Category Archive Home

JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetus Yesu Kristo, sifa na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.

Unafahamu kuwa shetani ambaye ni adui yetu, si kila wakati anafanya mambo yake kwa kutegemea jitihada zake tu, anajua  kabisa mambo mengine huwa hayatoki isipokuwa kwa kufuata kanuni ambazo tayari Mungu alishaziweka.

Na huwa anazitumia hizo kanuni, kutuharibu sana, lakini sisi kama wana wa ufalme, hatuzitumii kumuharibu yeye.

Kwamfano madhara aliyopanga kumletea  Ayubu, alitambua kuwa haiwezekani kwa njia ya kawaida kuyatekeleza ,. Ndipo akatumia njia ya juu Zaidi ya kujishusha, kwa kwenda KUJIHUDHURISHA mbele za Mungu,.

Akashusha kiburi chake hadi chini kabisa, akaungana na Malaika watakatifu wa Mungu, kupanda mbinguni, akaenda mbele ya uwepo wa Mungu, kwa unyenyekevu wote, akitumaini kuwa kwa kutenda kule, ni lazima tu Mungu atamwangalia, kwasababu Mungu ni Mungu wa uumbaji wote.

Na kweli baadaye Mungu alipomwona anatembea tembea mbele ya uwepo wake kwa muda mrefu, akaanzisha mazungumzo naye, Akamuuliza unatoka wapi shetani, akasema duniani, katika mizunguko yangu, ndipo shetani akatumia fursa hiyo ya mazungumzo, kupeleka na mashataka yake yote. Na mwisho wa siku akapatiwa haja yake.

Akashuka chini, akamfanya Ayubu kama alivyoweza kumfanya..

Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.

7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”.

Tunachopaswa tujue ni nini, Ikiwa mungu wa dunia hii, anajua siri ya mafanikio ya uharibifu wake, haitegemei tu nguvu zake mwenyewe, bali pia kwa kujihudhurisha mbele za Mungu ..Unategemea vipi wewe na mimi tusiwe watu wa namna hiyo?

Shetani anatushangaa sana, tunapomkimbia Mungu, anatushangaa sana tunapokwenda mbali na uwepo wa Mungu, kwa visingizio visivyokuwa na maana, hatutaki kwenda kumfanyia Mungu ibada hata mara moja kwa wiki tunasema tumechoka, kwasababu jumatatu tunakwenda kazini hivyo hatuna budi tulale!! Ndugu ukitegemea nguvu zako kuyaongoza haya Maisha jihesabie tu wewe ni MKIA Maisha yako yote. Ndivyo ilivyo..

Hilo shetani alijaribu akaona halifai, na wewe unalijaribu, alijua si kila wakati nitajiamulia tu mimi mwenyewe, kwa nguvu zangu..Lazima niwe na muda wangu wa kwenda kujinyenyekeza, tena kwa muda mrefu mbele za Mungu.

Ikiwa tunaona mikesha ni shida, hata mara moja kwa mwezi, tusahau Mungu kuanzisha mazungumzo yoyote na sisi. Ikiwa hatujizoezi kusali mara kwa mara, na kuutafuta uso wa Mungu hata kwa mifungo wakati mwingine, tujue tu mambo mengi sana tutafeli kuyatimiza maishani mwetu.

Faida za kujihudhurisha mbele za Bwana ni zipi?.

Tunapokuwa uweponi mwa Bwana muda mrefu, Mungu mwenyewe ataanzisha mazungumzo na sisi, atatuuliza, unasumbukia nini, una haja gani, unatafuta nini? Kama tu alivyofanya kwa shetani…Lakini akitutazama hatupo uweponi mwake, Tunazunguka zunguka tu duniani, na masumbufu ya Maisha haya kila wakati, siku saba kwa juma, siku 365 za mwaka, na yeye ataendelea na mambo yake, atatuacha tutaabike wenyewe..

Biblia inasema..

Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi..”

Ndugu tujizoezi, kumkaribia Mungu kila siku, ibada inayotoka rohoni iwe ni sehemu ya Maisha yetu, Na bila shaka tutaanza kumuona Mungu akisema na roho zetu.

Kumbuka uanzapo kufanya mambo kama hayo kwa bidii, hutasikia sauti kama sauti ikisema na wewe, bali rohoni Mungu atakuwa anazungumza na Maisha yako. Na mara utaona yote uliyokuwa unamwomba, au unayatamani yatendeke tangu zamani, Mungu anakufanikisha kwa njia ambazo hujazitazamia. Hivyo ndivyo Mungu anavyozungumza na watu.

Tukiijua kanuni hii, shetani atatuchukia sana, kwasababu tutakuwa tumeshajua siri ya mafanikio yetu, kama yalivyokuwa yake katika huu ulimwengu.

Kama wewe ni mtakatifu, anza sasa kumpa Mungu muda wako wa kutosha, huko ndiko kujihudhurisha mbele zake, usiwe na udhuru wa kutokwenda ibadani, usiwe na udhuru wa kutohudhuria mikesha na wenzako, usiwe na udhuru wa kutokufunga na kuomba, na kujifunza Neno kila siku. JIHUDHURISHE kwa kadiri uwezavyo mbele za Mungu.

Ndivyo Mungu atakavyoanzisha mazungumzo na wewe.

Bwana akubariki.

Ikiwa bado upo nje ya Kristo, kumbuka kuwa, hatuna muda mrefu hapa duniani, Unyakuo ni wakati wowote, kulingana na kutimia kwa dalili zote zilizotabiriwa katika maandiko, na kama hilo halitoshi fahamu kuwa mlango wa neema, umeshaanza kufungwa, usipoiamini injili, leo, kesho itakuwa ni ngumu Zaidi, na siku moja hutaiamini kabisa. Kwasababu neema haidumu milele, maandiko yanasema hivyo!.

Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha leo, mgeukie Kristo, injili tuliyobakiwa nayo sasa sio ya kubembelezwa, ni wewe mwenyewe uone hali halisi, umgeukie muumba wako.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

“Vya Kaisari mpeni kaisari”  ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.

Rudi nyumbani

Print this post

Wakanaani walikuwa ni watu gani?

Wakaanani walikuwa ni watu wanaoishi katika nchi ya Kaanani. Kumbuka Kaanani alikuwa ni mtu, ambaye tunamsoma katika Mwanzo 9:18, kuwa alikuwa ni mwana wa Hamu, ambaye aliuona utupi wa baba yake.

