Title September 2019

MBINGUNI NI WAPI?

Mbinguni ni mahali mbali sana na upeo wetu wa kufikiri, na umbali huo haupo katika mfumo wa kilometa, au maili hapana! bali kiufahamu…Katika miili hii ya damu na Nyama hatuwezi kufika mbinguni. Ni sawa uwaambie paka wote duniani au mbwa wote duniani, wajikusanye wafanye bidii wafike kwenye wafike kwenye kifaa kilichotengenezwa na wanadamu kinachoitwa satelite kilichopo kule juu sana mawinguni..

Unaona? jambo hilo haliwezekani..kwanini? kwasababu wao upeo wao upo mbali sana na upeo wa wanadamu…Ili wafike kwenye satelite kule mbinguni  ni sharti kwanza wawe wanadamu, wawe na ufahamu kama wa wanadamu ndipo waweze kufika kule.

Kadhalika na sisi tunahitaji kubadilishwa miili yetu, ifanane na malaika ndipo tuweze kufika mbinguni. Kwa jitihada zetu sisi kamwe hatuwezi kufika mbinguni, Malaika watakatifu walipo

Ubarikiwe!


Mada Nyinginezo:

NI UTHIBITISHO UPI UNAOONYESHA KUWA KUNA MBINGUNI NA KUZIMU?

JE! MBINGUNI KUTAKUWA NA KULA NA KUNYWA?

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?

KUCHEZA KARATA NI SAHIHI KWA MTU ALIYE MKRITO?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Dini ya kweli ni ipi?

Mpaka umefikia kuuliza hili swali, naimani ni mtu unayependa kuabudu kitu unachokifahamu..Na pia naamini unapouliza dini ya kweli ni ipi unamaanisha kuwa ni Imani ipi ya kweli..Leo duniani zipo dini zaidi ya 4300 zinazofuatwa na wengi, hiyo ni mbali na madhehebu na vikundi vidogo vidogo, vikihesabiwa na hivyo hata laki vinafika..Na kila moja inadai kuwa Mungu wake ni sahihi..Mpaka unashindwa kujua Mungu wa kweli yupo wapi,

Upo katika tovuti hii, ambayo ni ya kikristo, mfano nikikupa jibu la haraka kuwa ukristo ndio Imani sahihi, bila shaka unaweza ukaamini kuwa huyu mtu anataka kunivuta kwake. Vivyo hivyo ukienda na kwingine, Hivyo maneno matupi hata yakijaza dunia, hayawezi kubatilisha ukweli wa maneno matano tu.

Hivyo ikiwa kweli umekusudia kufahamu Dini ya kweli, na Mungu wa kweli, jambo ni rahisi, Mungu aliye Mungu wa kweli sikuzote huwa anajitetea mwenyewe na wala hajitetei…Hivyo kama umemaanisha kweli kumtafuta Mungu huyo tenga muda wako mwenyewe binafsi kisha piga magoti, halafu omba kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni, usipomaanisha hakuna kitu kinachoweza kukutokea mwambie Ee Mungu wa kweli jidhihirishe kwangu na nionyeshe njia ya kweli na dini ya kweli ya kukufikia wewe..

Ukishamaliza kuomba basi wewe tulia, njia atakayoileta mbele yako ifuate, mimi siwezi kukuelezea atakujibuje jibuje lakini akikujibu utafahamu kuwa amekujibu kwa mambo yatakayofuatana na wewe baada ya hapo.

Fanya hivyo na Mungu wa kweli bila shaka atajidhihirisha kwako, na huyo ndiye umfuate kwa moyo wako wote na kwa akili zako zote na kwa roho yako yote.

Ubarikiwe.


 

Mada Nyinginezo:

DINI NI NINI?.

NI UTHIBITISHO UPI UNAOONYESHA KUWA KUNA MBINGUNI NA KUZIMU?

JE! KUBET NI DHAMBI?

EPUKA MUHURI WA SHETANI.

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Dini ni nini, na Imani ya kweli ni ipi?

Dini ni nini? Dini ya kweli ni ipi? na Imani ya kweli ni ipi?

Dini ni tendo linalotokana na Imani fulani (mambo ya rohoni), pale tu mtu anapoamini uwepo wa Mungu au hata uwepo wa shetani au hata kitu chochote kisichoonekana cha kuabudiwa basi hapo hapo dini inazaliwa, ndipo hapo utaona mtu anajiwekea  miiko Fulani ya kufuata au utaratibu Fulani au ustaarabu Fulani kwamfano wanaoamwamini Buddha utaona wanao taratibu zao za kufuata ili kumwabudu mungu wao  ipasavyo ndipo hapo utakuta ni lazima wote wavae mavazi Fulani, au wapitie madarasa Fulani, au waishi maisha Fulani ya kujinyima au kutokushirikiana na jamii Fulani ya watu au kufunga, au kutokula aina Fulani ya vyakula n.k sasa hiyo ndiyo inayoitwa dini..

