Category Archive Home

Katika 1Yohana 5:6-9, (a) Ni kwa namna gani Yesu alikuja kwa maji na damu?

Kadhalika naomba kufahamu.. (b)Mashahidi watatu washuhudiao mbinguni wanatajwa, Neno ambaye ndiye Yesu bado ana nafasi ya mwana hata baada ya kutoka duniani? (c)mashahidi wa duniani (roho,maji na damu) wanaotajwa ni kwa namna gani wanashuhudia? BARIKIWA SANA !


JIBU: A) Kwanza ni muhimu kufahamu wakati, Bwana Yesu alipokuwa pale Kalvari, baada ya kuchomwa mkuki ubavuni na yule Askari wa Kirumi, kulitoka MAJI NA DAMU, ikiashiria kuwa dhambi zetu, zinaoshwa kwa damu na kwa njia ya maji. Ikiwa na maana kuwa mtu ili apate ondoleo la dhambi zake ni lazima akabatizwe kwanza kwa kuzamishwa katika MAJI mengi kama ishara, na ndipo dhambi zake ziweze kusafishika kwa DAMU ya Yesu Kristo. Na ndio maana Bwana alisema aaminiye na kubatizwa ataokoka…  

B) Na aliposema wapo watatu washuhudiao mbinguni na wapo watatu washuhudiao duniani, haikumaanisha kuwa kuna nafsi tatu za watu duniani na kuna nafsi tatu nyingine mbinguni. Hapana haimaanishi hivyo kwasababu maji yatashuhudiaje? Hayawezi kuongea wala kuhubiri injili, hivyo anaposema wapo watatu duniani yaani maji, damu na Roho anamaanisha zipo hatua tatu “mwanadamu kuzifuata ili kukamilika duniani” yaani mtu anapaswa aoshwe dhambi zake kwa kubatizwa katika MAJI, ili apate ondoleo la dhambi zake kwa DAMU ya Yesu na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu ambaye ndiye muhuri wa Mungu.Hatua hizi tatu ndizo zinazoshuhudia kwamba mwanadamu akizifuata hizo amekombolewa na kukamilishwa.  

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni MKABATIZWE kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”  

C) Na aliposema wapo watatu mbinguni hakumaanisha tena kuna nafsi tatu mbinguni kila moja inajitegemea, hapana! Biblia ilimaanisha kuwa zipo hatua tatu mbinguni MUNGU MMOJA alizozitumia “kumpatanisha mwanadamu na nafsi yake ”, hatua ya kwanza alizungumza na wanadamu kama Baba(yaani MUNGU JUU YETU), hatua ya Pili alizungumza nasi kama NENO(MUNGU PAMOJA NASI,EMANUELI,)

Waebr 1:1“Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika MWANA, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.”

Hatua ya tatu kazungumza nasi kama ROHO MTAKATIFU(MUNGU NDANI YETU), katika Roho Mtakatifu ndio utimilifu wa Mungu kuzungumza katika ukaribu zaidi, yeye ndiye atufundishaye mioyoni mwetu na kututia katika kweli yote,  

Yeremia 31:31 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.

32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.

33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; NITATIA SHERIA YANGU NDANI YAO, NA KATIKA MIOYO YAO; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

34 WALA HAWATAMFUNDISHA KILA MTU JIRANI YAKE, NA KILA MTU NDUGU YAKE, WAKISEMA, MJUE BWANA; KWA MAANA WATANIJUA WOTE, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena”.  

Kwahiyo kwa hatua hizi tatu mwanadamu amepatanishwa na kusogezwa karibu zaidi na Mungu….Tofauti na zile za kwanza(maji,damu, na Roho) ambazo ni mwanadamu anapaswa azifuate kukamilika mbele za Mungu, lakini hizi za mwisho(Baba, Neno na Roho) ni Mungu anazitumia kutupatanisha sisi na nafsi yake (au kutusogeza karibu zaidi na yeye)..  

Ubarikiwe sana.  


Mada zinazoendana:

JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA??

JE! HIZI ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI? NA JE ZINATOFAUTIANA NA ROHO MTAKATIFU?

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

BIDII YA MFALME YOSIA.

MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili

SWALI: Bwana alikuwa na maana gani kusema mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili?(Mathayo 5:39)


JIBU: Bwana Yesu aliposema mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili na sawasawa na pale aliposema pia “mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.”

Kama tunavyofahamu ukiwa kama mkristo ni lazima ukutane na vikwazo vingi kutoka kwa wasioamini, Hii ikiwa na maana kuwa kwa kufanya hivyo utakuwa umeushinda uovu na utafanikiwa kuiokoa roho ya mtu huyo badala ya kuingamiza. kwasababu kwa kufanya vile Biblia inasema utakuwa umempalia makaa ya moto kichwani pake,atakuwa akijiuliza kila siku ni kwanini sikutendewa kama mimi nilivyomtendea yeye?. hivyo baadaye atajiona yeye ndiye mwenye makosa na kugeuka na kutubu kwasababu yale makaa ya moto yatakuwa yanachoma ndani yake. Biblia inasema katika..

Mithali 25: 21 “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa;

22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu”. 

Lakini sasa mfano atakapokupiga na wewe ukamrudishia, au atakapochukua mali yako nawe ukaenda kuchukua ya kwake, atakapokuabisha na wewe ukamwaibisha, atachomwaje dhamira na kujiona kama yeye ni mwenye dhambi?, hivyo atabakia kuwa vilevile tu na kukuona wewe ni mtu wa kawaida tu kama watu wengine walivyo. Na ndio maana Bwana Yesu alisema tuushinde ubaya kwa wema, ili tuwe wakamilifu kama Baba yetu alivyo mkamilifu. Aliendelea kusema..

Mathayo 5:41 “Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili.

42 Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.

43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”

 Ubarikiwe sana.


Mada zinazoendana:

KISASI NI JUU YA BWANA.

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

SHUKURU KWA KILA JAMBO.

AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Katika Marko 2:2-12, Kwanini Bwana Yesu alichukua hatua ya KUSAMEHE dhambi kwanza kabla ya kumponya yule kiwete?

JIBU:Tukisoma

Marko 2:2 “Wakakusanyika watu wengi, isibaki nafasi hata mlangoni; akawa akisema nao neno lake.

3 Wakaja watu wakimletea mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne.

4 Na walipokuwa hawawezi kumkaribia kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye kupooza.

5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.

6 Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,

7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?

8 Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

9 Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

10 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),

11 Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.

12 Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe..”  

Ukichunguza hapo utaona kuwa jambo la kwanza; Bwana aliona Imani yao kwake, aliona ndani yao walikuwa na kitu cha ziada zaidi ya imani ya kuponywa, nayo ni Imani kwa Yesu Kristo…..Na tunajua kitu cha kwanza kilichomleta Bwana Yesu duniani ni kuokoa dhambi za watu, na vitu vingine baadaye… Ukisoma

Yohana 8:24 Bwana aliwaambia makutano ..

“Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu”

Unaona hapo? Ni lazima uwe na imani ya kumwamini mwana wa Mungu kwanza ndipo upate uzima… Inakupasa uamini kwanza. Na ndio maana jambo la kwanza alilolitamka yeye kama mkuu wa uzima wa roho za watu mara baada ya kuona Imani yao kwake, akamwambia sasa yule aliyekuwa amepooza..UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO…..Ni Neno zuri na la neema kiasi gani!!!   Lakini wale wengine waliokuwa pale mawazo yao yalikuwa tofauti, wao walitazamia tu, Bwana amponye yule mtu kisha amwambie nenda zako, halafu yule mtu akaendelee kuishi maisha ya dhambi kisha mwisho wa siku afe aende kuzimu!..na uponyaji wake wa mwili usimfaidie kitu baada ya maisha ya hapa duniani. Sasa Ukiendelea kusoma pale utaona Bwana anawauliza tena wale watu,

Marko 2:9 “VYEPESI NI VIPI, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

Unaona hapo, …Kwa mtu mwenye akili na anayethamini maisha yake ya rohoni atagundua kuwa ni afadhali usipone ugonjwa wako, lakini usamehewe dhambi zako…kuliko kuponywa halafu dhambi zako ziendeleee kubaki! Na ndio maana Bwana alimchagulia fungu lililo jema la kusamehewa dhambi zake kwanza, kisha baadaye aje amponye…   Na ndivyo tunavyopaswa na sisi kama wakristo kufanya hivyo sasahivi kama Bwana Yesu alivyofanya, tunakimbilia kuwaombea watu magonjwa ,kupokea miujiza, na mafanikio tunasahamu kuwafundisha watu habari za msamaha wa dhambi ambao ndio msingi wa Imani ya kikristo..

