Category Archive Home

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

Tukisoma kitabu cha Mithali sura ya 30 tunamwona mtu mmoja aliyeitwa Aguri bin Yake akiandika mithali ambazo ni mahusia aliyompa mtu mmoja anayeitwa Ithieli. Kati ya mambo mengi aliyokutana nayo katika maisha yake kuna manne yaliyomshangaza sana nayo ni haya tunayoyasoma katika mstari wa 18,


Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.


Ukiisoma hii mistari kwa juu juu utaona unaweza usione jambo lolote la kushangaza, lakini ukiitafakari kwa undani utagundua kweli alivyoviona vinamshangao mkubwa sana katika mienendo yao. Hapo amevitaja vitu vine, Kwanza ni TAI, pili NYOKA, tatu MERIKEBU, na nne MTU pamoja na Mwanamke..


Aguri alitafakari kutembea kwao kukamshangaza sana, kwa mfano alimtazama Tai jinsi anavyoweza kwenda kwa kasi hewani, akaona japokuwa amepewa miguu lakini haitegemei miguu yake katika mwendo wake, leo hii hakuna mnyama yoyote wala ndege yeyote mwenye mwendo wa kasi kama Tai,Vile vile akamtazama Mnyama nyoka, ambaye nawe pia unamfahamu jinsi alivyo hana miguu, lakini nyoka kama koboko anakimbia karibia mara 2 zaidi ya mwendo ya wanadamu wengi..Hivyo Aguri akaona kumbe hata miguu sio nyenzo pekee ya kuamua mwendo wa kiumbe hai, kwamba bila hicho mambo hayawezi kwenda..


Akachunguza tena, Merikebu bahari akaona haina magurudumu kama vifaa vingine vya usafiri mfano ma gari, baiskeli, treni au pikipiki lakini inauwezo wa tembea tena kwa kasi tu..hata ingepewa matairi bado yasingeweza kumsaidia katika mwendo kasi wake, kama tu vile miguu isivyomsaidia Tai kutembea kwa kasi, na kama vile miguu isivyotumika kwa nyoka kukimbia kwa kasi, jongoo anayefanana na nyoka mwenye miguu mingi kuliko nyoka na kuliko Wanyama wengi lakini bado hawezi kukimbia..


Hivyo Aguri akamalizia kuchunguza na mwendo wa mwingine ambao ulimshangaza naamini zaidi ya yote nayo ni ni mwendo wa Mtu pamoja na msichana, hapo ukisoma katika tafsiri nyingi inaeleza kwa undani zaidi inasema jinsi mtu na msichana wanavyopendana, au mwenendo wao katika upendo.


Mara nyingi nimekutana na watu wakikosoa ndoa za wengine, labda utaona mmoja anasema mbona kulikuwa na wanawake wazuri kuliko Yule kwanini amemwoa yule bibi-kizee?, mwengine atasema kwanza alishakuwa na watoto huko nyuma ni kitu gani kilichomfanya ampendee, mwingine anatasema alikuwa ni kahaba maarufu anayejulikana mtaa mzima, imekuwaje huyu jamaa kampenda?, mwingine atasema Yule mwanaume hana mwelekeo, hana pesa Yule mwanamke kampendea nini?..Mwingine atakuwa kweli anayopesa lakini mwanamke /mwanamume Yule hakumpenda kwa ajili ya mali zake, Hayo ni maswali ambayo yapo kila mahali, Uliyempenda wewe mwingine atajiuliza ulimpendea nini?


Hilo ndio jambo linaloshangaza, kati ya wawili wapendanao. Kile kinachodhaniwa kuwa kingekuwa chanzo cha wao kuwa pamoja kinagundulika kuwa sio.


Na ndivyo ilivyo Kristo na kanisa lake..Kristo ndio Mume wa kanisa, ametuoa sisi tulio kanisa lake..


2 Wakoritho 11:2 “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.”


Yeye hakutazama kuwa sisi tulikuwa ni wachafu kiasi gani, au tulikuwa hatustahili kiasi gani?, Aliacha enzi yake na utajiri wake wote, na mamlaka yake, kuja duniani kutukomboa sisi, mambo ambayo hata malaika hawana majibu nayo, kwanini alitupenda… akatoa uhai wake kwa ajili yetu sisi tusiostahili..Ukatazama ni kitu gani kizuri alichokiona kwetu, huwezi kukiona, ukitazama ni faida gani basi ataipata kutoka kwetu huwezi kuiona, ametupenda tu kwasababu ametupenda…Huo ni mwendo wa ajabu sana.


Vivyo hivyo na Kanisa lake halisi linarudisha upendo wa namna hiyo hiyo kwake. Japo sasa hatumwoni kwa macho lakini tunampenda, wengi watajiuliza mbona huyo Yesu mnayemtumika hamumwoni? Jibu ni kwamba Upendo tulio nao kwake hautegemei macho kujidhihirisha, ni zaidi ya macho, na hata kama tutamwona kwa macho bado hatutategemea macho yetu kumpenda yeye..Kuna kitu ndani yetu kinachotufanya tutamani kuwa naye siku zote, hakielezeki kwa namna ya kibinadamu.


