Biblia inamfananisha Bwana wetu Yesu Kristo na Melkizedeki kuhani wa Mungu aliye hai.. Na hiyo yote ni Kutokana na jinsi alivyofanana na Kristo kwa kila tabia aliyokuwa nayo.
Waebrania 7:1-3 [1]Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki; [2]ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani; [3]hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Waebrania 7:1-3 [1]Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
[2]ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;
[3]hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia utajiuliza ni kwanini siku ile Ibrahimu alipotoka kumwokoa ndugu yake Lutu ambaye alikuwa tayari ameshatekwa na maadui, Melkizedeki hakumpa zawadi nyingine zaidi ya MKATE NA DIVAI..
Jiulize ni kwanini iwe mkate na Divai, na ni kwanini uwe ni wakati ule? Na si mwingine..kwanini Melkizedeki asingempa Dhahabu na Lulu kama pongezi, au kwanini asingempa kondoo na mbuzi kama zawadi kwake..badala yake anampa divai na makate, kitu kidogo tu.. kuna nini?
Mwanzo 14:17-20 [17]Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. [18]Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. [19]Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi. [20]Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.
Kama tulivyotangulia kuona kuwa Melkizedeki anafananishwa na Yesu Kristo kwa kila kitu..Habari hiyo inajirudia kwa Kristo alipokuwa anaondoka duniani..
Hakuwaacha hivi hivi tu mitume wake, bali aliwapa uzima wake kwa mfano wa mkate na divai akasema huu ndio mwili wangu na damu yangu imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi, kuleni huu, na nyweni hii kwa ukumbusho wangu na kutangaza mauti yake inayowaokoa watu (Mathayo 26:28)
Sasa tarajio lake kubwa ni kutuona sisi tunashiriki ipasavyo..anatarajia kutuona tupo katika mazingira kama ya Ibrahimu..ambaye yeye hakuona vema kukaa tu hivi hivi angali ndugu yake Lutu amechukuliwa mateka..aliamua kutoka aende kumkomboa, kutoka mikononi mwa wale wafalme wa mbali.
Na ndipo Mungu alipouona moyo huo wa Ibrahimu akaona anastahili kushiriki mwili na damu ya Yesu Kristo.
Lakini je! Tujiulize na sisi tangu tulipoanza kwenda makanisani, na kushiriki meza ya Bwana mara zote hizo..Je! Ni ushuhuda gani Kristo anauona ndani yetu aone kwamba tumestahili kuishiriki meza yake.
Kila tendo la rohoni lina kanuni yake.. Ili ule uzima ambao Bwana Yesu alisema utaingia ndani yetu pale tu tunaposhiriki meza yake, uingie, ni lazima tujue kanuni zake vinginevyo tutakuwa tunafanya kazi bure tu.
Yohana 6:53-54 [53]Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. [54]Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Hivyo, tukumbuke hilo pia tukaribiapo nyumbani kwa Bwana anatazamia tuwaangazie na wengine nuru yetu ya wokovu tuliyoipokea..Ndipo tustahili vema kushiriki meza yake. Lakini kama tutakuwa ni watu wa kuingia kanisani na kutoka, baada ya hapo hatuna habari tena na Mungu. Ni heri tuache tu.
Bwana atasaidie katika hilo.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.
Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?
Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: BWANA YESU asifiwe mtumishi, mistari hii inanichanganya nisielewe vizuri, Neno la Mungu linasema;
Hesabu 23:19 Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?
Hapa biblia inasema hasemi uongo Wala hajuti, lakini ukisoma tena hapa inasema
1 Samweli 15:11 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha.
Nashindwa kuutambua ukweli Ni upi?
JIBU: Ukweli ni kwamba Mungu HAJUTI..Isipokuwa kuna wakati anajiweka katika mazingira ya kibinadamu ili tuzielewe hisia zake vema.
Na ndio maana mahali pengine utaona anazionyesha kazi zake kama vile zinamapungufu fulani, hazijakamilika..mpaka anatumia neno SI VEMA huyu mtu aishi peke yake nitamfanyia msaidizi, kana kwamba hakuliona hilo tangu mwanzo, lakini ukisoma mwanzoni kabisa katika kitabu cha Mwanzo 1:27 inatuambia tayati alishamuumba mwanaume na mwanamke katika mawazo yake..lakini katika utekelezaji anajifanya kama kasahau, ndio hapo anakuja kumuumba mwanamke baadaye sana baada ya uumbaji wote kukamilika Mwanzo 2:8..