Vivyo hivyo na katika ukristo, mtu yeyote mwenye imani ya kweli ya YESU Kristo ni lazima atakuwa na kiwango Fulani cha dini ndani yake, kwamfano ukiwa mkristo ni lazima utajikuta  wewe mwenyewe unajijengea utaratibu wa kuomba kila siku, utajikuta unajijengea utaratibu wa kufunga mara kwa mara, licha tu ya biblia kuagiza lakini utajikuta unahudhuria ibada kanisani kila wakati, utajikuta unajijengea utaratibu wa kutoa sadaka na kuwasaidia na wengine n.k.…Na ndio maana biblia inasema..

Yakobo 1:26 “Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.

27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.”

Hivyo dini ya kweli ni ipi? Ni hiyo hapo juu kwenye mstari wa 27..Lakini sasa hiyo  haimpi tiketi ya moja kwa moja kwenda mbinguni , bali inamrahishia tu njia ya kwenda mbinguni..tofauti na Imani nyingine kwao kushika dini ndio kuokoka, lakini katika ukristo usipomwamini YESU KRISTO na kuoshwa dhambi zako katika damu yake hata kama unashika dini vipi mbinguni huwezi kwenda…

Unaweza ukawa unafunga lakini kama maisha yako yapo mbali na Kristo kuzimu utakwenda, unaweza ukawa unahudhuria ibada kila siku na kushika mambo yote unayoambiwa kanisani kwako kufanya lakini kama hauna Roho Mtakatifu ni bure…Tofauti na dini nyingine ambao kwao  dini ni kitu cha kujivunia..

Hivyo kwa ufupi Dini ni njema kama itakuwa imeambata na imani ya kweli ipasavyo, ni sawa na shule yenye maabara na walimu wazuri, inamjengea mwanafunzi mazingira mazuri ya kufaulu siku za mwisho lakini shule pekee haimfanyi mwanafunzi afaulu mitihani kama hatakuwa na bidii yake binafsi..

Baada ya kujua dini ni nini na dini ya ukweli ni ipi…Ni vizuri kujua Imani ya kweli ni ipi?..Imani ya kweli ni ile iliyopo katika kumwamini Yesu Kristo kama mwana wa Mungu na aliyetumwa kuja kuwaokoa wanadamu. Hiyo ndiyo imani ya kweli..Imani nyingine tofauti na hiyo ni imani ya uongo na unayopotosha na kupeleka watu mautini.

Hivyo huu Si wakati wa kijivunia dini tena…bali kujivunia wokovu katika Yesu Kristo…Hivyo kama hujaokoka na kuingia katika Imani ya kumwamini Yesu Kristo..Bado hujachelewa ingawa mlango wa Neema upo karibuni kufungwa hivyo mgeukie Kristo leo kwa kutubu dhambi zako zote na kuoshwa kwa damu yake, naye atakusamehe na kukurehemu.

Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

KUNA TOFAUTI GANI KATI YA SALA NA DUA?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

HADITHI ZA KIZEE.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

SWALI LA KUJIULIZA!

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

YESU KWETU NI RAFIKI

Yesu kwetu ni rafiki, hwambiwa haja pia;tukiomba kwa Babaye, maombi asikiyaLakini twajikosesha, twajitweka vibaya; kwamba tulimwomba Mungu, dua angesikia.

Una dhiki na maonjo? Una mashaka pia.Haifai kufa moyo, dua atasikia.Hakuna mwingine mwema, wa kutuhurumia;atujua tu dhaifu; maombi asikia.

Je hunayo hata nguvu, huwezi kwendelea,ujapodharauliwa, ujaporushwa pia.Watu wangekudharau, wapendao dunia,hukwambata mikononi, dua atasikia.


Je! unajua historia ya wimbo huu?

Joseph Scriven alizaliwa mnamo 1819 katika familia ya kitajiri huko Banbridge, County Down, Ireland. Alihitimu digrii yake kutoka Chuo cha Trinity, huko Dublin mnamo 1842. Mpenzi wake alizama kwenye maji na kufa kwa bahati mbaya mnamo 1843, usiku kabla ya kuolewa.

 Mnamo 1845, akiwa na umri wa miaka 25, aliondoka nchi yake ya asili na kuhamia Canada, na kukaa Woodwood, Ontario. Alibaki Canada kwa muda mfupi tu baada ya kuugua, lakini akarudi mnamo 1847

Mnamo 1855, alipokaa na James Sackville huko Bewdley, Ontario, kaskazini mwa Port Hope, alipokea habari kutoka kwa Ireland ya mama yake kuwa mgonjwa sana. Aliandika shairi la kumfariji mama yake inayoitwa “Omba bila Kukata tamaa”. Baadaye iliwekwa kwa muziki na ikabadilishwa jina na Charles Crozat Converse, ikawa wimbo wa “Yesu kwetu ni Rafiki”. Scriven hakuwa na dhamira yoyote wala ndoto kwamba shairi lake litakuja  kuchapishwa kwenye gazeti na baadaye kuwa wimbo unaopendwa kati ya mamilioni ya Wakristo ulimwenguni.


