Category Archive Home

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

Bwana Yesu alisema maneno haya katika Mathayo 7:21-23.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; BALI NI YEYE AFANYAYE MAPENZI YA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa unaweza kujiuliza hayo “Mapenzi ya Mungu ndio yapi” Kwasababu hapo tunaona kumbe hata unaweza kutoa pepo lakini ukawa bado huyafanyi mapenzi ya Mungu…vile vile unaweza ukawa unatabiri na kutoa unabii na unabii huo ukatimia lakini, bado ukawa mbali na mapenzi ya Mungu.

Sasa Mapenzi ya Mungu ni yapi?..ambayo tukiyafanya hayo hata kama tutakuwa hatutoi pepo wala kutoa unabii wala kutabiri bado tuta urithi ufalme wa mbinguni?.

Tusome,

1 Wathesalonike 4:2 “Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.

3 Maana HAYA NDIYO MAPENZI YA MUNGU, KUTAKASWA KWENU MWEPUKANE NA UASHERATI;

4 KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE KATIKA UTAKATIFU NA HESHIMA;

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Umeyaona Mapenzi ya Mungu?
Kumbe Mapenzi ya Mungu si miujiza wala upako, bali UTAKATIFU..

Kumbe hata tukiwa na Imani kubwa ya kuweza kugeuza maji kuwa asali bado upo uwezekano mkubwa wa kupotea katika ziwa la moto, kama HATUNA UTAKATIFU.

Hii ni tahadhari kubwa sana kwetu..Lakini biblia inazidi kulithibitisha hilo kwetu katika..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA MUNGU ASIPOKUWA NAO” .

Ndugu yale maono unayoyaona katika ndoto, ni kweli ni ya kiMungu lakini hayo sio tiketi ya kukufikisha mbinguni, tiketi ya kukufikisha mbinguni ni utakatifu wa mwili na roho.

Ile imani uliyo nayo kiasi kwamba chochote utakachokisema kwa jina la Bwana kinatokea, sio tiketi ya kufika mbinguni kama hutaacha uasherati wako, au ulevi wako, au wizi wako au utukanaji wako.

Ile ahadi Mungu aliyokuonyesha kwa njia ya unabii au ndoto, sio tiketi ya wewe kuurithi uzima wa milele, kama hutadumu katika kuyafanya mapenzi ya Mungu (Yaani Utakatifu).

Uuimbaji unaoimba, unabii unaoutoa, lugha unazonena hazitakufikisha popote kama hutaamua kujitakasa kwa kuacha kuvaa vimini, kuacha kuvaa suruali (kama ni mwanamke), kuacha kujipaka uso rangi, kuacha kuvaa kope na kucha za bandia, kama hutaacha kuvaa hereni, wigi na kupaka lipstiki na kunyoa kiulimwengu..

Utauliza inamaana wanawake kuvaa suruali  na vimini sio mapenzi ya Mungu?..Jibu ni NDIO!. Rejea vizuri hiyo mistari…

“KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE KATIKA UTAKATIFU NA HESHIMA”.

Sasa jiulize vimini ni nguo za heshima?, Suruali ni nguo za heshima?..Je unaweza kwenda kumtambulisha mchumba wako kwa wazazi wako akiwa amevaa Suruali?? Au vimini??..Kama huwezi basi jua hayo sio mavazi ya heshima na hayafai..na mapenzi ya Mungu ni “kila mtu kuuweza mwili wake kwa utakatifu na Heshima

Kama hutaacha hayo yote, na umesikia kama hivi, basi siku ile utatimiza huu unabii unaosema.. “wengi watasema siku ile wakisema, hatukufanya hichi au kile” na Bwana atawakataa dhahiri.

Mimi na wewe na ndugu zetu tusiwe watu hao watakaotimiza huo unabii.

Bali tujiepushe na dhambi na kujitakasa, ndivyo tutakavyofanya mapenzi ya Mungu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je suruali ni vazi la kiume tu?

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Kama Malkia Esta alijipamba je! Kuna ubaya gani wanawake wa wakikristo wa leo kujipamba?.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Jibu: Uwezo na Uweza ni kitu kimoja.. tofauti ni kwamba kimoja kinatumika kwa Mungu na kingine kwa wanadamu.

Wanadamu na wanyama na shetani na malaika na viumbe vingine vyote vinao UWEZO wa kufanya mambo. Lakini havina UWEZA wa kufanya jambo.

Mwenye UWEZA wa kufanya jambo ni Mungu tu peke yake.