Hiyo ndio tabia ya Mungu. Anajiweka hivyo wakati mwingine ili kutufundisha sisi jambo.
Mara nyingine anajifanya kama hana mashauri bora ya kumzidi mwanadamu..utakumbuka kule jangwani Musa alimshauri Mungu aghahiri mawazo yake..lakini haimaanishi kuwa Mashauri yetu ni zaidi ya Mungu. Soma Kutoka 32:9-14
Halikadhalika hapa..anasema..yeye si mwanadamu hata ajute..ikiwa na maana mipango yake yote tayari alishaiona mwisho wake utakuwaje tangu mwanzo..kwamba huu utaishia katika uzuri au huu utaishia pabaya..kwamfano alipomuumba shetani, alijua kabisa ataasi, na atawapoteza malaika na wanadamu wengi..lakini akamuumba hivyo hivyo..
Hata sasa Mungu anajua kabisa mwisho wa kila mwanadamu na kila jambo..kwamfano katika habari hiyo ya Sauli..Mungu alijua atakuja kukengeuka huko mbeleni..lakini alimpa bado ufalme..
Na alipokuja kukengeuka kweli, ndio tunaona Mungu anamwambia Samweli najuta kwanini nimechagua Sauli awe mfalme..kuonyesha tu hisia zake juu ya Sauli ili sisi wanadamu tumuelewe. Lakini alifahamu kila kitu.
Halikadhalika hata sasa mambo kama hayo Mungu anayafanya rohoni, .Mungu kukusifia leo haimaanishi kuwa ndio tiketi ya mbinguni moja kwa moja…Mungu kukutia mafuta sasa na kuwaacha wengine, haimaanishi kuwa wewe ndio kipendwa cha Bwana, hata ukifanya dhambi atakusitiri tu siku ile kisa ni kuhani wake.
Ukweli ni kwamba wapo watu ambao wataishia kuwa manabii wa uongo, wengine wapinga-kristo, na jehanamu wataenda..lakini ushuhuda wa wito watakuambia ni Yesu mwenyewe alinitokea na kunituma..Akanipa na ishara za miujiza, lakini wanaishia motoni
Mathayo 7:21-23 [21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. [22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? [23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Swali ni je…umempa Kristo maisha yako na kusimama kweli kweli? Unahabari kuwa Karama pekee sio uthibitisho kuwa Mungu yupo na wewe? Wakati wowote anaweza kujutia na kughahiri huo wito wako, aliokupa kama unasua sua
Kama hujasimama imara, fanya hivyo sasa. Mgeukie muumba wako kwa kumaanisha kwasababu, kumbuka hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi
Bwana akubariki.
Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)
THAWABU YA UAMINIFU.
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
JE! NA SISI NI SHABA ILIAYO NA UPATU UVUMAO?
Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.
Podo ni kimfuko au kibegi kidogo aidha cha ngozi au malighafi nyingine, ambacho hutumika kubebea mishale.
Utalisoma Neno hilo katika vifungu hivi;
Mwanzo 27:1-3[1]Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa.[2]Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.[3]Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;
Soma pia Ayubu 39:23, Isaya 49:2, Yeremia 5:16
Lakini Hiyo inafunua nini rohoni? Sikuzote askari makini huwa habebi mchale mmoja anapokwenda vitani..atahitaji Furushi la mishale kujihakikishia ushindi wake dhidi ya adui zake. Na ndio hapo atahitaji podo la kuihifadhia hiyo mishale yake.
Ni kama mwanajeshi, hawezi kutegemea risasi moja kujihakikishia ushindi atakuwa na mkanda wa risasi, ili adui yake ajapo amshindilie vya kutosha..
Halikadhalika na sisi kama wakristo, hatuna budi kuwa na podo zetu zenye mishale mingi ya kumpiga yule adui.Hatumpigi shetani kwa maombi tu peke yake, vinginevyo tutakwama mahali.. tutampiga kwa mshale wa kuhibiri injili pia, kwa mshale wa kutenda matendo mema, kwa mshale wa kumtolea Mungu sadaka, kwa mshale wa kuwasaidia wenye uhitaji, kwa mshale wa utakatifu n.k.
