufu, ambaye asiyejielewa.

Lakini walifanya vile kwa lengo la kufanya dhihaka tu!, (na kuwadhalilisha wayahudi) na si vinginevyo!…Na walifanya hivyo kwasababu hawakumjua yeye ni nani?.. kwasababu laiti kama wangemjua kuwa huyo wanayemfanyia dhihaka ndiye Mfalme wa kweli wa mbinguni na duniani, na pia ni Mungu mwenyewe katika mwili, wasingelimsulubisha zaidi ya yote wangemwabudu.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8 ambayo wenye kuitawala dunia hii HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.

Sasa swali ni kwanini Bwana Yesu asingezuia hayo yatokee na ilihali alikuwa na uwezo huo?

Sababu zipo kuu (2).

 1. ILI SISI TUPATE WOKOVU.

Bwana Yesu asingelisulubiwa maana yake sisi tusingelipata wokovu…

 2. ILI AINULIWE JUU.

Bwana Yesu mwenyewe alisema… ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.. Maana yake siri ya kuinuliwa juu, wakati mwingine ni kujishusha…Ili uwe mkubwa kuliko wote sharti uwe mdogo kuliko wote, ili upate heshima kuliko wote, sharti ukubali kukosa heshima kuliko wote, hiyo  ni kanuni kubwa sana, ambayo Bwana Yesu aliijua..

Alifahamu kuwa ili anyanyuliwe juu kuliko vitu vyote, hana budi kukubali kuonekana si kitu sasa.

Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

3. KUTUPA SISI KIELELEZO.

Sababu ya mwisho ni ili kutufundisha sisi kuwa wema, kama yeye!… kama yeye mwenyewe alivyosema.. “mtu akupigaye shavu hili mgeuzie na la pili” au mtu akulazimishaye mwendo wa maili moja, nenda naye mbili..Kwasababu kwa kufanya hivyo, ataiona haki yako na mwisho atavutiwa na imani yako, na hata kumbadilisha kabisa… (Umeona askari hao hao waliomfanyia dhihaka, masaa machache tu mbele walikiri kuwa yeye kweli alikuwa Mwana wa Mungu, Marko 15:39).

Na sisi hatuna budi kuwa kama Bwana Yesu, tunapotukanwa tunapaswa tustahimili, tunapoudhiwa na kudhalilishwa tunapaswa tustahimili kama Bwana Yesu, kwasababu mwisho wake ni mzuri..

1Petro 2:19 “Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

20 Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.

23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.

24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.

25 Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu”.

Waebrania 12:3 “Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.

4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Kwanini hatuirithi neema kama tunavyoirithi dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Tofauti na tunavyoweza kudhani, kwamba pale unapoongezeka viwango vya kiroho, Au pale unapopiga hatua moja kwenda nyingine kwa Mungu  basi utajitambua, au utapata hisia Fulani ya kitofauti kwamba amehama ulimwengu mmoja na kwenda mwingine, au utahisi nguvu Fulani zimeongezeka ndani yako, Lakini sivyo. Ni ngumu sana kujitambua wewe mwenyewe..Bali mwingine ndiye atakayekutambua.

Tunamwaona Musa aliposhuka kutoka mlimani kuzungumza na Mungu kwa muda wa siku 40, usiku na mchana, hakujua kama lipo badiliko lolote, limetokea katika uso wake.

Lakini aliposhuka tu, mlimani wana wa Israeli ndio waliokuwa wa kwanza kumtambua na kumfunulia siri ambayo hakuijua kwa muda siku zote arobaini alizokuwa anamkaribia Bwana..

Kutoka 34:29 “Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye.

30 Basi Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, tazama, ngozi ya uso wake iling’aa; nao wakaogopa kumkaribia.

31 Musa akawaita; Haruni na wakuu wote wa kusanyiko wakarudi kwake; Musa akasema nao.

32 Baadaye wana wa Israeli wote wakakaribia; akawausia maneno yote ambayo Bwana amemwambia katika mlima Sinai”.

Hii ni kutukumbusha, Mtu uliyeokoka, ukiongeza ukaribu wako kwa Mungu, kwa hatua nyingine, ni ngumu sana kuona kama utukufu wako umeongezeka  ndani yako kwa hatua moja zaidi..Mfano unapoongeza kiwango chako cha maombi, utajiona wewe ni yule yule tu, kama ulivyokuwa juzi..Lakini tayari utukufu wako umeongezeka kwa ngazi moja juu Zaidi, isiyoijua au kuihisi wewe.

Unaposema, embu ngoja nianze kujizoesha kwenda mikesha kanisani kila ijumaa, unaweza kujiona upo vilevile tu, lakini ipo hatua kubwa sana umepiga.. Ukitaka kufahamu kuwa umepiga hatua, embu sema sikumoja niache kwenda mikesha, halafu uone, huo ukame utakaouhisi ndani ya nafsi yako, utakavyokuwa.

Unapojilinda kila siku na dhambi, ya uasherati, matusi, wizi, n.k. ni rahisi kutohisi ongezeko lolote, ndani yako, lakini fahamu kuwa utukufu wako umeongezeka sana, wale wa nje ndio watakaokuja kushuhudia, Pamoja na Mungu mwenyewe. Watu wengi wanaishiwa na nguvu njiani, kwasababu wanaona kama bidii wanayoizidisha kwa Mungu, haiwarejeshei, badiliko kubwa ndani yao, kama wanavyotarajia.