Ni nini tunaweza kujifunza kwa Joseph Scriven? Faraja kidogo kwa mama yake imekuwa faraja kwa mamilioni ya watu ulimwenguni…Lolote ufanyalo! au Kidogo umfanyiacho mtu aliye mnyonge, na aliye katika mashaka kinaweza Mungu anaweza kukifanya kuwa msaada kwa mamilioni ya wanyonge wengine mahali pengine.


Mada Nyinginezo:

JE! KUBET NI DHAMBI?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni udhaifu gani ulikuwa katika macho ya Lea mke wa Yakobo?

SWALI: Mwanzo 29:16 “Labani alikuwa na binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli. 17 Naye Lea macho yake yalikuwa DHAIFU, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso. 18 Yakobo akampenda Raheli akasema, Nitakutumikia miaka saba kwa kumpata Raheli, binti yako mdogo.”

Hapo Anaposema macho ya Lea yalikuwa dhaifu:Ni Udhaifu wakutokuona mbali au ni udhaifu wa namna gani huo??


JIBU: Biblia haituambii macho yake yalikuwa ni dhaifu kwa namna gani, kwamba ni makengeza, au yaliyolegea, au yenye kasoro ya kimaumbile kwamba ni makubwa sana au madogo sana au yanayoona karibu au mbali, hatujui lakini tunachojua ni kuwa alipofananishwa na mwenzake, Raheli alionekana ni mzuri kuliko yeye,…

Lakini Mungu hakuangalia hilo kama kigezo cha kuliunda taifa la Israeli, kwamba ampendelee Raheli zaidi ya Lea katika wana, kisa tu yeye ni mzuri wa sura na kwamba Yakobo kampenda zaidi…hapana kwanza utaona Lea ndiye aliyepewa uzao mkubwa zaidi, karibu nusu ya makabila yote ya Israeli yalitoka kwake isitoshe lile kabila la Bwana wetu Yesu Kristo kabila la YUDA lililoshinda makabila yote lilitoka kwa Lea…

Hivyo hiyo inatufundisha pia kutokukubaliwa na watu haimaanishi kuwa hatujakubaliwa na Mungu, Yabesi alikuwa ni mtu aliyezaliwa katika huzuni mpaka mama yake akamwita jina hilo ambalo lilimaanisha huzuni, Lakini Yabesi alijitahidi kuishi katika amani kwa heshima, kuliko ndugu zake wote, mpaka ikafikia wakati akamuomba Mungu dua amfanikishe katika mambo yake na Mungu akaisikia dua yake, mpaka habari yake leo hii tunaisoma katika biblia (1Nyakati 4:9-10,) …Hivyo ulemavu wowote mtu alionao haimaanishi kuwa hawezi kuwa jemadari katika ufalme wa mbinguni.

Ubarikiwe.


 

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA YABESI.

YESU MPONYAJI.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

JIPE MOYO.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

UNYAKUO.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni dhambi kuangalia movie?

Kama mkristo ili uweze kuenenda  kikamilifu katika safari yako ya wokovu hapa duniani bila dosari zozote zisizokuwa na sababu, ipo mistari miwili ya kuzingatia..

Wa kwanza ni huu:

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Na wa pili ni huu

Tito 2:11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;

12 nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate KUISHI KWA KIASI, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;

Tukiweza kutembea na kanuni hizo mbili yaani kuishi kwa Kiasi na kufanya jambo lolote kwa kumshirikisha Mungu, basi tuwe na uhakika kuwa njema zetu zitanyooka, Sasa tukirudi kwenye swali lililoulizwa kuhusu picha za video (movies), hatuwezi kusema moja kwa moja usiangalie kabisa, ni kweli hakuna asiyejua movie nyingi hazina maudhui yoyote ya kumfaa au kumjenga mkristo lakini bado hatuwezi kusema ni zote, ni kama tu vipindi vya TV vipo vilivyo vizuri na vipo vilivyo vibaya, hivyo hatuwezi kumwambia mtu asiangalie TV kabisa kwasababu kuna vipindi vibaya vingi, hapo tutakuwa tumepoteza shabaha ya kulitibu tatizo..kwasababu kwenye TV pia kuna vipindi vya mahubiri na taarifa ya habari ambavyo kwa namna moja au nyingine vinaweza kumjenga mtu kiroho au kumfunza au kumjuza.

Lakini tukiwa na kiasi, inamaana kuwa hata tukitazama movie tutazama kwa kiasi tena zile tu ambazo zinaonekana kuwa na manufaa kwa mkristo, lakini leo hii utaona mtu anatazama series, kuanzia asubuhi mpaka jioni, hana muda wa kusali, hana muda wa kujisoma biblia, hana muda wa kwenda kanisani, hana muda wa kwenda fellowship, sasa hapo hata kama movie hiyo inayo maadili kiasi gani, lakini kwa kukosa tu kile kitu kinachoitwa kiasi tayari imekuwa ni kikwazo kwake na dhambi..