Hapo ndipo tutakuwa tumezijaza podo zetu silaha.
Embu soma kwa makini vifungu hivi;
Zaburi 127:4-5[4]Kama mishale mkononi mwa shujaa, Ndivyo walivyo wana wa ujanani.[5]Heri mtu yule Aliyelijaza podo lake hivyo. Naam, hawataona aibu Wanaposema na adui langoni.
Nasi tujitahidi kujaza podo zetu silaha nyingi ili shetani asipate upenyo wa kutushambulia kirahisi.
Bwana akubariki
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?
Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).
KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.
Mjoli ni mfanyakazi-mwenza, Ni mtu unayefanya naye kazi moja inayofanana.. Kwamfano kama wewe ni mwalimu, ukakutana na mwalimu mwenzako huyo ni mjoli wako…Kama wewe ni mhubiri ukakutana na mhubiri mwenzako huyo ni mjoli wako, kama wewe ni mkulima ukakutana na mkulima mwenzako huyo ni mjoli wako..
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia..
Mathayo 18:23-35[23]Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.[24]Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talantaelfu kumi.[25]Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.[26]Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.[27]Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.[28]Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinarimia; akamkamata, akamshika koo, akisema, Nilipe uwiwacho.[29]Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.[30]Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.[31]Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.[32]Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;[33]nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?[34]Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.[35]Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.
Wafilipi 4:3[3]Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi naye, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.
Soma pia..Wakolosai 1:7 ,4:7, Ufunuo 19:10, 22:9.
Vivyo hivyo na sisi watakatifu ulimwenguni kote tuliookolewa na Yesu Kristo, kila mmoja ni mjoli kwa mwenzake. Hivyo hatuna budi kupendana, kutumikiana, kusameheana.. Maadamu tupo katika shamba moja na kazi moja, tunapaswa kuujenga ufalme wa Mungu kwa nguvu zetu zote. Huku tukizingatia misingi ya Biblia, na sio ya kidhehebu au kidini
Yule aliyemzuia Yohana asimsujudie alikuwa ni Mwanadamu au Malaika?
Makuruhi ni nini, kama tunavyosoma katika biblia?
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.
SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto.” (Marko 9:49)
JIBU: Kama tunavyofahamu kazi kubwa ya chumvi ni kiungo, kiasi kwamba chakula kinaweza kikawa ni kizuri kweli, kinavutia kwa macho, kina harufu nzuri, lakini kikikosa chumvi huwa kinapoteza ladha yote, haijalishi kilitengenezwa kwa viungo vingi kiasi gani.
Vivyo hivyo na sisi kwa Mungu, ili tuwe tumestahili kuingia katika ufalme wake wa mbinguni, ni lazima tuwe kama chakula kilichokamilika kwake, tukikosa ladha tu ya chumvi yake, kamwe hatuwezi kuuingia ufalme wake.
Sasa ili kuelewa vizuri chumvi hiyo tunaipate, au inakujaje kujaje ndani yetu, tusome Habari yenyewe, kuanzia vifungu vya juu yake kidogo, ili tupate picha kamili;
Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika; 44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [ 46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum; 48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki. 49 KWA SABABU KILA MTU ATATIWA CHUMVI KWA MOTO. 50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi”.
Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;
44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [
46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
49 KWA SABABU KILA MTU ATATIWA CHUMVI KWA MOTO.
50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi”.
Umeona, baada ya maagizo hayo, mwishoni kabisa Kristo ndio anasema na sisi tutatiwa chumvi lakini si kwa kitu kingine bali kwa MOTO.
Na moto wenyewe ndio huo, aliokuwa anauzungumzia hapo juu, kwamba kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate, unapokata kiungo chako, utasikia maumivu kweli, lakini ndio tiba ya kukufikisha mbinguni, ndio chumvi yenyewe inayokufanya ulete ladha mbele ya Mungu.
Hiyo ikiwa na maana kuwa, hata wewe, binafsi unafahamu kabisa vipo vitu ambavyo vinakukosesha vinakufanya usimrudie Mungu wako kikamilifu, inawezekana ni kazi Fulani, au kampani ya marafiki zako walevi, au wahuni, au wadada wenzako wadadisi, au ndugu zako, au binti yule, au kijana yule. Kumbuka Bwana amekupa amri hii, ikiwa wanakufanya uikose mbingu, Achana nao, haraka sana bila kuangalia nyuma.. wakatae..