Kumbuka huwezi kuuona uso wako..Ndivyo ilivyo nasi katika roho, hatuwezi kujiona wenyewe ndani yetu jinsi tunavyokuwa kiroho..Lakini walio nje ndio watakaotuona, hata kama hawatosema.

Ufalme wa Mungu ni kama mbegu, inayotupwa katika Shamba, ambayo biblia inasema, inakua kwa jinsi asivyojua mtu, Lakini mwisho wa siku ghafla tu, inatoa yenyewe matunda

Marko 4:26 “Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.

28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika”.

Hivyo, usihangaike sana, kujichunguza chunguza, kwasababu hutaona lolote. Lakini fahamu kuwa kila hatua unayoiongeza kwa Mungu, ina utukufu mkubwa sana kwako. Ndugu Usipunguze maombi, hata kama huoni chochote, usipunguze kushuhudia wengine Habari njema, usipunguze kumtolea Mungu kwa mali zako, hata kama huoni marejesho yoyote kutoka kwake, usipunguze kwenda ibadani na kuhudhuria mikesha. Kinyume chake ndio uzidishe, kuyatenda hayo.

Mwisho wa siku utukufu wako utaangaza sana kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa Mungu Musa, hadi wengine watakuogopa kwa jinsi ulivyomkaribia Mungu sana.

Ubarikiwe na Bwana.

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi// Ushauri/ Maswali/Whatsapp.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alisema “Msimwamkie mtu njiani”?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema, msimwamkie mtu njiani? (Luka 10:4).. Na wakati huo huo alisema katika Mathayo 5:47, kuwa “tukiwaamkia ndugu zetu tu!, tunatenda tendo gani la ziada”.

Jibu: Labda tuanzie kusoma kuanzia mstari wa kwanza…

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; WALA MSIMWAMKIE MTU NJIANI”.

Mwalimu anapotoa tangazo kwa wanafunzi wake na kuwaambia… “si ruhusa kuzungumza na mtu yeyote ndani ya chumba cha mtihani”.. Kwa kusema hivyo hajamaanisha kuwa “si ruhusa kuzungumza na mtu kila mahali” Hapana!.. bali ni katika chumba cha mtihani tu!..wakiwa mahali pengine wanaweza kuzungumza..

Na kadhalika Bwana hakuwakataza wanafunzi wake “kuwaamkia/kuwasalimia watu kabisa”..hapana!..bali wanapokuwepo katika “Safari ya uinjilisti” hapo ndipo “Alipowazuia wasiamkie amkie watu njiani”.

Sasa kwanini awazuie kufanya hivyo, wakiwa katika safari ya kwenda kuhubiri?

Ni kwasababu salamu zinacheleweza lile kusudi, na ni rahisi kumhamisha mtu kifikra kutoka katika mawazo ya kwenda kuhubiri mpaka kuanza kufikiri mambo mengine tofauti na yanayohusu injili anayokwenda kuhubiri..

Hebu tengeneza picha Mwanafunzi mmojawapo wa Bwana Yesu, anakwenda kuhubiri, halafu njiani anapita karibu na nyumba ya Mjomba wake..halafu anaingia kumsalimia, na katika mazungumzo anapewa taarifa mbalimbali aidha za misiba, au za watu wengine au nyingine zozote..

Au anapewa jukumu lingine la kufanya huko anakokwenda, labda anaambiwa ukifika mahali fulani naomba uninunulie kitu fulani, ukirudi nipitishie hapa, au ukifika mahali fulani nisiaidie kuulizia hili au lile, au ukifika sehemu Fulani kumbuka kumsalimia mtu Fulani, au huko unakokwenda kuwa makini nako kuna hatari n.k..

Ni wazi kuwa kuanzia huo wakati na kuendelea mawazo ya yule mwanafunzi yatakuwa yametawaliwa na yale aliyoyasikia kutoka kwa ndugu yake huyo, na yale ya injili yatakuwa yamemezwa…

Kwahiyo ili kulizuilia hilo.. ndipo Bwana akasema… “Msiwaamkie watu njiani”.. ili mawazo yao na akili zao ziwe katika Injili wanayokwenda kuihubiri..

Lakini watakapomaliza safari yao hiyo ya injili wapo huru kuwaamkia watu wowote pasipo kupendelea sawasawa na Neno hilo la Bwana katika Mathayo 5:47

Kadhalika na sisi, tunapokuwa katika uinjilisti, hatupaswi kuuchanganya na mambo mengine, tunapokuwa katika kuifanya kazi ya Mungu, hatuna budi akili zetu, mawazo yetu, kuyafunga yasiingiliwe na mawazo mengine.. (kadhalika tunapokuwa katika ibada ni sharti kuzima simu, ili kuongeza umakini katika kuomba, kusifu na kusikiliza Neno).

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Katika Marko 6:12 maandiko yanasema…“Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu”… Hizi deni ndio zipi??

Jibu: Mtu aliyekutukana ana deni kwako la kuja kukuomba radhi!..Hilo ni deni lake kwako, awe anajua au hajui…Na kulilipa ni yeye kuja kukuomba wewe radhi!.. Asipokuja kukuomba radhi basi hilo litabaki kuwa deni kwake. (wewe utakuwa unamdai). Labda wewe uamue kumsamehe tu!