Vilevile utamwona mwingine anatazama tamthilia za mapenzi, au movie zilizojaa mambo maovu maovu tu, hajui kuwa moyo wa mwanadamu unatabia ya kujazwa na kile kinachofanywa, au kinachozungumzwa au kinachowazwa muda mrefu, kwa mfano ukiwa mtu wa kutafakari Neno la Mungu kila saa na kila wakati basi lile Neno linakuwa sehemu ya maisha yako..Vivyo hivyo ukiwa ni mtazamaji wa movie ambazo hazina vimelea vyovyote vya ki-Mungu ndani yake basi utakuwa mtu wa kufuatana na hivyo unavyovitazama,..Huko huko ndipo roho za uzinzi zinapozaliwa, na uuaji, na ulevi na matusi n.k…Na hiyo yote ni kwasababu hujazingatia lile Neno linalosema lolote mfanyalo kwa Neno au Kwa tendo fanyeni yote kwa jina la Yesu Kristo…Yaani kwa lugha nyepesi kufanya kwa jina la Yesu Kristo ni kabla hujafanya unaangalia je! Hichi ninachokitazama kina umuhimu gani katika maisha yangu ya rohoni…kama hakina  unakiacha, kama kinayo unakitazama, huko ndio kufanya kwa jina la YESU.

Ukiweza kutembea na mistari hiyo miwili basi hakuna jambo lolote litakalokuwa dhambi kwako, sio movie, sio radio, sio tv, sio simu, sio computa n.k.

Bwana akubariki.


 

Mada Nyinginezo:

JE! KUBET NI DHAMBI?

KUCHEZA KARATA NI SAHIHI KWA MTU ALIYE MKRITO?

JE! KUCHORA TATTOO NI DHAMBI?

JE NI SAWA KWA MKRISTO KUUZA MAZAO YA KUTENGENEZEA POMBE KAMA VILE MTAMA?

NI UTHIBITISHO UPI UNAOONYESHA KUWA KUNA MBINGUNI NA KUZIMU?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO.(MATHAYO 8:21)?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Roho za Wanyama zinakwenda wapi baada ya kifo? Je! Watafufuliwa?

JIBU: Uumbaji wa Mungu umegawanyika katika sehemu kuu mbili…
 
Sehemu ya kwanza: Ni Viumbe vya kimbinguni …Viumbe hawa wa kimbinguni nao wamegawanyika katika sehemu kuu mbili, nao ni malaika na wanadamu…Malaika wanaishi mbinguni, na wanadamu wanaishi duniani…Ingawa asili yao wote ni mbinguni..Ndio maana kuna usemi usemao sisi ni wasafiri tu, ulimwenguni sio kwetu..(Waebrania 11:13-15 na 1Petro 2:11), Wanadamu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu na sura ya Mungu,
 
Kwa kawaida hata mtu akiwa na sura inayofanana sana na yako, ni dhahiri kuwa huyo anaweza kuwa mwanafamilia au mwenye tabia zinazoendana sana na wewe…Na kama ni mwanafamilia basi lolote litakalotokea aidha kifo, au sherehe, au chochote kile ni lazima familia yako ihusike,..Na sisi wanadamu kwasababu tunafanana na Mungu basi ni familia ya Mungu na hivyo tukifa tunamrudia Baba mkuu wa familia yetu, aliyetuzaa yaani Mungu. Uwe mwovu uwe mwema, hilo haliepukiki maadamu una umbo na sura ya mwanadamu…tayari asili yako ni kwa Mungu.
 
Na sehemu ya Pili ya uumbaji wa Mungu ni viumbe vya kidunia, ndio Wanyama, samaki, ndege, miti, hivi vyote navyo vina uhai. Lakini hivi havijaumbwa kwa mfano wa Mungu, Mungu hafanani na Wanyama…Mungu hana mkia kama simba wala hana pembe, wala hana matawi na mizizi kama miti ilivyo…
 
Hivi vimeumbwa kutoka katika ardhi soma (Mwanzo 1:12 na 1:24), hivyo familia yao ni katika ardhi…na vikifa haviendi popote Zaidi ya ardhini..kwasababu duniani ndio kwao…Vimeumbiwa udunia, havina mahali pa kwenda baada ya hapa…Ndio maana havijui kama kuna kitu kinachoitwa Kesho, wala havitafakari mwaka jana kulitokea nini na Kesho kutatokea nini, na wala havitafakari vipo wapi, hiyo ni kwasababu havisafiri vipo nyumbani kwao ambapo ndipo hapa duniani. Na kwasababu nyumbani kwao ni hapa duniani na vimetolewa kutoka katika ardhi kama biblia inavyosema basi vikifa habari yao ndio imeishia hapa hapa…Mnyama akifa habari yake ndio imeishia hapa hapa, hawana ufufuo, mti ukifa habari yake ndio imeishia hapo hapo, hakuna ufufuo, bakteria akifa habari yake ndio imeishia hapo hapo hakuna ufufuo na viumbe vingine vyote tofauti na wanadamu.
 
