Podo ni kimfuko au kibegi kidogo aidha cha ngozi au malighafi nyingine, ambacho hutumika kubebea mishale.
Utalisoma Neno hilo katika vifungu hivi;
Mwanzo 27:1-3[1]Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa.[2]Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.[3]Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;
Soma pia Ayubu 39:23, Isaya 49:2, Yeremia 5:16
Lakini Hiyo inafunua nini rohoni? Sikuzote askari makini huwa habebi mchale mmoja anapokwenda vitani..atahitaji Furushi la mishale kujihakikishia ushindi wake dhidi ya adui zake. Na ndio hapo atahitaji podo la kuihifadhia hiyo mishale yake.
Ni kama mwanajeshi, hawezi kutegemea risasi moja kujihakikishia ushindi atakuwa na mkanda wa risasi, ili adui yake ajapo amshindilie vya kutosha..
Halikadhalika na sisi kama wakristo, hatuna budi kuwa na podo zetu zenye mishale mingi ya kumpiga yule adui.Hatumpigi shetani kwa maombi tu peke yake, vinginevyo tutakwama mahali.. tutampiga kwa mshale wa kuhibiri injili pia, kwa mshale wa kutenda matendo mema, kwa mshale wa kumtolea Mungu sadaka, kwa mshale wa kuwasaidia wenye uhitaji, kwa mshale wa utakatifu n.k.
Hapo ndipo tutakuwa tumezijaza podo zetu silaha.
Embu soma kwa makini vifungu hivi;
Zaburi 127:4-5[4]Kama mishale mkononi mwa shujaa, Ndivyo walivyo wana wa ujanani.[5]Heri mtu yule Aliyelijaza podo lake hivyo. Naam, hawataona aibu Wanaposema na adui langoni.
Nasi tujitahidi kujaza podo zetu silaha nyingi ili shetani asipate upenyo wa kutushambulia kirahisi.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
Mjoli ni nini/ ni nani katika biblia?
Je ni kweli miaka yetu ya kuishi ni 80 tu (kulingana na Zaburi 90:10).
KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.
Rudi nyumbani
Print this post
Mjoli ni mfanyakazi-mwenza, Ni mtu unayefanya naye kazi moja inayofanana.. Kwamfano kama wewe ni mwalimu, ukakutana na mwalimu mwenzako huyo ni mjoli wako…Kama wewe ni mhubiri ukakutana na mhubiri mwenzako huyo ni mjoli wako, kama wewe ni mkulima ukakutana na mkulima mwenzako huyo ni mjoli wako..
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia..
Mathayo 18:23-35[23]Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.[24]Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talantaelfu kumi.[25]Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.[26]Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.[27]Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.[28]Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinarimia; akamkamata, akamshika koo, akisema, Nilipe uwiwacho.[29]Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.[30]Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.[31]Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.[32]Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;[33]nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?[34]Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.[35]Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.
Wafilipi 4:3[3]Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi naye, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.
Soma pia..Wakolosai 1:7 ,4:7, Ufunuo 19:10, 22:9.
Vivyo hivyo na sisi watakatifu ulimwenguni kote tuliookolewa na Yesu Kristo, kila mmoja ni mjoli kwa mwenzake. Hivyo hatuna budi kupendana, kutumikiana, kusameheana.. Maadamu tupo katika shamba moja na kazi moja, tunapaswa kuujenga ufalme wa Mungu kwa nguvu zetu zote. Huku tukizingatia misingi ya Biblia, na sio ya kidhehebu au kidini
Yule aliyemzuia Yohana asimsujudie alikuwa ni Mwanadamu au Malaika?
Makuruhi ni nini, kama tunavyosoma katika biblia?
JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.
EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.
SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto.” (Marko 9:49)
JIBU: Kama tunavyofahamu kazi kubwa ya chumvi ni kiungo, kiasi kwamba chakula kinaweza kikawa ni kizuri kweli, kinavutia kwa macho, kina harufu nzuri, lakini kikikosa chumvi huwa kinapoteza ladha yote, haijalishi kilitengenezwa kwa viungo vingi kiasi gani.
Vivyo hivyo na sisi kwa Mungu, ili tuwe tumestahili kuingia katika ufalme wake wa mbinguni, ni lazima tuwe kama chakula kilichokamilika kwake, tukikosa ladha tu ya chumvi yake, kamwe hatuwezi kuuingia ufalme wake.
Sasa ili kuelewa vizuri chumvi hiyo tunaipate, au inakujaje kujaje ndani yetu, tusome Habari yenyewe, kuanzia vifungu vya juu yake kidogo, ili tupate picha kamili;
Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika; 44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [ 46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum; 48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki. 49 KWA SABABU KILA MTU ATATIWA CHUMVI KWA MOTO. 50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi”.