Hali kadhalika na sisi tunapomfanyia Mungu dhambi, tunakuwa na deni kwake la KUUNGAMA! (Maana yake kukiri makosa yetu na kuomba radhi kwake)!. Hayo ni madeni kwetu kwa Mungu..

Kwa maana dhambi ni kosa lolote mtu analolifanya dhidi ya Mungu.

Lakini Bwana wetu Yesu alitufundisha kuwa ni lazima tuwasamehe watu madeni yao ili na sisi tusamehewe yetu!.. Maana yake, yale mambo ambayo wangepaswa waje waungame mbele yetu (yaani kukiri na kuomba radhi), wanapoungama basi tunawasamehe, na hata wasipokuja kuomba radhi vile vile tunapaswa tuwasamehe.

Na wakati mwingine watu wanatukosa pasipo hata wao kujua kama wametukosa, hivyo hawawezi kuja kutuomba radhi kwasababu hata hawajui kama wametukosea, (Hivyo wanabakia kuwa na madeni kwetu ambayo hawajui hata kama wanayo)..

Kadhalika na sisi tunamkosea Mungu kwa mambo mengi, ambayo wakati mwingine hatujui kama tunamkosea (Jambo linalotufanya tuwe na madeni mengi mbele za Mungu), hata pasipo sisi wenyewe kujua.

Kwahiyo tunapoomba hiyo sala ya Baba yetu!, na kusema “utusamehe deni zetu”.. Maana yake tunamsihi Mungu atusamehe yale makosa ambayo hatukuyatubia au yale tuliyoyafanya pasipo kujua kuwa ni makosa…Na Mungu ni mwaminifu, anatusamehe…lakini kama tu na sisi tutakuwa tayari kuwasamehe wengine madeni yao.

Swali ni Je!, na wewe umemsamehe yule aliyekutukana au kukusengenya au kukutapeli? au unasubiri aje kukuomba radhi?…nakuambia usingoje!..wewe msamehe hata bila yeye kukuomba radhi, ndivyo na Mungu atakavyokusamehe na wewe makosa ambayo hata wewe hukumwomba radhi!..

Bwana wetu Yesu Kristo, aliwasamehe wale wote, ambao walimsulubisha, (Aliwasamehe pasipo wao kumwomba msamaha).. kwakufanya vile alitupa na sisi kielelezo, kwamba na sisi tuwasamehe wenzetu kama yeye alivyotusamehe. Kwasababu tusipowasamehe watu makosa yao na Mungu wetu hatatusamehe sisi.

Mathayo 18:21“Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 YESU AKAMWAMBIA, SIKUAMBII HATA MARA SABA, BALI HATA SABA MARA SABINI.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

Rudi nyumbani

Print this post

Rushwa inapofushaje macho?

Biblia inasema rushwa inawapofusha macho hao waonao? (Kutoka 23:8) Ni kwa namna gani rushwa inaweza kumpofusha mtu macho?

Jibu: Tusome,

Kutoka 23:8 “Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki”.

Ili tuelewe vizuri, hebu tutafakari mfano ufuatao..

Hakimu mahakamani anaona kabisa mhalifu fulani amefanya kosa linalostahili kifungo (yaani macho yake yanaona kabisa lile ni kosa alilolifanya, na anapaswa ahukumiwe kulingana na sheria)..Lakini anapopewa rushwa, palepale anajiziba macho, na kumwachia yule mhalifu, na kulifunika kosa lake.. (Sasa kitendo hicho cha hakimu kujiziba macho na kulifunika kosa, ndicho kinachoitwa kupofuka macho).. na hiyo yote ni kwasababu ya rushwa!..Laiti asingepokea rushwa angelitazama kosa na kulihukumu jinsi inavyostahili..

Ndio maana biblia inasema…“Rushwa huwapofusha macho hao waonao”..Wanaona na kujua kabisa jambo Fulani sio sawa, lakini rushwa inawafanya wasilione kama ni kosa tena..(macho yao yamepofuka!).

Na sio tu!, kuwapofusha macho hao wanaoipokea, bali pia “inayapotoa maneno ya wenye haki”.. maana yake.. wale watu wastahilio kupata haki, hawapati hiyo haki, wanaonena maneno ya haki, maneno yao yanapotoshwa kwasababu ya rushwa iliyotolewa na mwingine.

Ni mara ngapi, watu wasio na hatia wanafungwa, kwasababu tu upande mmoja umetoa rushwa?..

Biblia utaona inazidi kuliweka hilo wazi katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati..

Kumbukumbu 16:19 “Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; WALA USITWAE RUSHWA; KWA KUWA RUSHWA HUPOFUSHA MACHO YA WENYE AKILI, NA KUGEUZA DAAWA YA WENYE HAKI”.

Na sisi kama wakristo hatupaswi kupokea wala kutoa rushwa!..kwasababu rushwa ina laana nyuma yake.

Mithali 17:23 “ASIYE HAKI HUTOA RUSHWA KIFUANI, Ili kuzipotosha njia za hukumu”.

