Title 2023

Kwanini Bwana Yesu ajulikane kama ‘Amina’ (Ufunuo 3:14)

Jibu: Turejee,

Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye ‘ALIYE AMINA’, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu”

Neno Amina maana yake ni “Na iwe hivyo”.. Neno hili kwa lugha ya kiingereza ni “Amen” Hivyo Popote panapotajwa “Amina” au “Amen” maana yake ni “na iwe hivyo”.

Sasa kwanini Bwana Yesu ajitambulishe kwa neno hilo?..

Ni kuyatofautisha maneno yake na wengine! Kwamba maneno yake ni Thabiti.

Sasa ili tuelewe vizuri, turejee pale Bwana Yesu aliposema kuwa “Mimi ndimi Njia, na Kweli na Uzima, mtu haji kwa Baba ila kwa njia yangu mimi (Yohana 14:6)”.

Tukiunyambua huo mstari vizuri, tunapata sentensi mbili 1. Yeye ndiye Njia, 2. Mtu haji kwa Baba ila kwa njia yake yeye.

Hapo Bwana anajiita kuwa yeye “Njia” anajifananisha yeye na kitu kisicho na uhai..lakini anazidi kufafanua ni kwa jinsi gani yeye ni njia kwa kuendelea kusema… “mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye” ikiwa na maana kuwa, kwa maneno ya Yesu na maisha yake, tukiyafuata hayo tutafika mbinguni (hayo ndio njia)… Njia zipo nyingi, lakini zote hizo hazimpeleki mtu mbinguni, isipokuwa njia ya Yesu tu! Ambayo ni Neno lake.

Sasa tukirejea tena hapo Bwana aliposema yeye  ni “Amina” utaona mbele kidogo anaendelea kufafanua ni kwa namna gani yeye ni “Amina”.

Ufunuo 3:14  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, SHAHIDI ALIYE MWAMINIFU NA WA KWELI, MWANZO WA KUUMBA KWA MUNGU”.

Anasema yeye ni Amina, Shahidi aliye mwaminifu, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Maana yake maneno yake ni hakika!, akisema amesema ni lazima iwe hivyo!.. Amina yake ni amina kweli.. wengine wanazo amina lakini zinaweza zisitimie kama walivyoseme. Lakini yeye (Yesu) maneno yake ni hakika!.. akisema basi ni lazima “ITAKUWA HIVYO KAMA ALIVYOSEMA” Ndio maana anaitwa Shahidi mwaminifu.. hajawahi kusema jambo halafu lisitimie..Ni mwaminifu kwa maneno yake siku zote.

Tusome,

Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

2Wakorintho 1:20 “Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi”.

Je umemtumainia huyu ambaye Maneno yake hayapiti?. Alisema “Aaminiye na kubatizwa ataokoka (Marko 16:16)” je unadhani kutakuwa na kanuni nyingine Zaidi ya hiyo?.. Alisema wadhalimu, na wachawi, na wazinzi, na walevi hawataurithi ufalme wa mbinguni, je unadhani anadanganya??..ni kweli itakuwa hivyo!, maneno yake kamwe hayapiti, Amina yake ni amina kweli..

Je umempokea Yesu?, je umebatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu?.. Kama bado basi tafuta kufanya hivyo mapema.

Maran atha?Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je! Moyo wako upo kweli kwake?

Kuna kauli Bwana Yesu alisema kuhusiana na watu kumwelewa Mungu na uweza wake kwetu, alisema..

Mathayo 13:14  “Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. 15  Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, WAKAELEWA KWA MIOYO YAO, WAKAONGOKA, NIKAWAPONYA”

Ametaja mambo makuu matatu,

  1. Kuona – Kwa macho
  2. Kusikia –kwa masikio
  3. Kuelewa – Kwa moyo

Hatua ya mwisho ambayo Mungu anatarajia, pindi anapomfundisha mtu, au kusema naye ni KUELEWA. Hivyo ataanza kwanza kwa kumwonyesha mambo kadha wa kadha, yatapita mbele yake, ataanza kusema na yeye kwa njia nyingi, aidha kwa wahubiri wake, au ndoto, au maono, au vitu vya asili, au kwa Neno lake, au kwa maisha yake mwenyewe.. Lakini  pamoja na njia zote hizo  bado mtu huyo anaweza asimwelewe Mungu, kama Moyo wako haupo kwake.

Jambo ambalo watu wengi hatujui, ni kwamba Mungu anazungumza na kila mmoja, Na kila mmoja anaonyeshwa maono mengi na Mungu, kila mtu ameshakutana na Mungu, aidha uso kwa uso au katika roho, haijalishi ni mwema au mwenye dhambi, Lakini ni wachache sana walioweza kuielewa sauti yake iliposema nao.