Marko 9:43 “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;
44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [
46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]
47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
49 KWA SABABU KILA MTU ATATIWA CHUMVI KWA MOTO.
50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi”.
Umeona, baada ya maagizo hayo, mwishoni kabisa Kristo ndio anasema na sisi tutatiwa chumvi lakini si kwa kitu kingine bali kwa MOTO.
Na moto wenyewe ndio huo, aliokuwa anauzungumzia hapo juu, kwamba kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate, unapokata kiungo chako, utasikia maumivu kweli, lakini ndio tiba ya kukufikisha mbinguni, ndio chumvi yenyewe inayokufanya ulete ladha mbele ya Mungu.
Hiyo ikiwa na maana kuwa, hata wewe, binafsi unafahamu kabisa vipo vitu ambavyo vinakukosesha vinakufanya usimrudie Mungu wako kikamilifu, inawezekana ni kazi Fulani, au kampani ya marafiki zako walevi, au wahuni, au wadada wenzako wadadisi, au ndugu zako, au binti yule, au kijana yule. Kumbuka Bwana amekupa amri hii, ikiwa wanakufanya uikose mbingu, Achana nao, haraka sana bila kuangalia nyuma.. wakatae..
Ni kweli inauma,unapoviacha hivyo vitu, au unapowaacha ni moto utausikia, lakini ndivyo unavyotiwa chumvi na Bwana. Kwasababu usipoukubali moto huo sasa, utakutana nao siku ile utakaposhuka Jehanum ukifa.
Huu si wakati, wa kuikumbatia dhambi hata kidogo, si wakati wa kumwangalia mtu Fulani anasema nini juu ya Maisha yako ya milele, mbinguni utakwenda peke yako, vilevile usipotubu jehanumu utakwenda peke yako. Ni heri upitie shida hapa duniani, kule ukaishi milele kwa rah a na Mungu, kuliko kupitia raha za kitambo hapa duniani, halafu kule ukaishia motoni milele.
Hivyo ndugu yangu kubali kutiwa chumvi sasa, kwa kukubali kuacha yale ambayo yameshikamana sana na wewe kwa wakati huu wa siku za mwisho.
Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”,
Bwana akubariki.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?
OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.
Nini tofauti kati ya moyo na roho?
UNYAKUO.
WhatsApp
SWALI: Je Wakati Mfalme Nebukadreza anawatupa Shadraka, Meshaki na Abednego kwenye tanuru la Moto, Danieli alikuwa wapi?
JIBU: Kwasababu biblia haiandiki kila habari, bali inachagua yale matukio muhimu tu, yatakayotusaidia, ndivyo ilivyo katika habari hii, haielezi habari za Danieli kwa wakati huo, alikuwepo wapi, lakini katika sintofahamu hiyo, tuna la kujifunza. Hivyo hapo mambo matatu yanawezekana,
La kwanza ni aidha Danieli hakuwepo, wakati huo, ambapo Nebudreza, anatoa amri, kwasababu utakumbuka kuwa yeye aliyewekwa juu ya waganga wote, na wenye hekima (Danieli 5:11). Hivyo kuna uwezekano, alipewa jukumu lingine la kwenda kulifanya nje ya Babeli kwa wakati huo , na mbio ilipopigwa yeye hakuwepo.
La pili, ni aidha, watu waliokuwa pamoja na mfalme agizo hilo halikuwahusu, kwasababu ukichunguza utaona, Nebukadreza, aliwaita wakuu wake wote waliokuwa katika majimbo yake yote ulimwenguni. Na lengo la kuwaita, lilikuwa ni kuwapima utiifu wao kwa serikali yake moja ya ulimwengu. Ndio maana akawalazimisha wakuu wote ambao wapo mbali naye waje kuisujudia sanamu yake. Hivyo kwasababu Danieli alikuwa katika jumba la mfalme agizo hilo halikumuhusu.
Danieli 2:49 “Tena, Danielii akamwomba mfalme, naye akawaweka Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wawe juu ya mambo yote ya uliwali wa Babeli; lakini huyo Danielii alikuwa akiketi katika lango la mfalme”.
Na mwisho, ni kwamba Danieli, tangu mwanzo alisimama katika misingi ya Imani yake, utakumbuka, walipoitwa na kutaka kulishwa Divai, pamoja na vyakula najisi, moja kwa moja walivikataa yeye pamoja na hao wenzake watatu. (Danieli 1:8-16) Hivyo uwezekano pia wa Danieli kumweleza mfalme misimamo wake, ulikuwepo, na mfalme akamwelewa, akamwacha peke yake asiisujudie miungu yake.