Mwanzo 9:18 “Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na HAMU ndiye BABA WA KANAANI”.

Wakanaani ndio watu waliokuwa wanamiliki sehemu kubwa ya Israeli, kabla wa nawa Israeli hawajaingia nchi hiyo, ndio maana nchi ya Israeli hapo kwanza ilikuwa inaitwa nchi ya Kaanani, kwasababu hao wakaanani, ndio walikuwa wameshikilia sehemu kubwa ya nchi hiyo, Zaidi ya mataifa mengine machache kama Wahiti, Wahivi na Wayebusi.

Wakanaani walitawala ardhi ile kuanzia Kusini mwa nchi ya Lebanoni, mpaka karibia na mipaka ya nchi ya Misri.

Wakaanani walikuwa ni watu waliokuwa wanaabudu miungu, hivyo desturi zao zilifarakana na sheria wa Mungu wa Israeli, kwani walikuwa ni wachawi, watu wanaobashiri, wanaojichora, wanaotazama nyakati za hatari, wanaowapitisha Watoto wao kwenye moto kwaajili ya sadaka kwa miungu yao. N.k.

Kwasababu ya machukizo hayo, ambayo pia yalichangiwa na laana Mungu aliyomlaani Hamu, kwa kosa la kuuona uchi wa Baba yake, ndipo Mungu akawaondoa katika nchi hiyo na kuwapa wana wa Yakobo (yaani wana wa Israeli).

Kumbukumbu 18:9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.

10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.

12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.

14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo”.

Mbali na kwamba Wakaanani walikuwa ni watu WASIOFAA, lakini pia biblia inarekodi kuwa walikuwa ni watu Hodari, wakubwa kimwili na walioendelea sana. Ndio maana utaona Musa alipowatuma watu wakaipeleleze ile nchi yao, wale wapelelezi walikuja na ripoti za kuogopesha, kwani walijiona nafsi zao kama mapanzi mbele ya hao Wakanaani.

Hesabu 13:32 “Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.

33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi”.

Jamii ya Wakaanani sasahivi haipo tena, imepotea (Bwana ndiye aliyeitowesha).

Ni nini tunachoweza kujifunza kwa Wakaanani?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kwamba mafanikio ya mtu au Taifa, sio kigezo cha kukubaliwa na Mungu.

Wakanaani walikuwa wameendelea kuliko Israeli, walikuwa na sayansi kubwa kuliko Israeli na mataifa mengi, lakini Mungu aliwaondoa katika ile nchi na kuwatowesha kabisa kwasababu walikuwa wanafanya machukizo.

Hiyo ni kutukumbusha na sisi watu wa siku za mwisho kuwa, Mafanikio ya kimwili sio kigezo cha kukubaliwa na Mungu. Leo hii kipimo cha kwanza cha mtu aliyebarikiwa na Mungu ni kiwango cha mali alicho nacho, na fedha alizonazo.. lakini Si utakatifu tena..

Bwana Yesu alisema..

Marko 8:36 “KWA KUWA ITAMFAIDIA MTU NINI KUUPATA ULIMWENGU WOTE, AKIPATA HASARA YA NAFSI YAKE?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?

38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Na Zaidi sana Neno la Mungu linatuhimiza tuutafute Utakatifu kwa gharama zote, kwasababu pasipo huo hatutamwona Mungu (Waebrania 12:14), Na utakatifu tunaupata kwa kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Wahiti ni watu gani?

Moabu ni nchi gani kwasasa?

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

Rudi nyumbani

Print this post

Je vazi alilovikwa Bwana Yesu lilikuwa la Zambarau au Jekundu?

Swali: Tunasoma katika Marko 15:17,na Yohana 19:2  kuwa Bwana alivikwa Vazi la rangi ya Zambarau, lakini tukirudi kwenye Mathayo 27:28 tunaona ni vazi Jekundu, Sasa vazi lipi ni sahihi hapo?.

Jibu: Tusome,

Marko 15:16 “Nao askari wakamchukua ndani ya behewa, ndiyo Praitorio (yaani, nyumba ya uliwali), wakakusanya pamoja kikosi kizima.

17 Wakamvika VAZI LA RANGI YA ZAMBARAU, wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani;

18 wakaanza kumsalimu, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”.

Tusome tena..

Mathayo 27:27 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28 WAKAMVUA NGUO, WAKAMVIKA VAZI JEKUNDU.

29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”

Sasa kwa mistari hii miwili ni rahisi kusema kuwa biblia inajichangaya.. lakini biblia kamwe haijichanganyi, kinachojichanganya ni fahamu zetu.

Sasa tukirudi kwenye hiyo mistari ni kwamba zamani mavazi waliyokuwa wanavaa watu wenye heshima, au mamlaka Fulani, yalikuwa ni ya rangi ya zambarau iliyochanganyikana na rangi nyekundu. Sehemu kubwa ilikuwa ni rangi ya Zambarau na sehemu ndogo ni nyekundu. Hivyo mtu atakayelitaja kama vazi la Zambarau au kama vazi jekundu, anakuwa hajakosea..

Kwa mfano unaweza kusoma…

Ufunuo 17:4 “Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, NA NYEKUNDU, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.

Pia unaweza kusoma Ufunuo 18:16, Luka 16:19.

Kwahiyo Marko na Mathayo…wote walikuwa sahihi..isipokuwa kila mmoja kaelezea rangi, iliyokuja ya kwanza kichwani mwake.

Lakini Zaidi sana tunachoweza kujiuliza ni kwanini Bwana wamvike vazi lile la Zambarau na nyekundu? Na si la rangi nyingine?.. Jibu ni kama tulivyojifunza hapo juu kuwa mavazi hayo yalivaliwa na watu wenye cheo au wafalme au mamalkia.. Kwahiyo walipomvika vazi hilo lengo lake ni ili wamdhihaki “mfalme wa wayahudi”..kwahiyo ni vazi kama la kumdhihaki ndio maana wakamvika na taji ya miiba, kwasababu watu wanaovaa mavazi kama hayo wanakuwa pia na taji za utukufu!.. Lakini Bwana Yesu walimvika Taji ya miiba.

Sasa kwa urefu juu ya Taji ya miiba, unaweza kufungua hapa >> Taji ya Miiba.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

AKAJIFUNGA VAZI LAKE, AKAJITUPA BAHARINI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Wahiti ni watu gani?

