Category Archive Home

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Kisiwa cha Patmo kipo nchi ya Ugiriki kwa sasa…Kisiwa hicho kipo mashariki mwa Taifa la Ugiriki na magharibi mwa nchi ya Uturuki, kama vile Zanzibar ilivyo mshahariki mwa nchi ya Tanzania ndivyo kilivyo hichi kisiwa cha Patmo kwa Ugiriki.

Kisiwa hicho ndicho Mtume Yohana, ambaye alikuwa mwanafunzi wa Bwana Yesu, alifungwa.

Warumi walimkamata Yohana na kumtupa katika kisiwa hicho, kwa lengo la kumtesa kwa kosa la kumhubiri Yesu. (Kwa maelezo kwa njia ya sauti, fungua hapa chini)

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=EhBLp-8-vPw[/embedyt]

Lengo la kumtupa Yohana katika kisiwa hicho cha Patmo, sio tu afe, bali afe kwa mateso. Kwani kisiwa hicho hakikukaliwa na mtu yeyote wakati huo, kwasababu kilikuwa ni kisiwa ambacho hakistawi nafaka, wala miti na zaidi sana, kilisifika kuwa na nyoka wengi.

Kwahiyo yoyote aliyetupwa katika kisiwa hicho, ilikuwa ni lazima afe kama hatakuja kuokolewa huko.

Lakini tunasoma, Yohana alipelekwa kule, kwaajili ya ushuhuda wa Neno la Mungu, wakati Jeshi la Warumi linaona limempeleka kwaajili ya mateso, yeye Yohana alijiona amepelekwa kwaajili ya ushuhuda…Kwamba akashuhudie mambo atakayokwenda kufunuliwa au kuambiwa na Mungu huko.

Ufunuo 1:9 “Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu”

Hii ikifunua kuwa sio kila jaribu baya, lengo lake ni baya!. Yohana asingepelekwa Patmo, tusingekuwa na kitabu cha ufunuo, hali kadhalika Bwana Yesu asingepelekwa msalabani, tusingepata wokovu.

Kisiwa cha Patmo, sasahivi kinakaliwa na watu, kutokana na kuongeza kwa idada kubwa ya watu ulimwengu na yenye kuhitaji makazi..vile vile, kuongezeka kwa teknolojia ya mawasiliano, na usafiriwa wa haraka, umekifanya kisiwa hicho kiweze kukalika na watu leo.

Kisiwa cha Patmo, jina lake mpaka leo halijabadilika, kinaitwa hivyo hivyo Patmo, kama vile Yerusalemu jina lake lisivyobadilika siku zote.

Wakazi wa kisiwa cha Patmo kwasasa hawazidi 4,000 kulingana na sensa za Ugiriki.

Na kisiwa hicho, hakina miujiza yoyote ya kiroho, kwamba yeyote afikaye kule basi atapata ufunuo kama aliopata Yohana.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Kutakabari ni nini katika biblia?.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

KWANINI KRISTO AFE?

Rudi nyumbani

Print this post

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele, amina. Karibu tuyatafakari maneno yake, maadamu siku zenyewe zimekaribia kuisha.

Ukisoma vitabu vya injili utaona jambo la kushangaza sana kuhusu Bwana Yesu. Utaona kuna wakati alikuwa anatembea kwa wazi kabisa katikati ya wayahudi, utalithibitisha hilo katika maneno yake mwenyewe aliyomwambia kuhani mkuu  katika Yohana 18:20, kupindi kifupi kabla ya kusulubiwa, Lakini kuna wakati hakutembea kwa wazi hata kidogo, bali alikwenda mbali na makazi ya watu, karibu na jangwa, akakaa huko yeye peke yake Pamoja na wanafunzi wake tu.

Yohana 11:53 “Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.

54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake”.

Unaweza ukajiuliza kwanini Bwana Yesu aonyeshe tabia kama hii? Ili hali alikuwa na uwezo wa kuishi analivyopenda Bila wasiwasi wowote, kwasababu Baba yake alikuwa Pamoja naye kumpigania na kumshindania asiuliwe kabla ya wakati?

Hiyo ni kutuonyesha kuwa, Kristo, hana utawala wa mabavu, ukimkataa, atakwenda mbali na wewe, na hutamwona haijalishi utamtafuta vipi. Ni jambo ambalo linaendelea sasa hivi katika roho ulimwenguni. Bwana Yesu anaulilia ulimwengu, lakini ulimwengu ndio kwanza unaipinga injili yake, unataka kuiua kabisa isiwaokoe watu.

Tukiona hivi tujue kabisa  Bwana ameshakwenda mbali na watu wa ulimwengu huu, kujificha. Siku hizi kupokea wokovu wa kweli ni ngumu kuliko ilivyokuwa zamani, kwasababu Kristo hapatikani tena kwa uwazi. Na ndio maana, utaona watu wengi wanasema wameokoka, lakini huoni nguvu za wokovu ndani yao..Si jambo la kawaida!!

Bwana huwa anajificha..

Yohana 12:36 “Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru. Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone“.

Ukirudi katika maandiko, utaona tena, alipokuwa Galiliya, alipita katikati yao lakini hakutana mtu yeyote ajue kuwa yupo mjini, bali alipita kimya kimya, akawa anawafundisha wanafunzi wake tu.

Marko 9:30 “Wakatoka huko, wakapita katikati ya Galilaya; naye hakutaka mtu kujua.

31 Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akawaambia, …”.

Hata sasa, Yesu anachofanya ni kujidhihirisha kwa watu ambao ni wanafunzi wake tu, usipofanyika mwanafunzi wa Yesu siku hizi za mwisho ni ngumu kuushinda ulimwengu. Mwanafunzi kulingana na (Luka 14:33), ni mtu ambaye amejikana nafsi na kudhamiria kweli kweli kumfuata Yesu.

Ukiwa tutakuwa na wokovu wa midomoni tu, na kusema tumeokoka, Na huku Maisha yetu yapo mbali na Kristo, tusijidanganye, bado hatujakutana na Bwana Yesu. Bali tumemsikia tu kwamba yupo.

Ndugu yangu hizi ni siku za mwisho, Bwana yupo kweli duniani anaokoa watu..Lakini si wote, anawatembelea watu, bali walio wanafunzi kwelikweli. Kuiona miujiza ya Yesu, kusikia injili, kwenda kanisani hakukufanyi uwe umeshamwona Yesu..Hivyo tuitambue tabii hii pia ya Bwana Yesu ili tuepukane na kujificha kwake, kwasababu anafanya hivyo sasa katika roho.

Kama hujaokoka, au ulikuwa unaishi Maisha ya uvuguvugu, yaani Maisha nusu nusu kwa Mungu basi fanya uamuzi wa kumgeukia sasa kwa  moyo wako wote, huku umejikana nafsi yako. Na Bwana Yesu atajidhihirisha kwako. Na atakusaidia kuushinda ulimwengu na kuishi Maisha ya utakatifu.

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Kigao ni nini? Na Je kinafunua nini kwa agano jipya?

Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

SWALI: Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume? Kulingana na (Warumi 16:1)

Warumi 16:1

16:1 “Namkabidhi kwenu Fibi, ndugu yetu, aliye mhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea;

2 kwamba mmpokee katika Bwana, kama iwapasavyo watakatifu; mkamsaidie katika neno lo lote atakalohitaji kwenu; kwa sababu yeye naye amekuwa msaidizi wa watu wengi, akanisaidia mimi pia”.


JIBU: Fibi hakuwa askofu wa makanisa, wala maandiko hayasemi hivyo, bali alikuwa ni “Mhudumu”..Yaani alikuwa akilihudumia kanisa la Kristo lililokuwa Kenkrea. Ni mwanamke aliyekuwa akilijali sana kanisa kwa kuwasaidia watu wengi, ikiwemo na mtume Paulo pia. Pengine kwa mali zake, kama walivyofanya wakina Yoana na Susana, waliomuhudumia Bwana kwa mali zako (Luka 8:3), au alivyokuwa Martha na Miriamu jinsi walivyompenda Bwana na kujitaabisha kwa ajili yake..

Au kama alivyokuwa Dorkasi, ambaye, kanisa zima lililokuwa Yafa lilimshuhudia, jinsi alivyotoa sadaka nyingi na kuwashonea watakatifu mavazi. Ndivyo ilivyokuwa pia kwa huyu mwanamke ambaye aliitwa Fibi. Pengine alikuwa anawakaribisha watakatifu na kuwapa makao nyumbani kwake, au alikuwa anachapisha injili za mitume na kuyasambazia makanisa yaliyokuwa Kenkrea.

Kwa ufupi ni kwamba Fibi likuwa ni muhudumu kweli kweli kwa Bwana, kiasi cha kuwafanya mitume wampe heshima ya kipekee katika kanisa.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa yeye naye alikuwa ni Askofu (Mwangalizi), wa makanisa kama mitume. Hapana andiko limeweka wazi kabisa kuwa mwanamke hana uongozi wowote katika kanisa. Ni kinyume na utaratibu wa Mungu.

1Timotheo 2:11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.

13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.

14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa”.

Lakini tunajifunza nini kwa Fibi?

Hii ni kuonesha jinsi gani mwanamke anaweza kumtumikia Bwana katika nafasi yake, na akawa na heshima kubwa katika kanisa la Kristo, mfano wa Fibi. Ni vizuri wewe kama mwanamke uifahamu nafasi yako, katika mwili wa Kristo, kisha simama katika hiyo, watazame kwanza wanawake wenzako katika biblia jinsi walivyoenenda, na jinsi walivyokuwa wanamtumikia Mungu na wewe waige, kabla hujakwenda kuwatazama kwanza mitume wanaume.

Hiyo ni muhimu sana kufahamu hilo, usije ukawa unapiga mbio bure, halafu baadaye unapokea thawabu isiyolingana na juhudi yako.

Ikiwa wewe ni mwanamke na utapenda kupata mafundisho ya namna hiyo yanayohusiana na huduma za wanawake katika kanisa, basi nitafute inbox kwa namba hizi +255693036618, nikutumie mafundisho hayo, au fungua link hii utakutana nayo, moja kwa moja >>>  https://wingulamashahidi.org/2021/07/21/masomo-maalumu-kwa-wanawake/

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

MAMA UNALILIA NINI?

Unyenyekevu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

KABILA LA BENYAMINI.

Jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu, Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia..

Katika wana wa Yakobo, aliyekuwa mdogo kiumri kuliko wote alikuwa ni Benyamini, ambaye alikuwa ni mdogo wake Yusufu. Huyu Benyamini ndiye mtoto pekee wa Yakobo ambaye hakupata kumfaidi mama yake mzazi, hata kunyonya kutoka kwa mama yake, hakunyonya kabisa..kwani siku ile anazaliwa tu!, ndipo na mama yake anakata roho.

Na siku anazaliwa mama yake alimwite “Benoni” maana yake “mwana wa uchungu wangu”..lakini baba yake alimbadilisha hilo jina na kumwita “Benyamini” maana yake “mwana wa mkono wangu wa kuume” (Mwanzo 35:16-20).

Kabila la Benyamini, wakati linaingia katika nchi ya ahadi, ndilo lililokuwa kabila lenye watu wachache kuliko yote.

Na Zaidi ya yote, baada ya kuingia katika nchi ya ahadi, maandiko yanaonesha kuwa kuna kipindi wabenyamini wengi waliuawa..wakabaki watu mia sita tu! (600). Na waliuawa kutokana na kosa la kumtendea ukatili yule Suri wa Mlawi, wa Bethlehemu-Yuda.

Kosa lile liligharimu Maisha ya wabenyamini wengi sana wakike na wakiume na watoto..na kama sio hekima ya Mungu kuingilia kati, basi kabila hili lingetoweka kabisa..Kwani waliosalia walikuwa ni wanaume 600 tu, katika kabila lote..na wengine wote walikufa..

Wakati makabila mengine kama Yuda yalikuwa na watu Zaidi ya milioni moja..kabila la Benyamini lilibakiwa na watu 600 tu!..(tena ni wanaume tu!, wanawake wote walikufa) na Zaidi ya yote bado ndio kabila dogo kuliko yote, kwani baba yao Benyamini ndiye aliyekuwa mdogo kuliko wote katika wa nawa Yakobo.

Waamuzi 21:17 “Wakasema, Lazima kuwa urithi kwa hao wa Benyamini waliopona, isiwe kabila kufutika katika Israeli”.

Hivyo lilikuwa ni kabila la kudharaulika kuliko yote!.. siku zote Wabenyamini hawakuwa watu wa heshima sana, ukilinganisha na makabila mengine kama Lawi, au Yuda au Efrahimu.

Lakini ijapokuwa ndio lilikuwa kabila dogo kuliko yote, na lenye watu wachache kuliko yote, na lililodharaulika kuliko yote, machoni pa watu.. lakini jicho la Mungu ni tofauti na la wanadamu, kwasababu Mungu haangalii kama wanadamu.

Ilipofika kipindi ambacho Israeli wanataka Mfalme wa kuwatawala mfano wa mataifa mengine yote, walikutana na jambo kinyume na mategemeo yao.

Wakati wanadhani kuwa pengine Mungu angemchagua mtu Fulani mashuhuri kutoka katika kabila mojawapo kubwa kubwa, tena lenye heshima.. kinyume chake, alimchagua mtu kutoka katika lile kabila dogo kuliko yote, tena katika ile familia ndogo kabisa.. Kinyume na matarajio yao. Na mtu huyo hakuwa mwingine Zaidi ya Mfalme Sauli.

1Samweli 9:21 “Basi Sauli akajibu, akasema, JE! MIMI SI MBENYAMINI, MTU WA KABILA ILIYO NDOGO KULIKO KABILA ZOTE ZA ISRAELI? NA JAMAA YANGU NAYO SI NDOGO KULIKO JAMAA ZOTE ZA KABILA YA BENYAMINI? kwa nini basi, kuniambia hivyo?”.

Sauli aliwatawala Israeli kwa muda miaka 40, sawasawa kabisa na alivyotawala Daudi na Sulemani.. Ijapokuwa Sauli alikuwa na kasoro kasoro nyingi, lakini Bwana alimchagua kuliongoza taifa lake takatifu kwa wakati huo.

Ni nini tunajifunza kwa kabila hili?

Tunachoweza kujifunza ni kuwa jicho la Mungu si la mwanadamu.. Yule ambaye anaonekana si kitu mbele za watu leo, yule anayeonekana kuwa hafai.. Mungu anaweza kumnyanyua kutoka mavumbini na kumpandisha juu.. Hivyo kwa vyovyote hatupaswi kujidharau, wala kuwadharau wengine.. wala tusiziogope dharau kwasababu jicho la Mungu ni tofauti na la wanadamu.

1Wakorintho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;

29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.

Bwana alilinyanyua kabila la Benyamini, anaweza kufanya kwako au kwa mwingine yeyote.. Mwamini Mungu, wala usijidharau.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

NA ABARIKIWE KILA AKUBARIKIYE, NA ALAANIWE KILA AKULAANIYE.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alivikwa taji ya miiba?

Taji ya miiba juu ya kichwa cha Bwana Yesu, iliashiria nini kiroho?..

Tusome,

Mathayo 27:27 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28 WAKAMVUA NGUO, WAKAMVIKA VAZI JEKUNDU.

29 WAKASOKOTA TAJI YA MIIBA, WAKAIWEKA JUU YA KICHWA CHAKE, NA MWANZI KATIKA MKONO WAKE WA KUUME; WAKAPIGA MAGOTI MBELE YAKE, WAKAMDHIHAKI, WAKISEMA, SALAMU, MFALME WA WAYAHUDI!

30 Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.

31 Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha”.

Kumbuka Pilato alipomuuliza Bwana Yesu kama yeye ni mfalme wa Wayahudi, Bwana hakukanusha… alimwambia “wewe wasema” maana yake “mimi ndiye”.

Hivyo wale Askari waliposikia Bwana Yesu kakiri kuwa ndiye  mfalme wa wayahudi, walicheka sana.. na kwasababu askari wa kirumi walikuwa wanawadharau wayahudi.. Hivyo ili kuwadhalilisha wayahudi.. ndio wakamvua zile nguo za thamani Bwana Yesu na kumvika vazi la jekundu, na kisha kumpa mwanzi (yaani fimbo)..na kumvika taji ya miiba…na mwisho kuinama kama vile wanamsujudia..

Lengo la kufanya vile ni kumweka katika mazingira kama ya kifalme… kwasababu kikawaida Mfalme anakuwa anavaa mavazi mekundu, pia anakuwa ameshika/anatembea na mwanzi wa thamani, na vile vile kichwani anakuwa na taji la thamani sana.. Lakini kwasababu hawa askari lengo lao lilikuwa ni kufanya dhihaka kwa wayahudi…ndio wakafanya hayo kwa Bwana Yesu, ili aonekane kama mfalme lakini asiye na utukufu, ambaye asiyejielewa.

Lakini walifanya vile kwa lengo la kufanya dhihaka tu!, (na kuwadhalilisha wayahudi) na si vinginevyo!…Na walifanya hivyo kwasababu hawakumjua yeye ni nani?.. kwasababu laiti kama wangemjua kuwa huyo wanayemfanyia dhihaka ndiye Mfalme wa kweli wa mbinguni na duniani, na pia ni Mungu mwenyewe katika mwili, wasingelimsulubisha zaidi ya yote wangemwabudu.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8 ambayo wenye kuitawala dunia hii HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.

Sasa swali ni kwanini Bwana Yesu asingezuia hayo yatokee na ilihali alikuwa na uwezo huo?

Sababu zipo kuu (2).

 1. ILI SISI TUPATE WOKOVU.

Bwana Yesu asingelisulubiwa maana yake sisi tusingelipata wokovu…

 2. ILI AINULIWE JUU.

Bwana Yesu mwenyewe alisema… ajikwezaye atashushwa, naye ajishushaye atakwezwa.. Maana yake siri ya kuinuliwa juu, wakati mwingine ni kujishusha…Ili uwe mkubwa kuliko wote sharti uwe mdogo kuliko wote, ili upate heshima kuliko wote, sharti ukubali kukosa heshima kuliko wote, hiyo  ni kanuni kubwa sana, ambayo Bwana Yesu aliijua..

Alifahamu kuwa ili anyanyuliwe juu kuliko vitu vyote, hana budi kukubali kuonekana si kitu sasa.

Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

3. KUTUPA SISI KIELELEZO.

Sababu ya mwisho ni ili kutufundisha sisi kuwa wema, kama yeye!… kama yeye mwenyewe alivyosema.. “mtu akupigaye shavu hili mgeuzie na la pili” au mtu akulazimishaye mwendo wa maili moja, nenda naye mbili..Kwasababu kwa kufanya hivyo, ataiona haki yako na mwisho atavutiwa na imani yako, na hata kumbadilisha kabisa… (Umeona askari hao hao waliomfanyia dhihaka, masaa machache tu mbele walikiri kuwa yeye kweli alikuwa Mwana wa Mungu, Marko 15:39).

Na sisi hatuna budi kuwa kama Bwana Yesu, tunapotukanwa tunapaswa tustahimili, tunapoudhiwa na kudhalilishwa tunapaswa tustahimili kama Bwana Yesu, kwasababu mwisho wake ni mzuri..

1Petro 2:19 “Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

20 Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.

23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.

24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.

25 Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu”.

Waebrania 12:3 “Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.

4 Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Kwanini hatuirithi neema kama tunavyoirithi dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

UNAVYOZIDI KUWA MWENYE HAKI, NDIVYO KUJITAMBUA KWAKO KUNAVYOPUNGUA.

Tofauti na tunavyoweza kudhani, kwamba pale unapoongezeka viwango vya kiroho, Au pale unapopiga hatua moja kwenda nyingine kwa Mungu  basi utajitambua, au utapata hisia Fulani ya kitofauti kwamba amehama ulimwengu mmoja na kwenda mwingine, au utahisi nguvu Fulani zimeongezeka ndani yako, Lakini sivyo. Ni ngumu sana kujitambua wewe mwenyewe..Bali mwingine ndiye atakayekutambua.

Tunamwaona Musa aliposhuka kutoka mlimani kuzungumza na Mungu kwa muda wa siku 40, usiku na mchana, hakujua kama lipo badiliko lolote, limetokea katika uso wake.

Lakini aliposhuka tu, mlimani wana wa Israeli ndio waliokuwa wa kwanza kumtambua na kumfunulia siri ambayo hakuijua kwa muda siku zote arobaini alizokuwa anamkaribia Bwana..

Kutoka 34:29 “Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye.

30 Basi Haruni na wana wote wa Israeli walipomwona Musa, tazama, ngozi ya uso wake iling’aa; nao wakaogopa kumkaribia.

31 Musa akawaita; Haruni na wakuu wote wa kusanyiko wakarudi kwake; Musa akasema nao.

32 Baadaye wana wa Israeli wote wakakaribia; akawausia maneno yote ambayo Bwana amemwambia katika mlima Sinai”.

Hii ni kutukumbusha, Mtu uliyeokoka, ukiongeza ukaribu wako kwa Mungu, kwa hatua nyingine, ni ngumu sana kuona kama utukufu wako umeongezeka  ndani yako kwa hatua moja zaidi..Mfano unapoongeza kiwango chako cha maombi, utajiona wewe ni yule yule tu, kama ulivyokuwa juzi..Lakini tayari utukufu wako umeongezeka kwa ngazi moja juu Zaidi, isiyoijua au kuihisi wewe.

Unaposema, embu ngoja nianze kujizoesha kwenda mikesha kanisani kila ijumaa, unaweza kujiona upo vilevile tu, lakini ipo hatua kubwa sana umepiga.. Ukitaka kufahamu kuwa umepiga hatua, embu sema sikumoja niache kwenda mikesha, halafu uone, huo ukame utakaouhisi ndani ya nafsi yako, utakavyokuwa.

Unapojilinda kila siku na dhambi, ya uasherati, matusi, wizi, n.k. ni rahisi kutohisi ongezeko lolote, ndani yako, lakini fahamu kuwa utukufu wako umeongezeka sana, wale wa nje ndio watakaokuja kushuhudia, Pamoja na Mungu mwenyewe. Watu wengi wanaishiwa na nguvu njiani, kwasababu wanaona kama bidii wanayoizidisha kwa Mungu, haiwarejeshei, badiliko kubwa ndani yao, kama wanavyotarajia.

Kumbuka huwezi kuuona uso wako..Ndivyo ilivyo nasi katika roho, hatuwezi kujiona wenyewe ndani yetu jinsi tunavyokuwa kiroho..Lakini walio nje ndio watakaotuona, hata kama hawatosema.

Ufalme wa Mungu ni kama mbegu, inayotupwa katika Shamba, ambayo biblia inasema, inakua kwa jinsi asivyojua mtu, Lakini mwisho wa siku ghafla tu, inatoa yenyewe matunda

Marko 4:26 “Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;

27 akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.

28 Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.

29 Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika”.

Hivyo, usihangaike sana, kujichunguza chunguza, kwasababu hutaona lolote. Lakini fahamu kuwa kila hatua unayoiongeza kwa Mungu, ina utukufu mkubwa sana kwako. Ndugu Usipunguze maombi, hata kama huoni chochote, usipunguze kushuhudia wengine Habari njema, usipunguze kumtolea Mungu kwa mali zako, hata kama huoni marejesho yoyote kutoka kwake, usipunguze kwenda ibadani na kuhudhuria mikesha. Kinyume chake ndio uzidishe, kuyatenda hayo.

Mwisho wa siku utukufu wako utaangaza sana kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa Mungu Musa, hadi wengine watakuogopa kwa jinsi ulivyomkaribia Mungu sana.

Ubarikiwe na Bwana.

Tafadhali shea na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi// Ushauri/ Maswali/Whatsapp.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu alisema “Msimwamkie mtu njiani”?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema, msimwamkie mtu njiani? (Luka 10:4).. Na wakati huo huo alisema katika Mathayo 5:47, kuwa “tukiwaamkia ndugu zetu tu!, tunatenda tendo gani la ziada”.

Jibu: Labda tuanzie kusoma kuanzia mstari wa kwanza…

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; WALA MSIMWAMKIE MTU NJIANI”.

Mwalimu anapotoa tangazo kwa wanafunzi wake na kuwaambia… “si ruhusa kuzungumza na mtu yeyote ndani ya chumba cha mtihani”.. Kwa kusema hivyo hajamaanisha kuwa “si ruhusa kuzungumza na mtu kila mahali” Hapana!.. bali ni katika chumba cha mtihani tu!..wakiwa mahali pengine wanaweza kuzungumza..

Na kadhalika Bwana hakuwakataza wanafunzi wake “kuwaamkia/kuwasalimia watu kabisa”..hapana!..bali wanapokuwepo katika “Safari ya uinjilisti” hapo ndipo “Alipowazuia wasiamkie amkie watu njiani”.

Sasa kwanini awazuie kufanya hivyo, wakiwa katika safari ya kwenda kuhubiri?

Ni kwasababu salamu zinacheleweza lile kusudi, na ni rahisi kumhamisha mtu kifikra kutoka katika mawazo ya kwenda kuhubiri mpaka kuanza kufikiri mambo mengine tofauti na yanayohusu injili anayokwenda kuhubiri..

Hebu tengeneza picha Mwanafunzi mmojawapo wa Bwana Yesu, anakwenda kuhubiri, halafu njiani anapita karibu na nyumba ya Mjomba wake..halafu anaingia kumsalimia, na katika mazungumzo anapewa taarifa mbalimbali aidha za misiba, au za watu wengine au nyingine zozote..

Au anapewa jukumu lingine la kufanya huko anakokwenda, labda anaambiwa ukifika mahali fulani naomba uninunulie kitu fulani, ukirudi nipitishie hapa, au ukifika mahali fulani nisiaidie kuulizia hili au lile, au ukifika sehemu Fulani kumbuka kumsalimia mtu Fulani, au huko unakokwenda kuwa makini nako kuna hatari n.k..

Ni wazi kuwa kuanzia huo wakati na kuendelea mawazo ya yule mwanafunzi yatakuwa yametawaliwa na yale aliyoyasikia kutoka kwa ndugu yake huyo, na yale ya injili yatakuwa yamemezwa…

Kwahiyo ili kulizuilia hilo.. ndipo Bwana akasema… “Msiwaamkie watu njiani”.. ili mawazo yao na akili zao ziwe katika Injili wanayokwenda kuihubiri..

Lakini watakapomaliza safari yao hiyo ya injili wapo huru kuwaamkia watu wowote pasipo kupendelea sawasawa na Neno hilo la Bwana katika Mathayo 5:47

Kadhalika na sisi, tunapokuwa katika uinjilisti, hatupaswi kuuchanganya na mambo mengine, tunapokuwa katika kuifanya kazi ya Mungu, hatuna budi akili zetu, mawazo yetu, kuyafunga yasiingiliwe na mawazo mengine.. (kadhalika tunapokuwa katika ibada ni sharti kuzima simu, ili kuongeza umakini katika kuomba, kusifu na kusikiliza Neno).

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Katika Marko 6:12 maandiko yanasema…“Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu”… Hizi deni ndio zipi??

Jibu: Mtu aliyekutukana ana deni kwako la kuja kukuomba radhi!..Hilo ni deni lake kwako, awe anajua au hajui…Na kulilipa ni yeye kuja kukuomba wewe radhi!.. Asipokuja kukuomba radhi basi hilo litabaki kuwa deni kwake. (wewe utakuwa unamdai). Labda wewe uamue kumsamehe tu!

Hali kadhalika na sisi tunapomfanyia Mungu dhambi, tunakuwa na deni kwake la KUUNGAMA! (Maana yake kukiri makosa yetu na kuomba radhi kwake)!. Hayo ni madeni kwetu kwa Mungu..

Kwa maana dhambi ni kosa lolote mtu analolifanya dhidi ya Mungu.

Lakini Bwana wetu Yesu alitufundisha kuwa ni lazima tuwasamehe watu madeni yao ili na sisi tusamehewe yetu!.. Maana yake, yale mambo ambayo wangepaswa waje waungame mbele yetu (yaani kukiri na kuomba radhi), wanapoungama basi tunawasamehe, na hata wasipokuja kuomba radhi vile vile tunapaswa tuwasamehe.

Na wakati mwingine watu wanatukosa pasipo hata wao kujua kama wametukosa, hivyo hawawezi kuja kutuomba radhi kwasababu hata hawajui kama wametukosea, (Hivyo wanabakia kuwa na madeni kwetu ambayo hawajui hata kama wanayo)..

Kadhalika na sisi tunamkosea Mungu kwa mambo mengi, ambayo wakati mwingine hatujui kama tunamkosea (Jambo linalotufanya tuwe na madeni mengi mbele za Mungu), hata pasipo sisi wenyewe kujua.

Kwahiyo tunapoomba hiyo sala ya Baba yetu!, na kusema “utusamehe deni zetu”.. Maana yake tunamsihi Mungu atusamehe yale makosa ambayo hatukuyatubia au yale tuliyoyafanya pasipo kujua kuwa ni makosa…Na Mungu ni mwaminifu, anatusamehe…lakini kama tu na sisi tutakuwa tayari kuwasamehe wengine madeni yao.

Swali ni Je!, na wewe umemsamehe yule aliyekutukana au kukusengenya au kukutapeli? au unasubiri aje kukuomba radhi?…nakuambia usingoje!..wewe msamehe hata bila yeye kukuomba radhi, ndivyo na Mungu atakavyokusamehe na wewe makosa ambayo hata wewe hukumwomba radhi!..

Bwana wetu Yesu Kristo, aliwasamehe wale wote, ambao walimsulubisha, (Aliwasamehe pasipo wao kumwomba msamaha).. kwakufanya vile alitupa na sisi kielelezo, kwamba na sisi tuwasamehe wenzetu kama yeye alivyotusamehe. Kwasababu tusipowasamehe watu makosa yao na Mungu wetu hatatusamehe sisi.

Mathayo 18:21“Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 YESU AKAMWAMBIA, SIKUAMBII HATA MARA SABA, BALI HATA SABA MARA SABINI.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

Rudi nyumbani

Print this post

Rushwa inapofushaje macho?

Biblia inasema rushwa inawapofusha macho hao waonao? (Kutoka 23:8) Ni kwa namna gani rushwa inaweza kumpofusha mtu macho?

Jibu: Tusome,

Kutoka 23:8 “Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki”.

Ili tuelewe vizuri, hebu tutafakari mfano ufuatao..

Hakimu mahakamani anaona kabisa mhalifu fulani amefanya kosa linalostahili kifungo (yaani macho yake yanaona kabisa lile ni kosa alilolifanya, na anapaswa ahukumiwe kulingana na sheria)..Lakini anapopewa rushwa, palepale anajiziba macho, na kumwachia yule mhalifu, na kulifunika kosa lake.. (Sasa kitendo hicho cha hakimu kujiziba macho na kulifunika kosa, ndicho kinachoitwa kupofuka macho).. na hiyo yote ni kwasababu ya rushwa!..Laiti asingepokea rushwa angelitazama kosa na kulihukumu jinsi inavyostahili..

Ndio maana biblia inasema…“Rushwa huwapofusha macho hao waonao”..Wanaona na kujua kabisa jambo Fulani sio sawa, lakini rushwa inawafanya wasilione kama ni kosa tena..(macho yao yamepofuka!).

Na sio tu!, kuwapofusha macho hao wanaoipokea, bali pia “inayapotoa maneno ya wenye haki”.. maana yake.. wale watu wastahilio kupata haki, hawapati hiyo haki, wanaonena maneno ya haki, maneno yao yanapotoshwa kwasababu ya rushwa iliyotolewa na mwingine.

Ni mara ngapi, watu wasio na hatia wanafungwa, kwasababu tu upande mmoja umetoa rushwa?..

Biblia utaona inazidi kuliweka hilo wazi katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati..

Kumbukumbu 16:19 “Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; WALA USITWAE RUSHWA; KWA KUWA RUSHWA HUPOFUSHA MACHO YA WENYE AKILI, NA KUGEUZA DAAWA YA WENYE HAKI”.

Na sisi kama wakristo hatupaswi kupokea wala kutoa rushwa!..kwasababu rushwa ina laana nyuma yake.

Mithali 17:23 “ASIYE HAKI HUTOA RUSHWA KIFUANI, Ili kuzipotosha njia za hukumu”.

Katika biblia utaona mojawapo ya sababu iliyomfanya Nabii Samweli akubalike mbele za Mungu na watu, na kuzidi kupata kibali cha kuiamua Israeli mpaka uzee wake, ni mwenendo wake wa kutokubali Rushwa..

1Samweli 12:1 “Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu.

2 Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo.

3 NAMI NIPO HAPA; BASI, MNISHUHUDIE MBELE ZA BWANA, NA MBELE YA MASIHI WAKE,NALITWAA NG`OMBE WA NANI? AU NALITWAA PUNDA WA NANI? AU NI NANI NILIYE MDHULUMU? NI NANI NILIYEMWONEA? AU KWA MKONO WA NANI NIMEPOKEA RUSHWA INIPOFUSHE MACHO? NAMI NITAWARUDISHIA NINYI.

4 NAO WAKASEMA, HUKUTUDHULUMU, WALA HUKUTUONEA, WALA HUKUPOKEA KITU KWA MKONO WA MTU AWAYE YOTE.

5 Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi”

Umeona?..Samweli hakuwahi kupokea rushwa Maisha yake yote, na ndio ikawa sababu ya yeye kudumu katika Uamuzi wa Israeli, Lakini sasa kinyume chake, wanawe wawili aliowazaa hawakuwa kama yeye, wao walikuwa wanapokea rushwa..

Jambo ambalo liliwafanya wana hao wa Samweli kutolewa katika kiti cha Uamuzi wa Israeli, na hiyo ni kwasababu tu ya RUSHWA walizokuwa wanazipokea kutoka kwa watu..na matokeo yake ikasababisha Israeli nzima kuingia katika dhambi ya kutaka mfalme, kutokana na kwamba waliona Watoto hao wa Samweli hawafai..

1Samweli 8:1 “Hata Samweli alipokuwa mzee, aliwafanya wanawe wawe waamuzi juu ya Israeli.

2 Na jina la mwanawe mzaliwa wa kwanza aliitwa Yoeli; na jina la wa pili Abiya; walikuwa waamuzi katika Beer-sheba.

3 ILA WANAWE HAWAKUENDA KATIKA NJIA ZAKE, BALI WALIZIACHA, ILI WAPATE FAIDA; WAKAPOKEA RUSHWA, NA KUPOTOSHA HUKUMU.

4 Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama”

5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote.

Hiyo ikitufundisha kuwa Rushwa, siku zote inatokosesha kibali mbele za Bwana na mbele za watu!…

Ukitaka udumu katika Nafasi yoyote uliyopo, ambayo ni Mungu kakuweka, basi kaa mbali na rushwa!.. ukitaka udumu katika utumishi (wa Mungu) kaa mbali na rushwa, ukitaka udumu katika kazi ya mikono unayoifanya basi kaa mbali na rushwa.. Wanadamu wengi wanaweza wasikuone unayoyafanya kwa siri, lakini Mungu anakuona, na yeye ndiye atakayekuvua hiyo nafasi..na Zaidi ya yote utakapokufa bila kuacha rushwa, basi utahukumiwa.

Ayubu 15:34 “Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, NA MOTO UTATEKETEZA MAHEMA YENYE RUSHWA”.

Bwana atusaidie..

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Ni kwanini Yesu alisema Na wakisikia wasikie, wasielewe Wasije wakaongoka?

Rudi nyumbani

Print this post

Unyenyekevu ni nini?

Unyenyekevu ni nini, kibiblia, ili mtu awe ni mnyenyekevu anapaswa aweje?


Tafsiri ya Unyenyekevu ni Kujishusha. Pale unapokuwa na uwezo wa kutumia nguvu, au sauti, au mamlaka, kuhimiza jambo, lakini unajishusha chini, kana kwamba wewe si kitu, huo ndio unaitwa unyenyekevu.

Unyenyekevu sio kushushwa, bali kujishusha. Na kinyume cha Unyenyekevu ni kiburi, yaani kujipandisha juu, kujiona wewe unaweza yote, wewe ni bora kuliko vyote, wewe una nguvu kuliko wote, wewe una sauti zaidi ya wote.

Unyenyekevu ni mgumu sana kuufikia, kwasababu asili ya mwanadamu ni kutaka kujipandisha juu. Lakini ukiupata unyenyekevu basi umepata mpenyo mkubwa sana wa kumfikia Mungu.

Kiwango cha unyenyekevu kinatofautiana, kwa jinsi mtu anavyoteremka ngazi moja chini, ndivyo kiwango chake cha unyenyekevu kinavyokuja juu, na pale anapoongeza ngazi nyingine na nyingine ndivyo unyenyekevu wake unavyofikia kilele cha juu sana.

Ni kwanini tuwe wanyenyekevu?

  1. Ni kwasababu Kristo naye alikuwa mnyenyekevu;

Wafilipi 2:6 “ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

2) Kwasababu Mungu anawapinga wenye kiburi

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

Mungu ni adui mkubwa kwa kiburi, hivyo tukilijua hilo ni kujitahidi sana tuwe mbali na kitu hicho.

Faida za kuwa wanyenyekevu ni zipi?

  1. Mungu anakuwa karibu nasi:

Mungu alikuwa karibu na Bwana Yesu, kuliko mtu mwingine yeyote, na hiyo yote ni kwasababu ya unyenyekevu wake:

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

     2) Mungu anatukweza juu;

Utaona baada ya Bwana Yesu kujishusha, Mungu alimkweza juu Zaidi ya vitu vyote ulimwenguni.

Wafilipi 2:8 “tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

Tunakuwaje wanyenyekevu?

  1. Kumuhesabu mwenzako ni bora kuliko nafsi yako mwenyewe.

Wafilipi 2:3 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake”.

     2) Kuuzuia ulimi:

Kuwa wa mwisho kunena, na kuzuia hasira zako, usitoe maneno ya majigambo;

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”.

  3) Kutojihesabia haki, mbele za Mungu:

Luka 18:9 “Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

10 Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

11 Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi”.

14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

     4) Kukubali kujishughulisha na mambo manyonge

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili”.

Si lazima, kila jambo la juu tung’ang’anie kulifanya. Bwana Yesu alikuwa ni Mungu, lakini akaona kule kuwa sawa naye sio kitu cha kushikamana nacho. Akawa kama mtumwa..Vivyo hivyo na sisi tupende utumwa kuliko ukubwa.

Mwisho kabisa tukumbuke kuwa Unyenyekevu kibiblia, upo kwa namna mbili; Unyenyekevu wa sisi kwa sisi, na unyenyekevu kwa Mungu. Vyote viwili vinakamilisha Unyenyekevu wa ki-Mungu. Kama vile ulivyo upendo. Ili tukamilike katika huo ni sharti, tupendane sisi kwa sisi, na vilevile tumpende Mungu.

Ndio maana Bwana Yesu aliwatawaza miguu watakatifu wake, akatupa na sisi kielelezo kuwa tunyenyekeane sisi kwa sisi, kama yeye alivyofanya.

Hivyo tuizingatie sana nguzo hii muhimu katika ukristo wetu. Ili tumfurahie Mungu wetu.

Bwana akubariki.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

Furaha ni nini?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

TUMAINI NI NINI?

Jehanamu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post