Ni kweli inauma,unapoviacha hivyo vitu, au unapowaacha ni moto utausikia, lakini ndivyo unavyotiwa chumvi na Bwana. Kwasababu usipoukubali moto huo sasa, utakutana nao siku ile utakaposhuka Jehanum ukifa.
Huu si wakati, wa kuikumbatia dhambi hata kidogo, si wakati wa kumwangalia mtu Fulani anasema nini juu ya Maisha yako ya milele, mbinguni utakwenda peke yako, vilevile usipotubu jehanumu utakwenda peke yako. Ni heri upitie shida hapa duniani, kule ukaishi milele kwa rah a na Mungu, kuliko kupitia raha za kitambo hapa duniani, halafu kule ukaishia motoni milele.
Hivyo ndugu yangu kubali kutiwa chumvi sasa, kwa kukubali kuacha yale ambayo yameshikamana sana na wewe kwa wakati huu wa siku za mwisho.
Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”,
“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?
OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.
Nini tofauti kati ya moyo na roho?
UNYAKUO.
WhatsApp
SWALI: Je Wakati Mfalme Nebukadreza anawatupa Shadraka, Meshaki na Abednego kwenye tanuru la Moto, Danieli alikuwa wapi?
JIBU: Kwasababu biblia haiandiki kila habari, bali inachagua yale matukio muhimu tu, yatakayotusaidia, ndivyo ilivyo katika habari hii, haielezi habari za Danieli kwa wakati huo, alikuwepo wapi, lakini katika sintofahamu hiyo, tuna la kujifunza. Hivyo hapo mambo matatu yanawezekana,
La kwanza ni aidha Danieli hakuwepo, wakati huo, ambapo Nebudreza, anatoa amri, kwasababu utakumbuka kuwa yeye aliyewekwa juu ya waganga wote, na wenye hekima (Danieli 5:11). Hivyo kuna uwezekano, alipewa jukumu lingine la kwenda kulifanya nje ya Babeli kwa wakati huo , na mbio ilipopigwa yeye hakuwepo.
La pili, ni aidha, watu waliokuwa pamoja na mfalme agizo hilo halikuwahusu, kwasababu ukichunguza utaona, Nebukadreza, aliwaita wakuu wake wote waliokuwa katika majimbo yake yote ulimwenguni. Na lengo la kuwaita, lilikuwa ni kuwapima utiifu wao kwa serikali yake moja ya ulimwengu. Ndio maana akawalazimisha wakuu wote ambao wapo mbali naye waje kuisujudia sanamu yake. Hivyo kwasababu Danieli alikuwa katika jumba la mfalme agizo hilo halikumuhusu.
Danieli 2:49 “Tena, Danielii akamwomba mfalme, naye akawaweka Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wawe juu ya mambo yote ya uliwali wa Babeli; lakini huyo Danielii alikuwa akiketi katika lango la mfalme”.
Na mwisho, ni kwamba Danieli, tangu mwanzo alisimama katika misingi ya Imani yake, utakumbuka, walipoitwa na kutaka kulishwa Divai, pamoja na vyakula najisi, moja kwa moja walivikataa yeye pamoja na hao wenzake watatu. (Danieli 1:8-16) Hivyo uwezekano pia wa Danieli kumweleza mfalme misimamo wake, ulikuwepo, na mfalme akamwelewa, akamwacha peke yake asiisujudie miungu yake.
Lakini kusema kwamba alitii amri ya mfalme, hilo jambo halipo, wala lisingewezekana kwa Danieli, kwasababu utakumbuka, hata baadaye sana, jaribio kama hilo lilitaka kufanyika, la kumzuia asimwabudu Mungu wake, lakini alikaidi amri yao bila kujali nani kasema, au adhabu gani imetolewa.
Lakini habari hii ya kutokuwepo kwa Danieli inatufundisha nini? Ni kwamba, upo wakati Mungu atakuepusha na majaribu ambayo nafasi ya kuyakwepa ni ndogo sana, lakini pia upo wakati Mungu atakupitisha katika majaribu ya adui. Mwanzoni kikombe kile hakikumuhusu Danieli, lakini mwishoni, alishiriki kikombe cha kutupwa katika tundu la Simba.