Wahiti ni watu gani, na wa Taifa gani kwa sasa?

Biblia haijaeleza kwa urefu, Habari ya Wahiti, lakini kulingana na maandiko, walikuwa ni watu Hodari na waliotawala sehemu ya nchi ya Israeli, katika upande wa kaskazini. Kumbuka Nchi ya Israeli hapo kwanza ilikuwa inakaliwa na watu wa mataifa, ambao ndio hao Wahiti, wengine ni Wayebusi, Wahivi, waperizi na Wakaanani.

Kulingana na historia, Wahiti, hawakumiliki tu sehemu ya nchi ya Israeli, enzi za zamani, bali pia historia inaonyesha walimiliki sehemu ya nchi ya Syria kwa sasa na mashariki mwa nchi ya Uturuki, ambayo zamani ilijulikana kama Asia ndogo.

Wahiti hawakuwa watu waliomwabudu Mungu wa Israeli, bali walikuwa wanaabudu miungu na walikuwa wanaishi katika desturi za kipagani; Na katika biblia kipindi cha Ibrahimu na Isaka, Wahiti walikuwepo tayari katika nchi ile, wanamiliki sehemu ya ardhi, ndio maana utaona Esau mwana wa Isaka alikwenda kujitwalia wake kutoka kwa hawa Wahiti.

Mwanzo 26:34 “Esau alipokuwa mwenye miaka arobaini, akamwoa Yudithi, binti Beeri, MHITI, na Basemathi, binti Eloni, Mhiti.

35 Roho zao Isaka na Rebeka zikajaa uchungu kwa ajili yao”.

Wahiti Pamoja na kwamba waliondolewa katika nchi ya Israeli, wakati waisraeli wanaingia katika nchi hiyo ya ahadi, lakini bado waliendelea kuwepo na kumiliki sehemu nyingine za dunia, na ndio maana utaona wakitajwa hata baada ya wana wa Israeli kurudi kutoka katika uhamisho wa Babeli.

Ezra 9:1 “Na mambo hayo yalipokwisha kutendeka, wakuu wakanikaribia, wakisema, Watu wa Israeli, na makuhani, na Walawi, hawakujitenga na watu wa nchi hizi, wamefanya sawasawa na machukizo yao, yaani, ya Wakanaani, na WAHITI, na Waperizi, na Wayebusi, na Waamoni, na Wamoabi, na Wamisri, na Waamori.

2 Maana wametwaa binti zao kuwa wake zao, na wake za watoto wao; basi mbegu takatifu wamejichanganya na watu wa nchi hizi; naam, mkono wa wakuu na mashehe umetangulia katika kosa hili”.

Wahiti waliondolewa katika nchi ya ahadi na Mungu, kwasababu ya matendo yao ya kipagani, ambayo yalikuwa kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kumbukumbu 9:4 “Usiseme moyoni mwako, Bwana, Mungu wako, atakapokwisha kuwasukumia nje mbele yako, ukasema, Ni kwa haki yangu alivyonitia Bwana niimiliki nchi hii; KWANI NI KWA AJILI YA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO.

5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; LAKINI NI KWA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA, MUNGU WAKO, AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo”.

Wahiti, waliendelea kuwepo miaka mingi, lakini nyakati za agano jipya hatuwaoni wakitajwa tena, ni wazi kuwa jamii hiyo ya watu ilipotea kabisa, mpaka leo hakuna jamii ya Wahiti duniani, kama vile walivyo Israeli.

Ikifunua kuwa wote wasiomcha Mungu, watapotea lakini wote wamtumainio Bwana watadumu milele.

Zaburi 125:5 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele”.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Rudi nyumbani

Print this post

 SWALI: Ni njia gani itumike kuwaongoza mabubu sala ya toba?

JIBU: Tukumbuke kuwa “sala ya Toba” sio wokovu, Sala ya toba ni njia mojawapo, inayotumiwa kuukaribisha wokovu ndani ya mtu, lakini sala kama sala yenyewe sio wokovu, Ikiwa na maana zipo njia nyingine, Na ndio maana huwezi kuona mahali popote mitume waliwaambia watu wafuatisha sala fulani, kwamba kwa hiyo ndio wataokoka..Huwezi kuona.

Wokovu unatoka moyoni. Pale mtu anapojitambua kuwa ni mwenye dhambi, na hivyo anahitaji kukombolewa kutoka katika mauti na Yesu Kristo, kitendo kinachompelekea kuyasalimisha maisha yake yote kwa Bwana Yesu ayaongoze, na kuachana na mambo ya ulimwengu, Huo ndio wokovu.

Sasa jambo kama hili likishatokea ndani ya mtu, udhihirisho wa nje ndio unafuata, ambao mojawapo ndio kukiri kwa kinywa chako, na cha pili ni Matendo yako.

Kutimiza lile andiko la Warumi 10:9

“Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka”.

Sasa mabubu, hawajajaliwa kuongea, hawawezi kumkiri Kristo kwa vinywa vyao..Lakini wanaweza kuonyesha kuwa wamemwanini Kristo kwa matendo yao. Wakifanya hivyo tayari huo ni wokovu tosha, kutoka kwa Bwana.. Hivyo mtu kama huyu ikiwa tayari ameshamwani Bwana muhimize tu, aanze kuenenda sawasawa na kuamini kwake.

Tutakumbuka kisa kile cha Yule mwanamke ambaye Bwana Yesu alisema alikuwa na dhambi nyingi, jinsi alivyomwendea na kulia sana miguuni pake, kudhihirisha majuto ya makosa yake, kisha kumpangusa kwa nywele zake, Utaona pale Bwana Yesu hakuzungumza naye maneno yoyote, kwamba njoo nikuongoze sala ya toba, au sema maneno haya au yale, hapana isipokuwa alipoona tu moyo wake wa toba ulivyomaanisha kwelikweli alimwambia.. “Mwanamke umesamehewa dhambi zako”

Luka 7:36-48

 “36 Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.

37 Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.

38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.

39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi…..

44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake

45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.

46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.

47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.

48 Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.

Hii kuonyesha kwamba, pale unaoonyesha geuko la kweli moyoni mwako, kabla hata hujazungumza chochote tayari umeshasamehewa.