Ni kwasababu gani hawaielewi? Ni kwasababu inahitaji MOYO ili kuielewa, Na sio macho au sikio. Kama moyo wako haupo kwake, sahau kumwelewa Mungu anaposema na wewe kwa njia yoyote ile. Hata kama itakuja kwa dhahiri, bado hutamwelewa. Sauti yake kwako itakuwa ni ngurumo tu, kama ilivyokuwa kipindi kile Bwana Yesu alipokuwa anazungumza na makutano kuhusiana na ufalme wa mbinguni.

Yohana 12:28  “Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena. 29  Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.30  Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu”

Ni kwanini iwe hivyo kwao? Ni kwasababu kilichowapeleka kwa Yesu sio wokovu wa Roho zao, au upendo wao kwa Mungu, kilichowapeleka kwake, ni miujiza, uponyaji, uzuri, mwonekano, mazingira, basi, hakuna jipya. Wakishapata walichokuwa wanakitafuta hao wanaondoka zao kuendelea na mambo yao ya dhambi ya sikuzote.

Ndio maana hakukuwa na hata mmoja ambaye aliyeelewa mifano yote Yesu aliyokuwa anaisema mbele ya umati. Isipokuwa wanafunzi wake tu, pamoja na wachache waliomfuata baada ya pale kutaka kufafanuliwa.

Ndugu ikiwa leo unakwenda kanisani kutimiza tu ratiba, kutazama kwaya, kuangalia watu wamevaaje, hata ukiwepo humo unasinzia, unaangalia muda utatoka saa ngapi, ni kweli utakutana na Mungu, atasema na wewe, utamwona, utahisi uwepo wake, utanena hata kwa lugha, utasisimka moyo. Lakini kumwelewa, haitakaa iwezekane. Kwasababu Mungu hajifunui kwa watu ambao  mioyo yao haipo kwake.Hana utaratibu huo.

Na sio tu kanisani, hata mahali popote pale, iwe ni shuleni, kazini, nyumbani, barabarani, Mungu huwa anazungumza, anasema kwa njia mbalimbali tena kirahisi sana, Lakini hutaelewa ikiwa huna moyo wa dhati kwa Mungu wako.

Alisema hivi;;

2Nyakati 16:9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, WALIOKAMILIKA MOYO KUELEKEA KWAKE…”

Alisema pia..

Mathayo 15:7  “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, 8  Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.

Yatupasa sasa tuondoe unafiki wa ndani, kwa kumaanisha kweli kweli kumpenda Mungu kwa moyo, ili sasa aanze kutufunulia sauti yake na kazi zake. Tukimfuata Kristo tujue kinachotupeleka kule ni Utakatifu na haki, na sio kwasababu tunashida tutimiziwe mahitaji yetu, hapo ndipo atapendezwa na sisi, na hatimaye, tutamwona kila inapoitwa leo.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

NIFANYE NINI ILI NIKUBALIWE NA YESU?

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)

Yohana 1:29 “Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”.

Bwana Yesu sehemu nyingine anajulikana hivi kama Mwana-kondoo kufuatia tabia ya kondoo ilivyo.

Kondoo ni mnyama mpole sana na mnyenyekevu, tofauti na Mbuzi.. Kondoo Anapokatwa manyoya yake huwa hajigusi anatulia sana, na pia hawezi kujichunga mwenyewe huwa anamtegemea mchungaji asilimia mia. Tofauti na mbuzi au Ng’ombe.

Lakini pamoja na hayo kondoo aliyekomaa ambaye tayari kashaota pembe ijapokuwa ni mpole lakini kuna vipindi vichache vichache anakuwa na hasira hususani wakati wa mvua, na pia anapokutana na kondoo mwingine aliye wajinsia kama yake. Hivyo Bwana Yesu hajajifananisha na kondoo aliyekomaa, kwasababu anazo kasoro nyingi.. bali anajifananisha na kondoo mchanga, (mwana-kondoo) ambaye bado hata hajaota pembe, ambaye hawezi kupambana, aliye mnyenyekevu na mpole.

Bwana Yesu naye ni mpole mfano wa huyo.. Maandiko yanamshuhudia hivyo..

Mathayo 21:5  “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.

Na yeye mwenyewe anajishuhudia hivyo  katika Mathayo 11:28.