Lakini kusema kwamba alitii amri ya mfalme, hilo jambo halipo, wala lisingewezekana kwa Danieli, kwasababu utakumbuka, hata baadaye sana, jaribio kama hilo lilitaka kufanyika, la kumzuia asimwabudu Mungu wake, lakini alikaidi amri yao bila kujali nani kasema, au adhabu gani imetolewa.
Lakini habari hii ya kutokuwepo kwa Danieli inatufundisha nini? Ni kwamba, upo wakati Mungu atakuepusha na majaribu ambayo nafasi ya kuyakwepa ni ndogo sana, lakini pia upo wakati Mungu atakupitisha katika majaribu ya adui. Mwanzoni kikombe kile hakikumuhusu Danieli, lakini mwishoni, alishiriki kikombe cha kutupwa katika tundu la Simba.
Nasi pia, kuna nyakati ngumu zitapita mbele yetu katika eneo la imani yetu, na Mungu atatuvusha salama bila hata ugumu wowote, lakini pia zipo nyakati ataziacha zipite juu yetu. Lakini yote katika yote, tunapaswa tuwe katika msimamo wetu kama vile Danieli.
Nyakati zote za mvua, na joto, misingi ya imani yetu isitikiswe.
DANIELI: Mlango wa 1
UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?
Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)
Nini maana ya kuutia moyo ufahamu? (Danieli 10:12)
Mwanzo 2:9
[9]BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Unaweza kujiuliza kulikuwa na sababu gani Mungu kuuweka mti wa ujuzi wa mema na mabaya pale bustanini wakati alikuwa anajua kabisa una kifo ndani yake?
Kwanini asingeuacha tu ule wa uzima na ile mingine ..ili mwanadamu aishi milele kwa furaha pale Edeni.
Je Ni kwamba Mungu hana mipango ya kueleweka kwa watu wake au?(tukizungumza kibinadamu)
Jibu la La! Nataka nikuambie mipango ya Mungu ni mikamilifu sikuzote na ni mizuri..tofauti na tunavyodhani kuwa ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya ulikuwa ni mbaya, haukustahili kuwepo pale.
Ukweli ni kwamba ule mti ulikuwa ni mzuri na unafaa sana, tena twamshukuru Mungu kwa kuuweka pale bustanini….Unajua ni kwasababu gani?
Ni kwasababu sisi kamwe tusingeweza kuwa kama Mungu, na malaika zake kama tusingepata ujuzi ndani yetu.
Kumbuka ujuzi ni jambo ambalo mwanadamu hakuumbiwa tangu mwanzo, si asili yetu..sisi tuliumbwa kutokujua mambo kama aibu, ustaarabu, mipango, maamuzi, ibada n.k hayo yote yalikuja baada ya kula matunda yale,
Sasa, Mungu aliliona hilo tangu mwanzo, hivyo akaona njia pekee ya kumkamilisha mwanadamu ili afanane na yeye ni kumpa ujuzi huo ndani yake..lakini aliona pia hatari yake..kwamba siku zote ujuzi una nguvu kubwa ya kupoteza,(1Wakorintho 8:1) hivyo akamtaadharisha mapema.
Ujuzi wa kujua mtu anahitaji kuishi katika nyumba na sio porini, kwamba anahitaji kujenga nyumba, kufanya biashara, kugundua vitu, kuvaa nguo na sio kukaa uchi, kujijengea mfumo n.k Mungu aliona mwisho wake utampoteza mtu, japo ujuzi wenyewe sio mbaya.
Ndipo akabuni njia ya kuweza kudhibiti tatizo hilo. Akaweka mti mwingine bustanini unaoitwa mti wa Uzima. Ambao mwanadamu akiyala matunda yake ataurejesha ule uzima ambao angeupoteza kwa kupokea ujuzi.
Na hapo mwanadamu atakuwa amepata faida mara mbili, kwanza ni kufanana na Mungu, pili ni kurejesha uzima wa milele.
Nachotaka ujue ni kuwa kila mwanadamu anayeishi duniani..ujuzi huu upo ndani yake..Na ndio maana unaweza kujiamulia mambo yako mwenyewe, unaweza kusema hapana au ndio..unaweza kusema nataka au sitaki..huwi kama mnyama, Au kama roboti bali una ujuzi wote wa kufanya unachotaka mwenyewe bila hata kumtegemea Mungu, mwanadamu au shetani..