VYEPESI NI VIPI??? Ni heri tukamuhubirie mtu habari za msamaha na toba, aokolewe roho yake hata kama hatapokea uponyaji, kuliko kuhubiri kila siku mimbarani pokea miujiza huku bado watu wanakufa katika dhambi zao. Ni vema tufanye vyote ikiwezekana kuliko kusahau habari za uponyaji wa roho za watu na kuegemea sehemu moja tu ya miujiza….VYEPESI NI VIPI? .  

Ubarikiwe sana.


Mada zinazoendana:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

KISASI NI JUU YA BWANA.

MTI UANGUKAPO, PAPO HAPO UTALALA.

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)


Rudi Nyumbani:

 

Print this post

Zile tunu (Dhahabu, uvumba na manemane) Mamajusi walizozitoa kwa Bwana (Mathayo 2) . ziliwakilisha nini?

JIBU:

Mathayo 2:10 “Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.

11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; DHAHABU na UVUMBA, na MANEMANE. 

Ukisoma hapo utaona zile zawadi wale mamajusi walizozipeleka ni tatu tu. Ndio tunu zenyewe nazo : (dhahabu, uvumba na manemane)…

Sasa hizi zawadi tatu kila moja ilikuwa na maana yake kubwa, Tukianza na dhahabu, wale mamajusi walifahamu kuwa aliyezaliwa ni mfalme na anastahili heshima ya kifalme na kitu chenye thamani kubwa kuliko vyote ambacho angestahili kupewa mfalme ni dhahabu, kwasababu dhahabu inaweza kubadilishwa na kuwa hata fedha na kutumiwa kwa matumizi mengine yeyote..kwahiyo hii zawadi ya dhahabu ilikuwa ni zawadi yenye manufaa kimaisha, tofauti na hizo zawadi mbili nyingine zilizobakia zenyewe zilikuwa na manufaa ya kiujumbe zaidi kuliko kimatumizi.. Kwa mfano zawadi ya UVUMBA.

Kwa kawaida uvumba sio zawadi tunaweza tukasema uzito wa kumfaa mtu kwa wakati wote, ni zawadi isiyokuwa na thamani kubwa sana,hivyo hatuwezi kivile kuiweka katika makundi ya zawadi kama zawadi , tuchukulie kwamfano Mtu kasafiri kutoka mbali tuseme Marekani halafu anakuletea zawadi ya msalaba au ufunguo..Kwa namna ya kawaida wewe unayoipokea huwezi kwenda kuiuza au kuitumia kwa matumizi yako yoyote, zaidi sana utafahamu moja kwa moja kuwa ni zawadi iliyobeba ujumbe Fulani wa ndani zaidi ya kinachoonekana, Mfano mwingine tunafahamu pale binti anapoagwa baada ya kuposwa na kwenda kuolewa huwa kuna baadhi ya zawadi zinaambatanishwa naye kutoka kwa watu wa nyumbani kwake, licha ya kupewa vitu vya ndani na mali..lakini kuna mambo madogo madogo utakuta anakabidhiwa pia na hayo ndio yana ujumbe mzito kuliko hata vile vitu vya thamani alivyopewa, kwamfano utakuta anapewa ufagio, au ungo,..Ikiwa na maana kuwa mwanamke anapaswa awe Msafi na awe anazingatia Mapishi n.k… 

Hivyo hivyo na wale mamajusi walipata ufunuo wa wanayemfauata ni nani, na ndio maana walikwenda na dhahabau lakini wakaongezea kubeba na Uvumba juu yake?.. 