Lakini mtu akifa roho yake inamrudia Muumba wake aliyeko mbinguni, kwa Baba wa familia yake. Na kuhukumiwa na yeye, ikiwa amestahili uzima basi ataishi milele, akiwa hajastahili basi anaangamizwa milele,.
 
Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI KUNA VIUMBE VINAVYOISHI SAYARI NYINGINE (ALIENS)?

NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU?

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “ENENDENI ULIMWENGUNI MWOTE,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE”?

NI NANI ALIYEIDHARAU SIKU YA MAMBO MADOGO?.

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni kweli Bwana alimaanisha hatutaonja mauti kabisa tukimwamini?(Yohana 11:25)

Naomba ufafanuzi wa huu mstari Yohana 11:25-26″  Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo? “

hususani hapo anaposema (naye kila aishiye na kuniamini mimi hatakufa kabisa hata milele.) ana maana gani?


JIBU: Tunajua Yesu Kristo ndio ule mti wa uzima uliozungumziwa katika bustani ya Edeni kule mwanzo kwamba ukila matunda yake utaishi milele, na matunda yake leo hii tunayajua ni NENO lake, na neno lake ndio UZIMA wenyewe na siku zote palipo na uzima hapana kifo. 

Tukichunguza katika mstari huo tunaona Bwana Yesu alizungumza kwa watu wa aina mbili tofauti,

Aina ya kwanza: ni “yeye aniaminiye mimi ajapokufa atakuwa anaishi”. Hili ni kundi ambalo linajumuisha watu wote waliomwamini Bwana watakaokufa watakuwa wanaendelea kuishi katika paradiso wakingojea ufufuo wa mwisho lakini kundi hili halikufanikiwa kufikia utimilifu wa imani ya kumwamini Mwana wa Mungu, hivyo basi itawapasa wafe lakini kwa kuwa walimwamini Mungu kwa sehemu ya imani watakuwa wanaendelea kuishi huko paradiso. Na ni watu wengi leo hii wanakufa katika hali hii.

Aina ya pili : “naye kila aishiye na kuniamini mimi hatakufa kabisa hata milele”. Hili ni kundi lililofikia imani timilifu ya kumwamini na kumjua sana mwana wa Mungu inayozungumziwa katika kitabu cha…

 (waefeso 4:13”hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; )


hata kufikia hatua ya kushinda kifo na mauti. Mfano wa watu kama hawa tunawaona kama Henoko, Eliya, na kanisa ambalo litakuja kunyakuliwa siku ya mwisho. Hata leo hii inawezekana mtu kutokuonja mauti kabisa tukimwamini mwana wa Mungu (YESU KRISTO) katika utimilifu wote, tutachukuliwa juu hatutakufa kama  ilivyokuwa kwa Eliya na Henoko, maana biblia inasema Eliya alikuwa ni mtu mwenye tabia sawa na sisi lakini kwa bidiii na kwa imani akachukuliwa juu. Mahali pengine Bwana Yesu alisema katika…

 Yohana 8:51 “Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.

52 Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.

53 Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?

54 Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. ” mstari huu unaelezea jinsi Bwana alivyokuwa akijaribu kuwaeleza juu ya jambo hili lakini wayahudi hawakutaka kulipokea.

Sehemu nyingine Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake,

Mathayo 16:28″Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake. “

leo hii zipo shuhuda nyingi duniani za watu waliochukuliwa na Bwana pasipo kuonja mauti lakini shetani anataka kuwafanya watu waamini kuwa hilo jambo haliwezekani kwamba ni manabii tu wa zamani ndio walikuwa na uwezo wa kufanya hivyo siku hizi hayo mambo hamna. usidanganyike katika kila kizazi Bwana ana watu wake wanaoshinda. Hivyo maneno haya yanatupa changamoto ya sisi kuongeza uhusiano wetu na Mungu kwasababu hata kanisa litakalokuja kunyakuliwa halitaonja mauti na ni lazima liwe na hiyo imani swali je! wewe unayo? kama hauna ndio wakati wa kuitafuta sasa maana Bwana Yesu mwenyewe alisema

Luka 18:8”……walakini atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”

kwahiyo ni lazima aione imani kwanza ndipo aje hivyo tuitafute hii imani vinginevyo hatutakwenda kwenye unyakuo kumbuka ni Kristo anayetungojea sisi tuwe wakamilifu ndipo aje kutuchukua na sio sisi tunayemngojea yeye.

Mungu akubariki.


 

Mada Nyinginezo:

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO.(MATHAYO 8:21)?

KUNA HUKUMU ZA AINA NGAPI?

KUPAYUKA PAYUKA KUNAKOZUNGUMZIWA KWENYE BIBLIA NDIO KUPI?

MWANZI ULIOPONDEKA.

HADITHI ZA KIZEE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUONGEZEKA KWA MAARIFA.