Lakini nakuambia hii ni hatari kubwa kwasababu uhuru huu wa kifikra umetufanya wanadamu ndio tuende mbali sana na Mungu wetu, tupotee kabisa, tuone Mungu ni nani, mbona tunaweza kufanya wenyewe bila yeye, rangi zetu pekee hazitoshi, tujichubue kidogo, tujichore tatoo kidogo tupendeze, tuvute sigara, tunywe pombe tuwe fresh, tuzini na Wanyama, kwani kuna shida gani? . Kwa kifupi ni kuwa tumepotea kama tutaishi katika hii hali pasipo kuifahamu kinga.
Tunauhitaji mti wa uzima. Na mti wenyewe ni YESU KRISTO. Hakuna namna utaweza kuishi kwa ujuzi wako, au akili zako bila Yesu Kristo kukusaidia. Mwisho wa siku utakufa tu na kupotelea motoni.
Yohana 14:6
[6]Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Watu wengi leo wanadhani elimu zao, ndio zitawapa maisha, wanadhani tafiti zao ndio zitawafikisha ng’ambo, wanadhani mawazo yao na imani zao na teknolojia zao na ustaarabu wao ndio zitakazowavusha..
Hawajui kuwa mioyo yetu sisi wanadamu huwa ni midanganyifu kuliko kitu chochote huku duniani.
Yeremia 17:9
[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Na ndio maana Bwana Yesu alisema “Mtakufa katika dhambi zenu, kama msiposadiki kuwa mimi ndiye.”(Yohana 8:24)..tusipookolewa..hakuna tumaini ndugu. Bwana Yesu ndiye mti wenyewe wa uzima. Shusha kiburi chako, yasalimishe maisha yako kwake..akusaidie.
Siku hizi ni za mwisho, wakati wowote parapanda inalia hakuna mtu asiyelijua hilo, ipo wazi kulingana na dalili tunazoziona sasa. Hii dunia inafikia mwisho, mtafute Yesu Kristo, akuokoke na udanganyifu wa ujuzi.
Kama hujaokoka basi mkaribishe leo Yesu katika maisha yako, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, kisha utapokea ondoleo la dhambi.
Mungu akubariki.
HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.
Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)
UFUNUO: Mlango wa 22
SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari”. Hii miamba yenye hatari ni ipi?
JIBU: Tusome..
Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa; 13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele”.
Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;
13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele”.
Hapa ni mtu Yuda alikuwa anawalinganisha wachungaji na mitume wa uongo kama miamba yenye hatari.
Sasa miamba inayomaanishwa hapo, si hii miamba tuionayo nchi kavu, hapana, bali ni ile miamba ya habarini ambayo baadhi yao inatabia ya kuchomoza juu hadi karibu na usawa wa bahari. Miamba hii ni hatari sana kwa mabaharia, kwasababu huwa haionekani, lakini meli inapopita karibu nayo, inaichana, kama sio kuiharibu kabisa na matokeo yake, ni aidha meli kugotea palepale, au kuzama kabisa.
Kama mabaharia wasipokuwa waangalifu, kwa kupita njia zilezile walizozithibitisha ni rahisi sana kukutana na hii miamba na kuzipoteza meli zao moja kwa moja.
Sasa hapo anaposema “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu”;
Anamaanisha, wachungaji hawa, au watumishi hawa wa uongo ni ngumu kuwatambua, kama tu vile miamba hii hatari ilivyo ngumu kuiona habarini, pale ambapo Habari inaonekana shwari na tulivu yafaa kwa kusafiria kumbe ndipo ilipojifichia, halikadhalika, watumishi hawa wa uongo, mahali ambapo mpo katika karamu zenu za Upendo, yaani wakati ambapo mnamfurahia Mungu wenu, mnatangaza Habari njema, mkidhani kuwa wapo na nyie, kumbe ni mbwa mwitu katika mavazi ya kondoo.
Mfano wa watu hawa alikuwa ni Yuda,alitembea na Bwana Pamoja na mitume wengine, lakini haikuwa rahisi kumgundua, hadi dakika ya mwisho, utaona alipokuwa katika mlo wa jioni, kama mpelelezi, hakuna aliyemtambua isipokuwa Bwana tu peke yake.
Mtume Paulo aliliona hilo hata wakati wa kuondoka kwake akasema..
Matendo 20:29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; 30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”.
Matendo 20:29 “Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;
30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”.
Hadi sasa, inasikitisha kuona watumishi wa namna hii wapo wengi katika kanisa la Mungu, ,hawaoni shida kuwadanganya watu, wengine ni wachawi, wengine ni matapeli, wengine wapo kwa lengo la kuzivuruga tu kazi za Mungu, ili watu watusiishi Maisha matakatifu, hawawahurumii watu wanaotaka kumjua Mungu, lakini cha ajabu ukiwaangalia kwa nje, wanalitaja jina la Yesu, wanaongoza makanisa, wanashiriki katika kampeni zote za kidini.