Sasa Kumbuka katika hekalu la Mungu, uvumba ulikuwa unavukizwa tu na makuhani baada ya sadaka kutolewa sasa ile damu ilichukuliwa na kupelekwa katika madhabahu ya dhahabu iliyokuwa kule patakatifu, na hapo ndipo uvumba ulikochomwa kujaza ile nyumba ya Mungu harufu nzuri ya manukato na utukufu, na kumbuka kazi hiyo aliifanya kuhani mkuu peke yake. Hii ikifunua kuwa Huyu aliyezaliwa Yesu Kristo, licha tu ya kuwa mfalme atakuja kuwa KUHANI pia, kwasababu kila kuhani lazima awe na uvumba mkononi mwake wa kuvukiza mbele za Mungu…Na Yesu Kristo ndiye kuhani mkuu wetu. Haleluya.

 Waebrania 4: 14 “Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu.

15 Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.

16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji”. 

Kwahiyo wale Mamajusi walipata ufunuo huo kuwa Yule atakuja kuwa kuhani mkuu pia..Jambo ambalo wengi wa waliokuwa pale hawakulifahamu hilo, mpaka alipokuja kupaa mbinguni, mitume ndio wakamwandikia habari zake. Kadhalika MANEMANE, ni zao lililotoka katika miti likiwa na maana ya “Uchungu”, manemane ilitumika kutengenezea dawa, Hivyo zawadi kama ile isingeweza kuonekana inafaa sana kwa mazingira kama yale ya furaha ya kuzaliwa Mfalme duniani, lakini walifanya vile kwasababu ilikuwa inabeba ujumbe mwingine wa ndani zaidi..

Kama tafsiri ya jina lake lilivyo ilifunulia kuwa mtoto aliyezaliwa licha ya kuwa mfalme atapitia mateso na uchungu mwingi, na hilo lilikuja kujidhirisha alipoteswa na kusulibiwa kwa ajili yetu… Wakati akiwa katika safari yake ya kwenda msalabani wale askari walimchanganyia mvinyo na manemane na kumnyeshwa, lakini Bwana aliitema kwa jinsi ilivyokuwa chungu,(Soma Marko 15:23)..Gharama Bwana aliyoilipa kwa ajili ya dhambi zetu ni kubwa sana, mfalme kufa na kuteswa msalabani kwa ajili ya mtu mwenye dhambi asiyestahili kwa chochote, hakika ni jambo la neema sana.

 Hivyo wale mamajusi Mungu aliwapa kuona mbali zaidi ya zile hazina walizozipeleka. Kama mamajusi ambao hawakuwa wayahudi walisafiri kutoka nchi za mbali kwa muda wa miaka miwili, ili tu kumwona mfalme YESU akiwa mchanga, tutapataje kupona sisi tulioshuhudia matendo yake makuu ya neema kuu namna hii ambayo kila siku yanatuita tutubu dhambi?. Tutapate kupona tukidharau leo! 

Ubarikiwe sana.


Mada zinazoendana:

NYOTA YA ASUBUHI.

WACHUNGAJI WA BWANA MAKONDENI.

UFUNUO: MLANGO WA 12

JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

MWEZI NI ISHARA GANI KWETU?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

JIBU: Hilo neno SHEHE lisikusumbue sana..kama tunavyofahamu lugha yetu ya Kiswahili maneno mengi yametoholewa kutoka katika lugha ya kiharabu..kwamfano neno shukrani, marhaba, salamu, sultani, sadaka, simba, msalaba,jehanamu, sheria, raisi,uasherati, hekalu, adhabu, adui, askari, lawama, dhamira,roho,damu, giza, tufani n.k. theluthi ya Lugha ya Kiswahili ni kiharabu.  (Hivyo kuna Neno shehe katika biblia pia)

Sasa kwasababu waarabu walikuwepo katika nchi yetu huku zamani zile na lugha yetu ilikuwa bado haijajitosheleza hivyo tukajikuta tunatumia maneno yao katika lugha zetu, na sio kiharabu tu hata na lugha nyingine za kigeni za watu waliotawala nchi yetu… Kwahiyo hilo neno SHEHE asili yake ni kiharabu, likiwa na maana ya Kiongozi, au mwalimu hususani anayehusiana na mambo ya kidini..na ndio maana ukisoma katika tafsiri nyingine za biblia mfano za kiingereza utaona linatumiwa neno Lords, or rulers badala yake…Neno hili unaweza ukaliona katika kitabu cha Yoshua 13:3,21, 17:7, 1Samweli 5:7,11, 6:4, Ezra 9:2 Nehemia 2:16.

