Kibiblia Kitanga ni sehemu ya mwisho wa mkono wa Mtu, au mnyama..kwa jina lingine ni kiganja.
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.
Danieli 5:24-25 [24]Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa. [25]Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
Huu ni ule wakati mfalme Belshaza wa Babeli alipokuwa ameketi nankufanyia anasa vyombo vitakatifu vya Mungu pamoja na makahaba wake..ndipo hapo hapo kiganja cha mkono kikatokea na kuanza kuandika ukutani maneno hayo, mene mene tekeli na peresi.
Utalisoma Neno hilo pia katika vifungu hivi.
Mambo ya Walawi 14:26-27 [26]kisha kuhani atamimina sehemu ya hayo mafuta katika kitanga cha mkono wake mwenyewe wa kushoto; [27]kisha kuhani atanyunyiza baadhi ya hayo mafuta yaliyo katika mkono wake wa kushoto, kwa kidole chake cha mkono wa kuume mara saba mbele za BWANA;
Mambo ya Walawi 11:27 [27]Tena kila mnyama aendaye kwa vitanga vyake, katika hao wanyama wote waendao kwa miguu minne, hao ni najisi kwenu; awaye yote atakayegusa mizoga yao, atakuwa ni najisi hata jioni.
Isaya 49:16 [16]Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.
Soma pia; ( 2Wafalme 9:35, Danieli 10:10,
Lakini Je nini tunaweza kujifunza kila tutazamapo kitanga/ vitanga vyetu.?
Ukiwa mwovu..kumbuka kuwa siku moja kitanga cha Mungu kitakuandikia hukumu kama kilivyomwandikia Belshaza mfalme wa Babeli..kama wewe ni mfanyaji wa anasa, ni mzinzi, ni mlevi, ni mchawi, unaabudu sanamu..Bwana atakuadhibu kwa hukumu mbaya sana. Ya mene, mene, tekeli na Peresi.
Ukifikia hii hatua basi habari yako inakuwa imeishia hapo hapo.
Lakini ikiwa wewe unampenda Mungu na kumcha yeye, na kuyafanya maagizo yake..Vilevile ameahidi atakuandika katika vitanga vyake…ikiwa na maana mtu akiandika jambo katika kiganja chake lengo lake ni ili asikusahau, si ndio?..Ndivyo ilivyo kwa Mungu, kwa watu wake wampendao..amewaandika katika viganja vyake kamwe hawezi kuwasahau.
Isaya 49:14-16 [14]Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau. [15]Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe. [16]Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”
Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: Biblia inaposema mwanamke ataokolewa kwa uzazi wake, inamaanisha nini?
1Timotheo 2:14 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa. 15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi”.
1Timotheo 2:14 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.
15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi”.
JIBU: Tofauti na inavyotafsiriwa na watu wengi, kwamba andiko hilo linamaanisha kuwa mwanamke yeyote ambaye atakuwa na watoto wa kulea, basi mwisho wa siku ataokolewa kwa kutimiza tu kusudi hilo. Mtazamo ambao sio sahihi na unakinzana na maandiko, Kwasababu kama kila mwanamke angekuwa anaokolewa kwa namna hiyo, hata wanawake wachawi nao wangeokolewa kwasababu na wao pia wanao watoto wa kulea.
Lakini biblia ilimaanisha nini kuandika hivyo?
Mtume Paulo aliandika maneno hayo, kuonyesha jinsi gani huduma ya mwanamke ambaye ana watoto jinsi ilivyo na nguvu hata kusababishia wokovu kwake mwenyewe IKIWA atawalea watoto wake katika misingi ya imani, upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi kama ilivyoainishwa hapo..Na sio kwa kuzaa tu basi.
Kwasababu atakuwa ameifanya huduma ya kuokoa kizazi kingine.. Tengeneza picha kama wanawake wote ulimwenguni wangekuwa wanatimiza wajibu wao huu wa kuwalea watoto wao katika misingi ya imani, leo hii, kusingekuwa na haja ya kuhubiri injili kwasababu watoto wote wangekuwa tayari wanamjua Mungu. Lakini injili imekuwa ngumu kwa kizazi cha sasa kwasababu jambo la kwanza mzazi analolithamini kwa mtoto wake ni elimu tu, Mungu ni ziada, mtoto akifaulu darasani ndio furaha yake kubwa, wakati hajui hata mstari mmoja wa biblia. Hajui hata pambio moja la kumsifu Mungu. Mzazi haoni aibu hata mtoto wake anakuwa hadi mtu mzima hajui biblia ina vitabu vingapi.
Kwahiyo hapo mtume Paulo alikuwa anaonyesha nguvu iliyopo katika mwanamke kulea watoto wake vema, ambayo mwisho wa siku itampelekea hata na wokovu wake mwenyewe. Kwamfano Mungu akiona mtoto Yule ambaye alilelewa katika misingi kama Samweli, amekuwa sababu ya wokovu kwa Israeli, unategemea vipi Mungu amwache mama aliyemlea?. Ni sawa tu na yule anayewavuta watu kwa Kristo, ambao biblia inasema kitendo hicho kina nguvu ya kuokoa roho ya mhubiri na kufunika wingi wa dhambi zake.
Yakobo 5:20 “jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi”.
Kwahiyo ikiwa wewe ni mwanamke na Mungu kakujalia watoto ujue jukumu lako la kwanza, la injili ni kwa watoto wako, hakikisha hao wanakuwa katika misingi ya kumcha Mungu, wafundishe, na pale wanapokosea Mungu kakupa ruhusu ya kuwaadhibu, lengo ni kuwaweka katika mstari wa kumcha Bwana, na sio kuwatesa. Ukifanya hivyo matokeo yake utakuja kuyaona baada ya haya maisha hapa duniani.
Tito 2:4 “ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; 5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.
Tito 2:4 “ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;
5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.
Raheli aliwalilia vipi watoto wake?
MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)
TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI.
Bwana wetu Yesu Kristo atukuzwa. Ni siku nyingine tena tumepewa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tujifunze Neno la Mungu, maadamu siku yenyewe inakaribia.