Huu ni wakati wa kuwa makini sana, Ni wakati ambao wewe kama mkristo, kuondoa uvivu wa kusoma biblia, tunadanganywa kwasababu hatuna maarifa ya kutosha kuhusu Mungu wetu na utendaji kazi wake. Hatuwezi kumshinda shetani kwa maneno tu, au kwa kumkemea, tutamshinda shetani kwa lile Neno lililokaa ndani yetu kwa wingi, ndiyo silaha ambayo Bwana Yesu aliitumia kumshinda shetani pale alipokuwa anajaribiwa nay eye kule jangwani.
Vinginevyo tukiyaendesha Maisha yetu hivi hivi tu kwa jinsi tunavyotaka, tujiandae kukutana na hii miamba yenye hatari, isiyoonekana. Tukiwa wavivu kujifunza biblia, hakuna namna tutamkwepa shetani, hakuna namna.
Bwana atusaidie.
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
Katika biblia ukiona neno “mwandamo wa mwezi”, au “mwezi mpya”, ujue ni neno lile lile moja linalomaanisha “siku ya kwanza ya mwezi”.
Katika agano la kale siku hii iliheshimiwa na kufanywa kama mojawapo ya siku takatifu, kama tu vile ilivyokuwa siku ya sabato, ambayo ni siku ya saba. Vivyo hivyo kila siku ya kwanza ya mwezi mpya, tarehe moja (kwa kalenda ya kiyahudi), ilikuwa ni takatifu kwao, na ni lazima watu wakamtolee Mungu sadaka za kuteketezwa, Sadaka za unga na vinywaji, Pamoja na kupiga tarumbeta juu ya sadaka hizo, (Hesabu 28:11-15), .Vilevile hukuruhusiwa kufanya shughuli yoyote au biashara yoyote(Nehemia 10:31-33)
Hesabu 28:11 “Tena katika mianzo ya miezi yenu mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa; nayo ni ng’ombe waume wadogo wawili, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza, wakamilifu, saba; 12 pamoja na sehemu ya kumi tatu za efa za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa kila ng’ombe; na sehemu ya kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa huyo kondoo mume mmoja;”
Hesabu 28:11 “Tena katika mianzo ya miezi yenu mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa; nayo ni ng’ombe waume wadogo wawili, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza, wakamilifu, saba;
12 pamoja na sehemu ya kumi tatu za efa za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa kila ng’ombe; na sehemu ya kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, kwa huyo kondoo mume mmoja;”
Hesabu 10:10 “Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu”.
Lakini kuna wakati wayahudi, walizifanya sikukuu hizo kama mazoea tu, wakawa hawazitoi katika utakatifu, bali kama agizo tu la kidini na huku nyuma mioyo yao ipo mbali na Mungu, hivyo hiyo ikamfanya Mungu akasirishwe nao na hatimaye kuzitaa sikukuu zao hizo za mwandamo wa mwezi.
Isaya 1:13 “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. 14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua”.
Isaya 1:13 “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.
14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua”.
Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;
Zaburi 81:3 “Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu”.
1Samweli 20:5 “Naye Daudi akamwambia Yonathani, Tazama, kesho ni mwandamo wa mwezi, nami hainipasi kukosa kuketi chakulani pamoja na mfalme; lakini niache nijifiche bondeni hata siku ya tatu jioni.
Soma pia, 2Nyakati 2:4, 8:13, Ezra 3:5, Hosea 2:11.
Jibu ni la! Kama tu vile hatujapewa takwa la kuitunza sabato kama sheria , vivyo hivyo, na katika mwandamo wa mwezi mpya.
Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; 17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.
Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”.
Ni kwamba tuthaminishe nyakati zetu mpya kwake. Wiki yako inapoisha na kuanza nyingine bila kumfanyia Mungu wako ibada, ni hatari kubwa sana, kama kwako ni jumapili, au jumamosi, ndio unamfanyia Mungu ibada, hakikisha unakutanika na wengine, kumwabudu Mungu wako, usiruhusu wiki yako ipite hivi hivi tu.
Halikadhalika, mwezi wako mpya unapoanza, usianze hivi hivi tu, bali chukua muda kwenda kumshukuru Mungu nyumbani kwake, ni muhimu sana. Ukiona wiki yako inapita hivi hivi tu, mwezi wako unapita hivi hivi tu, mwaka wako unapita hivi hivi tu, huna Habari na Mungu. Angalia Maisha yako ni lazima yatakuwa na kasoro Fulani tu.
Hivyo tujitahidi sana, tusiwe na mapengo pengo kwa Mungu wetu.
