Zaburi 42:7
[7]Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tutafakari pamoja Neno la Mungu.
Biblia inatuambia kila jambo tunalolifanya lina matokeo sawa rohoni. Ikiwa wewe ni mwizi malipo ya wizi utayapata rohoni, ikiwa wewe ni muuaji, malipo ya uuwaji utayapokea vilevile rohoni, mito ya maji inapoelekea huko huko ndipo inaporudia.
Ufunuo 13:10
Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.
Sasa hapo tumeona katika eneo la ubaya, je vipi katika upande wa Mema?
Maandiko hayo hayo yanatuambia kwamba Kilindi hupigia kelele kilindi.
maana yake ni nini?
kilindi ni mahali pa katikati kabisa mwa bahari. Sasa mwandishi wa zaburi anatumia mifano ya kitu halisi kana kwamba kinaongea… anasema Kinaita chapigia kelele kilindi. Na cha kushangaza ni kwamba hakiiti eneo lingine lolote la maji labda ufukweni.. au kwenye rasi, au ghuba.. hapana bali kinapigia kelele kilindi chenzake.
Kilindi chapigia kelele kilindi
Maana yake ni nini?
Tukitaka mambo ya ndani ya Mungu, mambo ya vilindini, lazima na sisi tuwe vilindini. Ni muunganiko wa ki-Mungu. kila kiwango kina sauti yake. kamwe hizo sauti haziingiliani, ni sawa na mbwa amwite tai kwa sauti yake ya kubweka, haiwezekani kuja inahitaji, ajifunze sauti yake ili yule tai aelewe, vinginevyo atakuwa anapiga kelele tu.
Na sisi vivyo hivyo kwa Mungu, wengi tunatamani tumwone Mungu kwa undani katika maisha yetu, lakini hatutaki tuzame ndani yake.
Mwandishi wa Zaburi mwanzoni kabisa kabla hajasema maneno hayo kwenye hiyo sura 42 anasema
Zaburi 42:2-3
[2]Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?
[3]Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako.
Kuonyesha ni mtu ambaye alimtamani sana Mungu wake.
Sehemu nyingine Daudi anasema..
Zaburi 63:1-8
[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.
[2]Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.
[3]Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.
[4]Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
[5]Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.
[6]Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.
[7]Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
[8]Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.
Umeona, usiku kucha, anamtafakari Mungu, kuonyesha ni mtu ambaye moyo wake upo kwa Mungu asilimia mia..unategemea vipi mtu kama huyo Mungu asijifunue kwake kwa viwango vile?
Nafasi hii pia mimi na wewe tunayo. Tumfuate Mungu wetu vilindini, ili ajifunue kwetu katika viwango vingine..
Na hiyo inakuja kwa kile Bwana Yesu alichosema..Tujitwike misalaba yetu tumfuate, tuwe tayari kuacha vyote visivyompendeza yeye na kumtii. Na kwa kufanya hivyo rohoni tunatafsirika kuwa tunamwita Mungu wa vilindini.
Anza sasa.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?
Je “Kaaba” ni nini na ipo kwenye biblia?, Na wanyama wanaochinjwa kuelekea Kaaba je tunaruhusiwa kuwala?.
Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.
Kama hujapitia sehemu ya kwanza ya Makala hii, inayohusu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu pamoja na unabii wake basi waweza fungua hapa >>> UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).
Leo tunaendelea na sehemu ya pili, na tutalitazama “Jiwe la Kaaba” na uhusiano wake na Imani ya kikristo.
“Kaaba” au kwa jina lingine al-Ka’ba al-Musharrafa ni jengo la “Jiwe Jeusi” lililopo katikati ya msikiti uitwao “Masjid al-Haram” uliopo mahali pajulikanapo kama “Makka”, huko nchini Saudi Arabia.
Jiwe hili linaaminika na dini ya kiislamu kuwa “nyumba ya mungu”. Na pia linaaminika kuwa ni ufunuo Mungu aliompa Abramu (Ibrahimu) pamoja na Ishaeli mwanae kama mahali pekee na sahihi alipopachagua Mungu pa kuabudia, kulingana na Quran, Al Imran 3:96 (Sasa kujua ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).
Zaidi inaaminika kuwa mahali hapo “Kaaba (hapo Makka)” ndipo mahali ambapo Malaika walikuwa wakimwabudu Mungu kabla ya mwanadamu kuubwa, na baadaye mwanadamu alipoumbwa ndipo Adamu akapajenga tena mahali hapo kama sehemu ya kumwabudu Mungu, na baadaye baada ya mafuriko ya Nuhu mahali hapo pakapotea, pakawa hapajulikani, na alipotokea Ibrahimu ndio akapata ufunuo wa mahali hapo (kujua usahihi na ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).
Baadaye kulingana na imani ya kiislamu, Abramu (Ibrahimu), aliambiwa awaambie wageni wote kutoka uarabuni na kila mahali wasafiri na kufika hapo kuhiji, na hiyo ndio sababu ya watu wa Imani ya kiislamu kuwasili huko Makka kuhiji kila mwaka.
Na si tu watu kuwasili pale, bali pia wanyama wachinjwapo wanaelekezwa (kibla) huko Maaka palipo na Kaaba.
Swali?.. Je ukweli wa mambo huu ni upi?
Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa Mwana wa Ahadi alikuwa ni Isaka mzao wa Sara, na si Ishmaeli aliyekuwa mzao wa kijakazi Hajiri.. Ingawa Mungu alimbariki pia Ishmaeli mwana wa Hajiri, lakini hakuwa amekusudiwa kubeba ahadi yoyote ya urithi wa mzaliwa wa kwanza, kwanini?.. kwasababu hakuwa mwana wa mke halali wa kwanza wa Abramu, na hiyo ndio sababu ya Sara kumfukuza Hajiri, na Mungu akawa upande wa Sara.
Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.
10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.
11 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.
12 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.
13 Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.
14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba”.
Sasa Imani ya kiislamu inaamini kuwa Ishmaeli(au Ismail) ndiye mwana wa ahadi halali wa Abramu, na biblia haisemi hivyo, na hapa ndipo MAKOSA YALIPOANZIA!!!!...Ndipo adui alipoanza kutengeneza MTI WAKE!!.
Na kwasababu hiyo, ya kuamini kuwa Ishmaeli ndiye mwana wa ahadi na si Isaka, basi ndipo zikazuka habari nyingine zisizo za kweli kwamba Abramu alishuka mpaka Makka na kupewa ufunuo uliopotea zamani kuwa mahali pa kuabudia ni hapo Makka, na pia zikatengenezwa habari nyingine kuhusiana na kisima maarufu kijulikanacho kama ZAMZAM, ambacho tutakuja kukiangalia katika Makala inayofuata na hatari yake kiroho.
Ukweli ni kwamba Abramu baada ya kumruhusu Hajiri aondoke na Ishmaeli, hakuendelea kufuatilia habari zake kwani Mungu alishamwambia amsikilize Sara, na ajihusishe na Isaka Zaidi ya Ishmaeli, hivyo si kweli kwamba Abramu aliwahi kushuka Saudi Arabia akiwa na Ishmaeli na kupewa ufunuo wa mahali hapo Makka, na hata biblia haionyeshi mahali popote jambo hilo.
Zaidi biblia inaeleza wazi kuwa baada ya Isaka kumzaa Yakobo, na Yakobo kulizaa Taifa la Israeli, kupitia Taifa hilo la Israeli alitokea Mfalme Daudi, ambaye baada ya kumpendeza sana Mungu, ndipo Mungu akauchagua mji wake Daudi (yaani Yerusalemu) uwe mahali pa kuweka nyumba yake na jina lake, na mahali pa kuabudia mpaka nyakati zake Masihi (yaani YESU).
2Nyakati 6:5 ”Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli;
6 LAKINI NIMEUCHAGUA YERUSALEMU, JINA LANGU LIWE HUMO; NA DAUDI NIMEMCHAGUA AWE JUU YA WATU WANGU ISRAELI”.
Na tangu wakati ambapo Hekalu la Mungu lijengwe na Sulemani, mwana wa Daudi pale Yerusalemu, wenye Imani ya kiyahudi ndio walikuwa wanatoka Mataifa mbali mbali kwenda kuabudu pale, kwamaana ndio mahali alipopachagua Mungu aliweke jina lake.
Na hata watu wakiwa mbali walikuwa wanaabudu kuelekea Yerusalemu mahali hekalu lile lilipojengwa, mfano wake ni nabii Danieli katika Danieli 6:10, soma pia 1Wafalme 8:29-30.
Hivyo watu waliendelea kuwasili Yerusalemu mahali pale ambapo Mungu alipachagua, kwa miaka mingi ndio maana hata kibla ya kwanza ya uislamu ilikuwa ni hapo hapo Yerusalemu, walipokuja kujenga msikiti, mahali hekalu lilipojengwa, ingawa walikuja kugeuza na kusema si hapo tena bali ni Makka, penye “Kaaba”.
Na Masihi alipokuja (YAANI YESU KRISTO) ndipo atakapoonyesha sehemu sahihi ya kuabudia, alipopachagua MUNGU kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu, na kwamba watu wote wakusanyike hapo ili wamwabudu MUNGU sawasawa na mapenzi yake.
Kwani watu wote walijua kuwa siku Masihi atakapokuja atasahihisha mambo yote, na kuonyesha njia sahihi, sasa njia hiyo ni ipi?? Tusome maandiko yafuatayo..
Yohana 4:19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, NANYI HUSEMA YA KWAMBA HUKO YERUSALEMU NI MAHALI PATUPASAPO KUABUDIA.
21 Yesu akamwambia, MAMA, UNISADIKI, SAA INAKUJA AMBAYO HAMTAMWABUDU BABA KATIKA MLIMA HUU, WALA KULE YERUSALEMU.
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. KWA MAANA BABA AWATAFUTA WATU KAMA HAO WAMWABUDU
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.
26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye”.
Umeona mahali sahihi alipopachagua Mungu pa Ibada?.. Si Yerusalemu tena, wala mahali pengine popote bali ni katika Roho Mtakatifu, na katika kweli ya MUNGU.
Maana yake kama mtu hana Roho Mtakatifu ndani yake basi hawezi kuwa na ibada halisi, kama hawezi kuutunza mwili wake na roho yake, basi hakuna mahali pengine popote duniani atakapoweza kumfanyia Mungu ibada akaikubali, kwasababu maandiko yanasema miili yetu ni HEKALU la ROHO MTAKATIFU (Soma 1Wakorintho 3:16 na 1Wakorintho 6:19).
Na Hekalu tafsiri yake ni sehemu ya nyumba ya ibada, hivyo ibada ya kwanza inaanza ndani ya mtu, hiyo ikiharibiwa mtu huyo hata aende wapi hawezi kumwona MUNGU wala kukutana na MUNGU, hata apae juu ya sayari zote, bado atakuwa mbali na Mungu na maombi yake hayasikilizwi.
Lakini kama akitakasika katika utu wake wa ndani na wa nje, basi mahali popote pale alipo ibada itakuwa inabubujika ndani yake, na hiyo ndio siri ya agano jipya.
Sasa swali ni je!, Wanaoenda Yerusalemu au Makka wanafanya makosa?