Mathayo 11:28  “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; KWA KUWA MIMI NI MPOLE na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30  kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Je umemfuata Yesu aliye mpole?..yeye anayeongea nawe kwa sauti ya upole moyoni mwako, kwamba utubu dhambi?.

Kama bado unasubiri nini?

Okoka leo na ukabatizwe na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu nawe utapata ondoleo la dhambi…na jina lako litaandikwa katika kitabu cha uzima cha mwana kondoo na utakuwa na nafasi katika mji ule, mbingu mpya na nchi mpya.

Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?

JE! UNAMPENDA BWANA?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Rudi nyumbani

Print this post

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu,

Je kibiblia ni jukumu la wachungaji peke yao kulichunga kundi? Na mitume na manabii hiyo si kazi yao??….. kama ndio basi huenda Bwana Yesu alikosea alipomwambia Petro ambaye ni Mtume, alichunge kundi lake..

Tusome,

Yohana 21:15  “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

16  Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, CHUNGA KONDOO ZANGU.

17  Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, LISHA KONDOO ZANGU”.

Kumbe kazi ya kuchunga, na kulisha kondoo si ya mchungaji peke yake, bali hata ya mitume, na waalimu na manabii na wainjilisti… Ikiwa na maana kama Bwana amekupa watu chini yako ni lazima ujue kuwa unawajibu wa kuwachunga na kuwalisha…pasipo kuweka visababu sababu.

Sasa leo hatutazungumzia sana kuhusiana na KUCHUNGA kondoo.. lakini tutalitazama jukumu la KULISHA KONDOO ulilopewa wewe kama mtumishi wa Mungu.

Awali ya yote ni muhimu kujua kondoo ni nani?

Kondoo ni mnyama asiyeweza kujiongoza mwenyewe na Bwana Yesu anao watu ambao siku zote hawataweza kusimama wenyewe (maana yake siku zote watahitaji msaada tu ili waendelee kudumu katika Imani na katika kuifanya kazi ya Mungu). Na kundi hili ni kubwa kuliko lile kundi la watumishi wa Mungu.

Kundi hili lisipochungwa vizuri na kulishwa ipasavyo linaharibika na kupotea kabisa, na shetani ndilo analolitafuta sana….

Sasa Bwana alimpa jukumu Petro, na anakupa jukumu wewe kama mtumishi wa Mungu, pasipo kujali karama yako, kuwa LISHA KONDOO WAKE lakini si tu kondoo bali pia WANA-KONDOO, Haya ni makundi mawili ambayo ni lazima ujifunze kuyatofautisha.

Tofauti ya kondoo na Mwana kondoo, ni hii; Kondoo aliyekomaa anajulikana kwa jina hilo la “Kondoo” na kondoo aliye chini ya umri wa mwaka mmoja anaitwa “mwana-kondoo”. Sasa Bwana alimwambia Petro alishe makundi hayo yote mawili, na anatuambia pia sisi..

Chakula cha kondoo aliyekomaa ni tofauti na cha yule mchanga.. huwezi kuwalisha wote chakula kinachofanana, kwani kundi moja litadhoofika.. ukimpa maziwa kondoo aliyekomaa, atadhoofika, vile vile ukimpa chakula kigumu kondoo mchanga ataathirika.. kwahiyo ni lazima ujifunze kukigawanya chakula kulingana na makundi ya watu walio chini yako.

Ni lazima uwe na chakula cha waongofu wapya, na chakula cha waliokomaa kiimani, na ni  sharti lazima Makundi yote yale chakula cha kushiba..

Ni lazima chakula chako kilenge kuwakuza wale kondoo wachanga (maana yake wakue kiroho) na kuwanenepesha wale kondoo waliokomaa (maana yake wajae maarifa). Tukiwa watumishi wa aina hiyo basi mbele zake Bwana tutaonekana tunampenda lakini kama hatuwalishi inavyopaswa na huku tunajivuna kuwa sisi ni watumishi wa Mungu, basi bado hatujalijua pendo la Kristo?.

Hivyo Kama Mtumishi wa Mungu jenga tabia ya kulitazama kundi lako (Sawasawa na Mithali 27:23)..usiseme mimi ni Mtume sina karama hiyo?, na huku unawalisha watu mambo yasiyowajenga, hata Petro alikuwa ni Mtume na si mchungaji lakini alipewa hilo jukumu na Bwana la kulisha vizuri kondoo watakaokuwa chini yake, usiseme mimi ni Nabii sina wito huo na huku unawalisha watu maono ya uongo na mafundisho manyonge…hata Musa alikuwa ni nabii lakini alibeba jukumu hilo la kuwalisha watu amri, na sheria za Mungu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

JE! UNAMPENDA BWANA?

