Kuna njia kuu sita(6)
Ni vema ukazifahamu hizi njia Mungu anazozungumza na watu, ili usitegemee tu njia moja uifahamuyo wewe, matokeo yake ukakosa shabaha ya kuzisikia sauti za Mungu kila siku maishani mwako zinapozungumza na wewe.
Hii ni Aidha kwa Sauti, ndoto, au maono,
Ni mojawapo ya njia ambayo Mungu anazungumza na watu. Na ndio inayojulikana na kutegemewa na wengi.
Ayubu 33:14-15
[14]Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. [15]Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;
Katika maisha yetu kwa namna moja au nyingine Mungu alishazungumza nasi kwa njia hii. Unaweza usione, maono au usisikie sauti lakini kila mtu huwa anaota. Na kwa njia hiyo Mungu huzungumza.
Hii ndio sauti ya Mungu namba moja ambayo inazungumza na mtu moja kwa moja na kwa wakati wote..ni sauti ambayo hailinganishwi na sauti nyingine zozote.
Ukiwa ni msomaji mzuri wa Neno, utamsikia Mungu katika nyanja zote za Maisha akikufariji, akikuonya, akikushauri, akikuongoza n.k. Ni pakeji iliyojitosheleza., ambayo hailinganishwi na njia nyingine yoyote.
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”
Ikiwa wewe umeokoka, na umejazwa Roho Mtakatifu, basi ujue mara nyingi sana Mungu atatumia amani yake moyoni mwako kuamua mambo mengi..
Na ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 10:11-13
[11]Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. [12]Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni. [13]Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.
[11]Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. [12]Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.
[13]Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.
Wakolosai 3:15a “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu;..”
Kuonyesha kuwa amani itokayo kwa Roho ni sauti ya Mungu kutuongoza, ikiwa umepoteza amani ghafla katika mazingira fulani kuwa makini sana hapo. Wakati mwingine ni Mungu anazungumza.
Hapa anaweza akachagua aidha apitie mtu mwovu au mtu mwema. Mara nyingi sana Mungu anazungumza na watu kupitia watumishi wake, yaani wahubiri, waalimu, wainjilisti n.k.
Yeremia 25:4
[4]Naye BWANA ametuma kwenu watumishi wake wote, hao manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini ninyi hamkusikiliza, wala hamkutega masikio yenu, msikilize.
Na mara nyingine tena anaweza kutumia watu wa kidunia kukuonya..kama vile maaskari, wakuu wa hii dunia n.k.
Hivyo ni kuzingatia sana unachokisikia au kufundishwa au kuonywa na watu, hususani watumishi wa Mungu..Mara nyingine sauti ya Mungu ipo nyuma yao.
Mazingira yanaweza yakawa ya kimaisha, au ya kihali…kwa mfano Mungu akitaka uelewe jambo fulani, wakati mwingine hatumii sauti ya moja kwa moja, kwasababu pengine unaweza kulichukulia juu juu tu au usimwelewe, hivyo atakupitisha katika maisha fulani au mazingira fulani, na kwa kupitia hayo utajua kabisa hapo ni Mungu alikuwa akisema na wewe.
Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Nebukadreza, yeye alionywa na Mungu, awe mnyenyekevu na amche Mungu, lakini hakusikia, kinyume chake akapuuzia ule unabii aliopewa na Danieli. Matokeo yake baada ya miezi 12, akageuzwa kuwa kama mnyama, akawa anaishi huko misituni akila majani kama ng’ombe..mpaka siku alipoelewa somo kuwa aliye juu ndiye anayetawala falme zote za duniani. Ndipo akajinyenyekeza ,hivyo Mungu akamrudishia ufalme wote wa dunia. (Danieli 4)
Sauti ya Mungu imejificha sana katika vitu vinavyotuzunguka na asili, kiasi kwamba tungefahamu vema basi tusingekuwa na ugumu wa kumwelewa Mungu.
Embu fikiri Bwana Yesu alivyotuambia..tafakarini Kunguru?..hawapandi hawavuni wala hawana maghala ya chakula lakini wanakula..Je sisi si mara nyingi zaidi ya hao? (Luka 12:24)
Hili ni neno ambalo lilikwepo tangu enzi na enzi kiasi kwamba watu wangekuwa wanalitafakari kabla hata ya Yesu, wasingekuwa na hofu ya maisha pale wanapotaka msaada kutoka kwa Mungu.
Vivyo hivyo utazamapo, bahari, milima, miti, zipo sauti nyingi sana za Mungu nyuma yake .. Chukua muda mwingi kutafakari, utaisikia sauti ya Mungu waziwazi.
Mungu alimwambia Ibrahimu angalia juu tazama nyota za mbinguni na mchanga wa baharini upate imani kwangu.
Hivyo ni vizuri ukapata maarifa haya usije ukaangamia kwa kutomwelewa Mungu. Leo hii watu wanategemea njia moja tu..ile ya moja kwa moja..yaani kusikia sauti, au kuona maono au kuota ndoto. Na kusahau hizi nyingine.. Ndio hapo utasikia wakisema nimeomba sana, nimelia sana Mungu aseme na nini, lakini sijawahi kumsikia.
Ni kwanini? Nikwasababu wanalazimishia njia hiyo hiyo moja Mungu aseme nao..
Hawajui kuwa Mungu hapangiwi fomula ya kuzungumza.Hivyo wewe uombapo..kuwa mtulivu, soma sana Neno mtafakari Mungu..subiri azungumze kwa jinsi apendavyo yeye. Atakujibu tu aidha kwa Neno lake, au mtumishi wake, au amani moyoni mwako, au kwa kutazama mambo ya asili, ukiona hivyo basi ujue ni Mungu huyo.
Hivyo kaa katika utulivu wa Roho, zingatia kusoma Neno..kwasababu maarifa kama haya utayapata katika biblia na sio kwa kuota au kuona maono.
Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.
MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.
MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?
Unyenyekevu ni nini?
ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: Naomba kufahamu maombolezo ya Hadadrimoni tunayoyasoma katika Zekaria 12:11 ni maombolezo gani hayo?
Zekaria 12:11 “Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido”.
JIBU: Hadadrimoni ni eneo lililokuwa sehemu ya bonde lijulikanalo kama Megido huko Israeli. Bonde hili lilisifika kwa vita, na Zaidi sana kuuawa kwa baadhi ya viongozi wakubwa. Hivyo kupelekea maombolezo makubwa sana kwa watu waliouliwa viongozi wao.
Mfano katika Habari hii, inamlenga mfalme Yosia, ambaye ndiye aliyekuwa tumaini la mwisho la Taifa la Israeli. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka, Yosia alikuwa mfalme aliyemcha Mungu sana kuliko wafalme wote wa Israeli,tukimwondoa Daudi, na yeye ndiye aliyefanikiwa kuondoa sanamu zote Israeli kipindi kile, Na ndiye mfalme ambaye kuzaliwa kwake kulitabiriwa miaka mingi sana kabla hajazaliwa.
Hivyo waisraeli walimwona kama ndiye tumaini pekee waliobakiwa nalo.
Lakini siku moja alitoka kwenda kupigana vita na mfalme wa Misri aliyeitwa Neko. Na kinyume na matazamio yake, aliuliwa, na mahali alipouliwa palikuwa ni hapo Hadadrimoni katika bonde la Megido.
Israeli nzima iliposikia, ilimwombolezea maombolezo makubwa sana, taa ya Israeli kuzima ghafla, mpaka wakamwekea kumbukumbuku lake la kila mwaka akumbukwe.
2Wafalme 23:29 “Katika siku zake, Farao-neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana na mfalme wa Ashuru, akafika mto Frati; naye mfalme Yosia akaenda kupigana naye; naye mfalme wa Misri akamwua huko Megido, hapo alipoonana naye”.
2Nyakati 35:25 “Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo”.
Hivyo Mungu akatumia kivuli hicho kueleza jinsi taifa la Israeli litakavyokuja kuomboleza huko mbeleni, siku watakapopewa neema ya kumtambua Kristo. Biblia inasema wayahudi watamwombolezea Yesu waliyemchoma, watalia kama vile mtu aliyefiwa na mwana wake wa pekee, mfano wa pigo la wamisri la kuuliwa wazaliwa wao wa kwanza, jinsi walivyokuwa na maombolezo makuu.
Kama vile, maombolezo ya Yosia katika bonde la Hadadrimoni, Waisraeli walivyombolezea mfalme wao, kwa uchungu mwingi, ndivyo itakavyokuwa siku hiyo watakapomwagiwa neema ya kumtambua Kristo..
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, KAMA MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI KATIKA BONDE LA MEGIDO. 12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, KAMA MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI KATIKA BONDE LA MEGIDO.
12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;
13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.
14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.
Ndugu, Kipindi si kirefu hii neema inayochezewa leo hii, itageuka na kuwarudia wayahudi. Kipindi hicho unyakuo utakuwa umeshapita, na Roho Mtakatifu hayupo tena kwetu sisi watu wa mataifa, bali kwa watu wake Israeli. Dunia itastaajabia, kuona watu hawa wametolea wapi moyo huo wa kujuta kwa ajili ya Yesu ambaye leo hii wanamkataa.
Kwani wayahudi hawa wakati huo, biblia inasema watajitenga, familia kwa familia, ukoo kwa ukoo, kila moja atakuwa na maombolezo yake makuu sana haradharani na sirini, kudhihirisha kazi ya Roho Mtakatifu juu yao. Sasa wakati huo ndio Mungu atakuwa anawaandaa ili kuwarudishia ufalme ambao waliutazamia kutoka kwa masihi wao, sawasawa na lile ulizo la mitume (Matendo 1:6)
Ndugu, ukishaona mabadiliko haya kwa wayahudi, ujue umeshaachwa katika unyakuo, vilevile hii dunia itakuwa na kipindi kifupi sana kisichozidi miaka 7 hadi iishe. Leo hii tumeshaona Israeli imekuwa taifa, wote wamesharudi kwao. Unadhani wanachosubiria ni nini kama sio kurudiwa wakati wowote.
Bwana Yesu alisema,
Mathayo 24:32 “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu”;
Mtini unawakilisha taifa la Israeli (Yer 24), Hivyo tuonapo Israeli leo hii inachipuka, tujue kuwa wakati wa mavuno umeshafika.
Je!, unalitambua hilo? Bado unaipuuzia hii neema ambayo hatuna nayo muda mrefu?. Una Habari kuwa unyakuo ni wakati wowote, na hatua zake tayari zimeshaanza?. Wakati tulionao sasa si wakati wa kubembelezewa wokovu, Injili imeshazagaa kila mahali, watu wote wameshasikia, ni wakati wa kujitakasa, wewe ambaye tayari umeshaokoka. Lakini kama bado upo nje ya neema kipindi hichi? Utakuwa ni wa ajabu kweli.
Unasubiria siku Fulani, neema ikufikie? wakati neema ya wokovu ipo tayari kila mahali, unasubiria ikufikieje tena? Tambua kuwa njia imeshasonga, na wengi wanatamani waingie wanashindwa, kwasababu upotofu mwingi upo duniani, na wewe bado tu unaisubiri.. Ni kuwa makini sana. Neema inakimbilia Israeli sasa, jicho la Bwana linaelekea kule sasa, kwani muda wetu umeshakwisha.
Bwana atusaidie.
SIKU YA TAABU YA YAKOBO.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.
Uru wa Ukaldayo ni nini?
SWALI: Shalom… Pastor naomba kuuliza je ni sahihi mtumishi kuongoza kanisa hajafunga ndoa? na anaweza kubatiza washirika? Amina.
JIBU: Kigezo cha mtu kuwa Kiongozi wa kanisa, na kufanya kazi zote za madhabahuni, ikiwemo kubatiza, kuwawekea watu mikono ya utumishi, n.k. vimetolewa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7
1 Timotheo 3 : 1-16
1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;
3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;
5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa, Hivyo yeyote anayelichunga kanisa, awe ni mchungaji, mwalimu, Mtume, maana yeye ndio mwangalizi basi vigezo hivyo vinamuhusu.
Lakini katika vigezo hivyo vyote, hakuna hata kimoja, kinachosema, ni lazima aoe.. Isipokuwa anasema Askofu ni lazima awe ni mume wa mke mmoja..Akiwa na maana kwamba ikiwa ni mwana-ndoa basi, anapaswa awe ni mume wa mke mmoja, na si Zaidi, kama anao wake wawili au watatu, tayari ameshakidhi vigezo vya kutostahili kuitwa mchungaji.
Lakini ikiwa ni mtu ambaye, hajaoa lakini ameshika vigezo vyote, hivyo, yaani, ni mtu asiyelaumika, si mlevi, mpole, si mpenda fedha, aliyeshuhudiwa na watu ni mwema, amekomaa kiroho. Basi huyo anavigezo vyote vya kuwa mchungaji, au kiongozi yoyote wa kanisa.
Mtume Paulo hakuwa ameoa, lakini alikuwa ni mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia, na mataifa mengine, Na Zaidi sana yeye ndiye aliyetoa mwongozi wa mafundisho ya ndoa.
Hivyo kuoa/ kutokuoa, si takwa, la kuwa askofu.
Kinyume chake mtume Paulo,alishauri watu wote wawe kama yeye (yaani wasioe), kwasababu watu wasiooa inawapa wigo mpana wa kumtumikia Mungu bila kuvutwa na mambo mengine, ikiwa wamemaanisha kweli kujikita kwa Bwana.
1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.
1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.
Lakini ikiwa huwezi kuishi Maisha hivyo, kwa jinsi ulivyoitwa, basi hakikisha unatumika kiuaminifu, hapo utakuwa umekidhi vigezo vya kulichunga kundi , kubatiza, n.k.
Shalom.
Ndoa na Talaka
Ndoa ya serikali ni halali?
Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?
Uvuvi bora hauchagui wa kuvua.
Askofu na mchungaji mkuu ni nani?
WANA-NDOA: Baba Mkwe, Na mama Mkwe.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetus Yesu Kristo, sifa na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.
Unafahamu kuwa shetani ambaye ni adui yetu, si kila wakati anafanya mambo yake kwa kutegemea jitihada zake tu, anajua kabisa mambo mengine huwa hayatoki isipokuwa kwa kufuata kanuni ambazo tayari Mungu alishaziweka.
Na huwa anazitumia hizo kanuni, kutuharibu sana, lakini sisi kama wana wa ufalme, hatuzitumii kumuharibu yeye.
Kwamfano madhara aliyopanga kumletea Ayubu, alitambua kuwa haiwezekani kwa njia ya kawaida kuyatekeleza ,. Ndipo akatumia njia ya juu Zaidi ya kujishusha, kwa kwenda KUJIHUDHURISHA mbele za Mungu,.
Akashusha kiburi chake hadi chini kabisa, akaungana na Malaika watakatifu wa Mungu, kupanda mbinguni, akaenda mbele ya uwepo wa Mungu, kwa unyenyekevu wote, akitumaini kuwa kwa kutenda kule, ni lazima tu Mungu atamwangalia, kwasababu Mungu ni Mungu wa uumbaji wote.
Na kweli baadaye Mungu alipomwona anatembea tembea mbele ya uwepo wake kwa muda mrefu, akaanzisha mazungumzo naye, Akamuuliza unatoka wapi shetani, akasema duniani, katika mizunguko yangu, ndipo shetani akatumia fursa hiyo ya mazungumzo, kupeleka na mashataka yake yote. Na mwisho wa siku akapatiwa haja yake.
Akashuka chini, akamfanya Ayubu kama alivyoweza kumfanya..
Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. 7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. 8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”.
Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu”.
Tunachopaswa tujue ni nini, Ikiwa mungu wa dunia hii, anajua siri ya mafanikio ya uharibifu wake, haitegemei tu nguvu zake mwenyewe, bali pia kwa kujihudhurisha mbele za Mungu ..Unategemea vipi wewe na mimi tusiwe watu wa namna hiyo?
Shetani anatushangaa sana, tunapomkimbia Mungu, anatushangaa sana tunapokwenda mbali na uwepo wa Mungu, kwa visingizio visivyokuwa na maana, hatutaki kwenda kumfanyia Mungu ibada hata mara moja kwa wiki tunasema tumechoka, kwasababu jumatatu tunakwenda kazini hivyo hatuna budi tulale!! Ndugu ukitegemea nguvu zako kuyaongoza haya Maisha jihesabie tu wewe ni MKIA Maisha yako yote. Ndivyo ilivyo..
Hilo shetani alijaribu akaona halifai, na wewe unalijaribu, alijua si kila wakati nitajiamulia tu mimi mwenyewe, kwa nguvu zangu..Lazima niwe na muda wangu wa kwenda kujinyenyekeza, tena kwa muda mrefu mbele za Mungu.
Ikiwa tunaona mikesha ni shida, hata mara moja kwa mwezi, tusahau Mungu kuanzisha mazungumzo yoyote na sisi. Ikiwa hatujizoezi kusali mara kwa mara, na kuutafuta uso wa Mungu hata kwa mifungo wakati mwingine, tujue tu mambo mengi sana tutafeli kuyatimiza maishani mwetu.
Faida za kujihudhurisha mbele za Bwana ni zipi?.
Tunapokuwa uweponi mwa Bwana muda mrefu, Mungu mwenyewe ataanzisha mazungumzo na sisi, atatuuliza, unasumbukia nini, una haja gani, unatafuta nini? Kama tu alivyofanya kwa shetani…Lakini akitutazama hatupo uweponi mwake, Tunazunguka zunguka tu duniani, na masumbufu ya Maisha haya kila wakati, siku saba kwa juma, siku 365 za mwaka, na yeye ataendelea na mambo yake, atatuacha tutaabike wenyewe..
Biblia inasema..
Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi..”
Ndugu tujizoezi, kumkaribia Mungu kila siku, ibada inayotoka rohoni iwe ni sehemu ya Maisha yetu, Na bila shaka tutaanza kumuona Mungu akisema na roho zetu.
Kumbuka uanzapo kufanya mambo kama hayo kwa bidii, hutasikia sauti kama sauti ikisema na wewe, bali rohoni Mungu atakuwa anazungumza na Maisha yako. Na mara utaona yote uliyokuwa unamwomba, au unayatamani yatendeke tangu zamani, Mungu anakufanikisha kwa njia ambazo hujazitazamia. Hivyo ndivyo Mungu anavyozungumza na watu.
Tukiijua kanuni hii, shetani atatuchukia sana, kwasababu tutakuwa tumeshajua siri ya mafanikio yetu, kama yalivyokuwa yake katika huu ulimwengu.
Kama wewe ni mtakatifu, anza sasa kumpa Mungu muda wako wa kutosha, huko ndiko kujihudhurisha mbele zake, usiwe na udhuru wa kutokwenda ibadani, usiwe na udhuru wa kutohudhuria mikesha na wenzako, usiwe na udhuru wa kutokufunga na kuomba, na kujifunza Neno kila siku. JIHUDHURISHE kwa kadiri uwezavyo mbele za Mungu.
Ndivyo Mungu atakavyoanzisha mazungumzo na wewe.
Ikiwa bado upo nje ya Kristo, kumbuka kuwa, hatuna muda mrefu hapa duniani, Unyakuo ni wakati wowote, kulingana na kutimia kwa dalili zote zilizotabiriwa katika maandiko, na kama hilo halitoshi fahamu kuwa mlango wa neema, umeshaanza kufungwa, usipoiamini injili, leo, kesho itakuwa ni ngumu Zaidi, na siku moja hutaiamini kabisa. Kwasababu neema haidumu milele, maandiko yanasema hivyo!.
Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha leo, mgeukie Kristo, injili tuliyobakiwa nayo sasa sio ya kubembelezwa, ni wewe mwenyewe uone hali halisi, umgeukie muumba wako.
Maran Atha.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
“Vya Kaisari mpeni kaisari” ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.
JIBU: Tukumbuke kuwa “sala ya Toba” sio wokovu, Sala ya toba ni njia mojawapo, inayotumiwa kuukaribisha wokovu ndani ya mtu, lakini sala kama sala yenyewe sio wokovu, Ikiwa na maana zipo njia nyingine, Na ndio maana huwezi kuona mahali popote mitume waliwaambia watu wafuatisha sala fulani, kwamba kwa hiyo ndio wataokoka..Huwezi kuona.
Wokovu unatoka moyoni. Pale mtu anapojitambua kuwa ni mwenye dhambi, na hivyo anahitaji kukombolewa kutoka katika mauti na Yesu Kristo, kitendo kinachompelekea kuyasalimisha maisha yake yote kwa Bwana Yesu ayaongoze, na kuachana na mambo ya ulimwengu, Huo ndio wokovu.
Sasa jambo kama hili likishatokea ndani ya mtu, udhihirisho wa nje ndio unafuata, ambao mojawapo ndio kukiri kwa kinywa chako, na cha pili ni Matendo yako.
Kutimiza lile andiko la Warumi 10:9
“Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka”.
Sasa mabubu, hawajajaliwa kuongea, hawawezi kumkiri Kristo kwa vinywa vyao..Lakini wanaweza kuonyesha kuwa wamemwanini Kristo kwa matendo yao. Wakifanya hivyo tayari huo ni wokovu tosha, kutoka kwa Bwana.. Hivyo mtu kama huyu ikiwa tayari ameshamwani Bwana muhimize tu, aanze kuenenda sawasawa na kuamini kwake.
Tutakumbuka kisa kile cha Yule mwanamke ambaye Bwana Yesu alisema alikuwa na dhambi nyingi, jinsi alivyomwendea na kulia sana miguuni pake, kudhihirisha majuto ya makosa yake, kisha kumpangusa kwa nywele zake, Utaona pale Bwana Yesu hakuzungumza naye maneno yoyote, kwamba njoo nikuongoze sala ya toba, au sema maneno haya au yale, hapana isipokuwa alipoona tu moyo wake wa toba ulivyomaanisha kwelikweli alimwambia.. “Mwanamke umesamehewa dhambi zako”
Luka 7:36-48
“36 Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani. 37 Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu. 38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu. 39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi….. 44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake 45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu. 46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu. 47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo. 48 Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.
“36 Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.
37 Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.
38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.
39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi…..
44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake
45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.
46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.
47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.
48 Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.
Hii kuonyesha kwamba, pale unaoonyesha geuko la kweli moyoni mwako, kabla hata hujazungumza chochote tayari umeshasamehewa.
Ndivyo ilivyo kwa mabubu, haijalishi hawataweza kukiri sala yoyote kwa vinywa vyao, lakini ikiwa moyoni mwao wameonyesha mabadiliko, hicho ndicho Mungu anachokitaka. Imekuwa desturi leo hii kuona kundi kubwa la watu wanasema wameongozwa sala ya toba na kumkiri Yesu , lakini ukitazama matendo yao hayaendani na walichokikiri. Huo ni unafki ambao unamchukiza Bwana sana.
Mathayo 15:7 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, 8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.
Mathayo 15:7 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,
8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.
Bwana anataka tumfuata na tumwabudu katika Roho na kweli. Na sio katika maneno matupu. Ikiwa mtu asiweza kuongea, amesimama katika wokovu, huyo mtu ni wa thamani sana mbele za Mungu
Swali ni je wewe, uliyemkiri Bwana, unayemsifu, unayemuhubiri, unayemtangaza. Je! Ni kweli kitokacho mdomoni mwako, kimeambatana na badiliko la ndani?
Majibu tunayo.
Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).
Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate. Ina maana gani?
Kuongozwa sala ya toba.
Dusumali ni nini katika biblia?
Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)
Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?
Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?
WhatsApp
SWALI 1: Je! Shetani anaweza kuumba, kama Mungu? Kama sio Mbona kipindi cha Farao, tunaona wale waganga waliweza kuleta vyura na nyoka, kama alivyofanya Musa. Je wale vyura aliwaumbaje, uhai alitolea wapi kama sio Mungu?
JIBU: Bwana Yesu anasema; Shetani ni mwongo, na sio tu mwongo, bali ni Baba wa huo;
Yohana 8:44 “..wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.
Maana yake ni kwamba ufalme wake ameujenga juu ya misingi ya uongo. Alitumia uongo kumnyang’anya Adamu nafasi yake ya umiliki. Vivyo hivyo hadi sasa anatumia uongo kuwadanganya watu wasiutambue ukweli wote kuhusu yeye.
Anataka kuwadanganya watu, wadhani kuwa yeye ana nguvu za kuweza kukaribiana hata na Mungu au anao uwezo wa kuumba kama Mungu. Lakini ukweli ni kwamba, shetani au kiumbe chochote kile hakiwezi kuumba hata sisimizi. Uwezo huo anao Mungu tu, peke yake.
Alichokifanya kipindi cha Farao, si kingine zaidi ya uongo. Kutokana na maarifa aliyokuwa nayo kipindi kile ambayo anayo hadi sasa, shetani anaweza kubaliki kitu fulani kionekane ni kitu kingine mbele tu ya macho ya watu, au hata kujibadilisha yeye, aonekane ni malaika wa kweli, kumbe ndani ni yeye Yule yule shetani..Biblia inatuambia uwezo huo anao..
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru”.
Hivyo tabia hiyo anayo.. kipindi kile hakuumba nyoka wenye pumzi ya uhai, kama nyoka wengine, au vyura wapya..bali alifanya kazi yake hiyo ya kubadilisha maumbile ya vitu mbele ya macho ya watu.. Kwa lugha ya sasa wanaita “kiini-macho” au “mazingaumbwe”, na ndio maana nyoka wa Musa, hakuwaona wale kama ni nyoka wenzake, wanaohitaji mapambano, bali aliona kama ni chakula tu, akala.
Ni sawa na mwanadamu ambaye amefikia maarifa ya kutoa ‘photocopy’ kitu orijino, Shetani naye hapo amepafikia.Lakini hana uwezo wa kutengeneza orijino.
Kama shetani angekuwa na uwezo wa kuumba chura, hata mbwa angeweza, hata ng’ombe pia angeweza, na sokwe nao. Na matokeo yake dunia, ingejawa na vitu vilivyoumbwa na Mungu, na vilivyoumbwa na shetani, leo hii tungesikia wale nguruwe si wa Mungu bali ni wa shetani, usiwaguse. Lakini hadi sasa hakuna rekodi ya kitu chochote kilichoumbwa na shetani, zaidi sana rekodi aliyonayo ni kuumba uovu na uasi duniani.
Pia tazama..
SWALI 2 : Je! Jini au pepo ni roho tu au pia wana miili inayoonekana, kiasi kwamba tunaweza kuwashika? Kama ndivyo Mbona Bwana Yesu alisema.
Luka 24:39 “Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.
JIBU: Ni kweli sawasawa na maneno ya Bwana Yesu, hakuna jini au pepo, au kiumbe chochote cha rohoni, chenye mwili, na kikaweza kuishi hapa duniani kama sisi.. Hakuna.
Kumbuka, Bwana Yesu alisema..
Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. 44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. 45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.
Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.
44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.
45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.
Maandiko hayo ni kutuonyesha kuwa, mapepo, hayana miili yao wenyewe ya kuishia hapa duniani, yanategemea watu,au wanyama,ili kutembea duniani, kama wakati ule yalivyomwomba Bwana yawaingie wale nguruwe. Lakini yenyewe kama yenyewe, hayawezi kusimama na kuwa kama wanadamu kutembea duniani.
Lakini Je! Wale wanaoshuhudia kwamba mapepo yanawatokewa, na pengine kuzuni nao, ni nini vile?
Mapepo yanaouwezo wa kujidhihirisha mbele ya mtu kwa taswira ya kitu fulani, aidha ya mtu, au kitu, kukutisha au kukufanya uogope, (Mathayo 14:26), au kukutokea katika ndoto,au maono.. lakini zaidi ya hapo yasiweza, kuendelea na kuchukua maumbile na kuwa kama mwanadamu mwingine na kuishi hapa duniani, kama vile kula, kunywa, kufanyabiashara, kuoa, au kuolewa n.k. huo uwezo hawana kwasababu hawana miili. Pepo haliwezi kuzaa na wewe.
Vinginevyo, shetani angeshajidhihirisha siku nyingi na kuwa mfalme wa dunia. Lakini mpaka sasa ni roho tu, na atabakia kuwa roho, mpaka atakapotupwa kwenye ziwa la moto na mapepo yake.
Lakini kumbuka ukiwa ni mtu wa kujishughulisha na mambo ya ushirikina, aidha wewe ni mganga, au mchawi, au ulishawahi kwenda huko, ukafanyiwa matambiko, au kufanyiwa mazindiko ya kipepo, au ukala vitu vyao, Huo nao ni mlango unaoongeza wigo mkubwa sana, wa shetani au mapepo yake, kujidhihirisha kwako, kwasababu umeingizwa katika mtandao wao wa kiroho, hivyo inakuwa rahisi sana kwao kujidhihirisha kwako, na pengine kuchukua umbile ya kitu chochote kukuletea madhara mwilini. Tofauti na mtu ambaye yupo mbali na mambo hayo.
Hivyo dawa pekee, ya kumfukuza shetani na majini yake, yasikutokee tokee au yasikufuate fuate ni kumkabidhi Yesu maisha yako. Kwa kumaanisha kabisa kuacha maisha ya dhambi, na baada ya hapo, ukazingatia kusoma NENO..
Kwasababu kuokoka ni sehemu ya kwanza, ya kuwekwa huru.. Ili kuukamilisha uhuru wako ni lazima Neno la Mungu likae ndani yako kwa wingi ili uweze kumshinda kabisa kabisa shetani.
Biblia inasema.
Bwana Yesu, alikuwa ni mtakatifu wa Mungu, ambaye hakutenda dhambi, lakini hilo halikumzuia shetani asimjie, na kuzungumza naye. Lakini utaona alimshinda kwa Neno la Mungu lililokuwa ndani yake, na si kitu kingine.
Vivyo hivyo na wewe, ikiwa tayari umeshaokoka, Jifunze sana Neno, ujue mamlaka, na haki uliyonayo katika Msalaba wa YESU KRISTO. Hiyo itakufanya usiishi maisha ya woga,wala wasiwasi wa nguvu zozote za giza, kwasababu utakuwa tayari umeshajua uwezo uliopewa jinsi ulivyo mkubwa kuliko wa ibilisi
Lakini ukiwa ni mkristo, mvivu, Neno husomi ujue kabisa shetani ataendelea kukusumbua tu, haijalishi utakuwa ni mwombaji kiasi gani.
Hivyo zingatia hayo mambo mawili.
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo, kumpa Yesu maisha yako, ili akusamehe na kukupa wokovu, na kuyafukuza maroho yote machafu yaliyokuvamia. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao hautakaa uujutie milele.
Hivyo fungua hapa, kwa mwongozo wa sala hiyo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?
Mjoli ni nani katika biblia?
Gombo ni nini?
Tatizo la visigino kuuma ni ishara ya nini kibiblia?..Au visigino kuwaka moto?.
1) Visigino kuuma.
Kama unafanya shughuli yenye kuhusisha miguu, kwamfano kulima au kutembea umbali mrefu, au michezo..basi ni jambo la kawaida visigino kuuma, au visigino kuwaka moto.
Suluhisho la tatizo hilo ni kupunguza shughuli hizo zinazohusisha miguu, na miguu itarudia hali yake.
Lakini kama huna shughuli zozote unazozifanya na umeenda hospitali na hujapata suluhisho, na hujui sababu, na pengine umeshafanyiwa hata na maombezi, na tatizo bado lipo palepale..
Basi suluhisho la tatizo hilo,linaweza kuwa la kimaandiko,na maandiko yafuatayo yatakufungua…
Yeremia 13:22 “Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya WINGI WA UOVU WAKO, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia”.
Jiangalie maisha yako ni wapi hapako sawa na Mungu..tubu makosa yako kwa Mungu kwa kumaanisha kuyaacha.
Angalia mahali unapofanyia kazi, au mahali unapoishi, jinsi unavyoenenda, tafakari mawazo ya mioyo yako, je yanampendeza Mungu?..
Je unao upendo?, Wewe ni mvumilivu, ni mtu wa kusamehe au wa vinyongo?, Je ni mtu unayemcha Mungu na kumwogopa?.
Kama sio basi hiyo ndio sababu kwanini visigino vyako vinauma, au vinawaka moto, na umekosa ufumbuzi kila mahali.
Litafakari sana hilo na Mungu akusaidie, yeye ni mwaminifu tukiungama dhambi zetu kwa lengo la kuziacha kabisa, anatusamehe na kuponya magonjwa yetu na majeraha yetu, kwasababu lengo lake sio sisi tuteseke, bali tuwe na furaha na tupate mema, ndio maana saa nyingine anaruhusu vitu fulani vitutokee ili tutubu, na mwishoni atubariki zaidi.
Maran atha!.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?
EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:
TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.
WITO WA MUNGU
Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)
JIBU: Hakuna mahali popote katika biblia inamtaja Mikaeli kuwa ndiye Bwana Yesu. Kinyume chake, maandiko yanamtofautisha Yesu na Malaika hata kwa asili aliyoitwaa, Biblia inasema.
Waebrania 2:16 “Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu”.
Ikiwa na maana, kudhihirishwa kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza, kulikuwa ni katika asili ya mwanadamu na sio Malaika. Na ndio maana utaona, Malaika nao, walimwona na kumtambua kwa mara ya kwanza, siku ile alipozaliwa katika mwili.
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Ni kweli Mikaeli ni mmoja wa Malaika wakuu mbinguni,na pengine Zaidi ya wote, Lakini hana sifa yoyote ya kudhaniwa kuwa yeye ndiye Kristo, kwani biblia inatuambia kuwa Kristo anaabudiwa sio tu na wanadamu, bali pia na malaika wote mbinguni(Waebrania 1:6), Lakini hakuna Malaika yoyote anayeabudiwa.
Pia Kristo alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi, Pamoja na kukemea pepo kwa uweza wake,lakini Malaika (akiwemo Mikaeli), hawana uwezo huo, wanajiona hawastahili mpaka wanasema Bwana mwenyewe na awakemee mashetani (Yuda 1:9)..
Na mwisho biblia inasema, hakuna mahali popote, Mungu alimwita Malaika yoyote “Mwanangu”, bali hao ni watumishi wake, watumikao kuwahudumia watakatifu, lakini kwa Bwana Yesu, Mungu alimwita mwana, kumtofautisha yeye na Malaika zake.
Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
Hivyo, Mikaaeli ni Malaika wa Bwana na atabakia kuwa hivyo. Lakini ikiwa utatamani kujua Zaidi aina za Malaika wa Mungu, na kazi zao na idadi zao, Fungua hapa >> Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?
Swali Je! Unatambua kuwa Mungu ameshawaweka tayari Malaika zake kwa ajili ya mapigo ya siku hizi za mwisho? Una Habari kuwa unyakuo upo karibuni sana kutokea, kuliko unavyoweza kudhani?
Kumbuka paraparanda ya Mungu ikilia leo, basi, Malaika hao wa mapigo, Mungu atawaachilia ulimwenguni mwote, wataipiga dunia kwa kwa zile baragumu saba, na vitasa saba. Wakati huo kutakuwa ni nyakati za shida sana ulimwenguni. Soma Ufunuo 8 &16, ujionee mpendwa. Ni Malaika mahususi wa kuleta mabaya duniani.
Zaburi 78:49 “Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya”.
Usitamani uwepo wakati huo ndugu yangu, Ni heri leo ukatubu na kumrudia muumba wako. Upokee uhakika wa kuurithi uzima wa milele. Ikiwa utataka kusoma juu ya mapigo hayo, fungua link hii>>
Neno Saumu lina maana gani katika biblia?
UNYAKUO.
Ninawi ni nchi gani kwasasa?
AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.
SWALI: Naomba kuelewa kwa undani Tofauti kati ya mbinguni, peponi, Kuzimu, Jehanamu, na Paradiso ni ipi?
JIBU:
Sehemu nyingi Biblia inaposema mbinguni, huwa inamaanisha moja kwa moja kule Mungu alipo Pamoja Malaika zake, Kule ambako Bwana Yesu alikwenda kutuandalia makao. Mahali ambapo sisi kama watakatifu bado hatujafika hata mmoja.
Ndio mbingu ya Tatu, ambayo Mtume Paulo alinyakuliwa kuonyeshwa baadhi ya vitu vilivyopo kule vipo kule ambavyo havielezeki kibinadamu, kwasababu upeo wetu ni mdogo. (2Wakorintho 12:1-4)
Ni juu sana, ambako, hatuna maelezo ya kutosha kupaelezea, mpaka tutakapofika.
2Nyakati 6:18 “Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga!”
Ni mbingu ya mangojeo, ambayo sio makazi yetu ya kudumu. Mtakatifu anayekufa sasa hivi anakwenda mahali panapoitwa Peponi/Paradiso, akisubiria, siku ya unyakuo ifike, arudi kaburini achukue mwili wake, kisha aungane Pamoja na wale watakatifu watakaokuwa hai wakati huo, na moja kwa moja safari ya kwenda mbinguni ianze, kule Bwana Yesu alipo.
Yule mwizi pale msalabani, Bwana alimwambia maneno hayo;
Luka 23:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. 43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.
Luka 23:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.
Wengine wanaiita mbingu ya pili, lakini vyovyote vile iitwavyo, bado ni mahali pa mangojeo pa watakatifu, Ndio kifuani pa Ibrahimu, yule maskini Lazaro alikwenda (Luka 16:19-31), ndio kule ambazo zile Roho zilizo chini ya madhahabu zilikuwa zinalia, zikiomba zilipiziwe kisasi kwa watesi wao.
Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. 10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi? 11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.
Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.
Vilevile huku ndio kule wale wafu waliofufuka na Bwana Yesu walipoelekea kwa mara ya kwanza. (Mathayo 27:52-53)
Hivyo leo, hii ukifa katika Kristo, basi unakwenda katika eneo hili la mbingu, ambalo ni lizuri sana. Ukisubiri ufufuo wa mwisho.
Kuzimu kibiblia ni Neno lililomaanisha makao ya wafu Au kaburini. Ambapo, waovu na wema walikuwa wanakwenda kabla ya Kristo kuja duniani, kuwatenganisha moja kwa moja kimakao,
Ayubu anasema
Ayubu 14:13 “Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!”
Daudi pia alipazungumzia, (Zaburi 16:10), kwamba Bwana hatomwacha huko milele.
Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, wakatifu walitoka huko makaburini, na kwenda peponi/ Paradiso. Mahali pa raha Zaidi pa juu na si makaburini tena. Hivyo wanaobakia makaburini au kuzimu ni waovu.
Ni mahali pa mangojeo pa waovu, ni mahali pa mateso, kama vile Paradiso palivyo mahali pa raha pa mangojeo kwa watakatifu, vivyo hivyo jehanamu nako, ni mahali pa mangojeo pa watu waovu wanaokufa sasa. Wanaadhibiwa huko, wakingojea siku ile ya hukumu ya mwisho ifike. Ili wapewe hukumu yao, katika hukumu ya kile kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo, kisha wakatupwe kwenye lile ziwa la moto, ambalo ndio mauti ya pili ilipo.
Ni sawa na mhalifu anayekamatwa sasa hivi, kabla ya kuhukumiwa kifungo, huwa anawekwa kwanza mahabusu, akisubiria siku ya kupandishwa kizimbani ifike, ahukumiwe kisha akatumikie kifungo chake Jela, Ndivyo ilivyo kwa watu waovu wanaokufa sasa, na waliokufa zamani. Wanakwenda katika sehemu hii ya mateso, ambayo si ya kawaida.
Bwana Yesu alisema..
Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [ 46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”
Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [
46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”
Swali, la kujiuliza ni Je! Tukifa leo, au Unyakuo ukitukuta leo, mimi na wewe tutakuwa wa upande upi? Katika mambo ambayo hupaswi kuyachukulia juu juu tu, basi ni mambo ya Maisha yako ya milele. Kwasababu ukishakufa hakuna nafasi ya pili tena. Kama umestahili Jehanamu basi utaendelea kuishi humo milele.
Ni heri ukamgeukie Kristo, maadamu muda mchache bado unao. Acha kutazama, mambo ya ulimwengu, kwani huwa yanapumbaza sana, kukufanya usione kama kuna mabaya yanakuja mbele, Moja ya hizi siku utajutia Maisha yako, uliishije endapo hukumpa Kristo Maisha yako leo.
Tubu dhambi zako, maanisha kumfuata Yesu.
Bwana atusaidie, kuyafahamu haya.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?
MILANGO YA KUZIMU.
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
Ni kawaida mwanadamu anapopitia matatizo mengi au shida nyingi, huwa anatamani hata afanane na mnyama asiyejua shida, anatamani angekuwa kama ndege apae zake aende mbali na makao ya watu akaishi humo.
Ndivyo Daudi alivyosema..kipindi ambacho anafukuzwa na Sauli huko majangwani, alisema..
Zaburi 55:5-8[5]Hofu na tetemeko limenijia, Na hofu kubwa imenifunikiza.[6]Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.[7]Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.[8]Ningefanya haraka kuzikimbia Dhoruba na tufani.
Lakini jinsi Mungu alivyotuumba, kamwe hatuwezi kuzitoroka dhoruba na tufani za maisha…fahamu kuwa watu wanaokuudhi ndio hao hao utaendelea kuishi nao, na kama hutaishi nao nyumba moja, basi kuna kipindi mtakutana tu katika nukta fulani ya maisha..
Maadui zako, watesi wako, pamoja na wachawi hakuna siku Mungu atakutenga nao akupeleke katika dunia yako mwenyewe uishi huko kwa starehe, hicho kipindi hutakaa ukifikie haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani.
Mungu anachokifanya kwetu ni kutulinda na kutuepusha tu na madhara yao, yasitufikie. Lakini kuishi katikati yao ni jambo endelevu mpaka mwisho.Bwana Yesu alisema;
Yohana 17:15[15]Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
Wakati mwingine, Mungu anapotaka kukupa rizki, anatumia hata njia ya hao hao, unakula katikati yao wakikuona..
Zaburi 23:5[5]Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
Hivyo ndugu uliyeokoka, acha kutaabika kwa ajili ya wanadamu, wala usipeleke akili zako mbali sana, ukidhania kuwa hao watu walio na wewe kama mwiba kuna siku watatoweshwa milele, uishi peke yako kwa starehe..Kanuni hiyo Mungu hajaichagua japo tunaitamani.
Zaidi sana jifunze kuyatimiza mapenzi ya Mungu katikati yao. Utakuwa na furaha katika maisha.Kumbuka Mbawa kama za njiwa hatujapewa wanadamu.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Kwanini wakristo wengi ni maskini?.
ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?