Kama mtu ataenda Yerusalemu kwa lengo la utalii, au kujifunza mambo, na pengine kumshukuru Mungu kwa atakayojifunza…hafanyi makosa lakini kama ni kwa lengo la Ibada, akiamini kuwa ile ni ardhi takatifu, hivyo atakokea kitu cha ziada, anakosea sana kwasababu Bwana Yesu alishasema.. saa yaja, nayo ipo, kwamba waabuduo halisi hawataenda tena Yerusalemu, bali watamwabudu katika roho na kweli.
Vile vile wanaoenda kuhiji Makka, wapo nje ya Imani kabisa, kwasababu hata huko Makka hapajaagizwa kabisa na Mungu, ni ufunuo wa ibilisi uliosambaa ili kuwafanya watu wasimwabudu MUNGU WA KWELI katika roho na kweli, badala yake katika makosa makubwa. Hivyo wanaokwenda kuhiji Makka wanahitaji msaada wa kumjua YESU, na NEEMA yake, ili watoke katika hayo makosa.
Hali kadhalika hakuna agizo lolote la mnyama achinjwapo basi aelekezwe Yerusalemu wala Makka, hayo pia ni maagizo ya ibilisi, ambayo yanalengo la kuingiza roho katika vile tuvilavyo.
Ikiwa nyama inauzwa buchani, Mkristo anaweza kuinunua akiongozwa na Amani ya Roho mtakatifu, na baada ya kuinunua anaweza kuitakasa kwa maombi, kisha akaitumia, lakini kama katika bucha hilo, wauzaji wamekiri waziwazi kuwa nyama hiyo imechinjwa kwa kuelekezwa kibla yoyote ile iwe ya Yerusalemu au Makka au penginepo popote nyama hiyo usinunue wala usile, kwasababu ya Dhamiri, ndivyo maandiko yasemavyo..
1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;
26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo
27 Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.
28 Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.
29 Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?”
Usikose mwendelezo wa sehemu inayofuata wa Kisima cha Zamzam, na mengineyo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?
Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 Nami nitaonekana kwenu, asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka
Huu ni utabiri ambao Mungu aliwaambia Israeli, pindi tu walipochukuliwa utumwani Babeli, akiwaahidia atawarudisha tena kwenye nchi yao baada ya miaka sabini. Na zaidi ya hayo akawapa pia na Neno la ahadi kwamba wakati huo wakimtafuta kwa mioyo yao yote, watamwona, watamwomba atawasikia, na wote watarejeshwa nyumbani ijapokuwa walichukuliwa mbali sana.
Na kweli utabiri huo ulikuja kutumia, kwani mwishoni mwa hiyo miaka sabini, mbiu ilipigwa waisraeli wote warudishwe kwao. Na aliwaonekania sana pindi waliporejea.
Ni neno la ahadi hata kwetu,
Kwamba tukimtafuta yeye kwa mioyo yetu yote, tutamwona. Kumbuka anasema “MIOYO YETU YOTE”. Kosa linatokea pale tunapompenda Mungu kwa sehemu, leo kwake kesho kwa shetani. Ndio Inayopelekea tusimwone Mungu katika ukamilifu wake wote. Mungu anahitaji vyako vyote vielekee kwake, ndipo tumwombe na kumwita ili atuitikie..
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Rudi Nyumbani
Darasa la Kwanza:
KUIFUNGUA BIBLIA.
Mwendelezo unakuja…..
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU
Katika mapokeo ya kikristo, moja ya eneo ambalo limezuia mikanganyiko mingi, ni eneo hili linalohusiana na “Uungu wa Mungu” . Migawanyiko ya madhehebu mengi unayoyaona sasa chimbuko kubwa hasaa ni hapa.
Wapo wanaoamini Mungu ni mmoja amegawanyika katika nafsi tatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu), lakini wapo wanaoamini Mungu ni mmoja mwenye nafsi moja (Hajagawanyika), yaani Yesu ni Yule Yule Yehova aliyekuwa zamani zile, wengine hawaamini kabisa kama Yesu anastahili kuwekwa katika nafasi ya uungu, wengine hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, bali ni nguvu tu ya Mungu, ni Yesu na Mungu tu basi. Je! Ukweli ni upi? Na Je tunapaswa tusimamie wapi?
Jambo la kwanza kufahamu, ni kuangalia kiini, cha kumjua Mungu? Kama kiini kimeharibika hapo ndipo penye shida kubwa. Tunaposema kiini, tunamaanisha idadi ya miungu. Cha ajabu ni kwamba makundi yote haya yanaamini “Mungu ni mmoja”, sawasawa na maandiko yanavyosema..
Marko 12:29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, BWANA MUNGU WETU NI BWANA MMOJA;
30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.
Tena kizuri zaidi ni kwamba wote wanaamini kazi ya Kristo ya ukombozi, wanaamini pia kazi za Roho Mtakatifu mioyoni mwetu.
Kinachotofautisha ni kutambua tu, nafasi zao za kiungu. Hilo tu, ambalo kimsingi halina nguvu sana, zaidi ya kuzitambua kazi zao mioyoni mwetu. Ni sawa na watu wawili wanaoshindania kama MUWA, ni jamii gani ya mmea, mmoja anasema ni tunda, mwingine anasema ni aina ya jani. Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, ukiulizwa swali hilo utasema ni nini?. Ni rahisi kusema “muwa” ni tunda, lakini kibaolojia muwa ni jamii ya “jani”, isipokuwa limerefu tu zaidi ya mengine na lina maji matamu, .
Sasa je! Kufahamu kama ni jani, au ni tunda? Maarifa hayo yanaweza kubadili asili yake? Kwamba ukifahamu sukari yake itaongezeka, au itawabadilikia maumbo. Wewe na yeye hamna tofauti, kiladha, isipokuwa kiufahamu tu.
