Jibu: Tusome,
Wafilipi 2:1 “Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako MATULIZO YO YOTE YA MAPENZI, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, 2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja”.
Wafilipi 2:1 “Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako MATULIZO YO YOTE YA MAPENZI, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,
2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja”.
Mapenzi yanayozungumziwa hapo ni ule Upendo wa Kristo kwetu, Matulizo ya mapenzi yanayonenwa hapo sio matulizo ya mapenzi ya mwili, bali ni Matulizo ya mapenzi ya KRISTO, (Yaani ile hali ya kupata pumziko ndani ya Pendo la Kristo).
Tunapomfahamu Yesu, na jisni anavyotupenda kwa kiwango anachotaka yeye tumfahamu….basi tunapata pumziko kubwa sana na utulivu mkubwa sana ndani ya roho zetu… (roho zetu zinatulia na kuwa na amani).
Biblia (Neno la Mungu) linasema..
Warumi 8:38 “Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Warumi 8:38 “Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.
Ukishajua kuwa hakuna Malaika yoyote anayeweza kumfanya Kristo akaacha kukupenda wewe baada ya kumuamini, ni lazima utapata Pumziko na utulivu ndani yako.
Ukishajua kuwa hakuna mwenye mamlaka yoyote duniani, awe kiongozi wa nchi au dunia, ambaye anaweza kumfanya Kristo akaacha kukupenda wewe, basi unapata utulivu ndani yako.
Ukishajua kuwa hakuna kiumbe chochote kilichopo duniani, au chini ya dunia..kitakachoweza kumfanya Kristo akakuchukia basi unapata Pumziko na utulivu usio wa kawaida. Unakuwa huangaiki tena..
Unapojua kuwa siku ile ulipomwamini Kristo, tayari dhambi zako zilifutwa, katika ulimwengu wa roho ulihamishwa kutoka katika nguvu za giza na kuingizwa katika Pendo hilo la Kristo.. basi unapata amani, utulivu na pumziko ndani yako.
Sasa pumziko hilo, na utulivu huo unaoupata kutokana na upendo wa Kristo kwako, ndio unaoitwa MATULIZO YA MAPENZI.
Nabii Isaya alilion Pendo la Yesu miaka mingi sana kabla ya kuja kwake, aliona Yerusalemu inakwenda kufarijiwa, mapigo yake ambayo Bwana alimwadhibu kutokana na dhambi zake, yanakwenda kuponywa, hofu yake inakwenda kuondolewa na Masihi ambaye atakuja.(na Yerusalemu itapokea Matulizo makubwa)..
Isaya 40:1 “Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu, asema Mungu wenu. 2 Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa Bwana adhabu maradufu kwa dhambi zake zote”.
Isaya 40:1 “Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa Bwana adhabu maradufu kwa dhambi zake zote”.
Je Umeyapata Matulizo ya Mapenzi leo?. Umetulizwa na Bwana Yesu, au unataabishwa na shetani?.
Kama hujampokea Yesu, basi huna utulivu ndani yako..wachawi watakusumbua, mapepo yatakusumbua, na vile vile hofu ya mauti itakusumbua. Hivyo mpokee Yesu leo, upate pumziko ndani yako.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami NITAWAPUMZISHA. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami NITAWAPUMZISHA.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?
JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.
TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:
Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?
Furaha ni nini?
Rudi nyumbani
Print this post
Huduma hizi 5 tunazisoma katika kitabu cha Waefeso..
Waefeso 4:11 “Naye alitoa wengine kuwa MITUME, na wengine kuwa MANABII; na wengine kuwa WAINJILISTI na wengine kuwa WACHUNGAJI na WAALIMU”.
Na madhumuni ya Bwana Yesu kuziweka huduma hizi tano (5), kama huduma za Uongozi katika kanisa ni kama mstari wa 12, unavyosema..
Tusome tena..
Wafeso 4:11 “naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; 12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa kristo ujengwe”.
Wafeso 4:11 “naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa kristo ujengwe”.
Kumbe lengo la kwanza ni “KUWAKAMILISHA WATAKATIFU”, na pili ni “KAZI YA HUDUMA ITENDEKE”, na tatu “MWILI WA KRISTO UJENGWE”. Na sio ili Kuwaharibu watakatifu, au kujitafutia utajiri, au Umaarufu.
Mtu yeyote anayejiita mtumishi wa Mungu, kama hayo Maono matatu hayapo ndani yake, basi ni mtumishi wa shetani!
Sasa tuangalie kwa ufupi kazi za Hizi huduma tano.. Zinashirikianaje kuujenga mwili wakristo, na kuwakamilisha watakatifu.
1. MITUME
Mitume kama jina lake lilivyo “ni watu waliotumwa”.. na kama wametumwa maana yake kuna aliyewatuma, na aliyewatuma ni lazima kawapa ujumbe.
Kwahiyo wahasisi wa Imani ya kikristo wa kwanza kabisa ni Mitume, Na mitume hao ni wale 11 pamoja na Mathiya wa 12. Hao ndio waliotumwa wa kwanza, kuitangaza Imani ya kikristo, kwa watu wote.
Lakini bado hao pekee wasingetosha kuitangaza Imani duniani kote, Hivyo Bwana Yesu alinyanyua Mitume wengine tofuati na hao 12, ambao ndani yake ndio akina Paulo na wengineo.
Hawa waliipeleka Imani ya kikristo duniani kote.
Na sio tu kulipeleka Neno la Mungu bali pia, kupanda Makanisa. Ndio maana utaona Mtume Paulo alipanda makanisa mengi sana, maeneno ya Galatia na Makedonia.