Ndivyo ilivyo kwa mabubu, haijalishi hawataweza kukiri sala yoyote kwa vinywa vyao, lakini ikiwa moyoni mwao wameonyesha mabadiliko, hicho ndicho Mungu anachokitaka. Imekuwa desturi leo hii kuona kundi kubwa la watu wanasema wameongozwa sala ya toba na kumkiri Yesu , lakini ukitazama matendo yao hayaendani na walichokikiri. Huo ni unafki ambao unamchukiza Bwana sana.

Mathayo 15:7 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,

8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.

Bwana anataka tumfuata na tumwabudu katika Roho na kweli. Na sio katika maneno matupu. Ikiwa mtu asiweza kuongea, amesimama katika wokovu, huyo mtu ni wa thamani sana mbele za Mungu

Swali ni je wewe, uliyemkiri Bwana, unayemsifu, unayemuhubiri, unayemtangaza. Je! Ni kweli kitokacho mdomoni mwako, kimeambatana na badiliko la ndani?

Majibu tunayo.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate. Ina maana gani?

Kuongozwa sala ya toba.

Dusumali ni nini katika biblia?

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Jibu: Kuna tofauti ya “Utasi” na “Utasa”.. Utasa ni hali ya mtu kutokuwa na uwezo wa kuzaa, lakini Utasi ni tatizo la udhaifu wa ulimi (yaani ulimi kuwa mzito), Mtu mwenye ugonjwa huu anakuwa hawezi kuongea vizuri, anakuwa hawezi kutamka maneno vizuri..Na wengi wenye tatizo hili wanakuwa wanazaliwa nalo.

Katika biblia tunaona ugonjwa huu ukitajwa mara moja tu!, kwa mtu mmoja ambaye Bwana Yesu..

Marko 7:32 “Wakamletea kiziwi, NAYE NI MWENYE UTASI, wakamsihi amwekee mikono.

33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,

34 akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.

35 Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, AKASEMA VIZURI”.

Maandiko yanasema Bwana Yesu ni Yule Yule, alimponya mtu huyo, hata leo bado anaponya!, na haponyi Utasi tu peke yake, bali anaponya kila shida.. Na uponyaji mkuu kuliko yote ambao Bwana anautoa ni uponyaji wa Roho zetu. Huo ndio muujiza mkubwa ambao Bwana anaweza kutufanyia endapo tukimwamini.

Anatuponya roho zetu na mauti ya kiroho, na anatuokoa na ghadhabu ya Mungu, iliyo karibuni kumwangwa kwa ulimwenguni kwa watenda dhambi.

Je umepokea uponyaji huo leo?.. kama bado Tubu, mwamini Yesu na ukabatizwe katika ubatizo sahihi na kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Rudi nyumbani

Print this post

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Jina la Bwana wetu, Yesu Kristo libarikiwe.. karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu.

Bwana Yesu alisema maneno haya katika Luka maneno haya..

Luka 16:8  “…..kwa kuwa wana wa ulimwengu huu katika kizazi chao wenyewe HUWA NA BUSARA KULIKO WANA WA NURU”.

Maana yake.. “Watu wa ulimwengu huu, wasiomjua Mungu, au walio mkataa Mungu, katika mambo yao wanayoyafanya yasiyo ya kiMungu, basi huyafanya kwa busara ya hali ya juu, Zaidi hata ya watu wanaokiri kumjua Mungu”.

Na hiyo ni kweli kabisa.. Huoni leo watu wa kidunia walivyo makini na kazi zao na shughuli zao?.. Utaona wanawahi kuamka mapema na kwenda kwenye shughuli zao hata kama ni haramu..(kamwe hawachelewi kazini).. Lakini leo hii, wana wa Mungu utaona kanisani wanachelewa na kuwa watu wa kutoa udhuru sana.

Lakini leo nataka tulitafakari jambo lingine, ambalo linafanywa na watu wa ulimwengu huu,  ambalo si la kiMungu lakini lina busara ndani yake!..(Na kupitia hilo, basi sisi tupate hekima).. kwasababu biblia imeruhusu tuwatazame watu na viumbe vya ulimwengu, jinsi vinavyoenenda katika mambo yao, na kisha tupate hekima na mafunzo kutoka kwao..

Kwamfano utaona hekima inatufundisha tuwatazame chungu, kisha tujifunze kuacha uvivu kutoka kwao…

Mithali 6:6 “Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima”.

Chungu ni “SIAFU”.. Jinsi gani Siafu, wanavyofanya kazi usiku na mchana na kwa ushirikiano, (kamwe huwezi kukuta siafu kapumzika, muda wote yupo bize na mambo yake).. Vile vile na sisi wakristo hatupaswi kuwa na kipindi chochote cha kupumzika pindi, tuwapo katika mambano ya kiimani, hatuna budi kuendelea kuomba, kukesha, kuhubiri na kuwa watakatifu, hakuna kuchukua likizo, wala kupumzika katika mambo hayo, mpaka mwisho wa safari yetu ya hapa duniani. Mapumziko yetu yapo mbinguni, kule ndio kuna pumziko la kweli.

Lakini leo, tulitafakari jambo lingine ambalo linaendelea katika Taifa moja la Afrika mashariki, na Taifa hilo ni Tanzania, na tukio lenyewe ni “MBIO ZA MWENGE WA UHURU”.

Je! Umewahi kusikia au kufuatilia, juu ya Mwenge wa Uhuru wa Tanzania?. Kama bado basi jifunze leo hapa..

Mwenge ni Taa, inayotumia utambi wenye mafuta, kama vile kibatari.. tofauti ya kibatari na mwenge ni kwamba mwenge ni mkubwa kuliko kibatari, hivyo unamulika sehemu kubwa zaidi..Na mwenge kazi yake ni moja tu!, nayo ni kutoa Nuru!

Taifa la Tanganyika baada ya kupata Uhuru, Lilitengeneza Mwenge mdogo na kuuwasha na kwenda kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro..(Ambapo ndio sehemu iliyoinuka kuliko zote katika Taifa hilo, na hata katika Afrika yote kwa ujumla).

Sawasawa na maneno ya Bwana Yesu aliyosema katika Luka..

Luka 11:33 “Hakuna mtu awashaye taa na kuiweka mahali palipositirika, au chini ya pishi; bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuuona mwanga”.

Na ndivyo, Taifa hilo lilivyoupandisha huo Mwenge, mahali pa juu kuliko pote.. Sasa sijui ni roho gani iliyowasukuma kufanya tendo hilo..