SIKUKUU 7 ZA KIYAHUDI ZINAFUNUA NINI KWETU?
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?
MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?
Huu mstari una maana gani?
Zaburi 91:1 “Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi”.
Maandiko hayo yanatuonyesha kumbe Mungu anao uvuli wake. Na uvuli huo hawakai watu wote ilimradi tu, bali wale tu wanaokaa katika mahali pake pa siri.
Sasa swali utajiuliza huko mahali pake pa siri ni wapi?
Kuna madaraja ya kumfikia Mungu, yapo yanayofikiwa na wakristo wa kawaida tu, wale wanaomtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, au mwezi kwa mwezi, lakini pia yapo yanayofikiwa na wakristo waliojikana, na kudhamiria kumfuata Kristo katika Maisha yao.
Hao wanaojikana ndio wanaofikia mahali pa siri pa Mungu.
Wanafananisha na makuhani, ambao, katika ile hema ya kukutania, au hekalu la Mungu, ni wao tu walikuwa na uwezo wa kupaingia patakatifu, na kule patakatifu pa patakatifu, palipo na kile kiti cha rehema cha Mungu.Kumbuka si kila mwisraeli, alifika pale, si kila mtu anayejiona anamcha Mungu aliweza kufika pale, kwa mtu wa kawaida ukijitahidi sana, uliishia katika ule ua wa hema ya kukutanikia, lakini ndani, sehemu za siri za Mungu walioweza kuingia makuhani tu.
Vivyo hivyo katika agano jipya, Mungu anao sehemu yake ya siri, na ni watu baadhi tu wanaoweza kufika huko, Mfano hai katika biblia ni mwanamke kama ANA, yeye, aliweza kupafikia hapo..na ndio maana alikuwa miongoni mwa watu wachache sana waliofunuliwa mpango wa Mungu wa wokovu,yaani kuja kwake Yesu duniani..
Lakini hiyo yote ni kwasababu alikuwa ni mwanamke aliyeupoteza ubinti wake, autumie kwa Mungu hadi uzee wake, haundoki hekaluni, mchana na usiku akisali na kufunga.
Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. 37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba. 38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.
Luka 2:36 “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.
37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.
38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.
Mwingine, ni Simeoni, naye pia biblia inasema alikuwa ni mtu wa haki, na anaye mcha Mungu, tena Zaidi alikuwa anautazamia wokovu wa taifa lake Israeli, yaani wakati wayahudi wapo bize na mali na fedha, yeye alikuwa kama Danieli, akiomba na kutafuta Habari za kuja kwa masihi duniani.
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. 26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. 27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, 28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, 29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema; 30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako”,
Makundi ya watu kama hawa, huwa wanaonjeshwa kitu kingine tofauti na watu wa kawaida, huo ndio uvuli wake Mungu. Wanapewa mafunuo ya ndani sana, wanapewa ulinzi wa majeshi ya Malaika wengi,mfano Elisha, wanajaliwa haja za mioyo yao na Mungu. Kwasababu tayari wapo chini ya uvuli wake.
Je! Na sisi tunaweza kufikia mahali hapo?
Kama jibu ni ndio,
Basi hatuna budi, kufanana na makuhani wa Mungu kweli, wana wa Lawi, ambao wametengwa na dhambi na unajisi, Si tu kumkiri Kristo na kuendelea kuishi Maisha ya juu juu, bali tujikane na nafsi zetu pia kwake, yaani tuwe tayari kujitwika na misalaba yetu tumfate Kristo. Tukubali ulimwengu utupite na mambo yake yote.
Na kwa kufanya hivyo kwa neema zake, atatufikisha mahali pake pa siri.
Bwana atusaidie sote.
Amen.
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Ni SIRI gani Paulo aliyokuwa anaimaanisha katika Waefeso 5:32?
Barazani pa Mungu ni wapi? Kama tunavyosoma katika Yeremia 23:18?
Bwana alimaanisha nini aliposema mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?
Mithali 15:10a “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;..”.
Mapigo ya Mungu yanatofautiana na mtu na mtu.. Tofauti na tunavyodhani kuwa muuaji ndiye atakayeadhibiwa sana siku ile kuliko mtu aliyeuacha wokovu.
Jibu la la! Maandiko yanatuambia, “Adhabu kali ina yeye aiachaye njia”, hasemi tu ‘adhabu’ ina yeye aichaye njia, hapana, bali adhabu KALI..
Bwana Yesu alirudia , maneno hayo hayo tena katika
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.