Habari ya uzima wako mtu wa Mungu, katika hizi siku za mwisho na za hatari kama bado upo nje ya wokovu jiulize sana, Na kama bado unaishi kwa kushikilia mapokeo ya kidini jifikirie mara mbili..Kwasababu biblia inatuambia dalili nyingine kubwa inayofungua ukarasa wa siku za mwisho ni Kuongezeka kwa maarifa.. Na maarifa ya kwanza biblia iliyomaanisha ni maarifa ya rohoni, lakini tunajua mambo ya mwilini sikuzote huwa yanafunua yale ya rohoni hivyo tunapoona maarifa yakiongezeka duniani kwa kasi basi tunajua kuwa ule wakati umeshawasili . Sehemu nyingine biblia inatuambia tujifunze katika ‘Maumbile, yaani vitu vya asili (NATURE)’ 1Wakorintho 11:14..

Ni wazi kuwa vitu tunavyoviona karibu vyote ulimwenguni kwa namna moja au nyingine vinatuhubiria injili pengine pasipo hata sisi kujua..Tunamwona Bwana Yesu alitumia mifano mingi ya asili kutufundisha sisi, kwamfano aliposema watafakarini ndege ni mfano wa maumbile ya asili, aliposema tena

“Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?”(Luka 12:54-56)

Unaona Yote hayo ni maumbile yakituhubiria injili..

Vivyo hivyo biblia pia inaposema Maarifa yataongezeka katika siku za mwisho, inamaanisha tunapaswa tujifunze katika hayo, kwasababu na rohoni ndivyo ilivyo.. tunasoma hilo katika

Danieli 12:4 “Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, NA MAARIFA YATAONGEZEKA.”

Hakuna mtu asiyejua ulimwengu wa sasa ni ulimwengu wa ushindani, ili uweze kuishi au kufanikiwa ni lazima uwe na akili timamu vile vile uwe mshapu, na hiyo yote ni kwasababu teknolojia iliyopo sasa ndiyo inayotufanya tuwe watu wa namna hiyo..

Embu jaribu kutafakari, siku hizi unaweza kusoma tangazo kwenye gazeti, au internet, linasema linahitaji wafanyakazi Fulani watakaojaza nafasi za wafanyakazi Fulani walioachishwa kazi,..na linawahitaji ndani ya saa 5-7 wawe wameshafika eneo la shirika kwa ajili ya mahojiano na watakaokidhi vigezo wataanza kazi mara moja Eneo husika ni Daresalaam..

Ukijiangalia wewe upo Kigoma kwa wakati huo, na mwingine yupo Bukoba, na mwingine Afrika ya kusini…. Je! Kwa akili ya harakaharaka unadhani usafiri utakao tumika hapo ni upi ili kufika eneo la kazi?, Je! Ni miguu?, au Baiskeli au gari?..Ni wazi kuwa hapo itahitajika kifaa kinachokwenda kasi zaidi nacho si kingine zaidi ya ndege tu,..Ukitumia usafiri mwingine utachelewa tu..

Sasa ndivyo itakavyokuwa kwa habari ya unyakuo. Kipindi kifupi kabla ya Unyakuo, Bwana atawaita watu wake kwa sauti nyingine kuu..Na sauti hiyo inajulikana kama Sauti ya Malaika mkuu ukisoma (Ufuno 10:3) utaliona hilo, Hicho ndicho kipindi ambacho watu wote waliovuguvugu na walio moto wataisikia hiyo sauti kwa mahubiri ya kipekee yatakayokuwa yanafundishwa na watumishi wa Mungu waaminifu duniani kote..Na wito huu utakuwa ndani ya Muda mchache sana, Bwana Yesu alitumia mfano wa wale wanawali 10, kueleza tukio hilo litakavyokuwa ambapo tunasoma 5 walikuwa werevu na 5 wapumbavu, pindi wote waliposikia sauti ya Bwana harusi tokea mbali, wote walinyanyuka kuzitengeneza taa zao, lakini wale wapumbavu walipoona wameishiwa mafuta walijaribu kuwaomba wale werevu wawapunguzie walau hata kidogo, lakini wale werevu waliwaambia hayatutoshi sisi na nyie, ni heri mkanunue ya kwenu ndani ya hichi kipindi kifupi kabla Bwana harusi hajatokea..

Lakini kwa bahati mbaya walikuwa wameshachelewa waliporudi walikuta mlango umeshafungwa.

Sasa ndivyo itakavyokuwa ndani ya hicho kipindi kifupi, Sauti kuu italia karibia ulimwengu mzima, tunapozungumza inaweza ikawa siku yoyote kuanzia sasa, Na watu watafahamu kabisa kuwa Bwana siku yoyote anawanyakuwa watu wake, lakini kwa bahati mbaya wakati huo wapo watu ambao watakuwa tayari wapo nyuma ya teknolojia ya kimbinguni,..Wakati wenzao wanatumia kifaa cha ndege kumfikia Mungu wengine watakuwa bado wapo kwenye miguu wengine bado kwenye baiskeli, wengine kwenye gari…

Na hiyo itawachelewesha kufikia malengo yao katika hicho kipindi kifupi sana..Na siku ya kuitwa juu mbinguni itakapofika Mlango utakuwa umeshafungwa, hakutakuwa na udahili tena..Hapo ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno kama biblia inavyosema utakapoona mbona Fulani niliyemjua hayupo, mbona huyu nilikuwa ninakwenda naye kanisani hayupo, wewe ndiye utakayeumia zaidi kuliko Yule mlevi wa Bar..kwasababu mlevi wa Bar hataamini chochote.