Mwanadamu ana UWEZO wa kuua lakini wa kuurudisha Uhai hana…kwasababu kuurudisha uhai ndani ya mtu kunahitaji UWEZA, na UWEZA huo anao Mungu tu.

1 Wakorintho 6:14 “Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa UWEZA wake”.

Vile vile mwanadamu na shetani wanao UWEZO wa kuipotosha roho, lakini Kuiokoa hawawezi!..Kwasababu kuiokoa roho ya Mwanadamu inahitajika UWEZA na sio UWEZO. NA Uweza huo ni Mungu tu! Ndio anao.

Warumi 1:16 “Kwa maana siionei haya Injili; KWASABABA NI UWEZA WA MUNGU UULETAO WOKOVU, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia”.

Swali ni je!..Unawatumainia wenye UWEZO au mwenye UWEZA?.

Shetani anao uwezo wa kukupa mali lakini si Uzima wa milele!, Wanadamu wana uwezo wa kukupotosha lakini wa kukuokoa hawawezi.

Mwanadamu anao uwezo wa kutibu, lakini kuponya hawezi, Mwenye Uwezo wa kuponya nk Mungu tu peke yake.

Unaweza kusoma pia juu ya Uweza wa Mungu katika Nehemia 1:10, Nehema 9:32, Marko 12:24, na Matendo 8:10.

Kwanini usimtumainie huyo mwenye uweza wa kufanya mambo yote, huyo ndio wa kumtumainia na vile vile wa kumwogopa..

Luka 12:5 “Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana UWEZA wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”.

Na sasa UWEZA huo wa kiungu upo juu ya Bwana Yesu Kristo pekee, ambaye mamlaka yote ya mbinguni na duniani, amekabidhiwa yeye.

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,Tumepewa mtoto mwanamume; Na UWEZA wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”.

Je umempokea Yesu?..kama bado unasubiri nini?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Roho Mtakatifu ni nani?.

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

Kuna njia kuu sita(6)

Ni vema ukazifahamu hizi njia Mungu anazozungumza na watu, ili usitegemee tu njia moja uifahamuyo wewe, matokeo yake ukakosa shabaha ya kuzisikia sauti za Mungu kila siku maishani mwako zinapozungumza na wewe.

1. Ya kwanza ni Njia ya moja kwa moja:

Hii ni Aidha kwa Sauti, ndoto, au maono,

Ni mojawapo ya njia ambayo Mungu anazungumza na watu. Na ndio inayojulikana na kutegemewa na wengi.

Ayubu 33:14-15

[14]Kwa kuwa Mungu hunena mara moja,  Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. [15]Katika ndoto, katika maono ya usiku,  Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

Katika maisha yetu kwa namna moja au nyingine Mungu alishazungumza nasi kwa njia hii. Unaweza usione, maono au usisikie sauti lakini kila mtu huwa anaota. Na kwa njia hiyo Mungu huzungumza.

  1. Kwa njia ya Neno lake:

Hii ndio sauti ya Mungu namba moja ambayo inazungumza na mtu moja kwa moja na kwa wakati wote..ni sauti ambayo hailinganishwi na sauti nyingine zozote.

Ukiwa ni msomaji mzuri wa Neno, utamsikia Mungu katika nyanja zote za Maisha akikufariji, akikuonya, akikushauri, akikuongoza n.k. Ni pakeji iliyojitosheleza., ambayo hailinganishwi na njia nyingine yoyote.

2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”

    3. Njia nyingine ni Amani.

Ikiwa wewe umeokoka, na umejazwa Roho Mtakatifu, basi ujue mara nyingi sana Mungu atatumia amani yake moyoni mwako kuamua mambo mengi..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 10:11-13

[11]Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. [12]Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.

[13]Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.

Wakolosai 3:15a “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu;..”

Kuonyesha kuwa amani itokayo kwa Roho ni sauti ya Mungu kutuongoza, ikiwa umepoteza amani ghafla katika mazingira fulani kuwa makini sana hapo. Wakati mwingine ni Mungu anazungumza.

   4. Kwa kupitia watu.

Hapa anaweza akachagua aidha apitie mtu mwovu au mtu mwema. Mara nyingi sana Mungu anazungumza na watu kupitia watumishi wake, yaani wahubiri, waalimu, wainjilisti n.k.

Yeremia 25:4

[4]Naye BWANA ametuma kwenu watumishi wake wote, hao manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini ninyi hamkusikiliza, wala hamkutega masikio yenu, msikilize.

