Title March 2022

Yohana Mbatizaji alibatiza watu kwa jina gani?.

Tunasoma Matendo 2:38, kuwa watu walibatizwa kwa jina la YESU. Lakini biblia haijataja Yohana Mbatizaji alitumia jina gani kumbatizia Bwana Yesu, Pamoja na makutano waliomjia ili awabatize?.


Jibu: Yohana Mbatizaji hakutumia jina lolote katika Ubatizo. Ubatizo wake ulikuwa ni ubatizo wa Toba, ambapo baada ya watu kusikia mahubiri yake na kutubu, aliwazamisha kwenye maji mengi kwa ishara ya kuoshwa dhambi zao kwa maji. (Hakuna jina lolote lililohusika).

Lakini baada ya Bwana Yesu kuja, maandiko yanasema mambo yote tunayafanya kwa jina lake (Jina la Yesu).

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO au KWA TENDO, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Umeona hapo?.. anasema lolote lifanyikalo kwa “Neno” au kwa “Tendo”.

Mfano wa mambo yafanyikayo kwa neno, ni kuomba, kutoa pepo, kubariki, kuimba, kutoa unabii n.k Hayo yote tunayafanya kwa jina la YESU. Ndio maana leo Pepo linatoka kwa jina la Yesu, vile vile tunapoomba tunatumia jina la YESU, n.k Mambo haya hapo kabla hayakuwepo, kwamba pepo linamtoka mtu kwa kutaja tu jina la mtu Fulani!.. Lakini yamekuja kuwezekana kwa mmoja tu, ambaye ni Bwana YESU, kwa jina lake tunafanya yote!.

Lakini sio hilo tu, bali maandiko yanasema pia, lolote tufanyalo kwa TENDO. Sasa mfano wa tendo, ndio huo Ubatizo!.) Kwamba tunazamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU. Yohana hakutumia jina la Yesu, ndio maana ubatizo wake ukakoma, lakini ubatizo wa jina la Yesu umedumu siku zote!! Na ndio unaoondoa dhambi!.

Matendo 19:1 “Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;

2 akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.

3 AKAWAULIZA, BASI MLIBATIZWA KWA UBATIZO GANI? WAKASEMA, KWA UBATIZO WA YOHANA.

4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu

5 WALIPOSIKIA HAYA WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU.

6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.”.

Umeona hapo?. Watu hao walirekebisha ubatizo wao, wakabatizwa tena kwa jina la BWANA YESU

Na sisi leo hii hatuna budi kubatizwa kwa jina la Bwana Yesu ili tupate ondoleo la dhambi.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Ubatizo ni nguzo muhimu sana na ya awali katika Ukristo, (Kila Mtu aliyemwamini Yesu ni lazima abatizwe). Na kumbuka lengo kuu la ubatizo sio wewe kupewa jina jipya. Hilo sio lengo la ubatizo, lengo la ubatizo ni kuzikwa kwa utu wako wa kale, na kufufuka katika upya.

Swali ni Je!  umebatizwa inavyopaswa kwa kuzamishwa na kwa jina la Bwana Yesu? Kama bado unasubiri nini?..Fanya hima ubatizwe ili uitimize haki yote!.na kumbuka pia ubatizo sio wa kunyunyiziwa wala wa uchangani, bali ni maji mengi! Na wa utu uzima.

Hivyo kama ulibatizwa pia utotoni, huna budi kubatizwa tena sasa, baada ya kujitambua, kwasababu wakati ule hukuwa umeokoka!, hukuwa umetubu..lakini sasa umejitambu, hivyo huna budi kubatizwa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga Namba hizi…

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

UFUNUO: Mlango wa 1

Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).

Rudi nyumbani

Print this post

Dameski ni wapi kwasasa?

Dameski ni mji ambao mtume Paulo alitokewa na Bwana Yesu, wakati akiwa anaelekea kuwaua wakristo ndani ya mji huo (Matendo 9:2-7). Mji wa Dameski mpaka leo upo!.. Ni moja ya miji ambayo haijabadilika jina lake mpaka leo, mingine mfano wa hiyo ni Yerusalemu na Bethlehemu.