Nasi pia, kuna nyakati ngumu zitapita mbele yetu katika eneo la imani yetu, na Mungu atatuvusha salama bila hata ugumu wowote, lakini pia zipo nyakati ataziacha zipite juu yetu. Lakini yote katika yote, tunapaswa tuwe katika msimamo wetu kama vile Danieli.
Nyakati zote za mvua, na joto, misingi ya imani yetu isitikiswe.
DANIELI: Mlango wa 1
UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?
Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)
Nini maana ya kuutia moyo ufahamu? (Danieli 10:12)
Mwanzo 2:9
[9]BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Unaweza kujiuliza kulikuwa na sababu gani Mungu kuuweka mti wa ujuzi wa mema na mabaya pale bustanini wakati alikuwa anajua kabisa una kifo ndani yake?
Kwanini asingeuacha tu ule wa uzima na ile mingine ..ili mwanadamu aishi milele kwa furaha pale Edeni.
Je Ni kwamba Mungu hana mipango ya kueleweka kwa watu wake au?(tukizungumza kibinadamu)
Jibu la La! Nataka nikuambie mipango ya Mungu ni mikamilifu sikuzote na ni mizuri..tofauti na tunavyodhani kuwa ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya ulikuwa ni mbaya, haukustahili kuwepo pale.
Ukweli ni kwamba ule mti ulikuwa ni mzuri na unafaa sana, tena twamshukuru Mungu kwa kuuweka pale bustanini….Unajua ni kwasababu gani?
Ni kwasababu sisi kamwe tusingeweza kuwa kama Mungu, na malaika zake kama tusingepata ujuzi ndani yetu.
Kumbuka ujuzi ni jambo ambalo mwanadamu hakuumbiwa tangu mwanzo, si asili yetu..sisi tuliumbwa kutokujua mambo kama aibu, ustaarabu, mipango, maamuzi, ibada n.k hayo yote yalikuja baada ya kula matunda yale,
Sasa, Mungu aliliona hilo tangu mwanzo, hivyo akaona njia pekee ya kumkamilisha mwanadamu ili afanane na yeye ni kumpa ujuzi huo ndani yake..lakini aliona pia hatari yake..kwamba siku zote ujuzi una nguvu kubwa ya kupoteza,(1Wakorintho 8:1) hivyo akamtaadharisha mapema.
Ujuzi wa kujua mtu anahitaji kuishi katika nyumba na sio porini, kwamba anahitaji kujenga nyumba, kufanya biashara, kugundua vitu, kuvaa nguo na sio kukaa uchi, kujijengea mfumo n.k Mungu aliona mwisho wake utampoteza mtu, japo ujuzi wenyewe sio mbaya.
Ndipo akabuni njia ya kuweza kudhibiti tatizo hilo. Akaweka mti mwingine bustanini unaoitwa mti wa Uzima. Ambao mwanadamu akiyala matunda yake ataurejesha ule uzima ambao angeupoteza kwa kupokea ujuzi.
Na hapo mwanadamu atakuwa amepata faida mara mbili, kwanza ni kufanana na Mungu, pili ni kurejesha uzima wa milele.
Nachotaka ujue ni kuwa kila mwanadamu anayeishi duniani..ujuzi huu upo ndani yake..Na ndio maana unaweza kujiamulia mambo yako mwenyewe, unaweza kusema hapana au ndio..unaweza kusema nataka au sitaki..huwi kama mnyama, Au kama roboti bali una ujuzi wote wa kufanya unachotaka mwenyewe bila hata kumtegemea Mungu, mwanadamu au shetani..
Lakini nakuambia hii ni hatari kubwa kwasababu uhuru huu wa kifikra umetufanya wanadamu ndio tuende mbali sana na Mungu wetu, tupotee kabisa, tuone Mungu ni nani, mbona tunaweza kufanya wenyewe bila yeye, rangi zetu pekee hazitoshi, tujichubue kidogo, tujichore tatoo kidogo tupendeze, tuvute sigara, tunywe pombe tuwe fresh, tuzini na Wanyama, kwani kuna shida gani? . Kwa kifupi ni kuwa tumepotea kama tutaishi katika hii hali pasipo kuifahamu kinga.