Na mara nyingine tena anaweza kutumia watu wa kidunia kukuonya..kama vile maaskari, wakuu wa hii dunia n.k.

Hivyo ni kuzingatia sana unachokisikia au kufundishwa au kuonywa na watu, hususani watumishi wa Mungu..Mara nyingine sauti ya Mungu ipo nyuma yao.

     5. Kwa kupitia mazingira.

Mazingira yanaweza yakawa ya kimaisha, au ya kihali…kwa mfano Mungu akitaka uelewe jambo fulani, wakati mwingine hatumii sauti ya moja kwa moja, kwasababu pengine unaweza kulichukulia juu juu tu au usimwelewe, hivyo atakupitisha katika maisha fulani au mazingira fulani, na kwa kupitia hayo utajua kabisa hapo ni Mungu alikuwa akisema na wewe.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Nebukadreza, yeye alionywa na Mungu, awe mnyenyekevu na amche Mungu, lakini hakusikia, kinyume chake akapuuzia ule unabii aliopewa na Danieli. Matokeo yake baada ya miezi 12, akageuzwa kuwa kama mnyama, akawa anaishi huko misituni akila majani kama ng’ombe..mpaka siku alipoelewa somo kuwa aliye juu ndiye anayetawala falme zote za duniani. Ndipo akajinyenyekeza ,hivyo Mungu akamrudishia ufalme wote wa dunia. (Danieli 4)

   6. Kwa kupitia vitu vya asili na viumbe.

Sauti ya Mungu imejificha sana katika vitu vinavyotuzunguka na asili, kiasi kwamba tungefahamu vema basi tusingekuwa na ugumu wa kumwelewa Mungu.

Embu fikiri Bwana Yesu alivyotuambia..tafakarini Kunguru?..hawapandi hawavuni wala hawana maghala ya chakula lakini wanakula..Je sisi si mara nyingi zaidi ya hao? (Luka 12:24)

Hili ni neno ambalo lilikwepo tangu enzi na enzi kiasi kwamba watu wangekuwa wanalitafakari kabla hata ya Yesu, wasingekuwa na hofu ya maisha pale wanapotaka msaada kutoka kwa Mungu.

Vivyo hivyo utazamapo, bahari, milima, miti,  zipo sauti nyingi sana za Mungu nyuma yake .. Chukua muda mwingi kutafakari, utaisikia sauti ya Mungu waziwazi.

Mungu alimwambia Ibrahimu angalia juu tazama nyota za mbinguni na mchanga wa baharini upate imani kwangu.

Hivyo ni vizuri ukapata maarifa haya usije ukaangamia kwa kutomwelewa Mungu. Leo hii watu wanategemea njia moja tu..ile ya moja kwa moja..yaani kusikia sauti, au kuona maono au kuota ndoto. Na kusahau hizi nyingine.. Ndio hapo utasikia wakisema nimeomba sana, nimelia sana Mungu aseme na nini, lakini sijawahi kumsikia.

Ni kwanini? Nikwasababu wanalazimishia njia hiyo hiyo moja Mungu aseme nao..

Hawajui kuwa Mungu hapangiwi fomula ya kuzungumza.Hivyo wewe uombapo..kuwa mtulivu, soma sana Neno mtafakari Mungu..subiri azungumze kwa jinsi apendavyo yeye. Atakujibu tu aidha kwa Neno lake, au mtumishi wake, au amani moyoni mwako, au kwa kutazama mambo ya asili, ukiona hivyo basi ujue ni Mungu huyo.

Hivyo kaa katika utulivu wa Roho, zingatia kusoma Neno..kwasababu maarifa kama haya utayapata katika biblia na sio kwa kuota au kuona maono.

Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

Unyenyekevu ni nini?

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Rudi nyumbani

Print this post

ENZI NA MAMLAKA AMEZIFANYA KUWA MKOGO

Jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Wakolosai 2:14 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;

15 AKIISHA KUZIVUA ENZI NA MAMLAKA, NA KUZIFANYA KUWA MKOGO KWA UJASIRI, akizishangilia katika msalaba huo”.

Je unajua maana ya Mkogo? (mkogo ni nini?)

Mkogo ni neno lenye maana ya “tamasha”.. kwamfano watu wanaofanya tamasha la sarakasi, ni sawa na kusema wanafanya “mkogo wa sarakasi”

Hivyo hapo maandiko yaliposema “Bwana Yesu amezivua enzi na Mamlaka na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri”..Maana yake “amezivua enzi na mamlaka na kuzifanya kuwa tamasha kwa ujasiri”.

Sasa swali, ni Enzi gani na Mamlaka gani, Bwana Yesu aliyavua?.. ni yake mwenyewe au mengine?

Jibu: Enzi na mamlaka yaliyovuliwa hapo na Bwana sio yake yeye mwenyewe.. bali ni yale ya NGUVU ZA GIZA. Bwana amemvua shetani juu ya huu ulimwengu na wanadamu kwa kifo chake pale msalabani.. Na baada ya kumvua, akayavaa yeye mamlaka hayo.. (kumbuka mamlaka hayo ya shetani alimvua Adamu, pale Edeni).

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, NIMEPEWA MAMLAKA YOTE MBINGUNI NA DUNIANI”.

Huu ulimwengu sasahivi upo chini ya mamlaka ya Bwana Yesu, shetani ni kama mpangaji tu!..nyakati na majira yatakapotimia ataondolewa moja kwa moja. Hivyo shetani sasahivi si kitu kwa Bwana Yesu..

Yohana 14:30 “Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, WALA HANA KITU KWANGU”.

Sasa ni wakati gani ambapo Enzi na mamlaka yalifanyika mkogo (yaani tamasha)?

Ni wakati Bwana Yesu akiwa msalabani, wakati dunia inaona ni kifo cha aibu, lakini Bwana yeye aliona ushindi, wakati wachache wanamhuzunikia na kumlilia pale msalabani.. yeye (Bwana) alikuwa anashangilia ushindi, na kuonyesha tamasha la wazi kwa ujasiri, jinsi shetani na majeshi yake yalivyokuwa yanavuliwa mamlaka pale msalabani.

Wakolosai 2:15 “akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo”.

Bwana leo hii anatawala mbinguni na duniani, shetani hana lolote mbele zake.

Je kwanini tusimtumainie leo huyo?.. Kwanini tusimfanye kuwa nguzo ya Maisha yetu?..yeye ambaye amemvua shetani mamlaka na enzi. Hata sasa tunapozungumza Bwana Yesu anamiliki vitu vyote vya mbinguni na duniani, na vilivyopo chini ya dunia, na vitu vyote vinapiga goti, na vitapiga goti mbele zake.

Tukimwelewa Yesu kwa namna hii, kamwe hatutamtamani shetani na Fahari zake, na pia hatutamwogopa shetani, wala hatutawaogopa wachawi.. Ukiona unahofu ya shetani, au wachawi na umesema umeokoka au umempokea Yesu, basi jua bado hujamjua Bwana Yesu vizuri.

Siku ukimjua na kumwelewa, hutabaki kama ulivyo.

Mpokee Yesu, mtumainie Bwana.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

ZUMARIDI NI MADINI GANI?

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Hapo ndipo, atakapompa Mungu Baba ufalme wake.

Rudi nyumbani

Print this post

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?.

Mshipi ni nini? na Ule mshipi wa dhahabu matitini ni nini?, na je! Yule Yohana aliyemwona ni mwanamke?, kama sio kwanini pametaja matiti?.


Jibu: Tusome,

Ufunuo 1:13 “na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa MSHIPI WA DHAHABU MATITINI”.

Tafsiri ya “Mshipi” ni mkanda. Unaweza kusoma pia Mathayo 3:4, na Matendo 21:11, na Zaburi 18:32 utaona jambo hilo hilo. Na mkanda huo unaweza kuwa umetengenezwa kwa malighafi yoyote, aidha kwa Ngozi, au kitambaa kigumu. Lakini lengo la mshipi, ni kubana sehemu ya kiuno au kifua.

Sasa Huyo Mtume Yohana aliyemwona katika maono, hakuwa mwanamke, bali alikuwa ni mwanaume, ambaye ni BWANA YESU KRISTO, Ndio maana ukiendelea mbele kidogo, utaona anajitambulisha..

Ufunuo 1:17 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 NA ALIYE HAI; NAMI NALIKUWA NIMEKUFA, NA TAZAMA, NI HAI HATA MILELE NA MILELE. NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU”.

Na kama tunavyojua mwenye funguo za mauti na kuzimu, na aliyekuwa amekufa na sasa yu hai, si mwingine Zaidi ya Bwana Yesu Kristo. Kwahiyo huyo bila shaka yoyote alikuwa ni Mkuu wa Uzima, Yesu Kristo mwenyewe.

Lakini ni kwanini biblia iseme alikuwa amevikwa mshipi matitini na si kifuani?

Ni kuonyesha tu eneo la mwili ambalo “Mshipi huo umefungwa”.. (kwamba ni eneo la kifua, ambalo ndio eneno la matiti kwa maumbile ya wanawake), lakini sio kwamba kwa Kutaja matiti kunamaanisha kuwa ana matiti, hapana!.. biblia kumtaja Bwana Yesu kama Mwanakondoo, haimaanishi Bwana anayo maumbile kama ya kondoo, au uso wa kondoo. Ni lugha tu!, ambayo inaujumbe Fulani katika roho.

Lakini swali la msingi la kujiuliza ni kwanini asionekane kavaa tu vazi lililofika tu miguuni, lakini avae lililofungwa na mshipi?

Kama tulivyotangulia kujifunza, kuwa mshipi unafungwa aidha kiunoni au kifuani.. Bwana Yesu anaon ekana kalijifunga kifuani, Yohana Mbatizaji alijifunga kiunoni.

Mathayo 3:4 “Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na MSHIPI WA NGOZI kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu”.

Na sisi hatuna budi kujifunga mishipi, viunoni mwetu, na Mshipi huo si mwingine Zaidi ya KWELI YA NENO LA MUNGU.

Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, HALI MMEJIFUNGA KWELI VIUNONI, na kuvaa dirii ya haki kifuani”

Tunapojivika utakatifu ambalo ndilo vazi letu refu lifikalo miguuni, (Ufunuo 19:8), na tunapojifunga KWELI YA NENO LA MUNGU KATIKA VIUNO VYA ROHO ZETU, hapo tunakuwa wakamilifu mbele za Mungu, na tunaweza kusimama, kushindana na uovu.

Je Umejifunga Neno la Mungu leo?,

Mfano wa Neno la Mungu ni hili..

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.

Na hili..

Mathayo 22:37 “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote”.

Je Wewe ni Rafiki wa dunia?, kama ndio basi Neno la Mungu hujalifunga kiunoni mwako, na hivyo upo katika hatari,  lifunge leo Neno la Uzima kiunoni mwako, ili uweze kusimama na kushinda katika siku za uovu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Kwanini biblia inaitaja mara kwa mara dhahabu ya Ofiri?

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

Rudi nyumbani

Print this post

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

SWALI: Naomba kufahamu maombolezo ya Hadadrimoni tunayoyasoma katika Zekaria 12:11 ni maombolezo gani hayo?

Zekaria 12:11 “Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido”.


JIBU: Hadadrimoni ni eneo lililokuwa sehemu ya bonde lijulikanalo kama Megido huko Israeli. Bonde hili lilisifika kwa vita, na Zaidi sana kuuawa kwa baadhi ya viongozi wakubwa. Hivyo kupelekea maombolezo makubwa sana kwa watu waliouliwa viongozi wao.

Mfano katika Habari hii, inamlenga mfalme Yosia, ambaye ndiye aliyekuwa tumaini la mwisho la Taifa la Israeli. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka, Yosia alikuwa mfalme aliyemcha Mungu sana kuliko wafalme wote wa Israeli,tukimwondoa Daudi, na  yeye ndiye aliyefanikiwa kuondoa sanamu zote Israeli kipindi kile, Na ndiye mfalme ambaye kuzaliwa kwake kulitabiriwa miaka mingi sana kabla hajazaliwa.

Hivyo waisraeli walimwona kama ndiye tumaini pekee waliobakiwa nalo.

Lakini siku moja alitoka kwenda kupigana vita na mfalme wa Misri aliyeitwa Neko. Na kinyume na matazamio yake, aliuliwa, na mahali alipouliwa palikuwa ni hapo Hadadrimoni katika bonde la Megido.

Israeli nzima iliposikia, ilimwombolezea maombolezo makubwa sana,  taa ya Israeli kuzima ghafla, mpaka wakamwekea kumbukumbuku lake la kila mwaka akumbukwe.

2Wafalme 23:29 “Katika siku zake, Farao-neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana na mfalme wa Ashuru, akafika mto Frati; naye mfalme Yosia akaenda kupigana naye; naye mfalme wa Misri akamwua huko Megido, hapo alipoonana naye”.

2Nyakati 35:25 “Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo”.

Hivyo Mungu akatumia kivuli hicho kueleza jinsi taifa la Israeli litakavyokuja kuomboleza huko mbeleni, siku watakapopewa neema ya kumtambua Kristo. Biblia inasema wayahudi watamwombolezea Yesu waliyemchoma, watalia kama vile mtu aliyefiwa na mwana wake wa pekee, mfano wa pigo la wamisri la kuuliwa wazaliwa wao wa kwanza, jinsi walivyokuwa na maombolezo makuu.

Kama vile, maombolezo ya Yosia katika bonde la Hadadrimoni, Waisraeli walivyombolezea mfalme wao, kwa uchungu mwingi, ndivyo itakavyokuwa siku hiyo watakapomwagiwa neema ya kumtambua Kristo..

Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, KAMA MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI KATIKA BONDE LA MEGIDO.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Ndugu, Kipindi si kirefu hii neema inayochezewa leo hii, itageuka na kuwarudia wayahudi. Kipindi hicho unyakuo utakuwa umeshapita, na Roho Mtakatifu hayupo tena kwetu sisi watu wa mataifa, bali kwa watu wake Israeli. Dunia itastaajabia, kuona watu hawa wametolea wapi moyo huo wa kujuta kwa ajili ya Yesu ambaye leo hii wanamkataa.

Kwani wayahudi hawa wakati huo, biblia inasema watajitenga, familia kwa familia, ukoo kwa ukoo, kila moja atakuwa na maombolezo yake makuu sana haradharani na sirini, kudhihirisha kazi ya Roho Mtakatifu juu yao. Sasa wakati huo ndio Mungu atakuwa anawaandaa ili kuwarudishia  ufalme ambao waliutazamia kutoka kwa masihi wao, sawasawa na lile ulizo la mitume (Matendo 1:6)

Ndugu, ukishaona mabadiliko haya kwa wayahudi, ujue umeshaachwa katika unyakuo, vilevile hii dunia itakuwa na kipindi kifupi sana kisichozidi miaka 7 hadi iishe. Leo hii tumeshaona Israeli imekuwa taifa, wote wamesharudi kwao. Unadhani wanachosubiria ni nini kama sio kurudiwa wakati wowote.

Bwana Yesu alisema,

Mathayo 24:32 “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu”;

Mtini unawakilisha taifa la Israeli (Yer 24), Hivyo tuonapo Israeli leo hii inachipuka, tujue kuwa wakati wa mavuno umeshafika.

Je!, unalitambua hilo? Bado unaipuuzia hii neema ambayo hatuna nayo muda mrefu?. Una Habari kuwa unyakuo ni wakati wowote, na hatua zake tayari zimeshaanza?. Wakati tulionao sasa si wakati wa kubembelezewa wokovu, Injili imeshazagaa kila mahali, watu wote wameshasikia, ni wakati wa kujitakasa, wewe ambaye tayari umeshaokoka. Lakini kama bado upo nje ya neema kipindi hichi? Utakuwa ni wa ajabu kweli.

Unasubiria siku Fulani, neema ikufikie? wakati neema ya wokovu ipo tayari kila mahali, unasubiria ikufikieje tena? Tambua kuwa  njia imeshasonga, na wengi wanatamani waingie wanashindwa, kwasababu upotofu mwingi upo duniani, na wewe bado tu unaisubiri.. Ni kuwa makini sana. Neema inakimbilia Israeli sasa, jicho la Bwana linaelekea kule sasa, kwani muda wetu umeshakwisha.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Neno “Uru” kama lilivyo katika Mwanzo 11:28, lina maana gani?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 11:28 “Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika URU wa Wakaldayo.

29 Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori aliitwa Milka, binti Harani, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.

Neno “Uru”. Maana yake ni ARDHI/HIMAYA.. Kwahiyo hapo biblia iliposema “Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika URU wa Wakaldayo”.. Maana yake ni kwamba “Tera alikufa katika Nchi/Himaya ya Wakaldayo”.

Kulingana na historia zilikuwepo “Uru” nyingi, enzi za kale, zilikuwepo Uru za Waashuri, Uru za Waajemi n.k.. Lakini iliyotajwa kwenye biblia ni moja tu ambayo ni Uru ya wakaldayo. (Kujua Wakaldayo walikuwa ni watu gani fungua hapa >> Wakaldayo)

Lakini kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa Abramu aliambiwa atoke katika  nchi aliyozaliwa “Uru wa Wakaldayo”, aende nchi nyingine.

Ikifunua kuwa Mungu anapomwita mtu anapaswa atoke pale alipo na kwenda sehemu nyingine kiroho.

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

 2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka

 3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”.

Je tangu ulipomwamini Yesu umetoka katika himaya ya ulevi?, umetoka katika himaya za wazinzi?, umetoka katika himaya za wachawi na washirikina, kama bado, ni Dhahiri kuwa bado hujaanza safari ya Wokovu. Anza leo kwa kujitenga na mambo hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

VIPINDI VINNE VYA MAISHA VILIVYO VIGUMU MTU KUMKUMBUKA MUUMBA WAKE.

Nini maana ya mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu huwa anadhihaki watu?

Je Mungu huwa anadhihaki watu kulingana na Mithali 1:26 na Zaburi 59:8?.

Jibu ni ndio!!..Mungu anadhihaki!!.. na sio tu kudhihaki, bali pia anafadhaisha, na vilevile anahuzunisha watu..

Lakini lengo la kudhihaki watu, au kuhuzunisha watu, au kufadhaisha watu ni tofauti na lengo kama tulilonalo sisi..

Sisi tunawadhihaki watu ili tuwakomoe, au ili tuwakomeshe, au ili  tuwatese.. Lakini Mungu lengo lake si hilo, yeye hatudhihaki ili atukomoe, au atukomeshe….Lengo lake yeye ni sisi tutubu, tugeuke, tuone aibu kwa njia zetu mbaya, kisha tutubu na kuacha njia zetu mbaya. Na tukishatubu basi anatufurahisha na kutufariji.

Ndio maana maandiko yanasema..

Mithali 1:23 “GEUKENI KWA AJILI YA MAONYO YANGU; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.

24 Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa; Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;

25 Bali mmebatilisha shauri langu, Wala hamkutaka maonyo yangu;

26 Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, NITADHIHAKI HOFU YENU IFIKAPO”.

Je! Unataka kudhihakiwa na Mungu siku ya msiba wako, au tabu yako..je unataka kuchekwa siku na shida yako?.

Kama hutaki basi jitenge na ulimwengu, na dhambi… Hizo ndizo zinazotuficha uso wa Mungu mbali nasi. Lakini habari njema ni kwamba, Bwana hafurahii misiba yetu, wala tabu zetu, lengo lake ni sisi tuone aibu,  tuache dhambi zetu… ili atupe faraja na furaha.

Maombolezo 3:31 “Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.

32 Maana AJAPOMHUZUNISHA atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.

33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Nini maana ya Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma?

JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Rudi nyumbani

Print this post

Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?

SWALI: Shalom… Pastor naomba kuuliza je ni sahihi mtumishi kuongoza kanisa hajafunga ndoa? na anaweza kubatiza washirika? Amina.


JIBU: Kigezo cha mtu kuwa Kiongozi wa kanisa, na kufanya kazi zote za madhabahuni, ikiwemo kubatiza, kuwawekea watu mikono ya utumishi, n.k. vimetolewa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7

1 Timotheo 3 : 1-16

1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.

Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa, Hivyo yeyote anayelichunga kanisa, awe ni mchungaji, mwalimu, Mtume, maana yeye ndio mwangalizi basi vigezo hivyo vinamuhusu.

Lakini katika vigezo hivyo vyote, hakuna hata kimoja, kinachosema, ni lazima aoe.. Isipokuwa anasema Askofu ni lazima awe ni mume wa mke mmoja..Akiwa na maana kwamba ikiwa ni mwana-ndoa basi, anapaswa awe ni mume wa mke mmoja, na si Zaidi, kama anao wake wawili au watatu, tayari ameshakidhi vigezo vya kutostahili kuitwa mchungaji.

Lakini ikiwa ni mtu ambaye, hajaoa lakini ameshika vigezo vyote, hivyo, yaani, ni mtu asiyelaumika, si mlevi, mpole, si mpenda fedha, aliyeshuhudiwa na watu ni mwema, amekomaa kiroho. Basi huyo anavigezo vyote vya kuwa mchungaji, au kiongozi yoyote wa kanisa.

Mtume Paulo hakuwa ameoa, lakini alikuwa ni mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia, na mataifa mengine, Na Zaidi sana yeye ndiye aliyetoa mwongozi wa mafundisho ya ndoa.

Hivyo kuoa/ kutokuoa, si takwa, la kuwa askofu.

Kinyume chake mtume Paulo,alishauri  watu wote wawe kama yeye (yaani wasioe), kwasababu watu wasiooa inawapa wigo mpana wa kumtumikia Mungu bila kuvutwa na mambo mengine, ikiwa wamemaanisha kweli kujikita kwa Bwana.

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.