Vivyo hivyo na kwenye uungu wa Mungu, Tunatafuta “UJUZI”. Na ujuzi ni mzuri, lakini mara nyingi tunapoung’ang’ania sana haujengi, bali huleta matengano, Ni upendo tu ndio unaojengwa.
1Wakorintho 8:1b…Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga
Ndio maana kwanini hatushangai kuona kanisa la kwanza, liliweza kutembea katika utimilifu wote wa ki-Mungu ijapokuwa hawakuwa na maarifa ya kutosha ya kutambua uungu wa Yesu, vema, isipokuwa baadaye sana katika nyaraka za mitume, ambayo hata hivyo waliita ‘Siri ya Mungu’. Lakini hao hao waliweza kumwabudu Kristo, lakini pia wakamwabudu Baba, bila shida yoyote, wapo waliotambua siri hii, lakini wapo ambao hawakutambua vema.
Kuonyesha kuwa hilo sio jambo la kung’ang’ania sana kana kwamba usipojua utakwenda kuzimu, kama inavyochukuliwa leo, mpaka kutupelekea matengano.
Ukweli ni kwamba Mungu wetu ni Yule Yule mmoja, isipokuwa ametenda kazi kwenye nafasi tatu tofauti kwa lengo la kumkamilisha mwanadamu, na sio yeye. Na sio kana kwamba ni watu watatu wamepatana katika jambo moja. Ni sawa na maji, mvuke na barafu. Vyote vitatu vikiwekwa pamoja vinaweza kuonekana na vitu tofauti tofauti kabisa, lakini ni kitu kile kile kimoja, ambacho ni maji. Ndivyo alivyo Mungu wetu.
Kutembea katika ofisi ya ubaba, na wakati huo huo mwana, na wakati huo huo Roho Mtakatifu, sio shida kwake, amefanya hivyo ili sisi tukamilishwe. Kama mwanadamu asingeanguka hakukuwa na haja ya Mungu kujifunua katika ofisi zote, angebakia katika ubaba wake ule ule mmoja,
Ni sawa na mtu aliyebuni simu, kama kusingekuwa na changamoto ya umbali ya nini mtu kuzungumza kupitia kifaa hicho?. Vivyo hivyo Mungu kuuvaa mwili, ni ili kutuunganisha sisi na yeye, katika mahusiano ambayo tuliyapoteza pale Edeni. Baadaye akaingia kabisa ndani yetu, kwa Roho wake Mtakatifu, kiasi kwamba sasa tunamwabudu Mungu wetu moja kwa moja ndani ya mioyo yetu.
Kwahiyo, Mungu wetu hajagawanyika. Ni Yule Yule mmoja, wala hana nafsi tatu, bali moja. Wala hakuna mahali kwenye maandiko yanathibitisha kuwa Mungu anazo nafsi tatu. Lakini hilo si jambo la kuzozana nalo, kwa wanaoamini Mungu anazo nafsi tatu, maadamu hawaamini miungu mingi. Akimwabudu Baba, ni Yule Yule, akimwambudu Yesu ni yuleyule Mungu, akimwabudu Roho bado haabudu Mungu mwingine zaidi yake yuleyule mmoja. Hilo ni suala tu la kiufahamu ambalo halimwondolei mtu wokovu.
Hivyo ikiwa wewe ni mkristo, umemwamini Kristo kama ni mwokozi wako, na mwenzako pia kampokea kama wewe tu ulivyopokea, lakini haamini kama ni Mungu bali ni mwana wa Mungu. Lakutosha, usishindanie mambo ambayo ni ya ujuzi. Mwombee tu, Mungu ampe ufahamu kamilifu, kwasababu kujua kama utatu mtakatifu ni sahihi au sio sahihi hilo haliwezi kumtenga na Mungu wake, maadamu haubudu nje ya hao. Tukue kiufahamu, tusimpe adui nafasi ya kuleta mtengano yasiyo na maana.
Kwa maarifa ya ndani zaidi kuhusu, mafundisho ya uungu wa Mungu pitia haya masomo >>>
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je msikiti wa Al-Aqsa ni nini, na unahusikaje katika unabii wa biblia?
Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.
MSIKITI WA Al-Aqsa
Msikiti wa Al-Aqsa ni msikiti uliopo katika mji wa YERUSALEMU, ndani ya Nchi ya Israeli, Msikiti huu unaaminika kuwa ni sehemu ya tatu ya utakatifu kulingana na dini ya kiislamu, Sehemu ya kwanza ikiwa ni Makka (au Mecca), ya pili ni Al-masjid an Nabawi iliyopo Medina (nchini Saudi Arabia), na ya tatu ndio hii Al-Asqa.
Msikiti wa Al-Aqsa umejengwa pembezoni mwa jengo maarufu kama “Kuba ya Mwamba” (au Dome of Rock), tazama picha chini.
Msikiti huu wa Al-Aqsa unaaminika ulijengwa na mtu aliyeitwa Umayyad caliph Abd al-Malik kati ya Karne ya saba (7) na ya nane (8), baada ya KRISTO. Na kulingana na dini ya kiislamu, inaaminika kuwa Muhamad ndipo alipopaa mbinguni na kwenda kupewa ufunuo wa kitabu cha Quran (Sasa kujua kama ni kweli au si kweli soma Makala hii mpaka mwisho)..
Mbali na kwamba katika msikiti huu ndio panaaminika kuwa mahali Muhamad alipopaa lakini pia zamani paliaminika na waislamu wa kwanza kuwa ndio maahali pa kutazama wakati wa sala, maarufu kama “kibla”. Hebu tuielezee hii Kibla kidogo..
Kibla ni neno la kiaramu lenye maana ya “Uelekeo”, Waislamu wanaposali kulingana na Imani yao, wanapaswa waelekee upande Fulani, sasa zamani Kibla ilikuwa ni katika huu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu Israeli, lakini baadae walikuja kubadilisha kulingana na kuwa mahali pajulikanapo kama Makka (Mecca) huko Saudi Arabia, ambapo ndipo Muhamad alipozaliwa.