Katika biblia utaona mojawapo ya sababu iliyomfanya Nabii Samweli akubalike mbele za Mungu na watu, na kuzidi kupata kibali cha kuiamua Israeli mpaka uzee wake, ni mwenendo wake wa kutokubali Rushwa..

1Samweli 12:1 “Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu.

2 Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo.

3 NAMI NIPO HAPA; BASI, MNISHUHUDIE MBELE ZA BWANA, NA MBELE YA MASIHI WAKE,NALITWAA NG`OMBE WA NANI? AU NALITWAA PUNDA WA NANI? AU NI NANI NILIYE MDHULUMU? NI NANI NILIYEMWONEA? AU KWA MKONO WA NANI NIMEPOKEA RUSHWA INIPOFUSHE MACHO? NAMI NITAWARUDISHIA NINYI.

4 NAO WAKASEMA, HUKUTUDHULUMU, WALA HUKUTUONEA, WALA HUKUPOKEA KITU KWA MKONO WA MTU AWAYE YOTE.

5 Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi”

Umeona?..Samweli hakuwahi kupokea rushwa Maisha yake yote, na ndio ikawa sababu ya yeye kudumu katika Uamuzi wa Israeli, Lakini sasa kinyume chake, wanawe wawili aliowazaa hawakuwa kama yeye, wao walikuwa wanapokea rushwa..

Jambo ambalo liliwafanya wana hao wa Samweli kutolewa katika kiti cha Uamuzi wa Israeli, na hiyo ni kwasababu tu ya RUSHWA walizokuwa wanazipokea kutoka kwa watu..na matokeo yake ikasababisha Israeli nzima kuingia katika dhambi ya kutaka mfalme, kutokana na kwamba waliona Watoto hao wa Samweli hawafai..

1Samweli 8:1 “Hata Samweli alipokuwa mzee, aliwafanya wanawe wawe waamuzi juu ya Israeli.

2 Na jina la mwanawe mzaliwa wa kwanza aliitwa Yoeli; na jina la wa pili Abiya; walikuwa waamuzi katika Beer-sheba.

3 ILA WANAWE HAWAKUENDA KATIKA NJIA ZAKE, BALI WALIZIACHA, ILI WAPATE FAIDA; WAKAPOKEA RUSHWA, NA KUPOTOSHA HUKUMU.

4 Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama”

5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote.

Hiyo ikitufundisha kuwa Rushwa, siku zote inatokosesha kibali mbele za Bwana na mbele za watu!…

Ukitaka udumu katika Nafasi yoyote uliyopo, ambayo ni Mungu kakuweka, basi kaa mbali na rushwa!.. ukitaka udumu katika utumishi (wa Mungu) kaa mbali na rushwa, ukitaka udumu katika kazi ya mikono unayoifanya basi kaa mbali na rushwa.. Wanadamu wengi wanaweza wasikuone unayoyafanya kwa siri, lakini Mungu anakuona, na yeye ndiye atakayekuvua hiyo nafasi..na Zaidi ya yote utakapokufa bila kuacha rushwa, basi utahukumiwa.

Ayubu 15:34 “Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, NA MOTO UTATEKETEZA MAHEMA YENYE RUSHWA”.

Bwana atusaidie..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni kwanini Yesu alisema Na wakisikia wasikie, wasielewe Wasije wakaongoka?

Rudi nyumbani

Print this post

Unyenyekevu ni nini?

Unyenyekevu ni nini, kibiblia, ili mtu awe ni mnyenyekevu anapaswa aweje?


Tafsiri ya Unyenyekevu ni Kujishusha. Pale unapokuwa na uwezo wa kutumia nguvu, au sauti, au mamlaka, kuhimiza jambo, lakini unajishusha chini, kana kwamba wewe si kitu, huo ndio unaitwa unyenyekevu.

Unyenyekevu sio kushushwa, bali kujishusha. Na kinyume cha Unyenyekevu ni kiburi, yaani kujipandisha juu, kujiona wewe unaweza yote, wewe ni bora kuliko vyote, wewe una nguvu kuliko wote, wewe una sauti zaidi ya wote.

Unyenyekevu ni mgumu sana kuufikia, kwasababu asili ya mwanadamu ni kutaka kujipandisha juu. Lakini ukiupata unyenyekevu basi umepata mpenyo mkubwa sana wa kumfikia Mungu.

Kiwango cha unyenyekevu kinatofautiana, kwa jinsi mtu anavyoteremka ngazi moja chini, ndivyo kiwango chake cha unyenyekevu kinavyokuja juu, na pale anapoongeza ngazi nyingine na nyingine ndivyo unyenyekevu wake unavyofikia kilele cha juu sana.

Ni kwanini tuwe wanyenyekevu?

  1. Ni kwasababu Kristo naye alikuwa mnyenyekevu;

Wafilipi 2:6 “ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

2) Kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

Mungu ni adui mkubwa kwa kiburi, hivyo tukilijua hilo ni kujitahidi sana tuwe mbali na kitu hicho.

Faida za kuwa wanyenyekevu ni zipi?

  1. Mungu anakuwa karibu nasi:

Mungu alikuwa karibu na Bwana Yesu, kuliko mtu mwingine yeyote, na hiyo yote ni kwasababu ya unyenyekevu wake:

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

     2) Mungu anatukweza juu;

Utaona baada ya Bwana Yesu kujishusha, Mungu alimkweza juu Zaidi ya vitu vyote ulimwenguni.