Na hata sasa Bwana anao mitume wake ambao anawatuma kuitangaza Imani ya kikristo mahali ambapo haijasikiwa kabisa, na vile vile kupanda makanisa ya Kristo, na si makanisa yao wenyewe.
2. MANABII
Manabii ni kundi lingine la watu ambalo Bwana anawaweka ndani ya Kanisa. Hawa kazi yao ni kulijenga kanisa kwa kutoa jumbe za Faraja na maonyo kutoka kwa Mungu moja kwa moja, na jumbe hizo ni kwaajili ya kulifariji kanisa na kulionya kwa mambo yanayoendelea au yanayokuja.
Kwamfano katika biblia, agano jipya tunamwona Nabii mmoja aliyeitwa Agabo, ambaye Bwana alikuwa anazungumza naye na kumpa jumbe za kulionya kanisa juu ya mambo yanayokuja..
Matendo 11:27 “Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia. 28 Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio. 29 Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi. 30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli”.
Matendo 11:27 “Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia.
28 Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio.
29 Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi.
30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli”.
Umeona hapo?.. Manabii kazi yao ilikuwa ni kutoa taarifa za mambo yajayo na kuyaambia makanisa, kwa faida ya kanisa.. na kwa kujitakia umaarufu wao, wala kutaka fedha kutoka kwa watu.
Hapo taarifa za unabii huo, zilipofika kwa makanisa yote, ndipo kila mtu akajiandaa kwa akiba ya kutosha.. Huoni hapo kanisa limejengeka?..lakini leo kuna manabii ambao hawaoni mambo yanayokuja lakini wanaona mifuko na pochi za watu. Na Zaidi ya yote hawawafundishi watu utakatifu bali mafanikio tu! (hawa ndio manabii wa uongo waliotabiriwa kuja katika siku za mwisho).
Lakini Pamoja na kuwepo na jopo kubwa la manabii wa uongo, wapo pia manabii wa kweli, kwasababu Roho Mtakatifu wa kweli bado yupo duniani na anatenda kazi.
3. WAINJILISTI.
Wainjilisti ni kundi lingine Bwana aliloliweka katika kanisa kwa lengo la kuwavuta watu katika Imani ya Kikristo, likitumia maandiko kumthibitisha Yesu Kristo ni Njia, kweli na Uzima. Vyombo hivi Bwana kaviweka maalumu kuvunja mapando ambayo yamepandwa na adui shetani ndani ya vichwa vya watu kuhusu Ukristo. Hivyo kupitia wainjilisti, watu wengi ambao, hawakuuelewa vizuri ukristo, au wamefundishwa isivyopaswa kuhusu Yesu, wanafunguka.
Mfano wa Wainjilisti katika biblia ni mtu mmoja aliyeitwa Apolo. Huyu alivunja misingi ya elimu za giza zilizokuwa zimepandwa ndani ya vichwa vya watu..
Matendo 18:23 “Hata akiisha kukaa huko siku kadha wa kadha akaondoka, akapita kati ya nchi ya Galatia na Frigia, mji kwa mji, akiwathibitisha wanafunzi. 24 Basi Myahudi mmoja, JINA LAKE APOLO, mzalia wa Iskanderia, MTU WA ELIMU, akafika Efeso; NAYE ALIKUWA HODARI KATIKA MAANDIKO. 25 Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; NA KWA KUWA ROHO YAKE ILIKUWA IKIMWAKA, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu. 26 Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi. 27 Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu. 28 Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo”.
Matendo 18:23 “Hata akiisha kukaa huko siku kadha wa kadha akaondoka, akapita kati ya nchi ya Galatia na Frigia, mji kwa mji, akiwathibitisha wanafunzi.
24 Basi Myahudi mmoja, JINA LAKE APOLO, mzalia wa Iskanderia, MTU WA ELIMU, akafika Efeso; NAYE ALIKUWA HODARI KATIKA MAANDIKO.
25 Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; NA KWA KUWA ROHO YAKE ILIKUWA IKIMWAKA, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu.
26 Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.
27 Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu.
28 Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo”.
Na tabia ya Wainjilisti ni kutokukaa sehemu moja, kwasababu Bwana ameweka ndani yao, roho ya kuhubiri, kama Apolo.
Na Wainjilisti wa kweli si wapenda fedha, wala wanaopenda umaarufu wala fasheni za kidunia. Wainjilisti wa kweli, ni wale wanaougua wanapoona watu wanafundishwa vitu visivyo sahihi kimaandiko kama Apolo.
4. WACHUNGAJI
Wachungaji ni kundi lingine ambalo Bwana ameliweka ndani ya kanisa, kwa lengo la kulichunga kundi (kanisa). Baada ya mtu kuamini kutokana na injili ya mitume au wainjilisti, hana budi kukaa katika ushirika wa kanisa. Na atakapokuwa katika kanisa hana budi kuchungwa kama vile kondoo.
Sifa za wachungaji wa kweli ni zile zile za Uaskofu zinazotajwa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7, kwamba asiwe mtu wa kupenda fedha, asiyekuwa mlevi,mwenye kuitunza nyumba yake vyema, na mwenye ushuhuda mzuri katikati ya watu.
Katika enzi za kanisa la kwanza wachungaji wa ukweli walikuwa ni wengi kuliko wa uongo, lakini katika siku hizi za mwisho, wachungaji wa uongo ni wengi kuliko wa ukweli, na hiyo yote ni kwasababu tunaishi katika siku za mwisho sawasawa na unabii, na siku yoyote Parapanda inalia.