Hivyo sasa waslamu wote wanaposali wanaelekea kibla huko Makka Saudi Arabia na si tena Yerusalemu, na pia mtu anapozikwa anaelekezewa huko Makka, na vile vile mnyama anapochinjwa anaelekezewa huko huko Makka (kujua usahihi wa jambo hili na kama wakristo wanaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo endelea kufuatilia Makala hizi)..
Sasa swali ni je! Huu msikiti ambao sasahivi upo pale Yerusalemu, unaoaminika na watu Zaidi ya Bilioni 1.9, kuwa ndio sehemu ya Tatu kwa utakatifu, je msikiti huu utaendelewa kuwepo pale milele au utakuja kuondolewa?.
Jibu: Kujua kama utaondolewa au la! Turejee Biblia..
Maandiko yanasema lile Hekalu la Kwanza lililojengwa na Sulemani, lilitengenezwa juu ya Mlima Moria, ambapo ni eneo lile lile Abrahamu alipotaka kwenda kumtoa mwanae Isaka kama sadaka ya kuteketezwa, na sasa ndio eneo hili hili ambalo msikiti wa Al-Aqsa umejengwa.
Na ilikuwaje Hekalu kuondolewa na msikiti kujengwa?..
Sababu iliyofanya Msikiti huo kujengwa mahali pale pale Hekalu lilipokuwepo… ni kuvunjwa kwa hekalu hilo mara ya kwanza na ya pili…na wayahudi (yaani waisraeli), kuondolewa katika nchi yao na kutapanywa katika mataifa yote mwaka ule wa 70 Baada ya Kristo.
Wayahudi walipoondolewa katika nchi yao kutokana na makosa yao kwa Mungu, ndipo Ngome ya kiarabu ikateka na kujenga msikiti huo.
Adhabu ya Mungu kwa Israeli, haikuwa ya milele, kwani aliahidi atawarudia tena, na kuwarudisha katika nchi yao, na tena watalijenga Hekalu. (soma Ezekieli 40-48), na kufikia mwaka 1948, Israeli walirejea nchini kwao na mpaka sasa wapo pale.
Na hatua ya kwanza ya matengenezo ni wao kuirudia torati waliyopewa na Musa, hivyo watalijenga Hekalu kama lile la kwanza na baadaye, watamwagiwa Neema na macho yao kufumbuliwa Zaidi kwa kumwamini Masihi YESU, aliye hekalu halisi, sawasawa na Warumi 11 (kwani kwasasa wengi wao hawaamini hivyo).
Warumi 11:1 “Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.
2 Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu………………………
25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.
Sasa kabla ya huo wakati wa Israeli kufumbuliwa macho,na kumjua Kristo kama Hekalu halisi, watasimamisha kwanza Hekalu la damu na nyama, na mahali litakapojengwa ni palepale lilipojengwa hekalu la kwanza. Na hapo si pengine bali ni eneo lile lile Msikiti wa Al-aqsa ulipo.
Maswali yafuatayo yananyanyuka:
Je! Ni ni kitatokea?..na je huo msikiti utaondolewa kupisha ujenzi wa Hekalu, na kama utaondolewa je utaondolewaje?..na ni lini?.
Jibu ni kwamba Msikiti ule ni lazima utaondolewa pamoja na ile Kuba ya Mwamba (Dome of Rock)!!, kwasababu Neno la Mungu limeshasema hivyo kwamba Hekalu litajengwa…na Neno la Mungu halijawahi kupita (kilichotabiriwa katika Ezekieli 40-47 kitatimia kama kilivyo), hakuna shaka juu ya hilo, haijalishi ni muda gani utapita!!.. Wakati utakapofika wa unabii huo kutimia msikiti wa Al-Aqsa utaondoka.
Ni kwa njia gani utaondolewa?.. hakuna anayejua kama ni kwa njia ya Amani, au kwa njia nyingine, lakini dunia nzima itatii tu kwasababu ni Bwana ndiye aliyeyasema hayo, na kuyapanga si MTU, wala WATU wala Taifa la Israeli, bali ni MUNGU mwenyewe!!, hivyo hata wakati wa kuondolewa hakuna atakayejisifu kuwa ni nguvu zake, bali Mungu mwenyewe ndiye atakayehusika hapo.
Na dalili zote zinaonyesha kuwa tumekaribia sana hicho kipindi, kwani waisraeli wameshakusanya utajiri mkubwa na utaalamu mwingi, kiasi kwamba endapo ikitokea ukaanza leo, basi hakuna kizuizi chochote cha kifedha wala kiutalaamu.
Na ujenzi huo unauhusiano mkubwa sana na mpinga-Kristo ajaye, ambapo biblia inasema atatafuta kuingia katika hekalu hilo, ili atafute kuabudiwa yeye kama Mungu (2Wathesalonike 2:4), na maandalizi ya mpinga-kristo yapo ukingoni..nafasi yake ipo tayari, kinachongojewa ni parapanda.
HOJA NYINGINE ZISIZO SAHIHI.
Je ni kweli Muhamad alipaa, na je ni kweli Qurani ni kitabu cha Mwenyezi Mungu?
Jibu ni la! Hakupaa!!..Kwasababu Biblia inatuambia manabii waliopaa ni wawili tu, Henoko na Eliya.. na BWANA YESU ambaye ndiye Mkuu wa Uzima. Hao ndio waliopaa, na wengine watakaopaa ni watu watakaofufuliwa na kwenda mbinguni siku ya unyakuo, na watakatifu watakaokuwa hai siku ya kurudi kwa Bwana, pamoja na wale manabii wawili waliotajwa katika Ufunuo 11, basi!