Tunauhitaji mti wa uzima. Na mti wenyewe ni YESU KRISTO. Hakuna namna utaweza kuishi kwa ujuzi wako, au akili zako bila Yesu Kristo kukusaidia. Mwisho wa siku utakufa tu na kupotelea motoni.
Yohana 14:6
[6]Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Watu wengi leo wanadhani elimu zao, ndio zitawapa maisha, wanadhani tafiti zao ndio zitawafikisha ng’ambo, wanadhani mawazo yao na imani zao na teknolojia zao na ustaarabu wao ndio zitakazowavusha..
Hawajui kuwa mioyo yetu sisi wanadamu huwa ni midanganyifu kuliko kitu chochote huku duniani.
Yeremia 17:9
[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Na ndio maana Bwana Yesu alisema “Mtakufa katika dhambi zenu, kama msiposadiki kuwa mimi ndiye.”(Yohana 8:24)..tusipookolewa..hakuna tumaini ndugu. Bwana Yesu ndiye mti wenyewe wa uzima. Shusha kiburi chako, yasalimishe maisha yako kwake..akusaidie.
Siku hizi ni za mwisho, wakati wowote parapanda inalia hakuna mtu asiyelijua hilo, ipo wazi kulingana na dalili tunazoziona sasa. Hii dunia inafikia mwisho, mtafute Yesu Kristo, akuokoke na udanganyifu wa ujuzi.
Kama hujaokoka basi mkaribishe leo Yesu katika maisha yako, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, kisha utapokea ondoleo la dhambi.
Mungu akubariki.
HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
UFUNUO: Mlango wa 22
SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari”. Hii miamba yenye hatari ni ipi?
JIBU: Tusome..
Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa; 13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele”.
Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;
13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele”.
Hapa ni mtu Yuda alikuwa anawalinganisha wachungaji na mitume wa uongo kama miamba yenye hatari.
Sasa miamba inayomaanishwa hapo, si hii miamba tuionayo nchi kavu, hapana, bali ni ile miamba ya habarini ambayo baadhi yao inatabia ya kuchomoza juu hadi karibu na usawa wa bahari. Miamba hii ni hatari sana kwa mabaharia, kwasababu huwa haionekani, lakini meli inapopita karibu nayo, inaichana, kama sio kuiharibu kabisa na matokeo yake, ni aidha meli kugotea palepale, au kuzama kabisa.
Kama mabaharia wasipokuwa waangalifu, kwa kupita njia zilezile walizozithibitisha ni rahisi sana kukutana na hii miamba na kuzipoteza meli zao moja kwa moja.
Sasa hapo anaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu”;
Anamaanisha, wachungaji hawa, au watumishi hawa wa uongo ni ngumu kuwatambua, kama tu vile miamba hii hatari ilivyo ngumu kuiona habarini, pale ambapo Habari inaonekana shwari na tulivu yafaa kwa kusafiria kumbe ndipo ilipojifichia, halikadhalika, watumishi hawa wa uongo, mahali ambapo mpo katika karamu zenu za Upendo, yaani wakati ambapo mnamfurahia Mungu wenu, mnatangaza Habari njema, mkidhani kuwa wapo na nyie, kumbe ni mbwa mwitu katika mavazi ya kondoo.
Mfano wa watu hawa alikuwa ni Yuda,alitembea na Bwana Pamoja na mitume wengine, lakini haikuwa rahisi kumgundua, hadi dakika ya mwisho, utaona alipokuwa katika mlo wa jioni, kama mpelelezi, hakuna aliyemtambua isipokuwa Bwana tu peke yake.
Mtume Paulo aliliona hilo hata wakati wa kuondoka kwake akasema..
Matendo 20:29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; 30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”.
Matendo 20:29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;
30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”.
Hadi sasa, inasikitisha kuona watumishi wa namna hii wapo wengi katika kanisa la Mungu, ,hawaoni shida kuwadanganya watu, wengine ni wachawi, wengine ni matapeli, wengine wapo kwa lengo la kuzivuruga tu kazi za Mungu, ili watu watusiishi Maisha matakatifu, hawawahurumii watu wanaotaka kumjua Mungu, lakini cha ajabu ukiwaangalia kwa nje, wanalitaja jina la Yesu, wanaongoza makanisa, wanashiriki katika kampeni zote za kidini.
Huu ni wakati wa kuwa makini sana, Ni wakati ambao wewe kama mkristo, kuondoa uvivu wa kusoma biblia, tunadanganywa kwasababu hatuna maarifa ya kutosha kuhusu Mungu wetu na utendaji kazi wake. Hatuwezi kumshinda shetani kwa maneno tu, au kwa kumkemea, tutamshinda shetani kwa lile Neno lililokaa ndani yetu kwa wingi, ndiyo silaha ambayo Bwana Yesu aliitumia kumshinda shetani pale alipokuwa anajaribiwa nay eye kule jangwani.
Vinginevyo tukiyaendesha Maisha yetu hivi hivi tu kwa jinsi tunavyotaka, tujiandae kukutana na hii miamba yenye hatari, isiyoonekana. Tukiwa wavivu kujifunza biblia, hakuna namna tutamkwepa shetani, hakuna namna.
Bwana atusaidie.
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
Katika biblia ukiona neno “mwandamo wa mwezi”, au “mwezi mpya”, ujue ni neno lile lile moja linalomaanisha “siku ya kwanza ya mwezi”.
Katika agano la kale siku hii iliheshimiwa na kufanywa kama mojawapo ya siku takatifu, kama tu vile ilivyokuwa siku ya sabato, ambayo ni siku ya saba. Vivyo hivyo kila siku ya kwanza ya mwezi mpya, tarehe moja (kwa kalenda ya kiyahudi), ilikuwa ni takatifu kwao, na ni lazima watu wakamtolee Mungu sadaka za kuteketezwa, Sadaka za unga na vinywaji, Pamoja na kupiga tarumbeta juu ya sadaka hizo, (Hesabu 28:11-15), .Vilevile hukuruhusiwa kufanya shughuli yoyote au biashara yoyote(Nehemia 10:31-33)
Hesabu 28:11 “Tena katika mianzo ya miezi yenu mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa; nayo ni ng’ombe waume wadogo wawili, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza, wakamilifu, saba; 12 pamoja na sehemu ya kumi tatu za efa za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa kila ng’ombe; na sehemu ya kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa huyo kondoo mume mmoja;”
Hesabu 28:11 “Tena katika mianzo ya miezi yenu mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa; nayo ni ng’ombe waume wadogo wawili, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza, wakamilifu, saba;
12 pamoja na sehemu ya kumi tatu za efa za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa kila ng’ombe; na sehemu ya kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa huyo kondoo mume mmoja;”
Hesabu 10:10 “Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu”.
Lakini kuna wakati wayahudi, walizifanya sikukuu hizo kama mazoea tu, wakawa hawazitoi katika utakatifu, bali kama agizo tu la kidini na huku nyuma mioyo yao ipo mbali na Mungu, hivyo hiyo ikamfanya Mungu akasirishwe nao na hatimaye kuzitaa sikukuu zao hizo za mwandamo wa mwezi.
Isaya 1:13 “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. 14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua”.
Isaya 1:13 “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.
14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua”.
Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;
Zaburi 81:3 “Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu”.
1Samweli 20:5 “Naye Daudi akamwambia Yonathani, Tazama, kesho ni mwandamo wa mwezi, nami hainipasi kukosa kuketi chakulani pamoja na mfalme; lakini niache nijifiche bondeni hata siku ya tatu jioni.
Soma pia, 2Nyakati 2:4, 8:13, Ezra 3:5, Hosea 2:11.
Jibu ni la! Kama tu vile hatujapewa takwa la kuitunza sabato kama sheria , vivyo hivyo, na katika mwandamo wa mwezi mpya.
Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; 17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.
Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.
Ni kwamba tuthaminishe nyakati zetu mpya kwake. Wiki yako inapoisha na kuanza nyingine bila kumfanyia Mungu wako ibada, ni hatari kubwa sana, kama kwako ni jumapili, au jumamosi, ndio unamfanyia Mungu ibada, hakikisha unakutanika na wengine, kumwabudu Mungu wako, usiruhusu wiki yako ipite hivi hivi tu.