5. WAALIMU
Hili pia ni kundi lingine Bwana Yesu aliloliweka ndani ya kanisa. Lengo kuwepo Waalimu ni kulifundisha Neno la Mungu, kwa watu walio makanisani. Waalimu wanakuwa na uwezo wa kufundisha, na kumfanya mtu aelewe, kama tu walimu wa elimu za kidunia walivyo. Lengo ni ili wakristo wajae ambayo Bwana anayahitaji..
Na siku hizi za mwisho waalimu wa uongo ni wengi, kuliko wa kweli. Kwasababu ile ile ya kuwa tunaishi katika siku za mwisho. Sifa kuu ya Waalimu wa Uongo ni kuhubiri mambo ya ulimwengu huu na kupenda fedha na mambo ya kiulimwengu.
Kwa hitimisho ni kuwa Roho Mtakatifu yupo mpaka sasa, na Mitume wa ukweli, Manabii wa ukweli, Wainjilisti wa ukweli, Wachungaji wa ukweli na Waalimu wa Ukweli, mpaka leo Bwana amewaweka katika makanisa yake.
Na pia karama huduma hizi zinaingiliana, kuna Mtu anaweza kuwa Mtume na pia akawa Mwinjilisti, hali kadhalika mwingine anaweza kuwa Mchungaji na akawa Mwalimu pia, na mwingine anaweza kuwa Mtume na kuwa mwalimu kama Mtume Paulo (1Timotheo 2:7), ndio maana utaona Mtupe Paulo, katoa mafundisho mengi sana katika nyaraka zake..na kwasababu alikuwa Mtume na hapo hapo Mwalimu.
Lakini kamwe hatupaswi kujisifia karama wala huduma tulizonazo, kwasababu Roho Mtakatifu hajavitoa vipawa hivyo kwa lengo la kutufanya sisi tuwe maarufu, au tuonekane wa tofauti..bali kwa lengo la kulijenga kanisa, na kuwakamilisha watakatifu.
Hekima ya Mungu ni kuu, sana. Na Bwana ni mzuri sana. Je! Umempokea Bwana Yesu, na kubatizwa? Na kupokea Roho Mtakatifu? Kama bado unasubiri nini?..kumbuka hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi.
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?
AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.
Kusemethi au kusemethu ni nafaka inayokaribia kufanana sana na Ngano kimwonekano na kiladha. Nafaka hii ni familia moja na nafaka ya Ngano.
Miaka ya zamani kabla ya Kristo, nafaka ya Kusemethi ndiyo iliyokuwa inatumika kama nafaka kuu ya kutengenezea mikate, Zaidi hata ya Ngano, lakini baada ya Kristo, Nafaka ya Ngano, ilianza kukubalika Zaidi duniani kote na kupata nguvu duniani kuliko Kusemethi. Kiasi kwamba mpaka kufikia leo hii ukitaja nafaka ya Kusemethi hakuna hata mtu anayeijua.
Ngano leo imepata nguvu kuliko Kusemethi, kama vile mafuta ya Alizeti, yalivyo na nguvu kuliko mafuta ya Mawese. Lakini Pamoja na hayo bado yapo maeneo machache ya dunia (Sehemu za Ulaya), wanalima Kusemethi na kuitumia kutengenezea mikate na vyakula vingine.
Katika biblia tunaona nafaka hii ikitajwa mara kadhaa, sehemu ya kwanza tunaona ikitajwa kipindi wana wa Israeli, wanaondolewa Misri na Bwana.
Kutoka 9:29 “Musa akamwambia, Mara nitakapotoka mjini nitamwinulia Bwana mikono yangu; na hizo ngurumo zitakoma, wala haitanyesha mvua ya mawe tena; ili upate kujua ya kuwa dunia hii ni ya Bwana. 30 Lakini, wewe na watumishi wako, najua ya kuwa ninyi hamtamcha Bwana Mungu bado. 31 Kitani na shayiri zilipigwa; maana shayiri zilikuwa na masuke na kitani zilikuwa katika kutoa maua. 32 Lakini ngano na KUSEMETHU hazikupigwa; maana, zilikuwa hazijakua bado”
Kutoka 9:29 “Musa akamwambia, Mara nitakapotoka mjini nitamwinulia Bwana mikono yangu; na hizo ngurumo zitakoma, wala haitanyesha mvua ya mawe tena; ili upate kujua ya kuwa dunia hii ni ya Bwana.
30 Lakini, wewe na watumishi wako, najua ya kuwa ninyi hamtamcha Bwana Mungu bado.
31 Kitani na shayiri zilipigwa; maana shayiri zilikuwa na masuke na kitani zilikuwa katika kutoa maua.
32 Lakini ngano na KUSEMETHU hazikupigwa; maana, zilikuwa hazijakua bado”
Vile vile tunaona ikitajwa katika kitabu cha Ezekieli.
Ezekieli 4:9 “Pia ujipatie ngano, na shayiri, na kunde, na dengu, na mtama, na KUSEMETHI, ukavitie vyote katika chombo kimoja, ukajifanyie mkate kwa vitu hivyo; kwa kadiri ya hesabu ya siku utakazolala ubavuni mwako; yaani, siku mia tatu na tisini utaula”.
Unaweza kusoma pia Isaya 28:23, utaona nafaka hiyo ikitajwa..
Kama kuna baadhi ya Mazao na vyakula vilivyokuwa vinakubalika zamani za kale, lakini leo hii vinaonekana havina thamani yoyote..vile vile vitu vingine vyote siku moja vitapita na kuwa si kitu, lakini wamtumainio Bwana watadumu milele.