Wafilipi 2:8 “tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

Tunakuwaje wanyenyekevu?

  1. Kumuhesabu mwenzako ni bora kuliko nafsi yako mwenyewe.

Wafilipi 2:3 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake”.

     2) Kuuzuia ulimi:

Kuwa wa mwisho kunena, na kuzuia hasira zako, usitoe maneno ya majigambo;

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”.

  3) Kutojihesabia haki, mbele za Mungu:

Luka 18:9 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi”.

14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

     4) Kukubali kujishughulisha na mambo manyonge

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili”.

Si lazima, kila jambo la juu tung’ang’anie kulifanya. Bwana Yesu alikuwa ni Mungu, lakini akaona kule kuwa sawa naye sio kitu cha kushikamana nacho. Akawa kama mtumwa..Vivyo hivyo na sisi tupende utumwa kuliko ukubwa.

Mwisho kabisa tukumbuke kuwa Unyenyekevu kibiblia, upo kwa namna mbili; Unyenyekevu wa sisi kwa sisi, na unyenyekevu kwa Mungu. Vyote viwili vinakamilisha Unyenyekevu wa ki-Mungu. Kama vile ulivyo upendo. Ili tukamilike katika huo ni sharti, tupendane sisi kwa sisi, na vilevile tumpende Mungu.

Ndio maana Bwana Yesu aliwatawaza miguu watakatifu wake, akatupa na sisi kielelezo kuwa tunyenyekeane sisi kwa sisi, kama yeye alivyofanya.

Hivyo tuizingatie sana nguzo hii muhimu katika ukristo wetu. Ili tumfurahie Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

Furaha ni nini?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TUMAINI NI NINI?

Jehanamu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Dusumali ni nini katika biblia?

Dusumali ni nini?, Mafurungu ni nini?, na Matalasimu ni nini?.. kama tunavyosoma katika Isaya 3:20?


Jibu: Tusome,

Isaya 3:20 “na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu”

 1. Dusumali ni nini?

Dusumali ni aina ya mavazi ambayo yalikuwa yanavaliwa kichwani..ambayo yalikuwa yanatengenezwa na malighafi tofauti tofauti kulingana na tamaduni za jamii husika. Na waliokuwa wanazivaa sana ni watu mashuhuri au viongozi wa jamii hiyo…Kwajamii za maeneo ya Afrika, dusumali zilikuwa zinatengenezwa na manyoya ya ndege(Tazama picha juu).. Maeneo ya Misri, zilikuwa zinatengenezwa kwa vitambaa maalum.

 2. Mafurungu ni nini?

Mafurungu ni urembo unaofungiwa katika miguu ya wanawake..(Tazama picha chini).

mafurungu

 3. Matalasimu ni nini?

Matalasimu ni vitu ambavyo watu wanavivaa shingoni, au wanajifungia katika sehemu za miili yao, kama kinga yao. (kwa lugha ya sasa zinaweza kuitwa hirizi).

Lakini mavazi haya yote ni ya kidunia.. na watu wa Mungu waliookoka (wakiume na wakike) hawapaswi kuyavaa, kwani ni machukizo, ndio maana utaona hapo katika hiyo isaya mlango wa 3, Bwana anasema atawapiga wavaao hayo, kwasababu matendo yao yanaendana na mavazi yao..

Isaya 3:16 “Bwana akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienenda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;

17 Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na Bwana ataifunua aibu yao”.

18 Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;

19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;

20 na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;

21 na pete, na azama”

Biblia inasema miili yetu ni HEKALU LA ROHO MTAKATIFU. Na si Nyumba tu!..bali hekalu (1Wakorintho 6:19)..Kama ni hekalu maana yake halipaswi kuvikwa hirizi, halipaswi kuvikwa vitu vya kikahaba.. kwani Mafurungu pamoja na vikuku na hazama, walikuwa wanavaa makahaba..

Kama binti wa kiMungu unapenda kujipamba basi biblia imetoa mwongozo mzuri wa namna ya kujipamba na kupendeza..

1Timetheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake NA WAJIPAMBE KWA MAVAZI YA KUJISITIRI, PAMOJA NA ADABU NZURI, NA MOYO WA KIASI; SI KWA KUSUKA NYWELE, WALA KWA DHAHABU NA LULU, WALA KWA NGUO ZA THAMANI;

10 BALI KWA MATENDO MEMA, KAMA IWAPASAVYO WANAWAKE WANAOUKIRI UCHAJI WA MUNGU”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Ni nani aliyesema Nitume mimi? katika (Isaya 6:8)

Shubaka ni nini kibiblia? (Mithali 7:6)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Kandake” (Matendo 8:27)

SWALI: Tunasoma yule mkushi alikuwa ni mwenye mamlaka chini ya Kandake Malkia wa Kushi.. Naomba kufahamu Neno Kandake lina maana gani?


JIBU: Filipo, Mhubiri wa injili, aliagizwa na Malaika wa Bwana, aende njia ya jangwani (Gaza), Lakini alipokuwa njia kushuka huko alikutana na huyu mkushi ambaye alikuwa ni towashi, ndipo akamuhubiria injili, na siku hiyo hiyo akabatizwa, baada ya hapo Filipo akatoweshwa na Roho Mtakatifu na kupelekwa  sehemu nyingine.