Na pia Quran sio kitabu cha mwenyezi Mungu chenye kumfikisha mtu mbinguni. Kinaweza kuwa kitabu chenye baadhi ya maonyo yaliyo sahihi ambayo mtu akiyafuata anaweza kuwa mzuri katika jamii, lakini si kuurithi uzima wa milele…Kwa ujumla kitabu hiko hakina mafundisho ya Uzima wa milele, kwasababu kinamkataa YESU kama NJIA PEKEE ya WOKOVU wa mwadamu.
Na kitabu chochote kisichoelekeza moja kwa moja Uzima wa milele uliopo ndani ya YESU, au mtu yeyote yule asiyeamini kuwa YESU ndiye BWANA, na Mwokozi, na ndiye njia pekee ya UZIMA, huyo mtu hana uzima wa milele haijalishi atakuwa anafanya mambo mengine yanayoonekana mazuri machoni pa watu, lakini kama hatamwamini Bwana YESU baada ya kumsikia, matendo yake hayo hayatamsaidia chochote, kwasababu hakuna mwanadamu atakayeweza kusimama kwa matendo yake peke yake.
Yohana 3:18 “ Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.
Usikose mwendelezo kuhusiana na Kibla ya wanyama na “Kaaba”, na kama wakristo tunaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo.. Pia usikose kufuatilia Makala hizi pamoja na nyingine nyingi, juu ya ukweli kuhusiana na Uislamu na Imani nyingine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?
Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?
1Wakorintho 7:28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
Awali ya yote katika vifungu hivi, Mungu hashinikizi kwamba watu wasioe au wasiolewe. Ndoa ni jambo jema, na lina faida nyingi sana katika maisha na pia katika huduma, kwasababu humsaidia mtu akae mbali na uzinzi na tamaa mbaya, (1Wakorintho 7:2). Pia huondoa upweke (Mwanzo 2:18), wawili wawapo mwili mmoja, ni nguvu zaidi na faraja.
Lakini Mungu anatoa pia uchaguzi, kwa mtu ikiwa anao uwezo wa kujizuia yaani kutawala hisia zake (1Wakorintho 7:9), akaishi hivyo hivyo, bila shida yoyote, ni vema zaidi kihuduma. Kwasababu humfanya asisongwe na mambo mengi ya kindoa.
Kwasababu mtu aliye kwenye ndoa ni wazi kuwa upendo wake utagawanyika kwa sehemu, biblia inasema atatafuta ampendezeje mume/mke wake.
1Wakorintho 7:32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.
Lakini pia atakutana na dhiki, zinazoambatana na ndoa. Kwamfano kutatua migogoro ya kifamilia, malezi ya watoto, kuwagharamikia, kuwasomesha,matibabu, kuwafuatilia, kuivisha familia yako, na mambo kama hayo. Ni dhiki ambazo, zinaongezeka, na hivyo hutinga ufanisi wako kwenye utendaji kazi wa injili. Paulo huiita “shida iliyo” sasa. Yaani Kusalitiana, upendo kupoa, kupishana, ni vitu ambavyo mara kwa mara hujitokeza katika maisha ya ndoa.
1Wakorintho 7:26 Basi, naona hili kuwa jema, kwa ajili ya shida iliyopo, kwamba ni vema mtu akae kama alivyo.
27 Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke
Hivyo kihuduma mtu ambaye hajaoa/kuolewa, hujipunguzia dhiki, kuliko yule aliye kwenye ndoa. Hiyo haimaanishi kuwa aliye kwenye ndoa hawezi kutenda kazi vizuri, hapana kazi anaweza itenda hata zaidi ya Yule ambaye hajaoa, isipokuwa tu kwake dhiki na shida zitaongezeka.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA
NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
Swali: Katika Yohana 5:22 na 27 tunaona biblia inasema kuwa Mungu amempa Mwana (Yaani Bwana Yesu) hukumu yote…. lakini tukiruka mpaka ile sura ya 12:47 tunaona tena Bwana YESU anakanusha kuwa yeye hamhukumu mtu?.. Je biblia inajichanganya hapa?.
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa Biblia ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu, hivyo kamwe hakina makosa…kinachoonekana kinajichanganya si Biblia, iliyo Neno la Mungu, bali ni tafakari zetu na pambanuzi zetu.
Sasa turejee mistari hiyo..
Katika Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, BALI AMEMPA MWANA HUKUMU YOTE………….
27 Naye AKAMPA AMRI YA KUFANYA HUKUMU kwa sababu ni Mwana wa Adamu”.
Hapa ni kweli Mwana kapewa mamlaka yote ya kufanya hukumu… Tusome tena ile Yohana 12:47..
Yohana 12:47 “Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, MIMI SIMHUKUMU; MAANA SIKUJA ILI NIUHUKUMU ULIMWENGU, ila niuokoe ulimwengu”.
Tukisoma mistari hiyo kwa juu juu, ni rahisi kuona kuwa maneno hayo yanajichanganya… lakini kiuhalisia hayajichanganyi hata kidogo.. kwani ni suala la kuelewa lugha tu hapo!.
Katika Yohana 5:22, Baba amempa Mwana hukumu yote, maana yake Amri ya kuhukumu amempa yeye.. Maana yake mamlaka yote kapewa (Bwana YESU), kama vile Farao alivyompa Yusufu mamlaka yote ya Misri.
Sasa kama Bwana YESU kapewa mamlaka yote ya kufanya hukumu… ni chaguzi lake yeye ni nani amhukumu na nani asimhukumu, ni wakati gani afanye hukumu na ni wakati gani asihukumu…(kwasababu vyote vipo mikononi mwake).