Na ndio maana ni muhimu tuyajue hayo kwamba suala la kwenda mbinguni sio jambo la kuotea tu, bali ni jambo la kimkakati, na mkakati huo ulishaanza tangu zamani na bado hata sasa unaendelea. Leo hii unaambiwa tafuta Roho Mtakatifu maana huyo ndio muhuri wa Mungu na ndiye atakayekuongoza na kukufanya kuwa mkamilifu unasema dhehebu langu linanitosha..Unapohubiriwa juu ya mambo ya ufalme wa mbinguni, unasema sisi tupo duniani, hatuishi mbinguni, injili unazozipenda ni za kuambiwa njoo pokea, unapoambiwa tengeneza mambo yako sasa hizi ni nyakati za hatari, unasema mbona hakuna dalili yoyote ya mwisho wa dunia, lakini biblia inasema siku hiyo itakuja katika siku ambazo zinaonekana kuwa za amani ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla.(1Wathesalonike 5:3).

Hivyo kama ikitokea leo hii Injili hiyo ya ajabu inahubiriwa duniani kote, na bado upo vuguvugu, basi hesabu kuwa utaachwa siku ile, na utabaki tu hapa duniani kwa ajili ya dhiki kuu…Tubu leo, ili saa ile itakapokaribia uwe mfano wa wale wanawali werevu waliokuwa na mafuta ya ziada katika taa zao. Na maarifa ya kutosha kwa ajili ya kumlaki BWANA MAWINGUNI..

Ubarikiwe.

Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Bwana atakubariki.


Mada Nyinginezo:

DANIELI: MLANGO WA 12.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

MIHURI SABA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.


Rudi Nyumbani:

 

Print this post

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.

Shalom mtu wa Mungu, karibu tutafakari maandiko pamoja.
 
Biblia inasema katika Kitabu cha Yohana 15:16 kwamba “Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni”
 
Tumepewa jukumu la kuzaa matunda, na matunda hayo yamegawanyika katika sehemu kuu mbili, sehemu ya kwanza ni matunda ya Haki, ambayo hayo yanatokana na utakatifu, tunayasoma hayo katika
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
 
Na aina ya pili ya Matunda, ni matunda ya KAZI, ambayo hayo yanatokana na kuwaleta watu kwa Kristo,
 
Wafilipi 1:21 “Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
 
22 Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui.”
 
Hivyo Kristo ametuweka tuzae aina hizi mbili za matunda…Matunda ya HAKI na Matunda ya KAZI..Hivi viwili vinakwenda pamoja…Na vyote vinahitaji Mafuta ya Roho Mtakatifu ili viweze kufanyika. Ili tuwe watakatifu tunahitaji Mafuta ya Roho Mtakatifu…Kwasababu kama jina lake lenyewe lilivyo..Roho Mtakatifu, hivyo kila ampataye yeye ni lazima atakuwa mtakatifu tu.
 
Kadhalika ili tuweze kuleta matunda mengi kwa Kristo tunamhitaji Roho Mtakatifu, kwasababu yeye ndiye anayehusika katika kumshawishi mtu ndani ya moyo wake amgeukie Kristo.. 1 Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu”
Na leo tutajifunza umuhimu wa Roho Mtakatifu katika kuzaa matunda katika hizi siku za mwisho.
Kazi ya kuwavuta watu kwa Kristo imefananishwa na kazi ya uvuvi…Sharti ni kwamba ili mtu akavue samaki ni lazima atimize masharti makuu 5..
 
Sharti la kwanza ni lazima awe na mtumbwi unaoelea, sharti la pili ni lazima awe anajua kuogolea, sharti la tatu ni lazima awe na nyavu au ndoano, sharti la 4 Ni lazima aende usiku na sharti la 5 na la mwisho ni lazima awe na TAA..Akitimiza masharti hayo 5 basi ni lazima apate samaki..hawezi kukosa chochote aendapo anavua baharini…
 
Masharti hayo hayo pia yanatumika katika roho kwa uvuvi wa watu…
 
Sharti la kwanza: Kama vile mvuvi ni lazima awe na mtumbwi unaoelea na ni lazima akae juu ya huo mtumbwi ili aweze kuvua…vivyo hivyo katika Uvuvi wa watu ni lazima mtu awe juu ya Mtumbwi unaoitwa YESU KRISTO, na ni lazima mtu awe juu ya huo mtumbwi sio mbali au nje ya huo mtumbwi…huko nje ni kwa watu wasiomjua Mungu, ulimwengu unafananishwa na bahari ambayo imejaa watu wasiomjua Mungu ambao wanahitajika kuvuliwa..Hivyo haiwezekani mtu aliye nje ya Kristo kuwahubiria watu waje kwa Kristo kama vile ilivyo ngumu mvuvi kuwa nje ya mtumbwi na kuvua samaki.
 