1Yohana 2:17 “Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, BALI YEYE AFANYAYE MAPENZI YA MUNGU ADUMU HATA MILELE”. Zaburi 125:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele. 2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, NDIVYO BWANA ANAVYOWAZUNGUKA WATU WAKE, TANGU SASA NA HATA MILELE”.
1Yohana 2:17 “Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, BALI YEYE AFANYAYE MAPENZI YA MUNGU ADUMU HATA MILELE”.
Zaburi 125:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.
2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, NDIVYO BWANA ANAVYOWAZUNGUKA WATU WAKE, TANGU SASA NA HATA MILELE”.
Je na wewe unamtumainia Bwana? Au ulimwengu?..
Maran atha.
Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)
Masuke ni nini? (Luka 6:1, Marko 4:28)
Uga ni nini? Na kazi yake ni ipi kibiblia?
Bisi ni nini? (Walawi 23:14, Ruthu 2:14)
YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.
Ijumaa kuu ni ijumaa ya mwisho kabisa ya Bwana wetu Yesu Kristo kuwepo hapa duniani, ni siku ile ambayo alipitia mateso mengi, na kusulibiwa, na kufa na kisha kuzikwa. Siku hii huadhimishwa na wakristo wengi ulimwengu, kama kukumbuka la mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo kila mwaka.
Lakini swali ni kwanini iitwe ijumaa kuu na sio ijumaa ya mateso au ya huzuni? Kwanini iwe kuu? Wakati siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya sana ya mamlaka ya giza, ya huzuni na masumbufu ya Yesu mwokozi wetu?
Ni kweli kwa jicho la nje! Ni siku isiyo nzuri, lakini kwa jicho la Roho ni siku ya furaha sana tena sana kwetu sisi wanadamu, Kwani ni siku ambayo kwa mara ya kwanza tulifutiwa mashtaka yetu ya hukumu, tangu tulipopoteza uzima pale Edeni. Kwani asingekufa Yesu, tusingepata msamaha wa dhambi.. Hivyo kifo chake, kilileta ukombozi mkuu sana kwetu, na matokeo yake hatupaswi kulia, kinyume chake tufurahie, kwani siku kama ya leo, karibia miaka 2000 iliyopita, tuliwekwa huru…Hivyo ni sahihi kuitwa ijumaa kuu na sio ijumaa ya mateso.
Ni sawa na mfano wa Samaki anayevuliwa, yeye kwa upande wakw kweli atapitia mateso ya kufa, lakini yule anayemvua atafurahia kupata kitoweo. Hivyo tunaweza kusema ni uchungu kwa Samaki lakini furaha kwa mvuvi..
Kifo cha Bwana wetu Yesu kilikuwa ni faida kubwa kwetu, kwasababu kama damu yake isingemwagika, tusingepata ondoleo la dhambi zetu (Waebrania 9:22).
Jibu ni La, desturi ya kutokula nyama (ya wanyama-damu moto), ni pokeo tu la kanisa katoliki, ambao kwa mujibu wao, wanafanya hivyo kwa heshima ya Kristo, kuutoa mwili wake, kama sadaka kwetu, kwasababu nyama ni chakula cha starehe, hawafanyi hivyo ili kuyatafakari mateso ya Bwana, na sio tu katika siku ya ijumaa kuu, bali pia siku ya jumatano ya majivu, pamoja na ijumaa nyingine zote, zinazofuata katika mfungo hawali nyama .
Lakini agizo hilo halipo mahali popote katika maandiko. Kama ukila haufanyi makosa, au usipokula vilevile haufanya makosa.
Jibu ni la!, Biblia haijatupa agizo wala katazo la mtu kuiadhimishi siku Fulani kwa Mungu wake.
Ni kwa jinsi yeye anavyoamini tu!.
Warumi 14:5 “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. 6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu”.
Warumi 14:5 “Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.
6 Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu”.
Hivyo ikiwa wewe hauoni kama siku ya ijumaa kuu inafaida yoyote kwako, basi usimuhukumu yule ambaye anaiadhimisha kwa Mungu wake, lakini pia wewe ambaye unaidhimisha usimuhukumu yule ambaye haiadhimishi. . Ikiwa unaona mfungo huo kwa kipindi hicho cha pasaka hauna maana kwako, hufanyi kosa, lakini pia usimuhukumu yule ambaye anafunga kwa ajili ya Bwana wake aliyemfia msalaba.Ndivyo ilivyo
Shalom.
Easter ni nini?. Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?
PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA PASAKA?
Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)
SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?
Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?
Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3
Swali: Katika Kumbukumbu 28:53, tunaona Mungu anasema watu watakula nyama za wana wao, na uzao wa tumbo lao, je alikuwa anamaanisha nini kusema hivyo?.
Kumbukumbu 28:53 “Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa BWANA, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako”.
Ukisoma kuanzia juu mstari wa kwanza wa sura hiyo ya 28, utaona baraka ambazo Mungu aliwaahidia wana wa Israeli endapo wataenda katika sheria zake na amri zake..kwamba watabarikiwa mjini na vijijini, hali kadhalika watabarikiwa waingiapo na watokapo..na zaidi sana uzao wa matumbo yao utabarikiwa.
Kumbukumbu 28:1 “Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako. 3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. 4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Kumbukumbu 28:1 “Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.
3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.
4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Lakini ukizidi kusogea mbele katika mstari wa 15, Utaona Mungu anatoa tahadhari na ole kwa hao hao Israeli kama endapo watamwacha na kwenda kuabudu miungu mingine, na kuzivunja amri zake, basi watakumbana na laana nzito.
Na mojawapo ya laana hizo waliambiwa kuwa watakula nyama za watoto wao kutokana na njaa Bwana atakayowapiga nayo.
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani…………. 49 BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake; 50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; 51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza. 52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa BWANA, Mungu wako. 53 NAWE UTAKULA UZAO WA TUMBO LAKO MWENYEWE, NYAMA YA WANA WAKO NA BINTI ZAKO aliokupa BWANA, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako”.
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani………….
49 BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;
50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana;
51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa BWANA, Mungu wako.
53 NAWE UTAKULA UZAO WA TUMBO LAKO MWENYEWE, NYAMA YA WANA WAKO NA BINTI ZAKO aliokupa BWANA, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako”.
Sasa unaweza kuuliza jambo hilo lilitimia lini?..kwamba wana wa Israeli walifikia hatua ya kula nyama za watoto wao.
Kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuna wakati Israeli ilimwacha Mungu, na matokeo ya kumwacha Mungu..Bwana akaruhusu jeshi la Shamu liwazunguke…na kwa hofu ya jeshi hilo kubwa, wana wa Israeli walijifungia ndani ya mji..(kumbuka miji ya zamani ilikuwa inazungushiwa ukuta pande zote). Hivyo mlango wa mji ukifungwa hakuna mtu anayeweza kuingia wala kutoka.
Kwahiyo Israeli walijifungia mjini kwa kipindi kirefu kwa hofu ya jeshi la washami lililopo nje.
Na matokeo ya kujifungia ndani kwa muda mrefu ni chakula kuisha ndani, na kuanza kufikiria kula mavi ya njiwa na kula wanyama wasiolika, ilifikia hatua kichwa cha punda kinaauzwa kwa fedha nyingi sana.
Na njaa ilipozidi watu wakaanza kula watoto wao, mpaka taarifa zikamfikia mfalme za wanawake wawili waliokuwa wanagombania kula nyama za watoto wao.
Tusome,
2 Wafalme 6:24 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. 25 Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. 26 Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. 27 Akasema, BWANA asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? 28 Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, MTOE MTOTO WAKO, TUMLE LEO, NA MTOTO WANGU TUTAMLA KESHO. 29 Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake. 30 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake”.
2 Wafalme 6:24 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria.
25 Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha.
26 Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme.
27 Akasema, BWANA asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni?
28 Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, MTOE MTOTO WAKO, TUMLE LEO, NA MTOTO WANGU TUTAMLA KESHO.
29 Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.
30 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake”.
Umeona?..Mungu kamwe hasemi uongo!..alisema siku watakayomwacha watakula watoto wao, na kweli ikatokea hivyo hivyo kama alivyosema siku walipomwacha na kuzivunja amri zake…walikula nyama za watoto wao waliowazaa wenyewe. (Unaweza kusoma pia Yeremia 19:9, Maombolezo 4:10, na Ezekieli 5:10).. utaona jambo hilo hilo.
Hiyo inatufundisha nini?
Inatufundisha kuwa maneno ya Mungu kamwe hayapiti..aliposema watu watakula nyama za watoto wao ni kweli ilitokea…hali kadhalika anaposema kuwa wazinzi na waasherati na waabudu sanamu hawataurithi uzima wa milele kwasababu wamemkataa yeye…basi neno hilo litatimia kama lilivyo na wala hasemi uongo..
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.
Na sio tu hasara ya kuukosa ufalme wa mbinguni, bali hata maisha ya mtu aliyemkataa Mungu akiwa hapa duniani, yatakuwa ni ya tabu tu siku zote, hatakuwa na furaha wala amani, hatafanikiwa wala kuwa na tumaini, na atakufa na kumbukumbu lake litasahauliwa.
Je umempokea Yesu?.
Kama bado ni nini unachosubiri? Kumbuka unyakuo wa kanisa upo karibu wakati wowote parapanda ya mwisho inalia na watakatifu watanyakuliwa, wewe ambaye hujaokoka.lwo hii utakuwa wapi siku hiyo??..au wewe uliye vuguvugu leo, siku ile utakuwa mgeni wa nani?.
Bwana akubariki.
Maran atha!.
WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:
Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?
Zile Rangi saba za Upinde wa Mvua zinawakilisha nini?
Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.
Mtu ni kiumbe cha kwanza kilichoumbwa na Mungu duniani, chenye mfano wake na sura yake, kilichoumbiwa utashi na ujuzi ndani yake, kilichotofautishwa na wanyama wote na viumbe vyote vilivyoumbwa na Mungu duniani Ndicho kinachoitwa mtu.
Tunasoma hilo katika,
Mwanzo 1:26
[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Lakini jina Binadamu/mwanadamu, ni neno lililozuka kufuatana na jina la mtu wa kwanza aliyeitwa Adamu.
Jina hilo alipewa na Mungu..Hivyo watu wote waliozaliwa na yeye waliita “wana wa Adamu”kwa kifupi “wanadamu” ambapo jina hilo kwa kiharabu linatamkwa “bin-Adam” ambapo sisi tunatamka “Binadamu”
Lakini ni mtu yule yule..isipokuwa asingeweza kuitwa binadamu siku ile ya kwanza alipoumbwa kwasababu alikuwa bado hajapewa jina, na pia halikuwa hana baba wa mwilini.
Ni sawa na Neno mwebrania na mwisraeli… kabla ya Yakobo kubadilishwa jina lake wana wote wa Ibrahimu hata Ibrahimu mwenyewe aliitwa Mwebrania..(Mwanzo 14:13)
Lakini Yakobo alipobadilishwa jina na kuitwa Israeli, utaona uzao wake wote baada ya pale ulizoeleka na kuitwa waisraeli mpaka leo. Lakini bado mahali pengine waliendelea pia kuitwa waebrania kwa asili yao.
Ndivyo ilivyo kwa mtu na mwanadamu. Ni yule yule kulingana na majira.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?
Uru wa Ukaldayo ni nini?
MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.
Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).
Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?
Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?
Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?
Jibu: Pasaka ni sikukuu ya kiyahudi, ambayo ilianza kuadhimishwa kipindi wana wa Israeli wanatoka nchi ya Misri, wakati ambao Mungu aliwaambia wapake damu ya mwanakondoo katika miimo ya nyumba zao ili Yule Malaika atakapopita asiweze kuwadhuru wazaliwa wao wa kwanza, Hivyo Yule malaika alipopita na kuikuta ile damu ya mwanakondoo katika miimo ya nyumba zao, alipita juu, (maana yake hakuingia katika hiyo nyumba kuua wazawaliwa wa kwanza).
Sasa kitendo hicho cha Malaika kupita juu, ndicho kinachoitwa Pasaka, (kwa lugha kiingereza “passover”). Kwa maelezo marefu kuhusu pasaka na umuhimu wake, na kama inaruhusiwa kusheherekewa mpaka sasa na sisi wakristo, fungua hapa >>PASAKA IPO KIBIBLIA?
Lakini swali lingine ni kuhusu Easter? Je Easter ni nini?, je ipo kwenye biblia? na je sisi wakristo tunaruhusiwa kuiadhimisha easter?.
Jibu: Neno Easter, halipatikani mahali popote katika biblia, kama jinsi pasaka linavyopatikana katika sehemu nyingi, katika biblia (Easter lenyewe halipo kabisa).
Sasa Easter kama haipo imetoka wapi katika Ukristo?
Asili ya Easter, ni mungu wa kipagani (wa kike), aliyeaminika kuleta “uzao” kama vile “baali” alivyokuwa.. mungu huyu aliabudiwa na jamii za watu wa Saxons, ambao kwasasa ni maeneo ya Ujerumani, na aliitwa “easter” kutokana na “mawio ya jua”. Upande jua linapochomoza, uliaminika kuwa ni upande wa neema na ndio unaomstahili huyu mungu mke, hivyo upande wa mashariki ni “East” kwa lugha ya kiingereza, kwahiyo kwa heshima ya mungu huyo wa uzao ndio wakamwita “easter”..yaani “wa mashariki”.
Na mungu huyu “easter” alikuwa anatolewa sadaka za kafara kipindi kile kile cha sikukuu za pasaka za kiyahudi, tarehe hizo zilikuwa zinagongana, kipindi ambacho Wayahudi wanasheherekea pasaka, ndio kipindi ambacho watu hao wa-Saxons na wengine wengi walikwenda kumtolea mungu wao huyo easter sadaka.
Kwasababu ni kawaida ya shetani kutafuta kuchanganya ukristo na upagani, alinyanyua watu kadhaa na kuoanisha siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu, na siku ya sadaka za mungu huyo “easter”. Hivyo ili desturi na kumbukumbu la mungu wao huyo “easter” lisife kabisa kabisa, ndipo wakaiita ile jumapili ya kufufuka kwa Bwana kama “jumapili ya easter”.
Sasa swali ni je! Na sisi wakristo tunaruhusiwa kuadhimisha easter kama sherehe ya kufufuka kwa Bwana Yesu?
Siku ya kufufuka Bwana Yesu, itabaki pale pale, na ni vizuri kuiadhimisha, kwasababu ni siku ya ushindi wetu, siku ya matumaini, na siku ya Shangwe, Mitume na watakatifu wote, kipindi wamejifungia ndani kwa hofu ya wayahudi, siku walipomwona Bwana kafufuka walifurahi furaha kuu.
Luka 24:34 “wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni. 35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate. 36 Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu. 37 Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho. 38 Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? 39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo. 40 Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake. 41 BASI WALIPOKUWA HAWAJAAMINI KWA FURAHA, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa?”.
Luka 24:34 “wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.
35 Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.
36 Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.
37 Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho.
38 Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?
39 Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo.
40 Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake.
41 BASI WALIPOKUWA HAWAJAAMINI KWA FURAHA, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa?”.
Hivyo na sisi hatuna budi kuiadhimisha siku hiyo kwa furaha nyingi, katika siku ile ile Bwana aliyofufuka, (yaani Jumapili ya pasaka), haijalishi watu wanaiitaje hiyo siku, watu wameipa jina gani, hata kama wangekuwa wameipa jina la “siku kumwabudu shetani” sisi hatutazami majina watu walioyapa siku, (tunaitazama siku yenyewe).. hata siku tulizozaliwa tukizifuatilia katika historia tutakuta zimepewa majina ya ajabu ajabu, lakini wau hawaachi kuziazimisha kisa tu zimepewa majina ya ajabu, au zimeangukia katika tarehe za kuadhimisha mambo mabaya..
Leo ukifuatilia katika historia au kumbukumbu, utakuta kila tarehe imengukia katika maandimisho fulani ya sikukuu za kipagani, hivyo hatuwezi kuacha kufanya mambo ya msingi katika hizo siku, na kuzifuata kalenda za kipagani.
Kwahiyo sisi wakristo tunasheherekea siku ya kufufuka kwa Bwana kama “jumapili ya ushindi” na si kama “easter”. Na hatusheherekei kipagani.
Siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu, tunapoiadhimisha kwa kwenda Bar, kulewa hapo tumeisheherekea easter, na si siku ya kufufuka kwa Bwana, siku ya jumapili ya kufufuka kwa Bwana tunapoisheherekea kwa kwenda disko, au kwenye kumbi za anasa, hapo tutakuwa tunamwadhimisha mungu “easter” na si “ufufuo wa Bwana”. Kwasababu waliokuwa wanamwadhimisha huyo mungu mke easter, katika siku hiyo walikuwa wanalewa na kucheza kipagani na kumtolea sadaka.
Lakini sisi wakristo hatuadhimishi/kusheherekea siku hiyo kipagani hivyo, bali siku ya kufufuka kwa Bwana ni siku ya kufanya ibada, ni siku ya kutafakari maisha yetu ya ukristo, tangu tumempokea Yesu mpaka sasa tumeshapiga hatua kiasi gani?..na kama tumerudi nyuma basi tutengeneze mambo yetu, ni wakati wa kutafakari ni mambo yako mangapi mazuri ya kiroho, yaliyokuwa yamekufa, na je yamefufuka!.. Kama bado ni wakati wa kutafuta kuyafufua.
Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?
Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”
Sharoni ni nini au ni wapi kibiblia?(1Nyakati 5:16)
SHUSHANI NGOMENI NI WAPI KWA SASA?
WhatsApp
SWALI: Naomba kufahamu Zaburi 102:6 inamaana gani? Mwandishi anaposema..
Zaburi 102:6
[6]Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.
[6]Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,
Na kufanana na bundi wa mahameni.
Mwari ni aina ya ndege ambao, wana midomo mirefu, na kifuko kikubwa shingoni ambacho wanatumia kuhifadhia chakula kabla hawajakimeza. Ni ndege ambao wanapendelea sehemu za maji maji ambapo inakuwa ni rahisi wao kupata samaki..(Tazama picha juu)
Lakini mwari anayezungumziwa hapa ni jamii nyingine ya jangwani tofauti na yule wa majini..Kwa kawaida ndege hawa(jamii zote) ni ndege wanaopenda sana kujitenga, huwezi wakuta wanatembea pamoja..na mara nyingine utawakuta wapo katika hali ya kupooza wakitumia masaa mengi hata siku wakiwa wameficha vichwa vyao chini ya mbawa zao. Kwa ufupi ni ndege wa upweke sana.
Ndivyo mwandishi wa zaburi alivyojifananisha na ndege hawa kwa upweke aliokuwa anaupitia
Lakini zaidi anajilinganisha pia na bundi wa mahameni.. Bundi ni ndege ambao wanajitenga pia..wanapendelea sehemu za majangwa au mapango au kwenye majumba yaliyoachwa zamani, au makaburini.
Katika hali hizo za unyonge huwa wanatoa milio ya ajabu ajabu hususani wakati wa usiku.
Wakati fulani niliwahi kwenda mlimani kusali, mlima huo ulikuwa mbali na makazi ya watu, na ulikuwa na mwamba mkubwa kwa nyuma..lakini kwa juu sikuona ndege yoyote isipokuwa bundi mmoja ambaye kila usiku unamsikia analia tu peke yake kwa kule juu…ni ndege wa upweke sana.
Ndivyo mtunzi wa Zaburi alivyokuwa anajifananisha na ndege hawa, kwa hali aliyokuwa nayo wakati huo.
Anasema tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.
Shomoro ni hawa ndege wadogo wanaotengeneza viota vyao kwenye pembe au mabati ya nyumba. Ni ndege ambao huwezi kuwakuta wanatembea mmoja mmoja.ikitokea hivyo ni aidha mmojawapo amekufa au mgonjwa.
Hivyo mtunzi wa Zaburi anaaeleza kimifano jinsi apitiavyo taabu kutoka kwa maadui wake, hali yake inavyofanana na hao ndege..jinsi aliavyo mbele za Mungu akimwomba amsikie.
Tusome tokea mistari ya juu kidogo;
Zaburi 102:1-8
1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie. 2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. 3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga. 4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu. 5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu. 6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni. 7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba. 8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.
1 Ee Bwana, usikie kuomba kwangu, Kilio changu kikufikie.
2 Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.
3 Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.
4 Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, Naam, ninasahau kula chakula changu.
5 Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu.
6 Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, Na kufanana na bundi wa mahameni.
7 Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro Aliye peke yake juu ya nyumba.
8 Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu Huapa kwa kunitaja mimi.
Umeona, lakini katika kuugua kwake kote, Bado, Mungu alikuwa tegemeo lake, na mwisho wa siku, ukiendelea kusoma utaona Mungu anasema..
Zaburi 102:16-21
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake, 17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao. 18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana. 19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi, 20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa. 21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,
16 Bwana atakapokuwa ameijenga Sayuni, Atakapoonekana katika utukufu wake,
17 Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.
18 Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, Na watu watakaoumbwa watamsifu Bwana.
19 Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, Toka mbinguni Bwana ameiangalia nchi,
20 Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, Na kuwafungua walioandikiwa kufa.
21 Watu walitangaze jina la Bwana katika Sayuni, Na sifa zake katika Yerusalemu,
Hii ni kuonesha kuwa maombi na dua za wacha Mungu si bure..Bwana anasikia na atawatoa katika taabu zao endapo hawataacha kumlilia.
Ikiwa unasumbuliwa na magonjwa au hali ambazo wewe mwenyewe umeshindwa kuziondoa..Fahamu kuwa ukimtumaini Bwana katika hali hiyo hiyo ya kuwa mwari na bundi atakuponya..kabisa kabisa, au kukupa haja yako.
Maombolezo 3:31-33
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. 32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. 33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.
32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
Bwana akubariki.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Lumbwi ni nini katika biblia?
Ayala, Paa na Kulungu ni wanyama gani?
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?
“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?
Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.
Tofauti na “Kima” mnyama ambaye anajulikana (jamii ya nyani), ukirudi katika biblia Neno hili lina maana nyingine pia.
Kima maana yake ni “thamani ya kitu katika pesa”.
Kwa mfano tukisema kima cha nazi ni Tsh. 1000. Maana yake ni kuwa thamani ya nazi ni sh. 1000.
Kwamfano Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;
Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.
Yaani thamani mke mwema, inazidi thamani ya madini ghali ya Marijani (Ruby).
Mathayo 27:9 “Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;” Walawi 27: 11 “Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani; 12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa. 13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako. 14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa”.
Mathayo 27:9 “Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;”
Walawi 27: 11 “Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani;
12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa.
13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako.
14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa”.
Soma pia Walawi 27:23, Ayub 18:28, Matendo 7:16
Je, kipo kima kinachozidi thamani ya Bwana Yesu?
Yuda alijaribu, kumsaliti Bwana kwa kima cha fedha, lakini Pamoja na kupokea mapesa yote, bado mwisho wa siku aliona, thamani yake hailinganishwi na utajiri wowote wa ulimwengu, ijapokuwa alikuwa ni mwizi lakini utaona alirudisha fedha zao zote, na kwenda kujinyonga.
Sasa Ikiwa watu waovu wanauona uthamani wa Bwana, hadi kwenda kujiua, iweje wewe uone kazi ni bora kuliko Bwana Yesu, anasa ni bora kuliko ibada?.
Je! thamani ya Bwana wako inazidi thamani ya huu ulimwengu? Bwana Yesu alisema Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima halafu upate hasara ya nafsi yako? Itakufaidia nini?
Tubu mgeukie Bwana..
Ikiwa hujampa Bwana Yesu Maisha yako, na upo tayari kufanya hivyo leo, kwa kumaanisha kabisa, basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)
Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17
Bushuti ni nini?
Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).
Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)
Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)
Kujuzu ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:4?
Ni eneo la pango ambalo lilikuwa karibu na mji wa Israeli unaoitwa Hebroni, ambalo Ibrahimu alilinunua kwa mtu mmoja aliyeitwa Efroni, kwa ajili ya maziko ya mke wake Sara.
Mwanzo 23:13 “Akamwambia Efroni, na watu wa nchi wanasikiliza, akisema, Tafadhali unisikilize; nitatoa kima cha shamba, nawe ukipokee kwangu, nami nitamzika humo maiti wangu. 14 Efroni akamjibu Ibrahimu, akamwambia, 15 Bwana wangu, unisikilize. Sehemu ya nchi, ambayo thamani yake ni shekeli za fedha mia nne, n’nini hii baina yako na yangu? Basi uzike maiti wako. 16 Ibrahimu akakubali maneno ya Efroni. Ibrahimu akampimia Efroni ile fedha aliyotaja masikioni mwa wazawa wa Hethi, shekeli za fedha mia nne za namna inayotumika na wenye biashara”.
Mwanzo 23:13 “Akamwambia Efroni, na watu wa nchi wanasikiliza, akisema, Tafadhali unisikilize; nitatoa kima cha shamba, nawe ukipokee kwangu, nami nitamzika humo maiti wangu.
14 Efroni akamjibu Ibrahimu, akamwambia,
15 Bwana wangu, unisikilize. Sehemu ya nchi, ambayo thamani yake ni shekeli za fedha mia nne, n’nini hii baina yako na yangu? Basi uzike maiti wako.
16 Ibrahimu akakubali maneno ya Efroni. Ibrahimu akampimia Efroni ile fedha aliyotaja masikioni mwa wazawa wa Hethi, shekeli za fedha mia nne za namna inayotumika na wenye biashara”.
Eneo hilo baadaye lilikuja kugeuka kuwa kaburi la kifamilia, kwani hapo hapo ndipo Ibrahimu alipokuja kuzikwa na watoto wake, halikadhalika, ndipo Yakobo na Esau walipomzikia baba yako Isaka,
Na wakati wakiwa kule Misri, Yakobo aliwaagiza Watoto wake,pia wakamzike katika kaburi hilo la familia, la Makpela.
Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti; 30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia. 31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea; 32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi”.
Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;
30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.
31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;
32 shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi”.
Eneo hilo kwasasa, pale Israeli limejengwa msikiti, ujulikanao kama “msikiti wa Ibrahimi”, japo wote wayahudi na waislamu, hakuna hata mmoja anaweza kusema anao umiliki wa moja kwa moja wa hapo.
Lakini Je pango la makpela lina umuhimu kwetu hadi sasa au kwa Wayahudi?
Pango hili, au lolote lile ambalo lilizikiwa watakatifu, halina umuhimu wowote katika Imani yetu, Zaidi ya mambo ya kihistoria tu. Myahudi au mkristo yoyote ukizikwa karibu na eneo hilo, hakutakufanya uende mbinguni, Wapo wengine wanafikiri, wakienda Yerusalemu na kuomba kwenye ule ukuta wa Nehemia wa maombolezo, ndio maombi yao yatasikiwa. Au wakienda kubatizwa katika mto Yordani kama Bwana Yesu ndio ubatizo wao utapokelewa, jambo ambalo sio kweli.
Halikadhalika na Pango hilo la makpela halina umuhimu wowote, kwa mtu yeyote, kuzikiwa pale.
Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?
Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?
Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.
MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?