1Petro 1:8 “Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona; ambaye ijapokuwa hamwoni sasa, mnamwamini; na kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye utukufu,”


Vile vile hatumpendi Bwana Yesu kwasababu ya utajiri wake,.Upendo wetu kwake ni zaidi ya hapo..


Hivyo wewe ndugu ambaye bado upo nje ya Kristo umeshajua ni kwasababu gani unaona ni ngumu kumtumikia Mungu usiyemwona au usiyetembea naye? ni kwasababu hujaingizwa bado kwenye pendo lake., Siku ukiingizwa hutahitaji macho ili kutembea naye, hutahitaji akupe kwanza kitu Fulani ndipo umpende..Kwani atajidhihirisha kwako kwa namna ya ajabu ambayo hata macho hayafikii hicho kilele.


Unasubiri nini? Yeye anasema “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini.(Zaburi 34:8)”


Mkaribishe sasa maishani mwako aanze kutembea na wewe mwendo ambao hata watu wa nje watashangaa unawezaje kuwa naye katika hali zote, utafanyika kuwa Bibiarusi na utaingia kwenye pendo ambalo litakusangaza hata wewe ambalo hutatamani hata utoke.


Warumi 8: 38 “ Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo,

39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.


Ufunuo 22: 17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.”


Ubarikiwe.Tafadhali “Share” na kwa wengine..


Mada Nyinginezo:

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

MSTARI HUU UNA MAANA GANI? “YUKO MWENYE HAKI APOTEAYE KATIKA HAKI YAKE”?

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.

MATUMIZI YA DIVAI.

WALIOITWA NI WENGI, ILA WATEULE NI WACHACHE.


Rudi Nyumbani:


Print this post

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

JIBU: Kwanza tunapaswa kufahamu kuwa si mapenzi ya Mungu sisi tupitie shida yeyote ile.Lakini zipo shida na dhiki ambazo Mungu huwa anaziruhusu ziwapate wale wateule wake kwa kutimiza kusudi Fulani, aidha kwa kuwafundisha, au kwa kuonyesha utukufu wake, au kwa kuwaonya, lakini mwisho wa siku shida hizi huwa zinaishia na mwisho mwema, na ndio maana mtume Paulo alisema mahali fulani katika 

2Wakorintho 12:9 “ Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.

Kadhalika zipo shida ambazo zinatokana wanadamu wenyewe, au tunaweza kusema zinasababishwa na wanadamu wenyewe na hizo hazipo ndani ya uwezo wa Mungu kuzizua bali kwa mwanadamu mwenyewe unajua ni kwasababu gani? Jaribu kuwazia mfano huu. Kama vile sisi wanadamu wenyewe kwa wenyewe hatupendi kuchaguliwa baadhi ya mambo kwamfano kijana anapofikia hatua ya kuoa au kuolewa, mzazi mwenye busara hatoweza kwenda kumlazimisha mtoto wake aoe mke amtakaye yeye hata kama msichana huyo atakuwa ni mzuri kiasi gani, au atakuwa na maadili kiasi gani, suala la maamuzi ni la mtu binafsi. Hivyo kitu pekee atakachoweza kufanya kama mzazi mwenye busara ni kumshauri tu, na kumpa mapendekezo mema lakini si kumlazimisha, hata kama anajua huyo mke mtoto wake aliyekwenda kumchagua atakuja kumletea madhara makubwa kiasi gani mbeleni, bado hana uwezo wa kumlazimisha asimwoe. 

Na ndivyo ilivyo kwa Mungu wetu, mara zote anaona madhara yanayokuja mbele yetu, na ni kweli anatamani kuyazuia, lakini jambo analoweza kulifanya yeye kama Mungu wetu, ni kututahadharisha, au kutuonyesha jinsi mwisho wake utakavyokuwa, ili tusipotee au tusidondoke kwenye madhara. Sasa suala la kuamua kuendea au kutokuiendea njia hiyo ni la mtu binafsi. Ikiwa mtu atakubali mashauri ya Mungu basi, Mungu atamwepushia mabaya yale lakini ikiwa hatakubali basi Mungu atamwacha aangamie, hata kama Mungu atakuwa na uwezo mkubwa kiasi gani wa kumwepusha, bado hatoweza kufanya hicho kitu.

Kwasababu Mungu katuumbia sisi ndani yetu uwezo wa kuchagua.Ikiwa mtu ni mzinzi, na huku Mungu alishamwonya kuwa wazinzi hawataurithi ufalme wa mbinguni, na mtu huyo bado anaendelea katika njia zake mbovu, Hapo Mungu hawezi kumzuia japo anajua kabisa njia yake mwisho wa siku ataishia kifo, halafu aende kwenye ziwa la moto. Alimwonya shetani, hata kabla hajawa shetani, lakini hakumlazimisha asihasi, japo alijua kuwa ataasi na mwisho wa siku kuishia motoni,Mungu alimwonya lakini hakutaka kusimama katika kweli kama malaika wengine watakatifu walivyokuwa. Na ndivyo ilivyo hata kwetu,Mungu katuwekea maamuzi yetu binafsi. Kukubali au kukataa. Hakuna kulazimishwa.