Sasa kwasababu yote yamewekwa chini ya mapenzi yake, basi mapenzi yake ni “kumtomhukumu mtu yoyote duniani”…sawasawa na maandiko hayo ya Yohana 12:47.. ingawa anayo mamlaka hayo ya kumhukumu mtu yoyote duniani kwasababu kashapewa na Baba.
Lakini hakutumia huo uwezo, wa kupitisha hukumu duniani kwa wote waliomkataa au wanaomkataa sasa, bali anawavumilia mpaka siku ya mwisho.. Mfano mzuri unaomwonyesha Bwana akiwa ameizuia hukumu yake ni ile habari tunayoisoma katika Luka 9:52-56.
Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu. 54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Huo ni mfano wa hukumu ambayo Bwana angeweza kuito kwa Wasamaria hao, lakini alizuia… utasoma tena jambo kama hilo hilo katika Mathayo 26:51-53.
Mathayo 26:51 “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.
53 AMA WADHANI YA KUWA MIMI SIWEZI KUMSIHI BABA YANGU, NAYE ATANILETEA SASA HIVI ZAIDI YA MAJESHI KUMI NA MAWILI YA MALAIKA?”
Kwahiyo ni kweli Bwana YESU amepewa hukumu yote, lakini hatumii uwezo wa hukumu yake yote, kwetu sisi tunaoishi sasa, laiti akifanya hivyo, hakuna mwenye mwili atakayepona.. Lakini anatuvumilia sana kwasababu hataki mtu yoyote apotee (2Petro 3:9).
Ila tukiudharau wingi wa huruma zake hizi, na kupuuzia Neema mpaka siku tunaondoka katika haya maisha au siku amerudi, basi tutahukumiwa na yeye pasipo huruma… Na atatuhukumu kupitia maneno yake hayo hayo.
Hivyo ndugu yangu, YESU sasa ni mwenye huruma na mvumilivu kwetu, lakini siku ile ya hukumu hatakuwa na huruma..kwahiyo si muda wa kudharau wema wake na uvumilivu wake kwetu, bali ni wakati wa kutengeneza maisha kabla ya ile siku ya hukumu..
Warumi 2:4 “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu,
6 atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
IKIWA MWENYE HAKI AKIOKOKA KWA SHIDA, MWENYE DHAMBI ATAONEKANA WAPI?
Tirano alikuwa nani na darasa lake lilikuwaje? (Matendo 19:9)
Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?
Swali: Katika Ayubu 14:12 tunasoma kuwa wafu hawafufuliwi, lakini katika 1Wakorintho 15:51 tunaona tena biblia inasema wafu watafufuliwa, sasa tuchukue ipi tuache ipi?.. au je biblia inajichanganya yenyewe?
Jibu: Biblia kamwe haijichanganyi, wala haijawahi kujichanganya, isipokuwa tafakari zetu ndizo zinachojichanganya au kuchanganyikiwa.
Turejee mistari hiyo na kisha tuone majibu yake kupitia biblia hiyo hiyo..
Ayubu 14:10 “Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia; Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi?
11 Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika;
12 Ni vivyo MWANADAMU HULALA CHINI, ASIINUKE; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa usingizini.”
Ni kweli hapa maandiko yanasema kuwa MWANADAMU HULALA CHINI, ASIINUKE TENA… lakini hebu turejee agano jipya katika kitabu kile cha Wakorintho tuangalie biblia inatuambiaje..
1Wakoritho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana PARAPANDA ITALIA, NA WAFU WATAFUFULIWA, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.
Na hapa maandiko yanatuambia, parapanda italia na wafu waliolala katika Kristo watafufuliwa. Sasa swali tuchukue lipi tuache lipi?, maneno kama hayo hayo yanarudiwa tena katika 1Wathesalonike 4:16.
Jibu ni Dhahiri kuwa “Wafu watafufuliwa siku ya mwisho”.. sawasawa na Yohana 5:25.
Kwanini maandiko hayo ya 1Wakoritho 15:51 yana nguvu kuliko yale ya Ayubu 14:12, yanayosema kuwa “wafu hawafufuliwi”?… Ni kwasababu Agano jipya ni ukamilifu wa agano la kale.
Manabii waliotangulia walifahamu mambo kwa sehemu, lakini Roho Mtakatifu katika agano jipya, amekamilisha yote na kufunua yote… Na kawaida ni kwamba unapokuja ule ufunuo mkamilifu, bali ule uliokuwa unajilikana kwa sehemu unabatilika ndivyo maandiko yasemavyo..
1Wakorintho 13:9 “Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika”.
Manabii wengi wa agano la kale hawakujua mengi kuhusiana na ufufuo, au mbingu mpya na nchi mpya, ingawa walikuwa wanafahamu siku moja watajua mambo yote..hivyo walitoa unabii kwa sehemu waliyopimiwa…lakini mwisho wa nyakati Roho Mtakatifu anakamilisha ufunuo wote sawasawa na hiyo 1Wakorintho 13:9-10.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Wafu watafufuliwa siku ya mwisho, na watahukumiwa.
Yohana 5:28 “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 NAO WATATOKA; WALE WALIOFANYA MEMA KWA UFUFUO WA UZIMA, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Na kumbuka hoja hii ya kufufuliwa kwa wafu ndiyo iliyoleta mgawanyiko mkubwa katikatika ya wayahudi hata kuzaliwa makundi (madhehebu) mawili ambayo ni MAFARISAYO NA MASADUKAYO, ambapo Mafarisayo waliamini ufufuo na masadukayo hawakuamini ufufuo kwa kutumia andiko hilo la Ayubu 14:12 pamoja na maandiko mengine machache..
Lakini Bwana YESU alikuja kuondoa huo utata kama tunavyosoma katika Mathayo 22:23-32..
Mathayo 22:23 “Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,
24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
29 Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.
30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.