Sharti la pili: Ni lazima mvuvi awe anajua kuogelea kabla hajaenda kuvua samaki…awe na uwezo endapo ikitokea ajali akaanguka ghafla majini awe na uwezo wa kurudi tena mtumbwini…sio endapo Kazama ndio anapotelea huko moja kwa moja…Kadhalika na mvuvi wa Roho za Watu ni lazima awe na uwezo wa kujihadhari na dunia, kwasababu dunia ni kama bahari, ukizama na ukiwa hujui namna ya kujitoa huko unazama moja kwa moja na kufia huko…Kwahiyo Ni kama tunaonywa kamwe tusidhubutu kwenda kuhubiri injili kama tunajua hatujaacha sisi wenyewe mambo ya ulimwengu huu, kama tunajua hatuwezi kuushinda na kujinusuru na ulimwengu…ni afadhali tusiende kuhubiri injili kabisa kuliko kwenda na kuzama huko… kwasababu endapo tukianguka tunakuwa tumeanguka moja kwa moja hakuna kurudi tena..
 
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
 
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa”
 
Sharti la Tatu: Ni lazima mvuvi awe na ndoano au nyavu…Ndoano au nyavu zinawakilisha Neno la Mungu, pamoja na ishara na miujiza…Vitu hivi biblia inasema waaminio wote vitaambatana nao…Ni lazima tulifahamu Neno ndipo tuende kuwahubiria wengine…
 
Sharti la Nne: Ni lazima mvuvi aende usiku kuvua, wavuvi wote wanaomaanisha kupata samaki huwa hawaendi mchana kwani wanajua hawatapata kitu, ni lazima aende usiku, kadhalika hata wakati huu wa sasa tunapaswa tuende ulimwenguni kote kulikojaa giza…Matendo ya dhambi yote ni matendo ya giza, na dunia yote imejaa giza kutokana na dhambi za wanadamu…lakini leo Utashangaa mtu anapambania awe mhubiri kanisani kila siku, lakini hataki kwenda mitaani mahali ambapo makahaba wapo, mahali penye giza…tukihubiri kanisani mahali ambapo kuna mwanga ni sawa tunaingia na mshumaa ndani ya nyumba ambayo tayari ina bulb inayowaka sana..Hivyo ni lazima tuenda na mitumbwi yetu, na nyavu zetu sehemu zenye giza mbali sana huko kuvua roho za watu. Na sisi wenyewe tukijihadhari tusipotelee huko.
 
Na Sharti la Tano Na la mwisho: Ni lazima mvuvi aende na TAA..Nyavu peke yake haitoshi kuwaleta samaki, ndoano peke yake haitoshi inahitajika taa…Wataalamu wa masuala ya uvuvi wanasema wakati wa usiku samaki wanapenda kufuata mahali penye mwangaza, hivyo wavuvi wengi hutwaa taa zao juu na kwenda nazo vilindini na hivyo samaki wanapoiona ile Nuru wanaisogelea na hivyo kunaswa…Na sisi tunahitaji Taa yenye Mafuta ili kuwavuta samaki wengi kwenye nyavu zetu, NA Mafuta yanawakilisha Roho Mtakatifu. Hivyo tunahitaji Roho Mtakatifu sana ili Taa zetu ziwe zinawaka sana, katika dunia hii ya giza ili waovu waonapo wamgeukie Bwana.
 
Wafilipi 2:15 “….mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao MNAONEKANA KUWA KAMA MIANGA KATIKA ULIMWENGU”
 
Ukiwa na Mtumbwi, ukiwa na ndoano, ukiwa na nyavu, na ukiwa na ujuzi wote wa kuogelea, kama huna TAA ni kazi bure…utakuwa umwekwenda baharini kubarizi tu na si kuvua..Kadhalika hata tukiwa na tumempa Bwana Maisha yetu, hata tukiwa tunalijua Neno vizuri na kujiepusha na dunia vizuri kama hatuna Roho Mtakatifu, kamwe shughuli ya kuwaleta wengine kwa Kristo itakuwa ngumu sana kwetu.
Hivyo leo tunajifunza tumtafute sana Roho Mtakatifu ajae ndani yetu, kwa maana pasipo yeye hakuna mtu yeyote atakaye vutwa kwa Mungu.
 
Yohana 6: 44 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Bwana akubariki sana. Wahubirie na wengine habari njema, waujue wokovu wa Bwana Yesu.
 
Bwana akubariki.



Mada nyinginezo:

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.

MUNGU MWENYE HAKI.

MLINZI, NI HABARI GANI ZA USIKU?

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

NGUVU YA UPOTEVU.


Rudi Nyumbani:

Print this post