Lakini Tafsiri ya Mwenge huo na sababu ya kuuwasha na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro, kulingana na waasisi wa Tanganyika, ilikuwa ni hii…

“Mwenge wa uhuru  ni Kiiashiria kinachoangaza nchi, lengo lake ni kuangaza Matumaini palipo na kukata tamaa, kuangaza Upendo palipo na Uadui, na kuhubiri heshima palipo na Chuki, na kutangaza amani katika nchi ya Tanganyika na hata nje ya mipaka ya nchi”.

Na zaidi sana, kifaa hicho hakikuishia kukaa tu juu ya mlima Kilimanjaro, bali kilishushwa na kufanywa kuzunguka nchi nzima, mkoa kwa mkoa, wiliaya kwa wilaya, kata kwa kata, na kitongoji kwa kitongoji.

Jambo ambalo lina hekima  ndani yake!.. “kibatari kilichopo juu ya Meza hakiwezi kumulika, sarafu iliyopotea chini ya uvungu wa kitanda..” ili kuipata sarafu iliyopo chini ya kitanda, au nyuma ya kabati, mtu hana budi kukitoa kibatari mezani, na kukishusha chini, aweze kumulika, na kama sarafu haipo chini ya uvungu, basi kibatari kile kitazungushwa katika nyumba nzima..mpaka ipatikane..

Na Mwenge wa Uhuru wa Tanganyika ni hivyo hivyo.. unazungushwa katika Taifa zima, kuhubiri mambo hayo matatu.. (Upendo, Tumaini, amani na Heshima).

Swali la kujiuliza, Je!, Mwenge wa Uhuru umesaidia kuleta Amani, upendo na Heshima katika Taifa hilo?.. Jibu ni ndio!.. Kwasababu WALIKUWA NA HEKIMA KATIKA MAMBO YAO, Mungu akawajalia adhimio lao!. Huoni leo Taifa la Tanganyika lina Amani?..huoni jinsi makabila mengi yanavyakaa Pamoja kwa kuheshimiana??..ingawa kuna makabila Zaidi ya 100, lakini yote hayo yanakaa kwa Umoja.

Kwa kuona umuhimu wa Amani, Upendo na Heshima, na kwa kutumia kiashiria hicho cha Mwenge, Mungu amelikirimia Taifa hilo, Mambo hayo; Amani, Upendo na Heshima. Na tangu Mwenge huo uwashwe juu ya mlima Kilimanjaro, mpaka leo haujazimwa, na ni moja ya alama ya nembo ya Taifa.

Lakini je!.. Na Sisi wakristo Mwenge wetu wa Uhuru uko wapi? (tumeuweka wapi)?..Upo unawaka au umeshazima kitambo?

Bwana alipokufa pale Kalvari, tulipata uhuru, kutoka dhambini..Na Bwana Yesu alisema matendo yetu ndiyo Mienge ya Uhuru wetu tulioupokea, kwamba hatuna budi kuyafanya yaangaze mbele za Watu..

Mathayo 5:14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Je Mwenge wako unaangaza?..Na kama ndio je unaangaza ukiwa wapi??.. Juu kabisa au chini peke yake!..Mwenge wa watu wa mataifa uliwekwa juu kabisa katika mlima mrefu kuliko yote, na vile vile ulikuwa ukizunguka zunguka kutafuta mahali uovu ulipojificha!…

Je wewe Mwenge wako upo wapi?..

Matendo yako ni taa kwa ulimwengu??..au ni vuguvugu, leo upo disko, kesho upo kanisani, leo unakunywa pombe kesho unaimba tenzi??.. leo unaimba kwaya kesho unazini.

Unadhani ni kwa faida ya nani?. Rejea leo kwa Bwana, na amua kumfuata kwa moyo mmoja, usiwe mtu mwenye moyo uliyegawanyika, kwasababu Bwana alisema atawatapika watu wa namna hiyo.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Rudi nyumbani

Print this post

WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA

Waebrania 10:25 “WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”.

Kukusanyika kunakozungumziwa hapo, ni kukusanyika na wapendwa wengine kanisani.

Mbinu ya kwanza shetani anayoitumia kuwaangusha watu, ni kuwatoa katika kundi!..(kuwatenga na kundi), atanyanyua kisa tu , ambacho kitamfanya huyo mtu akereke na aache kwenda kanisani. Na yule mtu kwa kudhani kuwa “kujitenga na wenzake, ndio atakuwa salama, kumbe ndio kajimaliza”.

Vifuatavyo ni visa vichache ambavyo shetani anawahubiria watu, lengo ni kuwatoa ndani ya kundi.

 1. IBADA INACHUKUA MUDA MREFU.

Ukishaanza kuona au kusikia hii sauti ndani yako inayokuambia kuwa “ibada ndefu sana”..basi jua ni shetani anakuhubiria kutaka kukutoa katika kundi, kwasababu anaona kuna hasara unataka kumletea katika ufalme wake.

Siku zote fahamu kuwa siku ya Bwana, ni amri kuwa yote iwe takatifu.. Ni heri ukose ibada za katikati ya wiki, lakini ya Siku ya Jumapili, siku hiyo ifanye takatifu yote kwa Bwana!..ukijiwekea hilo akilini, hutababaishwa na masauti ya shetani yanayokuambia ibada ni ndefu sana.

 2. KUSIKIA HABARI ZA WATU WENGINE.

Wengi shetani anawatoa katika makusanyiko, kuwasikilizisha kwanza habari mbaya za watu wengine wanaoshiriki nao katika kusanyiko hilo, au viongozi wa kanisa hilo. Mara watasikia mshirika Fulani kagombana na mwingine, au Mchungaji haelewani na mtu Fulani, au kafanya hiki au kile..

Na kwasababu hiyo basi wanaamua kuacha kwenda kanisani, kukusanyika kama ilivyokuwa kawaida yao, na kuishia kukaa tu nyumbani…wakidhani kuwa nyumbani ndio wapo salama, pasipo kujua kuwa ni shetani ndio kawatoa kule.

Siku zote fahamu kuwa hakuna mahali patakosa kasoro…kasoro kila mahali zipo, na zitaendelea kuwepo, hivyo kazi mojawapo ya wewe kukuweka pale ni ili uwe sababu ya kuziondoa hizo, kwa kuomba na kuonya, na sio kwa kukimbia na kuacha…

 3. KUKWAZWA NA MTU/BAADHI YA WATU KATIKA KANISA.

Hii ni sababu nyingine shetani anayoitumia kuwatenga watu wengi na kundi!.. utaona mtu kaaambiwa au kafanyiwa jambo moja tu, ambalo ameliona kuwa sio zuri! Lakini utaona hilo hilo analitumia kama sababu ya kutokanyaga tena kanisani.. Lakini akila wali na kukuta kipande kidogo cha jiwe, hamwagi chakula chote!. Lakini kwa Mungu anakuwa ni mtu wa kususa vitu vidogo..

Kumbuka ijapokuwa tunaitwa wakristo, bado hatutakosa kasoro kabisa, mchungaji hawezi kuwa mkamilifu saa zote, muumini mwanzako hawezi kuwa Malaika.. hivyo viwango unavyovitaka uvione hutaviona katika kanisa lolote lile duniani, unachopaswa kufanya ni kuwa mvumilivu, na kuendelea kudumu pale ukiomba na kupambana kurekebisha hizo kasoro..ili hatimaye zipotee kabisa ndani ya kanisa na si kuondoka..

Ukiondoka na kuamua kubaki nyumbani tu!, jua ni shetani ndio kakutoa katika kundi, kwasababu ameona utakuja kumsumbua huko mbeleni.

 4. HOFU YA MATOLEO.

Ni kweli kuwa katika siku hizi za mwisho, watatokea watu wa kupenda fedha hata katika madhabahu za Bwana, lakini usiitumie hiyo kama sababu ya wewe kuacha kwenda kanisani..

Kwasababu hata kama ukihimizwa kutoa, kama kweli na wewe unampenda Bwana huwezi kuchukia.. kwasababu unajua kabisa kwamba unamtolea Mungu, na si mwanadamu.. na hivyo thawabu zako zinazidi kuongezeka tu mbinguni.

Ukisikiliza hubiri la shetani linalokuambia usiende kanisani kwasababu utaambiwa utoe hela, afadhali ukae nyumbani tu!, jua kuwa upo katika hatari kubwa sana..

Kuna faida nyingi za kukusanyika Pamoja, lakini leo tutazitama faida 2 tu!

 1. UNAKUWA IMARA KATIKA IMANI.

Unaweza kusema nikiwa peke yangu, ninaweza kusimama… lakini nataka nikuambia..mtu anayelala hajui dakika aliyoingia usingizini, vile vile mtu aliye pekee yake siku za kwanza atajiona nafuu lakini ndivyo anavyozidi kupoa kidogo kidogo na mwisho kupotea kabisa..

Hebu soma maneno haya…

Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.

10 KWA MAANA WAKIANGUKA, MMOJA WAO ATAMWINUA MWENZAKE; LAKINI OLE WAKE ALIYE PEKE YAKE AANGUKAPO, WALA HANA MWINGINE WA KUMWINUA!

11Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?

12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi”.

Hivyo usiache kamwe kukusanyika Pamoja na wengine, kwasababu kuna vitu ambavyo ukiwa peke yako inakuwa ni ngumu kuvipata, mfano wa vitu hivyo ni Faraja, ari, motisha, hamasa,.. Na vile vile kuna vitu ambavyo ukiwa peke yako ni ngumu kuvifanya kikamilifu.. Mfano wa vitu hivyo ni maombi!.. ukiwa mwenyewe nyumbani ni ngumu kukesha kuomba.. lakini ukiwa kwenye mkesha mahali ambapo watu wote wanaomba.. ukitazama kushoto Jirani anaomba, ukitazama kulia mwingine anaomba ni lazima na wewe utapata nguvu ya kuomba.. lakini nyumbani peke yako ni ngumu.

Hiyo ni hekima ya kiMungu, hivyo usijione unayo hekima kuliko Mungu..

Ndio maana utaona ni kwanini Bwana Yesu alikuwa anawatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri, wawili wawili.. na si mmoja mmoja, ni kwasababu alikuwa anajua madhara ya mtu kwenda peke yake.

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu”

 2. UNAPATA BARAKA.

Kuna baraka mara dufu, ukiwa katika kanisa kuliko ukiwa nyumbani

Zipo baraka ambazo Mungu anaziachia kwa Watoto wake kwa umoja.. na hizo zinaachiliwa kanisani…Na baraka hizo ni za kiroho na kimwili..

Mathayo 18:18 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.

19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.

20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”.

Hapo Bwana Yesu hajasema.. “akikusanyika mmoja nyumbani kwake, atakuwa katikati yake”..sasa sio kwamba “kila unapokuwa peke yako Bwana anakuwa hayupo nawe” ..yupo na wewe lakini, si kama utakavyokuwa na wengine. Kwasababu Bwana siku zote anahubiri umoja na anapendezwa na umoja.. Lakini ukijitenga Bwana hawezi kupendezwa na wewe.

Mithal 18:1 “Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema”.

Hivyo mkatae leo shetani, na anza kwenda kukusanyika na wengine, hiyo ni kwa faida yako wewe, kumbuka siku zote kuwa shetani anafananisha na simba atafutaye mawindo..na anawawinda watu walioanza safari ya wokovu watu kwa njia nyingi, na ya kwanza ndio hiyo.. ya kuwatenda na kundi.

1 Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

KUOTA NYOKA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

SWALI 1: Je! Shetani anaweza kuumba, kama Mungu? Kama sio Mbona kipindi cha Farao, tunaona wale waganga waliweza kuleta vyura na nyoka, kama alivyofanya Musa. Je wale vyura aliwaumbaje, uhai alitolea wapi kama sio Mungu?


JIBU:  Bwana Yesu anasema; Shetani ni mwongo, na sio tu mwongo, bali ni Baba wa huo;

Yohana 8:44 “..wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.

Maana yake ni kwamba ufalme wake ameujenga juu ya misingi ya uongo. Alitumia uongo kumnyang’anya Adamu nafasi yake ya umiliki. Vivyo hivyo hadi sasa anatumia uongo kuwadanganya watu wasiutambue ukweli  wote kuhusu yeye.

Anataka kuwadanganya watu, wadhani kuwa yeye ana nguvu za kuweza kukaribiana hata na Mungu au anao uwezo wa kuumba kama Mungu. Lakini ukweli ni kwamba, shetani au kiumbe chochote kile hakiwezi kuumba hata sisimizi. Uwezo huo anao Mungu tu, peke yake.

Kama ni hivyo, ni nini alikifanya kipindi cha Farao?

Alichokifanya kipindi cha Farao, si kingine zaidi ya uongo. Kutokana na maarifa aliyokuwa nayo kipindi kile ambayo anayo hadi sasa, shetani anaweza kubaliki kitu fulani kionekane ni kitu kingine mbele tu ya macho ya watu, au hata kujibadilisha yeye, aonekane ni malaika wa kweli, kumbe ndani ni yeye Yule yule shetani..Biblia inatuambia uwezo huo anao..

2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.

Hivyo tabia hiyo anayo.. kipindi kile hakuumba nyoka wenye pumzi ya uhai, kama nyoka wengine, au vyura wapya..bali alifanya kazi yake hiyo ya kubadilisha maumbile ya vitu mbele ya macho ya watu.. Kwa lugha ya sasa wanaita “kiini-macho” au “mazingaumbwe”, na ndio maana nyoka wa Musa, hakuwaona wale kama ni nyoka wenzake, wanaohitaji mapambano, bali aliona kama ni chakula tu, akala.

Ni sawa na mwanadamu ambaye amefikia maarifa ya kutoa ‘photocopy’ kitu orijino, Shetani naye hapo amepafikia.Lakini hana uwezo wa kutengeneza orijino.

Kama shetani angekuwa na uwezo wa kuumba chura, hata mbwa angeweza, hata ng’ombe pia angeweza, na  sokwe nao. Na matokeo yake dunia, ingejawa na vitu vilivyoumbwa na Mungu, na vilivyoumbwa na shetani, leo hii tungesikia wale nguruwe si wa Mungu bali ni wa shetani, usiwaguse. Lakini hadi sasa hakuna rekodi ya kitu chochote kilichoumbwa na shetani, zaidi sana rekodi aliyonayo ni kuumba uovu na uasi duniani.

Pia tazama..

1 Jehanamu ni wapi?
2 Nini kinatokea baada ya kifo?
3 Freemason ni nini?
4 Siku ya unyakuo itakuwaje?
5 Upendo ni nini, je kuna aina ngapi za upendo?
6 Je! umepokea Kweli Roho Mtakatifu?
7 Mauti ya pili ni nini?
8 Faida za maombi
9 Jinsi ya kusoma biblia.
10 Je! kuna aina ngapi za malaika?

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Luka 24:39 “Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.

JIBU: Ni kweli sawasawa na maneno ya Bwana Yesu, hakuna jini au pepo, au kiumbe chochote cha rohoni, chenye mwili, na kikaweza kuishi hapa duniani kama sisi.. Hakuna.

Kumbuka, Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.

Maandiko hayo ni kutuonyesha kuwa, mapepo, hayana miili yao wenyewe ya kuishia hapa duniani, yanategemea watu,au wanyama,ili kutembea duniani, kama wakati ule yalivyomwomba Bwana yawaingie wale nguruwe. Lakini yenyewe kama yenyewe, hayawezi kusimama na kuwa kama wanadamu kutembea duniani.

Lakini Je! Wale wanaoshuhudia kwamba mapepo yanawatokewa, na pengine kuzuni nao, ni nini vile?

Mapepo yanaouwezo wa kujidhihirisha mbele ya mtu kwa taswira ya kitu fulani, aidha ya mtu, au kitu, kukutisha au kukufanya uogope,  (Mathayo 14:26), au kukutokea katika ndoto,au maono.. lakini zaidi ya hapo yasiweza,  kuendelea na kuchukua maumbile na kuwa kama mwanadamu mwingine na kuishi hapa duniani, kama vile kula, kunywa, kufanyabiashara, kuoa, au kuolewa n.k. huo uwezo hawana kwasababu hawana miili. Pepo haliwezi kuzaa na wewe.

Vinginevyo, shetani angeshajidhihirisha siku nyingi na kuwa mfalme wa dunia. Lakini mpaka sasa ni roho tu, na atabakia kuwa roho, mpaka atakapotupwa kwenye ziwa la moto na mapepo yake.

Lakini kumbuka ukiwa ni mtu wa kujishughulisha na mambo ya ushirikina, aidha wewe ni mganga, au mchawi, au ulishawahi kwenda huko, ukafanyiwa matambiko, au kufanyiwa mazindiko ya kipepo, au ukala vitu vyao, Huo nao ni mlango unaoongeza wigo mkubwa sana, wa shetani au mapepo yake, kujidhihirisha kwako, kwasababu umeingizwa katika mtandao wao wa kiroho, hivyo inakuwa rahisi sana kwao kujidhihirisha kwako, na pengine kuchukua umbile ya kitu chochote kukuletea madhara mwilini. Tofauti na mtu ambaye  yupo mbali na mambo hayo.

Hivyo dawa pekee, ya kumfukuza shetani na majini yake, yasikutokee tokee au yasikufuate fuate ni kumkabidhi Yesu maisha yako. Kwa kumaanisha kabisa kuacha maisha ya dhambi, na baada ya hapo, ukazingatia kusoma NENO..

Kwasababu kuokoka ni sehemu ya kwanza, ya kuwekwa huru.. Ili kuukamilisha uhuru wako ni lazima Neno la Mungu likae ndani yako kwa wingi ili uweze kumshinda kabisa kabisa shetani.

Biblia inasema.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana Yesu, alikuwa ni mtakatifu wa Mungu, ambaye hakutenda dhambi, lakini hilo halikumzuia shetani asimjie, na kuzungumza naye. Lakini utaona alimshinda kwa Neno la Mungu lililokuwa ndani yake, na si kitu kingine.

Vivyo hivyo na wewe, ikiwa tayari umeshaokoka, Jifunze sana Neno, ujue mamlaka, na haki uliyonayo katika Msalaba wa YESU KRISTO. Hiyo itakufanya usiishi maisha ya woga,wala wasiwasi wa nguvu zozote za giza, kwasababu utakuwa tayari umeshajua uwezo uliopewa jinsi ulivyo mkubwa kuliko wa ibilisi

Lakini ukiwa ni mkristo, mvivu, Neno husomi ujue kabisa shetani ataendelea kukusumbua tu, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani.

Hivyo zingatia hayo mambo mawili.