Matendo 8:26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.

27  Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu”

Lakini biblia inasema huyu mkushi alikuwa ni mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi.  Kandake ni jina la Mamalkia wote wa nchi ya Kushi (Kushi ndio nchi ya Ethiopia). Kumbuka sio jina la mtu binafsi bali ni jina la cheo. Kama vile ilivyokuwa kwa Farao, au Kaisari. Kwamba wafalme wote waliitwa Farao, au Kaisari. Ndivyo ilivyokuwa kwa mamalkia wote wa Kushi waliitwa Kandake.

Ndio huyu towashi aliwekwa chini ya umalkia huo ili kuilinda na kuitunza hazina yote ya taifa hilo la Kushi. Na unaweza kujiuliza ni kwanini awe ni towashi?. Ilikuwa ni desturi, kwa falme nyingi za zamani, pindi wanapotaka kuwaweka chini ya mamalkia wao, na chini ya sekta nyeti kama hizo za fedha. Waliwaasi, watumwa hao, ili kusudi kwamba wasivutwe na tamaa za mwili, na pia wasifikirie kuacha utumwa wao, na kujali familia zao( yaani Watoto wao na wake), Zaidi ya maslahi ya nchi. Hivyo hiyo ilikuwa inawafanya wawe wanyenyekevu na wawe makini sana katika kazi walizowekewa chini yao.

Inatufundisha nini?

Hata kuwekwa chini ya kazi maalumu za Mungu ni hivyo hivyo, Kunategemea sana uaminifu wetu. Rohoni tunapaswa tuwe kama matowashi. Tufe kwa Habari za tamaa za ulimwengu. Kiasi kwamba hata ukijaribiwa kwa mali, hali yako ni ile ile, ukijaribiwa kwa uzinzi, hutikisiki, ukijaribiwa kwa umaarufu, unabakia kuwa yule yule, kama Bwana Yesu, hugeuki kuwa nabii wa uongo.

Hapo ndipo Bwana anapopahitaji sote tupafikie, ili atuamini na kutuweka katika kazi zake maalumu. Hivyo Bwana anataka tufanane na matowashi rohoni mwetu. Kama alivyokuwa Ayubu mtumishi wake (Ayubu 31:1, 25)

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Nini kinatokea baada ya kifo

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Rudi nyumbani

Print this post

MADHARA YA KUTOIJUA KWELI YOTE!

Kuna madhara makubwa sana ya KUTOIJUA KWELI YOTE!.. Unaweza kuijua kweli tu!, lakini usiijue kweli yote…Watu wengi leo hii wanaijua kweli… “lakini hawaijui kweli yote”.. Jambo ambalo linafungua mlango mkubwa sana wa shetani kuleta Uharibifu.

Hebu tuangalie mfano wa watu wawili ambao waliijua kweli, lakini si YOTE!.

 1. MFALME ABIMELEKI

Ibrahimu, alimwambia Mfalme Abimeleki kuwa Sara ni “Dada yake” ..lakini hakumwambia kuwa Sara pia ni “mke wake”.. alimwambia vile kwa hofu ya kuuawa..kwasababu Sara alikuwa ni mzuri wa uso.

Sasa sio kwamba Ibrahimu alimdanganya Mfalme Abimeleki!.. hapana! Hakumdanganya kwasababu ni kweli Sara alikuwa ni dada Ibrahimu.. Wameshea baba mmoja, ila mama mbali mbali. Kwahiyo alikuwa ni kweli dada yake. Hivyo hakumwambia uongo Mfalme Abimeleki.. Lakini tatizo ni kwamba hakumwambia KWELI yote!.. alimwambia kweli iliyo NUSU tu!.. na matokeo yake ni kumletea Abimeleki hatari ya kuawa na Mungu..

Tusome,

Mwanzo 20:1 “Ibrahimu akaondoka huko kwenda nchi ya kusini, akakaa kati ya Kadeshi na Shuri, naye akatembea katika Gerari.

2 Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.

3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.

4 Basi Abimeleki alikuwa hakumkaribia, akasema, Ee Bwana, Je! Utaua hata taifa lenye haki?

5 Je! Hakuniambia mwenyewe, Huyu ni ndugu yangu? Na mwanamke mwenyewe naye alisema, Huyu ni ndugu yangu. Kwa ukamilifu wa moyo wangu, na kwa kuwa safi mikono yangu, nimefanya hivi.

6 Mungu akamwambia katika ndoto, Nami nimejua ya kwamba kwa ukamilifu wa moyo wako umefanya hivi, ndipo nami nikakuzuia usinitendee dhambi, kwa hiyo sikukuacha umguse.

7 Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao.

8 Abimeleki akaamka asubuhi na mapema, akawaita watumwa wake wote, akawaambia maneno hayo yote masikioni mwao, nao watu hao wakaogopa sana.

9 Kisha Abimeleki akamwita Ibrahimu, akamwambia, Umetutenda nini? Nimekukosa nini, hata ukaleta juu yangu na juu ya ufalme wangu dhambi kuu? Umenitenda matendo yasiyotendeka.

10 Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Umeona nini hata ukatenda jambo hili?

11 Ibrahimu akasema, Kwa sababu naliona, Yakini hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu.

12 NAYE KWELI NI NDUGU YANGU, BINTI WA BABA YANGU ILA SIYE MWANA WA MAMA YANGU, NDIPO AKAWA MKE WANGU”.

Umeona hapo mstari wa 12?.. “Ibrahimu hakusema uongo, alisema Kweli lakini si yote”

 2. HAWA

Hawa aliambiwa ukweli na shetani, lakini hakuambiwa ukweli wote!.. Aliambiwa kwa kula tunda, “Atakuwa kama Mungu, akijua mema na mabaya”..huo ni ukweli kabisa! Kwani alipokula tu lile tunda, alikuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya…

Mwanzo 3:22 “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele”

Lakini shetani hakumwambia ukweli wote kwamba, licha ya kuwa utakuwa kama Mungu akijua mema na mabaya lakini Zaidi ya hayo, atakuwa pia amejitenga mbali na uwepo wa MUNGU, na umemuasi Mungu moja kwa moja. (Hayo hakumwambia)..kwasababu laiti angemwambia Hiyo kweli yote!, Hawa asingelisogelea lile tunda!.

Umeona Madhara ya kutoijua kweli yote?..

Yalimletea Mfalme Abimeleki hatari ya kifo, kwa kumtwaa Sara.. vile vile, yalimletea Hawa anguko kubwa ambalo mpaka leo tunaona madhara yake.

Vile vile shetani leo hii, anawaambia watu ukweli, lakini hawaambii kweli yote!..na watu wanajitumainisha katika ile kweli, lakini hawataki kuitafuta kweli yote..

Kwamfano Neno linasema, kila amwaminiye Bwana Yesu amevuka kutoka mautini kuingia uzimani..

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Hiyo ni KWELI KABISA!..Lakini kweli yote inasema hatuna budi kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu na kuishi Maisha matakatifu baada ya hapo..

Mathayo 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Maana yake hatuishii kumwamini Bwana Yesu tu!, halafu basi..bali tunapaswa pia tubatizwe!..Na pia haiishii kubatizwa tu..bali pia tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu na tuishi Maisha matakatifu baada ya hapo ndipo tutakapomwona Mungu..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO”.

Na sio tu katika eneo la wokovu tunahitaji kuijua kweli yote, bali katika mambo mengine yote!.. leo hii watu wanaamini kuwa Mungu anaangalia moyo!..Hiyo ni kweli, lakini SI KWELI YOTE!.. Kweli yote inasema..

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”.

Na tena inasema..

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe”

Kwahiyo hatupaswi miili yetu, kuivika vibaya, hatupaswi kuichora, kuitoboa toboa, kuilevya, au kuiharibu kwa namna yoyote ile.(www wingulamashahidi org)

Sasa swali la kujiuliza?..Utawezaje kuijua KWELI yote!.

Ashukuriwe Mungu, kwa zawadi ya Roho aliyotumwagia.. huyo ndio suluhisho la mambo yote..

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, HUYO ROHO WA KWELI, ATAWAONGOZA AWATIE KWENYE KWELI YOTE; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe…”

Je! Leo unataka kuyajua mapenzi ya Mungu, katika ukamilifu wote?..unataka kuijua kweli yote ya Maisha yako ya kiroho na kimwili?..Basi tafuta Roho Mtakatifu…sasa utauliza, utampataje Roho Mtakatifu ndani yako?..Biblia imetupa kanuni..kuwa ni kwa kutubu, na kubatizwa..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 PETRO AKAWAAMBIA, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Bwana akubariki

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ni madhara gani yatampata mtu yule anayetafsiri Neno isivyopaswa!

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

Rudi nyumbani

Print this post

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.

Na pombe na sigara si ni vya Kaisari (yaani serikali imevihalalisha), hivyo si ni sawa kuvitumia..?

Jibu: Kumekuwa na tafsiri nyingi juu ya huo mstari “Vya Kaisari mpeni Kaisari na vya Mungu mpeni Mungu”… Wengine wanatafsiri vya Kaisari kama vitu vyote viovu vya ulimwengu.. Hivyo tumepewa ruhusa ya kuvifanya hivyo, lakini pia tusiache kuvifanya vya Mungu.. “Kwamba tunapoenda disko hapo tumempa Kaisari vya kwake, vile vile tunapoenda kanisa, hapo tumempa Mungu vya kwake”..

Lakini je! Hiyo ndio tafsiri yake au ndio maana ya huo mstari?

Tusome..

Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli

22 JE! NI HALALI TUMPE KAISARI KODI, AU SIVYO?

23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

24 Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.

25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu”.

Hapo utaona Vya Kaisari Bwana alivyovimaanisha ni “KODI” na mambo yote yanayofanana na hayo..(Kwa ufupi mambo yote mema)..kama Ushuru, uwajibikaji, utulivu, amani n.k

Ndio maana Bwana akawauliza swali, sarafu hiyo ina sura ya nani?..wakajibu ya Kaisari..na ndipo akajibu vya Kaisari mpeni Kaisari..Maana yake vile vyote Kaisari anavyovihimiza na kuvihitaji vya lazima  “basi apewe” kwasababu havihitaji kwa lengo baya!!.. bali zuri kwa watu wake!.