Kama vile “Utakatifu na utakaso” vinavyokwenda Pamoja, vivyo hivyo, “Dhambi na Unajisi” ni vitu vinavyokwenda bega kwa bega.
Tofauti na Dhambi na unajisi ni ipi?
Dhambi ni kitendo mtu anachofanya kinyume na Mungu, na huwa inaambatana na kuvunja sheria, au maagizo yake. Kama vile kuzini, kuua, kuabudu sanamu n.k.
Lakini unajisi ni kitendo mtu anachokifanya kinyume na yeye mwenyewe, ambacho mwisho wa siku kinampelekea, Mungu kujitenga naye au kumuacha kwa muda Fulani.
Mtu mwenye dhambi unajisi hauna nguvu kwake bali dhambi tu, ..Lakini mtu aliyeokoka vyote vina madhara kwake, yaani dhambi na unajisi.
Ni sawa na doa jeusi lililopo katika shati, jeupe, doa hilo lingekuwa katika shati jeusi, shati hilo lingeendelea kuvalika kwasababu doa halionekani, lakini likiwa katika shati jeupe hata kama litakuwa safi vipi, doa lile tayari limeshaharibu kila kitu. Sasa huo ndio unajisi. Ambao mtu mchafu, hauna madhara yoyote kwake, lakini kwa msafi ni pigo kubwa.
Sasa kabla kufahamu Zaidi, embu tuangalie kwa agano la kale baadhi ya unajisi ulikuwa katika mambo gani.
Zamani, ilikuwa ukila au ukishika mzoga wa wadudu, au Wanyama ambao ni najisi, adhabu yake ilikuwa na wewe unakuwa najisi, kwa muda wa siku nzima..
Walawi 11:23 “Lakini vyote vitambaavyo vyenye mabawa, vilivyo na miguu minne, ni machukizo kwenu. 24 Nanyi mtakuwa najisi kwa wanyama hao; kila atakayegusa mzoga wao atakuwa ni najisi hata jioni;
Walawi 11:23 “Lakini vyote vitambaavyo vyenye mabawa, vilivyo na miguu minne, ni machukizo kwenu.
24 Nanyi mtakuwa najisi kwa wanyama hao; kila atakayegusa mzoga wao atakuwa ni najisi hata jioni;
Soma pia Walawi 11:29-32
Halikadhalika, kulikuwa na unajisi, wa kujifungua, ikiwa mwanamke atajifungua tu, kile kitendo cha kutokwa damu, tayari ni unajisi ambao unakugharimu siku saba, Pamoja na hayo, unajisi huo ulimgharimu siku nyingine tena 33, au 66 ikiwa ni mtoto wa kiume.. Kufanya jumla ya siku 40 kwa wa kiume, na siku 80 kwa wakike.
Unajisi huu ulikuwa pia katika kugusa maiti, au kutokwa na uchafu mwilini Soma(Walawi 15:16-20). Ulikuwa unakuwa najisi kwa muda wa siku 7, baada ya kujitakasa.
Sasa nachotaka uone ni kuwa, makosa kama haya aliyafanya mtu juu yake mwenyewe, ambayo hata huwezi kuyaona katika zile amri 10, lakini Mungu aliyatazama sana.
Katika agano la kale, wapo ambao walikuwa wanajitahidi kutotenda dhambi, yaani hawazini, hawaabudu sanamu, hawaibi, wanazitunza sabato n.k.
Lakini walikuwa wanakoseshwa na vitu vidogo tu kama hivyo vya unajisi, Na hivyo vikawa vinatia doa ukamilifu wao. Na matokeo yake, wakawa hawaruhusiwi kuingia hemani kwa Mungu, au katika mkusanyiko wowote wa watakatifu kwa kipindi Fulani, kulingana na aina ya unajisi wenyewe.. kama ni siku moja, au wiki, au miezi..
JE! Katika agano jipya unajisi upoje?
Unajisi wa sasa sio kama ule wa zamani, wa kushika, au kuionja, au kutokwa na vitu mwilini hapana.. Unajisi wa sasa wa mtu upo moyoni, Bwana Yesu alisema hivi;
Mathayo 15:17 “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni? 18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi. 19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano; 20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi”.
Mathayo 15:17 “Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi”.
Kama tunavyosoma, hapo, yale mambo ambayo yanakutoka moyoni, kama vile tamaa, uzinzi, uasherati, n.k. Sasa kumbuka hasemi kufanya uzinzi, au uasherati, bali kukutoka..yaani mawazo ya uzinzi au ya uasherati, hayo ndiyo yanayokutia wewe unajisi, kama mtakatifu.
Unaweza kweli ukawa huzini na wanawake, lakini kuruhusu tu tamaa ndani yako, tayari umeshajitia unajisi, unaonekana kama vile tayari umezini sawasawa na maneno ya Bwana Yesu (Mathayo 5:28).
Na matokeo yake, inaweza kukuchukua kipindi Fulani kirefu, usiuone uwepo wa Mungu maishani mwako, kwasababu ya unajisi tu kama huo.
Pengine, unawasengenya wengine, unatukana, una chuki na wengine, kiburi, kijicho n.k.(Soma Marko 7:17-23) mambo kama hayo yanaweza kukufanya uikose furaha ya wokovu kwa kipindi kirefu sana, hata baada ya kutubu kwako.
Hivyo unajisi ni wakujiepusha nao sana wewe kama mtakatifu wa Mungu, unaweza ukawa hauuji lakini kitendo tu cha kumchukia ndugu yako, tayari ni sawa na muuji. Umeshajitia unajisi.
Ili uendelee kubaki katika uwepo wa Mungu wakati wowote, uulinde sana moyo wako.
Bwana atusaidie sana.
Lumbwi ni nini katika biblia?
JIEPUSHE NA UNAJISI.
UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.
SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.
KUONGOZWA SALA YA TOBA
Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu tuyatafakari maneno ya uzima, ambayo pekee ndio yanayoweza kutufanya sisi tuwe huru kweli kweli hapa duniani( Yohana 8:32).
Leo tutajifunza, kanuni mojawapo ya kibiblia ambayo itatusaidia sisi kuweza kupokea jumbe, au mafunuo, au maarifa sahihi kutoka kwa Mungu, Imenisaidia mimi, naamini pia itakusaidia na wewe.
Kanuni ya sisi kuzungumza na Mungu, ni tofauti na ya kwake kuzungumza na sisi. Sisi tukitaka kuwasiliana naye tunachofanya ni moja kwa moja kwenda katika uwepo wake, na kupiga magoti na kupelekea haja zetu kwake, Na tukishamaliza tutanyanyuka na kuondoka na kwenda katika shughuli zetu.
Lakini Mungu, hana utaratibu huo wa kuzungumza na wewe papo kwa papo, kwa wewe ufanyavyo. Na hiyo imewafanya watu wengi wakate tamaa, pale wanapoona hakuna mwitikio wowote, kutoka upande wa pili wa Mungu.
Lakini leo tutajifunza kanuni ambayo muhimu sana kuizingatia ikiwa wewe unataka kumsikia Mungu, au kupokea mafunuo sahihi kutoka kwake.
NA KANUNI YENYEWE NI “UTULIVU”
Sauti ya Mungu ya kweli ipo katika utulivu, na si mahali pengine, Eliya alikuwa ni nabii ambaye Bwana anazungumza naye na kumpa taarifa nyingi, lakini hakuwahi kuisikia sauti ya Mungu vizuri, hadi siku ile alipokuwa katika utulivu, na ndio maana utaona akaufunika uso wake, alipomsikia (kuonyesha kuwa amemwona Mungu, hivyo hastahili hata kuzungumza naye). Lakini mara nyingine zote huko nyuma hakuwahi kuufunika uso wake. Utajiuliza ni kwanini? Ni kwasababu Mungu hakuwa karibu naye kama alivyomwona siku hiyo, alipokaa katika utulivu (1Wafalme 19:9-13).
Elisha alipotaka kupokea taarifa sahihi, na maagizo kutoka kwa Bwana juu ya nini yafanye yale mataifa matatu yaliyotaka kuangamizwa na taifa la Moabu,..hakukurupuka tu na kuzungumza na Bwana, bali alitaka kwanza kukaa katika utulivu, akamwita mpiga kinanda,aimbe naye nyimbo za kumsifu Mungu, ndipo taarifa sahihi zikamshukia baadaye.
2Wafalme 3:14 “Elisha akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo, ambaye nimesimama mbele zake, kama singemwangalia uso wake Yehoshafati mfalme wa Yuda, singekutazama, wala kuonana nawe. 15 Ila sasa niletee mpiga kinanda. Ikawa, mpiga kinanda alipokipiga, mkono wa Bwana ukamjia juu yake. 16 Akasema, Bwana asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 17 Kwa kuwa Bwana asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu. 18 Na jambo hili ni jepesi machoni pa Bwana; pia atawatia Wamoabi mikononi mwenu”.
2Wafalme 3:14 “Elisha akasema, Kama Bwana wa majeshi aishivyo, ambaye nimesimama mbele zake, kama singemwangalia uso wake Yehoshafati mfalme wa Yuda, singekutazama, wala kuonana nawe.
15 Ila sasa niletee mpiga kinanda. Ikawa, mpiga kinanda alipokipiga, mkono wa Bwana ukamjia juu yake.
16 Akasema, Bwana asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 17 Kwa kuwa Bwana asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
18 Na jambo hili ni jepesi machoni pa Bwana; pia atawatia Wamoabi mikononi mwenu”.
Vilevile Mungu alipotaka kuzungumza na Musa, ili kumpa zile mbao mbili za amri na sheria yake, alimwita mlimani, , lakini utaona Musa hakwenda moja kwa moja tu,hadi kileleni bali ilimbidi asubirie chini kwa muda wa siku sita (6). Ndipo siku ya saba akasikia sauti ya Mungu ikimwita apande mlimani.
Kutoka 24:15 “Musa akapanda mlimani, lile wingu likaufunikiza mlima. 16 Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu. 17 Na kuonekana kwake ule utukufu wa Bwana kulikuwa kama moto uteketezao, juu ya mlima machoni pa wana wa Israeli. 18 Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani; Musa akawa humo katika ule mlima siku arobaini, mchana na usiku”.
Kutoka 24:15 “Musa akapanda mlimani, lile wingu likaufunikiza mlima.
16 Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu.
17 Na kuonekana kwake ule utukufu wa Bwana kulikuwa kama moto uteketezao, juu ya mlima machoni pa wana wa Israeli.
18 Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani; Musa akawa humo katika ule mlima siku arobaini, mchana na usiku”.
Kwa mifano hiyo michache ni kutuonyesha na sisi kuwa, tukitaka tumsikie Bwana, hatuna budi kuwa katika utulivu rohoni, kwamfano unapokwenda kuomba, usiishie kuzungumza tu maneno yako halafu basi unaondoka, mpe Bwana nafasi, kaa chini imba, baadaye tafakari uweza wa Mungu, soma biblia, tafakari tena, kisha rudia tena kuomba.. kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo wa Mungu, ndivyo unavyompa nafasi Mungu ya kushuka na kukuhudumia.
Ghafla tu utaona wingu linakushukia roho, na hapo hapo unapokea ufunuo au maarifa, au taarifa Fulani ambazo hukuwahi kuziwaza au kuzifikiri, hapo ujue tayari ni Mungu huyo, au utapokea amani Fulani, au ufumbuzi Fulani, au agizo Fulani, hapo ujue Mungu anazungumza na wewe. Lakini inahitaji utulivu wa kitambo kidogo, wakati mwingine hata masaa kadhaa. Ni kweli yapo majira utaomba tu na kuondoka, lakini yapo majira ni lazima ujiwekee muda kwa Mungu, apate nafasi ya kusema na wewe.
Vilevile, yafanya Maisha yako, yawe katika utulivu, ukiwa ni mtu wa kukesha tu mitandaoni, kuchat chat kwenye magroup, au muda wote kutazama tazama, tv au tamthilia, au muvi, miziki au michezo michezo, au kuzurura zurura, leo party hii, kesho ile.. Fahamu kuwa mambo kama hayo ni adui mkubwa sana wa Mungu kuzungumza na wewe, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani, hutakuwa unaona mwitikio wowote kutoka kwa Mungu. Hiyo ni kwasababu haupo katika utulivu.
Kuwa mtulivu maishani, tumia muda wako, kusikiliza nyimbo za sifa kama Elisha alivyokuwa anafanya, tumia weekend zako kwenda mikesha kuomba, soma sana biblia, punguza marafiki ambao ni maadui wa Imani yako, zungumza sana Habari za Kristo, katika mazungumzo hayo utaona ufunuo unaingia ndani yake, kwasababu Kristo kashaungana nawe katika kinywa chako kama ilivyokuwa kwa wale watu wawili wa Emau (Luka 24:13)
Ukizingatia hivyo. Utamsikia, kama sio kupokea mafunuo mengi kutoka kwake, daima jiweke katika utulivu.
Sote tunatamani Mungu azungumze nasi, lakini tumekuwa na wasiwasi, tukadhani kuwa Mungu yupo mbali sana, na anasema tu na watumishi wakubwa, au manabii, hawezi kusema na wewe. Ukweli ni kwamba, Karama ya mtu, sio kigezo cha Mungu kuzungumza naye, haijalishi atasikia sauti, au maono, au ndoto nyingi kiasi gani. Mungu anaweza kuzungumza na kila mtu, kulingana na njia yake mwenyewe aliyotaka azungumze naye.
Japokuwa Eliya alikuwa karibu sana na Mungu, na kupokea maono mengi, na taarifa nyingi kutoka kwa Yehova, lakini hakuwahi kumsikia Mungu mwenyewe, na ndio maana hakuwahi kuufunika uso wake, maana yake hakusitiri uovu wake, alipokuwa anaongea na Mungu hadi siku ile alipokaa katika utulivu na ndio akamsikia Bwana kwa mara nyingine.,
1Wafalme 19:9 “Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya? 10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe. 11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi; 12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu. 13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?”
1Wafalme 19:9 “Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?
10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.
11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;
12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya?”
SAUTI YA MUNGU IPO KATIKA UTULIVU.
Jambo ambalo, wakristo wa sasa tunalikwepa sana,
NI KIPI KINAMZUIA MUNGU KUZUNGUMZA NA SISI?
USIISHI KWA NDOTO!
TEGEMEA MUNGU KUZUNGUMZA NAWE KATIKA MAMBO MADOGO
KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.
SWALI: Biblia inamaana gani kusema Yesu atawachunga kwa fimbo ya chuma..kwanini iwe ya chuma?
Ufunuo wa Yohana 19:15 [15]Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
JIBU: Fimbo ya mchungaji sikuzote ni fimbo ya mti…ambayo ukichapwa haiwezi kukuletea madhara makubwa sana, zaidi ya maumivu tu mwilini..
Lakini tengeneza picha unapigwa kwa chuma iliyoundwa kwa mfumo wa fimbo..kama vile nondo ngumu..unategemea ni nini kitatokea hapo katika mwili? Sio kusikia tu maumivu lakini pia kuharibika kwa baadhi ya viungo kama vile misuli na mifupa kuvinjika kutatokea. Na kama ukipigwa sehemu mbaya kama vile kichwani..moja kwa moja ni mauti. Kwasababu anayekupiga hana lengo la kukuadhibu bali kukuharibu.
Ndivyo inavyomuonyesha Bwana Yesu, atakapokuja kuwa katika ule utawala wa miaka 1000 hapa duniani.
Kama vile tunavyosoma katika maandiko kuwa yeye ni mchungaji mwema (Yohana 10:14-16)..Ikiwa anamaanisha kuwa Leo hii anatuchunga kondoo wake kwa fimbo ya mti, na ndio maana anapotuadhibu hatuangamii kabisa kwasababu sisi ni kondoo anayetupenda na kututakia mema, anafanya hivyo kwa lengo la kitufanya tu tusitoke katika njia adui akatuangamiza.
Lakini atakapokuja na kutawala kama mfalme wa wafalme biblia inatuambia Amani itatawala duniani kote…kiasi kwamba waovu watakuwepo lakini kwa ule utiisho wake tu, hakuna dhambi yoyote itakayochukua nafasi, kwani adhabu zitakuwa kali kwa watu watakaojaribu kuipindisha amani.
Kwasababu wakati huo atakuwa hachungi kondoo tena kwasababu watakuwa wameshaokolewa, bali atashughulika na mbwa mwitu, hao ndio watapigwa kwa fimbo hiyo kali.
Isaya 65:20 [20]Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.
Hiyo ndio fimbo ya chuma..uovu wala waovu hawatavumilika kwa namna yoyote ile..Vilevile kushindwa kutekeleza maagizo ya ufalme wa Bwana Yesu utakumbana tu na fimbo hiyo ya chuma. Soma (Zekaria 14:17-20).
Kumbuka Jambo hilo atalitekeleza Kristo pamoja na watakatifu wake, wale ambao waliushinda huu ulimwengu wakaenda naye katika unyakuo.
Ufunuo wa Yohana 2:26-27 [26]Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, [27]naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.
Hivyo ni vizuri ukafahamu kuwa Kristo anazo fimbo mbili…Ni heri sasa ukubali kuchungwa naye kwa fimbo ya miti…wakati utafika kabla hata ya utawala wenyewe kuanza…fimbo hiyo ya chuma ataipitisha kwa ulimwengu mzima, kwa yale mapigo atakayoyashusha humu ulimwengu ili kuwaangamiza wote..
Si jambo la kulitamani hata kidogo. Ni heri umpe Kristo maisha yako leo hii ayaokoe, akupe uzima wa milele. Hizi ni nyakati za mwisho. Unyakuo upo mlangoni.
Ikiwa utapenda kupata somo lote la utawala wa miaka 1000 wa Yesu Kristo utakavyokuwa..nitumie ujumbe inbox kwa namba hii +255693036618..nikupe somo lake.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Biblia inasema;
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; 15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo”.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo”.
Mistari hiyo kwa namna nyingine tunaweza kusema; Tukikosa amani, na watu wote, tukikosa utakatifu pia basi tutapungukiwa na neema ya Mungu, na matokeo yake ni kuwa shina la uchungu litachipuka ndani, na kuwasababishia watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
Ni kweli mstari huu unalenga watakatifu wa Mungu..
Tukikosa, mambo hayo mawili, yaani Amani na watu wote, na Utakatifu, kuna uwezekano mkubwa sana wa hili shina la uchungu kuchipuka ndani yetu.
Jiulize kama wewe ni Mtakatifu je, una amani na watu wote? Ikiwa na maana una amani na watakatifu wenzako na watu wengine wa nje?..Ni jambo la kujitahidi sana, hata kama ni gumu ni lazima ujitahidi kama biblia inavyosema, kwasababu ukiukosa tu huo, matokeo yake ni kuwa UCHUNGU uchungu utaanza kuchipuka ndani yako.
Kibiblia Uchungu, ni hali ambayo inakuwa na mchanganyiko wa hasira, kinyongo, wivu, chuki, ghadhabu, na maumivu kwa mtu mwingine.
Na biblia inatuonyesha huwa linaanza kama mbegu, mpaka baadaye linachupuka na kuota mizizi mpaka kuwa shina nene. Na likishafikia hatua hiyo ya kuwa shina, kuliondoa ndani yako ni ngumu sana, litakusumbua kwa muda mrefu kweli, kwasababu tayari limeshakita mizizi kwenye moyo wako.
Hili shina limewasumbua sana wapendwa, hivyo tujitahidi sana tusilipe nafasi mioyoni mwetu..
Mfano mmojawapo katika biblia wa mtu aliyesumbuliwa na shina hili ni Mfalme Sauli.
Lilimwanza pale alipomwacha Mungu, na Mungu kuuhamisha ufalme wake kwenda kwa Daudi. Utaona alipojua hilo alianza kumchukia Daudi kidogo kidogo, badala akatae ile hali, akaendelea kumchukia Daudi kwa kila kitu mpaka baadaye akaonyesha kwa nje sasa yale yaliyokuwa ndani ya moyo wake, akaanza kuweka mikakati ya kumwinda na kumfukuza maporini na majeshi yake ili amuue, bila sababu yoyote. Ikawa ni ngumu tena, kulishinda lile shina la uchungu lililokuwa ndani yake.
Hata alipojaribu kutubu mara ya kwanza na ya pili juu ya jambo hilo la kumwinda Daudi bado alishindwa, kwasababu shina hilo limeshakita mizizi mkubwa ndani yake (1Samweli 24).
Hivyo na sisi, tumeonywa, tujitahidi sana, tena sana tuwe na amani na kila mtu, ni jukumu la kila mtakatifu, kila mshirika, kila mtumishi, si mchungaji, si nabii, si mtume, wote, jukumu hili ni letu, kuwa na amani na watu wote, tusiruhusu chuki, hasira, vinyongo, na wapendwa wenzetu, au ubaya wowote, vilevile na watu wa nje wa kidunia, tusigombane nao.
Kama wewe ni mchungaji, hakikisha huna neno na mshirika yoyote, au mchungaji mwenza, kama wewe ni mtendakazi kanisani, ondoa uadui wa siri na mtendakazi mwenzako, hata kama hakupendezi, jitahidi kwa upande wako uwe na amani na kila mtu kanisani.
Hiyo itatufanya tuwe mahali salama. Tuliepuke hili shina baya la adui mioyoni mwetu.
Yakobo 3:14 “Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. 15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. 16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. 17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki”.
Yakobo 3:14 “Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli.
15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.
16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya.
17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki”.
Waefeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27 wala msimpe Ibilisi nafasi”.
Waefeso 4:26 “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
27 wala msimpe Ibilisi nafasi”.
Shalom.
KIFAHAMU KIGEZO CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.
Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”
TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.
SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.
Tunaishi katika ulimwengu ambao, ukisimama tu kuhubiri, au kukemea dhambi, moja kwa moja utaambiwa UNAHUKUMU, Ukimweleza mtu madhara ya dhambi ya uzinzi kuwa mwisho wake, ni motoni, atakuambia, wewe ni nani mpaka utoe hukumu hiyo.
Wakati Fulani nilizungumza na watu Fulani ambao walikuwa wanatetea dhambi ya ushoga, nikawaambia watu wanaofanya matendo kama hayo, mwisho wao ni jehanamu walinishambulia, kisha wakanipa andiko, lile, ambalo linamzungumzia yule mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, ambapo mafarisayo walimpeleka kwa Yesu, kwa lengo la kumjaribu, kama na yeye ataridhia kupigwa mawe, lakini mambo yakawa tofauti badala ya kuwaruhusu wampige mawe akawaambia, “Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe”. Basi wote wakatawanyika wakamwacha yule mwanamke akiwa na Bwana peke yake.( Yohana 8:1-11)
Hivyo kwa Habari hiyo hawa watu nao wakaniambia, kama wale watu hawakumtupia yule mwanamke mawe, wewe ni nani utuhukumu sisi kwa tunachokifanya, humwogopi Yesu?.
Nikawaambia mimi siwezi kuwatupia ninyi mawe, lakini Yesu mwenyewe atawatupia ninyi mawe, wakati wenu ukifika.
Watu wanadhani Kristo atakuwa katika kiti chake cha rehema milele, kuchukuliana na dhambi zetu,, hawajui kuwa atasimama kama hakimu siku moja kuwahukumu na kuwaadhibu waovu wote,..Wanadhani, Bwana anafurahia uasherati wa mtu, au uzinzi wa mtu, wanadhani alifurahia pia Uzinzi wa yule mwanamke, ndio maana hakufanya chochote.
Nataka nikuambie ikiwa yule mwanamke angeendelea katika uzinzi wake, ni kweli angekwepa mawe ya wanadamu kwa wakati ule, lakini angekutana na mawe ya Kristo siku ile ya hukumu.
Wakati huo hakutakuwa na huruma yoyote katika macho ya Bwana Yesu, haijalishi wewe ni mtoto au mlemavu, au mzee, kama ulikufa katika dhambi, utahukumiwa na kutupwa motoni milele.
Hata kabla ya siku ya hukumu yenyewe kufika, siku ile ambayo atakuwa anarudi katika mawingu kuja kutawala kama mfalme, biblia inasema, ulimwengu mzima utamwombolezea (Ufunuo 1:7).. Na utamwombolezea kwasababu gani, kwasababu ya hayo mapigo atakayokuwa anawamwagia waasi wote katika huuu ulimwengu.
Inatisha sana kwasababu, Bwana Yesu atawaua watu wengi sana, wasiokuwa na idadi. Soma hapa;
Isaya 66:15 “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto. 16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI”.
Isaya 66:15 “Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.
16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI”.
Siku hiyo Wazinzi, mashoga, wafiraji, walevi, washirikina, watatamani milima iwaangukie, ili tu waiepuke hiyo ghadhabu ya Bwana Yesu, lakini haitakuwa hivyo; watashiriki tu mapigo yake.
Ufunuo 6:15 “Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima, 16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo. 17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama”?
Ufunuo 6:15 “Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,
16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.
17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama”?
Ndugu, yangu, huu wakati usitamani ukukute, kwasababu hata baada ya kupokea mapigo hayo makali kutoka kwa Bwana Yesu, bado utasimama katika kiti chake cha hukumu na kutoa hesabu ya mambo yote uliyokuwa unayafanya hapa duniani yasiyompendeza Mungu, na baada ya hapo utatupwa katika lile ziwa la moto uangamie milele na milele.
Tukiyatafakari haya kwa umakini, ndio tutajua ni kwa namna gani Bwana Yesu hapendezwi na dhambi hata kidogo, Kuona leo hii unatoa mimba hafanyi chochote, unatazama picha za ngono, hachukui hatua yoyote, unaiba hakuadhibu, unazini, unalewa, unaabudu sanamu, bado hajishughulishi na wewe..usipumbazike ukadhani, hali hiyo itaendelea hivyo hivyo milele, hata baada ya kufa.
Waebrania 10:31 “Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.
Ni heri ukayasalimisha Maisha yako leo kwa Bwana Yesu maadamu neema ipo, Wakati umekaribia, mambo yatabadilika ghafla, parapanda italia, kisha watakatifu wataondoka..Wewe ambaye utabakia katika huu ulimwengu, ndio utakayekutana na huo upande wa pili wa shilingi wa Bwana Yesu, ni kilio na kusaga meno!. Hutaamini kama huyu ndio yule Bwana aliyekuwa ananililia kila siku niache dhambi kwa sura ya upole, nikawa namdharau. Atakuuwa mwili na roho.
Mathayo 10:28b “… afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”.
Bwana atusaidie sana, ikiwa hujaokoka, embu anza Maisha yako upya na Kristo leo. Tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe katika jina la Bwana Yesu Kristo, ili upokee ondoleo la dhambi zako, na baada ya hapo Bwana atakusaidia. Hatuna muda tena, Yesu anarudi wakati wowote.
Kwa msaada ya kumpokea Yesu, basi wasiliana nasi kwa namba hizi; +255789001312 /+255693036618
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
UNYAKUO.
KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA…TUBU UMGEUKIE MUNGU
UPENDO WA MUNGU.
Imekuwa changamoto kubwa kwa mtu anayeokoka mara ya kwanza, au kwa yule mtu ambaye anahitaji kumwabudu Mungu katika njia sahihi, kutambua kanisa sahihi la kumfanya yeye amwabudu Mungu wake katika Roho na kweli.
Hiyo ni kutokana na kuzuka kwa imani nyingi potofu, na watu wenye nia mbaya, ambao lengo lao ni kuwapoteza watu na sio kuwaokoa.
Hivyo wewe kama mkristo huna budi kuwa mchunguzi sana, na Mungu pia ameruhusu tuwe watu wa namna hiyo sawasawa na (1Timotheo 4:1 )..kwasababu hizi ni zama za uovu.
Lakini pamoja na kwamba kuna makanisa na imani nyingi za uongo ulimwenguni, bado suluhisho sio kukaa nyumbani..kwasababu ni agizo la Bwana kwamba tusiache kukusanyika pamoja na wengine, kumwabudu yeye(Waebrania 10:25)..Na faida zake ni nyingi sana, tofauti na utakavyokwenda mwenyewe mwenyewe, wakati wote. Hata ukutanapo na jiwe katika chakula haikufanya wewe umwage chakula chote..utalitoa lile jiwe utaendelea kula..Vivyo hivyo na katika habari ya makanisa.
Lakini pia kumbuka kujiunga na kanisa sio tiketi ya wewe moja kwa moja kwenda mbinguni..lakini kanisa sahihi lina sehemu kubwa sana ya kukusaidia wewe kufika mbinguni.
Makanisa yanafananishwa na SHULE. Kwamfano mwanafunzi anayehitimu shule ya msingi..akienda sekondari, huwa anakutana na chaguzi nyingi sana za shule zikimwita..na kila shule inajinadi kuwa ina ufauluji mzuri, na mazingira mazuri ya kusomea..
Hivyo ni wajibu wa mwanafunzi mwenyewe kufanya uchunguzi wake mwenyewe je, ni kweli shule hiyo ina vigezo vya kumsaidia kufaulu? .Uchaguzi wa shule mbaya utamweka katika hatari kubwa sana ya kufeli haijalishi atakuwa na akili nyingi kiasi gani.
Lakini pamoja na kwamba shule itakuwa na ubora na ufauluji mzuri, bado bidii ya mwanafunzi mwenyewe binafsi inahitajika..
Hivyo vyote viwili vinasaidiana na vina umuhimu, na vinakwenda sambamba. Tengeneza picha mwanafunzi anayesema mimi siendi shule..nitatafuta tu namba yangu ya mtihani wa mwisho siku hiyo ikifika nikafanye.. nitakuwa najisomea peke yangu nyumbani kwa miaka yote hiyo.. Jiulize mwanafunzi kama huyo atafaulu kweli..lengo la shule kuwekwa ni kumsaidia mwanafunzi ufauluji wake, kwa kukutanishwa na waalimu wa kumsaidia na kumpa nidhamu ya usomaji bila kuvutwa na mambo mengine..
Halikadhalika ukristo na kanisa ni vitu vinavyokwenda sambamba, na ni wajibu wako kuchagua kanisa sahihi litakalokusaidia kufanikisha safari yako ya wokovu hapa duniani.
Mpaka hapo naamini umepata picha..hivyo vifuatavyo ni vigezo muhimu sana vya kuukusaidia kutambua kanisa sahihi ni lipi
1) YESU KRISTO ndio kiini cha imani hiyo.
Tunapouzungumzia ukristo, tunamzungumzia Yesu Kristo, kanisa lisilomfanya Kristo peke yake ndio msingi wa imani hiyo. Ni kanisa la uongo. Ukiona halimtaji Kristo kwa kila kitu..Kimbia hilo kanisa..ikiwa jina la nabii au kiongozi ndio linatamkwa na kupewa heshima kubwa kuliko Kristo..ondoka haraka sana hapo..
Vilevile ukiona Bwana Yesu analinganishwa na watakatifu wengine, kana kwamba na wenyewe ni wapatanishi wa dhambi zetu kama yeye..mfano wa Yosefu na Maria. Ondoka pia hapo, haijalishi litakuwa na wafuasi wengi au zuri kiasi gani.
Wakolosai 2:18-19 [18]Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili; [19]wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua Kwa maongeo yatokayo kwa Mungu.
2) Pili, kanisa la kweli Linaamini Biblia Takatifu tu ndio mwongozo wake.
Ni lazima liamini Biblia yenye vitabu 66, na si zaidi wala pungufu..yapo madhehebu ambayo yameongeza vitabu vya Apokrifa katika biblia na kuifanya iwe na vitabu 73.
Ukiona dhehebu hili ondoka hapo, vitabu vyovyote nje ya vile vinavyojulikana yaani 66 havijaviviwa Roho Mtakatifu.
Ufunuo wa Yohana 22:18 [18]Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
Halikadhalika yapo mengine yanaamini katika mapokeo, kama vile waaminivyo bibila takatifu hayo pia yakimbie ni upotevu na udanganyifu mwingi upo ndani yake.
Utapotezwa tu..
3) Tatu linafundisha mafundisho yanayolenga ufalme wa mbinguni.
Yohana mbatizaji alipoanza kuhubiri alisema tubu kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia..Bwana Yesu naye alihubiri kwa kusema tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia(Mathayo 3:2, 4:17)…mitume nao walihubiri na kufundisha vivyo hivyo.
Nasi pia tujue ukristo, ni habari za ufalme wa mbinguni na sio ufalme wa duniani..Ikiwa utakuwepo mahali unafundishwa na kushinikizwa tu juu ya mambo ya ulimwenguni wakati wote..yaani mali, na vitu vya ulimwenguni..hiyo ni ishara kuwa kanisa hilo ni la uongo..hivyo ondoka hapo.
Ndio zipo nyakati, hayo nayo yatafundishwa katika kanisa lakini sehemu yao iwe ndogo sana, yasiwe kiini cha mtu kuwepo kanisani kumwabudu Mungu. Kanisa ni habari za ulimwengu ujao.
4) Utakatifu na Upendo:
Huu nao ni msingi mwingine wa kanisa hai la Kristo, kufundishwa utakatifu na Upendo ambavyo vyote viwili ndio vinatajwa kama malango ya kumuona Mungu sawasawa na (Waebrania 12:14, na 1Yohana 4:7-8 ).
Kanisa ambalo, watu wake wanamwabudu Mungu watakavyo, wanawake na vijana wanavaa hohe hahe, wanaenda kanisani kama vile disco na hawaambiwi chochote, hawakemewi dhambi, hawaonywi..hilo sio kanisa hai.
5) Karama za Roho:
Alipo Roho Mtakatifu, atadhihirisha na uwepo wake pia, kama kanisa haliruhusu karama kama za uponyaji wa Roho, unabii, uinjilisti, lugha, maombi n.k. ni dalili kuwa hilo sio kanisa la Kristo.
Yapo ambayo yanaamini lakini hayahimizi, haya yanaweza yasiwe na shida..lakini yapo ambayo hayaamini kabisa kiasi kwamba lolote likitokea waweza fukuzwa kanisani..haya ndio uyakimbie, kabisa kwasababu yatakuua kiroho, ushindwe kumtumikia Mungu kwa karama aliyoiweka ndani yako.
1 Wakorintho 12:7-11 [7]Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. [8]Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; [9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; [10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; [11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
Hivyo kwa vigezo hivyo, naamini utakuwa umepata mwanga wa kujua kanisa la kweli ni lipi.
Hivyo chukulia kwa uzito suala hili, lipime kanisa lako, kwasababu wengi wameshafungwa katika kamba za makanisa ya uongo na bado wanaendelea nayo..Usiogope kutoka kwasababu atakayehukumiwa ni wewe sio hilo dhehebu.
Nikitakie uchaguzi mwema.
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.
Biblia inamfananisha Bwana wetu Yesu Kristo na Melkizedeki kuhani wa Mungu aliye hai.. Na hiyo yote ni Kutokana na jinsi alivyofanana na Kristo kwa kila tabia aliyokuwa nayo.
Waebrania 7:1-3 [1]Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki; [2]ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani; [3]hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Waebrania 7:1-3 [1]Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;
[2]ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;
[3]hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.
Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia utajiuliza ni kwanini siku ile Ibrahimu alipotoka kumwokoa ndugu yake Lutu ambaye alikuwa tayari ameshatekwa na maadui, Melkizedeki hakumpa zawadi nyingine zaidi ya MKATE NA DIVAI..
Jiulize ni kwanini iwe mkate na Divai, na ni kwanini uwe ni wakati ule? Na si mwingine..kwanini Melkizedeki asingempa Dhahabu na Lulu kama pongezi, au kwanini asingempa kondoo na mbuzi kama zawadi kwake..badala yake anampa divai na makate, kitu kidogo tu.. kuna nini?
Mwanzo 14:17-20 [17]Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. [18]Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. [19]Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi. [20]Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.