  1. Wokovu
  2. Neno

Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo, kumpa Yesu maisha yako, ili akusamehe na kukupa wokovu, na kuyafukuza maroho yote machafu yaliyokuvamia. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao hautakaa uujutie milele.

Hivyo fungua hapa, kwa mwongozo wa sala hiyo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Mjoli ni nani katika biblia?

Gombo ni nini?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

IJUE SIRI YA UTAUWA.

Maandiko yanasema..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU…”.

Utauwa, maana yake ni UUNGU!.. Hivyo maandiko yanaposema.. “Siri ya Utauwa ni kuu”..maana yake ni kwamba “Siri ya Uungu ni kuu (yaani ni pana sana na ya kipekee)”.

Na Uungu (Utauwa)..unaozungumziwa hapo ni “Uungu wa Mungu”. Maana yake yeye ni nani, yupoje, anaonekanaje, anatendaje kazi, n.k

Sasa Mtume Paulo, kwa neema za Mungu, alipewa kuijua sehemu ndogo ya Uungu wa Mungu..na pasipo mashaka yoyote ya ufunuo huo alioupokea, akaiandika hivi..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Hebu tuviangalie kwa ufupi, hivyo vipengele 6 vya siri hiyo ya Uungu wa Mungu, ambavyo Mtume Paulo alifunuliwa kwa uweza wa Roho.

 1. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI.

Sasa ni wakati gani Mungu alidhihirishwa katika Mwili?..bila shaka yoyote, ni kupitia Bwana Yesu Kristo.. kwahiyo kumbe Bwana Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili?.. Hakika hiyo ilikuwa ni siri ya kipekee.. Kumbe yule aliyekuwa anazungumza na akina Petro, alikuwa ni Mungu mwenyewe, kumbe yule aliyekuwa anaongea na mafarisayo alikuwa ni Mungu mwenyewe, kumbe yule aliyepandishwa msalabani alikuwa ni Mungu mwenyewe!.. Hiyo ilikuwa ni Siri kubwa sana.

Mtume Yohana naye aliiona siri hiyo kwa sehemu na kusema..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu…..

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

Umeona?, Tito naye aliiona hiyo siri kwa sehemu katika ..Tito 2:13 “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu” ..Na baadhi ya Mitume wa Bwana Yesu kama Tomaso, na  Manabii kama Isaya, walionyeshwa siri hiyo kwa sehemu. (Soma Yohana 20:28 na Isaya 9:6). Na zaidi sana Bwana mwenyewe, aliigusia siri hiyo katika Yohana 14:8-11.

 2. AKAJULIKANA KUWA NA HAKI KATIKA ROHO

Bila shaka hakuna mwingine aliyepata kibali, cha mambo ya rohoni kuliko Bwana Yesu, hakuna mtu aliyewahi kufanya miujiza mikubwa kuliko Bwana Yesu. Kwa mara ya kwanza pepo wameanza kutolewa kwa kukemewa na Bwana Yesu Kristo, Kwa mara ya kwanza wafu wanafufuliwa kwa kutamkiwa neno tu!, na idadi kubwa ya watu likuwa inaponywa kupitia jina lake..Hivyo katika roho hakuna mwingine aliyejulikana kuwa na Haki (yaani kupata kibali), kuliko Yesu.

 3. AKAONEKANA NA MALAIKA.

Ni wazi kuwa Malaika wanawaona watu wote, lakini hawawajui watu wote, Malaika wala shetani hawajui kilichopo ndani ya moyo wa wanadamu, siri hiyo ipo kwa Mungu tu!, na kwa mtu mwenyewe.

Vile vile Malaika hawajui sura ya mtu atakayezaliwa mwaka ujao..anayejua ni Mungu tu!.. Hivyo Malaika walikuwa hawamjua Masihi (ambaye ni Mungu katika mwili) atakuwaje kuwaje, na Zaidi sana walizijua sifa chache tu, lakini si zote..

Lakini siku ilipofika ya kuzaliwa kwake walimwona..na alipoishi na kuifanya kazi ya Mungu ndipo walimwelewa Zaidi.. Ndio likatimia hilo neno.. “akaonekana na Malaika”. Malaika wakamwona Mungu katika mwili.

 4. AKAHUBIRIWA KATIKA MATAIFA.

Ni nani mwingine aliyehubiriwa katika mataifa na anayehubiriwa sasa?.. bila shaka si mwingine Zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Marko 16:15 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe”.

 5. AKAAMINIWA KATIKA ULIMWENGU.

Yesu Kristo ndiye peke yake ndiye anayeongoza kwa kuaminiwa na watu wengi duniani kuliko mtu mwingine yoyote, dini karibia zote (za uongo na za ukweli) pamoja na shetani mwenyewe na mapepo yake wanaamini kuwa Yesu katumwa kutoka mbinguni. Dini hizo zinaweza zisimkiri wazi, lakini zinaamini kuwa Bwana Yesu katoka mbinguni.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Na zaidi sana siku ya Mwisho, kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri, kuwa Yesu Kristo ni Bwana.

Wafilipi 2:10 “ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

 6. AKACHUKULIWA JUU KATIKA UTUKUFU.

Yohana 3:13 “Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu”.

Kwa hoja hizi sita ni wazi kuwa Bwana Yesu ndiye siri ya Mungu, na ndiye Mungu mwenyewe aliyejidhihirisha katika mwili.

Sasa unaweza kuuliza kwanni Mtume Paulo auandike ufunuo huu kwetu, kwa uongozo wa Roho?.

Ni ili sisi tuzidi kuwa na Imani na Bwana Yesu, ili sisi tuzidi kumwamini, na kumtumainia?.. Je!, kwa kusikia kuwa Yesu ndiye Mungu, huoni inatuongezea Faraja sisi?, inatuongezea ujasiri na kuamini kuwa hakuna chochote kitakachoharibika, maadamu tunaye Mungu?..Hivyo Siri hiyo ni kwa faida yetu.

Lakini jukumu tulilonayo sisi, sio kusoma Habari hizi kama gazeti, bali kama Neno hai lenye kuleta mabadiliko ndani yetu.. Huu ni wakati wa kumwamini Bwana Yesu, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na vile vile kujitenga na dunia, na kukusanyika Pamoja na watakatifu wengine, huku tukiingoja ile ahadi tuliyoahidiwa ya mbingu mpya na nchi mpya.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?

MPINGA-KRISTO

AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU.

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Rudi nyumbani

Print this post