Leo hii inasikitisha kuona kuwa watu wengi wanakiri kwa vinywa vyao kuwa wameokoka, lakini kimatendo wapo mbali na Kristo, hawa wote ni kundi la wakristo walioicha njia, au waliojua mapenzi ya Bwana wao lakini wasiyafanye, wanaojua kuwa kutazama pornography hakumpendezi Mungu, lakini wanatazama, kuishi na mume/mke ambaye si wako ni dhambi mbele za Mungu lakini wao bado wanaendelea kuishi nao, tena wanazaa nao,
Wanaojua, kabisa kuvaa nguo za nusu uchi, na kujichubua ni dhambi, lakini bado wanaendelea kufanya mambo kama hayo,. Wachungaji na watumishi wanaojua kabisa, uasherati ni kosa kubwa sana kwa watu kama hao, lakini sasa imeshakuwa desturi yao. Hao ndio Kristo anaowazungumzia kuwa watakuwa na adhabu kali sana kule kuzimu.
Ndugu yangu, mateso yaliyopo kule, usidiriki kuyapima kwa akili zako, ni mahali ambapo hata hao wanaoteswa huko hawatamani, kukuona mtu kama wewe umefika huko, ni mateso makali sana, yasiyoelezeka, soma (Luka 16:27-29).
Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya;
Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [ 46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.] 47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum; 48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.
Marko 9:45 “Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum; [
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki”.
Ndugu,unaposikia injili halafu huitendei kazi, ujue kuwa inageuka na kuwa adhabu kwako, na kwa jinsi unavyoendelea kuisikia ndivyo unavyojiongezea mapigo. Yathamini Maisha yako ya rohoni, siku hizi ni za mwisho, Unyakuo ni wakati wowote, Bado hujui siku zako za kuishi hapa duniani zimebakia ngapi, sikuzote kifo huwa kinakuja ghafla tu, hakina hodi je! Mimi na wewe tumejiandaaje? Kwa injili zote hizi tulizozisikia?
Ni heri tuyasalimishe Maisha yetu kwa Bwana leo, atuokoe, na kutufungua, tumaanishe kabisa kumfuata yeye bila lawama yoyote, tuweke kando mambo ya ulimwengu yanayopita, tuutafute utakatifu kwa bidii, kwasababu pasipo huo kamwe mbingu hatutaiona (Waebrania 12:14),
Lakini Ikiwa utatamani kutubu leo, na kuanza Maisha yako upya na Bwana, katika kipindi hichi kifupi tulichobakiwa nacho, basi yeye yupo tayari kukusamehe.. Ukiiomba sala hii fupi ya TOBA, ukiisema kwa Imani, basi utapokea msamaha hapo hapo ulipo.. Hivyo kama upo tayari kuyasalimisha leo Maisha yako kwa Bwana.
Hapo ulipo unaweza kutafuta mahali pa utulivu peke yako, kisha piga magoti, nyosha mkono wako mmoja juu, kama ishara ya kuyasalimisha Maisha yako kwa Bwana. Kisha, ukishakuwa katika utulivu, sema maneno haya, kwa sauti:
BABA YANGU, NAJA MBELE ZAKO, NINAKIRI KUWA NIMEKUWA MWANA MWASI MBELE ZAKO KWA MUDA MREFU, KWA WINGI WA DHAMBI ZANGU, NIMESTAHILI ADHABU NA MAPIGO MAKALI KUTOKA KWAKO, NI KWELI BWANA NILIYAJUA MAPENZI YAKO LAKINI SIKUYATENDA. LAKINI LEO MIMI MWANAO (TAJA JINA LAKO) NIMEDHAMIRIA KUYAANZA MAISHA YANGU UPYA NA WEWE. NAOMBA UNISAMEHE BABA YANGU. KUANZIA LEO NINAACHA NJIA ZANGU MBAYA ZOTE, NINAMKATAA SHETANI NA KAZI ZAKE ZOTE, NINAUKATAA ULIMWENGU. NAOMBA DAMU YA MWANAO YESU KRISTO, UNISAFISHE NA KUNITAKASA KABISA. ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE. KAMA ULIVYOSEMA KATIKA NENO LAKO, YEYOTE AJAYE KWANGU SITAMTUPA NJE KWAKE. NAMI NAAMINI UMENIPOKEA, NA KUNIFANYA KIUMBE KIPYA LEO. NAOMBA UNIPE UWEZO WA KUUSHINDA ULIMWENGU NA KUUISHIA WOKOVU SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU. ASANTE BWANA YESU KWA NEEMA YAKO, NA MSAMAHA WAKO. AMEN.