Halikadhalika, mwezi wako mpya unapoanza, usianze hivi hivi tu, bali chukua muda kwenda kumshukuru Mungu nyumbani kwake, ni muhimu sana. Ukiona wiki yako inapita hivi hivi tu, mwezi wako unapita hivi hivi tu, mwaka wako unapita hivi hivi tu, huna Habari na Mungu. Angalia Maisha yako ni lazima yatakuwa na kasoro Fulani tu.
Hivyo tujitahidi sana, tusiwe na mapengo pengo kwa Mungu wetu.
SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?
MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?
Huu mstari una maana gani?
Zaburi 91:1 “Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi”.
Maandiko hayo yanatuonyesha kumbe Mungu anao uvuli wake. Na uvuli huo hawakai watu wote ilimradi tu, bali wale tu wanaokaa katika mahali pake pa siri.
Sasa swali utajiuliza huko mahali pake pa siri ni wapi?
Kuna madaraja ya kumfikia Mungu, yapo yanayofikiwa na wakristo wa kawaida tu, wale wanaomtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, au mwezi kwa mwezi, lakini pia yapo yanayofikiwa na wakristo waliojikana, na kudhamiria kumfuata Kristo katika Maisha yao.
Hao wanaojikana ndio wanaofikia mahali pa siri pa Mungu.
Wanafananisha na makuhani, ambao, katika ile hema ya kukutania, au hekalu la Mungu, ni wao tu walikuwa na uwezo wa kupaingia patakatifu, na kule patakatifu pa patakatifu, palipo na kile kiti cha rehema cha Mungu.Kumbuka si kila mwisraeli, alifika pale, si kila mtu anayejiona anamcha Mungu aliweza kufika pale, kwa mtu wa kawaida ukijitahidi sana, uliishia katika ule ua wa hema ya kukutanikia, lakini ndani, sehemu za siri za Mungu walioweza kuingia makuhani tu.
Vivyo hivyo katika agano jipya, Mungu anao sehemu yake ya siri, na ni watu baadhi tu wanaoweza kufika huko, Mfano hai katika biblia ni mwanamke kama ANA, yeye, aliweza kupafikia hapo..na ndio maana alikuwa miongoni mwa watu wachache sana waliofunuliwa mpango wa Mungu wa wokovu,yaani kuja kwake Yesu duniani..
Lakini hiyo yote ni kwasababu alikuwa ni mwanamke aliyeupoteza ubinti wake, autumie kwa Mungu hadi uzee wake, haundoki hekaluni, mchana na usiku akisali na kufunga.
Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. 37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba. 38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.
Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.
37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.
38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.
Mwingine, ni Simeoni, naye pia biblia inasema alikuwa ni mtu wa haki, na anaye mcha Mungu, tena Zaidi alikuwa anautazamia wokovu wa taifa lake Israeli, yaani wakati wayahudi wapo bize na mali na fedha, yeye alikuwa kama Danieli, akiomba na kutafuta Habari za kuja kwa masihi duniani.
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. 26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. 27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, 28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, 29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema; 30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,
Makundi ya watu kama hawa, huwa wanaonjeshwa kitu kingine tofauti na watu wa kawaida, huo ndio uvuli wake Mungu. Wanapewa mafunuo ya ndani sana, wanapewa ulinzi wa majeshi ya Malaika wengi,mfano Elisha, wanajaliwa haja za mioyo yao na Mungu. Kwasababu tayari wapo chini ya uvuli wake.
Je! Na sisi tunaweza kufikia mahali hapo?
Kama jibu ni ndio,
Basi hatuna budi, kufanana na makuhani wa Mungu kweli, wana wa Lawi, ambao wametengwa na dhambi na unajisi, Si tu kumkiri Kristo na kuendelea kuishi Maisha ya juu juu, bali tujikane na nafsi zetu pia kwake, yaani tuwe tayari kujitwika na misalaba yetu tumfate Kristo. Tukubali ulimwengu utupite na mambo yake yote.
Na kwa kufanya hivyo kwa neema zake, atatufikisha mahali pake pa siri.
Bwana atusaidie sote.
Amen.
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?
Barazani pa Mungu ni wapi? Kama tunavyosoma katika Yeremia 23:18?
Bwana alimaanisha nini aliposema mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?