Hivyo kwasababu ni Neno la kiharabu viongozi wa dini ya kiislamu walilitumia sana katika dini yao na ndio maana linaonekana kama ni neno la kiislamu lakini kiuhalisia sio..   kadhalika kama tu neno Rabi ni neno linalomaanisha mwalimu kwa kiyahudi, lakini kwasababu ni neno la lugha ya kiyahudi na linatumiwa sana na viongozi wa dini ya kiyahudi basi inachukuliwa hivyo mtu yeyote anayejiita Rabi yeye ni kiongozi wa dini ya kiyahudi lakini kiukweli sio hivyo hata kiongozi wa dini nyingine yoyote tofauti na ya kiyahudi anaweza kuitwa Rabi kwasababu maana halisi ya neno Rabi ni mwalimu…  

Kadhalika na Neno Mchungaji limezoeleka kutumiwa na viongozi wa dini ya kikristo, na halitumiwi na wengine lakini kiuhalisia hata kiongozi wa dini ya kibuddha anaweza kuitwa mchungaji.. Na ndivyo ilivyo hata kwa Neno shehe, kwahiyo pale katika maandiko neno hilo linasimama kama kiongozi wa imani wa dini husika kwa wayahudi na kwa wasio wayahudi.…  

Na pia katika agano jipya halijatumika sana hilo neno lakini badala yake yametumika maneno kama waalimu na wachungaji lakini kwa lugha ya kiharabu ndio hao hao.  

Ubarikiwe sana.


Mada zinazoendana:

KITABU CHA YASHARI KINACHOZUNGUMZIWA KATIKA 2SAMWELI 1:17-18, NI KITABU GANI?

IMANI “MAMA” NI IPI?

UNALITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI?.

EPUKA KUTOA UDHURU.

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

UFUNUO: MLANGO WA 11


Rudi Nyumbani:

Print this post

SAYUNI ni nini?

JIBU: Tukirudi Mwanzo kabisa Daudi alipoenda kuiteka Yerusalemu,na kufanikiwa eneo lile liliitwa ngome ya SAYUNI (2Samweli 5:7).Hivyo Sayuni kwenye biblia imetumika kama Mji wa Daudi au Mji wa Mungu (YERUSALEMU).. 

Kadhalika na lile eneo la mlima ambalo hekalu la Mungu lilijengwa liliitwa pia mlima Sayuni, ambalo lipo hapo hapo Yerusalemu (Yeremia 31:6,12). 

Sehemu nyingine biblia imetaja Sayuni kama watu wa Mungu yaani wayahudi;

 Isaya 60: 14 “Na wana wa watu wale waliokutesa Watakuja kwako [Israeli] na kukuinamia; Nao wote waliokudharau Watajiinamisha hata nyayo za miguu yako; Nao watakuita, Mji wa Bwana, Sayuni wa Mtakatifu wa Israeli” 

Unaweza kuona hapo. Kadhalika ukisoma pia (Zakaria 9:9, Sefania 3:14-19),biblia inamtaja Israeli kama binti Sayuni. Yote haya yanaonyesha pia Wayuhudi mbele za Mungu ni sawa na SAYUNI yake. Lakini tukirudi katika agano jipya neno Sayuni limezungumziwa kama ufalme wa watu wa Mungu wa rohoni. 

Waebrania 12: 22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,

23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,” 

Hapo Mtume Paulo kwa ufunuo wa Roho anaonyeshwa Sayuni hasaa ambayo Mungu aliikusudia kwa watu wake tangu zamani yaani hiyo Yerusalemu ya mbinguni kanisa la Mungu. Mtume Petro pia aliandika katika…

 1Petro 2: 6 “Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.

7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.

8 Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo.”

 Habari hiyo nayo inathibitisha kuwa kanisa ndiyo Sayuni ya Mungu na ndio pia Yerusalemu ya mbinguni,..na tunafahamu Kanisa msingi wake ni Yesu Kristo, na hapo hiyo Sayuni jiwe kuu lake la pembeni linaonekana nI YESU KRISTO BWANA WETU. Kwahiyo na sisi pia tujitahidi tuwe na sehemu katika hiyo SAYUNI/ YERUSALEMU mpya ya Mungu ambayo Mungu alishaanza kuiandaa na anaendelea kuiandaa hapa hapa duniani. 

Ubarikiwe.

MLIMA WA BWANA.

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Rudi nyumbani:

Print this post

Kwanini pale Bwana Yesu alichukua hatua ya kumsamehe dhambi kwanza kabla ya kumponya yule mtu mwenye kupooza?(Marko 2).

JIBU: Ubarikiwe dada tuisome kwanza habari yenyewe.. 

Marko 2: 1 “Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.

2 Wakakusanyika watu wengi, isibaki nafasi hata mlangoni; akawa akisema nao neno lake.

3 Wakaja watu wakimletea mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne.

4 Na walipokuwa hawawezi kumkaribia kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye kupooza.

5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.

6 Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,

7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?

8 Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

9 Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

10 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),

11 Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.

12 Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote,wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe” …

Kama ukichunguza utaona kuwa jambo la kwanza Bwana aliloliona ni ile Imani yao kwake, aliona ndani yao walikuwa na kitu cha ziada zaidi ya imani ya kuponywa, nayo ni Imani kwa Yesu Kristo…..Na tunajua kitu cha kwanza kilichomleta Bwana Yesu duniani ni kuokoa dhambi za watu, na vitu vingine baadaye…

Ukisoma Yohana 8:24 Bwana aliwaambia makutano ..“Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu”….

Unaona hapo?…Inakupasa uamini kwanza. Na ndio maana jambo la kwanza alilolitamka yeye kama mkuu wa uzima wa roho za watu mara baada ya kuona Imani yao kwake, akamwambia yule aliyekuwa amepooza..UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO…..Ni Neno zuri na la neema kiasi gani!!! Lakini wale wengine mawazo yao yalikuwa tofauti, wao walitazamia tu, Bwana amponye yule mtu kisha amwambie nenda zako, halafu yule mtu akaendelee kuishi maisha ya dhambi kisha mwisho wa siku afe aishie kupata hasara ya nafsi yake!..na uponyaji wake wa mwili usimfaidie kitu baada ya maisha ya hapa. 

Sasa Ukiendelea kusoma pale utaona Bwana anawauliza tena wale watu, Marko 2:9 “Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?, Sasa kwa namna ya kawaida kwa mtu mwenye akili za rohoni atagundua kuwa ni afadhali usipone ugonjwa wako, lakini dhambi zako ziwe zimesamehewa…kuliko kuponywa halafu dhambi zako ziendeleee kubaki! Na ndio maana Bwana alimchagulia fungu lililo jema la kusamehewa dhambi zake kwanza, kisha baadaye amponye… 

Na ndivyo tunavyopaswa na sisi kama wakristo kufanya sasahivi, tunakimbilia kuwaombea watu magonjwa ,wapokee miujiza, na mafanikio na huku tunasahamu kuwafundisha watu habari za msamaha wa dhambi ambao ndio msingi wa Imani ya kikristo.. vyepesi ni vipi??? Ni heri tukamuhubirie mtu habari za msamaha na toba, aokolewe roho yake hata kama hatapokea uponyaji kuliko kuhubiri kila siku mimbarani miujiza na uponyaji na huku bado watu wanakufa katika dhambi zao.

Au ni afadhali kufanya vyote kuliko kutupilia mbali habari za msamaha wa dhambi, na kushikamana na miujiza tu. 

Ubarikiwe .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

HOME

Print this post

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

JIBU: Kujiliwa na Neno la Mungu ni sawa sawa na kufunuliwa ujumbe unaomuhusu mtu au jamii fulani, na ujumbe huu Mungu anamshushia mtu aidha kwa njia ya ndoto, au maono, au sauti, au kutembelewa na malaika, au njia nyingine yoyote ya ki-Mungu. 

Kwahiyo unaposoma mahali popote kwenye biblia,unakutana na sehemu inasema Neno la Mungu lilimjia Isaya, au Yeremia au Yona, hap ni sawa na kusema, ujumbe utokao kwa Mungu umemfikia Isaya, au Yeremia au Yona awapelekee watu. Kadhalika hata sasa hivi Neno la Mungu, huwa linawajilia watu kwa njia mbalimbali, mt anapofunuliwa Neno lolote kwa njia ya ndoto, au maono au kuzuriwa na malaika, au katika biblia, na Neno hilo limebeba ujumbe wa kwenda kuwapelekea watu wengine, hiyo ni sawa tu na Neno la Mungu limemjia mtu huyo. Kadhalika unaposikia ndani wito wa kwenda kuwashuhudia wengine habari njema, hapo ni sawa na lile Neno linalosema

Marko 16:15 “Enendeni ulimwenguni kote mkahubiri injili kwa kila kiumbe”

limekujia, hivyo unapaswa ukauwasilishe huo ujumbe kwa wakati. Na kuna hatari za kutokutii Neno la Mungu linalokujia, na hatari zenyewe ndio kama zile zilizompata Nabii Yona na zile alizoonywa Nabii Ezekieli zikisema.. 

Ezekieli 3: 17 “Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.

18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.

20 Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako”.

 Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

BIBLIA INASEMA USIONGEZE WALA USIPUNGUZE NENO LA MUNGU, HUKO KUONGEZA NA KUPUNGUZA KUKOJE?

WANA WA MAJOKA.

JIWE LA KUKWAZA

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

MADHAIFU.

WITO WA MUNGU


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

JIBU: Kwanza sio sahihi kwa mtu aliyeamini kwenda kutwaa mke au mume asiye wa imani yake ya kikristo, kwasababu moja tu! nayo ni KUEPUKA KUGEUZWA MIOYO!..   Kumbuka jambo mojawapo ambalo Mungu aliwakanya sana wana wa Israeli hata kabla ya kufika nchi ya Ahadi ni suala la kuoa/kuolewa na watu wa jamii nyingine tofauti na wayahudi, na sio kwasababu labda ni wabaya, au hawavutii hapana, ni kwasababu moja tu! Watageuzwa mioyo yao wasiambatane na Mungu wa Israeli kinyume chake wataambata na miungu migeni. Na Mungu siku zote ni Mungu mwenye wivu!.   Tukisoma;

Nehemia 13:25 “………… nikawaapisha kwa Mungu, nikasema, Msiwaoze wana wao binti zenu, wala msiwatwae binti zao ili waolewe na wana wenu, wala na ninyi wenyewe.

26 Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. Tena alipendwa na Mungu wake, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; walakini WANAWAKE WAGENI WALIMKOSESHA HATA YEYE.

27 Basi, na sisi, je! Tuwasikilize ninyi kutenda neno hili baya, hata kumhalifu Mungu wetu kwa kuwaoa wanawake wageni?”  

Unaona hapo?. Mfalme Sulemani pamoja na hekima zake zote nyingi za kuweza kupambanua mambo lakini aligeuzwa moyo, na wale wanawake wa mataifa mpaka kufikia hatua ya kuivukizia uvumba miungu migeni, Unadhani itashindanaje kwa mkristo mwingine yeyote wa kawaida?. Unaweza ukasema aa! Mimi nitaweza kumtawala, lakini hilo haliwezekani Mungu sio mwongo, akisema atakugeuza, ni kweli atakugeuza,.Mwanzoni utaona kama inawezekana lakini mwisho wa siku utajikuta unaangukia katika shimo kama Sulemani.   Vivyo hivyo ukimsoma Mfalme Ahabu alikoseshwa na Yezebeli mchawi, Samsoni naye alikoseshwa na Delila. Wote hawa wake zao walikuwa ni wanawake wa kimataifa n.k.  

Kwahiyo unapokuwa mkristo unapaswa umtafute mtu mwenye imani moja na yako ya kikristo, au kama sio basi umgeuze kwanza amgeukie Kristo ndipo umuoe au uolewe naye, vinginevyo utakuwa unajiweka mwenyewe katika hali ya hatari kubwa ya kumkosea Mungu, na kuishia katika majuto…   Lakini kama ikitokea mlishaoana tayari huko nyuma na mtu mwingine kabla wewe hujawa mkristo, na wewe baadaye ukaja kuamini na Yule mpenzi wako hajaamini lakini bado anaona vema kuishi na wewe hapo biblia inasema haupaswi kumuacha, unatakiwa ukae naye katika hali yake hiyo hiyo pengine wakati ukifika kwa matendo yako mema ya kikristo yatambadilisha na yeye naye aamini…

Lakini kama akichukizwa na uamuzi wako wa wewe kuwa mkristo na anataka kuondoka…Hapo haufungiki, anaweza kwenda, na biblia inaruhusu kutwaa mke/mume mwingine ila katika Bwana tu ambaye ni mkristo mwenye imani moja na wewe.   Soma.

1Wakoritho 7: 12 “Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.

15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

16 Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?”  

Kwahiyo hairuhusiwi kuoa mtu ambaye sio wa IMANI moja nawe kulingana na maandiko.  

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

NDOA NA TALAKA:

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOA?

NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI ?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

NAPENDA KUJUA MAANA NA TOFAUTI KATI YA MYUNANI, MFARISAYO NA MSADUKAYO.

UKWELI UNAOPOTOSHA.

DUNIANI MNAYO DHIKI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Wapendwa nini maana ya hili andiko “Ushuhuda wa YESU ndio ROHO YA UNABII” (ufunuo 19:10)?

JIBU: Biblia inaposema ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii…inamaanisha kuwa mtu yeyote ambaye anajiona kuwa anayo roho ya kinabii ndani yake au anayejiita nabii, kama maisha yake au mahubiri yake hayalengi katika kumshuhudia YESU KRISTO BWANA WETU..basi huyo ni nabii wa uongo ushuhuda wake ni wa uongo!..hata kama atakuwa anaona maono kiasi gani, au anatabiri na kutenda miujiza kiasi gani huyo bado sio nabii wa kweli, ni nabii wa uongo..

Biblia inasema katika..

1 Yohana 5:9-11“9 Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana USHUHUDA WA MUNGU NDIO HUU, KWAMBA AMEMSHUHUDIA MWANAWE.

10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu ANAO HUO USHUHUDA NDANI YAKE Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.

11 Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.” 

Hivyo ili tumtambue kama huyu ni nabii kutoka kwa Mungu au la! …hatupaswi kukimbilia kuangalia miujiza anayofanya, au maono anayoona, tutampima kwa ushuhuda anaouhubiri (Neno la Kristo) je! anaturudisha kwa YESU? Anamuhubiri Yesu yule wa Kalvari? Yesu yule aliyesema mtu akinifuata ajikane nafsi yake ajitwike msalaba wake anifuate, Yesu yule aliyesema “itamfaidia nini mtu kupata ulimwengu mzima na kupata hasara ya nafsi yake” kama atamhubiri Yesu huyu basi hata asipofanya muujiza hata mmoja, au kutabiri huyo ni nabii wa kweli kwasababu anao ushuhuda wa Yesu Kristo ambayo ndio Roho ya unabii. Unamkumbuka Yohana mbatizaji, yeye hakuwahi kufanya muujiza hata mmoja, wala ishara yoyote..lakini ushuhuda wake ulikuwa ni nini?..ulikuwa ni kuwapeleka watu kwa YESU, na si kingine..lakini Bwana alimwambiaje?…yeye ni zaidi ya NABII..na hakuna aliyetokea kama yeye hata Musa hakuwa mfano wake. 

Lakini kitu gani kilichopo sasahivi…watu wanajiita manabii wanatabiri lakini hawana ushuhuda wa Yesu Kristo ndani yao, mungu wao ni tumbo, wanahubiri tu mafanikio ya ulimwengu huu na kukwepa mafundisho ya kumpeleka mtu mbinguni na toba, kama biblia inavyosema katika

Wafilipi 3:18-21 “18 Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, KUWA NI ADUI ZA MSALABA WA KRISTO;

19 mwisho wao ni uharibifu, MUNGU WAO NI TUMBO, utukufu wao u katika fedheha yao, WANIAO MAMBO YA DUNIANI.

20 KWA MAANA SISI, WENYEJI WETU UKO MBINGUNI; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

Kwahiyo roho yoyote isiyoturudisha kwa YESU KRISTO na maneno yake, hiyo ni roho ya Yule mwovu, ikivaa kinyago cha roho ya kinabii, hivyo ili ile Roho ya kinabii iwe juu yako inakupasa kumshuhudia YESU KRISTO katika maisha yako na katika huduma yako.

 Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinaendana:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

MJUE SANA YESU KRISTO.

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

CHAKULA CHA ROHONI.

SWALI LA KUJIULIZA!


 

Rudi Nyumbani:

Print this post