“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

Jibu: Turejee,

Mwanzo 4: 16 “Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni.

17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe”.

Henoko aliyeenda na Mungu hakuwa mwana wa Kaini, kwasababu Uzao wa Kaini wote ulilaaniwa, na hivyo hakutoka nabii yeyote wala mtu yeyote mwenye rekodi ya kumpendeza Mungu katika huo uzao, bali uzao wote uligharikishwa na ile gharika.

Swali kama ni hivyo kwanini Henoko aonekane hapa kama ni uzao wa Kaini?.

Jibu ni kwamba Huyu Henoko anayetajwa hapa katika (Mwanzo 4:16) sio yule aliyeenda na Mungu, bali alikuwa ni Henoko mwingine, kwasababu jina hilo ‘Henoko’ hakuwa nalo mtu mmoja tu!, bali ni wengi waliitwa kwa jina hilo, kama tu leo majina yetu yanavyoweza kuwa ya watu wengine mahali pengine.

Lakini yule Henoko, aliyekuwa mtumishi wa Mungu, na aliyempendeza Mungu alitokea katika Uzao wa Sethi na habari zake tunazisoma katika Mwanzo mlango wa 5.

Mwanzo 5:18 “Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. 

19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.

20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. 

21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. 

22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.

23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.

24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.

Huyo ndio Henoko aliyeenda na Mungu, ambaye alikuwa mwana wa Yaredi wa uzao wa Sethi, na alikuwa ni mtu wa saba kutoka kwa Adamu (Yuda 1:14). Lakini yule mwingine alikuwa mwana wa Kaini.

 Ni sawa Lameki aliyetajwa katika Mwanzo 4:18-19, ambaye alioa wake wawili, na yule aliyetajwa katika Mwanzo 5:28-31 ambaye alikuwa ni baba yake Nuhu… Hawa walikuwa ni Lameki wawili tofauti wenye tabia mbili tofauti, ingawa majina yao yalifanana…ndivyo ilivyo pia kwa hawa Henoko wawili tuliojifunza habari zao.

Sasa Ni jambo gani tunaloweza kujifunza kwa Henoko aliyeenda na Mungu?

Alikuwa ni mtu aliyeenda na Mungu; Maana yake Njia zake zilimpendeza Mungu mpaka kufikia hatua ya Mungu kumtwaa, na kabla ya Mungu kumtwaa biblia inasema alionyeshwa ujio wa Bwana, siku ile atakayokuja na watakatifu wake kwaajili ya vita vya Harmagedon na utawala wa miaka 1000 duniani.

Yuda 1:14  “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15  ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”

Bwana atusaidie na sisi tuwe watu wa kwenda  na Bwana katika njia zake kama alivyokuwa Henoko.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Wanefili walikuwa ni watu gani?

EPUKA MAKUNDI ILI UTAKATIFU WAKO UDUMU!.

Rudi nyumbani

Print this post

IPENDE BUSTANI YAKO.(Ilime, itunze)

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Ipo tabia ambayo tunapaswa tujifunze kuhusu Mungu. Kama tunavyojua, alipomaliza kuumba vitu vyote ndani ya zile siku saba, zoezi la mwisho kabisa lilikuwa ni Mungu kupanda bustani mashariki mwa Edeni. Tengeneza picha, bustani hiyo ilikuwaje! Bila shaka ilikuwa ni nzuri sana. Mungu alifanya kazi ya kuchukua Ua hili, Ua lile, ukoka huu, ukoka ule, mti huu wa kivuli, mti ule wa matunda kila moja mahali pake stahiki.. Yaani kwa ufupi Edeni ni bustani ambayo iliundwa kwa kila aina ya mmea, lakini katika mpangilio bora. Jambo lililoifanya bustani ile kuwa tofauti na maeneo mengine yote duniani.

Kwani huko kwingine kulijiotea otea, bila mpangilio maalumu. Japo pia napo kulikuwa pazuri lakini sio kama Edeni, kwasababu ile ni bustani iliyopandwa sio kujiotea. Lakini tunaona, asili ya ile Bustani. Ni kwamba ilihitaji kulimwa na matunzo baada ya pale ili iendelee kuwepo vilevile katika ubora wake. Hii ikiwa na maana kama isingetunzwa na kulimwa, ingepotea kabisa, na kufanana tu na sehemu nyingine yoyote ya dunia.