Kama maandiko yanavyosema katika…

1Wakorintho 13:3 “KWA MAANA WATAWALAO HAWATISHI WATU KWA SABABU YA MATENDO MEMA, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? FANYA MEMA, NAWE UTAPATA SIFA KWAKE;

4 kwa kuwa yeye ni MTUMISHI WA MUNGU KWAKO KWA AJILI YA MEMA…”

Umeona hapo?.. maandiko yanasema watawalao ni watumishi wa Mungu kwako KWA AJILI YA MEMA!!…Kwahiyo yote ya lazima ambayo Kaisari aliyahitaji kutoka kwa watu, ni mambo MEMA na si Mabaya!!

Sasa mambo hayo ni yapi?..ambayo Kaisari aliyahitaji na ambayo ni lazima “apewe”?

 1. KODI

Kaisari alihitaji “kodi” na lengo la kodi, sote tunajua kuwa sio Baya!….kwasababu kodi hazitumiki kwenda kumnufaisha yeye, bali kuwanufaisha wananchi wote, kwa kutengeneza miundo mbinu ya msingi, na matumizi mengine muhimu.. Hivyo Taifa lisilokusanya kodi haliwezi kuendelea.. Kwahiyo Kodi ni jambo ambalo halikinzani na Neno la Mungu..Ndio maana Bwana Yesu akaamuru tuwape kodi wenye mamlaka.

1Wakorintho 13:6 “KWA SABABU HIYO TENA MWALIPA KODI; KWA KUWA WAO NI WAHUDUMU WA MUNGU, WAKIDUMU KATIKA KAZI IYO HIYO.

7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima”.

 2. AMANI na UTULIVU.

Kaisari, alihubiri “Amani na utulivu”…kwasababu watu wakiwa watulivu, Ufalme wake utajengeka… hivyo hakuhitaji wauaji, hakuhitaji waasi, hakuhitaji watu wenye vurugu, hakuhitaji wezi, hakuhitaji wahuni n.k.

Hivyo mtu akiwa muuaji, (alikuwa hajampa Kaisari yaliyo yake)…kwasababu yeye alikuwa anahitaji watu walio wazuri (na ilikuwa ni amri sio ombi)…Ilikuwa si ruhusa kuua mtu, wala kujichukulia sheria mkononi n.k”.

Na mambo mengine yote ya lazima, (kumbuka yapo mambo ya lazima ambayo wenye mamlaka waliyaagiza na yapo yasiyo ya lazima).. Hakuna Mfalme anayewalazimisha watu wake wanywe pombe!..lakini atawalazimisha wawe na Amani na Utulivu na vile vile walipe kodi. Sasa mambo hayo ambayo ni ya Lazima, MENGI NI MAZURI!!.. Ndio maana Bwana aliamuru tuyafanye hayo.

Vile vile hata sasa… tunapaswa tunayo amri ya kumpa Kaisari yaliyo yake!.. (Tunapaswa tulipe kodi, au ushuru pale inapotubidi)..hali kadhalika sheria za nchi zinatulazimisha kuwa watulivu, watu wa amani na watiifu, na watu wa Staha..hatuna budi kuwa hivyo..(Na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumempa Kaisari yaliyo yake)..Kwasababu mambo hayo hayakinzani na Neno la Mungu.

Lakini swali ni je!.. Kama vya Kaisari ni Kodi, ushuru, na mambo mengine yanayofanana na hayo, je ya Mungu nayo ni yapi?..Ambayo Bwana Yesu alisema tumpe!. (..Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU..”.

Tusome,

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.

Bwana anahitaji tumwombe yeye Rehema, (anahitaji tutubu)!.. Hicho ndio kitu cha kwanza anachokihitaji kutoka kwetu..na wala si sadaka zetu!!.. Sasa sio kwamba sadaka zetu hazina maana kwake la!.. zina maana kubwa sana, lakini kinachotangulia ni Rehema..

Tusome,

Mathayo 23:23 “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, NA REHEMA, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, WALA YALE MENGINE MSIYAACHE”.

Umeona hapo?..sadaka tunapaswa kumpa Bwana, lakini REHEMA ni muhimu Zaidi.. Toba ni muhimu sana…

Na toba halisi ni ile inayoendana na matendo.. Maana yake tunatubu, kwa kumaanisha kuziacha dhambi!.. Hicho ndicho Mungu anachokihitaji kwetu.. Hali kadhalika hata baada ya kutubu, na kukaa katika Imani, hatuna budi kuendelea kujitakasa kila siku, kwa Neno la Mungu..(Hayo ndio mambo ambayo Mungu anayataka kutoka kwetu).

Je umeokoka?.. Umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo?, na kupokea Roho Mtakatifu?…Na hata kama umeshaokoka.. je unajitakasa kila siku kwa Neno la Mungu??

Kama bado basi bado hujaanza kuyafanya mapenzi ya Mungu, haijalishi unatoa sadaka kiasi gani?.. Sicho kitu cha kwanza Mungu anachokihitaji kutoka kwako, bali anahitaji wewe upate Rehema kutoka kwake kwa kutubu.

Hivyo kama leo hii ungependa kutubu na kumkaribia Mungu Zaidi.. basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba (katika mwisho wa somo), ili tuweze kukuongoza sala fupi ya Toba..ambayo itamkaribisha Bwana Yesu katika Maisha yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Mizimu ni nini?

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post