Mji wa Dameski upo katika nchi ya SYRIA kwasasa. Tamaduni za watu waliopo Dameski ni tofauti na za watu wa enzi za kale… Hivyo mji upo Pamoja na watu, lakini tamaduni ni nyingine si ile ya zamani.

Nabii Isaya alipewa ufunuo juu ya mji huo kuja, kuondolewa kabisa katika siku za mwisho..

Isaya 17:1 “Ufunuo juu ya Dameski. TAZAMA, DAMESKI UMEONDOLEWA USIWE MJI, NAO UTAKUWA CHUNGU YA MAGOFU.

2 Miji ya Aroeri imeachwa; itakuwa kwa makundi ya kondoo, nao watajilaza huko wala hapana atakayewatia hofu.

3 Na ngome ya Efraimu itakomeshwa, na ufalme wa Dameski, na mabaki ya Shamu; watakuwa kama utukufu wa wana wa Israeli, asema Bwana wa majeshi”.

Pia vita vya Ezekieli 38, vilivyotabiriwa kuja kupiganwa kati ya Israeli na mataifa ya kandokando Pamoja na Gogu, itaifuta kabisa mji huo.

Kwasababu kwasasa ni mji unaopinga Yerusalemu kama mji mtakatifu wa Mungu mwenyezi na urithi wa Israeli, na unafanya vita dhidi ya Taifa h. Kwasababu hiyo utaondolewa Pamoja na miji mingine baadhi kulingana na biblia.

Isaya 49:23 “Habari za Dameski. Hamathi umetahayarika, na Arpadi pia; Maana wamesikia habari mbaya; Wameyeyuka kabisa; Huzuni iko baharini, haiwezi kutulia.

24 Dameski umedhoofika; Umejigeuza kukimbia; tetemko limeushika; Dhiki na huzuni zimeupata, Kama za mwanamke katika utungu wake.

25 Imekuwaje mji wa sifa haukuachwa, mji wa furaha yangu?

26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo, asema Bwana wa majeshi.

27 Nami nitawasha moto katika ukuta wa Dameski, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

Nyungu ni nini kibiblia?(Ayubu 41:20,31, Waamuzi 6:19)

Rudi nyumbani

Print this post

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Tarshishi ni mji uliokuwepo nchi ijulikanayo kwasasa kama Lebanoni. Taifa la Lebanoni katika nyakati za kale ndio Taifa lililokuwa linaongoza kwa uzalishaji wa miti aina ya MIEREZI (Kujua Mierezi ni miti gani fungua hapa >> MIEREZI).

Mji mkuu wa Taifa la Lebanoni, ndio ulikuwa Tarshishi. Mji huu wa Tarshishi ndio uliokuwa unaongoza kwa wafanya biashara, na ndio uliokuwa kitovu cha biashara ulimwenguni. Nabii Yona alikimbilia mji huu kwasababu ulikuwa na fursa nyingi. (Kwa urefu juu ya mji wa Tarshishi na biashara zake na Taifa hilo linafunua nini kiroho, fungua hapa >>Tarshishi).

Asili ya mji wa Tarshishi ni mwana wa Yafethi aliyeitwa Yavani, ambaye huyu Yavani ndiye aliyewazaa wenyeji wa Tarshishi.

Mwanzo 10:1 “Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.

2 Wana wa Yafethi ni Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.

3 Na wana wa Gomeri ni Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.

4 NA WANA WA YAVANI NI ELISHA, TARSHISHI, Kitimu, na Warodani”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Ashuru ni nchi gani kwa sasa?

MADHARA YA KUFUATA MAMBO YAKO TU!

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Rudi nyumbani

Print this post

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Ninawi ni wapi?

Ninawi ni mji uliokuwepo kaskazini mwa Taifa la Iraq kwasasa. Mji huu kwasasa haupo, ila mahali pale ulipokuwepo mpaka leo pako!. Na mji huu ndio uliokuwa mji mkuu wa Taifa la Ashuru. (Kujua Taifa la Ashuru ni wapi kwasasa fungua hapa> ASHURU).

Mji wa Ninawi ndio Mji Nabii Yona aliagizwa na Mungu akahubiri Injili, ili watu wa mji ule watubu, lakini alikataa na kukimbilia mji wa Tarshishi. Kujua Mji wa Tarshishi kwasasa ni nchi gani basi fungua hapa> TARSHISHI.

Mji wa Ninawi haukuwa mji wenye watu wengi sana lakini ulikuwa umeendelea sana. Kipindi Nabii Yona anatumwa kwenda kuhubiri huko, biblia inarekodi mji ule kuwa na watu 120,000 tu!.

Yona 4:10 “Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;

11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?”

Ijapokuwa Mungu alikusudia kuuadhibu mji huu lakini wenyeji wake walitubu kwa mahubiri ya Yona. Na Bwana Yesu alikuja kutoa unabii kwa vizazi hivi vya siku za mwisho kuwa..

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; KWA SABABU WAO WALITUBU KWA MAHUBIRI YA YONA; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

Na sisi tunapaswa tutubu kwa mahubiri ya Bwana Yesu, ili tusije kuangukia hukumu siku ya Mwisho.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Babeli ni nchi gani kwasasa?

NINI MAANA YA KUTUBU

YONA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

Ashuru ni nchi gani kwa sasa?

Ashuru ni wapi?

Ashuru ilikuwa ni nchi iliyokuwepo maeneo ya Iraq, Uturuki, na Syria..Mataifa haya matatu yamechangia sehemu ya nchi hiyo ya Ashuru, kama vile mataifa matatu (Kenya, Uganda na Tanzania), yalivyo na sehemu katika ziwa Victoria, kadhalika na Iraq, Uturuki na Syria ni sehemu ya Taifa hilo liliokuwa linaitwa Ashuru.

Lakini kwasasa duniani hakuna Taifa linaloitwa Ashuru. Kwani baada ya mataifa hayo matatu kuzaliwa hilo la Ashuru likafa.

Na Uliokuwa mji mkuu wa Taifa la Ashuru, uliitwa NINAWI. Ninawi ndio mji Nabii Yona alioambiwa akahubiri Injili, lakini kinyume chake akakimbilia Tarshishi..Kujua Ninawi ni wapi kwa sasa fungua hapa>NINAWI.

Vile vile kujua Tarshihi ni wapi kwasasa fungua hapa > TARSHISHI.

Asili ya Taifa la Ashuru kibiblia ni kutoka kwa Nimrodi..

Mwanzo 10:8 “Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.

9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.

10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.

11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;

12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa”.

Lakini Taifa la Ashuru ndilo lililowachukua Israeli na kuwapeleka utumwani katika Taifa hilo. Lakini baadaye walirudi katika Taifa lao chini ya amri ya Koreshi Mwajemi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je wale waliomsulubisha Bwana, wataenda mbinguni, kwakuwa walisamehewa?

Bwana Yesu alisema “Baba uwasamehe kwakuwa hawajui walitendalo (Luka 23:34)”. Je kwa kusema hivyo ina maana wote walisamehewa dhambi zao, kiasi cha kwamba hata wangekufa pale wangeenda mbinguni?.


Jibu: Dhambi waliyosamehewa ni hiyo ya kumsulibisha Bwana, na Bwana Yesu aliwasamehe kutoka moyoni, na hivyo Baba aliwasamehe pia.
Lakini kusamehewa kosa hilo, haimaanisha wamesamehewa na mengine yote..haimaanishi wamesamehewa uuaji waliofanya jana, au matusi waliyotukana juzi, au mauaji waliyoyatekeleza wiki iliyopita, au wizi walioufanya mwezi uliopita.

Hapana!..walichosamehewa ni hicho kimoja tu!..yaani kosa hilo la kumsulubisha Bwana Yesu!.

Ni sawa na wewe leo umsamehe mtu aliyekutapeli jana, na hivyo ukaghairi kumpeleka polisi, hiyo haimaanishi kasamehewa dhambi zake zote za utapeli alizowafanyia na wengine. Wewe umemsamehe kweli na Mungu pia kamsamehe.

Lakini hatia za makosa mengine aliyowafanyia wengine bado hajasamehewa mpaka atakapotubu.

Vile vile na waliomsulubisha Bwana walisamehewa tu dhambi hiyo moja ya kumsulubisha Bwana, nyingine zilizosalia walipaswa watubu.(Waungame dhambi zao zote, ndipo wawe salama).

Zaidi sana kama walikufa bila kumwamini Yesu, vile vile watahukumiwa kwa dhambi hiyo, hatakama walisamehewa ile kumsulubisha Bwana.

Yohana 3:18 “Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

19 Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu”.

Hivyo kama Bwana Mungu alipanga kuwapiga kwa kosa la kumsulibisha Bwana, alighairi na kuyaondoa hayo madhara, lakini ghadhabu ya makosa mengine waliyoyafanya ilikuwa pale pale, na zaidi sana ghadhabu ya wao kutomwamini Bwana bado haikuondolewa. Hiyo inaondolewa kwa mtu kuyasalimisha maisha yek kwa Yesu.

Hiyo ikitufundisha kuwa tunapaswa tuungame dhambi zetu zote kwa Bwana.

1 Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.
Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Ni kawaida mwanadamu anapopitia matatizo mengi au shida nyingi, huwa anatamani hata  afanane na mnyama asiyejua shida, anatamani angekuwa kama ndege apae zake aende mbali na makao ya watu akaishi humo.

Ndivyo Daudi alivyosema..kipindi ambacho anafukuzwa na Sauli huko majangwani, alisema..

Zaburi 55:5-8
[5]Hofu na tetemeko limenijia,
Na hofu kubwa imenifunikiza.
[6]Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa,
Ningerukia mbali na kustarehe.
[7]Ningekwenda zangu mbali, 
Ningetua jangwani.
[8]Ningefanya haraka kuzikimbia
Dhoruba na tufani.

Lakini jinsi Mungu alivyotuumba, kamwe hatuwezi kuzitoroka dhoruba na tufani za maisha…fahamu kuwa watu wanaokuudhi ndio hao hao utaendelea kuishi nao, na kama hutaishi nao nyumba moja, basi kuna kipindi mtakutana tu katika nukta fulani ya maisha..

Maadui zako, watesi wako, pamoja na wachawi hakuna siku Mungu atakutenga nao akupeleke katika dunia yako mwenyewe uishi huko kwa starehe, hicho kipindi hutakaa ukifikie haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani.

Mungu anachokifanya kwetu ni kutulinda na kutuepusha tu na madhara yao, yasitufikie. Lakini kuishi katikati yao ni jambo endelevu mpaka mwisho.
Bwana Yesu alisema;

Yohana 17:15
[15]Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.

Wakati mwingine, Mungu anapotaka kukupa rizki, anatumia hata njia ya hao hao, unakula katikati yao wakikuona..

Zaburi 23:5
[5]Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.

Hivyo ndugu uliyeokoka, acha kutaabika kwa ajili ya wanadamu, wala usipeleke akili zako mbali sana, ukidhania kuwa hao watu walio na wewe kama mwiba kuna siku watatoweshwa milele, uishi peke yako kwa starehe..Kanuni hiyo Mungu hajaichagua japo tunaitamani.

Zaidi sana jifunze kuyatimiza mapenzi ya Mungu katikati yao. Utakuwa na furaha katika maisha.
Kumbuka Mbawa kama za njiwa hatujapewa wanadamu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

Wokovu wa kweli ni upi?

Je unaposema umeokoka, ni nini kinakupa uhakika huo?

Fahamu ni nini Bwana anataka kuona kwako, pindi tu unapookoka.

Ni kweli katika Warumi 10:9 biblia inasema;

“Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka”.

Lakini kukiri kunakozungumziwa hapo, sio sawa na inavyotafsiriwa sasa. Zamani, kukiri kulimaanisha kutangaza vita na ulimwengu, Pamoja na kuhatarisha Maisha yako pia . Kwani ukristo ulijulikana kama ni dini asi, dhidi ya Imani za kipagani.

Soma,

Yohana 9:22 “.. kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba mtu akimkiri kuwa ni Kristo, atatengwa na sinagogi”.

Hivyo watu wengi walikuwa wanauliwa, wengine wanafukuzwa mbali na jamii, kwa jambo hilo tu moja, la kumkiri Yesu hadharani. Kwahiyo mtu yeyote kabla ya kwenda kumtangaza  Yesu hadharani kuwa ndiye mwokozi wake, alijifikiria mara mbili kwanza.

Sasa jambo kama hili linatokea kweli sehemu baadhi ulimwenguni, lakini  sio kote. Kwani sisi tuliopo katika mazingira mchanganyiko kama haya. Neno kukiri tu kwa kinywa, sio kipimo tosha kwamba wewe umemfuata Yesu, kwasababu mtu yeyote anaweza kufanya hivyo hata mpagani, kwasababu hakuna hatari yoyote inaweza kumtokea kama akifanya hivyo. Kwasababu anakuwa ni kama tu kaongea.

Na ndio maana leo hii kuna idadi kubwa sana ya watu wanajiita wakristo wanasema wameokoka. Ukiwauliza wameokokaje watakuambia, kwasababu walimkiri Yesu kwa vinywa vyao, hilo tu.Na huku ukiangalia Maisha yao, hayana tofauti na watu wa kidunia.

Ndugu usidanganyike, wokovu wetu ili ufanane na ule wa watu wa zamani, hatuna budi tumkiri Yesu KWA MATENDO YETU. Tunaukataa ulimwengu na mambo yake yote, kivitendo.

Bwana Yesu alitabiri kuwa siku za mwisho, wengi watamwita ‘Bwana, Bwana’, kwa midomo tu, lakini matendo yao yapo mbali naye, lakini anasema atawafukuza Dhahiri.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Umeona? Ikiwa hao atakaowafukuza wanafanya miujiza mikubwa, na kutoa ishara nyingi, jiulize wewe ambaye hutendi lolote, na bado unatenda dhambi, unadhani utamwonga Mungu, kisa uliongozwa sala ya toba?

Ndugu, ni kuwa makini sana nyakati hizi, Ukisema umeokoka, uthibitishe wokovu wako kwa matendo kwamba umeuacha ulimwengu kweli kweli. Unaacha hivyo vimini, hizo suruali uvaazo binti,Uzinzi, anasa, punyeto, picha za ngono utazamazo mitandaoni.

Kuongozwa sala ya toba mara nyingi, sio tiketi ya kwenda mbinguni, bali badiliko lako ndilo litakalokuoa.

Bwana atufumbue macho yetu tulione hilo.

Print this post

Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?

Swali: Ayubu alijaribiwa na shetani, iweje biblia iseme “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni kuteketeza kondoo zake”?.


Jibu: Tusome,

Ayubu 1:14 “Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari”.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe..

Ikumbukwe kuwa Ayubu pamoja na watumwa wake wote hapo mwanzo hawakujua kuwa ni shetani ndiye anayewajaribu.. Ayubu alijua ni Mungu ndiye kamletea majaribu yote yale, ingawa hakujua sababu.. Halikadhalika watumwa wake wote na marafiki zake wote walijua ni Mungu ndiye katuma moto kuwateketeza wale kondoo na kumpiga Ayubu kwa mapigo yote yale. Ndio maana tunaona hata hapo huyo mtumwa akitaja huo moto, kana kwamba ni kutoka kwa Mungu.

Ni baadaye sana, Mungu alipomtokea Ayubu katika upepo wa kisulisuli na kumfunulia jambo lililokuwa linaendelea rohoni, jinsi shetani alivyopeleka mashitaka mbele zake dhidi yake Ayubu. Ndipo Ayubu alipoelewa sababu ya matatizo yote ni shetani, na aliyewaua wanawe ni shetani, na aliyeleta moto ni shetani na si Mungu…Lakini hapo mwanzo wakati anajaribiwa hakujua hilo.. yeye alijua ni Mungu tu!, ndio maana utaona Ayubu naye alisema..

Ayubu 1:21 “akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA ALITOA, NA BWANA AMETWAA; jina la Bwana na libarikiwe”.

Umeona hapo anasema BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA!!.. Maana yake alikuwa anajua kabisa kuwa aliyewaua wanawe wote 10 ni Mungu, na si shetani!. Ambapo kiuhalisia ni shetani ndiye aliyewaua isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa Mungu.

Hiyo inatufundisha nini?.

Tunaweza kupitia majaribu fulani tukadhani ni Mungu kayaleta kumbe ni shetani?..isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa Mungu. Na majaribu hayo yamegawanyika katika sehemu kuu (2)

 1. Majaribu ya shetani kwa Mtakatifu.

Kama umesimama katika imani kama Ayubu na unajikuta unapitia majaribu mazito!, kama magonjwa, misiba, dhiki, n.k basi fahamu kuwa ni Mungu kamruhusu shetani akujaribu.. Hivyo simama usiogope kwasababu mwisho wako utakuwa ni mzuri kuliko mwanzo, Kama ulivyokuwa wa Ayubu.

 2. Majaribu ya shetani kwa Mtu ambaye hajaokoka!

Kama hujampokea Yesu, na ni mtu wa kiulimwengu, na unajikuta katika majaribu mazito mazito kama misiba, magonjwa, dhiki, mateso. Jua ni Mungu kamruhusu shetani akujaribu kwa kukuletea hayo matatizo ili utubu umgeukie yeye. Lakini usipoitii sauti ya Mungu na kutubu basi shetani atakumaliza kabisa kabisa. Maana lengo lake yeye(shetani) ni wewe ufe katika dhambi na mateso.

Hivyo suluhisho la haraka hapo ni wewe kumpokea Bwana Yesu, akusafishe dhambi zako na kukuosha na kisha atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Na hivyo ule ulinzi wa kiMungu utaongezeka juu yako.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba shetani ndiye aliyeuleta ule moto!, na si Mungu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Tusome,

1 Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.

12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.

13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.

14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu

15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ILA YEYE MWENYEWE ATAOKOLEWA; LAKINI NI KAMA KWA MOTO.”.

Awali ya yote ni muhimu kufahamu aina za Hukumu za Mungu.

Kuna aina kuu mbili (2) za Hukumu; 1)Hukumu ya Waovu na 2)Hukumu ya watakatifu.

Hukumu ya waovu ni ile inayotajwa katika Ufunuo 21, ambayo inajulikana kama hukumu ya kiti cheupe cha Mungu. Katika hukumu hii, wafu wote waliokufa katika dhambi watafufuliwa na kuhukumiwa kulingana na matendo yao mabaya waliyokuwa wanaifanya…

Kadhalika ipo hukumu ya Watakatifu, ambayo hii itakuwa mbinguni.

Hii haitakuwa hukumu ya kulaumiwa bali ya thawabu.. Wale walioshinda watasimamishwa mbele za Bwana na kila mtu atapewa thawabu kulingana na utumishi wake hapa duniani. Waliofanya vizuri watapewa thawabu kubwa na wale ambao hawakufanya vizuri sana watapewa thawabu kidogo na wengine hawatapewa kabisa.. Ingawa wataingia mbinguni kwasababu walikuwa watakatifu!.

Hivyo hukumu hiyo inayozungumzwa hapo katika (1 Wakorintho 3:13) ya kazi ya kila mtu kupimwa kwa Moto!, sio hukumu inayowahusu waovu!,  la! bali inayowahusu wale walioshinda, (watakatifu) ambao wataingia mbinguni..

Kwahiyo hawa walioshinda kama huku duniani walikuwa watakatifu lakini katika eneo la utumishi, hawakufanya vizuri..(maana yake waliyapunguza maneno ya Mungu, hawakuwafundisha watu kweli yote)…aidha kutokanana na hofu fulani, au kuhofia shinikizo Fulani..basi siku ile watapata hasara kubwa sana mbinguni.

Kwamfano utaona kuna watu wanajua kabisa, kuwa pasipo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu, lakini baada ya kujua hayo, wanaogopa kuwasisitiza watu wawe watakatifu mwilini na rohoni kama wao walivyo, wakihofia kuwakwaza wale watu..utaona wanawaambia tu! Juu juu lakini kamwe hawazami ndani kuwaeleza madhara ya kutokuwa watakatifu. Mwisho wanajikuta wanatengeneza watu wengi ambao hawataenda mbinguni siku ya mwisho, kwasababu ni vuguvugu..bali watatupwa katika ziwa la moto.

Biblia inasema maneno ya Mungu ni kama Moto. Kwahiyo siku ile matunda yao yote yatajaribiwa kwa moto.. (watu wote waliowahubiria wao)..

Sasa moto ni nini?

Biblia inasema maneno ya MUNGU NDIO MOTO!

Yeremia 23:29 “Je! NENO LANGU SI KAMA MOTO? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?”

Na mfano wa maneno ya Mungu ambayo ni moto ni haya…

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU.”

Mtu yeyote tuliyemhubiria atajaribiwa kwa Maneno hayo katika siku ile ya Mwisho.. Na kama atafaulu kipimo hicho, maaana yake ataingia mbinguni, kule tulipo sisi, na hivyo sisi tuliyemhubiria tutapata faida!..hapo ndio litatimia hilo neno (… Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu).

Lakini matunda tuliyoyahubiria yakifeli hicho kipimo cha maneno hayo, basi yatatupwa katika ziwa la moto na sisi tuliyoyahubiria tutapata hasara!, (hakuna thawabu yoyote tutakayopewa)..na ndio litatimia hilo neno… “Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.”

Sasa kwanini hapo iseme..“Ataokolewa lakini kama kwa moto” ??

Kikawaida mtu anapopata hasara, na huku alitegemea kupata faida! Moyoni hatafurahia sana..tofauti na yule ambaye alitegemea kupata faida na kule akakuta kapata faida kubwa Zaidi.

Hivyo yule aliyepata hasara lakini kaokolewa, ataingia mbinguni huku akiwa amekosa vile alivyovitarajia,(maana alitarajia thawabu kubwa lakini hakuzipata) hivyo hiyo hali ya kukosa vile alivyovitarajia na huku anaona wengine wakivishwa mataji ya ushindi ndio inaitwa “kuokolewa kama kwa moto”.

Baadhi ya dini zinatumia andiko hili kuhalalisha Imani ya “toharani” kwamba mtu akifa katika dhambi, anaweza kupitishwa kwenye mateso ya moto kwa kitambo kichache kisha akatolewa kule.. kwasababu hapo imesema ..“Ataokolewa lakini kama kwa moto”.

Imani hiyo ni Imani potofu, kutoka kwa yule adui shetani, hakuna nafasi ya pili, kwa mtu atakayekufa katika dhambi (Waebrania 9:27). shetani kalipandikiza hilo fundisho katika baadhi ya dini, ili watu wastarehe katika dhambi huku wakiamini kwamba hata wakifa katika dhambi zao, basi ipo nafasi ya pili.. watapitishwa kwenye moto kidogo kisha watatolewa siku moja.

Usidanganyike, wala tusidanganyike!..mtu akifa leo katika dhambi, Habari yake imeisha..atakachotazamia ni hukumu na kisha kutupwa katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti.

Je! Na wewe leo unahubiri injili gani?..unajenga jengo la namna gani?, la nyasi, fito au Mawe ya thamani.

Mawe ya thamani ni wale watu wanaosikia injili ya kweli isiyoghoshiwa, ambayo haujachanganywa na chochote.

Nyasi na fito ni wale watu ambao wanahubiriwa kuwa Mungu haangalii mwili anaangalia tu roho!, ni wale wanaohubiriwa mambo ya ulimwengu tu, hawahubiriwi juu ya hatima ya roho zao.

Je na wewe unatengeneza watu wa namna gani?, unajenga jengo gani?

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10


Mada Nyinginezo:

Walakini ataokolewa kwa uzazi wake.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 2)

Nini maana ya ‘Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma’?

Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?

Rudi nyumbani

Print this post