31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema
32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai”
Kwahiyo wafu watafufuliwa, lakini swala la msingi ni je!.. sisi tutakuwepo upande upi wakati huo wa ufufuo?.. Je tutafufuliwa ili tukavikwe taji na kuurithi uzima wa milele, au kwaajili ya hukumu ya ziwa la Moto?
Kumbuka wote walio nje ya Kristo, ambao hawajampokea Bwana YESU na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake, wametabiriwa kuwa miongoni mwa watakaohukumiwa katika hukumu ya milele. Je umeokoka?..umebatizwa katika ubatizo sahihi?.. umejazwa Roho Mtakatifu?.
Kama bado unangoja nini?… Ni heri ukafanya maamuzi leo ya kubadili maisha yako.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
UTALIPWA KATIKA UFUFUO WA WENYE HAKI.
Hilo ndio jambo la kwanza. Kamwe huwezi kumshinda shetani ikiwa upo nje ya Kristo, Ndicho kilichowakuta wale wana wa Skewa, walipotaka kutoa pepo kwa jina la Yesu. Lakini Yule pepo akawaambia Yesu namjua, na Paulo namfahamu, lakini je ninyi ni akina nani?
Matendo 19:13 Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.
14 Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.
15 Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16 Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.
Wokovu, ni Kristo ndani yako, na kwa huo nguvu za adui zote huyeyuka mara moja. Mtu aliyempokea Yesu, shetani kamwe hamwezi, kwasababu anamwona Kristo ndani yake.
Unaweza ukawa umeokoka, lakini shetani akapata nguvu za kukusumbua kwa majaribu, kwasababu unashindwa kutumiza baadhi ya wajibu wako kwa mwamini, Yesu alisema..
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Yesu ijapokuwa alikuwa ni mkamilifu hana dhambi, alijaribiwa na adui, wewe ni nani usikutane na hayo? Usipokuwa mwombaji, uvivu ukakumeza, unaona shida kuomba kila siku, kuhudhuria mikesha ujue tayari upo majaribuni. Hata kama utajiona upo sawa, fahamu tu hapo ulipo kuna eneo Fulani adui anakusumbua, utakuja kugundua pindi utakapoanza kuwa mwombaji. Na ndio maana maisha ya wokovu hayatengwi na maombi. Shetani akimwangalia mwombaji anaona moto umemzunguka mkali, hawezi jiamulia tu kufanya analotaka kwake.
Warumi 16:19 Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20 Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Hapo anasema tuwe wajinga katika mambo mabaya. Ni nafasi kubwa kwa Mungu kumweka shetani chini ya miguu yetu. Kwamfano, unapokuwa hujui kuhusu mitindo mipya ya kidunia, sio mfuatiliaji wa miziki ya kidunia, muvi mpya mpya zilizotoka duniani, yaani kwa ufupi unapitwa na mambo ya kidunia yasiyokuwa na maana kwako, kinyume chake, unakuwa na ujuzi na hekima katika mambo ya rohoni jua hapo umemshinda shetani kwa sehemu kubwa. Hana kitu kwako, kwasababu bidhaa zake, huna mpango nazo, hununui chochote kwake. Kuipenda dunia ni kuwa adui wa Mungu, na rafiki wa shetani.
Kuweka Neno sio, kukariri vifungu vingi vya biblia, hapana, bali ni kufahamu “ukweli” (ufunuo) wa kila Neno unaloliweka moyoni mwako. Pale jangwani, Yesu alipokutana na shetani, alimjaribu kwa Neno hilo hilo,lakini Yesu akamwambia kweli yote ipoje.
Mathayo 4:6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Ni muhimu ukalifahamu Neno la Mungu katika kweli yake, na hiyo huchangiwa na kufundishwa kwa ufasaha Neno la Mungu na waalimu, kwasababu Roho Mtakatifu atasema na wewe kupitia wao. Lakini pia kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya moja kwa moja kukufundisha. Vinginevyo adui atakudanganya sana, hususani kupitia manabii wa uongo, kwasababu hulijui Neno vema.
Kulifahamu Neno, na kuijua kweli, ni jambo muhimu lakini bado shetani anaweza pata mianya ya kukunasa endapo hutaweza kulitii Neno. Penda utakatifu, penda kutendea kazi kile unachofundishwa. Yesu alisema, wapo watu wasikiao tu, lakini wapo wasikiao na kuyatendea kazi. Wote hujaribiwa kwa pepo, mafuriko na mvua za shetani. Sasa Yule aliyejijenga juu ya fundisho tu, na sio kutendea kazi fundisho, ndio huyo anayechukuliwa na mafuriko.
Mathayo 7:26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Mateso mengine huwapata watu kwasababu ya dhambi. Kuishi maisha matakatifu, humnyima adui mlango wa kukushambulia kwa namna yoyote. Liishi Neno.
Watu wengi hudharau ushuhudiaji. Tunapokuwa na moyo mmoja wa kuitenda kazi ya Mungu, adui hawezi kukaa juu ya anga hili, kutupinga. Tunalisoma wapi hilo? Utakumbuka wakati ule Bwana alipowatuma wanafunzi wake wawili wawili kuhubiri, waliporudi kwa furaha, huku wakimwambia Bwana hata mapepo yanawatii. Yesu akawaambia nalimwona shetani akianguka kutoka juu kama umeme. Kuonyesha kuwa kitendo cha wao kuhubiri adui alikuwa anaporomoka kwa kasi sana.
Mathayo 10:17 Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
Hivyo ukizingatia mambo hayo sita (6), Utakuwa sio tu umemdhibiti adui kila Nyanja, bali pia umemteka. Ni wajibu wako mimi na wewe kuboresha mahali ambapo hapako sawa, ili kwa pamoja tukaujenge ufalme wa Mungu na kuziangusha kazi za shetani.
Yakobo 4:7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: