Category Archive Home

Liwali ni nani?

Liwali ni mkuu wa mji au jimbo Fulani. (Gavana).

Kwamfano katika biblia tunaona, Pontio Pilato anatajwa kama Liwali wa Uyahudi sehemu ya kusini mwa Israeli,. Hivyo eneo lote la uyahudi yeye ndiye alikuwa kama mkuu wa majimbo hayo.

Mwingine ni Yusufu, biblia inasema, Farao alimweka kama Liwali wa nchi yote ya Misri.

Mwanzo 42:6 “Naye Yusufu alikuwa ni liwali juu ya nchi, ndiye aliyewauzia watu wote wa nchi. Nao ndugu zake Yusufu wakaja, wakainama kifudifudi mbele yake”.

Hivyo kazi yao haswaa ilikuwa ni sawa na ya wakuu wa mikoa wa sasa, au majimbo, ambapo kimsingi wanakuwa na mamlaka ya kuongoza shughuli zote za jimbo hilo kwa amri yao, wala hakuna chochote kinachoweza kufanyika bila idhini yao.

Hivi ni baadhi ya vifungu vya Zaida ambavyo utaweza kukutana na hilo neno;

Mathayo 27:1 “Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;

2 wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.

Mathayo 28:14 “Na neno hili likisikilikana kwa liwali, sisi tutasema naye, nanyi tutawaondolea wasiwasi.

15 Basi wakazitwaa zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Na neno hilo likaenea kati ya Wayahudi hata leo”.

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;

7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”.

Matendo 18:12, 23:24, 26:30

Ni nini twaweza zingatia  kuhusu hawa maliwali?

Bwana Yesu alisema, katika utumishi wetu, utafika wakati, tutaitishwa mbele ya mabaraza ya wafalme, na maliwali, kushitakiwa.Hivyo tukijikuta  katika mazingira kama hayo hatupaswi kuogopa, kwasababu Kristo ameahidi kuwa atakuwa na sisi katika mapito yetu yote.

Mathayo 10:18 “nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Bwana akubariki.

Je! Umeshamkabidhi Kristo Maisha yako?. Kama jibu ni hapana, na upo tayari kuokoka leo. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Au tutafute kwa namba zetu hapo chini, kwa msaada huo.

+255693036618/+255789001312

Mada Nyinginezo:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Je mwanamke Fibi, alikuwa ni askofu wa makanisa, kama mitume?

Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?

Mharabu ni nani katika biblia?

Bawabu ni nani/nini?

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Rudi Nyumbani

Print this post

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

Akida ni mkuu wa majeshi ya zamani, hususani majeshi ya kirumi. Akida mmoja alikuwa anaongoza kikosi cha askari 100,. Maakida wengi walikuwa wanachaguliwa na watalawa wao wakuu moja kwa moja toka Rumi,wengine katika mabaraza, wengine kutoka kwa maliwali, na wengine moja kwa moja kwa kupandishwa vyeo, baada ya kutumika kwa muda mrefu (miaka 15-20), katika shughuli za kijeshi.

Kazi yao kubwa ilikuwa ni kusimama mstari wa mbele katika vita kuliongoza kundi lote jeshini, pia kutekeleza mauaji ya wahalifu, au washitakiwa, mfano wa hawa ni Yule akida aliye simamia mateso na mauji ya Bwana Yesu pale Kalvari

Marko 15:39 “Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu”.

Pia walikuwa wanafanya kazi ya kutoa mafunzo ya kijeshi, kugawa majukumu, kusimamia ujenzi wa ngome na kuta za ulinzi za taifa. Walifanya pia kazi ya kuwalinda wafungwa na kuwahakikishia ulinzi wao pindi wasafirishwapo, Mfano wa Hawa, soma .(Matendo 23:23, 24:23, )

Pamoja na hilo, maakida wengine walikuwa ni watu wakatili, na wapenda rushwa,

Lakini ni jambo  gani Mungu anataka tujifunze nyuma ya watu hawa?

Ijapokuwa kazi hii, si kazi iliyoonekana kumrudishia Mungu utukufu, Lakini bado tunaona wapo maakida, kadha wa kadha katika biblia, waliompendeza Mungu katika utumishi wao, zaidi hata ya wayahudi wengi, waliokuwa wanajiona washika sheria na torati.

Kwamfano utaona Bwana Yesu alipokuwa katika ziara zake za kuhubiri na kufungua watu, alikutana na akida mmoja, ambaye aliustaajibisha sana moyo wake kwa imani aliyokuwa nayo, mpaka Bwana akasema hata katika Israeli,hakuna aliyekuwa na imani kubwa kama yake.

Mathayo 8:5 “Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,

6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.

7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.

8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona.

10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli.

11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;”

Utaona pia, kulikuwa na akida mwingine, aliyeitwa Kornelio, huyo alikuwa anatoa sadaka nyingi sana, na kuwasaidia watu, mpaka siku moja malaika wa Bwana anamtokea na kumpa maagizo ya kufanya ili aupokee wokovu kamili.

Matendo 10:1 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima”.

Umeona? Ni nini Mungu anataka tujue?

Ni kwamba Mungu hatazami sana mahali unapotumika, lakini anatazama uaminifu wako, moyo wako, utakatifu wako, bidii yako kwake. Unaweza ukawa unafanya kazi serikalini, lakini ukamtumikia Mungu vema, kwa kukataa rushwa, na kutenda haki, na Mungu akapendezwa nawe..Mfano wa Danieli, Maadamu, upo mahali ambapo hapakinzani na sheria ya Mungu na taifa, usijisikie vibaya kutumika unachopaswa kufanya ni kumtumikia tu Mungu kwa uaminifu wote, kuangaza nuru yako ya wokovu kwa wale watu, na kumpenda yeye na kukataa njia zote mbaya zinazokinzana na Neno lake.

Kwa kufanya hivyo Basi Mungu atakutumia kutimiza kusudi lake, alilolikusudia juu yako, na watu wake, mfano wa Kornelio na Yule akida ambayo alidhubutu hata kuwajengea wayahudi sinagogi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ORODHA YA WAFALME WA ISRAELI.

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?

Neno “Mashehe” tunaliona likitajwa katika biblia(Agano la kale); Hawa mashehe ni wakina nani?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Rudi nyumbani

Print this post

Sifa ni nini?

Sifa ni kitendo cha kumshuhudia Mungu, au kuyasimulia matendo makuu ambayo ameyafanya au aliyonayo, na huwa inaambata na mguso wa ndani unaomfanya mtu arukeruke, acheze, afurahie, aimbe, ashangalie, apige kilele kwa nguvu, kwa hayo aliyoyaona kwa Mungu wake.

Kwamfano tunapoona jinsi, mbingu na nchi, jua na mwezi, na milima na bahari, vilivyoumbwa kwa uweza na ukuu wa ajabu, hapo tunapata sababu ya kumshuhudia Mungu, au kumtangaza kwa namna zote aidha kwa kumwimbia, kushangalia kwa sauti ya juu,

Au labda ulikuwa na shida Fulani labda ugonjwa, ukaponywa, au hitaji la kazi, nyumba, chakula ukapatiwa na yeye. Hapo ndipo unapopata sababu ya kuyatangaza maajabu yake, kwa kumwimbia kwa nguvu sana. Hizo ndio sifa.

Mungu anasema..

Zaburi 68:32 “Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo”.

Zaburi 117:1 “Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote, mhimidin.

Zaburi 147:1 “Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri”.

Biblia inatuambia viumbe vyote na uumbaji wote, vinamsifu Mungu. Kwanini na sisi tusimwimbie yeye sifa zetu?.  Embu tazama pumzi uliyopewa bure, embu tazama mapigo ya moyo yanayodundishwa ndani yako bila tozo lolote, embu tafakari jua unaloangaziwa na Yehova. Kwanini usimsifu yeye?

Bwana anaketi juu ya sifa.. (Zaburi 22:3), Na yeye pekee ndiye anayestahili kuabudiwa.

Hivyo wote wamsifuo kwa Roho na Kweli, yeye yupo juu yao. Katika sifa kuta za Yeriko zilianguka, , \vifungo vya Gereza vililegezwa Paulo na Sila walipokuwa gerezani, katika sifa maadui waliuliwa bila vita yoyote kipindi cha Mfalme Yehoshafati.  Nasi pia tukiwa watu wa sifa, ni maombi tosha ya kutuweka huru na kutufungua.

Bwana atupe macho ya kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

BARAGUMU NI NINI?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Kuhimidi kibiblia ni kumpa Mungu sifa iliyochanganyikana na heshima na unyenyekevu wa hali ya juu sana,

Neno hili limeonekana  mara nyingi sana katika biblia,

Kwamfano hivi ni baadhi ya vifungu, ambavyo utakutana na Neno hilo;

Mwanzo 14:19 “Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi. 20 Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote”.

Waamuzi 5:3 “Sikieni, enyi wafalme; tegeni masikio, enyi wakuu; Mimi, naam mimi, nitamwimbia Bwana; Nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli”.

Zaburi 31:21 “Bwana ahimidiwe; kwa maana amenitendea Fadhili za ajabu katika mji wenye boma”.

Zaburi 34: 1 “Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima”.

Warumi 15:10 “Na tena anena, Furahini,Mataifa,pamoja na watu wake.

11 Na tena, Enyi Mataifa yote,msifuni Bwana; Enyi watu wote,mhimidini.

Ikiwa wewe ni mwanadamu mwenye pumzi huna budi kumuhimidi Mungu muumba wako sikuzote za  maisha yako. Ni lazima ujishushe, upige magoti, na kwa kumaanisha kabisa, umsifu kwa nguvu zako zote, umtukuze kwa wema wake wako, na kuliadhimisha jina lake.

Moja ya mambo ambayo yalimfanya Daudi awe kipenzi cha Mungu, ni tabia yake, ya kumuhimidi Mungu, tena mbele ya makusanyiko ya watu.

Zaburi 26:12 “Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana”.

Bwana atusaidie sote, tuwe na matamanio kama haya.  Kwasababu kama ilivyo chakula chetu sisi ni Neno la Mungu, halikadhalika chakula cha Mungu wetu ni Sifa. Hatuna budi kumlisha kila siku sifa zake, kwa kumuhimidi yeye.

Bwana akubariki.

Je umeokoka? Kama la unafahamu kuwa tunaishi katika vizazi ambacho unyakuo ni wakati wowote?. Tubu dhambi zako mgeukie Mungu, naye atakusaidia. Ikiwa utahitaji msaada ya kumkaribisha Kristo maishani mwako/ kubatizwa, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Rudi nyumbani

Print this post

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Mwana-haramu, au mwana wa haramu ni mtu aliyezaliwa nje ya Ndoa Takatifu.

Zamani katika jamii ya Israeli, Mungu aliwakataza wana wa Israeli, wasioane na watu wa mataifa. (Kumbukumbu 7:2-3). Wala wasioane ndugu kwa ndugu..

Walawi 18:5 “Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.

6 Mtu ye yote aliye wa kwenu ASIMKARIBIE MWENZIWE ALIYE WA JAMAA YAKE YA KARIBU ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana”.

Vile vile Bwana aliwakataza watu wasiingie kwa wake wa Jirani zao (Kumbukumbu 5:21, Kutoka 20:17).

Kwahiyo mtoto yeyote aliyepatikana kwa mojawapo ya hizo njia tatu, yaani kwa njia ya kukutana ndugu kwa ndugu, au kuoana mtu wa Israeli na mtu wa mataifa, au kwa kuzaa na mke wa Jirani yako au ambaye hamjaoana, mfano wa Yuda katika Mwanzo 38:24. Mtoto huyo aliyezaliwa aliitwa MWANA-HARAMU, Au MWANA WA HARAMU.

Na Mwana haramu, enzi za agano la kale hakuruhusiwa kuingia katika MKUTANO WA BWANA MILELE, na hata kizazi chake chote..

Kumbukumbu 23:2 “Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana”.

Lakini swali ni je! Mpaka sasa, wana wa Haramu,(yaani waliozaliwa nje ya ndoa, kimwili) hawakubaliwi na Bwana?

Jibu ni la!, katika Agano la kale, si tu wana haramu waliokuwa wanatengwa, bali hata walemavu na watu wenye ukoma, hawakuruhusiwa kuingia katika mkutaniko wa Bwana. Na Bwana aliruhusu vile, ili kufundisha Uana haramu wa kiroho jinsi ulivyo mbaya, ambao utakuja kufunuliwa mbeleni(katika Agano jipya). Ambao huo utatufanya sisi tusikubalike mbele za Mungu, milele!!.

Mwana wa Haramu kibiblia ni mtu ambaye Hajazaliwa mara ya Pili.

Je umewahi kujiuliza ni kwanini “Wokovu” unafananishwa na “kuzaliwa mara ya pili”.. jiulize kwanini biblia haijatumia neno “kutengenezwa upya” lakini imetumia neno “kuzaliwa mara ya pili”.. Tafsiri yake ni kwamba “hali tuliyopo” sasa ni “u-haramu”… hivyo tunapozaliwa upya, ili ule uharamu unaondoka, na kuwa wana HALALI!!.. Na hivyo tunakuwa na uwezo wa kushiriki baraka zote za Mungu kwasababu tumefanyika kuwa Watoto wa Mungu halali.

Wana wa Haramu, (ambao hawajazaliwa mara ya pili), wanafananishwa na mbegu zinazoharibika.. maana yake!, hazina uzima wa milele, lakini wana halali (yaani wale waliozaliwa mara ya pili), wanafananishwa na mbegu zidumuzo.

1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

Na tabia ya mtoto halali, (asiye haramu), huwa baba yake anamfunza, ikiwemo pia kumwadhibu pale anapokosea..

Mtume Paulo aliliandika hilo kwa uweza wa roho na kusema…

Waebrania 12.5 “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye;

6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

7 Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo MMEKUWA WANA WA HARAMU NINYI, WALA SI WANA WA HALALI.

9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?

10 Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.

Je umezaliwa mara ya pili?

Maana ya kuzaliwa mara ya pili, ni Kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Kwa jina la Yesu) na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu. (Matendo 2:38).

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA MARA YA PILI, HAWEZI KUUONA UFALME WA MUNGU.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Jibu: Tusome,

Luka 12:24 “Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana GHALA wala UCHAGA, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!”

“Ghala” ni chumba/nyumba ndogo ya kuhifadhia nafaka, lakini “Uchaga” ni jengo kubwa lililotengenezwa kwaajili ya kuhifadhia nafaka pamoja na aina nyingine ya vyakula vya mifugo na binadamu.

Hivyo Bwana Yesu aliposema, tuwatafakari kunguru, kwamba hawana “Ghala” wala “Uchaga”, alimaanisha kunguru hawana mahali pa kuhifadhia chakula kwaajili ya vipindi vigumu vinavyokuja mbeleni, Lakini muujiza ni kwamba ijapokuwa hawana sehemu za kuweka akiba ya chakula, unapokuja msimu wa kiangazi bado hawafi kwa njaa, wanaishi!!

Utakumbuka kisa cha Nabii Eliya, kipindi ambacho mbingu zimefungwa miaka mitatu na Nusu, kipindi ambacho watu na Wanyama wanakufa kwa kukosa chakula, utaona kunguru bado walikuwa wanaishi na wanakula vizuri, na hata Mungu kuwatumia hao kumpelekea chakula mtumishi wake.

1Wafalme 17:2 “Neno la Bwana likamjia, kusema,

3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.

4 Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; NAMI NIMEWAAMURU KUNGURU WAKULISHE HUKO.

5 Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani.

6 KUNGURU WAKAMLETEA MKATE NA NYAMA ASUBUHI, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito”.

Umeona?.. wakati watu wanakufa kwa njaa, Kunguru na Watoto wao wanakula mpaka wanasaza, mpaka wanakuwa na akiba ya kumpelekea Eliya, mtumishi wa Mungu.

Lakini sasa Bwana Yesu anakuja kusema katika Luka 12:24, kwamba TUWATAFAKARI HAO!!.. Kama Baba wa mbinguni anawapa chakula hao, na ijapokuwa hawana maghala wa uchaga, si Zaidi sisi endapo tukimwamini na kumtegemea yeye?.. Kwasababu sisi ni bora kuliko kunguru mara nyingi.

Baba yetu anatuhurumia sisi mara nyingi Zaidi, kuliko anavyowahurumia kunguru!. Tunapomtegemea yeye, hata kama tutapitia hali ngumu na za ukame kiasi gani, basi Bwana Yesu hatatuacha tupungukiwe kabisa…atakuwa na sisi na kutuhudumia kuliko anavyowahudumia kunguru.

Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”

Je umempokea Yesu leo?, je umefanyika mtoto wake?, kama bado kumbuka dunia si salama, wala haina mshahara wowote Zaidi ya mauti, dunia itakususha thamani Zaidi ya kunguru siku ya mateso, kipindi cha Eliya wote waliokuwa wanaitumainia dunia, walikufa kwa njaa, lakini kunguru wakawa wanaishi…wote waliokuwa wanaabudu mabaali waliangamia, lakini kunguru waliishi!..Lakini waliomtegemea Mungu waliishi na kudumu,

Mpokee Yesu leo kama bado hujampokea, pia ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Ukienda kuomba kazi yoyote halali, kikawaida huwezi kupewa majibu ya papo kwa papo na kuambiwa anza kazi leo, bila ya kutaka kwanza taarifa Fulani kutoka kwako, hata kama ni ile ndogo ya kufagia, vipo vigezo  vitaambatanishwa tu na kazi hiyo, aidha utaulizwa umri wako, au hali yako ya kiafya, au fani uliyonayo, au jinsia yako, au elimu yako n.k. Lakini ikiwa hujasoma vigezo vyao, halafu ukapeleka maombi yako kienyeji, Ni wazi kuwa barua yako itatupwa kapuni.

Vivyo hivyo na kwa Mungu, tunapopeleka maombi yetu, ni sharti tujue vigezo vya kujibiwa, vinginevyo, tutabakia kumlaumu Mungu, mbona tulifunga, na kukesha lakini hujasikia maombi yetu.

Hivi ndio vigezo vikuu vya maombi yetu kujibiwa na Mungu

  1. Kaa mbali na dhambi:

Hili ndio jambo la kwanza na la msingi; Dhambi ndiyo inayomdhoofisha Mungu, na kumdumaza kwenye eneo la kujibiwa maombi yetu.

Isaya 59:1 “”Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.

Hakikisha unakaa mbali na mambo yote yanayomchukiza Mungu, yaliyo ndani yako, mfano uzinzi, ulevi, uongo, rushwa, wivu, matusi n.k.

  1. Omba vizuri:

Kuomba vizuri, sio kupangalia maneno katika uombaji, hapana, bali kuomba jambo linalotimiza mapenzi ya Mungu.

Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Jiulize unachokiomba je kina  lengo gani, ni ili umkomoe yule adui yako?, au ili ukaongezee mtaji wa ile biashara yako ya bar?, au ili uonekane mwanamke wa kisasa mfano wa Yezebeli? Kama sivyo  ni Ili nini?..Fahamu kuwa Mungu anachunguza mioyo. Hakikisha unachokiomba ni kwa utukufu wa Mungu. Vinginevyo hutapokea chochote.

    3. Usiombe ili utazamwe na watu unajua kuomba:

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:5 “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mawazo yako yanapaswa yamwelekee Mungu, na sio Mungu Pamoja na wanadamu. Ukilijua hilo, basi hutaona sababu ya kujionyesha kwa watu ili wakupe utukufu.

     4. Omba kwa bidii:

Ukweli ni kwamba yapo maombi utahitaji kuonyesha bidii kwa Mungu ili uyapate, na sio kuomba dakika 5 halafu basi, hapo unaweza usipokee chochote, bali yakupasa kung’ang’ana mbele za Mungu ndipo yaje kutokea.

Yakobo 5:16 “… Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.

Hivyo ongeza misuli yako ya maombi. Hata ya masafa marefu na mikesha.

    5.  Usikate tamaa:

Yakupasa ujifunze uvumilivu. Uvumilivu ni muhimu sana ikiwa hujajibiwa leo, haimaanishi kuwa Mungu hajakusikia, bali omba tena kesho, na kesho kutwa, kwasababu ipo sababu kwanini hujakipata kwa muda huo.

Luka 18 : 1-8

18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?

    6. Jifunze kumtolea Mungu:

Ni jambo dogo, lakini linamatokeo makubwa sana rohoni. Sio kwamba Mungu anahaja na fedha zetu hapana, lakini umtoleapo unaonyesha upendo wako kwake. Ukipeleka maombi yako kwake, jijengee utaratibu pia wa kuambatanisha na sadaka, kwa kile ulichojaliwa, ikiwa ni senti mbili, au milioni 10, mpelekee Bwana. Wengi waliotenda hivi walifanikiwa.

Malaki 3:10 “”Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Hivyo kwa kuzingatia, mambo hayo sita, basi ni hakika Mungu atakujibu maombi yako. Na utamfurahia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

Namna ya kuomba

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Rudi nyumbani

Print this post

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Kujazi maana yake ni kulipa.

Kwamfano tusome Neno hilo jinsi lilivyotumika na kumaanisha katika maandiko;

Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.

3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;

4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Maana yake ni kwamba, unapokuwa mtu wa kutoa sadaka bila kuwa na nia ya kuonekana mbele za watu, basi Mungu atakulipa kwa utoacho.

Mathayo 6:6 “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mathayo 6:17 “Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Vilevile unapokuwa mtu wa kuomba na kufunga, lengo lako likuwa ni kujisogoza mbele za Mungu na sio kufanya mashindano, au kuonekana na watu kuwa ni wa kiroho sana, basi Mungu atakulipa kwa hicho ukifanyacho.

Ruthu 2:11 “Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo.

12 Bwana akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake”.

Tunaona pia hapa Boazi akimbariki Ruthu, kwa wema wake aliomfanyia mkwewe, na kumwambia Bwana akulipe kwa kazi yako njema.

Lakini ni ujumbe gani Bwana anapitisha katika haya?

Ni kuonesha kuwa hakuna tendo jema tutakalomfanyia Mungu asirudishe malipo, endapo tutafanya ipasavyo. Kama kweli utaomba mbele zake, utafunga kwa ajili yake, utamtolea sadaka zako, kama kweli utatenda wema wowote, fahamu kuwa hilo Bwana atakulipa tu kwa wakati wake, thawabu yako haitakupita.

Hivyo atukuzwe Mungu awezaye kutuona na kuturehemu na kutubariki. Sifa, heshima na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI
Wingu la Mashahidi
JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.



Loading





/

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wa Ulimwengu, Simba wa kabila la Yuda, na Mkuu wa wafalme wa dunia, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu, lililo mwanga wa njia yetu, na taa iongozayo miguu yetu.

Upo wakati wakati ambao tutahitaji Bwana atuguse mara ya pili, lakini ni vizuri kujua kanuni ya kupokea Uponyaji pindi tunapomsihi Bwana atuguse tena…

Hebu tusome kisa kimoja katika biblia na kisha tutafakari na tujifunze, kanuni ya kupokea uponyaji mkamilifu.

Tusome Marko 8:22-26, (Zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufi kubwa).

Marko 8:22 “Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.

23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, AKAMTEMEA MATE YA MACHO, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?

24 AKATAZAMA JUU, AKASEMA, NAONA WATU KAMA MITI, INAKWENDA.

25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, NAYE AKATAZAMA SANA; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.

26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.

Katika kisa hichi hebu tujiulize swali lifuatalo, kisha tuendelee mbele..

Je inawezekana mtu atazame juu halafu aone watu?, tena watu wenyewe wanatembea? Na tena wanatembea kwa kasi kama miti?… Nilitegemea hata angesema anaona “ndege wanaruka, wanakimbia kama miti”!! Lakini yeye anasema anaona watu!!……Bila shaka ulishawahi kusafiri na basi linalokwenda kasi, na njiani ukaona namna miti inavyoonekana kama inarudi nyuma kwa kasi sana…Ndivyo alivyoona huyu mtu alipotazama juu..aliona watu!..

Kwa kawaida, huu sio uponyaji!!.. Huyu mtu hakuwa amepata uponyaji wowote, bali alikuwa katika hatua za mwanzo za kupokea uponyaji..ni kama tu TV iliyowashwa ambayo bado haijakamata mawimbi!!..inakuwa inaonyesha tu chenga chenga…

Lakini tunaona tabia ya kipekee ya huyu kipofu baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili.

Utaona huyu kipofu mara ya kwanza alipoguswa, alitazama juu hakutumia muda mrefu kutazama, badala yake, kwa haraka haraka akakimbilia kumjibu Bwana kwa kusema “anaona watu kama miti”….. lakini baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili, ni kama alijifunza kitu kuwa hana budi kutokuwa na haraka ya mambo…utaona alitulia na KUTAZAMA SANA!! (pengine alitumia dakika kadhaa kutazama juu), akawa bado anaona ile ile miti, lakini hakuacha kutazama…..

Na alipozidi KUTAZAMA SANA, pengine akaanza kuona  ile miti inafutika kidogo kidogo, akaanza kuona anga linakuwa jeupe na kidogo kidogo akaanza kuona mawingu, na pengine akaanza kuona ndege wanaruka, na alipotazama mbele akamwona Bwana Yesu, ndipo akasema sasa ninaona!!! Haleluya.

Na sisi hatuna budi KUTAZAMA SANA!!..Tusiishie kutazama kidogo tu! tusiishie kuzungumza, wala kunung’unika, wala kukosoa, wala kutoa hitimisho, pale tunapoona uponyaji haujakamilika….bali turuhusu uponyaji wa Bwana ufanye kazi!… Tuwe na Subira huku tukiliamini Neno lake.

Kutazama sana, ni kudumu katika kumwamini Mungu, hata kama unaona lile tatizo bado halijatatuka… wewe endelea kumwamini Bwana na kusubiri, bila kutoa uso wako juu mpaka muujiza wako utakapokamilika..

Pengine ulimwomba Bwana kuhusu hali unayopitia ya kiroho au kimwili,  lakini uliishia kuona chenga chenga katika huo ugonjwa, au hilo tatizo..lakini sasa umeijua kanuni..Msii Bwana akuguse tena kwa mara nyingine, lakini safari hii USIRUHUSU IMANI YAKO IPUNGUE, WALA USIUKIRI UGONJWA.…Utaona muujiza wa ajabu, ukitendeka!!.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Mwerezi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

USIISHIE TU KUPATA HAKI, BALI PATA NA WOKOVU.

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe!. Karibu tuyatafakari maandiko,

Neno la Bwana wetu, lililo chakula cha roho zetu linasema hivi..

Warumi 10:10 “Kwa maana KWA MOYO mtu huamini HATA KUPATA HAKI, na KWA KINYWA hukiri HATA KUPATA WOKOVU”.

Ipo sababu kwanini Biblia imetenganisha hayo mambo mawili, HAKI na WOKOVU. Watu wengi leo wameishia kupata HAKI tu, lakini si WOKOVU.. Wapo wengi leo waliomwamini Bwana Yesu mioyoni mwao na kuishia kupata haki sawasawa na Warumi 5:1 na Wagalatia 2:16, lakini hawana WOKOVU, maishani mwao, Na Wokovu unakuja kwa kumkiri Yesu na maneno yake kwa kinywa!.

Wakati Bwana Yesu akiwa duniani, walikuwepo Mafarisayo na wakubwa wengi waliomwamini mioyoni mwao, lakini katika Vinywa vyao, hawakumkiri..na hivyo Imani yao ikahesabika si kitu!.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu WALIKUWAMO WENGI WALIOMWAMINI; lakini kwa sababu ya Mafarisayo HAWAKUMKIRI, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Umeona?. walivifunga vinywa vyao, kuhofia kutengwa na dini zao, au madhehebu yao, au wakubwa wenzao, au kuonekana washamba na waliorukwa na akili!!..

Ndugu unapomwamini Bwana Yesu na maneno yake, ndani ya moyo wako, hiyo bado haitoshi kukupa wewe wokovu.. Huna budi kumkiri kwa kinywa chako kila siku katika Maisha yako..  Wokovu wa siri siri, na wakujificha ficha huo sio wokovu kibiblia!!.. Bwana Yesu alisema mtu yeyote akimwonea yeye na maneno yake, yeye naye atamwonea haya mtu huyo mbele za baba yake na malaika zake.

Luka 9:26 “Kwa sababu kila ATAKAYENIONEA HAYA MIMI NA MANENO YANGU, Mwana wa Adamu ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu”.

Soma tena..

Mathayo 10:32 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, NAMI NITAMKIRI MBELE ZA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”.

Umeona?..kumbe unaweza kuwa umemwamini Bwana Yesu moyoni mwako, lakini kwasababu tu! Humkiri maishani mwako, siku ile naye akakukana!!..kumbe wokovu wetu unakamilika pia kwa kumkiri Bwana Yesu.

Wakati Fulani, Bwana Yesu alimponya kipofu mmoja, ambaye alizaliwa katika hali hiyo ya upofu.. Na baada ya kumponya..Wazazi wake yule kipofu, walimwamini Bwana Yesu kuwa ni Kristo, lakini kwa hofu ya kutengwa hawakumkiri kwa vinywa vyao, lakini mwanao ambaye alikuwa kipofu, alimwamini Bwana Yesu na kumkiri..

Yohana 9:18 “Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona.

19 Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa?

20 Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu;

21 lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe.

22 Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu WALIWAOGOPA WAYAHUDI; kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba MTU AKIMKIRI KUWA NI KRISTO, ATATENGWA NA SINAGOGI.

23 Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye”.

Umeona hawa wazazi, walikuwa na Imani mioyoni mwao, lakini Imani yao haikuwasaidia..Bwana Yesu hakuwafuata…lakini mbele kidogo, utaona Bwana anamfuata yule kipofu, na kujidhihirisha kwake kwasababu alimkiri..

Yohana 9:33 “Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote.

34 Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje.

35 YESU AKASIKIA KWAMBA WAMEMTOA NJE; NAYE ALIPOMWONA ALISEMA, WEWE WAMWAMINI MWANA WA MUNGU?

36 NAYE AKAJIBU AKASEMA, NI NANI, BWANA, NIPATE KUMWAMINI?

37 YESU AKAMWAMBIA, UMEMWONA, NAYE ANAYESEMA NAWE NDIYE.

38 AKASEMA, NAAMINI, BWANA. AKAMSUJUDIA”.

Leo Bwana Yesu ajidhihirishi kwa wengi, kwasababu hiyo moja tu!.. ya KUTOMKIRI YEYE!!.. Tunampenda na kumwamini kweli Yesu, lakini hatuwezi kumkiri mbele ya mabosi zetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wanafunzi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wafanyakazi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya ndugu zetu…huku tukidhani kuwa ndio tunao wokovu..kumbe bado hatuna wokovu!!!.

Vile vile ukiyaonea haya maneno yake yote ya kwenye biblia..bado hauna wokovu!!.. Haijalishi unalijua Neno kiasi gani, au unaijua biblia kiasi gani…

Siku zote kumbuka hilo, Wokovu wetu unakamilika na KUMKIRI BWANA YESU NA MANENO YAKE!!!!..(Usilisahau hilo kamwe).

Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, KATIKA KINYWA CHAKO, na katika MOYO WAKO; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post