Ubarikiwe


 

Mada zinazoendana:

JE! MUNGU ANASABABISHA AJALI, KWAMFANO AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE KUZAMA?

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MVUTO WA TATU!


Rudi Nyumbani:

Print this post

Katika Warumi 8:18-25. Je! Viumbe vinatazamiaje kwa shauku kufunuliwa kwa Mwana wa MUNGU?

JIBU: Jambo lisilofahamika na wengi ni kwamba, viumbe navyo vitakuwepo katika ulimwengu ujao (Mbingu Mpya na nchi Mpya)..Mungu alipoiumba dunia hakuwaumba wanadamu peke yao, bali aliwaumba pamoja na wanyama na ndege, Na Mwanadamu alipoasi, laana aliyolaaniwa haikumpata Mwanadamu peke yake bali hata na wanyama, mwanadamu alipoambiwa atakufa, na wanyama pia walikufa, Mwanadamu alipoambiwa atazaa kwa uchungu wanyama nao pia walizaa kwa uchungu.  

Mungu alipoiangamiza dunia kwa gharika, wanyama nao waliangamizwa..na kadhalika Mungu alipowaokoa baadhi ya wanadamu wachache katika safina (Nuhu na wanawe) pia kulikuwepo na baadhi ya wanyama waliookoka na gharika. Hivyo mahali popote mwanadamu alipo wanyama nao wapo, kwasababu waliumbwa kwa ajili ya mwanadamu.   Kwahiyo kama vile sisi wanadamu tunavyotamani siku ya kufunuliwa kwetu, yaani siku tutakayoiingia Mbingu Mpya na Nchi Mpya, siku ambayo hatutakiona tena kifo, wala uchungu, wala shida na wanyama na viumbe vyote vivyo hivyo vinatamani kama sisi. Navyo vinatamani kutoka katika laana hii ya dhambi, na kuingia uhuru wa Umilele.

  Biblia inasema katika ulimwengu ujao ulimwengu utakuwa na Amani, kutakuwa hakuna dhiki kwa wanyama, wala tabu. Wanyama hawatakulana tena, simba atakula majani kama ng’ombe, na mbwa mwitu atakaa pamoja na mwanakondoo.

  Isaya 11: 6 “Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza.

7 Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe.

8 Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira.

9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yanavyoifunika bahari”.

Kwahiyo wanyama na viumbe vyote vinatamani siku ya kuwekwa kwao huru kufike, kama sisi tunavyotamani siku hiyo ifike.

  Mungu akubariki.


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

JE! NI KWELI KUNA VIUMBE VINAVYOISHI SAYARI NYINGINE (ALIENS)?

NUHU ALIWALETAJE WANYAMA WOTE KWENYE SAFINA

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

SEHEMU ISIYO NA MAJI.

KISASI NI JUU YA BWANA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

JIBU: Wakati ule Mtume Petro alipokuwa kule Yafa katika nyumba ya Yule mtu mtengenezaji ngozi, siku moja aliumwa na njaa sana, na alipotaka kwenda kuandaa chakula biblia inasema alizimia na kuona maono, na ndani ya maono yale aliona kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka juu na ndani yake imebeba viumbe vya aina zote duniani, wanyama wa kila namna. Na Bwana akamwambia Petro aende kuwachinja ale. Lakini kama tunavyosoma Petro alimjibu Mungu na kumwambia tangu azaliwe hajawahi kula vitu vilivyo najisi. Na ndipo hapo Mungu akamwambia nilivyovitakasa mimi usiviite wewe najisi.(Matendo 10). 

Sasa pale ni jambo gani BWANA alikuwa anataka kumwonyesha Petro, Tukisoma ile habari, kuanzia mwanzo utaona kuwa kulikuwa na mtu mmoja mcha Mungu aliyeitwa Kornelio, Ni mtu ambaye hakuwa myahudi, wala hakujua sheria zozote za kiyahudi, Ni Mtu wa mataifa, lakini kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu alipewa neema ya kuwa mmojawapo wa wateule wa Mungu. Sasa kumbuka kabla ya hapo watu wa mataifa kule Israeli walijulikana kama najisi, hivyo hawakuruhusiwa kuchangamana na wayahudi kwa namna yoyote ile ya ibada. Lakini Mungu alimwambia Petro nilivyovitakasa mimi usiviite wewe najisi najisi, Ondoke uende katika nyumba ya Kornelio akawahubirie injili, akawabatize na wao pia wapokee habari njema za Yesu Kristo waokoke. Hivyo vile viumbe vya aina tofauti tofauti alivyoviona Petro, najisi, na visivyo najisi, vitambaavyo, virukavyo, vyenye miguu minne, nguruwe, bundi, popo, mbuzi, pweza,karungu-yeye, kivunja-chungu n.k.

Vilikuwa vinawakilisha jamii tofauti tofauti za watu waliopo duniani. Na ndio maana baada ya Petro kupata ufunuo huo ndio utaona kuanzia huo wakati nao pia wakaanza kuhubiri injili kwa watu wa mataifa pia, jambo ambalo hapo kabla walikuwa hawafanyi, walikuwa wakihubiri wa wayahudi tu peke yao. Japo YESU alishatangulia kuwapa maagizo hayo kabla lakini hawakumwelewa. Sasa ndio tukirudi kwenye huo mstari ambao Bwana aliwaambia mitume wake siku ile aliyokuwa anapaa kwenda mbinguni akisema “Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.” Alimaanisha waende wakahubiri injili kwa kila jamii ya watu waliopo ulimwenguni bila kuchagua hawa ni wayahudi, hawa si wayahudi, bila kujali rangi, dini zao, utamaduni wao, taifa lao, lugha zao n.k. Ilimradi ni mwanadamu basi injili ni lazima imfikie. Lakini Bwana hakumaanisha tukawahubirie kuku, na panya, na mijusi, na konokono injili.

Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

AGIZO LA UTUME.

INARUHUSIWA KULA NYAMA YA NGURUWE KWA MKRISTO WA KWELI?

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wala msimwite mtu baba duniani; Bwana anamaanisha nini kusema hivyo?

JIBU: Neno hilo halimaanishi kuwa hatupaswi kabisa kumwita mtu yeyote baba duniani hata wazazi wetu, hapana kama ni hivyo basi Mungu angekuwa anapingana na Neno lake pale aliposema “Waheshimu baba yako na mama yako (Kutoka 20:12)”

unaona?. Lakini tunapaswa kufahamu maneno hayo Bwana aliwalenga watu wa namna gani, ukisoma mistari hiyo kuanzia juu utaona kuwa aliwalenga wale mafarisayo na masadukayo ambao wao, walipenda kuchukua nafasi ya Mungu duniani kwa kila kitu, walitaka watu wawaone kama pasipo uwepo wao, hawawezi kumjua Mungu, pasipo watu kuongozwa na wao hawawezi kumfikia Mungu, yaani kwa ufupi walikuwa wanachukua nafasi ya Kristo duniani. Na ndio maana tukisoma tangu juu tunaona Bwana akiwaambia maneno haya..

Mathayo 23:1Kisha Yesu akawaambia makutano na wanafunzi wake, akasema,

2 Waandishi na Mafarisayo WAMEKETI KATIKA KITI CHA MUSA;

3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.

4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.

5 Tena matendo yao yote huyatenda ILI KUTAZAMWA NA WATU; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;

6 hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi,

7 na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.

8 Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.

9 WALA MSIMWITE MTU BABA DUNIANI; MAANA BABA YENU NI MMOJA, ALIYE WA MBINGUNI.

10 WALA MSIITWE VIONGOZI; MAANA KIONGOZI WENU NI MMOJA, NAYE NDIYE KRISTO”.

Mambo hayo hayo ndio tunayoweza kuyaona leo hii katika Kanisa la kirumi (Katoliki), ofisi ya kiPapa inajulikana kama “ofisi ya baba mtakatifu” na watu humweshimu yeye kama mpatanishi wa dhambi zao, na anaonekana kama ni mtu aliye na kibali cha karibu zaidi kwa Mungu zaidi ya watu wengine wote, hivyo amepewa heshima ya kipekee, anaketi mbele katika masinagogi (Katika umoja wa makanisa) ili atazamwe na ulimwengu wote kuwa yeye ni baba mtakatifu. Sasa Heshima kama hizo ambazo zinazohusianishwa na uhusiano na vyeo mbele za Mungu kwamba mtu Fulani ni mwenye cheo Fulani cha kipekee mbele za Mungu zaidi na wengine, ndizo Kristo alizokuwa anazikemea, kwamba tusimwite mtu yeyote Baba kwa namna hiyo, au kiongozi, au Rabi. Kwasababu sisi sote ni ndugu na hakuna aliye juu ya mwenziwe.  

Pale Mtume Paulo alipomwita Timotheo na Tito wanae, alikuwa anaonyesha uhusiano aliokuwa nao kama mtumishi wa Mungu aliyewazaa katika injili, na kuwalea, kwa mfano wa Baba kwa mwanawe, lakini hakuwa na maana kuwa yeye yupo juu ya mwenzake, wala hakutanua hirizi zake wala kuongeza matamvua yeye, kiasi cha kukaa masokoni kupewa heshima na watu, kwamba ni sharti aanze yeye mbele za Mungu kisha wao, na kwamba pasipo yeye hawawezi kumfikia Mungu, Hapana na hakuna mahali popote Paulo alisisitiza yeye aitwa aitwe Baba.

Utaona nyaraka zake zote Mtume Paulo, alianza na “Mimi Paulo, mfungwa na Mtumwa wa Yesu, sehemu nyingine anasema mimi Paulo mtume wa Yesu Kristo”..Lakini hutaona sehemu yoyote anaanza kwa kusema “Mimi Paulo, Baba Mtakatifu wa kanisa takatifu korintho”..hapana hutaona hicho kitu.  

Lakini inasikitisha zaidi kusikia leo hii watu wanagombania kuitwa baba, na wengine kwa nguvu, hata kama huyo mtu hana mahusiano yeyote ya kiiamani na yeye anayetaka amwite, bado atataka aitwe tu baba, hayo ndiyo Kristo aliyoyakataa, hiyo ni roho ya mpinga-kristo.

Lakini ikiwa ubaba wowote hautahusianishwa na kuchukua nafasi yoyote ya Kristo, huo hauna shida yoyote, ni kama tu vile unavyomwita mzazi wako baba au mama, hiyo haikuchukui nafasi yeyote linapokuja suala la kumwabudu Mungu, kwasababu unajua Baba yako aliye mbinguni ndiye anayestahili kupewa heshima zote za ibada na za kiungu.

Vivyo hivyo ikiwa utatoa heshima yako kwa kiongozi wako yeyote, au mwalimu wako, kanisani, hakikisha kuwa hilo halichukui nafasi ya Kristo, mnapokuja kwenye suala la kumwabudu Mungu basi sisi wote ni ndugu na tunapaswa kupeleka heshima zote, shukrani zote, na maombi yote kwa Mungu na sio kwa mwanadamu yeyote kama kanisa katoliki lifanyavyo kwa mapadre wao na Papa, na baadhi ya makanisa ya kiroho ambayo yanamfanya mtu mmoja kama ndio kila kitu kwao, huku wakimwita baba na pasipo yeye wanajihisi hawawezi kumwabudu Mungu. Hizo ni ibada za sanamu.

  Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?

MAANDALIZI YA UJENZI WA HEKALU LA TATU YAPO TAYARI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kwa nini tunasema tunamwabudu MUNGU aliye hai ,Je! wale wanaomwabudu shetani sio mungu wao aliye hai?

JIBU: Embu tutafakari mfano huu, utatusaidia kupata majibu ya maswali yetu. Tunajua kuwa Dunia tunayoishi sasa hivi ni dunia ya utandawazi na kugunduliwa kwa Kompyuta kumefanikisha kurahisisha mambo mengi sana, Komputa sasa inAaweza kufanya mambo ambayo mwanadamu pekee angeweza kufanya, unaweza ukaiuliza swali lolote na ikakusaidia kupata sehemu kubwa ya majibu yako, inaweza kukusaidia kufanya mahesabu yako, inaweza ikakusaidia kuwasiliana na mtu mwingine aliye mbali, inaweza ikakuonyesha picha, inaweza ikakuhifadhia kumbukumbuku zako, inaweza ikakusaidia kutafiti, na hata kufanya kazi n.k. Kwa ufupi komputa sasa tunaweza kusema ni chombo ambacho kina ufanisi mkubwa karibia na mwanadamu, tunaweza kusema kina uhai fulani, Na uhai huo ni wazi kabisa hakijapewa na mwingine zaidi ya mwanadamu. 

Lakini pamoja na hayo tunajua hata kiwe na ufanisi mkubwa kiasi gani, bado tu uhai wake hauwezi kuwa halisi kama wa mwanadamu mwenyewe, vipo vitu vingi kitashindwa kufanya ambavyo mwanadamu angeweza kufanya, kwamfano Komputa haiwezi kufariji, haiwezi kupima hisia za mtu, komputa haiwezi kuonyesha fadhili, komputa ukiiomba chakula haiwezi kukupa, komputa haiwezi kuona mambo ya mbeleni ili kuchukua tahadhari n.k..yenyewe inaongozwa na kwa yale tu mwanadamu aliyoyapachika ndani yake, nje ya hapo haiwezi kujichagulia mambo yake yenyewe. Vivyo hivyo tukirudi kwa Mungu wetu.

Tunajua sisi sote tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, na kama vile alivyo hai, na sisi basi tutakuwa hai, lakini uhai tulionao si kama ule wa kwake, sisi ni mfano wa Komputa zilizotengenezwa na Mungu, tunaouwezo wa kuonyesha tabia zote za Mungu lakini haimaanishi tutakuwa na ule uhai halisi kabisa kama wa Mungu mwenyewe, wa kufikia hatua ya kuweza hata kuumba, kufanya kila kitu, kuona mambo yote ya mbeleni yanayokuja, kuchipusha chakula ardhini, hatuwezi pia kujihakikishia uzima wetu wa milele kama sio kutoka kwake. Hivyo tunavyosema Tunamwabudu Mungu aliye HAI, tunamaanisha Mungu awezaye kufanya mambo yote, Mungu anayetoa uhai katika mambo yote, Mungu ambaye hashindwi na lolote,Shetani hawezi kuumba chochote,japo anaishi, hajui hata kesho yake itakuwaje sasa ataitwaje mungu aliye hai? Yeye kapewa tu sehemu ya uhai kama sisi tulivyopewa, hawezi kusema sasa nataka jua lizime, au leo mimea yote duniani ikauke,hana uwezo huo hivyo hawezi kuitwa Mungu aliye hai.. Neno zuri labda linaweza kumstahili yeye kuitwa nao hao wanaomwabudu ni “mungu aliyepewa pumzi”, lakini sio Mungu aliye hai aliye hai ni mmoja tu! anayekaa mbingu za mbingu.

Isaya 46:9 “kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; 10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote. 11 Nikiita ndege mkali kutoka mashariki, mtu wa shauri langu toka nchi iliyo mbali; naam, nimenena, nami nitatekeleza; nimekusudia, nami nitafanya.”

 Ubarikiwe.


Mada zinazoendana:

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!

NINI MAANA YA ELOHIMU?

SIKU ZA MAPATILIZO.

UPENDO


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

SWALI: Kaini baada ya kumuua ndugu yake Abeli, alikimbilia katika nchi ya Nodi, Naomba kufahamu Je! Huko alipatia wapi mke na kuzaa naye watoto? (Mwanzo 4:16).

JIBU: Ukisoma Mwanzo 5:1-5 utaona inasema….

“1Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.
3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.
4 Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, AKAZAA WANA, WAUME NA WAKE
5 Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na the lathini, naye akafa.”

Sasa kwenye Mstari huo wa 4 utaona kuwa kumbe mbali ya Kaini na Abeli kuzaliwa na Adamu kulikuwa na wana wengine wa kike na wakiume waliokuja kuzaliwa kwenye familia yao pia, na ndio huko huko Kaini alipojitwalia mke.

SWALI: Kama KAINI alitwaa mke ambae alizaliwa na Adamu na Hawa ambao ni wazazi wake kwahiyo alimuoa dada yake je,kwahiyo nihalali kumuoa mwanamke ambae ni dada yangu wa damu?”.


JIBU: Kumbuka hata Adamu mwenyewe hakwenda kumtwaa mke kutoka kwenye familia nyingine, bali katika ubavu wake mwenyewe, hivyo kama ni undugu basi Adamu na hawa wana undugu mkubwa zaidi ya Dada na kaka…

Unaona? Mungu aliruhusu iwe hivyo mwanzoni kwa ajili ya uzazi, ili watu waongezeke, lakini baadaye Mungu alitoa maagizo kuwa ni makosa mtu kutwaa ndugu wake wa karibu na kumfanya kuwa mke wake..

Mambo ya walawi 18:6 “Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana”.

Na pia mstari wa 9 unasema…

9″ Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue”.

Kwahiyo ni machukizo kuoa ndugu yako yoyote yule wa karibu.

Ubarikiwe

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

UZAO WA NYOKA.

SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?

IMANI NI KAMA MOTO.

SAUTI AU NGURUMO?

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini MUNGU Anampa Nabii Hosea maagizo ya Kumuoa mwanamke kahaba? (Hosea 3)

JIBU: Mungu alimpa maagizo nabii Hosea kuoa mke aliye kahaba, sio kwasababu Mungu, anahalalisha usherati, hapana! Kusudi la Mungu kufanya vile ni kutaka kuwaonyesha wana wa Israeli ni jinsi gani wao wanavyofanya uasherati katika roho zao mbele zake kwa kuyaacha maagizo yake.. Kwahiyo nabii Hosea alipooa mke wa uzinzi, ilikuwa kama ishara ya Bwana kutaka kuwaonyesha wana wa Israeli mambo wanayoyafanya mbele zake…

Sasa Bwana alitaka endapo watu watakapomwuliza Hosea kwanini ameoa mke ambaye ni mzinzi…ndipo Hosea awajibu, kama mimi ninavyoudhiwa na huyu mwanamke mzinzi ndivyo na ninyi (wana wa Israeli) mnavyomuudhi Bwana kwa kufanya uzinzi mbele zake kwa kulihalifu agano lake na kuabudu miungu migeni, ukisoma habari ile yote kwa urefu utaona jambo hilo. 

Sio mara ya kwanza Bwana kutoa ishara kupitia maisha ya watu, ukisoma biblia mahali pengine utaona Nabii ezekieli Bwana anamwagiza ale kinyesi, mahali pengine akate nywele zake kwa upanga azigawanye sehemu tatu….sehemu nyingine anaambiwa ahame nyumba yake kwa kutoboa ukuta, huku amejifunika macho kumwonyesha Mfalme wa Yuda Sedekia kwamba wakati majeshi ya wakaldayo yatakapouzingira mji kwa miaka miwili, yeye atatoroka kwa njia ya kutoboa ukuta wa mji, na hatimaye watamkamata na kumtoboa macho yake sawasawa na nabii Ezekieli alivyoonyesha… 

Ezekieli 12:1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,

2 Mwanadamu, wewe unakaa kati ya nyumba iliyoasi, watu ambao wana macho ya kuona, ila hawaoni, wana masikio ya kusikia, ila hawasikii; kwa maana ni nyumba iliyoasi.

3 Basi, mwanadamu, funga tayari vyombo kwa uhamisho, ukahame wakati wa mchana mbele ya macho yao; nawe utahama toka mahali pako hapa mpaka mahali pengine mbele ya macho yao; labda watafahamu, wajapokuwa ni nyumba iliyoasi.

4 Nawe utatoa vyombo vyako, wakati wa mchana, mbele ya macho yao, kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa; nawe mwenyewe utatoka, wakati wa jioni, mbele ya macho yao, kama watu watokavyo katika kuhamishwa.

5 Toboa mahali ukutani mbele ya macho yao, ukachukue vitu kwa kuvipitisha pale.

6 Mbele ya macho yao utajitwika begani pako, na kuvichukua nje gizani; utafunika uso wako, hata usiione nchi; kwa maana nimekuweka uwe ishara kwa nyumba ya Israeli.

7 Nikafanya vile vile kama nilivyoamriwa; nalitoa vyombo vyangu wakati wa mchana kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa, na wakati wa jioni nikautoboa ukuta kwa mkono wangu; nikavitoa gizani, nikavichukua begani, mbele ya macho yao.

8 Asubuhi neno la Bwana likanijia, kusema,

9 Mwanadamu, nyumba ya Israeli, je! Nyumba ile iliyoasi, hawakukuambia, Unafanya nini wewe?

10 Waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Ufunuo huu wamhusu mkuu wa Yerusalemu, na nyumba yote ya Israeli walio kati yao.

11 Sema, Mimi ni ishara kwenu; kama mimi nilivyotenda, wao nao watatendwa vile vile; watahamishwa, watakwenda kufungwa.

12 Naye mkuu aliye kati yao atachukua begani katika giza; naye atatoka kwenda zake; watatoboa mahali ukutani, wapate kuvichukua vyombo vyao nje; atafunika uso wake, kwa sababu hataiona nchi kwa macho yake.

13 Tena wavu wangu nitautandika juu yake, naye atanaswa kwa mtego wangu; nami nitampeleka Babeli, mpaka nchi ya Wakaldayo; lakini hataiona, angawa atakufa huko.

14 Nami nitawatawanya kwa pepo zote wote wamzungukao ili wamsaidie, na vikosi vyake vyote; nami nitaufuta upanga nyuma yao.

15 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; nitakapowatawanya kati ya mataifa, na kuwatupa-tupa katika nchi zote” 

Ukizidi kusoma utaona mahali pengine Nabii mmoja Bwana alimwagiza amwambie mtu ampige mpaka atoke majeraha.

 1 Wafalme 20: 35 “Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.

36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.

37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha.”

 Sasa mambo haya yote ni ishara ya Bwana kutaka kuzungumza na wana wa Israeli kwa kupitia maisha ya watu, kwahiyo hiyo ndio sababu ya Mungu kumwambia Nabii Hosea akaoe mke wa kikahaba..na pia kumbuka Hosea mwenyewe hakuwa mzinzi ni yule mwanamke aliyeambiwa amwoe ndiye aliyekuwa ni kahaba. Kwa jinsi hiyo hiyo mambo hayo yanavyochukiza mbele za watu ndivyo hivyo hivyo yanavyochukiza mbele za Mungu, pale watu wanapoasi maagano yake. 

Ubarikiwe!


Mada zinazoendana:

RAHABU.

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

MSHAHARA WA DHAMBI:

JE! ULEVI NI DHAMBI?

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

VITA BADO VINAENDELEA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! shetani anaweza kuyajua Mawazo ya mtu ,hata kama mtu huyo hatayatamka?

JIBU: Biblia haituelezi kuwa kama kuna mtu yeyote anayejuwa mawazo ya mtu isipokuwa mtu mwenyewe na Mungu peke yake basi. Mungu peke yake ndio yupo kila mahali, yeye peke yake ndio anajua kila kitu, na yeye peke yake ndiye anayeweza mambo yote..Kwasababu yeye ndio muumba wa vyote.   Hilo tunalithibitha katika vifungu hivi vya maandiko.

  Zaburi 139: 1 “Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.

2 Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali.

3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.

4 Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana.

5 Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako.

6 Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia. 7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?

8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.

9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari;

10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.

11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; 12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.

13 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu”.  

Unaona ni sawa tu! na mtu ambaye anamiliki account ya facebook,sasa mwenye uwezo pekee wa kuiingia na kutoka ni mmiliki wa account hiyo na aliyetoa account hiyo ambao ni facebook basi! Hao wawili tu ndio wenye uwezo wa kufanya lolote juu ya account hiyo lakini mtu mwingine wa nje! hata kama na yeye atakuwa anamiliki shirika kubwa kiasi gani linaloweza kufanana na facebook, hawezi hata kidogo kuwa na uwezo wa kudukua taarifa za account yako ya facebook, labda wewe umfunulie au shirika la facebook lenyewe limpe taarifa zako.  

Vivyo hivyo moyo wa mwanadamu shetani hawezi kuuingia wala kufahamu mawazo yaliyopo ndani yake, isipokuwa wewe mwenyewe umfunulie au Mungu.

Lakini pia kumbuka biblia inamwita shetani lile joka la zamani, Hii ikiwa na maana kuwa amekuwepo duniani tangu zamani na hiyo inampa faida kuwatazama wanadamu kwa muda mrefu na kuelewa baadhi ya tabia walizonazo, hivyo anaweza akawa anauwezo wa kuhisi mawazo ya mtu yakoje na haraka akamuundia njia ya kumwangamiza kulingana na anachokitamani, lakini kufahamu moja kwa moja fikra za mtu kama vile Mungu hilo hawezi, uwezo huo wa kuyasoma mawazo ya mtu mwingine hata sisi wanadamu tumepewa,..unaweza ukamuangalia mtu katika mazingira Fulani ukajua anachowaza, lakini huwezi kuingia ndani ya kichwa chake na kujua kila kitu ndani yake.

 Na ndio maana utaona shetani alipokuwa anamjaribu hata Yesu alikuwa anamwambia ikiwa wewe ndiwe! Kuonyesha kuwa alikuwa hana hata uhakika wa uhusiano wa Yesu na Baba yake ulivyo maana kama angelijua hilo asingepoteza hata muda wake kumuuliza Bwana maswali yaliyoonekana kuwa ni ya kitoto kwa Bwana .

Lakini pia shetani anaowezo wa kutuma fikra zake ndani ya mtu, anaweza akatuma kwa kupitia ndoto, kwa kutumia mawazo, au hata kwa njia ya maono. Na hayo huwa yanakuja na nguvu Fulani kukushawishi kufanya mambo yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu. Kama mtu akiwa anaendelea kuyatafakari badala ya kuyakataa basi ndivyo anavyompa shetani wigo mpana wa kuyamiliki maisha yake.

Na ndio maana biblia inasema inatupaswa tuwe na uwezo wa kuteka kila fikra ipate kumtii Kristo. Jambo lolote linalokuja kwenye mawazo yetu, au ndoto, au chochote kile kama kinapingana na kanuni za Mungu ni kutokipa nafasi, kukikataa kwa nguvu, na chenyewe mwisho wa siku kitaondoka.  

2 Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;”.

  Hivyo, kuhusu shetani kufahamu mawazo ya mtu kana kwamba anasikia radio, hilo jambo haliwezi, japo anao uwezo wa kuhisi mtu au anachokiwaza au kumsoma mawazo yake kwa kuchunguza tabia za huyo mtu na mienendo yake, na mazungumzo yake mara kwa mara.  

Ubarikiwe.  

Mada Nyinginezo:

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

TUNAMWABUDU MUNGU ALIYE HAI ,JE! WALE WANAOMWABUDU SHETANI SIO MUNGU WAO ALIYE HAI?

BIDII YA MFALME YOSIA.

PEPETO LA MUNGU.

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

MPINGA-KRISTO


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kutoka 10:1 “BWANA anasema atampa Farao moyo Mgumu, asimtii, je! hapo Bwana Atamhukumu Farao kama mkosaji siku ile?”

JIBU: Ndio atamuhukumu kama mkosaji, na ndio maana utaona zile adhabu zote zilimpata!! Hata kufiwa na mtoto wake wa kwanza…Na baada ya kufa kama hakupewa moyo wa kutubu, basi bado ataenda jehanamu ya moto. Kumbuka Moyo wa kutubu na moyo wa kumtafuta Mungu, ni Mungu mwenyewe ndio anaotoa sio sisi tunaoamua kwa juhudi zetu..ndio maana Bwana Yesu alisema katika

 “Yohana 6:44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka;”

Umeona hapo? Nguvu ya mtu kumfuata Mungu ni Mungu mwenyewe ndiye anayekujalia..vinginevyo haiwezekani kumtafuta Mungu wala kumfuata.Sasa Kwanini Mungu amjalie Musa moyo mlaini wa kumkubali na Farao ampe moyo mgumu wa kumkataa??..hatujui na wala hatuwezi kumuuliza Mungu hayo maswali, ndivyo ilivyompendeza yeye, ni sawa na tumuulize Mungu alitokea wapi?? Hayo ni maswali tusiokuwa na majibu nayo….Yapo juu ya upeo wa fikra zetu. Na ndio maana mtume Paulo alisema katika.. 

Warumi 9.13 “Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.

14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!

15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.

16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

17 Kwa maana maandiko YASEMA JUU YA FARAO, ya kwamba, nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.

18 BASI, KAMA NI HIVYO, ATAKAYE KUMREHEMU HUMREHEMU, NA ATAKAYE KUMFANYA MGUMU HUMFANYA MGUMU.

19 Basi, utaniambia, MBONA ANGALI AKILAUMU? Kwa maana NI NANI ASHINDANAYE NA KUSUDI LAKE?

20 La! Sivyo, Ee binadamu; WEWE U NANI UMJIBUYE MUNGU? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?” 

Unaona hapo? Biblia inasema pia wapo watu ambao hawajakusudiwa uzima wa milele, watu ambao majina yao hayajaandikwa katika kitabu cha uzima kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu (Ufunuo 17:18 na Ufunuo 13:8)..Swali ni Ni wakina nani hao?? Jibu ni kwamba Hatuwajui, Mungu ndie anayewajua…sisi sio kazi yetu kuwafahamu, jukumu tulilopewa ni kuhubiri injili kwa kila kiumbe kana kwamba wote wote wamekusudiwa uzima wa Milele,…Na kujitahidi kuishi kulingana na maagizo yake na amri zake,ili tuwe na uhakika sisi sio miongoni mwa hilo kundi lililoandikiwa kupotea milele.Kwasababu dalili kuu inayotambulisha kuwa umekusudiwa uzima wa milele ni pale mtu anapoitii na kubadilika, kadhalika dalili kubwa inayoweza kumtambulisha kama mtu huyo hajakusudiwa uzima wa milele, ni pale anapoupinga wokovu ndani ya moyo wake. 

Ubarikiwe!


Mada zinazoendana:

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.

SIFA TATU ZA MUNGU.

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

FUVU LA KICHWA.

ANGALIA JINSI USIKIAVYO:


Rudi Nyumbani:

Print this post