Kama tulivyotangulia kuona kuwa Melkizedeki anafananishwa na Yesu Kristo kwa kila kitu..Habari hiyo inajirudia kwa Kristo alipokuwa anaondoka duniani..
Hakuwaacha hivi hivi tu mitume wake, bali aliwapa uzima wake kwa mfano wa mkate na divai akasema huu ndio mwili wangu na damu yangu imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi, kuleni huu, na nyweni hii kwa ukumbusho wangu na kutangaza mauti yake inayowaokoa watu (Mathayo 26:28)
Sasa tarajio lake kubwa ni kutuona sisi tunashiriki ipasavyo..anatarajia kutuona tupo katika mazingira kama ya Ibrahimu..ambaye yeye hakuona vema kukaa tu hivi hivi angali ndugu yake Lutu amechukuliwa mateka..aliamua kutoka aende kumkomboa, kutoka mikononi mwa wale wafalme wa mbali.
Na ndipo Mungu alipouona moyo huo wa Ibrahimu akaona anastahili kushiriki mwili na damu ya Yesu Kristo.
Lakini je! Tujiulize na sisi tangu tulipoanza kwenda makanisani, na kushiriki meza ya Bwana mara zote hizo..Je! Ni ushuhuda gani Kristo anauona ndani yetu aone kwamba tumestahili kuishiriki meza yake.
Kila tendo la rohoni lina kanuni yake.. Ili ule uzima ambao Bwana Yesu alisema utaingia ndani yetu pale tu tunaposhiriki meza yake, uingie, ni lazima tujue kanuni zake vinginevyo tutakuwa tunafanya kazi bure tu.
Yohana 6:53-54 [53]Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. [54]Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Hivyo, tukumbuke hilo pia tukaribiapo nyumbani kwa Bwana anatazamia tuwaangazie na wengine nuru yetu ya wokovu tuliyoipokea..Ndipo tustahili vema kushiriki meza yake. Lakini kama tutakuwa ni watu wa kuingia kanisani na kutoka, baada ya hapo hatuna habari tena na Mungu. Ni heri tuache tu.
Bwana atasaidie katika hilo.
MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.
Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?
Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?
WhatsApp
SWALI: BWANA YESU asifiwe mtumishi, mistari hii inanichanganya nisielewe vizuri, Neno la Mungu linasema;
Hesabu 23:19 Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?
Hapa biblia inasema hasemi uongo Wala hajuti, lakini ukisoma tena hapa inasema
1 Samweli 15:11 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha.
Nashindwa kuutambua ukweli Ni upi?
JIBU: Ukweli ni kwamba Mungu HAJUTI..Isipokuwa kuna wakati anajiweka katika mazingira ya kibinadamu ili tuzielewe hisia zake vema.
Na ndio maana mahali pengine utaona anazionyesha kazi zake kama vile zinamapungufu fulani, hazijakamilika..mpaka anatumia neno SI VEMA huyu mtu aishi peke yake nitamfanyia msaidizi, kana kwamba hakuliona hilo tangu mwanzo, lakini ukisoma mwanzoni kabisa katika kitabu cha Mwanzo 1:27 inatuambia tayati alishamuumba mwanaume na mwanamke katika mawazo yake..lakini katika utekelezaji anajifanya kama kasahau, ndio hapo anakuja kumuumba mwanamke baadaye sana baada ya uumbaji wote kukamilika Mwanzo 2:8..
Hiyo ndio tabia ya Mungu. Anajiweka hivyo wakati mwingine ili kutufundisha sisi jambo.
Mara nyingine anajifanya kama hana mashauri bora ya kumzidi mwanadamu..utakumbuka kule jangwani Musa alimshauri Mungu aghahiri mawazo yake..lakini haimaanishi kuwa Mashauri yetu ni zaidi ya Mungu. Soma Kutoka 32:9-14
Halikadhalika hapa..anasema..yeye si mwanadamu hata ajute..ikiwa na maana mipango yake yote tayari alishaiona mwisho wake utakuwaje tangu mwanzo..kwamba huu utaishia katika uzuri au huu utaishia pabaya..kwamfano alipomuumba shetani, alijua kabisa ataasi, na atawapoteza malaika na wanadamu wengi..lakini akamuumba hivyo hivyo..
Hata sasa Mungu anajua kabisa mwisho wa kila mwanadamu na kila jambo..kwamfano katika habari hiyo ya Sauli..Mungu alijua atakuja kukengeuka huko mbeleni..lakini alimpa bado ufalme..
Na alipokuja kukengeuka kweli, ndio tunaona Mungu anamwambia Samweli najuta kwanini nimechagua Sauli awe mfalme..kuonyesha tu hisia zake juu ya Sauli ili sisi wanadamu tumuelewe. Lakini alifahamu kila kitu.
Halikadhalika hata sasa mambo kama hayo Mungu anayafanya rohoni, .Mungu kukusifia leo haimaanishi kuwa ndio tiketi ya mbinguni moja kwa moja…Mungu kukutia mafuta sasa na kuwaacha wengine, haimaanishi kuwa wewe ndio kipendwa cha Bwana, hata ukifanya dhambi atakusitiri tu siku ile kisa ni kuhani wake.
Ukweli ni kwamba wapo watu ambao wataishia kuwa manabii wa uongo, wengine wapinga-kristo, na jehanamu wataenda..lakini ushuhuda wa wito watakuambia ni Yesu mwenyewe alinitokea na kunituma..Akanipa na ishara za miujiza, lakini wanaishia motoni
Mathayo 7:21-23 [21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. [22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? [23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Swali ni je…umempa Kristo maisha yako na kusimama kweli kweli? Unahabari kuwa Karama pekee sio uthibitisho kuwa Mungu yupo na wewe? Wakati wowote anaweza kujutia na kughahiri huo wito wako, aliokupa kama unasua sua
Kama hujasimama imara, fanya hivyo sasa. Mgeukie muumba wako kwa kumaanisha kwasababu, kumbuka hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi
Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)
THAWABU YA UAMINIFU.
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
JE! NA SISI NI SHABA ILIAYO NA UPATU UVUMAO?
Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.