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya…15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Watunza bustani wanaelewa jambo hili, mahali ambapo wanazipanda, huwa ni lazima mara kwa mara, wawepo kung’oa majani-shambulizi yanayojitokeza, wanafyeka ukoka unapozidi kimo, wanatia mbolea panaposua sua, na wanainyeshea bustani kila siku, na wakati mwingine kuiwekea uvuli. Hivyo ni kazi ambayo inamgharimu mtunza bustani kuwepo pale wakati mwingi.

Ndivyo ambavyo Mungu alimpa jukumu hilo Adamu, kwamba aitunze bustani na kuilima, kwasababu hilo halikuwa jukumu lake tena. Tafsiri yake ni kwamba ili aendelee kukaa katika mahali pazuri pa nchi. Hana budi kupalima na kupatunza. Asipofanya hivyo pataendelea kuwa kama sehemu nyingine tu ya dunia.

Lakini Adamu, hakuweza kudumu katika bustani ile kwasababu aliyakaidi maagizo ya Mungu.

Hii ikifunua nini?

Kila mtu ameandaliwa Edeni yake hapa duniani, ambayo atamfurahia Mungu wake katika hiyo. Si kila mazingira Mungu amekuwekea wewe kumfurahia yeye, si kila mahali ni Edeni yako. Ipo sehemu maalumu, ambapo hapo Mungu anakuundia kisha wewe unapatunza baada ya hapo.

Na sehemu yenyewe ni ndani ya Kristo.

 Maana yake ni kuwa ukishaokoka, tayari Mungu amekuwekea mema yako mbeleni. Hivyo kuanzia huo wakati huna budi kuanza kuistawisha bustani yako kwa kuitilia mbolea mara kwa mara, kuinyeshea maji, kuipalilia, kuichonga n.k.. Ndio hapo, linakuja suala la Maombi ya mara kwa mara, mikesha, mifungo, kutafakari Neno, kufanya ibada za sifa,  kutoa sadaka, kujitenga na dhambi, na kushuhudia.

Unapokuwa mtu wa namna hii ndivyo unavyoifanya bustani yako kupendeza siku baada ya siku rohoni, ndivyo inavyojitofautisha na sehemu nyingine za dunia, kwa uzuri wake. Matokeo yake ni kuwa Dunia yako itakuwa ya neema sikuzote yenye furaha, Amani na mafanikio, yenye kububujika maziwa na asali. Lakini ukikaa tu ukasubiri, ukasema Mungu atatenda, huku huyatunzi  maneno ya Mungu ndani yako, sahau kuona mabadaliko yoyote maisha yako yatakuwa hayana tofauti na yale ya kale, kwasababu kazi ya utunzaji sio ya Mungu bali ni yako. Wewe umemsubiria Mungu, wakati Mungu alishamaliza kazi yake.

Litunze sana Neno la Mungu, kwa kuliishi sio kulisikia tu. Kwani wanaofanya hivyo wanafungua milango mingi sana ya kiroho, Kanisa la Filadelfia ndio kanisa pekee lililopendwa na Kristo kwasababu liliyatunza maneno yake, na matokeo yake likafunguliwa mlango wa mafanikio mbele yake.

Ufunuo 3:8  “Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe UMELITUNZA NENO LANGU, wala hukulikana jina langu”.

Hivyo anza sasa kujibidiisha kulitendea kazi Neno la Mungu. Kwa jinsi unavyolitunza ndivyo utakavyoona mabadiliko yako.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Tunaishi katika dakika za nyongeza tu? Dalili zote zilizotabiriwa kuhusiana na kurudi kwa pili kwa Yesu zimeshatimia?. Wasubiri nini? Ukifa leo utajibu nini mbele ya kiti cha enzi cha Mungu?  Tubu sasa ukabatizwe, upokee ondoleo la dhambi zako. Ikiwa bado hujafanya hivyo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo; +255693036618/+255789001312

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

EDENI YA SHETANI.

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Rudi nyumbani

Print this post

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia!.

Usipoujua ufunuo umhusuyo Yesu hutaona sababu ya kumwamini wala kumfuata, vile vile usipopata ufunuo wa kutosha uhusuo ubatizo hutaona umuhimu wa kubatizwa! (utaona ni habari tu ya kawaida, kwamba ukibatizwa au usipobatizwa vyote ni sawa tu).

Nataka nikuambie ndugu, ubatizo ni tendo la muhimu sana kuliko wengi tunavyodhani. Na leo nataka tuone ni jinsi gani agizo la Ubatizo lilivyoambata na Toba, kwamba baada ya kutubu ni lazima kubatizwa.

Hebu tuyasome maneno yafuatayo ya Bwana Yesu..

Luka 24:46  “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47  na kwamba mataifa yote “WATAHUBIRIWA KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI, kuanza tangu Yerusalemu”.

Nataka tuone na kuutafakari kwa kina huo mstari wa 47 unaosema kuwa mataifa yote watahubiriwa “KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI”

Hili ni agizo ambalo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake kwamba watu wote ni lazima wahubiriwe habari ya toba na ondoleo la dhambi kwa jina lake.

Mitume walilisikia hili agizo la Bwana, na walilishika  sasa hebu tuangalie ni kwa namna gani walilitekeleza,..je walikwenda kuwaambia tu watu “watubu waondolewe dhambi zao au kuna la ziada walilifanya ”

Tusome kitabu cha Matendo 2:36-38

Matendo 2:36  “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona hapa! Petro anawaambia watu “watubu na kubatizwa kwa jina lake Yesu, wapate ondoleo la dhambi zao”.. na sio tu “Tubuni mpate ondoleo la dhambi”….. sasa linganisha na yale maagizo Bwana aliyowapa akina Petro kuwa “wakawahubirie watu wote kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi”.

Kumbe kuhubiriwa habari ya Toba na ondoleo la dhambi ni pamoja na ubatizo!.. Maana yake ili mtu apate ondoleo kamili la dhambi zake ni lazima pia akabatizwe (Katikati ya Toba na ondoleo la dhambi, kuna ubatizo ambao shetani kawafumba watu macho wasiuone)..Ndio maana ni ngumu leo hii wengi kushinda dhambi, kwasababu mzizi wa dhambi katika maisha yao haujaondolewa, kwasababu wameukosa ubatizo sahihi.

Mitume sehemu zote walihubiri hivi, kwamba watu baada ya kutubu ni lazima wakabatizwe ili dhambi zao ziondolewe… na mitume kamwe wasingeweza kufanya kitu chochote kilicho kinyume na maagizo ya Bwana Yesu…ikiwa na maana kuwa walimwelewa sana Bwana pale aliposema kuwa wakawahubirie mataifa yote kwa jina lake, kwamba ubatizo pia kwa jina lake ni sehemu ya mahubiri yao.

Swali ni je!, na wewe umebatizwa kwa maji mengi na  katika ubatizo sahihi wa jina la Bwana Yesu?.. Kumbuka, kama ulibatizwa utotoni basi fahamu kuwa watoto wachanga hawabatizwi kwasababu bado hawajatubu, (kujitambua hawajajitambua watawezaje kutubu?) ni sharti kwanza wahubiriwe wamwamini Mwokozi na kujijua kuwa wao ni wenye dhambi ndipo watubu na kubatizwa.  Bwana akubariki.

Tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa, na kama utahitaji msaada Zaidi wa namna ya kupata ubatizo karibu na mahali ulipo basi utawasiliana nasi kupitia namba zetu hapa chini.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

HUNA SHIRIKA NAMI.

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Rudi nyumbani

Print this post

Wakolosai 3:5 inamaana gani?

SWALI: Wakolosai 3:5 inamaana gani?. Tofauti kati ya tamaa mbaya na kutamani ni ipi?


JIBU: Wakolosai 3:5 Inasema..

  “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;”

Hapo anaanza kwa kusema vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi. Ikiwa na maana kuwa kuna viungo vya duniani ambavyo kazi yake kimsingi ni kutimiza mapenzi ya duniani (ya shetani). Tofuati na vile vya ki mbinguni ambavyo vinatimiza mapenzi ya Mungu. Viungo hivi sio mikono, miguu, macho, masikio au pua hapana, bali viungo vya rohoni.

Viungo vya kimbinguni vimeelezwa kwenye mstari wa 12-17. Lakini vya duniani ndio hivi vinavyozungumziwa hapa katika mstari wa 5, ambavyo tunapaswa tuviue. Navyo ni;

1) Uasherati.

Uasherati unajumuisha kitendo chochote cha zinaa nje ya ndoa pamoja na mambo yafanywayo kinyume na asili. Ikiwemo Uzinzi, ufiraji, na ulawiti. Vitu hivi havipaswi vipewe nafasi kwa mtakatifu yoyote.

2) Uchafu

Uchafu ni kinyume na usafi. Mtu mchafu kimsingi anakuwa amebeba takataka katika mwili wake. Vivyo hivyo, mtu ambaye anaruhusu takataka za hii dunia zimtawale ni mchafu kiroho. Mfano wa takatakata hizi ni miziki ya kidunia, anasa, matusi, ulevi, kubeti, mazungumzo yasiyofaa, kutazama vitu visivyojenga mitandaoni, ushabiki n.k. Epuka kujitia unajisi na vitu vya ki-ulimwengu.

3) Tamaa mbaya.

Kuzipa tamaa za mwili nafasi ya kukutawala. Na matokeo ya tamaa hizi mbaya kukutawala ndani yako, utaishia, ni kutazama picha chafu, muda wote kuwa na mazungumzo ya kizinzi, kuchat na jinsia tofauti na wewe kusikokuwa na sababu, kuvaa mavazi ya namna hiyo au kujiwekwa kimwili uvutie uzinzi kwa mwengine. Tabia hizi ndani yako unapaswa uziue.

4) Mawazo mabaya.

Mawazo mabaya ni kinyume cha mawazo mazuri. Mtu mwenye mawazo mazuri huwaza yaliyo mazuri, ya kujenga. Lakini mwenye mawazo mabaya sikuzote ni kubomoa. Mawazo hayo ni pamoja na wivu, rushwa, uongo, wizi, uuaji, unafki, visasi,. Hivi havipaswi kuonekana ndani ya mkristo.

5) Kutamani.

Kutamani kunakozungumziwa hapa sio kule kwa tamaa za mwili, hapana, bali tamaa ya mambo ya kidunia, mfano tamaa ya kuwa na mali, tamaa ya kufanana na watu wa kidunia, wanamiziki, wanamitindo n.k., na hizo ndizo zinazompelekea mtu, kugeuza vitu hivyo kuwa kama mungu wao, kuvitafuta na kuvisumbukia sikuzote .Na ndio maana mwandishi anamalizia kwa kusema “Ndiyo ibada ya sanamu” maana yake rohoni vinaonekana ni miungu kwao. Jiepushe na kutamani.

Hivyo  tukifanikiwa kuviua viungo hivi, basi mwili hauwezi kuwa na matunda yoyote, kwasababu hakuna kiungo chake hata kimoja kina uhai. Lakini pia anasema,

Wakolosai 3:12  Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13  mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14  Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15  Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.

16  Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

17  Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.

Hivyo ndivyo viungo vya kimbinguni, Tujitahidi vituvae.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Nini maana ya huu mstari “sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje”

WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Rudi nyumbani

Print this post

Birika walilooga Makahaba lilikuwaje?

Swali: Katika kifo cha Ahabu, biblia inasema alikufa na gari lake likaenda kuoshwa katika birika ambalo wanaoga Makahaba, (1Wafalme 22:38)..hili birika walilokuwa wanaoga makahaba lilikuwaje?

Jibu: Turejee.

1Wafalme 22:37 “Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria. 

38 Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la Bwana alilolinena. 

39 Na mambo yote ya Ahabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na nyumba ya pembe aliyoijenga, na miji yote aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?”

Ikumbukwe Ahabu alimwua Nabothi Myezreeli na kumdhulumu kiwanja chake, (1Wafalme 21:1-16), na baada ya kumwua ndipo unabii ukaja kupitia Eliya, kumwambia kuwa atakufa na damu yake italambwa na mbwa kama alivyomwua Nabothi (soma 1Wafalme 21:17-27).

Baada ya miaka mitatu, ndipo unabii huo unakuja kutimia, Mfalme Ahabu alikufa alipokuwa vitani na damu yake ikalambwa na mbwa mahali pale pale mbwa walipolamba damu ya Nabothi.

Lakini tunasoma tena jambo lingine lililoambatana na kifo cha Ahabu, kwamba mahali pale gari lake lilipooshwa ni mahali pia Makahaba wanapooga.

Sasa biblia haijaeleza kwa kina hili birika ambalo walikuwa wanaoga makahaba lilikuwaje. Lakini ni wazi kuwa hili halikuwa birika la kiyahudi, Kwani mabirika/ mabwawa ya kiyahudi yalikuwa yanatumika na makuhani na watu wa kawaida katika kuoga(kutawadhia) ili kujitoa unajisi.

Walawi 15: 16 “Na mtu ye yote akitokwa na shahawa yake, ndipo ataoga mwili wake wote majini, naye atakuwa najisi hata jioni”.

Soma pia Walawi 15:13, Kumbukumbu 23:10-11.

Lakini hili Birika/bwana hili ambalo makahaba walikuwa wanaoga, lilikuwa katika mji wa Samaria mtaa wa Yezreeli, ambao ndio ulikuwa kitovu cha ibada zote za mungu baali. Hivyo hili halikuwa bwawa la dini ya kiyahudi, bali lilikuwa ni bwawa la mungu baali. Huenda makahaba walikuwa wanaoga hapo kulingana na desturi zao za kibaali, kwani desturi nyingi za dini ya kibaali zilikuwa zinakaribia kufanana na za dini ya kiyahudi.. (mfano wa hizo utaona ni ile sadaka Ahabu aliyoitoa katika 1Wafalme 18:20-30).

Hivyo huenda nao pia walikuwa na desturi kama hiyo ya wayahudi ya kujiosha katika mabwawa/mabirikia.

Lakini lililo kubwa la kujifunza hapo ni kuwa Neno la Mungu kamwe halipiti.. Alisema Ahabu atakufa na damu yake italambwa na mbwa, na kweli alikufa sawasawa na neno hilo miaka mitatu baadaye, katika kifo cha aibu zaidi hata ya  kile alichomuua Nabothi.

Na vile vile alisema, kuwa atarudi tena pamoja na ujira wake kulimlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo, Neno hilo halitapita, ni lazima litimie na sasa tupo katika siku za kurudi kwake, muda wowote unyakuo unatokea!

Ufunuo 22:12  “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13  Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14  Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”

Je umeokoka kikweli kweli au bado una uvuguvugu?…Ufunuo 3:16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”.

Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

BIRIKA LA SILOAMU.

USIMPE NGUVU SHETANI.

Baali alikuwa nani?

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

Rudi nyumbani

Print this post

Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).

Jibu: Turejee,

Matendo 21:25 “Lakini kwa habari za watu wa Mataifa walioamini, tuliandika na kutoa hukumu yetu ya wao kujilinda nafsi zao na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na kitu kilichosongolewa, na uasherati”


Vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu ni vyakula vyote vinavyotolewa kwa maagizo ya kishetani.
Mfano wa vyakula hivyo ni vile vya kimila au vya waganga wa kienyeji.

Mfano wa vya kimilia ni vile ambavyo mtu anakula au analishwa kwa lengo la kumkinga na madhara fulani ya kiroho kama uchawi au kumpatanisha na roho fulani..


Ndio hapo utakuta mtu anaambiwa alete mbuzi, au kondoo na kisha yule kondoo achinjwe kama sadaka/kafara kwa mizimu na kisha ale sehemu ya nyama ya huyo mnyama aliyetolewa sadaka… Sasa endapo mtu huyo akila hiyo nyama au sehemu ya hiyo nyama tayari anakuwa amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Au utakuta mtu anaenda kwa mganga wa kienyeji na yule mganga anamwambia ili tatizo lake litatulike basi alete mnyama fulani aidha mbuzi, au ng’ombe au kuku na achinjwe kama kafara na nyama yake au damu yake inywewe na mhusika.. Mtu anayekula hiyo nyama anakuwa tayari amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Au anaweza asiambiwe alete mnyama, bali akaambiwa alete hata nafaka fulani na kisha ile nafaka ikatolewa kwa miungu na mtu akaambiwa ashiriki sehemu ya ile nafaka..sasa mtu huyo endapo akila kile chakula au sehemu ndogo ya kile chake basi anakuwa amekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu.


Na mtu anayekula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, anakuwa anajiungamanisha na ile madhabahu ya kishetani..ndivyo biblia inavyosema.


1 Wakorintho 10:19-22 “Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?
20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.
21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?


Hiyo ni tahadhari kwetu kuwa tujiepushe na vyakula vya namna hiyo kwani ni hatari kiroho.
Lakini kama umealikwa mahali na umetengewa chakula ambacho kimetolewa sadaka kwa sanamu na ukala bila kujua kuwa kilikuwa kimetolewa sadaka kwa miungu, hapo hupaswi kuogopa kwasababu lile andiko ya kwamba “tutakula vitu vya kufisha navyo havitatudhuru (Marko16:18)” litatimia juu yako.


Lakini kama umeshajua kuwa chakula hicho ni cha miungu basi hupaswi kula kabisa..


Je umewahi kula au kulishwa chakula cha namna hiyo katika familia yenu au ukoo wenu au kwa waganga wa kienyeji?..Kama ndio basi fahamu kuwa siku ulipokula tayari ulijiungamanisha na hiyo miungu, na hivyo roho za hiyo miungu zitayaongoza maisha yako siku zote.


Hivyo suluhisho ili uweze kufunguka ni wewe kwanza kutubu mbele za Bwana kwa kumaanisha na kisha kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38) na mwisho kupokea Roho Mtakatifu..Kwa hatua hizo utakuwa umefunguliwa moja kwa moja.


Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Rudi nyumbani

Print this post