BABA YANGU, NAJA MBELE ZAKO, NINAKIRI KUWA NIMEKUWA MWANA MWASI MBELE ZAKO KWA MUDA MREFU, KWA WINGI WA DHAMBI ZANGU, NIMESTAHILI ADHABU NA MAPIGO MAKALI KUTOKA KWAKO, NI KWELI BWANA NILIYAJUA MAPENZI YAKO LAKINI SIKUYATENDA. LAKINI LEO MIMI MWANAO (TAJA JINA LAKO) NIMEDHAMIRIA KUYAANZA MAISHA YANGU UPYA NA WEWE. NAOMBA UNISAMEHE BABA YANGU.
KUANZIA LEO NINAACHA NJIA ZANGU MBAYA ZOTE, NINAMKATAA SHETANI NA KAZI ZAKE ZOTE, NINAUKATAA ULIMWENGU. NAOMBA DAMU YA MWANAO YESU KRISTO, UNISAFISHE NA KUNITAKASA KABISA.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNISAMEHE. KAMA ULIVYOSEMA KATIKA NENO LAKO, YEYOTE AJAYE KWANGU SITAMTUPA NJE KWAKE. NAMI NAAMINI UMENIPOKEA, NA KUNIFANYA KIUMBE KIPYA LEO. NAOMBA UNIPE UWEZO WA KUUSHINDA ULIMWENGU NA KUUISHIA WOKOVU SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU.
ASANTE BWANA YESU KWA NEEMA YAKO, NA MSAMAHA WAKO.
AMEN.
Basi ikiwa umeisema sala hiyo ya Imani, fahamu kuwa Mungu anatazama moyo wako, na sio sala tu. Yupo mwanamke ambaye alikuwa na dhambi nyingi, lakini kwa jinsi alivyomaanisha tu mbele za Yesu, kabla hata hajaomba msamaha au kujieleza chochote, muda huo huo Bwana alimwambia “umesamehewa dhambi zako”. Hiyo ni kuonyesha kuwa Toba hasaa haipo katika maneno matupu tu, bali katika moyo.(Luka 7:36-50)
Na wewe pia ikiwa toba yako, imeambatana na kuachana na huyo mume/mke wa mtu, imeambatana na kuacha kutazama picha za ngono mitandaoni milele, imeambatana na kuacha kuishi na huyo girlfriend/boyfriend ambaye hamjaona naye.. Ujue kuwa msamaha kutoka kwa Bwana umeshaupokea.
Hivyo, kuanzia leo, anza kuishi Maisha ya kuukulia wokovu, na kama hukubatizwa unapaswa ubatizwe, Ikiwa utahitaji msaada huo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 0693036618/0789001312 tutakusaidia kwa neema za Bwana.
Bwana akubariki sana.
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.
Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?
Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?
SWALI: Huu mstari una maana gani ?
Mithali 20:12 [12]Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
JIBU: Utajiuliza ni kwanini haijasema “Sikio na jicho” Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili..badala yake inasema ..
Sikio lisikialo, na jicho lionalo, BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
Hii ni kuweka msisitizo katika kazi zao jinsi zinavyojitegemea…sikio haliwezi kuona, wala jicho kusikia, kwasababu kila moja limeundiwa mfumo wake tofauti wa kipekee..Lakini kutokufanana kwao haviwafanyi viwe na miungu miwili tofauti..bali ni Mungu yule yule mmoja aliyeviumba vyote.
Hata sasa tunapaswa tutambue kuwa Mungu ni Mungu anayeumba vitu katika mionekano tofauti tofauti..mmoja atamfanya mchina mwingine mwafrika, sio kwamba kuna itilafu au mapungufu katika jamii fulani ndio maana ikawa hivyo hapana.. ndivyo Mungu alivyotaka watu wake wasiwe na mionekano na maumbile yanayofanana, amependa tu iwe hivyo
Vilevile katika Kanisa Mungu ameweka vipawa mbalimbali..mwingine mwinjilisti, mwingine mwalimu, mwingine mchungaji..hata katikati ya hao wainjilisti au manabii bado kawatofautisha wote wasifanane..
Kutokuhubiri kwa kufoka au kwa utulivu kama yule hakukufanyi wewe usiwe na karama ile..
1 Wakorintho 12:4-6 [4]Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. [5]Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. [6]Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
Hivyo tuonapo tofauti hizi, ndani ya kanisa lake, au ulimwenguni tusinyoosheane vidole na kusema yule sio Mungu, maadamu tupo katika mstari ule ule wa imani, hatupaswi kushangaa sana au kulazimisha mambo yote yafanane..bali tukumbuke tu huu usemi..
Itambue nafasi yako, Mungu aliyokuchagulia, kisha isimamie hiyo kwa bidii kwasababu vyote ni kwa utukufu wake mwenyewe.
https://wingulamashahidi.org/wp-admin/post.php?post=18939&action=edit#
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?