Lakini ikiwa huwezi kuishi Maisha hivyo, kwa jinsi ulivyoitwa, basi hakikisha unatumika kiuaminifu, hapo utakuwa umekidhi vigezo vya kulichunga kundi , kubatiza, n.k.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ndoa na Talaka

Ndoa ya serikali ni halali?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Uvuvi bora hauchagui wa kuvua.

Askofu na mchungaji mkuu ni nani?

WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.

Rudi nyumbani

Print this post

Wayebusi walikuwa ni watu gani?

Wayebusi walikuwa ni “wana wa Kaanani”. Kujua Wakaana walikuwa ni watu gani unaweza kufungua hapa >> Wakaanani.

Lakini Watoto wa Kaanani ndio walikuwa hawa “Wayebusi”. Hivyo Wayebusi hawakuwa kabila kubwa, ukilinganisha na Kaanani, baba yao, na waliishi katika sehemu ndogo tu ya nchi ya Kaanani.

Mwanzo 10:15 “Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,

16 na MYEBUSI, na Mwamori, na Mgirgashi ”.

Wayebusi kama walivyokuwa Wakaanani na Wahivi, na Wahiti, walikuwa ni watu wanaoabudu miungu, na kufanya mambo ambayo yalikuwa ni machukizo mbele za Bwana, kwani walikuwa wanafanya uchawi, wanaloga, wanawapitisha wana wao kwenye moto kama sadaka kwa miungu yao n.k

Kumbukumbu 18:9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.

10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.

12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.

14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo”.

Kutokana na machukizo hayo, Mungu aliwaondoa katika nchi ya Kaanani, kama alivyowaondoa wakaanani wenyewe Pamoja na Wahivi na Wahiti.

Lakini hata baada ya kuondolewa na Yoshua, walisalia wachache waliokaa katika baadhi ya miji..na mojawapo ya mji waliokuwa wanakaa ni Yerusalemu.

Yoshua 15:63 “Tena katika habari ya Wayebusi, hao wenye kukaa Yerusalemu, wana wa Yuda hawakuweza kuwatoa; lakini hao Wayebusi walikaa pamoja na wana wa Yuda huko Yerusalemu hata hivi leo”.

Mji wa Yerusalemu hapo kwanza, kabla haujaitwa Yerusalemu, ulikuwa unaitwa YEBUSI, kufuatia jina la hawa Wayebusi, na ulikuwa unakaliwa na hawa Wayebusi, lakini baadaye kipindi cha wafalme, Daudi alikuja kuutwaa na kuwaondoa katika mji huo na kuuita Yerusalemu..

Waamuzi 19:10 “Lakini huyo mtu hakukubali kukaa usiku huo, ila akainuka, akaenda zake, akafika mkabala wa Yebusi (huo ndio Yerusalemu); nao walikuwako pamoja naye punda wawili waliotandikwa; suria yake naye alikuwa pamoja naye”.

2Samweli 5:6 “Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia humo”.

Jamii ya Wayebusi, sasa haipo tena, imepotea kabisa..Na Bwana ndiye aliyeipoteza, kutokana na Machukizo waliyokuwa wanayafanya!.

Na kama maandiko yanavyosema, Bwana Mungu ni yule yule, jana, leo na hata milele, habadiliki..Maana yake ni kwamba aliyokuwa anayachukia enzi hizo ndiyo anayoyachukia mpaka leo. Kama aliwatowesha Wayebusi na wakaanani, basi atawatowesha pia watu wafanyayo hayo, katika siku za mwisho.

Na nyakati hizi za mwisho, maasi yamekuwa makubwa kuliko hata waliokuwa wanayafanya Wayebusi na Wakaanani.

Hadi leo watu wanaua Watoto wao, (kwa kutoa mimba na kafara), hadi leo watu wanafanya uchawi na ushirikina n.k, mambo hayo ndio yanayotujulisha kuwa tunaishi katika siku za Mwisho, na ghadhabu ya Mungu inakaribia kumwagwa duniani kote.

Lakini hekima ya Mungu inatuonya tutoke katika vifungo vya dhambi, kwa kumpokea Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, na kubatizwa kwa jina lake na kwa Roho wake, ili tuokoke na ghadhabu ijayo.

Matendo 2:40 “Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Wakaanani walikuwa ni watu gani?

Wahiti ni watu gani?

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

Ni wayahudi wa aina gani wanaotajwa kuwa sinagogi la shetani? (Ufunuo 2:9, Ufunuo 3:9)

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Rudi nyumbani

Print this post